Upload
faykiss
View
311
Download
0
Embed Size (px)
DESCRIPTION
wedding song suggestions
Citation preview
UTUKUFU KWA MUNGU MBINGUNI
Kiitikio
Utukufu kwa Mungu Mbinguni (wololo)
Na amani duniani kwa watu,
Kwa watu, kwa watu wenye mapenzi mema (*2)
1. Tunakusifu, twakuheshimu, twakuabudu, twakutukuza, twakushukuru mfalme wa mbingu, mwana wa pekee, mwana wa baba (ee-Bwana)
2. Unaye ondoa makosa yetu, tuhurumie, tusikilize, Kuume kwa Baba unapoketi, mtakatifu mkuu tuhurumie (Ee-Bwana)
3. Pamoja na Roho Mtakatifu, ndani yake Baba unatukuzwa, Muu-ngu mmoja anayeishi, na kutawala milele yote (Ee-Bwana)
NITALITANGAZA NENO LAKE BWANA
Kiitikio:
Nitalitangaza neno lake Bwani katika lugha mbali mbali ee *2
1. Wa Kamba, waimbe na kumsifu bwana, Wa Kikuyu, waimbe na kumsifu bwana, Wa Luyha, waimbe na kumsifu bwana, Wa Meru, waimbe na kumsifu bwana,
2. Wa Luo….
Wa Masaai… Wa Taita… Wa Swahili …
3. Wa Nandi ... Wa Kisii … Wa Suba …. Wa Maragoli…
4. Wa Embu …. Wa Pokomo …. Wa Arabu …. Wa Kalenjin …
5. Wahindi ….. Wa Somali …. Wa Moraan …. Wa Sudanese ….
6. Wa Zambia …. Wa Espanya …. Wa Burkina …. Na wa Congo … NIJAPOSEMA KWA LUGHA
1. Nijaposema kwa lugha kushinda malaika (jamani) kama misina upendo mimi ni kitu bure
Kiitikio
Upendo hauna wivu, Upendo hauoni mabaya, Upendo hauna chuki, Upende haujivuni *2
2. Nijapohubiri sana, mbeleya watu wengi (jamani) kama mi sina upendo mimi ni kitu bure *2
3. Nijapo jitoa mwili niungue motoni (jamani) kama mi sina upendo mimi ni kitu bure *2
WHAT RETURNS TO YAHWEH
1. What returns to Yahweh can I make *2 For blessings of every kind from Him that I Have received
Chorus
What returns to Yahweh? What returns can I make? What returns to Yahweh? What returns can I make? What returns to Yahweh for blessings of every kind from Him that I have received *2
2. He created me the Lord, and he adopted me the Lord, For blessings of every kind from Him that I have received
3. He purifies and strengthens me by the Spirit, the Spirit of Power, For blessings of every kind from Him that I have received
SASA WAKATI UMEFIKA
Kiitikio:
Sasa wakati umefika wa kushika nilicho nacho (mimi) kwa wema niende kwa Mungu nitoe zawadi. Sasa wakati kwenda mbele ya mungu wangu (mimi) aone nilivyoandaa zawadi ya leo
Nitamwambia Bwana pokea (hiki) kidogo nilichonacho kwani Mungu wewe wanijua (mimi) siwezi hata kueleza, nakusihi sana baba unipokee nigawie na Baraka niwe salama
1. Mema yote niliyo nayo yametoka kwa Mungu, hivyo nami ni kosa kusahau kumshukuru, kwani kuwepo hapa leo
hii ni kazi ya nani kamwe mimi sitapata uwezo, pasipo mungu.
2. Mema yote aliyotenda Mungu nijibu nini na vipi? Mbona hofu yazidi kuwa ndani ya moyo wangu, mbele ya Bwana Munug wangu kufanya siri ni bure, yeye ndiye mpanga mambo yote ya wanadamu
3. Pumzi inayonipa uhai inatoka kwa nani? Bila Mungu hakika mwanadamu siwezi kitu, nimepata nafasi leo ya kwenda kutoa zawadi, heri niende ya kesho siyo yangu ajua Baba
4. Ewe Mwumba wa vyote duniani na vyote vya mbinguni, mimi leo nakuja kwako Baba nihurumie, Baba wewe unayetawala kulala na kuamka kwangu, juu yangu take nini Baba lisifanyike
MTAKATIFU
Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu Bwana Mungu wa majeshi
Mbingu na dunia zimejaa utukufu, Mbingu na dunia, Mbingu na dunia, Mbingu na dunia zimejaa utukufu wako, zimejaa utukufu wako
Kiitikio
Hosanna juu, Hosanna juu, Hosanna juu, Hosanna juu mbinguni *2
Mbarikiwa yeye ajaye kwa jina, mbarikiwa yeye, mbarikiwa yeye, mbarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana
OH LORD MY GOD
1. Oh, Lord, My God, when I’m in awesome wonder, consider all the world thy hand has made; I see the stars, I hear the rolling thunder, thy power throughout the universe displayed.
Chorus:
Then sings my soul, my saviour God to thee; how great thou art, how great thou art *2
2. When through the woods and forest glades I wander, and hear the birds sing sweetly in the trees; when I look down from lofty mountain grandeur; and hear the brook, and feel the gentle breeze.
3. And when I think that God, His son not sparing, sent Him to die, I scarce can take it in; that on the cross, my burden gladly bearing; He bled and died, to take away my sin.
4. When Christ shall come with shout of acclamation, and take me home, what joy shall fill my heart; when I shall bow in humble adoration, and there proclaim: my God, How great thou art.
BWANA MUNGU NASHANGAA
1. Mungu wangu nashangaa kabisa, nikifikiri jinsi wewe ulivyo, nyota ngurumo vitu vyote pia, viumbavyo kwa uwezo wako
Kiitikio
Roho yangu na ikuimbie jinsi wewe ulivyo mkuu *2
2. Nikitembea pote duniani, ndege huimba nawasikia, milima hupendeza macho sana, upepo nao ufurahia.
3. Nikikumbuka vile wewe Mungu, ulivyo mpeleka mwanao afe, azichukue dhambi zetu zote, kutatambua ni vigumo mno.
4. Yesu mwokozi atakaporudi, kunichukuwa kwenda mbinguni, nitaimba sifa zake milele, wote wajue jinsi ulivyo.
CHEREKO
Kiitikio:
Chereko chereko, leo ni furaha, wana meremeta, hawa maharusi,
Tupige ngoma vinanada, makofi vegelegele, chereko, chereko, furaha leo *2
1. Watu wote tuimbe turukeruke juu, leo ni furaha
2. Wote wapendanao wameungana leo, kweli ni furaha
3. Vifijo visikike mayowe ya furaha, kweli leo shangwe
MOYO WANGU WAMTUKUZA BWANA
Kiitikio:
(Moyo) Moyo wangu wamtukuza Bwana (Roho) Roho yangu inafurahi *2
1. Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake, hivyo tangu leo watu wote wataniita mwenye heri
2. Kwa sababu Mwenyezi Mungu, Amenifanyia makuu, jina lake ni takatifu, jina lake ni takatifu
3. Huruma yake ni kwa wote, wote wale wanaomcha, kizazi hata na kizazi, kizazi hata na kizazi
4. Huyatenda mambo makuu, kwa nguvu za mkono wake, wenye kiburi hutawanya, wenye kiburi hutawanya
5. Hushusha wote wenye vyeo, kutoka viti vya enzi, hao wote wanyenyekevu, wote hao huwainua
6. Huwashibisha wenye njaa, na matajiri huwaacha, waende mikono mitupu, waende mikono mitupu
7. Hulilinda Taifa lake, tuele na mtumishi wake, ‘kikumbuka huruma wake, ‘kikumbuka huruma wake
8. Kama alivyo wahidia, baba zetu kuwaahidi, Ibrahimu na uzao wake, Ibrahimu na uzao wake
9. Atukuzwe Baba na Mwana, naye Roho Mtakatifu, leo kesho hata milele, kwa shangwe milele Amina.