57
Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 1 RIPOTI YA KAMATI YA FEDHA, BIASHARA NA KILIMO YA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR KWA MWAKA WA FEDHA 2018/2019 1. UTANGULIZI Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ni miongoni mwa Kamati nane za Kudumu za Baraza la Wawakilishi iliyoundwa kwa mujibu Kanuni ya 106, Jadweli la Kwanza la Kanuni za Kudumu za Baraza la Wawakilishi, Toleo la mwaka 2016. Kamati hiyo imepangiwa kutekeleza majukumu yafuatayo: i. Kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Kamati yaliyotolewa kwenye ripoti ya Kamati ya mwaka uliotangulia. ii. Kufuatilia utekelezaji wa Sera na Mipango ya Wizara husika kwa kadiri Spika atakavyoelekeza kwa mujibu wa malengo yaliyowasilishwa Barazani wakati wa usomaji Bajeti na Hotuba nyengine za Waziri alizotoa katika Baraza. iii. Kufuatilia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ya Kitaifa na ya Wananchi ya Wizara husika. iv. Kuchunguza na kufuatilia mapato na matumizi ya kila mwaka ya Serikali na kuona kwamba matumizi yaliyofanywa yalizingatia thamani halisi ya fedha. v. Kuchambuwa mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya Wizara husika ya mapato na matumizi ya kila mwaka. vi. Kushughulikia Miswada ya Sheria itakayokabidhiwa kwake na Spika. vii. Kuchambuwa ahadi zote za Wizara zilizo chini ya Kamati kama zitakavyokuwa zikitolewa katika Baraza na kufatilia utekelezaji wa ahadi hizo. viii. Kuzingatia na kutekeleza jambo jengine lolote litakalopelekwa kwake na Spika. Katika kutekeleza majukumu yaliyopo hapo juu, Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inasimamia utekelezaji wa majukumu ya Wizara zifuatazo: Wizara ya Fedha na Mipango; Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi; na Wizara ya Biashara na Viwanda. 1.1 MUUNDO WA KAMATI Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo imeundwa na Wajumbe saba na Makatibu wawili wafuatao: 1. Mhe. Dkt. Mwinyihaji Makame - Mwenyekiti; 2. Mhe. Hamida Abdalla Issa - Makamu Mwenyekiti; 3. Mhe. Ali Salum Haji - Mjumbe; 4. Mhe. Wanu Hafidh Ameir - Mjumbe; 5. Mhe. Masoud Abrahman Masoud - Mjumbe; 6. Mhe. Moh’d Mgaza Jecha - Mjumbe; 7. Mhe. Nadir Abdul-latif Yussuf - Mjumbe;

RIPOTI YA KAMATI YA FEDHA, BIASHARA NA KILIMO YA BARAZA … · 2019-02-15 · Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha

  • Upload
    others

  • View
    84

  • Download
    1

Embed Size (px)

Citation preview

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 1

RIPOTI YA KAMATI YA FEDHA, BIASHARA NA KILIMO YA BARAZA LA WAWAKILISHI

ZANZIBAR KWA MWAKA WA FEDHA 2018/2019

1. UTANGULIZI

Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ni miongoni mwa Kamati nane za Kudumu za

Baraza la Wawakilishi iliyoundwa kwa mujibu Kanuni ya 106, Jadweli la Kwanza la

Kanuni za Kudumu za Baraza la Wawakilishi, Toleo la mwaka 2016. Kamati hiyo

imepangiwa kutekeleza majukumu yafuatayo:

i. Kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Kamati yaliyotolewa kwenye ripoti

ya Kamati ya mwaka uliotangulia.

ii. Kufuatilia utekelezaji wa Sera na Mipango ya Wizara husika kwa kadiri Spika

atakavyoelekeza kwa mujibu wa malengo yaliyowasilishwa Barazani wakati wa

usomaji Bajeti na Hotuba nyengine za Waziri alizotoa katika Baraza.

iii. Kufuatilia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ya Kitaifa na ya Wananchi ya

Wizara husika.

iv. Kuchunguza na kufuatilia mapato na matumizi ya kila mwaka ya Serikali na

kuona kwamba matumizi yaliyofanywa yalizingatia thamani halisi ya fedha.

v. Kuchambuwa mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya Wizara husika ya

mapato na matumizi ya kila mwaka.

vi. Kushughulikia Miswada ya Sheria itakayokabidhiwa kwake na Spika.

vii. Kuchambuwa ahadi zote za Wizara zilizo chini ya Kamati kama zitakavyokuwa

zikitolewa katika Baraza na kufatilia utekelezaji wa ahadi hizo.

viii. Kuzingatia na kutekeleza jambo jengine lolote litakalopelekwa kwake na Spika.

Katika kutekeleza majukumu yaliyopo hapo juu, Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo

inasimamia utekelezaji wa majukumu ya Wizara zifuatazo:

Wizara ya Fedha na Mipango;

Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi; na

Wizara ya Biashara na Viwanda.

1.1 MUUNDO WA KAMATI

Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo imeundwa na Wajumbe saba na Makatibu wawili

wafuatao:

1. Mhe. Dkt. Mwinyihaji Makame - Mwenyekiti;

2. Mhe. Hamida Abdalla Issa - Makamu Mwenyekiti;

3. Mhe. Ali Salum Haji - Mjumbe;

4. Mhe. Wanu Hafidh Ameir - Mjumbe;

5. Mhe. Masoud Abrahman Masoud - Mjumbe;

6. Mhe. Moh’d Mgaza Jecha - Mjumbe;

7. Mhe. Nadir Abdul-latif Yussuf - Mjumbe;

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 2

8. Ndg. Asma Ali Kassim - Katibu; na

9. Ndg. Said Khamis Ramadhan - Katibu.

1.2 UTARATIBU WA KAZI ZA KAMATI

Katika utekelezaji wa kazi zake chini ya Kanuni ya 108 ya Baraza la Wawakilishi, Kamati

ilifanya kazi kwa utaratibu wa kupokea taarifa tofauti za kila robo mwaka (quarterly

reports) za utekelezaji wa malengo ya Bajeti ya Wizara, kupokea taarifa za utekelezaji wa

Maagizo ya Kamati, kukutana na wadau mbali mbali wa sekta zinazosimamiwa na

Kamati pamoja na kukagua baadhi ya maeneo na miradi mbali mbali inayosimamiwa na

Wizara zinazohusika ili kuona hatua za utekelezaji zilizofikiwa.

Kwa mwaka wa fedha 2018/2019, hadi Kamati inawasilisha ripoti yake mbele ya Baraza

hili tukufu ilifanya kazi zake kwa mizunguko mitatu kwa muda wa wiki sita, Unguja,

Pemba na Tanzania Bara.

1. Mzunguko wa kwanza ulianzia tarehe 27 Agosti, 2018 hadi tarehe 31 Septemba,

2018 Unguja na tarehe 03 Septemba, 2018 hadi tarehe 07 Septemba, 2018 Pemba.

2. Mzunguko wa pili ulianzia tarehe 05 Novemba, 2018 hadi tarehe 09 Novemba,

2018 Unguja na tarehe 12 Novemba, 2018 hadi tarehe 16 Novemba, 2018

Tanzania Bara.

3. Mzunguko wa tatu ulianzia tarehe 14 Januari, 2019 hadi tarehe 18 Januari, 2019

Pemba na tarehe 21 Januari, 2019 hadi tarehe 25 Januari, 2019.

Ripoti hii imeandaliwa kwa kufuata maelekezo ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984,

Sheria ya Baraza la Wawakilishi na Kanuni zake (Toleo la 2016), Taarifa za utekelezaji wa

malengo ya Wizara, ziara mbali mbali za ndani na nje ya Zanzibar, Taarifa za utekelezaji

wa maagizo ya Kamati na ripoti mbalimbali zilizotokana na tafiti zilizofanywa na Wizara

zinazosimamiwa na Kamati hii.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 3

2. WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

Wizara ya Fedha na Mipango ndio roho ya nchi yetu kiuchumi ambayo inasimamia

makusanyo yote ya Serikali na kufanya malipo kwa Taasisi za Serikali ili ziweze

kutekeleza majukumu yao ipasavyo. Aidha, Wizara hii pia ndio inayohusika na upangaji

wa Bajeti kuu ya Serikali na mpango mzima wa matumizi yaliyokusudiwa. Kwa mwaka

2018/2019, Wizara ya Fedha na Mipango ilipanga kutekeleza Programu Kuu zifuatazo:

a) Programu kuu ya Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya Fedha na Mipango;

b) Programu kuu ya Usimamizi na Uwekezaji wa Mali za Umma;

c) Programu kuu ya Usimamizi wa Bajeti na Fedha za Umma;

d) Programu kuu ya Usimamizi wa Mfuko Mkuu wa Serikali;

e) Programu kuu ya Kuratibu Mipango ya Kitaifa na Maendeleo ya Watendakazi;

f) Programu kuu ya Usimamizi wa Uchumi Mkuu; na

g) Programu kuu ya Utawala na Uendeshaji wa Tume ya Mipango.

Programu hizo zinatekelezwa na Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Idara zifuatazo:

i. Idara ya Mipango, Sera na Utafiti;

ii. Idara ya Uendeshaji na Utumishi;

iii. Idara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali;

iv. Idara ya Bajeti;

v. Idara ya Fedha za Nje;

vi. Idara ya Mitaji ya Umma;

vii. Idara ya Hesabu za Ndani;

viii. Idara ya Fedha za Kodi;

ix. Mamlaka ya Ununuzi na Uondoshaji wa Mali za Umma; na

x. Ofisi Kuu Pemba.

Mbali na Idara hizo na kutokana na umuhimu wake, Wizara ya Fedha na Mipango

inakamilisha muundo wake kwa Taasisi zifuatazo zinazojitegemea:

i. Tume ya Mipango

ii. Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB);

iii. Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ);

iv. Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA);

v. Mfuko wa Barabara (ZFR);

vi. Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC);

vii. Bodi ya Rufaa za Kodi Zanzibar (Tax Appeal Board);

viii. Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF);

ix. Mahkama ya Rufaa za Kodi; na

x. Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 4

Kadhalika, Wizara ya Fedha na Mipango inazo Taasisi kadhaa ambazo ni za Muungano

lakini zinafanya kazi zake hapa Zanzibar. Taasisi hizo ni:

i. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA);

ii. Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA);

iii. Benki Kuu ya Tanzania (BOT); na

iv. Tume ya Pamoja ya Fedha (JFC) - Tawi la Zanzibar.

Katika kuhakikisha fedha za Serikali zilizotolewa kwa Wizara ya Fedha na Mipango na

zinatumika kama ilivyokusudiwa, Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ilifanya vikao

tofauti kuhoji utekelezaji wa Programu ambazo Wizara imeingiziwa fedha na kufanya

ziara kadhaa zilizolenga kujionea na kutathmini thamani ya halisi ya fedha “Value for

Money”. Aidha, Kamati ilikusudia pia kuangalia mafanikio yaliyopatikana na

changamoto zilizopo katika utekelezaji wa Programu za Wizara ya Fedha na Mipango

pamoja na miradi ya Maendeleo.

2.1 UTEKELEZAJI WA PROGRAMU ZA WIZARA

Kwa mwaka wa fedha 2018/2019, utekelezaji wa Programu zote za Wizara ya Fedha na

Mipango ulipangiwa kuingiziwa jumla ya shilingi 154,764,013 bilioni. Hadi kufikia

Disemba 2018, jumla ya shilingi 134.68 bilioni ziliingizwa kutekeleza mambo tofauti sawa

na asilimia 89 ya makadirio. Aidha, kwa kipindi hicho, jumla ya shilingi 21.02 bilioni

zilipangwa kukusanywa ambapo hadi kufikia Disemba 2018, jumla ya shilingi 18.99

bilioni sawa na asilimia 90 ya makadirio zimekusanywa. Tathmini ya utekeleza

unaotokana na matumizi ya fedha hizo unaonekana katika utekelezaji wa Programu Kuu

zifuatazo.

2.2 PROGRAMU KUU YA URATIBU NA UENDESHAJI WA WIZARA

Programu hii imekusudia kuweka mazingira bora kwa wafanyakazi, kuwa na mipango na

sera ya sekta za fedha iliyoimara nchini itakayosaidia kukuza uchumi pamoja na

kuhakikisha shughuli zilizopangwa kwa sekta ya fedha zinatekelezwa. Utekelezaji wa

Programu hii unafanywa na Idara ya Mipango, Sera na Utafiti, Idara ya Uendeshaji na

Utumishi na Afisi Kuu Pemba. Miongoni mwa mambo ambayo yametekelezwa na

Programu hiyo ni:

2.3 UJENZI WA AFISI YA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO PEMBA

Kamati inaipongeza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kufikiria na kutekeleza Mradi

mkubwa wa Ujenzi wa Afisi mpya ya Wizara ya Fedha na Mipango Pemba kwa pesa

zake wenyewe. Hakika ujenzi wa Afisi hizo ambazo zitatumiwa na Wizara tatu za Serikali

(Wizara ya Fedha na Mipango Pemba na Taasisi zake, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria,

Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Taasisi zake pamoja na Wizara ya Kazi,

Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto utaondoa changamoto kwa watendaji ya

kufanya kazi katika mazingira yasiyoridhisha. Kamati imeridhihwa na ubora wa ujenzi

huo inaonekana wazi kwamba jengo litakapomalizika litakuwa limezingatia thamani

halisi ya fedha “value for money”. Kadhalika, jengo hilo pia ni la kisasa na limezingatia

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 5

uwepo wa miundombinu ya watu wasiojiweza kwa kuwatengenezea mazingira mazuri

yatakayowawezesha kufika hadi katika ukumbi mkubwa wa mikutano uliopo juu ya

jengo na kutumia huduma mbali mbali ikiwemo vyoo maalum vilivyojengwa kwa ajili

yao.

Jengo hilo limejengwa na Kampuni ya Mzalendo “Quality Building Contractor” (QBC)

na kusimamiwa na Mshauri Elekezi “Zanzibar Consultant Limited” lilianza mwezi wa

Septemba, 2016 kukiwa na dhana ya kujengwa ghorofa mbili na kutarajiwa kumalizika

mwezi Machi, 2018. Baada ya kufanya tathmini ya ujenzi huo, Wizara iliona kwamba

ujenzi huo uwe wa ghorofa tatu na kupelekea muda wa kukamilika kwake kuwa

Disemba, 2018. Kutokana na ukosefu wa baadhi ya vifaa vikiwemo aluminium,

umefanya ujenzi huo ukadiriwe kumalizika mwishoni mwa mwezi wa Februari, 2019.

Ujenzi huo wenye ukubwa wa eneo la mita za mraba 9,988 umepangwa kutumia shilingi

13.6 Bilioni hadi kumalizika kwake ambapo hadi Kamati inatembelea jengo hilo, jumla

ya shilingi 11.4 Bilioni zilikuwa tayari zimeshalipwa. Majengo yatakuwa na baadhi vifaa

muhimu vikiwemo “transformer” tatu na “switch gear” yake, sehemu kubwa ya kuegesha

gari, vipoza hewa 202 na “lift” nne ambapo moja ni kwa matumizi ya ukumbi pekee.

Aidha, jengo litakuwa na vifaa vya uhakika vya kiusalama vinavyotumia teknolojia ya

kisasa ikijumuisha “CCTV Camera, fire horse” na “portable fire extinguisher, fire detector,

call point” vitakavyoshughulikia ajali za moto kabla moto haujawaka.

CHANGAMOTO

1. Upungufu wa baadhi ya vifaa vikiwemo ‘aluminium’ za Madirisha na Milango.

Hili limetokana na kuzorota kwa taratibu za utoaji wa vifaa hivyo bandarini

baada ya Watendaji wa TBS kuhitaji kufanya ukaguzi zaidi ili kujiridhisha

kutokana na kunatetesi kuwa mzigo ulioingizwa umezidi na hauendani na

maelezo yaliyoainishwa katika nyaraka husika.

2. Ucheleweshwaji wa vifaa vya ujenzi uliopelekea kubadilika badilika kwa muda wa

ujenzi.

3. Kutokuwepo kwa vifaa vya ukaguzi wa watu watakaoingia katika jengo hilo.

Vifaa hivi havijazingatiwa kuwemo katika mkataba.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Wizara ihakikishe inamsimamia ipasavyo Mkandarasi wa ujenzi huo ili afuatilie

kwa karibu upatikanaji wa vifaa vianavyohitajika kwa wakati.

2. Kamati inaitaka Wizara iwe makini katika kusimamia ujenzi huo na kuepuka

sababu za mara kwa mara zisizokuwa na mashiko zinazopelekea kuongezeka kwa

muda wa ujenzi.

3. Wizara ichukuwe hatua muafaka ya kuweka vifaa vya ukaguzi katika mlango

mkubwa wa kuingia katika jengo.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 6

4. Wizara ihakikishe inaingia mikataba na kampuni za usafishaji zenye uwezo wa

kusafisha pamoja na kuisimamia kwa ukaribu sana kampuni hiyo ili iweze

kutekeleza kazi zake ipasavyo.

2.4 UJENZI WA JENGO LA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR (PBZ) WETE

Jengo la Tawi la Benki ya Watu wa Zanzibar Wete hapo awali lilikuwa likitambuliwa

kama Hoteli ya Serikali lilianza rasmi kufanyiwa matengenezo makubwa tarehe 25

Oktoba, 2018 chini ya Mjenzi “Grasshopper Building Construction Ltd.” na Mshauri

Elekezi Benki ya Watu wa Zanzibar. Ujenzi huo utakaokuwa na ghorofa tatu,

unatarajiwa kukamilika tarehe 25 Februari, 2019 na kutumia jumla ya shilingi bilioni

1,210,917,239,000 (ikijumuisha kodi) kutoka katika Mfuko Mkuu wa Serikali. Hadi

Kamati inatembelea jengo hilo katika mwezi wa Januari 2019, jumla ya shilingi milioni

145,200,000 tayari zilikuwa zimelipwa na Serikali ambapo ujenzi ulifikia asilimia hamsini

ya utekelezaji.

Kamati inaipongeza Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kwa kutekeleza

kivitendo azma ya kuwapelekea karibu wananchi wake huduma za kibenki pamoja na

kutumia fedha nyingi kujenga na kuimarisha majengo mbali mbali ya kutolea huduma

hizo. Kufanya hivyo kutapelekea wafanyakazi na wateja wa benki hiyo wawe katika

mazingira mazuri (better conducive working environment). Jengo hilo litakuwa na

huduma zote zinazopatikana katika tawi lolote la Benki ya Watu wa Zanzibar zikiwemo

maeneo ya wapokeaji na watoaji fedha (tellers), chumba cha kuhifadhia fedha, mashine

mbili za kielektroniki (ATM), Ofisi za Bodi ya Mapato Zanzibar, vyumba vya kulala

wafanyakazi (floor ya juu), ukumbi mkubwa, vifaa vya usalama (CCTV Camera) na

sehemu za kuegesha gari. Licha ya mipango hiyo mizuri, bado jengo linakabiliwa na

changamoto zifuatazo:

CHANGAMOTO

1. Udogo wa eneo la kuegeshea gari kwa vile eneo liliopo linategemewa kuchukua

gari zisizozidi kumi na moja.

2. Kukosekana mazingira rafiki yatakayowawezesha ndugu zetu walemavu kufika

katika ghorofa ya pili na tatu za jengo hilo.

3. Kutozibwa vizuizi vya pembeni mwa ngazi kunakoweza kusababisha usumbufu

kwa watoto au kupenya na kuanguka.

4. Fedha alizolipwa Mjenzi ni kidogo sana ukilinganisha na kazi iliyofanyika, hili

linaweza kuisababishia Serikali kuongeza muda wa ujenzi kwa kushindwa

kutekeleza wajibu wao.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 7

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Wizara kupitia PBZ iwatafute wanaomiliki wa eneo lililowazi liliopo karibu na

jengo hilo ili waweze kulinunua na kulifanya kuwa ni eneo la maegesho ya gari.

2. Wizara ya Fedha na Mipango wafanye utaratibu wa kutengeneza miundombinu

itayowezesha watu wenye ulemavu kupata fursa ya kuingia na kufurahia huduma

zitakazotolewa na Benki hiyo.

3. Wizara ihakikishe Mjenzi anakamilishiwa malipo yake haraka iwezekanavyo.

4. Wizara ihakikishe inaziba vyuma vinavyosaidia mtu anapopanda au kushuka ngazi

ili watoto wasiweze kupenyeza miguu yao na kuwahatarishia maisha yao.

5. PBZ iwe makini kumsimamia mjenzi ili aezeke bati kwa umakini wa hali ya juu

kwa vile kuna nyumba nyingi zilizoezekwa kwa mabati kama hayo (Danida)

zinavuja.

2.5 BODI YA RUFAA ZA KODI ZANZIBAR

Bodi ya Rufaa za Kodi Zanzibar ni chombo cha Serikali kilichoundwa na Sheria Nam. 1 ya

mwaka 2006 ikiwa na lengo la kusikiliza kesi za madai ya walipaji kodi ambao

hawakuridhishwa na maamuzi yaliyofanywa na Taasisi za kodi (TRA na ZRB). Bodi hii

ina jumla ya wajumbe wanne ambao wanateuliwa na Waziri wa Fedha na Mipango

pamoja na Mrajis anaeteuliwa na Jaji Mkuu.

Chanzo kikuu cha malalamiko hayo ni Taasisi za kodi kutozingatia ipasavyo taratibu za

ulipaji kodi kwa mujibu wa Sheria au pande mbili kushindwa kukubaliana na makadirio

ya kodi (Tax assessment) yaliyofanywa na Taasisi ya Kodi. Bodi hio ina hadhi ya

Mahakama ya Mkoa (Quasi judicial) ambapo Mrajis wake ni Hakimu wa Mahakama ya

Mkoa.

Kiutendaji, Bodi imeanza rasmi kutekeleza majukumu yake mwaka 2013 (2010 - 2012

hapakuwa na shauri lililowasilishwa mbele ya Bodi). Hadi Kamati ilipoitembelea Bodi

hiyo ilikuwa na jumla ya mashauri 10 ambapo mashauri 6 yaliwasilishwa na ‘Zanzibar

Telecom Limited’ (Zantel) dhidi ya TRA. Bodi tayari imeshatoa uamuzi wa shauri moja

linalowahusu Zan Tours Limited dhidi ya ZRB kwa kukubaliana kuliondoa shauri hilo

katika Bodi.

Kamati imeshangazwa na hali iliyopo kwamba Bodi hiyo bado haijitegemei moja kwa

moja badala yake inapata bajeti yake kupitia Wizara ya Fedha na Mipango, suala hili

linazorotesha utendaji wa Bodi hiyo kwa vile hushindwa kutoa maamuzi yanayofaa kwa

wakati kwani baadhi ya muda hulazimika kutembelea maeneo ambayo wao wanaona

yatawasaidia katika kuharakisha kutoa maamuzi lakini wanashindwa kutokana na

upungufu wa fedha.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 8

CHANGAMOTO

1. Kutojitegemea kikamilifu kwa Bodi ya Rufaa za Kodi ni changamoto sugu

inayokwamisha utendaji wa Bodi hiyo kwani inategemea kupata fedha za

uendeshaji kutoka Wizara ya Fedha na Mipango.

2. Ukosefu wa Afisi ya uhakika ya kuendeshea shughuli zao.

3. Kushindwa kukaa pamoja kwa Mlalamikaji na Mlalamikiwa kupitia vielelezo vya

makadirio ya kodi katika kipindi ambacho Mlalamikaji anapinga makadirio hayo

katika Taasisi husika. Kinachofanyika Taasisi (hususan ZRB) huwa wanachukua

vielelezo Ofisini kwa hatua ya maamuzi bila ya kumshirikisha Mlalamikaji.

4. Kutokuwepo kwa Maofisa husika wakati kesi inapoletwa mbele ya Bodi

isipokuwa huwa wanakuwepo wanasheria tu. Hili hutokezea katika kesi

zinazoihusu ZRB.

5. Bodi kutokuwa na uwezo wa kufuatilia katika maeneo husika ili kujiridhisha kati

ya maelezo yanayotolewa na vielelezo husika. Mfano kwenda Ofisi za Uhamiaji

Uwanja wa ndege au katika Ofisi za Watembeza Watalii kuhakiki wageni

waliopita kuelekea Hoteli inayolalamikiwa ili kupata picha kwa kiasi gani Hoteli

hiyo imeingiza kipato na kushindwa kulipa makadirio yaliyopangwa.

6. Mianya iliopo kwenye sekta za ukusanyaji wa kodi hupelekea mrundikano wa kesi

kwenye Bodi hiyo.

7. Kuwepo kwa kesi nyingi zisizokua na msingi ambazo hutokana na

wafanyabiashara wasio waaminifu kukwepa kodi na wanapobainika hukwazana

na taasisi za kodi na hatimaye kufungua kesi ya rufaa za kodi.

8. Baadhi ya wakusanya kodi hukosa uadilifu kwenye kazi zao jambo ambalo

linaikosesha mapato nchi yetu.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Wizara ichukue hatua zifaazo kuhakikisha Bodi hiyo inakuwa ni chombo

kinachojitegemea kikamilifu ikiwemo kupatiwa Ofisi na kutengewa fedha za

kutosha kama zilivyo Bodi nyengine.

2. Taasisi za Kodi zikae pamoja na Walalamikaji wao wanaoweka pingamizi ya

makadirio ya Kodi waliyopatiwa ili kutatua tofauti iliyopo baina yao na

kupunguza idadi ya kesi zitakazopelekwa katika Bodi.

3. Wizara iitake ZRB ipeleke Maofisa wanaohusika na lalamiko na sio kuwaachia

wanasheria pekee wakati lalamiko linapofikishwa katika Bodi ili iwe rahisi kufikia

maamuzi.

4. Wizara ihakikishe kwamba inaiwezesha ipasavyo Bodi ili iweze kuyatembelea

maeneo ambayo yatawasaidia katika kuharakisha kutoa maamuzi.

5. Taasisi za kukusanya Kodi zihakikishe zinafuata utaratibu kikamilifu ili kupunguza

pingamizi na malalamiko ya Kodi yanayowasilishwa katika Bodi.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 9

6. Watendaji wa taasisi za ukusanyaji wa kodi wawe waadilifu na wasikubali

kurubuniwa na wajanja wachache wenye nia ya kukwepa kodi.

7. Kamati inaitaka ZRB kuimarisha mfumo wake wa makadirio ya walipa kodi

(assessment) ili kupunguza wimbi la malalamiko na kesi za rufaa za kodi

zinazowakabili.

2.6 BODI YA RUFAANI ZA KODI YA TANZANIA BARA

Kamati ilifanya ziara ya kubadilishana uzoefu katika Bodi ya Rufaani za Kodi pamoja na

Baraza la kodi Tanzania Bara mara baada ya kupata maelezo kutoka Bodi ya Rufaa za

Kodi Zanzibar. Vyombo hivyo vimeundwa kwa ajili ya kuweka usawa kati ya

wafanyabiashara na Taasisi za kodi nchini. Miongoni mwa kazi zinazofanywa na

vyombo hivyo ni kusikiliza na kutoa hukumu ya rufaa za kodi ambapo upande

usioridhika na uamuzi uliotolewa na Bodi utakata rufaa kwenye Baraza la kodi. Upande

usioridhika na maamuzi yaliyotolewa na Baraza utakata rufaa Mahakama ya Rufaa ya

Tanzania kwani hukumu inayotolewa na Baraza hilo ni sawa na hukumu ya Mahakama

Kuu. Aidha, vyombo hivyo hutoa ushauri kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania pamoja na

uelewa kwa wananchi kuhusu masuala ya kodi.

Bodi ina wajumbe kumi na mbili ambao wanaongozwa na Mwenyekiti akisaidiana na

Makamo Wenyeviti watatu ambapo mmoja kati ya hao lazima atoke Zanzibar.

Lakushangaza, muda mrefu umepita Bodi haijawahi kupata Makamo Mwenyekiti kutoka

Zanzibar kwa vile chombo kinachosikiliza na kutoa maamuzi ya kesi zinazotoka taasisi za

kodi (Bodi ya Mapato Zanzibar na Mamlaka ya Mapato Tanzania) kipo Zanzibar. Kwa

upande wa Baraza, linatakiwa kuwa na wajumbe wasiopungua kumi na mbili.

Mwenyekiti wake ni lazima awe na sifa za kuwa Jaji pamoja na Makamo Wenyeviti

watatu ambao watateuliwa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania mmoja wapo

akitokea upande wa Zanzibar ambaye atateuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania akishirikiana na Rais wa Zanzibar.

Vyombo hivyo vinaongozwa na sheria inayoitwa: Tax Revenue Appeal Act, Cap 408.

Mwaka 2015, Baraza la Kodi lina Mwenyekiti lakini nafasi za Makamo Wenyeviti bado

hazijajazwa. Kimsingi, hali hiyo inatokana na mgongano wa kisheria kati ya sheria ya

Tanzania Bara na ile ya Zanzibar Namba Nam. 1 ya mwaka 2006. Aidha, kuna baadhi ya

kesi walizowahi kuzitolea uamuzi ikiwemo kesi ya Zantel ikaelezwa kwamba Bodi haina

uwezo wa kutoa maamuzi. Mbali na hayo, kuna utofauti wa uwezo wa mamlaka

kuamua kesi kwa vile Baraza (Tribunal) inahadhi ya kuwa sawa na Mahakama kuu ya

Zanzibar.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 10

CHANGAMOTO

1. Kuna mgongano wa kisheria unasababisha Bodi kushindwa kufikia malengo yake.

2. Bado Makamo Mwenyekiti kutoka Zanzibar hajateuliwa kushiriki katika shughuli

za Baraza.

3. Inaonekana hakuna mashirikiano ya dhati kati ya vyombo hivyo viliopo Tanzania

Bara na Zanzibar.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kuna haja Bodi zote mbili za rufaa ya kodi kukaa pamoja kujadili utofauti uliopo

hususan wa kisheria na kiutendaji.

2. Kamati inashauri kuanzishwa mashirikiano ya kiutendaji baina ya bodi hizo kwa

lengo la kuiletea tija nchi zetu.

2.7 PROGRAMU KUU YA USIMAMIZI NA UWEKEZAJI WA MALI ZA UMMA

Programu hiyo imekusudia kusimamia mitaji ya umma ili kuhakikisha inakwenda

sambamba na mabadiliko ya kiuchumi pamoja na kuwepo kwa uwazi na usawa wa

tathmini ya bidhaa zinazonunuliwa katika taratibu za manunuzi. Utekelezaji wa

Programu hiyo unafanywa na Mamlaka ya kukuza uwekazaji Zanzibar, Idara ya Mitaji ya

Umma, Mamlaka ya Manunuzi na Uondoshaji wa Mali za Umma na Idara ya Uhakiki

Mali. Miongoni mwa mambo ambayo yamefuatiliwa na Kamati ni:

2.8 MAMLAKA YA KUKUZA UWEKEZAJI ZANZIBAR (ZIPA)

Katika miaka ya 1980, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilifanya maamuzi ya kubadilisha

mfumo wa uchumi kwa kuzishirikisha kikamilifu Sekta binafsi katika kuuendeleza uchumi

wa nchi (engine of growth). Katika kulisimamia hilo, Serikali iliunda vyombo tofauti

ikiwemo Kituo cha Uwekezaji Zanzibar (ZIC), Mamlaka ya Maeneo huru, Bandari huru,

Mamlaka ya Uwekezaji Vitega Uchumi na hatimae hivi karibuni kumeundwa Mamlaka

ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA). Hii ni Mamlaka inayojitegemea iliyopo chini ya

usimamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango.

Hiki ndicho chombo kikuu Zanzibar chenye uwezo wa kutoa ruhusa na ithibati ya

uwekezaji kwa Mtanzania au Mgeni kuwekeza katika maeneo ya Zanzibar. Serikali ya

Mapinduzi ya Zanzibar kwa makusudi iliamua kuunda chombo hiki kwa kutambua

umuhimu wa sekta binafsi kutoka ndani na nje ya nchi kujitokeza kuwekeza na kuchangia

katika maendeleo ya kiuchumi ya nchi yetu hususan katika masuala ya hoteli, ujenzi wa

maeneo ya kufurahishia watoto na ujenzi wa nyumba za kisasa za makaazi. Kwasasa,

ZIPA imefanikiwa kuunda Kituo cha Uwekezaji (one stop centre) ndani ya Ofisi yake

iliyopo Maruhubi ambapo Maofisa wengi wa taasisi za Serikali wanafanya kazi zao katika

Ofisi hiyo ili kuwarahisishia wawekezaji kuanza Miradi waliyoikusudia kuitekeleza ndani

ya siku tatu iwapo amekamilisha taratibu zote zinazohitajika. Ni ukweli usiofichika kuwa

kukamilika kwa kituo cha huduma kwa wawekezaji kutasaidia sana kuondoa urasimu

ambao wawekezaji walikuwa wanakumbana nao.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 11

Kamati ya Fedha, Bisahara na Kilimo kwa pamoja imesikitishwa sana na hali ya

uwekezaji katika Kisiwa cha Pemba ambayo haitowi hata matumaini kwa wawekezaji

kuvutika na kuamua kuweka mitaji yao kwa lengo la kutoa huduma lakini pia kupata

faida ya kile walichowekeza. Hili limegunduliwa na Kamati baada ya kuarifiwa kwamba

baadhi ya wawekezaji wanaondoka nchini hususan wakati wa kiangazi kutokana na

ukosefu wa maji Mahotelini.

Sambamba na hayo, maeneo huru ya Micheweni ambayo yametengwa maalum kwa

uwekezaji Pemba yana mipango mingi iliyomo vitabuni lakini hakuna mwendelezo

(improvement) wowote uliofanywa katika maeneo hayo kutokana na ukosefu wa

miundombinu ya barabara, maji safi na salama, umeme na bandari itakayowawezesha

wawekezali kuingiza malighafi kwa urahisi nchini.

Afisi Kuu ya ZIPA Pemba imekagua miradi 13 ya hoteli ambapo miradi sita inaendelea

kutoa huduma (imekamilika), miradi sita iko kwenye hatua ya ujenzi na mradi mmoja

mpya umefanyiwa ukaguzi wa awali. Kwa upande wa uendelezaji wa maeneo huru ya

Micheweni, Mamlaka imelipima eneo lenye urefu wa 3.7 km ambalo linatarajiwa

kujengwa barabara kwa kiwango cha fusi na inajiandaa na zoezi la ulipaji wa fidia kwa

wananchi watakaoathirika na ujenzi wa barabara hiyo.

CHANGAMOTO

1. Mapato yanayokusanywa yameonekana kuwa ni kidogo sana ukilinganisha na

idadi ya miradi ya uwekezaji iliyopo.

2. Kutoshirikishwa ipasavyo kwa ZIPA wakati wa uanzishwaji wa baadhi ya miradi

ya uwekezaji, jambo ambalo huiweka ZIPA kwenye wakati mgumu pale

wanapohusishwa kwenye utatuzi wa migogoro ya miradi hiyo.

3. Kukosekana kwa Miradi ya Uwekezaji katika Viwanda vya kusarifu, kusindika

mazao ya kilimo yakiwemo mwani, Machungwa, embe na tungule ambayo ndio

yanayoendana na mazingira tuliyonayo Zanzibar.

4. Wizara ya Ardhi haijayatambua maeneo ya Wawekezaji na kuikabidhi ZIPA kama

walivyoelekezwa na Serikali na kudai kwamba wanasubiri ‘Master plan’ ya

maeneo yote ya nchi nzima ikamilike wakati maeneo ya uwekezaji yanajulikana.

5. Kukataliwa kupatiwa eneo na Idara ya Misitu kwa ajili ya Muwekezaji kujenga

Hoteli (Vault) huko katika Msitu wa Kiuyu Mbuyuni, Pemba.

6. Baadhi ya wenyeji wasiopenda maendeleo ya nchi yetu hufanya udangavyifu wa

kuomba eneo la kuwekeza kutoka ZIPA na kulipa gharama ndogo anazotakiwa

Mzawa lakini baadae huwauzia Wageni.

7. Baadhi ya watendaji katika Taasisi za Serikali wanakuwa wazito kutekeleza wajibu

wao kwenye masuala ya uwekezaji nchini na kupelekea kuchelewa au

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 12

kutotekelezwa kabisa kwa baadhi ya miradi au mwekezaji kuamua kuondoka

nchini na kuwekeza kwengine.

8. Kutopewa na Serikali asilimia 100 ya ruzuku ya mishahara na matumizi mengine

kwa ZIPA ambapo kwa sasa wanapatiwa asilimia 80.

9. Kutokuwepo kwa kiwanja cha Ofisi ya Baraza la Wawakilishi, ZIPA inasema hilo

sio eneo la uwekezaji isipokuwa ni eneo la wananchi wa Fumba kama ilivyokuwa

kabla ya “Master Plan” ya mwanzo. Kwa hivyo, jukumu la kutoa maeneo kama

hayo lipo Wizara ya Ardhi, ingawa “Master Plan” yote ya Fumba wahusika wakuu

ni ZIPA.

10. Maslahi duni kwa watendaji wa ZIPA ambao wanafanya kazi na wawekezaji

ambao ni watu wenye fedha za kutosha.

11. Mshahara mdogo anaolipwa Mkurugenzi Mtendaji wa ZIPA kwani analipwa

mshahara uliosawa na Mkurugenzi wa kawaida tofauti na wadhifa na cheo chake.

12. Kukwama kwa Miradi ya Uvuvi kunakosababishwa na Idara ya Uvuvi yenyewe

kukosa kutoa mashirikiano kwa ZIPA.

13. Ucheleweshwaji wa vibali vya ukodishwaji ardhi (Land Lease) kwa wawekezaji

wenye nia ya kuwekeza nchini unapelekea baadhi yao kuvunjika moyo na kukosa

hamu ya kuendeleza miradi yao.

14. Upungufu wa watendaji wa Mamlaka kwa upande wa Pemba. Mamlaka ina jumla

ya watendaji 8 ambapo kati yao wawili wako masomoni na watatu ni walinzi

katika Afisi na maeneo huru ya Micheweni.

15. Uhaba wa fedha za kuitangaza ipasavyo Zanzibar kuwa ni eneo zuri la kuwekeza.

16. Ukosefu wa Afisi kuu ya kudumu kwa upande wa Pemba ambapo watendaji

hufanya shughuli zao kwenye mazingira yasiyoridhisha.

17. Ukosefu wa elimu juu ya faida za uwekezaji kwa vijana waliopo Pemba hususan

maeneo ya vijijini unawafanya vijana hao kuchukia uwekezaji nchini na hivyo

kushindwa kutumia fursa za ajira zinazotokana na uwekezaji katika maeneo yao.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kamati inaishauri ZIPA kuchukua juhudi za makusudi kuhakikisha mapato

wanayokusanya yanaongezeka.

2. Wizara ya Fedha na Mipango ishirikiane na Wizara husika kuhakikisha kwamba

kabla Mradi haujaanza kutekelezwa ni lazima upitie ZIPA kama inavyoelekezwa

na sheria ya Uwekezaji nchini.

3. ZIPA iongeze juhudi katika kuhamasisha wawekezaji wa viwanda vya kusindika

matunda.

4. Wizara ya Fedha na Mipango ikae na Wizara inayoshughulikia Ardhi kumaliza

changamoto ya kutotambuliwa kwa maeneo ya uwekezaji nchini.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 13

5. Kamati inaitaka Wizara kukaa na Wizara inayoshughulikia Kilimo ili kutatua

changamoto ya kutokubaliwa kwa Mwekezaji wa Mradi wa kujenga Hoteli

(Vault) kwa kuzingatia kwamba Mradi huo usiharibu maliasili na mazingira ya

msitu ulipo.

6. Kamati inaitaka Wizara kukaa na Wizara ya Utumishi wa Umma kushughulikia

suala la “Scheme of Service” ya ZIPA ambayo wameiandaa kwa muda mrefu bila

ya kushughulikiwa.

7. ZIPA ifanye ufuatiliaji na tathmini ya Miradi iliyoruhusiwa ili kuchunguza kama

hakuna udanganyifu uliofanyika na kupatiwa kibali cha uwekezaji mwenyeji kwa

bei ya chini na baadae kumuuzia Mgeni.

8. Kamati inaitaka Wizara kuwachukulia hatua zinazostahiki wale wote

watakaogundulika kufanya udanganyifu na kuwauzia maeneo wawekezaji wageni

kinyume na taratibu.

9. Wizara ya Fedha na Mipango ikae na Wizara inayoshughulikia Ardhi ili

kuhakikisha Mpango wa Matumizi ya Ardhi katika eneo la Makaazi ya watu

Fumba unakwamuka ili kuweka mazingira mazuri kwenye upande wa uwekezaji.

10. Wizara iwapatiye ZIPA asilimia 100 ya ruzuku ya mishahara na matumizi mengine

badala ya asilimia 80 inayotolewa hivi sasa ili waweze kuijipanga na kutekeleza

majukumu yao ipasavyo.

11. Kamati inashauri Wizara ya Fedha na Mipango ihakikishe inakutana na Wizara

inayoshughulikia Utumishi wa Umma kuyapitia upya maslahi ya Mkurugenzi

Mtendaji wa ZIPA ili aweze kuwa tofauti na mshahara wa Wakurugenzi wengine.

12. Wizara ya Fedha na Mipango ihakikishe inakutana na Wizara inayoshughulikia

Kilimo kutatua changamoto ya kukwama kwa Miradi ya Uvuvi.

13. Wizara ihakikishe inaanzisha kituo cha huduma kwa wawekezaji “One Stop

Center” kwa upande wa Pemba ili iwaondolee usumbufu wawekezaji wanaohitaji

kuwekeza kisiwani humo.

14. Kamati inapendekeza kuongezwa watendaji wa ZIPA kisiwani Pemba ili waweze

kukidhi mahitaji ya utendaji wenye ufanisi mkubwa.

15. Kamati inashauri Serikali kuitengea ZIPA fungu maalum kwa ajili ya kuitangaza

Zanzibar ndani na nje ya nchi.

16. Kamati inaitaka Wizara ya Fedha na Mipango ikutane na Wizara inayoshughulikia

Ardhi kushauriana na hatimae kuipatia Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar

Mpango Mkuu “Master Plan” ya Uwekezaji kwa ajili ya kuifanyia kazi.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 14

2.9 MRADI WA “MPAPINDI HOLIDAY AND DIVING COMPANY LIMITED”

Mradi huu uliopo kwenye kijiji cha Makangale, Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa

Kaskazini Pemba, ulithibitishwa na Mamlaka ya Ukuzaji Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA),

ulisajiliwa na kupewa hati ya ukodishwaji wa Ardhi (land lease) mwaka 2004 ukiwa chini

ya umiliki wa raia wawili wa kigeni wa Afrika Kusini Bwana Marek Kloryga na Mkewe

wenye hisa sawa za umiliki.

Mwekezaji alipewa cheti cha ruhusa ya ujenzi wa vibanda vya kulaza wageni mwaka

2005 na shughuli za ujenzi wa mradi huo zilianza rasmi katika mwezi wa Septemba,

2006. Mwaka 2007, shughuli za ujenzi wa mradi huo zilisita kutokana na kuishiwa mtaji

na kuamua kuingia ubia na Bwana Ray Champion. Haikuchukua muda, wabia hao

walipelekana Mahakamani kutokana na mbia mmoja (Ray Champion) kulitangaza eneo

hilo kuwa lake na anataka kulikabidhisha kwa mtu mwengine.

Mwekezaji aliomba kubadilishiwa hati ya ukodishwaji ardhi kutoka jina la “Mpapindi

Holiday and Diving Company Ltd.” na kuwa “Pemba Sports Fishing Club” ili aepukane

na changamoto zilizomkabili hapo awali na kuingia kwenye kesi iliyodumu kwa zaidi ya

miaka saba.

Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo imesikitishwa na taarifa ya upotevu wa ramani ya

eneo la mradi huo jambo ambalo limeitia aibu kubwa kwa nchi yetu. Kitendo hicho

kimewaweka njia panda wawekezaji hao kwa kushindwa kuingia kwenye mkataba wa

matumizi ya ardhi kwa muda wa miaka 30 na kupelekea kuikosesha nchi yetu fedha za

kigeni.

CHANGAMOTO

1. Mradi kukabiliwa na kesi Mahakamani katika kipindi cha awali cha uanzishwaji

wake jambo lililositisha uendelezaji wa mradi huo na kuchukua muda mrefu hadi

kumalizika kwa kesi hiyo mwaka 2016.

2. Uchelewaji wa upatikanaji wa hati ya ubadilishaji wa jina la mradi ambayo

Mwekezaji ameiomba kwa Bodi ya Uhaulishaji Ardhi Zanzibar kwa muda wa

mwaka mzima ni suala jengine linalokwamisha mradi huu.

3. Kuwepo kwa migogoro ya mara kwa mara ya kujitokeza watu wanaodai umiliki

wa sehemu ya eneo hilo.

4. Ukatwaji wa miti hususan muda wa usiku hupelekea kuathiri msitu wa maumbile

uliopo katika eneo hilo.

5. Sura ya udanganyifu na ubabaishaji wa mwekezaji.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 15

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kamati inaitaka Wizara ya Fedha na Mipango kufanya kikao cha dharura baina

yake na Wizara inayohusika na Ardhi na Taasisi zote zinazohusika ili kutatua

changamoto zilizopo.

2. Serikali ifuate ipasavyo vigezo ilivyojiwekea kisheria kwa ajili ya uwekezaji

unaofaa nchini.

3. Kamati inaitaka Mamlaka inayohusika kutayarisha ramani nyengine ya eneo hilo

haraka iwezekanavyo ili hatua za mradi huo ziendelee na wananchi wapate

manufaa yaliyokusudiwa.

4. ZIPA iwe makini inaposhughulikia maombi ya uwekezaji na kujiridhisha na

mwekezaji husika kabla ya kuuthibitisha mradi huo.

2.10 UTEKELEZAJI KWA TAASISI ZINAZOJITEGEMEA

2.10.1 BODI YA MAPATO ZANZIBAR (ZRB)

Bodi ya Mapato Zanzibar ilianzishwa mwaka 1996 na kuanza kazi rasmi mwaka 1998.

Hiki ndio chombo kikuu Zanzibar na ni roho ya Serikali katika ukusanyaji mapato kupitia

ongezeko la thamani yaani ‘VAT’, kodi ya zuio la biashara (excise duty), kodi ya Hoteli

na kodi nyengine za ndani. Kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2018/2019,

taasisi hiyo ilipangiwa kukusanya jumla ya shilingi 103.26 bilioni ambapo hadi kufikia

Disemba 2019, jumla ya shilingi 90.80 bilioni zilikusanywa sawa na asilimia 88 ya

makadirio. Kwasasa Bodi hiyo ina mpango wa kuanzisha mfumo wa ulipaji kodi kwa

kutumia mashine za ‘EFD’ pamoja na kwenda kwenye mfumo wa ‘E-Service’ ambayo

itampa fursa mlipa kodi kulipia kodi yake na kupata huduma papo hapo.

CHANGAMOTO

1. Makusanyo yanayotokana na TRA (excise duty) huwa yanachelewa kuingizwa

katika hesabu ya ZRB.

2. Bado kuna wafanyabiashara ambao hawatowi risiti wakati wa mauziano

yanapofanyika.

3. Kutotumika kwa mashine za EFD kunasababisha mapato mengi kupotea.

4. Kukosekana utaratibu wa kuwapatia wananchi wanye mahitaji ya leseni mbili au

tatu kwa wamiliki wa magari mengi.

5. Ushuru mdogo kwa gari nyingi mbovu ambazo zinaingia Zanzibar hasa za abiria,

taxi na daladala.

6. Bado kuna myanya mingi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

7. Kutokuwepo kwa wataalamu wa kutosha wa ukusanyaji mapato katika ngazi ya

Serikali za Mitaa hususan ukizingatia mfumo wa ugatuzi.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 16

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. ZRB ichukue juhudi za makusudi kuhakikisha mapato yanatoyotoka na makusanyo

kutoka TRA yanaingia nchini na kuchangia kwenye mfuko mkuu wa Serikali.

2. Serikali iharakishe uwekaji wa mfumo mpya wa utoaji risiti kwa njia za

kielektroniki.

3. ZRB ianzishe utaratibu wa mtu mmoja kuwa na leseni mbili au zaidi. Kufanya

hivyo kutawaepusha wananchi wenye magari zaidi ya moja na kupata usumbufu

wa askari barabarani.

4. ZRB ihakikishe inaongeza Ushuru kwa gari mbovu zinazoingizwa Zanzibar, ili nchi

yetu isiwe jaa la bidhaa mbaovu zikiwemo za magari.

5. Wizara ya Fedha na Mipango ihakikishe inawapatia mafunzo ya kutosha

watendaji wa Serikali za Mitaa juu ya ukusanyaji wa mapato.

6. Wizara ihakikishe inanzisha mfumo wa ulipaji kodi kwa njia ya Mtandao (E-

services).

7. Kamati inasisitiza ZRB kuwapatia mafunzo watendaji wa Bodi ya Mapato

Zanzibar (ZRB) ambao wanahusika moja kwa moja na matumizi ya mashine za

EFD kabla ya kuwasili mashine hizo nchini ili kurahisisha matumizi yake.

8. Wizara kupitia ZRB iandae programu za mafunzo kwa watumiaji wa mashine hizo

(wafanyabiashara) ili kuhakikisha mashine zinatumika ipasavyo na kuongeza pato

la Taifa kama inavyotegemewa.

2.10.2 MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA)

Mamlaka ya Mapato Tanzania ilianzishwa mwaka 1995 lakini ilianza kazi rasmi mwaka

1996. Mamlaka hiyo inaongozwa na Bodi ya Wakurugenzi ikiwa na majukumu ya msingi

ya kukusanya kodi pamoja na kuishauri Serikali kuhusu masuala ya kodi. Katika

ukusanyaji wa kodi, awali walikuwa wakitumia mfumo wa utoaji mizigo Bandarini wa

‘Ascudo Plus Plus’ lakini mfumo huo ulikuwa na changamoto nyingi kwa vile uliundwa

mahsusi kutumika kwa nchi zisizokuwa na Bahari au Bandari (land locked countries).

Kwa vile Tanzania inazo Bandari kadhaa ambazo zinatumika kupokea mizigo kutoka

sehemu tofauti, mfumo wa Ascudo haukuweza kutoa huduma ipasavyo kwani

iliwalazimu Maofisa wa teknolojia ya habari kufuatilia wao wenyewe mizigo iliyoingia

na kwa vile mizigo huwa mingi husababisha foleni, muda mwingi kupotea na kulikuwa

na mdororo wa utoaji mizigo.

Ili kuondosha changamoto hizo, Mamlaka iliamua kutumia mfumo unaoitwa ‘Tanzania

Customs Intergrated System (Tancis)’ ambao umetengenezwa na Wakorea wakishirikiana

na wataalamu wazalendo katika mifumo yake mingi ya utoaji mizigo Bandarini na katika

baadhi ya maeneo waliedelea kutumia ‘Ascudo Plus Plus’. Aidha, kuna mifumo mingine

imeunganishwa na mfumo wa Tancis ikiwemo mfumo wa usalama ambao unasaidia

mifumo mingine kufanya kazi. Kuwepo kwa mfumo huo, unazisaidia hata mifumo

mingine ya Serikali kupata taarifa kamili za kodi wanapoingia katika mfumo wa Tancis.

Faida kubwa za mfumo huo ni: unaongeza mapato, kupunguza muda na gharam za

usafirishaji biashara; inaongeza uwazi; utaratibu wa malipo ya ukaguzi unakuwa rahisi,

unapunguza wafanyakazi wasiokuwa na ulazimu mkubwa mfano unatoa ripoti

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 17

wenyewe, hivyo hakuna haja ya kuwepo muandikaji ripoti; kawaida mfumo wa Ascudo

hauruhusu kufanya mabadiliko mpaka uombe ridhaa kutoka Ulaya kwa aliyeutengeneza

wakati Tancis baada ya kufanyiwa marekebisho, mfumo hivi sasa unaruhusu marekebisho

kufanywa na Maofisa wa TRA wenyewe.

Tarehe 11 Januaari, 2019 mfumo wa Tancis umeanzishwa rasmi na kutumika Zanzibar.

Mfumo huo umeonesha mafanikio makubwa ikiwemo urahisi na ufanisi katika utekelezaji

wake. Matumizi ya mfumo huo, unawafanya Maofisa wa TRA kuweza kujua ufanisi wa

kazi wa Bandari zote ziliopo Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wake wakiwa wapo

Ofisini.

CHANGAMOTO

1. Upungufu wa Wafanyakazi katika Ofisi za TRA hususan wataalamu wa ‘ICT’

wanaotumika kuendesha mfumo wa Tancis.

2. Kukosekana eneo la kutosha la kukagulia na kuhifadhia mizigo inayoteremshwa

kutoka katika meli kupitia kwenye makontena.

3. Kuwepo kwa eneo dogo wanalotumia Maofisa wa TRA Bandarini Zanzibar

kufanyia kazi zao ambalo baadhi ya wakati huwafanya wafanyabiashara

kukusanyika wakisubiri huduma.

4. Matumizi mabaya ya misamaha ya kodi kwa baadhi ya taasisi za dini ambao

huitumia fursa hiyo kwa maslahi binafsi.

5. Kuwepo kwa ujanja wa baadhi ya wafanyabiashara kupunguza makadirio ya

gharama za mizigo kwa nia ya kukwepa kulipa kodi stahiki.

6. Kuwepo kwa wadaiwa sugu wa kodi.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Ni busara Wizara ya Fedha na Mipango ikashauriana na Mamlaka ya Mapato

Tanzania kuajiri wafanyakazi wapya ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa kodi

Bandarini.

2. Wizara ya Fedha na Mipango ikutane na Shirika la Bandari Zanzibar kuzungumzia

suala la uwezekano wa kutumia Taasisi za Serikali au binafsi kuandaa eneo nje ya

Bandari hiyo kwa lengo la kuweka makontena.

3. TRA inalazimika kufuatilia kwa umakini mkubwa misamaha yote ya kodi

inayotolewa ili kujiridhisha inatumika kama masharti yake yanavyoelekeza.

4. TRA iendelee kutafuta njia mbadala za kuwashughulikia wanaokwepa kulipa

ushuru pamoja na wadaiwa sugu.

2.10.3 BENKI YA WATU WA ZANZIBAR (PBZ) - MTAA WA LUMUMBA, DSM

Tawi la PBZ Lumumba ni moja katika ya matawi matatu yaliopo Jijini Dar es Salaam.

Matawi mengine yapo TAZARA na Kariakoo. Matawi yote hayo yana jumla ya

wafanyakazi 51 wa kudumu lakini pia wanao wafanyakazi wa Mkataba. Matawi hayo

yanafanya kazi katika majengo ya kukodi ambapo zaidi ya shillingi milioni 900 hutumika

kwa mwaka kwa ajili ya kulipia gharama za kodi ya majengo hayo. Mpango uliopo ni

kufungua tawi jengine katika mji wa Dodoma ifikapo Juni, 2019.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 18

Kamati inaipongeza Benki ya Watu wa Zanzibar kwa juhudi wanazozichukua katika

utekelezaji wa majukumu yao hususan kwa kufanikiwa kuweka mfumo mpya na

wakisasa unaoweza kwenda sambamba na ushindani wa soko la ndani na nje ya

Zanzibar. Kuwepo kwa mfumo huo, kutaiwezesha PBZ kumudu kutoa huduma za “Visa”

na “Master card” kwa wateja wake, kuruhusu matumizi ya kibenki mtandaooni

“Internet Banking System” na kuongeza wigo wa kuwa na wateja wengi na mawakala

wa benki. licha ya mafanikio hayo, Kamati bado haijaridhishwa na ufanisi wa huduma

zinazopatikana kupitia “ATM mechine” kwani wateja wanaendelea kulalamika kwa

kukosekana fedha katika mashine hizo, kuwepo kwa fedha ndogo ndogo tupu na

huharibika mara kwa mara.

CHANGAMOTO

1. Matawi ya PBZ Dar es salaam ni machache sana.

2. Bado PBZ haijafanikiwa kuwavutia wafanyakazi wengine kufungua ‘account’

katika benki hiyo hususan katika kambi za jeshi.

3. PBZ haijafungua Matawi mengine katika maeneo ya Arusha na Mwanza.

4. PBZ bado haijajitangaza ipasavyo ndani na nje ya nchi.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. PBZ ichukue juhudi za makusudi kufungua matawi mengine Dar - es Salaam.

2. PBZ ihakikishe inaweka vivutio vya kutosha ili wafanyakazi wa Wizara tofauti za

Muungano ziweze kufungua ‘account’ katika benki hiyo.

3. PBZ ifungue Matawi mengine katika maeneo ya Arusha na Mwanza.

4. Ili kuimarisha utendaji na kuongeza wateja zaidi, PBZ ijitangaze ndani na nje ya hi.

2.10.4 MFUKO WA HIFADHI YA JAMII (ZSSF)

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) ni Taasisi ya SMZ iliyoundwa kwa sheria Nam. 2 ya

mwaka 1998 kwa lengo kuu la kuwahifadhi wanachama waliostaafu kwa mujibu wa

sheria na wanapopatwa na majanga ambayo husitisha au kupunguza kipato chao

kutokana na sababu mbali mbali kama vile , ulemavu, maradhi au kifo. Mfuko pia

huongeza wigo kwa kukusanya michango mbali mbali kutoka kwa wanachama wake

(Taasisi za Serikali na Binafsi) ili michango hiyo iweze kuwasaidia wanachama hao baada

ya kumaliza utumishi wao. Katika kuhakikisha Mfuko huo unakuwa endelevu, ZSSF

hutumia michango hiyo kuiwekeza kwenye miradi tofauti ili iweze kuzalisha faida.

ZSSF ina miradi mbalimbali ambayo imewekeza kwa ajili ya uendelezaji wa mfuko.

Miongoni mwa Miradi hiyo ni ujenzi wa nyumba za kisasa za Makaazi ziliopo Mbweni

wenye ukubwa wa eneo la mita za Mraba 55,000 kwa ajili ya wananchi wa kipato cha

kati. Mradi huo umeanza mwaka 2015 na kutarajiwa kumaliza mwaka 2018 ambao

unasimamiwa na Kampuni ya Habconsult Ltd. ya Dar es Salaam na mjenzi wake ni

Kampuni ya Dezo Civil Contractor ya Dar es Salaam. Mradi huo umepanga kujenga

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 19

jumla ya majengo 18 yenye ghorofa saba kila moja ambazo zinatarajiwa kuwa na

vyumba 253 kwa nyumba za kati ya vyumba viwili, vitatu na vinne kwa gharama ya

shilingi 43.7 bilioni. Nyumba hizo ni za biashara ambazo zitanunuliwa kwa fedha taslim

au malipo ya kodi kwa nia ya kumiliki au kupitia mkopo wa Benki. Ujenzi wa majengo

matano ya awamu ya kwanza unakamilishwa ikiwa ni pamoja na kukabidhiwa wateja

nyumba zao.

Hadi Kamati ilipotembelea mfuko huo mwezi wa Agosti 2018, jumla ya Tsh. 16.41 bilioni

zimeshatumika kutekeleza ujenzi huo na Tsh. 839 milioni

zimeshalipwa na wananchi tofauti kwa ununuzi wa nyumba 20. Aidha, Serikali ya

Mapinduzi Zanzibar imeonesha nia ya kununua majengo matano; moja la vyumba vinne,

moja la vyumba vitatu na matatu ya vyumba vitatu wakati Benki Kuu ya Tanzania (BOT)

ilitarajiwa kusaini mkataba wa jengo moja la vyumba vitatu. Gharama za nyumba hizo ni

Tsh. 168.82 milioni kwa nyumba yenye vyumba viwili, Tsh. 190.84 milioni kwa nyumba

yenye vyumba vitatu na Tsh. 249.56 milioni kwa nyumba ya vyumba vinne.

Kimsingi, Kamati haikuridhishwa na kiwango cha ujenzi wa nyumba hizo kwani vifaa

vilivyotumika ni vya kiwango cha chini haviendani na gharama halisi za mradi huo.

Kadhalika, ujenzi huo haukulenga kumsaidia mwananchi wa kipato cha chini na cha kati

kumudu gharama za ununuzi wa nyumba hizo kwani Kamati imegundua kuwa

mwananchi wa kipato cha kati atalazimika kutumia muda mwingi hadi atafikia katika

kiinua mgongo ili kulipia gharama za nyumba ya vyumba viwili. Kwa mantiki hiyo,

mradi haukukidhi azma ya Marehemu Mzee Abeid Aman Karume, Rais wa Kwanza wa

Zanzibar ya kuwapatia makaazi bora wakwezi na wakulima, ikizingatiwa kwamba mradi

huo unaendeshwa kwa michango yao lakini huwanufaisha wananchi wa kipato cha juu.

Kupitia Programu Kuu ya kutoa hifadhi ya jamii, ZSSF imeanza kuendeleza ujenzi wa

jengo la kibiashara la Michenzani Makontenani. Aidha, mradi wa ujenzi wa nyumba za

kisasa za Kwahani umeanza na Serikali tayari imeshakubaliana na Kampuni za CCECC na

LINGHANG GROUP kutekeleza mradi huo.

CHANGAMOTO

1. Kuna uwezekano mkubwa wa Mkandarasi kushindwa kukamilisha nyumba hizo

ndani ya wakati.

2. Kushindwa kukabidhi hati ya umiliki wa nyumba hizo kwa watu

waliokwishakamilisha malipo kutokana na Bodi ya ‘Condominium’ kushindwa

kukutana.

3. Kutokuwepo eneo la kutosha la kuegesha gari katika mradi huo lenye kukidhi

haja ya watu watakaotarajiwa kukaa katika nyumba hizo.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 20

4. Kukosekana kwa vifaa vya kuashiria uwepo wa moto (fire detectors) katika

majengo hayo.

5. Kutopatikana Mkurugenzi Mwendeshaji mara tatu katika ziara za kamati ingawa

ratiba imethibitishwa na afisi yake.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. ZSSF ihakikishe inajenga majengo bora, ya kisasa na ya bei nafuu ambayo

wananchi wa kawaida wataweza kuzimudu.

2. Kamati inaitaka ZSSF ihakikishe Mkandarasi anakamilisha mradi huo kwa wakati.

3. Wizara kwa kushirikiana na ZSSF ihakikishe wanunuzi wa nyumba za mradi huo

wanapatiwa hati za umiliki wa nyumba hizo mara tu baada ya kukamilisha

malipo.

4. ZSSF ihakikishe inatumia mbinu mbadala itakayowezesha kupatikana kwa eneo la

kutosha la kuegesha magari ili kukidhi haja ya watu wanaotarajiwa kukaa katika

nyumba hizo.

5. ZSSF ihakikishe kunakuwepo kwa vifaa vya kuashiria uwepo wa moto (fire

detectors) katika majengo hayo.

2.10.5 SHIRIKA LA BIMA ZANZIBAR

Shirika la Bima Zanzibar limeanzishwa mwaka Juni, 1969 Chini ya Sheria ya Mitaji ya

Umma Nam. 4 ya 2002 ikiwa na dhima kuu ya kuwarudishia hali waliyokuwa nayo

wateja wao kabla majanga hayajawakumba. Utendaji wa Taasisi hii unasimamiwa na

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima ya Tanzania (TIRA).

Kamati inalipongeza Shirika la Bima Zanzibar kwa hatua ya maendeleo iliyofikia ya

kuonesha mfano kwa Mashirika au Taasisi nyengine za Serikali kwa kutawanya matawi

yake hadi kufika Dar - es Salaam, Mwanza, Mbeya, Dodoma na maeneo mengine ya

Tanzania Bara. Shirika limefikia mafanikio hayo kutokana na mashirikiano makubwa kati

yake na Bodi ya Wakurugenzi inayosimamia kazi zake. Kadhalika, Shirika limejenga jengo

lake la kisasa liliopo Mpirani na kulikodisha kwa taasisi mbalimbali zikiwemo Benki ya

Watu wa Zanzibar na Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF).

Changamoto kubwa inayolikabili shirika hili ni matumizi makubwa ya fedha za kulipia

gharama za fidia kwa wanachama. Hali hii inazorotesha uimarikaji wa mapato ya Shirika

hilo kwani kuna baadhi ya wanachama huwa wananunua gari zilizokuwa zimeshatumika

na kufanya makisio ya gari mpya au wakiona vyombo vyao vimeshachakaa huvichoma

moto kwa makusudi na kudai malipo. Lakushangaza na kubwa zaidi kuna baadhi ya

vyombo mara tu baada ya kusajiliwa havichukui muda huharibika na kuendelea

kuharibika huku vikidai mrejesho kutoka Shirika.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 21

CHANGAMOTO

1. Bado Taasisi inatumia majengo ya kukodi tena kwa gharana kubwa huko

Tanzania Bara.

2. Ajali nyingi zinatokea na kusababisha kuongezeka kwa madai kutoka kwa

wanachama.

3. Taasisi imetumia gharama kubwa katika utengenezaji wa Meli ya M.V Mapinduzi

II kwa vile imekatiwa Bima lakini haikukaa muda mrefu ikaharibika bila ya

kufahamika kwa uwazi sababu za msingi za maharibiko hayo. Shirika la Bima la

Zanzibar kwa kushirikiana na taasisi nyengine za bima (co insurer) zimeingia

mkataba na Shirika la Meli kwa ajili ya Bima kwa M.V Mapinduzi II ambapo mara

tu baada ya maharibiko hulazimika kufidia gharama za matengenezo ambazo ni

kubwa mno.

4. Baadhi ya Kampuni za Bima hazilipi fedha za vitabu vilivyojaa na kupatiwa vitabu

vyengine.

5. Baadhi ya Wafanyakazi wa Shirika hilo huwa si waaminifu kwani hutoa siri na

nyaraka za shirika kwa watu wasiostahiki.

6. Kukosekana Bima ya wakulima kwa vipando vyao.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kamati inalishauri Shirika kuwa na mpango wa kununua kiwanja au jengo kwa

ajili ya kulitumia kama Ofisi ya Shirika huko Tanzania Bara na kulikodisha kwa

taasisi nyengine ili kujiongezea mapato.

2. Shirika lishirikiane ipasavyo na Jeshi la Polisi pamoja na Taasisi nyengine ili liweze

kutoa elimu kuhusu umuhimu wa Bima na mbinu bora zitakazotumiwa kukinga

ajali.

3. Kamati inalitaka Shirika kuwa makini na wadanganyifu wanaoweka makadirio ya

gari mpya wakati wa ukataji bima ingawa gari aliloingiza nchini limeshatumika.

4. Kamati inalitaka Shirika kuwafuatilia mawakala wote wasiolipa malimbikizo ya

madeni yao na kukataza kabisa utoaji wa vitabu vya Bima pasi na kulipia kitabu

cha awali alichopewa wakala.

5. Kamati inalishauri Shirika kuwa makini sana wakati wa kuingia mikataba ya Bima

kwani baadhi ya vyombo huwa havichukui muda mrefu vinaharibika na

kulisababishia Shirika kulipa gharama.

6. Shirika liweke adhabu kali na kuzitekeleza kivitendo kwa wale wote

watakaobainika wanatoa siri za Afisi.

7. Kamati inalishauri Shirika kuanzisha Bima maalum kwa ajili wakulima, wafugaji na

wavuvi nchini.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 22

2.11 PROGRAMU KUU YA USIMAMIZI WA MFUKO MKUU WA SERIKALI

Programu hiyo imekusudia kufanya malipo maalum ya Serikali pamoja na kufanya

malipo ya madeni ya Serikali. Utekelezaji wa Programu hiyo unafanywa na Idara ya

Muhasibu Mkuu wa Serikali.

Kwa kipindi kirefu, Baraza hili lilikuwa likinyanyua sauti ya pamoja kutaka Wizara ya

Fedha na Mipango itekeleze kivitendo utaratibu wa kuwabadilisha Wahasibu (job

rotation) ili kuondosha kuzoeleka katika taasisi zao. Hatua hii ni muhimu kwa kuwalinda

wahasibu na Makampuni, taasisi na watu wenye kipato kikubwa kuwarubuni na kuathiri

utendaji wao. Lakushangaza, zoezi hilo jema limewekewa vikwazo na baadhi ya

Viongozi wa Umma kwa kutumia nafasi zao vibaya na kuwafanya watendaji

wanaohusika kuwa na wasiwasi wa maisha yao.

Kamati inakemia vikali kitendo hicho na kuwataka Viongozi wa umma kuacha tabia hiyo

kwani utekelezaji wa uhamisho huo unafanywa kwa mujibu taratibu za kifedha kwa

lengo la kuimarisha demokrasia katika utendaji. Iwapo desturi kama hizo zitakuwa

zinaendelezwa, ufanisi hautopatikana na kuathiri watendaji wanaochapa kazi kwa

maslahi ya Zanzibar.

Kamati inaupongeza mfuko kwa kutumia jumla ya shilingi 6.87 bilioni kuwalipa pencheni

wastaafu 13,000 kila mwezi. Licha ya mafanikio hayo, Mfuko pia umetumia jumla ya

4.00 bilioni kuwalipa mafao (kiinua mgongo) wananchi ambao wamemaliza utumishi

wao kwa mujibu wa sheria.

CHANGAMOTO

1. Baadhi ya Viongozi kuingilia utendaji wa Mfuko na kuathiri utekelezaji wa

majukumu ya msingi ya mfuko huo.

2. Baadhi ya wakati hutokea wastaafu wetu kuchelewa kupata viinua mgongo vyao.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kamati inawashauri Viongozi wa Umma na watendaji wengine kuacha kuingilia

masuala ya uhamisho wa Wahasibu kwani masuala hayo yanafanywa kwa mujibu

wa taratibu zinavyoelekeza.

2. Kamati inaishauri Wizara kulishughulikia ipasavyo na kwa wakati suala la malipo

ya kiinua mgongo na pencheni kwa watumishi wetu mara tu baada ya kustaafu.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 23

2.12 PROGRAMU KUU YA UTAWALA NA UENDESHAJI WA TUME YA MIPANGO

Kamati inatoa pongezi kwa mradi huu kwa ujenzi wa mitaro ya kupitishia maji machafu

inayojengwa katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo kwa binti Amran, Kwerekwe na

Sebleni. Mwelekeo wa matokeo wa miradi hiyo inaonekana kuleta mafanikio makubwa

kwani wananchi wa Jang’ombe na maeneo ya jirani yamebakia kuwa makavu tofauti na

siku zilizopita ambapo katika kipindi cha mvua za masika au vuli, wananchi wetu

huamua kuhama kutokana na kuingiliwa na maji ya mvua.

Kwa vile Tume ndio chombo kikuu cha kuratibu utekelezaji wa ZUSP, Kamati inatoa

pongezi kwa mradi wa ujenzi wa mitaro ya kupitishia maji machafu inayojengwa katika

maeneo mbalimbali nchini ikiwemo kwa binti Amran, Mwanakwerekwe na Sebleni.

Mradi huo umeleta mafanikio makubwa kwa kuwaondolea usumbufu wa kutuama maji

ya mvua kwa wananchi wa maeneo mbali mbali. Kamati inaiomba ZUSP kuchukua

juhudi za makusudi kuhakikisha miundombinu iliyoharibiwa ikiwemo barabara na maji

inarudishwa katika hali yake ya awali ili iendelee kuwahudumia wananchi wetu.

ZUSP imepanga kutekeleza Mradi wa kuweka taa za Barabarani (street light II) katika

maeneo ya barabara za Unguja yenye kilomita 15.4 na kilomita 17 kwa Pemba. Barabara

zitakazopatiwa huduma hizo kwa Unguja ni barabara ya Uwanja wa ndege - Mnazi

Mmoja, Mwanakwerekwe - Kiembesamaki na Kinazini Kariakoo mpaka Kilimani. Kwa

upande wa Pemba ni barabara za miji yote mitatu ya Pemba (Mkoani, Chake chake na

Wete) ikijumuisha barabara za Limbani - Wete Miji, Mtemani - Bopwe, Mtemani -

Kinyasini na Abdalla Mzee - Bandarini. Mradi huo utakapomaizika, utaiweka miji yetu

iking’ara muda wote wa usiku.

CHANGAMOTO

1. Kuchukua muda mrefu kumalizika kwa baadhi ya miradi.

2. Kuharibiwa kwa miundombinu kunakosababishwa na ujenzi wa Miradi hiyo

ikiwemo mabomba ya maji na barabara.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kamati inashauri Wizara kuelekeza nguvu zake kwenye maeneo ya ng’ambo

ambayo yana idadi kubwa ya wakaazi na ni jirani sana na mji wetu.

2. Kamati inaitaka Tume kubuni miradi mingine itakayokuwa na maslahi na nchi

yetu.

3. Kamati inaitaka Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar kwa kushirikiana na

Wizara ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa makini sana wakati

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 24

nchi yetu inapohitaji mikopo kwani imebainika kuwa, baadhi ya washirika wa

maendeleo hutoa masharti magumu na yasiyokuwa na maslahi kwa nchi zetu.

4. Kamati inaitaka Wizara kufanya usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo

nchini, kwani kumejitokeza wimbi la miradi ambayo haikamiliki kwa wakati

kutokana na sababu mbalimbali na kuitia hasara Serikali.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 25

3. WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI

Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi ni moja kati ya Wizara muhimu ambayo

imebeba sekta zinazoigusa jamii moja kwa moja kwani takriban zaidi ya asilimia arubaini

ya wananchi wetu wanategemea kipato chao kupitia sekta hizo. Kwa upande wa

mchango wa sekta hizo kiuchumi, kiasi cha asilimia 29.7 ya pato la nchi yetu

limechangiwa na sekta hii muhimu ya kilimo. Kutokana na umuhimu wake, Serikali

imewekeza katika sekta hiyo ili kusaidia kupunguza umasikini katika nchi yetu.

a) Programu kuu ya Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya Kilimo;

b) Programu kuu ya Maendeleo ya Kilimo;

c) Programu kuu ya Maendeleo ya Rasilimali za Misitu na Maliasili zisizorejesheka;

d) Programu kuu ya Maendeleo ya Mifugo;

e) Programu kuu ya Maendeleo ya Uvuvi;

Programu hizo zinatekelezwa na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kupitia

Taasisi na Idara zifuatazo:

i. Idara ya Mipango, Sera na Utafiti;

ii. Idara ya Uendeshaji na Utumishi;

iii. Idara ya Kilimo;

iv. Idara ya Misitu na Maliasili zisizorejesheka;

v. Idara ya Umwagiliaji maji;

vi. Idara ya Uhakika wa Chakula na Lishe;

vii. Idara ya Maendeleo ya Mifugo;

viii. Idara ya Maendeleo ya Uvuvi;

ix. Taasisi ya Utafiti wa Kilimo;

x. Chuo cha Kilimo Kizimbani;

xi. Wakala wa Serikali wa Huduma za Matrekta na zana za kilimo.

xii. Wakala wa Utafiti wa Mifugo;

xiii. Kampuni ya Uvuvi Zanzibar (ZAFICO); na

xiv. Afisi Kuu Pemba.

3.1 UTEKELEZAJI WA PROGRAMU KUU ZA WIZARA

Katika kipindi cha Julai hadi Disemba 2018, Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi

ilipanga kuingiziwa jumla ya shilingi 38.13 bilioni ambapo hadi Disemba, Wizara

iliingiziwa shilingi 58,087,125,299 sawa na asilimia 152 ya makadirio kwa ajili ya

kutekeleza Programu zake. Kamati imetembelea na kupitia ripoti mbali mbali za Wizara

hiyo na kugundua mambo yafuatayo:

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 26

3.2 PROGRAMU KUU YA UENDESHAJI NA URATIBU WA WIZARA YA KILIMO

Programu hiyo imekusudia kuweka mazingira bora kwa wafanyakazi, kuwa na mipango

na sera ya sekta za fedha iliyoimara nchini itakayosaidia kukuza uchumi pamoja na

kuhakikisha shughuli zilizopangwa kwa sekta ya fedha Pemba zinatekelezwa. Utekelezaji

wa Programu hiyo unafanywa na Idara ya Mipango, Sera na Utafiti, Idara ya Uendeshaji

na Utumishi na Afisi Kuu Pemba.

3.3 OFISI YA AFISA MDHAMINI PEMBA

Afisi ya Afisa Mdhamini - Pemba ni Afisi muhimu ambayo inasimamia na kuratibu Idara

zote zinazofanya kazi chini ya Wizara ya kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Pemba.

Pamoja na juhudi kubwa zinazochukuliwa na Afisi ya Wizara ya Kilimo Pemba, Kamati

imebaini kuwa bado zao la mwani halijawanufaisha wananchi wetu kama

ilivyokusudiwa. Licha ya ugumu wa ukulima wa mwani, asilimia kubwa ya wananchi wa

ukanda wa pwani hujihusisha na kilimo hicho lakini bado bei ya zao hilo ni ndogo

isiyolingana kabisa na hali ya maisha.

Kamati inaipongeza Serikali kwa mipango yake ya kuanzisha kiwanda cha kusarifu

mwani na inashauri utekelezaji wa mpango huo ufanyike haraka iwezekanavyo ili

kuwaondolea wananchi ugumu wa maisha kwa kuongeza thamani ya zao hilo.

CHANGAMOTO

1. Vyanzo vingi vya mapato havijasimamiwa ipasavyo na kuweza kuiongezea

mapato Serikali.

2. Bado wakulima wetu wanaendelea kulima kilimo cha zamani cha mpunga na

kupelekea kipato chao kuwa kidogo.

3. Maofisa ugani hawaonekani kuwafikia wakulima kwenye maeneo yao na

kuwapatia msaada wa kitaalamu pale wanapohitaji.

4. Halmashauri zetu hazina uwezo wa kutosha kuhakikisha wakulima wetu

wanapata elimu ya ukulima wenye tija.

5. Baadhi ya misingi ya umwagiliaji maji imejengwa kwa udongo kwenye mabonde

ya mpunga na kupelekea kuharibika mara kwa mara hususan katika kipindi cha

mvua.

6. Uchelewaji mkubwa wa upatikanaji wa pembejeo za kilimo cha mpunga

zikiwemo mbegu na mbolea.

7. Baadhi ya makampuni ya mwani husafirisha kwa mwani mbichi na kupelekea

kuharibu bei ya mwani na taswira nzima ya nchi yetu katika soko la Kimataifa.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 27

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO WA KAMATI

1. Afisi ihakikishe inavitambua vyanzo vya mapato vilivyopo ambavyo bado

havijaanza kukusanywa pamoja na kuibua vyanzo vyengine vipya.

2. Afisi itoe elimu ya kutosha kwa wakulima ili waweze kulima kilimo cha kisasa cha

kibiashara ambacho kinatumia eneo dogo lakini kipato chake huwa kikubwa.

3. Pamoja na Serikali kuamua kugatua baadhi ya maeneo yake na kuyapeleka

Halmashauri, bado utendaji wa Halmashari hizo upo chini, hivyo Afisi ihakikishe

inatoa ushirikiano wa hali na mali katika kuendeleza kilimo na hata kuwashirikisha

katika vikao vyao.

4. Afisi ihakikishe pembejeo za kilimo zinapatikana kwa wakati ili wakulima waweze

kulima kwa wakati na kufaidika na kilimo chao.

5. Afisi ijikite zaidi na ujenzi wa mitaro ya maji kwa kutumia saruji ili kuiwezesha

kudumu kwa kipindi kirefu.

6. Afisi ihakikishe inawaelimisha wananchi kuhusu athari za uuzaji mwani mbichi

katika Soko la Kimataifa na kuwachukulia hatua wale wote wanaohusika na

kadhia ya kusafirisha mwani mbichi nje ya nchi.

3.4 PROGRAMU KUU YA MAENDELEO YA KILIMO

Programu hiyo imekusudia kuboresha uzalishaji wa kilimo kwa kuongeza eneo la

umwagiliaji maji kwa kutumia teknolojia na usimamizi endelevu, kuimarisha na

kuendeleza tafiti za kilimo na maliasili pamoja na kuongeza wataalamu wa fani ya kilimo

na mifugo, kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za kilimo kwa wakulima na

kuhakikisha upatikanaji wa chakula na lishe. Utekelezaji wa Programu hiyo unafanywa

na Idara ya Umwagiliaji maji, Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Kizimbani, Idara ya Kilimo na

Idara ya Uhakika wa Chakula na Lishe. Miongoni mwa mambo ambayo Kamati iliyaona

kwenye Programu hiyo ni:

3.5 SHAMBA LA RAZABA - MAKURUNGE BAGAMOYO

Shamba la RAZABA ni lenye historia ndefu inayodhihirisha udugu na umoja wa

Watanzania. Shamba hilo lililopo Bagamoyo lina ukubwa wa hekta 26,812 ambalo

lilitolewa na Rais wa awamu ya Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Marehemu Mwalimu Julius K. Nyerere kwa Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar

Mheshimiwa Aboud Jumbe Mwinyi mwaka 1977, kwa lengo la kuiwezesha Zanzibar

kuwa na eneo la ardhi kwa uendelezaji wa sekta ya mifugo ili iweze kumudu ongezeko

la idadi ya wakaazi wake ambayo inaongezeka siku hadi siku.

Baada ya muda mrefu kupita bila ya shamba hilo kuendelezwa, Serikali ya Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania ilikabidhiwa hekta 20,595 kwa ajili ya kuzitumia kwenye

shughuli za maendeleo ambapo hekta 10,000 tayari amepewa mwekezaji kwa ajili ya

uanzishaji wa kiwanda cha sukari. Eneo la Zanzibar lililobakia ni jumla ya hekta 6,217

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 28

ambazo hadi Kamati inafika katika eneo hilo hakuna shughuli zozote za uzalishaji

zinazoendelea.

CHANGAMOTO

1. Uvamizi wa shamba hilo unaofanywa na wananchi kwa ajili ya makaazi na

uanzishaji wa mabwawa ya samaki. Jumla ya kaya 80 zilivamia katika shamba hilo

kwa ajili ya makaazi.

2. Kuna wafugaji binafsi ambao wamehodhi sehemu ya shamba hilo na kulitumia

kwa shughuli zao za ufugaji.

3. Kuwepo kwa Bandari bubu zipatazo 19 katika ukanda wa pwani wa shamba hilo

ni suala linalohatarisha usalama wa wananchi wa Bagamoyo na Taifa kwa ujumla.

4. Igawa eneo lililopo shamba hilo ni ndani ya ukanda wa Uwekezaji Kiuchumi

(EPZ), shamba haliwezi kutumika kwa ajili ya uwekezaji kutokana na kukosekana

hati miliki.

5. Kutoendelezwa kwa shamba hilo kunasababisha watu tofauti kuvutiwa na

kudanganywa kwa kuuziwa viwanja.

6. Uhaba wa walinzi wa shamba hilo.

7. Walinzi wa shamba hilo kutishiwa maisha na wananchi waliovamia shamba.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kwa vile shamba hivi sasa limekabidhiwa kwa Chuo cha Kilimo Kizimbani, Kamati

inaishauri Serikali kufikiria maudhui ya awali ya shamba hilo kwa kuwashirikisha

wafanyabiashara binafsi wanaoleta ng’ombe wa kuchinja ili walitumie shamba

hilo na Serikali kutoza kodi.

2. Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi izifanyie matengenezo makubwa

nyumba za makaazi ya wafanyakazi wake waliopo Bagamoyo.

3. Wizara ihakikishe inaongeza idadi ya walinzi kwenye shamba hilo.

4. Kamati inaitaka Wizara kuimarisha maslahi ya Wafanyakazi wake walioppo

Bagamoyo.

5. Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Serikali ya Wilaya ya Bgamoyo ifanye

juhudi za makusudi kuwaondoa wavamizi wa shamba la Makurunge. Kamati

imeshtushwa na taarifa kwamba baadhi ya wavamizi hao wanaishi shambani hapo

kwa muda mrefu na tayari wameshazaa na kujukuu.

3.6 KILIMO CHA MBOGA KISAKASAKA

Kilimo ni sekta inayoajiri asilimia kubwa ya wananchi katika nchi nyingi zinazoendelea.

Wakulima huamua kujikita kwenye kilimo cha mazao mbalimbali kutokana na mazingira

yao. Kamati ilitembelea jumla ya wakulima 89 wa mazao ya mbogamboga katika eneo

la Kisakasaka ili kujua maendeleo waliyofikia na changamoto wanazokabiliana nazo

katika shughuli zao za kila siku.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 29

Kamati iliarifiwa kuwa Mabwana na Mabibi shamba hawawajibiki ipasavyo

kuwatembelea wakulima katika maeneo ya kilimo na kuwashauri njia za ukulima bora na

kukabiliana na changamoto zinazojitokeza. Kamati imesikitishwa na kitendo hicho

kinachosababisha usumbufu kwa wakulima na kupelekea kutumia njia za kienyeji kuhami

mazao yao jambo ambalo hupunguza mavuno.

CHANGAMOTO

1. Kuwepo kwa wadudu waharibifu wa mazao katika maeneo wanayolima.

2. Ukosefu wa maji ya uhakika kwa ajili ya umwagiliaji shambani. Hadi wakati

Kamati ilipowatembelea, wakulima hao walikuwa wakiendesha shughuli za

umwagiliaji kwa njia za kizamani ambazo hutumia nguvu na muda mwingi.

3. Ukosefu wa miundombinu mizuri ya barabara inayopelekea wakulima kusafirisha

mazao kwa njia zisizo rasmi kutokana na ukweli kwamba barabara wanayopaswa

kuitumia haipo katika hali ya kuridhisha.

4. Ushindani mkubwa wa soko unaochangiwa zaidi na uingizwaji wa tungule kutoka

Tanzania Bara hususan katika msimu wa mavuno ya tungule kwa wakulima wetu.

5. Migogoro ya ardhi inayowakabili wakulima kwenye maeneo yao kutokana na

watu wachache kuhodhi ardhi bila ya kuitumia na hivyo kuwakosesha wengine

fursa za kujiajiri.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kamati inaitaka Wizara kushughulikia suala la upatikanaji wa maji kwa ajili ya

kukidhi mahitaji ya umwagiliaji wa kisasa kwa njia ya matone (drip irrigation).

2. Wizara iwapatie wakulima wetu utaalamu wa kulima kilimo cha vitunguu kwani

inasemekana ardhi ya eneo la kisakasaka inakubali zao hilo.

3. Wizara ihakikishe inawapatia wakulima pembejeo za kilimo ili wazalishe kwa

wingi zao hilo.

4. Kamati inaisisitiza Wizara ya Kilimo kufanya tafiti mbalimbali kuhusu ardhi na

matumizi yake ili kuwaelekeza wananchi walime kilimo bora kwa maslahi yao na

Taifa hili.

5. Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Biashara ihakikishe inadhibiti soko kwa

kuzuwia bidhaa zinazotoka nje ya nchi ambazo zinazalishwa nchini kutoingia

Zanzibar ili wakulima wetu waweze kupata soko la bidhaa wanazozalisha.

6. Kamati inaitaka Wizara ishirikiane na Halmashauri husika kuwasimamia vyema

Mabwana na Mabibi shamba na kuhakikisha wanawapatia wakulima wetu

msaada unaostahiki.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 30

3.7 KILIMO CHA MPUNGA BONDE LA CHAANI KIKOBWENI

Bonde la Mpunga la Chaani Kikobweni lina ukubwa wa ekari 165 zinazolimwa na

wakulima 187 kati yao 133 ni wanawake na 54 wanaume. Bonde hilo lina wakulima wa

kilimo cha juu (kinachotegemea mvua) na wengine wanalima kilimo cha umwagiliaji maji

kinachosimamiwa na Kamati za wakulima waliogawika kwa mujibu wa maeneo

waliyotoka. Kituo kina matrekta manne, mawili ni mazima lakini mawili mabovu

yanasubiri matengenezo.

Kwa mwaka wa fedha 2018/2019, Wizara ilipangiwa kutumia jumla ya shilingi 1.5 bilioni

kwa ajili ya ununuzi wa pembejeo za kilimo. Kiwango hicho ni kidogo ikilinganishwa na

jumla ya shilingi 4.5 bilioni zilizotengwa kwa mwaka uliopita. Kwasasa jumla ya Ekari 53

tayari zimeshaendelezwa kwa ajili ya Kilimo cha Umwangiliaji maji na wakulima wake

wameshapatiwa pembejeo kwa asilimia mia moja kupitia Mradi wa ERPP. Mradi huo

unaosimaniwa na Idara ya Umwagiliaji maji umelenga kuzalisha mbegu bora za msingi

kilo 400, kuandaa ziara ya mafunzo kwa Jumuiya za umwagiliaji kutoka skimu 16 Unguja

na Pemba, kujenga na kutengeneza miundombinu katika skimu tisa za umwagiliaji maji.

Mradi huo umejenga msingi wa saruji mita 1,200 Mtwango (canal lining) na mita 600

Kwalembona.

Kamati imebaini mapungufu makubwa ya upatikanaji wa pembejeo kwa wakulima wa

juu (wanaotegemea mvua) ambao wanahudumiwa na Serikali. Tofauti kubwa iliyopo

katika ununuzi wa pembejeo baina ya wakulima wa juu na wa umwagiliaji ni suala

linalohitaji kufikiriwa kwa kina kwani wakulima wa juu wanachangia shilingi 26,000

wakati wakulima wa umwagiliaji wanachangia shilingi 13,000 kwa lita. Aidha, huduma

za ulimaji na uburugaji pia haziridhishi kwa wakulima wa juu kwani Kamati iliarifiwa

kuwa wakulima wachache tu ndio waliolimiwa ingawa msimu wa kilimo ulikuwa

ukingoni.

CHANGAMOTO

1. Uhaba wa Matrekta ya kufanyia kazi.

2. Upungufu wa Pembejeo za kilimo hususan kwa wale wanaolima kilimo cha

mpunga wa kutegemea mvua.

3. Mwamko mdogo wa baadhi ya wakulima kuchangia fedha za kupatiwa huduma

za matrekta kwa wakati mwafaka.

4. Ukosefu wa banda la kuhifadhia vitendea kazi.

5. Ukosefu wa banda la wakulima kwa ajili ya kufanyia shughuli zao.

6. Upungufu wa mafundi wa matrekta katika kituo hicho kwani kituo kina fundi

mmoja tu ambae hana uzoefu wa kutosha.

7. Upungufu wa ziara za viongozi kuwatembelea wakulima husuan katika kipindi

cha maandalizi ya kulima.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 31

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Wizara ya kilimo ihakikishe inaongeza idadi ya Matrekta katika kituo cha kilimo

cha Chaani Kikobweni kwa ajili ya kulimia na kuburugia kwani wakulima

wamehamasika na wameonesha uwezo mkubwa wa kujitolea na kuchangia fedha

za kupatiwa huduma hiyo.

2. Wizara ihakikishe inatoa pembejeo za kilimo kwa wakulima wote tena bila ya

kuwepo tafauti ya bei na aina ya kilimo mtu anacholima kama cha umwagiliaji au

cha kutegemea mvua.

3. Idara ya kilimo pamoja na kamati ya wakulima wa Chaani Kikobweni

wawahamasishe wakulima wao kufanya malipo ya huduma za matrekta mapema

iwezekanavyo ili waweze kulimiwa mapema.

4. Kamati inaishauri Wizara ya kilimo kujenga banda la kuhifadhia matrekta na

kuyanunusuru kuathiriwa na jua kali au mvua ili kuyazidishia uhai wa maisha yao.

5. Viongozi wa Serikali na kisiasa wawe wafanye ziara kwa wakulima mara kwa

mara ili waweze kugundua changamoto wanazokabiliana nazo na mafanikio halisi

waliyofikia.

3.8 PROGRAMU KUU YA MAENDELEO YA RASILIMALI ZA MISITU NA MALIASILI

ZISIZOREJESHEKA

Programu hiyo imekusudia kukuimarisha na kuendeleza uhifadhi wa misitu na kuimarisha

mazingira ya misitu. Utekelezaji wa Programu hiyo unafanywa na Idara ya Misitu na

Maliasili zisizorejesheka. Miongoni mwa mambo ambayo Kamati iliyagundua kwenye

Programu hiyo ni:

Kamati iliarifiwa kwamba kwa kipindi hiki, nchi yetu inajitosheleza kwa rasilimali ya

mchanga ambapo maeneo matatu yaliyopendekezwa kwa ajili ya uchimbaji

yamekaguliwa na kufanyiwa tathmini ya kina cha mchanga kilichopo. Kwa kipindi cha

Julai - Disemba 2018, makusanyo halisi ya uzalishaji wa mawe, mchanga na kokoto ni

jumla ya shilingi 240,355,000.

Licha ya hali hiyo, Kamati inaitaka Wizara iwe makini na uvunaji wa rasilimali hizo

ikizingatiwa jiografia ya nchi yetu ni visiwa. Ni dhahiri kuwa umakini mkubwa

unahitajika katika matumizi ya rasilimali hizo ili ziweze kutumika kwa muda mrefu na

kuepukana na uagizaji wa mchanga kutoka nje ya nchi.

3.9 MSITU WA HIFADHI YA VUMAWIMBI NGEZI

Msitu wa Hifadhi ya Vumawimbi Ngezi ni msitu mkubwa kuliko misitu yote iliyopo

Pemba na ndio msitu wa pili kwa ukubwa Zanzibar baada ya Msitu wa Hifadhi ya

Jozani. Msitu huo ulianza kuhifadhiwa tokea mwaka 1959 na mwaka 2004 ukatambulika

rasmi kuwa ni Msitu wa Hifadhi ya Vumawimbi. Msitu huo wenye hekta 2,900

umezungukwa na vijiji 10 vyenye wakaazi 21,000. Kutokana na utafiti uliofanywa na

wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kuna aina 355 ya miti inayopatikana

ndani ya msitu huo ambayo 11 inaweza kutumika kwa matumizi ya utengenezaji wa

dawa tofauti. Aidha, msitu huo una miti mingi ambayo haipatikani popote duniani.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 32

Kamati inaipongeza Wizara kwa juhudi inazozichukua za kuhamasisha wananchi

kuendelea kufanya utalii wa ndani kwa kutembelea maeneo yaliyomo Zanzibar na sio

kuamua kwenda nje wakati hayo wanayoyafuata huko mengine yanapatikana hapa hapa

Zanzibar. Licha ya changamoto zilizopo, Msitu umeweza kuendeleza hadhi yake ya kuwa

msitu wa Hifadhi, kwa ujenzi wa Mkahawa na eneo la Mapokezi na kubakiza asilimia

thelathini ya makusanyo yanayotokana na msitu huo ili yatumike kwa maendeleo ya

Hifadhi.

CHANGAMOTO

1. Kuwepo kwa mbwa wanaoingia katika msitu na kuua wanyama waliomo ndani

ya msitu.

2. Baadhi ya wanavijiji wanaouzunguka msitu huo wanapika pombe za kienyeji

(gongo) ndani ya msitu huo.

3. Kuvamiwa kwa msitu na baadhi ya watu kwa kukata miti. Historia inaonesha

Msitu uliwahi kuvamiwa na watu kutoka Kenya waliokuwa na Misumeno ya

moto na kukata magogo.

4. Uhaba mkubwa wa walinzi wa msitu huo kwani msitu una jumla ya walinzi 8

wanafanya shughuli za doria.

5. Ubovu wa barabara ya kufika katika eneo la msitu.

6. Msitu umepitiwa na njia katikati na kusababisha watu kupita kila wakati, jambo

hilo huleta usumbufu hususan katika masuala mazima ya kiulinzi.

7. Madai ya wananchi kuhodhi eneo la msitu huo. Kumejitokeza ukoo wa Mjaja na

kusema sehemu ya msitu imemilikiwa na wazee wao tangu zamani. Hivyo mara

kwa mara hujaribu kujenga na Idara hulazimika kubomoa.

8. Kujitokeza baadhi ya watu kutaka kuweka uwekezaji ndani ya msitu hususan kwa

kujenga hoteli.

9. Ukosefu wa mkahawa kwa ajili ya wageni wanaotembelea eneo hilo.

10. Ukosefu wa njia za ndani zinazotumika kuingia katika ziwa Taufik lililomo katika

msitu huo ili kuwawezesha watalii kufika hadi katikati ya ziwa hilo na kujionea

viumbe vilivyomo ndani yake.

11. Kutokuwepo kwa kipaa kilichojengwa juu ya mashine za zamani zilizokuwa

zikitumika kupasulia mbao pamoja na maelezo yanayoelezea historia ya mashine

hizo.

12. Kukosekana kwa vyoo ndani ya msitu ambavyo vingeweza kutumiwa na watu

wanaoutembelea msitu huo.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 33

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO WA KAMATI

1. Kamati inaitaka Wizara kulitumia eneo lililowekwa kwa ajili ya uwekezaji na eneo

la msitu libakie kuwa ni eneo la Hifadhi ya Taifa wala lisijengwe hoteli au nyumba

za makaazi.

2. Wizara ihakikishe inalifuatilia suala la ujenzi wa barabara itakayouzunguka msitu

kupitia eneo la Machopeni na kuungana na kijiji cha Makangale.

3. Wizara ihakikishe miti yote hatarishi kwa maisha ya miti mingine ambayo imo

ndani ya Msitu inadhibitiwa ipasavyo.

4. Wizara ihakikishe mbwa wanaoingia katika msitu na kuua wanyama waliomo

ndani ya msitu wanadhibitiwa.

5. Idara ya Misitu na Maliasili zisizorejesheka ihakikishe inadhibiti wapika ulevi

(gongo) ndani ya msitu.

6. Wizara ihakikishe inadhibiti uvamizi wa watu wote wanaoingia katika msitu na

kukata miti.

7. Wizara ihakikishe inatatua changamoto ya uhaba mkubwa wa walinzi wanaolinda

msitu huo.

8. Wizara ihakikishe inatatua mgongano uliopo kati ya watendaji wa msitu na ukoo

wa Bwana Mjaja unaodai sehemu ya msitu inamilikiwa na wazee wao tangu

zamani.

9. Wizara ihakikishe hakuna mtu atakaeruhusiwa kuwekeza katika eneo la msitu

pamoja na kutafuta hatimiliki ya maeneo ya msitu na yale ya uwekezaji.

10. Idara ya Misitu na Maliasili zisizorejesheka ihakikishe inakamilisha ujenzi wa

sehemu ya mapokezi na mkahawa kwa ajili ya wanaotembelea eneo hilo la msitu

huo.

11. Wizara ihakikishe inajenga vijia vidogo vidogo vitakavyomuwezesha Mtalii

kuingia na kufika katika maeneo ya vivutio yaliyomo katika msitu huo bila

usumbufu.

12. Wizara ihakikishe inazihifadhi kwa kuzijengea kipaa pamoja na kuziwekea

maelezo mashine za zamani zilizokuwa zikitumika kupasulia mbao.

13. Ni wajibu wa Wizara kujenga vyoo ndani ya msitu ambavyo vitaweza kutoa

huduma kwa watu wanaoutembelea msitu huo.

14. Idara ya misitu itafute mbinu za kuyaondoa maji yanayotuwama kipindi cha mvua

kwenye njia kuu iliyopita katika msitu huo.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 34

3.10 MSITU WA KIUYU MBUYUNI

Msitu wa Kiuyu Mbuyuni ni msitu wa zamani sana uliotangazwa kuwa msitu wa hifadhi

tangu mwaka 1987 ukiwa na hekta 770 lakini kwa sasa msitu huo una hekta 270. Hivi

karibuni kuna Mwekezaji amejitokeza kutaka kujenga hoteli ndani ya msitu huo kupitia

Mradi unaoitwa ‘Vault’ utakaochukua hekta 150 za msitu huo. Kamati inaitaka Wizara

kupiga marufuku uwekezaji wa kujenga hoteli ndani ya msitu huo isiyokuwa rafiki na

mazingira kwa ajili ya kuulinda msitu.

CHANGAMOTO

1. Kutofahamika ipasavyo maeneo ya msitu huo kwani eneo lililotangazwa katika

Gazeti Rasmi la Serikali ni kubwa ukilinganisha na uhasilia ulivyo hivi sasa.

2. Kutokezea kwa Muwekezaji kutaka kuwekeza ndani ya msitu husika kwa kujenga

hoteli inayoaminika haitokuwa rafiki na mazingira ya uendelezwaji wa Msitu.

3. Kukosekana kwa njia ya kufika katika eneo la Msitu.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Wizara ichukue juhudi za makusudi kutoa uelewa kwa jamii kuhusu uwepo wa

msitu wa Kiuyu Mbuyuni na maeneo yake ili eneo lililotangazwa katika Gazeti

Rasmi la Serikali liweze kueleweka na kuhifadhika.

2. Wizara ihakikishe eneo la msitu huo linafikika ipasavyo.

3.11 PROGRAMU KUU YA MAENDELEO YA MIFUGO

Programu hiyo imekusudia kuongeza uzalishaji na ubora wa mifugo na mazao yake

pamoja na kuimarisha huduma za utibabu wa mifugo kwa wanajamii. Utekelezaji wa

Programu hiyo unafanywa na Idara ya Maendeleo ya Mifugo. Miongoni mwa mambo

ambayo yametekelezwa na Programu hiyo na Kamati kuyatolea ushauri ni:

3.12 JUMUIYA YA WAFUGAJI KUKU

Jumuiya ya Wafugaji kuku iliopo Mwanakwerekwe imeanzishwa mwaka 2016 ikiwa na

lengo la kuwawezesha wafugaji wa kuku Zanzibar kufuga katika kiwango kinachotakiwa,

kuwapatia elimu ya ufugaji bora pamoja na kuhakikisha wafugaji hao wanapata

vifaranga vilivyo bora.

Kamati imegundua kuwepo kwa mahitaji makubwa ya kuku hususan kwenye sekta ya

utalii ambayo wafugaji wetu wa ndani hawajaweza kuyakidhi. Kwa mantiki hiyo, Kamati

inaiomba Wizara ya Kilimo kuwasaidia wafugaji wetu kwa kuwapatia utaalamu wa

ufugaji wa kisasa utakaowawezesha kuzalisha kuku wengi katika ubora unaokubalika.

Kadhalika, Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara ya Biashara zihakikishe kuku

wanaoingizwa ndani ya Zanzibar kutoka nje wanawekewa kodi kubwa ili waweze

kuwanyanyua wafugaji wa ndani.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 35

CHANGAMOTO

1. Ukosefu wa fedha za kununulia dawa na vyakula vya kuku.

2. Ukosefu wa machinjio ya kisasa.

3. Utaratibu unaotumika kuwapatia mikopo wafugaji hao ni mgumu

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kamati inashauri wafugaji wa kuku wapatiwe ruzuku ya kununulia dawa, mayai,

vifaranga na vyakula vya kuku kama wanavyopatiwa wakulima wa mpunga.

2. Wizara kwa kushirikiana na Serikali za mitaa kujenga machinjio ya kisasa

yatakayotoa huduma bora na kulinda afya za walaji.

3. Wizara iwahamasishe wakulima kulima mahindi ili yaweze kukobolewa na

kutumika kama chakula cha kuku.

4. Wafugaji wa kuku wapatiwe mikopo nafuu itakayowawezesha kumudu gharama

za uendelezaji wa shughuli zao.

5. Kamati inaitaka Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara ya Biashara

kukifufua kiwanda cha chakula cha kuku kilichokuwepo hapo awali na

kukabidhiwa wafugaji wa kuku kukiendesha.

6. Wizara ya Kilimo na Wizara ya Biashara ipange fungu maalum kwa ajili ya

kuwasaidia wafugaji kuku kwa kuwapatia mikopo nafuu.

7. Wizara ihakikishe kodi zinazotozwa kwa wafugaji kuku zinapunguzwa kwani

inawasababishia gharama kubwa za uzalishaji.

3.13 PROGRAMU KUU YA MAENDELEO YA UVUVI

Programu hiyo imekusudia kuongeza uzalishaji wa samaki na mazao mengine ya baharini

pamoja na kuendeleza uvuvi wa kienyeji na kusimamia rasilimali za baharini kwa

matumizi endelevu. Utekelezaji wa Programu hiyo unafanywa na Idara ya Maendeleo ya

Uvuvi. Miongoni mwa mambo ambayo yametekelezwa na Programu hiyo ni:

3.14 MRADI WA KUSIMAMIA UVUVI KUSINI MAGHARIBI MWA BAHARI YA HINDI

(SWIOFISH)

Mradi wa kusimamia Uvuvi Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi (SWIOFISH), huu ni

mradi unaosimamiwa na Idara ya Maendeleo ya Uvuvi ambao umelenga kutoa huduma

za kutengeneza mpango wa utekelezaji wa uvuvi wa kipaumbele wa pweza, samaki wa

miambani na samaki wa jamii ya dagaa, kujenga Ofisi mbili za uhifadhi wa mazingira ya

maeneo ya Hifadhi ya ghuba ya “Changuu Bawe Marine Conservation Areas”

(CHABAMCA) na “Tumbatu Marine Conservation Areas” (TUMCA). Mradi pia

umelenga kukarabati Ofisi za maeneo ya Hifadhi ya MIMCA, MENAI na PECCA pamoja

na kusimamia ujenzi wa Bandari ya Uvuvi (Jetty) katika eneo la Kampuni ya Uvuvi

ZAFICO.

Mradi umeshampata mjenzi wa Ofisi mbili za CHUMBAMCA na TUMCA na Mkataba

wake tayari umesharudi kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ambapo ushauri

na maelekezo yaliyotolewa yameshafanyiwa kazi. Aidha, ukarabati wa Ofisi za MENAI

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 36

na MIMCA unaendelea wakati PECCA umeshakamilika. Kwa upande wa ujenzi wa

Bandari ya Uvuvi, tangazo la kumpata Mshauri Elekezi wa kuandaa mchoro

limeshatolewa.

3.15 KAMATI ZA WAVUVI MENAI, PECCA NA MIMCA.

Kwa vipindi tofauti, Kamati ilipata fursa ya kukutana na Kamati za uvuvi Unguja na

Pemba ambazo zinawaunganisha wavuvi kutoka maeneo mbalimbali nchini. Kamati hizo

zimeundwa kisheria kwa lengo la kusaidia uhifadhi wa mazingira ya ukanda wa bahari na

kupelekea upatikanaji wa mazao mengi ya baharini. Kamati za uvuvi zimegawika katika

sehemu kuu tatu, kamati ya MIMCA inayofanya kazi zake za uhifadhi katika ukanda wa

Kaskazini Unguja wakati kamati ya MENAI ukanda wa Kusini Unguja na kamati ya

PECCA inashughulika na uhifadhi wa ukanda wa bahari wa Pemba.

Kamati hizo zinasaidia katika uhifadhi wa matumbawe ambayo ndiyo mazalio ya samaki,

kuimarisha ulinzi wa maeneo ya hifadhi ya bahari, kupiga vita uvuvi haramu, kutatua

migogoro ya wavuvi na ndio chombo kikuu kinachounganisha baina ya wavuvi na

Serikali.

Kupitia ziara hizo, Kamati iligundua mambo kadhaa ambayo yanazorotesha maendeleo

ya uvuvi nchini yakiwemo ukosefu wa mtaji kwa ajili ya kuvua uvuvi wa kisasa jambo

ambalo hupelekea kupata mavuno kidogo. Visiwa vyetu vina idadi kubwa ya wavuvi

ambao wanaendesha shughuli zao kwa njia za asili. Wavuvi hao hujikuta wanafanya kazi

kila uchao bila ya kujua hatma yao na familia zao kutokana na kipato duni

wanachojipatia (chungu jiko). Ili kupambana na hali hiyo, Kamati ya Fedha, Biashara na

Kilimo inaishauri Serikali kuharakisha mpango wake wa kuwapatia vyombo vya kisasa

wavuvi wetu. Sambamba na hilo, Kamati ya PECCA inaiomba Serikali kutoingizwa

samaki kutoka nchi za nje (perdue) kisiwani Pemba kama wanavyoingizwa kwa kasi

kisiwani Unguja. Kufanya hivyo kutawakosesha soko la ndani la samaki wao na kurejesha

nyuma juhudi zao za kupambana na umasikini.

Tunaipongeza Serikali kwa uamuzi uliochukuwa wa kuwapatia vyombo wavuvi wa

Zanzibar kupitia mradi wa MACEMP ili kuongeza kipato chao kulingana na kazi

wanayoifanya. Hata hivyo, Kamati haikufurahishwa na utaratibu uliotumika wa

kuvigawa vyombo hivyo kupitia Waheshimiwa ambao walivigawa bila ya kuzingatia

mahitaji halisi ya wavuvi, hatimae vyombo vingi viliishia kuuzwa na kutofikia lengo

lililokusudiwa. Tunaiomba Serikali inapochukua hatua ya ugawaji wa vyombo iwapatie

wahusika watakaonufaika na vyombo hivyo.

Licha ya visiwa vyetu kuwa na utajiri mkubwa wa mazao ya baharini, bado wavuvi wetu

hawajafanikiwa kuyavuna ipasavyo kutokana na kutokuwa na utaalamu na nyenzo za

kuyafikia. Hivyo, Kamati inaiomba Serikali kuwapatia utaalamu wa uvuvi wa kisasa,

kuwatengenezea viwanda vya samaki na kuwapatia meli kubwa za uvuvi ili waweze

kupata samaki walio bora kwani uvuvi unaoendeshwa hivi sasa ni wa kiwango cha chini

ambao hauna tija kubwa kwao.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 37

Kwa masikitiko makubwa, Kamati imerudishwa nyuma na utendaji wa baadhi ya

Viongozi wa Serikali yetu kwa kitendo cha kutaka kuwanyang’anya wanakamati ya

PECCA baadhi ya maeneo yaliyomo ndani ya hifadhi (kisiwa cha Misali, Uvunje na Njau)

kwa ajili ya kuyaendeleza kiutalii bila ya kushauriana na Kamati. Kitedo hicho

kimeikasirisha PECCA na kutaka eneo lao la hifadhi lisitumike kinyume na madhumuni ya

awali kwa maslahi ya wachache.

CHANGAMOTO

1. Upungufu mkubwa wa vitendea kazi ikiwemo boti za uokozi na ukaguzi, vespa na

gari za kuwapitia wavuvi wengine wadogo na kuwaokoa hususan katika nyakati

za upepo unaosababisha maafa makubwa kwa wavuvi.

2. Uvamizi wa maeneo ya hifadhi kwa matumizi mbadala.

3. Upungufu mkubwa wa mapato ya kuendeshea shughuli za uvuvi. Kamati za uvuvi

hazina mapato ya kutosha jambo ambalo husababisha mzunguko wa fedha kuwa

mdogo kiasi cha kushindwa kukidhi mahitaji yao ya msingi.

4. Utaratibu wa ukataji leseni za uvuvi kwenye Halmashauri unawakwaza wavuvi

wetu kwani huendesha shughuli zao katika sehemu tofauti.

5. Usumbufu wanaoupata wavuvi wakiwa katika shughuli zao pale wanapolazimika

kuchukua mafuta ya akiba kwa njia ya mageloni.

6. Kutonufaika na fedha za mnada katika masoko yao.

7. Kukosekana kwa mashirikiano ya kutosha kati ya Wavuvi na wawekezaji nchini.

8. Changamoto zilizojitokeza kwenye mfumo wa doria kwani wavuvi

wanapopeleka taarifa za kuwepo muhalifu, askari wa KMKM wanachelewa kufika

katika eneo husika.

9. Kutofuatwa kwa Kanuni ya Uhifadhi wa Bahari ambayo imeeleza wazi kwamba

asilimia 30 ya mapato yanayotokana na maeneo ya hifadhi yatumiwe kwa

maendeleo kamati hizo.

10. Mgongano wa maslahi baina ya Kamati za Uvuvi na Halmashauri kwa baadhi ya

masoko ambayo yamegatuliwa ilhali ujenzi wake umefanywa kwa nguvu za

wavuvi wenyewe.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kutokana na ukweli kwamba maeneo ya hifadhi yanalindwa na wananchi

wenyewe kupitia Kamati za Uvuvi kwa njia ya kujitolea, Kamati inaitaka Wizara

ya Kilimo na Serikali kwa ujumla kuwaunga mkono wananchi hao na kuilinda

hifadhi hiyo kwa kuwapatia vyombo vya ulinzi vikiwemo boti ya doria.

2. Kamati inaishauri Wizara kuanzisha Viwanda vya Kisasa vya Kusarifu Samaki na

pweza nchini ili kuinua hali za wavuvi wetu.

3. Wizara izisaidie utaalamu Kamati za uvuvi ili waweze kujiongezea kipato na

kuendesha maisha yao.

4. Serikali iwapatie ruhusa maalum wavuvi wanaovua sehemu za mbali kuchukua

mafuta ya ziada kwenye vyombo vyao. Jambo la msingi ni kuhakikisha mafuta

hayo yanahifadhiwa katika vyombo salama na kutumika kwa mujibu wa ruhusa

iliyotolewa.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 38

5. Serikali ilifuatilie kwa haraka mgogoro uliopo kati ya wavuvi wa Uvinje na

mwekezaji kabla haujaleta athari.

6. Wizara ya Kilimo ishirikiane na Wizara ya Serikali za Mitaa kuwaondoshea wavuvi

mzigo wa kulipa fedha zisizostahiki kwa sheha.

7. Kamati inaitaka Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara ya Serikali za Mitaa

kuwaondolea usumbufu wavuvi kwa kuendelea na mfumo wa ukatishaji wa leseni

kupitia Idara ya Uvuvi ikizingatiwa kwamba wavuvi ni watu wa kuhamahama

kutoka sehemu moja hadi nyengine kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zao.

Utaratibu wa kukatisha leseni kwenye Halmashauri unawakwaza wavuvi hao.

8. Wizara ihakikishe Kanuni ya Uhifadhi wa Uvuvi Baharini inafuatwa kwa

kuwapatia Kamati za Wavuvi asilimia 30 ya mapato yanayotokana na hifadhi zao.

9. Idara ya Uvuvi ipatiwe fedha nyengine za kuanzisha maeneo tengefu ya uhifadhi

wa matumbawe.

10. Idara ya Uvuvi iandike miradi ya kukabiliana na changamoto za tabia nchi na

kuziwasilisha kwa washirika wa maendeleo.

11. Wizara ihakikishe inawapa taaluma wavuvi ya jinsi gani wataweza kutengeneza

matumbawe bandia na kuyatumia katika kuhifadhi bahari inayowazunguka.

3.16 UFUGAJI WA PWEZA

Katika hatua za kusimamia uvuvi na wavuvi wetu, kamati ilifika kijiji cha Mtende

kuonana na Wananchi waliokubaliana kufunga pweza ili kuongeza faida katika zao hilo.

Utaratibu huo umeanza mwaka 2017 na hadi kamati inatembelea eneo hilo tayari

walikuwa wameshafunga na kufungua uvunaji wa pweza kwa vipindi viwili ambapo

kipindi kimoja kinachukua miezi mitatu.

Wafugaji wa pweza huzalisha takriban tani nne kwa siku ya mwanzo ya bamvua na

hupungua kidogo kwa siku zinazofuatia. Kiwango hicho ni kikubwa lakini hakiwapatii

manufaa makubwa wazalishaji kutokana na kutokuwa na viwanda vya kusarifu pweza

nchini. Matokeo yake ni kuongezeka kwa wafanyabiashara wa pweza ambao hununua

bidhaa hiyo na kupeleka nchi jirani zenye viwanda.

Kamati imesikitishwa na baadhi ya wananchi wa maeneo hayo waliodai kuwa ufungaji

wa pweza unaongeza ukali wa maisha kwa vile hukosha shughuli ya kufanya katika

kipindi wanachofunga pweza kutokana na kutokuwa na shughuli mbadala ya

kuendeshea maisha yao kwa kipindi hicho. Hivyo, Kamati inawasihi wananchi wa

maeneo hayo kutafuta shughuli nyengine za kiuchumi kama ukulima wa mazao ya

chakula na biashara ili kunyanyua kipato chao.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 39

CHANGAMOTO

1. Kuvamiwa kwa eneo lililofungwa na wavuvi wa vijiji vya karibu hususan siku

wanayofungua uvunaji.

2. Kukosekana ulinzi madhubuti katika eneo lililofungwa (bwachi).

3. Kukosekana kwa boti za doria katika eneo hilo ambapo wavamizi hushindwa

kukamatwa.

4. Baadhi ya wavuvi wanaovamia eneo hilo huvua kwa kutumia njia zisizokubalika

na kuharibu bahari na rasilimali zilizomo.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Wizara ihakikishe inaanzisha maeneo mengine ya kufungwa kwa ajili ya kufuga

pweza.

2. Idara ya Uvuvi iwahamasishe wavuvi na wananchi wanaoishi katika maeneo hayo

kuweka ulinzi ikiwa ni pamoja na kuwapatia vitendea kazi.

3. Wizara ihakikishe inawapatia boti ya doria wavuvi wa eneo hilo.

4. Wizara kupitia Idara ya Uvuvi ihakikishe inawahamasisha na kuwaelimisha wavuvi

kuhusu athari za uvuvi haramu kwa maliasili za bahari kwa maslahi yetu na vizazi

vijavyo.

3.17 UKULIMA WA MWANI

Mwani ni zao la biashara lililoanza kuzalishwa nchini mwetu mwanzoni mwa miaka ya

tisini. Kilimo cha mwani kimeajiri asilimia kubwa ya akina mama wa vijiji vya ukanda wa

Kusini Unguja na sehemu mbalimbali nchini. Awali, wakulima hao walijishughulisha na

harakati za kilimo cha choroko, uvumbikaji wa makumbi kwa ajili ya kutengeneza

kamba, uanikaji wa dagaa na kujipatia riziki zao. Kamati ilipata fursa ya kukutana na

wakulima wa mwani wa ukanda wa kusini na kufahamishwa namna wanavyoendesha

shughuli zao. Changamoto kubwa iliyopo Zanzibar na Duniani kiujumla ni mabadiliko ya

tabia nchi ambayo huwafanya wakulima wa mwani kusogea mbele zaidi baharini

(kwenye maji mengi) kuendesha shughuli zao. Hatua hiyo imewaweka katika wakati

mgumu kutokana na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji.

Kuna aina mbili kuu za mwani ambazo wakulima wetu wamezoea kuzilima hapa

Zanzibar za Cottonee na Spinosum. Mwani wa aina hiyo huwa hauna soko kubwa

ulimwenguni lakini kuna mwani wa Agar glacelaria ambao unalimwa sana Indonesia

ndio wenye soko duniani. Mwani wa aina hiyo haupo sana hapa kwetu visiwani lakini

Wizara ya Kilimo imo katika utafiti wa kuangalia wapi unaweza ukalimwa pamoja na

kutafuta wawekezaji kuwekeza katika eneo hilo. Pamoja na Wizara kuendelea na utafiti,

kuna taarifa kwamba mwani wa aina hiyo umeonekana maeneo ya bahari ya Fumba na

baadhi ya sehemu za Pemba.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 40

Kisiwa cha Fundo kina wakulima wengi wa mwani mnene wanaolima kwa kiwango

kikubwa. Lakushangaza ni kwamba, hadi leo wakulima hao hawajaendelezwa na

kupelekea kushindwa kuzalisha ipasavyo mwani katika msimu uliopita mara baada ya

kukumbwa na upepo mkali uliosababisha mwani kukatika na kupotea baharini.

Kufuatia ziara ya Mheshimiwa Rais nchini Indonesia, matunda yake yameanza kuonekana

kwani Wizara ya Biashara na Viwanda imo kwenye hatua za mwisho za maandalizi ya

ujenzi wa kiwanda cha kusarifu mwani Zanzibar na hivi karibuni Serikali ya Mapinduzi

Zanzibar inategemewa kutia saini makubaliano ya ujenzi huo kati yake na Kampuni

kutoka Indonesia. Kamati inaamini kwamba kuwepo kwa kiwanda hicho kutainua soko

la zao hilo, kuimarisha maisha ya wakulima wetu pamoja na kuiongezea mapato Serikali

yetu.

CHANGAMOTO

1. Bei ndogo ya mwani ambayo hailingani kabisa na uzito wa kazi yenyewe na ukali

wa maisha unaowakabili wakulima.

2. Upungufu mkubwa wa vifaa unaopelekea baadhi ya wakulima kukopa vifaa hivyo

vikiwemo kamba za kufungia mwani bahari na mitaimbo ya kutobolea miamba.

3. Ukosefu wa vyombo vya kupakilia mwani (vihori) kwa ajili kubebea mwani

kutoka baharini kuja nao nchi kavu.

4. Kilimo cha mwani kimekumbwa na wadudu waharibifu ambao huathiri mwani na

kupelekea upungufu wa mapato kwa wakulima.

5. Uhaba wa maeneo ya kuendeshea shughuli za mwani kutokana na kujengwa kwa

mahoteli katika fukwe ambazo wakulima wa mwani walizitumia kwa ajili ya

kuanikia mwani. Hii inatokana na ukweli kwamba ujenzi wa Mahoteli

haujazingatia mpango wa ujenzi wa kuacha mita thelathini kutoka ufukwe wa

bahari.

6. Ushiriki mdogo wa vijana kwenye kilimo cha mwani unaotokana na mapato

yasiyoridhisha kwa wakulima na kushawishika zaidi kuingia kwenye sekta ya

utalii.

7. Bado boti za kubebea mwani hazijananunuliwa wala hazijapangiwa fungu lake

kama ilivyoelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwamba kutanunuliwa

boti 500.

8. Kufanyiwa hadaa na baadhi ya masheha kwa kuwalazimisha kutoa kodi

iliyokuwa haina utaratibu unaoeleweka wanapomaliza mavuno ya mwani na

kuusafirisha kwa gari.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 41

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kutokana na kilio kikubwa cha wakulima wa mwani nchini, Kamati inaiomba

Serikali kuu kupitia Wizara ya Kilimo na Wizara ya Biashara kuandaa utaratibu

maalum wa kusimamia uzalishaji, ununuzi na uuzaji wa zao la mwani kwa njia

zitakazowanufaisha wakulima kama lilivyo zao la karafuu.

2. Wizara iendelee kufanya tafiti ili kujua aina za mwani zinazostawi nchini mwetu

na zinazoweza kuzalishwa kwa kiwango kikubwa na wakulima wetu.

3. Kamati inaishauri Wizara ya kilimo na Wizara ya Biashara kujenga viwanda vya

mwani ili kuongeza thamani ya zao hilo na kuwapatia tija wananchi.

4. Kamati inaiomba Wizara kuwashirikisha wakulima wa mwani na wananchi wa

maeneo ya uwekezaji kwenye vikao vya maamuzi vinavyofanywa baina yake na

wawekezaji ili kuwa na makubaliano ya pamoja kwa maslahi ya pande zote.

5. Kamati inaishauri Wizara kuwahamasisha wakulima wa mwani kuanzisha biashara

nyengine kupitia vikundi vyao ili kujikwamua na hali ngumu ya maisha,

6. Kamati inaiomba Serikali kuongeza fungu la bajeti kwa Idara ya Maendeleo ya

Uvuvi na Mazao ya Baharini ili iweze kujinunulia vifaa na madawa ya kuwapatia

wakulima kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mwani wa kiwango na ubora

unaokubalika.

7. Kamati inapendekeza kwamba kiwanda cha mwani kijengwe kusini Unguja kwani

ndio sehemu yenye wakulima wengi na uzalishaji mkubwa wa mwani.

8. Wizara iwaandae wakulima wa mwani kwa kuwatengenezea mazingira bora ya

kulima mwani wa kisasa ili waweze kukidhi mahitaji ya kiwanda

kitakachojengwa.

3.18 SOKO LA SAMAKI NA MBOGA MBOGA - TUMBE

Soko la Samaki na mboga mboga - Tumbe lilianza kujengwa mwaka 2011 chini ya

ufadhili wa MACEMP (kupitia Kampuni ya ujenzi ya Ngogo iliyopo Iringa Tanzania Bara)

kwa gharama ya Shilingi 1,074,881,077 na kufunguliwa rasmi na Mheshimiwa Rais wa

Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein mwaka 2015.

Kwa bahati mbaya, baada ya kutumika kwa miezi miwili soko hilo likakumbwa na

migogoro kadhaa kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni na Wavuvi wa maeneo

hayo iliyochangiwa zaidi na itikadi za kisiasa. Hadi kufikia 2017, Soko likaanza tena

kutumika likiwa chini ya usimamizi wa Kamati ya Maendeleo ya Uvuvi, Halmashauri ya

Wilaya ya Micheweni na Kamati ya Soko.

Kamati ilitembelea Soko hilo mwezi wa Agosti, 2018 na kukuta changamoto nyingi

zinazolikabili ikiwa ni pamoja na kutoingizwa ndani ya soko mashine ya kuzalishia baridi

ya kuhifadhia Samaki kwa takriban miaka minane. Hali hiyo ilisababishwa na mlango wa

kupitishia kuwa mdogo ukilinganisha na mashine husika. Vile vile kulikuwa na tatizo la

kutoingia vizuri hewa safi ndani ya soko kutokana na kuwepo madirisha na bati

lisilopitisha mwangaza, ukosefu wa sehemu kubwa ya kuuzia samaki (Mnada) kwani

eneo lipo la kutosha lakini bado halijatengenezwa na kuwekwa sawa. Pia soko lilikuwa

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 42

na ukosefu wa maji kutokana na kuondolewa huduma hiyo na ZAWA kwa madai ya

kushindwa kufanya malipo.

Kamati inampongeza Afisa Mdhamini wa Wizara ya Kilimo kwa kuisimamia Idara ya

Maendeleo ya Uvuvi na kutekeleza ushauri wa Kamati kivitendo kwa kukamilisha zoezi

zima la kuweka ndani mashine ya barafu na kuuza barafu hiyo kwa wavuvi.

CHANGAMOTO

1. Ukosefu wa mikopo kwa wavuvi itakayowasaidia kununua mashine za boti na

kuongeza kipato katika uvuvi wao.

2. Kukosekana kwa mshauri wa matumizi bora ya soko hilo, vyanzo vya mapato na

ugawaji wake.

3. Uwezekano wa kumudu kuihudumia mashine kubwa ya kuzalisha barafu. Pamoja

na kuwepo mafundi kutoka Tanzania Bara wanaoiendesha mashine hiyo kwasasa,

mahitaji ya kuwepo wataalamu wazalendo ni lazima. Kwa vile mashine ni kubwa

sana na ya pekee kwa Zanzibar ambayo inahitaji fedha na uangalifu wa hali ya

juu.

4. Mahitaji makubwa ya fedha kulipia umeme kwani mashine inatumia “unit” 15

kwa saa moja.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO WA KAMATI

1. Wizara ya Kilimo ihakikishe inawapatia utaalamu wafanyakazi watakaoendesha

mashine ya kuzalishia barafu na ubaridi wa kuhifadhia Samaki.

2. Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni

ihakikishe inaweka utaratibu mzuri wa kulipa gharama za matengenezo pamoja na

umeme wa mashine ya barafu.

3. Kamati inaiagiza Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya

Micheweni itafute chombo maalum cha uokozi kwa wavuvi watakaopata ajali

baharini.

4. Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Afisi ya Halmashauri ya Wilaya ya

Micheweni iandae utaratibu wa kuwapatia mikopo wavuvi itakayowasaidia

kununua mashine za boti na kuongeza kipato katika uvuvi wao.

5. Kamati inaishauri Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya

Micheweni kutafuta mtaalamu wa kuwashauri juu ya matumizi bora ya soko hilo,

vyanzo vyake vya mapato na ugawaji wake.

6. Kamati inazitaka Kamati za uvuvi nchini kuunganisha nguvu zao na kutatua

changamoto zinazowakabili wavuvi wote kwa ujumla.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 43

7. Ili kuendeleza masoko nchini, Kamati inawataka madalali kuwa waadilifu na

kuhakikisha fedha zinaingia kwenye mfuko wa soko kama zilivyopangwa na

kutumika kwa ajili ya utoaji huduma za soko.

8. Kamati inashauri Serikali za Wilaya kusimamia vyema taratibu za uendeshaji wa

masoko nchini.

3.19 WAKALA WA SERIKALI WA HUDUMA ZA MATREKTA NA ZANA ZA KILIMO

Serikali ya awamu ya kwanza chini ya Uongozi wa Marehemu Mzee Abeid Aman

Karume, iliweka azma ya kukiendeleza kilimo kwa kutumia Matrekta kwa lengo la

kuwaondoshea njaa wananchi wake kwa kuwaandalia mazingira mazuri ya uhakika wa

chakula na lishe bora, kuwapunguzia umasikini na kuongeza pato la mtu mmoja mmoja

na Taifa kwa ujumla na kufikia nchi yenye uchumi wa kati. Kulipa nguvu suala hilo,

ilinunua matrekta hamsini ya awali. Mwaka 1966, Karakana ya Matrekta iliundwa

Mbweni na mwaka 2017, Wakala wa Serikali wa Huduma za Matrekta na Zana za

Kilimo kupitia Hati iliyosainiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la

Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein iliundwa ikiwa pamoja na mengine

inatekeleza azma ile ile ya Rais wa Kwanza ya kukiendeleza kilimo cha Matrekta

Zanzibar.

Wakala una wafanyakazi 127 (Unguja 96 na Pemba 31) wengi wao wapo katika hatua ya

kukaribia kustaafu. Wakala una matrekta 74 (Unguja 47 na Pemba 27) ya aina ya ”New

Holland, Mahindra & Mahindra na Massey Ferguson ambapo matrekta 34 ni mazima na

yanaendelea kufanya kazi vizuri (Unguja 24 na Pemba 10), matrekta 27 mabovu lakini

yanaweza kutengenezeka (Unguja 18 na Pemba 9) wakati matrekta 13 mabovu wala

hayawezi kutengenezeka (Unguja 5 na Pemba 8).

Lengo kuu la Wakala ni kutoa huduma bora za matrekta kwa Wakulima wetu kwa

kununua vipuri kwa ajili ya kuyafanyia matengenezo matrekta mabovu ambayo

yanaweza kutengenezeka. Tokea Wakala uanzishwe ulikuwa unaongozwa na Tangazo la

Kisheria ”Legal Notice” ambapo ulipelekea kukabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo

upungufu wa fedha, vifaa na vitendea kazi pamoja na upungufu mkubwa wa

wafanyakazi, Ili kupunguza na ikibidi kuondosha baadhi ya changamoto, kwa

kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Wizara ya Kilimo tayari imekamilisha

Mswada wa kuanzisha Wakala wa Serikali wa Huduma za Matrekta na Zana za Kilimo

(Government Agency for Tractors and Farm Machineries Services) 2018 na katika

mkutano huu utasomwa kwa mara ya pili.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 44

CHANGAMOTO

1. Ufinyu wa bajeti unaoukabili wakala husababisha ucheleweshaji wa utoaji wa

huduma kwa wakati, kwa ufanisi na kwa utaratibu unaokubalika.

2. Wafanyakazi wengi wa Wakala wanakaribia umri wa kustaafu na utalaamu wao

hauendani na mahitaji ya sasa.

3. Uchakavu wa vifaa, mashine, vitendea kazi na miundombinu ya majengo na

maeneo ya kutendea kazi ya Wakala unapelekea kuwa na gharama kubwa za

uendeshaji.

4. Kuchelewa kulimiwa na kuburugiwa kwa wakulima wa mpunga

kunakosababishwa zaidi na kuchelewa kufanyiwa matengenezo matrekta kabla ya

msimu kuanza.

5. Kutotumika ipasavyo kwa baadhi ya mashine (Mashine ya kuchongea) kwa vile

siku hizi watu huwa hawachongi vifaa vya gari zao isipokuwa huwa wananunua

vilivyotumika (Used items).

6. Ukosefu wa zana za kisasa za kilimo kwa wakulima wetu jambo ambalo

limepelekea kushuka kwa kiwango cha uzalishaji wa mazao ya kilimo.

7. Baadhi ya vifaa vya kuonea na kuchomea “welding” vimeharibika na kuathiri

utendaji na afya za wafanyakazi.

8. Karakana haina usafi wa kutosha kwani baadhi ya sehemu zimezongwa na

mabuibui.

9. Mwamko mdogo wa wananchi kuhusu kuchangia huduma za trekta za shilingi

30,000 kwa kulima na shilingi 30,000 kwa kuburuga.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kutokana na umuhimu wa Wakala huu, Kamati inaishauri Serikali kuipatia fungu

lake la fedha.

2. Kwa kushirikiana na Bodi ya Wakurugenzi, Wizara iwasilishe maombi ya ajira za

wafanyakazi wapya Serikalini ili kufanya kazi za wakala kwa ufanisi.

3. Kamati inautaka Wakala uhakikishe unavifanyia matengenezo vifaa chakavu,

mashine pamoja na miundombinu ya majengo.

4. Wizara ihakikishe inatangaza zabuni ya ununuzi wa vipuri vya matrekta mapema

iwezekanavyo ili matrekta yawahi kutengenezwa na wananchi wawahi kulimiwa

na kuburugiwa maeneo yao kwa wakati unaotakiwa.

5. Wakala wa Matrekta Pemba ihakikishe inachukua juhudi ya kusafisha na kuondoa

taka zote zilizopo katika Karakana ya wawi.

6. Wizara ihakikishe Matrekta mabovu yanatengenezwa haraka ili yawahi

kuwatumikia wananchi bila ya kuchelewa muda wa kuchimbua na kuburuga

maeneo ya wananchi.

7. Wizara ihakikishe inaipatia Wakala zana za kisasa za kufanyia kazi.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 45

8. Wizara kupitia Wakala wa Matrekta iwahamasishe wananchi kuhusu kuchangia

huduma za malipo ya trekta.

9. Kamati inautaka Wakala kuihimiza Kampuni ya “Luma international Ltd.”

iliyoshinda zabuni ya kununua vifaa vya mategenezo vya Wakala kuviwasilisha

kabla ya wakati wa kulima kumalizika.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 46

4. WIZARA YA BIASHARA NA VIWANDA

Katika awamu hii ya ushajiishaji maendeleo kupitia uchumi wa viwanda Tanzania na

Zanzibar kwa ujumla, Wizara ya Biashara na Viwanda imebeba mzigo huo kuhakikisha

inapanga mipango madhubuti itakayowesha upatikanaji wa Viwanda hususan

vinavyoendana na maumbile na mazingira ya kisiwa chetu. Ili kufanikisha hilo, Wizara

imeandaa Programu Kuu nne zifuatazo kwa lengo la kututoa hapa tulipo na kuelekea

katika uchumi wa kati unaotegemea zaidi viwanda.

a) Programu kuu ya Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya Biashara na Viwanda;

b) Programu kuu ya Maendeleo ya Viwanda na Ujasiriamali;

c) Programu kuu ya Ukuzaji na Uendelezaji wa Biashara;

d) Programu kuu ya Viwango na Tathmini ya Ubora;

Programu hizo zinatekelezwa na Wizara ya Biashara na Viwanda kupitia Taasisi au Idara

zifuatazo:

i. Idara ya Mipango, Sera na Utafiti;

ii. Idara ya Uendeshaji na Utumishi;

iii. Idara ya Biashara na Ukuzaji Masoko;

iv. Idara ya Maendeleo ya Viwanda na Ukuzaji Ujasiriamali;

v. Shirika la Biashara la Taifa (ZSTC);

vi. Baraza la Kusimamia Mfumo wa Utoaji Leseni (BLRC);

vii. Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS);

viii. Baraza la Taifa la Biashara Zanzibar;

ix. Tume ya Ushindani Halali wa Biashara na Kumlinda Mtumiaji (FCC);

x. Wakala wa Maendeleo ya Viwanda Vidogo Vidogo, Vidogo na vya Kati

(SMIDA);

xi. Wakala wa Usajili wa Biashara na Mali Zanzibar (PBRA); na

xii. Afisi Kuu - Pemba.

4.1 UTEKELEZAJI WA PROGRAMU KUU ZA WIZARA

Kwa mwaka wa fedha 2018/2019, Wizara ya Biashara na Viwanda iliidhinishiwa

matumizi ya jumla ya shilingi 11,363.8 milioni ambapo kwa kipindi cha Julai hadi

Disemba jumla ya shilingi 3544.22 milioni ziliingizwa na kutumika. Kwa upande wa

mapato, jumla ya shilingi 1,513.061 milioni zilikadiriwa kukusanywa na Wizara kwa

mwaka wa fedha 2018/2019.

4.2 PROGRAMU KUU YA MAENDELEO YA VIWANDA NA UJASIRIAMALI

Programu hiyo imekusudia kuongeza pato la sekta ya uzalishaji viwandani pamoja na

kuimarisha mazingira mazuri ya maendeleo ya Wajasiriamali wadogo na wakati.

Utekelezaji wa Programu hiyo unafanywa na Idara ya Viwanda na Wakala wa

Maendeleo ya Viwanda Vidogo Vidogo, Vidogo na vya Kati (SMIDA). Miongoni mwa

mambo ambayo yametekelezwa na Programu hiyo na Kamati kuyatolea ushauri ni:

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 47

4.3 KIWANDA CHA KUSARIFU TUNGULE

Hichi ni kiwanda cha wajasiriamali kinachomilikiwa na kikundi cha “Gando

Enterpreneurship Program (GEP)” chenye wanachama 948 waliopo katika maeneo

tofauti kisiwani Pemba. Kikundi hichi kilianza mwaka 2012 kwa uendelezaji wa shughuli

za kilimo zilizolenga kuwatoa wajasiriamali kwenye kilimo cha matumizi ya nyumbani na

kuanzisha kilimo cha biashara. Hadi Kamati ilipowatembelea, jumla ya vikundi 55

vimeendelezwa chini ya mwamvuliwa wa GEP. Bidhaa wanazozalisha ni pamoja na

tomato, chili “sauce”, jamu, sabuni za maji, “lotion” na mafuta ya mgando. Kikundi

kimefanikiwa kupata mashine za kusarifu tungule kupitia mradi wa MIVARF ambapo

walichangia asilimia 25 na Mradi kutoa asilimia 75 zilizobakia. Kikundi hicho kina

mpango wa kujenga chumba cha kuhifadhia tungule ili ziweze kukaa kwa muda mrefu

bila ya kuharibika.

Kuwepo kwa GEP kumepelekea kupatikana umoja wa wajasiriamali wadogo, kuinua

pato la mwananchi mmoja mmoja, kuzalisha fikra za pamoja kati ya wajasiriamali na

kuwaweka pamoja wajasiriamali na taasisi mbalimbali za Serikali kama ZBS na Wizara ya

Biashara na Viwanda. Kutokana na jitihada zilizooneshwa na wajasiriamali hao, kuna

umuhimu mkubwa kwa Wizara ya Biashara na Viwanda kuwasaidia hata kwa kuwapatia

mikopo kwani uwezo wa kulipa wanao. Ni busara kwa Serikali kurahisisha upatikanaji

wa vifungashio nchini ili kupunguza gharama za usafiri na ushuru. Hatua hio ni muhimu

katika kuwajengea uwezo Wajasiriamali wadogo kuzalisha kwa gharama nafuu na hivyo

kuwawezesha kumudu ushindani wa biashara uliopo sokoni.

CHANGAMOTO

1. Upungufu wa mtaji hususan wa uendeshaji wa kiwanda cha kusarifu tungule.

Mara kadhaa kikundi hicho hukosa fedha hata za kununulia malighafi (tungule).

2. Ukosefu wa jengo la kisasa litakalowawezesha kufikia kiwango cha kiwanda

kinachostahiki kuzalisha bidhaa mbalimbali zikiwemo za chakula.

3. Kutokamilika matengenezo chumba cha baridi (coldroom) kunapelekea uzalishaji

wa bidhaa zao kusita mara tu msimu wa tungule unapomalizika.

4. Kiwanda kinakabiliwa na ushindani wa kibiashara na wazalishaji wakubwa.

5. Kukabiliwa na gharama kubwa za ununuzi vifungashio kutoka Tanzania Bara au

Nairobi.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Kamati inaiomba Serikali iandae mkakati maalum wa kuwapatia vifungashio hivyo

nchini ili angalau wapunguze gharama za usafirishaji.

2. Kamati inaitaka Wizara ya Biashara na Viwanda kwa kushirikiana na taasisi

nyengine za Serikali na wadau binafsi wawe wabunifu wa kutafuta mwendelezo

wa mradi (project sustainability) ili kuyaendeleza yale mazuri yanayoanzishwa na

mradi husika.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 48

3. Kikundi kichukue juhudi za kujitangaza ili kiweze kutambulika na kupata soko la

bidhaa kinazozalisha.

4.4 KIWANDA CHA SUKARI CHA MAHONDA

Kiwanda cha sukari cha Mahonda kilianzishwa miaka ya 1960 chini ya usimamizi wa

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. Kwa kipindi

cha takriban miaka 15 kiwanda kilikuwa hakifanyi kazi. Mwaka 2015, kiwanda hicho

kilitengenezwa kwa kuwekwa mashine mpya na za kisasa zilizopelekea uzalishaji

kuongezeka hadi kufikia tani 400 kwa mwezi ambazo zilizokuwa zikiongezeka maradufu

siku hadi siku na kufikia tani 800. Kiwanda kina uwezo wa kuzalisha hadi tani 1,250

kutegemeana na upatikanaji wa malighafi. Katika kutekeleza azma ya Serikali ya

kukifufua kiwanda hicho, Serikali iliahidi kukipatia kiwanda ardhi ya kutosha ya hekta

6,644 kwa ajili ya kuzalisha malighafi ya miwa pamoja na kuhakikisha soko la sukari

itakayozalishwa linapatikana.

Baada ya kumaliza matengenezo na kuanza kazi, kiwanda kilikabiliwa na changamoto

kubwa ya kuwepo tani nyingi za sukari kiwandani pasi na kupata soko. Serikali ilikuja na

maamuzi ya busara ya kuzuia uvamizi usiokuwa na tija katika biashara ya Sukari kwa

kuchagua wafanyabiashara sita wakubwa Zanzibar waliopewa kibali cha kuleta Sukari

Zanzibar. Matokeo yake takriban tani 6,000 zilizokuwepo, tani 5,600 zimeshanunuliwa

na kubakia tani 400 kwa sasa. Miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana kwamba Serikali

imepata kodi ya zaidi ya shilingi 1.3 milioni na kuajiri Wazanzibari zaidi ya 800 kwa ajira

ya moja kwa moja na ajira isiyokuwa ya moja kwa moja kiwandani.

CHANGAMOTO

1. Kiwanda kutopatiwa ardhi ya kutosha kama ilivyoahidiwa na Serikali.

2. Kuyumba kwa soko la sukari kwani kuna tani 400 kwasasa zimebakia ghalani.

3. Bado kuna wafanya biashara wanakwepa kununua sukari katika kiwanda hicho.

4. Nyumba ambazo Kiwanda imepewa na Serikali zilikuwa mbovu na haziko katika

hali nzuri. Baadhi ya nyumba hizo milango ilikuwa ishatolewa.

5. Kiwanda hakijakabidhiwa nyumba zake ambazo Serikali iliamua wakabidhiwe

lakini baadhi ya nyumba hizo bado zinakaliwa na watu wengine.

6. Uelewa mdogo wa Wakulima wanaoshughulikia ukataji miwa katika mashamba

ya Kiwanda.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 49

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Wizara ihakikishe inakipatia Kiwanda ardhi ya kutosha kama ilivyoahidiwa na

Serikali.

2. Wizara ihakikishe inaipatia soko sukari inayozalishwa Mahonda kwani mpaka

Kamati inatembelea kiwanda hicho kuna tani 400 zilikuwa zimebakia ghalani.

3. Wizara iwapatie Wakulima wa miwa elimu ya msingi itakayowawezesha

kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kupelekea kupata mavuno bora kwa

maslahi yao, kiwanda na Taifa kwa ujumla.

4.5 ZIARA YA KAMATI KATIKA VIWANDA VYA KUSAGA UNGA, KUCHAKATA NA

KUTENGENEZA JUISI YA EMBE - MKURANGA NA MWANDEGE.

Kamati ya fedha, Biashara na Kilimo ilipata fursa ya kutembelea viwanda tofauti

vinavyosimamiwa na “Bakhresa Group of Companies”, vikiwemo Kiwanda cha unga

kilichopo Mtoni Unguja kilichoanzishwa mwaka 1990 na kufufuliwa upya mwaka 2010,

Kiwanda cha kuzalisha unga kilichopo Buguruni (TAZARA) kilianzishwa mwaka 1983 na

viwanda vya kuchakata na kutengeneza juisi ya embe viliopo Mkuranga Mwandege na

Vingunguti. Lengo la ziara hiyo ni kuongeza uelewa juu ya uzalishaji wa viwanda vyetu

vya ndani kuelekea kwenye uchumi wa viwanda. Kamati inaamini kwamba kujifunza

kwa kuona itajenga uwezo wa kuchukua mazuri yaliyojitokeza, changamoto

wanazokabiliana nazo na njia wanazitumia kukabiliana na changamoto hizo ili waweze

kuishauri Wizara husika njia bora za kuendeleza viwanda nchini kwa maslahi ya Taifa

letu.

Kamati imeelezwa kuwa viwanda vyote vya Kampuni ya Bakhresa viliopo Kipawa,

Mzizima, Buguruni na Zanzibar vinauwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 3,000 za unga kwa

siku ambavyo vimetoa ajira kwa Watanzania wengi na kupunguza mzigo wa upungufu

wa ajira nchini.

Kwa upande wa viwanda vya kuchakata na kutengeneza juisi ya embe hutumia embe

aina ya Dodo, Boribo na Viringe kutengenezea juisi. Embe hizi hupatikana kwa wingi

Bagamoyo, Mtwara, Lindi, Rufiji, Dodoma, Tabora, Tanga na Moshi. Kiwanda

kinashindwa kuchukua embe kutoka Zanzibar kwa sababu huwa zina wadudu wengi

jambo ambalo linaweza kuhatarisha usalama wa bidhaa wanayoitengeneza pamoja na

watumiaji bidhaa hiyo. Baadhi ya wakati watendaji wa kampuni huwatembelea

wakulima na kuwapatia mbegu na utaalamu utakaowasaidia kulima kwa ufanisi na

kupata mavuno bora.

Kiwanda cha Bakhresa kilichopo Maruhubi ni miongoni mwa viwanda vya mwanzo vya

Bakhresa kilichokuwa kikizalisha mtindi na samli. Mwaka 1990, kiwanda hicho kilifungwa

kwa ajili ya kufanyiwa matengenezo na mwaka 2010 kilifunguliwa upya na kujikita na

uzalishaji wa unga wa ngano pekee. Kiwanda hicho kimeajiri wafanyakazi 125 hadi 130

na kinauwezo wa kuzalisha tani 1,020 kwa siku.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 50

CHANGAMOTO

1. Kutokana na udogo wa Bandari yetu, meli kubwa za mizigo hushindwa kufika

nchini na kusababisha Serikali kukosa mapato tuliyojipangia.

2. Kuwepo kwa utitiri wa kodi wanazolipa wafanyabiashara na wawekezaji nchini.

Kuna takriban kodi tisa wanazolipa wafanyabiashara hao zikiwemo ZRB, TRA,

ZFDA, ZBS, Mkemia Mkuu, Ofisi ya ‘Atomic Energy’, ZIPA, Kamisheni ya Kazi

pamoja na Manispaa. Ni jambo la kushangaza kwamba baadhi ya kodi hizo

zinaingiliana na kuwapa wakati mgumu wawekezaji nchini.

3. Matumizi mabaya ya msamaha wa kodi unaotolewa na Serikali kwa bidhaa

muhimu za chakula kwa kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Wafanyabiashara wengi huitumia fursa hii kuingiza bidhaa hizo kwa wingi na

kuuza kwa bei ya kawaida mara tu baada ya kumalizika mwezi huo. Kitendo

hicho huwapatia faida kubwa wafanyabiashara hao na kuwapa changamoto

kubwa wazalishaji wa ndani.

4. Ukosefu wa wafanyakazi kutoka Zanzibar katika baadhi ya fani ikiwemo fani ya

ufundi wa mfumo wa umeme katika mashine na kupelekea kiwanda kuchukua

wataalamu kutoka nje ya Zanzibar, hali hiyo huwaongezea gharama za uzalishaji.

5. Kukatika umeme mara kwa mara bila ya taarifa kunawasababishia usumbufu wa

kuzianzisha upya mashine.

6. Kutokupewa virutubisho vya unga kutoka Serikalini.

7. Kuvamiwa kwa malori ya kiwanda na wakaazi wa maeneo ya karibu wakati wa

kuingiza ngano.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Ni vyema Wizara ya Biashara na Viwanda ikakaa na Wizara ya Elimu na Mafunzo

ya Amali kuangalia uwezekano wa kuwasomesha vijana wetu fani ya ufundi wa

mfumo wa umeme katika mashine ili waweze kumudu ushindani uliopo Afrika

Mashariki na kwengineko.

2. Wizara ya Biashara na Viwanda ianzishe utaratibu wa kuwapatia ruzuku ya

virutubisho wamiliki wa Viwanda vya unga.

3. Wizara ishirikiane na Taasisi za kodi ili waweze kuandaa utaratibu wa malipo ya

kodi katika Taasisi moja (one stop center). Hili litawapunguzia muda

wafanyabiashara na kukuza faida zao.

4. Wizara kwa kushirikiana na Taasisi za kodi iandae vipeperushi vitakavyotoa taarifa

za mabadiliko ya vielelezo anavyotakiwa mfanyabiashara aende navyo katika

Taasisi za Kodi wakati wa kuongeza muda leseni yake.

4.6 PROGRAMU KUU YA VIWANGO NA TATHMINI

Programu hiyo imekusudia kuandaa na kuimarisha viwango ili kumlinda mtumiaji.

Utekelezaji wa Programu hiyo unafanywa na Taasisi ya viwango Zanzbar. Miongoni

mwa mambo ambayo yametekelezwa na Programu hiyo na Kamati kuyatolea ushauri ni:

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 51

4.7 TAASISI YA VIWANGO ZBS PEMBA

Taasisi ya Viwango ni miongoni mwa vyombo muhimu Zanzibar vilivyoanzishwa kwa

lengo la kukagua na kudhibiti ubora wa vifaa na vyakula viliopo au vinavyoingizwa

Zanzibar kutoka nje. Chombo hicho kimeundwa na sheria Nambari 1 ya mwaka 2011.

Kwa upande wa Pemba, Taasisi hiyo ina Ofisi tatu (Mkoani, Chake chake na Wete)

pamoja na wafanyakazi watano ambapo wawili ndio wataalamu wa ukaguzi

wanaofanya kazi katika Bandari ya Wete na Mkoani.

Kamati imesikitishwa na uchache wa watendaji wa Taasisi hio kwa upande wa Pemba

ikizingatiwa kwamba wafanyakazi hao wanatakiwa kufanya kazi kwenye bandari zote za

Pemba bila ya kuwa na usafiri wa uhakika wa kuwafikisha kwenye maeneo yao ya kazi.

Hali hiyo hupelekea uwezekano wa kuingia bidhaa zisizokua na ubora kisiwani humo

hususan wakati wa usiku.

Kwa upande wa ZBS Wete, Taasisi imepewa sehemu ndani ya jengo la Shirika la Bandari

wakati ZBS Mkoani imepewa Ofisi katika jengo la ZTC ambalo linafanya kazi zake kwa

mujibu wa sheria. Kwa upande wa Chake chake wanayo Ofisi wanayoendelea kuifanyia

matengenezo itakayotumika kama Ofii kuu ya ZBS Pemba. Sambamba na ufinyu wa Afisi

za kufanyia kazi, ZBS inakabiliwa na uchache wa vifaa vya kufanyia ukaguzi ikiwemo

mtandao wa intaneti unaowawezesha kuwasiliana na Taasisi nyengine na viwango

duniani.

CHANGAMOTO

1. Ufahamu mbaya wa wananchi kuhusu majukumu ya ZBS yanagongana na ZFDA.

2. Ukosefu wa baadhi ya vifaa muhimu na vya msingi katika upimaji wa bidhaa

tofauti zikiwemo mafuta ya ‘service’ za gari, vifaa vya kupimia ubora wa mipira

ya gari, vifaa vya ujenzi pamoja na bidhaa za vyakula.

3. Kuwepo kwa baadhi ya bidhaa hadi leo zinatumia alama ya ubora ya sehemu

nyengine ikiwemo TBS ya Tanzania Bara wakati bidhaa hizo zinazalishwa na

kutumika Zanzibar.

4. Uhaba wa wafanyakazi na udogo wa Ofisi.

5. Ukosefu wa fedha za utekelezaji wa malengo yao kwani fedha wanayoiomba

huwa haipatikani kwa asilimia mia moja.

6. Gharama kubwa za upatikanaji wa nembo ya ubora ya ZBS kwa wajasiriamali.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. ZBS ihakikishe inatoa mafunzo kwa wananchi kuwaelewesha tofauti iliyopo na

mipaka yake kiutendaji na ZFDA kwani kidhahania wananchi wanaona Taasisi

hizo zinafanya kazi zinazofanana.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 52

2. Wizara ya Biashara na Viwanda kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango

ihakikishe inaipatia ZBS fedha za kutosha ili waweze kununua vifaa vya msingi

katika shughuli zao za ukaguzi na upimaji.

3. ZBS itoe taalum ya viwango vinavyoinishwa katika bidhaa tofauti ikiwemo saruji

ili iwaeleweshe wananchi pamoja na Waheshimiwa Wawakilishi matumizi sahihi

ya bidhaa hizo.

4. ZBS ipige marufuku bidhaa zinazozalishwa Zanzibar na kutumika Zanzibar

kutumia alama ya ubora isiyokuwa ZBS.

5. ZBS iwashauri wafanyabiashara kuwachukua maofisa wa wake kuwasaidia upimaji

au ukaguzi wa bidhaa hususan wanapoenda kununa ili kuepuka kununua bidhaa

isiyokidhi viwango na hatimae kuangamizwa au kurudishwa ilipotoka.

6. ZBS ifuatilie kwa karibu suala la ajira ya wafanyakazi wake wapya watatu na

kupeleka maombi mengine ya wafanyakazi kwa ajili ya Afisi ya Pemba.

4.8 PROGRAMU KUU YA UENDESHAJI NA URATIBU WA WIZARA

Programu hiyo imekusudia kutoa huduma za uendeshaji na manunuzi kwa ufanisi,

kufanya mapitio na kuoanisha sera za biashara, viwanda na kufanya utafiti pamoja na

kuratibu shughuli za Wizara Pemba. Utekelezaji wa Programu hiyo unafanywa na Idara

ya Mipango, Sera na Utafiti, Idara ya Uendeshaji na Utumishi na Afisi Kuu Pemba.

4.9 UONGOZI NA WATENDAJI WA WIZARA

Katika mwezi wa Agosti 2018, Kamati ilikutana na uongozi na watendaji wa Wizara na

kuarifiwa kwamba Wizara ya Biashara na Viwanda inao uwezo kwa mujibu wa sheria

kudhibiti bei ya baadhi ya bidhaa zikiwemo unga na sukari. Kwa nia njema, Wizara pia

hutoa msamaha wa kodi hususan katika mwezi Mtukufu wa Ramadhan kwa bidhaa ya

tende ili kuwapunguzia makali ya maisha wananchi wetu. Lakushangaza, msamaha huo

hutumika kama njia ya kuwanufaisha wafanyabiashara na familia zao. Kwa mantiki hiyo,

kuna haja kwa Wizara kuchukua maamuzi magumu ya kudhibiti vitendo hivyo kwa

kuzuia misamaha hiyo au kuruhusu baadhi ya wafanyabiashara chini ya usimamizi

maalum.

Hivi karibuni, wananchi wengi wameanza kujishughulisha na biashara ya dagaa na

kulisafirisha nchi jirani ili kijiongezea kipato. Kuwepo kwa shughuli hizo kumepunguza

kiwango cha utegemezi kwa kuajiri wananchi mbalimbali. Kamati imebaini kuwa

biashara ya dagaa ni yenye tija kubwa kwa wananchi wetu, lakini bado inakabiliwa na

tatizo la kukosa usimamizi wa vyombo vinavyohusika na kupelekea wajanja wachache

kufaidika zaidi kupitia nguvu za wananchi wetu. Hivyo, Kamati inaishauri Wizara

kuwapatia utaalamu wa njia bora za uanikaji wa dagaa vijana hao ili kuongeza thamani

na mapato yake.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 53

Wizara pia imesimamia uchumaji wa Karafuu na utoaji wa mikopo, ununuzi pamoja na

uuzaji wa Karafuu ndani na nje ya nchi yetu. Kwa mwaka 2017/18, jumla ya wachumaji

193 wameanguka katika mikarafuu ambapo 176 walianguka Pemba na waliobakia ni kwa

upande wa Unguja. Kati ya hao, wachumaji 152 tayari wameshalipwa fidia ambapo

jumla ya shilingi 106,530,000 zilitumika.

Kwa mwaka wa fedha 2017/18, jumla ya shilingi 191,000,000 milioni zilitolewa kwa

wachumaji Karafuu na hadi Kamati inatembelea Afisi ya Ofisa Mdhamini jumla ya shilingi

179,760,000 zililipwa sawa na asilimia 94 ya fedha zote na kubakia jumla ya shilingi

11,240,000 mikononi mwa wananchi ambao wengi wao walipata hasara kutokana na

mvua kubwa zilizowakabili hususan katika kipindi cha uvunaji. Pamoja na fedha nyingi

kupatikana kutokana na biashara ya karafuu lakini mzunguko wa fedha hizo ni mdogo

kwani hazionekani kuwekwa katika Benki zetu. Sambamba na hayo Kamati imeshauri

Wizara mambo yafuatayo:

CHANGAMOTO

1. Ukusanyaji mdogo wa mapato kupitia vyanzo vinavyosimamiwa na Wizara hii

ulikuwa chini kwa kipindi ambacho kamati ilipoitembelea.

2. Wakala wa Maendeleo ya Viwanda Vidogo Vidogo, Vidogo na vya Kati (SMIDA)

wamepatiwa fedha kidogo sana ukilinganisha na walichokiomba au mahitaji yao

kwani wameshindwa hata kuweka mazingira mazuri ya kufanyia kazi.

3. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ushindani wa kibiashara nchini jambo ambalo

linarudisha nyuma wafanyabiashara wadogo wadogo.

4. Ukosefu wa usimamizi bora wa biashara ya dagaa.

5. Bado kuna baadhi ya wafanya biashara hawajarudisha fedha walizokopeshwa na

ZSTC.

6. Uhaba wa wafanyakazi katika shamba la Mtakata.

7. Ukosefu wa hatimiliki ya shamba la Mtakata.

8. ZSTC bado wanawalipa wafanyabiashara za uvunaji karafuu kwa fedha taslim.

Utaratibu wa aina hiyo husababisha wizi kutokea.

9. Wafanyabiashara hawahifadhi fedha zao Benki na kusababisha mzunguko mdogo

wa fedha pamoja na kuhatarisha usalama wao kwa kuvamiwa na kuibiwa.

10. Kutolipwa fidia kwa baadhi ya wachumaji karafuu walioanguka katika mikarafuu

MAONI NA USHAURI WA KAMATI

1. Wizara iandae mikakati madhubuti kuhakikisha ukusanyaji wa mapato

unaongezeka.

2. Wizara ihakikishe SMIDA inapatiwa fedha kama walivyopanga ili iweze kufikia

lengo la uchumi wa viwanda Zanzibar.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 54

3. Kamati inaishauri Wizara kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wafanyabiashara

wote watakaobainika wanauza bidhaa zilizopitwa na wakati wa matumizi yake ili

kuwalinda wananchi wetu na madhara makubwa yanayoweza kuwapata.

4. Kamati inaishauri Wizara kuwaelimisha Wajasiriamali kujitangaza kwa kutumia

fursa za maonyesho yanayofanyika katika Maadhimisho ya Sherehe za Mapinduzi

ya Zanzibar za kila mwaka, siku ya Wakulima Sabasaba - Dar es Salaam na

yanayofanyika nje ya nchi.

5. Wizara iweke utaratibu mzuri wa uendeshaji wa biashara ya dagaa kwa upana

wake kwani inatoa ajira kwa wananchi wengi na ni biashara yenye tija.

6. Wizara ihakikishe inawalipa fidia wachumaji karafuu waliobakia ambao

walioanguka katika mikarafuu.

7. Wizara ichukue juhudi za makusudi kuhakikisha wafanyabiashara wa karafuu

wanafungua hesabu “account” Benki ya Watu wa Zanzibar.

8. Wizara kupitia ZSTC iwafuatilie wafanyabiashara ambao hawajarudisha fedha

walizokopeshwa kwa kuvuna karafuu.

9. Wizara ihakikishe hatimiliki ya shamba la Mtakata inapatikana.

10. Wizara ihakikishe wafanyakazi wa kutosha wanakuwepo katika shamba la

Mtakata.

4.10 JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA, WENYE VIWANDA NA WAKULIMA

(CHAMBERS OF COMMERCE)

Jumuiya ya Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Wakulima ni moja ya Jumuiya

isiyokuwa ya Serikali yenye mchango mkubwa katika uimarishaji wa uchumi wa Zanzibar

kwa vile ndio chombo kikuu kinachoweza kuwaunganisha wafanyabiashara na wakulima

na kuwakutanisha na Serikali yao kushauriana kuhusu mambo ya msingi yatakayofanyiwa

kazi na kuleta tija nchini. Pamoja na mambo mengine, Jumuiya hiyo kwa upande wa

Pemba inakabiliwa na changamoto kubwa zifuatazo:

CHANGAMOTO

1. Kuwepo mapungufu katika Jumuiya hiyo kwa kutokuwa na nafasi ya muwakilishi

kutoka upande wa Pemba.

2. Utitiri wa kodi kwa Wajasiriamali wadogo zinazowasababishia kutopata

maendeleo ya biashara.

3. Kukosekana kwa wafadhili wanaochangia fedha kwa ajili ya maendeleo ya

Jumuiya hiyo.

4. Ukosefu wa Viwanda vidogo vya kusarifu mazao yanayozalishwa Zanzibar ili

yaweze kuhifadhiwa na kutumika kwa muda mrefu zaidi.

5. Wakulima wa mboga na mwani kutopatiwa ruzuku kutoka Serikalini kwa ajili ya

kuendeleza shughuli zao.

6. Ukosefu wa Afisi kwa Jumuiya ya Wafanyabiashara Wenye Viwanda na Wakulima

Pemba.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 55

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Jumuiya ya Wafanyabiashara Wenye Viwanda na Wakulima Pemba ipatiwe fursa

ya kuwa na wawakilishi kutoka Pemba.

2. Katiba ya Jumuiya hiyo irekebishwe na kuwepo kufungu kitakachoeleza Pemba

kuwa ni zoni.

3. Wajasiriamali wapunguziwe kodi ili waweze kumudu gharama za uendeshaji wa

biashara zao.

4. Jumuiya ihakikihe inajipanga vyema katika utekelezaji wa majukumu yao na sio

kutegemea wafadhili.

5. ZBS iweke gharama toshelevu itakayowawezesha Wajasiriamali kupata alama ya

ubora wa ZBS.

6. Wizara ihakikishe inaimarisha sekta ya Viwanda kwa kujenga viwanda vidogo

vidogo ili wananchi wapate ajira na soko la kuuzia bidhaa wanazozizalisha.

7. kama ilivyo katika karafuu, wakulima wa Mwani na mboga nao wapatiwe ruzuku

au mikopo.

8. Kuna haja yakufanya utafiti utakaobainisha wazi sababu zinazopelekea kufa kwa

miche ya Mikarafuu iliokuwa imeatikwa kinyume na mabotea.

9. Jumuiya ipatiwe Ofisi yake kwa upande wa Pemba ili viongozi waweze kukutana

na kuyatafutia maamuzi changamoto zinazojitokeza.

4.11 JUMUIYA ZA WAFUGAJI WA NYUKI

Katika mwezi wa Novemba, 2018 Kamati ilizitembelea Jumuiya za wafugaji wa nyuki na

vikundi vya kufuga nyuki vilivyotokana na Jumuiya hizo Unguja na Pemba. Kwa upande

wa Unguja, Kamati ilitembelea Jumuiya ya Wafugaji nyuki Zanzibar “ZABA” yenye Ofisi

yake kitogani ambayo ina jumla ya wanachama 194 illiyounganisha wafugaji wa nyuki

1,046 wa Unguja. Lengo la Jumuiya hiyo ni kutoa taaluma kwa wafugaji nyuki kuhusu

ufugaji wakisasa, kuhamasisha uzalishaji wa asali bora inayomfikia mlaji kwa kusarifiwa

kwa mashine na bila ya kuguswa kwa mkono. Chini ya ufadhili wa Jumuiya

inayojitegemea ya MLFM & CARIPLO ya Italy, jumuiya hiyo imejenga Ofisi yake ya

kisasa na kupatiwa baadhi ya vifaa vikiwemo mashine ya kukamulia, kuchujia na

kihifadhia asali.

Kuwepo kwa Jumuiya hiyo kumesaidia kuzaliwa kwa vikundi tofauti vya ufugaji nyuki

ikiwemo kikundi cha ukulima wa nyuki kiliopo Paje kiitwacho “Paje Woman Bee

Farmer” (PAWOBEFA) kilichoanzishwa mwaka 2016.

Kamati pia ilifika katika Jumuiya ya Wafugaji wa nyuki Pemba (PEBA) iliyopo

Machomane Pemba ambayo ilianzishwa mwaka 2013 na kupata usajili wake rasmi

mwaka 2014 ikiwa na wajumbe waanzilishi 20 (wanaume 15 na wanawake 5). Kwasasa

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 56

Jumuiya ina wanachama 62 inayowaunganisha wafugaji nyuki wote waliopo Pemba

pamoja na kuwapatia mafunzo ya uendeshaji wa shughuli zao ikiwemo matumizi ya

miundombinu ya ufugaji wa nyuki wa kisasa ili waweze kupunguza umasikini na

kujiongezea kipato. Mwaka 2017, Jumuiya hiyo imekamilisha ujenzi wa Ofisi yak echini

ya ufadhili wa IFAD, kununua kompyuta moja, vifaa vya kisasa vya kutengenezea na

kupimia asali, nta pamoja na ununuzi wa nguo za kuvunia asali. Kwasasa Jumuiya inalo

soko la kutosha kwani wamepata mnunuzi anataka lita 5,000 za asali halisi. Licha ya

mafanikio hayo, Jumuiya inakabiliwa na changamoto zifuatazo:

CHANGAMOTO

1. Jumuiya hizo zina uhaba wa vitendea kazi ikiwemo pikipiki na gari za kufuatilia

wafugaji waliopo katika maeneo tofauti ya Unguja na Pemba, ‘rain boot’, na

masanduku ya kufugia nyunki.

2. kuwepo kwa wadudu waharibifu wanaoathiri asali kama vile sisimizi, siafu,

koyokoyo, uvi na mijusi, nondo kichwa, mbawa kavu na chawa wa nyuki.

3. Ukosefu wa elimu ya kutosha hususan kwa wanachama wao.

4. Uhaba wa rasilimali fedha.

5. Kuzuiliwa kwa masanduku na pikipiki za jumuiya na watendaji wa Wizara ya

Kilimo.

MAONI, USHAURI NA MAAGIZO YA KAMATI

1. Wizara kupitia SMIDA izisaidie Jumuiya hizo kwa kuwapatia mikopo

itakayowawezesha kukuza mtaji na kununulia baadhi ya vitendea kazi.

2. Wizara ya Biashara na Viwanda ikutane na Wizara ya Kilimo kulitafutia suluhisho

tatizo la kuzuiliwa kwa masanduku na pikipiki za Jumuiya hizo.

3. Wizara kupitia Idara ya Misitu ihakikishe inafuatilia kwa karibu na kutafuta dawa

ya kuulia wadudu wote wanaozorotesha ukulima wa Asali Pemba na Unguja.

4. Wizara iweke utaratibu wa kuwapatia wanajumuiya elimu ya ufugaji nyuki wa

kisasa japo kwa kuchukua wanachama wawili na kuwaelimisha na wao kuwa

mabalozi kwa kuwafundisha wakulima wenzao.

5. Wizara kwa kushirikiana na ZBS itengeneze mazingira ya kuwaelekeza na

kuwasaidia Jumuiya kufikia viwango vya kupata alama ya ubora na kuwapatia

alama hiyo kwa gharama nafuu.

Ripoti ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo inayotokana na ufuatiliaji utekelezaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Biashara na Viwanda pamoja na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2018/2019. 57

5. HITIMISHO

Kwa ujumla, Kamati imefanikisha majukumu yake ya kufuatilia utekelezaji wa kazi zake

ilizojipangia katika Wizara na taasisi zilizo chini ya Wizara hizo zilizoainishwa katika

ripoti hii. Kamati inazipongeza Wizara na Taasisi hizo kwa mashirikiano yao ya dhati

kwa Kamati katika kufanikisha kazi zake pamoja na juhudi zinazochukuliwa katika

utekelezaji wa kazi zao. Kamati inaziomba Taasisi hizo ziongeze juhudi ili kuimarisha

uchumi na maendeleo ya nchi yetu.

Wizara zinazosimamiwa na Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo zichukuwe juhudi za

makusudi kutekeleza ipasavyo maagizo yote yaliyotolewa na Kamati hii kwa lengo la

kuwapatia wananchi wetu huduma bora na kuongeza Pato la Taifa.

Kamati pia inapenda kutoa shukurani kwa wale wote waliofanikisha kazi za Kamati kwa

mwaka wa fedha 2018/2019 na kuwezesha taarifa za Kamati kutayarishwa na kuwasilisha

kunakohusika. Kamati inawashukuru kwa dhati viongozi na watendaji wote wa Serikali

na Baraza la Wawakilishi kwa utendaji mzuri wa shughuli zao za kila siku.

XXXXXXXXXXXXX Mwisho XXXXXXXXXXXXX