19
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Taifa ya Takwimu Wizara ya Fedha Dar es Salaam Aprili, 2011

Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniaya Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango iliundwa kutokana na iliyokuwa Idara Kuu ya Takwimu (Central Bureau of Statistics) ambayo ilikuwa inafanya kazi chini

  • Upload
    others

  • View
    10

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

  • Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    Wizara ya Fedha

    Dar es Salaam

    Aprili, 2011

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    1

    Dibaji

    Ofisi ya Taifa ya Takwimu ilizinduliwa rasmi tarehe 26 Machi, 1999 kuwa Wakala wa Serikali

    (Executive Agency) kwa mujibu wa Sheria ya Wakala wa Serikali Na. 30 ya mwaka 1997.

    Kabla ya Uhuru, Takwimu zilikuwa zinakusanywa kwa kutumia sheria ya Takwimu ya mwaka

    1949 (Statistics Ordinance of 1949 – chapter 443). Sheria hii ilikuwa inatumika katika nchi za

    kikoloni za Afrika Mashariki ambazo ni Kenya, Uganda na Tanganyika. Kupitia sheria hii, Idara ya

    Takwimu ya Afrika Mashariki ilipewa mamlaka ya kuratibu mfumo (Muundo) wa takwimu za

    uchumi na jamii wa nchi tatu.

    Baada ya Uhuru mwaka 1961, mamlaka ya kukusanya, kuhifadhi na kuchapisha takwimu

    yalitokana na sheria ya Takwimu Na. 33 ya mwaka 1961; Sheria ambayo nayo ilifutwa kwa Sheria

    ya Takwimu Na. 1 ya mwaka 2002. Kutokana na Sheria hiyo, Ofisi ya Taifa ya Takwimu imepewa

    majukumu ya kuendesha, kusimamia na kuratibu shughuli zote za kitakwimu Tanzania Bara. Hivi

    sasa Ofisi ya Taifa ya Takwimu ipo kwenye mchakato wa kupata sheria mpya ikiwa ni sehemu ya

    Mpango Mkakati wa Kuboresha na kuimarisha Takwimu Tanzania.

    Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kamati ndogo iliyoundwa kutayarisha kitabu hiki.

    Dkt. Albina A. Chuwa

    MKURUGENZI MKUU

    OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    2

    1. Utangulizi

    Tanzania ilianza kuwa na Ofisi ya Takwimu mara tu baada ya Uhuru mwaka 1961. Kabla ya

    Uhuru Ofisi hii ilikuwa Nairobi, Kenya. Ofisi ya Takwimu ilipitia mabadiliko mengi hadi

    kufikia kuitwa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (National Bureau of Statistics - NBS) iliyozinduliwa

    rasmi tarehe 26 Machi, 1999 kuwa Wakala wa Serikali (Executive Agency) kwa mujibu wa

    Sheria ya Wakala wa Serikali Na. 30 ya mwaka 1997. Ofisi ya Taifa ya Takwimu ikiwa chini

    ya Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango iliundwa kutokana na iliyokuwa Idara Kuu ya Takwimu

    (Central Bureau of Statistics) ambayo ilikuwa inafanya kazi chini ya Sheria ya Takwimu Na.

    33 ya mwaka 1961 (Statistics Ordinance No. 33 of 1961), Sheria ambayo nayo ilifutwa kwa

    Sheria ya Takwimu Na. 1 ya mwaka 2002.

    2. Historia ya Takwimu Kabla ya Uhuru ( mwaka 1946 - 1961)

    Historia ya Takwimu Tanzania Bara ilianza toka wakati wa Wakoloni walipokuwa

    wakitutawala. Kwa bahati mbaya taarifa za wakati huo hazikuweza kuhifadhiwa na hivyo

    hatujui ni namna gani waliendesha shughuli za kitakwimu hapa nchini. Lakini kutokana na

    uwekaji wa kumbukumbu za kihistoria kama nyingine zilivyo, hili limekuwa ni pengo kubwa

    ambalo linahitaji kuzibwa. Kitengo cha Takwimu kilianzishwa mwaka 1946 chini ya “East

    African Governors‟ Conference” na ofisi yake ilikuwa na makao yake huko Nairobi, Kenya.

    Katika kipindi hicho takwimu zilikuwa zikikusanywa na wataalam kutoka Nairobi na

    uchambuzi wake ulifanyika huko huko. Baada ya kuanzishwa kwa “East African High

    Commission”, kitengo hiki kilibadilishwa jina na kuitwa “East African Statistical Department”.

    Idara hii ilikuwa inawajibika kwa kazi zifuatazo:

    Kuhakikisha wanatoa machapisho ya kitakwimu kama Serikali za Kikoloni za

    Wajerumani na Waingereza walivyokuwa wanatoa siku za nyuma,

    Kufanya uchambuzi wa matokeo ya Sensa na tafiti mbalimbali ambazo ziliandaliwa na

    „East African Statistical Department‟, na

    Kuandaa mfumo wa takwimu.

    Ili kuhakikisha shughuli za kitakwimu zinaendelea vizuri hapa Tanganyika, ilibidi kufunguliwa

    ofisi mwezi Januari, 1949 hapa Dar es Salaam, ingawa Ofisi ya Nairobi bado ilikuwepo.

    Mnamo mwaka 1954/55, Ofisi ya Dar es Salaam ilibadilishwa jina na kuitwa „Tanganyika

    Unit‟. Kuanzia wakati huo ofisi hii iliongezewa majukumu mbalimbali ya ukusanyaji na

    uchambuzi wa takwimu.

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    3

    3.0 Historia ya Takwimu Baada ya Uhuru

    3.1 Muundo wa Taasisi Ulivyobadilika Tangu Mwaka 1961

    Baada ya kupata Uhuru mwaka 1961, Kitengo hiki kilianzishwa chini ya Hazina kutoka

    iliyokuwa “Tanganyika Unit of East African Statistical Department, Nairobi” na kuwa

    „Statistics Division‟ chini ya Hazina na ofisi zake zilikuwa katika jengo hilohilo la Hazina.

    Baada ya mabadiliko hayo, Mtakwimu Mkuu wa kwanza alikuwa raia wa Uingereza

    aitwaye Nd. D.C. Upton, na aliongoza ofisi hii mpaka mwaka 1964. Hata hivyo, mnamo

    mwaka 1962, jina la ofisi hii lilibadilishwa na kuwa Maktaba ya Takwimu „Central

    Statistical Bureau (CSB)‟. Nd. C. Patel, ndiye aliyeiongoza CSB kuanzia mwaka 1964 hadi

    mwaka 1966 na baadae Nd. D.D. Johnson alikaimu kama Mtakwimu wa Serikali. Ofisi hii

    CSB ilibaki kuwa chini ya Hazina mpaka mwaka 1964, ambapo ilihamishiwa chini ya Ofisi

    ya Rais na Baraza la Mawaziri. Baada ya uhamisho huo, Ofisi hii ilihamia jengo la

    Mkaguzi Mkuu wa Serikali, Mtaa wa Kivukoni Front, ghorofa ya kwanza.

    Mnamo mwaka 1966, CSB ilibadilishwa jina na kuitwa „Central Bureau of Statistics

    (CBS)‟, na kuwa chini ya Wizara ya Uchumi na Mipango. Baada ya mabadiliko hayo Ofisi

    hii ilihama toka jengo la “Exchequer and Audit Department” na kuhamia jengo la Lehman

    ghorofa ya kwanza katika jengo la Clock Tower, kwenye makutano ya Samora Avenue na

    Mission Street. Dkt. G. Jacobsson, raia wa Sweden ndie alikuwa anaongoza CBS kama

    Mtakwimu wa Serikali.

    Mwaka 1967, kulifanyika sensa ya watu ya kwanza baada ya Uhuru kwa maana hiyo

    kulihitajika nafasi ya kutosha kwa ajili ya kazi ya uchambuzi wa Sensa ya Watu ya mwaka

    1967. Hivyo, Kitengo cha Sensa ya watu kilihamia Mtaa wa Mkwepu No. 9 na mpaka leo

    bado jengo hilo linatumika na Ofisi ya Taifa ya Takwimu.

    Kuanzia mwaka 1970 mpaka 1973, Ndugu Joshua J. Mpogolo

    alikuwa Msimamizi Mkuu wa tatu tokea tulipopata Uhuru mwaka

    1961 na kuwa na cheo kilichoitwa Mkurugenzi wa Takwimu. Yeye

    ndie alikuwa Mtanzania wa kwanza kushika nafasi hii. Mnamo

    mwaka 1974, jina la CBS lilibadilishwa na kuwa „Bureau of

    Statistics (BOS)‟.

    Ndugu Joshua J. Mpogolo

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    4

    Mwaka 1974/75 Wizara ya Uchumi na Mipango iliunganishwa na Wizara ya Fedha na BOS ikawa Idara

    katika Wizara ya Fedha na Mipango. Ofisi zake zilikuwa jengo la Casino, Mtaa wa Kivukoni na cheo cha

    Ndugu J. J. Mpogolo kilibadilishwa na kuwa Kamishina wa Takwimu. Kuanzia mwaka 1980 mpaka 1986,

    Idara hii ilihamishiwa tena Wizara ya Mipango na Uchumi baada ya mabadiliko ya wizara hizi kati ya

    mwaka 1986 – 1989 na baadae tena ikawa chini ya Wizara ya Fedha, Uchumi na Mipango.

    Kuanzia mwaka 1990, BOS ilikuwa chini ya Tume ya Mipango. Mnamo

    mwaka 1980 mpaka 1998, BOS iliendelea kutumia majengo ya Casino

    ambapo Ndugu Nathanael K. Mbalilaki alikuwa Msimamizi Mkuu wa

    nne kama Mtakwimu Mkuu wa Serikali.

    Mnamo Machi, 1999, baada ya BOS kuwa Wakala wa Serikali,

    jina la ofisi hii lilibadilishwa na kuwa Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    (NBS), ikiongozwa na Ndugu Cletus P.B. Mkai kama Mkurugenzi

    Mkuu kuanzia mwaka 1998. Ofisi zake ziliendelea kuwepo jengo

    la Casino na kuwa chini ya Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango.

    Ndugu C. P. B. Mkai alistaafu mwaka 2007 na Dkt. Albina A.

    Chuwa alichukua nafasi yake na kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi

    ya Taifa ya Takwimu.

    Dkt. Albina A. Chuwa amekuwa ni mwanamke wa kwanza

    kushika cheo hiki tangu kuanzishwa kwa Ofisi hii mwaka 1949.

    Kabla ya mwaka 1980, Idara zilikuwa zikiongozwa na Wakuu wa

    Idara bila kuwa na muundo maalum. Muundo rasmi ulianza

    mwaka 1980 wakati walipoteuliwa wakuu wa Idara na kuitwa

    Watakwimu Wakuu wa Serikali Wasaidizi (Assistant Government

    Statisticians). Muundo huu uliendelea kutumika hadi ilipoanzishwa

    Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).

    Ndugu Nathanael K. Mbalilaki

    Ndugu Cletus P. B. Mkai

    Dkt. Albina A. Chuwa

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    5

    Muundo mpya wa NBS ulipitishwa na Idara Kuu ya Utumishi mwaka 1999 wakati NBS

    inaanzishwa kuwa Wakala wa Serikali. Muundo huu una ngazi kuu tatu za uongozi kama

    ifuatavyo:

    i) Ngazi ya Kwanza ni MKURUGENZI MKUU,

    ii) Ngazi ya Pili ni WAKURUGENZI ambapo kuna Wakurugenzi wanne kama

    ifuatavyo;

    a) Mkurugenzi wa Fedha, Utawala na Masoko,

    b) Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii,

    c) Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi, na

    d) Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu.

    iii) Ngazi ya Tatu ni WAKUU WA IDARA (MAMENEJA). Wakati NBS inaanza kama

    Wakala ilikuwa na Idara 10 na baadae kufikia Idara 13 hadi sasa kama

    inavyoonyeshwa hapa chini:

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    6

    Idara ya Takwimu

    za Viwanda na Ujenzi

    Idara ya Takwimu

    za Biashara, Usafirishaji, Utalii na

    Uhamiaji

    Idara ya Teknolojia

    ya Habari na Masoko

    Idara ya Shughuli za Kitakwimu

    Idara ya Uratibu, Viwango na Mbinu za

    Kitakwimu

    Mkurugenzi Mkuu

    Idara ya Utumishi

    na Utawala

    Idara ya Takwimu

    za Ajira na Bei

    Kurugenzi ya Fedha Utawala, na Masoko

    Idara ya Takwimu za Kilimo

    MUUNDO WA UONGOZI WA NBS KWA SASA

    Idara ya Takwimu za Mazingira na

    Uchambuzi wa Takwimu

    Idara ya Takwimu za Kodi

    Idara ya Fedha

    Mkaguzi wa Ndani

    Kurugenzi ya Sensa ya Watu na Takwimu za

    Jamii

    Kurugenzi ya Takwimu

    za Uchumi

    Kurugenzi ya Uendeshaji Shughuli za Kitakwimu

    Idara ya Takwimu za Jamii

    Idara ya Takwimu za Pato la Taifa

    Mwanasheria

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    7

    MUUNDO WA UONGOZI WA NBS KWA SASA

    Dr. Albina Chuwa

    Mkurugenzi Mkuu

    WAKURUGENZI

    Stanley Mahembe

    Kurugenzi ya Fedha Utawala, na Masoko

    Ephraim Kwesigabo Kurugenzi ya Sensa ya

    Watu na Takwimu za Jamii

    Morrice Oyuke

    Kurugenzi ya Takwimu za Uchumi

    Radegunda Maro Kurugenzi ya Uendeshaji

    Shughuli za Kitakwimu

    MAMENEJA

    Lilian Karumna

    Idara ya Fedha

    Aldegunda Komba Idara ya Takwimu za Jamii

    Daniel Masolwa

    Kaimu Idara ya Takwimu za Pato la Taifa

    Ahmed Makbel Idara ya Uratibu, Viwango

    na Mbinu za Kitakwimu

    Gabriel G. Madembwe

    Idara ya Utumishi na

    Utawala

    Irenius Ruyobya

    Idara ya Takwimu

    za Ajira na Bei

    Said Aboud

    Idara ya Takwimu za Kilimo

    Wilfred Mwingira

    Idara ya Shughuli za Kitakwimu

    Mwanaidi Mahiza

    Idara ya Teknolojia ya

    Habari na Masoko

    Mathias Masuka Idara ya Takwimu

    za Kodi

    Joy Sawe

    Idara ya Takwimu za

    Viwanda na Ujenzi

    Valerian Tesha

    Idara ya Takwimu za Biashara, Uusafiri Usafirishaji, Utalii na Uhamiaji

    Sango Simba Idara ya Takwimu za Mazingira na

    Uchambuzi wa Takwimu

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    8

    3.2 Sheria za Kuendesha Ofisi ya Taifa ya Takwimu Zilizokuwepo Tangu Uhuru Hadi Sasa

    Kabla ya Uhuru, Takwimu zilikuwa zinakusanywa kwa kutumia sheria ya Takwimu ya mwaka

    1949 (Statistics Ordinance of 1949 – chapter 443). Sheria hii ilikuwa inatumika katika nchi za

    kikoloni za Afrika Mashariki ambazo ni Kenya, Uganda na Tanganyika. Kupitia sheria hii,

    Idara ya Takwimu ya Afrika Mashariki ilipewa mamlaka ya kuratibu mfumo (Muundo) wa

    takwimu za uchumi na jamii wa nchi tatu.

    Baada ya uhuru mwaka 1961, Mamlaka ya kukusanya, kuhifadhi na kuchapisha takwimu

    yalitokana na sheria ya Takwimu Na. 33 ya mwaka 1961. Kupitia sheria hii, Ofisi ilipewa

    majukumu yafuatayo;-

    (i) Kufanya sensa ya watu,

    (ii) Kukusanya, kuhifadhi, kuchambua na kuchapisha takwimu zinazohusiana na

    uchumi, jamii na utamaduni, na

    (iii) Kuratibu mfumo wa takwimu za kiuchumi na kijamii.

    Mwaka 1997, Serikali ilitunga sheria ya Wakala wa Serikali Namba 30 ya mwaka 1997. Lengo

    la Serikali lilikuwa ni kuziwezesha Wizara kuunda wakala zitakazotoa huduma kwa ufanisi

    zaidi kwa wateja wake na umma kwa ujumla kwa kutumia mbinu mpya za kiutendaji. Tarehe

    26 Machi 1999, Ofisi ya Taifa ya Takwimu ilizinduliwa rasmi kuwa Wakala wa Serikali.

    Baada ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu kuwa wakala, mchakato ulianza wa kutunga sheria mpya

    ya Takwimu Na. 1 ya mwaka 2002 ambayo iliifuta sheria ya Takwimu ya mwaka 1961.

    4. Majukumu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    Kutokana na Sheria ya Takwimu Namba 1 (Statistics Act) ya mwaka 2002, Ofisi ya Taifa ya

    Takwimu imepewa majukumu ya kuendesha, kusimamia na kuratibu shughuli zote za

    kitakwimu Tanzania Bara. Majukumu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu kama yalivyoainishwa

    kwenye kifungu cha 5(1) cha Sheria ya Takwimu, Na. 1 ya mwaka 2002 ni kama ifuatavyo:

    a. Kuendesha Sensa ya Watu na Makazi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

    b. Kuandaa mpango wa kitaifa wa takwimu kwa ajili ya utoaji wa takwimu rasmi za

    Serikali na kuuhuisha mara kwa mara,

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    9

    c. Kuandaa viwango vya kitakwimu na kuhakikisha vinatumika na wazalishaji wote wa

    takwimu rasmi nchini ili kuleta uwiano na ulinganifu wa takwimu zinazozalishwa ndani

    ya nchi na kimataifa,

    d. Kuratibu shughuli zote za kitakwimu nchini,

    e. Kukusanya na kusambaza takwimu na taarifa zinazohusiana nazo,

    f. Kuwa kitovu cha utunzaji wa takwimu zote rasmi katika nchi,

    g. Kuwasaidia watumiaji wa takwimu katika kupata takwimu za kimataifa,

    h. Kutoa huduma ya kitakwimu na msaada wa kitaalamu kwa asasi mbalimbali na umma

    kwa ujumla, na

    i. Kuwa kitovu cha rejea kwa Mashirika ya Kimataifa na makampuni ya kigeni

    yanayohitaji taarifa za kitakwimu kuhusu Tanzania.

    5. Sensa, Tafiti na Matukio Muhimu Yaliyofanyika Tangu Mwaka 1961

    Tangu baada ya Uhuru mwaka 1961 NBS imeweza kufanya sensa, tafiti na kushiriki katika

    warsha na mikutano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa. Mafanikio makubwa yalipatikana

    baada ya NBS kuanzishwa na kuweza kutoa takwimu na viashiria mbalimbali vya kiuchumi na

    kijamii vilivyoiwezesha Serikali kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo kitaifa. Sensa,

    tafiti na matukio hayo ni kama ifuatavyo:

    a. Sensa ya Watu na Makazi 1967, 1978, 1988 na 2002,

    b. Utafiti wa Mapato na Matumizi wa Kaya Binafsi tangu ikiitwa „The family Budget

    Survey 1963, HBS 1969, HBS 1976/77, 1991/1992, 2001 na HBS 2007‟,

    c. Hali ya Uchumi wa Tanzania 1966/67, 1968/69, 1970/71, 1972/73, 1981, 1989, 1991,

    1997, 1999 mpaka 2009,

    d. Sensa ya Kilimo 1971/1972, 1993/95, 2002/03 na 2007/2008,

    e. Utafiti wa Afya ya Mama na Mtoto (DHS) 1991/92, 1994, 1996, 2004/05 na 2010,

    f. Utafiti wa Watu wenye Uwezo wa Kufanya Kazi 2000/01 na 2006,

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    10

    g. HIV/AIDS 2003/04,

    h. HIV/AIDS na Malaria 2007,

    i. Utafiti wa Wenye Ulemavu 2008,

    j. National Panel Survey 2008/09,

    k. Tanzania Social Economic Database (TSED),

    l. Statistical Abstract,

    m. Kusimamia kikamilifu Chama cha Watakwimu Tanzania (TASTA),

    n. Kuandaa na kushiriki katika maadhimisho ya Siku ya Takwimu Afrika kila mwaka,

    o. Kushiriki kwa mara ya kwanza kuadhimisha Siku ya Takwimu Duniani ambayo ilianza

    mwaka 2010,

    p. Kushiriki katika kuweka takwimu za Tanzania kwenye mtandao wa IMF zikielezea

    mbinu zitumikazo katika kutoa takwimu mbalimbali za nchi yetu (General Data

    Dissemination System) - (GDDS) kuanzia Julai, 2001, na

    q. Kushiriki katika kuandaa na kuboresha takwimu za Jumuiya ya Afrika Mashariki

    ikiwemo kuandaa, kuboresha na kuweka takwimu katika „database‟ ya Jumuiya ya

    Afrika Mashariki.

    6. Mafanikio na changamoto zilizopatikana tangu mwaka 1961

    A. Mafanikio

    i) Kuanzishwa Mpango Kabambe wa Kitaifa wa Kuimarisha na Kuboresha Takwimu

    Tanzania. Maeneo makuu matano ambayo Mpango huu umejikita ni kama

    ifuatavyo:

    1. Uboreshaji wa miundo ya taasisi na sheria ya takwimu,

    2. Uendelezaji na uboreshaji raslimali watu,

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    11

    3. Uimarishaji wa miongozo ya ukusanyaji takwimu,

    4. Kuimarisha upatikanaji na usambaji wa takwimu,

    5. Upatikanaji wa majengo ya ofisi na vitendea kazi.

    ii) Kuongeza ubora na kupanua wigo wa uzalishaji wa takwimu za msingi (core

    statistics) kama vile Pato la Taifa, Mfumuko wa Bei, takwimu za viashiria

    mbalimbali vya kijamii na kiuchumi,

    iii) Kuaminika kimataifa katika utoaji takwimu, ambapo Tanzania imechaguliwa kuwa

    mjumbe kwenye Kamisheni ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa (UN Statistical

    Commission) kwa kipindi cha miaka minne kuanzia 2011 hadi 2015.

    iv) Kuimarika kwa ushirikiano na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi

    ya Zanzibar kwa kuendelea kufanya vikao vya pamoja kila baada ya miezi mitatu

    kwa lengo la kujadili maendeleo ya takwimu nchini.

    v) Kuwasilisha majedwali ya Hali ya Uchumi kwa Wizara yenye dhamana na takwimu

    kila ifikapo tarehe 31 Machi ya kila mwaka ili kuiwezesha Serikali kupanga

    mipango yake inavyostahili,

    vi) Kuanzisha mfumo endelevu wa kijiografia wa ukusanyaji, utunzaji na usambazaji

    wa takwimu na taarifa nchini,

    vii) Katika kuendeleza na kuboresha nyanja za uchambuzi na usambazaji wa takwimu za

    uchumi na kijamii kwa ajili ya ulinganisho na nchi nyingine duniani, NBS

    imeendelea kushirikiana na mashirika ya kimataifa, kama vile:

    - Mashirika ya Umoja wa Mataifa (UN),

    - Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF),

    - Benki ya Dunia (WB),

    - Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB),

    - Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID),

    - Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID)

    - Shirika la Maendeleo la Canada (CIDA)

    - Idara ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa (UNSD), n.k.

    viii) Kwa upande wa rasilimali watu kwa kipindi cha miaka 5 iliyopita, NBS imeongeza

    watumishi wake kutoka 138 mwaka 2006/7 hadi kufikia 182 mwaka 2010/11.

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    12

    Sanjari na hilo, NBS inao wataalam 125 wenye shahada mbalimbali ambao ni

    asilimia 69 ya watumishi wote,

    ix) Serikali imeendelea kuongeza bajeti ya NBS kutoka Tshs 2.6 bilioni mwaka 2004/05

    hadi Tshs 8.0 bilioni mwaka 2010/11 kwa ajili ya kufanikisha majukumu ya Taasisi

    hii.

    x) Kutoa viashiria na taarifa mbalimbali za kitakwimu zinazohitajika katika kutathmini

    utekelezaji wa mikakati na mipango mbalimbali ya maendeleo katika kuisaidia

    serikali kutoa maamuzi sahihi – mfano MKUKUTA kwa Tanzania Bara, MKUZA

    kwa Tanzania Zanzibar, Malengo ya Milenia ya mwaka 2015, na Dira ya Maendeleo

    ya Taifa ya mwaka 2025 kwa Tanzania Bara na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya

    mwaka 2020 kwa Tanzania Zanzibar.

    xi) Kuzindua na kusimamia utekelezaji wa Mkataba wa Huduma Bora kwa Mteja wa

    mwaka 2010.

    xii) Kuongezeka kwa matumizi ya takwimu kutokana na uhamasishaji unaofanyika

    kupitia vipindi vya redio, luninga, magazeti na uzinduzi mbalimbali wa makala.

    xiii) Kuongezeka kwa ushirikishwaji wa wanawake katika ngazi ya maamuzi kutoka

    asilimia sifuri mwaka 1999 hadi asilimia 40 mwaka 2011.

    B. Changamoto

    i. Katika miaka ya 1980 - 1998 kulikuwa na ukosefu wa fedha, fedha zilikuwa

    zinatolewa kwa ajili ya mishahara tu, fedha za vitendea kazi na ukusanyaji wa

    takwimu hazikutolewa hivyo „administrative records data‟ ndio zilizokuwa

    zinatumika,

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    13

    ii. Fani ya Takwimu kwa muda mrefu haikupewa kipaumbele hasa katika

    kupandishwa vyeo (promotions) ikilinganishwa na Wachumi ambao wao

    walikuwa wanapata vyeo kwa mtiririko kila mwaka,

    iii. Serikali ilisitisha ajira mpya kwa kipindi kirefu katika miaka ya 1980 na hii

    ilisababisha upungufu mkubwa wa rasilimali watu katika fani ya takwimu,

    iv. Mapungufu ya Sheria ya Takwimu Na. 1 ya 2002 kutotoa uhuru (professional

    autonomy) na fursa ya NBS kuelekeza Wizara, Idara na Taasisi za Serikali kuhusu

    njia bora ya kukusanya, kuchambua na kuziwasilisha takwimu kwa usahihi kwa

    kutumia viwango vya takwimu vilivyokubalika kitaifa na kimataifa. Hali

    kadhalika, Mfumo wa Taifa wa Kutoa na Kusambaza Takwimu nchini (National

    Statistical System – NSS) kutotambuliwa na Sheria hii,

    v. Kuboresha maslahi ya watumishi ili kuhimili ushindani katika soko la ajira,

    vi. Ufinyu wa bajeti ya kujenga uwezo wa Watakwimu hasa katika shughuli za

    kuboresha utoaji wa takwimu za msingi zinazohitajika na Serikali ikiwa na pamoja

    na kufungua Ofisi za Takwimu za Wilaya ili kuendana na Sera ya Serikali ya

    ugatuaji madaraka kwa wananchi,

    vii. Ukosefu wa majengo ya uhakika kwa Ofisi ya Taifa ya Takwimu makao makuu na

    mikoani pia,

    viii. Uhaba wa vitendea kazi hasa wakati wa ukusanyaji wa takwimu na uchambuzi

    kwa mfano magari, kompyuta na kadhalika,

    ix. Kutokidhi mahitaji ya wateja kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya takwimu

    nchini hali iliyotokana na mabadiliko ya kiuchumi na kijamii duniani,

    x. Upungufu wa wanawake katika fani ya Takwimu,

    xi. Kutokuwepo kwa sera ya Utoaji na Uhamasishaji wa utumiaji wa Takwimu toka

    Taifa hadi ngazi ya Vijiji,

    xii. Ukosefu wa taarifa sahihi za uzalishaji bidhaa na huduma kwa wakati kutoka

    katika vyanzo vya Takwimu, na

    xiii. Ufinyu wa bajeti unaosababisha kutotolewa kwa viashiria muhimu kama vya

    kupima hali ya uchumi katika ngazi ya wilaya na mikoa.

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    14

    C. Namna ya Kukabiliana na Changamoto Hizi

    i. Kwa kuwa hivi sasa kuna mkakati unaoendelea wa Kitaifa wa

    kuboresha na kuimarisha Takwimu Tanzania, suala la sheria ya

    Takwimu kubadilishwa litashughulikiwa katika zoezi hili ambalo

    limeishaanza na linategemewa kumalizika mwaka 2016,

    ii. Vitendea kazi vinatarajiwa kuongezwa kutoka serikalini, wadau wa maendeleo na

    kupitia Mpango Kabambe wa Kuimarisha na Kuboresha Takwimu (Tanzania

    Statistical Master Plan - TSMP),

    iii. Katika kuongeza ubora wa takwimu zinazokusanywa, Ofisi itaendelea kufanya

    ukaguzi mikoani mara kwa mara kuhakikisha takwimu zinazokusanywa zina ubora

    unaokubalika,

    iv. Kuhusu ukosefu wa wanawake katika fani hii ya takwimu, Ofisi inakusudia

    kufanya uhamasishaji kwa wanafunzi wa kike wanaosoma sekondari ili waweze

    kusoma hesabu na hatimaye kuingia katika fani hii,

    v. Katika kuboresha maslahi ya Watumishi, Ofisi inatarajia kutumia taarifa

    itakayotolewa na Mtaalam Mshauri kupitia TSMP, mapendekezo ya kuboresha

    maslahi ya watumishi yatawasilishwa Serikalini baada ya kufanya upembuzi

    unaostahili,

    vi. Kuhusu upatikanaji na usambazaji duni wa takwimu katika ngazi mbalimbali,

    Ofisi itaendelea na jitihada za kuhakikisha Takwimu zinapatikana na kusambazwa

    katika ngazi ya taifa hadi vijijini kwa kupitia mikutano, machapisho, warsha ,

    vipindi vya redio na luninga ili wadau waweze kutumia takwimu hizi kwa kupanga

    mipango ya maendeleo na sio kukisia/kukadiria tu,

    vii. Katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa Ofisi, NBS kwa kupitia Mpango wa

    TSMP iko kwenye mchakato wa kufanya tathmini ya mazingira (Environmental

    Impact Assessment) kupitia Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo

    la Makao Makuu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu,

    viii. Kuhusu ufinyu wa Bajeti, Ofisi itaendelea kufanya majadiliano na Serikali pamoja

    na wadau wa maendeleo kuhusu uwezekano wa kuongeza bajeti ya NBS ili

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    15

    takwimu na viashiria mbalimbali ziweze kutolewa hadi ngazi ya mikoa na wilaya,

    na

    ix. Kuhusu ukosefu wa taarifa sahihi kutoka vyanzo vya takwimu, Ofisi itaendelea

    kuielimisha umma na wadau wa takwimu umuhimu wa kutoa taarifa sahihi na kwa

    wakati.

    7. Mwelekeo wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu katika miaka 50 ijayo

    a. Uboreshaji wa Ukusanyaji wa Takwimu

    i. Majengo na vitendea kazi

    Ukuaji wa shughuli za kitakwimu kunaenda sanjari na mahitaji ya majengo ya Ofisi

    ya Taifa ya Takwimu ikiwemo Ofisi za Mikoa pamoja na vitendea kazi kama magari

    na vinginevyo. Aidha, ukuaji huu unahusisha pia kuendela kuboresha utumiaji wa

    vifaa vya ”teknohama” pamoja na programu za uchambuzi wa takwimu kwa ajili ya

    kuboresha upatikanaji wa takwimu kwa wadau mbalimbali. Mipango ya baadae ni

    kuhakikisha vituo vya uchambuzi wa takwimu vinaanzishwa katika mikoa sanjari na

    uimarishwaji wa Chuo Cha Takwimu cha Afrika Mashariki.

    Mpaka sasa NBS bado inatumia majengo ya kukodi kwa baadhi ya Idara zake,

    mkakati uliopo ni kujenga jengo la takwimu (Takwimu House) kupitia Mpango

    Kabambe wa Koboresha Takwimu.

    ii. Mafunzo

    Uendelezaji wa raslimali watu utafanywa kwa kujenga uwezo wa watumishi kwa

    kuwaongezea ujuzi na maarifa ya ukusanyaji, uchambuzi na uwasilishaji wa takwimu

    zinazoonyesha hali halisi. Mafunzo hayo yatakuwa ya muda mfupi na mrefu kwa

    mujibu wa mahitaji,

    iii. Uimarishaji wa Miongozo ya Ukusanyaji wa Takwimu

    Kutaundwa miongozo ya ukusanyaji na uchambuzi wa takwimu itayokubalika

    kimataifa, kuwa na matumizi sahihi ya misamiati, tafsiri, mbinu nzuri katika

    ukusanyaji takwimu pamoja na kuwa na mihimili imara ya sampuli kwa tafiti za

    kiuchumi na kijamii. Aidha, mfumo wa kijiografia (Geographical Information System)

    utaimarishwa ili kuongeza matumizi ya takwimu kwa sababu hufikisha ujumbe kwa

    haraka zaidi unapotumika.

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    16

    iv. Kuongeza mahusiano na nchi za nje na ofisi za kimataifa kuhusu uboreshaji, ukusanyaji,

    uchambuzi na usambazaji wa takwimu.

    b. Uboreshaji wa Bajeti ya NBS

    i. Ni matarajio ya NBS kuwa Serikali itaendelea kuongeza bajeti ya NBS ili

    takwimu na viashiria mbalimbali ziweze kutolewa kwa watumiaji wa ndani na

    nje,

    ii. Serikali itaendelea kuipa uwezo NBS kifedha ili kuboresha mafungu ya fedha

    ziendazo Ofisi za Taifa za Takwimu mikoani kwa ajili ya kazi za ukusanyaji wa

    takwimu maana mahitaji ya takwimu yameongezeka katika ngazi zote za

    utawala na wadau kwa ujumla.

    c. Maboresho Mengine ya Takwimu

    Ofisi ya Taifa ya Takwimu inatarajia kufanya yafuatayo kwa miaka ijayo:

    i. NBS itaendelea kuboresha Vizio katika utoaji wa GDP na CPI kwa kutumia

    Utafiti wa Mapato na Matumizi katika Kaya Binafsi (HBS) na vyanzo na tafiti

    nyingine,

    ii. Kuboresha muundo wa Taasisi na Sheria ya Takwimu,

    iii. Kuendelea kupanua wigo kwa kufanya tafiti mbalimbali kupitia “Commissioned

    Work” ili kuongeza mapato,

    iv. Kuendelea kuratibu na kusimamia utekelezaji wa TSMP katika Wizara, Idara na

    Taasisi mbalimbali za Serikali,

    v. Kuendelea na maandalizi ya zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya 2012, zoezi

    hili litaendelea kwa kufanya kazi za uchambuzi, usambazaji na utunzaji wa

    takwimu hadi mwaka 2015. Kuanzia mwaka 2016 maandalizi ya Sensa ya Watu

    na Makazi ya mwaka 2022 yataanza, na

    vi. Katika kuboresha fani ya takwimu nchini, NBS itaendelea na juhudi za kufufua

    na kuimarisha Chama cha Watakwimu Tanzania (Tanzania Statistical

    Association - TASTA).

  • Miaka 50 Ya Uhuru wa Tanzania Bara, Makala ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu

    17

    8. Hitimisho

    Pamoja na changamoto zinazoikabili Ofisi ya Taifa ya Takwimu katika suala zima la

    maandalizi ya Sensa, juhudi zimewekwa ili kuhakikisha kuwa maandalizi yanakamilika

    ipasavyo. Sensa ijayo ina umuhimu wa kipekee kwani ndiyo itakuwa chanzo kikuu cha

    takwimu zitakazotumika kupima ni kwa kiasi gani Tanzania imefanikiwa katika kutekeleza

    Malengo ya Milenia ya mwaka 2015 pamoja na programu nyingine za maendeleo

    zilizowekwa na Serikali.

    Vilevile, Ofisi ya Taifa ya Takwimu itaendelea kutoa Takwimu za Pato la Taifa kwa kila

    mwaka, Mchango wa shughuli za Kiuchumi kwa mwaka, Wastani wa Pato la Mtanzania

    kwa mwaka na kutayarisha Takwimu za Pato la Taifa kwa robo mwaka.

    Moja ya lengo la Mpango Kabambe wa Kitaifa wa Kuboresha na Kuimarisha Takwimu ni

    kuwa na mfumo imara na bora wa kitaifa wa kuratibu, kukusanya, kuhifadhi na kusambaza

    takwimu rasmi hapa nchini. Kwa maana hiyo, utekelezaji wa Mpango huu utaboresha

    upatikanaji wa takwimu bora, sahihi na kwa wakati ambazo zitasaidia Serikali na Taasisi

    mbalimbali kufanya maamuzi sahihi ya kisera na pia kupima viashiria muhimu vya

    kutathmini utekelezaji wa MKUKUTA/MKUZA, Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Tanzania

    Bara ya mwaka 2025 na Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Tanzania Zanzibar ya mwaka

    2020.

    Aidha, kupitia Mpango huu vitengo vya takwimu katika ngazi mbalimbali za Serikali

    vitaanzishwa au kuboreshwa ili uzalishaji wa takwimu uweze kukidhi mahitaji ya wadau

    mbalimbali.

  • OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU

    Dira

    Dira ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu ni kuwa chanzo cha kuaminika katika kutoa takwimu rasmi

    nchini.

    Dhamira

    Dhamira ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu ni kuuwezesha mchakato wa kufanya maamuzi kwa kutoa

    takwimu bora na zinazokubalika kwa wakati, kuratibu shughuli za kitakwimu na kuhamasisha

    utumiaji wa methodolojia na mbinu za kitakwimu.