12

Ndiyo, kuishi pamoja - es.theret.orges.theret.org/wp-content/uploads/2015/07/RET_BDI_Ndiyo_kuish_pamoja_SW... · sasi muhewa nawakimbizi bakakimbiya mu ma nyumba yabo. Ile ali yenye

  • Upload
    others

  • View
    1

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Ndiyo, kuishi pamoja

2

Hiki kitabu cha ushuhuda kimeandikwa kwa ajili ya wa kimbizi wakongomani wa kambi ya

Gasorwe, Musasa na Bwagiriza wenye kutaka mifano mizuri juu ya kupata bidii

na uwakika kamili kama inawezekana kwao kusahahu yale yote yaliyopita kwa ajili ya amani.

Kwa wakimbizi wote wakongomani wa kambi ya Gasorwe, Musasa na Bwagiriza wenye kupima, kwa kila siku na kila mukutano ginsi ya

kupendezesha maisha…

©RET

Maandishi na picha : Roland Rugero Design na graphism : Edine NSABIMANA Mtafsiri: Didier MWAMBA

Kitabu hiki kimewapa nafasi wakimbizi wapate wakati wakusimuliya wanayo ishi na mawazo yao; bila kwamba ni maoni ya RET.

Mwezi wa kwanza 2012, Bujumbura-Burundi

3

« Wamefika Burundi kwa kukimbiya kifo kwa wakati inchi ya Jamuhuri yaki demokrasia ya Kongo watu wakiuwana mu makabila. Wale wale wenye walikuwa wakipigana inchini Kongo wakajikuta wote wakimbizi katika makambi zimoja :

Namna gani tutaishi pamoja bila kuaminiyana ?»

Wakati hapo awali (au mbele), « ilikuwa rahisi kuona mtu akichota maji na kuzijaza debe kumi bila kujali chochote ikionekana alifika wa kwanza tu, wakati huu kila mmoja anajaza debe lake na anampa nafasi aliye nyuma yake (kwenye foleni), anasema mama mmoja huko Musasa huku akijielekeza kufua nguo.

4

«Kama hatuna aya mafundisho ya amani yenye kupanwa na shirika la RET watu wataishiya

mukumalizana ! » anasema katika luga ya kiswahili Mama Angelika. Mwenye kuwa na macho yakushangazwa, na apo tukiwa katika kambi la wakimbizi wakongomani wa Gasorwe. Huyu Mama ni mwenye kufika inchini Burundi mu mwaka wa 2000, wakati vita vikipamba moto mu mashariki ya Jamuhuri ya demokrasia ya Kongo. Kama yeye, ma elfu ya Bafu-lero, Babembe, Bashi, Basonge, Barundi (benye kuzaliwa kisha mwaka wa 1972 mu mashariki ya Zaïre ya zamani), Ba-nyamulenge, Babembe, Baluba, Balulu, Batabwa, Bandande, Bangwande, Baban-gubangu, Barega… wakiwa ngambo ya ziwa Tanganyika mu makambi ya maisha magumu, bamingi ngambo ya Rugombo (Cibitoke), kando kando ya mupaka wa Kongo na Burundi.

CHEWUSI, mwenye myaka makumitano, muzaliwa wa Mushimuka (Sud-Kivu) ni mufulero. Aliweza kufisha bwana yake, “mwenye alihuliwa wakati aliendaka kuloba juu ya kupata chakula cha fami-liya kama wengine, na akaacha wayati-ma wengi” ameeleza Mama huyu akiwa mwenye uzuni. Umoja mubatoto wake wa miaka minane aliwezaka kuzama mu mashuwa yenye yeye na wengine wa-likuwa wakikimbiya amo, wakati nyumba zao zili kuwa zikiwaka moto.

Nyuma yake, aliacha mtoto wake wa kwanza mwanaume akiwa muzima kwa-huruma ya umoja ya muwale bauwaji.

Ma hadisi za kufanana hizi ni nyingi kati-ka watoto bila bazazi, majamaa bila baba, wa mama ambao walikuwa wakingali na

olewa wakapoteza wa bwana zao, ndoto na maisha zenye kuvunjwa za maelfu za wa kongomani wenye walijikuta ukimbi-zini.

Kitu cha kushangaza, hakuna mwenye anajisikiya mu kongomani! Kila mumoja anatanguliza kabila yake mbele ya yote.

Mu mwaka wa 2002, Serekali ya Burun-di iliweza kukamata mupango ya kua-misha wakimbizi wote wenye walikuwa wakipatikana ku mupaka wa Kongo na Burundi kisha mauwaji ya Banyamu-lenge ba Gatumba, kienye kilikuwa hakiwaziwe kikafanyika. Wa adui wa jana wakajikuta pamoja mumakambi ya wakimbizi ya Gasorwe mu 2002, kisha nyuma sana, Mwaro, mbele ya kambi ya Musasa kufunguliwa mu 2007 (juu ya watu wengi Gasorwe) na Bwagiriza (ye-nye kuwa amo mafamiliya yenye kutoka mu kambi ya Mwaro).

HAIWEZEKANE KUISHI PAMOJA

Ni EBA anaeleza «mupira wa 2010» yenye ilikuwa kati ya timu ya kambi ya Gasorwe na ile ya Bwagiriza. Ile ya Bwa-giriza ilikuwa ya Banyamulenge na ile ingine ilikuwa yenye “kuchangiwa ndani kabila zingine”. EBA alikuwa muamuzi: “Mupira ilianza 12h50. Kisha dakika 25, timu ya Gasorwe ikapigwa goli moja. Nyuma kidogo, umoja mu wachezaji aka-mupiga konongo muchezaji wa timu ya Bwagiriza. Sikuona kitu, na nikaitishwa, wakati nilimuuliza muchezaji ageuke ni-kaona kweli kama alikuwa akitoka damu mu kinywa”. Nikaamuwa kumupa bila kukawiya kadi ya njano kwa ule alicheza mubaya.

5

Kisha dakika kidogo, ule ule muchezaji mwenye alitoka kupewa kadi ya njano akamupiga muchezaji wa timu ya Bwagi-riza ngumi. EBA akaona na akamupa kadi nyekundu; mbele ya bapolisi kuja kumu-chukuwa na kumufunga.

Wakati watu wenye kuunga mkono timu ya Gasorwe waliona kama banafukuza ule muchezaji mupendwa wabo wakain-giya wote mu kiwanja na bakaanza ku-lomba ule muchezaji arudiye.

Wapolisi wakalazimishwa kurudiya na kuondowa muamuzi, mufanyakazi umoja wa HCR mwenye alikuwa akifata mupira na mukubwa wa kambi ya Bwagiriza mwenye alikuwa akisindikiza timu.

« Kupitiya bio ya dirisha ya chumba yenye nilikuwa amo, nilikuwa naona majiwe ye-nye biko natupiyana, mafimbo na damu kumuangika, na polisi ilikuwa yenye kuzi-diwa » akikumbuka EBA.

Mwisho, polisi ikalazimishwa kupiga ma-sasi muhewa nawakimbizi bakakimbiya mu ma nyumba yabo.

Ile ali yenye kutisha kati ya Banyamu-lenge na zingine makabila ilikuwa ikipa-tikana popote: «Ata Barundi abakukuwa naweza kuingiya mu kambi kwa sababu ya mafimbo na boga basibakule» anasema ELIE, murundi mwenye miaka 21 akiishi Kabanga (Muyinga).

Eba, ku shoto, na wanafunzi wa shule la msingi uko Gasorwe ( Muyinga)

6

Mawazo mabaya yenye bamoja ba-likuwa nayo juu yabingine aikuwa inaru-husu atamasikilizano.

AMISI anakumbuka mufano moja « Mu-fulero mwenye aliendaka kutongoza binti mumoja wa Banyamulenge. Wakati fami-liya ya ule binti ilijuwaka, bakaenda kwa-bo ule kiyana bakabomola nyumba kwa kuonesha kama abataki na binti wao »

Ikiwa Gasorwe, Bwagiriza wala Musasa kila busubuyi ilikuwa kuchambana wa-kati tunakuya kushota mayi: « Tulikuwa tunachambana saa zote, apakukuwa mutu mwenye alikuwa akiachia mwen-zake ashote mayi kabisa wakati ulikuwa ukiona kama ule mwengine siyo wa kabila lako » anatuakikishiya FURAHA mwenye miaka 18, muzaliwa wa Sange (Sud-Kivu).

Kila neno ilikuwa inasikika vibaya na ilikuwa inaweza leta vita kati ya maka-bila yenye ilikuwa haiyasahabu bienye bilipita ngambo ya Tanganyika.

Aiwezekane kusema maisha mabaya ye-nye tunaishi mu kikabila: Umri wa miaka 28, APENDEKI, mama wa batoto tatu na mukaaji wa kambi ya Gasorwe tokeya 2002 anakumbuka gisi mupaka miezi ine wala tano “Kila kabila ilikuwa inasaidiya wagonjwa wabo... Na wakati nilikuwa sina chakula, bili nikuiya nguvu kulomba bengine basiyokuwa bakabila yangu.”

CHIBALONZA, mama wa batoto saba wa mu ile ile kambi ya Gasorwe akikisha ku ngambo yake “Kama bikikufikiya una-piga mutoto wa munyamulenge mwenye alikosa ilikuwa ni vita mupaka na weye bakurudishiye.”

KISHA RET (Refugee Education Trust) IKAKUJA

Tarehe moja mwezi wa munane mwaka wa 2011, shirika la RET (Refugee Edu-cation Trust) ikaanza sehemu ya pili ya mupango wa mafundisho ya amani mu ma kambi ma tatu, kisha kufanya uchun-guzi, uchaguzi na mafundisho kwa vija-na makumi kenda wa shirika la warafiki walimu wa amani (PEPs) kwa sehemu ya kwanza.

Kwa mwanzo ilikuwa kutokuaminiyana kati ya wale vijana, wa PEPS, bengi baki-pitisha madakika ya kusema juu ya ama-ni, mavumiliyano, kuitikana... (Angaliya aya maneno walimu wa RET wanazun-gumuziya):

«Wale watu waliyo chaguliwa walikuwa wakionesha adabu kwa muda mdogo, kisha nyuma banajiendeya” anakumbuka ALINE, umoja mu wale wa vijana walimu wa Bwagiriza.

Walikuwa wenye kuzoweya mafundisho kuhusu ukimwi, usafi, afya, “Akuna mutu katika wakaaji wa zile kambi tatu zenye tulikuwa tukitumikiya mwenye alikuwa anaaminiya kazi zetu » anasema DIVINE, umoja mu wa vijana wa kabila ya Banya-mulenge mu kambi ya Musasa.

Kisha, pole pole, «Kwa kuzidi kutuam-biya juu ya amani, kuheshimiyana, kuvumiliyana, na bingine, wa rafiki wa shirika la RET wakafika kutuelewesha kama tuko bote bakongomani ata kama hatuna kabila moja » anasema SANTOS BIGABO akiakikisha ule musimamizi wa bakimbizi ba kambi ya Musasa tokeya mwaka 2009. GUSTAVE, mwenye umri

7

ya miaka makumi mbili na mbili anaongeza « Kuelewa lazima la ku-vumiliyana ilitengeza maisha yetu ya kila siku muma bikundi. Ndiyo, ma kabila ziko, alakini tunapashwa kuishi pamoja mu mapendo ata kama tunapishana.»

Mufano umoja wa mabadiriko katika maisha yetu ya kila siku? «Nakumubuka mbele ya mupango ya maadibisho ya amani, ilikuwa aiwezekane kulopola moto kwa jira-ni kama siyo wa kabila yako” anaen-deleya kusema bwana BIGABO. Na “kisha walimu wa shirika la RET wa-kapata kuvumiliya, wakatembeleya ma miya ya ma nyumba ili kufunza watu ni nini kuvumiliyana na kusai-diyana. Matokeyo: maelewano kati ya jirani ikaongezeka.»

Akiwa aki ikala katika nyumba yake, NAZANINKA akiwa anafika Gasorwe mu mwaka wa 2002, ku-tokeya jimbo la Shaba (Katanga). Ku mwanzo akukuwa mwenye kufu-rahi, wakati alikuwa akifata mafun-disho yenye kuletwa na shirika la RET: « Walikuwa wakitupa moyo kwa kuishi mu amani, mu upendo, na kuwa wavumi-livu... lakini aikuwa nyepesi kutokana na hali yenye ilikuwa mu ma kambi za bakim-bizi kisha ku uwana uko Kongo» anaeleza uyo mama mwenye kuwa na kijana wa miaka kumi na nane.

Kisha, sijuwi kueleza namuna ingine, alakini nikasikiya amu ya kuishi vema na bingine katika masikilizano. Nawaza kama njoo bienye bilifikiyaka bingine nabo. Munajuwa, kuna wakati ingine mu maisha, unajiuliza maswali nyepesi

sana. Kwa nini kuangaliya kilicho mwin-gine? Kweli aiwezekane kuishi na wen-gine katika urafiki na masikilizano? Kweli aiwezekane kuishi bila kuto kuaminiyana na kuchukiyana?

Aya maswali yalikuwa yakirudi sana kwangu mangaribi, kisha mukutano wa kwanza yenye ilikuwa inaongozwa na watumishi wenye kueleza watu wa shi-rika la RET. Tuliweza kuzungumuziya kwa mufano juu ya upendo kwa ndugu wala jirani na mangaribi nikaweza kuifikiriya. Namuna gani kupenda mutu mwenye iko

NAMUNA GANI KUPATIYA WATOTO

MAISHA MEMA ?

8

mubenye baliweza ku kuuwiya? Nilikuwa mwenye kuuzunika, wakati wengine wakifurahi. Nawaza kama polepole na ma-fundisho ya shirika la RET ku ami-niyana ikarudi. Watumishi wenye kueleza batu bakatuomba kuishi pamoja na kuwa na masikilizano mema. Matunda ya ile kuaminiya ziko pale. Leo tunasikilizana na njoo mana batoto yetu banache-za pamoja, banachangiya chaku-la, bienye bilikuwa habifanyikake zamani.”

Na kwa kuonesha ile umoja na kuvumiliyana yenye kuwa kati ya mafamiliya mbali mbali, NAZA-NINKA anaonesha mutoto wake wa mwisho mwenye kusema swa-hili. Na mama huyu anamukuba-liya kucheza na benzake ba mia-ka... Anamupatiya ile uvumilivu yenye alipata kwenye watumishi wenye kueleza la shirika la RET.

Ata kama NAZANINKA anaaki-kisha «mabadiriko ya mafikiri ya ma elfu ya watu ni kazi ya muda », alakini ana-sema tena «Mafamiliya mengi aisite tena kulomba mboga wala chumvi kwa jirani, bila kutizama ma kabila. Na iyo ni kwa neema ya makutano ya wa memba wenye kufundisha mushirika la RET, wenye kutowa mafundisho gisi yakuheshimiyana, kusikilizana, kuvu-miliyana, kuelewana, na bingine. Njala, magonjwa, kiwu haichaguwe mutu: Na ni lazima ya mutu wote.»

Kwani mbele, « ilikuwa nyepesi kwa mama wa batoto kushota maji ata ma

mbegeti mengi bila kuachiya bengine ila leo ile yote inakwisha badirika. Inakuwa unashota mbegeti moja kisha unaachiya mwingine naye ashote » wanasema wa mama tuliyo kuta Musasa bakiwa na furaha. Wote walikuwa ni wenye kufata mafundisho ya shirika la RET kufatana na kuvumiliyana. Umoja wabo akaongeza: «usifanyiye mwingine kienye aupendi bakufanyiye.»

Mabadiriko kufatana na kazi iliyo fanywa na walimu wa RET ni yenye kuonekana

Suite page 10

« Kuna wakati maishani mtu anajiuliza maswali ya kawaida. Sababu gani kumsen-

geya kila mara mwenzako ? »

9

WA MEMBA WALIMU WA AMANI ...

Kwa kukamilisha matendo ya mipango ya kufundisha watu amani Bwagiriza, wanamemba walimu wanaenda kila siku ya ine ku wajirani ya kambi kuchangiya nabo mazungumuzo, anasema STEPHANE. Kwa shabaa: “ya kukutana na bakaaji ya hapo (warundi), kuzungumuziya masikilizano kati yabo na wakimbizi kwani kuliwayi kuwa matatizo kati ya izi kundi mbili wakati izi kambi zilifunguliwaka. Mpaka hivi kuna wakati kunafikaka matatizo kati ya murundi na mukimbizi. Na tunatatuwaka matatizo bila fujo tukifata mafundisho tulipata na shirika la RET kwa njiya ya kuvumiliyana na kuheshimiyana” anafasiliya MUTABAZI, mwana memba mwalimu. “Juu kukuwe amani katika maroho za batu, inaomba amani ikuwe ndani na inje ya kambi” anamaliziya huyu baba wa jamaa aliyefika Burundi mu mwaka wa 2004.

- Ni timu ya vijana makumitatu kukila kambi (Bwagiriza, Gasorwe na Musasa) waliyo chaguliwa kisha kupita mashindano na kufunzwa na shirika la RET - Wana kazi ya maasiliyano, kujulisha, kufundisha, kuamasisha, kushauriya na kuwa mifano

- Wamejitoleya kuwa mifano ku barafiki yao na kumakabila yao, kwa kuwa tayari kuongeza elimu, kufundisha wa rafiki na kabila zao, na kuwasikiliza balicho sema. - Wanaongoza mikutano za makabila na banajiunga kwa kubadirisha mwenendo na gisi ya kuamasisha siku kwa siku

10

wakati tukisabiya malalamiko yenye il-ikuwa ikibebwa mbele ya walinda amani mu aya ma kambi ma tatu ya wakimbizi wa kikongomani: « mbele ya iyi kazi, kushwa-na yote wala kugombana ilikuwa inaishiya mbele ya polisi kwa kufungwa wala kube-belewa » anasema GORETH, umoja mu wa vijana wa PEPs pale pa Gasorwe.

Kufatana na kazi ya wa memba walimu kati ya aya makambi ma tatu «tumekuwa wapatanishaji kati ya mafamiliya. Na ndani ya maisha ya kila siku, siko tena tu GORETH, alakini niko mama mushauri mwenye kusaidiya watu kusikilizana. Kwa kifupi bana-niangaliya namuna ingine» anaongeza tena mama huyu.

Iyo hadabu anapewa mama GORETH katika kambi siyo tu apo, ata nyumbani kwake bwana yake anaheshimu kazi yake: «Asirikake ata kama banakuja kumulamusha busiku kwa kupatanisha bibi na bwana benye balikuwa bakishwana wala kugombana! Anabisikiya muzuri sana kwani situmike juu yangu mwenyewe, alakini juu ya batu bote na kupatanisha watu wenye kuitwa kuishi pamoja. Wakiwa wa Kon-gomani, sivyo?», anaongeza huyo mama, akiwa mwenye kutuliya na kufurahi.

Na akaeleza: «Jioni moja, walikuya ku-nitafuta mbiyo mbiyo juu kulikuwa kie-nye hakiendeke kati ya bwana umoja na bibi yake. Ule bwana aliweza kugabula chumba mara mbili kwa kutumikisha kitambala juu asionane na bibi yake. Na ile hali ilikuwa ilishafanya myezi mbili

banaishi hivo... Auwezi kutatuwa hali kama hiyo, kama weye moya hauko mu amani wala abiendeke mu nyumba yako! Nika-zungumuza na baba wa nyumba akiwa mwenye kusirika sana, na nimue-leweshe kama kufa-nya hivo ni kumu-zarahu bibi yake mwenye alilagaka kama atamupenda na atamuheshimu siku zote za maisha yabo, nikamuzun-gumuziya kufatana na kuvumiliyana zaidi kwa mutu aliye kuwa mama wa batoto yake na

akafika mukunielewa. Ile ile busiku, akatowa kitambala yenye ilikuwa ina-gabula chumba yabo, na akamulomba bibi yake musama. Tokeya pale ba-naishi kwa amani.»

Wabwana wenye kutumiya mali za fa-miliya gisi banajitakiya katika kambi ya Gasorwe, mukupitiya vijana wa Bwagi-riza benye balikuwa banapenda pombe sana na bulevi, leo hali inabadirika.

Walimu wa shirika la RET wanazungumuziya neno kama izi :> Mafunzo ya amani

> Namuna ya kutatuwa mizozo kati ya watu

> Kumupenda ndugu wala jirani

> Kuvumiliyana

> Kufanana kwetu na kutokutanisha

> Ubaguzi na ubakaji wa bamama

> Kutengana na kuwa pamoja

> Maoni na tabiya

> Mawasiliano na kusikiliza wengine kwa kweli

11

SANTOS BIGABO,musimazi wa bakimbizi ba kambi ya

Musasa: “Juu ya kutuliza hali kati ya wakaaji ba kambi,

na ofisi kuu ya bakimbizi (HCR) na wakubwa wa inchi

ya Burundi ilitukuiyaka nguvu mwanzo. Alakini shirika

la RET imetusaidiya sana na tunajisikiya tunaungana

sana sisi wakimbizi na tunafikiya kipindi kingine.”

«Kutokana na kazi za wana mem-ba walimu wenye walitufundisha namuna za kutatuwa mizozo, leo kunakuwa heshima kati ya ma bunyumba », anasema BILELO, mama wa batoto sita. Mbali zaidi, PATRICK, mukaaji wa Bwagiriza anafurahishwa na kuundwa kwa makundi ya vijana mu makambi ya Ruyigi: « Yenye inabasai-diya kucheza mupira, kufanya mashindano ya michezo za zamani na za leo, kuimba wala kuchapa, ...» na ile yote nikuto-kana na kazi za shirika la RET.

Izi sifa zote nikutokana na kazi za wamemba walimu wa RET. Shirika la RET iliunda timu mbili, ngambo moya wa kongomani wa makabila mbalimbali na ngambo ingine warundi benye budongo. « Sikuwayi kuwaziya kama siku moya naweza kui-kala na mubembe na kuchangiya naye chakula» anatupa akicheka NAMITAVU, uyo Munyamulenge.

Wana memba walimu wa amani (PEPs) wanazungumuziya furaha na kicheko na kuaminiyana kati yabo bakiwa katika kundi ya kazi, « mbali na bienye tulikuwa tukiishi mwanzo. Chuki tulikuwa nazo katika makabila, mbele shirika la RET itua-like kama wana memba walimu wa amani zilikuwa nguvu mpaka inaonekana ku kila tendo. Gisi abingiwezekana tuende ku-fundisha wengine bitu hatuaminiye, ilitu-bidi sisi wenyewe kujifunza kuaminiyana, na kuitika kila moya moya gisi alipo, na makosa yake, na mazuri yake...» anaon-geza akieleza uyu mwana mama wa umri makumi tatu. Na kumaliziya: « Nawaza

kama chuki inapoteyaka wakati mimi na weye tuna elewa kama mwingine anahamu ya kula, kuvala, na kufurahi... ata kama tunaweza kuwa mbali mbali ».

MAKANDA, huyu baba wa watoto ine, aishiye Gasorwe anasema hivi: « Kazi yetu yote nikutumika mu namuna yakumue-lewa mwingine. Wakati tuliwezafika mu kambi, mwingine ilikuwa ni kusema adu-hi, inapashwa kumupisha mbali, mwenye inafaa kujilinda naye... Wakati unaelewa kama mwingine ni mutu kama na weye masikilizano inabadirika. Alakini njia gani kupitiya ? Kwa sasa, wanyamulenge, wa-fulero, wabembe, wa mushi, na wengine wote... wanasaidizana. Wanasindikizana ku maziko bila kusita, ata kumubeba mwingine akiwa mgonjwa kwa mugan-ga bila kuuliza kabila yake. Mabadiriko makubwa haya yamefanyika kukiwa tu myezi misaba...»

12

Kweli, kuishi pamoja na kujifunza kuchangia...