136
1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Tano – Tarehe 11 Septemba, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu. NDG. ASIA MINJA – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO (K.n.y WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba (Intergovernmental Agreement – IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Uganda kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (East Africa Crude Oil Pipeline – EACOP) kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania). MHE. DEO F. NGALAWA - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI): Maoni ya Kamati ya Nishati na Madini kuhusu Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba (Intergovernmental Agreement – IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

  • Upload
    others

  • View
    3

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

1

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

BUNGE LA TANZANIA____________

MAJADILIANO YA BUNGE___________

MKUTANO WA NANE

Kikao cha Tano – Tarehe 11 Septemba, 2017

(Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi)

D U A

Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua

NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu.

NDG. ASIA MINJA – KATIBU MEZANI:

HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI

Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:-

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO(K.n.y WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA):

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba(Intergovernmental Agreement – IGA) baina ya Serikali yaJamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri yaUganda kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bomba la KusafirishaMafuta Ghafi la Afrika Mashariki (East Africa Crude Oil Pipeline– EACOP) kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania).

MHE. DEO F. NGALAWA - MAKAMU MWENYEKITI WAKAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI):

Maoni ya Kamati ya Nishati na Madini kuhusu Azimiola Bunge la Kuridhia Mkataba (Intergovernmental Agreement– IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Page 2: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

2

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

na Serikali ya Jamhuri ya Uganda kuhusu Mradi wa Ujenzi waBomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EastAfrica Crude Oil Pipeline – EACOP) kutoka Hoima (Uganda)hadi Tanga (Tanzania).

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y MSEMAJI MKUU WAKAMBI RASMI YA UPINZANI KWA WIZARA YA NISHATI NAMADINI):

Maoni ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzanijuu ya Wizara ya Nishati na Madini kuhusu Azimio la Bunge laKuridhia Mkataba (Intergovernmental Agreement – IGA) bainaya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikaliya Jamhuri ya Uganda kuhusu Mradi wa ujenzi wa Bomba laKusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (East Africa CrudeOil Pipeline – EACOP) kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga(Tanzania).

NAIBU SPIKA: Katibu.

NDG. ASIA MINJA – KATIBU MEZANI:

MASWALI NA MAJIBU

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tutaanza naOfisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Dkt. Raphael MasungaChegeni, Mbunge wa Busega, sasa aulize swali lake.

Na. 52

Kuunganisha Mashirika ya Hifadhi ya Jamii

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:-

Mafao ya wanachama wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamiina Mashirika mengi ya Hifadhi ya Jamii yamekuwa na utatakuhusu fao la kujitoa. Je, Serikali inatoa tamko gani ikiwa nipamoja na uwezekano wa kuunganisha mifuko hiyo nakuondoa mkanganyiko kwa wanachama?

Page 3: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

3

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANANA AJIRA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya MheshimiwaWaziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa RaphaelMasunga Chegeni, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wamkataba wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) Na. 102 wa mwaka1952, fao la kujitoa sio miongoni mwa mafao yaliyoainishwakatika mkataba huo. Kwa hapa Tanzania fao la kujitoa niutaratibu wa wanachama kujitoa na kuchukua mafao yakokatika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa mafao ya penshenikabla ya kufikisha umri wa kustaafu. Utaratibu huuumezoeleka miongoni mwa wanachama wa mifuko hiyona hata kuonekana ni mojawapo ya mafao ya hifadhi yajamii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambuachangamoto ya kipato inayowakabili wafanyakazi walewanaopoteza ajira, Serikali itawasil isha Bungenimapendekezo ya marekebisho ya Sheria za Hifadhi ya Jamiiyatakayoanzisha fao la upotevu wa ajira (unemploymentbenefit) kwa wafanyakazi watakaokuwa wanapoteza ajirakabla ya kufikisha umri wa kustaafu kazi. Fao hili litakuwalinatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa mafao yapensheni.

(b) Mheshimiwa Spika, Serikali inatambuachangamoto ya wingi wa mifuko inayoikabili Sekta ya Hifadhiya Jamii. Ili kukabiliana na changamoto hiyo, mwaka 2015Serikali ilifanya tathmini ya mifuko yote ya pensheni kwa lengola kuangalia uwezekano na namna bora ya kuiunganisha.Matokeo ya tathmini hiyo yalionesha kuwa inawezekanakuunganisha mifuko hiyo na kubaki na michache kwakuzingatia hali halisi ya mahitaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na matokeo yatathmini hiyo, Serikali imeandaa mapendekezo yakuunganisha mifuko mitano inayotoa mafao ya pensheni na

Page 4: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

4

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

kubaki na michache iliyo imara. Mapendekezo hayoyameshajadiliwa na wadau wa kukubaliwa. Hatuainayoendelea hivi sasa ni kuwasilisha mapendekezo hayokatika vikao maalum vya Serikali ili Serikali itoe kibali. Matokeoya kuunganisha mifuko hiyo ni pamoja na kupunguzagharama za uendeshaji, kuboresha mafao na kuifanyamifuko kufanya kazi kwa ufanisi na kwa uendelevu katikakipindi cha muda mrefu ujao.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Raphael Chegeni swalila nyongeza.

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa NaibuSpika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri yaMheshimiwa Naibu Waziri ambayo yamejikita katika kuelezeauhalisia wa mifuko hii na changamoto zilizopo, nina maswalimawili madogo ya nyongeza.

Kwanza, kwa vile inaonekana wazi kwambawatumishi wengi na hasa wanachama wa mifuko hiiwanapokuwa wameachishwa kazi au wametorokwa nawaajiri wao wanahangaika sana kuweza kujikimu katikamaisha yao na hiyo sio hiari yao isipokuwa wameachishwakazi au wametorokwa na waajiri. Sasa Serikali haionikwamba kuna haja hawa watu ambao wanapatadhahama hii, wasaidiwe kuchukua mafao yao ili wajikimukatika maisha yao wakati wakitafuta kazi zingine za kuwezakujipatia kipato?

Swali la pili, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziriamekiri kabisa kwamba mifuko hii ina changamoto nyingisana, ikiwa ni pamoja na gharama za uendeshaji ambayoinakula mifuko ya wanachama hawa, lakini pili kutokanana kwamba mifuko hii imekuwa mingi mno na utitiri ambaomafao yao hata hayana tija kwa wanachama wenyewe.

Je, ni lini sasa Serikali, kufuatia kauli ya MheshimiwaRais siku ya sherehe ya Mei Mosi Moshi katika Mkoa waKilimanjaro alipotaka Serikali ilete hoja hapa Bungeni,Muswada wa kuweza kuigawa mifuko hii kutoka utiriri huu

Page 5: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

5

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

na kubakiwa na angalau mifuko miwili tu ambayo itakuwana sekta ya umma au na sekta binafsi?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Raphael Chegeni umeanzana ni lini, hujamalizia sasa swali lako ni lipi kwenye swali lakola pil i. Sekunde tano, usirudie maelezo, maelezoameshayasikia, lakini swali lako ni nini, yaani maana umeulizani lini halafu ukaanza maelezo bila kusema sasa swalo lakoni lini nini yaani? Malizia.

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa NaibuSpika, ni kwamba ni lini Serikali itatii maagizo ya MheshimiwaRais kwa kuleta Muswada hapa Bungeni ili tuweze kurekebishasuala la mifuko hii? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri Ofisi ya WaziriMkuu majibu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANANA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake lakwanza naomba tu nirudie majibu yangu ya msingi yakwamba katika kuliangalia suala hili la fao la kujitoa kamalilivyokuwa linaitwa, sisi kama Serikali na kupitia maazimioya Bunge hili mwaka 2012 ambayo ilisema Serikali iangalieutaratibu mzuri wa kushughulika na suala hili la fao la kujitoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kama nilivyosematayari tumekwishaanza maandalizi ya kuja na utaratibumwingine mbadala ambao utamfanya mfanyakazi waKitanzania yule ambaye ataachishwa kazi na hajafikisha umrihuo wa miaka 60 wa kuchukua mafao yake, tuone namnaya kuweza kuliweka sawa na kumsaidia asipate shida katikamuda huu wote wakati bado anasubiria kupata ajiranyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo kwa sababu jambohili linakuja Bungeni, nimuombe tu Mheshimiwa Mbungeavute subira. Muda sio mrefu tutawasilisha mapendekezo yetuhayo na ninyi kama Wabunge mtapata nafasi za kuwezakuchangia na kutushauri vema sisi kama Serikali. (Makofi)

Page 6: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

6

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lke la pili; ni lini tutatiimaagizo ya Mheshimiwa Rais ya kuunganisha mifuko hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimuondoe hofuMheshimiwa Mbunge ya kwamba sisi baada ya tamko laMheshimiwa Rais kazi hiyo imefanyika mara moja na katikamajibu yangu ya msingi nimesema tayari tumeshakutana nawadau, tumezungumza namna bora ya kuunganisha mifukohii na muda sio mrefu tutatoa pia taarifa sehemi ambayotumefikia na tutawapa pia the way forward ya namnaambavyo mifuko hii itakuwa. Hivyo Mheshimiwa Mbungevuta subira tu, hii yote iko katika mipango na agizo laMheshimiwa Rais tumelitii na tumelitekeleza. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge nimewaona.Nitoe tu ushauri ili tuweze kwenda vizuri, maswali ya nyongezayawe kwa kifupi maana muda wetu hautoshi, tunajua tunasaa moja na nusu.

Mheshimiwa Richard Mbogo swali la nyongeza.

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Badala ya kuwa na fao la kupoteza ajira, kwa niniSerikali isilete sheria na kuibadilisha katika mafao ya mtuapewe angalau theluthi moja ya mafao yake baada yakuwa amepoteza ajira?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya WaziriMkuu, majibu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANANA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nirejee tumaneno yangu ambayo nimeyasema pale awali katika jibula msingi ya kwamba Serikali tutaleta mapendekezo yetu naBunge hili litakuwa na nafasi ya kuweza kutushauri vema.Mimi nafikiri katika hali hii ambayo tumefikia hivi sasa,Waheshimiwa Wabunge mtuvumilie na msubiri muonemapendekezo ya Serikali na baada ya hapo mtatushaurituone namna bora ya kuweza kulifanya jambo hili tuondoematatizo kwa wafanyakazi wetu. (Makofi)

Page 7: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

7

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kasuku Bilago, swali lanyongeza.

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante kwa nafasi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili mfanyakazi aliyemalizakazi kwa kustaafu au kupoteza kazi aweze kulipwa mafaoyake katika mifuko ya Hifadhi ya Jamii, ni pamoja na kupatabarua yake ya mwisho. Wafanyakazi waliopatikana na vyetifake hawajapata mafao yao kutoka kwenye Mifuko yaHifadhi ya Jamii kwa sababu hawana barua za kumaliza huoufanyakazi fake.

Je, Serikali iko tayari kuwapa barua zao il iwakahangaike kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi yaWaziri Mkuu majibu. (Kicheko)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE,KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa NaibuSpika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Wazirikwa majibu yake mazuri na majibu fasaha na huo ndiyoutaratibu wa Serikali katika kushughulikia yale ya awali.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika jibu la MheshimiwaBilago, swali hil i la mafao ya watumishi ambaowameonekana kwamba ni watumishi wenye vyeti fake naambao wamepatikana na masuala kadha wa kadha katikautumishi wao, limekuwa likijibiwa na Serikali mara kadhaandani ya Bunge lako Tukufu na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Utumishi wa Umma. Ninaomba Mheshimiwa Mbunge naWaheshimiwa Wabunge wengine wote waendelee kuvutasubira, yale ambayo yamekuwa yakijibiwa na Waziri mwenyedhamana ya Utumishi wa Umma hayo ndiyo ambayoyatakuja kutekelezwa baada ya Serikali kufikia maamuzi yaleambayo Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya Utumishiwa Umma amekuwa akieleza humu ndani ya Bunge lakoTukufu kila siku.

Page 8: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

8

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendeleana Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mheshimiwa Oscar RwegasiraMukasa Mbunge wa Biharamulo Magharibi sasa aulize swalilake.

Na. 53

Kero ya Kutopandishwa Madaraja kwa Walimu nchini

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:-

Walimu Wilayani Biharamulo na kwingineko nchiniwanalalamika kwamba jitihada zao kwenda masomonikujiendeleza zinafuatiwa na kusitishwa kwa upandaji wamadaraja yao katika utumishi wa umma. Pale ambapomwalimu kapanda daraja kunaenda sanjari na yeye kuwamasomoni.

Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kero hii nakukatishwa tamaa kwa walimu wetu?

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri waNchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali laMheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge waBiharamulo Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tunawapongeza walimuwote na wataalam mbalimbali wanaojiendeleza kwa lengola kuongeza ufanisi wao wawapo kazini. Kwa utaratibu wasasa kupanda daraja kunaendana na matokeo ya ufanisikazini baada ya kupimwa jinsi mtumishi alivyotekelezamalengo yake. Kwa utaratibu uliopo, mwalimualiyejiendeleza hadi ngazi ya stashahada au shahadaanapaswa kubadilishiwa muundo baada ya kuwasilisha vyetivyake kwa mwajiri wake. Hivyo, waajiri wote wanapaswakuzingatia taratibu za utumishi kwa kutenga bajeti kwawatumishi walio katika maeneo yao.

Page 9: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

9

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Oscar Mukasa, swali lanyongeza.

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Wazirilakini naomba kufahamu kwamba kwa maelekezo hayoambayo Serikali imeyatoa kwa waajiri kutekelezaupandishwaji wa madaraja hayo.

Je, Serikali iko tayari sasa kuratibu suala hilo ilikuhakikisha kwamba tunafanya uhakiki wa walimu wotewenye malalamiko haya ili yapatiwe utatuzi.

Swali la pili, kwa sababu pia yako malalamiko kutokakwenye Halmashauri zetu kwamba Walimu wanapokwendakujiendeleza unatokea upungufu wa Walimu kwenye shulewanazotoka.

Je, Serikali iko tayari kutumia vizuri fursa ya Chuo KikuuHuria ili yenyewe kwa ngazi ya Serikali Kuu iratibu namna yakuwasaidia Walimu wajiendeleze kwa kupitia Chuo KikuuHuria bila kuathiri uwepo wao kwenye shule zao?Ninakushukuru.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, majibu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hoja yaMheshimiwa Oscar ni kwamba kufanya tathmini ya kuratibuvizuri mchakato huu, naomba tulipokee hili kwa sababulengo kubwa ni kwamba kama Serikali tuna haja yawatumishi mbalimbali ambao malalamiko yao yapo yawezekufanyiwa kazi kwa sababu tunajua yakifanyiwa kazi vizurindiyo wataweza kufanya kazi vizuri wanapokuwa ofisinimwao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo MheshimiwaMukasa nadhani hii ni hoja ya mapendekezo na sisi

Page 10: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

10

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

tutaangalia jinsi gani tuweze kuratibu vizuri ili haki yamfanyakazi iweze kupatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili katika eneola pili ni kwamba jinsi gani tufanye kwamba tutoe maelekezoya watumishi wote kada ya ualimu kutumia Chuo KikuuHuria. Nadhani tuweke hili dirisha wazi kwa sababu kilamwalimu ana preference yake na kitu gani anachokihitaji,isipokuwa jambo la misngi ni lazima tuweke mipango mizurilengo ni kwamba walimu watakapoenda kujiendeleza basitusiwe na mapungufu makubwa katika maeneo yetu.Tunajua kwamba tatizo hili limekabili maeneo mbalimbalilakini hoja hii ni hoja ya msingi nadhani hili sasa katikamamlaka ya Serikali za Mitaa tutatoa maelekezo mahsusi yakiutawala/kiofisi kwamba nini kifanyike kama walimuwangapi wanatakiwa wakiondoka wengine wabaki, iliwatoto wasiathirike.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo katika mchakatowetu ambao tunaufanya hivi sasa lengo kubwa ni kuajiriwalimu wapya tunajua kwamba tukiongeza idadi ya Walimututaweza kupunguza kwa kiwango kikubwa tatizo hiliambalo liko hivi sasa katika Halmashauri zetu. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Elimu.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasihii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Naibu Wazirikwa majibu mazuri, lakini nataka kuweka msisitizo tukwamba msimamo wa Serikali kuhusu wanafunzi kujiungana vyuo vikuu ni kwamba mwanafunzi anachaguamwenyewe mahali ambapo anataka kusoma, kwa hiyoutaratibu huo unawahusu watarajiwa wote wa vyuo vikuuikiwa ni pamoja na walimu. Kwa hiyo, Serikali itaendeleakuweka tu mazingira mazuri ili wanafunzi waweze kuendeleakuwa na fursa ya kwenda mahali wanapotaka lakini Serikalihaiwezi ikampangia mtu kinyume na matakwa yake. (Makofi)

Page 11: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

11

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Mheshimiwa Bobali swalila nyongeza.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Naibu Spika,nakushuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tabia kwenyeHalmashauri wanapokwenda masomoni baadhi yawatumishi kwenye Halmashauri, Halmashauri zinakuwazinagharamia hususan wale walioko kwenye ngazi ya paleHalmashauri. Lakini si kwa kada za ualimu na kada zingine.

Je, nini kauli ya Serikali kwamba Halmashaurizinagharamia masomo kwa wale watumishi waliopo ndaniya Halmashauri pale pale au kwa watumishi wa Halmashaurinzima? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, majibu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu nikwamba kuna utaratibu wa mapendekezo ya watukuonyesha preference yao kwamba watu wanataka kwendakusoma, hili mara nyingi sana huwa inawekwa katikamchanganuo wa kibajeti katika kila Idara, kwamba kila Idaraina utaratibu na mipango yake kwamba mwaka huu kunawatu wangapi wataenda kusoma. Kwa hiyo, jambo hili siowale wa Makao Makuu peke yake hapana, jambo hili maanayake ni kwa Halmashauri nzima, kama kuna Halmashauriambayo inafanya kuwapa upendeleo maalum wale waliopoMakao Makuu peke yake, hilo ni kosa na halikubaliki.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, utaratibu ni kwambampango wa bajeti wanapopanga bajeti wanapangamwaka huu Idara fulani tutapeleka watu fulani kusomakatika level fulani ambayo inaingizwa katika bajeti, thenunaweka hilo open door policy katika hiyo Idara, kila mtuaweze ku-apply kuangalia nani ata-qualify katika kipindihicho kuweza kupata fursa ya masomo, kwa sababu mkate

Page 12: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

12

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

huo ni mkate wa Halmashauri nzima siyo watu maalum katikaMakao Makuu ya Halmashauri.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Salma Kikwete swali lanyongeza.

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante na naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, walimu wengi walipatafursa ya kwenda kujiendeleza na waliweza kujiendeleza, palewanapokuwa wanafanya hayo masomo yao katika ngaziya shahada wanapokwenda kwenye ile Block TeachingPractice walimu hawa wanapangiwa kwenye shule zasekondari na wanapomaliza bado walimu hawawanarejeshwa kwenye shule za msingi. Wanaporejeshwakwenye shule za msingi, yale waliyosomea hayapo kwenyeshule za msingi bali yapo kwenye shule za sekondari.

Serikali hapa ina utaratibu gani wa kubadilisha auwa kutengeneza mitaala kuhusiana na shule za msingi iliwakitoka kule warudi kule kule walikotoka? (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Mamayangu Salma Kikwete anazungumzia changamoto za jinsigani tuweze kuboresha elimu yetu kwa watu walioko katikavyuo wanapoenda kwenye katika zile field practical nawanapoenda kufundisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni wazo kwa sababubahati nzuri Mheshimiwa ni mwalimu anajua changamotogani zipo na vipi tuziboreshe. Mimi naomba tulichukue hilikama wazo jema, kwamba nini tufanye hasa katika sualazima la mitaala kiujumla wake, hata hivyo, tuangalie ni jinsigani wanafunzi wetu wanapokuwa katika masomo, kile kituambacho anaenda kufanyia field practical na iwe bestpractice akienda kwenye kazi. Kwa hiyo, nasema huu niushauri mzuri, Serikali tumeuchukua, tunachukua mawazomazuri, kwa sababu tuko katika mchakato wa kuboresha

Page 13: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

13

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

elimu yetu iwe elimu shindani tunachukua mawazo haya kwaajili ya kuyafanyia kazi vizuri. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Elimu.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TAKNOLOJIA:Mheshiwa Naibu Spika, ahsante sana. nampongezaMheshimiwa kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuongezea tukwamba lengo la kufanya mafunzo kwa vitendo ni kutoafursa kwa wanafunzi kuweza kufanya kwa vitendo kileambacho wanajifunza. Katika teaching practice jambokubwa ambalo linaangaliwa ni ule mfumo wa ufundishajiyaani kwa kingereza tunaita pedagogical skills, jinsi ambavyomwalimu anaweza akalihimili darasa, anaweza akafanyayale ambayo yanatakiwa kumudu darasa lake. Kwa hiyo,mwalimu ambaye anajifunza mafunzo ya sekondari principalza darasani kwenda kujifunza, hata akienda kufanya katikashule za msingi hakuna jambo lolote ambalo linaharibika.Ndio maana wapo walimu wa sekondari wanapangiwakwenda kufundisha shule za msingi kwa sababukinachoangaliwa ni ule uwezo wa mwalimu kufanya uleufundishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na ninianachokifundisha, ukiangalia maudhui ya mtaala katikaelimu ya msingi ni ya kiwango cha chini kuliko ya sekondari.Kwa hiyo, ni dhahiri kwamba mwalimu ambaye ana uwezowa kufundisha sekondari atakuwa ni mwalimu mzuri sanakatika kufundisha shule za msingi. (Makofi)

Na.54

Ujenzi wa Barabara ya Rujewa - Mbarali

MHE. ORAN M. NJEZA (K. n. y MHE. HAROON M.PIRMOHAMED) aliuliza:-

Mji Mdogo wa Rujewa ni kitovu cha shughuli za

Page 14: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

14

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

biashara na Makao Makuu ya Wilaya ya Mbarali na kwabahati mbaya barabara nyingi za mji huo hazipitiki kutokanana ubovu. Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniaaliahidi kujenga kilometa tano za barabara kwa kiwangocha lami.

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo kwa wananchiwa Mbarali?

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri waNchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali laMheshimiwa Haroon Mulla Pirmohamed, Mbunge wa Mbarali,kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha2016/2017, Halmashauri Wilaya ya Mbarali iliidhinishiwa nakupokea shilingi milioni 793.02 kwa ajili ya matengenezo yabarabara kilomita 20, kalavati kubwa 17 na matengenezoya madaraja matano. Serikali itafanya kila liwezekanalo iliahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais iweze kutekelezwa ndani yamiaka mitano ya utekelezaji wa Ilani. Halmashauri imepangakuweka kipaumbele na kutenga bajeti katika mwaka wafedha 2018/2019 ili kuanza utekelezaji wa ahadi ya kujengakilometa tano za barabara kwa kiwango cha lami kwausimamizi wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini (TARURA).

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Oran Njeza, swali lanyongeza.

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika,nashukuru sana vilevile nishukuru kwa majibu mazuri yaMheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili yanyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kazi zilizokuwazinaendelea zilizokuwa zinafanywa na Halmashauri na hizo

Page 15: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

15

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

zimehamishiwa kwenye TARURA sasa hivi. Je, ni lini TARURAwataanza na kuendeleza hizo kazi?

Swali la pili, kama ilivyo katika Mji Mdogo wa Rujewavilevile Mheshimiwa Rais aliahidi kumalizia ujenzi wa kituocha mabasi cha Mbalizi katika Mji Mdogo wa Mbalizi.

Je, ni lini kazi hiyo ya kujenga kituo cha mabasi chaMji Mdogo wa Mbalizi kitaanza? Ahsante.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwelitumekuwa na kipindi cha mpito ambapo kazi za ujenzi wabarabara katika Halmashauri zilikuwa zikisimamiwa ndaniya Halmashauri zetu, lakini chini ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI.Sasa hivi tumeunda Wakala wa Barabara Vijijini na Mijiniambao unaitwa TARURA sasa umeshaanza kuchukuamajukumu hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, tunafahamuwazi kwamba kulikuwa na mikataba mingine na kazimbalimbali zilikuwa zinaendelea na tulitoa maelekezo katikaofisi yetu kwamba zile kazi zote kutokana na mikatabailiyokuwa inaendelea ambazo ziliingiliwa na Halmashauri kazizile zilipaswa kuendelea, isipokuwa taratibu za malipo ndiozilikuwa zinafanyiwa utaratibu maalum. Tulitoa maelekezohaya kwa Mameneja wa TARURA katika nchi nzima katikaJamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, wakatimwingine kulikuwa na uelewa tofauti katika baadhi yamaeneo, baadhi ya maeneo kazi zilikuwa zinaendelea vizurilakini sehemu zingine kazi zilisimama, kazi kubwa iliyofanyikani kuhamisha zile akaunti ziweze kufanya kazi vizuri iliutaratibu uendelee kufanyika kama ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na concern yakoMheshimiwa Oran naomba niiagize Halmashauri yako Menejakama kuna changamoto ambayo ameipata katika ofisi yaketuwasiliane na ofisi na hasa na Mtendaji Mkuu wa TARURAampe maelekezo ya kutosha nini kifanyike, ili kazi kule siteisiendelee kukwama, ziendelee kufanyika.

Page 16: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

16

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la ujenzi wastendi hii ya Mbarali, naomba nilichukue hili halafu nijuekwamba kuna kitu gani kilichokubaliwa na imefikia hatuagani? Changamoto iko wapi? Hili naomba niwahakikishieofisi yangu itasimamia kwa sababu ahadi ya MheshimiwaRais lazima itekelezwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilichukue jambohili tutaenda kulifanyia kazi haraka iwezekanavyo, kuangalianini tufanye ili kuhakikisha ile stendi inatengenezwa.(Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mwalongo swali lanyongeza.

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa NaibuSpika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, TARURA imepokea kazi hiziza barabara katika Halmashauri zetu, sasa katika masualahaya ya barabara katika Halmashauri tulikuwa tunakarabatibarabara hata katikati ya msimu, inaweza ikatokea mvuanyingi ikasomba barabara, Halmashauri ikatoa lori, wananchiwanashiriki kujenga ile barabara.

Je, katika kipindi hiki cha TARURA, wataendeleakufanya hiyo Kazi? Kwa sababu sasa TARURA haina malori,Halmashauri ina malori haina mafungu ya barabara, lakiniTARURA wana mafungu hawana malori. Hapa huu utaratibuwa kurekebisha hizi barabara utakuwaje? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, majibu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hili jambo walakwanza halina mashaka, kwa sababu jukumu hili sasa likochini ya TARURA. Lakini ufahamu siyo Halmashauri yako pekeyake, kuna Halmashauri mbalimbali wengine wana greda.Nafahamu magreda haya au malori haya sio kwambayatakuwa yanafanya kazi peke yake lakini inawezekana ni

Page 17: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

17

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

kitega uchumi cha kwenu ninyi kama Halmashauri. WakatiTARURA inafanya kazi yake, wakati inatekeleza kupitia Menejawa TARURA katika ngazi husika lazima kama utaratibu wakukodi malori utafanywa katika utaratibu ule usiokuwa nakikwazo. Kwa hiyo, kama mna malori yenu, mna magredayenu ambayo nanyi ni sehemu ya kitega uchumi kwenubarabara zitakapokuwa zinajengwa katika maeneo yalekama mtakuwa na utaratibu wa kukodisha jukumu kubwani kwamba TARURA itemize wakibu wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, MheshimiwaMwalongo naomba usihofu kila kitu kitaenda vizuri, ni kipindicha mpito tu kina mashaka kwa sababu ni jambo jipya lakinijambo hili litakuwa halina matatizo ya aina yoyote, tutafikamuda mtaona kila kinaenda vizuri katika Halmashauri zetu.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Pascal Haonga swali lanyongeza.

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika,tatizo la miundombinu ya barabara katika Mji Mdogo waRujewa linafanana kabisa na ubovu wa miundombinu yabarabara katika Mji Mdogo wa Mloo, Jimbo la Mbozi.

Je, nini ahadi ya Mheshimiwa Waziri kwa wananchiwa Mloo kuhusu miundombinu mibovu ya barabara ambayoni tatizo la muda mrefu sana?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, majibu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, MheshimiwaHaonga unapozungumza suala la Mloo nafahamu kwambachangamoto kubwa ya Wabunge wengi humu ni suala zimala miundombinu ya barabara katika Halmashauri zetu. Ndiyomaana nawashukuru sana katika Mpango ule wa bajetimwaka huu mmeona tumetenga bajeti kubwa karibuni yashilingi bilioni 263. Lengo kubwa ni kwamba barabara za vijijinizenye vikwazo na zile barabara nyingine tuweze kuzihudumia.

Page 18: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

18

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Kwa hiyo, naomba niseme kwamba katika eneo la kwakoulilozungumza na kwa sababu tumeshawaajiri watu tenatunawapa performance contract ya jinsi gani kila menejakatika Halmashauri anapoenda kule afanye kazi yake natutaipima na meneja atakaposhindwa ku-deliver maanayake hatokuwa na hiyo nafasi atapewa mtu mwingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ondoa hofu nikwamba tutakuwa katika mkakati wa kutofanya kazi tenakimazoea katika utaratibu wa sasa, na kwa sababu jambohili liliahidiwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi lazimatuwe na TARURA tutaenda kutekeleza kwa nguvu zote,naomba ondoa hofu katika eneo la Mloo tutalifanyia kaziharaka iwezekanavyo. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mipata swali la nyongeza.

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante sana kwa kunipa nafasi. Wakati wa kampeniMheshimiwa Rais alitembelea Namanyere na akatoa ahadikwamba akipita tutapata kilometa tano za barabara yalami. Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo amekuwa akilisemamara kwa mara lakini mpaka sasa halijatekelezwa.

Nataka kujua Serikali ina mpango gani kutekelezaahadi ya Mheshimiwa Rais?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, majibu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na hatanilipotembelea Namanyere Mheshimiwa Keissy alizungumzakatika mkutano nilipokuwa ninaongea na Watumishi kuhusuahadi hiyo sambamba na ahadi ya maji ambapo bwawalilikuwa linaendelea kujengwa.

Mheshimiwa Mipata kwa sababu nafahamu paleNamanyere ndiyo Makao yenu Makuu ya Mji kwa ahadi hii yaSerikali na sisi ametupa dhamana kuhudumu katika ofisi yake,

Page 19: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

19

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

tutafanya kila liwezekanalo katika kipindi hiki cha miakamitano, ahadi ya Mheshimiwa Rais kupitia TARURAtutaitekeleza, tutakapofika mwaka 2020 tusiwe nachangamoto nyingine yoyote katika suala la hiyo kilometatano Mheshimiwa Rais alizoziahidi. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendeleana Mheshimiwa Joseph Kizito Mhagama, Mbunge waMadaba sasa aulize swali lake.

Na. 55

Kuhusu Ukosefu wa Ardhi ya Kilimo Kijiji chaNgadinda Madaba

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza:-

Zaidi ya wananchi 181 wa kijij i cha NgadindaHalmashauri ya Madaba wanalima ndani ya Wilaya yaNamtumbo kwa sababu ya kukosa eneo katika kijiji chao.Baraza la Madiwani lilishauri sehemu ya shamba la hekta 6,000la Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi lililopo ndani ya kijijihicho ambalo lilikabidhiwa kwa Halmashauri ya Wilaya ililitumike kwa shughuli za kilimo na sehemu ibaki kwa ajili yamifugo. Hivi sasa wafugaji toka maeneo mbalimbali nchiniwapo katika shamba hilo lakini wakulima hawajatengewaeneo.

(a) Je, Serikali haioni kwamba kitendo hicho niubaguzi na kinaweza kuchochea migogoro kati ya wafugajina wakulima?

(b) Je, ni lini Serikali itasikiliza kilio cha muda mrefucha wananchi wa Ngadinda cha kutengewa eneo la kilimo?

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri waNchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali a

Page 20: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

20

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Mheshimiwa Joseph Kizito Mhagama, Mbunge wa Jimbo laMadaba, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya yaSongea mwaka 2014 iliunda Tume ya kuchunguza matumiziya shamba hilo ambalo lilikuwa linamilikiwa na Wizara yaKilimo, Mifugo na Uvuvi na kubaini kuwa shamba hilohalitumiki vizuri kwa shughuli za ufugaji. Kwa msingi huo Tumeilipendekeza hekta 4000 wapewe wananchi wa Kijiji chaNgadinda na eneo linalobaki la hekta 2000 libaki kwa shughuliza uwekezaji na ufugaji. Hata hivyo, baada ya Halmashauriya Wilaya ya Wilaya ya Songea kugawanywa na kupataHalmashauri mpya ya Wilaya ya Mababa uamuzi huohaukutekelezwa. Hivyo, Halmashauri ya Madaba inatakiwakujadili suala hili katika vikao vya Halmashauri na kufanyauamuzi kuhusu matumizi ya shamba hilo kwa kuzingatiamaslahi ya wakulima na wafugaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyoelezwa katikasehemu (a) ya jibula msingi, Halmashauri ndiyo yenye jukumula kujadili na kukubaliana kuhusu matumizi ya shamba hilolililokuwa linatumika kwa shughuli za ufugaji. Serikali itatoaushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha maslahi ya wakulimana wafugaji yanazingatiwa kuhusu matumizi ya shamba hilo.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Joseph Mhagama, swalila nyongeza.

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante kwa kunipa nafsi ya kuuliza maswali mawili yanyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile vikao halali vyaHalmashauri ya Wilaya ya Songea vilishamaliza jukumu lakihalmashauri kuhusu matumizi ya eneo hili la ardhi; na kwavile katika mazungumzo na ufuatiliaji Wizara ya Kilimowalishaelekeza kwamba sasa Mkoa ukabidhi sehemu yaeneo la shamba hilo kwa wananchi ili waweze kuendeleana shughuli za kil imo; na kwa vile msimu wa kil imoumekaribia sana na wananchi hawana sehemu ya kulima

Page 21: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

21

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

mazao ya chakula, na kwa vile wafugaji tayari wameanzakufuga katika eneo hilo.

Je, Serikali ipo tayari sasa kutoa maelekezo kwa Serikaliya Mkoa kuhusu kutekeleza jukumu hil i harakaiwezekanavyo?

Pil i, iwapo zoezi hil i l itaendelea kuchelewakutekelezwa, je, Serikali ipo radhi sasa kuruhusu wananchiwa Ngadinda na kwa vile mipaka inafahamika, kuiagizaSerikali ya kijiji iweze kuanza kushirikiana na wananchikuwatengea maeneo hayo waweze kuanza kuzalisha?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, majibu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanzanimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa hizo initiative zotewalizozifanya mpaka wamefikia hapo. Mimi nafahamukwamba kama hatua nyingi za msingi zimeshafanyikakikubwa zaidi ni sehemu yetu ya Mkoa. Nichukue fursa hiikuiagiza Ofisi ya Mkoa wa Ruvuma iangalie jinsi gani yakufanya kama mijadala yote imeshakamilika iende harakakurekebisha jambo hili ili wakulima na wafugaji tusiwe namgogoro tena katika eneo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunajua wazi kwambajambo hili likiwa na ukakasi wake mwisho wa siku tunakujakuzalisha matatizo makubwa sana ya uvunjivu wa amani.Kwa hiyo, nitumie fursa hii kuiagiza timu ya Mkoa wetu waRuvuma iende ikalifanyie kazi jambo hilo harakaiwezekanavyo na ikiwezekana mpaka mwezi wa Kumijambo hilo liwe limekamilika na ofisi yetu ya TAMISEMI tupatetaarifa ya jinsi gani jambo hilo limekamilishwa kwa sababuvikao vyote halali kwa taarifa niliyoipata kutoka kwa Mbungezimeshakamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili kwambakukiruhusu kijiji kwenda kuhakikisha kwamba wanaenda

Page 22: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

22

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

kugawa hilo eneo, naomba tuvute subira kwanza, timu yaMkoa ifanye kazi yake vizuri baadaye tukishapata taarifatutajua nini kifanyike. Lengo kubwa kama unavyowapiganiawananchi wako Serikali itaingilia kati kwa nguvu zote sisitukishirikiana na Wizara ya Kilimo tutafanya kila liwezekanaloeneo lile liwe katika utaratibu mzuri, wananchi wa eneo lilewaweze kupata ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ondoa hofuMheshimiwa Mbunge tunalifanyia kazi jambo hili.(Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mama Anne KilangoMalecela.

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika,nashukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu wananchi waMadaba wameonesha kuhamasika sana kulima tangawizi,hata mimi ninalima tangawizi Madaba. Je, Serikali haionikwamba kiwanda cha Mamba Miamba ambacho kitakuwatayari by March next year, kitahitaji tangawizi nyingi sana siyokutoka Same tu pamoja na Madaba.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapatia wananchiwa Madaba ardhi ya uhakika ili walime tangawizi kwa wingi?(Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, majibu kwa kifupi.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naombatuchukue kilio cha mama vilevile kama kilio cha MheshimiwaJoseph Mhagama. Serikali inaona umuhimu huo na tutafanyakila liwezekanalo kuhakikisha mambo pale yanakaasawasawa wananchi walime tangawizi waje, kulisha katikakiwanda cha Mama Anne Kilango Malecela. (Makofi)

Page 23: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

23

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Mheshimiwa MbarakaKitwana Dau.

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika,ninakushukuru kwa fursa hii.

Tatizo la mgogoro wa shamba la Madaba linafananasana na tatizo la shamba la Kigomani na Utumaini lililopoWilayani Mafia.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kujaMafia kukaa na wadau wa Halmashauri pamoja na Viongoziwengine kutatua tatizo hilo?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, majibu.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanzanimshukuru Mheshimiwa Mbunge na lile deni letu tumeshatoashilingi milioni 50 tumemaliza kituo cha afya, hongera sanaMheshimiwa Mbunge kwa ujenzi wa theatre. Hata hivyo,katika jambo hili mimi naomba nilichukue, lakini kabla mimisijaja kule nimuagize Mkuu wa Wilaya ya Mafia kwanza aendeakalishughulikie jambo hili na ikiwezekana tupate taarifaamelishughulikia vipi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitakapopata hiyo taarifajinsi gani limeshughulikiwa jambo hili na mgogoro huohaukuisha, na mimi nitaona jinsi gani ya kufanya, lakinikwamba nitatumia vyombo vyangu vya chini kule kwanza,Mkuu wa Wilaya ya Mafia aanze kuifanya kazi hiyo harkaiwezekanavyo kumaliza hilo tatizo na ofisi yetu ipate taarifandani ya mwezi mmoja, j insi gani mgogoro huoumeshughulikiwa kwa kadiri iwezekanavyo. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendeleana Wizara ya Fedha na Mipango, Mheshimiwa JaphetNgailonga Hasunga, Mbunge wa Vwawa, sasa aulize swalilake.

Page 24: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

24

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Na. 56

Kushuka kwa Thamani ya Shilingi ya Tanzania

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:-

Kushuka kwa thamani ya shil ingi ya Tanzaniakumetokana na kuruhusu kutoza bidhaa mbalimbali nahuduma kwa dola na kuathiri thamani ya fedha yetu.

Je, Serikali inachukua hatua gani za kuimarisha shilingiyetu na kupiga marufuku matumizi ya fedha za kigeni nchini?

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri waFedha na Mipango, napenda kujibu swali la MheshimiwaJaphet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwawa, kamaifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kushuka au kupanda kwathamani ya shil ingi hakutokani na kuruhusu bidhaambalimbali na huduma kutozwa kwa dola, bali hutokanana misingi ya shughuli mbalimbali za kiuchumi (MicroEconomic Fundamentals) na hali halisi ya uchumi wa nchitunazofanyanazo biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kushuka au kupanda kwathamani ya shilingi kunaweza kusababishwa na mambomakuu yafuatayo:-

(i) Nakisi ya urari wa biashara; nakisi ya urari wabiashara ya nje ya nchi (balance of payments) husababishasarafu kushuka thamani kama mauzo ya bidhaa nje ya nchini madogo ikilinganishwa na ununuzi wa bidhaa kutoka nje.hali hiyo, hufanya thamani ya shilingi kushuka kwa sababumahitaji yetu ya fedha za kigeni ni makubwa kuliko mapatoya mauzo yetu nje ya nchi.

(ii) Mfumuko wa bei; pamoja na mambo mengine

Page 25: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

25

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

mfumuko wa bei husababishwa na ongezeko kubwa la ujazowa fedha kuliko uzalishaji wa bidhaa na huduma mbalimbalikatika nchi. Aidha, thamani ya fedha hupungua iwapomfumuko wa bei wa ndani ni mkubwa kuliko mfumuko wabei katika nchi tunazofanyanazo biashara ni za nje ya nchi.

(iii) Tofauti ya misimu (seasonal factors); upatikanajiwa fedha za kigeni kutokana na biashara za msimuhusababisha kusesereka au kutoserereka kwa shilingi yaTanzania. Kwa mfano, mapato mengi ya fedha za kigenikutikana na biashara ya nje huongezeka wakati wa nusu yapili ya kila mwaka yaani kati ya Julai na Disemba, ikiwa nikipindi cha mavuno na kilele cha utalii hivyo, thamani yashilingi huimarika au kuwa na utulivu zaidi katika kipindi katiya Julai na Disemba.

Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu zinaonesha kuwapamoja na kuwepo kwa sheria ya kutotumia kabisa fedhaza kigeni nchini Afrika ya Kusini, lakini sarafu ya nchi hiyoimapatwa na misukosuko mikubwa zaidi ya shilingi yaTanzania. Hata thamani ya sarafu nyingine kubwa dunianikama vile Yen ya Japan, Renminbi ya China na Euro zimekuwazikiyumba kwa kasi zaidi ya shilingi ya Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuimarisha thamani yashilingi Benki Kuu inaendelea kudhibiti mfumuko wa bei, iliusitofautiane sana na wabia wetu wa biashara. Pia BenkiKuu imedhibiti biashara ya maoteo (speculation) katika sokola fedha za kigeni, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwamiamala ya fedha za kigeni inayofanywa na benki kwa ajiliya shughuli za kiuchumi tu na sio biashara ya maoteo. Halihii itasaidia upatikanaji wa fedha za kigeni katika soko larejareja na hivyo kupunguza shinikizo la kuporomoka kwathamani ya shilingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vema ikaeleweka kuwapamoja na hatua zil izochukuliwa na zinazoendeleakuchukuliwa na Benki Kuu, ufumbuzi wa kudumu wakutengemaa kwa thamani ya shilingi hutegemea zaidikupungua kwa nakisi ya urari wa biashara ya bidhaa, huduma

Page 26: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

26

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

na uhamisho wa mali nchi za nje. Hii itawezekana tu endapotutaongeza uzalishaji na kuwa na ziada ya kuongeza mauzoyetu nje ya nchi na pia kupunguza uagizaji wa bidhaa nahuduma zisizo za msingi kutoka nje.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Japhet Hasunga, swali lanyongeza.

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika,kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa NaibuWaziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, mpaka sasa hivi kuna baadhi yamakampuni ya watu binafsi na wafanyabiasharawanaendelea kutoza na kupanga bei kwa kutumia dolabadala ya Tanzanian shillings.

Je, Serikali haioni hiyo inaidhalilisha shilingi yetu nakuonesha kwamba, hawana imani na shilingi ya Tanzania?

Swali la pili, kwa kuwa moja ya eneo ambalo linatumiafedha nyingi sana na kusababisha kutokuwepo kwa urarimzuri wa nchi ni uagizaji wa vyakula mbalimbali kutoka njeya nchi wakati vyakula hivyo vinaweza kuzalishwa ndani yanchi, maeneo kama mafuta ya kula, sukari na mazaomengine ambayo yanaweza kuzalishwa hapa nchini. Kwamwaka tunatumia zaidi ya shilingi trilioni 2.8 kwa ajili yakuagiza mazao yanayotokana na vyakula vinavyowezakuzalishwa hapa na kutoa ajira kwa wananchi.

Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuzuia uagizajiwa baadhi ya vyakula kutoka nje ya nchi ili kuinua ualishajiwa ndani ya nchi na kuokoa shilingi? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa NaibU Waziri wa Fedha naMipango, majibu.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: MheshimiwaNaibu Spika, swali lake la kwanza kwamba katika watuambao wanaweka bei kwa kutumia dola wanaidhalilisha

Page 27: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

27

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

shilingi yetu, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba,tulipitisha sheria katika Bunge lako Tukufu kwamba siyo kosakuweza kuweka bei kwa currency ambayo siyo ya Tanzania,kosa ni ni kukataa pesa shilingi ya Tanzania pale ambapomteja anataka kulipa na yule mwenye duka akakataakupokea hilo ndio kosa, lakini siyo kosa katika kuweka beihiyo kwa currency ambayo sio shilingi yetu ya Tanzania, kamaTaifa tuliona inafaa na ndiyo maana tunaendelea kutekelezasheria hii tuliyopitisha mwaka 1992.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuzuia ku-importbidhaa ambazo zinazalishwa hapa nchini. Napenda kulijibuBunge lako Tukufu kwamba, ndiyo maana Serikali ya Awamuya Tano inasisitiza kwamba uchumi wa viwanda ili tuwezekuzalisha bidhaa zetu za kutosheleza ndani ya nchi yetu.Tutakapokuwa tumeweza kuzalisha bidhaa hizi kwa kiwangoambacho kinatosheleza hatuna sababu ya kuendelea ku-import na tutaweza kurekebisha sheria zetu ili tuweze sasakutumia bidhaa zetu, lakini kusema sasa tupige marufukuwakati bado kuna uhitaji wa bidhaa hizi, haitakuwa sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuendelee kuiunga mkonoSerikali yetu katika kuiendea Tanzania ya Viwanda, tunauhakika ndani ya miaka mitano mpaka kumi tutakuwatumeweza kujitosheleza kwa bidhaa zetu ndani ya Tanzania.(Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kangi Lugola, swali lanyongeza.

MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante sana.

Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwa kinywa chakekatika majibu yake ya msingi kwamba, kushuka au kupandakwa thamani ya shilingi yetu hakuna uhusiano na utozaji wabidhaa au huduma kwa dola.

Je, anataka kuwaaminisha wachumi wote Tanzaniana duniani kote na Bunge hili kwamba hata miaka mitano

Page 28: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

28

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

tukiamua kutumia dola tu bila kutumia shilingi na baadayetukairejea baada ya miaka mitano tutakuta uchumi wetuhaujaathirika na wala shilingi yetu haijaathirika?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha naMipango, majibu.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: MheshimiwaNaibu Spika, si kuwaaminisha Wachumi, kama nilivyosemanimeeleza sababu ya kushuka kwa thamani ya currencyyoyote ile hata kama sio shilingi ya Tanzania. Kuwekaquotation kwa bei ambayo siyo shilingi ya Tanzania si sababumahsusi, lakini naomba kumwambia Mheshimiwa KangiLugola kwamba ni asilimia 0.1 tu ya watu ambao wanawekaquotation kwa bei ambayo sio shilingi ya Tanzania ambaowako tayari kupokea fedha hii kwa kutumia currency ilewaliyo-quote. Zaidi ya asilimia 99.9 ya Watanzania nawafanyabiashara wanaoweka quotation kwa pesa ambayosio T-Shillings wako tayari kupokea bei yao na kuuza bidhaazao na kupokea shilingi ya Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Kangi Lugolakama nilivyosema ziko indicators. Viko viashiria mbalimbalivinavyosababisha kushuka kwa uchumi na hatuna sababuya kusema kwamba tuweze kuweka miaka mitano tufanyequotation na tusitumie shilingi yetu ya Tanzania. Nimesemakupitia Sheria ya Benki Kuu ya mwaka 2006, Kifungu cha 26 nishilingi ya Tanzania ndiyo legal tender document ambayoinaruhusiwa ndani ya Taifa letu. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Hussein Mohamed Bashe,swali la nyongeza.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa NaibuWaziri, ninauliza swali moja la nyongeza.

Kutokana na ripoti ya BOT latest ya mwezi Juni,inaonesha kwamba export volume yetu imeshuka kutokadola milioni 4.5 mpaka dola milioni 3.8 wakati huo huo prices

Page 29: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

29

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

za commodities kwenye soko la dunia imeendelea kushukana import volume yetu ya capital goods imeendelea kushuka.

Je, Serikali ina mpango gani kutokana na variableshizi zote nilizozitaja kuhakikisha kwamba, miezi mitatu mpakasita ijayo stability ya shilingi yetu inaendelea kuwa imara kwasababu indications zote zinaonesha kwamba, shilingi yetuinaendelea kushuka kila siku kutokana na hali ya uchumi nauzalishaji?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha naMipango, majibu.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: MheshimiwaNaibu Spika, kama ambavyo amesema ni kweli kwambaexport volume yetu imeshuka, na mimi katika jibu langu lamsingi nimesema katika miezi ambayo Taifa letu huwalinapanda katika exportation ni kuanzia Julai mpakaDisemba na ndio kipindi hiki. Kwa hiyo, nimuombe tuMheshimiwa Bashe kwamba ndani ya kipindi hiki kwa sababundio tunazalisha na tunavuna export yetu itapanda mudasiyo mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimesema kwenye jibulangu la msingi kwamba tuendelee kuiunga dhamira yaSerikali yetu, Tanzania ya Viwanda ndiyo itakayotuwezeshakuongeza export volume yetu na kuweza kupunguzaimportation ya bidhaa ambazo tutazizalisha ndani ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe WaheshimiwaWabunge tuendelee kumuunga Mheshimiwa Rais wetukatika dhamira yake hii na sisi kama wasaidizi wake tukoimara katika kumsaidia kuhakikisha kwamba, thamani yashilingi yetu inaendelea kuimarika na export volume kulinganana viwanda ambavyo tayari sasa vimeanza kufanya kazi,itaongezeka muda siyo mrefu. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndaniya Nchi.

Page 30: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

30

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: MheshimiwaNaibu Spika, nampongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri,lakini nilitaka nimpe Taarifa tu Mheshimiwa Hussein Bashekwamba, katika record za hivi karibuni nchi yetu ina reservenyingi na ina over five months of imports kutokana nacredibility ya Government Policy. Kwa maana hiyo, kushukakwa imports wala hakujaathiri sana matarajio ya kuharibikakwa ustahimilivu wa mfumuko wa bei kutokana na kwamba,Serikali ina reserve nyingi za kutosha na kwa maana hiyoexport zitakapokuwa zimeongezeka zitakutana na reserveza kutosha ambazo hazitaleta uharibifu wowote kwenyembadilishano wa fedha pamoja na mfumuko wa bei.(Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendeleana Mheshimiwa Dkt. Mathayo David Mathayo, Mbunge waSame Magharibi, sasa aulize swali lake.

Na. 57

Kuongeza Ukwasi Kwenye Benki kwa Wananchi

MHE. MATHAYO D. MATHAYO aliuliza:-

Je, Serikali ina mikakati gani ya kuongeza ukwasikatika benki na kwa wananchi wa kawaida ili washirikianena Serikali katika kujenga uchumi wa mtu mmoja mmoja,kaya na taifa kwa ujumla?

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri waFedha na Mipango, napenda kujibu swali la MheshimiwaMathayo David Mathayo, Mbunge wa Same Magharibi, kamaifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kufikia malengo ya Serikaliya kuimarisha uchumi na kudumisha utulivu wa mfumukowa bei, Benki Kuu hutekeleza Sera ya Fedha inayolengakudhibiti ukwasi ili uendane na mahitaji halisi ya uchumi. Kati

Page 31: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

31

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

ya Julai, 2016 na Julai, 2017 kiwango cha ukwasi katikamabenki kwa ujumla wake kiliongezeka kutoka asilimia 35.53hadi asilimia 38.41 kwa mtiririko huo. Kiwango cha ukwasiwa asilimia 38.41 ni kizuri zaidi katika uchumi ikilinganishwana kiwango cha chini cha asilimia 20 kinachotakiwa na BenkiKuu ya Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuimarika kwa ukwasi kwamwaka 2017 kunatokana na hatua mbalimbali za kiserazinazochukuliwa na Benki Kuu. Miongoni mwa hatua hizo nikutoa mikopo ya muda mfupi kwa mabenki, kununua fedhaza kigeni katika soko la jumla la fedha za kigeni (InterbankForeign Exchange Market) na kushusha riba inayotozwa kwabenki za biashara na Serikali wanapokopa Benki Kuu kutokaasilimia 16 hadi asilimia 12 mwezi Machi, 2017 na kutokaasilimia 12 hadi asilimia tisa mwezi Agosti, 2017.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua nyingineiliyochukuliwa na Benki Kuu ni pamoja na kushusha kiwangocha sehemu ya amana ambayo mabenki yanatakiwakuhifadhi Benki Kuu kutoka asilimia 10 hadi asilimia Nane (8)kuanzia mwezi Aprili, 2017.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na hatuambalimbali zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwana Benki Kuu, hali ya ukwasi katika sekta ya fedha, hususanbenki ni nzuri na hakuna vihatarishi vya kuleta madhara hasikatika uchumi wetu. Aidha, Benki Kuu itaendelea kuchukuahatua mbalimbali za kuimarisha masoko ya fedha kwa lengola kuhakikisha kwamba, yanaendeshwa kwa ufanisi naushindani na hivyo kusaidia kuongeza ukwasi miongoni mwamabenki na taasisi nyingine za kifedha.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Mathayo Mathayoswali la nyongeza.

MHE. MATHAYO D. MATHAYO: Mheshimiwa NaibuSpika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii kuuliza swalila nyongeza.

Page 32: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

32

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Aidha, napenda kumpongeza Naibu Waziri kwakujibu maswali yake vizuri na kitaalam. Nina maswalimadogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Benki Kuuimepunguza riba ya mabenki ya biashara yanapokopakutoka kwenye Benki Kuu hadi kufikia asilimia tisa na kwakuwa pia, imepunguza amana kutoka asilimia kumi hadiasilimia nane ya kiwango cha fedha ambazo mabenki hayaya biashara yanatakiwa yahifadhi Benki Kuu. Je, Benki Kuuimefuatilia na kuona kwamba, mabenki ya biasharayanatoza riba nzuri au yametoa punguzo zuri la riba kwawananchi ambao wanakopa kwenye mabenki hayo?

Swali la pili, kwa kuwa katika nchi zinazoendeleaasilimia 70 ya fedha zinakuwa mikononi mwa wananchi naasilimia 30 inakuwa kwenye mabenki pamoja na Serikali. Je,Benki Kuu imefanya utafiti na kuona, kwa sababu sasa hivitukiangalia fedha katika mzunguko kwa wananchi wakawaida zimepungua sana.

Je, Benki Kuu imefanya utafiti na kujua kwamba, fedhahizi ziko wapi ili waweze kutunga Sera ambazo zitarudishafedha hizi kwenye mabenki ya biashara pamoja na wananchiili maisha yaweze kuwa mazuri, lakini wananchi pia washirikivizuri katika shughuli za kujenga nchi yao? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha naMipango, majibu.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: MheshimiwaNaibu Spika, ni kweli tumeshusha kama nilivyosema kwenyejibu langu la msingi na kwa sasa tunafanya ufuatiliaji kuonakwamba, riba zinazotozwa na benki zetu za biasharapamoja na taasisi za kifedha zinashuka ku-respond katikajitihada hizi ambazo zimefanywa na Serikali kupitia Benki Kuu.Tutakapomaliza ufuatiliaji huu na sasa hivi tuko katika vikaombalimbali na mabenki haya kuona ni jinsi gani sasawanaweza kurejesha riba chini ili wananchi wetu wawezekukopa, tutaleta taarifa katika Bunge lako Tukufu.

Page 33: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

33

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili,napenda kumwambia Mheshimiwa Mathayo kuwa ni sahihikwamba asilimia 30 tu ya pesa ndiyo iko benki, asilimia 70 ikokwa wananchi. Kinachoonekana kwa sasa ni kwamba Serikalitumeimarisha mfumo wetu wa ukusanyaji wa kodi. Yulemfanyabiashara aliyekuwa akifanya biashara bila kulipa kodiakijidanganya ile ni faida yake, sivyo ilivyo kwa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba WaheshimiwaWabunge mtuunge mkono tuweze kukusanya kodiinavyostahiki na ili Watanzania sasa tuishi katika uchumiambao Taifa letu na wananchi wanastahili kuishi. Kiuhalisiafedha bado iko ya kutosha katika mikono ya wananchi kamaalivyokiri yeye Mheshimwa Mbunge aliyeuliza swali kwambaasilimia sabini ya pesa yetu iko kwa wananchi na uchumiwetu unaendelea vizuri.

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, aah,sikuwaona mmesimama mwanzo naona sasa hivimmesimama wote kwa kasi. Mheshimiwa Mwakajoka, swalila nyongeza.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa NaibuSpika, ahsante. Kumekuwa na tafsiri ambayo siyo sahihi sanakwa vijana ambao wananunua Kwacha kwenye mpaka waTunduma na Zambia ambapo fedha hizo, Wazambiawanapokuwa wamekuja kununua bidhaa kwenye Mji waTunduma wanakuja na Kwacha na baadaye vijanawananunua zile Kwacha na Serikali imekuwa ikisemakwamba vijana wale hawalipi kodi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kununua zileKwacha, wanakwenda Lusaka kununua dola na baada yakununua zile dola wanakuja ku-change kwenye benki zetuza Tanzania. Hawa wafanyabiashara wa Kwacha wanakuwatayari wamelipa kodi.

Je, Serikali haioni kwamba nao pia ni walipa kodikatika Taifa hili na badala yake wanaendelea kuwasumbua?Wataacha lini? Ahsante.

Page 34: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

34

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri naona upotayari kujibu japokuwa swali siyo la nyongeza hilo, naona niswali la msingi, tofauti kabisa. Mheshimiwa Naibu Waziri waFedha na Mipango.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: MheshimiwaNaibu Spika, katika mipaka ambayo kuna black market yakutisha ndani ya Taifa letu ni mpaka alioutaja wa Tundumana ndiyo maana wiki iliyopita Mheshimiwa Waziri wa Fedhaalikuwa mpakani kule na sasa tumeimarisha na tutahakikishaMheshimiwa Mwakajoka tunakusanya kodi yote. Hawawezikutoa Kwacha huku wakaenda kuibadilisha na wakarudinchini bila kukusanya kodi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeapa kulinda nakuweza kukusanya kodi yetu, tutaikusanya kodi hii kwa kilamtu anayefanya biashara hii. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Shally Raymond, swali fupila nyongeza.

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika,nakushukuru sana. Kwa kuwa uhusiano wa benki na mtu wakawaida ambaye hafanyi biashara, ni kuweka hela yake iliapate faida na pia kwa usalama; na sasa hivi tunashuhudiakwamba hata mitandao ya simu mtu unaweza ukawekezahela yako. Ni lini sasa benki hizi zitakaa chini na kuonakwamba kuna umuhimu wa kuongeza faida (interest rate)kwa wale wanaoweka hela zao kwenye savings account?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha naMipango, majibu.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: MheshimiwaNaibu Spika, kama ambavyo nimekuwa nikisema tangumwaka 1991 nchi yetu iliingia katika soko huru katika masualaya kifedha nchini na interests zinazopangwa na mabenki yetukatika savings accont huwa zinawekwa kulingana na uhalisiawa soko. Ina maana faida inapatikana kwa mabenki na kwawananchi. Kwa kumbukumbu ambazo tunazo Wizara ya

Page 35: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

35

Fedha na Mipango, interest hii imekuwa ikiongezeka mwakahadi mwaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe angalizo kwa mabenkiyetu kuangalia kwamba wana balance interest wanayotozawaone interest wanayowapa wananchi kwa kuweka pesahizi katika akaunti zao hasa savings account.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina uhakika katika hilimabenki yetu yanafanya kazi vizuri kuhakikisha waowanapata na wateja wao ambao ni wananchi wanapatavizuri kwa kuwa tupo katika soko huria na wanapambanakuweza kupata wateja kuweka pesa katika benki zao.

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendeleana Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa MaryamSalum Msabaha, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swalilake.

Na. 58

Uuzwaji wa Silaha Kiholela Nchini

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA aliuliza:-

Kumekuwa na uuzwaji wa silaha kiholela kama vilemapanga na visu katika barabara zetu ikiwemo Ubungokwenye mataa hali ambayo inaleta hofu kwa raia wema.

Je, Serikali inalichukuliaje suala hilo ambalo ni hatarisana kwa usalama wa raia?

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri waMambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali laMheshimiwa Maryam Salum Msabaha, Mbunge wa VitiMaalum, kama ifuatavyo:-

Page 36: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

36

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kumekuwepo nauuzaji holela wa silaha za jadi katika maeneo mbalimbali yabarabara zetu ikiwemo katika makutano ya barabara yaMandela na Morogoro eneo la Ubungo, Jijini Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisiinatambua uwepo wa tatizo hilo na tayari hatua mbalimbaliza kudhibiti hali hiyo zimechukuliwa ikiwa ni pamoja nakufanya operesheni za mara kwa mara na kukamata wauzajiwa silaha za jadi barabarani kama vile mapanga, mikuki,upinde na mishale. Aidha, elimu inaendelea kutolewa kwawafanyabiashara wa bidhaa za silaha hizokutowapatia wauzaji wasio na eneo maalum la kufanyiabiashara hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi kwakushirikiana na mamlaka nyingine za Serikali linaandaautaratibu maalum wa uuzaji wa bidhaa za aina hii na kutoaelimu kwa umma kuhusu madhara ya biashara hii nakuwashauri wananchi waipige vita na kuepuka kujihusishanayo.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Maryam Msabaha, swali lanyongeza.

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa NaibuSpika, ahsante. Naomba kumuuliza Naibu Waziri maswalimawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania imekuwa kisiwacha amani, lakini kuna genge la wahuni ambalo hatujuiwanapata wapi silaha za kijeshi na kushambulia raiawasiokuwa na hatia.

Je, Serikali haioni sasa imefika wakati muafakakufanya doria katika sehemu zote za mipaka na barabaranina hata katika vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikishagenge hili halina nguvu kwa sababu linachafua taswira yaTanzania katika medali za kitaifa? (Makofi)

Page 37: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

37

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa badosilaha hizi zinaendelea kuuzwa sehemu za starehe kama vileminadani na sehemu mbalimbali na kuhatarisha amani yaambao wanafika katika kupata huduma katika sehemu hizo.

Je, Serikali ina mikakati gani ya ziada kuhakikisha sualahil i kuuza silaha holela linakomeshwa na walewanaokamatwa wachukuliwe sheria kali ili suala hili likomemara moja? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mamboya Ndani ya Nchi, majibu.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni bahati mbaya sanaMheshimiwa Mbunge hajalitaja jina la kundi ambaloamelizungumza, lakini kimsingi nataka nimueleze tu kwaufupi kwamba hali ya matumizi ya silaha kufanya uhalifunchini imepungua, ndiyo maana hata ukiangalia takwimutokea Juni, 2016 mpaka Agosti, 2017, hakuna matukiomakubwa ya mauaji ya kutumia silaha za jadi nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, utaona ni kazikubwa ambayo Serikali imefanya kupitia Jeshi la Polisi kuwezakudhibiti wahalifu na magenge mbalimbali ambayoyamekuwa yakitumia silaha hizo za jadi kwa ajili ya kufanyauhalifu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba mafaniko hayoyamepatikana kwa sababu gani? Kuna mikakati mingiambayo imefanyika ili kuweza kufikia malengo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tumeendelea kutoaelimu kwa Umma kuhusiana na makundi ambayo yamekuwayakijitokeza, kwa mfano, maeneo ya Kanda ya Ziwa kunawatu walikuwa wanaitwa wakata mapanga, ukija hukuMbeya na kadhalika, wapo watu ambao walikuwawanafanya mauaji kwa vikongwe kwa imani za kishirikina.Kwa hiyo, Jeshi la Polisi kwa kupitia utaratibu wake wa ulinzishirikishi tumekuwa tukifanya jitihada kubwa sana za kutoa

Page 38: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

38

elimu kwa jamii ili kufahamu madhara ya matumizi ya silahaza jadi, hasa matumizi ya kujichukulia sheria mkononi kwajamii, hilo moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, l ingine, tumekuwatukiendelea kufanya doria na ukaguzi barabarani kuwezakusimamisha magari na watu ambao wakipita na silaha hizoza jadi na kuwakamata na kuwachukulia hatua za kisheria.Hii doria imekuwa ikiendelea na ndiyo maana mpaka sasahivi tumeweza kufanikiwa kwa mujibu wa takwimu ambazonimezieleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tumeendeleakuhakikisha kwamba huduma zetu za Jeshi la Polisi zinashukakatika ngazi ya Tarafa na Kata. Tuna Ofisi za Ukaguzi katikangazi ya Tarafa na Kata ili kusogeza huduma ya Polisi karibuna wananchi kuweza kukabiliana na matukio mbalimbali yauhalifu ya aina kama hii ambayo Mheshimiwa Mbungeamezungumza. Kwa hiyo, nikiri tu kwamba kwa jumla kazikubwa imefanyika na mafanikio yake mpaka sasa hivi ndiyohaya ambayo nimeyaeleza, ni makubwa ya kuridhisha kwakiasi fulani.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Yussuf, swali fupi.

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika,nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Watanzania wengi niwakulima, wafugaji na wavuvi. Kwa mantiki hiyo, kisu napanga ni kitendea kazi muhimu na adhimu kwa kukamilishakazi zao. Kama ni misuse, hata tai inaweza kutoa maisha yamtu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nini tafsiri sahihi ya nenosilaha? Naomba majibu.

NAIBU SPIKA: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,majibu.

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: MheshimiwaNaibu Spika, tafsiri ya silaha tunaitafsiri kufuatana na mazingira

Page 39: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

39

inapotumika. Kama mtu amebeba fimbo na anachunga,tunaelewa kwamba mazingira ya anakochunga anastahilikuwa na fimbo hiyo. Leo hii kama mtu anaingia Bungeni naamebeba kisu, ile inageuka kuwa silaha ambayo iko katikamatumizi ambapo haitakiwi kuwa na huyo mtu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo hivyo, kama mtuanaenda kuangalia mpira (Ndondo Cup), hata kama kwenyeutamaduni wake anatakiwa kuwa na mkuki, hatutarajiiaende nao kwenye uwanja wa michezo, tunatarajia aendenao anakochunga ambako anaweza akakutana labda nawanyama wakali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maana hiyo, hatauholela tunaoungelea kama ambavyo silaha zote zinautaratibu wa maeneo ambapo zinatakiwa kuuzwa,tunatarajia pia hata kwenye matumizi ziwe katika mazingirayanapotakiwa kutumika. Hatuwezi tukaruhusu Watanzaniakila mmoja akawa anatembea na silaha popote anapojisikiakuwa nayo kwa sababu udhibiti wake utakuwa ni hatari kwanamna ya kuweza kuhakikisha wale wasiopenda au wasiona silaha wanaweza wakapata athari popote pale ambapomwenye silaha anaweza akaamua kuitumia. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Waheshimiwa Wabungetunaendelea na Wizara ya Maji na Umwagiliaji. MheshimiwaOliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, swali lakelitaulizwa kwa niaba na Mheshimiwa Alex Raphael Gashaza.

Na. 59

Mamlaka ya Mji – Ngara

MHE. ALEX R. GASHAZA (K.n.y. MHE. OLIVER D.SEMUGURUKA) aliuliza:-

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara kuna matatizomakubwa sana ya maji kiasi kwamba wananchi wa maeneohayo wanaona kuwa kupata maji ya bomba ni kama ndotoisiyowezekana na wamekuwa wakilipishwa gharama ya maji

Page 40: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

40

hata kwa wateja ambao hawapati kabisa huduma ya majikwa kipindi cha mwezi husika ikiambatana na shilingi 1,500kila mwezi kwa ajili ya mita ya maji.

(a) Je, Serikali inakubaliana na tozo ya shilingi 1,500ya lazima kwa malipo ya mita?

(b) Je, Serikali inawaambia nini wananchiwanaotozwa bili za maji wakiwa hawajapata huduma yamaji?

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali laMheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa VitiMaalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika uendeshaji wamamlaka na utoaji bora wa huduma ya maji, tozo ya shilingi1,500 ilipitishwa na EWURA mwaka 2011 kwa mchanganuoufuatao:-

(i) Shilingi 500 service charge; na

(ii) Shilingi 1,000 meter rent.

Mheshimiwa Naibu Spika, tozo hii iliendana na bei yamaji inayotumika hadi sasa. Kutokana na tarrifs mpya zaEWURA ambazo zimeondoa tozo hiyo kwa sasa Mamlaka yaMaji Mjini Ngara inaandaa andiko la mpango wa biashara(business plan) litakalowasilishwa EWURA kwa ajili ya mapitioya bili hiyo na kupata bili mpya ya maji inayoendana nawakati uliopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na malalamikoyaliyopo kuhusu baadhi ya wananchi kupelekewa ankarawakati hawapati huduma ya maji, Wizara itafuatilia kwa kinakujua kama ni kweli tatizo hilo lipo na endapo itabainikahatua stahiki zitachukuliwa.

Page 41: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

41

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Alex Gashaza, swali lanyongeza.

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika,namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri.Sambamba na hilo naomba kuuliza maswali mawili yanyongeza kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Ngara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwepo na miradi yavijiji kumi ambayo imechukua muda mrefu bila kukamilika.Kwa mfano, mradi wa Kijiji cha Mbuba, Munjegwe, Kanazi,Kabarenzi na Mkibogoye, je, ni lini miradi hii itakamilika?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, nichukue nafasihii kwanza kumpongeza Mheshimiwa Waziri, kwambatumepata shilingi milioni 24 kwa ajili ya pampu ya K9, lakinikwa namna ya kipekee nampongeza Mheshimiwa Rais waJamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 20 alipokuwaNgara alitupatia shilingi milioni 13 kwa ajili ya kununua pampuya maji ili kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Ngara.Imeshafungwa na maboresho yamefanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na ahadi yakeni pamoja na kuanzisha mradi ambao unaweza ukawasuluhisho kwa Vijiji vyote vya Wilaya ya Ngara na Wilaya yajirani kwa kutumia mradi wa vyanzo vya maji, Mto Kagera,Mto Luvubu na Mlima Shunga na akaahidi kwamba ataagizaWaziri na watendaji kufika kwa ajili ya kuangalia namna yakufanya usanifu wa mradi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Waziri na timu yake yawataalam yupo tayari baada ya Bunge hili kuambatana namikwenda Ngara ili kuona uwezekano wa kusanifu mradi huuambao utakuwa ni suluhisho kwa vijiji vyote vya Wilaya yaNgara na Wilaya jirani? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Maji naUmwagiliaji, majibu.

Page 42: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

42

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: MheshimiwaNaibu Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwakufuatilia huduma ya maji katika Wilaya yake ya Ngara nahasa Mji wa Ngara ambapo Mheshimiwa Rais alipatembeleana akaweza kutoa fedha za kutengneza pampu ili wananchiwa pale waweze kupata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika maswali yake yanyongeza, Mheshimiwa Mbunge ameulizia baadhi ya Vijijiambavyo anasema havijakamilika. Nitoe tu taarifa kwambaSerikali imetenga shilingi 1,500,000,000 katika bajeti yake yamwaka 2017/2018 kwa maana ya kuendelea kukamilishamiradi hiyo inayoendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kama nipotayari kwenda naye Ngara, mimi nipo tayari na nimepangabaada ya Bunge hili nitakwenda Ngara kuangalia hudumaya maji katika Mkoa mzima wa Kagera. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Martha Mlata, swali lanyongeza.

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Natambua kwamba tatizo la uhaba wa majilinawakumba sana wanawake wote Tanzania. Nilikuwanaomba Mheshimiwa atusaidie hasa kwenye Mkoa wetu waSingida, hakuna mradi wowote mkubwa wa maji ambaoumeanzishwa kwa ajili ya kuokoa tatizo la maji katika Mkoawa Singida.

Je, ni l ini sasa Serikali itaenda kuwakomboawanawake wa Mkoa wa Singida kwa tatizo la maji? Ahsante.(Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Maji naUmwagiliaji, majibu.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: MheshimiwaNaibu Spika, ni kweli watu wanaopata adha kubwa katikasuala la maji hasa vijijini ni akina mama na Serikali inatambua

Page 43: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

43

jambo hilo na ndiyo maana katika mwaka huu wa fedha2017/2018 tumetenga shilingi bilioni 237. Hizi zinakwendakwenye Halmashauri zote katika kutekeleza miradi ambayoiko viji j ini na hususan miradi hiyo ikikamilika itakuwaimeondoa hii adha ya akina mama wanaopata shida yamaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali kama tunampango wa kupeleka mradi mkubwa, katika bajeti ambayoimetengwa hiyo ya shilingi bilioni 237, kwanza tunatakatukamilishe miradi ambayo tayari Serikali ilishawekeza. Kwahiyo, ikishakamilika miradi hii tutaangalia mahitaji sasa yaziada na tutaona namna gani tuweze kutafuta mradimkubwa wa kuweza kuwafikishia wananchi wa Mkoa waSingida. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mlowe, swali la nyongeza.

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika,nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali lanyongeza. Mheshimiwa Waziri amekuwa akiahidi kila siku juuya bili kupanda kwa wananchi wetu. Hapa ninavyoongeanina bili ya maji ya shilingi 700,000 ambapo maji hayatokilakini unaletewa bili.

Sasa naomba kujua, je, ni lini, tunaomba ututajiekabisa Mheshimiwa Waziri utatekeleza ahadi hii kwawananchi wetu kwa sababu wanaumia sana? Ahsante sana.(Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mlowe, tusaidie, hiyo bili niya kipindi gani? Maana isije ikawa ni ya mwezi mmoja; iliMheshimiwa Waziri ajue anachojibu. Hiyo bili ya shilingi700,000 ni ya muda gani? Hiyo uliyoishika wewe hapo ni yamuda gani?

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Bili hii ni ya miezi mitatu, lakini maji hayatoki kabisa.(Makofi)

Page 44: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

44

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Maji naUmwagiliaji, majibu.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: MheshimiwaNaibu Spika, nimeshatoa maelekezo kwenye mamlaka zotekwamba haiwezekani mtu akalipa bili ya maji ambayohajatumia. Kwenye mamlaka zote tumeweka bodi zakusimamia uendeshaji wa mamlaka zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba sana nduguzangu, kama kuna mtu ambaye kapelekewa bili ambapohakupata maji, basi mahali pa kupeleka ni pale kwenye bodi,maana hili ni suala mahususi ili liweze kushughulikiwa.Hatuwezi kuwa na jibu la moja kwa moja kwa sababu siyowote wanaopata bili ya maji ambayo hawajatumia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kuna special case,naomba uniletee. Pia Mheshimiwa Mbunge akiwa kwenyeJimbo lake apeleke kwenye mamlaka ile, hasa kwenye Bodiya Wakurugenzi inayosimamia uendeshaji wa mamlaka hiziili mtu alipie maji aliyotumia tu, kulingana na Sera yetu yaMaji ya mwaka 2002 na Sheria Namba 12 ya mwaka 2009,kwamba ni lazima wananchi tutachangia huduma ya maji.Sasa katika kuchangia ni pamoja na kulipa bili, lakini kamabili ina mzozo, basi tutalishughulikia jambo hili na kuwezakulimaliza.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Flatei Massay, swali lanyongeza.

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika,nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali lanyongeza. Mradi wa Maji wa Haydom unafanana kabisa najinsi ambavyo matatizo ya Ngara yalivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi huu wa Haydomumekaa miaka saba, mkandarasi amechukua pesa na mudawa kukabidhi mradi umeshafika. Mkurugenzi kafanya jitihadampaka leo mradi haujaisha.

Page 45: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

45

Je, Mheshimiwa Waziri atanisaidiaje sasa kuisaidiaHalmashauri yangu ule mradi wa Haydom ukaisha nawananchi wakapata maji?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri, japokuwa hilo nikama swali la msingi, i la sasa linahusu maji, naonaMheshimiwa Mbunge ameona aulize hapo hapo. (Kicheko)

Mheshimiwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: MheshimiwaNaibu Spika, ni kweli, ipo miradi mingi ambayo ukamilishajiwake umechukua muda mrefu na sababu mojawapo ni amakulikuwa na matatizo ya mkandarasi au kulikuwa na matatizoya vyanzo au kulikuwa na matatizo ya kutokulipwa. Sasatulipoingia awamu hii, maana hii ni miaka saba, sisi tunamiaka miwili, tumeanza kwanza kufuatilia miradi mmojabaada ya mwingine na kuhakikisha kwanza Wakandarasiwanarudi. Miradi mingi wakandarasi walikuwa wameondokakwenye utekelezaji ikiwa ni pamoja na huo mradi wakeambao umechukua miaka saba.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Mkandarasi amerudina sasa hivi tunawapa fedha kwa kazi ambazo wamefanya.Kwa hiyo, nitafuatilia huu mradi anaousema ili niweze kuonanini kinachoendelea na tuweze kumwambia MheshimiwaMbunge ni lini kazi ile ingeweza kukamilika? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea.Mheshimiwa Dkt. Rashid Mohamed Chuachua, Mbunge waMasasi, sasa aulize swali lake.

Na. 60

Uhaba wa Maji Jimbo la Masasi

MHE. DKT. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:-

Katika Jimbo la Masasi, Kata za Marika, Mumbaka,Matawale, Sululu, Mwenge, Mtapika, Temeke na

Page 46: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

46

Chanikanguo, kuna tatizo kubwa la maji wakati eneo lakatikati ya mji linanufaika na maji ya mradi wa Mbwinji.

Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kutosha kwa ajiliya upanuzi wa mradi wa maji wa Mbwinji ili usambaze majikatika vijiji vya Jimbo la Masasi?

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali laMheshimiwa Rashid Mohamed Chuachua, Mbunge waJimbo la Masasi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Safi waMasasi, Nachingwea kutoka chanzo cha Mbwinjiunahudumia wakazi wa Miji ya Masasi na Nachingweapamoja na baadhi ya vijiji vya Halmashauri za Wilaya yaMasasi Nachingwea na Ruangwa. Jumla ya wakazi wapatao188,250 wanahudumiwa na mradi huo uliojengwa kwagharama ya shilingi bilioni 31 na kuzinduliwa na MheshimiwaRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Awamu yaNne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete tarehe 24 Julai,2014.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, Serikaliimeendelea kuunganisha vijiji zaidi ili kuongeza upatikanajiwa maji kupitia mradi huo. Kwa sasa baadhi ya vijiji katikaKata za Marika, Mumbaka, Matawale, Sululu, Mwenge,Mtapika, Temeke na Chanikanguo, vimeanza kupata majina vijiji vilivyobaki katika Kata hizo vitaendelea kuunganishwakutoka kwenye mradi huo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika bajeti yamwaka 2016/2017 Serikali ilitoa kiasi cha shilingi milioni 500kwa ajili ya kuendelea kuunganisha vijiji vilivyobaki na katikabajeti ya mwaka 2017/2018 Serikali imetenga shilingi bilionimoja ambapo hadi sasa shilingi milioni 370 zimeshatolewakwa ajili ya kuendelea kuunganisha vijiji vilivyobaki kwenyeMradi wa Masasi, Nachingwea.

Page 47: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

47

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Rashid Chuachua,swali la nyongeza.

MHE. DKT. RASHID M. CHUACHUA: Mheshimiwa NaibuSpika, ahsante sana. Napenda kumwuliza Mheshimiwa Wazirimaswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa Kata nyingi katika Kataalizozitaja hakuna hata kijiji kimoja chenye maji ya bomba,na kwa sababu Serikali imetenga fedha katika mwakauliopita wa bajeti, shilingi milioni 599 na fedha hizi badohazijakwenda katika Halmashauri yangu wakati wananchiwameshachimba mifereji kwa ajili ya maandalizi.

Je, Serikali itapeleka lini fedha hizi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwaHalmashauri yangu imeandika barua ya kuomba uchimbajiwa visima katika vijiji kumi vya Halmashauri yangu vilivyopopembezoni, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya uchimbajiwa visima hivi? Ahsante sana. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waziri wa Maji na Umwagiliaji, majibu.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: MheshimiwaNaibu Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza MheshimiwaChuachua kwa namna alivyoweza kuwahamasishawananchi wa Masasi kujitolea kuchimba mitaro ili ile Mamlakaya MWANAWASA iweze kuunganisha. Nilifika pale na nikaonahiyo kazi, tukacheza na ngoma. Kwa hiyo, nakupongeza sanaMheshimiwa Chuachua na nataka huu mfano uigwe naWaheshimiwa Wabunge wengine, kwamba ni vizuritukahamasisha wananchi pale inapowezekana, kujitoleakuchimba mitaro ili kazi iweze kwenda haraka na wananchiwaweze kupata maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake kwambani lini fedha zitapelekwa? Tayari nimeshaidhinisha kupelekwafedha, hasa kuanzia Masasi Mjini kwa ile kazi ambayo nilionainaendelea. Kwa hiyo, nimeshaidhinisha fedha, kwa hiyo, sasa

Page 48: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

48

hivi ziko njiani, muda siyo mrefu watazipata ili wawezekuunganisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pilikuhusu ombi la visima, hili naomba nilipokee kwa sababuameliuliza kama swali la nyongeza, nilipokee, nitakwendakuangalia tuone namna gani tutasaidia kuweza kuchimbavisima hivyo.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Hassan Masala, swali lanyongeza.

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante sana. Kazi iliyofanyika Masasi ya kuchimba mitaro,kazi hiyo iliyofanyika pia katika Wilaya ya Nachingwea katikaKata za Naipanga, Chiwindi, Rahaleo, Mkotokweana pamojana Stesheni. Kupitia nguvu za Mbunge na wananchitumechimba zaidi ya kilometa 15. Sasa fedha iliyoletwa nichache na sasa hivi ni mwezi, mabomba yaliyoletwa kwaajili ya mradi huu yameshindwa kukidhi mahitaji ya mradimzima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupata jibu laMheshimiwa Waziri, ili nguvukazi za wananchi zilizotumikazisipotee, ni lini fedha hii ambayo imeombwa kwa ajili yamradi huu italetwa ili tuweze kukamilisha kazi ambayotumeianza? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa WAziri wa Maji naUmwagiliaji, majibu.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: MheshimiwaNaibu Spika, kwanza naye nimpongeze kama amewezakuhamasisha wananchi kuchimba mtaro wa kilometa 15 iliiwe kazi rahisi kwetu sisi kuweka mabomba. Tayari mabombamengi yameshapelekwa, yapo Masasi na Nachingwea kwaajili ya kuyalaza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la fedha, fedhatunazipeleka kulingana na namna tunavyopokea. Kwa hiyo,

Page 49: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

49

fedha za Mfuko wa Maji zinazokuja kwa mwezi ni kamashilingi bilioni kumi. Kwa hiyo, hizi ndizo tunazogawanakuwapelekea kila Halmashauri, pale ambapo inaonekanakuna kazi inayoendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie MheshimiwaMbunge kwamba kazi ambayo imeanza haitaachwa,tutapeleka hiyo fedha mapema iwezekanavyo.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Yahaya Massare, swali lanyongeza.

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogola nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo yaliyopo hukoMasasi, yanafanana kabisa na matatizo yaliyopo katika Mjiwa Itigi wenye vij i j i saba vya Kihanju, Songambele,Tambukareli, Majengo, Ziginari, Itigi Mjini na Mlowa, hakunakabisa mtandao wa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tulishaandikabarua kwa Wizara kuomba wataalam wa Wizara wajewatufanyie upembuzi yakinifu na Wizara ikatujibu kwambahaina wataalam kwa sasa na kwamba tushirikiane na Mkoa,na tukaandika barua ya kuomba kiasi kidogo tu, shilingimilioni 40 kwa ajili ya kutusaidia bajeti ili wataalam hawawa Mkoa na wale wa Halmashauri waweze kufanyaupembuzi yakinifu ili tuwapatie maji wananchi wa Itigi.

Je, ni lini sasa Serikali itaisaidia Halmashauri ya Itigihizo hela kidogo tu ambazo zitafanya nasi tupatemchanganuo wa kujua ni nini tunahitaji ili Wizara iwezekutupa pesa za kujenga miundombinu ya maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Maji naUmwagiliaji, majibu.

Page 50: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

50

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: MheshimiwaNaibu Spika, kwanza kabisa kuhusu fedha za uendeshaji aukufanyia usanifu wa kazi kwenye Halmashauri yake, katikahii bajeti ya shilingi bilioni 237 tuliyoitoa, kazi yake kubwakwanza ni kujenga miundombinu kama ipo lakini pia fedhahizo zinatumika kwa usanifu, usimamizi na kadhalika; lakinipia na uendeshaji wa ofisi ni fedha hiyo hiyo. Kwa hiyo, katikabajeti ambayo Halmashauri yake ya Itigi imetengewa kwamwaka 2017/2018 naomba watumie sehemu ya hiyo fedhaili waweze kufanya hiyo kazi ambayo Mheshimiwa Mbungeanaizungumzia. Kama wanaleta maombi, maana tutawapahizo fedha, lakini tutakata kwenye allocation ambayowametengewa kwa mwaka 2017/2018.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Catherine Ruge, swali lanyongeza.

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Naibu Spika,nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Napendanimuulize Mheshimiwa Waziri swali dogo la nyongeza. Tatizola uhaba wa maji katika Wilaya ya Serengeti hasa vijijini,limekuwa ni kubwa na la muda mrefu na kuanzia mwaka2007 mpaka sasa hivi Serikali bado inatekeleza mradi wa majikatika vijiji kumi, ila mpaka ninavyozungumza kuna miradimiwili katika vijiji vya Kenyana, Nyamitita na Kibanjabanjahaijakamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujua, ni lini sasamiradi hii itakamilika ili wananchi wa maeneo husika wawezekupata maji safi na salama?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Maji naUmwagiliaji, majibu.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: MheshimiwaNaibu Spika, Mheshimiwa Catherine amezungumzia baadhiya miradi ambayo ipo kwenye Halmashauri yake na kuniulizani lini miradi ile itakamilika?

Page 51: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

51

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme tukwamba itabidi nifuatilie niweze kujua, kwa sababu hili niswali la nyongeza, siwezi kuwa najua kila kijiji katika nchinzima, mradi ule uko katika status gani? Kwa hiyo, naombasana tuonane naye, anakaribishwa ofisini i l i tuwezekuangalia. Nitampa status na taarifa kamili ni lini miradi ileitakamilika.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Lucy Mayenga, swali fupi.

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante sana. Kwa kuwa tatizo hili la maji lipo kwenyecategories mbalimbali kwa nchi nzima, wapo watu ambaohawana kabisa miradi katika maeneo yao kwa sisi Wabungehapa ndani Bungeni, lakini pia yapo maeneo ambayo miradiipo lakini haijakamilika kutokana na sababu mbalimbali, lakiniyapo maeneo katika nchi yetu ambayo maji yanapatikanalakini kumekuwa na manung’uniko ya chini chini yawananchi kwamba jinsi bili zinavyotoka kunakuwa hakunausawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo haya yamekuwayakisemwa kwa wananchi kwa muda mrefu na yamekuwatakribani kila Mbunge anaposimama hapa wengiwamekuwa wakigusia kuhusu tatizo la kutokuwa na usawawakati wa kutoa bili.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara badala ya kusemakwamba wananchi au sisi Wabunge twende kwenye bodikutoa malalamiko au wananchi waende kule kwenye taasisiza kutoa huduma ili kwenda kupeleka malalamiko yetu.

Je, Wizara hii haioni sasa umefika wakati kuchukuliatatizo hili kwa ukubwa wake kama tatizo la kitaifa, kuundatimu maalum itakayopita kila maeneo na kuweza kujuakwamba maeneo haya yana matatizo haya tuwezekuyatatua vipi na eneo hili matatizo yake tuweze kutatuavipi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Page 52: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

52

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Maji naUmwagiliaji, majibu.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: MheshimiwaNaibu Spika, Mheshimiwa Lucy Mayenga ameuliza swali zaidiya moja; anazungumzia habari ya matatizo ya upatikanajiwa maji, lakini pia anachanganya tena na masuala ya bili.Sasa ni vitu viwili tofauti. Masuala ya upatikanaji wa maji,Serikali inaendelea kutekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili la matatizo ya bilinimeshalitolea majibu, labda nirudie kwa kuweka msisitizo.Ni kwamba Wizara inatambua yapo maeneo ya mtu mmojammoja kulalamikia bil i, siyo kwamba kila mmojaanalalamikia bili. Sasa nasema, kama ni isolated cases,hatuwezi kuchukulia kama ni tatizo la Kitaifa. Hili ni tatizo lamtu mmoja ambaye ana tatizo, amepewa bili ya miezi mitatuhajapata maji.

Sasa hili naomba tulifuatilie kwa maana ya kwa huyomtu ambaye anatuletea ni isolated case tuishighulikie. Siyojambo la kusema tulitolee mwongozo kama Taifa kwamaana ya kwamba tumeshakubaliana kwamba maji ili yaweendelevu, upatikanaji wake ni lazima tuchangie.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kulipa bili ni lazimaili tuwe na uhakika wa kuwa na maji. Sasa kama kunamatatizo mahali, tutayashughulikia kwa mujibu wa sheriana kwa mujibu wa taratibu tulizojiwekea.

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendeleana Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee naWatoto, Mheshimiwa Lucy Simon Magereli, Mbunge wa VitiMaalum, sasa aulize swali lake.

Na. 61

Huduma ya Dawa za Kurefusha Maisha

MHE. LUCY S. MAGERELI aliuliza:-

Page 53: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

53

Kwa mujibu wa Ripoti ya Kamati ya Bunge ya Masualaya UKIMWI ya Februari, 2017 fedha za wafadhili zinaendeleakupungua na baadhi yake kuwa na masharti yasiyoendanana mila na desturi za Kitanzania.

Je, Serikali imejipangaje kuendeleza hudumazilizokuwa zikitolewa na wafadhili, hususan dawa za kurefushamaisha?

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WAZEE NA WATOTO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri waAfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, naombakujibu swali la Mheshimiwa Lucy Simon Magereli, Mbunge waViti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuhakikishie kwambaWadau wa Maendeleo wameendelea kutoa msaada wadawa za kurefusha maisha (Antiretroviral Drugs - ARVs) mbalina kwamba Serikali imeendelea kupinga maadili mbalimbaliyasiyoendana na mila na desturi za Kitanzania kwa kutoamiongozo mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikishatunajipanga vyema na upatikanaji, hususan wa dawa zakurefusha maisha (ARVs), Serikali kwa sasa imeanzisha MfukoMaalum wa UKIMWI unaojulikana kama AIDS Trust Fund (ATF).Mfuko huu utachangiwa na Serikali, mashirika, sekta binafsipamoja na wahisani.

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo kuu la mfuko huu nikuchangia upatikanaji wa dawa za kurefusha maisha hapanchini.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Lucy Magereli, swali lanyongeza.

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Naibu Spika,nakushukuru.

Page 54: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

54

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa swali langulilirejea Taarifa ya Kamati ya Mambo ya UKIMWI iliyotolewandani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaFebruari mwaka huu, nilitarajia majibu ya Mheshimiwa Waziriyawe at least na takwimu ambazo sasa zitaunga mkono hojaya Taarifa ya Kamati au zitatengua ile hoja ya Taarifa yaKamati kwamba fedha za wafadhili katika eneo hilizimepungua sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa swali langu,Mheshimiwa Naibu Waziri anisaidie kwamba hao wadaualiowataja ni wadau gani ambao wameendelea kutoasupport katika eneo hili? Kwa sababu tunafahamu fedha zamambo ya UKIMWI zimekuwa zikichangiwa kwa asilimiakubwa sana na PEFA na Global Fund ambao kwa sehemukubwa wame-pull out.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa sijajua haoaliowazungumzia hapa Mheshimiwa Naibu Waziri ambaoanasema wanachangia kwa kiasi kikubwa kinyume na Taarifaya Kamati ni akina nani? Napenda kufahamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kumekuwa namaendeleo kadhaa ya kitabibu na kimaabara ambayoyanaonesha majaribio yaliyofanikiwa katika upatikanaji wachanjo na hata tiba ya Virusi vya UKIMWI. Je, Serikali inamaelezo gani kuhusu maendeleo haya na taarifa hiziambazo zinatokana na vyombo mbalimbali? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Majibu kwakifupi.

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII,JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, swalila kwanza, kwamba ni wadau gani? Kwa mujibu wa sheriaambayo inaanzisha Mfuko wa UKIMWI Tanzania, malengomakuu ya mfuko huu ni kukusanya pesa ambazo zitakwendakuweka uendelevu wa pesa ambazo zitakuja kuwazinatumika sustainably kwenye kununua dawa za UKIMWI kwa

Page 55: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

55

kiwango cha asilimia 60, lakini pia kutoa huduma za kingakwa asilimia 25, pia kwa asilimia 15 kusaidia kwenye mwitikiowa UKIMWI kwa maana ya kujenga mazingira mbalimbaliwezeshi hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mfuko huu unamalengo ya kuwa endelevu na ulianzishwa kwa malengokutokana na mabadiliko yaliyofanyika kwenye Sheria yaUKIMWI ambayo ilianzisha TACAIDS mwaka 2001 SheriaNamba 22 kwa ajili ya kutengeneza sustainability kwenye eneola upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya HIV/Aids.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa mfuko huu badoni mchanga sana na umezinduliwa mwaka 2016 tu mweziDisemba na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano zaTanzania, Mama Samia Suluhu Hassan na kwa mwaka wafedha uliopita tulitenga kiwango cha shilingi bilioni 5.5 namwaka huu tumetenga shilingi bilioni tatu. Kwa hiyo, ndiyotumeanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa wadau ni akina nani?Wadau wa kwanza ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano waTanzania kupitia bajeti yake, lakini pia tunatarajia mfuko huuutakusanya vyanzo vingine vya fedha kutoka kwa wananchikwa ujumla ambao watajitokeza kuchangia kutoka kwenyesekta binafsi, asasi za kiraia, asasi za hiari, lakini pia wadauwa maendeleo hawazuiliwi pia kuchangia kwenye mfukohuo. Malengo yetu ni kwamba tuweze kufikia angalau asilimia30 ya kujitosheleza kwenye fedha za dawa za kupunguzamakali katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, chanjo ya virusivya UKIMWI bado inaendelea kufanyiwa utafiti duniani,jitihada bado zinaendelea. Nasi Tanzania ni washiriki katikatafiti mbalimbali ambazo zitapelekea kupatikana kwachanjo kwa siku zijazo, lakini kwa sasa tuko katika hatua zaawali sana za Kisayansi za kutafuta chanjo hiyo na badohakujawa na mwangaza mkubwa sana kwamba labdakatika kipindi cha miaka kadhaa tunaweza tukawa tumefikiahatima ya kuwa na chanjo ya virusi vya UKIMWI.

Page 56: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

56

Kwa hiyo, tuendelee kuvumilia wakati wanasayansiwakifanya kazi yao kwenye maabara zetu. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waziri wa Afya.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEENA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sanaMheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, lakininimesimama kwa sababu Mheshimiwa Mbunge LucyMagereli anazungumzia upatikanaji wa dawa za ARV.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie Bunge lakoTukufu kusema kwamba tunazo ARV ambazo kuanzia mweziOktoba, 2016 zinatolewa kwa kila Mtanzania atakayepimana kukutwa na maambukizi ya VVU.

Mheshimiwa Naibu pika, sasa kwa nini nimesimama?Kati ya watu wenye maambukizi ya VVU, wanawakewanaotumia ARV ni asilimia 73, wanaume ni asilimia 48 tu.Kwa hiyo, nitoe wito kwa wanaume wote Tanzania watumiedawa za ARV ili kwa pamoja tuweze kupunguza maambukiziya VVU nchini. Acheni kujiona nyie mna misuli, ni wababe,dawa za ARV zipo, tumieni ili tuweze kupunguza maambukiziya UKIMWI. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama hapa kwasababu kati ya maambukizi mapya ya vijana wetu wenyemiaka 15 mpaka 24 kwa wavulana ni asilimia nane nawasichana ni zaidi ya asilimia 80. Maana yake hawawanaume ndiyo wanarudi tena kwa watoto wadogo nahivyo kufanya kuwepo kwa maambukizi mapya ya VVU naUKIMWI.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeona nitumie fursa hiiWaheshimiwa Wabunge wakawahamasishe wanaumewatumie ARV, zipo bure, zinapatikana na mtu yeyoteakipima anapata bila shida. Ahsante sana. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi yaWaziri Mkuu.

Page 57: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

57

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, (SERA,BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU):Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa WaziriMkuu ninampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri, lakininampongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Afya kwa majibuya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama hapa ilikuweza kulithibitishai Bunge lako kwamba mfuko huu ambaoulianzishwa kwa Sheria Namba 6 ya mwaka 2015 naunasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, umeanza kufanya kazinzuri sana pamoja na uchanga wake.

Mheshimwa Naibu Spika, maagizo ya Kamati kamaalivyosema Mbunge aliyeuliza swali, yalikuwa na malengoya kuhakikisha kwamba Serikali inasimamia mfuko huu naunaanza kufanya kazi.

Mheshimwa Naibu Spika, naomba niliarifu Bunge lakoTukufu kwamba Waheshimiwa Wabunge wa Kamatiinayohusika na masuala ya UKIMWI waliiagiza Serikali, kwarasilimali ndogo iliyopatikana ni lazima sasa mfuko uanzekuhakikisha unatoa fedha kupeleka Wizara ya Afya ilikushughulika na dawa na kuongeza maisha yaWatanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Kifungu cha6(1) cha Sheria hiyo, mfuko unakaribia kutoa, umeshapitishakwenye Bodi jumla ya shilingi za Kitanzania bilioni 1.45 kwaajili ya kununua dawa za septrine na kwa ajili ya kujengaKituo cha Upimaji Mererani na kujenga kituo kingine chaupimaji kwenye Visiwa ndani ya Ziwa Victoria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naombaniwathibitishie Wabunge kwamba Kamati ilifanya kazi nzurina Serikali imepokea maagizo hayo na tayari mfuko wetuumeanza kuonesha kwamba tunaanza kujitegemea ndaniya Serikali yetu ingawa wafadhili bado wanaendeleakutusaidia. (Makofi)

Page 58: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

58

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendeleana Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi. Mheshimiwa RoseCyprian Tweve, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swalilake.

Na. 62

Kufanya Mapinduzi Katika Sekta ya Kilimo

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:-

Pamoja na kwamba sekta ya kilimo ndiyo yenye kuajiriWatanzania walio wengi, lakini sekta hiyo imekuwa namaendeleo hafifu kutokana na watumishi wachache wenyeujuzi wa kutosha na ukosefu wa vitendea kazi kama vilepikipiki, zana za kufundishia na kadhalika.

Je, Serikali ina mkakati gani wa makusudi wa kufanyamapinduzi ya kil imo kwa kuwa na wataalam wakutosha?

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri waKilimo, Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la MheshimiwaRose Cyprian Tweve, Mbunge wa Viti Maalum, kamaifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua kuwaSekta ya Kilimo ni muhimu na ndiyo yenye kuajiri Watanzaniawengi, hivyo mapinduzi ya kilimo pamoja na mambomengine yatachangiwa uwepo na wataalam wa kutoshawenye taaluma na ujuzi stahiki ili waweze kushauri matumiziya teknolojia na kanuni bora za kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimuhuo, Serikali imeweka mikakati mbalimbali ili kuleta mapinduziya kilimo ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya MaafisaUgami wenye ujuzi ili kila Kata na kijiji kiwe na Afisa Uganimmoja. Aidha, Serikali inaendelea kuboresha na kuwezesha

Page 59: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

59

Vituo vya Kilimo na Vituo vya Rasilimali za Kilimo za Katakwa ajili ya kufundisha teknolojia mbalimbali za kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia mwaka2016/2017, Serikali imeajiri Maafisa Ugani 8,756 sawa na asilimia43 ya mahitaji ya Maafisa Ugani 20,374 katika ngazi ya kijiji,Kata na Wilaya. Jumla ya wataalam wa kilimo 8,000 ngaziya Astashahada na Stashahada waliohitimu mafunzo katikaVyuo vya Kilimo wameajiriwa katika maeneo mbalimbalinchini. Aidha, Serikali inaendelea kusomesha vijana tarajalina kuwaajiri kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati mingine ni pamojana kuboresha huduma za ugani kwa kusambaza teknolojiaza kilimo bora kwa wakulima kwa kutumia njia mbalimbalihususan shamba darasa, vipindi vya redio na luninga,mchapisho na Maonesho ya Kilimo - Nane Nane.

Aidha, Serikali itaendelea kutoa ushauri wa kitaalamna kuandaa miongozo na mafunzo ya huduma za ugani,ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa kazi za ugani nakuboresha usambazaji wa teknolojia za kilimo bora kwawakulima nchini.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Rose Tweve, swali lanyongeza.

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika,namshukuru sana Mheshimiwa Waziri. Pamoja na maelezohayo, Mheshimiwa Waziri atakubaliana nami kabisa kwambakumekuwa na dhana potofu kuwa kilimo kimekuwa kamalast resort. Hata ukiongea na watoto wetu wa shule,ukiwauliza unataka kuwa nani? Mmoja atakwambia daktari,mwanasheria, engineer na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nilitaka nipate maelezoya Mheshimiwa Waziri, ni mikakati gani sasa kama Wizaraau incentives gani mmeziweka ili iwe kivutio kwa hawaWatanzania na vijana wetu ambao kuna tatizo kubwa launemployment? Hilo ni la kwanza. (Makofi)

Page 60: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

60

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, katika maelezo yanguya mwanzo niliongelea suala la wataalam nashukuru kuwaMheshimiwa Waziri ameli-address lakini kwenye ukosefu wavitendea kazi, Watanzania wamekuwa wakiwalaumu sanawataalam hasa hawa Maafisa Ugani kuwa wamekaa tuMaofisini, lakini ukiangalia tatizo kubwa ni ukosefu wavitendea kazi. Sasa napenda nipate maelekezo, ni mkakatigani kama Wizara mmeweka kuhakikisha hawa wataalamwetu wanapata vitendea kazi kama vile pikipiki na zana zakufundishia ili tuweze kuleta mapinduzi ya hii Sekta ya Kilimo?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, majibu kwa kifupi.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuweka mazingira ya kilimokuvutia watu wengi zaidi hususan vijana, naombanimahakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sasa kilimokinavutia sana na ndiyo maana hata baadhi yenuWaheshimiwa Wabunge ni wakulima hodari. Kwa hiyo, kizurikinajiuza, kil imo kinalipa, tayari kuna watu wengiwamenufaika na hivyo niwasihi tu vijana kwamba kilimo kinamanufaa. Vilevile Serikali imeweka mazingira mazuri sana yakuwavutia vijana na ndiyo maana tumeweka taratibu za waokupata mitaji, tumeanzisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo,tuna Mfuko wa Pembejeo, lakini vilevile hata Benki za binafsizinatoa mikopo. Kwa hiyo, niseme tu kwamba kilimo kinavutia,kuna uwezeshaji, kwa hiyo, vijana wanakaribishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni kuhusianana wataalam, Maafisa Ugani kutokuwa na vitendea kazi. Hililimezungumzwa sana, lakini mara nyingi vilevile imekuwa niksingizio. Kinachohitajika kwa Afisa Ugani anapokuwepokwenye eneo lake la kazi ni elimu ile aliyonayo ajaribukuitumia kuwafikishia wananchi. Mara nyingi katika ngazi yakijiji huwezi kulalamika kwamba kwa sababu sina pikipiki,basi siwezi kuwafikia wananchi. Watendaji wengine waSerikali walioko katika ngazi hizo wanafanya kazi zao.

Page 61: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

61

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, pamoja na ukwelikwamba kuna hitaji la kuhakikisha kwamba hivyo vitendeakazi viweze kupatikana lakini tunawasihi kwamba isiwe nikisingizio. Lazima watumie elimu ambayo wanayo kwasababu ni ajira yao ili kujaribu kuhakikisha kwamba wananchiwanapata elimu ya kilimo bora.

NAIBU SPIKA: Ahsante. Waheshimiwa Wabunge,tunaendela na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.Mheshimiwa Kiteto Zawadi Koshuma, Mbunge wa VitiMaalum sasa aulize swali lake.

Na. 63

Serikali Kuwezesha SIDO

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:-

SIDO pamoja na majukumu mengine inatoa hudumakwa viwanda vidogo na vya kati kwa kutoa mikopo, mafunzona vitendea kazi.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuiwezesha SIDOkutimiza majukumu yake?

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJIalijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali laMheshimiwa Kiteto Zawadi Koshuma, Mbunge wa VitiMaalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kutambuaumuhimu wa SIDO katika ujenzi wa uchumi wa Taifa letuimekuwa na mipango na mikakati mbalimbali yakuliwezesha Shirika hili kutimiza majukumu yake. Kupitia BajetiKuu ya Serikali, SIDO inatengewa fungu kwa ajili ya kujengamiundombinu ya ofisi ya maghala ya viwanda (industrialsheds). Kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali imetengajumla ya shilingi bilioni 7.04 kwa ajili ya kujenga miundombinu

Page 62: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

62

tajwa hapo juu katika Mikoa ya Katavi, Manyara, Kagera,Geita na Simiyu. Nafurahi kutamka kuwa tayari shilingi bilionitano kati ya bilioni saba zilizopangwa kufanikisha jukumuhilo hapo juu zimeshatolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hutoa fedha za mitajikwa SIDO kupitia Mfuko wa Kuendeleza Wajasiriamali (NEDF).Mfuko huu uliainzishwa mwaka 1994 kwa mtaji wa shilingimilioni 800 na mpaka sasa Serikali imechangia shilingi bilioni5.05 ambazo zimezungushwa na wajasiriamali na kufikiashilingi bilioni 62.8 kwa mwaka wa fedha 2017/2018; na kwamwaka huu sasa tumetenga shilingi bilioni 7.14 kwa ajili yamfuko huu; na mahususi tutaelekeza juhudi zetu katikauanzishaji wa viwanda vidogo sana na viwanda vidogo chiniya mkakati wa Wilaya Moja, Bidhaa Moja (ODOP).

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali pia ina mkakati wakuwatafutia SIDO wabia wa nje ili waweze kuwasaidiakufikisha huduma kwa wananchi hasa wafanyabiashara nawenye viwanda vidogo. SIDO inashirikina na Shirika laviwanda la India (National Small Industry Corporation of India)katika masuala ya kukuza teknolojia. Ushirikiano huounahusisha uanzishwaji wa kiatamizi cha teknolojia za ainambalimbali katika Mitaa ya Viwanda eneo la Vingunguti Dares Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, SIDO imewezesha kuingiaubia na Shirika la maendeleo la Sweden na wamepatiwashil ingi bil ioni 1.8 kuanzisha Kongano. Vilevile SIDOimewezeshwa kuingia Ubia na Shirika la Maendeleo ya Uchumila Canada (Economic Development Associates) ambaounawezesha kutoa mafunzo ya kuimarisha na kuendeshabiashara katika ukanda wa Mtwara na Lindi na ukanda waMorogoro mpaka Arusha.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kiteto Koshuma, swali lanyongeza.

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika,kwa kuwa SIDO ndiyo mlezi wa viwanda vidogo vidogo

Page 63: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

63

pamoja na vya kati ambapo tunatarajia viwanda hivi viwezekuelekea katika kuwa viwanda vikubwa na hivyo kuwezakuwezesha uchumi wa viwanda kuendelea hapa nchiniTanzania na Waziri amekiri kabisa kwamba Serikaliinalitambua hilo na imekuwa ikitenga fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, utakubaliana na mimikutenga fedha na kupeleka fedha ni kitu kingine. Kwa taarifanilizonazo kabisa ni kwamba Serikali kwa mwaka 2015/2016ilitenga shilingi milioni 500; mwaka 2016/2017 Serikali ilitengashilingi bilioni 2.4; na kwa mwaka 2017/2018 kwa majibu yaMheshimiwa Waziri, Serikali imetenga shilingi bilioni 7.14.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali pamoja na kutengafedha hizi zimekuwa haziendi. Kwa maana hiyo,tunategemea nini?

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kauli mbiuya viwanda ambayo tumeona Mheshimiwa Rais amekuwaakiisema kweli itaweza kutimia kwa mwenendo huu wakutokupeleka fedha? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, wanawake waMkoa wa Mwanza wamekuwa wakijishughulisha na shughuliza viwanda vidogo vidogo, lakini changamoto kubwawaliyokuwanayo ni kukosekana kwa vifungashio ambavyowanavipata kwa gharama za juu sana na hivyo kushindwakujiendeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua kwambaSerikali inawezaje kuwasaidia wanawake wa Mkoa waMwanza ili waweze kupata kiwanda cha vifungashio iliwaweze kujikwamua kiuchumi? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji, majibu.

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nikiri na ninakubaliananaye. Ujenzi wa uchumi wa viwanda endelevu unatokana

Page 64: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

64

na viwanda vinayoitwa LGI (Local Grown Industries) siyo hiziFDI. Hawa wanatafuta green pasture, wataondoka na Serikaliinalitambua hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2016 tulipaswakupewa shilingi bilioni 2.4, hatukupewa. Tumeiomba Serikalitupewe shilingi bilioni 7.04; nina imani Serikali itatoa pesa hizona ninazifuatilia. Napenda niishie hapo na Kamati yanguimefanyia kazi na tusipotoa pesa hizo, hivi viwanda tunavyoitaFDI, hao ni kware. Huwezi kulisha kware ukawaacha watotowa kuku. Naomba niishie hapo.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la vifungashio ni tatizokwa wajasiriamali wadogo wote. SIDO tumeamua kuwekezakatika kiwanda cha vifungashio na hicho kitatoa vifungashiokwa akina mama wote na wajasiriamali wadogo. Nachukuafirsa hii kuwahimiza wajasiriamali wanaoweza kuwekezakwenye biashara hii wawekeze katika vifungashio. Tunatumiapesa nyingi za kigeni kuagiza vifungashio kutoka nje ya nchi.

NAIBU SPIKA: Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,Mheshimiwa Shaabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto,sasa aulize swali lake.

Na. 64

Matumizi ya Teknolojia ya Graphogemu-Kiswahili katikaKufundisha Katika Kufundishia

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:-

Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa(SEKOMU) kilichopo Lushoto kwa mafanikio makubwakimeweza kutumia teknolojia rahisi inayoitwa Grapho Game,kwa kiswahili ni Grafo Gemu kupunguza idadi kubwa yawanafunzi wasiojua kusoma na kuandika darasa la kwanza

Page 65: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

65

na la pili katika shule kadhaa zilizopo Wilaya ya Lushoto naBagamoyo na pia SEKOMU kwa kutumia teknolojia hiyoimewezesha watu wazima kujua kusoma na kuandika katikakijiji cha Kwemishai – Kibohelo – Lushoto.

(a) Je, Serikali haioni kwamba ni wakati muafakasasa kuwatumia wataalam walioko SEKOMU akiwemomtalaam aliyeshiriki kutayarisha maudhui katika teknolojiaambayo imeweka msisitizo katika mbinu za kufundishiakusoma ya kifoniki ambayo hujikita katika utambuzi wa sautiza herufi zinazounda maneno?

(b) Je, Serikali haioni ni jambo muhimu kabisa kwakupitia mpango huu muhimu na maalum kama walivyofanyanchi ya Zambia na Finland kuidhinisha matumizi ya teknolojiahiyo iwe kama teknolojia suluhisho (IT Solution) kwa ajili yakuwasaidia watoto wa madarasa ya mwanzo ya elimu yamsingi wenye changamoto ya kujua kusoma na kuandika?

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIAalijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri waElimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali laMheshimiwa Shaabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto,lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Seriakli inatambua umuhim,u wakuimarisha stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK)kwa wanafunzi wanaosoma madarasa ya chini hususan elimuya awali, darasa la kwanza hadi darasa la nne na watuwazima wasiojua kusoma na kuandika kwa kuwa stadi hizozinawawezesha kupata umahiri katika stadi za KKK.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itawasiliana namtaalam wa Grafo Gemu (kiswahili) ili kufahamu jinsiteknolojia hiyo inavyofanya kazi. Wizara itakapojiridhisha naufanisi wa matumizi ya teknolojia hiyo, itafuata taratibustahiki na kuidhinisha matumizi ya teknolojia hiyo shuleni.

Page 66: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

66

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Shabani Shekilindi, swali lanyongeza.

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawiliya nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, wakati Wazirianaendelea kufanya utafiti juu ya Grafo Gemu, je, Serikaliina mpango mkakati gani wa haraka wa kuweza kuwapatiabaadhi ya vifaa il i wataalam wetu hao waendeleekuwasaidia watoto wetu pamoja na kwamba suala hililitakuwa ni suala la Kitaifa?

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kwa kuwa Serikali yaAwamu ya Tano ni ya hapa kazi tu; je, Mheshimiwa Waziriyupo tayari kuongozana na mimi wakati Bunge likiahirishwaili akaone juhudi za wataalam hawa watokao SEKOMUwanaofanya kazi kubwa kuwasaidia watoto wetu hasamama yangu mtaalam anaitwa mama Gorosho? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, majibu.

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimezungumzakwamba Wizara ingependa kujiridhisha namna ganiteknolojia hiyo inavyofanya kazi na namna gani inavyowezakuwanufaisha wanafunzi wengi zaidi na wananchi kwaujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo kawaida yetusisi Waheshimiwa Mawaziri wengi tumekuwa tukiambiwakutembelea maeneo na tunafanya hivyo. Kwa hiyo,nimwambie tu kwamba nitakuwa tayari kutembelea katikaeneo la Mheshimiwa Mbunge ili kujiridhisha lakini vile vilekuona uwezekano wa kutoa vifaa ambavyo vitahitajika kamaambavyo ameomba. Namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwaufuatiliaji wake. (Makofi)

Page 67: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

67

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tunaendelea.Mheshimiwa Pauline Phillip Gekul, Mbunge wa Babati Mjinisasa aulize swali lake.

Na. 65

Mapitio ya Sera ya Elimu Bure

MHE. PAULINE P. GEKUL aliuliza:-

Serikali iliwahi kuliahidi katika Bunge hili kuwa inafanyamapitio ya Sera ya Elimu Bure na kwamba ingeleta Bungenimambo yanayohitaji kuboreshwa:-

Je, ni lini mapitio hayo yatakamilika?

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIAalijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wangu,naomba kujibu swali la Mheshimiwa Pauline Phillip Gekul,Mbunge wa Babati Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara yaElimu, Sayansi na Teknolojia iliamua kuondoa malipo ya adakwa elimu msingi inayojumuisha elimu ya awali pamoja nadarasa la kwanza hadi kidato nne kama utekelezaji wa Seraya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 Ibara ya 3.1.5 na Ilaniya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020 Ibara ya52(a). Lengo la Sera hii ni kuhakikisha kuwa watoto wotewenye umri wa kwenda shule wanapata fursa hiyo bilakikwazo chochote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na umuhimu wamaamuzi hayo ya Serikali kwa ustawi wa wananchi na Serikalikwa ujumla mwezi wa Februari mwaka 2017 Wizara ilifanyaufuatiliaji kuhusu utekelezaji wa Sera hii ili kubainisha mafanikiona changamoto kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wake.

Page 68: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

68

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumtaarifuMheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu kuwa Serikaliitatumia matokeo na mapendekezo ya ufuatiliaji uliofanyikakutatua changamoto zilizojitokeza ili kuhakikisha lengo laSerikali la kutoa fursa kwa watoto wote wenye umri wakwenda shule linafikiwa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Pauline Gekul, swali lanyongeza.

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika,nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili yanyongeza. Swali la kwanza; kwanza ni vizuri Serikali ikakirikwamba imeshindwa katika Sera hii ya Elimu Bure na nitatoamfano. Fedha wanazopeleka katika shule zetu asilimia 35 nifedha kwa ajili ya utawala na chini ya utawala kuna mambomatano yafuatayo: Kuna stationery, maji, walinzi, umeme nadharura. Nitoe mfano katika sekondari moja ya Babati,sekondari ya Bagara – wanapeleka milioni moja na laki sabaasilimia 35 ni 302, 4716.55. Katika 324,000 mlinzi analipwa150,000, maji 200,000 acha stationery, acha dharura, kwa haliya kawaida walinzi wameshaondoka katika shule zetu. Majiyamekatwa katika shule zetu za msingi na sekondari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa nini hawataki kuelezaukweli kwamba wameshindwa kutekeleza sera hii kwasababu shule zetu zimeachwa sasa na hakuna maji. Naombamajibu ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; MheshimiwaWaziri katika majibu yake anasema kwamba tangu Februari2017…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Gekul, tusaidie ufupishokidogo maelezo ya la pili kwa sababu la kwanza umechukuamuda mrefu sana.

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika,sijakupata.

Page 69: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

69

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

NAIBU SPIKA: Fupisha maelezo ya swali lako lanyongeza la pili kwa sababu swali lako la nyongeza la kwanzalimechukua muda zaidi.

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, swalila pili; Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa wamefanya uchambuzihuu tangu Februari, 2017 mpaka sasa hawajarekebisha haya,ni kwa nini sasa wasiruhusu wazazi wachangie maji na walinzikatika shule zao kwa sababu sasa ukitaka kuchangia tuwanasema Serikali inapeleka fedha wakati Serikali haipeleki.Watoe mwongozo tuchangie kuliko watoto wetu wakose majina walinzi waache shule zetu. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, majibu.

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; Serikalihaijashindwa! Narudia tena kusema, Serikali haijashindwa!Kwa nini nasema Serikali haijashindwa? Nimeshatembeleamikoa mingi sasa hivi, nimeshatembelea shule nyingi sasa hivi,kimsingi wanashukuru sana kwamba sasa kuna utaratibu wawazi wa kupeleka fedha hizo kwenye shule. Wao wenyewewanapanga, isipokuwa, lazima nikiri bado yapo matatizomachache yanayohitaji kurekebishwa. Tatizo mojawapolilikuwa ni kutokuwa na ubora wa takwimu. Kuna baadhi yashule zilikuwa hazijaweza kuleta takwimu zilizo sahihi na hapondipo tulipoweza kubaini hata wanafunzi hewa na hivyotukaweza hata ku-save baadhi ya fedha takriban shilingimilioni 720 zilizokuwa zinaenda zikiwa hewa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Mheshimiwa Rais nasisi kupitia Wizara hizi mbili tumekuwa tukisema kila wakatikwamba, wazazi wasijitoe katika kuendelea kusaidia elimunchini. Pale panapoonekana kuna mahitaji ya msingi zipotaratibu zimeshatolewa mwongozo, Kamati za Shulekushirikiana na wazazi kuweza kuendelea kushirikiana naSerikali katika kutatua.

Page 70: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

70

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, nadhaninimejibu yote kwa ujumla. Kwa hiyo, ninachomwomba tuMheshimiwa kule kwenye jimbo lake aendelee kuhakikishaanashirikiana na Kamati za Shule lakini pia na uongozi kuonakwamba elimu hii tunaishughulikia wote kwa pamoja na hilisio suala la kusema nani afanye, nani asifanye! Mzazi anaowajibu wa kwanza katika kuhakikisha mwanafunzi wakeanasoma vizuri. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendeleana Wizara ya Nishati na Mdini, Mheshimiwa Abdallah Haji AllyMbunge wa Kiwani sasa aulize swali lake.

Na. 66

Faida na Changamoto za Mfumo wa Vyama Vingi

MHE. ABDALLA HAJI ALI aliuliza:-

Uzalishaji wa mafuta na gesi ni suala la Muungano nakwa kuzingatia ukweli kwamba visima vya gesi vyasongosongo na Mnazi Bay Mkoani Lindi na Mtwara vimekuwavikizalisha gesi muda mrefu sasa:-

(a) Je, uzalishaji wa gesi kwa siku kwa visima hivyoni mita za ujazo kiasi gani?

(b) Je, tangu uzalishaji ulipoanza mapato yafedha yamekuwa kiasi gani kwa mwaka na yanatumikaje?

NAIBU SPIKA: Upande wa Serikali si jui ni nanianasimama, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo naUvuvi kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI (K.n.yWAZIRI WA NISHATI NA MADINI) alijibu:

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali laMheshimiwa Abdalla Haji Ali, Mbunge wa Kiwani, lenyesehemu (a) na (b), kama ifuatavyo.

Page 71: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

71

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa wastani jumla ya futiza ujazo milioni 145 za gesi asilia huzalishwa kwa siku katikavisima vya uzalishaji gesi asilia vya Songosongo na Mnazi Bayambako kiasi cha futi za ujazo milioni 90 huzalishwa kwenyevisima vya Songosongo na kiasi cha futi za ujazo milioni 55huzalishwa katika visima vya Mnazi Bay.

Mheshimiwa Naibu Spika, gesi asilia inayozalishwahutumika kuzalisha umeme katika mitambo ya SONGASmegawatt 189; Kinyerezi, megawatts 150; Ubungo Imegawatts 102; Ubungo II megawatts 129; Somangafungumegawatts 7.5; Tegeta megawatts 45; na Mtwara megawatts18. Aidha, kiasi kingine cha gesi asilia hutumika kama chanzocha nishati kwenye viwanda 42 vilivyounganishwa pamojana matumizi madogo kwenye nyumba kwa ajili ya kupikiana kuendeshea magari.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha jumla ya shilingi bilioni488 zimekusanywa kutoka kwenye mauzo ya gesi asilia kwamiaka sita tangu 2011 hadi 2016 sawa na wastani wa kiasicha shil ingi bil ioni 81.3 kwa mwaka. Mapato hayahuwasilishwa Hazina kwa mujibu wa taratibu husika.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Abdallah Haji Ali swali lanyongeza.

MHE. ABDALLA HAJI ALI: Mheshimiwa Naibu Spika,nakushukuru. Kwa masikitiko tu kidogo kwamba hili sualatunasema ni la Muungano lakini katika majibu ya Naibu Wazirinaona hakutaja upande wa pili hata neno moja, sijui kamatumo au hatumo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawilimadogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Sheria yaMafuta na Gesi ni ya Muungano na hivyo kila nchi inastahikikupata gawio stahiki kutokana na mauzo ya gesi. Je, ni kiasigani cha gawio kilichopelekwa kwa Hazina ya Zanzibar tangumauzo haya ya gesi yafanyike?

Page 72: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

72

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kitaalamtunaambiwa kwamba gesi inayozalishwa Tanzania ni gesi safikabisa, yaani haihitaji gharama kubwa kufanyiwa mchakatokwa matumizi. Sasa tulitegema kwamba umeme unaotokanana uzalishaji kutokana na gesi hii ungekuwa rahisi kwawatumiaji lakini kila siku umeme unapanda bei. Ni kwasababu gani? Ahsante. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi kwa niaba ya Waziri wa Nishati naMadini.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI (K.n.y.WAZIRI WA NISHATI NA MADINI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikweli kama alivyosema kwamba suala la gesi asilia ni sualala Muungano kwa mujibu wa Ibara ya 4 ya Katiba ya Jamhuriya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 na Nyongeza yakwanza ya Katiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu gawio la Zanzibarkutokana na mapato ya gesi ni suala la takwimu, ningeombaniweze kulifanyia kazi halafu niweze kumpatia MheshimiwaMbunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pilikwamba katika hali ya kawaida gesi inatakiwa iwezekuzalisha umeme ambao ni bei rahisi, naomba nimhakikishietu Mheshimiwa Mbunge kwamba huo ndiyo ukweli na tokatuanze kuzalisha umeme kwa kutumia gesi tumeweza kuokoafedha nyingi sana. Kwa mwaka inakadiriwa tunaokoa dolaza Kimarekani bilioni 1.6 ambapo kama tungetumia umemewa kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimweleze tukwamba pamoja na bei ya umeme kuendelea kubadilikabadilika lakini bado itabakia kwamba tokea tumeanzakutumia umeme wa gesi tumeweza kupunguzagharama kubwa sana za fedha tunazotumia katika kuzalishaumeme.

Page 73: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

73

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tumefikamwisho wa kipindi chetu cha maswali na majibu. Nitaletamatangazo tuliyonayo mezani…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mwongozowako…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Jaku nina uhakika hutakikuanza kukumbushwa Kanuni sasa hivi kwa sababu hizo nifujo.

Tutaanza na wageni walioko jukwaa la Spika, wageniwanne wa kwangu mimi kutoka Umoja wa Mabunge Duniani(IPU) Mheshimiwa Win Masiko, huyu ni Mbunge kutoka Bungela Uganda, karibu sana na utupelekee salamu zetu kwaMheshimiwa Spika huko mwanamama matata kabisaMheshimiwa Kadaga. (Makofi)

Tunaye pia mgeni mwingine anaitwa HilaryGbedemah kutoka Ghana, karibu sana. Tunaye pia ProfesaMasheti Masingila kutoka Kenya. (Makofi)

Naona kuna wageni wengine pale lakini sijapatamajina yao. Karibuni sana wageni mliokaa jukwaa la Spika,kwenye Bunge letu. (Makofi)

Tunaye mgeni mwingine ambaye amekaa hapo niMstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Mkoani KlimanjaroMheshimiwa Raymond Robert Mboya, karibu sana. (Makofi)

Tunao pia wageni wa Waheshimiwa Wabunge, kundila kwanza ni wageni 100 wa Mheshimiwa Julius Kalanga Laizerambao ni wanafunzi 90 na Walimu 10 kutoka Mwalimu AnnaEnglish Medium Pre and Primary School, Mkoani Arusha.Karibuni sana. (Makofi)

Tunao pia wageni 40 wa Mheshimiwa ZuberiKuchauka ambao ni wanafunzi wa Liwale High School naWalimu wao kutoka Mkoa wa Lindi. Karibuni sana na

Page 74: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

74

nimepewa taarifa Waheshimiwa Wabunge kwamba hii shulendiyo iliyoongoza kimkoa kwa matokeo mazuri Mkoani Lindi.(Makofi)

Tunao pia wageni wa Mheshimiwa Esther NicholausMatiko ambao ni familia yake wakiongozwa na Nicolson naMaria. Karibuni sana, hawa wameongozana na wadogo zakeambao wanaitwa Marwa na Jessica. (Makofi)

Wageni wengine ni wa Mheshimiwa Shabani Shekilindiambao hawa ni wataalam wa kutafsiri Grafo Gemu ambayoiliuliziwa swali hapo kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili nahawa wanatoka Chuo cha Kumbukumbu ya SebastianKolowa yaani SEKOMU Lushoto. Karibuni sana. (Makofi)

Tunao pia wanafunzi ambao wametembelea Bungekwa ajili ya mafunzo na hawa ni wanafunzi 80 na Walimuwatatu kutoka Bwawani Secondary School ya MkoaniMorogoro, sijui hawa watakuwa wamekaa sehemu gani.Pengine hawakupata nafasi ya kuingia. Karibuni sana wageniwetu.

Waheshimiwa Wabunge ninayo matangazomengine. Tangazo lingine linatoka kwa Manager wa BungeSports Club Mheshimiwa John Kadutu. Mheshimiwa Kadutuanawatangazia Waheshimiwa Wabunge kwamba siku yaJumamosi tarehe 9 Septemba, 2017 Bunge Sports Clubilipigwa mabao mawili kwa moja na timu inayotoka kwaMheshimiwa Spika, Salasala Vison Group – jamani shangilienitimu ya Spika ilishinda. (Makofi)

Naona Waheshimiwa Wabunge mmezoeakushangilia timu ya Bunge Sports Club, safari hii timu yaMheshimiwa Spika ilishinda na hapa Mheshimiwa Kadutuanajaribu kusema kwamba ni kwa sababu Mheshimiwa Spikaaliomba. Mlifungwa tu Waheshimiwa, kubalini kushindwa!(Makofi)

Pia tarehe 10 Septemba, 2017 Bunge Sports Club ilirudikwenye makali yake kwa kuwafunga bila huruma timu ya

Page 75: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

75

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Muungano Veterans ya hapa Dodoma magoli matatu kwabila. Nyota wa mchezo huo alikuwa Mheshimiwa VenanceMwamoto na huyu ni kocha wa timu. (Makofu)

Waheshimiwa Wabunge ninayo hapa taarifa yaMheshimiwa Spika, anapenda kuwajulisha kuwa tarehe 8Septemba, 2017 alipokea taarifa kutoka kwa Kaimu KatibuMkuu wa CUF Mheshimiwa Magdalena Sakaya kuwa katikakikao chao cha tarehe 6 Septemba, 2017 walichaguaviongozi wa Kambi ya Wabunge wa Chama hicho hapaBungeni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Maftaha Abdallah Nachuma atakuwaMwenyekiti; Mheshimiwa Rukia Kassim Ahmed atakuwaKatibu; Mheshimiwa Maulid Said Mtulia atakuwa Mnadhimuna Mheshimiwa Sonia Jumaa Magogo atakuwa MwekaHazina wao. (Makofi)

Hivyo, basi Mheshimiwa Spika, anawatangaziamabadiliko hayo ya uongozi wa Chama cha wananchi (CUF)hapa Bungeni na Mheshimiwa Spika ameahidi ushirikiano wakutosha katika kutekeleza majukumu yao. (Makofi)

Waheshimiwa Wabunge ninalo pia tangazo kutokakwa Makamu Mwenyekiti wa TWPG, Mheshimiwa Suzan Lyimoanatangaza kuwa na miwani ambayo iliachwa wakati wafamily planning seminar ambayo ilikuwa siku ya ijumaa tarehe8, Morena Hotel. Kwa hiyo, aliyepoteza miwaniama aliyesahau miwani amwone Mheshimiwa SuzanLyimo.

Pia yupo Mheshimiwa ambaye alisahau simu yaketarehe 9 kwenye semina ya kuhusu CEDAW ambayo ilifanyikapia Morena, naye aliyesahau simu hiyo amwone MheshimiwaSusan Lyimo atapatiwa hiyo simu yake.

Waheshimiwa Wabunge, baada ya matangazo hayotutaendelea na ratiba iliyo mbele yetu.

MBUNGE FULANI: Mwongozo wa Spika

Page 76: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

76

MWONGOZO WA SPIKA

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kuchauka

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika,asante, nasimama kwa kanuni ya 68(7) naomba mwongozowako kwa kuokoa muda sitoisoma. Naomba mwongozowako kwa sababu kumekuwa na utaratibu kunaleta wagenikuwaona wanafunzi kuja kujifunza lakini wageni hawa maranyingi wamekuwa wakikwama pale mapokezi na matokeoyake wanaingia ukumbini baada ya Spika kuingia. Penginewanachelewa zaidi wanakuja mpaka kipindi cha katikati yamaswali. Sasa naomba mwongozo wako kwa utaratibu hiiile dhana ya wanafunzi hawa kuja kujifunza inakuwa badohaijakamilika.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbarouk.

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Nimesimama kwa kanuni ya 68(7) nikirejea kwenyemajibu ya Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Olenasha akijibu swalila nyongeza kutoka swali namba 62 alizungumza kwambaSerikali imeanzisha Benki ya Wakulima, mimi nashukuru na hiloni jambo jema.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba mwongozowako kuna tatizo linalojitokeza katika mabenki au taasisi zafedha hazikubali hatimiliki za vijiji ambazo wanazo wananchiwetu wa kule vijijini ambao ni wakulima akinamama, vijanana wazee. Sasa hizo hatimiliki za mila hazikubaliki lakiniamewahamisisha hapa vijana wajiunge katika shughuli zakilimo kwa kuwa Watanzania wengi wamenufaika. Sasanaomba mwongozo wako, watanufaika vipi hali ya kuwahata hiyo mikopo yenyewe hatimiliki za kimila walizokuwanazo hazikubaliki na taasisi za fedha? Ahsante.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Jaku.

MHE. JAKU HASHIM JAKU: Mheshimiwa Naibu Spika,nimesimama kwa kanuni ya 68(7) nafikiri haina haja ya kutaka

Page 77: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

77

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

kuisoma ili kupoteza muda wako. Hoja zangu zilikuwa ni mbili.Kumetokea kitendo hapa ambacho kinawezakutugombanisha na Rais wetu, hasa back bencher wa Bunge.

Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha alipokuwa akijibuswali alisema tumuunge mkono Mheshimiwa Rais.Kinachoonekana kwa Mawaziri na Manaibu Mawaziri maranyingi huwa akijibu hapa hatumuungi mkono. Kwa maanahiyo sisi back bencher humu hatumuungi mkono, ni kitu chakusikitisha sana na kinatugombanisha na wapiga kura wetu.Nahitaji mwongozo wako hapo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili la kibinadamu zaidina ubinadamu huo umeonesha wewe ulipotoa garikumuhudumia Mheshimiwa Tundu Antipas Lissu, Mbunge waSingida Mashariki kumpeleka hospitali umeoneshaubinadamu mkubwa wa hali ya juu, gari ya familia yakonikupongeze kwa hilo. Pia nimpongeze sana MheshimiwaWaziri wa Afya na Mheshimiwa Mwigulu Nchemba kwakuonyesha ubinadamu wao bila kujali itikadi ya vyama nahuu ndio ubinadamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu, hili ni lakibinadamu zaidi ulifikiri na ubinadamu wenyewe umeanzakuonyesha wewe na hata sisi Wabunge katika posho zetukukatwa. Ningeomba tu ili kutaka kujua hali ya mgonjwaukateua watu kama watatu au wanne kwenda kuangaliahali ya Mheshimiwa Tundu Antipas Lissu Mughwai ili kuridhiakibinadamu hili nafikiri halitotaka muda, hili ni la kibinadamu,halimo katika kanuni zetu ni ungwana zaidi. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Musukuma.

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika,nikushukuru sana na mimi nasimama kwa kanuni ya 68(7).Wakati Waziri wa Afya akijibu swali hapo la MheshimiwaMagereli, amerudia mara mbili kauli ambayo kiukweli sisiwanaume haijatuweka kwenye mazingira mazuri.Amezungumza naomba kunukuu kwamba “anawaombawanawake wote wawalazimishe wanaume wao waende

Page 78: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

78

kunywa dawa za ARV’s, sasa ni wanaume wote na wazimaau wanaume wanaoumwa, nataka tu mwongozo wako.(Kicheko)

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Naibu Spika,asante, napenda kutumia kanuni juu ya jambo lililotokea leona linalotokana na taarifa ambayo umetusomea hapainayotokana na maagizo ya Spika, kwamba isomwe hapa.Katika taarifa hiyo, umeeleza kwamba kuna uongozi mpyawa Kambi ya Upinzani CUF ndani ya Bunge ambayoumetusomea orodha yake lakini sisi tunajua kwamba tunauongozi rasmi wa Kambi ambao tuliuchagua kwa kura nawakati huo tukiwa watu 42 tukapiga kura na uongozi huohaujaezuliwa kwa njia yoyote.

Mheshimiwa Naibu Spika, na juzi tulichaguamwenyekiti wetu kwa sababu Bi. Riziki hayupo tukamchaguabwana Abdallah Mtolea kuwa Mwenyekiti na piatukamchagua Mweka Hazina wetu mwingine na hatuailiyofuata ilikuwa ni kuliarifu Bunge. Mwongozo wangu natakakujua hivi nani anayeamua uongozi wa chama, walio wengiau walio wachache? Je, tokea lini Bunge hili ndani yakekukawa na uongozi mbili bila ule mwingine kuondoka,kujiuzulu au kuvuliwa madaraka? Naomba mwongozo wako.(Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nimeombwamiongozo kadhaa hapa. Wa kwanza ni mwongozouliyoombwa na Mheshimiwa Kuchauka ambaye ametoamaelezo kwamba, wako wageni ambao huwa wanakwamasehemu za kuingilia magetini na hivyo kuchukua muda mrefupale na kukuta humu Bungeni wakati mwingine wanaingiaMheshimiwa Spika, akiwa ameshaingia.

Kimsingi hili ni jambo ambalo linatakiwa kufanyiwa kazikiutawala kuliko kutolewa mwongozo na kiti kwa sababu zilekanuni nadhani tutafika mahali mtu akitaka kusimama nayoaisome yeye mwenyewe kwanza, kwa sababu jambounaloliombea mwongozo unataka kujua kama linaruhusiwahumu ndani au haliruhusiwi ndio unataka mwongozo wa Kiti.

Page 79: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

79

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Sasa jambo hilo haliko kwenye eneo hilo, kwa hiyoniseme na watu wa Katibu wako hapa mezani,watampelekea ujumbe wako Mheshimiwa Kuchauka lakinisi jambo linalohitaji kutolewa mwongozo na kiti.

Nimeombwa pia mwongozo na MheshimiwaMbarouk Mussa akitoa maelezo kwamba wakati likijibiwaswali la 62 Mheshimiwa Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo naUvuvi alitoa maelezo ya kuanzishwa kwa benki ya wakulima.Yeye anasema tatizo lipo kwamba benki zinakataa hati milikiza kimila sasa, hawa watu watanufaika vipi na mikopo kutokakwenye hiyo benki.

Mambo mawili, la kwanza, Mheshimiwa Spikaalishawahi kutoa maelekezo hapa ama mwongozo hapakwamba namna maswali yalivyojibiwa, mtu anayewezakuwa na hoja na swali hilo ni yule aliyeuliza swali. Kwa hiyo,huo ni upande mmoja.

Upande wa pil i kwamba jambo hil i kwambalinaruhusiwa ama haliruhusiwi humu ndani mabenki siyoambayo yako humu ndani. Kwa hiyo, kwa kuwa hilo jambohatushughuliki nalo hapa ndani sitalitolea mwongozo, lakininaamini Waziri kwa namna ulivyoeleza amepata taarifa hiyokwamba hati za kimila zinakataliwa na yeye ataona namnabora ya kushauriana na hiyo benki iliyo chini ya Wizara yake.

Mheshimiwa Jaku na yeye ametoa maelezo kuhusumajibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipangokwamba alipokuwa akitoa maelezo ya maswali yaliyoulizwaalikuwa akisisitiza kwamba tumuunge mkono MheshimiwaRais na juhudi zake za kukusanya kodi na mambo mengineambayo aliyaeleza ambayo sitaki kuyarudia.

Kwa maelezo ya Mheshimiwa Jaku, anaona maelezokama hayo ni kana kwamba humu ndani Mawaziri pekeendio wanaomuunga mkono Mheshimiwa Rais, lakini walewanaouliza maswali ambao Mheshimiwa Jaku anasema niback benchers wao ni kana kwamba hawamuungi mkonoRais kwa kuuliza maswali.

Page 80: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

80

Niseme hivi, hizi ni lugha za kawaida wala hazina lengola kugombanisha na hata namna alivyolizungumzaMheshimiwa Naibu Waziri sidhani kama alimaanisha kwambahaungwi mkono, alimaanisha kwamba twende pamojakatika mambo haya na kumwelewa majibu aliyokuwaakiyatoa hapa mbele. (Makofi)

Ametoa maelezo tena kwa namna nyingine kwamba,kiti kitoe mwongozo kufanya jambo la kibinadamu la kuteuaWabunge kwenda kumwona Mheshimiwa Tundu Lissu kulealikolazwa. Nimtaarifu tu Mheshimiwa Jaku pengine anawezakuwa hana taarifa, lakini Mheshimiwa Lissu kule aliko yuko naMheshimiwa Freeman Mbowe ambaye ni Mbunge, yuko piana Mheshimiwa Msigwa naye ni Mbunge. Kwa hivyo,Mheshimiwa Spika anapata taarifa kutoka kwa hao waliokohuko na kama ambavyo mlishataarifiwa kwa maelezo marefusana aliyotoa Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mboweanawasiliana naye, kwa hiyo, tusipate wasiwasi wowote.

Nimeombwa pia mwongozo na MheshimiwaMusukuma, kuhusu msisitizo aliotoa Mheshimiwa Waziri waAfya kwamba kina mama ambao wao kwa asilimia kubwana ametaja nadhani zaidi ya 70 kwamba wao wanakunywadawa, maana yake ni wale walioathirika ndio wanaokunywadawa. Sasa akasema wale akinamama wawasaidie waumezao ili na wao wanywe dawa.

Kwahiyo, Mheshimiwa Musukuma usitie shaka, walewaliopima kama mama amepima na anatumia dawa amawameenda wote wamepima wanapaswa kutumia dawahalafu mama anatumia yeye hatumii, huyu mama ninauhakika hataki kubaki mjane. Kwa hiyo, Mheshimiwa Wazirialikuwa anasisitiza tu kwamba ili mama asibaki mjane basiamsaidie na aweze kunywa hizo dawa, lakini pengineMheshimiwa Waziri kwa hizo takwimu ulizotoa sina hakikakama na humu Bungeni zinahusika, labda utusaidie hichokipimo ili na sisi tupime humu halafu tuone namna bora yakuweza kwenda nalo hilo, ili tuone takwimu zetu zinaendavipi. (Makofi)

Page 81: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

81

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Nimeombwa pia mwongozo na Mheshimiwa AllySaleh kuhusu taarifa niliyoisoma ya Mheshimiwa Spika, kuhusuuongozi wa Kambi ya CUF. Mheshimiwa Ally Saleh ametoamaelezo ambayo nisingependa kuyarudia lakini kimsingianataka kujua nani anaamua uongozi, ni wengi amawachache. Waheshimiwa Wabunge Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni tunawajua viongozi wake, lakini pamoja nakwamba kuna Kambi Rasmi, vyama pia vinakuwa na uongoziwao.

Sasa uongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) ndiowanaoulizia Mheshimiwa Ally Saleh na kwamba taarifa yaMheshimiwa Spika imetaja viongozi ambao yeye anafahamuviongozi wengine ambao wamechaguliwa. Sasa kwamaelezo aliyotoa ni kwamba pengine kwamba taarifa zakikao hiki Chama cha CUF inavyoonekana kina makundimawili, kundi moja limefanya uchaguzi bado halijamtaarifuSpika, kundi moja limefanya uchaguzi limemtaarifu Spika.

Mheshimiwa Ally Saleh naona unapunga mkono namaelezo uliyoyatoa mwenyewe, ukinitaka niitishe hansardnitaita. Umesema hivi, tumefanya kikao, tulikuwa katikamchakato wa kutaka kumweleza Mheshimiwa Spika, sasa hilolina tofauti na hili ninaloeleza mimi hapa, kwa hiyo, tuliakidogo.

Sasa Waheshimiwa wabunge hii taarifa imesomwakama ilivyoletwa hapa mezani. Mambo yaliyoko kwenyekambi mahususi ya Chama cha Wananchi (CUF), mimi naonaninyi mtakapofikia mahali ambapo mnataka kuzungumza naSpika na kuona uongozi ni upi mtafanya hivyo, lakini Bungehili hatutaweza kuanza kujadili jambo hilo sasa hivi. (Makofi)

Kwa hivyo, niwaombe kama ambavyo taarifa hiiimekuja naamini hata hiyo nyingine Mheshimiwa Spikaatakavyoamua italetwa hapa. Kwa hivyo, siwezi kulielezeajambo hilo kwamba linaruhusiwa ama haliruhusiwi hapandani kwa sababu chaguzi za ndani ya CUF hazijafanyikahapa ndani. (Makofi)

Page 82: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

82

Waheshimiwa Wabunge, nimeletewa tangazo linginehapa na Mheshimiwa Maulid Mtulia anasema ana wageniwake hapa ambao wametokea Dar es Salaam wakiongozwana Dkt. Jamal Adam Katundu, karibuni sana.

Kwa hiyo, baada ya hapo, tutaendelea na ratibayetu. Katibu.

NDG. ASIA MINJA- KATIBU MEZANI:

HOJA ZA SERIKALI

MAAZIMIO

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba (IntergovernmentalAgreement – IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri yaMuungano wa Tanzania na Serikali ya Jamuhuri ya

Uganda kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bomba laKusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki

(East Africa Crude Oil Pipeline – EACOP)kutoka Hoima (Uganda) hadi

Tanga (Tanzania)

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO(K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa NaibuSpika, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwakutujalia uzima na kutuwezesha kuwepo hapa Bungeni leotukiendelea kutekeleza majukumu yetu. Aidha, nakupongezakwa namna ambavyo wewe Mheshimiwa Naibu Spika naMheshimiwa Spika, mnavyoliongoza na kuliendesha Bungehili mkisaidiwa na Wenyeviti.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jamhuri ya Muungano waTanzania na Jamhuri ya Uganda ni Nchi Wanachama waJumuiya ya Afrika Mashariki iliyoundwa tarehe 30 Novemba,1999 ambayo malengo yake ni pamoja na kuimarishaushirikiano kati ya Nchi Wanachama kwenye maeneo yakisiasa, kiuchumi, kijamii, kiteknolojia, utafiti, ulinzi na masualaya kisheria.

Page 83: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

83

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya 101(1) ya mkatabakuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki inahamasishaNchi Wanachama kushirikiana katika utafiti, uendelezaji nautumiaji wa rasilimali mbalimbali za nishati zilizomo katikaukanda wa Afrika Mashariki. Vilevile Ibara ya 101(2)(a) yamkataba huo inasisitiza kuhusu ushirikiano katika ujenzi wamabomba ya usafirishaji wa mafuta na gesi asilia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Jamhuri yaUganda kupitia kampuni za kimataifa za TOTAL, TULLOW naCNOOC iligundua kuwepo kwa mafuta ghafi takribanimapipa bilioni 6.5 katika eneo la Albetini nchini Uganda.Kufuatia ugunduzi huo Serikali ya Uganda ilianza kutafuta njiaya kusafirisha mafuta hayo kwa njia ya bomba (PipelineRoute) kutoka eneo la Kabale, Nchini Uganda kwendakwenye Soko la Kimataifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuchambua njia yaBomba Serikali ya Uganda iliainisha njia takribani tatu,ikiwemo ile ya kutoka Hoima Nchini Uganda hadi Bandari yaTanga, Nchini Tanzania; mchakato na majadilianombalimbali baina ya Serikali ya Uganda nan chi nyingine zaJumuiya ya Afrika Mashariki, ikiwemo Tanzania, yalifanyikakutathmini njia bora ya kusafirisha mafuta hayo kwendakatika soko la Kimataifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo tarehe 22 hadi 24Aprili, 2016 Mawaziri wanaosimamia masuala ya Nishatikutoka Nchi za Uganda, Kenya na Tanzania walikutana JijiniKampala kwa ajili ya kuhitimisha mazungumzo kuhusu njiaitakayotumika kutekeleza mradi huo. Mkutano wa Mawaziriulifuatiwa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Uganda, Kenya,Rwanda, Tanzania na Sudan Kusini kuhusu ushoroba waKaskazini (Nothern Corridor Intergration Projects) uliofanyikatarehe 23 Aprili, 2016.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mkutano huo Rais waJamhuri ya Uganda, Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni,alitangaza rasmi kuwa njia ya kutoka Kabale, Uganda kupitiaMikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida,

Page 84: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

84

Dodoma, Manyara hadi Bandari ya Tanga, Tanzania, ndionjia iliyochaguliwa na Serikali ya Uganda katika ujenzi wamradi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi yaliyogunduliwaNchini Uganda kwenda kwenye soko la Kimataifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia hatua hiyo, tarehe26 Mei, 2017, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniana Jamhuri ya Uganda zilisaini Mkataba wa Kimataifa waMradi wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki(The Inter-Governmental Agreement between the UnitedRepublic of Tanzania and the Republic of UgandaConcerning The Pipeline System of The East African CrudeOil Pipeline Project).

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya Serikali ya Ugandakuchagua njia ya bomba la mafuta kupitia nchini Tanzaniana kisha kusainiwa kwa mkataba huu isingefanikiwa kamasio juhudi, umahiri na uongozi thabiti wa Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John PombeJoseph Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Watanzanianapenda kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Raiskwa kufanikisha kutekelezwa kwa mradi huu mkubwa wakimataifa. Aidha, nawapongeza Mawaziri, Makatibu Wakuuna Wataalam wote walioshiriki kufanikisha hatua hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Bomba la MafutaGhafi la Afrika Mashariki utajumuisha ujenzi wa bomba lamafuta ghafi lenye urefu wa kilometa 1,445 ambapo kati yahizo kilometa 1,149 zitakuwa upande wa Tanzania na kilometa299 zitakuwa upande wa Uganda. Bomba hilo litakuwa nakipenyo cha sentimeta 24 na litakuwa na uwezo wakusafirisha mapipa ya mafuta ghafi 216,000 kwa siku nalitapita katika mikoa minane, wilaya 24 na vijiji vipatavyo 124vya Tanzania Bara. Ujenzi wa bomba hilo unatarajiwakugharimu takribani Dola za Kimarekani bilioni 3.5.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkataba huuumegawanyika katika Sehemu kuu Nne, ambapo Sehemu

Page 85: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

85

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

ya Kwanza ambayo inahusisha Ibara ya kwanza (1), inawekamasharti ya kuhusu ufafanuzi na tafsiri ya manenoyaliyotumika katika mkataba huo, utaratibu wa kuanzakutumika na kuridhiwa kwa mkataba pamoja na mashartimengine ya utangulizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya 1(2) (b), inazitakakila nchi mwanachama kuanza mchakato wa kuridhiamkataba huu ndani ya siku 30 tangu kusainiwa kwa mkataba.Aidha, Ibara ya 1(3) inaweka masharti kuwa kila nchimwanachama itatunga sheria wezeshi ya mradi kwa ajili yautekelezaji wa mkataba huu iwapo zitaona inafaa. Ibara ya1(8) inaweka masharti kuwa, kila nchi mwanachama itaingiamkataba na kampuni ya mradi wa bomba (Host GovernmentAgreement – HGA) kwa kuzingatia masharti ya mkataba huuna masharti mengine ambayo itaona yanafaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sehemu ya Pili ya Mkatabainaweka masharti kuhusu wajibu wa jumla (GeneralObligations) kwa nchi wanachama na inaanzia Ibara ya pili(2) hadi Ibara ya 15 kama ifuatavyo:-

(i) Ibara ya pili (2) inaweka masharti kuhusuushirikiano baina ya nchi wanachama zitakazotekeleza mradihusika. Aidha, Ibara hii inaitaka kila nchi kuanzisha Kamati yaMashauriano ambayo itakuwa ni chombo cha kubadilishanataarifa na kushauriana juu ya masuala ya mkataba huupamoja na mradi wenyewe. Vilevile Ibara hii inaeleza namnanchi wanachama zitakavyoshirikiana pamoja na kampuni yamradi kukagua mradi na kubadilishana taarifa kuhusu ukaguzihusika.

(ii) Ibara ya tatu (3) inaainisha masharti kuhusuHaki za Ardhi. Kwa mujibu wa Ibara hii kila nchi mwanachamaitatoa ardhi kwa kampuni ya mradi wa bomba kwa kuzingatiasheria, kanuni na taratibu za nchi husika. Aidha, Ibara hiiinazitaka nchi wanachama kuzingatia Sheria za Nchi na zaKimataifa katika ulipaji wa fidia kwa wananchi na kuhakikishawananchi na wadau wote wanaohusika katika ulipaji wa fidiawanashirikishwa. (Makofi)

Page 86: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

86

(iii) Ibara ya nne (4) na tano (5) zinaweka mashartiyanayoiruhusu Jamhuri ya Uganda kupitisha mafuta ghafinchini Tanzania kwa kutambua kuwa, Jamhuri ya Ugandahaina bahari (Land Locked) na kwa kuzingatia Mkataba waUmoja wa Mataifa kuhusu Sheria ya Bahari, mwaka 1982 (TheUnited Nations Convention The Law of The Sea). Aidha, kilanchi mwanachama imepewa wajibu wa kuchukua hatuamuhimu na kutoa vibali vinavyotakiwa. Ibara hiyo, imeainishamasharti ya kuhusu kutoathiri shughuli za mradi (NonInterruption of Project Activities).

(iv) Ibara ya sita (6) inaainisha masharti kuhusuulinzi na usalama. Kila nchi mwanachama imepewa jukumuna wajibu wa kuhakikisha kuwepo kwa ulinzi na usalama wamiundombinu ya mradi husika kwa kuzingatia sheria za nchihusika na misingi ya haki za binadamu.

(v) Ibara ya saba (7) inaweka masharti kuhusumasuala ya fedha za kigeni (Foreign Exchange) ambapo kilanchi mwanachama itatoa na kuongeza vibali vya mradi kwakampuni kuhusiana na fedha za kigeni na masuala muhimuya shughuli za mradi.

(vi) Ibara ya nane (8) inaainisha masharti kuhusuuhuru wa uingizaji au uingiaji wa watu na uingizaji wa bidhaana huduma (Freedom of Movement of Person, Goods andServices) baina ya nchi wanachama kwa ajili ya utekelezajiwa mradi kwa kuzingatia sheria za nchi husika na mipangoya ushiriki wa wazawa na ununuzi wa bidhaa na huduma zandani (National Content Plans).

(vii) Ibara ya tisa (9) inaeleza kuhusu ushiriki wawazawa na ununuzi wa bidhaa na huduma za ndani(National Content). Ibara hii inazitaka nchi wanachama kwakushirikiana na kampuni ya mradi wa bomba kuandaampango wa kuwawezesha wazawa na makampuni ya ndanikushiriki katika mradi (National Content Plan).

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango huo utahakikishakuwa mradi unatumia bidhaa na huduma mbalimbali

Page 87: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

87

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

pamoja na rasilimali watu kutoka nchi husika. Aidha, kampuniya mradi itatakiwa kutoa mafunzo ya kitaalam kuhusuuendeshaji wa bomba la kusafirisha mafuta na kuhamasishaujuzi wa kiufundi, kuhamisha ujuzi wa kiufundi (Transfer ofTechnology) kwa wazawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, mpango huo utapaswakuonesha fursa zilizopo kwenye mradi kwa kuzingatia ratibaya utekelezaji katika kipindi cha ujenzi na uendeshaji iliwazawa waweze kufahamu fursa mbalimbali zilizopo kwenyemradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, endapo bidhaa au hudumazinazohitajika hazipatikani katika nchi wanachama basi,kampuni ya mradi wa bomba itaruhusiwa kutumia mzabuniwa nje kwa kigezo kuwa mzabuni huyo anahusisha wazawakatika utekelezaji wa shughuli husika, ili kuwajengea uwezo.

(viii) Ibara ya 10 inaipatia kampuni ya mradi hakiya kumiliki mafuta ghafi katika mradi wa bomba (Title andOwnership of Petroleum in the EACOP System).

(ix) Ibara ya 11 inaainisha masharti kuhusumuundo, umiliki na uendeshaji wa mradi. Ibara hii pamojana mambo mengine inaelekeza kuwa mradi wa bombautaanzishwa na kuendeshwa na sekta binafsi kupitia kampunimaalum ya mradi. Kampuni hiyo, inaundwa na wanahisa nakutoa fursa kwa Serikali zote mbili au taasisi zake kuwa nahisa katika kampuni hiyo. Aidha, kila mwanahisa atawajibikakugharamia hisa zake kwa mujibu wa mkataba wa wana-hisa utakaoingiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara hii pia, inatoa fursakwa Serikali ya Tanzania kufanya majadiliano na kampuni yamradi wa bomba kuhusu uendeshaji wa Bandari ya Tangakatika eneo la Chongoleani.

(x) Ibara ya 12 inatoa fursa kwa nchi wanachamakutumia bomba hilo endapo kutakuwa na ugunduzi wamafuta katika maeneo mengine. Vilevile Ibara hii inatoa fursa

Page 88: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

88

kwa nchi jirani kutumia bomba hilo kusafirisha mafuta kwakuzingatia vigezo vitakavyowekwa kwenye Mkataba waHGA.

(xi) Ibara ya 13 inaweka masharti kuhusu vibali naleseni zitakavyotolewa na nchi wanachama katika utekelezajiwa mradi wa bomba.

(xii) Ibara ya 14 inaainisha masharti yanayozitakanchi wanachama kutotaifisha uwekezaji au mali za mradi wabomba (Expropriation). Hata hivyo, Ibara hiyo inatoa fursakwa nchi wanachama kutaifisha mali za mradi wa bombaiwapo itakuwa ni kwa manufaa ya umma na kwa kuzingatiasheria, kanuni na taratibu za nchi husika.

(xiii) Ibara ya 15 inaweka masharti kuhusu masualaya mazingira, jamii, usalama kazini, viwango vya kiufundi nahaki za wafanyakazi. Aidha, Ibara hii inazitaka nchiwanachama kushirikiana na kuhakikisha kwamba, kampuniya mradi inaendesha shughuli zake kwa kuzingatia sheria zanchi husika pamoja na Sheria za Kimataifa zinazohusumasuala ya mazingira, usalama wa watu, uendeshaji wamitambo na haki za wafanyakazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sehemu ya Tatu yaMkataba inahusisha Ibara ya 16 ambayo inaainisha mashartikuhusu mfumo wa kodi (Fiscal Regime). Ibara hii inaelezakuwa, mfumo wa kodi katika mradi huu utakuwa kwa mujibuwa sheria za kodi za nchi mwanachama, kama ilivyoainishwakatika kiambatisho Na. 2 cha mkataba huu. Kiambatishohicho kimeweka misingi ya uainishaji (Harmonization) wamasuala mbalimbali ya kikodi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sehemu ya Nne, inaainishamasharti ya jumla ya mkataba (Financial Provisions) nainahusisha Ibara ya 17 hadi Ibara ya 26. Masharti hayo nipamoja na:-

Uhai wa Mkataba (State Succession) Ibara ya 17;kushindwa kutekeleza mkataba kutokana na sababu

Page 89: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

89

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

zisizozuilika yaani force majeure, Ibara ya 18; utatuzi wamigogoro, Ibara ya 19; sheria inayoongoza mkataba, Ibaraya 20; marekebisho ya mikataba na kupokea wanachamawapya (Subsequent Modification and Accessionn), Ibara ya21; ukiukwaji wa masharti ya mkataba, Ibara ya 22; mudawa mkataba, Ibara ya 23; kusitisha mikataba ya utekelezajiwa mradi, Ibara ya 24; hifadhi, lugha na viambatishovya mkataba (Reservation, Language and Annexes),Ibara ya 25; na uwasilishaji na usajili mkataba, Ibara ya26.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Masharti ya Utatuziwa Migogoro itakayojitokeza wakati wa utekelezaji wamkataba huu, Ibara ya 19 inaainisha kuwa mgogoro wowoteutatatuliwa kwanza kwa njia za kidiplomasia na nchiwanachama kupitia Kamati ya mashauriano na kwamba,iwapo muafaka hautafikiwa mgogoro husika utafikishwakatika Baraza la Usuluhishi kwa mujibu wa Kanuni zaUsuluhishi za Mahakama ya Haki ya Jumuiya ya AfrikaMashariki.

Mheshimiwa Naibu Spika, Baraza hilo litakaa sehemuambayo nchi wanachama watakubaliana. Endapo nchiwanachama zitashindwa kukubaliana basi, baraza hilolitakaa London, Uingereza.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya maelezo hayo,sasa naomba kuwasilisha Azimio la Bunge la KuridhiaMkataba wa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba laMafuta Ghafi la Afrika Mashariki kati ya Serikali ya Jamhuri yaMuungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Uganda(Inter-governmental Agreement between United Republic ofTanzania and Republic of Uganda Concerning The PipelinesSystem of The East Africa Crude Oil Pipeline Project (EACOPProject) kama ifuatavyo:-

KWA KUWA, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naJamhuri ya Uganda ni Nchi Wanachama wa Jumuiya yaAfrika Mashariki.

Page 90: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

90

NA KWA KUWA, Ibara ya 101(1) ya Mkataba waKuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki inahamasishanchi wanachama kushirikiana katika utafiti, uendelezaji nautumiaji wa rasilimali mbalimbali za nishati zilizomo katikaUkanda wa Afrika Mashariki na Ibara ya 101(2)(e) ya Mkatabahuo inasisitiza ushirikiano katika ujenzi wa miundombinu yausafirishaji wa mafuta na gesi asilia;

NA KWA KUWA, jamhuri ya Muungano wa Tanzaniana Jamhuri ya Uganda zimeanza kushirikiana katika ujenziwa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadiTanga, Tanzania;

NA KWA KUWA, katika Mkutano wa Kumi na Tatu waWakuu wa Nchi za Afrika Mashariki kuhusu ushoroba waKaskazini (13th Summit of The Nothern Corridor IntergrationProjects) uliofanyika Kampala, Uganda tarehe 23 Aprili, 2016pamoja na mambo mengine ilikubaliwa kuwa bomba lamafuta ghafi litajengwa kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga,Tanzania;

NA KWA KUWA, katika utekelezaji wa maamuzi yamkutano huo tarehe 26 Mei, 2017 Jamhuri ya Muungano waTanzania na Jamhuri ya Uganda zilisaini Mkataba waKimataifa wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi laAfrika Mashariki (Inter-governmental Agreement between theUnited Republic of Tanzania and the Republic of UgandaConcerning The Pipelines System of The East African CrudeOil Pipeline Project);

NA KWA KUWA, Mkataba huo umetambua nakuzingatia Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Sheria yaBahari wa 1982 (The UN Convention on The Law of The Sea)ambao unazipatia nchi zisizokuwa na bahari (Land Locked)haki ya kupitisha watu, mizigo, bidhaa na kutumia njia yausafirishaji kupitia nchi zenye bahari;

NA KWA KUWA, Ibara ya 1(2)(b) ya Mkataba waKimataifa wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la

Page 91: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

91

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

Afrika Mashariki inaelekeza kuwa Mkataba huo utaanzakutumika baada ya kuridhiwa kwa mujibu wa sheria nataratibu za nchi wanachama;

NA KWA KUWA, kutokana na Mkataba huu Jamhuriya Muungano wa Tanzania itanufaika kama ifuatavyo:-

(a) Kuongezeka kwa mapato ta Serikali kutokanana kodi za zuio na kodi ya mapato ya kampuni zitakazotozwawakati wa ujenzi na uendeshaji wa mradi.

(b) Kuongezeka kwa mapato ya Serikali kwatakribani Dola za Kimarekani 12.2 kwa pipa la mafuta ghafi,litakalosafirishwa kupitia Bandari ya Tanga kulingana nakiwango cha hisa za Serikali ya Jamhuri ya Muungano waTanzania.

(c) Kuongezeka kwa mapato ya Serikali kupitiaBandari ya Tanga wakati wa ujenzi na uendeshaji wamradi.

(d) Kuimarika kwa huduma mbalimbali katikaBandari ya Tanga kutokana na shughuli za mradi namiundombinu itakayojengwa kwa ajili ya mradi huo ikiwemobarabara.

(e) Kuimarika kwa mahusiano ya kidiplomasia,ulinzi na usalama kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniana Jamhuri ya Uganda pamoja na Nchi za Jumuiya ya AfrikaMashariki kwa ujumla.

(f) Kuchochea shughuli za kiuchumi na kibiasharakwa jamii katika maeneo ambapo bomba la mafuta ghafilitapita.

Page 92: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

92

(g) Kuongezeka kwa fursa za ajira kwaWatanzania ambapo takribani watu 10,000 wataajiriwawakati wa ujenzi na ajira zipatazo 1,000 wakati wa uendeshajiwa mradi.

(h) Kuongezeka kwa uwekezaji wa nje (ForeignDirect Investiment) nchini.

(i) Kuchochea shughuli za utafutaji mafutanchini, hususan katika maeneo ya Ziwa Eyasi na ZiwaTanganyika.

(j) Kutumika kwa mkuza wa bomba kujengamiundombinu mingine, bomba la kusafirisha gesi asilia nakadhalika litakalowezesha kufunguka kwa ushoroba waKaskazini (Nothern Corridor) wa biashara, hususan katika Nchiza Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia yaKongo na Sudani Kusini.

(k) Kuimarika kwa uwezo na uzoefu waWatanzania kushiriki katika masuala ya majadiliano, ujenzina uendeshaji wa miradi ya mabomba ya kusafirisha mafuta.

HIVYO BASI, kwa kuzingatia yatokanayo na mkatabahuu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa mujibuwa Ibara ya 63(3)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano waTanzania ya Mwaka 1977, Bunge la Jamhuri ya Muunganowa Tanzania katika Mkutano wa Nane linaombwa kutafakarimapendekezo yaliyomo katika Azimio hili na KuazimiaKuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa ujenzi waBomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (Inter-governmental Agreement between the United Republic ofTanzania and the Republic of Uganda Concerning ThePipeline System of The East African Crude Oil Pipeline Project).

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja.(Makofi)

Page 93: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

93

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.

(Hoja ilitolewa iamuliwe)

NAIBU SPIKA: Hoja imeungwa mkono, tutaendeleana utaratibu wetu, sasa nimwite Mwenyekiti wa Kamati yaKudumu ya Bunge ya Nishati na Madini. Mheshimiwa DeoNgalawa kwa niaba ya Mwenyekiti.

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA MAKAMU MWENYEKITIWA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI:Mheshimiwa Naibu Spika, ifuatayo ni taarifa ya Kamati yaKudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Azimio la BungeKuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzi waBomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki, kati yaSerikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali yaJamhuri ya Uganda (Inter-governmental Agreement Betweenthe United Republic of Tanzania and the Republic of UgandaConcerning the Pipeline System of the East African Crude OilPipeline Project).

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya53(6)(b) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016,naomba kuwasilisha Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bungeya Nishati na Madini, kuhusu Azimio la Bunge la KuridhiaMkataba wa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzi la Bomba laKusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki kati ya Serikali yaJamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri yaUganda (Intergovernmental Agreement Between the UnitedRepublic of Tanzania and the Republic of UgandaConcerning the Pipeline System of the East African Crude OilPipeline (EACOP) Project).

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa fasili ya (9)ya Kanuni ya 6, ikisomwa pamoja na fasili ya 1(b) ya Kanuniya 7, katika Nyongeza ya Nane ya Kanuni za Kudumu zaBunge, Toleo la Januari, 2016, Kamati ya Kudumu ya Bungeya Nishati na Madini, inalo jukumu la kushughulikia Miswada

Page 94: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

94

ya Sheria na Mikataba inayopendekezwa kuridhiwa na Bungeiliyo chini ya Wizara ya Nishati na Madini.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, kwa kuzingatiamasharti ya Kanuni ya 53(3) ya Kanuni za Bunge, uliletakwenye Kamati ya Nishati na Madini hoja ya Serikali kuhusuBunge kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzila Bomba la Kusafirishia Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki katiya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikaliya Jamhuri ya Uganda (Inter-governmental AgreementBetween the United Republic Of Tanzania and the RepublicOf Uganda Concerning The Pipeline System of the East AfricanCrude Oil Pipeline Project), ili Kamati iweze kuishughulikia.

Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 4 Septemba, 2017,Kamati ilikutana katika Ukumbi wa Utawala Kuu, Chuo kikuucha Dodoma (UDOM) na kupata maelezo ya Serikali kuhusupendekezo la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Mradi waUjenzi wa Bomba la Kusafirishia Mafuta Ghafi la AfrikaMashariki kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano waTanzania na Serikali ya Jamhuri ya Uganda.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati ilipotekeleza jukumulake kuhusiana na hoja hii, ilizingatia masharti ya Kanuni ya117(8) na 117(9) kuhusu utaratibu wa Kamati pamoja nakuwaalika wadau. Katika hatua hii, Kamati iliwaalika wadaukwa ajili ya kupata maoni yao. Hata hivyo, kutokana na ufinyuwa muda ambao Kamati ilikuwa nao katika kushughulikiahoja hii, wadau wengi hawakuweza kuwasilisha maoni yaona hata ambao waliweza kuwasilisha, waliwasilisha kwa njiaya maandishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati inaishukuru sanaTaasisi ya Utawala wa Maliasil i (Natural ResourcesGovernance Institute) kwa maoni ya msingi iliyowasilishakwenye Kamati ambayo yametoa mchango mkubwa sanakatika kujadili Azimio hili. Nafurahi kutamka kuwa utaratibuhuu wa kuwaalika wadau kutoa maoni yao kuhusu hojainayoshughulikiwa na Kamati, ni wa msingi na ni muhimu kwajamii ya kidemokrasia kama Tanzania. Aidha, ni utaratibu

Page 95: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

95

unaolisaidia Bunge kuendelea kudhihirisha kwamba nichombo halisi cha uwakilishi wa wananchi chenye jukumula kukidhi matarajio yao wakati wa mchakato wa kuridhiamikataba ya kimataifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mambo ya msingiyaliyozingatiwa na Kamati. Ili kuliwezesha Bunge kutekelezamadaraka yake ipasavyo kwa mujibu wa Ibara ya 63(3)(e)ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka1977, Kamati ilizingatia mambo mbalimbali muhimu katikauchambuzi wa hoja hii ya Serikali ambayo leo tunawasilishataarifa yake. Baadhi ya mambo hayo ni pamoja na:-

Kuangalia Katiba ya Jamhuri ya Muungano waTanzania, sheria za nchi zinazohusiana moja kwa moja namaudhui ya mkataba unaopendekezwa, pamoja nakutafakari kuhusu kiwango cha manufaa au madharayanayoweza kupatikana kwa nchi kuridhia au kutokuridhiamkataba huu kama ulivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na maelezo yaSerikali ambayo yaliwasilishwa na Naibu Waziri wa Nishati naMadini, Kamati ilipitia na kuchambua kikamilifu maudhui yamkataba huu wa makubaliano baina ya pande mbili husika.Mantiki ya kufanya hivyo ni kuliwezesha Bunge kujiridhishaiwapo taratibu za msingi zimezingatiwa na kuelewa vyemajinsi ambavyo nafasi ya Tanzania katika diplomasia nauhusiano wa kimataifa itaendelea kudumishwa kutokana nahatua ya kuridhia au kutokuridhia mkataba huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, chimbuko la mkataba huuwa makubaliano baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muunganowa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Uganda, kuhusuMkataba wa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzi la Mafuta Ghafila Afrika Mashariki kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muunganowa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Uganda. Ni katika Kikaocha Kumi na Tatu cha Jumuiya ya Afrika Mashariki,kilichofanyika Kampala - Uganda, tarehe 23 Aprili, 2016,Wakuu wa Nchi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naJamhuri ya Uganda walikutana na kuanzisha mazungumzo

Page 96: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

96

ambayo hatimaye yalizaa uamuzi wa kushirikiana katika ujenzina uendeshaji wa Mradi wa Bomba la Kusafirisha MafutaGhafi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza uamuzihuo, nchi hizi mbili zimeazimia kutekeleza uwekezaji nauendeshaji wa mradi huo kwa kuzingatia Sheria za Kimataifakatika utaalam, mazingira na maslahi ya kijamii, pamoja nakuhamasisha na kulinda uwekezaji ili kuleta ufanisi katikamaendeleo, umiliki na utekelezaji wa muda mrefu wa mifumoya nchi zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na maelezo yamtoa hoja, Kamati ilitaka kujiridhisha kuhusu hali iliyofikiwakatika mkataba huu kwa kuangalia kama unayo nguvu yakisheria na kubaini kuwa, kifungu cha 2(c) cha Sehemu Bambayo inahusu Corporate Income Tax, katika kiambatishocha pili cha mkataba, kinahitaji kutazamwa kwa umakinikwani kinaweza kisiwe na maslahi kwa Taifa iwapo kampuniinayotekeleza mradi itakosa uaminifu na kutangaza kupatahasara kila mwaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kifungu hicho kinaruhusuhasara iliyobainika kuhusiana na utekelezaji wa mradi kabla,wakati au baada ya kipindi cha msamaha wa kodikusogezwa mbele katika mwaka wa fedha unaofuata iwapohaikufanyiwa kazi katika mwaka wa fedha husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Kamati ina mashakajuu ya Ibara ya saba (7) ya mkataba huu ambayo inahusufedha za kigeni (foreign exchange). Kwa mujibu wa kifunguhiki, kampuni itakayokuwa inatekeleza mradi inaruhusiwakuhamisha fedha kwenda nje ya Uganda na Tanzania bilakizuizi na kubakiza fedha katika nchi hizo ambazo fedhaitapelekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati inaona kama Ibarahii inakinzana na Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana naUmiliki wa Maliasili [The Natural Wealth and Resources(Permanent Sovereignty)] ya Mwaka 2017 ambayo inaruhusu

Page 97: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

97

fedha zinazotokana na mgawo wa faida tu ndiyo ziwekwenje ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mambomengine, utekelezaji wa mkataba huu ambao ulisainiwatarehe 26 Mei, 2017 Kampala, Uganda baada ya makubalianobaina ya nchi mbili za Tanzania na Uganda, unaendasambamba na malengo yaliyobainishwa katika Ibara ya101(1) ya Mkataba wa Kuanzishwa kwa Jumuiya ya AfrikaMashariki, inayohamasisha nchi wanachama kushirikianakatika utafiti, uendelezaji na utumiaji wa rasilimali mbalimbaliza nishati zilizomo katika Ukanda wa Afrika Mashariki. VilevileIbara ya 101(2)(e) ya mkataba huo inasisitiza kuhusu ushirikianokatika ujenzi wa mabomba ya usafirishaji wa mafuta na gesiasilia.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, kwa kutambuakwamba Tanzania na Uganda ni miongoni mwa nchiWanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyoundwatarehe 30 Novemba, 1999 ambayo miongoni mwa malengoya kuanzishwa kwake ni kuimarisha ushirikiano kati yawanachama kwenye maeneo ya kisiasa, kiuchumi, kijamii,kiteknolojia, utafiti, ulinzi na masuala ya kisheria, Kamati yaKudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, ilizingatia ushirikianobaina ya nchi hizi na faida za uwekezaji wa Mradi wa Ujenziwa Bomba la Mafuta Ghafi wakati wa kuifanyia kazi hojailiyopo mbele ya Bunge hili kwa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, maoni na ushauri waKamati. Baada ya maelezo hayo, naomba sasa kutoa maonina mapendekezo ya Kamati kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati inaishauri Serikalikuhakikisha inakuwa makini wakati wa utekelezaji wamkataba huu kwa kuzingatia mustakabali wa manufaa yakiuchumi kwa Taifa kwa ujumla na kwa wananchi wanaoishikatika maeneo ambayo mradi huu utatekelezwa. Aidha,Serikali ihakikishe wananchi hao wanashirikishwa kikamilifuikiwa ni pamoja na kuhamasishwa kutumia fursa za kiuchumizitakazojitokeza kutokana na utekelezaji wa mradi huu.

Page 98: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

98

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati inashauri Serikalikuhakikisha inatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kulipafidia ya ardhi kwa wananchi ambao watalazimika kuachiamaeneo yao ili kupisha utekelezaji wa mradi. Aidha, malipohayo yafanyike kikamilifu kwa wakati na kwa viwango stahikiili kuepusha migogoro ambayo inaweza kujitokeza na kuathiriutekelezaji wa mradi kwa muda uliopangwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa miongoni mwamambo yanayoweza kuathiri utekelezaji wa miradi yauwekezaji ni kukosekana kwa mazingira ya usalama na utulivukatika maeneo ambayo miradi hiyo inatekelezwa, Kamatiinaishauri Serikali kuhakikisha inaimarisha ulinzi na usalamakatika maeneo yote ambayo mradi huu utatekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni mara yakwanza kwa nchi yetu kutekeleza mradi wa thamani kubwana wa aina hii, Kamati inashauri Serikali kuhakikisha inatoaelimu ya kutosha kwa wananchi juu ya umuhimu wa mradihuu kwa maendeleo ya Taifa letu hivyo wanapaswakuuthamini na kushiriki katika kuulinda na kuutunza ili uwezekuwa na manufaa kwao na kwa vizazi vijavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wajumbewameonesha mashaka kuhusu kifungu cha 2(c) cha sehemuB ambayo inahusu Corporate Income Tax, katika Kiambatishocha Pili cha Mkataba, kwani kinaweza kutumiwa nawawekezaji wasio waaminifu kuihujumu nchi yetu. Kifunguhicho kinaruhusu hasara iliyobainika katika utekelezaji wamradi kabla, wakati au baada ya kipindi cha msamaha wakodi kusogezwa mbele katika mwaka wa fedha unaofuataiwapo haikufanyiwa kazi katika mwaka wa fedha husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati inaishauri Serikali iwemakini na kifungu hiki wakati wa utekelezaji wa mradi ilikampuni zitakazohusika kutekeleza mradi zisijaribu kukitumiakutangaza kupata hasara kila mwaka na hivyo kuikoseshaSerikali mapato stahiki.

Page 99: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

99

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Ibara ya saba(7) ya mkataba huu inairuhusu kampuni itakayotekeleza mradikusafirisha fedha nje ya Uganda na Tanzania na kuzihifadhihuko bila kizuizi chochote, Kamati inaishauri Serikali kuangaliakwa umakini Ibara hii ili kuepuka kukinzana na Sheria yaMamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Maliasili [TheNatural Wealth and Resources (Permanent Sovereignty)] yaMwaka 2017 ambayo inazuia wawekezaji kusafirisha fedhakwenda nje ya nchi isipokuwa zile zinazotokana na mgawowa faida iliyopatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, hitimisho, napenda kutoapongezi za dhati kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania, kwa juhudi zake na umahirialiouonesha katika kuhakikisha Tanzania inapata fursa yamradi huu mkubwa wa ujenzi wa bomba la kusafirisha mafutakutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania), ambaoutachangia kwa kiasi kikubwa kufungua milango ya kiuchumikwa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna ya pekee,niwashukuru sana Mheshimiwa Spika na Naibu Spika kwauongozi wenu mahiri na miongozo ambayo imeiwezeshaKamati kushughulikia kikamilifu hoja uliyoileta kwenye Kamatihadi kufikia hatua hii ya kuwasilisha maoni ya Kamati.Niwashukuru pia Wenyeviti wote wa Bunge kwa uratibu nausimamizi mzuri wa shughuli za Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru pia NaibuWaziri wa Nishati na Madini, Mheshimiwa Dkt MedardKalemani, Makatibu Wakuu pamoja na wataalam wote waWizara hii kwa ushirikiano walioutoa kwa Kamati wakati wakushughulikia Azimio hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa moyo wa dhati kabisa,nawashukuru Wajumbe wote wa Kamati ya Bunge ya Nishatina Madini, kwa ushirikiano walioutoa wakati wa kupitia,kuchambua na hatimaye kuandaa maoni juu ya Azimio hili

Page 100: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

100

ambayo nimeyawalisha mbele ya Bunge hili Tukufu. Majinayao naomba yaingie moja kwa moja kwenye Kumbukumbuza Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa, napendakumshukuru Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah;Mkurugenzi wa Idara ya Kamati Bw. Athumani Hussein;Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Fedha na Uchumi Bw. MichaelChikokoto; Makatibu wa Kamati Bi. Mwanahamisi Munkundana Bi. Felister Mgonja pamoja na Msaidizi wa Kamati Bi.Kokuwaisa Gondo kwa kuratibu shughuli za Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha nanaunga mkono hoja. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana.

TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YANISHATI NA MADINI KUHUSU AZIMIO LA BUNGE KURIDHIA

MKATABA WA KIMATAIFA WA MRADI WA UJENZI WABOMBA LA KUSAFIRISHA MAFUTA GHAFI LA AFRIKA

MASHARIKI KATI YA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANOWA TANZANIA NA SERIKALI YA JAMHURI YA UGANDA

(INTERGOVERNMENTAL AGREEMENT BETWEEN THE UNITEDREPUBLIC OF TANZANIA AND THE REPUBLIC OF UGANDA

CONCERNING THE PIPELINE SYSTEM OF THE EAST AFRICANCRUDE OIL PIPELINE (EACOP) PROJECT) KAMA

ILIVYOWASILISHWA MEZANI _________________

1.0 UTANGULIZI

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 53 (6)(b) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016naomba kuwasilisha Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bungeya Nishati na Madini, kuhusu Azimio la Bunge la KuridhiaMkataba wa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzi la Bomba laKusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki, kati ya Serikali yaJamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri yaUganda (Intergovernmental Agreement Between the United

Page 101: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

101

Republic of Tanzania and the Republic of Uganda concerningthe Pipeline System of the East African Crude Oil Pipeline(EACOP) Project).

Kwa mujibu wa fasili ya (9) ya Kanuni ya 6, ikisomwapamoja na fasili ya 1(b) ya Kanuni ya 7, katika Nyongeza yaNane ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016,Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, inalojukumu la kushughulikia Miswada ya Sheria na Mikatabainayopendekezwa kuridhiwa na Bunge iliyo chini ya Wizaraya Nishati na Madini.

Aidha, kwa kuzingatia masharti ya Kanuni ya 53(3) yaKanuni za Bunge, ulileta kwenye Kamati ya Nishati na madini,Hoja ya Serikali kuhusu Bunge kuridhia Mkataba wa Kimataifawa Mradi wa Ujenzi la Bomba la Kusafirishia Mafuta Ghafi laAfrika Mashariki kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano waTanzania na Serikali ya Jamhuri ya Uganda(Intergovernmental Agreement Between The United RepublicOf Tanzania And The Republic Of Uganda Concerning ThePipeline System Of The East African Crude Oil Pipeline(EACOP) Project), ili Kamati iweze kuishughulikia.

Mheshimiwa Spika, tarehe 04 Septemba, 2017 Kamatiilikutana katika Ukumbi wa Utawala Kuu, Chuo kikuu chaDodoma (UDOM) na kupata maelezo ya Serikali kuhusupendekezo la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Mradi waUjenzi la Bomba la Kusafirishia Mafuta Ghafi la Afrika Masharikikati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naSerikali ya Jamhuri ya Uganda (Intergovernmental AgreementBetween The United Republic Of Tanzania and The Republicof Uganda Concerning The Pipeline System of The East AfricanCrude Oil Pipeline (EACOP) Project).

Mheshimiwa Spika, Kamati ilipotekeleza jukumu lakekuhusiana na hoja hii, ilizingatia masharti ya Kanuni ya 117(8) na 117 (9) kuhusu utaratibu wa Kamati pamoja nakuwaalika wadau. Katika hatua hii, Kamati iliwaalika wadaukwa ajili ya kupata maoni yao, hata hivyo kutokana na ufinyuwa muda ambao Kamati ilikuwa nao katika kushughulikia

Page 102: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

102

hoja hii, Wadau wengi hawakuweza kuwasilisha maoni yao,na hata ambao waliweza waliwasil isha kwa njia yamaandishi tu.

Kamati inaishukuru sana Taasisi ya Utawala wa Maliasili(Natural Resources Governance Institute - NRGI) kwa maoniya msingi iliyowasilisha kwenye Kamati ambayo yametoamchango mkubwa sana katika kujadili Azimio hili. Nafurahikutamka kuwa Utaratibu huu wa kuwaalika wadau kutoamaoni yao kuhusu hoja inayoshughulikiwa na Kamati, ni wamsingi na ni muhimu kwa Jamii ya Kidemokrasia kamaTanzania. Aidha, ni utaratibu unaolisaidia Bunge kuendeleakudhihirisha kwamba, ni chombo halisi cha uwakilishi wawananchi chenye jukumu la kukidhi matarajio yao wakatiwa mchakato wa kuridhia mikataba ya kimataifa.

1.1 MAMBO YA MSINGI YALIYOZINGATIWA NAKAMATI

Mheshimiwa Spika, ili kuliwezesha Bunge kutekelezamadaraka yake ipasavyo kwa mujibu wa Ibara ya 63(3) (e)ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka1977, Kamati ilizingatia mambo mbalimbali muhimu katikauchambuzi wa hoja ya hii ya Serikali, ambayo leotunawasilisha Taarifa yake. Baadhi ya mambo hayo ni pamojana kuangalia Katiba ya Jamhuri ya Muungano, Sheria za nchizinazohusiana moja kwa moja na maudhui ya Mkatabaunaopendekezwa, pamoja na kutafakari kuhusu kiwangocha manufaa au madhara yanayoweza kupatikana kwa nchiyetu kuridhia au kutokuridhia Mkataba huu kama ulivyo.

Pamoja na maelezo ya Serikali ambayo yaliwasilishwana Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Kamati ilipitia nakuchambua kikamilifu maudhui ya Mkataba huu wamakubaliano baina ya pande mbili husika. Mantiki ya kufanyahivyo ni kuliwezesha Bunge kujiridhisha iwapo taratibu zamsingi zimezingatiwa na kuelewa vyema jinsi ambavyo nafasiya Tanzania katika diplomasia na uhusiano wa kimataifaitaendelea kudumishwa kutokana na hatua ya kuridhia aukutokuridhia Mkataba huu.

Page 103: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

103

Mheshimiwa Spika, chimbuko la Mkataba huu wamakubaliano baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano waTanzania na Serikali ya Jamhuri ya Uganda, kuhusu Mkatabawa Kimataifa wa Mradi wa Ujenzi la Bomba la KusafirishaMafuta Ghafi la Afrika Mashariki kati ya Serikali ya Jamhuri yaMuungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Uganda(Intergovernmental Agreement Between The United Republicof Tanzania and The Republic of Uganda Concerning ThePipeline System of The East African Crude Oil Pipeline (EACOP)Project), ni katika Kikao cha kumi na tatu cha Jumuiya yaAfrika Mashariki, kilichofanyika Kampala Uganda, tarehe 23Aprili, 2016. Wakuu wa nchi za Jamhuri ya Muungano waTanzania na Jamhuri ya Uganda walikutana na kuanzishamazungumzo ambayo hatimaye yalizaa uamuzi wakushirikiana katika ujenzi na uendeshaji wa mradi wa Bombala kusafirisha Mafuta Ghafi.

Katika kutekeleza uamuzi huo nchi hizi mbilizimeazimia kutekeleza uwekezaji na uendeshaji wa mradihuo kwa kuzingatia Sheria za Kimataifa katika utaalam,mazingira na maslahi ya kijamii, pamoja na kuhamasisha nakulinda uwekezaji, ili kuleta ufanisi katika maendeleo, umilikina utekelezaji wa muda mrefu wa mifumo katika nchi zao.

Mheshimiwa Spika, pamoja na maelezo ya Mtoahoja, Kamati ilitaka kujiridhisha kuhusu hali iliyofikiwa katikaMkataba huu kwa kuangalia kama unayo nguvu ya kisheriana kubaini kuwa, kifungu cha 2(c) cha Sehemu B ambayoinahusu Corporate Income Tax, katika Kiambatisho cha Pilicha Mkataba, kinahitaji kutazamwa kwa umakini kwanikinaweza kisiwe na maslahi kwa taifa iwapo kampuniinayotekeleza mradi itakosa uaminifu na kutangaza kupatahasara kila mwaka.

Kifungu hicho kinaruhusu hasara iliyobainika kuhusianana utekelezaji wa mradi kabla, wakati au baada ya kipindicha msamaha wa kodi kusogezwa mbele katika mwaka wafedha unaofuata iwapo haikufanyiwa kazi katika mwaka wafedha husika.

Page 104: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

104

Mheshimiwa Spika, aidha Kamati ina mashaka juuya Ibara ya 7 ya Mkataba huu ambayo inahusu fedha za kigeni“foreign exchange”. Kwa mujibu wa kifungu hiki kampuniitakayokuwa inatekeleza mradi inaruhusiwa kuhamisha fedhakwenda nje ya Uganda na Tanzania bila kizuizi na kubakizafedha katika nchi hizo ambazo fedha itapelekwa. Kamatiinaona kama ibara hii inakinzana na Sheria ya Mamlaka yaNchi kuhusiana na Umiliki wa Maliasili [The Natural Wealth andResources (Permanent Sovereignty)] ya Mwaka 2017 ambayoinaruhusu fedha zinazotokana na mgawo wa faida tu ndiyoziwekwe nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mambo mengine,utekelezaji wa Mkataba huu ambao ulisainiwa tarehe 26 Mei,2017 Kampala, Uganda baada ya makubaliano baina yanchi mbili za Tanzania na Uganda, unaenda sambamba namalengo yaliobainishwa katika Ibara ya 101 (1) ya Mkatabawa Kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki,inayohamasisha nchi wanachama kushirikiana katika utafiti,uendelezaji na utumiaji wa rasilimali mbalimbali za Nishatizilizomo katika Ukanda wa Afrika Mashariki. Vilevile Ibara ya101 (2) (e) ya Mkataba huo inasisitiza kuhusu ushirikiano katikaujenzi wa mabomba ya usafirishaji wa mafuta na gesi asilia.

Aidha, kwa kutambua kwamba, Tanzania na Ugandani miongoni mwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya AfrikaMashariki, iliyoundwa tarehe 30 Novemba, 1999 ambayomiongoni mwa malengo ya kuanzishwa kwake ni kuimarishaushirikiano kati ya nchi wanachama kwenye maeneo yakisiasa, kiuchumi, kijamii, kiteknolojia, utafiti, ulinzi na masualaya kisheria, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini,ilizingatia ushirikiano baina ya nchi hizi na faida za uwekezajiwa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi wakati wakuifanyia kazi hoja iliyopo mbele ya Bunge hili kwa sasa.

1.2 MAONI NA USHAURI WA KAMATI

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo,naomba sasa kutoa maoni na mapendekezo ya Kamatikama ifuatavyo:-

Page 105: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

105

Mheshimiwa Spika, Kamati inaishauri Serikalikuhakikisha inakuwa makini wakati wa utekelezaji waMkataba huu, kwa kuzingatia mustakabali wa manufaa yakiuchumi kwa Taifa kwa ujumla na kwa Wananchi wanaoishikatika maeneo ambayo Mradi huu utatekelezwa. Aidha,Serikali ihakikishe wananchi hao wanashirikishwa kikamilifuikiwa ni pamoja na kuhamasishwa kutumia fursa za kiuchumizitakazojitokeza kutokana na utekelezaji wa mradi huu.

Mheshimiwa Spika, Kamati inashauri Serikalikuhakikisha inatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kulipa fidiaya ardhi kwa Wananchi ambao watalazimika kuachiamaeneo yao ili kupisha utekelezaji wa mradi. Aidha, malipohayo yafanyike kikamilifu kwa wakati na kwa viwango stahikiili kuepusha migogoro ambayo inaweza kujitokeza na kuathiriutekelezaji wa mradi kwa muda uliopangwa.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa miongoni mwamambo yanayoweza kuathiri utekelezaji wa miradi yauwekezaji ni kukosekana kwa mazingira ya usalama nautulivu katika maeneo ambayo miradi hiyo inatekelezwa,Kamati inaishauri Serikali kuhakikisha inaimarisha ulinzi nausalama katika maeneo yote ambayo mradi huuutatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ni mara ya kwanzakwa nchi yetu kutekeleza mradi wa thamani kubwa na waaina hii, Kamati inashauri Serikali kuhakikisha inatoa elimu yakutosha kwa Wananchi juu ya umuhimu wa mradi huu kwamaendeleo ya Taifa letu hivyo wanapaswa kuuthamini nakushiriki katika kuulinda na kuutunza ili uweze kuwa namanufaa kwao na kwa vizazi vijavyo.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wajumbewameonesha mashaka kuhusu kifungu cha 2(c) cha SehemuB ambayo inahusu Corporate Income Tax, katika Kiambatishocha Pili cha Mkataba, kwani kinaweza kutumiwa naWawekezaji wasio waaminifu kuihujumu nchi yetu. Kifunguhicho kinaruhusu hasara iliyobainika katika utekelezaji wamradi kabla, wakati au baada ya kipindi cha msamaha wa

Page 106: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

106

kodi kusogezwa mbele katika mwaka wa fedha unaofuataiwapo haikufanyiwa kazi katika mwaka wa fedha husika.

Kamati inaishauri Serikali iwe makini na kifungu hiliwakati wa utekelezaji wa mradi ili kampuni zitakazohusikakutekeleza mradi zisijaribu kukitumia kutangaza kupatahasara kila mwaka, na hivyo kuikosesha Serikali mapatostahiki.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Ibara ya 7 ya Mkatabahuu inairuhusu Kampuni itakayotekeleza mradi kusafirishafedha nje ya Uganda na Tanzania na kuzihifadhi huko bilakizuizi chochote, Kamati inaishauri Serikali kuangalia kwaumakini ibara hii ili kuepuka kukinzana na Sheria ya Mamlakaya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Maliasili [The Natural Wealthand Resources (Permanent Sovereignty)] ya Mwaka 2017ambayo inazuia wawekezaji wa kusafirisha fedha kwendanje ya nchi isipokuwa zile zinazotokana na mgawo wa faidailiyopatikana.

2.0 HITIMISHO

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa pongezi za dhatikwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kwa juhudi zake na umahiri aliouonesha katika kuhakikishaTanzania inapata fursa ya mradi huu mkubwa wa ujenzi wabomba la kusafirisha mafuta kutoka Hoima Uganda hadiTanga Tanzania, ambao utachangia kwa kiasi kikubwakufungua milango ya kiuchimi kwa nchi yetu.

Kwa namna ya pekee, nakushukuru sana wewe binafsikwa Uongozi wako mahiri na miongozo ambayo imewezeshaKamati kushughulikia kikamilifu hoja uliyoileta kwenye Kamatihadi kufikia hatua hii ya kuwasilisha maoni ya Kamati.Niwashukuru pia Mheshimiwa Naibu Spika na Wenyeviti wotewa Bunge, kwa uratibu na usimamizi mzuri wa shughuli zaBunge.

Mheshimiwa Spika, nawashukuru pia Naibu Waziri waNishati na Madini Mhe. Dkt Medard Kalemani (Mb), Makatibu

Page 107: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

107

Wakuu pamoja na wataalam wote wa Wizara hii kwaushirikiano walioutoa kwa Kamati wakati wa kushughulikiaAzimio hili.

Kwa moyo wa dhati kabisa, nawashukuru Wajumbewote wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, kwaushirikiano walioutoa wakati wa kupitia, kuchambua nahatimaye kuandaa maoni juu ya Azimio hili ambayonimeyawalisha mbele ya Bunge hili Tukufu. Majina yao nikama yanavyoonekana katika orodha hapa chini, na kwaruhsa yako naomba yaingie kwenye Kumbukumbu Rasmi zaBunge.

i. Mhe. Doto Mashaka Biteko, Mb - Mwenyekitiii. Mhe. Deogratius Ngalawa, Mb- M/Mwenyekitiiii. Mhe. Mohamed Juma Khatib, Mb Mjumbeiv. Mhe. Ally Mohamed Keissy, Mb “v. Mhe. Yussuf Kaiza Makame, Mb “vi. Mhe. Mwantakaje Haji Juma, Mb “vii. Mhe. Daimu lddi Mpakate, Mb “viii. Mhe. Oscar Rwegasira Mukasa, Mb “ix. Mhe. Stella Ikupa Alex, Mb “x. Mhe. Bahati Ali Abeid, Mb “xi. Mhe. Mauled Said Abdalah Mtulia, Mb “xii. Mhe. Desderius John Mipata, Mb “xiii. Mhe. Vedastus Mathayo Manyinyi, Mb “xiv. Mhe. Susan Limbweni Kiwanga, Mb “xv. Mhe. Joyce Bitta Sokombi, Mb “xvi. Mhe. Catherine Valentine Magige, Mb “xvii. Mhe. Katani Ahmad Katani, Mb “xviii. Mhe. Zainabu Mussa Bakar, Mb “xix. Mhe. Haroon Mulla Pirmohamed, Mb “xx. Mhe. Maryam Salum Msabaha, Mb “xxi. Mhe. Anne Kilango Malecela, Mb “xxii. Mhe. Dunstan Luka Kitandula, Mb “xxiii. Mhe. Wilfred Muganyizi Lwakatare, Mb “xxiv. Mhe. Innocent Lugha Bashungwa, Mb “xxv. Mhe. John Wegesa Heche, Mb “xxvi. Mhe. Bupe Nelson Mwakang’ata, Mb “

Page 108: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

108

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa napendakumshukuru Katibu wa Bunge Dkt. Thomas D. Kashililah;Mkurugenzi wa Idara ya Kamati Bw. Athumani Hussein;Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Fedha na Uchumi Bw. MichaelChikokoto; Makatibu wa Kamati Bi Mwanahamisi Munkundana Bi Felister Mgonja pamoja na Msaidizi wa Kamati BiKokuwaisa Gondo kwa kuratibu shughuli za Kamati.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naungamkono hoja.

Deogratius Ngalawa, (Mb)M/MWENYEKITI

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI

7 Septemba, 2017

NAIBU SPIKA: Sasa nitamwita Msemaji wa KambiRasmi ya Upinzani kuhusu Wizara ya Nishati na Madini.

MHE. DEVOTA M. MINJA (K.n.y. MHE. JOHN J. MNYIKA- MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI KWA WIZARA YANISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naombaniwasilishe mezani maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusuAzimio la Kuridhia Mkataba Baina ya Serikali ya Jamhuri yaMuungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya UgandaKuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrikaya Mashariki (Inter-governmental Agreement Between theUnited Republic of Tanzania and the Republic of UgandaConcerning the Pipeline System of the East African Crude OilPipeline). Yanatolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 53(6)(c) yaKanuni za Bunge, Toleo la Januari, 2016.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kutoa polena pongezi nyingi kwa Waheshimiwa Wabunge toka pandeshindani na chama tawala kwa kazi kubwa waliyoifanyakatika kipindi ambacho Bunge letu lilikuwa mapumzikoni lakiniWabunge mlikuwa kazini.

Page 109: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

109

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa heshima kubwanichukue fursa hii kuwapongeza na kuwashukuru wajumbewote wa Kamati ya Nishati na Madini kwa ushirikianomkubwa wakati wa kutekeleza majukumu yao ya Kibungendani ya Kamati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba bombahili la kusafirishia mafuta ghafi kutoka Uganda hadimwambao wa Bahari ya Hindi ilikuwa ni kazi iliyohusu zaidiushawishi mpana, kwani kulikuwa na ushindani mkubwakutoka kwa ndugu zetu wa nchi jirani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bomba hili la mafuta ghafila Afrika ya Mashariki litakuwa na urefu wa kilometa 1,445.Kati ya kilometa hizo kwa upande wa Tanzania inazo kilomita1,149 zilizo katika Mikoa nane na katika Wilaya 24 za TanzaniaBara na kilometa 296 zilizobakia zipo upande wa Uganda.

Mheshimiwa Naibu Spika, mbinu za kushinda mradimkubwa kama huu bila ya kuwepo kwa zabuni ni dhahirilazima vivutio vikubwa viliwekwa mezani kama ambavyomaelezo ya Mheshimiwa Waziri yanavyosomeka. Hoja yamsingi, je, vivutio hivyo vilivyotolewa ili kupata mradi huovinawiana na manufaa yatakayopatikana kwa upande wawatu wetu? Ingekuwa ni vyema Bunge letu hasa ngazi yaKamati ikapatiwa taarifa ya upembuzi yakinifu kwa mradihuu ili hapo baadaye tusijeanza kulaumiana sisi Wabungeambao tumebariki jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kutoa utangulizihuo wa jumla, naomba sasa kuangalia baadhi ya vipengelevya mkataba huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya kwanza (1), kifungucha nne (4) cha mkataba kinaeleza kuwa hakuna sheria yandani au ya kimataifa itakayokuwa juu ya mkataba huu.Katika mkutadha huo huo ukiangalia Ibara ya 19 inayohusuutatuzi wa migogoro kuhusiana na mkataba huu kwa pandehusika, kifungu cha pili (2) kinatamka wazi kwamba

Page 110: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

110

wasuluhishi watakutana London na hawatatoka miongonimwa pande hizi zilizofungiana mkataba huu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuweka kumbukumbusawa ni kwamba Bunge hili tarehe 4 Julai, 2017, lilipitishaSheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Rasilimalina Maliasili ya mwaka 2017. Katika sheria hiyo, Sehemu yaTatu, kifungu cha 11 kinapiga marufuku mashauri yoteyanayohusu utajiri wa rasilimali na maliasili zetu kufanyika njeya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa mujibu wa tafsiriya maneno ya sheria hiyo ardhi ni sehemu ya rasilimali asili zanchi yetu na katika uwepo wa bomba la mafuta ardhi binafsina za umma zitakumbwa na kadhia hiyo ya upishwaji wabomba la mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mantiki hiyo, nikwamba mkataba huo ambao Mheshimiwa Rais alisaini(Instrument of Power) tarehe 24 Mei, 2017 na kumuidhinishaMheshimiwa Profesa Palamagamba John Kabudi, Waziri waKatiba na Sheria kusaini mkataba huu kwa niaba ya Serikali.Tarehe 26 Mei, 2017, Mheshimiwa Profesa Kabudi alisaini kwaniaba ya Serikali. Aidha, mwezi wa Sita, Serikali kupitiaMawaziri wa Katiba na Sheria ikaleta Miswada miwili iliyohusuumiliki wa rasilimali na maliasili za nchi vifungu tajwa kuhusukuzuia mashauri kufanyika nje ya Jamhuri ya Muungano waTanzania, vifungu hivyo vimeelezea kwa kirefu. Hoja yaKambi Rasmi ya Upinzani, ni kwa nini Bunge linaingizwakwenye mtego kwa kutunga sheria zinazokinzana?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya 2(3)(a) inasemakwamba, any confidential information supplied by one stateparty to another shall not be further disclosed by the receivingstate party without prior consent of the supplying state party.Kambi Rasmi ya Upinzani inaona kwamba kifungu hiki nikifungu hatari sana kwani hata Bunge kama taasisiinayowakilisha wananchi haitakuwa na haki ya kuona taarifahizo hadi pale kibali cha kufanya hivyo kitolewe na nchi,shirika au mkataba huu. (Makofi)

Page 111: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

111

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi, mtazamo wetu,ni dhahiri mkataba huu unaweza kuwa kama ile mikatabaya uchimbaji wa madini iliyosainiwa miaka zaidi ya kumiiliyopita ambayo makosa yake yanaonekana hivi sasa nabaadhi ya watendaji waliwajibishwa wakiwemo Mawaziri.Mikataba ya madini na utafiti wa mafuta imekuwa ikifanywakwa siri kwa kiasi kikubwa na kuwa watendaji wa taasisi mojaya Serikali walifikia hatua ya kuwekwa ndani na Kamati mojaila bado hawakuwa tayari kutoa mikataba hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tunatoa angalizo kuwamkataba huu usiwe kama mikataba waliyokuwawanaitumia wakoloni na wazee wetu wa makabilambalimbali ili kuchukua rasilimali zilizokuwepo kwa njia yaudanganyifu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya tatu (3) yamkataba inayohusu haki ya kumiliki ardhi inasema kwambakila nchi mwanachama itachukua hatua stahiki kuhakikishakwamba utwaaji wa ardhi na umilikishwaji wa ardhi hiyokwa kampuni ya mradi utalindwa na nchi wanachama lakinikwa kadhia nzima ya utwaaji huo wa ardhi ni lazima uwekwenye mazingira ambayo ni kwa manufaa ya kampuni.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kambi Rasmi ya Upinzaniinaeleza kuwa, ardhi ni rasilimali inayopanda thamani kilakukicha na hivyo mauzo ya ardhi za vijiji kwa wananchi nilazima yafanywe kwa kuangalia thamani ya soko na sivinginevyo. Kinyume cha hapo hujuma kwa mradi inawezakutokea kutokana na wamiliki kutokuridhika na hivyokutokutoa ushirikiano. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya nne (4) inatoauhuru wa kusafirisha mafuta ya Tanzania na kutoa haki zotekwa nchi ya Uganda hadi bandarini, kwa maana nyingine nikuwa Bandari ya Chongoleani, Tanga ni mali ya Uganda napia haki hiyo ambayo Tanzania tumeitoa kwa Ugandainaenda pia kwa wamiliki wa meli zitakazokuja kununuamafuta. Kambi Rasmi ya Upinzani inataka kufahamu ni kwa

Page 112: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

112

jinsi gani Mamlaka ya Bandari itajihusisha au itahusika nabiashara hii ya kutoa huduma za meli za mafutazitakazokuwa zinatia nanga katika bandari hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya 10 inahusu umilikiwa mafuta yaliyomo kwenye bomba. Kambi Rasmi yaUpinzani inashindwa kuelewa ni kwa nini vifungu vya Ibarahiyo vinaeleza kuwa hakuna mshirika atakayekuwa na hakiya kudai mafuta na mali yake bali ni yule atakayefanyautaratibu wa kibiashara na mmiliki wa meli kwa kushirikianana makampuni ya pamoja yaliyoundwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kampuni ya pamojaambayo inapewa mamlaka makubwa katika biashara hii yabomba, mkataba haukusema kuwa itasajiliwa wapi katikamataifa haya wanachama. Kambi Rasmi ya Upinzani inawasiwasi kwamba kampuni hii inaweza kusainiwa aukusajiliwa offshore kwenye nchi ambazo hazikuhusiana kabisana ulipaji wa kodi za nchi maarufu kama uchakachuaji nautunzaji wa fedha chafu kama baadhi ya makampuniyaliyoingizwa hapa nchini na kuchukua rasilimali zetu kamaile ya Meremeta ilivyokuwa na mwisho wa siku kubakikulaumiana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kambi Rasmi ya Upinzaniinaitaka Serikali kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu umiliki wamafuta hayo yanayotoka Uganda na kusafirishwa nje kupitiabandari mpya itakayojengwa katika Kijiji cha Chongoleani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa uchambuzi huo, KambiRasmi ya Upinzani inaona lingekuwa ni jambo la busara kwaBunge hili kutokuridhia Azimio hili hadi pale mikatabaitakapopitiwa vizuri na kujiridhisha kuhusiana na vifunguambavyo tunaona vinaathiri Watanzania moja kwa moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo,naomba kuwasilisha. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana.

Page 113: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

113

MAONI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI KUHUSU AZIMIO LAKURIDHIA MKATABA BAINA YA SERIKALI YA JAMHURI YAMUUNGANO WA TANZANIA NA SERIKALI YA JAMHURI YA

UGANDA KUHUSU MRADI WA UJENZI WA BOMBA LA MAFUTAGHAFI LA AFRIKA YA MASHARIKI (INTERGOVERNMENTAL

AGREEMENT BETWEEN THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIAAND THE REPUBLIC OF UGANDA CONCERNING THE PIPELINESYSTEM OF THE EAST AFRICAN CRUDE OIL PIPELINE (EACOP)

Project) KAMA YALIVYOWASILISHWA MEZANI

“Yanatolewa kwa Mujibu wa Kanuni ya 53(6) (c ) ya Kanuni zaBunge, Toleo la Januari, 2016”

Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kutoa pole napongezi nyingi kwa Waheshimiwa wabunge toka upandeshindani na chama tawala kwa kazi kubwa mliyoifanya katikakipindi ambacho Bunge letu lilikuwa mapumzikoni lakiniwabunge mlikuwa kazini.

Mheshimiwa Spika, Pia kwa heshima kubwa nichukuefursa hii kuwapongeza na kuwashukuru wajumbe wote waKamati ya Nishati na Madini kwa ushirikiano mkubwa wakatiwa kutekeleza majukumu yetu ya kibunge ndani ya Kamati.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Bomba hili lakusafirishia mafuta ghafi kutoka Uganda hadi mwambao waBahari ya Hindi ilikuwa ni kazi iliyohusu zaidi ushawishi mpana,kwani kulikuwa na ushindani mkubwa kutoka kwa ndugu zetuwa nchi jirani.

Mheshimiwa Spika, bomba hili la mafuta Ghafi laAfrika ya Mashariki litakuwa na urefu wa kilometa1,445; katiya kilometa hizo kwa upande wa Tanzania inazo kilomita 1,149zilizo katika mikoa 8 na katika wilaya 24 za Tanzania Bara nakilometa 296 zilizobakia zipo upande wa Uganda.

Mheshimiwa Spika, mbinu za kushinda mradimkubwa kama huu bila ya kuwepo kwa zabuni ni dhahirilazima vivutio (incentives)vikubwa viliwekwa mezani kamaambavyo maelezo ya Mheshimiwa Waziri yanavyosomeka.

Page 114: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

114

Hoja ya msingi je vivutio hivyo vilivyotolewa ili kupata mradihuo vinawiana na manufaa yatakayopatikana kwa upandewetu? Ingekuwa ni vyema Bunge letu hasa ngazi ya kamatiikapatiwa taarifa ya upembuzi yakinifu kwa mradi huu ilihapo baadae tusijeanza kulaumiana sisi wabunge ambaotumebariki jambo hili.

Mheshimiwa Spika, baada ya kutoa utangulizi huowa jumla, naomba sasa kuangalia baadhi ya vipengele vyaMkataba huu.

Mheshimiwa Spika, ibara ya 1 kifungu cha 4 chamkataba kinaeleza kuwa hakuna sheria ya ndani au yakimataifa itakayokuwa juu ya mkataba huu. Katikamkutadha huo huo ukiangalia Ibara ya 19 inayohusu utatuziwa migogoro kuhusiana na mkataba huu kwa pande husika,kifungu cha 2 kinatamka wazi kwamba wasuluhishiwatakutana London na hawatatoka miongoni mwa pandehizi zilizofungiana mkataba huu.

Mheshimiwa Spika, kwa kuweka Kumbukumbu sawani kwamba Bunge hili tarehe 04/07/2017 lilipitisha sheria yaMamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Rasilimali namaliasili ya mwaka 2017 {The Natural Wealth and Resources(Permanent Sovereignty) ACT,2017}. Katika sheria hiyo sehemuya III kifungu cha 11 kinapiga marufuku mashauri yoteyanayohusu utajiri wa rasilimali na maliasili zetu ni marufukukufanyika nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwamujibu wa tafsiri ya maneno ya sheria hiyo ardhi ni sehemuya rasilimali asili za nchi yetu, na katika uwepo wa bomba lamafuta ardhi binafsi na za umma zitakumbwa na kadhia hiyoya upishwaji wa bomba la mafuta.

Mheshimiwa Spika, kwa mantiki hiyo ni kwambaMkataba huu ambao Mheshimiwa Rais alisaini “instrumentof Power” tarehe 24/ 05/2017 akimuidhinisha Prof.Paramagamba John Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheriakusaini Mkataba huu kwa niaba ya Serikali.

Page 115: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

115

Mheshimiwa Spika, tarehe 26/05/2017 MheshimiwaProf. Kabudi alisaini kwa niaba ya Serikali.

Aidha, Mwezi wa sita, Serikali kupitia kwa Waziri waKatiba na sheria ikaleta miswada miwili inayohusu umiliki warasilimali na Maliasili za nchi na vifungu tajwa kuhusu kuzuiamashauri kufanyika nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniavifungu hivyo vimeelezea kwa kirefu. Hoja ya Kambi Rasmiya Upinzani ni kwa nini Bunge linaingizwa kwenye mtego wakutunga sheria zinazokinzana?

Mheshimiwa Spika, Ibara ya 2 kifungu cha 3 (a)kinachosema kwamba;

“Any confidential information supplied by one stateParty to another shall not be further disclosed by the receivingstate Party without the prior consent of the supplying StateParty”

Kambi Rasmi ya Upinzani inaona kwamba kifungu hikini kifungu hatari sana kwani hata Bunge kama taasisiinayowakilisha wananchi haitakuwa na haki ya kuona taarifahizo hadi pale kibali cha kufanya hivyo kitolewe na nchimshirika wa Mkataba huu. Hivyo basi kwa mtazamo wetu nidhahiri mkataba huu unaweza kuwa kama ile Mikataba yaUchimbaji wa Madini iliyosainiwa miaka zaidi ya kumi iliyopitaambayo makosa yake yanaonekana sasa na baadhi mabaadhi ya watendaji kuwajibishwa wakiwemo Mawaziri.Mikataba ya Madini na utafiti wa mafuta imekuwa ikifanywakwa siri kwa kiasi kikubwa kuna watendaji wa taasisi moja yaSerikali walifikia kuwekwa ndani na Kamati moja ila badohawakuwa tayari kutoa mikataba. Aidha, tunatoa angalizokuwa mkataba huu usiwa kuwa kama mikataba waliyokuwawanaitumia wakoloni kwa wazee wetu wa makabilambalimbali ili kuchukua rasilimali zilizokuwepo kwa njia yaudanganyifu.

Mheshimiwa Spika, Ibara ya 3 ya Mkataba inayohusuHaki ya kumilki Ardhi, inasema kwamba kila nchimwanachama itachukua hatua stahiki kuhakikisha kwamba

Page 116: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

116

utwaaji wa ardhi na umilikishwaji wa ardhi hiyo kwa Kampuniya mradi utalindwa na nchi mwanachama, katika kadhianzima ya utwaaji huo wa ardhi na ni lazima uwe kwenyemazingira ambayo ni kwa manufaa kwa Kampuni.

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzaniinaelewa kuwa ardhi ni rasilimali inayopanda thamani kilakukicha, hivyo mauzo ya ardhi za vijiji au wananchi ni lazimayafanywe kwa kuangalia thamani ya soko na sio vinginevyo.Kinyume cha hapo hujuma kwa mradi inaweza kutokeakutokana na wamiliki kutokuridhika na hivyo kutokutoaushirikiano.

Mheshimiwa Spika, Ibara ya 4 inayotoa uhuru wakusafirisha mafuta kwa Tanzania kutoa haki zote kwa nchi yaUganda hadi Bandarini, kwa maana nyingine ni kuwa Bandariya Chongoleani-Tanga ni mali ya Uganda na pia haki hiyoambayo Tanzania tumeitoa kwa Uganda inaenda pia kwaWamiliki wa Meli zitakazokuja kununua mafuta.

Mheshimiwa Spika,Kambi Rasmi ya Upinzani inatakakufahamu ni kwa jinsi gani Mamlaka ya Bandari itajihusisha/itahusika na biashara hii ya kutoa huduma kwa meli za mafutazitakazokuwa zinatia nanga katika Bandari hiyo.

Mheshimiwa Spika, Ibara ya 10 inayohusu umiliki wamafuta yaliyomo kwenye Bomba. Kambi Rasmi inashindwakuelewa kwani vifungu vya Ibara hiyo vinaeleza kuwa hakunamshirika atakayekuwa na haki ya kudai kuwa mafuta ni maliyake, bali ni Yule atakaye fanya utaratibu wa kibiashara nammiliki wa meli kwa kushirikiana na kampuni ya pamojailiyoundwa.

Mheshimiwa Spika, Kampuni ya pamoja ambayoinapewa mamlaka makubwa katika biashara hii ya Bomba,mkataba haukusema kuwa itasajiliwa wapi katika mataifahaya wananchama. Kambi Rasmi ya Upinzani inawasiwasikwamba Kampuni hii inaweza kusajiliwa “off shore” kwenyenchi ambazo hazihusiana na ulipaji wa kodi na nchi maarufukwa uchukuaji na utunzaji wa fedha chafu, kama ambavyo

Page 117: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

117

baadhi ya makampuni yaliyoingizwa hapa nchi na kuchukuarasilimali zetu kama ile ya meremeta ilivyokuwa na mwishowa siku tukabaki kulaumiana tu.

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitakaSerikali kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu umiliki wa mafutahayo yanayotoka Uganda na kusafirishwa nje kupitia bandarimpya itakayojengwa katika kijiji cha Chongoleani.

Mheshimiwa Spika, kwa uchambuzi huo Kambi Rasmiya Upinzani inaona lingekuwa ni jambo la busara kwa Bungehili kutokuridhia azimio hili hadi pale mkataba utakapopitiwavizuri na kujiridhisha kuhusiana na vifungu ambavyo tunaonavinaathari kwa watanzania moja kwa moja.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naombakuwasilisha.

………………………………….Devota M. Minja (Mb)

K.n.y Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi yaUpinzani-Wizara ya Nishati na Madini.

11.09.2017

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge,tumeshamsikiliza Mheshimiwa Waziri, mtoa hoja, Kamati napia Msemaji wa Upinzani.

Ninayo majina hapa ya walioomba kuchangia, kwahiyo tutaanza na uchangiaji halafu mtoa hoja atapewa fursaya kuhitimisha. Tutaanza na Mheshimiwa Mussa Mbarouk,atafuatiwa na Mheshimiwa Profesa Anna Tibaijuka.

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Kwanza nianze kuunga mkono hoja ya Kambi Rasmiya Upinzani. (Makofi)

Page 118: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

118

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini baada ya kusemahayo, nami nina yangu machache ya kuzungumza.

Mheshimiwa Naibu Spika, labda kwanza nianze kwakumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ametujalia afya njemana kuweza kukutana katika Kikao chetu hiki cha Bunge nahatimaye kuipitia taarifa hii ya Intergovernment AgreementBetween the United Republic of Tanzania and the Republic ofUganda Concerning the Pipeline System of the East AfricanCrude Oil Pipeline Project.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo,nami nina yangu ya kushauri. Kwanza, nishukuru kwambamradi huu umekuja kwenye Jimbo letu la Tanga ambayoitakuwa ndiyo last destination. Vilevile niwashauri waleambao mradi huu utapita katika maeneo yao, katika mikoanane, wilaya 24 na vijiji takribani mia moja na ushehe.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe kwanza tushirikishewananchi wetu katika suala hili lakini vilevile na Serikali nayoitoe maandalizi maalum kwa sababu wananchi wengi huumradi wamekuwa wakiusikia juujuu, lakini hapa nishukurukwamba Kamati yetu ya Nishati na Madini imelifanyia kazivizuri na imetoa baadhi ya tahadhari na hata Kambi Rasmiya Upinzani katika baadhi ya maeneo ambayo nikipata nafasinikayataja huko mbele, imetoa tahadhari, lakini makubwazaidi ninayoona ni haya yafuatayo.

Kwanza, Serikali iwe makini katika kila hatua kuepukatabia ya kusaini mikataba ambayo baadaye inakujakuonekana kuwa mikataba mibovu kama ilivyosemwa naKamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusu malipo yafidia, yazingatie bei ya soko la ardhi iliyopo sasa na pasiwena visingizio. Kwa mfano katika eneo la Chongoleaniwananchi kule wamelipwa eka moja kwa thamani ya shilingimilioni mbili na baadhi walikuwa wakitaka ufafanuzi zaidikujua kwa nini wanalipwa pesa hiyo kwa sababu wapo watuambao walikuwa wamenunua, ule ni Ukanda wa Pwani

Page 119: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

119

kabisa, wapo watu waliokuwa wamenunua eka moja kwazaidi ya hata milioni 10, lakini baada ya kutaka ufafanuzitukaenda kwa Mkuu wa Mkoa wakaitwa wataalam wa ardhiwao wakasema tu moja kwa moja kwamba bei ya milionimbili iliwekwa kabla hapajawekwa miundombinu.

Mheshimiwa Naibu Spika, hilo kwa kweli lilileta taabukidogo kwa sababu binafsi kwa maoni yangu niliwahikuwaeleza kwamba lazima mjue wakulima hawa maeneoyao ambayo yalikuwa ndiyo chanzo chao cha mapatoyanachukuliwa. Zao kubwa katika maeneo ya Chongoleanini minazi, mihogo, midimu, milimao, michungwa na mambomengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, labda nikueleze tu, ndimukatika maeneo ya Chongoleani imekuwa na faida kubwasana kwa sababu mdimu mmoja unaweza kutoa visalfetiviwili na kila kiroba cha ndimu kikifikishwa katika soko la Dares Salaam ni sawasawa na Sh.40,000. Kwa hiyo, mti mmojawa mdimu unaweza kutoa katika zao la awamu mojaSh.80,000 ya Kitanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo niliiomba Serikalikwamba kwa kuwa wananchi wale maeneo yaoyanachukuliwa basi watafutiwe maeneo mbadala. Vilevilepia kama tunavyojua kwamba kuna thamani ya ardhi nathamani ya mimea, kwa hiyo, yote hayo niliitaka Serikaliiyazingatie. Sasa nawashauri Waheshimiwa Wabungewengine ambapo mradi huu utapita wawe makini na hilo ilitusije tukawarudisha wananchi wetu katika lindi la umaskini.

Mheshimiwa Naibu Spika, lazima tujue kwamba kilimoni uti wa mgongo wa Taifa letu. Kwa kuwa Serikali kwakushirikiana na Serikali ya Uganda tunaamua kuchukuamaeneo yale ya wananchi, basi lazima wananchi waletuwatafutie maeneo mbadala kwa ajili ya shughuli zao zakilimo. Kwa mfano, katika eneo la Chongoleani lipo shambala mkonge linalomilikiwa na Kampuni ya Amboni Limitedambayo sasa hivi imebadilisha jina inaitwa Cotel CompanyLimited. Shamba lile limekuwa haliendelezwi, kwa hiyo,

Page 120: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

120

naiomba Serikali hususan Mheshimiwa Rais alifutie hatishamba lile la Amboni ambalo liko eneo moja linaitwaMwanyungu na wananchi wale ambao maeneo yaoyamechukuliwa wapewe maeneo ya Mwanyungu sasa katikashamba la mkonge ili waendelee na shughuli zao za kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivi kwa sababuwengi wamekuwa wakilalamika kwamba maeneoyamechukuliwa lakini fedha waliyolipwa haikidhi kwendakununua mashamba au ardhi maeneo mengine. Waleambao nyumba zao zimepitiwa na mradi pamoja nakwamba ni nyumba za tope lakini kwa fedha waliyopewalabda mtu anaweza akawa ana eka nne amepata labdashilingi milioni nane na fidia ya mimea labda amepata shilingimilioni nne, shilingi milioni 12 leo huwezi ukajenga nyumbayenye hadhi na ya kisasa, kwa sababu lengo letu ni kwambawananchi wetu waishi katika maisha bora na nyumbaambazo zina huduma zote za kibinadamu. Kwa hiyo, miminiombe tu kwamba Serikali iwe makini katika kufidiawananchi wetu lakini pia kuwapatia maeneo mbadala yakilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusiana na sualazima la first priority kwa wale wakazi ambao wanapitiwa namradi. Kwa mfano, zimetajwa ajira hapa takribani 10,000ambazo zitajitokeza katika mradi, lakini kutakuwa na zileajira ambazo ni permanent takribani 1,000. Sasahatukuchanganuliwa hapa katika hizi ajira 1,000 labdazitagawanyika vipi ki-percentage, kwamba katika 1,000asilimia kadhaa itatoka Uganda, asilimia kadhaa itatokaTanzania. Tuwe makini hapa, tusije tukakuta zile ajira 1,000zote zinatoka kwa wananchi wa Uganda.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe tena viongozi wangazi mbalimbali ambao wanapitiwa na maeneo ya mradikuanzia Waheshimiwa Wabunge, Madiwani, hata Wenyevitiwa Vijiji na Vitongoji wawe wanashirikishwa kwa karibukatika zoezi zima la mradi huu. Kwa sababu lengo ni mradihuu uwe na manufaa kwa Watanzania isije ikawa tena mradiumekwishaanza panaanza manung’uniko ya hapa na pale.

Page 121: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

121

Mheshimiwa Naibu Spika, binafsi nashukuru katikaJimbo langu nimeshiriki kwa asilimia kadhaa au kwa asilimiatakribani 70 katika haya masuala yote ya mradi, ndiyo maanaumeona pia hata Tanga hapakutokea manung’uniko mengikuhusiana na mradi huu. Kwa hiyo, naishauri Serikali kuleambapo mradi huu utapita wananchi, Viongozi wa Vijiji,Mitaa, Madiwani, Waheshimiwa Wabunge washiriki kikamilifu.Waelewe in and out katika kila kinachoendelea katika mradihuu ili baadaye tusije tukaja tukabeba lawama.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile pia nawakumbushaWaheshimiwa Wabunge, mtakaposhiriki kikamilifu katikamradi huu tukawatetea wananchi wetu itakuja kuwa nisababu mojawapo ya wewe kurudi tena humu Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo,nakushukuru. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbarouk, naona una imaninzuri sana ya kurudi humu ndani. (Makofi/Kicheko)

Tunaendelea na Mheshimiwa Profesa Anna Tibaijukaatafuatiwa na Mheshimiwa Juma Nkamia.

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa NaibuSpika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Sina budi kuanzakwa kusema naunga mkono hoja tena kwa furaha kubwasana. Ungekuwa unaruhusu kidedea humu tungesemaneema, neema, neema imefunguliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu imepata bahatinzuri, bahati kubwa kwamba hayawi hayawi yanakuwa,hatimaye makubaliano haya au mkataba huu ukawaumesainiwa na sasa hivi unaendelea kuwa mkataba unaitwatreaty. Kwa hiyo, naomba kwanza niseme kama Watanzaniatujue tofauti ya mkataba huu na ile mikataba ya madini,mikataba ya madini, those are contracts, ile ni mikataba yamakampuni, lakini hii ni treaty maana yake makubaliano katiya Serikali na Serikali. (Makofi)

Page 122: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

122

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba kabisakusema tusipotoshe Watanzania kwa sababu tunataka kutoamawazo mbadala. Katika suala hili tuungane kama Taifa nakama Bunge, kwanza kumpongeza Rais wetu kwamba hapaameingiza goli, hapa utake usitake goli limeingia na hongerasana, tunashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili mimi nimelifuatiliakwa muda mrefu na najua kwamba ilichukua muda. Haikuwakitu rahisi kwa mtu kufanya maamuzi kutoa zile concessionskama tulivyoona pale Chongoleani kwa wale tuliokwendakuwawakilisha. Katika hili nawashukuru sana kwamba na ninyimlihakikisha kwamba Waheshimiwa Wabunge wa Kamatimbalimbali tulishiriki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba niunganekabisa na Taarifa ya Kamati kama ilivyotolewa. Niwapongezesana kwa kufanyia kazi mkataba huu. Nimesikiliza sanamapendekezo na mimi nakubaliana nayo. Sasa nasimamahapa kuongezea tu yale ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, mimibomba hili linapita katika kata sita za Jimbo langu. Bombahili linapotoka Ngenge linaingia Burungula, likitoka Burungulalinakwenda Mubunda, likitoka Mubunda linapiga kona likoKarambi, likitoka Karambi linaingia Kimwani, likitoka Kimwanilinaingia Nyakabango likipinda likitafuta Chato. Kwa hiyo,jamani ni mambo makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa niaba yawananchi na naungana na Waheshimiwa Wabungewengine walionitangulia waliosema kwamba sisi kazi yetuni nini, kazi yetu kwanza ni kuuelewa mkataba huu na kuusifuna kujua kwamba katika mkataba wa nchi kwa nchi ni giveand take, huwezi kusema kwamba utachukua kila kitu uwezekuleta bomba Tanzania, au siyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, bomba hili lilikuwa na njiatatu na mnajua kwamba Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli

Page 123: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

123

alikazana sana kulitoa Kenya kulileta huku, si kazi ndogo,naomba kabisa Bunge hili tumpigie makofi. Katika kulileta,katika mikataba, dhana ya treaty, dhana ya mikataba lazimauwe na concessions, sasa tuko katika kipindi ambachotunaangalia mikataba yetu, hatutaki kuingia katika mikatabamibovu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mikataba mibovuinatokana na usiri, sasa tuko hapa tunajadili jambo naKamati imeshaona mkataba unavyokwenda, sasa kuboresha,lakini watakapokuja wanaweza kuja wakasema tunapatanini. Mimi nilikuwepo Chongeleani, Tanga na MheshimiwaRais alisema faida tutakazozipata kwa hesabu ya haraka,mapipa 216,000 kwa siku na bei inaweza ikayumba lakini kwabei ya chini tuliyoambiwa zilikuwa ni dola 12 kwa pipa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa kila siku tunauwezo wa kupata dola 2,592,000, hapo utasema kwambaDkt. Magufuli hakucheza jamani? Alicheza, kwa sababumafuta haya sio ya kwetu, mafuta ni ya Waganda lakini nasisi tumeingia pale kwa sababu tumepata ushoroba, kwahiyo tulinde amani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuhimiza kwawananchi wangu, tungependa amani. Sisi kazi yetu lazimatuwe na ulinzi shirikishi, ulinzi wa kitaalam lakini pia ulinzishirikishi. Kulinda bomba hili litakuwa ni jukumu la Watanzaniawote. Tumelipata kwa sababu ya utulivu ambao kwa kweliwahenga waliufanyia kazi na sisi tunaendeleza. Kwa hiyo,ulinzi ndicho kitu kikubwa ambacho nakiona hapa lakini piana fursa na ajira ambazo Mheshimiwa Waziri ameshasemakatika hotuba yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi katika suala la ulinzinaomba sasa tusiibue migogoro ya ardhi. Naposimama hapakule kwangu kuna watu wanapima ardhi katika hizi katanilizozitaja ambapo bomba linapita na mimi kama Mbungewa eneo wala sina taarifa yoyote. Kwa hiyo, naomba jamanihapa Serikali, Mheshimiwa Waziri, msituchanganye na

Page 124: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

124

Mheshimiwa Waziri wa Mifugo naomba utusimamie. Sualahili, Waheshimiwa Mawaziri, mimi ntakuwa mkweli, nikionamnasuasua mimi nakimbia naenda kwa Waziri Mkuu, naaminiwatatusaidia huko ngazi za juu kama ikibidi lakini tusifikehuko.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kabisa katikaupimaji wa ranchi, watu wanaosema wanapima ranchikatika maeneo ambapo bomba linapita wanatuchanganya.Wananchi sasa hivi kuna taharuki kubwa sana, wananchiwanalia kabisa nbagila bati twafa twafa. Sasa kilio kuletwafa, twafa, wakati tunasubiri bomba, sasa bomba likijaupimaji wa bomba utakwendaje? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, watu wamezungumziafidia, fidia ni muhimu na wanaochanganya mambo ya ardhi,ile ardhi itatwaliwa kwa fidia kwa mujibu wa sheria inakuwasasa bomba litapita katika ardhi ushoroba itakuwa ni maliya Serikali, haitakuwa tena mali ya watu binafsi. Huwezikupitisha bomba la Serikali katika ardhi ya watu binafsi,itatwaliwa ile ardhi lakini mimi mwenyewe kama nilivyosema,tutasimamia haki.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa hili na weweutuwekee nguvu, hao watu ambao wako kule Mulebawanawachanganya wananchi, naomba Serikali,Mheshimiwa Waziri ananisikia, naomba watusaidie.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais alipofikaBiharamulo alisema kwamba suala la mifugo ni ufugaji wakisasa sasa, mambo ya kurandaranda na mifugo hakunatena. Kwa hiyo, tunakwenda kupima ardhi lakini kwa taratibu.Huwezi kupima ardhi za vijiji bila kuzihawilisha kwanza. Mimininavyojua mchakato wa kuhawilisha ardhi mpaka Raisanatoa notice ya miezi mitatu, sasa hiyo notice ya kwendakuipima Muleba imetoka lini? (Makofi)

Page 125: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

125

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hili pia niliwasilishe,na suala lenyewe ni tete tena linavuruga bomba la mafuta,maana yake ni kwamba linakwenda kuvuruga amanitunayoizungumzia. Naomba barua hii ambayo Mwenyekitiwa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba, pia kwa MheshimiwaMwijage yeye mdomo wake hawezi akasema zaidi hapalabda lakini mimi nalitaja wazi wazi hapa. Wananchi waMuleba hawawezi kutuelewa mimi na Mwijagehatutaeleweka na Wabunge wengine hapa kutoka Mkoawa Kagera tusipozungumza suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hili pia litavurugaamani, linapandikiza mgogoro wa ardhi, sisi hatukubali natunaomba Serikali itusaidie, naamini watendajiwamekurupuka, wamekwenda kule bila kufuata utaratibunaomba mtusaidie na naomba barua hii niiwasilishe kwakona iwe sehemu ya Hansard. Kusema kwamba huwezi kwendakupima kata sita, kata kumi. Hata na kule Kaskazini piawameathirika hata sisi wawakilishi wa wananchi hatunahabari, wananchi wanatupigia simu katika taharuki kubwasana. Wakati Mheshimiwa Rais alipokuwa Biharamuloalifafanua…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Tibaijuka malizia maelezoyako dakika moja.

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa NaibuSpika, nakushukuru sana. Kimsingi ni siku ya furaha, ni walewanaotaka kutuharibia hao ndio tujadiliane nao lakininadhani hili ni jambo jema limekuja Tanzania, vijanachangamkeni, jifunze mgambo, mkalinde bomba la mafuta.Ahsante sana.

NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Mheshimiwa JumaNkamia tutamalizia na Mheshimiwa Vedastus Manyinyi.

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika,nakushukuru sana na mimi kwa kunipa nafasi hii ili niwezekuchangia kwenye hoja iliyo mbele yetu. Awali ya yote

Page 126: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

126

nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai mimi nasote tuliomo humu ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza kabisaniishukuru na kuipongeza sana Serikali ya Jamhuri yaMuungano wa Tanzania chini ya Mheshimiwa Rais Dkt. JohnPombe Magufuli kwa kufanikisha mradi huu wa bomba lamafuta kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu ni muhimu sanakwetu, na wote tunafahamu kwamba kulikuwa na kamamashindano hivi kati ya nchi hizi za Afrika Mashariki kuhusubomba lipite hili wapi, lakini baada ya Serikali ya Tanzaniakufanikiwa na mradi huu kuzinduliwa kule Tanga kwa kweliimekuwa ni faraja kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Chemba bombahili linapita si chini ya kilometa 170 kutoka mpakani na Kitetohadi mpakani na Singida. Linapita Mrijo, Chandama,Songolo, Goima, Paranga, Farqwa, Kwamtoro, Ovada hadiKinyamshindo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu, wananchi nivizuri wakaelezwa mapema ili wasiendeleze baadhi yamaeneo yao kwamba bomba hili litapita wapi. Lakini piaitakuwa vyema sana kwa wale ambao wataguswa na eneolao kuchukuliwa wakalipwa fidia yao stahiki kwa kipindimuafaka, litakuwa limewasaidia sana. Pia ni mradi mzurikwasababu ukiangalia kwa siku, Mama Tibaijuka alikuwaanajaribu kupiga hesabu pale na mimi nimejaribu kupigahesabu hapa kwamba kwa siku Tanzania tunapata dola2,708,325, it’s a huge amount of money na hii hela itatusaidiasana.

Sasa mimi ombi langu ni kwamba ni vizuriWaheshimiwa Wabunge pamoja na Madiwani wa maeneohusika. Kwa sababu nimeanza kuona kuna tatizo moja dogotu na ningeomba kuishauri Serikali; kwambawanawashirikisha sana Wakuu wa Mikoa na Wakuu waWilaya. Hawa ni watendaji wa Serikali, lakini wanaoulizwa

Page 127: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

127

maswali ni Wabunge na Madiwani. Mbunge ukienda mahaliwananchi wanakuuliza hebu tuambie bomba likipita hapasisi tutafaidika nini? Mbunge unashindwa kutoa majibukwasababu aliyekwenda kuhudhuria hivi vikao vingi vingihivi ni Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa na nashukuru sanabaadhi ya Waheshimiwa Wabunge ambako bomba hililinapita walishirikishwa kule Tanga.

Ningetoa rai kwamba sasa tunapokwenda kwenyeprocess hii ya ku-finalize hili suala Waheshimiwa Wabungena Waheshimiwa Madiwani wa maeneo husika ni vizuriwakashirikishwa. Seriakli msi-ignore sisi ni wawakilishi wawananchi tu lakini sisi ndiyo responsible kwenye maswali yawananchi. Kwa nia njema tu, tushirikisheni ili na sisi twendevizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, kiwango hiki chafedha tutakachokipata ni kikubwa kidogo. Maeneo mengibomba hili litakapopita vijiji vingi havina maji, na ndiyomaana mimi na Wabunge wenzangu wa Mkoa wa Dodoma,Manyara na hata Tanga bomba lilikopita ndiko ilikopimwabarabara ya lami kutoka Handeni - Kiberashi - Kibaya - Mrijo,Chemba - Donsee - Farqwa - Porobanguma - Kwamtorompaka Singida. Kwa hiyo nadhani ni wakati muafaka saaSeriakli ijenge ile barabara kwa kiwango cha lami ili hatausimamizi na usalama wa bomba hili uwe mzuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuyasema hayanakushuru sana na ninaipongeza sana Serikali na naungamkono. Jambo hili ni jambo jema sana kwentu, ni jambojema kwa Watanzania wote tuungane ili tufike paleMheshimiwa Rais wetu anataka tufike pamoja na chamachetu, chama tawala. Ahsante sana.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Vedustus Manyinyi, halafuMheshimiwa Mtoa Hoja ajiandae.

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa NaibuSpika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia

Page 128: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

128

katika hoja iliyopo mbele yetu inayohusiana na bomba lamafuta kutoka Uganda mpaka Tanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kila jambohuwa linakuwa na mapingamizi, lakini tuseme tu kwelikwamba kwa kazi hii aliyoifanya Mheshimiwa Rais yakuhakikisha kwamba bomba hili tunaweza kupewa huumradi ni kazi ambayo anastahil i kupongezwa sana,kwasababu kwanza ni mradi ambao umechukua mudamfupi sana, lakini wote tunafahamu ni kwa kiasi ganiwenzetu wa Kenya walivyokuwa wanautaka mradi huu kwaudi na uvumba, lakini imekuwa bahati nzuri tuimewezakuupata.

Mheshimiwa Naibu Spika, yako manufaa ya wazi waziambayo yatatokana na mradi huu maana hili bombalitakapojengwa maana yake ni kwamba hata barabarakatika maeneo hayo yote zitapita na watu wetu ambaowako katika maeneo hayo watafaidika zaidi katika biasharazao mbalimbali, watafaidika na ajira ambazo zitatokanana mradi huu. Hii ikiwa ni pamoja na Serikali itaendeleakupata kodi katika mradi huu, lakini na ile tozo ya upitishajiwa mafuta kwa sababu lile bomba linalopita katika nchiyetu, kwamba tuta-charge kile kitu kinaitwa throughputambayo kwetu sisi vilevile tutafadika nayo mbali na kodimbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niseme tu kwambakatika hili bomba linaliopita kama ingewezekana, maananimeambiwa kwamba bomba hili tunalijenga sisi, Serikali yaUganda pamoja na Kampuni za mafuta ikiwemo Total. Basikama tungeweza ni vizuri na sisi nasi kama Serikalitungeongeza nguvu zaidi au mtaji mkubwa ilio kwenye lilegawiwo tutakalokuwa tunapata basi tuweze kupata kiasikikubwa zaidi kuliko ambacho tunachoweza kupata kwasasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba, jambolingine ambalo limenifurahisha ni pale ambapo Serikai iliamuakuweka nafasi kubwa ambayo itapitisha bomba la gesi,

Page 129: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

129

ikiwezekana na miundombinu mingine labda bomba lamafuta ghafi lakini ikiwezekana na bomba la gesi

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niseme, kamainawezekana hebu Serikali ione uwezekano wa kupitishabomba la mafuta kutoka Tanga litakalokwenda sambambampaka kule Uganda. Hilo bomba kama endepo litakuwepovilevile litakuwa na manufaa makubwa. Kwanza, kama nigharama za fidia tutakuwa tumeshalipa kwa hiyo tayari eneotutakuwa nalo. Hata hivyo leo itoshe tu kusema kwambawenzetu majirani mafuta yanafika Mombasa lakiniwanaweza kuuza Uganda, Rwanda, Burundi na hata DRCkushinda sisi siyo kwa sababu nyingine, ni kwa sababu wanabomba la mafuta linalotoka Mombasa mpaka Kisumu;Mombasa mpaka Eldoret.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa sababu na sisinafasi hii tumeipata, ukweli wa ni kwamba ukiweka bombakutoka Tanga la mafuta likaenda mpaka Uganda maanayake sisi tutakuwa tumeshaminya zaidi ya kilometa 400,tutakuwa tuna kilometa 400 chini ya wao. Kwa hiyo tafsiriyake ni kwamba gaharama za mafuta kufika kwenye hizonchi zitakuwa ni ndogo kwahiyo vilevile tutaendeleakufaidika zaidi kuliko wao kwa hiyo, hiyo kwetu itakuwacompetitive advantage kama nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nitahadharishe tu juufaida ambayo tunayo lakini hatuiangalii sana, kwambasambamba na hili bomba la mafuta gahfi tulilonalo tunayomiradi kama hii. Kwa mfano liko bomba hili la TAZAMAambalo linatoka Dar es salaam mpaka kwa wenzetu kuleZambia pale Kapirimposhi na Ndola.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hili bomba hatulitumiisana, ni bomba la mafuta ghafi pamoja na mafuta masafi,lakini cha ajabu ni kwamba tunaacha kutumia lile bombalakini malori mengi yanapitisha mafuta kupeleka huko namtokeo yake ni kwamba kwanza yanaendelea kuharibubarabara lakini na gharama za uendeshaji nazo zinakuwakubwa. Kwa hiyo, ni vizuri tukaangalia namna tunavyoweza

Page 130: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

130

kutumia hii miundombinu ambayo kwangu mimi ninaaminikabisa kwamba tukiitumia vizuri inaweza ikatuletea faidazaidi; ukilinganisha kwamba kwa Tanzania kijiografiatumekaa vizuri, kwamba inatupa nafasi nzuri zaidi ya kufanyabiashara na wenzetu wanaotuzunguka kuliko wenztu ambaowako pembezoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo bada ya kusemahayo, na mimi naunagana na wenzangu kwa kuipongezaSerikali kwa kazi hii ambayo wameifanya kwa haraka, lakininiseme tu kwamba naunga mkono hoja. Ahsante sana.

NAIBU SPIKA: Ahsante sana. Sasa nimwite mtoa hojaMheshimiwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezokwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria uje uhitimishe hoja.

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO(K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa naibuSpika, nianze kwa kuwapongeza Waheshimiwa Wabungewote kwa kuonesha kupitia michango yao mbalimbali hapa,kwa kweli mshikamano na Serikali katika suala hili kimsingisimuoni hata mmoja ambaye anaona kwamba huu mradihauna tija kwetu. Wote wanaunga mkono, na ni maeneomachache tu ambayo Waheshimiwa Wabunge wanatakakufanyike fine tuning (marekebisho ya uboreshaji) na kuipaSerikali tahadhari hapa na pale, hayo tunayapokea. (Makofi)

Waheshimiwa Wabunge waliochangia hoja hii nisaba, sita kwa kuongea na mmoja kwa maandishi; na hojakubwa ambayo nimeiona katika michango yote hapa,pengine nianze na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini; nikuwa mkataba huu ukiuangalia kwa umakini unakinzanana Sheria yetu ya mamlaka ya nchi kuhusiana na umiliki warasilimali na maliasili na unaiona hoja hiyo hiyo ikitolewa naKambi Rasmi ya Upinzani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nil ikuwa naombaniiongelee kwa kifupi hoja hiyo. Naomba nianze kusisitizakwamba Sheria yetu hii ya Maliasili na Rasilimali tuliyoipitisha,ya sovereignty inahusu maliasili zetu. Katika mkataba huu na

Page 131: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

131

mradi huu, tunachokiongelea hapa ni mafuta ya Uganda.Sisi ni wasafirishaji, sisi tuna lori lakini mikungu ya ndizi iliyokondani tunayoitoa Kyela kuileta Dar es Salaam si yetu ndiyomaana naona maudhui ya sasa hayaoani na yale ya Sheriaya permanent sovereignty.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukumbuke kwa mfano juzihapa tumepitisha Sheria hapa ya Azimio la Bonde la MtoSongwe lililetwa tena hilo suala. Sasa hizi ni shared resources,sasa wakati tunakuta nchi mbili zenye sovereignty zimekaapamoja, lakini sisi sheria yetu ndiyo ikachukua pre-dorminantsna ikawa na over-riding effect kupita sheria zao wenyewepia wenzetu upande wa pili hilo katika sheria za kimataifasijawahi kuliona. Mnakaa chini mnajadiliana na mkataba huuni zao la makubaliano kati ya nchi mbili zenye sovereignty.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunafaidika na kodi, kwaajira pamoja biashara kadhaa zitakazojitokeza. Mimi pengineniungane na Profesa Tibaijuka hapa amesisitiza pia. Hebutuone tofauti kati ya mkataba, tuna mikataba ya madini naSerikali, ni tofauti na mikataba kati ya Serikali na Serikaliambazo ni international treaties ipo tofauti kubwa naombatusiichanganye. Mimi nakushukuru sana Profesa Tibaijukakwahuo mchango wako.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tumepokea hojanzuri tu kutoka kwa Kambi Rasmi ya Upinzani lakini kuhusukifungu cha pili kiko katika ukurasa wa tatu wa hotuba yaKambi ya Upinzani; kwamba kifungu hiki kinazuia taarifa nakwamba inafanana kabisa na mikataba inayoingiwa kisirisirina mpaka hata Bunge hili linanyimwa hizo taarifa. Nilitakatu kusema kuwa kifungu hiki hakizuii utoaji wa taarifa, balikinaweka utaratibu bora tu wa kutoa taarifa hiyo kwakuitaarifu nchi iliyotoa taarifa nayo iweze kutoa taarifa yake,ni heshima tu. Ni sawa na kusema leo hii sisi Wabunge tunahaki ya kuwa na mikataba, lakini huendi tu wewemwenyewe moja kwa moja kwenda kuchukua, unapitia kwaSpika. Sasa huo utaratibu wa kupitia kwa Spika ikaonekanani kizuizi hilo itakuwa ni tatizo.

Page 132: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

132

Mheshimiwa Naibu Spika, nil itaka kusema tukwamba, haya tu ni makubaliano kati ya nchi na nchi, niutaratibu tu kama ule ambao tumejiwekea hapa hata wamikataba, hebu pata ridhaa basi ya nchi mwenzako.Mwenzano amekupa taarifa sasa wewe unaisambaza tumaan taarifa inahitajika na Bunge. Mimi nina uhakika kwaushirikiano tulionao, Uganda si nchi ya kigeni, si nchi iliyo njeya bara hili, ni majirani zetu, wote tuko chini ya East AfricanCommunity mimi nina uhakika mambo yatakuwa mazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile si kweli kuwatumetoa uhuru mkubwa mno kwa Uganda kiasi cha kwambatumewapa hata umilikiwa wa Chongoleani ya Tanga,habana. Tulichofanya sisi ni kuipa Uganda haki ambazozinasimamiwa na sheria za kimataifa. Uganda ni land lockedstate na land locked state zote duniani zina haki zao sawahasa ukisoma Sheria yetu hii UN Convention on the Law ofthe Sea, wana haki ya kupewa treatment ya kupitisha mizigoyao, kuwapa haki sawa, wasijisikie kwamba wanapotezakwa kufanya hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo wameongea wotewanaoguswa na bomba, nimefurahi sana. MheshimiwaMussa Mbarouk anasema tuwe waangalifu na fidia ya ardhikwa wananchi wetu. Mimi nafikiri hil i ni wazo zuri,tumelipokea na tunaomba sasa Serikali haina mikono mingi,sisi wawakilishi wa wananchi bomba litapita kwenye maeneoyetu, sisi tuwe mstari wa mbele kutetea haki za wananchiwetu hasa upande wa ardhi. Serikali itaweza kuchukua hatuatukisikia wawakilishi wa wananchi mko mstari wa mbele nakusema hapana, hapa kunaonekana kuna hitilafu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna hoja yakuwapa priority aliyotoa Mheshimiwa Mbarouk, kwambatutoe priority ya ajira kwa wale wanaopitiwa na mradi, hiyoni sahihi kabisa, hili ni suala la utekelezaji. Hata hivyo naombanisisitize kwamba mradi huu tumesema unatekelezwa naprivate sector ambayo inahitaji efficiency, inahitaji kukimbiliafursa. Huwezi tu umekaa chini ya mwembe sasa wewe kwasababu unapita kwako basi ubembelezwe ili ukafanye kazi

Page 133: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

133

pale. Tuchangamkie fursa na Waheshimiwa Wabunge tuwemstari wa mbele kuchangamkia fursa kwa niaba yawananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa ProfesaTibaijuka kwa kweli nakushukuru sana kwa michango yako.Mimi nafikiri…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri subiri kidogo.Waheshimiwa Wabunge kwa mujibu wa Kanuni ya 28(2)nataka kuongeza muda wa nusu saa ili tumalizie hoja hii yaMheshimiwa Waziri hapa. Kwa hivyo nitawahoji maana fasilihii inaitaka niwahoji.

(Hoja Ilitolewa Iamuliwe)(Hoja Iliamuliwa na Kuafikiwa)

NAIBU SPIKA: Sawa, ili kumbukumbu zikae sawa sawa,Wabunge wamehojiwa kuongeza nusu saa na wamekubali.Mheshimiwa Waziri.

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO(K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa NaibuSpika, nashukuru kwa ongezeko hili la muda ingawasijawatendea haki wale wa mwanzo nilikuwa nakimbia kwasababu najua muda ulikuwa umekwisha. Hata hivyo,naomba tu nimshukuru sana Mheshimiwa Profesa Tibaijuka,ameongelea suala la ulinzi. Kwa kweli suala la ulinzi ni kitumuhimu sana kwetu wote Watanzania. Bomba hili ambalolinalopita nchini kwetu lina faida, lina tija kwa Taifa na kamaalivyosema, ni wajibu wetu mkubwa Watanzania wotekuhakikisha usalama wa hili bomba.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Nkamia nayevilevile kama ilivyo kwa Mbarouk, kama ilivyo kwa ProfesaTibaijuka, wote wamepitiwa na hili bomba na MheshimiwaNkamia amesisitiza kuhusu ulipwaji wa fidia stahili na kwamuda muafaka. Mimi nafikiri hili ni suala la muhimu,tunalipokea kama Serikali, ni masuala haya ya utekelezajiambayo lazima angalizo tulichukue. Lakini vilevile kuna kitu

Page 134: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

134

kimoja ambacho ningependa nikiongelee kidogo,ameongelea kuhusu suala la kiwango cha pesatutakachopata kila siku, amesema ni kikubwa sana. Najuatunafaidika, lakini tusije tuka-exaggerate kiasi cha kupatatukafika mahali ambapo sasa kesho asubuhi tukadaiwa kilamtu anunuliwe bajaj.

Mheshimiwa Naibu Spika, kiwango cha pesatutakachopata, tukisoma vizuri maelezo niliyoyatoa nikwamba kila pipa lita-generate dola 12.2; sawa, kwa sikukutakuwa na mapipa 216,000 lakini pesa hiyo si kwamba yoteinakuja Tanzania, kisome vizuri kile kifungu, tukisoma vizurikile kifungu ni pesa inatosha kwa sababu hapa tunaongeleaeconomies of scale, hatimaye tunapata pesa ya kutosha;lakini si kwa kiasi ambacho kilioneshwa na MheshimiwaNkamia kwamba hiyo yote sasa inakuja kwetu hapana!Itakwenda in proportion na hisa zetu. Naomba tuisome vizurihiyo provision, itakwenda in proportion na hisa. Pamoja naangalizo hilo bado pesa ni nzuri, tunafaidika at the end ofthe day.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kumshukurusana Mheshimiwa Vedastus Manyinyi ambaye kwa kweli nikama amerudia tu hoja za wenzako zote. Hata hivyo nisisitizekitu kimoja; kwamba mradi huu haujadondoka kwetu kamazawadi au kama embe dodo tu umekaa chini ya mtilikadondoka, tumeupigania kama Taifa. Ndiyo maanatumemshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa aliyofanya yakidiplomasia kuweza kushawishi nchi jirani kwamba njia borakupitisha bomba hilo ni Tanzania na faida ni kubwa sana,na ndiyo maana hata ukiisoma hotuba ya upinzani hiloimekubali kabisa kwamba kwa kweli huu mradi una tijakubwa kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe wito tu kwaWatanzania kwamba lazima maeneo ambayo mradiunapita na vilevile Mkoa wa Tanga wenyewe ambapo ndiyohatma ya hilo bomba kuishia naomba jamanituzichangamkie fursa tele ambazo zinajitokeza. Nilipokuwa

Page 135: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

135

Tanga kwenye mkutano wa biashara tulikuwa naMheshimiwa Mbarouk, nilitoa taarifa kwamba tayari kunawatu (agents) wapo Tanga na Dar es Salaam wakishawishimakampuni yatakayokuwa based Tanga pale kwamba aah!Sehemu nzuri kukaa ni jirani tu hapa, kuna mahoteli mazurimnakuja kwa gari asubuhi au kwa helikopta. Sasa hiyoWatanzania tumeshajifunza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna sehemu tulikuwatunachoronga kule Songosongo, watu walikuwa wanakujana ndege asubuhi kulala. Ni fursa sasa kujenga mahoteli yakutosha, fursa sasa kujenga miundombinu ya maisha ya kilasiku kwa sababu watakaokuwepo Tanga wana watotowatahitaji kwenda shule, wana familia zitahitaji hospitali,wana familia zitahitaji hospitali, maduka ya dawa mazurina huduma mbalimbali. Ndiyo maana nasema, la msingikabisa hapa si Serikali tena, ni sisi Watanzania kuchangamkiafursa zilizopo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja.(Makofi)

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.

NAIBU SPIKA: Hoja imeungwa mkono. SasaWaheshimiwa Wabunge, nitawahoji.

(Hoja Ilitolewa Iamuliwe)(Hoja Iliamuliwa na Kuafikiwa)

(Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba (Inter-governmentalAgreement – IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamuhuri yaUganda kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bomba la

Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki(East Africa Crude Oil Pipeline – EACOP)

kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania) liliridhiwa na Bunge)

Page 136: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1510754052-11 SEPTEMBER 2017.pdf · linatolewa na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayotoa

NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)

136

NAIBU SPIKA: Walioafiki wameshinda, kwa hiyo Azimiohili limeridhiwa na Bunge. (Makofi)

Waheshimiwa Wabunge, nichukue fursa hiikuwashukuru sana kwa kazi nzuri mliyoifanya kwa ngazi yaKamati kwa niaba yetu sisi sote, lakini pia kwa michangoyenu hapa ndani ambayo imempa fursa Mheshimiwa Wazirikutoa ufafanuzi kwa yale ambayo yalikuwa penginehatukuyaelewa vizuri.

Pia nichukue fursa hii kuipongeza sana Serikali kwakuhakikisha jambo hili linaenda kwa haraka kama ambavyoMheshimiwa Rais angependa liende. Mmefanya vyemakutuletea Wabunge ili tuweze kujua ni mambo ganiyanaendelea kuhusu bomba hili, na tumepata fursa sasa yakuipitia na mwisho kupitisha azimio la kuridhia mkataba huu.

Kwa hiyo, tuwatakie kila la kheri katika utekelezaji,na sisi tunaamini kwa sababu kuna changamoto nyingi sanakatika Wizara ya Nishati na Madini, kila wakati huwa kunajambo.

Sasa tunaomba Serikali katika mkataba huu tujetuyasikie mazuri tu wakati mnatoa taarifa kupitia Kamati,Kamati itakapokuwa inatueleza hapa kuhusu utekelezaji basimambo yawe yameenda vizuri kama ambavyo leommepata fursa ya kutueleza hapa.

Waheshimiwa Wabunge, kabla sijaahirisha shughuliza Bunge niwatake wale ambao Kamati zao zinaendeleana kazi kwenda mchana huu kwenye hizo Kamati ili mkapatekukamilisha kazi ambazo kesho tunatakiwa kuzitazama hapaBungeni.

Baada ya kusema hayo, naahirisha shughuli za Bungempaka kesho, siku ya Jumanne saa tatu asubuhi.

(Saa 7.10 Mchana Bunge lilisitishwa mpaka Siku yaJumanne, Tarehe 12 Septemba, 2017, Saa Tatu Asubuhi)