25
Karibuni katika teknologi a ya BIOGAS By Fisherman

Presentation on Biogas Technology

  • Upload
    mvuvi

  • View
    92

  • Download
    23

Embed Size (px)

Citation preview

Karibuni katika

teknologia ya

BIOGASBy Fisherman

Biogas Ni nini?• Ni gesi inayotokana na

uchachukaji wa vinyesi vya wanyama au masalia ya Mashambani / jikoni katika mazingira yasiyo na hewa ya Oksijeni (anaerobic digestion).

HAKUNA HEWA YA OKSIJENI

Kinyesi + maji/mkojo(Wanga + mafuta + protini + maji)

Biogesi Mbolea tope chujio

Uchachukaji/uvundaji Pasipo na hewa

Post treatment Mimea

Nishati

Bio-gas kama Teknolojia ilitoka wapi?

• Teknolojia ya biogas imekuwepo duniani kwa muda mrefu sana. Iliingia nchini Tanzania kupitia shirika la SIDO takribani miaka ya 1970 kutokea nchini India. Kwa wakati huu India walikuwa wanatumia muundo wa pipa linaloelea (Floating Drum) na ndiyo muundo SIDO walioeneza hapa nchini.

Historia inaendelea…• Muundo huu ulionekana kuwa na changamoto

ya pipa la chuma kupata kutu kutoboka na kumwongezea mteja gharama kubwa ya ukarabati.

• Baada ya kuzaliwa kwa Tasisi ya CAMARTEC (Centre of Agriculture Mechanization And Rural TEChnology-1983) Wataalamu walifanyia marekebisho muundo wa mtambo wa kichina uitwao “Chinese Fixed Dome” na hivyo kuzalisha aina ya mtambo uitwao “ CAMARTEC FIXED DOME PLANT”.

Miaka michache baadayemaboresho yalifanyika tenakatika harakati za kupunguzagharama za ujenzi wa mitambona kuzalisha aina mpya inaoitwa“ MODIFIED CAMARTEC DOME -

MCD”. Aina hii ya mtambo ambayondiyo tunayoineza kwa sasainaweza kupatikana kwa ujazowa kiwango cha 4m3, 6m3, 9m3

na 13m3 na rahisi kujenga.

Historia inaendelea…

JINSI MTAMBO ULIVYO KWA NDANI

0-line

LSL

HSL

Historia inaendelea…• Kwa kushirikiana na Tasisi ya SNV mwaka 2011

Watafiti walibuni aina ya mtambo unaostawi maeneo ya wafugaji yaliyokithiri kwa ukame. Mtambo huu unaitwa, “SOLID STATE DIGESTER- SSD”. Mitambo hii imepata umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi kutokana na ubora wake katika uzalishaji wa gesi. Juhudi hizi zimetoa fursa kwa kila Mtanzania (mfugaji) mwenye nia kujenga Mtambo unaoendana na mazingira anamoishi.

Chemba Ya Kukorogea

CHEMBA YA KUINGIZIA MBOLEA

Chemba ya

majaribio

Chemba Mtanuko

Mdomo wa kutoleambolea

Nini kinachosababisha bio-gas iwake?• Kinachoiwezeshesha bio-gas kuwaka ni

gesi aina ya “Methen”ambayo ndiyo nyingi katika aina tatu za gesi zinazozaliwa wakati wa uchakachukaji.

- Methene (CH4) ………….…70 – 75%

- Hydrogen Sulphide (H2S) ..1 – 5% - Carbon Dioxide (CO2)…..25 – 30%

SIFA ZA GESI-VUNDE(BIOGAS)

• Haina moshi• Hailipuki kama ikivuja ndani ya chumba• Ina nguvu ya kupika chakula kwa muda

mfupi• Haisababishi masizi kwenye sufuria• Inamwondolea mteja gharama za

kununua gesi kila wakati.

Vigezo Vinavyompa Fursa Mteja Kujenga Mtambo Wa Bio-gas.

•MIFUGO•MAJI•KIPATO•NIA

MATUMIZI YA BIOGAS• Kupikia jikoni• Kuwasha taa• Kupoozeshea

chakula(FRIJI)• Kuendesha

mitambo.

FAIDA ZINGINE ZA TEKNOLOGIA YA BIO-GAS

Utunzaji wa mazingira na kupunguza uharibifu wa utando ulioko angani

“ozone layer”

Jinsi miyele ya jua inavyopozwa na utando angani (Ozone layer)

Mbinu za kupunguza gharama za ujenzi.

• Ruzuku kutoka kwa mfadhili (200,000)• Kuchagua aina ya mtambo mtambo unaolingana na uwezo

wa familia.• Kutafuta taarifa za upatikanaji wa vifaa.• Kuunganisha wateja kwa baadhi ya vifaa, mf. Chicken wire,

wire mersh, mchanga, nk.• Mafunzo ya mafundi wapatikanao maeneo husika. (Hadi

sasa tuna mafundi 56 ambao wameunda vikundi 11 vya ujasiriamali- BCEs)

• Kuunganisha wateja na tasisi za kutoa mikopo, mf. SACCOS, BANK (MRCB-Mwanga).

KARIBU KWENYE SEHEMU YA PILI YA KILIMO HAI

NA TOPE-CHUJIO

TOPE CHUJIO NININI??

”Ni mabaki ya Samadi

yanayopatikana yakiwa katika hali ya tope/uji mzito baada ya mtambo wa bio-gas kuzalisha gesi”.

UBORA WA TOPE CHUJIO

•Naitrojeni 35 – 50%•Fosforas (P205) 18 – 25%•Potasiam (K20)– 15 – 20%

N P K

Mahindi ambayo hayakuwekwa Tope-chujio Mahindi ambayo yaliyowekwa Tope-chujio

CHANGAMOTO ZA TOPE-CHUJIO

• Upatikanaji wake si rahisi inapohitajika.• Inapokuwa katika hali ya uji-uji ina usumbufu

katika kusafirisha kwenda shambani.• Baadhi ya wafugaji wanajiskia kinyaa

kutumia Tope-chujio lililounganishwa na choo.

• Hakuna tekinolojia ya kutosha iliyopo kuhusu matumizi bora ya tope-chujio.

CHANGAMOTO ZA MRADI WA BIOGAS kwa ujumla.

• Baadh ya Wateja kushindwa kununua vifaa vinavyohitajika katika ujenzi kwa wakati.

• Baadhi ya wateja kushindwa kurejesha mikopo yao kwa taasisi husuka. Mf. Mwanga Bank(MRCB)

• Wateja wengi kutokuwa na taarifa za kuwepo kwa mradi katika maeneo yao (lack of Awareness).

• Kupunguzwa kwa ruzuku kutoka kwa Mfadhili.• Ukosefu wa elimu ya kutosha kuhusu matumizi sahihi

ya tope-chujio.• Mwitikio wa serikali ni mdogo kiushirikiano.

Asanteni na Karibuni tena.

Biogas kwa maisha bora.