33
1 TAASISI YA UTAFITI NA UTETEZI WA MASUALA YA ARDHI (HAKIARDHI) KONGAMANO LA MIAKA 10 YA SHERIA ZA ARDHI TANZANIA 27-29 MEI 2009

TAASISI YA UTAFITI NA UTETEZI WA MASUALA YA ...ihi.kazi.pro/wordpress/wp-content/uploads/2017/08/NALAF...Waziri alielezea umuhimu wa kuwepo mifumo imara ya usimamizi na matumizi ya

  • Upload
    others

  • View
    10

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

1

TAASISI YA UTAFITI NA UTETEZI WA MASUALA YA

ARDHI

(HAKIARDHI)

KONGAMANO LA MIAKA 10 YA SHERIA ZA ARDHI TANZANIA

27-29 MEI 2009

2

YALIYOMO

1.0 UTANGULIZI ................................................................................................................................. 4

1.1 IGIZO KWA NJIA YA USHAIRI KUTOKA PARAPANDA THEATRE GROUP. ................................................ 4 1.2 MGENI RASMI - NAIBU WAZIRI WA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA – NDUGU AGGREY

MWANRI ............................................................................................................................................... 4 1.3 MADA: I - CHANGAMOTO ZA URASIMISHAJI ARDHI KATIKA MFUMO WA SASA WA MILKI– NA ENG. L.

M. SALEMA, (MKURABITA)................................................................................................................ 6 1.3.1 Washiriki walichangia mada kama ifuatavyo: .......................................................................... 7 1.3.2 Maoni ya Mkurabita ............................................................................................................... 8 1.3.3. Maoni kutoka kwa Mgeni Rasmi - Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa....... 8

2.0 MADA II – TATHMINI YA SERIKALI JUU YA UTEKELEZAJI WA SHERIA ZA ARDHI,

UZOEFU, MAFUNZO NA CHANGAMOTO - MWASILISHAJI JANE KAPONGO, WIZARA YA

ARDHI NA MAENDELEO YA MAKAZI ............................................................................................ 9

2.1 MADHUMUNI YA WIZARA ................................................................................................................ 9 2.3 MAONI NA MCHANGO WA WASHIRIKI ................................................................................................ 9 2.4 MAONI YA WIZARA ....................................................................................................................... 10 2.5 MASWALI NA USHAURI................................................................................................................. 10 2.6 MWONGOZO KUTOKA WIZARA YA ARDHI ....................................................................................... 11

3.0 MADA: MTAZAMO WA ASASI ZA KIRAIA JUU YA UMADHUBUTI, UDHAIFU NA

CHANGAMOTO ZA MFUMO WA MILKI YA ARDHI TANZANIA – MWASILISHAJI –

OXFAM/HAKIARDHI ........................................................................................................................ 11

3.1 MAMBO YALIYOJITOKEZA ............................................................................................................. 12 3.2 MATOKEO ..................................................................................................................................... 12 3.3 MASWALI NA MAONI .................................................................................................................... 12 3.4 MAELEZO KUTOKA KWA MWASILISHI ............................................................................................ 13

4.0 MADA - UZOEFU NA CHANGAMOTO ZA MFUMO WA UTATUZI WA MIGOGORO YA

ARDHI – NA BAHATI MLOLE, MSAJILI WA MABARAZA YA ARDHI – WIZARA YA ARDHI. .... 13

4.1 MAONI NA MASWALI KUTOKA KWA WASHIRIKI ............................................................................... 14 4.2 MWONGOZO KUTOKA WIZARA YA ARDHI ...................................................................................... 15

5.0 MADA – UTEKELEZAJI WA MIPANGO YA MATUMIZI BORA YA ARDHI, UZOEFU,

CHANGAMOTO NA MAFUNZO - NA GERALD MANGO – MKURUGENZI MKUU, TUME YA

TAIFA YA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI ............................................................................. 15

5.1 MCHANGO WA MAWAZO KUTOKA KWA WASHIRIKI ......................................................................... 16 5.2 MCHANGO KUTOKA KWA MWASILISHI WA MADA KUTOKA WIZARA YA ARDHI ................................ 16

6.0 MADA YA CRT - ELIKARIBU GAYEMI, UJAMAA CRT RESOURCE TRUST .................... 17

6.1 CHANGAMOTO ............................................................................................................................... 17 6.2 MAWAZO YA WASHIRIKI ................................................................................................................ 18

6.3 NAFASI YA MWANAMKE KATIKA UMILIKI WA ARDHI............................................... 18

MASWALI NA MAONI YA WASHIRIKI .......................................................................................... 19

6.4 MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI – HAKIARDHI, DKT. NG’WANZA

KAMATA ............................................................................................................................................. 19

7.1 UZOEFU KUTOKA KENYA KWENYE MASUALA YA ARDHI - MWASILISHI: ODENDA LUMUMBA ........... 20 7.2 HITIMISHO ........................................................................................................................... 23 7.3 MASWALI KWA UPANDE WA KENYA ......................................................................................... 23

7.4 MAJIBU .................................................................................................................................... 23

3

8.0 UZOEFU WA UGANDA KWENYE MASUALA YA ARDHI - MWASILISHI: ESTHER

OBAIKOL ............................................................................................................................................ 24

8.1 CHANGAMOTO KWA TAASISI BINAFSI ........................................................................................ 24 8.2 HITIMISHO ........................................................................................................................... 25

9.0 UZOEFU WA RWANDA KWENYE MASUALA YA ARDHI - MWASILISHI: JOHN

MUYENZI ............................................................................................................................................. 25

9.1 UZOEFU KATIKA KUTENGENEZA NA KUTEKELEZA SERA NA SHERIA ZA ARDHI ............................. 25 9.2 CHANGAMOTO ZINAOIKUMBA SEKTA YA ARDHI NCHINI RWANDA .............................................. 26

10.0 MJADALA WA MCHANA ...................................................................................................... 27

11.0 MAAZIMIO YA KONGAMANO ............................................................................................ 28

11.1 USHIRIKI WA WANANCHI NA WANAVIJIJI KATIKA MAAMUZI YANAYOHUSIANA NA ARDHI HUSUSANI

KWENYE NGAZI YA VIJIJI. NINI KIFANYIKE? .......................................................................................... 28 11.2 UWEKEZAJI KATIKA ARDHI YA VIJIJI UNAENDANA SANA NA MAMBO HAYA MAWILI:- ...................... 29 11.3 KWANINI MIGORORO KWENYE SEKTA YA ARDHI IPO KWA KIWANGO CHA JUU WAKATI SHERIA ZA

UTATUZI ZIPO? .................................................................................................................................... 30 11.4 NINI KIFANYIKE ILI WANAWAKE WAFAIDIKE NA SHERIA ZA ARDHI NAMBA 4 NA 5 ZA MWAKA 1999?

........................................................................................................................................................... 31 11.5 FIDIA ZA ARDHI NA KUPATIWA ENEO MBADALA. JE, LINAKIDHI MAHITAJI YA WAFIDIWA? NINI

KIFANYIKE? ........................................................................................................................................ 31 11.6 HUDUMA ZA ARDHI ( UPIMAJI, UTOAJI WA HATI) HAZIENDANI NA HALI HALISI. NINI KIFANYIKE? ... 31 11.7 UKOMO WA KIASI CHA ARDHI ANACHOWEZA KUPATA MTU MMOJA NA KUMILKI KIHALALI. ............. 32 11.8 KILIMO CHA MASHAMBA MAKUBWA NA UHAKIKA WA CHAKULA KWA WANANCHI NA TAIFA KWA

UJUMLA. ............................................................................................................................................. 32 11.9 MFUMO WA UMILIKI WA WAFUGAJI- UTAMBUZI ........................................................................... 32

12.0 KUFUNGA KONGAMANO ........................................................................................................ 33

4

TAASISI YA UTAFITI NA UTATUZI WA HAKI ZA ARDHI

Kongamano la Miaka 10 ya Sheria za Ardhi Tanzania 27-29 Mei 2009

1.0 Utangulizi

Mkurugenzi Mtendaji wa HAKIARDHI - Ndugu Yefred Myenzi aliwakaribisha

washiriki wa Kongamano saa 3.58 asubuhi na kuwafahamisha lengo la Taasisi la

kukutanisha wadau mbalimbali kujadiliana na kushirikishana uzoefu wao kuhusu

masuala mbalimbali yaliyojitokeza katika kipindi cha miaka 10 tangu sheria za ardhi

namba 4 na sheria ya ardhi ya vijiji namba 5 zilipotungwa na Bunge.

Kongamano hili litawahusisha waalikwa kutoka nchi jirani za Afrika Mashariki ili

kushirikisha maendeleo katika mifumo yao ya milki ya ardhi na utekelezaji wa sheria zao

kwa lengo la kujifunza uzoefu wao na kujenga mahusiano na ushirikiano katika masuala

ya ardhi.

Mkurugenzi Mtendaji alisema mada mbalimbali zitajadiliwa kuhusu masuala ya ardhi

kutoka asasi za kiraia na sekta binafsi. Mada hizo zitajikita katika tathmini, mafunzo na

changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa sheria za ardhi kwa vipengele

mbalimbali tangu 1999 hadi 2009. Aliwaomba washiriki kuchangia mawazo, kujadili na

kupendekeza nini kifanyike ili kuboresha upatikanaji wa haki ya ardhi kwa kila

Mtanzania.

Baada ya Utambulisho, Mgeni rasmi - Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za

Mitaa – Ndugu Aggrey Mwanri alifika na kukaribishwa na washiriki wote.

1.1 Igizo kwa njia ya ushairi kutoka Parapanda Theatre Group.

Igizo maalum juu ya matatizo ya ardhi – ujumbe wa barua pepe ambayo ilivuta hisia za

washiriki wote na kutoa changamoto kwa washiriki kwamba watumie nafasi hii

“KUZUNGUMZA”.

1.2 Mgeni Rasmi - Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – Ndugu Aggrey Mwanri

Naibu Waziri aliomba radhi kwa kuchelewa na kusema amekuja kwa niaba ya Waziri

Celina Kombani ambaye bahati mbaya ilibidi aende kwenye majukumu mengine ya

Kitaifa. Waziri aliwakaribisha nchini kwa niaba ya Serikali ya Tanzania washiriki

kutoka nchi jirani za Mozambique, Kenya, Uganda na Rwanda na kuwashukuru

waandaaji wa Kongamano hili muhimu kumwalika na kuahidi kushiriki kwa jinsi muda

utakavyomruhusu. Mh. Waziri alielezea umuhimu wa kuwepo mifumo imara ya

usimamizi na matumizi ya ardhi vinginevyo migogoro itakuwa haiishi. Alitoa wito kwa

Asasi za Kiraia n.k. kutumia nafasi zao na rasilimali walizonazo kuunga mkono juhudi za

serikali kuwa na mtandao wa asasi zote za masuala ya ardhi kwa kutoa elimu juu ya

sheria za ardhi na elimu ya uraia kuwawezesha wananchi kujua haki zao. Aliwaomba

5

wadau waungainshe nguvu ili kuwe na mfumo mmoja wa utoaji elimu kwa wananchi

ambao hatimaye unawezesha ufuatiliaji na kupima mafanikio kwa nchi kuliko mashirika

haya yakifanya kazi katika maeneo ambayo tayari serikali imeshatekeleza

yanayofundishwa.

Mh. Waziri alisema kuna changamoto nyingi katika kuhakikisha sheria zinatekelezwa:

Tanzania imebarikiwa na kuonekana kuwa kimbilio la wawekezaji wanaotafuta

nishati mbadala inayotokana na mimea. Ni vyema kutahadharisha matumizi ya

ardhi inayofaa kwa uzalishaji wa chakula isitumiwe kuwa maeneo ya kilimo cha

nishati uoto. Alitoa rai kwa serikali za vijiji kuwa makini katika kuidhinisha

maeneo kwa ajili ya uwekezaji wahakikishe wananchi wanajikimu kwa chakula.

Matumizi ya ardhi ya vijiji yafuate taratibu kama ilivyo katika sheria za ardhi na

serikali za mitaa. Hii inapunguza malalamiko yasiyo ya lazima. Kumekuwa na

malalamiko ya mara kwa mara kuwa vyombo vya utekelezaji vinafanya maamuzi

bika kuwashirikisha. Hii huleta migogoro.

Kuna wananchi wakorofi ambao wamekuwa wanakalia maeneo makubwa bila

kuyaendeleza. Pale inapobainika wananchi wanahodhi ardhi kubwa bila

kuifanyia maendeleo serikali ya kijiji iwajibike kuwashauri kupitia mkutano

mkuu wa kijiji ili kuwe na matumizi bora ya ardhi husika.

Aligusia pia migogoro ya wakulima na wafugaji ambayo imejitokeza mara kwa

mara. Mh. Alishauri mabaraza na mahakama za ardhi viachiwe kufanya kazi bila

kungiliwa na kila kundi liheshimu maamuzi ya vyombo hivyo. Halmashauri za

Wilaya na vijiji vitenge maeneo ya shughuli mbalimbali na kuweka mipaka ili

kila mtumiaji wa ardhi asimwingilie mwingine katika eneo lake.

Umuhimu wa umilikishwaji ardhi kisheria bila kutumia rushwa.

Aliwaomba wananchi kuepukana na matumizi ya maeneo yaliyohifadhiwa ili

kuepusha bomoa bomoa zisizo za lazima. Mh.Waziri alisema anaamini washiriki

watatumia nafasi hii ya Kongamano kuibua na kujadili masuala muhimu kwa

maendeleo ya taifa ili kusaidia serikali kufikia hatua ya juu kabisa katika

kumletea maendeleo Mtanzania. Aliwashukuru waandaaji wa Kongamano

kuwaalika washiriki kutoka Halmashauri za Wilaya na kusema kwa nafasi zao

hao ndio watendaji kila siku wa masuala ya ardhi na watabadilishana uzoefu na

kujifunza mbinu ambazo zinaweza kutumika kukabiliana na changamoto

zinazotokana na kazi zao.

Mheshimiwa Waziri alitambua uwepo wa washiriki kutoka Kenya, Rwanda na

Uganda na kuelezea kwamba swala la ardhi limeibua mjadala mkubwa sana

kwenye jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu namna inavyopaswa kuwa na

mfumo unaozingatia maslahi ya kila mwanajumuiya na kwamba mkusanyiko huu

utakuwa na mjadala wenye mwelekeo wa kupata suluhu ya kudumu kwa matatizo

6

yenye sura ya Afrika Mashariki. Alimaliza kwa kuwaomba washiriki watumie

mwanya wa ushiriki mpana wa Kongamano hili kutoa maazimio

yanayotekelezeka kwa kila mdau aliyeshiriki ili kutoa mwongozo wa namna ya

kukamilisha sehemu kidogo zilizobakia katika utekelezaji wa sheria za ardhi.

Mkurugenzi Mtendaji wa HAKIARDHI alimshukuru mgeni rasmi kwa Hotuba nzuri

ambayo kwa kuifikiria haraharaka ni kama imetoa tathmini, changamoto za uwekezaji na

uhakika wa chakula. Pia ameshukuru kwamba Serikali inatambua mchango wa Asasi za

Kiraia katika swala zima la masuala ya ardhi. Pia alimshukuru Waziri kwa kukubali

kuwa mshiriki.

Mkurugenzi Mtendaji alipitia ratiba na kuwafahamisha washiriki mada zitakazojadiliwa:

SIKU YA KWANZA – 27/5/2009

1.3 Mada: I - Changamoto za Urasimishaji Ardhi katika mfumo wa sasa wa Milki– Na Eng. L. M. Salema, (MKURABITA)

Eng. Salema kutoka MKURABITA alitoa mada kuhusu Mpango wa Kurasimisha

Rasilimali ambapo alieleza kuwa umiliki salama na endelevu wa ardhi ni nyenzo

muhimu ya kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Alisema kama unamiliki ardhi

na unatumia nje ya sheria zilizopo wewe ni mnyonge. Kama una shamba au ranchi na

huna kitambulisho kwamba hilo shamba ni lako – (hati) huwezi kuaminika hata benki

hata kama kwenye shamba hilo kuna nyumba kubwa.

Eng. Salema aliwafahamisha washiriki sababu za serikali kuanzisha mpango huu kuwa ni

baada ya kufanya tathmini na kugundua kwamba shughuli za biashara sekta isiyo rasmi

ina wananchi wengi zaidi kwa hiyo juhudi za dhati ni lazima zifanywe ili kurasimisha.

Kwa mfano utafiti uliofanywa (2004-2006) ulibainisha kuwa 88% ni sekta isiyo rasmi.

Miji mikubwa 70% ya wananchi wanaishi makazi ambayo hayajapimwa.

Wananchi wanatakiwa kuhakikisha ardhi waliyonayo inatambuliwa kisheria na ili uweze

kutumia ardhi hiyo ni lazima uisajili kisheria ili yeyote anayeweza kupata taarifa aweze

kupata. Utafiti uliofanyika nchi kadhaa kuhusu mpango huu umedhihirisha kwamba:

Wamiliki wanahamasika kuwekeza kwenye ardhi yao

Migogoro ya mipaka na hata matumizi unapungua kwenye ardhi iliyorasimishwa.

Thamani ya ardhi inaongezeka

Wananchi wanapata mikopo katika mabenki kwa kutumia ardhi kama dhamana.

Pamoja na hayo, serikali inatambua kuna umuhimu wa maboresho katika sheria za ardhi,

yametolewa mapendekezo kwamba usajili ufanyike ngazi ya Wilaya bila matatizo.

Sheria inasema ardhi ni mali ya umma na Rais ndiye mwenye dhamana. Je ni kweli

wananchi wanakubali ardhi ni mali ya umma?. Je Tuendelee kusema au tutengeneze

kanuni rasmi au tukubali ardhi inaweza kumilikiwa na mtu binafsi. Tumetizama sera.

7

nyingi zinagusa sheria ya ardhi. (Zingine zote zinazoitambua sera ya ardhi kama ardhi

mama. Majukumu chini ya Wizara ya Ardhi/TAMISEMI. Katika kubadili mfumo –

Kuwe na tume ambayo wadau wakijadiliana wana mamlaka ya kuamua mambo

muhimu.

Vijana waweze kupima mashamba ya vijiji vyao

Tumependekeza – ndani ya Wizara ya Ardhi kuwe na agency ya kupanga/kupima

na kupokea kodi za ardhi/real estate agency. Mijini na baadae vijijini.

Umiliki wa ardhi uwe mikononi mwa Watanzania. Tusiwape watu wa nje ardhi

yetu kwa sababu migogoro mingi inatokana na hiyo.

Ili ardhi ilete tija lazima kuwe na namna kwa mfano usipoiendeleza (plot e.g.)

kwa muda fulani unaweza kunyang‟anywa. Badala ya mtu kunyang‟anywa –

atozwe kodi.

MKURABITA inathibitisha kwamba ardhi ikirasimishwa inalipa. Na imependekeza

wizara ya Ardhi ifanye kazi ya kupanga matumizi muhimu ya ardhi. Pamoja na kwamba

hatujatamka kwamba nchi yetu ni ya kibepari, tuzungumze kwamba ili kilimo kishamiri

tuwe na kilimo cha kisasa ambacho tunaweza kuwa na kada ya wakulima wazuri.

Pamoja na kurekebisha sheria – kujenga uwezo ili urasimishaji ufanyike mamlaka

ya chini.

Katika hali yetu ya maendeleo tunategenea sekta isiyo rasmi na ukimwambia mtu

akopee hati yake na jirani yake ameuziwa nyumba juzi kwa ajili ya kutolipa

inatisha. Kuwe na mpango maalum wa kumwezesha huyu asipoteze chake.

Tupeni mawazo yenu ili kuboresha hapa.

1.3.1 Washiriki walichangia mada kama ifuatavyo:

i. Wakulima wadogo wadogo watanufaika vipi na mpango huu?

ii. Inakuwaje tuukumbatie mfumo wa ubepari wakati tunajua hata siku moja

haujaleta manufaa kwa mwananchi wa kawaida?

iii. Je elimu ya mpango huu imetolewa ya kutosha? Juu ya umiliki, matumizi au

kuuza kwa ajili ya faida yao? Je watalindwa? Bila kuuza kwa watu wa nje?

iv. Umilikaji wa ardhi – kama ardhi ni ya kwangu na familia na eneo ni langu je

nitakuwa na ukomo? kwa mfano umiliki wa miaka 33 au 99. Je baada ya hapo

nitakuwa sio Mtanzania?

8

1.3.2 Maoni ya Mkurabita

Watu wengi wanafikiri kwamba MKURABITA ilianzishwa kwa msukumo wa

De Sotto. Hii si kweli. Kabla ya hapo, chama cha CCM kilifanya maamuzi

wananchi wamilikishwe ardhi. Baadae Dr. De Sotto na Mkapa walikaa.

Mawazo yao yalifanana kwamba kuna watu wengi wanamiliki mali isiyo

rasmi. Kukafanyika Kongamano mwaka 2003 ambalo lilihudhuriwa na watu

mbalimbali. Alichosema De Sotto ni kwamba kama wananchi watabaki bila

kurasimishiwa wataendelea kuwa duni vinginevyo kule Peru walifanikiwa.

Kuna maboresho na mapendekezo yaliyotolewa ila hatuwezi kukataa kwamba

ni ukweli sekta isiyo rasmi haifai.

Watu wanafikiri kurasimisha ardhi ni ubepari. Ule ni wa Carl Max. Ubepari

wa sasa ni tofauti, unatambua mchango wa mtu. Wanataka kuwe na amani.

Wala hauendeshwi na serikali ni shirikishi (corporate world) ndio inafanya

kazi. Ni swala la utaalam.

Kuhusu kwamba elimu haitoshi – Kuna mpango wa elimu wa miaka 10. Hii

ni pamoja na namna ya kulinda haki za wamiliki. Kwa sasa watu wengi

wametambua thamani ya ardhi na wanauza sana. Wakiwa na hati watapata

pesa zaidi. Tena zipatikane katika ngazi ya kijiji. Halmashauri za kijiji hata

sasa zinashughulikia mikataba mingi kuliko Commissioner wa Ardhi.

Kuhusu kama ni mpango wa serikali kunyang‟anya ardhi – Eng. Salema

alisema, kwanza milki ya kimila haina ukomo. Ukomo uko kwenye ardhi ya

mijini. Na haiwezi kunyang‟anywa bila kutumia sheria. Hamna sababu ya

kuwa na woga.

1.3.3. Maoni kutoka kwa Mgeni Rasmi - Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Mazingira ya kwetu hakuna ubepari kwamba njia za uchumi zimejengwa kwa kutowajali

wengine na kuwatupa nje. Hapa tunazungumzia mahusiano ya uzalishaji mali.

MKURABITA ukisema unalima pamba – unatumia harvester. Moja ya namna ya

kuwasaidia wananchi wanyonge ni kuwaunganisha kwenye ushirika. Kama unataka

kuwasaidia utapitia pale. Vinginevyo utawafanya wawe vibarua. Mashirika kama benki

– hawatawajua. Serikali imeingiza “msuli” intervention. Tunapigania ushirika ndio

unaoweza kusaida. Je ni kweli ukisharasimisha wananchi watatoka? Kuna soko huria na

limekubalika, kazi yake ni nini? Hii iko katika „sheria ya utashi na urari‟. Law of demand

and supply.

Watu wazugumze „planned market economy.‟ Unaweza kusema tuweke sheria.

Tunachopigania hapa ni faida nyingi – „super profit‟. Wenzetu nchi za Ulaya wanaweka

ruzuku katika kilimo, mifugo ili kusaidia mipango katika kipindi cha mpito.

Baada ya maswali na majibu Mratibu wa Kongamano William Ole Nasha

alimshukuru Naibu Waziri na washiriki wote waliochangia na kuahidi kuendelea

kujadili.

9

2.0 MADA II – TATHMINI YA SERIKALI JUU YA UTEKELEZAJI WA SHERIA ZA ARDHI, UZOEFU, MAFUNZO NA CHANGAMOTO - Mwasilishaji Jane Kapongo, Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi

Mada hii ilitolewa na Dada Jane Kapongo ambaye alielezea majukumu ya Wizara ya

Ardhi Mijini na Vijijini. Dira hasa ni kuwa mlezi wa umiliki na ulinzi wa ardhi nchini.

Na dhima yake ni kuwa na mazingira wezeshi. Alisema Wizara ya ardhi imefanya juhudi

kubwa ya kuwaelimisha wananchi kuhusu sheria za ardhi na yeye binafsi amehusika

kwenye kuendesha mafunzo hayo.

2.1 Madhumuni ya Wizara

Kuimarisha usalama wa milki za ardhi

Kuboresha mtandao wa kijiographia nchini

Kuweka mpango endelevu wa watu/nyumba zinazokidhi mahitaji

Kuendeleza utafiti wa vifaa vya ujenzi wa nyumba bora kwa bei nafuu

Ushirikiano/mawasiliano na uratibu wa masuala ya kitaifa/kimataifa na kikanda.

Mtoa mada aliwafahamisha washiriki wa Kongamano umuhimu wa wizara ya Ardhi

kushirikiana na Asasi za Kiraia katika kutekeleza sheria za ardhi kwa sababu mlengwa

wa wote ni mwananchi. Bahati mbaya sana hata katika kupanga bajeti ya serikali sekta

zinazopewa umuhimu zaidi ni Afya/Kilimo/Elimu, n.k. na sio ardhi.

Alisisitiza umuhimu wa kuwa na wataalam/wateule wa masuala ya sheria za ardhi ili

utekelezaji uwe rahisi.

2.3 Maoni na mchango wa washiriki

Mshiriki mmoja alisita kukubaliana na swala zima la elimu juu ya sheria.

Alisema watu wengi haijawafikia. Kuna umuhimu sana kwa wananchi kutoa

elimu hii. Bila hizi ASASI kazi ya Wilaya inaweza kuwa ngumu. Aliunga

mkono ushirikiano na kutoa mfano kwamba sehemu anayotoka (Arusha) hamna

sehemu ya utatuzi wa migogoro na hata kama milki ingetolewa bila elimu bado

migogoro itakuwepo.

Mtafiti wa Nishati Uoto vijijini- alisema Sheria za ardhi ni tatizo. Tatizo la fidia

kwa wawekezaji wanaochukua mashamba ya wananchi ni kubwa mno. Fidia ni

ndogo sana. Wananchi hawana ujuzi wa hesabu hata za ekari. Utawaelekezaje

kama hawaelewi sheria na hawaijui.

Uendelezaji wa ardhi ni changamoto vijijini kuliko mijini. Kama Wizarani kuna

mikopo ya ujenzi wa nyumba kwa ajili ya wafanyakazi – Je Wizara inawasaidiaje

waliopata viwanja kupata mikopo hii?

10

2.4 Maoni ya Wizara

2.4.1 Mafunzo - Idara ya utawala na usimamizi wa ardhi - ndani kuna kitengo

ambacho Sheria ya Ardhi Na. 4 na 5 zinapatikana. Hapa kitengo hiki hushirikiana na

wadau wote katika utekelezaji wa sheria za ardhi. Inaratibiwa na WB/EU.

2.4.2 Fidia – Ndani ya sheria imeelezwa namna ya kudai fidia. Iwapo mtu wa nje

anataka kuchukua sehemu. Kuna utaratibu maalum kuhusu fidia.

Watu hawaelewi sheria. Pamoja na elimu inayotolewa – „public awareness‟ ngazi

ya mkoa. Inatakiwa ngazi ya juu zaidi. Mtoa mada alikubaliana na washiriki

kwamba kuna sehemu Wizara haijafika ndio maana inatambua kazi za NGOs.

Utoaji wa vifaa – Kuna miongozo ya kutoa sheria za ardhi na migogoro ya ardhi.

Kuna kamati maalum ya watu 9 inayosimamia miongozo hii.

2.4.3 Utatuzi wa Migogoro

Kama Wizara kuna mabaraza hasa sehemu zenye migogoro mingi. Kutathmini kama

wajumbe wamechaguliwa vizuri bila „conflict of interest‟.

2.4.4 Mikopo ya Nyumba

Mikopo ya nyumba ni kwa watumishi wa serikali tu. Utaratibu wa kupata ni kwamba

ukipata kiwanja unatakiwa upate hati/mchoro/mchanganuo wa ujenzi na unapewa

mkopo ambao unakatwa kwenye mshahara wako.

2.5 Maswali na Ushauri

2.5.1. Swala la mikopo ya nyumba kama ni kwa wafanyakazi wa serikali tu ifutwe.

2.5.2 Je mikopo kwa ajili ya kupima viwanja. Wananchi wanaweza kupewa fidia

kwa kupata ardhi mbadala au fedha. Fidia hiyo ili iweze kuwafikia wananchi ina

thamanishwa kiasi gani. Tunataka kujua eneo kiasi gani ni bei gani?

2.5.3 Vyeti vya kimila – Katika vijiji vingine hamna hata fomu na kupata cheti

cha kijiji ni vigumu. Je wananchi wafanyeje.

2.5.4 Mikopo kwa ajili ya wafanyakazi – Watekelezaji wenyewe wanajigawia

mikopo na viwanja – kuna dhana ya upendeleo, wananchi watapata kweli?

2.5.5 Ukuaji wa miji na vijiji – Wote tunajua kuwa ili mtu aendelee tunahitaji

ardhi/watu na siasa safi. Vijiji havijapata vyeti kwa hiyo ardhi haijapatikana.

2.5.6 Utekelezaji wa vijiji na mpango bora. Kuna matatizo mengi ya mipaka

vijijini. Kama hayatatatuliwa, tunawekeza kwenye matatizo ya baadae. Kama

juhudi zisipofanyika, kuna watu watakaopimiwa sehemu zenye matatizo ambazo

zinaweza kuwa hata haziko kijijini kwao. Mfano mzuri ni Rufiji. Matatizo

mengine ni ya Wizara ya Ardhi – wananchi kuna mambo tunayofahamu ya

kughushi taarifa ambazo sio sahihi. Tunapandikiza matatizo.

11

Mwongozo:

Mshiriki mmoja alishauri kwa sababu hili ni kongamano – sio busara kuelekeza

maswali kwa mtoa mada – washiriki wachangie na kutafuta utatuzi. Alisema fidia

kweli ni tatizo kubwa – sheria Na. 4 ilisema utaanzishwa mfuko unaosaidia na kanuni

imeshatungwa.

2.6 Mwongozo kutoka Wizara ya Ardhi

Kuhusu kufuta mikopo, watu wengine hawana pa kukopea. Serikali inaweza

kutumia ardhi kama rasilimali mtu anaposhindwa kulipa. Mtumishi anakatwa

kutokana na mshahara wake.

Mpimaji wa viwanja ni Halmashauri ambazo ziko chini ya serikali za mitaa.

Sheria No. 5 ni mpya, kama sio mtaalam wa maswala ya ardhi. Pale ambapo

tunatekeleza inatakiwa tuungane na Halmashauri husika

Utatuzi wa Migogoro ya mipaka – Kwa mujibu wa sheria Halmashauri za kijiji

husika ndio zinashughulikia. Vijiji haviwezi kupata cheti kama kuna migogoro ya

mpaka wa kijiji.

Sehemu iliyopimwa viwanja – watu wanalipwa fidia. Viwanja vinatangazwa na

mwananchi yeyote yuko huru kununua. Sasa hivi wananchi wameamka na

wanathamini maeneo yaliyopimwa. Na ni vyema kuchukua yanapotangazwa.

Wilaya ya Rufiji – Wizara imeamua kuanzisha idara zinazoshughulika na

matatizo ya ardhi. Kwa kuwa watu wa Rufiji wameeleza matatizo yaliyopo, mtoa

mada aliahidi kuyapeleka ofisini kwa utatuzi.

SIKU YA PILI - 28/05/09

3.0 MADA: MTAZAMO WA ASASI ZA KIRAIA JUU YA UMADHUBUTI, UDHAIFU NA CHANGAMOTO ZA MFUMO WA MILKI YA ARDHI TANZANIA – Mwasilishaji – Oxfam/HAKIARDHI

Malengo ya Sheria ya Ardhi 1999 ambayo ndio kiini cha tathmini hii yalielezewa.

Matokeo – baada ya sheria za ardhi kutungwa.

Je haki zilizokuwepo zinafuatwa? Mchambuzi alielezea jinsi hali ilivyo – Sheria

inaeleza wazi kwamba mtu akiondolewa kwenye eneo lake atapata fidia lakini

watu hawapati.

Pia tumeona kuwa sheria ya kimila ina matatizo.

Sehemu za Ihefu, Kilosa,Mabwegere, Nkasi, Mpanda, Mvomero, Mwanga, Same,

Mikumi n.k. watu wameondolewa bila sheria kufuatwa. Japo sheria zipo wazi.

Watendaji wapo mstari wa mbele kuumiza watu kwa maamuzi mabaya bila kuwa

na madaraka hayo kisheria. Maamuzi ya viongozi wa hali ya juu – yanatishia

watu.

Wawekezaji walioacha maeneo miaka mingi wanaondoa wafugaji katika maeneo

hayo

Kuondolewa wafugaji maeneo mbalimbali

12

Hata ripoti ya „Control & Auditor General‟ imeonesha jinsi ambavyo fidia

haiwafikii wananchi.

Kesi ya NAFCO – tumeona zilianza muda mrefu – ranchi zinagawanywa kwa

watu wachache.

Kuna swala la viongozi kujitwalia ardhi na kuwakosesha wananchi haki yao

Lengo ni kuhakikisha hamna mtu anamiliki ardhi kubwa kuliko mwingine

Sheria haikulinda maslahi ya wananchi

Lengo la sheria ya ardhi ni kuhakikisha ardhi inagawanya kulingana na vigezo

vya matumizi

Watu wamehodhi ardhi kubwa huku wananchi wakigombania ardhi ndogo

Kiasi cha fedha kilitengwa kwa walioondolewa Ruaha National park –lakini fedha

hazijulikani zilipo.

Kuwe na taratibu na sheria zanazomsaidia mwananchi

Kuna tatizo katika mkakati wa utekelezaji wa sheria ya ardhi. Hata kwenye

mabaraza bado kuna migogoro mikubwa. Wale wanaotunga sheria hawazifuati.

3.1 Mambo yaliyojitokeza

Rushwa, Migogoro kati ya wakulima na wafugaji, Migogoro kati ya wakulima

wadogowadogo na wawekezaji, Matatizo ya fidia, Mgongano wa maslahi,

Sheria/matamshi ya siasa, Wafugaji kuhamishwa, n.k.

3.2 Matokeo

Umaskini, watoto hawaendi shule, huduma za elimu duni, kutumia nguvu bila sababu,

rushwa, watoto hawapati ada ya kwenda shule kutokana na wazazi wao kukosa mahali pa

kulima, mifugo ilikufa mingi, vurugu kwa mfano. Kilosa/Mpanda. Risasi zilitumika.

Uchomaji wa nyumba za wananchi – Kilosa, kutozwa faini na kuchukuliwa mali za

wananchi, zilioneshwa shuhuda na risiti ambazo wananchi wamelipishwa kwa kuweko

kwenye maeneo ambayo wana haki kuwepo. Uvunjaji wa heshima na haki za binaadam.

“Ukiuliza wafugaji waende wapi, nami nitakuuliza walitoka wapi”

3.3 Maswali na Maoni

Kama ilivyoelezwa, Ihefu – wananchi hawalipwi fidia. Je ni kiasi gani ambacho

hakijalipwa? Nini kimefanyika kuhakikisha wananchi wanapata haki yao?

Fact Finding – kama kweli wafugaji wanaonewa – serikali ina mpango

gain unaofanyika ili wafugaji wapate haki zao. Bado kuna maeneo watu

wanatakiwa wapate elimu. Tuangalie pande zote.

Pale Chuo cha Ardhi kuna „master plan na land use plan‟ vijijini.

Matatizo mengi yangeweza kuepukika kama hizi zingetumika vizuri.

Siasa inatawala kwa wataalam kwa sababu kama wataalam watafanya kazi

zao bila kuingiliwa na wanasiasa, tutaepuka migogoro mingi.

13

Utekelezaji wa Sheria – Hatua gani imechukuliwa kuhakikisha kwamba

serikali inasaidia kutekeleza sheria? Nini kifanyike ili kuhakikisha elimu

inatolewa. Kama elimu haitolewi, miaka kumi ijayo kutakuwaje?

Serikali inachangia ukiukwaji wa sheria. Jamii inaamini serikali lakini

wananchi hawapatiwi haki zao (fidia).

Mshiriki mmoja alisema Mada imelenga kwenye mapungufu tu – Je huu

ndio mtazamo wa Asasi za Kiraia? Watekelezaji wa sheria ni

serikali.halmashauri/CSOs au wote pamoja? Ardhi ya umma haiko chini

ya wana vijiji. Na anaamini yako mazuri pia ambayo inabidi kukiri.

Kuhusu swala la fidia, mwananchi alipwe kutokana na bei halisi ya soko.

Awepo mtoaji na mpokeaji. Thamani ya ardhi pia izingatiwe. Aidha

mhusika apewe fidia na kupewa eneo jingine sio kumlipa fidia bila kujali

atakwenda wapi.

Athari za kuhamishwa ziangaliwe. Chanzo ni nini. Je tathmini

imefanyika na ninapohamishiwa kuna fidia. Na je huduma ambazo

mwananchi alikuwa anapata alipokuwa atazipata aendapo?

Sheria kama ilivyo inasema fidia ifanywe kwa haki na usawa na kwa

wakati unaostahili. Sheria ya ardhi ya 2004 – thamani ya mazao

inatambuliwa. Hata kama kuna maendelezo. Kuna malipo ya usumbufu.

Usafiri wa Tani 7 kwa kilomita kama 20. Interest rate wa muda wa

malipo.Je madhara ya kuhamishwa ni yapi na faida ni ipi.

3.4 Maelezo kutoka kwa Mwasilishi

Fidia imezungumziwa kwa kina karibu na watoa mada wote na pia washiriki

wamechangia. Inawezekana ni hisia lakini wananchi wanalalamika ndio maana

tunazungumza. Labda ni hisia zangu lakini sio binafsi. Haya ndio yaliyojitokeza.

Je sheria imeshindikana. Kutekelezeka? Kulikuwa na matatizo ndio maana

sheria ikatungwa. Mengi yamewekwa lakini utekelezaji wake haupo.

Kwa kuongea tunatatua. Kwa mfano wananchi waende wapi? Nikijibu walitoka

wapi? Jinsi matamshi ya viongozi wa serikali yanavyokatisha tamaa – je

itawasaidia?

4.0 MADA - Uzoefu na Changamoto za mfumo wa Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi – Na Bahati Mlole, Msajili wa Mabaraza ya Ardhi – Wizara ya Ardhi.

Mtoa mada (B. Mlole) aliwafahamisha washiriki wa Kongamano kwamba mfumo wa

utatuzi wa migogoro uliundwa baada ya Tume ya Rais ikiongozwa na Prof. Shivji

kubaini kuwa kuna migogoro mingi ya ardhi. Ilipendekezwa kwamba chombo hiki

kianzie kijiji mpaka ngazi ya kitaifa. Aliainisha vyombo vya utatuzi wa migogoro kuwa

ni:

14

Baraza la Ardhi la Kijiji

Baraza la Kata

Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya

Mahakama Kuu – Kitengo cha Ardhi

Mahakama ya Rufaa.

Iliundwa (Land Disputes Courts Act) Sheria ya Utatuzi wa Migogoro No. 2, 2002

ambayo ilianza kutumika 1.10.2003. Haikuwezekana kuanza mapema kwa sababu

ilianza kanuni. Kwa hiyo tunapofanya tathmini, kipimo kiwe miaka 41/2 iliyopita.na sio

miaka 10 kama ilivyo sheria za ardhi. Migogoro mingi ya ardhi hasa kwa mijini

inatokana na kugawa sehemu moja kwa watu zaidi ya mmoja ama kwa kukosa

kumbukumbu au kwa makusudi. Aidha Maafisa Ardhi wa Wilaya hawana mamlaka ya

kufuta milki yeyote. Kwa upande mwingine wananchi pia ni chanzo cha migogoro.

Katika kuunda mabaraza Wizara inatoa kipaumbele kwa Wilaya zenye migogoro mingi

na ambazo zipo mbali na mabaraza ambayo tayari yanafanya kazi. Matatizo mengi na

migogoro yalianza kusikilizwa Novemba 2004.

Kwa.mfano migogoro ya upangishaji nyumba, wanandoa wanapogombea mali, kuweka

nyumba rehani n.k. Kwa miaka 41/2 kulikuwa na mashauri 38,023. Mashauri 20,374

yamepatiwa ufumbuzi na mengine yanaendelea kufanyiwa kazi.

Sheria inasema vyombo vya utekelezaji viimarishwe kuanzia ngazi ya vijiji mpaka Taifa.

Lakini chombo hiki kiko chini ya Wizara tatu, i.e. TAMISEMI, Wizara ya Ardhi na

Wizara ya Sheria na Katiba. Na wakati mwingine utekelezaji unachukua muda mrefu

japo kuna mwongozo wa mabaraza migogoro mingi hususan ile isiyosimamiwa na

mawakili inachukua wastani wa mwezi 1 hadi miezi 6. Kwa sababu hiyo wananchi

wengi wamefikia hatua ya kuongeza au kupunguza thamani za mali zao ili waweze

kufungua kesi katika Mabaraza ya ardhi na nyumba ya Wilaya badala ya kwenda katika

mabaraza ya kata au mahakama kuu – kitengo cha ardhi. Hii inadhihirisha kwamba

wananchi wanaelewa thamani ya ardhi. Pia mabaraza ya Kata/Vijiji hayafuati sheria na

mara nyingi ni kwa sababu hayajaundwa kama inavyotakiwa.

Maafisa ardhi wazingatie sheria kwa kufuata waraka wa TAMISEMI. Wananchi pia

washirikishwe kuchangia hoja.

Wakurugenzi waelekeze sheria

Swala la Elimu – vijiji ambavyo havina vitabu vya sheria waende kuchukua.

Changamoto kwa waliopo vituo vya sheria – kuwasaidia wananchi wanaokosa haki zao

kwa kutoelewa sheria.

4.1 Maoni na maswali kutoka kwa washiriki

Ardhi nchini kwetu haikuwa mali ya Taifa – imekuwa hivyo baada ya serikali

kuchukua hatua. Kuna wakati Kampuni fulani ya Belgium walikuwa na eneo

likaitwa lao na linaitwa Belgium bandarini. Mwl. Nyerere akataifisha.

15

Maana ya kusema tuna ardhi ya kutosha - si kweli. (Takwimu za Tz. Bara na

Visiwani) Inabidi tuishi na kufikiria watoto wetu wataishi vipi. Unapompa mtu

ardhi kwa miaka 99 kweli unajali vizazi vijavyo?

Mfano – uwekezaji 1966 Korogwe. Tatizo la kutoa ardhi bila kutizama kesho

ndio matatizo anayopata Rais Mugabe Zimbabwe.

Wafugaji – ukisema nataka ranch unapata – ukisema nataka sehemu ya malisho ni

tatizo. Tukitaka nchi yetu iwe na amani tutenge maeneo ya kutosha ya ufugaji na

kilimo.

Kupima vijiji na kugawa ardhi kwa wanavijiji ni muhimu.

Parapanda arts walisema tuzungumze. Rais Kikwete alisema ataunda serikali

inayosikiliza nasi tunasema serikali itusikilize.

Jambo la kusikitisha kusikia kwamba Rais anachukua ardhi ya wananchi.

Viongozi wa nchi ambao tumewapa madaraka wanachukua ardhi – wanawapa

watoto wao. Sheria inasemaje kuhusu hilo. Je wakubwa wako nje ya sheria?

Inavyotokea kwa mfano – Waziri Mkuu akijibu swali la John Cheyo

alivyomuuliza wafugaji wanapofukuzwa waende wapi na kujibu kwani wametoka

wapi. Ina maana hao – sheria zibadilishwe ili kila mtu aweze kurudi alikotoka?

Baraza la ardhi la Kata linashughulikia pia makosa ya jinai pamoja na migogoro

ya ardhi. Kesi inapowafikia ya ardhi inajinaishwa.

Fidia sio kweli fidia zinalipwa na serikali kuu. Wakati mwingine ni Halmashauri

husika.

Watendaji wanavunja Katiba na sio utekelezaji wa sheiria ya ardhi. Kama ofisi ya

ardhi haipo – au kijiji hakina masjala na Halmashauri za kijiji haziweki

kumbukumbu inakuwa vigumu.

Wawekezaji kuna kitu vijiji havijui. Wanataka mwekezaji apewe hati ya mila.

Vinginevyo akipewa hati ya kawaida ardhi inakuwa sio ya kijiji tena.

Wahariri/waandishi wa habari/watoa mada wasiogope mabosi. Unaposema someni

sheria? Wewe sheria hukusoma inayosema huyo mwananchi umlipe? Watu wa serikali

mnajipendelea. Tunapokuja tungeondoka tumeridhika lakini huduma haziridhishi. Haya

ni mawazo ya wananchi tunataka baraza la Taifa la Ardhi bila kubadilisha katiba – sheria

zitabadilishwaji?

4.2 Mwongozo kutoka Wizara ya Ardhi

Swala la Baraza la Kitaifa haliko katika mfumo wa mabaraza yaliyoongelewa

5.0 MADA – Utekelezaji wa Mipango ya matumizi Bora ya Ardhi, Uzoefu, Changamoto na mafunzo - Na Gerald Mango –

Mkurugenzi Mkuu, Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi

16

Misingi na malengo ya sheria ya mipango ya matumizi ya ardhi namba 6, 2007 ni

kuwezesha usimamizi na ufanisi wa matumizi ya ardhi yote nchini, kuwezesha wamiliki

na watumiaji wa ardhi kuwa na matumizi endelevu na uzalishaji bora katika ardhi, baada

ya kugundua kuwa vijijini hamna mwendelezo mzuri na wala uhakika wa milki. Pia

mpango huu unahakikisha maendeleo endelevu. Kuna jitihada ya kupambana na

uharibifu wa mazingira ya ardhi na vyanzo vya maji ambao unahusisha malengo ya

milenia, MKUKUTA na Dira ya Taifa. Pia kuboresha kilimo ili kuchangia pato la taifa.

Kuhakikisha hakuna uharibifu wa vyanzo vya maji kama ilivyotokea Bonde la Usangu.

Kuhakikisha upatikanaji maji ya umwagiliaji na nishati ya umeme.

Sera mbambuka za mipango ya matumizi ya ardhi

Mipango mbalimbali ilianzishwa kuhakikisha matumizi bora ya ardhi kama National

Environment Action Plans (NEAP), Sera ya Taifa ya ardhi 1995 – iliyolenga kuhakikisha

miliki za ardhi na kurahisisha umilikaji wa rasilimali ardhi kwa wananchi, Sera ya

Mazingira ya 1997, Kamati ya Mazingira ya Bunge, Sera ya Maafa, Sera muhimu za

rasilimali ardhi zilizoundwa k.m. madini, kilimo na mifugo, wanyamapori, uvuvi, misitu,

maji, nishati, makazi na miundombinu.

5.1 Mchango wa mawazo kutoka kwa washiriki

Vijiji vichache sana ndivyo vilivyofikiwa na mpango huu. Je kuna uhalali gani kuwa

mpango wa Taifa kama haujafikia sehemu kubwa?

Wanavijiji wamepewa majukumu makubwa na uwezo wao ni mdogo. Hawana hiyo

Land use plan. Tunachokosa hapa ni cost benefit analysis. Mwananchi wa chini

anaendelea kukandamizwa.

Sheria yetu ya ardhi inatoa kibali kiasi gani na ana masharti gani? Kwa mfano Malaysia

lazima kuwe na mzawa kama unataka kuwekeza. Sheria ya uwekezaji inashirikisha vipi

wazawa?

Wilaya zilizoko ndani ya mpango huu kwa mfano wafugaji wa Ihefu walipelekwa vijiji

kadhaa. Walipofika walishindwa kuendeleza ufugaji. Kwa sababu aina ya majani

haikufaa mifugo yao. Mnada haujawahi kuuza hata ngombe mmoja. Sehemu kama

Kisarawe kuna josho moja tu – Maeneo kwa ujumla hayafai yana mbung‟o wengi.

Namna gani wadau wanahusishwa? Je kuna utafiti uliofanywa kujua sababu kwa nini

hawaendi sehemu husika walikohamishiwa? .

5.2 Mchango kutoka kwa Mwasilishi wa Mada kutoka Wizara ya Ardhi

Ndugu Mango alikiri kuwa hiyo ni changamoto. Mkakati gani wa kutekeleza? Mafunzo

hayajafanyika.

17

Aliomba mashirika yasiyo ya kiserikali washirikiane na Wizara na Serikali kwa ujumla

kubadilishana mawazo kuona jinsi ya kutatua tatizo hili.

Mpango wa Taifa unatafsiri sera – sio utekelezaji. Tume inajenga uwezo wa

Halmashauri za Wilaya.

Wawekezaji – hatuamini uwekezaji toka nje. Tunasema Wizara ya Kilimo isitegee

wawekezaji wa nje. Hakuna atakayetekeleza haya. Watauza na kupeleka nje.

Mwekezaji ni mwananchi mwenyewe. Vijana wawezeshwe waendeleze Kilimo

wapatiwe pembejeo na vifaa vya kisasa vya kilimo kama tractor na ardhi ya kutosha. Hao

ndio wawekezaji tunaoongea.

6.0 MADA YA CRT - Elikaribu Gayemi, Ujamaa CRT Resource Trust

Hii inajumuisha wafugaji/waokotaji matunda.

Kuboresha maisha ya watu – kufundisha haki zao, kujenga uwezo wa watu, maisha yao

kwa kutumia maisha.

CRT iko Ngorongoro, Mbulu, Hanang, Simanjiro, Kiteto na Karatu.

Kazi kubwa ya CRT ni kutoa mafunzo ya sheria za ardhi ambazo hutoa mwongozi wa

kuendesha mikutano mikuu ya kijiji, matumizi bora ya ardhi, mabaraza ya vijiji, namna

ya kusimamia maliasili na utawala bora.

Pia uundaji wa sheria ndondogo ili kusimamia rasilimali. Kuchora ramani eneo la

mifuko, kilimo na makazi na kuwaelezea wananchi jinsi ya kupata vyeti vya kumiliki

ardhi.

6.1 Changamoto

Wananchi wanalazimika kugawa ardhi kufuata ramani za vijiji

Kuna mkanganyiko wa sheria ya ardhi ya vijiji na Sheria ya wanyamapori

Serikali mara nyingi hutumia nguvu iliyo nayo kuingilia mamlaka halali za vijiji

Upimaji wa vijiji ni gharama sana

Mara nyingine siasa hutumika badala ya sheria

Mara nyingi ardhi iliyotengwa kwa ajili ya wafugaji haiheshimiwi na ubinafsi

unatawala na inashangaza miaka kumi ya sheria za ardhi bado ardhi ya wafugaji

inatambuliwa kama ardhi isiyo na shughuli yeyote.(iliyo wazi) mfano Sukenya,

NAFCO, etc.

Wafugaji bado hawatambuliwi kama wachangiaji wa uchumi wa taifa

18

Bado utumiaji wa ardhi kwa wafugaji unaangaliwa kama sio mzuri na matokeo

yake wafugaji wanahamishwa mara nyingi bila kujali sehemu wanazokwenda.

Mfano mzuri ni wa Kilosa

Wakati umefika kwa Serikali kutambua kwamba wafugaji ni muhimu kwa uchumi wa

Taifa na kuelewa kuwa kubinafsisha ardhi ya wafugaji ni kukataa kwamba ardhi ya vijiji

hivyo sio ya wananchi wa sehemu hiyo ambao ni wafugaji. Kuna haja ya kufanya utafiti

wa kujua wafugaji wanaishije na kutafuta njia ya kuwaingiza katika mpango mkakati wa

mipango ya kuendeleza taifa.

6.2 Mawazo ya washiriki

1. Tanzania tuna tatizo kukubali ufugaji asilia ni ufugaji endelevu. Shinikizo serikali

iwepo sera kutambua ufugaji asilia kama ni mfumo wa maisha.

Usalama wa maeneo ya ufugaji ngazi ya vijiji ni mdogo au haupo

Kufanya utaratibu wa vijiji vinavyopakana vyenye matumizi ya pamoja wapange

mipango yao pamoja

Benki ya ardhi tumeambiwa ipo, nani anaweza kujua kuna nini ndani ya benki

hiyo isije ikawa watu wanahangaika kumbe ardhi wanayohaingaikia iko kwenye

benki tayari

2. Matatizo ya wafugaji – watendaji wamekubali wamekosa. Kuna sheria gani na

fidia gani imetolewa kwa mfano mfugaji mmoja aliuziwa ngombe wake badala ya

shs. Laki tatu kwa ngombe waliuzwa 8,000/= Hii ni upotevu wa mali na ni

uhalifu pia.

3. Wanakijiji wanawapa wawekezaji ardhi na baadae hao wawekezaji wanapata hati.

Ardhi mwanzoni ilikuwa ya kimila na baadae inabadilishwa kuwa ya hati. Na

anakuja kiongozi na kusikia haya anakaa kimya.

4. Ufugaji – kuna upungufu wa malisho, Ni matatizo makubwa. Zamani kulikuwa

na utaratibu wa sheria – kupunguza wanyama ambao hawana afya sijui siku hizi

vipi Na je, ili kuweza kuepuka migogoro ni vigezo gani vitatumika?

5. Wanaopanga ni watu husika. Wanakubaliana. Wanatakiwa wawepo wakulima.

Eneo endelevu – Kigezo ni mazingira. Timu ni kukusanya takwimu ya matumizi

ya baadae. Wakati mwingine wafugaji hawafiki kwenye mikutano matokeo yake

mipango inapangwa na watu wengine.

Mwekezaji kupata ardhi

Mfano Kituo cha uwekezaji (TIC) ili apate ardhi lazima kuwe na raia - asilimia 51%.

Kuna wageni wajanja akishaoa anakuwa amehalalishwa. Na kwa kijijini lazima

kuwe na muhtasari wa Halmashauri kwanza. Lazima kijiji kiwe na Land Plan.

Sasa hivi maombi mengi yamekwama kwa sababu hiyo. Ili Rais ahamishe milki

lazima mwekezaji aende kijiji husika aelezee manufaa ya umma yatakayopatikana

na uwekezaji wake – Maelezo yanaenda kwa Commissioner wa Ardhi naye baada

ya kuridhika yanapelekwa kwa Rais.

6.3 Nafasi ya Mwanamke katika umiliki wa ardhi

19

Sheria za ardhi na sera zimetoa fursa kwa wanawake. Tumepiga hatua. Kiwango

cha haki hamna mafanikio sana – kuna mila ambazo zimeshindwa kumkwamua

mwanamke.

Wajane na waume wapya – analazimishwa kuolewa ili arithi mali za mume wake.

Hii ni tabia hatarishi hasa maambukizi ya magonjwa n.k.

Maswali na maoni ya washiriki

Ni kweli wanawake wananyanyasika. Mfano toka Kilombero.

Wanawake wa Datooga-Iraqw pia mila zinawaumiza. Wanafanya kazi nyingi shambani

na kufuga lakini hawarusiwi hata kushiriki katika mipango ya fedha zinatopatikana

kutokana na jasho lao.

Uzoefu - tulipotoa elimu ya miliki bado desturi zinashida. Katika sehemu nyingine

kumetolewa elimu ya umilikaji wa ardhi kwa wanawake. Katika vijiji vingine upimaji

wa mashamba kwa ajili ya wote – wanawake na wanaume umefanyika ili kuwapa

wanawake fursa ya kumiliki ardhi.

Uwakilishi kwenye mabaraza – wakina mama hawajajengewa uwezo. Kama uwakilishi

hauleti maslahi kwa wenzao.

Ukweli ni kwamba makabila mengi nchini bado yana mila potofu. Makabila mengine

ukoo ni kwa mama kwa hiyo hao ni rahisi wanawake kumiliki ardhi.

Kuna mambo mengi yanakwamisha hili, mahari ni tatizo kubwa tu. Kwa mfano

wasukuma. Kama tumeweza kubadilisha maneno – kwamba wanawake huolewa na sio

kwamba watu huoana. Mwanamke anatumikia mahari aliyolipiwa. Unyanyapaa

umezidi. Wanawake wakiwezeshwa kama wanavyopewa viti maalum wawekewe mfuko

maalum. Ni bora wananchi wenyewe wakasimamia matumizi ya ardhi. Jukumu

alilopewa Rais ni kubwa mno. Watendaji wake wanamchezea. Uhawilishaji – tulisema

kuhawilisha ardhi inaweza kuleta matatizo. Kila inapotokea matatizo ya ardhi wanavijiji

ndio wanaoumia na sehemu kubwa ya waTanzania wanaishi vijijini (80%).

Vipande vitakavyotolewa havina maana. Ardhi ya watu ikitakiwa inachukuliwa. Hakuna

mwananchi wa Tanzania anayekalia nje ya utaratibu wa sheria.

Tuna benki – ziada ya pesa ipo – wanaitoa wapi. Sehemu kubwa ni ya wananchi.

Wananunua dhamana za serikali (government bonds). Hiyo hiyo ya umma inanunua –

pesa inamlipa mlaji – ambazo ni zetu. Kuna viini macho vinafanyika.

6.4 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi – HAKIARDHI, Dkt. Ng’wanza Kamata

20

Akichangia mada alisema uundwaji wa sheria 1999 – sheria 2001 ilianza kutumika.

Mabenki yamesema sheria haijakaa vizuri kuwawezesha kukopesha. Mh. Mkapa

akasema nimeshinikizwa sana. Msukumo ulitoka wapi – haukutoka kwa wananchi.

7.0 SIKU YA TATU 29/05/2009

Kongamano lilianza kwa Washiriki wote kujiandikisha saa 3.00 asubuhi.

Hii ndio ilikuwa siku rasmi ya kufunga kongamano hili lililoishi kwa jumla ya siku tatu.

Katika siku hii mada mbali mbali pia zilijadiliwa kwa mapana na marefu lakini kubwa

zaidi kwa siku hii ilikuwa ni kupata uzoefu kwenye masuala ya ardhi uliotolewa na

wawakilishi wa asasi zinazoshughulika na masuala ya ardhi kutoka nchi za Kenya,

Uganda na Rwanda.

7.1 Uzoefu kutoka Kenya kwenye Masuala ya Ardhi - Mwasilishi: Odenda Lumumba

Katika kuwasilisha uzoefu huu, mwasilishi aligusia mambo mengi sana kuanzia kwenye

ngazi ya mwanakijiji, mwananchi wa kawaida, taasisi za kiraia na za kibinafsi na serikali

kuu na zile za mitaa kwenye suala zima la kuhakikisha kuwa watu wote wa nchi husika

wanafaidika na rasilimali hii muhimu ya ardhi. Mwasilishi pia aligusia udhaifu uliopo

kwenye mifumo ya kusimamia ardhi ndani ya nchi za Afrika ya Mashariki. Pia hakusita

kuzungumzia uimara wa mifumo hii pale tu itakapoweza kutumika vyema na kuwa

chachu ya kuwaletea maendeleo endelevu Wananchi na sio wageni wanaokuja ndani ya

nchi zetu kutengeneza Faida kubwa ya ziada wakati wananchi wakiwa hawana hata hiyo

akiba ya kuanzia.

Mwasilishi aliendelea kwa kusema yafuatayo:

Suala la ardhi kamwe haliwezi kubadilika ikiwa wale wasomi wachache

wanaotuongoza kwenye nchi zetu hawatobadilika. Viongozi wetu ndio

waliotufikisha hapa tulipo leo, ambapo Wananchi wengi hawana ardhi ya kutosha

kwaajili ya makazi na kilimo. Mfano mzuri ni nchini Kenya ambapo inaaminika

kuwa Wananchi wa tabaka la juu walioko kwenye serikali, mashirika ya umma na

wamiliki wa makampuni makubwa ndio wanaomiliki maeneo makubwa ya ardhi

wakati Wananchi wa kawaida wakiwa wamejikusanya kwenye maeneo

yaliyofurika watu na nyumba zisizo na mpangilio sahihi (squatters) wakiwa na

vijipande vya maeneo ya kukaa.

Taasisi kubwa za kigeni mfano Shirika la fedha duniani (IMF) pamoja na Benki ya dunia

(WB) ndio zimekuwa na sauti kubwa sana kwenye maamuzi ya nchi zetu za kiafrika.

Sauti hii imepelekea viongozi na wataalamu wetu kusubiri hadi sera na sheria zetu

ziidhinishwe na mashirika haya ndio zianze kutumika. Na kwa kiwango kikubwa

mashirika haya yamekuwa yanazilazimisha serikali zetu kufuata yale ambayo

yatawanufaisha wawekezaji kutoka nje ya nchi. Mfano mzuri ni sera ya ardhi ya nchi ya

Kenya ambayo imekaa sasa takribani miaka saba (7) pasipo kupitishwa kutokana na

shinikizo la mashirika haya. Pia kuna mifano kama ya nchini Zimbabwe ambapo baada

21

ya serikali kupitisha mfumo ambao hungewasaidia wazawa kumiliki ardhi kupitishwa,

nchi hiyo imewekewa vikwazo vya kiuchumi na nchi nyingi za Ulaya na Amerika.

Kuhusiana na suala la Shirikisho la Afrika ya Mashariki na suala zima la umiliki

wa ardhi kwa pamoja. Hapa jambo kubwa linalotakiwa kufanywa na serikali zetu

ni kuwajengea imani ya kutosha wanachi wa nchi zote kuwa hakuna yeyote

atakayepoteza haki yake kwenye ardhi aliyokuwa anamiliki. Pia serikali za nchi

zote inabidi kuwaeleza wananchi kuwa hakuna ardhi ya nchi moja itakayovamiwa

na wanchi wa nchi nyingine kwa kisingizio cha kuwa kuna ardhi nyingi na ya

kutosha. Mfano mzuri ni wasiwasi walionao Wananchi wa nchi ya Tanzania kuwa

kuifanya ardhi iwe ya pamoja kutapelekea wao kupoteza ardhi yao ambayo

wameitunza kwa miaka mingi sasa. Wananchi wa pande zote za Shirikisho la

Afrika Mashariki watakuwa katika nafasi nzuri ya kufanya maamuzi yatakayo

kuwa na manufaa kwa pande zote.

Nchi za Afrika ya Mashariki sio masikini kwa maana ya rasilimali, ni matajiri

sana lakini ufukara wetu upo ndani ya viongozi wetu tuliowachagua na kuwateua

kuongoza sekta muhimu mfano za ardhi, madini, wanyamapori, misitu, maji na

nyinginezo nyingi. Viongozi hawa wamekuwa wakiwajali sana wageni

wanaokuja kwa majina ya wawekezaji na kusahau kuwawezesha Wananchi

wazawa ili waendeleze uchumi wa nchi yao.

Wageni kutoka ng‟ambo wamekuwa wakipewa hakimiliki za ardhi na serikali

zetu wakati huo huo wenyeji wakibaguliwa waziwazi. Wenyeji hawaonekani

kama wana uwezo wa kuwekeza kama hawa wageni kutoka Ulaya, Amerika,

Uarabuni na Asia.

Sheria nyingi hasa kwenye maeneo ya ardhi, madini na wanyamapori

zinaonekana kama vile zimewekwa kwa lengo moja tu la kumnyanyasa mwenyeji

dhidi ya matajiri na wageni. Ukiangalia hata kwa nchi kama Tanzania

wanaolalamika kudhulumiwa ardhi zao na viongozi wakubwa ni wananchi na

wakulima wadogo wadogo walioko vijijini. Lakini wakati huo huo kuna sheria

namba tano (5)ya ardhi ya mwaka 1999, Sheria ya Ardhi ya Vijiji. Sasa inakuwa

ngumu kuelewa kwanini bado huyu mwanakijiji anaendelea kudhulumiwa haki

yake wakati kuna sheria zilizotungwa kumlinda.

Serikali za Afrika ya Mashariki zimekuwa na kisingizio kuhusiana na kinachoitwa

soko huria. Viongozi wetu wanasema kuwa kinachoharibu uchumi na umiliki

wetu wa ardhi ni soko huria. Lakini ukweli ni kuwa soko haliwezi kujiendesha

pasipo sisi wenyewe kutaka nini kifanyike. Soko siku zote huelekezwa na sio

lenyewe kutuelekeza sisi. Soko hili ndio lililopekea watu wachache kujilimbikizia

ardhi na rasilimali nyingine nyingi kutokana na wao kumiliki uchumi wa nchi.

Tatizo la ukabila pia bado ni kubwa sana kwenye nchi zetu za Afrika ya

Mashariki. Kumekuwepo na mapigano ya mara kwa mara kwenye baadhi ya

makabila yakigombania ardhi kwenye mipaka yao. Mfano mzuri ni nchini Kenya

22

ambapo mara kwa mara kumekuwa kunaibuka mapigano yanayohusianisha

makabila mbali mbali. Lakini hata nchini Tanzania kumekuwepo na mapigano

haya kwa miaka ya karibuni tofauti na kipindi cha utawala wa Rais wa kwanza

Hayati Mwalimu Julius Nyerere. Mapigano haya yamekuwa yanapelekea

uharibifu wa mali ndani ya ardhi pamoja na Wananchi kuyakimbia maeneo yao.

Swali la kujiuliza hapa ni kwamba ikiwa nchi za Afrika Mashariki zinafanana

sana kwenye maeneo mengi ya mifumo ya kumilki ardhi, iweje leo shirikisho la

Afrika Mashariki lishindwe kuundwa kutokana na suala la ardhi?. Kuna mambo

mengi sana yanayofanana kuliko yale yanayotofautiana. Mfano kwenye kumilki

kimila ni Uganda pekee ambayo haina umiliki huu lakini nchi nyingine zote zina

mfumo huo. Suala la dola kumiliki rasilimali linafanana kwa nchi zote. Tofauti

kubwa ni kwenye milki ya hatima (radical titles) kwani kwa Tanzania mamlaka

hiyo iko chini ya Rais wakati kwa Kenya na Uganda ipo chini ya Wananchi.

7.1.1 Mwasilishi wa mada pia alifafanua mambo ya muhimu na ya kuzingatia kwa

nchi za Afrika ya Mashariki katika kulinda rasilimali za nchi zao husika. Mambo

haya ni kama yafuatayo:-

1. Taasisi zetu za kiraia ndizo zenye jukumu la kulinda rasilimali za nchi zetu.

Taasisi hizi zina jukumu la kuwaelimisha Wananchi umuhimu wa kuzilinda

rasilimali hizi kwa kuzishinikiza serikali zetu kuweka sera na sheria

madhubuti za kulinda rasilimali hizi. Pia kuna kila sababu ya taasisi hizi

kuwaonyesha Wananchi kuwa wanazo sababu za kuomba ushirikishwaji

kwenye maamuzi yanayohusiana na rasilimali zao mfano ardhi na madini.

2. Suala la mipaka linapelekea kukosekana kwa ujirani mwema baina ya nchi za

Afrika Mashariki. Kumekuwa na migogoro mingi baina ya nchi hizi na

mifano mizuri ni baina ya Uganda na Kenya ambapo kwa sasa kuna

kukosekana kwa amani kwenye mpaka baina ya nchi hizi kwenye eneo la

Migingo. Pia hapo kwenye miaka ya 1970 hali hii ilishatokea baina ya

Tanzania na Uganda; pia miaka ya karibuni kumekuwa na mgogoro kwenye

mpaka wa Rwanda na Uganda. Migogoro ya aina hii ni ya kushughulikia kwa

umakini wa hali ya juu ili isiathiri kuundwa kwa shirikisho la Afrika ya

Mashariki.

3. Kuwepo na mabadiliko ya dhati kwenye taasisi na idara za kiserikali kama

nchi za Afrika Mashariki zinataka mabadiliko ya dhati kwenye kuleta ulinzi

wa rasilimali za nchi hususani ardhi na madini. Ni kweli kabisa kuwa idara za

serikali zinachangia sana kwenye kubinafsisha rasilimali za nchi kwa wageni

ambao wanakuja kwa majina ya wawekezaji. Ndio maana kuna kila sababu ya

kufanya mabadiliko ya kitaasisi pamoja na ya watendaji ndani ya taasisi hizi.

23

7.2 HITIMISHO

Ardhi ndio suala lililo mbele ya uundwaji wa shirikisho la Afrika Mashariki. Ni suala la

kuzungumza na kufikia muafaka ili liondoe ugomvi na vita hapo baadae baina ya nchi

husika.

Ni suala la wazi na la msingi sana kwa kila mtu, taasisi, serikali na kila kikundi pasipo

kujali itikadi za kisiasa, kidini au kikabila. Wananchi wajipange kwa sababu eneo la

Afrika Mashariki linahitaji ukombozi. Hili vuguvugu la ukombozi inabidi lianzie

Tanzania na kwenda nchi nyingine. Tuangalie isije kuwa muongo huu mmoja sio kwaajili

ya Faida ya watu wote ila Faida kwa watu wachache wenye elimu na ujanja wa kutumika

mamlaka za serikali watakavyo wao.

7.3 Maswali kwa upande wa Kenya

1. Tueleze uzoefu wa MKURABITA kwa nchi ya Kenya?

2. Ni jambo zuri kuwa na ardhi ya pamoja Afrika Mashariki lakini wananchi wa

Tanzania tunasita kwasababu tupo wengi na nchi hizo nyingine hazina ardhi ya

kutosha kwa sehemu kubwa kutokana na mifumo yao ambayo ina utofauti Fulani

na Tanzania. Halafu pia kuna tatizo la uwekezaji kwenye ardhi ya Tanzania

jambo linalotupa wasiwasi wa kuendelea kupoteza ardhi yetu?

3. Wakati Tanzania tuna ardhi ya jumla kwenye maeneo ya mijini na vijijini. Lakini

kwa Uganda, Kenya na Rwanda hawana ardhi ya aina hii. Je, huoni kuwa

litakuwa tatizo kwa upande wa Tanzania?

4. Pia kiuchumi Tanzania iko nyuma ukilinganisha na Kenya. Je, huoni suala la

kuacha ardhi iwe wazi itapelekea kudidimiza zaidi uchumi wetu?

7.4 Majibu

Mwasilishi alijibu maswali haya kwa kifupi na kwa ujumla kama ifuatavyo.

Tuache suala la kuwatenga Wakenya kwenye ardhi. Kwa sababu lazima tujue

kuwa ni nani hasa tunayemtenga. Mbona tayari familia za matajiri tayari zina

maeneo makubwa ya ardhi hapa nchini Tanzania maeneo ya mkoa wa Arusha.

Kwahiyo kukataa kwenu Watanzania kuwa na ardhi ya shirikisho ni kuwazuia

wanyonge wengi kutoka Kenya na sio wale matajiri wakubwa ambao tayari wana

maeneo makubwa tayari nchini Tanzania.

24

8.0 Uzoefu wa Uganda kwenye masuala ya ardhi - Mwasilishi: Esther Obaikol

Mwasilishi ni Mkurugenzi wa Taasisi ya masuala ya ardhi ya nchini Uganda yaani,

Uganda Land Alliance (ULA). Mwasilishi katika uwasilishi wake alizungumzia masuala

mengi yanayohusiana na ardhi nchini Uganda na Afrika Mashariki kwa ujumla. Baadhi

ya mambo muhimu aliyoyagusia ni pamoja na yale mambo yanayoendelea

kushughulikiwa kwenye sera na sheria za ardhi nchini Uganda. Baadhi ya mambo ya

muhimu sana yaliyopo kwenye mchakato huo ni pamoja na:-

Kuandikisha maeneo ambayo yameachwa na wakoloni lakini bado hayamilikiwi

na wananchi wa kawaida. Hii itasaidia kila mtu kumiliki ardhi.

Kuangalia makundi madogo na wafugaji ili wapate ardhi ya kutosha. Kwa sasa

makundi haya yanapata tabu kwenye kupata ardhi ya matumizi.

Utatuzi wa migogoro kwenye jamii zinazohama hama kutoka eneo moja kwenda

eneo jingine. Mfano jamii za Kimaasai na Karamajong”.

Kuimarisha mila kwenye utatuzi wa mogogoro ya ardhi kwa kuimarisha vyombo

vya kimila kwenye maeneo husika. Hili ni suala muhimu sana kwani litasaidia

kwenye kumaliza migogoro mingi inayoibuka katika maeneo ya vijijini.

Utambuzi wa haki za wanawake kama wazalishaji wakubwa kwenye ardhi na

kuanzia ngazi ya familia, ukoo na taifa kwa ujumla. Kutambua umilki wa ardhi

kwa wanawake kutapelekea wao kuwa na nguvu kubwa kwenye ardhi na kuipatia

jamii maendeleo makubwa.

Kuingiza suala la jinsia kwenye utawala na usimamizi wa ardhi kwa njia ya

kimila. Hii itasaidia kuepuka unyanyaswaji na uonevu wa kundi moja dhidi ya

kundi jingine. Na inaaminika kuwa kuwepo kwa usawa baina ya makundi ya

kijinsia kutapelekea uzalishaji kuongezeka kwa hali ya kuridhisha zaidi.

8.1 Changamoto kwa taasisi binafsi

Mwasilishi kwa kuuchukua uzoefu wake wa nchini Uganda pia alielezea kwa undani

changamoto nyingi zinazozikabili taasisi za kibinafsi kwenye maeneo yao ya kazi.

Changamoto hizo ni kama zifuatavyo

Kuna siasa nyingi sana kwenye masuala ya ardhi nchini Uganda jambo

linalopelekea kukosekana kwa muafaka kwenye usuluhishi wa kesi za ardhi. Hii

imechangiwa sana na Viongozi wa serikali kuingilia masuala yanayohusiana na

ardhi kwa masilahi yao binafsi na familia zao.

25

Kukosekana kwa sera na sheria za mazingira kitu kinachopelekea kuwepo na

ugumu katika kuwabana wale wanaoharibu mazingira ambao wengi wao ni

wamiliki wa makampuni makubwa na viwanda vikubwa.

Wananchi wengi wana uelewa mdogo wa masuala ya muhimu ya kijamii

yanayowaathiri wao na maisha yao hali inayopelekea kudhulumiwa haki zao

za kimsingi. Uelewa huu mdogo unasababishwa na juhudi ndogo za serikali

katika kuwaelimisha wananchi kuhusiana na sera na sheria mbalimbali.

Kukosekana kwa habari za kutosha na za uhakika kuhusiana na masuala ya

ardhi kwa wananchi hasa wanaoishi maeneo ya vijijini.

Mfumo mfu wa haki za ardhi nchini Uganda kutokana na waongozaji wabovu

kutoka serikalini.

Mwamko mdogo kwenye masuala ya ardhi kwa wananchi wa Uganda.

8.2 HITIMISHO

Kimsingi changamoto na matatizo kwenye masuala ya ardhi ni mengi sana kwenye nchi

za eneo la Afrika Mashariki na hayatofautiani kwa kiasi kikubwa sana kutoka nchi moja

hadi nyingine. Kwahiyo kuna kila sababu ya wananchi wa pande zote mbili kukaa na

kuyaangalia kwa makini masuala haya na kuweka mustakabali wa kudumu kwenye

kulinda ardhi na rasilimali nyingine kwenye ukanda huu.

9.0 Uzoefu wa Rwanda kwenye masuala ya ardhi - Mwasilishi: John Muyenzi

Mwasilishi alizungumzia mambo mengi sana yanayohusiana na ardhi ya nchi ya Rwanda

na mgawanyo wake kwa wananchi wa nchi yake. Pamoja na hayo alizungumzia pia

matatizo yanayoikumba sekta ya ardhi nchini Rwanda akihusianisha na eneo zima la

Afrika Mashariki. Rwanda ina jumla ya 26, 338 skwea (square) kilomita na ina jumla ya

watu 10, 473,282

9.1 Uzoefu katika kutengeneza na kutekeleza sera na sheria za ardhi

Mwaka 1999 kulikuwepo na kongamano la kimataifa lililoenda kwa jina la Land and

Villagelization, taasisi ya RISID ndio walioandaa kongamano hilo. Ni kutoka katika

mapendekezo ya kongamano hili ndipo serikali ilipoyachukua na kuyaingiza kwenye sera

ya sheria ya ardhi. Katika mapendekezo haya mambo ya kimsingi yaliyochukuliwa na

kuingizwa kwenye sera hii ni kama vile:-

Wanawake walipata uwezo wa kupata na kumiliki ardhi sawa na wanaume

kwenye familia zao au/na pale anapofariki mume.

26

Watoto wote wakawa na uwezo sawa wa kupata na kumiliki ardhi toka kwa

wazazi wao kwa njia ya kurithi au kupewa kama zawadi au sehemu ya mali

stahiki kama sehemu ya familia.

Mwaka 2004 ndio sera ya ardhi ilipotungwa na kupitishwa na mwaka 2005 sheria ya

ardhi ilipitishwa. Sheria iliyoitwa Organic Land Law ambayo pamoja na mambo mengine

inalinda ardhi zote za kimila na hati. Hakuna unyanyasaji wa kijinsia katika kumiliki

ardhi. Mume na mke wana haki sawa katika kumiliki ardhi. Mtoto wa kike na kiume

wana haki sawa ya kupata na kumiliki ardhi.

Kazi za sasa zinazofanywa na serikali ya Rwanda kwenye sekta ya ardhi

Mgawanyo wa ardhi kwenye eneo la Jimbo la Mashariki ya Rwanda, kwenye

mikoa ya Nyagatare, Gatsibo, Kirehe, na Kayonza.

Mpango bora wa matumizi ya ardhi kwenye maeneo ambayo hayajafanyiwa

mpango huu ili kuilinda ardhi kukaa bure pasipo na matumizi yanayoeleweka.

9.2 Changamoto zinaoikumba sekta ya ardhi nchini Rwanda

Watu wengi wanategemea ardhi kidogo kwaajili ya makazi na kilimo. Hii ni

kutokana na kuwa ardhi ya Rwanda ni kidogo ukilinganisha na idadi ya watu

waliopo Rwanda.

Ndoa za mitala bado ni eneo linaloleta utata katika umiliki wa ardhi nchini

Rwanda pamoja na kwamba kuna sera na sheria ya ardhi. Wanaume wa Rwanda

wamekuwa wakiongoza kwa kuoa wanawake wengi wakati ardhi waliyonayo ni

kidogo jambo linalosababisha matatizo makubwa linapokuja suala la urithi.

9.3 Maswali

1. Rwanda ina mpango gani kwenye kasi ya ongezeko la ongezeko la watu

ukitegemea kuwa eneo la ardhi waliyonayo ni dogo sana ukilinganisha na idadi ya

watu?

2. Kuna mpango wowote wa serikali ya Rwanda kutambua watu wanaomiliki ardhi

kwa majina tofauti tofauti?

9.4 Mwasilishi wa mada alijibu Maswali haya kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Kimsingi siwezi kusema kuwa Rwanda tuna sera ya uzazi wa mpango. Ila serikali

iliyopo madarakani kwa sasa inasema kuwa nchi ya Rwanda haina rasilimali

kama vile madini n.k kwahiyo watu wake ndio rasilimali yake muhimu zaidi

katika kujiletea maendeleo.

Pia ni kweli kabisa kuwa asilimia tisini (90%) ya Wanyarwanda wote

wanategemea kilimo. Kwahiyo serikali inajaribu kuwaambia watu wajiondoe

kwenye kilimo na kutegemea sekta nyingine ili kukuza uchumi wa nchi kwa kasi

nzuri kwa njia ya utegemezi wa kisekta kama vile viwanda n.k.

27

Lakini pia mfumo wa Rwanda hauruhusu wageni kupewa ardhi kwa kiwango

kikubwa kwa sababu moja kubwa ambayo ni uhaba wa ardhi hiyo ambayo hata

wananchi wake wenyewe haiwatoshelezi kwa kiwango kinachotakiwa.

10.0 Mjadala wa mchana

Baada ya chakula cha mchana na kabla ya kufunga kongamano Washiriki walikaa kwa

Majadiliano ya jumla. Lengo la Majadiliano hayo likiwa ni kupata uelewa wa jumla wa

nini Washiriki walichojifunza kwa muda wa siku zote tatu. Washiriki katika mjadala huu

waliangalia katika mada zote zilizowasilishwa kwenye kongamano. Katika mjadala huu

masuala yafuatayo yalijadiliwa:-

1. Suala la ardhi ni suala ambalo linahitaji kuzungumzwa kwa umakini mkubwa

sana hasa suala la kuwepo na ardhi ya Shirikisho la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Watanzania ni lazima kwanza wajitosheleze wenyewe na kuridhika kuwa wana

ardhi ya kutosha ndipo wenzetu wa nchi za jirani waanze kufikiriwa ni maeneo

gani watapata.

2. Inawezekanaje Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi kukopesha pesa

wafanyakazi wa umma? Je wao ni benki ya mikopo?. Serikali lazima ingalie

uwezekano wa kila raia wa Tanzania kujipatia mkopo huu wa kuwawezesha

kujijengea makazi yao ya kudumu pasipo kuwepo na ubaguzi wa raia huyu

anafanya kazi katika sekta ya umma au ya binafsi.

3. Kwa jinsi upimaji huu wa viwanja unavyofanywa hasa kwenye maeneo ya jiji la

Dar es Salaam, inaonekana wazi kabisa kuwa unafanywa kwa manufaa ya watu

wachache ambao wana pesa zao kuliko kufanywa kwa manufaa ya wananchi wote

wa Tanzania bila kujali uwezo wao wa kipesa au kivyeo.

4. Zilipotungwa sera na sheria za ardhi za mwaka 1995 na 1999 kwa mfuatano huo

wananchi wengi wa Tanzania walijua sasa wamepona na uonevu waliokuwa

wakifanyiwa na watu waliokuwa na uwezo wa kipesa na kielimu. Lakini leo

tunaadhimisha miaka kumi ya sheria za ardhi namba nne (4) na namba tano (5) za

1999 bado wananchi wanaendelea kuteseka kwa kiwango kikubwa zaidi. Kwanza

kwa mtazamo wa kina zaidi utagundua kuwa matatizo kwenye sekta ya ardhi ndio

yameongezeka zaidi hasa baada ya kuanza kuingia hawa wanaoitwa wawekezaji

kwenye ardhi ya kijiji na kukingiwa kifua na serikali kuu na serikali za mitaa

wakati wananchi wa kawaida wakibaki bila ya kuwa na usaidizi wa aina yoyote

ile.

28

11.0 MAAZIMIO YA KONGAMANO

Siku ya mwisho ya kongamano wawasilishi pamoja na Washiriki walikaa kwa pamoja na

kujadiliana kwa kina yale yote waliyoweza kukaa na kuyapata ndani ya siku zote tatu za

kongamano hili la maadhimisho ya miaka kumi (10) ya sheria za ardhi za mwaka 1999

nchini Tanzania. Maazimio haya yalifikiwa kwa lengo moja tu nalo ni kuyatekeleza yale

yote ambayo wataazimia hapo na kuwa ndani ya waandaaji, yaani taasisi za

(HAKIARDHI na PINGOS FORUM), serikali ya Tanzania pamoja na Washiriki wote

kila mmoja kwa nafasi yake. Maazimio hayo yaliyofikiwa ilikuwa kama ifuatavyo:-

11.1 Ushiriki wa wananchi na wanavijiji katika maamuzi yanayohusiana na ardhi hususani kwenye ngazi ya vijiji. Nini kifanyike?

Washiriki walichangia kama ifuatavyo:-

Tupange ni kwa jinsi gani wanavijiji wanaweza kufahamu masuala muhimu na ya

Kimsingi yanayohusiana na ardhi kwenye vijiji vyao kwa mujibu wa sheria

zilizopo.

Suala sio kutoeleweka kwa mfumo wa sheria za ardhi. Ila tatizo kubwa ni

kwamba mifumo hii ilianzia juu kwenda chini ndio maana wananchi wengi

hawayaelewi kwa undani masuala haya yanayohusiana na sera na sheria za ardhi.

Kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria na maamuzi halali ya wananchi

kunakofanywa na baadhi ya Viongozi wasio waadilifu na walio mafisadi wa

rasilimali za nchi yetu ya Tanzania hasa hasa kwenye sekta ya kilimo.

Kumekuwa hakuna utatuzi wa dhati wa migogoro ya ardhi nchini hasa kwenye

maeneo ya vijijini toka mwaka 1995. Hali hii imetokana na kutoshirikishwa kwa

wananchi kwa kiwango kinachoridhisha kutoka ngazi ya wilaya hadi ya kijiji.

Viongozi wamekuwa wakifanya maamuzi ya kibabe pasipo kujali masilahi ya

wananchi walio wengi.

Wanavijiji wapelekewe mafunzo ya katiba na sheria mbalimbali ili kufahamu haki

zao za Kimsingi. Mafunzo haya yaanze kutolewa kuanzia ngazi ya shule ya

msingi na kuendelea.

Ikumbukwe pia kuwa taasisi za kiraia na taasisi za kidini zina jukumu kubwa sana

la kutoa elimu ya kiraia kwa wananchi hasa wa mikoani na vijijini ambao

inaonekana kama wamesahauliwa na serikali. Ingawa serikali inatakiwa ijue kuwa

ni jukumu lake kutoa elimu kwa wananchi wake.

Wanawake hasa wa vijijini wanatakiwa kuelimishwa kuhusiana na haki zao za

Kimsingi ili waweze kushiriki kikamilifu kwenye mfumo mzima wa kutoa

maamuzi yanayowagusa kuanzia ngazi ya familia hadi ya kijiji ili waweze

kufaidika na sheria mbalimbali Mfano wa sheria za ardhi za mwaka 1999, namba

29

4 na 5. Hii imetokana na sheria kutoa fursa kwa wanawake lakini bado hawana

ushiriki mkubwa na unaotakikana.

Wanakijiji inabidi waelimishwe umuhimu wa kutafuta taarifa sahihi kabla ya

kufanya maamuzi yoyote mazito yanayohusiana na rasilimali zilizoko kwenye

maeneo yao kama vile ardhi.

Serikali iache kuingilia maamuzi ya wananchi, Mfano mzuri ni maamuzi

yanayofikiwa kwenye vikao halali ya mikutano mikuu ya vijiji ambayo

inaingiliwa na Halmashauri za Wilaya. Viongozi wa Halmashauri za Wilaya

wamekuwa wakipuuzia maamuzi ya wanavijiji na kufanya kinyume na

walichoamua hasa hasa kwenye sekta ya ardhi.

11.2 Uwekezaji katika ardhi ya vijiji unaendana sana na mambo haya mawili:-

(i) Ukiukwaji wa taratibu husika.

(ii) Kukosekana kwa uwezo wa kujadiliana baina ya wanavijiji na wawekezaji.

Nini kifanyike?

Washiriki walichangia kama ifuatavyo:-

Serikali iache kukumbatia wawekezaji kwa kusikiliza taarifa zao pekee pasipo na

kuziona za muhimu pasipo kuwasikiliza wananchi wa kawaida wanaojua mambo

mabaya ya kinyanyasaji wanayofanyiwa na wawekezaji hawa kwenye maeneo yao

wanayoishi.

Bunge lihusishwe kwenye mchakato mzima wa uwekezaji na wawekezaji kwa

sababu ndio wawakilishi wakubwa wa wananchi. Na wabunge wengi wanajua

matatizo ya wananchi kuliko wanavyojua mawaziri na watendaji wengine wa

serikali ambao ndio wanaosaini mikataba na wawekezaji hawa ambayo mwisho wa

siku yanakuwa na madhara kwa wananchi wa maeneo husika. Mfano mzuri ni huko

mkoani Shinyanga, wilaya ya Kahama ambako kuna uharibifu mkubwa wa

mazingira kwenye maeneo ya machimbo ya madini.

Lengo la sheria za ardhi za mwaka 1999 kwanza litimizwe ambalo ni kuwasaidia

wanavijiji wa Tanzania halafu ndio wawekezaji waletwe kwenye maeneo

yanayobaki baada ya wanakijiji kujitosheleza kwa kiwango cha kutosha.

Serikali iache wanavijiji wenyewe ndio waingie mikataba na wawekezaji hawa. Hii

itasaidia kuondoa kiburi cha hawa wawekezaji ambao baada ya kuchukua ardhi

huanza kufanya yale wanayojisikia ikiwa ni pamoja na kuwanyanyasa wananchi

pasipo na sababu za Kimsingi.

Wawekezaji wapewe maelekezo ya Kimsingi kuwa ili kupata ardhi ya kijiji ni

lazima wapiti kwenye mikutano mikuu ya vijiji na waache tabia ya kuwahonga

baadhi ya wananchi kama walivyofanya wazungu enzi za ukoloni. Hii imetokea

30

maeneo ya wilaya za Rufji na Kisarawe mkoani Pwani ambako wawekezaji

waliwahonga

11.3 Kwanini migororo kwenye sekta ya ardhi ipo kwa kiwango cha juu wakati sheria za utatuzi zipo?

Washiriki walichangia kama ifuatavyo:-

Elimu ni tatizo kubwa sana, Mfano kwenye mabaraza ya ardhi ya vijiji na kata

hayana elimu ya kutosha kuhusiana na nini wanachotakiwa wafanye. Kwa hiyo

kinachotakiwa Kimsingi ni kuongeza elimu kwa wahusika ili kupunguza

migogoro hii.

Migogoro ni sehemu ya maisha kinachotakiwa ni serikali na taasisi za kibinafsi ni

kutoa elimu ili vyombo vinavyohusika ili kuviwezesha kutoa maamuzi sahihi. Hii

itasaidia kupunguza migogoro ya ardhi kwa kiwango kikubwa hasa kwenye

maeneo ya vijijini.

Tatizo ni utekelezaji mbovu wa sheria hizi kwa baadhi ya watendaji wa serikali

kuanzia ngazi ya kijiji hadi ya taifa. Maafisa ardhi wa wilaya wamekuwa chanzo

kikubwa cha kusababisha migogoro iongezeke kwa kutoa maamuzi ambayo

yanawakanganya wananchi. Kuwepo na ushirikiano wa dhati baina ya

watekelezaji wa sheria na wananchi wa maeneo husika.

Mpango bora wa matumizi ya ardhi ndio mtatuzi mkubwa wa migogoro ya ardhi.

Hii ni kwasababu utapelekea migogoro baina ya makundi mbalimbali kupungua,

Mfano baina ya wakulima na wafugaji, vijiji na vijiji na baina ya taasisi za

serikali na wanavijiji.

Wawekezaji ndio chanzo cha migogoro ya ardhi kwenye maeneo ya vijijini. Hali

hii imetokana na wao kuingia kwa kutofuata taratibu zinazotakiwa kisheria jambo

linalopelekea kuibuka migogoro baina yao na wanavijiji. Kinachotakiwa ni kwa

wawekezaji hawa kufuata sheria zilizowekwa pamoja na kuheshimu taratibu za

maisha za eneo wanalofanya uwekezaji.

Muingiliano wa sheria moja kwa nyingine pia ni chanzo cha kuongezeka kwa

migogoro ya ardhi kwenye maeneo mengi ya nchi. Mfano pale ambapo sheria ya

ardhi inaziba mianya sheria nyingine kama za Wanyamapori na Madini zinatoa

mianya kwa maeneo hayo kuvamiwa na kuchukuliwa na wageni. Cha kufanya ni

kuhakikisha kuwa kunakuwepo na muhoanisho baina ya sheria mbalimbali ili

kukwepa mikanganyo isiyo ya lazima.

31

11.4 Nini kifanyike ili wanawake wafaidike na sheria za ardhi namba 4 na 5 za mwaka 1999?

Washiriki walichangia kama ifuatavyo:-

Kuwepo na mfuko maalum wa kuwasaidia wanawake wanyonge kupata ardhi ya

makazi na kilimo ili kuwepo na usawa kwenye uchumi baina ya wanaume na

wanawake.

Wanawake wapewe elimu maalum ili kuwawezesha kuzijua haki zao za Kimsingi

kwenye ardhi na kwenye familia zao hasa pale inapotokea wanataka

kudhulumiwa haki zao na waume zao au ndugu za waume zao kwenye mirathi.

Taasisi za kiraia kama vile Mtandao wa Kijinsia Nchini Tanzania (TGNP) watoe

elimu za haki za wanawake kwenye maeneo ya vijijini na kuacha kukaa na

kufanya maeneo ya mjini. Hii ni kutokana na kuwepo matatizo mengi ya

unyanyasaji wa wanawake maeneo ya vijijini yanayopelekea wao kupoteza haki

zao.

11.5 Fidia za ardhi na kupatiwa eneo mbadala. Je, linakidhi mahitaji ya wafidiwa? Nini kifanyike?

Kimsingi fidia hii haitoshi pekee kwa sababu mara nyingi inakuwa hailingani na

eneo halilotoka huyu mfidiwa. Wananchi wamekuwa wakipewa maeneo madogo

kulinganisha na kule waliko ondolewa.

Wananchi wanaofidiwa maeneo huwa wanalalamika kupelekwa mbali na huduma

za kijamii. Maeneo wanayopewa mara nyingi yanakuwa na uhaba wa huduma za

kijamii kama vile maji, shule, hospitali na dispensary, umeme pamoja na barabara

nzuri. Hali hii inapelekea wananchi kupoteza nguvu kubwa kwenye kutafuta

huduma hizi.

Wananchi wapewe somo la fidia ili waweze kuelewa aina ya fidia wanazotakiwa

kupatiwa kutokana na kuhamishwa kwenye eneo Fulani na serikali kupisha ujenzi

au maendelezo yoyote yale yenye Faida kwenye uchumi wa taifa.

Mara nyingi wafidiwa wamekuwa hawapewi fedha za kujengea

wanapohamishiwa maeneo mapya. Kutokupewa fedha za ujenzi kumepelekea

wengi wao kushindwa kujenga tena maishani mwao na kuziacha familia zao

zikiwa hazina nyumba za kujisetiri.

11.6 Huduma za ardhi ( Upimaji, Utoaji wa hati) haziendani na hali halisi. Nini kifanyike?

32

Washiriki walichangia kama ifuatavyo:-

Maafisa ardhi wa Halmashauri za Wilaya wawe wanatoa elimu kwa wanavijiji

kabla ya kuanza kufanya kazi za upimaji na utoaji wa hati za umilki wa ardhi ili

kuepukana uibukaji wa migogoro ya mara kwa mara.

Sheria zifuatwe ili wananchi wote bila kujali cheo chake ili kuwepo na huduma

sawa za upimaji na utoaji wa hatimiliki za ardhi.

Serikali ishirikiane na taasisi za kiraia katika kutoa elimu ya matumizi bora ya

ardhi na kuondoa migogoro ya ardhi baina ya vijiji ili kuruhusu upimaji wa ardhi

ya vijiji na kuweza kutoa hatimiliki za ardhi kwa mujibu wa sheria.

Maafisa upimaji wa ardhi wa mijini na vijijini waache kuomba rushwa kutoka

kwa wananchi wanaohitaji kupimiwa maeneo yao ili kupata hatimiliki za ardhi.

11.7 Ukomo wa kiasi cha ardhi anachoweza kupata mtu mmoja na kumilki kihalali.

Sheria ya ardhi namba 4 na 5 za 1999 zinaweka wazi kwenye vifungu vyake kiasi

ambacho mtu mmoja anaweza kupata na kumiliki kwa wakati mmoja. Kwa

Mfano kifungu cha 76 kinaweka kiwango cha mtu mmoja mmoja kumiliki ardhi.

11.8 Kilimo cha mashamba makubwa na uhakika wa chakula kwa wananchi na taifa kwa ujumla.

Washiriki walichangia kama ifuatavyo:-

Serikali kama iko makini na kupunguza njaa miongoni mwa wananchi wake basi

iache kuwaruhusu wawekezaji kuingia kwenye maeneo ambayo yapo tayari kwa

kilimo cha mazao ya chakula. Mfano mzuri ni kule wilaya ya Mbarali ambako

mashamba ya Kapunga yaliyokuwa maarufu kwa kilimo cha mpunga yamepewa

kwa wawekezaji wanaolima mazao ya nishati mbadala (jatropha).

Serikali pia isiruhusu mashamba makubwa yauzwe kwa matajiri wakubwa

ambayo huyageuza matumizi kwa kujenga hoteli kubwa na kufanya wananchi

waliokuwa wanategemea chakula kutoka kwenye mashamba hayo kubaki na njaa

isiyokuwa na kikomo.

11.9 Mfumo wa umiliki wa Wafugaji- utambuzi

Washiriki walichangia kama ifuatavyo:-

33

Serikali itenge maeneo ya Wafugaji na yaachwe kuingiliwa na wakulima na

watumiaji wengine. Pia maeneo haya yaheshimiwe na jamii nzima pasipo

kusumbuliwa na mamlaka nyingine yoyote ile. Kufanya hivi kutasababisha

kupungua kwa migogoro na mapigano baina ya wakulima na Wafugaji.

Nyanda za malisho kitaifa zianzishwe kwenye maeneo yenye rutuba nzuri kwa

ufugaji. Kuanzishwa kwa nyanda hizi kutapekea hata Wafugaji kujifunza mbinu

bora za ufugaji wa mifugo pasipo kuingilia mashamba ya wakulima na pasipo

kuharibu vyanzo vya maji na mazingira.

12.0 KUFUNGA KONGAMANO

Kongamano lilifungwa jioni ya tarehe 29/05/09 na mwenyekiti wa bodi ya

wakurugenzi ya taasisi ya HAKIARDHI Dk. Ngw‟anza Kamata. Ambaye pamoja na

mambo mengine aliwaomba Washiriki wote kutoka ndani ya jiji la Dar es Salaam na

wale wa mikoani pamoja Washiriki wote kutoka kwenye taasisi nyingine za kiraia

hata wale wa serikali kuu na serikali za mitaa kutumia yale yote yaliyojadiliwa kwa

siku zote tatu katika kuhakikisha kuwa kila mtu anapata haki yake kwenye sekta nyeti

ya ardhi.

Mwenyekiti aliwakumbusha Washiriki kuwa ardhi ni rasilimali muhimu sana kwenye

maisha ya kila siku ya Watanzania wote hasa wale wenye kipato cha chini. Lakini

wananchi hawa wamekuwa wakidhulumiwa ardhi yao na watu wachache walioko

ndani ya dola na nje ya dola lakini kwa kushirikiana na baadhi ya watu wa kwenye

dola.

Na katika soko hili la ardhi hasa ya vijiji hakuna fursa inayotolewa kwa wanunuzi na

wauzaji kukaa na kujadili bei ya ardhi hiyo inayouzwa pasipo wao kushirikishwa.

Tiba ya matatizo haya ya ardhi ni kwa tabaka hili la chini kufahamu haki zake na

kuzidai pasipo uoga wa aina yoyote ile. Cha msingi hapa ni kwa tabaka onewa

kuanzisha vuguvugu. Vuguvugu la kulinda maslahi ya wengi litasaidia pale mtu

mmoja wa Rufiji atakapoguswa basi watu wa Kilombero, Ngorongoro, Hanang na

kwingineko wajue wameguswa wote kwa kuwa wapo kwenye tabaka moja.