Upload
others
View
4
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
TAKWIMU ZA WAFUNGWA NA MAHABUSU
TANZANIA BARA MWAKA
2013 NA 2014
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Dar es Salaam
Ofisi ya Taifa ya Takwimu
Wizara ya Fedha
Dar es Salaam
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
i
YALIYOMO
Orodha ya Majedwali ........................................................................................................................... v
Orodha ya Michoro ........................................................................................................................... viii
Majedwali Ambatanisho ..................................................................................................................... ix
Maana ya Vifupisho ............................................................................................................................ xi
Dibaji .................................................................................................................................. xii
Shukrani ................................................................................................................................. xiii
Muhtasari ................................................................................................................................. xiv
SURA YA KWANZA ......................................................................................................................... 1
USULI ............................................................................................................................................... 1
1.0 Utangulizi ............................................................................................................................... 1
1.1 Jiografia na Utawala............................................................................................................... 1
1.2 Jeshi la Magereza ................................................................................................................... 2
1.2.1 Majukumu ya Jeshi la Magereza ........................................................................................... 2
1.2.2 Takwimu za Jeshi la Magereza ............................................................................................. 2
1.2.3 Kitengo cha Takwimu cha Jeshi la Magereza ....................................................................... 3
SURA YA PILI ................................................................................................................................... 4
HALI YA MAGEREZA NCHINI .................................................................................................... 4
2.0 Utangulizi ............................................................................................................................... 4
2.1 Muhtasari wa Hali ya Magereza ............................................................................................ 4
SURA YA TATU ................................................................................................................................ 5
TAKWIMU ZA WAHALIFU WALIOKUWEPO MAGEREZANI ..............................................
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
ii
5
3.0 Utangulizi ............................................................................................................................... 5
3.1 Takwimu za Wahalifu kwa Mikoa na Jinsi ............................................................................ 5
3.2 Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Umri ........................................................ 7
3.3 Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Jinsi na Tabia .............................................. 9
3.4 Wafungwa wa Adhabu ya Kifo Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Hali ya Rufaa. ....... 11
3.5 Wafungwa Watu Wazima na Vijana Waliobaki Magerezani kwa Jinsi na Aina ya
Kosa .................................................................................................................................. 12
3.6 Wafungwa Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo ...... 14
3.7 Mahabusu Watu Wazima na Vijana Waliokuwepo Magerezani Kusubiri Kesi kwa
Jinsi, Aina ya Kosa na Muda Waliokaa Gerezani ................................................................ 16
3.8 Wahalifu Wenye Ugonjwa wa Akili Waliobaki Magerezani .............................................. 20
3.9 Wahalifu wanawake wajawazito na wenye watoto.............................................................. 20
3.10 Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani, kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Nchi
Walizotoka ........................................................................................................................... 22
3.11 Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya Kosa na Jinsi ................... 24
SURA YA NNE ................................................................................................................................. 26
WAHALIFU WALIOPOKELEWA MAGEREZANI KUTOKA MAHAKAMANI ................ 26
4.0 Utangulizi ............................................................................................................................. 26
4.1 Wahalifu Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani, kwa Jinsi na Mkoa .............. 26
4.2 Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Umri, Jinsi na
Mikoa .................................................................................................................................. 29
4.3 Wafungwa Warudiaji Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na
Mkoa .................................................................................................................................. 32
4.4 Wafungwa Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa
Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo ........................................................................... 34
4.5 Wafungwa Vijana Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina
ya kosa na Urefu wa Kifungo .............................................................................................. 37
4.6 Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Kushindwa
Kulipa Faini kwa Mkoa na Urefu wa Vifungo .................................................................... 40
4.7 Wafungwa Wagonjwa wa Akili Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani
kwa Jinsi na Mkoa ............................................................................................................... 41
4.8 Wahalifu Wanawake Wajawazito na Wenye Watoto Waliopokelewa Magerezani
Toka Mahakamani kwa Aina ya Kosa ................................................................................. 41
4.9 Mahabusu Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa
Jinsi, Aina ya kosa na Muda wa Kusubiri Hukumu ............................................................. 42
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
iii
4.10 Mahabusu Vijana Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina
ya kosa na Muda wa Kusubiri Hukumu ............................................................................... 44
4.11 Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi
na Nchi Walizotoka .............................................................................................................. 45
4.12 Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi
na Nchi Wanazotoka ............................................................................................................ 46
SURA YA TANO .............................................................................................................................. 49
WAHALIFU WALIOHAMISHWA KUTOKA GEREZA MOJA KWENDA JINGINE ........ 49
5.0 Utangulizi ............................................................................................................................. 49
5.1 Wahalifu Waliohamishwa kwa Jinsi na Mkoa ..................................................................... 49
5.2 Wafungwa wenye Ugonjwa wa Akili kwa Jinsi na Mkoa Waliopokelewa kutoka
Magereza Mengine ............................................................................................................... 51
SURA YA SITA ................................................................................................................................ 52
WAHALIFU WALIOTOKA MAGEREZANI ............................................................................. 52
6.0 Utangulizi ............................................................................................................................. 52
6.1 Wahalifu Waliotoka Magerezani Mwaka 2013 na 2014 ..................................................... 52
6.2 Wafungwa Walioachiwa kwenda Kutumikia Kifungo cha Nje kwa Jinsi na Mkoa ............ 55
6.3 Wafungwa Walioachiwa Baada ya Kulipa Faini kwa Urefu wa Kifungo na Mkoa ............ 58
6.4 Wahalifu Waliotoroka Magerezani Chini ya Ulinzi Halali Magerezani kwa Jinsi na
Mkoa .................................................................................................................................. 59
6.5 Wahalifu Waliofariki Magerezani kwa Jinsi na Mkoa ........................................................ 60
SURA YA SABA .............................................................................................................................. 62
WAHALIFU WALIOPEWA ADHABU KWA MAKOSA YA UTOVU WA NIDHAMU
WAKIWA MAGEREZANI ............................................................................................................ 62
7.0 Utangulizi ............................................................................................................................. 62
7.1 Wahalifu Waliopewa Adhabu Magerezani kwa Aina ya Adhabu na Mkoa ........................ 62
SURA YA NANE .............................................................................................................................. 65
MAHABUSU WALIOHUKUMIWA ADHABU ZA VIFUNGO WAKIWA MAGEREZANI 65
8.0 Utangulizi ............................................................................................................................. 65
8.1 Mahabusu Waliohukumiwa Wakiwa Magerezani kwa Jinsi na Mkoa ................................ 65
SURA YA TISA ................................................................................................................................ 67
HITIMISHO ..................................................................................................................................... 67
9.0 Utangulizi ............................................................................................................................. 67
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
iv
9.1 Hitimisho .............................................................................................................................. 67
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
v
Orodha ya Majedwali
Jedwali 3.1: Idadi ya Wahalifu Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Jinsi, Tanzania Bara,
2013 na 2014 ............................................................................................................... 6
Jedwali 3.2: Idadi ya Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Umri, Tanzania Bara,
2013 na 2014 ............................................................................................................... 8
Jedwali 3.3: Idadi ya Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Jinsi na Tabia,
Tanzania Bara, 2013 na 2014 ................................................................................... 10
Jedwali 3.4: Idadi ya wafungwa wa Adhabu ya Kifo Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na
Hali ya Rufaa, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ........................................................... 11
Jedwali 3.5: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima na Vijana Waliobaki Magerezani kwa Jinsi
na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ....................................................... 13
Jedwali 3.6: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi na
Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara, 2013 na 2014 .................................................... 14
Jedwali 3.7: Idadi ya Mahabusu Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi na Aina ya Kosa,
Tanzania Bara, 2013 na 2014 ................................................................................... 16
Jedwali 3.8 Idadi ya Wahalifu Wanawake Wajawazito na Wenye Watoto kwa Aina ya
Kosa, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ......................................................................... 21
Jedwali 3.9: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi na Aina
ya Kosa Tanzania Bara, 2013 na 2014 ..................................................................... 22
Jedwali 3.10: Idadi ya .Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya Kosa
na Jinsi Tanzania Bara, 2013 na 2014 ...................................................................... 24
Jedwali 3.11: Idaddi ya Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi na Nchi
Walizotoka, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ............................................................... 25
Jedwali 4.1: Idadi ya Wahalifu Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi
na Mkoa , Tanzania Bara, 2013 na 2014 .................................................................. 27
Jedwali 4.2: Idadi wa Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa
Umri, Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara, 2013 .............................................................. 30
Jedwali 4.3: Idadi ya Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani Kwa
Umri, Jinsi na Mkoa , Tanzania Bara, 2014 ............................................................. 30
Jedwali 4.4: Idadi ya Wafungwa Warudiaji Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Jinsi, Mkoa na Urudiaji wa Kifungo, Tanzania Bara, 2013 ........ 32
Jedwali 4.5: Idadi ya Wafungwa Warudiaji Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Jinsi, Mkoa na Urudiaji wa Kifungo, Tanzania Bara, 2014 ........ 33
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
vi
Jedwali 4.6: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara,
2013 .......................................................................................................................... 35
Jedwali 4.7: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara,
2014 .......................................................................................................................... 36
Jedwali 4.8: Idadi ya Wafungwa Vijana Waliopokolewa Magerezani Kutoka Mahakamani
kwa Jinsi, Aina ya kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara, 2013 ...................... 38
Jedwali 4.9: Idadi ya Wafungwa Vijana Waliopokolewa Magerezani Kutoka Mahakamani
kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara, 2014 ..................... 39
Jedwali 4.10: Idadi ya Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa
Kushindwa Kulipa Faini kwa Mkoa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara, 2013
na 2014 ...................................................................................................................... 40
Jedwali 4.11: Idadi ya Wahalifu Wanawake Wajawazito na Wenye Watoto Waliopokelewa
Magerezani Toka Mahakamani Kulingana na Aina ya Kosa, Tanzania Bara,
2013 na 2014 ............................................................................................................. 42
Jedwali 4.12: Idadi ya Mahabusu Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Muda wa Kusubiri Hukumu,
Tanzania Bara, 2013 na 2014 ................................................................................... 43
Jedwali 4.13: Idadi ya Mahabusu Vijana Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani
kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Muda wa Kusubiri Hukumu, Tanzania Bara, 2013
na 2014 ...................................................................................................................... 44
Jedwali 4.14: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Jinsi na Nchi Walizotoka, Tanzania Bara, 2013 na 2014. .......... 45
Jedwali 4.15: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Jinsi na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ................. 46
Jedwali 4.16: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Jinsi na Nchi Walizotoka, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ........... 47
Jedwali 4.17: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Jinsi na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ................. 48
Jedwali 5.1: Idadi ya wahalifu Waliohamishwa kwa Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara, 2013 na
2014 .......................................................................................................................... 50
Jedwali 6.1: Idadi ya Wahalifu Waliotoka Magerezani kwa Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara,
2013 .......................................................................................................................... 53
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
vii
Jedwali 6.2: Idadi ya Wahalifu Waliotoka Magerezani kwa Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara,
2014 .......................................................................................................................... 54
Jedwali 6.3: Idadi Ya Wafungwa Walioachiwa kwenda Kutumikia Kifungo cha Nje kwa
Jinsi na Mkoa , Tanzania Bara, 2013 na 2014 .......................................................... 56
Jedwali 6.4: Idadi ya Wafungwa Walioachiwa Baada ya Kulipa Faini kwa Urefu wa
Kifungo na Mkoa , Tanzania Bara, 2013 na 2014. ................................................... 58
Jedwali 6.5: Idadi ya Wahalifu Waliotoroka Magerezani Chini ya Ulinzi Halali kwa Jinsi na
Mkoa , Tanzania Bara, 2013 na 2014 ....................................................................... 59
Jedwali 6.6: Idadi ya Wahalifu Waliofariki Magerezani kwa Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara,
2013 na 2014. ............................................................................................................ 61
Jedwali 7. 1: Idadi ya Wahalifu Waliopewa Adhabu Magerezani kwa Aina ya Adhabu na
Mkoa , Tanzania Bara, 2013 ..................................................................................... 63
Jedwali 7.2: Idadi ya Wahalifu Waliopewa Adhabu Magerezani kwa Aina ya Adhabu na
Mkoa, Tanzania Bara, 2014 ...................................................................................... 64
Jedwali 8.1: Idadi ya Mahabusu Waliohukumiwa Wakiwa Magerezani kwa Jinsi na Mkoa,
Tanzania Bara, 2013 na 2014 ................................................................................... 66
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
viii
Orodha ya Michoro
Mchoro 3.1: Wahalifu Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Jinsi, Tanzania Bara, 2013 na
2014 .............................................................................................................................. 7
Mchoro 3.2: Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Umri, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ............. 9
Mchoro 3.3: Wafungwa wa Adhabu ya Kifo Waliobaki Magerezani na Hali ya Rufaa,
Tanzania Bara, 2013 na 2014 ..................................................................................... 12
Mchoro 3.4: Wafungwa Watu Wazima na Vijana Waliobaki Magerezani, Tanzania Bara,
2013 na 2014 .............................................................................................................. 14
Mchoro 3.5: Idadi ya Wafungwa Waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya Kosa na Urefu wa
Kifungo, Tanzania Bara, 2013 na 2014. .................................................................... 15
Mchoro 3.6: Mahabusu Watu Wazima na Vijana Waliokuwepo Magerezani, Tanzania Bara,
2013 na 2014 .............................................................................................................. 17
Mchoro 3.7: Idadi ya Mahabusu Watu Wazima Waliokuwepo Magerezani na Kusubiri Kesi
kwa Aina ya Kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania Bara, 2013 na 2014....... 18
Mchoro 3.8: Idadi ya mahabusu vijana waliokuwepo magerezani na kusubiri kesi kwa aina
ya kosa na muda waliokaa gerezani, Tanzania Bara 2013 na 2014. .......................... 19
Mchoro 3.9: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi
Walizotoka, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ................................................................ 23
Mchoro 4.1: Wahalifu Waliopokelewa MaGerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na
Mikoa, Tanzania Bara, 2013 na 2014 ........................................................................ 28
Mchoro 4.2: Wafungwa Warudiaji Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani,
Tanzania Bara, 2013 na 2014 ..................................................................................... 34
Mchoro 6.1: Idadi ya Wahalifu Waliotoka Magerezani, Tanzania Bara, 2013 na 2014 .............. 55
Mchoro 6.2: Wafungwa Walioachiwa kwenda Kutumikia Kifungo cha Nje kwa Jinsi na
Mkoa , Tanzania Bara, 2013 na 2014. ....................................................................... 57
Mchoro 6.3: Wahalifu Waliotoroka Magerezani Chini ya Ulinzi Halali, Tanzania Bara, 2013
na 2014. ...................................................................................................................... 60
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
ix
Majedwali Ambatanisho
Jedwali Na. 1: Idadi ya Wahalifu Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Jinsi na Aina ya
Uhalifu, Tanzania Bara, 2013 ................................................................................. 68
Jedwali Na. 2: Idadi ya Wahalifu Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Jinsi na Aina ya
Uhalifu Tanzania Bara, 2014 .................................................................................. 69
Jedwali Na. 3: Idadi ya Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Umri na Jinsi,
Tanzania Bara, 2013 ............................................................................................... 70
Jedwali Na. 4: Idadi ya Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Umri na Jinsi,
Tanzania Bara, 2014 ............................................................................................... 71
Jedwali Na. 5: Idadi ya Wafungwa wa Adhabu ya Kifo Waliobaki Magerezani kwa Mkoa,
Jinsi na Hali ya Rufaa, Tanzania Bara, 2013 na 2014 .......................................... 722
Jedwali Na. 6: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya
Kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara, 2013 .................................................. 73
Jedwali Na. 7: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya
kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara, 2014 ................................................... 74
Jedwali Na. 8: Idadi ya Mahabusu Watu Wazima waliokuwepo Magerezani, Kusubiri Kesi
kwa Aina ya kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania Bara, 2013 .................. 75
Jedwali Na. 9: Idadi ya Mahabusu Watu Wazima Waliokuwepo Magerezani, Kusubiri Kesi
kwa Aina ya Kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania Bara, 2014 ................. 76
Jedwali Na. 10: Idadi ya Mahabusu Vijana Waliokuwepo Magerezani, Kusubiri Kesi kwa
Aina ya Kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania, Bara, 2013 ........................ 77
Jedwali Na. 11: Idadi ya Mahabusu Vijana Waliokuwepo Magereani, Kusubiri Kesi kwa
Aina ya kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania Bara, 2014 .......................... 78
Jedwali Na. 12: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi Walizotoka
na Aina yaKosa, Tanzania Bara, 2013 ………………………………………… 79
Jedwali Na. 13: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi
Walizotoka na Aina yaKosa, Tanzania Bara, 2014 ................................................ 80
Jedwali Na. 14: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi
Walizotoka na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 ............................................... 81
Jedwali Na. 15: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi
Walizotoka na Ainan ya Kosa, Tanzania Bara, 2014 ............................................. 82
Jedwali Na. 16: Idadi ya Wahalifu Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa
Mkoa, Aina ya Muharifu na Jinsi, Tanzania Bara, 2013 ........................................ 84
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
x
Jedwali Na. 17: Idadi ya Wahalifu Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa
Mkoa, Aina ya Muharifu na Jinsi, Tanzania Bara, 2014 ........................................ 85
Jedwali Na.18: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Nchi Walizotoka na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 ......... 86
Jedwali Na.19: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka
Mahakamani kwa Nchi Walizotoka na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2014 ......... 87
Jedwali Na. 20: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Toka
Mahakamani kwa Nchi na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 ............................. 88
Jedwali Na. 21: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Toka
Mahakamani kwa Nchi na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2014 ............................. 89
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
xi
MAANA YA VIFUPISHO
A/INSP - Mkaguzi Msaidizi wa Magereza
ASP - Mrakibu Msaidizi wa Magereza
CGP - Kamishna Jenerali wa Magereza
CP - Kamishna wa Magereza
CPL - Corporal
Dkt - Daktari
DPRK - Korea ya Kaskazini
DRC - Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
EASTC - Chuo cha Takwimu cha Mashariki na Kusini mwa Afrika
Ke - Mwanamke
Me - Mwanaume
MKUKUTA - Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania
NBS - Ofisi ya Taifa ya Takwimu
O/I - Mkuu wa Gereza
RPO - Mkuu wa Magereza wa Mkoa
SP - Mrakibu wa Magereza
S/SGT - Sajin Taji
SGT - Sajenti
SSP - Mrakibu Mwandamizi wa Magereza
TPS - Jeshi la Magereza Tanzania
TSMP - Mpango Kabambe wa Kuboresha Takwimu Tanzania
TPF - Jeshi la Polisi Tanzania
UK - Uingereza
V - Vijana
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
xii
DIBAJI
Jeshi la Magereza Tanzania Bara limeanza kutoa
taarifa za kitakwimu za wafungwa na mahabusu
waliopo magerezani kwa lengo la kuonesha idadi ya
wahalifu waliopo, aina za wahalifu, hukumu, sifa na
tabia za wahalifu hao.
Taarifa hizi zitaliwezesha Jeshi la Magereza
kuboresha maeneo mbalimbali kama vile rasilimali
watu, fedha na vifaa ili kuweza kupanga mikakati na
mbinu mbalimbali zitakazotuwezesha kuwahifadhi
na kuwarekebisha wafungwa waliopo magerezani
mpaka watakapomaliza adhabu zao kwa mujibu wa
sheria.
Hivi sasa Jeshi limebaini kuwa upo umuhimu wa
kuboresha taarifa zake ili ziweze kwenda na
wakati. Aidha, Jeshi la Magereza, kwa kushirikiana
na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) chini ya
Mpango Kabambe wa Kitaifa wa Kuboresha na Kuimarisha Takwimu Tanzania, litakuwa linatoa
taarifa mbalimbali za kitakwimu kutokana na data za ndani ya jeshi. Taarifa hizo, zitakuwa ni
pamoja na za wafungwa na mahabusu kila baada ya kipindi cha robo mwaka ambazo baadae
zitatumika kuandaa taarifa za mwaka mzima.
Taarifa hizi zitaonesha hali halisi itakayoliwezesha jeshi hili kujipanga vyema ili kuweza kuyafikia
malengo yaliyowekwa, mojawapo likiwa ni kupunguza uhalifu kama ilivyoainishwa kwenye
MKUKUTA.
Dkt. Juma A. Malewa,
Kamishna Jenerali wa Magereza,
Jeshi la Magereza Tanzania Bara,
DAR ES SALAAM.
Dkt. Juma A. Malewa
Kamishna Jenerali wa Magereza
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
xiii
SHUKRANI
Katika kukamilisha kazi hii, maofisa na askari magereza,
wataalam kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, pamoja na wadau
mbalimbali wamehusika wakiongozwa na Mrakibu
Mwandamizi wa Magereza Marco Kilumbo. Shukrani za
kipekee ziwaendee Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt.Juma
A. Malewa, Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini kwa kutoa
maelekezo mbalimbali yaliyofanikisha kukamilika kwa kazi hii
pamoja na kuwatia moyo watendaji wakati wa kuandaa taarifa
hii na Dkt. Albina Chuwa, Mkurugenzi Mkuu, Ofisi ya Taifa ya
Takwimu ambaye kwa kupitia mradi wa TSMP aliwaruhusu
wataalamu wake washirikiane na watendaji wa Magereza
kufanikisha uandaaji wa Taarifa hii. Pia shukrani ziwaendee
Kamishina Jenerali wa Magereza Mstaafu, John C. Minja na
Kamishna wa Magereza Mstaafu, D.L. Chamulesile ambao
kwa njia moja ama nyingine wameshiriki katika kutoa ushauri
uliofanikisha kukamilika kwa kazi hii.
Aidha, shukrani za kipekee ziwaendee wataalamu walioshiriki katika uandishi wa ripoti
hii;Valerian Tesha (NBS), SP-Emmanuel Pagali (TPS), ASP-Joseph Siwale (TPS), ASP-Deodatus
Kazinja (TPS), S/SGT-Magdalena Landa (TPS), SGT-Ruth Mshiu (TPS), SGT-Consolatha Ragije
(TPS), SGT-Desdery Mallya (TPS), CPL-Regnald Shaban (TPS), Ibrahimu Masanja
(NBS),Eliaranya Lema (NBS), Clement Mwakanyamale (DPP) na SP-Andrew Mapunda (TPF).
Mwisho, shukrani za dhati ziwaendee wataalamu wote kutoka Chuo cha Takwimu cha Mashariki na
Kusini mwa Afrika (EASTC) kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha taarifa hii na kuiweka
katika kiwango kinachokubalika.
Gaston K. Sanga,
Kamishna wa Fedha na Utawala,
Makao Makuu ya Jeshi la Magereza.
DAR ES SALAAM.
Gaston K.Sanga
Kamishna wa Fedha na Utawala
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
xiv
MUHTASARI
Taarifa hii rasmi ya kitakwimu ni ya kwanza kutolewa na Jeshi la Magereza Tanzania Bara. Taarifa
inahusu wafungwa na mahabusu waliokuwa magerezani katika kipindi cha mwaka 2013 na 2014.
Pia inatoa ufafanuzi wa kina katika maeneo makuu sita (6). Eneo la kwanza ni wahalifu wote yaani
wafungwa na mahabusu waliobaki magerezani mwishoni mwa mwaka 2013 na 2014, pili ni
wafungwa na mahabusu waliopokelewa magerezani kutoka mahakamani kwa mwaka 2013 na
2014, tatu ni wafungwa na mahabusu waliohama na kuhamia katika magereza mengine kwa sababu
mbalimbali. Eneo la nne linahusu wafungwa na mahabusu walioachiwa huru kwa sababu
mbalimbali kama vile kumaliza adhabu zao kwa mujibu wa sheria. Eneo la tano linahusu mahabusu
waliohukumiwa kifungo wakiwa magerezani na mwisho ni wafungwa na mahabusu waliopewa
adhabu mbalimbali wakiwa magerezani.
Baada ya uchambuzi huo wa kina, hitimisho limetolewa kwa lengo la kuboresha hali ya magereza
nchini.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
1
SURA YA KWANZA
USULI
1.0 Utangulizi
Sura hii inaangalia Jiografia ya nchi na majukumu ya msingi ya Jeshi la Magereza Tanzania Bara.
Takwimu zitakazotolewa na Jeshi la Magereza zitasaidia katika kupanga kwa makini mipango ya
kuhakikisha uwepo wa rasilimali za kutosha, kusimamia na kutathmini matokeo ya utekelezaji wa
mipango mbalimbali ya maendeleo. Rasilimali hizi zinahusisha watumishi (rasilimali watu), fedha
na vitendea kazi, ofisi, vyombo vya usafiri na makazi bora ya askari na wafungwa. Kuhakikisha
kuwapo rasilimali hizi ni muhimu katika kuweka mazingira bora ya utekelezaji wa mikakati na
program mbalimbali za maendeleo katika Jeshi.
Aidha, kuna haja ya kuliboresha Jeshi la Magereza kuwa la kisasa zaidi kwa kutumia tekonolojia ya
kisasa katika utekelezaji wa majukumu yake ya msingi kama ilivyoainishwa katika Sheria ya
Magereza Na. 34 ya Mwaka 1967. Hatua hii itachangia pia katika kuleta amani na utulivu nchini
pamoja na kuendeleza na kudumisha usalama katika jamii kwa kuwahifadhi na kuwarekebisha
wahalifu ili watokapo magerezani wawe raia wema watakaoshiriki katika shughuli mbalimbali za
kiuchumi na kijamii kwa ajili ya maendeleo ya nchi.
1.1 Jiografia na Utawala
Tanzania ni jamhuri ya muungano wa nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar. Nchi hizi ziliungana
mwaka 1964. Tanzania ni miongoni mwa nchi tano (5) zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Nchi nyingine ni Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi. Ipo kati ya latitudo 10 na 12
0 Kusini na na
kati ya Longitudo 290 na 41
0 Mashariki mwa Greenwich. Ina eneo lenye ukubwa wa kilometa za
mraba 945,087. Nchi hii imepakana na Kenya na Uganda upande wa Kaskazini na Msumbiji
upande wa Kusini. Mashariki imepakana na Bahari ya Hindi, upande wa Magharibi nchi za
Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na upande wa Kusini Magharibi
imepakana na nchi za Malawi na Zambia.
Tanzania ina maziwa makuu matatu; Victoria, Tanganyika na Nyasa. Ina vivutio vingi vya kitalii
ukiwemo Mlima Kilimanjaro ambao ni mrefu kuliko yote Afrika na umefunikwa na theluji kwa
kipindi chote cha mwaka pamoja na mbuga za wanyama, mambo ya kale na fukwe nzuri katika
Pwani ya Tanzania Bara na katika visiwa vya Zanzibar.
Hali ya hewa ya Tanzania ni ya kitropiki kwa kipindi chote cha mwaka, ambapo maeneo mengi
yana misimu miwili ya mvua za masika na vuli. Shughuli kubwa za kiuchumi ni kilimo, ufugaji,
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
2
utalii, uchimbaji wa madini, viwanda na huduma mbali mbali. Lugha kuu ya Taifa ni Kiswahili
inayozungumzwa na takribani watu wote pamoja na kuwa Tanzania ina makabila zaidi ya 120.
Tangu mwaka 1992, Tanzania inafuata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa. Dola ya
Tanzania ina mihimili mitatu; Bunge, Serikali na Mahakama. Nchi hii ina mfumo wa Serikali mbili,
Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kiutawala; Tanzania
imegawanyika katika mikoa 30 ambapo 25 ipo Tanzania Bara na 5 ipo Tanzania Zanzibar.
1.2 Jeshi la Magereza
Jeshi la Magereza lilianzishwa rasmi tarehe 25 Agosti, 1931 baada ya mgawanyiko wa jeshi la
Polisi na Magereza.Kwa sasa linaongozwa na Sheria ya Magereza Na. 34 ya mwaka 1967. Jeshi la
Magereza limechangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta amani na utulivu kwa kufanya kazi zake
kikamilifu na kwa uadilifu mkubwa na kwa kuzingatia misingi ya haki za binadamu na utawala
bora.
1.2.1 Majukumu ya Jeshi la Magereza
Majukumu ya Jeshi la Magereza kama yalivyoainishwa katika Sheria Na. 34 ya 1967 ni kuchangia
katika kuleta amani na kuendeleza na kudumisha usalama katika jamii kwa kufanya yafuatayo:-
i. Kuhifadhi wafungwa wa aina zote wanaowekwa chini ya ulinzi halali kisheria ndani ya
magereza;
ii. Kuandaa na kutekeleza programu za urekebishaji wa wafungwa na kuwafundisha wafungwa
shughuli za uzalishaji na ujuzi mbalimbali kwa njia ya vitendo na ushauri;
iii. Kuendesha shughuli za huduma za watuhumiwa (mahabusu) kwa mujibu wa sheria; na
iv. Kutoa ushauri katika kuzuia na kudhibiti uhalifu na urekebishaji wa wahalifu.
Hivi sasa; Jeshi la Magereza lipo katika mchakato wa kufanya maboresho kwa lengo la kuwa ni
Jeshi la kisasa linalofanya kazi zake kwa ufanisi, uwajibikaji na weledi wa hali ya juu ili kutimiza
malengo yake liliyojiwekea kwa kiwango cha juu.
1.2.2 Takwimu za Jeshi la Magereza
Jeshi la Magereza lina Takwimu za aina tatu: Takwimu za kiutawala, Takwimu za uhalifu na
Takwimu za uzalishaji mali. Takwimu za utawala zinahusu rasilimali watu, vifaa na fedha; takwimu
za uhalifu zinahusu mchakato mzima wa kuwapokea, kuwahifadhi kwa ajili ya kutekeleza adhabu
kama ni wafungwa au kuwapeleka mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi zao kama ni mahabusu.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
3
Vilevile kuwaachia huru wafungwa kwa mujibu wa sheria. Takwimu za uzalishaji mali zinahusu
taarifa zote za uzalishaji katika miradi mbalimbali ya magereza ikiwemo kilimo, ufugaji na
shughuli za viwanda vidogo vidogo. Takwimu hizi hulisaidia Jeshi la Magereza katika kupanga
mipango yake ya kiutendaji na kimaendeleo. Aidha, sura ya 3 mpaka ya 8 ya ripoti hii zinatoa
taarifa za kitakwimu za wafungwa na mahabusu katika magereza yetu kwa mwaka 2013 na 2014.
1.2.3 Kitengo cha Takwimu cha Jeshi la Magereza
Kitengo cha Takwimu cha Jeshi la Magereza kipo katika Kurugenzi ya Mipango. Kitengo hiki
hupokea taarifa mbalimbali kutoka katika magereza, huzichambua, huzihifadhi, pamoja kuzitumia
kuandaa taarifa za mwaka kwa kushirikiana na vitengo vingine.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
4
SURA YA PILI
HALI YA MAGEREZA NCHINI
2.0 Utangulizi
Katika kipindi cha mwaka 2013 na 2014 hali ya ulinzi na usalama magerezani ilikuwa imara na
hakukuwa na tukio lolote lisilo la kawaida. Pamoja na changamoto nyingi ambazo zilikwamisha
utendaji katika baadhi ya majukumu ya kila siku, Jeshi la Magereza lilijitahidi sana kuyatatua na
kufanya kazi zake kwa ufanisi wa kuridhisha.
2.1 Muhtasari wa Hali ya Magereza
Taarifa hii inajumuisha takwimu za mwaka 2013 na 2014, na ulinganisho wa takwimu hizi
umefanyika ili kubaini mwenendo wa magereza Tanzania Bara. Ulinganifu huu unahusu idadi ya
wahalifu waliobaki magerezani mwishoni mwa mwaka 2013 na 2014, wahalifu waliopokelewa
katika miaka hiyo, wahalifu waliohamishwa kutoka gereza moja hadi jingine kwa sababu
mbalimbali, wahalifu walioachiwa magerezani kwa sababu mbalimbali, wahalifu waliopewa
adhabu kwa utovu wa nidhamu na mahabusu waliohukumiwa adhabu za vifungo wakiwa
magerezani.
.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
5
SURA YA TATU
TAKWIMU ZA WAHALIFU WALIOKUWEPO MAGEREZANI
3.0 Utangulizi
Taarifa hii ni ya wahalifu waliokuwepo magerezani mwishoni mwa mwaka 2013 na 2014. Katika
magereza yote kulikuwa na wahalifu 33,807 kwa mwaka 2013 na 33,517 mwaka 2014 (Jedwali 3.1
na Mchoro 3.1 ). Idadi ya mwaka 2014 ilikuwa pungufu kwa wahalifu 290 ambao ni sawa na
asilimia 0.9 ikilinganishwa na idadi ya mwaka 2013.
Kati ya wahalifu waliokuwepo magerezani tarehe 31.12.2013, mahabusu walikuwa 17,214 (Jedwali
Ambatanisho 1) sawa na asilimia 50.9 na wafungwa 16,593 sawa na asilimia 49.1. Mwaka 2014
mahabusu walikuwa 16,926 sawa na asilimia 50.5 ambapo wafungwa walikuwa 16,591 sawa na
asilimia 49.5.
3.1 Takwimu za Wahalifu kwa Mikoa na Jinsi
Takwimu zinaonesha kuwa mwaka 2013 wahalifu wanaume walikuwa 32,215 sawa na asilimia
95.3, wanawake 1,243 sawa na asilimia 3.7 ambapo wahalifu vijana walikuwa 349 sawa na asilimia
1.0. Ambapo, mwaka 2014 wanaume wahalifu walikuwa 31,930 sawa na asilimia 95.2, wanawake
1,326 sawa na asilimia 4.0 na vijana 261 sawa na asilimia 0.8.
Mkoa wa Dar es Salaam ulikuwa na wahalifu wengi kuliko mikoa mingine kwa miaka yote miwili
ambapo mwaka 2013 walikuwa 4,144 na mwaka 2014 walikuwa 4,360. Mkoa wa Ruvuma ulikuwa
na wahalifu wachache (529) mwaka 2013 ., ambapo mwaka 2014 Mkoa wa Lindi ulikuwa na
wahalifu wachache (410).
Pamoja na kuwa na wahalifu 33,807 mwaka 2013 na 33,517 mwaka 2014, uwezo wa magereza
nchini ni kuhifadhi wahalifu 29,552 tu. Kwa hiyo idadi ya wahalifu ya mwaka 2013 na 2014 ni
zaidi ya idadi inayoruhusiwa kisheria.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
6
Jedwali 3.1: Idadi ya Wahalifu Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Jinsi, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa
2013 2014
Watu Wazima
V
Jumla
Watu Wazima
V
Jumla Me Ke Me Ke
Arusha 1,156 32 0 1,188 1,191 51 1 1,243
Dar es Salaam 4,015 113 16 4,144 4,197 146 17 4,360
Dodoma 1,826 56 18 1,900 1,656 50 16 1,722
Iringa 1,229 64 3 1,296 1,080 56 14 1,150
Kagera 1,848 163 4 2,015 2,150 95 6 2,251
Kigoma 1,403 89 79 1,571 1,147 72 10 1,229
Kilimanjaro 1,429 66 10 1,505 1,447 62 0 1,509
Lindi 575 11 5 591 400 10 0 410
Manyara 912 37 0 949 982 35 0 1,017
Mara 1,743 47 19 1,809 1,923 106 19 2,048
Mbeya 2,072 73 8 2,153 1,773 74 1 1,848
Morogoro 1,588 69 42 1,699 1,604 75 40 1,719
Mtwara 812 25 0 837 743 24 1 768
Mwanza 3,317 159 108 3,584 3,158 137 82 3,377
Pwani 823 14 0 837 925 15 0 940
Ruvuma 510 18 1 529 680 23 0 703
Rukwa 892 32 6 930 891 40 14 945
Singida 855 47 24 926 813 55 2 870
Shinyanga 1,711 68 6 1,785 1,876 85 24 1,985
Tabora 1,984 34 0 2,018 2,087 43 0 2,130
Tanga 1,515 26 0 1,541 1,207 72 14 1,293
Jumla 32,215 1,243 349 33,807 31,930 1,326 261 33,517
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
7
Mchoro 3.1: Wahalifu Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Jinsi, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
3.2 Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Umri
Wafungwa wengi waliobaki magerezani kwa mwaka 2013 na 2014 ni wale wenye umri kuanzia 15
hadi miaka 50 ambapo mwaka 2013 walikuwa 14,219 sawa na asilimia 85.7 na mwaka 2014
walikuwa 14,518 sawa na asilimia 87.5 (Jedwali 3.2 na Mchoro 3.2).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
8
Wafungwa wa umri huu ndiyo hasa nguvu kazi ya taifa letu hivyo hakuna budi juhudi kubwa .
zifanyike kuwarekebisha ili watakapotoka wawe raia wema watakaojenga taifa lao.
Jedwali 3.2: Idadi ya Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Umri, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa
2013 2014
Miaka
15 - 20
Miaka
21 - 25
Miaka
26 - 50
Zaidi ya
miaka 50 Jumla
Miaka
15 - 20
Miaka
21 - 25
Miaka
26 - 50
Zaidi ya
miaka 50 Jumla
Arusha 71 117 105 210 503 101 153 119 94 467
Dar es Salaam 641 163 816 310 1,930 629 134 729 375 1,867
Dodoma 170 194 637 107 1,108 156 198 533 95 982
Iringa 122 150 100 54 426 147 204 94 23 468
Kagera 163 244 450 130 987 172 196 455 265 1,088
Kigoma 213 222 328 95 858 145 131 393 32 701
Kilimanjaro 79 345 224 38 686 89 437 315 26 867
Lindi 96 74 174 22 366 42 30 119 21 212
Manyara 61 75 204 104 444 33 206 253 35 527
Mara 205 89 206 141 641 320 60 319 123 822
Mbeya 100 191 324 446 1,061 126 151 349 247 873
Morogoro 218 276 383 100 977 166 356 369 101 992
Mtwara 142 51 192 41 426 144 51 220 55 470
Mwanza 521 367 687 222 1,797 429 333 686 212 1,660
Pwani 82 155 162 19 418 100 305 171 54 630
Ruvuma 54 106 101 21 282 131 134 145 33 443
Rukwa 102 51 312 24 489 69 112 245 24 450
Singida 56 118 173 35 382 45 98 154 19 316
Shinyanga 169 287 221 60 737 200 195 304 75 774
Tabora 274 221 641 83 1,219 293 396 524 88 1,301
Tanga 81 327 336 112 856 67 292 246 76 681
Jumla 3,620 3,823 6,776 2,374 16,593 3,604 4,172 6,742 2,073 16,591
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
9
Mchoro 3.2: Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Umri, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
3.3 Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Jinsi na Tabia
Kitabia, kuna aina mbili za wafungwa magerezani, kwanza ni wafungwa wenye tabia nzuri (Star).
Hawa ni wafungwa waliohukumiwa kifungo magerezani kwa mara ya kwanza au kwa mara ya pili
ambao historia ya uhalifu wao, tabia zao na aina ya makosa ya nyuma waliyotenda wanaonekana
wanafaa kwa urekebishaji na mafunzo. Kundi la pili ni wafungwa wa kawaida (Ordinary) ambao ni
wale waliokosa sifa ya kuwa Star.
Walikuwepo wafungwa 16,593 magerezani mwaka 2013 na kati yao 10,539 sawa na asilimia 63.5
walikuwa wafungwa wenye tabia nzuri (star) na 6,054 sawa na asilimia 36.5 walikuwa wafungwa
wa kawaida (ordinary). Kwa mwaka 2014 wafungwa walikuwa 16,591 na kati yao 10,958 sawa na
asilimia 66.0 walikuwa wafungwa wenye tabia nzuri (star) na 5,633 walikuwa wafungwa wa
kawaida (ordinary) sawa na asilimia 34.0 kama Jedwali 3.3 linavyoonesha.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
10
Jedwali 3.3: Idadi ya Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Jinsi na Tabia, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa
2013 2014
Tabia nzuri Tabia ya kawaida Jumla
Kuu
Tabia nzuri Tabia ya kawaida Jumla
Kuu Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla M Ke V Jumla
Arusha 329 5 0 334 166 3 0 169 503 111 3 0 114 346 6 1 353 467
Dar es Salaam 509 0 0 509 1,391 29 1 1,421 1,930 404 0 0 404 1,437 26 0 1,463 1,867
Dodoma 415 9 8 432 663 13 0 676 1,108 349 18 5 372 608 2 0 610 982
Iringa 298 14 0 312 114 0 0 114 426 377 11 0 388 80 0 0 80 468
Kagera 663 29 1 693 294 0 0 294 987 853 23 3 879 209 0 0 209 1,088
Kigoma 601 26 20 647 211 0 0 211 858 490 17 8 515 185 1 0 186 701
Kilimanjaro 603 15 0 618 67 1 0 68 686 768 13 0 781 82 4 0 86 867
Lindi 271 3 5 279 86 1 0 87 366 154 2 0 156 56 0 0 56 212
Manyara 376 11 0 387 57 0 0 57 444 477 10 0 487 40 0 0 40 527
Mara 457 7 4 468 171 2 0 173 641 677 14 5 696 121 5 0 126 822
Mbeya 723 19 2 744 312 1 4 317 1,061 697 18 0 715 155 3 0 158 873
Morogoro 439 4 24 467 473 30 7 510 977 589 12 13 614 330 30 18 378 992
Mtwara 298 6 0 304 118 4 0 122 426 309 6 1 316 154 0 0 154 470
Mwanza 1,056 38 6 1,100 692 4 1 697 1,797 905 24 25 954 703 3 0 706 1,660
Pwani 238 4 0 242 175 1 0 176 418 340 3 0 343 287 0 0 287 630
Ruvuma 209 1 0 210 72 0 0 72 282 302 8 0 310 133 0 0 133 443
Rukwa 373 6 2 381 108 0 0 108 489 357 8 9 374 76 0 0 76 450
Singida 306 11 3 320 61 1 0 62 378 166 10 0 176 140 0 0 140 316
Shinyanga 438 20 2 460 276 0 1 277 737 551 29 0 580 190 4 0 194 774
Tabora 1,097 4 0 1,101 112 6 0 118 1,219 1,167 9 0 1,176 125 0 0 125 1,301
Tanga 524 7 0 531 325 0 0 325 856 585 23 0 608 72 1 0 73 681
Jumla 10,223 239 77 10,539 5,944 96 14 6,054 16,593 10,628 261 69 10,958 5,529 85 19 5,633 16,591
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
11
3.4 Wafungwa wa Adhabu ya Kifo Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Hali ya Rufaa.
Jedwali 3.4 na Mchoro 3.3 vinaonesha idadi ya wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kifo
waliokuwepo magerezani. Mwaka 2013 walikuwepo wafungwa 391, ikilinganishwa na wafungwa
410 kwa mwaka 2014, ikiwa ni ongezeko la wafungwa 19 sawa na asilimia 4.9.
Jumla ya wafungwa 391 wa mwaka 2013 walikata rufaa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania. Kati ya
hao, 233 sawa na asilimia 59.6 rufaa zao zilikataliwa na wafungwa 158 sawa na asilimia 40.4
waliendelea kusubiri kusikilizwa kwa rufaa zao. Mwaka 2014 wafungwa waliokata rufaa na rufaa
zao zikakataliwa walikuwa 212 sawa na asilimia 51.7, ambapo 198 sawa na asilimia 48.3
waliendelea kusubiri kusikilizwa kwa rufaa zao. Wafungwa ambao rufaa zao zilikataliwa
wanasubiri utekelezaji wa hukumu ya kifo. (Jedwali Ambatanisho 5).
Jedwali 3.4: Idadi ya wafungwa wa Adhabu ya Kifo Waliobaki Magerezani kwa Mkoa na Hali ya Rufaa,
Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa
2013 2014
Rufaa
zilizokataliwa
Rufaa ambazo
hazijasikilizwa Jumla
Rufaa
zilizokataliwa
Rufaa ambazo
hazijasikilizwa Jumla
Arusha 6 10 16 6 8 14
Dar es Salaam 40 13 53 40 37 77
Dodoma 60 49 109 56 45 101
Iringa 0 0 0 0 0 0
Kagera 0 0 0 0 0 0
Kigoma 0 0 0 0 0 0
Kilimanjaro 0 2 2 0 2 2
Lindi 1 6 7 1 1 2
Manyara 0 1 1 0 0 0
Mara 0 0 0 0 0 0
Mbeya 6 25 31 8 18 26
Morogoro 0 0 0 0 0 0
Mtwara 6 3 9 5 6 11
Mwanza 29 32 61 28 50 78
Pwani 0 0 0 0 0 0
Ruvuma 0 0 0 0 0 0
Rukwa 0 0 0 0 0 0
Singida 0 0 0 0 0 0
Shinyanga 0 0 0 0 2 2
Tabora 25 8 33 29 19 48
Tanga 60 9 69 39 10 49
Jumla 233 158 391 212 198 410
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
12
Mchoro 3.3: Wafungwa wa Adhabu ya Kifo Waliobaki Magerezani na Hali ya Rufaa, Tanzania Bara, 2013
na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
3.5 Wafungwa Watu Wazima na Vijana Waliobaki Magerezani kwa Jinsi na Aina ya Kosa
Wafungwa watu wazima waliokuwepo magerezani mwaka 2013 walikuwa 16,502 wakilinganishwa
na 16,503 wa mwaka 2014 ambao ni zaidi ya mfungwa 1 tu. Mwaka 2013 kosa liliofanywa na
wafungwa wengi kuliko makosa mengine lilikuwa wizi ambalo lilikuwa na wafungwa 3,883.
Lakini, mwaka 2014 kosa la kuvunja nyumba ndilo lililokuwa na wafungwa wengi kuliko
mengineambapo lilikuwa na wafungwa 2,476.
Aidha mwaka 2013 jumla ya wafungwa vijana waliokuwepo katika magereza yote Tanzania Bara
walikuwa 91, ikilinganishwa na wafungwa 88 wa mwaka 2014, ambao ni pungufu kwa wafungwa 3
sawa na asilimia 3.3. Ingawa .mwaka 2013,kosa lililokuwa na wafungwa wengi kuliko mengine ni
kuvunja nyumba, kwa mwaka 2013 na 2014 wafungwa wengi vijana waliokuwepo magerezani
walihukumiwa kwa makosa ya wizi ( Jedwali 3.5 na Mchoro 3.4).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
13
Jedwali 3.5: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima na Vijana Waliobaki Magerezani kwa Jinsi na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Aina ya Kosa
2013 2014
Watu Wazima Vijana Watu Wazima Vijana
Me Ke Jumla Me Ke Jumla Me Ke Jumla Me Ke Jumla
Mauaji 561 22 583 7 0 7 621 21 642 0 0 0
Mauaji (adhabu ya kifo
kuwa kifungo) 120 0 120 0 0 0 154 1 155 0 0 0
Kuua bila kukusudia 821 45 866 1 0 1 1,212 50 1,262 8 0 8
KujaribuKujaribu kuua 167 8 175 5 1 6 182 6 188 5 0 5
Unyang’anyi 2,363 8 2,371 13 0 13 2,269 19 2,288 10 0 10
Wizi 3,794 89 3,883 14 1 15 2,223 59 2,282 16 1 17
Kuvunja nyumba 2,178 32 2,210 16 0 16 2,441 35 2,476 11 0 11
Kupatikana na dawa za
kulevya 530 5 535 7 0 0 448 20 468 4 0 4
Kupatikana na nyara za
serikali 374 1 375 1 0 1 562 4 566 4 0 4
Makosa ya kujamiiana 909 5 914 4 1 5 1,785 17 1,802 8 1 9
Kupatikana na silaha na
risasi 449 10 459 3 0 3 693 12 705 4 0 4
Kujeruhi 1,030 45 1,075 5 0 5 1,268 41 1,309 7 0 7
Kuchoma nyumba moto 119 0 119 0 0 0 185 15 200 2 0 2
Makosa ya rushwa 23 2 25 0 0 0 19 2 21 0 0 0
Kupatikana na pombe ya
moshi (gongo) 165 10 175 0 0 0 394 21 415 2 0 2
Uzembe na uzururaji 153 2 155 0 0 0 191 0 191 0 0 0
Makosa mengineyo 2,411 51 2,462 11 1 12 1,510 23 1,533 5 0 5
Jumla 16,167 335 16,502 87 4 91 16,157 346 16,503 86 2 88
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
14
Mchoro 3.4: Wafungwa Watu Wazima na Vijana Waliobaki Magerezani, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
3.6 Wafungwa Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo
Jedwali 3.6 na Mchoro 3.5 vinaonesha idadi ya wafungwa waliokuwepo magerezani Tanzania Bara
kwa aina ya kosa, jinsi na urefu wa kifungo kwa mwaka 2013 na 2014. Kwa miaka yote miwili
takwimu zinaonesha kwamba kifungo chenye wafungwa wengi kuliko vingine ni cha zaidi ya
mwaka mmoja hadi mitatu. Mwaka 2013 wafungwa walikuwa 3,268 sawa na asilimia 19.8, na
mwaka 2014 walikuwa 2,606 sawa na asilimia 15.8. Aidha, kosa lililokuwa na wafungwa wengi
kuliko makosa mengine lilikuwa wizi ambalo mwaka 2013 lilikuwa na wafungwa 3,883 sawa na
asilimia 23.5 na mwaka 2014 walikuwa 4,413 sawa na asilimia 26.7 (Majedwali Ambatanisho 6 na
7).
Jedwali 3.6: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi na Urefu wa Kifungo,
Tanzania Bara, 2013 na 2014
Urefu wa kifungo 2013 2014
Me Ke Jumla Me Ke Jumla
Hadi miezi 6 1,536 40 1,576 1,834 83 1,917
Zaidi ya miezi 6 hadi mwaka 1 2,568 107 2,675 2,293 54 2,347
Zaidi ya mwaka 1 hadi miaka 3 3,185 83 3,268 2,534 72 2,606
Zaidi ya miaka 3 hadi miaka 5 2,444 41 2,485 2,340 39 2,379
Zaidi ya miaka 5 hadi miaka 10 1,983 25 2,008 1,667 30 1,697
Zaidi ya miaka 10 hadi miaka 15 1,237 8 1,245 1,117 15 1,132
Zaidi ya miaka 15 hadi miaka 20 684 7 691 700 12 712
Zaidi ya miaka 20 hadi miaka 30 1,177 3 1,180 1,520 11 1,531
Zaidi ya miaka 30 526 0 526 1,001 1 1,002
Kifungo cha maisha 453 4 457 756 14 769
Adhabu ya kifo 374 17 391 395 15 410
Jumla 16,167 335 16,502 16,157 346 16,503
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
15
Mchoro 3.5: Idadi ya Wafungwa Waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo,
Tanzania Bara, 2013 na 2014.
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
16
3.7 Mahabusu Watu Wazima na Vijana Waliokuwepo Magerezani Kusubiri Kesi kwa
Jinsi, Aina ya Kosa na Muda Waliokaa Gerezani
Mwaka 2013 walikuwepo mahabusu 17,214 waliobaki magerezani kusubiri hukumu, kati yao watu
wazima walikuwa 16,956 na vijana walikuwa 258. Mwaka 2014 mahabusu walipungua na kufikia
16,926 ambapo watu wazima walikuwa 16,753 na vijana walikuwa 173. Idadi ya mahabusu watu
wazima iliyopungua ni 288 ambao ni asilimia 1.7. Kwa miaka yote miwili kosa liliokuwa na
mahabusu wengi kuliko mengine ni mauaji. Kosa hili lilikuwa na mahabusu 4,693 mwaka 2013 na
3,829 mwaka 2014 (Jedwali 3.7). Makosa haya ya mauaji yamewafanya baadhi ya mahabusu
kusubiri kwa zaidi ya miaka kumi (10) kufikia hatma ya mashauri yao (Jedwali Ambatanisho 8 na
9; Mchoro 3.7.
Jedwali 3.7: Idadi ya Mahabusu Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013
na 2014
Aina ya Kosa
2013 2014
Watu wazima Vijana Watu wazima Vijana
Me Ke Jumla Me Ke Jumla Me Ke Jumla Me Ke Jumla
Mauaji 4,323 319 4,642 45 6 51 3,450 339 3,789 31 9 40
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa
kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3 0 3
Kuua bila kukusudia 903 27 930 5 1 6 854 14 868 5 1 6
Kujaribu kuua 1,099 91 1,190 8 0 8 1,457 114 1,571 21 0 21
Unyang'anyi 2,186 62 2,248 29 1 30 1,991 23 2,014 0 0 0
Wizi 1,667 105 1,772 30 4 34 1,826 128 1,954 23 2 25
Kuvunja nyumba 877 28 905 19 0 19 1,268 33 1,301 0 1 3
Kupatikana na dawa za
kulevya 503 12 515 11 1 12 781 21 802 6 0 6
Kupatikana na nyara za
Serikali 417 18 435 17 0 17 492 4 496 3 0 3
Makosa ya kujamiiana 848 26 874 13 1 14 626 18 644 20 0 20
Kupatikana na bunduki au
risasi 135 6 141 2 0 2 192 6 198 1 0 1
Kujeruhi 545 36 581 8 0 8 648 32 680 3 0 3
Kuchoma moto nyumba 91 26 117 3 1 4 204 5 209 4 0 4
Makosa ya rushwa 89 15 104 1 1 2 97 0 97 1 0 1
Kupatikana na pombe ya
moshi 789 109 898 31 1 32 864 62 926 26 0 24
Uzembe na uzururaji 149 6 155 4 1 5 36 2 38 0 0 0
Makosa mengineyo 1,427 22 1,449 14 0 14 987 179 1,166 11 2 13
Jumla 16,048 908 16,956 240 18 258 16,048 908 16,753 158 15 173
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
17
Mchoro 3.6: Mahabusu Watu Wazima na Vijana Waliokuwepo Magerezani, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
18
Mchoro 3.7: Idadi ya Mahabusu Watu Wazima Waliokuwepo Magerezani na Kusubiri Kesi kwa Aina ya
Kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
19
Mchoro 3.8: Idadi ya mahabusu vijana waliokuwepo magerezani na kusubiri kesi kwa aina ya kosa na
muda waliokaa gerezani, Tanzania Bara 2013 na 2014.
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
20
3.8 Wahalifu Wenye Ugonjwa wa Akili Waliobaki Magerezani
Hawa ni watu wenye ugonjwa wa akili ambao wanaweza wakawa wamefanya kosa/uhalifu au
kutofanya kosa lakini kuwepo kwao uraiani, ni hatari kwao wenyewe na kwa jamii
inayowazunguka. Mwaka 2013 kulikuwa na wahalifu 5 wenye ugonjwa wa akili, kati ya yao mmoja
alikuwa Mkoa wa Dodoma na 4 walikuwa Tabora. Aidha, mwaka 2014 kulikuwa na mahabusu
mmoja tu aliyekuwa mgonjwa wa akili na alikuwa mkoani Dodoma.
3.9 Wahalifu wanawake wajawazito na wenye watoto
Mwaka 2013 walikuwapo wafungwa wajawazito 9 na wafungwa wenye watoto 16, ambao
walikuwa na watoto 18. Aidha, mwaka huo huo mahabusu wajawazito walikuwa 30, mahabusu
wenye watoto 82 ambao walikuwa na watoto 87. Mwaka 2014 walikuwepo wafungwa wajawazito
6 na wafungwa 10 wenye watoto 10. Kwa mwaka huo huo mahabusu wajawazito walikuwa 27,
mahabusu wenye watoto 78 wakiwa na watoto 85. Sababu kubwa zilizowaweka wahalifu wa kike
gerezani ni makosa ya mauaji na wizi (Jedwali 3.8).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
21
Jedwali 3.8 Idadi ya Wahalifu Wanawake Wajawazito na Wenye Watoto kwa Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Aina ya Kosa
2013 2014
Wafungwa Mahabusu Wafungwa Mahabusu
Wajawazito
Wenye watoto
Wajawazito
Wenye watoto
Wajawazito
Wenye watoto
Wajawazito
Wenye watoto
Idadi ya
wafungwa
Idadi
ya
watoto
Idadi ya
mahabusu
Idadi
ya
watoto
Idadi ya
wafungwa
Idadi
ya
watoto
Idadi ya
mahabusu
Idadi
ya
watoto
Mauaji 0 5 5 11 40 40 1 1 1 10 53 58
Mauaji (adhabu ya kifo
kuwa kifungo) 0 0 0 3 5 5 0 0 0 1 3 4
Kuua bila kukusudia 0 0 0 2 0 0 0 1 1 2 1 1
Kujaribu kuua 0 0 0 0 1 1 0 1 1 1 2 2
Unyang'anyi 1 0 0 0 0 0 0 0 0 1 1 1
Wizi 3 5 6 4 6 6 0 2 2 3 4 4
Kuvunja na kuiba 0 0 0 0 2 3 0 0 0 2 2 2
Kupatikana na dawa za
Kulevya 0 1 1 0 1 1 1 0 0 1 3 3
Kupatikana na nyara za
serikali 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kujamiiana 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na
silaha/risasi 1 1 1 0 2 2 0 1 1 0 0 0
Kujeruhi 1 2 2 4 5 6 2 2 2 0 4 4
Kuchoma nyumba
moto 0 0 0 0 0 0 1 1 1 0 0 0
Rushwa 0 0 0 0 1 1 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na pombe
haramu (gongo) 0 1 1 0 1 1 0 0 0 0 0 0
Uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa mengineyo 3 1 2 6 18 21 1 1 1 6 5 6
Jumla 9 16 18 30 82 87 6 10 10 27 78 85
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
22
3.10 Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani, kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Nchi
Walizotoka
Wafungwa wasio raia wa Tanzania waliokuwapo magerezani mwaka 2013 ni 1,359, wakati mwaka
2014 walikuwa 873 ambao ni pungufu kwa wafungwa 486 sawa na asilimia 35.8. Wengi wa
wafungwa hao walitoka katika nchi za Ethiopia na Burundi ambapo kwa mwaka 2013 wafungwa
wengi walitoka Ethiopia ambapo walikuwa 660 sawa na asilimia 48.6. Mwaka 2014 wafungwa
wengi walitoka Burundi idadi yao ilikuwa 460 sawa na asilimia 52.7 (Jedwali 3.9, Majedwali
Ambatanisho 12 na 13 na Michoro 3.9).
Aidha, kwa miaka yote miwili wafungwa wengi wasio raia wa Tanzania walikuwa wanaume
ambapo mwaka 2013 walikuwa 1,339 (asilimia 98.5) kulinganisha na wafungwa wa kike 20
(asilimia 1.5) na mwaka 2014 wanaume walikuwa 868 (asilimia 99.4) na wanawake walikuwa 5
(asilimia 0.6). Mwaka 2013 na 2014 kulionekana kulikuwa na wafungwa wengi wa makosa
mengineyo kama vile kuingia nchini bila kibali, kupigana, kutukana na n.k (Jedwali 3.9).
Jedwali 3.9: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi na Aina ya Kosa Tanzania
Bara, 2013 na 2014
Aina ya Kosa
2013 2014
Me Ke Jumla Me Ke Jumla
Mauaji 43 0 43 8 0 8
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 1 0 1 0 0 0
Kuua bila kukusudia 10 3 13 14 0 14
Kujaribu kuua 0 0 0 0 0 0
Unyang’anyi 62 0 62 67 0 67
Wizi 56 5 61 67 0 67
Kuvunja nyumba 19 1 20 16 0 16
Kupatikana na madawa ya kulevya 5 0 5 3 0 3
Kupatikana na nyara za serikali 6 0 6 3 0 3
Makosa ya kujamiiana 40 0 40 23 0 23
Kupatikana na bunduki na risasi 37 0 37 20 0 20
Kujeruhi 14 3 17 8 0 8
Kuchoma moto nyumba 0 0 0 3 1 4
Makosa ya rushwa 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na pombe ya moshi 0 0 0 2 0 2
Uzembe na uzururaji 0 0 0 0 0 0
Makosa mengine 1,046 8 1,054 634 4 638
Jumla 1,339 20 1,359 868 5 873
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
23
Mchoro 3.9: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi Walizotoka, Tanzania
Bara, 2013 na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
24
3.11 Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya Kosa na Jinsi
Mwaka 2013 jumla ya mahabusu 841 wasio raia wa Tanzania walikuwepo magerezani. Wakati
mwaka 2014 walikuwa 583 wakiwa ni pungufu kwa mahabusu 258 sawa na asilimia 30.7
wakilinganishwa na wale wa 2013. Mahabusu 280 sawa na asilimia 33.3 waliokuwepo magerezani
mwaka 2013 ni raia wa Burundi Jedwali 3.11 na 3.12). Mwaka 2014 mahabusu walikuwa 243
(asilimia 41.7), wengi wao wakiwa ni watuhumiwa wa makosa mengineyo (kama vile kuingia
nchini bila kibali, kupigana,kutukana na n.k).
Kwa miaka yote miwili, wengi wa mahabusu wasio raia wa Tanzania walikuwa wanaume. Mwaka
2013 wanaume walikuwa 797(asilimia 94.8) kulinganisha na mahabusu wa kike walikuwa 44
(asilimia 5.2) ambapo mwaka 2014 wanaume walikuwa 545 (asilimia 93.5) na mahabusu
wanawake walikuwa 38 (asilimia 6.5) Jedwali 3.10.
Jedwali 3.10: Idadi ya .Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya Kosa na Jinsi
Tanzania Bara, 2013 na 2014
Aina ya Kosa
2013 2014
Me Ke Jumla Me Ke Jumla
Mauaji 107 5 112 74 10 84
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 3 0 3 0 0 0
Kujaribu kuua 3 0 3 12 0 12
Unyang’anyi 11 0 11 49 0 49
Wizi 79 4 83 41 4 45
Kuvunja nyumba 97 1 98 11 0 11
Kupatikana na madawa ya kulevya 37 9 46 70 0 70
Kupatikana na nyara za serikali 15 0 15 8 0 8
Makosa ya kujamiiana 37 0 37 13 0 13
Kupatikana na silaha na risasi 5 0 5 6 0 6
Kujeruhi 16 6 22 30 8 38
Kuchoma moto nyumba 0 0 0 0 0 0
Makosa ya rushwa 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na pombe ya moshi 0 0 0 4 0 4
Uzembe na uzururaji 6 0 6 0 0 0
Makosa mengineyo 381 19 400 227 16 243
Jumla 797 44 841 545 38 583
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
25
Jedwali 3.11: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Jinsi na Nchi Walizotoka,
Tanzania Bara, 2013 na 2014
2013 2014
Nchi Walizotoka Me Ke Jumla Nchi Walizotoka Me Ke Jumla
Bulgaria 1 - 1 Burundi 227 17 244
Burundi 265 15 280 China 3 - 3
Cameroon - 1 1 Colombia 1 - 1
China 3 - 3 Congo 20 - 20
Congo 2 - 2 DRC 3 - 3
DRC 4 - 4 Ethiopia 26 - 26
Ethiopia 222 - 222 Ujerumani 1 - 1
Ghana 1 - 1 Ghana 1 - 1
Ugiriki 1 - 1 Ugiriki 1 - 1
Guinea 1 - 1 Guinea 1 - 1
India 1 - 1 Hong Kong 29 - 29
Indonesia 1 - 1 India 1 - 1
Iran 2 - 2 Indonesia 1 - 1
Ireland 1 - 1 Iran 20 - 20
Kenya 46 2 48 Ireland 1 - 1
Korea ya Kaskazini 1 - 1 Kenya 22 2 24
Liberia 2 1 3 Liberia 2 - 2
Lithuania - 1 1 Malawi 1 - 1
Nigeria 16 3 19 Msumbiji 1 - 1
Pakistan 1 - 1 Nigeria 23 - 23
Guinea Bissau 1 - 1 Pakistan 10 - 10
Rwanda 146 13 159 Guinea Bissau 1 - 1
Sierra Leone 1 - 1 Rwanda 71 11 82
Vietam 1 - 1 Viet am 1 - 1
Somalia 2 - 2 Somalia 12 - 12
Afrika Kusini 3 1 4 Afrika Kusini 1 - 1
Tonga - 1 1 Zimbabwe 1 - 1
Uganda 71 6 77 Uganda 60 8 68
Uingereza 1 - 1 Uingereza 1 - 1
Marekani 1 - 1
Zambia 1 - 1
Jumla 797 44 841 Jumla 545 38 583
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
26
SURA YA NNE
WAHALIFU WALIOPOKELEWA MAGEREZANI KUTOKA MAHAKAMANI
4.0 Utangulizi
Sura hii inaangalia wahalifu wote waliopokelewa magerezani kutoka mahakamani kwa mwaka
2013 na 2014. Lengo ni kufahamu aina ya wahalifu kwa jinsi, umri, kosa na muda waliokaa
gerezani wakisubiri kesi zao, urefu wa vifungo na uraia wa mhalifu.
4.1 Wahalifu Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani, kwa Jinsi na Mkoa
Mwaka 2013 jumla ya wahalifu 123,911 walipokelewa magerezani wakilinganishwa na wahalifu
118,439 wa mwaka 2014 ambao ni pungufu kwa wahalifu 5,472 sawa na asilimia 4.4. Kati ya
wahalifu wote 123,911 waliopokelewa magerezani mwaka 2013, wafungwa walikuwa ni 21,886
sawa na asilimia 17.7 na mahabusu walikuwa 102,025 sawa na asilimia 82.3. Vivyo hivyo kati ya
wahalifu 118,439 wa mwaka 2014 wafungwa walikuwa 21,485 sawa na asilimia 18.1 na mahabusu
walikuwa 96,954 sawa na asilimia 81.9.
Mkoa uliopokea wahalifu wengi kuliko mikoa mingine ni Dar es Salaam ulipokea wahalifu 14,484
mwaka 2013 na 15,495 mwaka 2014. Lindi ndiyo mkoa uliopokea wahalifu wachache kuliko mikoa
mingine ambapo 2,152 walipokelewa mwaka 2013 na 1,864 mwaka 2014.
Aidha, mwaka 2013 wahalifu wanaume walikuwa 113,986 sawa na asilimia 92.0, wanawake
walikuwa 8,356 sawa na asilimia 6.7 na wahalifu vijana walikuwa 1,569 sawa na asilimia 1.3. Kwa
mwaka 2014 wahalifu wanaume walikuwa 107,651 sawa na asilimia 90.9, wanawake walikuwa
8,686 sawa na asilimia 7.3 na wahalifu vijana walikuwa 2,102 sawa na asilimia 1.8 (Jedwali 4.1 na
Mchoro 4.1).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
27
Jedwali 4.1: Idadi ya Wahalifu Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na Mkoa ,
Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa
2013 2014
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 4,082 283 - 4,365 4,238 360 1 4,599
Dar es Salaam 13,467 904 113 14,484 13,898 1,383 214 15,495
Dodoma 5,254 392 31 5,677 4,911 400 53 5,364
Iringa 3,738 269 22 4,029 3,931 324 28 4,283
Kagera 7,485 635 24 8,144 8,125 546 47 8,718
Kigoma 4,501 436 179 5,116 4,302 366 157 4,825
Kilimanjaro 5,303 474 39 5,816 5,008 425 35 5,468
Lindi 2,022 108 22 2,152 1,748 101 15 1,864
Manyara 4,014 341 - 4,355 3,631 287 - 3,918
Mara 7,970 669 137 8,776 7,127 689 298 8,114
Mbeya 6,274 616 30 6,920 7,277 712 27 8,016
Morogoro 4,446 287 342 5,075 3,944 293 281 4,518
Mtwara 2,870 191 1 3,062 2,499 179 4 2,682
Mwanza 11,611 901 307 12,819 10,948 838 602 12,388
Pwani 2,913 71 6 2,990 2,592 120 4 2,716
Ruvuma 2,815 182 16 3,013 2,680 163 4 2,847
Rukwa 3,058 224 53 3,335 3,267 249 51 3,567
Singida 3,873 277 17 4,167 3,591 314 40 3,945
Shinyanga 8,180 551 192 8,923 5,220 442 194 5,856
Tabora 4,186 199 4 4,389 3,687 161 2 3,850
Tanga 5,924 346 34 6,304 5,027 334 45 5,406
Jumla 113,986 8,356 1,569 123,911 107,651 8,686 2,102 118,439
Chanzo Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
28
Mchoro 4.1: Wahalifu Waliopokelewa MaGerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na Mikoa, Tanzania
Bara, 2013 na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
29
4.2 Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Umri, Jinsi na
Mikoa
Mwaka 2013 kundi kubwa la wafungwa walipokelewa magerezani ni lile la wenye miaka zaidi ya
15–50, ambalo lilikuwa na wafungwa 20,424 sawa na asilimia 93.3. Wakati 2014 walikuwa 19,991
sawa na asilimia 93.0.
Mikoa iliyopokea wafungwa wengi wa umri huo kuliko mikoa mingine ni Dar es Salaam na
Mwanza. Mwaka 2013 mkoa wa Dar es Salaam ulipokea wafungwa 1,820 na mwaka 2014 mkoa
wa Mwanza ulipokea wafungwa 1,853 (Jedwali 4.2 na 4.3). Aidha, mikoa iliyopokea wahalifu
wachache wa umri huo kuliko mikoa mingine ni Mtwara na Lindi. Mwaka 2013 mkoa wa Mtwara
ulipokea wafungwa 436 na mwaka 2014 mkoa wa Lindi ulipokea wafungwa 501. Umri huu ndiyo
unaotegemewa katika shughuli za uzalishaji hivyo kuwepo kwao magerezani ni pengo katika ujenzi
wa taifa letu.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
30
Jedwali 4.2: Idadi wa Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Umri, Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara, 2013
Mkoa
Miaka 15-20 Miaka 21-25 Miaka 26-50 Zaidi ya miaka 50 Jumla
kuu Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 56 15 0 71 103 7 0 110 216 14 0 230 167 4 0 171 582
Dar es Salaam 551 49 2 602 416 57 0 473 707 38 745 42 10 0 52 1,872
Dodoma 116 6 10 132 221 12 0 233 576 46 0 622 87 7 0 94 1,081
Iringa 133 0 0 133 233 19 0 252 159 17 0 176 26 3 0 29 590
Kagera 149 16 11 176 349 20 369 617 36 0 653 100 13 0 113 1,311
Kigoma 255 14 19 288 338 34 0 372 573 48 0 621 71 3 0 74 1,355
Kilimanjaro 142 5 12 159 241 20 0 261 463 26 0 489 58 4 0 62 971
Lindi 154 2 10 166 157 13 0 170 260 4 0 264 11 0 0 11 611
Manyara 145 9 0 154 294 15 0 309 225 24 0 249 48 3 0 51 763
Mara 175 4 26 205 199 19 0 218 530 29 0 559 131 9 0 140 1,122
Mbeya 115 8 24 147 335 9 0 344 668 69 0 737 54 4 0 58 1,286
Morogoro 121 4 108 233 480 12 0 492 564 39 0 603 55 4 0 59 1,387
Mtwara 66 4 0 70 107 10 0 117 238 11 0 249 19 1 0 20 456
Mwanza 396 14 60 470 475 23 0 498 787 40 0 827 88 5 0 93 1,888
Pwani 125 1 6 132 249 5 0 254 305 14 0 319 46 2 0 48 753
Ruvuma 175 20 4 199 346 29 0 375 225 11 0 236 34 0 0 34 844
Rukwa 115 3 9 127 124 8 0 132 402 23 0 425 30 4 0 34 718
Singida 85 4 5 94 145 7 0 152 401 28 0 429 49 5 0 54 729
Shinyanga 176 9 22 207 336 17 0 353 739 43 0 782 113 6 0 119 1,461
Tabora 78 7 4 89 302 4 0 306 324 16 0 340 56 3 0 59 794
Tanga 291 9 1 301 291 8 0 299 588 37 0 625 85 2 0 87 1,312
Jumla 3,619 203 333 4,155 5,741 348 0 6,089 9,567 613 0 10,180 1,370 92 0 1,462 21,886
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Jedwali 4.3: Idadi ya Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani Kwa Umri, Jinsi na Mkoa , Tanzania Bara, 2014
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
31
Mkoa
Miaka 15 - 20 Miaka 21 - 25 Miaka 26 - 50 Zaidi ya Miaka 50 Jumla
kuu Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 57 10 1 68 221 6 0 227 212 27 0 239 34 12 0 46 580
Dar es Salaam 27 30 1 58 76 32 0 108 969 31 1000 84 39 0 123 1289
Dodoma 97 4 13 114 180 12 0 192 537 48 0 585 75 8 0 83 974
Iringa 112 7 0 119 245 14 0 259 335 12 0 347 47 0 0 47 772
Kagera 263 15 29 307 397 35 432 770 52 822 164 6 0 170 1731
Kigoma 301 5 10 316 284 10 0 294 620 38 0 658 59 2 0 61 1329
Kilimanjaro 71 5 7 83 399 28 0 427 376 23 0 399 41 8 0 49 958
Lindi 52 1 3 56 94 3 0 97 331 17 0 348 17 1 0 18 519
Manyara 136 3 0 139 192 10 0 202 439 32 0 471 65 8 0 73 885
Mara 181 18 32 231 204 22 0 226 555 49 0 604 80 4 0 84 1145
Mbeya 300 17 22 339 423 23 0 446 658 47 0 705 98 8 0 106 1596
Morogoro 125 13 71 209 258 8 0 266 612 32 0 644 105 12 0 117 1236
Mtwara 69 3 4 76 135 3 0 138 325 19 0 344 19 4 0 23 581
Mwanza 280 18 169 467 440 30 0 470 855 61 0 916 113 1 0 114 1967
Pwani 218 2 4 224 301 4 0 305 319 13 0 332 28 0 0 28 889
Ruvuma 190 11 2 203 171 9 0 180 187 21 0 208 33 3 0 36 627
Rukwa 111 7 18 136 204 6 0 210 315 17 0 332 65 0 0 65 743
Singida 102 6 10 118 137 8 0 145 291 25 0 316 40 5 0 45 624
Shinyanga 164 13 8 185 196 15 0 211 547 40 0 587 77 6 0 83 1066
Tabora 118 8 2 128 349 9 0 358 268 13 0 281 60 1 0 61 828
Tanga 197 4 4 205 343 19 0 362 491 26 0 517 59 3 0 62 1146
Jumla 3,171 200 410 3,781 5249 306 0 5,555 10,012 643 0 10,655 1,363 131 0 1,494 21,485
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
32
4.3 Wafungwa Warudiaji Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na
Mkoa
Kwa kawaida mfungwa anapopokelewa kutoka mahakamani taarifa zake za nyuma huangaliwa ili
kubaini kama ameshawahi kuhukumiwa kifungo. Sifa hizi huwa katika makundi matatu, kwanza ni
wale waliohukumiwa kifungo kwa mara ya kwanza (first offender), pili ni wale waliokuhukumiwa
kifungo kwa mara ya pili (one previous conviction) na tatu ni wale walio kuhukumiwa kifungo
gerezani zaidi ya mara mbili (recidivist). Wafungwa waliofungwa kuanzia kifungo cha pili na
kuendelea huitwa warudiaji.
Katika miaka yote miwili wengi wa wafungwa warudiaji waliopokelewa magerezani ni wale
waliohukumiwa kwa mara ya pili. Mwaka 2013 wafungwa wa kifungo cha pili walikuwa 1,786
ambayo ni sawa na asilimia 68.7 na wa zaidi ya vifungo viwili walikuwa 815 ambayo ni sawa na
asilimia 31.3. Vivyo hivyo mwaka 2014 wafungwa wa kifungo cha pili walikuwa 1,808 sawa na
asilimia 65.9 na waliofungwa zaidi ya mara mbili walikuwa 936 sawa na asilimia 34.1 (Majedwali
4.4 na 4.5 pia katika Mchoro 4.2). Takwimu hizi zinaonesha kuwa bado kuna wafungwa wengi
warudiaji magerezani, ambao wanapewa adhabu za vifungo baada ya kumaliza vifungo vyao vya
awali kwa makosa mbalimbali. Hivyo juhudi kubwa inahitajika katika kuwarekebisha ili wasirudie
kutenda makosa.
Jedwali 4.4: Idadi ya Wafungwa Warudiaji Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi,
Mkoa na Urudiaji wa Kifungo, Tanzania Bara, 2013
Mkoa
Kifungo cha Pili Zaidi ya Kifungo cha Pili Jumla Kuu
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 188 10 0 198 126 6 0 132 314 16 0 330
Dar es Salaam 24 0 0 24 10 0 0 10 34 0 0 34
Dodoma 79 0 0 79 17 0 0 17 96 0 0 96
Iringa 83 1 0 84 51 0 0 51 134 1 0 135
Kagera 49 0 0 49 44 0 0 44 93 0 0 93
Kigoma 59 1 0 60 3 0 0 3 62 1 0 63
Kilimanjaro 152 16 0 168 22 0 0 22 174 16 0 190
Lindi 87 1 0 88 53 0 0 53 140 1 0 141
Manyara 63 2 0 65 43 0 0 43 106 2 0 108
Mara 71 5 5 81 6 0 0 6 77 5 5 87
Mbeya 80 1 1 82 23 0 0 23 103 1 1 105
Morogoro 103 2 2 107 130 3 40 173 233 5 42 280
Mtwara 39 1 0 40 12 0 0 12 51 1 0 52
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
33
Mkoa
Kifungo cha Pili Zaidi ya Kifungo cha Pili Jumla Kuu
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Mwanza 86 0 2 88 19 0 1 20 105 0 3 108
Pwani 91 3 0 94 43 0 0 43 134 3 0 137
Ruvuma 99 0 0 99 29 0 0 29 128 0 0 128
Rukwa 32 0 0 32 6 0 0 6 38 0 0 38
Singida 44 1 0 45 10 0 0 10 54 1 0 55
Shinyanga 44 4 1 49 31 0 0 31 75 4 1 80
Tabora 64 3 0 67 20 0 0 20 84 3 0 87
Tanga 185 2 0 187 67 0 0 67 252 2 0 254
Jumla 1722 53 11 1786 765 9 41 815 2487 62 52 2601
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Jedwali 4.5: Idadi ya Wafungwa Warudiaji Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi,
Mkoa na Urudiaji wa Kifungo, Tanzania Bara, 2014
Mkoa Kifungo cha Pili Zaidi ya kifungo cha Pili Jumla
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 171 12 0 183 48 0 0 48 219 12 0 231
Dar es Salaam 9 3 0 12 2 0 0 2 11 3 0 14
Dodoma 52 0 0 52 14 0 0 14 66 0 0 66
Iringa 166 0 0 166 130 0 0 130 296 0 0 296
Kagera 100 0 1 101 135 0 0 135 235 0 1 236
Kigoma 28 1 0 29 13 0 0 13 41 1 0 42
Kilimanjaro 117 12 0 129 77 3 0 80 194 15 0 209
Lindi 76 0 0 76 59 0 0 59 135 0 0 135
Manyara 68 1 0 69 33 2 0 35 101 3 0 104
Mara 64 1 0 65 4 0 0 4 68 1 0 69
Mbeya 79 1 0 80 30 0 0 30 109 1 0 110
Morogoro 118 2 2 122 64 0 1 65 182 2 3 187
Mtwara 45 0 0 45 24 0 0 24 69 0 0 69
Mwanza 107 0 6 113 18 1 3 22 125 1 9 135
Pwani 125 0 0 125 53 0 0 53 178 0 0 178
Ruvuma 66 0 0 66 35 0 0 35 101 0 0 101
Rukwa 43 0 0 43 5 0 0 5 48 0 0 48
Singida 47 1 1 49 47 0 0 47 94 1 1 96
Shinyanga 28 1 0 29 20 0 0 20 48 1 0 49
Tabora 65 9 0 74 32 1 0 33 97 10 0 107
Tanga 180 0 0 180 80 0 2 82 260 0 2 262
Jumla 1754 44 10 1808 923 7 6 936 2677 51 16 2744
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
34
Mchoro 4.2: Wafungwa Warudiaji Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani, Tanzania Bara, 2013
na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
4.4 Wafungwa Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa
Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo
Wafungwa watu wazima 21,553 walipokelewa magerezani mwaka 2013 na wafungwa 21,075
walipokelewa mwaka 2014. Mwaka 2013 wengi wa wafungwa hao walikutwa na hatia ya kosa la
wizi ambao walikuwa 5,207 sawa na asilimia 24.2 yakifuatiwa na wafungwa wa kosa la kujeruhi
wakiwa 2,416 sawa na asilimia 11.2. Vilevile mwaka 2014 wengi wa wafungwa walikutwa na hatia
ya kosa la wizi na walikuwa 5,036 sawa na asilimia 23.9 (Jedwali 4.6 na 4.7)
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
35
Jedwali 4.6: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo,
Tanzania Bara, 2013
Aina ya Kosa
Chini ya miezi
6
Miezi 6 hadi
mwaka
Zaidi ya
mwaka 1-3
Zaidi ya Miaka
3 - 5
Zaidi ya
miaka 5-10
Zaidi ya
miaka 10-15
Zaidi ya
miaka 15-
20
Zaidi ya
miaka 20-
30
Zaidi ya
miaka 30
Kifungo
cha
maisha
Kunyongwa
Jumla
Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke
Mauaji 40 8 15 6 50 8 5 5 13 0 18 0 3 0 1 0 1 0 32 0 70 2 277
Mauaji (adhabu ya
kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 11 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 17 2 32 2 109 14 13 7 105 8 53 0 24 0 0 0 18 0 8 0 0 0 412
KujaribuKujaribu
kuua 21 1 20 0 24 1 1 1 7 1 9 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 86
Unyang'anyi 49 0 205 0 144 0 0 0 110 0 139 1 70 0 296 0 18 0 3 0 0 0 1,035
Wizi 1,760 134 1,590 110 1,173 107 45 20 156 20 19 0 12 0 23 0 38 0 0 0 0 0 5,207
Kuvunja na kuiba 472 20 689 30 687 20 13 8 128 0 24 2 2 0 12 0 3 0 0 0 0 0 2,110
Kupatikana na dawa
za kulevya 91 8 122 3 107 3 4 3 38 0 12 0 12 0 2 1 0 0 0 0 0 0 406
Kupatikana na nyara
za serikali 148 0 78 6 206 7 2 1 40 1 1 0 119 0 29 0 1 0 6 0 0 0 645
Kujamiiana 137 0 197 0 171 0 0 0 55 0 24 0 33 0 282 0 25 0 193 0 0 0 1,117
Kupatikana na
silaha/risasi 12 0 47 0 71 1 0 0 78 0 37 0 21 0 24 0 20 0 0 0 0 0 311
Kujeruhi 627 70 820 98 681 34 8 7 40 6 22 0 0 0 0 0 2 0 0 1 0 0 2,416
Kuchoma nyumba
moto 77 1 88 3 35 3 0 0 11 0 1 0 0 0 1 0 0 0 8 0 0 0 228
Rushwa 3 0 10 0 23 1 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 39
Kupatikana na
pombe ya moshi 205 30 124 30 41 7 2 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 440
Uzururaji 117 6 102 4 9 2 0 0 41 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 281
Makosa mengineyo 1,880 142 2,650 158 1,489 53 5 4 141 3 8 1 5 0 1 0 2 0 1 0 0 0 6,543
Jumla 5,656 422 6,789 450 5,020 261 98 57 965 39 367 4 301 0 671 1 128 0 251 1 70 2 21,553
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
36
Jedwali 4.7: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo,
Tanzania Bara, 2014
Aina ya kosa
Chini ya
miezi 6
Miezi 6 hadi
mwaka 1
Zaidi ya
mwaka 1-3
Zaidi ya
miaka 3-5
Zaidi ya
miaka 5-10
Zaidi ya
miaka 10-
15
Zaidi ya
miaka 15-20
Zaidi ya
miaka 20-
30
Zaidi ya
miaka 30
Kifungo
cha
maisha
Kunyongwa
Jumla
Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke
Mauaji 50 8 32 6 61 8 1 1 22 0 10 0 0 0 4 0 0 1 3 0 59 2 268
Mauaji (adhabu
ya kifo kuwa
kifungo)
0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila
kukusudia 12 2 35 3 147 19 12 12 205 14 82 4 29 1 6 0 7 1 2 0 0 0 593
Kujaribukuua 36 0 41 1 20 3 1 1 19 0 8 0 0 0 1 0 0 0 1 0 0 0 132
Unyang'anyi 124 1 64 0 133 0 0 0 91 0 91 0 56 0 275 0 10 0 2 0 0 0 847
Wizi 1,236 83 1,738 114 1,363 66 11 11 329 9 25 0 4 0 8 0 36 0 3 0 0 0 5,036
Kuvunja na kuiba 1,003 49 998 30 729 22 7 7 133 0 45 0 3 0 13 0 1 0 0 0 0 0 3,040
Kupatikana na
dawa ya kulevya 63 5 151 5 144 5 2 2 19 1 8 0 14 0 2 0 0 0 0 0 0 0 421
Kupatikana na nyara za serikali
88 2 126 14 205 8 1 1 46 0 11 0 139 1 38 0 2 0 6 0 0 0 688
Kujamiiana 13 0 11 0 30 0 3 3 36 0 3 0 4 0 253 0 20 0 124 0 0 0 500
Kupatikana na
silaha/risasi 10 3 11 5 56 0 0 0 37 1 12 0 1 0 1 0 8 0 1 0 0 0 146
Kujeruhi 412 44 666 65 399 39 8 8 54 3 5 0 1 0 1 0 0 4 2 0 0 0 1,711
Kuchoma nyumba
moto 67 11 63 2 48 2 0 0 7 0 1 20 0 0 2 0 0 0 3 0 0 0 226
Rushwa 3 0 10 0 23 1 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 38
Kupatikana na pombe moshi
105 40 122 31 39 2 1 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 341
Uzururaji 74 11 48 0 13 0 0 0 38 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 184
Makosa
mengineyo 2,083 181 2,599 196 1,529 68 7 7 204 9 15 0 3 0 3 0 0 0 0 0 0 0 6,904
Jumla 5,379 440 6,715 472 4,939 243 54 54 1,241 37 316 24 254 2 607 0 84 6 147 0 59 2 21,075
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
37
4.5 Wafungwa Vijana Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina
ya kosa na Urefu wa Kifungo
Jedwali 4.8 linaonesha kwamba, mwaka 2013 wafungwa vijana 333 walipokelewa magerezani
kutoka mahakamani, wakilinganishwa na wafungwa 410 wa mwaka 2014 (Jedwali 4.8) ambalo ni
ongezeka la wafungwa 77 sawa na asilimia 23.1. Wengi wa wafungwa vijana walihukumiwa kwa
kosa la wizi ambalo mwaka 2013 lilikuwa na wafungwa 67 na mwaka 2014 wafungwa 99.
Wafungwa vijana walifungwa vifungo vya chini ya miezi 6 mpaka vifungo vya maisha kulingana
na aina ya kosa.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
38
Jedwali 4.8: Idadi ya Wafungwa Vijana Waliopokolewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina ya kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara,
2013
Aina ya Kosa
Chini ya miezi
6
Miezi 6 hadi
mwaka 1
Zaidi ya
mwaka 1- 3
Zaidi ya
miaka 3-5
Zaidi ya
miaka 5-10
Zaidi ya
miaka 10- 15
Zaidi ya
miaka 15- 20
Zaidi ya
miaka 20 -
30
Zaidi ya
miaka 30
Kifungo
cha maisha Kunyongwa
Jumla
Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke
Mauaji 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2
Mauaji (adhabu
ya kifo kuwa
kifungo)
0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 0 0 0 0 16 4 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 20
Kujaribu kuua 0 0 0 9 5 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 14
Unyang'anyi 3 0 0 0 1 0 0 0 1 0 8 0 2 0 1 1 0 0 0 0 0 0 17
Wizi 20 3 10 5 9 4 7 2 0 0 0 2 5 0 0 0 0 0 0 0 0 0 67
Kuvunja na kuiba 6 1 5 8 2 0 3 2 8 0 2 5 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 45
Kupatikana na dawa
ya kulevya 3 4 0 3 0 1 0 0 0 0 0 2 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 14
Kupatikana na nyara
za serikali 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 2
Kujamiiana 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 2 3 0 1 0 7 0 0 0 16
Kupatikana na
silaha/risasi 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 4 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 7
Kujeruhi 10 1 4 5 7 2 19 5 0 0 0 3 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 57
Kuchoma nyumba
moto 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Rushwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na
pombe haramu
(gongo)
3 6 0 3 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 14
Uzururaji 8 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 8
Makosa mengineyo 11 3 7 14 6 3 2 0 0 0 0 2 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 50
Jumla 68 18 26 47 46 14 32 10 9 0 10 20 17 2 4 1 1 0 8 0 0 0 333
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
39
Jedwali 4.9: Idadi ya Wafungwa Vijana Waliopokolewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara,
2014
Aina ya Kosa
Chini ya
miezi 6
Miezi 6 hadi
mwaka
Zaidi ya
mwaka 1-3
Zaidi ya
miaka 3-5
Zaidi ya
miaka 5-10
Zaidi ya
miaka 10-15
Zaidi ya
miaka 15-20
Zaidi ya
miaka 20-30
Zaidi ya
miaka 30
Kifungo
cha maisha Kunyongwa
Jumla
Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke
Mauaji 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2
Mauaji (adhabu
ya kifo kuwa
kifungo)
0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila
kukusudia 0 0 0 0 0 0 3 2 0 0 0 0 0 0 3 1 0 0 0 0 9
Kujaribu kuua 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1
Unyang'anyi 1 0 0 0 1 0 0 2 1 21 5 4 0 0 0 0 0 0 0 35
Wizi 45 14 13 5 12 1 6 1 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 99
Kuvunja na
kuiba 7 9 4 1 5 3 14 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 45
Kupatikana na
dawa za kulevya 2 0 5 0 2 1 2 0 0 0 0 5 0 0 0 0 0 0 0 0 17
Kupatikana na
nyara za serikali 6 0 0 0 0 0 0 0 11 1 0 5 0 0 0 0 2 0 0 0 25
Kujamiiana 7 0 0 0 0 0 0 0 1 0 7 2 0 2 11 0 0 0 30
Kupatikana na
silaha/risasi 0 0 0 0 0 0 0 0 15 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 15
Kujeruhi 9 0 9 5 7 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 33
Kuchoma
nyumba moto 0 0 0 0 0 0 4 0 0 0 7 0 4 0 0 1 0 0 0 0 0 16
Rushwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na
pombe haramu
(gongo)
4 0 7 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 12
Uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa
mengineyo 32 15 12 3 7 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 71
Jumla 115 38 51 15 34 5 34 0 32 1 31 0 26 0 6 0 8 1 13 0 0 0 410
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
40
4.6 Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Kushindwa Kulipa
Faini kwa Mkoa na Urefu wa Vifungo
Wafungwa 6,457 walipokelewa magerezani kutoka mahakamani mwaka 2013 kwa kushindwa
kulipa faini wakilinganishwa na wafungwa 5,654 wa mwaka 2014, ambao ni pungufu kwa
wafungwa 803 sawa na asilimia 12.4. Wengi wa wafungwa walioshindwa kulipa faini ni wale
waliohukumiwa kwenda magerezani kifungo cha zaidi ya miezi mitatu. Idadi yao ilikuwa 4,881
mwaka 2013 na 4,346 mwaka 2014. Mikoa iliyokuwa na idadi kubwa kuliko mingine ya wafungwa
walioshindwa kulipa faini ni Mbeya uliokuwa na wafungwa 766 kwa mwaka 2013 na Mkoa wa
Kigoma wafungwa 657 mwaka 2014 (Jedwali 4.10).
Jedwali 4.10: Idadi ya Wafungwa Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Kushindwa Kulipa
Faini kwa Mkoa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa
2013 2014
Chini ya
mwezi 1 Mwezi 1 - 3
Zaidi ya
miezi 3 Jumla
Chini ya
mwezi 1 Mwezi 1 – 3
Zaidi ya
miezi 3 Jumla
Arusha 0 10 15 25 0 20 10 30
Dar es Salaam 7 162 289 458 114 143 350 607
Dodoma 114 86 198 398 20 70 63 153
Iringa 0 7 64 71 14 25 110 149
Kagera 13 44 42 99 9 83 85 177
Kigoma 0 23 366 389 1 21 635 657
Kilimanjaro 545 4 89 638 13 9 51 73
Lindi 4 24 185 213 4 12 90 106
Manyara 0 0 0 0 0 1 119 120
Mara 0 63 287 350 0 64 303 367
Mbeya 13 77 676 766 8 157 215 380
Morogoro 0 40 234 274 0 29 205 234
Mtwara 0 9 117 126 0 10 141 151
Mwanza 8 74 498 580 5 99 488 592
Pwani 0 26 97 123 3 117 108 228
Ruvuma 8 47 194 249 8 55 162 225
Rukwa 0 0 82 82 0 5 147 152
Singida 10 33 199 242 0 32 134 166
Shinyanga 11 40 417 468 0 27 247 274
Tabora 0 12 234 246 20 10 155 185
Tanga 26 36 598 660 28 72 528 628
Jumla 759 817 4,881 6457 247 1,061 4,346 5,654
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
41
4.7 Wafungwa Wagonjwa wa Akili Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa
Jinsi na Mkoa
Jumla ya wahalifu 5 ambao ni wagonjwa wa akili, walipokelewa magerezani kutoka mahakamani
mwaka 2013 mkoani Tabora. Mwaka 2014 walipokelewa kutoka mahakamani jumla ya wahalifu 5
katika mikoa ifuatayo: Tabora (3), Morogoro (1) na Mwanza (1). Kati yao wanaume ni 4 na
mwanamke 1.
4.8 Wahalifu Wanawake Wajawazito na Wenye Watoto Waliopokelewa Magerezani Toka
Mahakamani kwa Aina ya Kosa
Mwaka 2013 walipokelewa wafungwa wajawazito 60 na wafungwa wanawake 94 wenye watoto
104. Aidha, mahabusu wajawazito waliopokelewa walikuwa 124 na mahabusu wenye watoto 314,
wakiwa na watoto 336. Mwaka 2014 walipokelewa wafungwa wajawazito 47, wafungwa
wanawake 74 wenye watoto 81, wakati mahabusu wajawazito waliopokelewa ni 182, mahabusu
wenye watoto 373 wakiwa na watoto 403 (Jedwali 4.11).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
42
Jedwali 4.11: Idadi ya Wahalifu Wanawake Wajawazito na Wenye Watoto Waliopokelewa Magerezani Toka
Mahakamani Kulingana na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Aina ya Kosa
2013 2014
Wafungwa Mahabusu Wafungwa Mahabusu
Waja
wazit
o
Wenye watoto
Wajawazi
to
Wenye watoto
Waja
wazit
o
Wenye watoto
Waja
wazit
o
Wenye watoto
Idadi ya
wafung
wa
Idadi
ya
watot
o
Idadi ya
mahabus
u
Idadi
ya
watot
o
Idadi ya
wafung
wa
Idadi
ya
watot
o
Idadi ya
mahabus
u
Idadi
ya
watot
o
Mauaji 8 6 6 24 66 68 2 6 7 37 115 116
Mauaji
(adhabu ya
kifo kuwa
kifungo)
3 5 5 2 5 6 4 3 3 2 14 14
Kuua bila kukusudia
2 3 3 1 9 10 2 3 4 4 9 10
KujaribuKujari
bu kuua 7 3 4 3 11 12 1 1 1 4 5 5
Unyang'anyi 1 12 12 7 11 11 1 3 3 7 14 14
Wizi 12 13 13 20 39 41 13 12 12 23 47 55
Kuvunja na
kuiba 1 2 2 6 7 7 1 4 5 16 11 11
Kupatikana na dawa za
kulevya
1 3 3 1 6 6 1 3 3 7 11 15
Kupatikana na nyara za
serikali
0 0 0 1 1 1 0 0 0 1 1 1
Kujamiiana 0 0 0 0 1 1 0 0 0 0 1 1
Kupatikana na silaha/risasi
1 0 0 2 0 0 1 1 1 0 1 1
Kujeruhi 8 10 11 11 40 40 8 9 10 12 35 36
Kuchoma
nyumba moto 0 0 0 0 0 0 2 2 3 11 16 16
Rushwa 1 2 2 2 3 4 0 0 0 5 5 5
Kupatikana na pombe haramu
(gongo)
0 12 12 0 1 1 0 0 0 5 7 7
Uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3 3
Makosa mengineyo
15 23 31 44 114 128 11 27 29 48 78 93
Jumla 60 94 104 124 314 336 47 74 81 182 373 403
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
4.9 Mahabusu Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi,
Aina ya kosa na Muda wa Kusubiri Hukumu
Jumla ya mahabusu watu wazima waliopokelewa magerezani kutoka mahakamani kusubiri hukumu
kwa mwaka 2013 ni 100,789, wakilinganishwa na 95,262 wa mwaka 2014, ambao ni pungufu kwa
mahabusu 5,527 sawa na asilimia 5.5. Wengi wa mahabusu hawa walishtakiwa kwa makosa la wizi,
ambapo mwaka 2013 walikuwa 18,490 na mahabusu 18,762 kwa mwaka 2014. Mahabusu wote
walikuwa wamekaa gerezani kipindi kisichozidi miaka 2 (Jedwali 4.12).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
43
Jedwali 4.12: Idadi ya Mahabusu Watu Wazima Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina ya Kosa na Muda wa Kusubiri Hukumu,
Tanzania Bara, 2013 na 2014
Aina ya Kosa
2013 2014
Chini ya miezi 2 Miezi 2-6 Zaidi ya miezi 6-
miaka 2 Jumla
Chini ya miezi 2 Miezi 2-6 Zaidi ya miezi 6-
miaka 2 Jumla
Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke
Mauaji 2,640 182 4,292 376 5,542 475 13,507 2,108 217 3,028 297 4,121 447 10,218
Mauaji (adhabu
ya kifo kuwa
kifungo)
0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila
kukusudia 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
KujaribuKujaribu
kuua 3,103 345 3,961 311 2,585 159 9,699 3,395 321 2,715 234 1,847 131 8,643
Unyang'anyi 2,599 66 4,016 90 3,305 84 10,160 2,703 83 3,065 79 3,553 95 9,578
Wizi 6,656 415 5,360 1,355 4,444 260 18,490 7,924 574 5,873 375 3,857 159 18,762
Kuvunja na kuiba 2,645 138 2,275 101 1,960 41 7,160 4,258 168 2,463 100 1,474 17 8,480
Kupatikana na
dawa za kulevya 1,379 30 1,087 46 929 85 3,556 1,157 21 1,077 20 727 15 3,017
Kupatikana na
nyara za serikali 787 31 726 41 602 27 2,214 607 19 385 30 539 28 1,608
Kujamiiana 1,682 190 1,738 109 1,153 137 5,009 1,862 197 1,694 123 958 129 4,963
Kupatikana na
silaha/risasi 628 35 451 6 297 5 1,422 558 5 201 170 934
Kujeruhi 1,924 280 1,169 189 1,078 58 4,698 2,658 313 1,706 156 1,119 96 6,048
Kuchoma
nyumba moto 695 118 395 50 177 13 1,448 536 61 503 36 158 9 1,303
Rushwa 656 59 391 24 126 17 1,273 566 21 445 39 135 6 1,212
Kupatikana na
pombe haramu
(gongo)
2,783 415 2,929 261 2,675 164 9,227 3,324 325 2,397 219 1,768 125 8,158
Uzururaji 1,287 99 344 27 94 6 1,857 665 33 191 5 40 934
Makosa
mengineyo 2,494 355 3,933 238 3,906 143 11,069 3,241 545 3,769 236 3,336 277 11,404
Jumla 31,958 2,758 32,302 3,224 28,873 1,674 100,789 35,562 2,903 29,512 1,949 23,802 1,534 95,262
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
44
4.10 Mahabusu Vijana Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina
ya kosa na Muda wa Kusubiri Hukumu
Mahabusu vijana waliopokelewa magerezani kutoka mahakamani mwaka 2013 walikuwa 1,236,
wakilinganishwa na 1,692 wa mwaka 2014, ambalo ni ongezeko la mahabusu vijana 456 sawa na
asilimia 36.9. Aidha mahabusu hao walikuwa wamekaa magerezani kwa kipindi kisichozidi miaka
2. Mwaka 2013, wengi wa mahabusu (171) walishtakiwa kwa kosa la wizi. Vile vile mwaka 2014
wengi wa mahabusu (374) walishtakiwa kwa kosa la wizi (Jedwali 4.13).
Jedwali 4.13: Idadi ya Mahabusu Vijana Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi, Aina
ya Kosa na Muda wa Kusubiri Hukumu, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Aina ya Kosa
2013 2014
Chini ya
miezi 2 Miezi 2-6
Zaidi ya
miezi 6 -
miaka 2 Jumla
Chini ya
miezi 2 Miezi 2-6
Zaidi ya
miezi 6 -
miaka 2 Jumla
Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke Me Ke
Mauaji 22 4 50 35 35 0 146 33 17 97 6 135 21 309
Mauaji (adhabu ya
kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kujaribukuua 65 3 81 3 10 0 162 65 8 16 1 8 1 99
Unyang'anyi 46 0 59 0 22 0 127 6 0 9 0 11 0 26
Wizi 78 9 62 4 12 6 171 173 33 88 35 44 1 374
Kuvunja na kuiba 22 0 28 0 7 3 60 67 2 48 0 27 0 144
Kupatikana na dawa
za kulevya 34 5 23 0 14 0 76 9 0 4 0 24 0 37
Kupatikana na nyara
za serikali 3 0 8 0 3 0 14 2 0 0 0 0 0 2
Kujamiiana 17 0 35 0 13 0 65 102 18 26 0 18 0 164
Kupatikana na
silaha/risasi 0 0 6 1 0 0 7 0 0 0 0 0 0 0
Kujeruhi 22 1 30 0 0 0 59 48 0 45 11 1 0 105
Kuchoma nyumba
moto 0 0 0 0 0 0 0 9 5 11 0 0 0 25
Rushwa 7 0 1 0 0 0 8 28 0 0 0 0 0 28
Kupatikana na
pombe haramu
(gongo)
106 1 14 2 10 0 133 23 15 15 1 4 9 67
Uzururaji 20 4 21 4 1 0 50 27 2 0 0 0 0 29
Makosa mengineyo 98 21 28 3 6 2 158 147 20 40 8 63 5 283
Jumla 540 48 446 52 139 11 1,236 739 120 399 62 335 37 1,692
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
45
4.11 Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na
Nchi Walizotoka
Jumla ya wafungwa wasio raia wa Tanzania 1,836 walipokelewa magerezani kutoka mahakamani
mwaka 2013 wakilinganishwa na wafungwa 1,999 wa mwaka 2014 ambalo ni ongezeko la
wafungwa 163 sawa na asilimia 8.9. Mwaka 2013 wengi wa wafungwa walikuwa raia wa Ethiopia
(1,017) na mwaka 2014 wengi wa wafungwa walikuwa raia wa Burundi (1,076). Kwa miaka hii
miwili, wafungwa wanaume wasio raia walikuwa 1,812 na wafungwa wanawake 24 kwa mwaka
2013, ambapo mwaka 2014 wafungwa wanaume wasiokuwa raia walikuwa 1,953 na wanawake
walikuwa 46. Hili ni ongezeko la wafungwa wanaume 141 sawa na asilimia 7.8 na wanawake 22
sawa na asilimia 91.7 (Majedwali 4.14 na 4.15).
Jedwali 4.14: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na
Nchi Walizotoka, Tanzania Bara, 2013 na 2014.
Nchi Walizotoka 2013 2014
Me Ke Jumla Me Ke Jumla
Burundi 687 13 700 1,037 39 1,076
China 0 0 0 1 0 1
Congo 10 1 11 50 1 51
DRC 16 6 22 3 0 3
Ethiopia 1,017 - 1,017 664 0 664
Hong Kong 0 0 0 61 0 61
India 2 0 2 1 0 1
Kenya 22 2 24 28 1 29
Malawi 1 0 1 0 0 0
Liberia 0 0 0 5 0 5
Nigeria 1 0 1 7 0 7
Rwanda 38 1 39 68 1 69
Somalia 11 0 11 2 0 2
Afrika Kusini 0 0 0 1 0 1
Sudan 0 0 0 1 1 2
Turkey 0 0 0 1 0 1
Uganda 6 1 7 20 3 23
Zambia 1 0 1 3 0 3
Jumla 1,812 24 1,836 1,953 46 1,999
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
46
Jedwali 4.15: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na
Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Aina ya Kosa 2013 2014
Me Ke Jumla Me Ke Jumla
Mauaji 0 0 0 3 0 3
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 2 0 2 0 0 0
Kujaribu kuua 0 0 0 4 0 4
Unyang’anyi 7 0 7 11 0 11
Wizi 13 0 13 34 1 35
Kuvunja nyumba 1 0 1 3 0 3
Kupatikana na dawa za kulevya 1 0 1 3 1 4
Kupatikana na nyara za serikali 2 0 2 3 0 3
Makosa ya kujamiiana 2 1 3 6 0 6
Kupatikana na bunduki na risasi 5 0 5 3 0 3
Kujeruhi 0 0 0 9 1 10
Kuchoma moto nyumba 0 0 0 2 0 2
Makosa ya rushwa 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na pombe ya moshi 0 0 0 0 0 0
Uzembe na uzururaji 0 0 0 1 0 1
Makosa mengineyo 1,779 23 1,802 1,871 43 1,914
Jumla 1,812 24 1,836 1,953 46 1,999
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
4.12 Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na
Nchi Wanazotoka
Kwa mwaka 2013 mahabusu wasio raia wa Tanzania waliopokelewa magerezani walikuwa 1,530
wakilinganishwa na 2,552 wa mwaka 2014 ikiwa ni ongezeko la mahabusu 1,022 sawa na asilimia
66.8. Mwaka 2013 mahabusu wengi wa mahabusu walikuwa ni raia wa Ethiopia (632) na mwaka
2014 wengi ni kutoka Burundi (1,287).
Aidha kwa miaka yote miwili, mahabusu wengi wasiokuwa raia walikuwa wanatuhumiwa kwa kosa
la wizi ambapo mwaka 2013 idadi yao ilikuwa 73 na mwaka 2014 ilikuwa 76. Mahabusu wanaume
wasio raia kwa mwaka 2013 walikuwa 1,442 na mwaka 2014 walikuwa 2,406 ambalo ni ongezeko
la wanaume 964 sawa na asilimia 66.9. Mahabusu wanawake wasio raia kwa mwaka 2013
walikuwa 88 na mwaka 2014 walikuwa 146 ambalo ni ongezeko la wanawake 58 sawa na asilimia
65.9 (Jedwali 4.16 na 4.17).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
47
Jedwali 4.16: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na
Nchi Walizotoka, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Nchi Walizotoka
2013 2014
Jinsi Jumla
Jinsi Jumla
Me Ke Me Ke
Angola 0 0 0 1 0 1
Burundi 513 53 566 1,184 103 1,287
Cameroon 0 1 1 3 0 3
China 1 0 1 2 1 3
Colombia 0 0 0 1 0 1
Congo 15 0 15 110 9 119
DRC 43 3 46 7 1 8
Ethiopia 632 0 632 562 0 562
Estonia 0 0 0 0 1 1
Finland 0 0 0 1 0 1
Ujerumani 0 0 0 1 0 1
Ugiriki 1 0 1 1 0 1
Hong Kong 0 0 0 220 0 220
India 7 1 8 7 2 9
Iran 0 0 0 18 0 18
Kenya 96 5 101 74 8 82
Lebanon 0 0 0 1 0 1
Liberia 0 1 1 2 1 3
Malawi 2 1 3 11 2 13
Msumbiji 2 0 2 1 0 1
Nigeria 11 0 11 20 1 21
Pakistan 4 0 4 12 0 12
Romania 0 0 0 2 0 2
Rwanda 85 18 103 113 14 127
Sherisheri 0 0 0 1 0 1
Vietnam 1 0 1 1 0 1
Somalia 9 3 12 16 0 16
Zimbabwe 0 0 0 2 0 2
Sudan 0 0 0 1 0 1
Uganda 15 1 16 26 3 29
Marekani 0 0 0 1 0 1
Zambia 0 0 0 4 0 4
Bangladesh 3 0 3 0 0 0
Bulgaria 1 0 1 0 0 0
Madagascar 0 1 1 0 0 0
Uingereza 1 0 1 0 0 0
Jumla 1,442 88 1,530 2,406 146 2,552
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
48
Jedwali 4.17: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Jinsi na
Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Aina ya Kosa
2013 2014
Me Ke Jumla Me Ke Jumla
Mauaji 37 0 37 45 3 48
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 0 0 0 0 0 0
Kujaribu kuua 1 0 1 21 4 25
Unyang’anyi 40 0 40 3 0 3
Wizi 68 5 73 67 9 76
Kuvunja nyumba 15 1 16 25 0 25
Kupatikana na dawa za kulevya 16 2 18 46 4 50
Kupatikana na nyara za serikali 12 0 12 3 0 3
Makosa ya kujamiiana 12 0 12 40 0 40
Kupatikana na bunduki au risasi 5 0 5 23 0 23
Kujeruhi 20 4 24 28 0 28
Kuchoma moto nyumba 2 0 2 2 0 2
Makosa ya rushwa 2 0 2 5 1 6
Kupatikana na pombe ya moshi 1 0 1 0 0 0
Uzembe na uzururaji 0 0 0 3 0 3
Makosa mengineyo 1,211 76 1,287 2,095 125 2,220
Jumla 1,442 88 1,530 2,406 146 2,552
Chanzo: Magereza Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
49
SURA YA TANO
WAHALIFU WALIOHAMISHWA KUTOKA GEREZA MOJA KWENDA JINGINE
5.0 Utangulizi
Kutokana na sababu mbalimbali, wahalifu huhamishwa kutoka gereza moja kwenda jingine. Baadhi
ya sababu hizo ni pamoja na kuhitajika mahakamani, matibabu, masomoni, shughuli za uzalishaji
na sababu za kiusalama.
5.1 Wahalifu Waliohamishwa kwa Jinsi na Mkoa
Mwaka 2013 wahalifu 11,505 walihamishwa kutoka gereza moja kwenda jingine kutokana na
sababu mbalimbali. Mwaka 2014 idadi waliohamishwa ilipungua na kufikia 10,966 ikiwa ni
pungufu ya wahalifu 539 sawa na asilimia 4.9. Kati ya wahalifu waliohamishwa mwaka 2013,
wafungwa walikuwa 9,122 na mahabusu walikuwa 2,383 wakati mwaka 2014 wafungwa walikuwa
8,680 na mahabusu 2,286. Mikoa iliyohamisha wahalifu wengi kuliko mingine ni Mbeya
iliyohamisha wahalifu 1,544 mwaka 2013 na Kagera iliyohamisha wahalifu 1,130 mwaka 2014
(Jedwali 5.1).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
50
Jedwali 5.1: Idadi ya wahalifu Waliohamishwa kwa Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa
2013 2014
Wafungwa Mahabusu Jumla
kuu
Wafungwa Mahabusu Jumla
kuu Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 167 2 0 169 78 6 0 84 253 198 3 0 201 60 3 0 63 264
Dar es Salaam 652 14 0 666 46 3 0 49 715 620 0 0 620 73 3 0 76 696
Dodoma 453 3 0 456 168 17 0 185 641 612 4 0 616 199 36 2 237 853
Iringa 133 2 0 135 32 2 0 34 169 157 1 0 158 27 2 0 29 187
Kagera 643 1 0 644 240 26 0 266 910 799 17 1 817 276 37 0 313 1,130
Kigoma 714 2 1 717 75 14 0 89 806 651 4 3 658 51 3 0 54 712
Kilimanjaro 185 6 0 191 39 2 0 41 232 195 4 0 199 71 8 0 79 278
Lindi 239 2 0 241 24 6 0 30 271 171 1 0 172 8 0 0 8 180
Manyara 74 0 0 74 22 2 0 24 98 200 2 0 202 19 0 0 19 221
Mara 466 4 2 472 69 4 0 73 545 561 4 5 570 84 9 0 93 663
Mbeya 1,230 1 0 1,231 307 6 0 313 1,544 699 3 0 702 89 9 0 98 800
Morogoro 463 6 30 499 12 1 2 15 514 481 9 10 500 43 0 0 43 543
Mtwara 287 0 0 287 61 3 0 64 351 246 0 0 246 51 6 0 57 303
Mwanza 645 7 5 657 247 19 0 266 923 573 21 5 599 335 25 2 362 961
Pwani 135 2 0 137 95 5 0 100 237 139 0 0 139 21 0 0 21 160
Ruvuma 583 3 0 586 36 3 0 39 625 604 0 0 604 28 2 0 30 634
Rukwa 744 1 1 746 63 1 0 64 810 510 0 0 510 9 1 0 10 520
Singida 86 0 0 86 25 3 0 28 114 96 0 3 99 41 7 0 48 147
Shinyanga 590 10 0 600 391 25 1 417 1,017 418 9 1 428 330 11 0 341 769
Tabora 198 10 0 208 170 4 0 174 382 336 0 0 336 264 8 0 272 608
Tanga 320 0 0 320 27 1 0 28 348 304 0 0 304 30 3 0 33 337
Jumla 9,007 76 39 9,122 2,227 153 3 2,383 11,505 8,570 82 28 8,680 2,109 173 4 2,286 10,966
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
51
5.2 Wafungwa wenye Ugonjwa wa Akili kwa Jinsi na Mkoa Waliopokelewa kutoka
Magereza Mengine
Mwaka 2013 ni wafungwa wawili tu wenye ugonjwa wa akili waliopokelewa katika Mkoa wa
Dodoma, wakati mwaka 2014 hapakuwa na mfungwa yoyote mwenye ugonjwa wa akili
aliyepokelewa kutoka magereza mengine.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
52
SURA YA SITA
WAHALIFU WALIOTOKA MAGEREZANI
6.0 Utangulizi
Sura hii inahusu wahalifu waliotoka magerezani mwaka 2013 na 2014. Kwa kawaida wahalifu
hutoka magerezani kwa sababu mbalimbali kama ifuatavyo; kumaliza adhabu zao kwa mujibu wa
sheria, kupata msamaha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenda kutumikia
kifungo cha nje, kulipa faini aliyoamriwa na mahakama, kutoroka chini ya ulinzi halali, kufariki
dunia na mahabusu anapopata wito wa kwenda mahakamani.
6.1 Wahalifu Waliotoka Magerezani Mwaka 2013 na 2014
Majedwali 6.1 na 6.2 na Mchoro 6.1 vinaonesha kwamba kwa mwaka 2013 jumla ya wahalifu
117,911 walitoka magerezani wakilinganishwa na wahalifu 112,510 waliotoka mwaka 2014. Idadi
hiyo ni pungufu ya wahalifu 5,401 sawa na asilimia 4.6. Kati yao, wafungwa ni 20,381 na
mahabusu 97,530 kwa mwaka 2013 ambapo mwaka 2014 wafungwa walikuwa 19,940 na
mahabusu 92,570. Wengi wa wahalifu waliotoka magerezani ni kutoka mikao ya Dar es salaam na
Mwanza, ambapo Mkoa wa Dar es Salaam walitoka wahalifu 14,432 kwa mwaka 2013, Mkoa wa
Mwanza walitoka wahalifu 11,469 kwa mwaka 2014.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
53
Jedwali 6.1: Idadi ya Wahalifu Waliotoka Magerezani kwa Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara, 2013
Mkoa Wafungwa Mahabusu Jumla
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 627 31 12 670 3,596 244 5 3,845 4,223 275 17 4,515
Dar es Salaam 1,762 82 14 1,858 11,669 809 96 12,574 13,431 891 110 14,432
Dodoma 1,050 78 7 1,135 3,943 310 11 4,264 4,993 388 18 5,399
Iringa 860 24 4 888 2,935 243 24 3,202 3,795 267 28 4,090
Kagera 1,190 63 17 1,270 5,722 468 14 6,204 6,912 531 31 7,474
Kigoma 1,104 52 11 1,167 3,284 319 109 3,712 4,388 371 120 4,879
Kilimanjaro 1,153 65 12 1,230 4,974 468 17 5,459 6,127 533 29 6,689
Lindi 476 16 5 497 1,469 94 12 1,575 1,945 110 17 2,072
Manyara 411 46 2 459 2,347 204 0 2,551 2,758 250 2 3,010
Mara 712 79 23 814 5,686 621 102 6,409 6,398 700 125 7,223
Mbeya 1,120 30 20 1,170 5,740 530 4 6,274 6,860 560 24 7,444
Morogoro 1,159 63 49 1,271 3,242 219 226 3,687 4,401 282 275 4,958
Mtwara 446 21 5 472 2,250 160 1 2,411 2,696 181 6 2,883
Mwanza 1,704 89 54 1,847 8,720 749 178 9,647 10,424 838 232 11,494
Pwani 356 26 8 390 3,492 109 0 3,601 3,848 135 8 3,991
Ruvuma 550 30 7 587 520 260 10 790 1,070 290 17 1,377
Rukwa 625 43 10 678 2,253 171 33 2,457 2,878 214 43 3,135
Singida 461 33 10 504 2,330 214 6 2,550 2,791 247 16 3,054
Shinyanga 1,001 61 27 1,089 6,624 301 279 7,204 7,625 362 306 8,293
Tabora 1,020 59 15 1,094 4,824 213 12 5,049 5,844 272 27 6,143
Tanga 1,200 79 12 1,291 3,764 260 41 4,065 4,964 339 53 5,356
Jumla 18,987 1,070 324 20,381 89,384 6,966 1,180 97,530 108,371 8,036 1,504 117,911
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
54
Jedwali 6.2: Idadi ya Wahalifu Waliotoka Magerezani kwa Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara, 2014
Mkoa
Wafungwa Mahabusu Jumla
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Kuu
Arusha 657 42 15 714 3,627 386 0 4,013 4284 428 15 4,727
Dar es Salaam 1,331 79 40 1,450 8,570 719 211 9,500 9901 798 251 10,950
Dodoma 919 66 17 1,002 4,755 312 38 5,105 5674 378 55 6,107
Iringa 987 35 0 1,022 3,032 167 26 3,225 4019 202 26 4,247
Kagera 1,091 68 24 1,183 5,214 219 21 5,454 6305 287 45 6,637
Kigoma 887 59 33 979 4,005 165 178 4,348 4892 224 211 5,327
Kilimanjaro 721 60 28 809 4,259 388 38 4,685 4980 448 66 5,494
Lindi 512 21 5 538 1,254 78 12 1,344 1766 99 17 1,882
Manyara 483 29 0 512 1,310 242 0 1,552 1793 271 0 2,064
Mara 869 36 22 927 3,103 455 179 3,737 3972 491 201 4,664
Mbeya 1,010 51 36 1,097 4,879 571 4 5,454 5889 622 40 6,551
Morogoro 1,102 63 37 1,202 2,731 315 202 3,248 3833 378 239 4,450
Mtwara 649 30 11 690 1,848 138 5 1,991 2497 168 16 2,681
Mwanza 1,819 94 33 1,946 8,542 737 244 9,523 10361 831 277 11,469
Pwani 584 44 19 647 2,057 101 2 2,160 2641 145 21 2,807
Ruvuma 678 64 13 755 2,686 147 14 2,847 3364 211 27 3,602
Rukwa 548 20 10 578 2,324 88 92 2,504 2872 108 102 3,082
Singida 628 46 13 687 4,457 458 95 5,010 5085 504 108 5,697
Shinyanga 1,015 69 19 1,103 5,126 574 205 5,905 6141 643 224 7,008
Tabora 957 56 15 1,028 4,614 536 8 5,158 5571 592 23 6,186
Tanga 1,002 53 16 1,071 5,260 466 81 5,807 6262 519 97 6,878
Total 18,449 1,085 406 19,940 83,653 7,262 1,655 92,570 102,102 8,347 2,061 112,510
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
55
Mchoro 6.1: Idadi ya Wahalifu Waliotoka Magerezani, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
6.2 Wafungwa Walioachiwa kwenda Kutumikia Kifungo cha Nje kwa Jinsi na Mkoa
Mwaka 2013 wafungwa 1,139 waliachiwa kwenda kutumikia kifungo cha nje wakilinganishwa na
wafungwa 1,205 walioachiwa mwaka 2014. Hili ni ongezeko la wafungwa 66 sawa na asilimia 5.8.
Mkoa ulioachia wafungwa wengi kuliko mikoa mingine ni Mbeya, ambapo mwaka 2013 uliachia
wafungwa 183 na mwaka 2014 wafungwa 208 kama inavyoonesha kwenye Jedwali 6.3.
Mfungwa yeyote anaruhusiwa kutumikia kifungo cha nje ikiwa:
Amehukumiwa kutumikia kifungo kisichozidi miezi 12 gerezani
Amefungwa baada ya kushindwa kulipa faini au fidia hata kama kifungo chake ni zaidi ya
miezi 12.
Lengo kubwa la kuwaachia wafungwa kwenda kutumikia kifungo cha nje ni kupunguza
msongamano magerezani.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
56
Jedwali 6.3: Idadi Ya Wafungwa Walioachiwa kwenda Kutumikia Kifungo cha Nje kwa Jinsi na Mkoa ,
Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa 2013 2014
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 3 2 0 5 1 0 0 1
Dar es Salaam 124 48 0 172 116 31 0 147
Dodoma 10 11 0 21 15 8 0 23
Iringa 8 0 0 8 7 1 0 8
Kagera 77 13 0 90 102 25 0 127
Kigoma 45 14 1 60 17 10 0 27
Kilimanjaro 42 7 0 49 64 17 0 81
Lindi 3 1 0 4 1 1 0 2
Manyara 23 2 0 25 35 1 0 36
Mara 87 15 0 102 56 21 0 77
Mbeya 162 19 2 183 180 28 0 208
Morogoro 24 5 3 32 35 8 3 46
Mtwara 8 0 0 8 13 2 0 15
Mwanza 82 13 2 97 129 13 0 142
Pwani 14 1 0 15 17 0 0 17
Ruvuma 24 0 0 24 7 1 0 8
Rukwa 18 0 0 18 7 3 0 10
Singida 23 7 0 30 33 6 0 39
Shinyanga 129 18 0 147 130 10 0 140
Tabora 22 5 0 27 20 1 0 21
Tanga 17 5 0 22 24 6 0 30
Jumla 945 186 8 1,139 1,009 193 3 1,205
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
57
Mchoro 6.2: Wafungwa Walioachiwa kwenda Kutumikia Kifungo cha Nje kwa Jinsi na Mkoa , Tanzania
Bara, 2013 na 2014.
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
58
6.3 Wafungwa Walioachiwa Baada ya Kulipa Faini kwa Urefu wa Kifungo na Mkoa
Jumla ya wafungwa 2,826 waliachiwa huru mwaka 2014 baada ya kulipa faini wakilinganishwa na
wafungwa 3,138 walioachiwa mwaka 2013. Huu ni pungufu ya wafungwa 312 ambayo ni sawa na
asilimia 9.9. Wengi wa wafungwa waliolipa faini ni wale waliofungwa gerezani zaidi ya miezi
mitatu. Kwa mwaka 2013, jumla yao ilikuwa ni 2,008 wakilinganishwa na wafungwa 2,211 kwa
mwaka 2014 . Hili ni ongezeko la wafungwa 203 ambayo ni sawa na asilimia 10.1.
Aidha, mikoa iliyoachia wafungwa wengi kuliko mikoa mingine waliolipa faini ni Kilimanjaro na
Dar es salaam. Mkoa wa Kilimanjaro uliachilia wafungwa 527 kwa mwaka 2013 na Mkoa wa Dar
es Salaam uliachilia wafungwa 361 kwa mwaka 2014 (Jedwali 6.4).
Jedwali 6.4: Idadi ya Wafungwa Walioachiwa Baada ya Kulipa Faini kwa Urefu wa Kifungo na Mkoa ,
Tanzania Bara, 2013 na 2014.
Mkoa
2013 2014
Chini ya
Mwezi 1
Mwezi 1
hadi miezi 3
Zaidi ya
Miezi 3 Jumla
Chini ya
Mwezi 1
Mwezi 1
hadi miezi 3
Zaidi ya
Miezi 3 Jumla
Arusha 2 1 3 6 0 2 1 3
Dar es Salaam 7 156 185 348 66 71 224 361
Dodoma 39 53 139 231 16 40 49 105
Iringa 0 6 37 43 10 12 52 74
Kagera 4 33 34 71 9 41 71 121
Kigoma 0 16 184 200 0 10 301 311
Kilimanjaro 441 4 82 527 2 5 58 65
Lindi 4 16 64 84 1 9 34 44
Manyara 0 0 0 0 2 13 40 55
Mara 0 27 115 142 0 16 165 181
Mbeya 6 37 131 174 7 41 86 134
Morogoro 0 9 118 127 0 17 114 131
Mtwara 0 10 74 84 0 8 90 98
Mwanza 4 49 195 248 0 57 225 282
Pwani 0 13 50 63 1 35 46 82
Ruvuma 0 37 163 200 16 40 97 153
Rukwa 0 0 23 23 0 1 57 58
Singida 10 79 38 127 0 15 56 71
Shinyanga 2 43 198 243 0 22 237 259
Tabora 0 5 50 55 0 3 54 57
Tanga 5 12 125 142 2 25 154 181
Jumla 524 606 2,008 3,138 132 483 2,211 2,826
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
59
6.4 Wahalifu Waliotoroka Magerezani Chini ya Ulinzi Halali kwa Jinsi na Mkoa
Wahalifu 272 walitoroka magerezani mwaka 2013 wakilinganishwa na waharifu watoro 250 kwa
mwaka 2014, ambao ni pungufu ya watoro 22 sawa na asilimia 8.1. Kati ya wahalifu waliotoroka
mwaka 2013, wafungwa walikuwa ni 263 sawa na asilimia 96.7 na mahabusu walikuwa 9 sawa na
asilimia 3.3. Mwaka 2014 wafungwa waliotoroka magerezani walikuwa 239 sawa na asilimia 95.6
na mahabusu 11 sawa na asilimia 4.4.
Mikoa iliyoongoza kwa utoro wa wahalifu ni Tanga, Morogoro na Rukwa. Mkoa wa Tanga ulikuwa
na wahalifu watoro 23 kwa mwaka 2013 na Morogoro na Rukwa ilikuwa na wahalifu watoro 25
kila mmoja kwa mwaka 2014.
Mwaka 2014 waharifu watoro walipungua kulinganishwa na mwaka 2013 kutokana na
kuimarishwa kwa ulinzi magerezanikama inavyoonesha katika Jedwali 6.5 na Mchoro 6.3.
Jedwali 6.5: Idadi ya Wahalifu Waliotoroka Magerezani Chini ya Ulinzi Halali kwa Jinsi na Mkoa ,
Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa
2013 2014
Wafungwa Mahabusu Jumla
Kuu
Wafungwa Mahabusu Jumla
Kuu Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 6 0 0 6 0 0 0 0 6 6 0 0 6 0 0 0 0 6
Dar es Salaam 13 0 0 13 1 0 0 1 14 14 0 0 14 2 0 0 2 16
Dodoma 19 0 0 19 0 0 0 0 19 12 0 0 12 0 0 0 0 12
Iringa 6 0 0 6 1 0 0 1 7 12 0 0 12 0 0 0 0 12
Kagera 7 0 0 7 4 0 0 4 11 12 0 0 12 0 0 0 0 12
Kigoma 20 0 1 21 1 0 0 1 22 16 0 0 16 0 0 0 0 16
Kilimanjaro 5 0 0 5 0 0 0 0 5 9 0 0 9 1 0 0 1 10
Lindi 5 0 0 5 0 0 0 0 5 5 0 0 5 1 0 0 1 6
Manyara 8 0 0 8 0 0 0 0 8 8 0 0 8 0 0 0 0 8
Mara 13 0 0 13 1 0 0 1 14 6 0 0 6 1 0 0 1 7
Mbeya 16 0 0 16 0 0 0 0 16 16 0 0 16 1 0 0 1 17
Morogoro 20 0 0 20 0 0 0 0 20 24 0 1 25 0 0 0 0 25
Mtwara 8 0 0 8 0 0 0 0 8 11 0 0 11 0 0 0 0 11
Mwanza 22 0 0 22 0 0 0 0 22 18 0 0 18 1 0 0 1 19
Pwani 8 0 0 8 1 0 0 1 9 11 0 0 11 0 0 0 0 11
Ruvuma 4 0 0 4 0 0 0 0 4 0 0 0 0 1 0 0 1 1
Rukwa 22 0 0 22 0 0 0 0 22 25 0 0 25 0 0 0 0 25
Singida 6 0 0 6 0 0 0 0 6 8 0 0 8 0 0 0 0 8
Shinyanga 20 0 0 20 0 0 0 0 20 5 0 0 5 0 0 0 0 5
Tabora 11 0 0 11 0 0 0 0 11 8 0 0 8 3 0 0 3 11
Tanga 23 0 0 23 0 0 0 0 23 12 0 0 12 0 0 0 0 12
Jumla 262 0 1 263 9 0 0 9 272 238 0 1 239 11 0 0 11 250
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
60
Mchoro 6.3: Wahalifu Waliotoroka Magerezani Chini ya Ulinzi Halali, Tanzania Bara, 2013 na 2014.
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
6.5 Wahalifu Waliofariki Magerezani kwa Jinsi na Mkoa
Jumla ya wahalifu 209 walifariki magerezani mwaka 2013 wakiliganishwa na wahalifu 223 mwaka
2014 ikiwa ni ongezeko la wahalifu waliofariki 14 sawa na asilimia 6.7.
Kati ya wahalifu waliofariki mwaka 2013 walikuwa 103 sawa na asilimia 49.3 na mahabusu 106
sawa na asilimia 50.7, wakati mwaka 2014 wafungwa waliofariki walikuwa 101 sawa na asilimia
45.3 na mahabusu 122 sawa na asilimia 54.7.
Wengi wa wahalifu hao walifariki kwa magonjwa ya HIV/AIDS (UKIMWI), upungufu wa damu
(ANAEMIA), kifua kikuu (TB), MALARIA na Mashinikizo ya moyo (HEART FAILURE).
Mikoa iliyoongoza kwa vifo vya wahalifu magerezani ni Mwanza na Dar es salaam. Mkoa wa
Mwanza ulikuwa na idadi ya vifo 35 kwa mwaka 2013 na Dar es salaam ulikuwa na idadi ya vifo
35 kwa mwaka 2014 (Jedwali 6.6).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
61
Jedwali 6.6: Idadi ya Wahalifu Waliofariki Magerezani kwa Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara, 2013 na 2014.
Mkoa
2013 2014
Wafungwa Mahabusu Jumla
Kuu
Wafungwa Mahabusu Jumla
Kuu Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 3 0 0 3 0 0 0 0 3 0 0 0 0 1 0 0 1 1
Dar es Salaam 18 0 0 18 11 2 0 13 31 14 0 0 14 21 0 0 21 35
Dodoma 6 0 0 6 3 0 0 3 9 4 1 0 5 8 0 0 8 13
Iringa 6 0 0 6 11 0 0 11 17 9 0 0 9 15 1 0 16 25
Kagera 8 0 0 8 3 0 0 3 11 9 0 0 9 17 0 0 17 26
Kigoma 0 0 0 0 6 0 0 6 6 2 0 0 2 2 0 0 2 4
Kilimanjaro 4 0 0 4 4 0 0 4 8 3 0 0 3 2 0 0 2 5
Lindi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 1 0 0 0 0 1
Manyara 2 0 0 2 1 0 0 1 3 1 0 0 1 1 0 0 1 2
Mara 1 0 0 1 11 1 0 12 13 4 0 0 4 5 0 0 5 9
Mbeya 4 0 0 4 6 1 0 7 11 8 0 0 8 7 0 0 7 15
Morogoro 6 0 0 6 7 0 0 7 13 8 0 0 8 6 0 0 6 14
Mtwara 2 0 0 2 2 0 0 2 4 0 1 0 1 3 0 0 3 4
Mwanza 18 0 0 18 16 1 0 17 35 16 0 0 16 13 0 0 13 29
Pwani 2 0 0 2 1 0 0 1 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Ruvuma 1 0 0 1 1 0 0 1 2 1 0 0 1 0 0 0 0 1
Rukwa 3 0 0 3 2 0 0 2 5 0 0 0 0 5 0 0 5 5
Singida 1 0 0 1 1 0 0 1 2 1 0 0 1 1 0 0 1 2
Shinyanga 7 0 0 7 5 0 0 5 12 4 0 0 4 5 0 0 5 9
Tabora 10 0 0 10 9 0 0 9 19 12 0 0 12 9 0 0 9 21
Tanga 1 0 0 1 1 0 0 1 2 2 0 0 2 0 0 0 0 2
Jumla 103 0 0 103 101 5 0 106 209 99 2 0 101 121 1 0 122 223
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
62
SURA YA SABA
WAHALIFU WALIOPEWA ADHABU KWA MAKOSA YA UTOVU WA
NIDHAMU WAKIWA MAGEREZANI
7.0 Utangulizi
Kwa mujibu wa Kanuni za Magereza za Mwaka 2003, Mkuu wa Gereza (O/IC) ana mamlaka ya
kumwadhibu mhalifu yeyote akifanya makosa ya utovu wa nidhamu akiwa gerezani isipokuwa kwa
adhabu ya viboko ambayo inahitaji uthibitisho kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Magereza.
Adhabu ambazo Mkuu wa Gereza ana mamlaka ya kutoa kwa mhalifu ambaye yupo gerezani ni
pamoja na kupoteza siku za msamaha, kupewa chakula kidogo, kutengwa katika chumba cha
adhabu na hata kupelekwa mahakamani ikibidi. Kabla ya utekelezaji wa adhabu Mganga wa Gereza
ni lazima athibitishe uwezo wa mhalifu husika kuimudu adhabu aliyopewa. Lengo la adhabu hizo ni
kurekebisha tabia za wahalifu wakiwa magerezani, ili waweze kubadilika na kuwa wafungwa
wenye nidhamu mara wamalizapo adhabu zao.
7.1 Wahalifu Waliopewa Adhabu Magerezani kwa Aina ya Adhabu na Mkoa
Jumla ya wahalifu 1,093 waliadhibiwa mwaka 2013 wakilinganishwa na wahalifu 892
walioadhibiwa mwaka 2014 ikiwa ni pungufu wa wahalifu 201 sawa na asilimia 18.4. Wahalifu
wengi walipewa adhabu za kupoteza siku za msamaha ambapo kwa mwaka 2013 waliopewa
adhabu hiyo walikuwa 529 na mwaka 2014 walikuwa 598. Hili ni ongezeko la wahalifu 69 sawa na
asilimia 13.0. Mikoa iliyoadhibu wahalifu wengi zaidi kuliko mingine ni Dar es Salaam ambapo
kwa mwaka 2013 wahalifu 191 waliadhibiwa na Mkoa wa Morogoro kwa mwaka 2014 wahalifu
121 waliadhibiwa ( Majedwali 7.1 na 7.2).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
63
Jedwali 7. 1: Idadi ya Wahalifu Waliopewa Adhabu Magerezani kwa Aina ya Adhabu na Mkoa , Tanzania
Bara, 2013
Mkoa
Adhabu ya Viboko Kupunguziwa Siku za
Msamaha
Chakula
Kidogo
na
ku
fun
giw
a v
yu
mb
a v
ya
ad
ha
bu
na
on
yo
Jumla
tu
na
ku
pu
ng
uza s
iku
za
msa
ma
ha
na
ch
ak
ula
kid
ogo
na
ku
fun
giw
a v
yu
mb
a v
ya
ad
ha
bu
na
ku
pu
ng
uza s
iku
za
msa
ma
ha
na
na
ku
pu
ng
uziw
a s
iku
za
na
ku
pu
ng
uziw
a s
iku
za
msa
ma
ha
na
ch
ak
ula
na
ch
ak
ula
kid
ogo
na
ku
fun
giw
a
tu
na
ch
ak
ula
kid
ogo
na
ku
fun
giw
a vy
um
ba
vy
a
ad
ha
bu
na
ch
ak
ula
kid
ogo
na
tu
na
ku
fun
giw
a v
yu
mb
a v
ya
ad
ha
bu
Arusha 0 9 0 0 0 0 0 0 51 18 23 0 22 0 0 0 123
Dar es Salaam 1 0 0 0 0 0 0 0 64 0 16 2 0 0 108 0 191
Dodoma 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Iringa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kagera 6 2 5 0 3 0 4 0 30 0 2 0 5 0 0 0 57
Kigoma 0 0 0 0 0 0 0 0 18 0 0 0 0 0 0 0 18
Kilimanjaro 0 0 0 0 0 0 0 0 26 14 0 0 12 0 0 0 52
Lindi 0 0 0 0 0 0 0 0 27 0 0 0 0 0 5 0 32
Manyara 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Mara 0 0 0 0 0 0 0 0 4 0 0 0 1 0 0 0 5
Mbeya 0 0 0 0 0 0 0 0 21 0 3 2 1 0 8 0 35
Morogoro 0 0 0 0 0 0 0 0 35 0 0 0 0 0 0 0 35
Mtwara 12 9 18 0 0 0 0 0 30 0 0 0 0 0 0 0 69
Mwanza 3 0 0 0 0 0 0 0 94 54 0 0 23 0 0 0 174
Pwani 0 0 0 0 0 0 0 0 17 0 0 0 0 0 0 0 17
Ruvuma 0 0 0 0 0 0 0 0 4 6 0 0 0 4 0 0 14
Rukwa 0 0 0 0 0 0 0 0 45 0 0 0 10 0 0 0 55
Singida 0 0 0 0 0 0 0 0 14 0 0 0 1 0 0 0 15
Shinyanga 0 0 0 0 0 0 0 13 5 1 12 0 4 0 0 0 35
Tabora 4 0 0 0 0 0 0 0 18 0 0 1 0 45 0 0 68
Tanga 0 0 0 0 0 0 0 0 26 0 2 7 0 59 4 0 98
Jumla 26 20 23 0 3 0 4 13 529 93 58 12 79 108 125 0 1,093
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
64
Jedwali 7.2: Idadi ya Wahalifu Waliopewa Adhabu Magerezani kwa Aina ya Adhabu na Mkoa, Tanzania
Bara, 2014
Mkoa
Adhabu ya Viboko Kupunguziwa Siku za
Msamaha
Chakula
Kidogo
na
ku
fun
giw
a v
yu
mb
a v
ya
ad
ha
bu
na
on
yo
Jumla
tu
na
ku
pu
ng
uza s
iku
za m
sam
ah
a
na
ch
ak
ula
kid
ogo
na
ku
fun
giw
a v
yu
mb
a v
ya
ad
ha
bu
na
ku
pu
ng
uza s
iku
za m
sam
ah
a n
a
ku
fun
giw
a
na
ku
pu
ng
uziw
a s
iku
za
msa
ma
ha
na
ch
ak
ula
kid
ogo
na
ku
pu
ng
uziw
a s
iku
za
msa
ma
ha
na
na
ch
ak
ula
kid
ogo
na k
ufu
ng
iwa
vy
um
ba v
ya
ad
ha
bu
tu
na
ch
ak
ula
kid
ogo
na
ku
fun
giw
a vy
um
ba
vy
a a
dh
ab
u
na
ch
ak
ula
kid
ogo
na k
ufu
ng
iwa
vy
um
ba v
ya
ad
ha
bu
tu
na
ku
fun
giw
a v
yu
mb
a v
ya
ad
ha
bu
Arusha 0 0 0 0 0 0 0 0 46 0 0 0 5 0 0 0 51
Dar es
Salaam 6 14 0 1 0 0 0 0 2 0 0 2 0 20 22 0 67
Dodoma 0 0 0 0 0 0 0 0 12 0 3 0 0 0 1 0 16
Iringa 2 0 0 0 0 0 0 0 3 0 0 0 0 0 0 0 5
Kagera 6 4 6 0 2 0 1 0 15 0 6 0 6 0 0 0 46
Kigoma 1 0 0 0 0 0 0 0 19 0 0 0 4 0 1 0 25
Kilimanjaro 0 0 0 0 0 0 0 0 26 0 0 0 7 0 0 0 33
Lindi 0 0 0 0 0 0 0 0 25 0 0 0 12 0 8 0 45
Manyara 0 0 0 0 0 0 0 0 16 0 0 0 0 0 0 0 16
Mara 0 0 0 0 0 0 0 0 62 1 0 0 0 0 0 0 63
Mbeya 0 0 0 0 0 0 0 0 6 0 0 0 0 0 0 0 6
Morogoro 0 0 0 0 0 0 0 0 121 0 0 0 0 0 0 0 121
Mtwara 0 2 0 0 0 0 0 0 49 0 3 0 0 0 0 0 54
Mwanza 3 0 0 0 0 0 0 0 88 0 0 0 23 0 0 0 114
Pwani 0 0 0 0 0 0 0 0 21 0 0 0 0 0 2 0 23
Ruvuma 0 0 0 0 0 0 0 0 12 2 0 0 0 0 0 0 14
Rukwa 0 0 0 0 0 0 0 0 33 8 0 0 6 4 0 0 51
Singida 0 11 0 0 0 0 0 0 8 0 0 0 11 0 0 0 30
Shinyanga 0 0 0 0 0 0 0 0 15 1 0 4 0 4 6 1 31
Tabora 0 0 0 0 0 0 0 0 4 8 0 0 4 15 0 0 31
Tanga 13 5 10 0 0 0 0 0 15 2 0 0 0 4 1 0 50
Jumla 31 36 16 1 2 0 1 0 598 22 12 6 78 47 41 1 892
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
65
SURA YA NANE
MAHABUSU WALIOHUKUMIWA ADHABU ZA VIFUNGO WAKIWA
MAGEREZANI
8.0 Utangulizi
Mahabusu ni wahalifu waliopokelewa magerezani wakituhumiwa kutenda makosa mbalimbali
ambapo Magereza huwapeleka mahakamani ili kusikiliza kesi zao, hatimaye kuhukumiwa adhabu
za vifungo au huachiwa huru.
8.1 Mahabusu Waliohukumiwa Wakiwa Magerezani kwa Jinsi na Mkoa
Kutokana na takwimu za mwaka 2013, mahabusu 4,380 walihukumiwa adhabu za vifungo wakiwa
magerezani, wakilinganishwa na mahabusu 4,251 wa mwaka 2014, ikiwa ni pungufu ya mahabusu
129 sawa na asilimia 2.9. Kati ya hao wa mwaka 2013 wanaume walikuwa 4,195 sawa na asilimia
95.8 wanawake 129 sawa na asilimia 2.9 na vijana 56 sawa na asilimia 1.3. Kwa mwaka 2014
mahabusu wanaume walikuwa 4,071 sawa na asilimia 95.8, wanawake 143 sawa na asilimia 3.4 na
mahabusu vijana 37 sawa na asilimia 0.9.
Aidha, mkoa ambao mahabusu wengi walihukumiwa adhabu za vifungo wakiwa magerezani kuliko
mikoa mingine ni Mwanza ambapo mahabusu 761 walihukumiwa kwa mwaka 2013 na mahabusu
836 walihukumiwa kwa mwaka 2014 (Jedwali 8.1).
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
66
Jedwali 8.1: Idadi ya Mahabusu Waliohukumiwa Wakiwa Magerezani kwa Jinsi na Mkoa, Tanzania Bara,
2013 na 2014
Mkoa 2013 2014
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 30 0 0 30 0 0 0 0
Dar es Salaam 66 0 0 66 51 0 0 51
Dodoma 183 14 0 197 187 11 0 198
Iringa 166 2 0 168 246 10 0 256
Kagera 174 4 0 178 208 2 0 210
Kigoma 15 1 0 16 199 4 0 203
Kilimanjaro 235 7 0 242 247 7 0 254
Lindi 11 0 0 11 10 0 0 10
Manyara 180 2 0 182 42 0 0 42
Mara 302 13 0 315 258 12 0 270
Mbeya 262 13 0 275 318 11 0 329
Morogoro 169 5 14 188 121 6 14 141
Mtwara 163 1 0 164 223 4 0 227
Mwanza 799 19 18 836 714 25 22 761
Pwani 106 1 0 107 183 3 0 186
Ruvuma 205 0 0 205 129 1 0 130
Rukwa 152 11 7 170 136 1 0 137
Singida 55 3 0 58 68 6 0 74
Shinyanga 443 18 17 478 417 29 1 447
Tabora 80 0 0 80 97 0 0 97
Tanga 399 15 0 414 217 11 0 228
Jumla 4,195 129 56 4,380 4,071 143 37 4,251
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu, 2013 na 2014
67
SURA YA TISA
HITIMISHO
9.0 Utangulizi
Baada ya kuangalia kwa makini hali halisi ya Magereza yetu nchini, taarifa hii ya kitakwimu
itasaidia Jeshi la Magereza kupanga mipango, kufanya maamuzi sahihi na kutathmini matokeo kwa
kutumia takwimu ili kuwalinda na kurekebisha wahalifu wamalizapo adhabu zao wawe raia wema.
Aidha, mapendekezo hayo yawawezeshe kwenda kushiriki katika shughuli mbali mbali za
maendeleo kwa lengo la kuboresha maisha yao binafsi na kutoa mchango unaohitajika katika
kupambana na umaskini ili kukuza uchumi wa nchi yetu. Hii itasaidia kuondoa mtazamo hasi wa
baadhi ya watu kwamba magereza ni sehemu ya mateso, badala yake jamii itambue kuwa magereza
ni sehemu au shule ya mafunzo ya kurekebisha tabia za wakosaji.
Kwa kufanya hivyo kutasaidia kujenga mazingira salama kwa wananchi, taasisi mbalimbali,
wawekezaji na Taifa kwa ujumla kama ilivyoainishwa katika malengo ya MKUKUTA.
9.1 Hitimisho
Taarifa hii imeangalia takwimu mbalimbali za wafungwa na mahabusu waliokuwa magerezani kwa
kipindi cha miaka miwili kuanzia Januari 1, 2013 hadi Desemba 31, 2013 na Januari 1, 2014 hadi
Desemba 31, 2014. Pamoja na mafanikio mbalimbali ambayo Jeshi la Magereza limeyapata katika
kutekeleza majukumu yake, bado zipo changamoto mbali mbali ambazo zinazohitajiwa kutafutiwa
ufumbuzi ili kuongeza ufanisi katika suala zima la kuwarekebisha wahalifu.
Kupatikana kwa takwimu ni jambo muhimu, lakini kuzitumia katika kutekeleza majukumu
mbalimbali ni muhimu zaidi. Kwa maana hiyo ni muhimu Jeshi la Magereza liwezeshwe ipasavyo
kwa kupatiwa rasilimali (watu, fedha na vifaa ) za kutosha ili kuimarisha kitengo cha takwimu.
Aidha upatikanaji wa takwimu bora utalisaidia Jeshi la Magereza kuimarisha huduma za
urekebishaji wa wahalifu kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia. Ili kuleta mafanikio
yanayokusudiwa ni muhimu serikali itoe kipaumbele kwa kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya
kuimarisha huduma za urekebishaji wa wahalifu magerezani.
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
68
Majedwali Ambatanisho
Jedwali Na. 1: Idadi ya Wahalifu Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Jinsi na Aina ya Uhalifu, Tanzania Bara, 2013
Mkoa
Mahabusu Wafungwa Jumla
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 661 24 0 685 495 8 0 503 1,156 32 0 1,188
Dar es Salaam 2,115 84 15 2,214 1,900 29 1 1,930 4,015 113 16 4,144
Dodoma 748 34 10 792 1,078 22 8 1,108 1,826 56 18 1,900
Iringa 817 50 3 870 412 14 0 426 1,229 64 3 1,296
Kagera 891 134 3 1,028 957 29 1 987 1,848 163 4 2,015
Kigoma 591 63 59 713 812 26 20 858 1,403 89 79 1,571
Kilimanjaro 759 50 10 819 670 16 0 686 1,429 66 10 1,505
Lindi 218 7 0 225 357 4 5 366 575 11 5 591
Manyara 479 26 0 505 433 11 0 444 912 37 0 949
Mara 1,115 38 15 1,168 628 9 4 641 1,743 47 19 1,809
Mbeya 1,037 53 2 1,092 1,035 20 6 1,061 2,072 73 8 2,153
Morogoro 676 35 11 722 912 34 31 977 1,588 69 42 1,699
Mtwara 396 15 0 411 416 10 0 426 812 25 0 837
Mwanza 1,569 117 101 1,787 1,748 42 7 1,797 3,317 159 108 3,584
Pwani 410 9 0 419 413 5 0 418 823 14 0 837
Ruvuma 229 17 1 247 281 1 0 282 510 18 1 529
Rukwa 411 26 4 441 481 6 2 489 892 32 6 930
Singida 488 35 21 544 367 12 3 382 855 47 24 926
Shinyanga 997 48 3 1,048 714 20 3 737 1,711 68 6 1,785
Tabora 775 24 0 799 1,209 10 0 1,219 1,984 34 0 2,018
Tanga 666 19 0 685 849 7 0 856 1,515 26 0 1,541
Jumla 16,048 908 258 17,214 16,167 335 91 16,593 32,215 1,243 349 33,807
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
69
Jedwali Na. 2: Idadi ya Wahalifu Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Jinsi na Aina ya Uhalifu Tanzania Bara, 2014
Mkoa
Mahabusu Wafungwa Jumla
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 734 42 0 776 457 9 1 467 1,191 51 1 1,243
Dar es Salaam 2,356 120 17 2,493 1,841 26 0 1,867 4,197 146 17 4,360
Dodoma 699 30 11 740 957 20 5 982 1,656 50 16 1,722
Iringa 623 45 14 682 457 11 0 468 1,080 56 14 1,150
Kagera 1,088 72 3 1,163 1,062 23 3 1,088 2,150 95 6 2,251
Kigoma 472 54 2 528 675 18 8 701 1,147 72 10 1,229
Kilimanjaro 597 45 0 642 850 17 0 867 1,447 62 0 1,509
Lindi 190 8 0 198 210 2 0 212 400 10 0 410
Manyara 465 25 0 490 517 10 0 527 982 35 0 1,017
Mara 1,125 87 14 1,226 798 19 5 822 1,923 106 19 2,048
Mbeya 921 53 1 975 852 21 0 873 1,773 74 1 1,848
Morogoro 685 33 9 727 919 42 31 992 1,604 75 40 1,719
Mtwara 280 18 0 298 463 6 1 470 743 24 1 768
Mwanza 1,550 110 57 1,717 1,608 27 25 1,660 3,158 137 82 3,377
Pwani 298 12 0 310 627 3 0 630 925 15 0 940
Ruvuma 245 15 0 260 435 8 0 443 680 23 0 703
Rukwa 458 32 5 495 433 8 9 450 891 40 14 945
Singida 507 45 2 554 306 10 0 316 813 55 2 870
Shinyanga 1,135 52 24 1,211 741 33 0 774 1,876 85 24 1,985
Tabora 795 34 0 829 1,292 9 0 1,301 2,087 43 0 2,130
Tanga 550 48 14 612 657 24 0 681 1,207 72 14 1,293
Jumla 15,773 980 173 16,926 16,157 346 88 16,591 31,930 1,326 261 33,517
Chanzo:Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
70
Jedwali Na. 3: Idadi ya Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Umri na Jinsi, Tanzania Bara, 2013
Mkoa Miaka 15 - 20 Miaka 21 - 25 Miaka 26 - 50 Zaidi ya miaka 50 Jumla
kuu Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 67 4 0 71 116 1 0 117 104 1 0 105 208 2 0 210 503
Dar es Salaam 631 9 1 641 154 9 0 163 812 4 0 816 303 7 0 310 1,930
Dodoma 160 2 8 170 193 1 0 194 619 18 0 637 106 1 0 107 1,108
Iringa 122 0 0 122 147 3 0 150 93 7 0 100 50 4 0 54 426
Kagera 154 8 1 163 236 8 0 244 445 5 0 450 122 8 0 130 987
Kigoma 191 2 20 213 212 10 0 222 315 13 0 328 94 1 0 95 858
Kilimanjaro 79 0 0 79 341 4 0 345 212 12 0 224 38 0 0 38 686
Lindi 91 0 5 96 71 3 0 74 173 1 0 174 22 0 0 22 366
Manyara 60 1 - 61 72 3 0 75 197 7 0 204 104 0 0 104 444
Mara 200 1 4 205 82 7 0 89 205 1 0 206 141 0 0 141 641
Mbeya 92 2 6 100 187 4 0 191 311 13 0 324 445 1 0 446 1,061
Morogoro 180 7 31 218 272 4 0 276 363 20 0 383 97 3 0 100 977
Mtwara 138 4 - 142 49 2 0 51 188 4 0 192 41 - 0 41 426
Mwanza 508 6 7 521 358 9 0 367 667 20 0 687 215 7 0 222 1,797
Pwani 82 0 0 82 153 2 0 155 159 3 0 162 19 0 0 19 418
Ruvuma 54 0 0 54 105 1 0 106 101 - 0 101 21 0 0 21 282
Rukwa 99 1 2 102 50 1 0 51 308 4 0 312 24 0 0 24 489
Singida 52 1 3 56 113 5 0 118 168 5 0 173 34 1 0 35 382
Shinyanga 163 3 3 169 280 7 0 287 212 9 0 221 59 1 0 60 737
Tabora 271 3 - 274 218 3 0 221 637 4 0 641 83 0 0 83 1,219
Tanga 80 1 - 81 323 4 0 327 334 2 0 336 112 0 0 112 856
Jumla 3,474 55 91 3,620 3,732 91 0 3,823 6,623 153 0 6,776 2,338 36 0 2,374 16,593
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
71
Jedwali Na. 4: Idadi ya Wafungwa Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Umri na Jinsi, Tanzania Bara, 2014
Mikoa
Miaka 15 - 20 Miaka 21 - 25 Miaka 26 - 50 Zaidi ya miaka 50 Jumla
kuu Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 99 1 1 101 153 0 0 153 115 4 0 119 90 4 0 94 467
Dar es Salaam 625 4 0 629 128 6 0 134 727 2 0 729 361 14 0 375 1,867
Dodoma 149 2 5 156 198 0 0 198 517 16 0 533 93 2 0 95 982
Iringa 145 2 0 147 198 6 0 204 91 3 0 94 23 0 0 23 468
Kagera 163 8 3 172 191 4 196 446 8 455 262 3 0 265 1,088
Kigoma 132 5 8 145 127 4 0 131 384 9 0 393 32 0 0 32 701
Kilimanjaro 87 2 0 89 429 8 0 437 310 5 0 315 24 2 0 26 867
Lindi 42 0 0 42 28 2 0 30 119 0 0 119 21 0 0 21 212
Manyara 32 1 0 33 203 3 0 206 248 5 0 253 34 1 0 35 527
Mara 310 5 5 320 48 12 0 60 317 2 0 319 123 0 0 123 822
Mbeya 120 6 0 126 147 4 0 151 338 11 0 349 247 0 0 247 873
Morogoro 127 8 31 166 351 5 0 356 340 29 0 369 101 0 0 101 992
Mtwara 142 1 1 144 50 1 0 51 216 4 0 220 55 0 0 55 470
Mwanza 402 2 25 429 326 7 0 333 671 15 0 686 209 3 0 212 1,660
Pwani 99 1 0 100 305 0 0 305 169 2 0 171 54 0 0 54 630
Ruvuma 129 2 0 131 133 1 0 134 140 5 0 145 33 0 0 33 443
Rukwa 58 2 9 69 110 2 0 112 241 4 0 245 24 0 0 24 450
Singida 42 3 0 45 95 3 0 98 150 4 0 154 19 0 0 19 316
Shinyanga 193 7 0 200 186 9 0 195 290 14 0 304 72 3 0 75 774
Tabora 292 1 0 293 392 4 0 396 520 4 0 524 88 0 0 88 1,301
Tanga 64 3 0 67 288 4 0 292 231 15 0 246 74 2 0 76 681
Jumla 3,452 66 88 3,604 4,086 85 0 4,172 6,580 161 0 6,742 2,039 34 0 2,073 16,591
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
72
Jedwali Na. 5: Idadi ya Wafungwa wa Adhabu ya Kifo Waliobaki Magerezani kwa Mkoa, Jinsi na Hali ya Rufaa, Tanzania Bara, 2013 na 2014
Mkoa
2013 2014
Rufaa Zilizokataliwa
Rufaa ambazo
Hazijasikilizwa Jumla
Kuu
Rufaa Zilizokataliwa
Rufaa ambazo
Hazijasikilizwa Jumla
Kuu Me Ke Jumla Me Ke Jumla Me Ke Jumla Me Ke Jumla
Arusha 6 0 6 9 1 10 16 6 0 6 7 1 8 14
Dar es salaam 40 0 40 13 0 13 53 40 0 40 34 3 37 77
Dodoma 55 5 60 46 3 49 109 55 1 56 41 4 45 101
Iringa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kagera 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kigoma 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kilimanjaro 0 0 0 2 0 2 2 0 0 0 2 0 2 2
Lindi 1 0 1 6 0 6 7 1 0 1 1 0 1 2
Manyara 0 0 0 1 0 1 1 0 0 0 0 0 0 0
Mara 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Mbeya 5 1 6 23 2 25 31 7 1 8 17 1 18 26
Morogoro 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Mtwara 6 0 6 3 0 3 9 5 0 5 6 0 6 11
Mwanza 26 3 29 30 2 32 61 26 2 28 48 2 50 78
Pwani 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Ruvuma 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Rukwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Singida 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Shinyanga 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 2 2
Tabora 25 25 8 0 8 33 29 0 29 19 0 19 48
Tanga 60 0 60 9 0 9 69 39 0 39 10 0 10 49
Jumla 224 9 233 150 8 158 391 208 4 212 187 11 198 410
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
73
Jedwali Na. 6: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya Kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara, 2013
Aina ya Kosa Chini ya
Miezi 6
Miezi 6 Hadi
Mwaka 1
Zaidi ya
Mwaka 1
Hadi 3
Zaidi ya
Miaka 3
Hadi 5
Zaidi ya
Miaka 5
Hadi 10
Zaidi ya
Miaka 10
Hadi 15
Zaidi ya
Miaka15
Kifungo
cha Maisha
Hukumu
ya Kifo Jumla
Mauaji 0 0 9 11 9 24 13 127 390 583
Mauaji (adhabu ya kifo
kifungo) 0 0 0 6 9 24 31 50 0 120
Kuua bila kukusudia 13 20 156 192 291 95 72 27 0 866
Kujaribu kuua 5 24 33 19 38 16 39 1 0 175
Unyang’anyi 39 102 96 185 246 592 1,097 13 1 2,371
Wizi 599 904 920 795 429 109 127 0 0 3,883
Kuvunja nyumba 125 433 596 564 365 64 63 0 0 2,210
Kupatikana na dawa za
kulevya 23 105 99 142 92 29 45 0 0 535
Kupatikana na nyara za serikali 39 56 64 43 56 32 85 0 0 375
Makosa ya kujamiiana 7 11 40 44 32 21 529 230 0 914
Kupatikana na bunduki na
risasi 13 16 32 35 85 97 181 0 0 459
Kujeruhi 219 322 286 124 111 13 0 0 0 1,075
Kuchoma nyumba moto 8 32 16 22 15 14 3 9 0 119
Makosa ya rushwa 0 11 1 3 8 2 0 0 0 25
Kupatikana na pombe ya
moshi 61 68 28 12 2 0 0 0 0 171
Uzembe na uzururaji 19 18 11 2 3 102 0 0 0 155
Makosa mengineyo 406 553 881 286 217 11 112 0 0 2,466
Jumla 1,576 2,675 3,268 2,485 2,008 1,245 2,397 457 391 16,502
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
74
Jedwali Na. 7: Idadi ya Wafungwa Watu Wazima waliokuwepo Magerezani kwa Aina ya kosa na Urefu wa Kifungo, Tanzania Bara, 2014
Aina ya Kosa Chini ya
miezi 6
Miezi 6
hadi
mwaka 1
Zaidi ya
mwaka 1-3
Zaidi ya
miaka 3-5
Zaidi ya
miaka 5-
10
Zaidi ya
miaka 10-15
Zaidi ya
miaka 15
Kifungo
cha maisha
Hukumu
ya kifo Jumla
Mauaji 58 38 69 2 18 9 5 303 402 904
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa
kifungo 0 0 0 0 4 1 0 0 8 13
Kuua bila kukusudia 14 38 166 24 219 86 44 2 0 593
Kujaribu kuua 36 42 23 2 19 8 1 1 0 132
Unyang’anyi 521 264 233 120 171 91 341 2 0 1,743
Wizi 1,319 1,229 1,429 22 338 25 48 3 0 4,413
Kuvunja nyumba 399 610 540 14 133 45 17 0 0 1,758
Kupatikana na dawa za kulevya 68 156 149 78 20 8 16 0 0 495
Kupatikana na nyara za serikali 90 140 213 2 46 11 180 6 0 688
Makosa ya kujamiiana 13 11 30 6 36 3 277 447 0 823
Kupatikana na bunduki na risasi 13 16 56 0 38 12 10 1 0 146
Kujeruhi 456 731 438 16 57 5 6 2 0 1,711
Kuchoma moto nyumba 22 65 50 0 7 21 2 3 0 170
Makosa ya rushwa 3 10 24 0 1 0 0 0 0 38
Kupatikana na pombe ya moshi 83 141 41 2 0 0 0 0 0 267
Uzembe na uzururaji 75 48 13 0 38 0 0 0 0 174
Makosa mengineyo 470 510 920 301 213 15 6 0 0 2,435
Jumla 3,640 4,049 4,394 589 1,358 340 953 770 410 16,503
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
75
Jedwali Na. 8: Idadi ya Mahabusu Watu Wazima waliokuwepo Magerezani, Kusubiri Kesi kwa Aina ya kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania Bara,
2013
Aina ya Kosa Chini ya
Miezi 2
Miezi Miwili
Hadi 6
Zaidi ya Miezi 6
Hadi Miaka 2
Zaidi ya
Miaka 2-4
Zaidi ya
Miaka 4-6
Zaidi ya
Miaka 6-8
Zaidi ya
Miaka 8-10
Zaidi ya
Miaka 10 Jumla
Mauaji 849 951 1,582 873 268 100 16 3 4,642
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kujaribu kuua 742 347 594 78 3 2 0 0 1,766
Unyang’anyi 629 726 772 93 28 0 0 0 2,248
Wizi 862 606 233 60 11 0 0 0 1,772
Kuvunja nyumba 377 318 156 40 14 0 0 0 905
Kupatikana na dawa za kulevya 173 203 112 20 7 0 0 0 515
Kuatikana na nyara za serikali 147 137 125 26 0 0 0 0 435
Makosa ya kujamiiana 435 250 137 44 8 0 0 0 874
Kupatikana na silaha na risasi 66 37 20 18 0 0 0 0 141
Kujeruhi 300 165 66 50 0 0 0 0 581
Kuchoma nyumba moto 67 41 3 6 0 0 0 0 117
Makosa ya rushwa 63 25 16 0 0 0 0 0 104
Kupatikana na pombe ya moshi 530 220 108 37 1 2 0 0 898
Uzembe na uzururaji 72 52 31 0 0 0 0 0 155
Makosa mengineyo 1058 516 205 10 14 0 0 0 1,803
Jumla 6,370 4,594 4,160 1,355 354 104 16 3 16,956
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
76
Jedwali Na. 9: Idadi ya Mahabusu Watu Wazima Waliokuwepo Magerezani, Kusubiri Kesi kwa Aina ya Kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania Bara,
2014
Aina ya Kosa Chini ya
Miezi 2
Miezi Miwili
Hadi 6
Zaidi ya Miezi 6
Hadi Miaka 2
Zaidi ya
Miaka 2-4
Zaidi ya
Miaka 4-6
Zaidi ya
Miaka 6-8
Zaidi ya
Miaka 8-10
Zaidi ya
Miaka 10 Jumla
Mauaji 803 795 914 859 280 108 26 4 3,789
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kujaribu kuua 874 0 298 170 23 5 4 0 1,374
Unyang’anyi 529 775 561 116 20 9 4 0 2,014
Wizi 895 588 373 81 10 7 0 0 1,954
Kuvunja nyumba 714 331 195 47 14 0 0 0 1,301
Kupatikana na dawa za kulevya 264 136 179 57 6 1 0 0 643
Kupatikana na nyara za serikali 147 136 188 18 3 0 0 0 492
Makosa ya kujamiiana 316 141 128 24 21 1 0 0 631
Kupatikana na bunduki na risasi 82 69 42 2 2 0 1 0 198
Kujeruhi 346 225 81 26 0 0 0 0 678
Kuchoma nyumba moto 121 53 25 8 2 0 0 0 209
Makosa ya rushwa 61 21 14 3 0 0 0 0 99
Kupatikana na pombe ya moshi 438 272 181 29 6 0 0 0 926
Uzembe na uzururaji 27 8 3 0 0 0 0 0 38
Makosa mengineyo 690 621 482 72 1 5 0 0 1,871
Jumla 6,307 4,171 3,664 1,512 388 136 35 4 16,217
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
77
Jedwali Na. 10: Idadi ya Mahabusu Vijana Waliokuwepo Magerezani, Kusubiri Kesi kwa Aina ya Kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania, Bara, 2013
Aina ya Kosa Chini ya
miezi 2
Miezi miwili
hadi 6
Zaidi ya miezi 6
hadi miaka 2
Zaidi ya
miaka 2-4
Zaidi ya
miaka 4-6
Zaidi ya
miaka 6-8
Zaidi ya
miaka 8-10 Zaidi ya 10 Jumla
Mauaji 32 7 15 3 0 0 0 0 57
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kujaribu kuua 7 1 0 0 0 0 0 0 8
Unyang’anyi 10 4 16 0 0 0 0 0 30
Wizi 23 10 1 0 0 0 0 0 34
Kuvunja nyumba 11 8 0 0 0 0 0 0 19
Kupatikana na dawa za kulevya 4 5 3 0 0 0 0 0 12
Kupatikana na nyara za serikali 9 8 0 0 0 0 0 0 17
Makosa wa kujamiiana 6 3 5 0 0 0 0 0 14
Kupatikana na bunduki na risasi 2 0 0 0 0 0 0 0 2
Kujeruhi 6 2 0 0 0 0 0 0 8
Kuchoma nyumba moto 0 3 1 0 0 0 0 0 4
Makosa ya hushwa 1 1 0 0 0 0 0 0 2
Kupatikana na pombe ya moshi 5 6 21 0 0 0 0 0 32
Uzembe ne uzururaji 4 1 0 0 0 0 0 0 5
Makosa mengineyo 7 4 3 0 0 0 0 0 14
Jumla 127 63 65 3 0 0 0 0 258
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
78
Jedwali Na. 11: Idadi ya Mahabusu Vijana Waliokuwepo Magereani, Kusubiri Kesi kwa Aina ya kosa na Muda Waliokaa Gerezani, Tanzania Bara, 2014
Aina ya Kosa Chini ya
miezi 2
Miezi 2
hadi 6
Zaidi ya miezi
6 hadi miaka 2
Zaidi ya
miaka 2 - 4
Zaidi ya
miaka 4 - 6
Zaidi ya
miaka 6 - 8
Zaidi ya
miaka 8 - 10
Zaidi ya
miaka 10 Jumla
Mauaji 26 15 4 3 1 0 0 0 49
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kujaribu kuua 19 2 0 0 0 0 0 0 21
Unyang’anyi 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Wizi 17 6 2 0 0 0 0 0 25
Kuvuja nyumba 3 0 0 0 0 0 0 0 3
Kupatikana na dawa za kulevya 5 1 0 0 0 0 0 0 6
Kupatikana na nyara za serikali 2 0 1 0 0 0 0 0 3
Makosa ya kujamiiana 18 1 1 0 0 0 0 0 20
Kupatikana na bunduki na risasi 1 0 0 0 0 0 0 0 1
Kujeruhi 2 1 0 0 0 0 0 0 3
Kuchoma moto nyumba 4 0 0 0 0 0 0 0 4
Makosa ya rushwa 1 0 0 0 0 0 0 0 1
Kupatiikana na pombe ya moshi 24 0 0 0 0 0 0 0 24
Uzembe na uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa mengineyo 8 4 1 0 0 0 0 0 13
Jumla 130 30 9 3 1 0 0 0 173
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
79
Jedwali Na. 12: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi Walizotoka na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013
Aina ya Kosa
Nchi Walizotoka
Jumla
Bu
run
di
Co
ng
o
DR
C
Eth
iop
ia
Ira
n
Ken
ya
Nig
eria
Rw
an
da
So
ma
lia
Ug
an
da
Mauaji 2 0 0 40 0 1 0 0 0 0 43
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 1
Kuua bila kukusudia 7 0 1 0 0 0 0 4 0 1 13
Kujaribu kuua 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Unyang’anyi 50 7 0 0 0 5 0 0 0 0 62
Wizi 43 0 1 0 0 0 0 8 0 9 61
Kuvunja nyumba 18 0 0 0 0 0 0 2 0 0 20
Kupatikana na dawa Za kulevya 3 0 0 0 1 0 0 1 0 0 5
Kupatikana na nyara za serikali 2 0 0 0 0 0 0 4 0 0 6
Makosa ya kujamiiana 34 1 1 0 0 0 0 2 0 2 40
Kupatikana na bunduki na risasi 37 0 0 0 0 0 0 0 0 0 37
Kujeruhi 2 0 0 0 0 0 0 14 0 1 17
Kuchoma nyumba moto 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa ya rushwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na pombe ya moshi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Uzembe na uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa mengineyo 368 4 5 620 0 4 1 38 5 9 1,054
Jumla 566 12 8 660 1 11 1 73 5 22 1,359
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
80
Jedwali Na. 13: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi Walizotoka na Aina yaKosa, Tanzania Bara, 2014
Aina ya Kosa
Nchi Walizotoka
Jumla
Bu
run
di
Ch
ina
Co
ngo
DR
C
Eth
iop
ia
Gre
ece
Ho
ng
Kon
g
Ind
ia
Ira
n
Ken
ya
Lib
eria
Ma
law
i
Rw
an
da
S.A
Ug
an
da
Za
mb
ia
Mauaji 0 0 0 1 0 1 0 1 0 3 0 0 2 0 0 0 8
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa
kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 4 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 8 0 1 0 14
Kujaribu kuua 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Unyang’anyi 37 0 1 7 0 0 0 0 0 12 0 1 6 0 3 0 67
Wizi 46 0 2 0 0 0 0 0 0 1 0 0 8 1 9 0 67
Kuvunja nyumba 2 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 12 0 16
Kupatikana na madawa ya kulevya 1 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 1 0 0 0 3
Kupatikana na nyara za serikali 0 1 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 1 0 3
Makosa ya kujamiiana 16 0 0 1 0 0 0 0 0 1 0 0 1 0 4 0 23
Kupatikana na bunduki na risasi 13 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 5 0 20
Kujeruhi 1 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 1 0 5 0 8
Kuchoma nyumba moto 4 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 4
Makosa ya rushwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na pombe ya moshi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 2
Uzembe na uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa mengineyo 336 0 12 0 198 0 30 1 0 5 1 0 46 0 7 2 638
Jumla 460 1 17 9 198 1 30 2 1 26 1 1 76 1 47 2 873
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
81
Jedwali Na. 14: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi Walizotoka na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013
Aina ya Kosa
Bu
lga
ria
Bu
ru
nd
i
Ca
mero
on
Ch
ina
Co
ng
o B
ra
za
vil
le
DR
C
Eth
iop
ia
Gh
an
a
Gre
ece
Gu
inea
Ind
ia
Ind
on
esi
a
Ira
n
Irela
nd
Ken
ya
D.P
.R o
f K
ore
a
Lib
eria
Lit
hu
an
ia
Nig
eria
Pa
kis
tan
Gu
inea
Bis
sau
Rw
an
da
Sie
rra
Leo
ne
Vie
t N
am
So
ma
lia
Afr
ika
Ku
sin
i
To
ng
a
Ug
an
da
Uin
gereza
Ju
mla
Mauaji 0 25 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 24 0 0 0 0 0 0 61 0 0 0 0 0 2 0 112
Mauaji (adhabu ya
kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila
kukusudia 0 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3
Kujaribu kuua 0 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3
Unyang’anyi 0 6 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 5 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 11
Wizi 1 73 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 3 0 0 1 1 0 1 0 83
Kuvunja nyumba 0 91 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 6 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 98
Kupatikana na dawa
za kulevya 0 0 0 0 0 0 0 1 0 1 0 1 2 1 5 1 3 1 19 1 1 0 1 0 0 3 1 3 1 46
Kupatikana na
nyara za serikali 0 3 0 3 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 7 0 1 0 0 0 0 0 15
Makosa ya
kujamiiana 0 1 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 34 0 37
Kupatikana na
bunduki na risasi 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 5
Kujeruhi 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 21 0 0 0 0 0 0 0 22
Kuchoma moto
nyumba 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa ya ruswa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na
pombe ya moshi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Uzembe na
uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 6 0 0 0 0 0 0 0 6
Makosa mengineyo 0 72 1 0 2 3 221 0 1 0 0 0 0 0 3 0 0 0 0 0 0 60 0 0 1 0 0 36 0 400
Jumla 1 280 1 3 2 4 222 1 1 1 1 1 2 1 48 1 3 1 19 1 1 159 1 1 2 4 1 77 1 841
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
82
Jedwali Na. 15: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliokuwepo Magerezani kwa Nchi Walizotoka na Ainan ya Kosa, Tanzania Bara, 2014
Aina ya
Kosa
Bu
ru
nd
i
Ch
ina
Co
lom
bia
Co
ngo
Bra
zavil
le
DR
C
Eth
iop
ia
Ger
ma
ny
Gh
an
a
Gre
ece
Gu
inea
Ho
ng K
on
g
Ind
ia
Ind
on
esi
a
Ira
n
Irela
nd
Ken
ya
Lib
eria
Ma
law
i
Mo
zam
biq
ue
Nig
eria
Pa
kis
tan
Gu
inea
0B
issa
u
Rw
an
da
Vie
t N
am
So
ma
lia
Afr
ika
Ku
sin
i
Zim
ba
bw
e
Ug
an
da
Uin
ger
eza
Ma
rek
an
i
Zam
bia
Ju
mla
Mauaji 67 0 0 4 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 6 0 0 0 0 0 0 5 0 1 0 0 0 0 0 0 84
Mauaji
(adhabu ya
kifo kuwa
kifungo)
0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila
kukusudia 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kujaribu
kuua 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 12 0 0 0 0 0 0 0 0 12
Unyang’any
i 32 0 0 9 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 7 0 0 0 49
wizi 45 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 45
Kuvunja
nyumba 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 11 0 0 0 11
Kupatikana
na dawa za
kulevya
0 0 1 0 0 0 0 1 1 1 0 0 1 20 1 4 2 0 1 21 10 1 0 0 0 1 0 2 1 1 0 70
Kupatikana
na nyara za
serikali
0 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 4 1 0 0 0 0 0 0 0 8
Makosa ya
kujamiana 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 12 0 0 0 13
Kupatikana
na bunduki
na risasi
4 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 6
Kujeruhi 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 36 0 0 0 38
Kuchoma
moto 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
83
Aina ya
Kosa B
uru
nd
i
Ch
ina
Co
lom
bia
Co
ngo
Bra
zavil
le
DR
C
Eth
iop
ia
Ger
ma
ny
Gh
an
a
Gre
ece
Gu
inea
Ho
ng K
on
g
Ind
ia
Ind
on
esi
a
Ira
n
Irela
nd
Ken
ya
Lib
eria
Ma
law
i
Mo
zam
biq
ue
Nig
eria
Pa
kis
tan
Gu
inea
0B
issa
u
Rw
an
da
Vie
t N
am
So
ma
lia
Afr
ika
Ku
sin
i
Zim
ba
bw
e
Ug
an
da
Uin
ger
eza
Ma
rek
an
i
Zam
bia
Ju
mla
nyumba
Makosa ya
rushwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kupatikana
na pombe
ya moshi
0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 4 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 4
Uzembe na
uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa
mengineyo 95 0 0 5 2 26 1 0 0 0 29 1 0 0 0 8 0 1 0 2 0 0 61 0 11 0 0 0 0 0 1 243
Jumla 244 3 1 20 3 26 1 1 1 1 29 1 1 20 1 24 2 1 1 23 10 1 82 1 12 1 1 68 1 1 1 583
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
84
Jedwali Na. 16: Idadi ya Wahalifu Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Mkoa, Aina ya Muharifu na Jinsi, Tanzania Bara, 2013
Mkoa
Mahabusu Wafungwa Jumla
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V jumla
Arusha 3,540 243 0 3,783 542 40 0 582 4,082 283 0 4,365
Dar es Salaam 11,751 750 111 12,612 1,716 154 2 1,872 13,467 904 113 14,484
Dodoma 4,254 321 21 4,596 1,000 71 10 1,081 5,254 392 31 5,677
Iringa 3,187 230 22 3,439 551 39 0 590 3,738 269 22 4,029
Kagera 6,270 550 13 6,833 1,215 85 11 1,311 7,485 635 24 8,144
Kigoma 3,264 337 160 3,761 1,237 99 19 1,355 4,501 436 179 5,116
Kilimanjaro 4,399 419 27 4,845 904 55 12 971 5,303 474 39 5,816
Lindi 1,440 89 12 1,541 582 19 10 611 2,022 108 22 2,152
Manyara 3,302 290 0 3,592 712 51 0 763 4,014 341 0 4,355
Mara 6,935 608 111 7,654 1,035 61 26 1,122 7,970 669 137 8,776
Mbeya 5,102 526 6 5,634 1,172 90 24 1,286 6,274 616 30 6,920
Morogoro 3,226 228 234 3,688 1,220 59 108 1,387 4,446 287 342 5,075
Mtwara 2,440 165 1 2,606 430 26 0 456 2,870 191 1 3,062
Mwanza 9,865 819 247 10,931 1,746 82 60 1,888 11,611 901 307 12,819
Pwani 2,188 49 0 2,237 725 22 6 753 2,913 71 6 2,990
Ruvuma 2,035 122 12 2,169 780 60 4 844 2,815 182 16 3,013
Rukwa 2,387 186 44 2,617 671 38 9 718 3,058 224 53 3,335
Singida 3,193 233 12 3,438 680 44 5 729 3,873 277 17 4,167
Shinyanga 6,816 476 170 7,462 1,364 75 22 1,461 8,180 551 192 8,923
Tabora 3,426 169 0 3,595 760 30 4 794 4,186 199 4 4,389
Tanga 4,669 290 33 4,992 1,255 56 1 1,312 5,924 346 34 6,304
Jumla 93,689 7,100 1,236 102,025 20,297 1,256 333 21,886 114 8,356 1,569 123,911
Chanzo:Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
85
Jedwali Na. 17: Idadi ya Wahalifu Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Mkoa, Aina ya Muharifu na Jinsi, Tanzania Bara, 2014
Mkoa
Mahabusu Wafungwa Jumla
Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla Me Ke V Jumla
Arusha 3,714 305 0 4,019 524 55 1 580 4,238 360 1 4,599
Dar es
Salaam 12,742 1,251 213 14,206 1,156 132 1 1,289 13,898 1,383 214 15,495
Dodoma 4,022 328 40 4,390 889 72 13 974 4,911 400 53 5,364
Iringa 3,192 291 28 3,511 739 33 0 772 3,931 324 28 4,283
Kagera 6,531 438 18 6,987 1,594 108 29 1,731 8,125 546 47 8,718
Kigoma 3,038 311 147 3,496 1,264 55 10 1,329 4,302 366 157 4,825
Kilimanjaro 4,121 361 28 4,510 887 64 7 958 5,008 425 35 5,468
Lindi 1,254 79 12 1,345 494 22 3 519 1,748 101 15 1,864
Manyara 2,799 234 0 3,033 832 53 0 885 3,631 287 0 3,918
Mara 6,107 596 266 6,969 1,020 93 32 1,145 7,127 689 298 8,114
Mbeya 5,798 617 5 6,420 1,479 95 22 1,596 7,277 712 27 8,016
Morogoro 2,844 228 210 3,282 1,100 65 71 1,236 3,944 293 281 4,518
Mtwara 1,951 150 0 2,101 548 29 4 581 2,499 179 4 2,682
Mwanza 9,260 728 433 10,421 1,688 110 169 1,967 10,948 838 602 12,388
Pwani 1,726 101 0 1,827 866 19 4 889 2,592 120 4 2,716
Ruvuma 2,099 119 2 2,220 581 44 2 627 2,680 163 4 2,847
Rukwa 2,572 219 33 2,824 695 30 18 743 3,267 249 51 3,567
Singida 3,021 270 30 3,321 570 44 10 624 3,591 314 40 3,945
Shinyanga 4,236 368 186 4,790 984 74 8 1,066 5,220 442 194 5,856
Tabora 2,892 130 0 3,022 795 31 2 828 3,687 161 2 3,850
Tanga 3,937 282 41 4,260 1,090 52 4 1,146 5,027 334 45 5,406
Jumla 87,856 7,406 1,692 96,954 19,795 1,280 410 21,485 107,651 8,686 2,102 118,439
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
86
Jedwali Na.18: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Nchi Walizotoka na Aina ya Kosa, Tanzania Bara,
2013
Aina ya Kosa
Bu
run
di
Co
ngo
DR
C
Eth
iop
ia
Ind
ia
Ken
ya
Ma
law
i
Nig
eria
Rw
an
da
So
ma
lia
Ug
an
da
Za
mb
ia
Ju
mla
Mauaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Mauaji (adhabu ya kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 1 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2
Kujaribu kuua 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Unyang’anyi 3 0 0 0 0 4 0 0 0 0 0 0 7
Wizi 5 0 0 0 0 4 0 1 1 0 2 0 13
Kuvunja nyumba 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1
Kupatikana na dawa za kulevya 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1
Kupatikana na nyara za serikali 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2
Makosa ya kujamiiana 1 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3
Kupatikana na bunduki na risasi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 5 0 0 5
Kujeruhi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuchoma moto nyumba 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa ya rushwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na pombe ya moshi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Uzembe na uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa mengineyo 686 11 19 1,017 2 16 1 0 38 6 5 1 1,802
Jumla 700 11 22 1,017 2 24 1 1 39 11 7 1 1,836
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
87
Jedwali Na.19: Idadi ya Wafungwa Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Kutoka Mahakamani kwa Nchi Walizotoka na Aina ya Kosa, Tanzania Bara,
2014
Aina ya Kosa
Bu
run
di
Ch
ina
Co
ngo
DR
C
Eth
iop
ia
Ho
ng
Kon
g
Ind
ia
Ken
ya
Lib
eria
Nig
eria
Rw
an
da
So
ma
lia
Afr
ika
ya
Ku
sin
i
Su
dan
Utu
ruk
i
Ug
an
da
Za
mb
ia
Jumla
Mauaji 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 1 0 3
Mauaji (adhabu ya
kifo kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kujaribu kuua 0 0 4 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 4
Unyang’anyi 2 0 0 0 0 0 0 5 0 0 0 0 0 0 0 4 0 11
Wizi 16 0 3 0 0 0 0 1 0 0 5 0 0 0 0 9 1 35
Kuvunja nyumba 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 3
Kupatikana na dawa
za kulevya 3 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 4
Kupatikana na nyara
za serikali 0 1 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3
Makosa ya kujamiiana 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3 0 0 0 0 0 0 6
Kupatikana na
bunduki na risasi 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3
Kujeruhi 6 0 2 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 10
Kuchoma moto
nyumba 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 2
Makosa ya rushwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kupatikana na pombe
ya moshi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Uzembe na uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 1
Makosa mengineyo 1,042 0 40 3 664 61 1 16 5 7 59 2 1 2 1 8 2 1,914
Jumla 1,076 1 51 3 664 61 1 29 5 7 69 2 1 2 1 23 3 1,999
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
88
Jedwali Na. 20: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Toka Mahakamani kwa Nchi na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2013
Aina ya Kosa
Ba
ng
lad
esh
Bu
lga
ria
Bu
run
di
Ca
mer
oon
Ch
ina
Co
ngo
DR
C
Eth
iop
ia
Ug
irik
i
Ind
ia
Ken
ya
Lib
eria
Ma
dag
asc
ar
Ma
law
i
Msu
mb
iji
Nig
eria
Pa
kis
tan
Rw
an
da
Vie
tna
m
So
ma
lia
Ug
an
da
Uin
ger
eza
Ju
mla
Mauaji 0 0 12 0 0 0 1 1 0 0 17 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 31
Mauaji (adhabu ya kifo
kuwa kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila kukusudia 0 0 0 0 0 0 5 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 6
Kujaribu kuua 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 1
Unyang’anyi 0 0 19 0 0 0 0 0 0 1 20 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 40
Wizi 0 1 18 0 0 0 3 1 0 0 14 0 0 2 1 0 0 28 0 2 3 0 73
Kuvunja nyumba 0 0 5 0 0 0 0 0 0 0 5 0 0 0 0 0 0 5 0 0 1 0 16
Kupatikana na dawa za
kulevya 0 0 5 0 0 1 0 0 0 0 6 1 0 1 0 4 0 0 0 0 0 0 18
Kupatikana na nyara za
serikali 0 0 4 0 1 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 4 0 1 0 0 1 12
Makosa ya kujamiiana 0 0 0 0 0 0 11 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 12
Kupatikana na bunduki na
risasi 0 0 3 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 5
Kujeruhi 0 0 11 0 0 1 2 0 1 1 1 0 0 0 0 0 0 4 0 0 3 0 24
Kuchoma moto nyumba 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 2
Makosa ya rushwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2
Kupatikana na pombe ya
moshi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1
Uzembe na uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Makosa mengineyo 3 0 489 1 0 13 24 630 0 4 32 0 1 0 1 7 0 63 0 10 9 0 1,287
Jumla 3 1 566 1 1 15 46 632 1 8 101 1 1 3 2 11 4 103 1 12 16 1 1,530
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Taarifa ya Wafungwa na Mahabusu 2013 na 2014
89
Jedwali Na. 21: Idadi ya Mahabusu Wasio Raia Waliopokelewa Magerezani Toka Mahakamani kwa Nchi na Aina ya Kosa, Tanzania Bara, 2014
Aina ya Kosa A
ng
ola
Bu
ru
nd
i
Ca
mer
oo
n
Afr
ika
ya
Ka
ti
Ch
ina
Co
lom
bia
Co
ngo
Bra
zavil
le
DR
C
Eth
iop
ia
Fin
lan
d
Uje
ru
ma
ni
Gre
ece
Ho
ng K
on
g
Ind
ia
Ira
n
Ken
ya
Leb
an
on
Lib
eria
Ma
law
i
Msu
mb
iji
Nig
eria
Pa
kis
tan
Ro
ma
nia
Vie
tnam
So
ma
lia
Zim
ba
bw
e
Su
da
n
Ug
an
da
Ma
rek
an
i
Zam
bia
Ju
mla
Mauaji 0 34 0 0 0 0 7 0 0 0 0 0 0 0 0 6 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 47
Mauaji (adhabu ya
kifo kuwa
kifungo) 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kuua bila
kukusudia 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 1
Kujaribu kuua 0 14 0 0 0 0 9 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 23
Unyanag’anyi 0 3 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3
Wizi 0 22 0 0 0 0 12 0 0 0 0 0 0 4 0 4 0 0 1 0 0 1 0 0 0 1 0 9 0 1 55
Kuvunja
nyumba 0 11 0 0 0 0 10 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 24
Kupatikana na
dawa za
kulevya 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 1 0 2 18 8 0 1 0 0 9 9 0 0 0 0 0 0 1 0 50
Kupatikana na
nyara za
serikali 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 3
Makosa ya
kujamiiana 0 3 0 0 0 0 35 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 38
Kupatikana na bunduki au
risasii 0 21 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 2 0 0 0 0 0 0 0 0 0 23
kujeruhi 0 7 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 5 0 0 2 0 0 0 0 0 9 0 0 3 0 0 26
Kuchoma moto nyumba 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1
Makosa ya
rushwa 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 5 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 6
Kupatikana na
pombe ya
moshi 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Uzembe na
uzururaji 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 1
Makosa mengineyo 1 1,170 3 1 3 0 46 8 562 1 1 0 220 2 0 50 1 2 10 1 10 2 2 1 7 0 1 15 0 3 2,123
Jumla 1 1,287 3 1 3 1 119 8 562 1 1 1 220 9 18 82 1 3 13 1 21 12 2 1 16 2 1 29 1 4 2,424
Chanzo: Jeshi la Magereza Tanzania Bara
JESHI LA MAGEREZA TANZANIA BARA
DIRA:
Kuwa Jeshi la kurekebisha wahalifu lenye utaalamu wa hali ya juu linaloendeshwa katika kanuni na
viwango vilivyowekewa kitaifa na kimataifa.
DHIMA:
Kutekeleza wajibu ipasavyo katika kuimarisha ulinzi wa jamii kupitia usimamizi wa vifungo na
kuwasimamia wahalifu, huduma za mahabusu, programu na huduma zinazoshughulikia mahitaji ya
urekebishaji wa wahalifu na ushauri wa Sera kuhusu uzuiaji uhalifu na ushughulikiaji wa wahalifu.