46
1 Fataawa Za Wanachuoni [06] Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

Fataawa Za Wanachuoni (6)

Embed Size (px)

DESCRIPTION

Fataawa Za Wanachuoni (6)

Citation preview

1

����������������� ������������������

Fataawa Za Wanachuoni

[06]

Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

2

Dibaji:

Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili

kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji

elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya

Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo.

Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta faida kwa ndugu

zetu Waislamu, na ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) Ajaalie kazi hii niwe

nimeifanya kwa kutafuta Radhi Zake (Subhaanahu wa Ta´ala), na Amlipe kila

Aliyeisambaza kwa ndugu mwengine na Awalipe ndugu wasomaji wote kwa

jumla.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

3

Fataawa zilizomo ni hizi zifuatazo:

1. Kuna Dalili Inayokataza Mahari Yasiwe Makubwa?

2. Baba Hataki Kuwaozesha Mabinti Zake Kwa Kukhofia Riziki Zao

3. Biashara Ya Kompyuta

4. Kafunga Mwezi Mzima Wa Muharram, Kapatia?

5. Kuna Muda Maalumu Wa Mtu Kufanya Kijicho?

6. Je Siku Ya ´Aashuraa Kuna Chakula Maalumu?

7. Kuuza Katika Maeneo Ya Msikitini Kama Bustani La Msikitini N,k

8. Mwanaume Anaruhusiwa Kuvaa Pete?

9. Mtu Anataka Kulipa Deni Katika Pesa Za Zakaah

10. Imamu Kakumbuka Kuwa Nguo Yake Ina Madhiy1 Ndani Ya Swalah

11. Mtoto Kupitia Mbele Ya Mwenye Kuswali

12. Mwanamke Anatokwa Na Upepo Kwenye Tupu Ya Mbele, Hukumu Ya

Swalah Yake

13. Mwanamke Mgonjwa Anastanji2 Na Kujiosha Kwa Maji Ya Zamzam

14. Hukumu Ya Unyevu3 Umtokao Mwanamke

15. Hadiyth Ya Waislamu Kupeana Zawadi Ili Wapendana

16. Mfumo Wa Kusoma Kwa Dada Salafiy

17. Kafunga Sunnah Kisha Baadae Kaamua Kula

1 Ni maji meupe yanayonata yanayotoka katika sehemu za siri kwa sababu ya kuwaza tendo la ndoa au kutokana na matamanio yaliyozidi ya kimwili kwa kutazama, kushika, kushikwa n.k. Kawaida mtu hafahamu kwa uhakika kinachotoka. Inawatoka wanaume na wanawake, japokuwa kwa wanawake inakuwa ni nyingi zaidi. Wanazuoni wamekubaliana kuwa ni najisi. 2 Ni kuondosha chenye kutoka kwenye njia mbili sawa ye mbele au ya nyuma 3 Majimaji, Utoko umtokao mwanamke

4

18. Talaka Inatokana Na Alivyokusudia (Nia) Ya Mume

19. Dada Anataka Kubadilisha Rangi Ya Nywele Zake Nyeusi

20. Twawaaf Ya Kuaga Ni Wajibu Katika ´Umrah?

21. Kuswali Swalah Za Sunanh Kabla Ya Swalah Ya Ijuma

22. Ewe Kaka Wa Kiislamu, Mtume Wako Akuamrisha Kufuga Ndevu

23. Nasaha Kwa Wale Wenye Kueneza Uvumi, Kusema Uongo Na

Usengenyaji

24. Kipigo Cha Kutia Adabu Kinachoruhusu

25. Hukumu Ya Kubaki Macho Baada Ya Swalah Ya ´Ishaa

26. Du´aa Nzuri Wakati Mwanamke Anataka Kuzaa

27. Wazazi Wanataka Binti Aende Kusoma Masomo Ya Mchanganyiko

Holland

28. Imamu Na Muadhini Hawatakiwi Kuwa Ahl-ul-Bid´ah; Kama Suufiy,

Ash´ariy, Mu´taziliy, Jahmiy

29. Hukumu Ya Muislamu Kuwa Na Urafiki Na Makafiri

30. Kakasirika Sana Ramadhaan Akala, Nini Hukumu Yake?

31. Ufafanuzi Wa Mwanamke Kulipa Swawm Zilizompita Katika Mwezi

Wa Ramadhaan

32. Kijana Kila Anapotubia Anarudi Kufanya Dhambi Tena

33. Kaswali Maghrib Msikitini Kisha Akaswali Tena Nyumbani Na Ahli

Zake

34. Kaoa Mwanamke Wa Ahl-ul-Kitaab Ambae Hataki Kuingia Katika

Uislamu

35. Mgonjwa Mwenye Kutayamamu4 Na Sasa Kapatwa Na Janaba

36. Kwanini Ndoa Nyingi Za Ulaya Zina Matatizo Na Zinavunjika?

4 Kuweka twahawa (Wudhuu) kwa kutumia udongo msafi

5

37. Mume Na Mke Wanaishi Ufaransa, Mume Anasema Waswali Kama

Wasafiri

38. Nasaha Ya Shaykh al-Waswaabiy Kwa Wenye Kutaka Kuoana

39. Aina Mbalimbali Za Sigara Za Hukumu Zake

40. Hukumu Ya Kubadilisha Rangi Nywele Nyeusi

41. Baadhi Ya Sifa Zinazopasa Kuwa Na Mke Mtarajiwa

42. Nasaha Kwa Yule Aliemlaani Mke Wake

43. Inajuzu Kula Nyama Za Wakristo Na Mayahudi Wa Leo?

44. Je Mkaaji Eda Haruhusiwi Kutoka Nyumbani Kabisa?

45. Hukumu Ya Uchawi Katika Uislamu

46. Kubadilisha Nywele Kwa Kuweka Rangi Nyeusi

47. Swawm Za Ramadhaan Huwekwa Nia Mara Moja Au Kila Siku?

48. Je Salaf Waliwahi Kutofautiana Kunako ´Aqiydah?

49. Baadhi Ya Vitabu Bora Vilivyozungumzia Siyrah Ya Mtume (´alayhis-

Salaam)

50. Kitabu Cha Majina Ya Mtume (´alayhis-Salaam)

51. Kuwaweka Wazazi Katika Nyumba Ya Wazee

Wanachuoni waliomo ni hawa wafuatao:

1. Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

2. Zayd bin Haadiy al-Madkhaliy

3. Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Waswaabiy

6

Bismillaahi Rahmaani Rahiym

1. Kuna Dalili Inayokataza Mahari Yasiwe Makubwa?

Swali:

Je, kuna dalili katika Sunnah inayokataza ukubwa wa mahari?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Kakataza ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhu) mahari makubwa. Bora zaidi

mahari yawe madogo kwa kufuata Sunnah. Hakika ´Aaishah (Radhiya

Allaahu ´anha) anasema:

"Hakuzidisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika mahari ya

mke wake wala mabanati zake zaidi ya Dirhamu tano.” [Hadiyth hii

imepokelewa na Muslim]

Na uongofu bora ni uongofu wa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam).

Atakaezidisha na akawa anaweza hilo hakuna ubaya. Kama alivyosema

Allaah:

“Na mkitaka kubadilisha mke mahali pa mke, na hali mmoja wao mmempa

chungu ya mali, basi msichukue katika hayo kitu chochote.” (04:20)

Nukta muhimu:

”Na hali mmoja wao mmempa chungu ya mali.” (04:20)

Ikiwa anaweza hakuna ubaya. Wala watu hawahukumiwi hukumu moja,

fulani alitoa kiwango fulani nawe toa kiwango fulani. Fulani anaweza kuwa

na uwezo, na huyu mwengine akawa hana uwezo.

7

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4750

2. Baba Hataki Kuwaozesha Mabinti Zake Kwa Kukhofia Riziki Zao

Swali:

Ipi hukumu ya baba ambaye hataki kuwaozesha mabinti zake kwa ajili ya

riziki zao?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Huchukuliwa kuwa ni dhalimu. Na Allaah Hawapendi madhalimu. Anasema

Allaah:

�ا� أ���� ��� � وا������� أ

”Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.” (76:31)

Riziki yao iko kwa Allaah. Akimuozesha binti yake riziki yake iko kwa Allaah.

Ajitahidi kumuozesha kwa mwanamume mwema ambaye atamsaidia katika

dini na dunia yake. Haijuzu kwake kumkatalia kwa kitu alichomhalalishia

Allaah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4706

8

3. Biashara Ya Kompyuta

Swali:

Ipi hukumu ya uuzaji wa kompyuta?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Akijua kuwa mtu huyu ataitumia katika kufanya maasi, haijuzu kwako

kumsaidia katika maasi na uadui. Kutokana na kauli ya Allaah (´Azza wa

Jalla):

�� ا��� وا���وان �ا � و ���و

”Wala msisaidiane katika dhambi na uadui.” (05:02)

Na ama akiwa hajui na akamdhania mtu huyo vizuri, In Shaa Allaah hakuna

neno.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4707

4. Kafunga Mwezi Mzima Wa Muharram, Kapatia?

Swali:

9

Atakaefunga mwezi wa Muharram wote au baadhi ya siku chache, je kitendo

chake hiki kapatia?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ndio ni sahihi. Muulizaji anasema kwa kuwa nimesikia katika Hadiyth:

"Swawm bora kwa Allaah baada ya Ramadhaan ni Swawm ya mwezi wa

Allaah Muharram. "Jibu ni ndio, Hadiyth hii ni sahihi.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4708

5. Kuna Muda Maalumu Wa Mtu Kufanya Kijicho?

Swali:

Je, kuna muda maalumu katika Kitabu na Sunnah ambao hutokea kijicho kwa

wale wenye vijicho?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Elimu ya jambo hili iko kwa Allaah (´Azza wa Jalla). Allaah Hufanya

Atakacho. Wewe ni juu yako kujitibu nafsi yako kwa kufanya Ruqyah ya

Kishari´ah na Allaah Hufanya Atakacho. Na haya ni kama maradhi mengine

yote. Ujitibu kwa yale aliyokuruhusu Allaah na lini maradhi yataisha, elimu

ya hili ni kwa Allaah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4710

10

6. Je Siku Ya ´Aashuraa Kuna Chakula Maalumu?

Swali:

Je kuna chakula maalumu siku ya ´Aashuraa?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Wewe ndugu hakuna chakula maalumu siku ya ´Aashuraa. Hili huenda ikawa

ni katika matendo ya Mashia, kwa kuwa Mashia wana Ghuluu5 katika siku ya

´Aashuraa na wana Bid´ah nyingi.

Ama Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah hawana chakula maalumu siku ya

´Aashuraa, isipokuwa wao hufunga siku ya Tasuua´ na siku ya ´Aashuraa. Na

ataefunga zaidi ya siku mbili Allaah Amjaze mtu huyo kheri, kama ilivyo

Fatwa ya Shaykh Ibn Baaz na Shaykh Ibn ´Uthaymiyn (Allaah Awarehemu)

kupendekezwa kufunga mwezi wa Muharram wote.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4711

7. Kuuza Katika Maeneo Ya Msikitini Kama Bustani La Msikitini N,k

5 Kuchupa mipaka

11

Swali:

Hukumu ya kuuza katika maeneo ya Msikitini?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Pale ambapo ni maeneo ya Msikitini haijuzu kuuza, kutokana na ujumla wa

Hadiyth (inayokataza kuuza Msikitini).

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4712

8. Mwanaume Anaruhusiwa Kuvaa Pete?

Swali:

Hukumu ya kuvaa pete kwa kijana?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Hakuna tofauti kati ya kijana wala mzee, hukumu yao ni moja. Na pete

hakubainisha ni pete ipi, ikiwa ni ya dhahabu ni Haramu kwa wanaume.

Ikiwa ni ya fedha ni Sunnah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4713

12

9. Mtu Anataka Kulipa Deni Katika Pesa Za Zakaah

Swali:

Mtu ambaye mali yake imeeneza Niswaab6, na yeye ana madeni kwa baadhi

ya watu. Je, anaweza kulipa madeni hayo kwa kulipa Zakaah?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Fatwa za wanachuoni zinasema kuwa jambo hili halijuzu, kwa kuwa

anajihami mali yake kwa kutoa Zakaah. Lakini ampe fakiri Zakaah. Na fakiri

ikiwa ndio huyo aliyekuwa akimdai hakuna ubaya. Kwa sharti isiwe

alikubaliana naye kabla, mimi nakukopa na wewe utanirudishia. Hii ni

khiyana haijuzu.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4714

10. Imamu Kakumbuka Kuwa Nguo Yake Ina Madhiy7 Ndani Ya Swalah

Swali:

Akikumbuka Imamu kuwa katika nguo yake kuna Madhiy, atoke katika

Swalah au aitimize?

6 Kiwango cha chini cha kutolewa Zakaah 7 Ni maji meupe yanayonata yanayotoka katika sehemu za siri kwa sababu ya kuwaza tendo la ndoa au kutokana na matamanio yaliyozidi ya kimwili kwa kutazama, kushika, kushikwa n.k. Kawaida mtu hafahamu kwa uhakika kinachotoka. Inawatoka wanaume na wanawake, japokuwa kwa wanawake inakuwa ni nyingi zaidi. Wanazuoni wamekubaliana kuwa ni najisi.

13

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa Madhiy ni najisi. Akiweza kuvua nguo hii aivue na aendelee na

Swalah. Na akiwa hawezi atoke (ndani ya Swalah) na paingie nafasi yake mtu

mwengine.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=283

11. Mtoto Kupitia Mbele Ya Mwenye Kuswali

Swali:

Akipita mtoto mdogo wakiume au wakike mbele ya mwenye kuswali,

anaharibu Swalah?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni hapana, haiharibu. Lakini usimwache mtoto uhuru moja kwa moja, na

ikiwa atapita haaribu Swalah. Anaeharibu Swalah ni mwanamke aliye

baleghe8, lakini ambae hajabaleghe haaribu Swalah lakini inapungua kidogo.

Ikiwa Mtume alizuia mtoto wa kondoo asipite mbele yake mpaka tumbo lake

likagusa kwenye ukuta, itakuwa mtoto mdogo! Hali kadhalika kwa mtoto.

8 Shaykh Swaalih al-Fawzaan anasema kauli yenye nguvu kwa wanachuoni ni kwamba Swalah haiharibiki bali thawabu ndio hupungua, sawa awe mwenye kupitia ni mwanamke au mwengine yeyote. Wa Allaahu A´alaam.

14

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4854

12. Mwanamke Anatokwa Na Upepo Kwenye Tupu Ya Mbele, Hukumu Ya

Swalah Yake

Swali:

Mwanamke katawadha kisha anatokwa na upepo wakati wa kuswali

anapoenda kwenye Rukuu na Sujuud, akaamua kuswali hali ya kuwa amekaa

ili asitokwe na upepo.

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ikiwa Swalah ni ya faradhi kusimama ni nguzo (lazima). Na ikiwa ni Swalah

ya Naafilah9, akiswali hali ya kuwa amekaa hakuna ubaya.

Na kutokwa na upepo katika tupu ya mwanamke hakutengui Wudhuu.

Kutenguako Wudhuu ni kutokwa na upepo katika tupu ya nyuma.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4855

13. Mwanamke Mgonjwa Anastanji10 Na Kujiosha Kwa Maji Ya Zamzam

9 Swalah ya Sunnah 10 Ni kuondosha chenye kutoka kwenye njia mbili sawa ye mbele au ya nyuma

15

Swali:

Mwanamke ni mgonjwa, anajiosha kwa maji ya Zamzam bafuni na anastanji

nayo. Je, hili linajuzu?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ikiwa anajitibu kwa hili hakuna ubaya. Kwa kuwa kustanji kunachukuliwa ni

dawa. Hakuna ubaya In Shaa Allaah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4856

14. Hukumu Ya Unyevu11 Umtokao Mwanamke

Swali:

Anauliza kuhusu unyevunyevu umtokao mwanamke?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Fatwa za wanachuoni zinasema kuwa unatengua Wudhuu. Pia Fatwa ya al-

Lajnah ad-Daa´imah inasema hali kadhalika - Fatwa ya Shaykh Ibn Baaz.

Anatakiwa kustanji na aoshe sehemu ilipopatwa nguo yake na unyevu huo,

kisha atawadhe.

11 Majimaji, Utoko umtokao mwanamke

16

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4857

15. Hadiyth Ya Waislamu Kupeana Zawadi Ili Wapendana

Swali:

Hadiyth (ombeaneni Du´aa mtapendana), je makusudio yake ni watu kupeana

zawadi au ni uongofu?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ni watu kupeana zawadi. Kumpa ndugu yako Muislamu zawadi, naye

akakurudishia zawadi. Zawadi inasababisha mapenzi, kama kutoleana Salaam

baina ya Waislamu pia yasababisha mapenzi baina yao.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4858

16. Mfumo Wa Kusoma Kwa Dada Salafiy

Swali:

17

Yuko na dada ambaye ni Salafiyyah na anataka kuanza kuhifadhi Qur-aan,

aanze na kuhifadhi Qur-aan au kuhifadhi ´Aqiydah?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Akiweza afanye yote mawili kuhifadhi Qur-aan na kuhifadhi ´Aqiydah. Qur-

aan kwa mfano ahifadhi Aayah 5-10 kwa siku na ´Aqiydah baadhi ya masuala.

Hali kadhalika Hadiyth, kila siku Hadiyth. ´Aqiydah, Qur-aan na Hadiyth.

Kila siku kwa mfano Hadiyth moja, kila siku kwa mfano Aayah 5, na kila siku

baadhi ya masuala kuhusiana na ´Aqiydah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4702

17. Kafunga Sunnah Kisha Baadae Kaamua Kula

Swali:

Kuna kunuia kufunga Swawm ya Naafil, akala wala hakutimiza Swawm yake.

Je huku ni kuharibu ´amali na kunaingia katika Kauli Yake Allaah:

�!��� �ا أ� و �#"

“Wala msiviharibu vitendo vyenu.” (47.33)

´Allaamah al-Waswaabiy:

18

Imekuja katika Hadiyth, anasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Mwenye kufunga Swawm ya sunnah na msafiri wanakhiari, wakitaka

watafunga na wakitaka watakula."

Hakuna ubaya akila na lau angelitimiza Swawm yake ingelikuwa bora.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4701

18. Talaka Inatokana Na Alivyokusudia (Nia) Ya Mume

Swali:

Ipi hukumu mume kamwambia mke wake "Nikirudi kwenye ghala mimi si

mumewe tena", kisha akajirudi?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Hili itatokana na nia yake. Je, makusudio yake ni talaka kwa hili? Hili

itatokana na nia yake. Ikiwa makusudio yake ni talaka atakuwa kamtaliki. Na

ikiwa hakukusudia talaka, itakuwa si talaka. Kasema Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam):

"Vitendo vinategemea (vinalipwa kwa) nia na kila mtu atapata kwa mujibu wa

kile alichokusudia."

(Akimwambia) wewe si mke wangu, wewe si mke wangu mwema, au

nimridhiae. Itatokana na anachokusudia (nia yake).

19

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4700

19. Dada Anataka Kubadilisha Rangi Ya Nywele Zake Nyeusi

Swali:

Dada anauliza kuhusu kubadilisha rangi ya nywele nyeusi kichwani?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ikiwa nywele za kichwani ni nyeusi hakuhitajiki kuzibadili. Tayari ziko

kwenye asili yake rangi nyeusi. Haifai kupoteza muda na mali katika mambo

yasiyokuwa na faida. Zinazobadilishwa ni nywele zenye rangi nyeupe (mvi),

kwa kuwa zimebadilika zilikuwa nyeusi. Mtu anabalidisha kwa rangi yoyote

isipkuwa nyeusi tu. Rangi nyeusi haijuzu mtu kujibadilisha kwayo. Kutokana

na Hadiyth inayokataza hilo.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4698

20. Twawaaf Ya Kuaga Ni Wajibu Katika ´Umrah?

Swali:

20

Twawaaf ya kuaga katika ´Umrah ni wajibu au ni Mustahab12?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ni Mustahab. Yaani katika Hajj ni wajibu na katika ´Umrah ni Mustahab.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4237

21. Kuswali Swalah Za Sunanh Kabla Ya Swalah Ya Ijuma

Swali:

Je, inajuzu kwa mtu kuswali kabla ya Swalah ya Ijumaa Nawaafil kadhaa, na

je ni sahihi kuwa masuala haya yana khilafu kwa wanachuoni, na ipi kauli

yenye nguvu?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Kasema hili Shaykh Al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) katika taaliki yake katika

Subul-us-Salaam na pamoja na maneno ya Swan-´aan pia katika Subul-us-

Salaam kuwa: "Hakuna ubaya kwa Muislamu kuswali kabla ya Swalah ya Ijumaa

katika Naafil (sunnah) au Swalah ya Dhuhaa apendacho." Na Ijumaa huwa haina

Sunnah za kabla, bali Sunnah zake ni baada. Kwa hiyo anaweza kuswali kabla

ya Ijumaa Swalah za Naafil, kadiri na Allaah Atavyomuwezesha. Hakuna

ubaya In Shaa Allaah.

12 Imependekezwa

21

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=4238

22. Ewe Kaka Wa Kiislamu, Mtume Wako Akuamrisha Kufuga Ndevu

Swali:

Hukumu ya kunyoa ndevu au kutoa kitu humo?

´Allaamah al-Waaswabiy:

Kufuga ndevu ni wajibu. Na kuzinyoa au kutoa kitu humo ni Haramu. Kwa

kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Kuweni kinyume na washirikina; fugeni ndevu kwa wingi na punguzeni

masharubu." [Muttafaq, Ibn ´Umar]

Mtume (´alayhis-salaam) anakuamrisha kufuga ndevu. Wewe zifuge na wala

usitoe humo kitu. Na anakuamrisha kuacha masharubu, usiyafanye marefu

wala usiyatoe yote.

Na Allaah Anasema:

�اب أ��� أن �-�#�� ,01/ أو (-�#�� ,��+�ر ا��(� ()��'�ن � أ&%ه

“Basi nawatahadhari wanaokhalifu amri yake, usije ukawapatamsiba au

ikawapata adhabu chungu.” (24:63)

Usijiamini. Kumbuka yule mtu aliekuwa anakula kwa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) kwa mkono wake wakushoto, akamwambia "Kula kwa

22

mkono wakulia!", akasema "Siwezi". Akamwambia "Hutoweza kamwe."

Hakuna kilichomzuia ila ni kiburi. Hakika Mtume alimuamrisha kula kwa

mkono wakulia, akasema hapana siwezi. Akamuombea Du´aa kumwambia

"Hutoweza."

Wewe pia usijiamini. Akikuamrisha Allaah au Mtume Wake (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) basi tekeleza. Na akikukataza Allaah au Mtume Wake kwa

kitu, basi jitenge nacho.

�ا �1��, 30 �4���6�ل ,)�وه و&� إن و&� آ�4�� ا�% ;�(� ا��:�ب وا�:�ا هللا هللا

”Na anacho kupeni Mtume chukueni, na anachokukatazeni jiepusheni nacho.

Na mcheni Allaah. Hakika Allaah ni Mkali wa kuadhibu.” (59:07)

Chanzo: http://www.olamayemen.net

23. Nasaha Kwa Wale Wenye Kueneza Uvumi, Kusema Uongo Na

Usengenyaji

Swali:

Ipi nasaha zenu kwa mwenye kueneza uvumi, usengenyaji na uongo?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Nasaha kwetu na kwao ni kuwa tuchunge nafsi zetu ila kwa kheri tu. Na

tuchunge ndimi zetu daima na kila siku, uwe ulimi utasema kheri tu na

23

kutosema shari. Na walikuwa wakisema baadhi ya Salaf: "Sijaona kitu

kinachostahiki zaidi gereza kama ulimi." Ulimi ufungwe, kwa maana usisemi kitu

ila kwa mambo yanayofaa na kuruhusu. Mbali na hayo ni madhara matupu.

Nasaha kwetu na wengine ni kuhifadhi ulimi na kuacha dhambi hii kubwa;

usengenyaji, uvumi - ni kueneza ufisadi kati ya watu wawili au kundi kwa

kusema uongo, kutoa ushuhuda wa uongo, na maneno ya kijinga yasiyokuwa

na kheri, na filamu za uongo, yote haya hayajuzu kuwa na mtu mwenye

imani. Mtu awe na tahadhari kwayo na mtu ajishughulishe na mambo yenye

faida na yeye katika dunia yake, kaburi yake na Akhera yake kwa kuchunga

matendo ya ulimi.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2307

24. Kipigo Cha Kutia Adabu Kinachoruhusu

Swali:

Mwalimu anaweza kumpiga mwanafunzi kumuogopeshe ili arejee kufanya

jambo fulani au kuacha jambo fulani, je hili pia linangia katika tishio

(dhuluma)?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kipigo cha kumuweka (kumtia) adabu mwalimu mnasihiaji Mukhlisw kwa

mwanafunzi, kipigo cha kumuweka adabu kidogo halaumiwi kutokana na

maslahi kwake (mwanafunzi) na kumkinga na yatayomdhuru katika uhai

wake na Mustaqbal wake.

24

Pia kipigo cha baba kwa mtoto wake, na kwa mleaji - kama mtu mkubwa kwa

mdogo.

Hali kadhalika mume kwa mke wake katika baadhi ya hali kama ambavyo

Allaah Alivyotoa idhini hio. Hichi huitwa kipigo cha kuweka adabu na

kutengeneza. Ataekifanya hana makosa wala haingii katika kufanya dhuluma.

Lakini ikiwa atachupa mipaka katika kupiga, hapo atachukuliwa amefanya

dhuluma. Na ikiwa atapiga bila ya haki hata kama kitakuwa ni kipigo kidogo,

atachukuliwa ni dhalimu na siku ya Qiyaamah Allaah naye Atamlipiza.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2308

25. Hukumu Ya Kubaki Macho Baada Ya Swalah Ya ´Ishaa

Swali:

Je inajuzu kutoka kwenda kutembea na familia baada ya (Swalah ya) ´Ishaa?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kuwa macho baada ya ´Ishaa hairuhusiwi ila kwa msafiri au mwenye

kuswali, au mtafutaji elimu (mwanafunzi), au kusaidia kidogo katika mambo

ya Waislamu. Kama kwa mwenye wilaya katika wilaya ya Waislamu sawa

iwe kwa jumla au hususan. Mbali na hayo kuwa macho inadhuru na huenda

ikawa sababu ya kukosa Swalah ya Jamaa´ah, bali hata Swalah kwa wakati

wake.

25

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2309

26. Du´aa Nzuri Wakati Mwanamke Anataka Kuzaa

Swali:

Dada kutoka Ubeljiji anauliza. Ni Du´aa ipi ambayo mwanamke anaweza

kuomba wakati wa kuzaa?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Amuombe Allaah Amuweke wepesi. Na Du´aa iliyojumuisha mengi ni yeye

aseme:

"Allaahumma anta Rabbiy, Laa ilaaha illa Anta. Khalaqtaniy wa ana ´abduka, wa

anna ´alaa ahdika wa wa´adika mastatwa´atu. A´udhubika min-sharri maaswanaatu.

Abu-ulaka bi ne´ematika 'alayyah wa abu-u bidhambi, faghfirliy innahu laa yaghfiru

dhunuuba illa anta."

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2310

27. Wazazi Wanataka Binti Aende Kusoma Masomo Ya Mchanganyiko

Holland

26

Swali:

Dada kutoka Holland anauliza kuhusu masomo yake ambayo ni

mchanganyiko. Nidhamu kwao (Holland) hawezi mwanamke kuacha shule

ila mpaka aeneze miaka kumi na nane, na wazazi wake wanamuhimiza asome

kwa kuwa mji (serikali) itawakata pesa kiasi fulani ikiwa hatokamilisha

masomo yake mpaka aeneze miaka kumi na nane, afanye nini?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Tunawanasihi wazazi wake kuhama kutoka katika mji wa kikafiri na kwenda

katika mji wa Kiislamu. Wajitahidi sana wazazi wake mpaka aweze kuhama

kutoka katika mji wa kikafiri na kwenda katika mji wa Kiislamu. Isitoshe mji

wa Kiislamu achague mji ambao unatekeleza Shari´ah za Kiislamu na wala

kusewepo masomo ya mchanganyiko. Ama kusema ana udhuru, hana

udhuru:

"Hakuna utiifu kwa kiumbe katika kumuasi Muumba."

Haifai kwake kwenda katika masomo ambayo ni mchanganyiko katika mji

huu na mji huo, na ufisadi huko unakuwa wazi kabisa. Ahifadhi heshima

yake, dini yake na karama yake na akae nyumbani kwake. Na anaweza

kusoma kwa njia zenye usalama In Shaa Allaah.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2312

28. Imamu Na Muadhini Hawatakiwi Kuwa Ahl-ul-Bid´ah; Kama Suufiy,

Ash´ariy, Mu´taziliy, Jahmiy

Swali:

27

Muulizaji kutoka UK. Hakuna katika Msikiti wetu muadhini, vipi

tutamchangua muadhini na kwa kitu gani tutaangalia kwa mwenye kufaa

kutoa adhaana?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Kwa hakika ni kwamba ni lazima kwa waliohai kuwa na Msikiti, na ni lazima

kwa Msikiti kuwepo na Imamu na muadhini, ili watu wahifadhi wakati na

waswali Jamaa´ah.

Kwa Imamu anashurutishwa awe mtu mwenye ´Aqiydah sahihi na mjuzi. Na

muadhini anashurutishwa awe mtu mwenye ´Aqiydah sahihi, iliyo salama;

Asiwe Suufiy, Ash´ariy, Mu´taziliy, Jahmiy wala asiwe mwenye ´Aqiydah

(Itikadi) potofu.

Bali anatakiwa awe katika Manhaj ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah na awe na

´Aqiydah yao katika mlango wa Majina na Sifa za Allaah na yanayofanana na

hayo katika mambo makubwa kuhusu ´Aqiydah na Tawhiyd. Awe ni mtu

anaehifadhi wakati (wa Swalah), mtu anajua Fiqh - katika twahara yake,

usomaji wake, Swalah yake kiasi ambacho akikwama Imamu muadhini

asimame nafasi yake na aswalishe Jamaa´ah.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2314

29. Hukumu Ya Muislamu Kuwa Na Urafiki Na Makafiri

Swali:

28

Ipi hukumu ya kufanya urafiki na makafiri na ipi sura ya kufanya nao urafiki?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ufanyaji urafiki na makafiri unalioharamishwa ni kukubaliana na dini yao, na

kupenda dini yao. Akimpenda Muislamu Mkristo kwa Ukristo wake na

Myahudi kwa Uyahudi wake, na mwenye kuabudu moto kwa hilo basi hapo

atakuwa kama wao13. Na urafiki kama huu umeharamishwa.

3�<, �!0 & ����&�0� و&� (1

”Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika wao.”

(05:51)

Ama urafiki wa kikazi tu; kununua na kuuza, na kubadilishana mambo yenye

manufaa, na khidma makafiri kwa Waislamu. Hakika si katika urafiki hata

ikiwa Muislamu atafanya kazi kwa kafiri ili apate mshahara wake. Hakuna

ubaya. Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliweka mfanya kazi

siku ya kuhamia kwake kwenda Madiynah mtu ambaye alikuwa ni kafiri ili

amuoneshe njia ya kwenda Madiynah na akampa mshahara wake. Jambo hili

kuhusu urafiki linahitajia ufafanuzi.

Ataejenga nao urafiki na akawapenda kwa dini yao anakufuru. Kwa dalili ya

Aayah hii. Ama urafiki kwa maana kufanya nazo kazi katika jambo la maslahi

tu, hakuna ubaya na wala si katika jambo limelokatazwa.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2286

13 Kafiri

29

30. Kakasirika Sana Ramadhaan Akala, Nini Hukumu Yake?

Swali:

Kuna mtu alighadhibika mchana wa Ramadhaan ghadhabu (hasira) nyingi

akala, nini juu yake?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ni juu yake kulipa na ni juu yake kufanya tawbah. Kwa kuwa ghadhabu

haimfanyi mtu akala, lakini jambo kama hili ni nadra kupatikana kwa watu.

Kufanya jambo kama hili ni juu yake kutubia kwa Allaah na ni juu yake

kulipa siku moja kulipa siku hii.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2285

31. Ufafanuzi Wa Mwanamke Kulipa Swawm Zilizompita Katika Mwezi

Wa Ramadhaan

Swali:

Mume alikuwa karibu sana na mke wake mchana wa Ramadhaan akatokwa

na manii, nini juu yake?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ni juu yake kulipa. Kwa kuwa hakufikwa na hilo ila baada ya kufikiria sana.

Analazimika kulipa (siku hiyo) na hana juu yake kafara. Alipe siku moja.

30

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2284

32. Kijana Kila Anapotubia Anarudi Kufanya Dhambi Tena

Swali:

Mimi ni kijana nimefanya dhambi nikatubia, kisha nikatubia kwa Allaah

lakini nikarejea tena katika dhambi hii, ipi nasaha zako kwangu?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Rejea uombe tena Tawbah yakweli na wala usikate tamaa kwa Rahmah za

Allaah. Lakini rejea uombe Tawbah yakweli na uwe mkweli kwa Allaah

(´Azza wa Jalla). Atakusamehe Allaah dhambi yako na Ataifanya kuwa mema.

Lakini kuwa mkweli katika Tawbah yako na Allaah (Tabaaraka wa Ta´ala).

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2283

33. Kaswali Maghrib Msikitini Kisha Akaswali Tena Nyumbani Na Ahli

Zake

31

Swali:

Tuliswali Swalah ya Maghrib Jamaa´ah Msikitini kisha nikarejea nyumbani

wakaniomba ahli zangu niwaswalishe Jamaa´ah, ipi hukumu? Je huchukuliwa

kwangu hii kuwa ni Witr ilihali yajulikana kuwa hakuna Witr mbili katika

usiku mmoja?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ni sawa kwake kufanya hivyo, inajuzu. Kwa kuwa ni kwa ajili ya kuwafunza.

Muulizaji:

Je, huchukuliwa kwangu kuwa ni Witr?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Hapana si Witr. Mchana hakuna Witr.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2281

34. Kaoa Mwanamke Wa Ahl-ul-Kitaab Ambae Hataki Kuingia Katika

Uislamu

Swali:

32

Nimeoa mwanamke wa Ahl-ul-Kitaab14 kabla ya kuwa na msimamo, na

nimepewa Fatwa na baadhi ya wanafunzi kuwa na subira nae mpaka hapo

atapoingia katika Uislamu, na kumeshapita miaka mitatu na bado hajaingia

katika Uislamu na sina nae watoto, na kwa sasa niko na matatizo nae, ipi

nasaha zako?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Bila wasiwasi wowote Shari´ah inajuzisha kuoa mwanamke wa Ahl-ul-Kitaab

hata kama hatosilimu. Inajuzu kwake hilo. Kwa dalili ya Qur-aan. Ama

kuhusiana na matatizo hilo ni jambo la kawaida hata baina ya mume na mke

ambao ni Waislamu, na baina ya hawa Ahl-ul-Kitaab. Ni juu yake kuangalia

ambavyo anaweza kupatana nae ikiwa bado anataka kubakia nae, na ikiwa

matatizo yao haikuwezekana, itakuwa ni kama Alivyosema Allaah atampa

Allaah kila mmoja wasaa wake.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2280

35. Mgonjwa Mwenye Kutayamamu15 Na Sasa Kapatwa Na Janaba

Swali:

Mgonjwa ambaye hatawadhi kwa ajili ya maradhi na akapatwa na janaba

akatayamamu kisha akaswali, na baada ya siku nne akapona. Je ni lazima

kwake kuoga kutokana na janaba ilihali tayari kisha tayamamu?

14

Mayahudi au manaswara

15 Kuweka twahawa (Wudhuu) kwa kutumia udongo msafi

33

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni ndio. Ni lazima aoge kwa janaba. Ama Swalah kishaziswali kwa

kutayamamu kwa kuwa alikuwa hawezi kutumia maji. Swalah kishaziswali

na hatozilipa. Na janaba anatakiwa kuoga baada ya kuwa sasa anaweza

kutumia maji.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=551

36. Kwanini Ndoa Nyingi Za Ulaya Zina Matatizo Na Zinavunjika?

Swali:

Muulizaji kutoka Amerika, katika miji ya kimagharibi kuna matatizo mengi

baina ya mume na mke, mfano wa hilo kuna mtu alimuhama mke wake kwa

sababu ya kutomtii?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Matatizo ya watu hayatotatulika isipokuwa kwa Uislamu. Watu

wakishikamana na Uislamu watapata suluhu ya matatizo yao. Hakuna suluhu

isipokuwa ni Uislamu. Kuhusiana na Waislamu tunawanasihi warejee kwa

wanachuoni katika kutatua masuala mbali mbali mpaka hapo matatizo yao

yatatatulika kwa idhini ya Allaah.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=556

34

37. Mume Na Mke Wanaishi Ufaransa, Mume Anasema Waswali Kama

Wasafiri

Swali:

Muulizaji kutoka Ufaransa anauliza, mume wake anachelewesha Swalah ya

´Ishaa mpaka katikati ya usiku, na anasema kwa kuwa sisi tunaishi katika mji

wa kikafiri na anamwambia "Usiswali Rawaatib16 kwa kuwa sisi nia yetu ni

safari"

´Allaamah al-Waswaabiy:

Wewe ni mkazi, vipi utasema nia yetu ni safari? Wewe ni mkazi hivyo

unatakiwa kuswali Rawaatib. Wewe unasema nia yetu ni safari, je wewe

unafupisha pia Swalah za Rakaa nne (kama msafiri)?! Huu ni mgongano!

Kuswali (Swalah) za faradhi Rakaa nne kisha msiswali Rawaatib, kisha

unasema nia yetu ni safari. Wewe ni mkazi unatakiwa kuswali Swalah kama

wakazi. Ninawanasihi kuhamia katika mji wa Kiislamu, na kutafuta elimu ya

Kishari´ah (ya dini), na kuwa na ufahamu katika dini. Hii dunia haitodumu

kwenu, wala nyinyi hamtodumu katika dunia hii. Kimbilieni katika kutafuta

elimu ili muweze kumuabudu Allaah kwa Baswiyrah (elimu).

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=554

16 Swalah za Sunnah

35

38. Nasaha Ya Shaykh al-Waswaabiy Kwa Wenye Kutaka Kuoana

Swali:

Vipi inakuwa ndoa ya Kishari´ah?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Inakuwa kwa kutimiza masharti yake na nguzo zake. Ndoa ya Kishari´ah ina

sharti zake na ina nguzo zake. Zikitimia sharti na nguzo zake hapo ndo

inakuwa ya Kishari´ah (inayokubalika kidini). Ninamnasihi yule ambaye

anataka kuoa ajifunze kwanza Ahkaam za ndoa ili asije kutumbukia katika

jambo ambalo linaenda kinyume na Shari´ah ilihali naye hajui. Anasema

Allaah:

��ن �4% إن 104� �� �ا أھ< ا���@6�,

“Basi waulizeni wenye ukumbusho (wanachuoni) kama nyinyi hamjui.”

(16:43)

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=558

39. Aina Mbalimbali Za Sigara Za Hukumu Zake

Swali:

Hukmu ya kuvuta aina mbalimbali za sigara?

36

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kuwa yote haya ni katika maovu. Na kasema Allaah (´Azza wa Jalla)

katika kumsifu Mtume Wake Muhammad (´alayhis-Salaam):

ABC#(�ا ���� م و(+< ��� ا�"�#�ت و(+%

“Na anawahalalishia vizuri, na anawaharimishia viovu.” (07:157)

Na haya ni katika hayo.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=564

40. Hukumu Ya Kubadilisha Rangi Nywele Nyeusi

´Allaamah al-Waswaabiy:

Usibadili maumbile ya Allaah. Nywele nyeusi zinabaki asli yake nyeusi, kama

alivyoziumba Allaah. Zikibadilika, yaani zikiwa nyeupe huyu ndiye

anayebadili bila ya (rangi) nyeusi. (Kama anavyosema Mtume):

"Badilisheni, ila epukeni (kutumia rangi) nyeusi."

Na bora zaidi ni mtu kutumia hina.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=563

37

41. Baadhi Ya Sifa Zinazopasa Kuwa Na Mke Mtarajiwa

Swali:

Ipi nasaha zako kwa anayeoa kwa wale wasiyo katika jamii yake ambapo

anaishi, (mwanamke) kutoka magharibi kwa mfano?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Ndugu yetu anatakiwa kuoa mwanamke Muislamu, mwema, mtiifu, mwenye

msimamo, atakaekusaidia katika mambo ya dini yako.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=567

42. Nasaha Kwa Yule Aliemlaani Mke Wake

Swali:

Ipi hukumu kwa yule anaemlaani mke wake?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

38

"Kumlaani Muislamu ni kama kumuua." [Muttafaq, kutoka kwa Thaabit bin

Dhwahaa]

Tunamwambia yule anaemlaani mke wake atubie kwa Allaah na ajitahidi

kumbembeleza hata ikibidi kumpa mali mpaka amsamehe (mke wake).

Hakika kumlaani Muislamu ni katika madhambi makubwa.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=566

43. Inajuzu Kula Nyama Za Wakristo Na Mayahudi Wa Leo?

Swali:

Je inajuzu kula michinjo ya Mayahudi na Manaswara katika zama zetu hizi?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni ndio, ikiwa watachinja katika njia za Kishari´ah. Iwe kuchinja na si

kutumia mashine, kunyonga, kuipiga kwa kitu na mfano wa hayo. Na itajiwe

jina la Allaah (kabla ya kuchinja) na si jina la Yesu.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=572

39

44. Je Mkaaji Eda Haruhusiwi Kutoka Nyumbani Kabisa?

Swali:

Je kwa mwenye kukaa Eda kwa kufa mume wake anaweza kutoka nje ya

nyumba na mmoja katika jamaa zake?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Hakuna neno kukitokea haja (dharurah), kama kumzuru jirani yako, au katika

jamaa zako. Ila hutakiwi kubaki isipokuwa katika nyumba ya mume wako.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=570

45. Hukumu Ya Uchawi Katika Uislamu

Swali:

Mchawi akienda Msikitini na akasimama na mimi katika safu. Je, naweza

kukata safu?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni ndio, kwa kuwa mchawi ni kafiri na swalah yake ni batili. Ikijulikana

kama kweli ni mchawi anajulikana kwa watu huyu ni kafiri, alinganiwe

kuingia katika Uislamu na aambiwe kuomba Tawbah kutokana na dhambi

40

yake hio. Anatakiwa kutubia kabla ya kujiunga na safu kwa kuwa hata

akiswali Swalah yake ni batili mpaka aingie upya katika Uislamu. Kama

Alivyosema Allaah:

�راG0 �0�ه ھ#�ء &�I, >� �ا &� �� وK�&0� إ�� &�

“Na tutayaendea yale waliyoyatenda katika vitendo vyao, tuvifanye kama

mavumbi yaliyo tawanyika.” (25:23)

Matendo yake atayafanya Allaah siku ya Qiyaamah mavumbi yaliyo

tawanyika - Swalah zake, Swawm zake, Swadaaqah, Hajj, ´Umrah na ´amali

zingine zote njema hatozikubali Allaah kwa kuwa ni kafiri. Kwanza

anatakiwa kukufuru Mashaytwaan na amuamini Allaah. Kama Alivyosema

Allaah:

�:, M� �&N)ت و�O�"�� %'!) ��, PQ�ا �& �; ��� K� �#�� ا�% R��6 م ��� وهللا�-'����%وة ا���:� ا TU�16ا

“Kwani Uongofu umekwisha pambanuka na upotofu. Basi anayemkataa

Shaytwaan na akamuamini Allaah bila ya shaka amekamata kishikio

madhubuti kisichovunjika. Na Allaah ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.”

(2:256)

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=569

46. Kubadilisha Nywele Kwa Kuweka Rangi Nyeusi

41

Swali:

Inajuzu kwa mke wangu kubadilisha rangi ya nywele zake (kwa kuweka

rangi) nyeusi? Yaani nywele zake ni nyeupe, anauliza inajuzu kubadili kwa

kuweka rangi nyeusi?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Jibu ni kwamba haijuzu. Nywele ambazo ni nyeupe unazibadili kwa rangi

yoyote isipokuwa tu rangi nyeusi. Kama ilivyokuja katika Hadiyth:

"Zibadilisheni, na epukeni (rangi) nyeusi."

Na hili ni kwa wanamume na wanawake.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=574

47. Swawm Za Ramadhaan Huwekwa Nia Mara Moja Au Kila Siku?

Swali:

Swawm ya Ramadhaan mtu huweka nia mara moja au ni lazima kuweka upya

nia kila siku? Na je nia inakuwa na saa maalumu au inakuwa wakati wowote

wa usiku?

´Allaamah al-Waswaabiy:

42

Ni wajibu kuweka upya nia kila siku kutokana na kauli sahihi (yenye nguvu)

ya wanachuoni. Kwa kuwa kila siku moja huchukuliwa ni tendo la kivyake na

inahitajia nia yake.

Ama swali lako la pili, ni katika wakati wowote wa usiku unaweza kuweka

nia.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=1718

48. Je Salaf Waliwahi Kutofautiana Kunako ´Aqiydah?

Swali:

Wanasema baadhi ya watu kwamba Salaf walitofautiana katika baadhi ya

masuala ya ´Aqiydah, kwa mfano "Je alimuona Mtume wa Allaah ( 3�� �� هللا V

�� Mola Wake Usiku wa Mi´iraaj?", na kuwa hili lilitokea zama za (و6

Maswahabah. Je, maneno haya ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hawakutofautiana katika masuala ya ´Aqiydah ewe ndugu. Masuala ya

´Aqiydah ni kuonekana Allaah Peponi. Ni kwamba waumini watamuona

Peponi. Ama duniani hakuna yeyote ataemuona. Hakuna yeyote ataemuona,

hata Mtume (´alayhis-Salaam) hakumuona, wala hakumuona Muusa (´alayhis-

Salaam) . Alisema:

P� K�ل رب أر�P أ��% إK T���ل �� �%ا

"Nionyeshe nikutazame." Allaah Akasema: "Hutoniona." (07:143)

43

Hili ni hapa duniani. Hawana tofauti katika ´Aqiydah. Hii ni tofauti je,

alimuona yeyote duniani au haikutokea. Hii sio tofauti katika ´Aqiydah.

Kuonekana Allaah Peponi hili wamekubaliana wote Ahl-us-Sunnah wal-

Jamaa´ah wala hawatofautiani.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2750

49. Baadhi Ya Vitabu Bora Vilivyozungumzia Siyrah Ya Mtume (´alayhis-

Salaam)

Swali:

Ni kitabu kipi bora kilichopokea sifa za Mtume ( ����3 و6 �� هللا V)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Vitabu vipo vingi ewe ndugu. Ni vitabu vya Siyrah. Vipo vingi, na miongoni

mwavyo ni "Zaad-il-Ma´aad" cha Ibnul Qayyim, "Siyrat-un-Nabiy (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam)" cha Ibnu Hishaam mukhtasari yake. Hadiyth

sahihi zilizopokelewa kuzungumzia Siyrah ya Mtume ( ����3 و6 �� هللا V).

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2749

44

50. Kitabu Cha Majina Ya Mtume (´alayhis-Salaam)

Swali:

Ni kitabu kipi ulichotaja ambacho kilicho na majina ya Mtume ( ��V 3�� هللا

�� ?(و6

´Allaamah al-Fawzaan:

“Jalaal-ul-Afhaam was-Swalaatu was-Salaam ´aala Khayri an-Naam” cha

Ibnul Qayyim.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2754

51. Kuwaweka Wazazi Katika Nyumba Ya Wazee

´Allaamah al-Fawzaan:

Kulinda udugu kunaleta athari duniani na Akhera. Na ikiwa kuulinda udugu

kunapelekea kuishi kwa muda mrefu, na kunapelekea ukunjufu wa ziriki,

hivyo wema kwa wazazi itakuwa aula zaidi kwa kuwa wao wako karibu zaidi

kuliko vyote.

Kuwatendea wema wazazi kunapelekea Allaah Anapanua maisha yako na

Anakurefushia umri wako. Na kutowatendea haki kunapelekea kuwa na umri

45

mfupi na ugumu wa kupata riziki. Kama ambavyo kuwatendea wema

tunapelekea katika urefu wa umri na riziki kuongezeka. Na jazaa (malipo) ni

sawa na alivyotenda mtu.

�ن و �WIون �إ &� 104� ���

”Wala hamtalipwa ila yale mliyokuwa mkiyatenda.” (36:54)

Unafikiria nini kwa ambacho kimezoeleka leo, kwa masikitiko makubwa

katika jamii za Kiislamu wakati wazazi wanapokuwa wazee wanatupwa

katika nyumba za Ihsaan, au nyumba za wazee kama wanavyoziita. Mtoto

ndie anaefanya hivyo anawaweka wazazi wake au mmoja wao katika nyumba

za wazee. Utafikiria kana kwamba si watoto wake, au utafikiria ya kwamba ni

wazazi wa watu hawa wanaofanya kazi katika nyumba za wazee. Yaa

Subhaana Allaah! Je, (anaefanya hivi) ni mtu kweli au ni mnyama?! Laa

hawlah wala Quwwata illa biLlaah. Huu ni katika ukosefu mkubwa wa

adabu. Hili halifanywi na yule ambaye kwenye moyo wake kuna khofu kwa

Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).

Ungelijisikiaje lau mtoto wako angelikufanyia kitendo hiki?! Unapo zeeka na

kuwa mgonjwa wanakuchukua na kukuweka katika nyumba ya wazee.

Ungelijisikiaje? Ungeliwakasirikiaje? Na dhambi ipi ambayo mtoto wako

angeliibeba? Kwanini wewe unaomba haki yako na wewe hutimizi haki

ambayo iko juu yako?! Amche Allaah kila Muislamu.

Ukosefu wa adabu kwa wazazi umeenea sana katika zama hizi, nyoyo

zimekuwa ngumu na wandugu kufarakana. Tumejiwa na maadui wa

magharibi na makafiri; ambao hawana familia wala nyumba isipokuwa

nyumba zao ni kama nyumba za minyama. Nyumbani kwao wanaishi

wenyewe au na mbwa. Ama kukuta anaishi na wazazi wake, na watoto wake,

na ndugu zake, hapana! Hili halipo katika miji mingi ya kikafiri.

Jambo la kusikitisha ni kwamba baadhi ya Waislamu leo wanataka kuwaiga.

Wanataka kuwatupa wazazi wao au mmoja wao katika manyumba ya wazee

na ili wawe zao huru. Na kama ana aina fulani ya hisia huenda akaja siku ya

Idi kuwasalimia, kuwazuru tu. Au baada ya siku ndo anawapitia na

kuwasalimia. Na anachukulia kuwa hii ndo haki kubwa alionayo juu yao.

46

Ni juu ya Muislamu kutanabahi na kumcha Allaah; na ajue kuwa anachofanya

(anachotendea mwengine) naye atatendewa. Na atalipwa kwa kitendo chake,

na asitangulize katika haki za wazazi wawili chochote isipokuwa tu utiifu

(haki) za Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Ikiwa anataka ujira na anataka

thawabu asitangulize chochote katika matendo isipokuwa haki za wazazi,

isipokuwa tu haki za Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).

Na kwa haya, namuomba Allaah (Jalla wa ´Alaa) kwa Majina Yake Mazuri na

Sifa Zake kuu Awaongoze watoto na vizazi vya Waislamu. Na tunamuomba

Awarudishe Waislamu katika Uislamu wao kwa sura nzuri inayotakikana. Na

Awafanye Waislamu wawe ni wenye kupendana na Ayafanye manyumba yao

kuwa mazuri. Tunamuomba Allaah vile vile Awaepushe na kujifananisha na

makafiri na wanafiki, na wale ambao wamekata na kuvunja udugu wakawa

kama minyama au wakapotea zaidi. Wa laa hawla wa Quwwata illa biLlaah.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=e91nM8dW-10

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.