Upload
others
View
25
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
Ripoti ya Ufuatiliaji na Uwajibikaji kwa Jamii (SAM)
Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Wilaya ya Nyamagana
2018
Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto
Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto
Halmashauri ya Jiji la Mwanza
Wilaya ya Nyamagana
Ripoti ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji Jamii
Oktoba 2018
Zoezi la SAM limetekelezwa na Sikika kwa Hisani ya Mradi waIMPACT unaofadhiliwa na:
(SAM exercise was implemented by Sikika through specific support from IMPACT Project on behalf of)
1
Timu ya SAM Wilayani Nyamagana inatambua umuhimu wa wadau waliojitolea kwa lengo la kuijengea
jamii uwezo na maarifa ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji kwa Jamii, yaani Social Accountability Monitoring
(SAM). Mradi huu ulifanikiwa kuwaleta pamoja wadau mbalimbali katika kusimamia rasilimali na
huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto zitolewazo kwa umma. Hili ni jambo kubwa lenye thamani
na linalostahili shukrani.
Kwa heshima tunapenda kuwatambua kwa nafasi ya pekee taasisi za Aga Khan Foundation na Sikika
kwa kuendesha miradi ya afya na hususanii ile inayolenga kuboresha upatikanaji wa huduma za afya
ya uzazi, mama na mtoto. Pia, tunawashukuru sana kwa kuwajengea wananchi uwezo na maarifa ya
kuwa sehemu ya kupanga, kufuatilia na kutathimini utekelezaji wa mipango kuanzia ngazi ya jamii
mpaka Halmashauri.
Kipekee tunaushukuru uongozi wote wa Halmashauri ya Nyamagana kwa ushirikiano walio uonesha
kipindi chote cha utekelezaji wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya Dk. Philis M. Nyimbi, Mstahiki Meya
wa Jiji Mh. James Marwa Bwire na Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Mwanza, Ndugu Kiomon Kibulwa
Kibamba. Pia, tunamshukuru Mganga Mkuu Dkt. Juma Mfanga na Timu ya Menejimenti ya Afya kwa Jiji
(CHMT), wakuu wote wa idara, waganga wafawidhi wa vituo, wananchi na wadau wote walioipa timu
ushirikiano wa dhati muda wote wa zoezi la SAM.
Mwisho naishukuru timu ya SAM kwa kuwa pamoja kipindi chote cha utekelezaji wa SAM mpaka
kukamilisha ripoti hii. Natumaini kuwa maarifa haya yatatumika kwa uendelevu ili kuboresha afya ya
uzazi, mama na mtoto wilayani.
Asanteni Sana
Mh. Germina Kabola (Diwani)
Mwenyekiti wa Timu ya SAM Nyamagana
Shukrani
2
Yaliyomo
Shukrani..........................................................................................................................................1
Yaliyomo...........................................................................................................................................3
Orodha ya Vifupisho.........................................................................................................................4
Muhtasari.........................................................................................................................................5
Sehemu ya Kwanza.........................................................................................................................6
1.0 Utangulizi...................................................................................................................................6
1.1 Mchakato wa Utekelezaji wa Zoezi la SAM..............................................................................6
1.2 Muundo wa Timu ya SAM Wilaya ya Nyamagana 2018............................................................7
1.3 Mafunzo ya Nadharia na Uchambuzi wa Nyaraka.....................................................................7
1.3.1 Mipango na Mgawanyo wa Rasilimali........................................................................7
1.3.2 Usimamizi wa Matumizi.............................................................................................8
1.3.3 Usimamizi wa Utendaji..............................................................................................8
1.3.4 Usimamizi wa Uadilifu kwa Umma............................................................................8
1.3.5 Usimamizi wa Uwajibikaji..........................................................................................8
Sehemu ya Pili................................................................................................................................9
2.1 Mafanikio ya mipango ya afya - Nyamagana 2017/18..............................................................9
2.2 Uandaaji wa Nyaraka...............................................................................................................10
2.3 Utekelezaji wa Shughuli za Idara ya Afya 2017/18..................................................................11
2.3.1 Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana.......................................................................................14
2.3.2 Vituo vya Afya na Zahanati..................................................................................................17
Sehemu ya Tatu............................................................................................................................18
3.1 Utawala na Fedha..................................................................................................................18
3.1.1. Usimamizi Shirikishi................................................................................................18
3.1.2. Hali ya Mapato na Matumizi....................................................................................19
3.1.3. Mfumo wa Ukusanyaji wa Mapato.........................................................................19
3.1.4. Akaunti za Vituo.....................................................................................................19
3.1.5. Mafunzo kwa watumishi.........................................................................................20
3.1.6. Bodi na Kamati za Usimamizi wa Vituo vya Afya...................................................20
3.1.7. Mbao za Matangazo na Sanduku la Maoni..............................................................21
3
3.2 Rasilimali Watu katika Afya....................................................................................................22
3.2.1 Ikama ya Watumishi................................................................................................22
3.2.2 Malipo ya Stahiki za Watumishi..............................................................................22
3.2.3 Tathimini ya Utendaji kazi.......................................................................................23
3.3 Dawa na Vifaa Tibai................................................................................................. 23
3.3.1 Hali ya Upatikanaji wa Dawa Muhimu....................................................................23
3.3.2 Hali ya Upatikanaji wa Vifaa ..................................................................................23
3.3.3 Vyumba na Kabati za Kuhifadhia Dawa.................................................................23
3.4 Miundombinu ya Afya.............................................................................................................24
3.4.1 Vizimba vya Kuchomea Taka na Shimo la Kondo la Uzazi....................................25
3.4.2MfumowaMajiSafi................................................................................................25
3.4.3.HaliyaVyoonaUsafiwaMazingira......................................................................26
3.4.4 Ujenzi na Ukarabati wa Majengo na miundombinu ya barabara............................26
3.4.5 Nyumba za Watumishi............................................................................................27
3.4.6 Nishati ya Umeme...................................................................................................27
3.4.7 Usalama na Utulivu katika Vituo vya Kutolea Huduma...........................................28
Sehemu ya Nne............................................................................................................................29
4.0 Mapendekezo.........................................................................................................................29
4.1 Maazimio ya Pamoja...............................................................................................................31
4.2 Hitimisho.................................................................................................................................32
Kiambatanisho 1...........................................................................................................................33
Kiambatanisho 2...........................................................................................................................33
4
Orodha ya Vifupisho
SAM Social Accountability Monitoring (Ufuatiliaji wa Uwajibikaji kwa Jamii)
CMT Council Management Team (Timu ya Menejimenti ya Jiji)
CHMT Council Health Management Team (Timu ya Menejimenti ya Afya kwa Jiji)
WDC Ward Development Committee (Kamati ya Maendeleo ya Kata)
CAG Controller Audit General (Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali)
WEO WardExecutiveOfficer(AfisaMtendajiwaKata)
HFGC Health Facility Govening Committee (Kamati ya Usimamizi wa Kituo)
DHSB District Health Service Board (Bodi ya Afya ya Wilaya)
CSO Civil Society Organizations (Asasi za Kiraia)
RBF Result Based Financing (Mpango wa Malipo kwa Ufanisi)
RCH Reproductive and Child Health (Afya ya Uzazi na Watoto)
IMPACT Improving Access to Maternal and Newborn Health in Mwanza,Tanzania (Mradi
wa Kuboresha Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto mkoa wa Mwanza)
5
Muhtasari
Mchakato wa Ufuatiliaji wa Uwajibikaji kwa Jamii - Social Accountability Monitoring (SAM) una
lengo la kuiwezesha jamii kushiriki katika kupanga, kufuatilia na kutathimini utekelezaji wa mipango
kuanzia ngazi ya jamii mpaka Halmashauri. Lengo kuu la SAM ni kuimarisha mifumo kwa kuhimiza
Ushirikishwaji, Ufuatiliaji na Uwajibikaji Jamii kwa watoa huduma. Vilevile, kuwapa wananchi uelewa
kuhusu haki na wajibu wao kwenye jamii kama ilivyoainishwa katika sera, kanuni, taratibu na sheria za
nchi na mikataba ya kimataifa ambayo Tanzania imeridhia.
Zoezi la SAM limeendeshwa wilayani Nyamagana kwa kuijengea uwezo jamii ambayo iliweza kufanya
uchambuzi wa taarifa mbalimbali pamoja na kufuatilia utekelezaji wa mipango na miradi mbalimbali
inayotekelezwa katika vituo vya kutolea huduma za afya hususani huduma ya afya ya uzazi, mama na
mtoto.
Uchambuzi huo ullibainisha takribani jumla ya hoja 53 ambapo zimegawanyika katika makundi
yafuatayo:
• Hoja zilizofutwa baada ya ufafanuzi – 1
• Hoja zilizoibuliwa na zimeanza kushughulikiwa – 6
• Hoja zilizochukuliwa na menejimenti kwa ajili ya uchambuzi wa kina na uhakiki ili kujiri-
dhisha – 5
• Hoja zilizotolewa pongezi na ushauri – 10
• Hoja zilizopatiwa ufafanuzi wa kina na kukidhi haja kwa ajili ya maboresho – 31
Kwa ujumla wadau walikubaliana idara ishughulikie hoja hizo kwa kuboresha mifumo ya uandaaji wa
mipango na ripoti kwa kuzingatia miongozo ya serikali na kuimarisha uwepo na usimamizi wa kamati
za vituo. Vilevile, kuboresha huduma katika hospitali ya wilaya, vituo vya afya na zahanati hususani
huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto ili kuimarisha uzazi salama. Kuimarisha miundombinu kama
vile, mifumo ya utupaji na uteketezaji taka na utambuzi wa mipaka ya vituo ili kudhibiti shughuli nyingine
zisizohusiana na huduma za afya kufanyika ndani ya maeneo ya vituo vya kutolea huduma.
Farida Mzambili, mjumbe wa timu ya SAM akiwasilisha ripoti ya SAM kwa wadau wa afya, Nyamagana
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana, Dkt. Philis Nyimbi akitoa maelekezo ya namna bora ya utekelezaji
wa maazimio ya SAM kwa wadau wa afya
6
Sehemu ya Kwanza 1.0 UtanguliziDhana ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji kwa Jamii (SAM) ni dhana shirikishi inayohimiza uwajibikaji wa
pamoja kati ya wananchi (wenye wajibu na haki) na watoa huduma (wenye wajibu na dhamana)
ilikuhakikisha upatikanaji endelevu wa mahitaji muhimu ya jamii.
Utekelezaji wa SAM katika Wilaya ya Nyamagana ulilenga kuiwezesha jamii kufahamu haki na wajibu
wao katika upatikanaji wa huduma ya afya ya uzazi, mama, baba na mtoto. Lengo ni kuwezesha
wananchi kushiriki katika kusimamia rasilimali zilizopo na kuwa na mipango ya pamoja kwa kuzingatia
miongozo, sera, sheria za nchi na mikataba ya kimataifa ambayo Tanzania imeridhia.
Miongoni mwa nyenzo zilizotumika kuandaa ripoti hiini:
a) Toleo la IV la Mwongozo wa Uandaaji wa Mpango Kabambe wa Afya (CCHP) la Mwaka
2011.
b) Muongozo wa uandaaji wa mipango ya vituo vya afya na zahanati.
c) Mpango kabambe wa afya 2017/2018 na ripoti za utekelezaji kwa kila robo mwaka.
d) Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977.
e) Mkataba wa Kimataifa wa ICESCR wa 1966.
1.1 Mchakato wa Utekelezaji wa Zoezi la SAMUshirikiano wa pamoja kati ya Sikika na Aga Khan Foundation ulifanikisha kukamilisha maandalizi ya
awali ikiwemo mikutano na viongozi wa serikali katika ngazi mbalimbali. Hatua hiyo ilihusisha viongozi
na wasimamizi wa Jiji la Mwanza na wilaya ya Nyamagana kwa utambulisho wa mradi na dhana ya
ufuatiliaji wa uwajibikaji kwa jamii na utekelezaji wake hivyo kutoa fursa ya kufanya mikutano ya jamii
ngazi ya kata ili kupata wawakilishi wa jamii na kuunda timu ya SAM yenye wajumbe 15.
Utekelezaji wa zoezi la SAM umegawanyika katika sehemu tatu. Sehemu ya kwanza ni mafunzo kwa
timu kuhusu dhana na mchakato wa utekelezaji zoezi la SAM. Sehemu ya pili ilihusisha uchambuzi wa
nyaraka mbalimbali kama zilivyotajwa hapo juu na kufanya uhakiki vituoni ili kupata uthibitisho wa hoja
zilizojitokeza katika uchambuzi. Katika sehemu hii pia timu ya SAM ilikutana na CHMT na CMT kwa
pamoja ili kupata ufafanuzi wa hoja zilizojitokeza kwenye uchambuzi na uhakiki vituoni. Sehemu ya
tatu, timu iliandaa ripoti ya hoja zinazohitaji kujadiliwa na kuwekewa mikakati na muda wa maboresho
(action plan) katika mkutano wa wadau wa afya kwa halmashauri.
1.2 Muundo wa Timu ya SAM Wilaya ya Nyamagana 2018Timu ya SAM kwa wilaya ya Nyamagana ina wajumbe 15 wanaowakilisha makundi mbalimbali;
uwakilishi pia ulizingatia jinsia na umri. Kundi la kwanza ni wananchi hususani vijana ambao sio tu
kwamba wana haki ya kupata huduma bora na wana wajibu wa kushiriki katika kuboresha huduma hizi
7
lakini pia wao ndio walengwa na wanufaika watarajiwa wa huduma ya afya ya uzazi. Kundi la pili ni
watendaji kutoka ngazi mbalimbali ambao kimsingi wana wajibu wa kutoa huduma bora kwa wananchi.
Kundi la tatu ni wasimamizi walioko kisheria wenye wajibu wa kuhakikisha utawala bora na uwajibikaji
unakuwepo katika kutoa huduma kwa wananchi. Jedwali No. 1 linaonesha idadi ya uwakilishi kutoka
kila kundi.
Jedwali 1: Timu ya SAM Wilaya ya NyamaganaUwakilishi kutoka kwenye Jamii Watendaji Wasimamizi
Wananchi (ME&KE)
WananchiMahitaji Maalum
WAVIU Mashirika ya Kijamii
Watend-aji wa Kata
Timu ya Afya ya
Hal-mashauri
Timu ya Utawala ya Hamashau-
ri
Madiwani(ME & KE)
Bodi ya Afya ya Wilaya
Kamati ya Afya ya Kituo
5 1 1 1 1 1 1 2 1 18 3 4
1.3 Mafunzo ya Nadharia na Uchambuzi wa NyarakaTimu ilipatiwa mafunzo ya uchambuzi wa nyaraka muhimu za afya za wilaya za mwaka 2017/18.
Taarifa zilizochambuliwa zilijumuisha mpango mkakati wa halmashauri, mpango kabambe wa afya wa
halmashauri (CCHP), ripoti za utekelezaji wa mpango wa afya kwa kila robo mwaka na mihtasari ya
vikao vya baraza la madiwani. Mafunzo yalihusisha hatua 5 zilizoakisi mfumo wa uwajibikaji katika
uandaaji wa mipango na utekelezaji wa bajeti. Hatua hizo ni kama ifuatavyo;
1.3.1 Mipango na Mgawanyo wa RasilimaliTimu ya SAM ilipata fursa ya kujifunza uandaaji wa mpango mkakati wa wilaya na mpango kabambe
wa afya; hususani dhana, muundo na umuhimu wa ushiriki wa wananchi na wadau wengine katika
uandaaji wa mipango. Vilevile, timu ilijifunza namna ya kutathmini mahitaji na mgawanyo wa rasilimali
kwa kuzingatia vipaumbele vya upatikanaji wa huduma za afya hususani katika kipengele cha mama,
baba, mtoto na uzazi salama.
Bw. Fredrick Ngao kutoka Sikika akiendesha mafunzo kwa wajumbe wa timu ya SAM
Wajumbe wa timu ya SAM wakifanya uchambuzi wa taarifa za Halmashauri
8
1.3.2 Usimamizi wa MatumiziTimu iliweza kufanya ulinganifu wa vipaumbele, mipango, mapato na matumizi katika kutekeleza
mipango ya afya. Kwa kutumia ripoti za utekelezaji wa mipango na fedha, timu iliangalia matumizi ya
fedha katika kila robo mwaka. Pia timu ilitathmini njia za usimamizi wa mifumo na vyombo mahususi
vilivyoko katika halmashauri katika usimamizi wa matumizi ya rasilimali fedha kwa kuzingatia miongozo,
kanuni na sheria za matumizi ya fedha za umma.
1.3.3 Usimamizi wa UtendajiTimu ya SAM ilifanikiwa kufanya ulinganifu wa mipango na ufanisi wa huduma zitolewazo na watoa
huduma vituoni. Maazimio katika nyaraka mbalimbali na hali halisi ya utekelezaji wake vilitoa mwanga
na uelewa namna ambavyo usimamizi katika utekelezaji wa mipango unavyofanyika.
1.3.4 Usimamizi wa Uadilifu kwa UmmaMifumo na mamlaka zenye dhamana ya kuchukua hatua za kinidhamu kwa watoa huduma zilitathiminiwa
na timu kwa kuwa ni nguzo muhimu katika kuimarisha uadilifu. Timu iliangalia namna ambavyo sheria
na miongozo iliyopo inawawezesha watoa huduma kutekeleza majukumu yao na jinsi ambavyo sheria
namiongozohuziwezeshamamlakazanidhamukufuatilianakudhibitimatumizimabayayaofisina
uzingatiaji wa miongozo ya matumizi ya fedha za umma. Mamlaka hizi ni pamoja na baraza la madiwani,
bodi na kamati za afya, mkaguzi wa fedha wa ndani, mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali.
1.3.5 Usimamizi wa UwajibikajiTimu ilichambua nyaraka kwa kuangalia namna ambavyo vyombo vya usimamizi vinavyowajibika
katika kila hatua. Kuanzia jamii kuibua vipaumbele vyake, ushirikishwaji katika kamati za afya za vituo,
kamati ya maendeleo ya kata (WDC), bodi ya afya ya wilaya na Baraza la Madiwani. Timu ilijifunza ni
maeneo na fursa zipi ambazo jamii inaweza kushiriki na kuboresha huduma za afya ya uzazi, mama
na mtoto.
1.4 Maeneo yaliyotembelewa kwa UhakikiBaada ya mafunzo na uchambuzi, timu ilipata fursa ya kutembelea baadhi ya vituo ili kuona uhalisia
wa utekelezaji wa huduma za afya hususani huduma za mama, baba na mtoto. Vilevile, timu ilitumia
fursa hii kufanya uhakiki wa hoja zilizojitokeza kwenye uchambuzi kwa kufanya majadiliano na watoa
huduma au kuangalia (observations). Vituo tisa vya kutolea huduma za afya vilivyotembelewa ni
vile ambavyo viko kwenye mradi unaofadhiliwa na AgaKhan Foundation ujulikanao kama Mradi wa
Kuboresha Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto (IMPACT). Kiambatanisho Na. 1 kinaonyesha
vituo vilivyotembelewa na timu ya SAM.
9
Sehemu hii inazungumzia masuala mbalimbali yaliyobainishwa na timu wakati wa utekelezaji wa zoezi
la SAM. Maeneo makuu matatu yameripotiwa: mafanikio ya mipango ya afya, uandaaji wa nyaraka na
utekelezaji wa shughuli za mpango kabambe wa afya na uhakiki vituoni.
Sehemu hii pia inabainisha masuala yaliyohitaji ufafanuzi kutoka Timu ya Menejimenti ya Jiji (CMT)
na Timu ya Menejimenti ya Afya kwa Jiji (CHMT), vilevile inatoa mchanganuo wa namna kila suala
lilivyopatiwa ufafanuzi na kuingizwa katika mpango wa pamoja wa wadau unaobainisha namna ya
kuboresha huduma za Afya hususanii huduma ya afya ya uzazi, mama na mtoto.
2.1 Mafanikio ya mipango ya afya - Nyamagana 2017/18Tathmini ya timu ya SAM ilibaini kuwa katika kipindi cha mwaka 2017 – 2018, Idara ya Afya ilifanikiwa
kutekeleza mambo mbali mbali katika kuinua ufanisi wa huduma zitolewazo na idara na vituo vyake
vya huduma katika halmashauri ya manispaa ya Nyamagana:
(i) Kuongeza vituo viwili vya huduma: Zahanati za Isebanda na Bulale.
(ii) Watumishi wapya 11 ambao wamepangwa kwenye vituo mbalimbali kulingana na uhitaji wa
watumishi.
(iii) Ukarabati wa zahanati 9 kwa kutumia fedha za mfuko wa fedha kwa matokeo (Result Based
Financing – RBF) ili kuweka majengo katika ubora wa huduma na pia kuweka mazingira
bora kwa watoa huduma na watumiaji.
(iv) Kufunga mfumo wa umeme wa jua katika Hospitali ya Nyamagana ambao uimeimarisha
huduma za dharura na kuimarisha huduma zitumiazo nishati ya umeme.
(v) Upatikanaji wa dawa na vifaa tiba vituoni umeimarika toka 80% (2016/2017) mpaka 95%
(2017/2018).
(vi) Kuboresha miundombinu ya msingi katika kituo cha Igoma ikiwa ni pamoja na vyoo,
vichomea taka, mashimo ya kutupia kondo la nyuma baada ya akina mama kujifungua,
umeme,majisafinasalamanapiamifumoyamajitakanavifaavyauhifadhiwatakangumu
na hatarishi.
(vii) Halmashauri kwa kutumia fedha za vyanzo vyake vya ndani inajenga zahanati 4
ambazo zipo kwenye hatua mbalimbali jambo ambalo ukamilikaji wake utapunguza adha ya
watumia huduma kutembea umbali mrefu kufuata huduma hususani akina mama wajawazito
na wale wenye watoto wachanga.
Sehemu ya Pili
10
(viii) Kwa mwaka wa fedha 2018/19 idara ilianza kufanya upanuzi mkubwa wa kituo cha Afya Igo
ma ili kupunguza msongamano katika baadhi ya vituo, uimarishaji wa huduma kwa vifaa na
wataalam hivyo kutoa huduma bora zaidi hasa huduma za uzazi.
(ix) Mpango kabambe wa afya wa wilaya umezingatia vipaumbele vyote 13 vya afya.
Kipaumbele cha huduma ya uzazi, mama na mtoto kilibainishwa bayana katika Uk. XVI,
Jedwali Na. 2.2. Uchambuzi umeonesha uwepo wa mchanganuo wa bajeti na mahitaji yote muhimu ya
kuokoa vifo vya mama na mtoto.
2.2 Uandaaji wa Nyaraka2.2.1 Uandishi wa Nyaraka
Timu inapongeza Halmashauri ya Jiji na idara ya afya kwa kuzingatia miongozo ya uandaaji wa
Mpango Mkakati wa Jiji, Mpango Kabambe (2017/18) na Ripoti za Utekelezaji (2017/18). Mipango na
ripoti hizi zimezingatia kwa kiasi kukubwa miongozo kwa kuainisha taarifa muhimu hususani malengo,
viashiria, vipaumbele na taarifa za bajeti.
Hoja ya Timu
Timu inashauri menejimenti kuongeza umakini wa uhakiki wa taarifa ili ziwe bora na kuakisi uhalisia
na kuondokana na dosari kama kunakili taarifa zilizopita “copy and paste” kama ilivyoonekana wakati
wa uchambuzi wa taarifa. Kwa mfano, katika ripoti ya robo ya 1 ukurasa (uk) wa 8 na ripoti ya robo ya
2 uk. wa 9 taarifa ni moja; kukarabati vifaa tiba na jokofu la mnyororo baridi vituo vya Afya Igoma na
Makongoro. Pia timu haikuona uidhinishwaji wa Mpango Kabambe 2017/2018, hivyo inashauri ni vema
idara ihakikishe mipango inaidhinishwa na mamlaka husika.
Chanzo, SAM 2018: Mjumbe wa CMT akifafanua jambo wakati wa kikao cha ndani baina ya timu ya SAM na menejimenti
11
Majibu ya Menejimenti
Baada ya majadiliano ya timu, menejimenti iliahidi kufanyia kazi ushauri ili kuboresha mipango ya Jiji,
idara ya afya na ya vituo vya huduma kwa mwaka ujao wa fedha kwani kwa sasa mipango yote ime-
shaanza kutekelezwa vituoni.
2.3 Utekelezaji wa Shughuli za Idara ya Afya 2017/18Kipengele hiki kinaonyesha maoni ya timu yaliyotokana na hoja mbalimbali zilizotokana na uhakiki
katika ngazi ya hospitali, vituo vya afya na zahanati.
2.3.1 Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana
i) Kuzalisha zana za kukusanya taarifa na kuchapa kadi za mama wajawazito na watoto ifikapo Juni 2018.Hoja ya timu
Uchambuzi wa timu ulibaini kuwa shughuli ilipangwa kufanyika katika robo zote nne za mwaka, lakini
fedha zilipokelewa na utekelezaji ulifanyika katika robo ya tatu pekee. Vilevile, uhakiki katika vituo
ulibaini kuwa baadhi ya kina mama hudurufu (hutoa nakala ngumu) kadi za mama wajawazito na
watoto kutokana na upungufu wa kadi hizo vituoni. Timu ilipenda kufahamu kwanini katika robo ya
kwanza na pili kadi hizi hakikuchapwa na je, idara iliweka mkakati upi kukabiliana na changamoto hiyo?
Majibu ya Menejimenti
Suala hili lilisababishwa na kuchelewa kutolewa kwa fedha za mfuko wa afya wa pamoja (Health
Basket Fund - HBF) ambazo ziliingia mwishoni mwa robo ya pili na utekelezaji ukafanyika robo ya tatu.
Aidha, baadhi ya vituo vilivyodurufu kadi hizo vilitumia fedha za mpango wa malipo kwa Ufanisi (Result
based Financing – RBF).
Maoni ya timu
Timu ilipendekeza kuwa ni vema serikali ikazingatia muda wa utoaji wa fedha kwa Idara ili kutoathiri
utoaji wa huduma za afya ya uzazi, wajawazito na watoto unaosababishwa na ucheleweshwaji wa
fedha.
ii) Ukusanyaji wa damu salama kwa kiwango cha uniti 1,200 ifikapo juni 2018Hoja ya timu
Uchambuzi wa timu ulionyesha kuwa idara ilipokea na kutumia jumla ya shilingi 9,561,517/= kati ya
shilingi 17,300,000/= zilizopangwa kwa ajili ya ukusanyaji wa damu salama. Kwa kuzingatia umuhimu
wa damu salama kwa huduma za mama na mtoto, timu ingependa kufahamu kama kuna athari zozote
zilizotokana na kutopata fedha zote za kufanyia shughuli hii (kukusanya damu salama).
Majibu ya Menejimenti
Lengolilikuwakukusanyaunit1200zadamunahalikufikiwa.Aidha,hospitaliililazimikakutafutadamu
12
kwenye Taasisi nyingine kama Hospitali ya Bugando na SekouToure ili kuweza kuokoa maisha. Hata
hivyo, jamii inajengewa uelewa wa umuhimu wa kuchangia damu kwa hiari ili kuweza kuwa na hifadhi
ya damu salama ya kutosha.
(iii) Kufanya mafunzo elekezi ya usimamizi wa lishe kwa wahudumu wa afya 71Hoja ya timu
Uchambuzi ulibaini shilingi 6,400,000/=zilitengwa kwa ajili ya mafunzo na kupangwa kufanyika kila
robo ya mwaka lakini haikufanyika na ripoti hazikutoa ufafanuzi wowote. Hivyo, timu iliomba kujua idara
ilikabilianajenachangamotoyausimamizihafifuwalishenaupimkakatiuliopokwasasa?
Majibu ya Menejimenti
Shughuli hii haikutekelezwa kutokana na kutopokelewa kwa fedha za utekelezaji. Aidha, elimu ya lishe
inaendelea kutolewa kwa mama wajawazito wanapohudhuria kliniki kwenye vituo vya kutolea huduma.
Utekelezajizaidiutafanyikafedhazitakapopatikanailikufikialengokuu.
Maoni ya Timu
Timu inashauri wizara ya afya iweke asilimia mahususi ya bajeti kwa ajili ya huduma ya lishe ili kutatua
tatizo litokanalo na athari za lishe kwa mama wajawazito na watoto wachanga.
iv) Ununuzi wa virutubisho kwa watoto 280 wenye dalili za utapiamlo chini ya miaka mitanoHoja ya timu
Uchambuzi wa timu ulibaini jumla ya shilingi 21,000,000/= zilitengwa kwa ajili ya ununuzi wa virutubisho
hivyo hata hivyo ununuzi haukufanyika na hakukuwa na maelezo katika ripoti ya utekelezaji. Hivyo
timu ilipenda kufahamu ni kwa nini shughuli hii haikutekelezwa? Je, kuna mkakati gani kukabiliana na
changamoto hiyo ya utapiamlo.
Majibu ya Menejimenti
Shughuli hii haikutekelezwa kutokana na kutokuwepo kwa fedha za utekelezaji. Aidha, idara imejielekeza
kuhakikisha inasimamia uandaaji wa mipango ya vituo ili kuhakikisha shughuli zinapangwa kulingana
na vipaumbele na rasilimali zilizopo.
Maoni ya Timu
Timu inashauri idara kuongeza usimamizi wa uandaaji, utekelezaji na utoaji wa taarifa katika ngazi za
vituo ili kukuza ufanisi.
(v) Upanuzi wa jengo la mionzi katika Hospital ya Nyamagana Hoja ya timu
Uchambuzi wa timu ulibaini kuwa jumla ya kiasi cha shilingi 19,588,006/= ilipangwa katika robo ya
kwanza kutoka chanzo cha mfuko wa pamoja wa afya kwa ajili ya upanuzi wa jengo. Aidha, katika
taarifa za utekelezaji timu ilibaini kuwa upanuzi wa jengo la mionzi haukufanyika hata hivyo vyoo katika
13
hospitali vilibainika kujengwa. Timu ilipenda kufahamu kwa nini ujenzi ulibadilika na mpango wa
upanuzi wa jengo la mionzi uliishia wapi?
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti inaendelea kufuatilia usahihi wa taarifa hii ili kuweza kujiridhisha na kutoa ufafanuzi zaidi.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru kwa majibu na itaendelea kufuatilia na kupata majibu sahihi ili kuboresha uandaaji na
utoaji wa taarifa na huduma.
(vi) Ujenzi wa jengo la utawala Hoja ya timu
Uchambuzi ulibaini kuwa jengo la utawala lilipangwa kujengwa kwa gharama ya shilingi 481,069,341/=
kutoka chanzo cha mapato ya ndani na kupangwa kufanyika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha
2017/18 lakini halikutekelezwa. Timu iliomba ufafanuzi kwanini ujenzi haukufanyika, na ni lini
utatekelezwa? Pia CHMT inavyokabiliana na jengo la utawala.
Majibu ya Menejimenti
Utekelezaji wa shughuli hii ulikwama kutokana na baadhi ya vyanzo vya mapato vya halmashauri
kuhamishiwa serikali kuu, hivyo kupelekea kuwa na makusanyo kidogo. Aidha menejimenti inapata
adhakwakukosekanakwa jengo lautawalahivyokumelazimikakuwanaofisimaeneo tofautihali
inayopelekea utendaji kuwa mgumu.
Maoni ya Timu
Timu inashauri menejimenti ya halmashauri kulipa kipaumbele suala hili kwa kuliweka katika mipango
ijayo ili kuondoa kadhia ili kuleta ufanisi wa kiutendaji na huduma za afya.
(vii) Ununua wa mashine ya mionziHoja ya timu
Uchambuzi ulibaini kuwa mashine ya mionzi haikununuliwa japo iliwekwa kwenye mpango na bajeti.
Hivyo, timu ilipenda kujua mashine ya mionzi itanunuliwa lini na je, hospitali kwa sasa ina utaratibu gani
kwa huduma za mionzi?
Majibu ya Menejimenti
Hospitali imeweka mikakati mbalimbali ya kuongeza mapato ili kuweza kununua dawa, na vifaa
tiba hususani mashine ya mionzi ili kuboresha huduma za afya. Aidha katika kipindi hiki wagonjwa
wamekuwa wakipata huduma hii kwenye hospitali za Bugando na SekouToure.
Maoni ya Timu
Timu ilipendekeza idara itekeleze mikakati iliyoweka angalau katika kipindi cha robo ya tatu (Januari –
14
Machi 2019) ili kuboresha huduma hii muhimu ya vipimo kwa mama wajawazito.
(viii) Kununua seti (kit) za dawa, maabara na meno Hoja ya timu
Uchambuzi ulibaini kuwa manunuzi haya yalitengewa kiasi cha shilingi 85,686,199/=. Robo ya kwanza
imeonesha ununuzi wa seti mbili kwa shilingi 16,684,158/= na robo ya pili zilinunuliwa setimbili kwa
3,435,021/=. Timu ilipenda kujua gharama ya kila seti na kwa nini bakaa ya shilingi 6,565,795/= haiku-
tumika wakati uhitaji wa vifaa ulikuwepo? Na, kwa nini seti saba badala ya nne kama ilivyokusudiwa?
Majibu ya Menejimenti
Kutokana na mfumo wa vituo kununua dawa na vifaa tiba vyenyewe kumekuwa na baadhi ya vituo
kutokuwasilisha maombi yao hali inayopelekea vituo kubaki na fedha mwisho wa robo au mwaka.
Aidha vituo vinaendelea kujengewa uwezo namna ya uagizaji wa dawa na vifaa tiba. Pia kumekuwa na
ongezeko la seti za dawa toka 4 hadi 7 hali hii imesababishwa na aina ya dawa zilizoagizwa pamoja
na mabadiliko ya gharama za dawa wakati wa ununuzi.
2.3.2 Vituo vya Afya na Zahanati(i) Ukarabati vifaa tiba na friji katika vituo vya Makongoro na IgomaHoja ya timu
Uchambuzi ulibaini ukarabati ulipangwa kufanyika kwa jumla ya shilingi 1,500,000/= kwa robo zote nne.
Hata hivyo uchambuzi ulionesha kuwa robo 1 na 2 zilinunuliwa seti za vifaa tiba badala ya ukarabati wa
vifaa vya Hospitali na Friji kama ilivyopangwa ila robo ya nne ndo ukarabati ukafanyika. Timu iliomba
ufafanuzi juu ya mkanganyiko huu na zipi zilikuwa sababu za mabadiliko hayo?
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti inaendelea kufuatilia kwenye vituo husika ili kuweza kubaini ni kwa namna gani mfumo
uliweza kufanya malipo nje ya utaratibu.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru kwa majibu na itaendelea kufuatilia ili kupata uhalisia wa suala hili.
(ii) Kununua dawa na vifaa tiba - seti 8 kila mojaHoja ya timu
Uchambuzi ulionesha bajeti iliyotengwa kwa shughuli hii ilikuwa shilingi 95,522,203/= lakini kiasi
kilichopokelewa ni shilingi 10,902,428/=. Na, kati ya hizo, fedha zilizotumika ni shilingi 6,301,384/=
hivyo kuacha bakaa ya shilingi 4,601,044/= ambayo haikuonekana na wala hakukuwa na maelezo
yoyote. Timu iliomba kupata ufafanuzi wa fedha hizo ambazo hazijaonekana katika bakaa ya robo ya
nne.
15
Majibu ya Menejimenti
Kwa utaratibu wa mfumo wa kuandalia bajeti na kutolea taarifa, kiasi cha fedha kilichopokelewa na
kilichotumika kikiingizwa kwenye mfumo bakaa hutokea. Aidha, ufuatiliaji unaendelea kuona ni kwa nini
mfumo ulishindwa kuonesha salio wakati kuna fedha zilipokelewa.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru kwa majibu na itaendelea kufuatilia ili kuthibitisha kama ni suala la mfumo ama ni
sababu nyinginezo.
(iii) Ununuzi wa kadi za wajawazito na watoto kwa vituo vya Makongoro na Igoma Hoja ya timu
Uchambuzi ulibaini jumla ya shilingi 4,810,000/= zilitengwa kutumika katika kila robo ya mwaka. Kazi
hii ilifanyika robo ya nne hivyo timu iliomba kupata ufafanuzi juu ya namna vituo vilivyojiendesha kwa
robo ya kwanza, pili na tatu bila kadi hizo muhimu.
Majibu ya Menejimenti
Katika kipindi cha robo ya 1 hadi 3 vituo vilitumia fedha za RBF kuhakikisha vinakuwa na kadi za
wajawazito. Aidha, fedha zilipopokelewa robo ya 4 manunuzi yalifanyika kwa kutumia mfuko wa pamoja.
(iv) Ununuzi wa “Valve” 25 za gesiHoja ya timu
Uchambuzi umebaini kuwa ununuzi ulipangwa kufanyika kwa gharama ya shilingi 625,000/= kwa robo
ya kwanza. Hata hivyo ununuzi wa valve 60 badala ya 25 ulifanyika katika robo ya nne kwa shilingi
625,000/= wakati fedha iliyopokelewa ni Tshs 563, 770/=. Timu iliomba ufafanuzi juu ya ongezeko la
idadi ya “valve” na fedha zilizotumika zilitoka wapi wakati fedha zilizopokelewa zilikuwa pungufu.
Majibu ya Menejimenti
Manunuzi ya ‘valve’ yalifanyika kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya fedha ikiwa ni pamoja na fedha za
papo kwa papo, RBF na HBF. Vyanzo hivyo vilipelekea idadi kuongezeka kutoka ‘valve’ 25 hadi 60, hii
ilitokana na umuhimu wa vifaa hivyo vinavyotumika kwenye majokofu ya kuhifadhia chanjo.
Maoni ya Timu
Timu ilishukuru kwa majibu, pia ilishauri maelezo ya aina hii yawekwe katika kipengele cha maoni ili
kupunguza maswali kwa watumia taarifa.
(v) Uchapishaji wa miongozo 300 ya usimamizi wa ustawi wa mtoto kwa zahanati 50 Hoja ya timu
Uchapishaji ulipangwa kufanyika kwa bajeti ya shilingi 5,400,000/= kwa robo ya pili pekee. Hatahivyo
miongozo 150 tu ndio ilichapishwa na sio 300 kama ilivyopangwa. Timu ilipenda kujua kwa uchapishaji
ulikuwa pungufu na huku fedha ikiwa imetumika karibu yote kwa nusu ya kazi?
16
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti imeona changamoto hii ya makisio, hali hii kwa sehemu kubwa inachangiwa na uelewa
mdogo wa waandaaji wa mipango ngazi ya vituo. Aidha Menejimenti inaendelea kuwajengea uwezo
watumishi ili waweze kuandaa mipango inayoakisi mahitaji na vipaumbele.
(vi) Ukarabati wa majengo ya zahanati Hoja ya timu
Uchambuzi ulionesha kuwa ukarabati ulipangwa kufanyika robo zote kwa shilingi 175,540,200/= kwa
chanzo cha matumizi mengineyo (Other Charges-OC). Kiasi chote kilichotengwa kilipokelewa na
matumizi yameonesha fedha zilitumika zaidi ya kiasi iliyopokelewa ambapo kuna ongezeko la shilingi
6,706,734 ambalo halionekani chanzo. Timu ilipenda kupata ufafanuzi wa mkanganyiko huo wa chanzo
kutojulikana.
Majibu ya Menejimenti
Ukarabati ulifanyika kwa fedha za RBF zilizopokelewa awamu ya kwanza baada ya bajeti kuwasilishwa.
Maoni ya Timu
Timu ilishukuru kwa majibu lakini inashauri maelezo ya aina hii yawekwe katika kipengele cha maoni ili
kupunguza maswali kwa watumia taarifa.
(vii) Ununuzi wa seti (kit) 4 za dawa kwa zahanati 12 Hoja ya timu
Kiasi cha shilingi 114,396,678/= kilitengwa kwa ajili ya ununuzi wa seti 4 za dawa na ununuzi ulipangwa
kufanyika robo zote za mwaka. Ripotii ya utekelezaji ununuzi wa seti hizo za dawa zikiwemo dawa za
msingi za matibabu ya awali kwa afya ya kinywa na meno (dental supplies) ngazi ya zahanati. Timu
ilipenda kupata ufafanuzi juu ya ununuzi wa dawa hizi katika ngazi ya zahanati wakati huduma za
kinywa na meno hazipo kwenye zahanati?
Majibu ya Menejimenti
Katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya hususani wilaya zilizopo mjini, vituo
vilielekezwa kutenga kiasi cha fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa za msingi za matibabu ya awali kwa
afya ya kinywa na meno kwenye ngazi ya zahanati kabla ya matibabu ya kina katika ngazi za juu kama
vituo vya afya na hospitali.
(viii) Ununuzi wa seti (kit) 12 za dawa kwa zahanati Hoja ya timu
Ununuzi wa seti za dawa ulipangwa kufanyika kwa kutumia fedha kutoka NHIF kiasi cha shilingi
17,451,197/= kwa kila robo. Utekelezaji umeonesha manunuzi ya shilingi 68,000/= pekee yalifanyika
kutokana na changamoto ya upungufu wa fedha japo katika robo ya tatu kulikuwa na bakaa ya shilingi
454,590/=. Aidha, katika robo ya nne imeonekana bakaa ya shilingi 1,284,590/= tofauti na shilingi
17
454,590 zilizotoka robo ya tatu. Timu iliomba ufafanuzi ni kit zipi ziligharimu fedha ndogo kiasi hicho
tofauti na mpango na kwa nini kumekuwa na bakaa tofauti tofauti?
Majibu ya Menejimenti
Utekelezaji wa shughuli zilizopangwa kwa vyanzo vya fedha vya makusanyo ya kituo unategemea na
makusanyo halisi. Aidha maboresho yanaendelea kufanyika kwenye vituo ili kuimarisha vyanzo vya
mapato ya ndani pamoja na uhakiki wa fomu za Bima zinazojazwa kabla ya kuwasilishwa NHIF. Lengo
likiwa kupunguza dosari zinazoweza kusababisha fomu kurejeshwa na kituo kukosa mapato.
Maoni ya Timu
Timu ilishukuru kwa majibu japo suala la bakaa halijipatiwa ufafanuzi, hivyo timu inasisitiza idara
kuendelea kuchambua na kutoa ufafanuzi kuhusu bakaa ya shilingi 1,284,590/=
Mwenyekiti wa wa timu ya SAM, Bi. Germina Kabola akichangia mada wakati wa mafunzo ya zoezi la SAM wilaya ya Nyamagana
18
Sehemu ya Tatu
Masuala yatokanayo na uhakiki vituoni
3.1 Utawala na Fedha3.1.1. Usimamizi Shirikishi
Katika vituo vya huduma vilivyotembelewa timu ilitaka kujua maswala mbalimbali yanayohusu
usimamizi shirikishi na jinsi yanavyolenga kuboresha huduma ya Mama, Baba na Mtoto.
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kujua katika kipindi cha mwaka 2017/2018 na robo ya kwanza 2018/2019 idara ilifanikiwa
kwa kiasi gani kufanya usimamizi shirikishi katika robo zote? Na je ni changamoto zipi ambazo timu ya
usimamizi /CHMT inazokumbana nazo katika kutekeleza usimamizi shirikishi?
Majibu ya Menejimenti
Ziara za usimamizi shirikishi zilifanyika kwenye vituo vya huduma za afya japo kulikuwa na changamoto
mbalimbali zikiwa ni pamoja na:-
• Uhabawamagariyakufanyiaziara(Idarainagarimojatuzimakwashughulizautawala).
• Uhabawamafutauliosababishwanakiasikidogochapesakilichopangwawakatiwabajeti.
• KucheleweshwakwafedhazaMfukowaPamojaambapokunashughulizausimamizi
3.1.2. Hali ya Mapato na MatumiziUhakiki wa timu vituoni ulibaini uwepo wa hali duni ya mapato ya ndani ukilinganisha na makadirio ya
makusanyo. Hata hivyo taarifa za mapato na matumizi ya vituo ziliwekwa katika mbao za matangazo
kwa ajili ya matumizi ya umma.
Hoja ya Timu
Timu imeipongeza idara na vituo kwa kusimamia na kuhakikisha uwepo wa taarifa za mapato na
matumizi katika mbao za matangazo. Hata hivyo, ingependa kufahamu mkakati uliopo wa kuongeza
mapato katika vituo.
Wajumbe wa timu ya SAM wakifanya zoezi la uhakiki vituoni
19
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti imepokea pongezi hizi na inaendelea kuboresha masuala ya uwazi na uwajibikaji
hususani kwenye fedha na bajeti katika ngazi za vituo vya huduma kwa ujumla.
3.1.3. Mfumo wa Ukusanyaji wa MapatoUhakiki wa timu katika vituo vyote ulionesha kuwa sehemu kubwa ya mapato yanatokana na malipo
ya ‘papo kwa papo’ huku mfumo wa ukusanyaji kwa TIKA ukionesha kutokuwa hai jambo linaloweza
kuathiri uendelevu wa huduma vituoni.
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kufahamu mkakati uliopo kuimarisha TIKA ama CHF iliyoboreshwa ili kuongeza mapato
na kumpunguzia mwananchi wakawaida mzigo wa malipo ya papo kwa papo.
Majibu ya Menejimenti
Idara inaendelea na mikakati mbalimbali inayoelekezwa kwa ajili ya kuboresha Bima za Afya za Jamiii
ikiwemo CHF ya sasa kuwa CHF iliyoboreshwa. Aidha, katika kufanikisha hilo idara imenunua jumla
ya simu za kiganjani 36 kwa lengo la kuimarisha uandikishaji wa wanachama wa CHF kwenye mfumo
mpya na taratibu za kuwapata waratibu na kuwapa mafunzo zinaendelea.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru kwa ufafanuzi na mikakati na itaendelea kufuatilia utekelezaji hususani uandikishaji
wa wanachama na hali ya utoaji wa huduma.
3.1.4 Akaunti za Vituo Uhakiki wa timu umejiridhisha na uwepo wa akaunti za vituo na zimeonekana kubandikwa katika mbao
za matangazo
Pongezi
Timu inapongeza idara na vituo kuhakikisha uwepo wa akaunti za vituo na kuwa na uwazi wa taarifa
za fedha.
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti inaendelea kuhakikisha akaunti za vituo vya huduma zinatumika kulingana na taratibu na
miongozo iliyopo pamoja na kutoa taarifa za fedha zilizo sahihi kwa umma.
3.1.5 Mafunzo kwa watumishiUhakiki wa timu umebaini kuwa mafunzo kazini hutolewa mara kwa mara hatahivyo kuna uhitaji
mkubwa wa mafunzo ya muda mrefu kwa watumishi wengi.
Hoja ya Timu
Timu ingependa kujua mkakati ulipo kuhakikisha kuna uwiano wa watumishi kupata mafunzo
20
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti imekuwa ikiandaa mpango wa mafunzo kila mwaka kulingana na mahitaji, pia watumishi
wamekuwa wakishiriki mafunzo ya muda mfupi na mrefu yanayokuwa yanatolewa na wadau mbalimbali
kulingana na uhitaji na huduma zinazotolewa kwenye vituo.
Maoni ya Timu
Timu inashauri utaratibu wa mafunzo uwe endelevu na uzingatie uwiano wa watumishi vituoni.
3.1.6. Bodi na Kamati za Usimamizi wa Vituo vya AfyaUhakiki wa timu katika vituo vyote vilivyotembelewa ulionesha uwepo wa kamati za usimamizi wa vituo
hata hivyo baadhi ya kamati zilikuwa na changamoto za kimuundo na kiutendaji.
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kujua kama bodi ya afya imeanza kutekeleza majukumu yake hususani kupitia na
kuidhinisha mipango na ripoti za utekelezaji.
Pia, ni muongozo na utaratibu upi unaotumika kupata wajumbe na wenyeviti wa kamati za usimamizi
wa vituo kwani baadhi ya kamati zimeonesha kuwa wenyeviti wake ni wenyeviti wa mitaa? Kwa
mfano Zahanati za Sahwa na Buhongwa. Pia timu ilipenda kujua taratibu za mafunzo na miongozo ya
uendeshaji wa kamati.
Majibu ya Menejimenti
Wajumbe wa Bodi ya Afya ya Wilaya walishapatikana/chaguliwa na taratibu za uzinduzi wa Bodi
utafanyika kabla ya 15, Oktoba 2018. Aidha, utaratibu wa uundaji wa kamati za vituo unaendelea
kuelekezwa kwenye vituo ili kuweza kupata wajumbe wanao stahili kusimamia kituo na tija kuonekana,
lengo likiwa ni kuboresha huduma za afya.
Maoni ya Timu
Timu inashauri menejimenti ishirikiane na uongozi wa kata na mitaa kurekebisha dosari zilizopo
kwenye kamati za vituo. Kwa mfano katika zahanati za Buhongwa na Sahwa kumeonekana wenyeviti
wa mitaa kuhodhi vyeo vya uenyekiti wa kamati ya afya ya vituo kinyume na miongozo jambo linaloleta
mgongano wa maslahi na uwajibikaji.
3.1.7. Mbao za Matangazo na Sanduku la MaoniUhakiki wa timu umeonesha uwepo wa mbao za matangazo na sanduku la maoni japo katika Hospitali
yaWilaya sanduku lamaoni limedondoka hivyo kuwekwa sehemuambayo si rafiki kwa wapokea
huduma.Masandukumengi hayakuwa na kufuli mbili na pia hayako sehemu rafiki hivyo kufifisha
uwajibikaji na usiri.
21
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kuipongeza idara na vituo kwa kuhakikisha uwepo wa mbao zenye taarifa na sanduku la
maoni. Aidha, timu ilishauri idara kusimamia kamati za vituo kupanga na kuhakikisha masanduku yana
kufuli mbili na funguo zinakaa kwa M/Kiti wa kamati na katibu.
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti inaendelea kufanya maboresho kwenye suala la wateja/wagonjwa kutambua haki zao
pamoja na wajibu wa watoa huduma ili waweze kutoa maoni yao. Aidha, maboresho yanafanyika
kwenye vituo kuhakikisha kunakuwa na masanduku ya kutolea maoni yaliyopo kwenye sehemu za
wazi ambapo mteja anapoweza kuweka maoni bila kuwa na kipingamizi.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru kwa ufafanuzi na itaendelea kufuatilia maboresha yaliyobainishwa na utawala.
Bi. Edna Selestine kutoka Aga Khan akitoa utangulizi juu ya Mradi wa Kuboresha Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto kwa madiwani, wilayani Nyamagana
22
3.2 Rasilimali Watu katika afya3.2.1 Ikama ya WatumishiUhakiki wa timu katika vituo tisa vilivyotembelewa umebaini uhaba wa watumishi vituoni ukilinganisha
na ikama inayopelekea uwiano wa wingi wa kazi na mtumishi kutokuwa sawa. Kwa mfano katika vituo
vya Nyamagana, Buhongwa na Igoma vilionyesha kuzidiwa na wagonjwa huku baadhi ya vituo vengine
vikionekana kuwa na wagonjwa wachache.
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kupata ufafanuzi kuhusu mgawanyo wa watumishi na sababu zinazopelekea baadhi ya
vituo kuwa na wagonjwa wengi huku vingine vikibaki na idadi ndogo.
Majibu ya Menejimenti
Mgawanyo wa watoa huduma unazingatia Ikama ya (2014-2019) pamoja na wingi wa wagonjwa
kwenye baadhi ya vituo. Japokuwa kwa sasa kuna upungufu wa 24% ya watumishi wa kada mbalimbali,
idara inahakikisha watumishi waliopo wanagawanywa kwa usahihi na wale wanaoajiriwa na kuhamia
wanapangwa kulingana na mahitaji na uwiano.
3.2.2 Malipo ya Stahiki za WatumishiKatika vituo vyote tisa vilivyotembelewa, kulikuwapo na madai ya stahiki za watumishi hususani
zinazotokana na kutoa huduma za mkoba.
Hoja ya Timu
Timu ingependa kupata ufafanuzi kuhusu madai ya stahiki hizo kwa kuwa kutokulipwa stahiki kwa
wakati kunaweza kuathiri ari ya utendaji kazi.
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti imekiri kuwepo kwa madai mbalimbali ya stahiki za watumishi kama likizo, wito wa
dharura(on-call), na matibabu. Aidha, idara imejipanga kuhakikisha inapunguza madai haya kwa
kulipa pindi fedha zinapokuwepo. Kwa mfano, katika kipindi cha mwezi Agosti zaidi ya watumishi 25
wametengewa fedha za kulipwa posho za likizo na taratibu za malipo zimeanza. Pindi fedha za mfuko
wapamojazitakapofikawatumishiwanaodaiposhozahudumayamkobawatalipwakwanizilikuwa
zimetengwa kwenye bajeti.
Maoni ya Timu
Timu inapongeza kwa jitihada hizo na itaendelea kufuatilia hali ya utekelezaji wa mkakati huo ngazi ya
menejimenti na ngazi ya vituo.
3.2.3 Tathimini ya Utendaji kaziSuala la maadili ya watumishi lilijitokeza kwa baadhi ya vituo hususani zahanati ya Fumagila na
kituo cha Afya Igoma. Utendaji umeonekana kutoridhisha kwani wagonjwa walilalamika lugha chafu,
23
kutokuthaminiwa na watoa huduma kutokuwepo kazini kwa wakati. Kwa mfano, katika zahanati ya
Fumagilawatumishiwannetukatiyatisawalikuwepokituoniwakatitimuilipofikasaa5asubuhi.
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kufahamu kama idara ya afya inatambua changamoto hizo na upi mkakati uliopo
kurekebisha changamato hizo.
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti imeendelea kuwaelekeza watumishi taratibu na maadili ya utumishi wa umma pamoja na
kuwakemea wale wanaobainika kutoa lugha mbaya kwa wagonjwa au kwa wahudumu wenzao. Aidha,
Ofisihaitositakumchukuliahatuazakinidhamumtumishiatakayebainikakwaushahidiwakukiuka
taratibu za Utumishi wa Umma.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru na kupongeza idara dhamira hiyo kwani hatua hizo ni za kiuwajibikaji.
3.3. Dawa na Vifaa Tiba3.3.1 Hali ya Upatikanaji wa Dawa MuhimuUhakiki wa timu umebaini uwepo wa dawa katika vituo vyote. Timu inapenda kuipongeza idara kwa
kuhakikisha upatikanaji wa dawa katika vituo. Pamoja na pongezi hizo, timu inashauri idara kuhakikisha
upungufu wa dawa vituoni unakuwa historia kwa kuweka mikakati endelevu.
3.3.2 Hali ya Upatikanaji wa Vifaa TibaUhakiki wa timu umeonesha vifaa tiba havitoshelezi katika vituo vya kutolea huduma. Kwa mfano
ukosefu wa kifaa cha kupimia wingi wa damu kituo cha Sahwa, uhaba wa vifaa vya kutolea huduma za
dawa ya usingizi katika hospitali ya Nyamagana (kipo kimoja na uhitaji ni mkubwa kwa wastani kila saa
moja mtoto mmoja huzaliwa hospitali hapo na baadhi huhitaji upasuaji).
Hoja ya Timu
Timu ingependa kufahamu mkakati uliopo kurejesha huduma za dawa za usingizi na kifaa cha
kumsaidia mtoto mchanga kupumua ili kuokoa maisha ya wakina mama na watoto wachanga.
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti inapenda kukiri kuwa hospitali ya wilaya ilikuwa na changamoto ya huduma ya usingizi
kwa kipindi cha wiki 3 lakini kwa sasa vifaa na dawa zimenunuliwa na huduma za upasuaji wa dharura
zinaendelea kutolewa kama kawaida.Aidha, kutokana na ufinyu wa jengo la wazazi kuna baadhi
ya vifaa vinalazimika kuwepo kimoja ama viwili na pindi upanuzi wa jengo utakapokamilika huduma
zitaboreka zaidi.
24
3.3.3 Vyumba na Kabati za Kuhifadhia DawaUhakikiwatimukatikavituovilivyotembelewaumeoneshauwepowavyumbafinyuvisivyokidhimahitaji
ya uhifadhi wa dawa na kabati za kutunzia dawa zisizoridhisha.
Hoja ya Timu
Timu ingependa kufahamu mkakati uliopo wa kutatua changamoto hiyo vituoni.
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti imeendelea kuwaelekeza watumishi taratibu na maadili ya utumishi wa umma pamoja na
kuwakemea wale wanaobainika kutoa lugha mbaya kwa wagonjwa au kwa wahudumu wenzao. Aidha,
Ofisihaitositakumchukuliahatuazakinidhamumtumishiatakayebainikakwaushahidiwakukiuka
taratibu za Utumishi wa Umma.
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti inakiri kuwepo na changamoto ya miundombinu katika vituo vya huduma suala ambalo
linafanyiwa kazi na idara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali mathalani shirika kisilo la kiserikali
AGPAHI wanaokarabati majengo ya kuhifadhia dawa kwenye baadhi ya zahanati.
3.4 Miundombinu ya Afya3.4.1 Vizimba vya kuchomea Taka na Shimo la Kondo la UzaziUhakiki wa timu katika vituo vilivyotembelewa umeonesha uwepo wa vichomea taka na shimo la kondo
la uzazi vyenye ubora katika vituo vya Nyamagana, Igoma, Bugarika, Shadi na Sahwa.
Hata hivyo, vituo vya Fumagila na Buhongwa havikuwa kabisa na vichomea taka wala shimo la kondo
la uzazi. Aidha kwa vituo vya Makongoro na Mkolani kuna vichomea taka na shimo la kondo visivyo na
ubora.KwaupandewaMakongorohusafirishatakakatikaHospitaliyaNyamaganakwauteketezaji.
Karibu vituo vyote, mashimo ya kondo la uzazi hayana kufuli na imeonekana kondo kuchanganywa na
mifuko ya nailoni kitu kinachoweza kupelekea kuchelewa kuoza na kuwahi kujaa shimo.
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kujua idara ina mkakati upi kuondoa changamoto hizo zilizoainishwa?
Majibu ya Menejimenti
Ujenzi wa mashimo ya kuchomea taka pamoja na utupaji wa kondo la nyuma la mama anapomaliza
kujifungua unaendelea kwenye vituo mbalimbali visivyokuwa na huduma hiyo kwa kutumia fedha za
uchangiaji na RBF. Aidha suala la utupaji wa kondo pamoja na mifuko ya nailoni si sahihi, menejimenti
itaendelea kutoa maelekezo ya utupaji sahihi.
25
3.4.2 Mfumo wa Maji SafiUhakiki wa timu umeonesha kuwa vituo vya Fumagila, Igoma, Makongoro, Bugarika vina mifumo
thabitiyamajisafina taka.Aidha,pamojanahospitaliyaNyamaganakuwanamfumowamajiya
MWAUWASA, kuna ukosefu wa mifumo ya kuhifadhi maji. Pia zahanati ya Shadi ilionekana kukatiwa
maji tangu mwezi wa tano ambapo ankara ya maji waliyopewa ya laki mbili haikuwa inaakisi matumizi.
Aidha katika vituo vingine mifumo ya kuhifadhi maji haikuwa na maji kabisa jambo linaloweza kuathiri
usalama na afya wa watoa na watumia huduma.
Hoja ya Timu
Timu ilingependa kujua mkakati uliopo kufunga mfumo wa uhifadhi maji Hospitali ya Nyamagana na
kurejesha maji katika kituo cha Shadi ambacho kimekatiwa maji.
Majibu ya Menejimenti
Maji ni muhimu sana hususani kwenye taasisi zinazohusika na kutoa huduma za kijamii, Idara
inahakikishavituovyakevyotevinafikiwanahudumayamajikwakushirikishaofisiyaMhandisiwa
Maji wa Jiji. Aidha hospitali inarekebisha mifumo yake ya maji na kwa na tanki za kuhifadhi.
Kushoto: Mifuko ya nailoni ikiwa imetupwa katika shimo la kutupia kondo la uzazi kinyume na utaratibu, zahanati ya SahwaKulia: Wajumbe wa timu ya SAM pamoja na mtoa huduma katika kituo cha Igoma wakihakiki ubora wa kichomea taka
26
3.4.3. Hali ya Vyoo na Usafi wa MazingiraUhakiki wa timu katika vituo vilivyotemebelewa umeonesha uwepo wa vyoo na hali ya usafi kwa
sehemu kubwa inaridhisha isipokuwa miundombinu inahitaji maboresho. Mfano; Milango ya vyoo vya
zahanati ya Fumagila. Timu inaipongeza idara na vituo kwa kuboresha mazingira ya vyoo.
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti inapokea pongezi hizo na kuahidi kuboresha huduma za vyoo sio kwa vituo vya kutolea
huduma tu bali hata ngazi ya kaya ili kuhakikisha wilaya haipati magonjwa ya mlipuko yakiwemo
kipindupindu na kuhara.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru kwa ufafanuzi na inapongeza kwa mkakati wa kufika ngazi ya kaya. Itaendelea
kufuatilia utekelezaji wa mkakati huo.
3.4.4 Ujenzi na Ukarabati wa Majengo na miundombinu ya barabaraUhakiki wa timu vituoni umeonesha kuwa hospitali ya Nyamagana inahitaji mkakati maalumu ili
kuboresha wa miundombinu pamoja na majengo kwa kuwa majengo mengi hayakidhi hadhi ya hospitali.
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kujua mkakati uliopo ili kuboresha hospitali ya wilaya.
Majibu ya Menejimenti
Hospitali ya wilaya haikidhi vigezo, hii inatokana na kuhuishwa kutoka kituo cha afya kuwa Hospitali
mwaka 2007. Hali hii inapelekea kukosekana kwa miundombinu ya msingi ikiwemo jengo la utawala,
wodi ya wanaume, jengo la kuhifadhia maiti na mengineyo. Aidha, Idara inaendelea kuboresha
miundombinu hiyo kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali, shukrani ziwaendee AGPAHI wanaojenga
jengo la kinamama na jengo la huduma za upasuaji.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru kwa ufafanuzi na itaendelea kufuatilia utekelezaji wa mikakati hiyo.
Wajumbe wa timu ya SAM wakifanya
uhakiki wa wa hali ya vyoo katika
zahanati ya Fumagila wilayani
Nyamagana
27
3.4.5 Nyumba za WatumishiUhakiki wa timu katika vituo vilivyotembelewa umebaini kuwa baadhi ya zahanati hazina nyumba
za watumishi, na zilizopo zinahitaji ukarabati. Katika zahanati ya Mkolani, timu iligundua kuwa kuna
nyumba moja ya watumishi japo anayeishi si mtumishi wa kituo hicho kwani alihamishiwa hospitali ya
Nyamagana. Vilevile, nyumba hiyo inahitaji ukarabati.
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kupata ufafanuzi ikiwa mtumishi wa kituo kingine anaweza kuishi katika nyumba za vituo
vingine. Pia, usimamizi wa nyumba na mtumishi huyo uko chini ya mfawidhi wa kituo kipi?
Majibu ya Menejimenti
Wilaya ina uhaba wa nyumba za watumishi kwa zaidi ya 80%, hali inayopelekea watumishi kupanga
aukutumiagharamakubwakufikakwenyevituovyaovyakutoleahuduma.Aidha,wilayainaendelea
na mkakati wa kujenga nyumba za watumishi. Suala la mtumishi wa hospitali anayeishi katika nyumba
yazahanatiyamkolani;ofisiinalifanyiakazi.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru kwa ufafanuzi na inashauri halmashauri iendelee kuhakikisha ujenzi wa nyumba
unatekelezwa ili kuboresha mazingira ya kazi vituoni.
3.4.6 Nishati ya UmemeUhakiki wa timu umeonesha uwepo wa nishati ya umeme na unafanya kazi katika vituo vingi
vilivyotembelewa isipokuwa zahanati ya Shadi.
Pongezi
Timu inaipongeza idara na vituo kwa kuhakikisha uwepo wa nishati ya umeme na inafanya kazi katika
maeneo mengi.
Majibu ya Menejimenti
Idara imepokea pongezi hizo na inaendelea kuhakikisha vituo visivyo na umeme mfano zahanati ya
Shadi vinafungiwa umeme na taratibu zinaendelea kwa sasa.
28
3.4.7 Usalama na Utulivu katika Vituo vya kutolea HudumaKatika zahanati ya Buhongwa imeonekana jamii kuingilia eneo la zahanati kwa kukata wigo na kuhifadhi
matenga ya nyanya na vifaa vya biashara. Hali hii inaweza kuondoa utulivu na kuhatarisha usalama
katika zahanati.
Hoja ya Timu
Timu ilipenda kufahamu mkakati uliopo usalama na utulivu katika vituo vya kutolea huduma unakuwepo
Majibu ya Menejimenti
Menejimenti itawasiliana na uongozi wa serikali za mitaa na kamati za vituo kuhakikisha vituo vinakuwa
kwenye hali ya usalama muda wote na maeneo ya vituo yanalindwa na kuheshimiwa.
Maoni ya Timu
Timu inashukuru kwa dhamira iliyooneshwa ila inapenda kushauri suala la wafanyabiashara wa nyanya
katika kituo cha Buhongwa linashughulikiwa kwa haraka.
Diwani kutoka kata ya Mhandu wilayani Nyamagana Mh. Sima Constantine akichangia jambo katika mkutano wa Madiwani wakati wa utekelezaji wa zoezi la SAM
29
4.0 Mapendekezo
Timu ya SAM imetoa mapendekezo yafuatayo;
1. Kuimarisha Mifumo ya Uwajibikaji: Kwa kuwa mfumo wa SAM unaakisi vizuri namna ya kusimamia
mzunguko wa mipango na bajeti wa serikali, timu ya SAM inapendekeza mamlaka na vyombo vya
usimamizi vya Jiji kuanza mchakato wa kutumia mfumo huu ili kuimarisha ufuatiliaji na usimamizi
wa rasilimali za umma na huduma zitolewazo kwa umma.
2. Kuboresha Uandaaji wa Mipango na Ripoti za afya kama vile mpango kabambe wa afya wa wilaya
na vituo, ripoti za utekelezaji na fedha n.k.
3. Kuimarisha usimamizi katika vituo ili kuweza kugundua changamoto zilizoko na kuzipatia ufumbuzi
kwa wakati.
4. Kuboresha majengo na miundombinu mingine ili kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za uzazi
kwa jamii.
Sehemu ya Nne
30
4.1 Maazimio ya PamojaMaazimioyaliyofikiwakwapamojanawadauyalilengakuboreshamaeneoyaliyobainishwana timu
kwa idara na halmashauri kuyafanyia kazi ikishirikiana na wadau mbalimbali ili kuboresha upatikanaji
wa huduma ya afya kwa Mama, Baba na Mtoto.
Jedwali 2: Maazimio ya UtekelezajiNa Azimio Utekelezaji Muhusika1 Kuboresha Uandaaji na
Uandishi wa NyarakaKuongeza umakini wakati wa uandaaji wa nyaraka mbalimbali kwa kuzingatia miongozo na kanuni ili kuondoa kasoro zilizobainishwa na timu ya SAM katika mipango ijayo.
CHMT
CMT
2 Kuboresha Mifumo ya Uwajibikaji, Usimamizi na Uangalizi
Kuweka kufuli mbili kwenye masanduku ya maoni, Kubandika wa taarifa kwenye mbao za matangazo kwa ajili ya umma (bajeti za vituo, majina ya wajumbe wa kamati, majina na namba za simu za waganga wafawidhi) ili kukuza utawala bora katika ngazi zote.
CHMT
HGGC
DHSB
Kamati ya huduma za Jamii na Baraza la Madiwani
3 Mwingiliano wa shughuli za jamii na vituoni
Kumaliza Changamoto ya muingiliano wa jamii/wafanyabiashara katika zahanati ya Buhongwa kwa kushirikisha uongozi wa mtaa, kata na jamii.
WEO Buhongwa
4 Kuimarisha Usimamizi Shirikishi
Kutoa taarifa juu ya mwenendo wa huduma na maadili ya watoa huduma na watumia huduma kwa kuzingatia miongozo inayobainisha wazi haki na wajibu wa watoa na wapokea huduma kwa ngazi zote.
CHMT
HGGC
DHSB
5 Kufuatilia na kufanyia kazi madai na stahili mbalimbali za watumishi
Kufuatilia, kufanyia kazi na kulipa stahiki mbalilimbali za watumishi ili kuimarisha ufanyaji kazi bila kuathiri ari ya watumishi.
CHMT
31
6 Kuboresha mafunzo kazini kulingana na mahitaji
Kutoa mafunzo kazini kulingana na mahitaji pamoja na upatikanaji wa fedha au wadau mbalimbali wanaofanya kazi na Jiji.
CHMT
7 Kuimarisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba
Kuimarisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba vituoni.
CHMT
Hospitali
Vituo vya afya
Zahanati
8 Uboreshaji wa miundombinu ya kuhifadhia dawa
Vituo kwa kushirikiana na halmashauri ya jiji kuweka mikakati na mipango kwa mwaka 2019/20 kuboresha miundombinu ya kuhifadhia dawa ikiwa ni pamoja na vyumba na makabati ya kuhifadhia dawa na vifaa tiba katika vituo.
CHMT
Hospitali
Vituo vya afya
Zahanati
9 Mkakati wa kupata magari kwa ajili ya huduma za afya
Idara kushirikiana na Jiji kuweka kwenye mipango ya 2019/20 kupata magari hasa sehemu ya utawala na vituo vya afya ili kuimarisha utaratibu wa huduma haswa wagonjwa/kina mama wajawazito na hata kuwapeleka rufaa.
CMT
CHMT
Hospitali
Vituo vya afya
Zahanati
10 Kuwashirikisha viongozi wa mitaa
Kuwaandikia barua yenye kuwataka viongozi wa mitaa/vijiji, kuimarisha ushiriki na ushirikishwaji wa jamii katika maswala ya afya ya uzazi.
CHMT
WEOs
32
4.2 HitimishoUtekelezwaji wa zoezi la SAM kwa Jijila Mwanza ulianza kwa kupitia hatua mbalimbali na umekamilika
katika sehemu yake ya kwanza kwa mafanikio makubwa hasa kutokana na ushirikiano uliotolewa na
viongozi wa wilaya, jiji, Aga Khan Faundation na wadau wote wa afya. Ni jambo linalotia faraja kwa
wadau wote kuonyesha mwamko wa kuboresha huduma za afya ya Mama, Baba na Mtoto. Hivyo ni
matumaini makubwa kwamba changamoto na mapendekezo yaliyotolewa yatafanyiwa kazi kwa wakati
naIdarayaAfyanawadauwenginekamailivyoafikiwakatikakikaochandaninakilechamrejesho
kwa wadau wa afya. Utekelezaji wa maazimio kwa wakati utachangia katika kuboresha upatikanaji wa
huduma za afya hasa huduma za afya ya mama, baba na mtoto. Vilevile, utekelezaji utaipa nguvu timu
ya SAM na jamii nzima ya Nyamagana kushiriki kikamilifu katika kuboresha huduma za afya katika
maeneo yao.
33
Kiambatanisho 1Vituo vilivyotembelewa na timu ya SAM
1. Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana
2. Kituo cha Afya Igoma3. Kituo cha Afya Makongoro4. Zahanati ya Bugarika5. Zahanati ya Buhongwa6. Zahanati ya Fumagila7. Zahanati ya Mkolani8. Zahanati ya Sahwa9. Zahanati ya Shadi
Kiambatanisho 2
Wajumbe wa Timu ya Ufuatiliaji Uwajibikaji Jamii (UJJ) /SAM-2018Na JINA JINSIA UWAKILISHI1 ADAM H. MALUZUKU ME WEO - BUHONGWA2 ADELFINA E MWENURA KE MWAKILISHI JAMII3 EDITH JOHN KE CHMT
4 EDWARD MISALABA ME MWAKILISHI JAMII5 FARIDA MZIMBIRI KE TAHEA MWANZA6 FORTUNATA SWAI KE CMT7 GERMINA P. KABOLA KE DIWANI8 IBRAHIM N. ENOCK ME CHAWATA9 NATUS MAGORI ME M/KITI BODI YA AFYA10 NYEMBE ROBERT NYEMBE ME M/KITI ZAHANATI SAHWA11 PENDO PASCHAL KE VIKUNDI WANAWAKE12 SAPHIA RAMADHAN KE MWAKILISHI JAMII13 VICENT L.TEGGE ME MADIWANI14 WINFRIDA PETER KE MWAKILISHI JAMII15 YUSTO A. KEMBO ME KAMATI YA AFYA KATA
Sikika inafanya kazi ya kuhimiza uboreshaji wa mifumo ya afya na
usimamizi wa fedha kupitia uwajibikaji jamii na uraghibishi
katika ngazi zote za serikali
Nyumba Na.69Ada Estate, Kinondoni Barabara ya Tunisia Mtaa wa WaverleyS.L.P 12183Dar es Salaam, Tanzania.Simu: +255 22 26 663 55/57
Nyumba Na. 340 Mtaa wa Kilimani S.L.P 1970 Dodoma, Tanzania. Simu: 0262321307 Nukushi: 0262321316
Ujumbe mfupi: 0688 493 882 Nukushi: +255 22 26 680 15Barua pepe: [email protected] Tovuti: www.sikika.or.tzTwitter: @sikika1Facebook: Sikika1Instagram: Sikika1