RIPOTI KUU YA MWAKA YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA WA FEDHA ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI 2017
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Barabara ya Samora, S.L.P. 9080, Dar es Salaam.Simu ya Upepo: ‘Ukaguzi’ Simu: 255(022)2115157/8, Tarakishi: 255(022)2117527,
Barua pepe: [email protected], tovuti: www.nao.go.tz
Kwa Majibu Tafadhali Nukuu Kumb.Na. FA 27/249/01/2016/2017 31 Machi 2018
Mh. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ikulu, S.L.P. 9120, 1 Barabara ya Barack Obama, 11400 DAR ES SALAAM. Yah: Kuwasilisha Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kuhusu Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kwa Mwaka Ulioishia Tarehe 30 Juni, 2017 Kwa mujibu wa Ibara ya 143 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (kama ilivyorekebishwa) na Kifungu cha 34 (1)(c) cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na.11 ya mwaka 2008 (kama ilivyorekebishwa), ninawasilisha kwako ripoti ya saba inayohusu miradi ya maendeleo kwa mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2017. Nawasilisha.
Prof. Mussa J. Assad MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 i
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Ilianzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 143 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) Madaraka na wajibu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali vimeelezwa kwenye Ibara ya 143 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (kama ilivyorekebishwa) na kufafanuliwa zaidi katika Kifungu cha 10(1) cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na.11 ya mwaka 2008 (kama ilivyorekebishwa) pamoja na Kanuni za Ukaguzi wa Umma za mwaka 2009. Dira Kuwa Taasisi ya Hali ya Juu Katika Ukaguzi wa Sekta ya Umma.
Dhamira Kutoa Huduma ya Ukaguzi wa Hesabu Yenye Tija ili Kuimarisha Uwajibikaji na Thamani ya Fedha Katika Kukusanya na Kutumia Rasilimali za Umma.
Katika kutoa huduma zenye ubora, ofisi hii inaongozwa na vigezo vya msingi vifuatavyo:
Uadilifu: Sisi ni asasi adilifu inayotoa huduma kwa namna isiyo na upendeleo.
Ubora: Sisi ni weledi tunaotoa huduma zenye ubora kwa kuzingatia viwango kubalifu vya ukaguzi.
Uaminifu: Tunazingatia na kudumisha kiwango cha juu cha uaminifu na kuzingatia utawala wa sheria.
Kuwalenga watu: Tunamakinikia zaidi matarajio ya wadau wetu kwa kujenga utamaduni mzuri wa kuhudumia mteja na kuwa na watumishi wataalamu na wenye motisha ya kazi.
Uvumbuzi: Sisi ni asasi ambayo wakati wote inahamasisha utamaduni wa kupokea na kuendeleza mawazo mapya kutoka ndani na nje ya asasi.
Matumizi bora ya rasilimali: Sisi ni asasi inayothamini na kutumia rasilimali za umma ilizokabidhiwa kwa umakini mkubwa.
Tunatimiza haya kwa kufanya yafuatayo:-
Kuchangia katika matumizi bora ya fedha za umma kwa kuhakikisha kwamba wakaguliwa wetu wanawajibika kutunza rasilimali walizokabidhiwa;
Kusaidia kuimarisha ubora wa utoaji huduma kwa kuchangia ubunifu kwa matumizi bora ya rasilimali za umma;
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 ii
Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wadau wetu kuhusu mapungufu katika uendeshaji wa shughuli zao;
Kuwahusisha wadau wetu katika mfumo wa ukaguzi; na
Kuwapa wakaguzi nyenzo za kufanya kazi ambazo zitaimarisha uhuru wa ofisi ya ukaguzi.
© Kwa mujibu wa Kifungu cha 39 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na. 11 ya mwaka 2008 (ilivyorekebishwa), Ripoti hii imekusudiwa kwa matumizi ya Mamlaka za Serikali. Hata hivyo, mara baada ya kupokelewa na Spika na kuwasilishwa Bungeni, ripoti hii huwa ni kumbukumbu ya umma na usambazaji wake hauwezi kuzuiwa.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 iii
Yaliyomo Dira....... ................................................................................... i Dhamira ..................................................................................... i Orodha ya Majedwali ...................................................................... v Vifupisho ................................................................................... vi Dibaji .....................................................................................viii Shukrani ................................................................................... x i. Utangulizi ............................................................................... xii ii. Hoja Muhimu Zilizojitokeza Wakati Wa Ukaguzi ................................ xii iii. Utekelezaji wa Mapendekezo ya Ukaguzi Yatokanayo na Ripoti za Kaguzi za
Miaka Iliyopita .................................................................... xv iv. Mwelekeo wa Hati za Ukaguzi Zilizotolewa..................................... xvi SURA YA KWANZA .......................................................................... 1 USULI NA TAARIFA ZA UJUMLA ............................................................ 1 1.0 Utangulizi .......................................................................... 1 1.1 Mamlaka na Umuhimu wa Ukaguzi ................................................ 1 1.2 Wajibu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali .................... 2 1.3 Muundo wa Kazi za Ukaguzi katika Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi .................... 2 1.4 Mawanda na Viwango vya Ukaguzi Vinavyotumika ............................... 3 1.5 Wajibu wa Maafisa Masuuli ........................................................ 4 SURA YA PILI ............................................................................... 5 HALI YA UTEKELEZAJI WA MAPENDEKEZO YA RIPOTI ZA KAGUZI ZA MIAKA YA NYUMA . 5 2.0 Utangulizi .......................................................................... 5 2.1 Hali ya Utekelezaji wa Mapendekezo ya Kaguzi Zilizopita ....................... 5 SURA YA TATU ............................................................................. 8 AINA NA MWENENDO WA HATI ZA UKAGUZI ZILIZOTOLEWA ............................. 8 3.0 Utangulizi .......................................................................... 8 3.1 Aina za Hati za Ukaguzi ........................................................... 9 3.2 Mwelekeo wa Hati za Ukaguzi .................................................... 11 3.3 Vigezo Vilivyosababisha Kutoa Hati Za Mashaka Na Hati Zisidhoridhisha ....... 12 SURA YA NNE ............................................................................. 13 UTENDAJI WA KIFEDHA WA MIRADI ...................................................... 13 4.0 Utangulizi ......................................................................... 13 4.1 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) ............................. 13 4.2 Fedha za Mfuko wa Afya (HBF) ................................................... 15 4.3 Mfuko wa Barabara ............................................................... 17 4.4 Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Awamu ya Tatu – Mpango Uhaulishaji wa Fedha
kwa Kaya Maskini ................................................................. 19 4.5 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP) ............................... 20 4.6 Miradi Mingine .................................................................... 23
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 iv
SURA YA TANO ............................................................................ 24 MUHTASARI WA MATOKEO YA UKAGUZI .................................................. 24 5.0 Utangulizi ......................................................................... 24 5.1 Masuala ya Usimamizi wa Fedha na Bajeti ...................................... 24 5.2 Masuala Yanayohusu Manunuzi na Usimamizi wa Mikataba ..................... 27 5.3 Utekelezaji wa Miradi ............................................................ 29 SURA YA SITA ............................................................................. 30 HITIMISHO NA MAPENDEKEZO ............................................................ 30 6.0 Utangulizi ......................................................................... 30 6.1 Hitimisho la Jumla ................................................................ 30 6.2 Mapendekezo ya Jumla ........................................................... 32 VIAMBATISHO ............................................................................. 35
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 v
Orodha ya Majedwali
Jedwali Na. 1: Utekelezaji wa Mapendekezo Katika Ripoti za Kaguzi za Miaka ya Nyuma ...................................................................................... 6
Jedwali Na 2: Muhtasari wa Hati za Ukaguzi Zilizotolewa .............................. 9 Jedwali Na. 3: Mwelekeo wa hoja za ukaguzi ............................................ 12 Jedwali Na. 4: Jumla ya Fedha za Mpango wa Maendeleo Sekta ya Kilimo
Zilizopokelewa na Kuhamishwa ....................................................... 14 Jedwali Na. 5: Jumla ya Fedha Zilizokusanywa Kutumwa Mfuko wa Uchangiaji wa
Afya ........................................................................................ 16 Jedwali Na. 6: Fedha zilizotumwa kwa Watekelezaji wa Miradi ...................... 17 Jedwali Na. 7: Mwenendo wa Makusanyo ya mapato kwa Miaka ...................... 18 Jedwali Na. 8: Ufadhili wa Mfuko Mradi wa Maendeleo ya Jamii ..................... 20 Jedwali Na. 9: Vyanzo vya Fedha Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji ....... 21 Jedwali Na. 10: Ufadhili ...................................................................... 22
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 vi
Vifupisho
AfDB Benki ya Afrika ya Maendeleo Afrika
AFROSAI-E Umoja wa Taasisi za ukaguzi Afrika Zinazozungumza Kiingereza
ASDP Programu ya Maendeleo katika Sekta ya Kilimo
CCHP Mpango Kabambe wa Afya
DADPs Mipango ya Maendeleo ya Kilimo katika Wilaya
DFID Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Uingereza
DK Dola za Kimarekani
GIZ Shirika la Kijamii la Kijerumani la Ushirikiano wa Kimataifa
Global Fund Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na Malaria, UKIMWI na Kifua Kikuu
HBF Mfuko wa Uchangiaji wa Afya
IDA Shirika la Maendeleo la Kimataifa
IFAC Shirikisho la Kimataifa la Wahasibu na Wakaguzi
IFAD Mfuko wa Kimataifa kwa Maedeleo ya Kilimo
INTOSAI Shirika la Kimataifa la Asasi Kuu za Ukaguzi
ISSAIs Viwango vya Kimataifa vya Ukaguzi vya Ofisi za Ukaguzi wa Umma
JICA Shirika la Maendeleo la Nchi ya Japani
JMT Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
LAAC Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa
LGFM Randama ya Fedha ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa
NAOT Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi
NWIF Mfuko wa Uwekezaji wa Maji Kitaifa
OPEC Umoja wa Nchi Zinazozalisha Mafuta
PAA Eneo la Mamlaka la Mradi
PAC Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali
RSSP Programu ya Msaada katika Sekta ya Barabara
SDR Haki ya kutoa fedha
Sh. Shilingi za Kitanzania
SNAO Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Sweden
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 vii
TAMISEMI Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
TANROADS Wakala wa Barabara Tanzania
TASAF Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
TEMESA Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania
TPRS Mpango wa kupunguza Umaskini Tanazania
TRA Mamlaka ya Mapato Tanzania
TSSP Programu ya Msaada wa Sekta ya Usafiri
UN Umoja wa Mataifa
UNDP Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa
UNICEF Sherika la Umoja wa Mataifa Linalohudumia Watoto
USAID Shirika la Misaada la Watu wa Marekani
VAT Kodi ya Ongezeko la Thamani
WB Benki ya Dunia
WSDP Programu ya Maendeleo katika Sekta ya Maji
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 viii
Dibaji Taarifa hii ni majumuisho ya matokeo ya kaguzi za miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017. Hii ni taarifa ya saba ya miradi ya maendeleo ambayo inajumuisha miradi mikubwa minne inayofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) na Wahisani wa Maendeleo kupitia
mifuko ya pamoja na Mfuko wa Barabara ambao huchangiwa na chanzo cha mapato ya ndani yatokanayo na kodi ya mafuta. Miradi minne ya maendeleo ambayo huchangiwa kwa pamoja ni Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP), Mfuko wa Uchangiaji wa Afya (HBF), Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), na Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP). Aidha, tumekagua miradi mingine inayofadhiliwa na Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Africa, Wakala wa Umoja wa Mataifa (UN), na makubaliano ya kifedha baina ya nchi mbalimbali.
Ripoti hii ya ukaguzi itawasilishwa kwa Mheshimiwa Rais kwa mujibu wa Ibara ya 143 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (kama ilivyorekebishwa) na Kifungu 34(1) & (2) cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na.11 ya mwaka 2008. Inajumuisha taarifa muhimu zilizo katika ripoti za ukaguzi walizopewa menejimenti za watekeleza miradi. Ni matarajio yangu kuwa ripoti hii itawasaidia wadau wa miradi ya maendeleo kuweza kutathimini kama fedha zimetumika kwa malengo yaliyokusudiwa. Pia itasaidia kutathmini mchango katika maendeleo ya jamii kiuchumi. Aidha, itasaidia kutathmini kama thamani ya fedha imepatikana.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 ix
Kwa mujibu wa Ibara ya 143(2)(c)(4) ya Katiba ya JMT ya mwaka 1977 (kama ilivyorekebishwa), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anatakiwa, angalau mara moja kila mwaka, kufanya ukaguzi na kutoa taarifa ya ukaguzi wa hesabu hizo kwa Rais wa JMT ambaye ataiwasilisha bungeni. Aidha, uhuru wa ofisi yangu umeimarika katika kutimiza jukumu lake la kikatiba kutokana na kutungwa kwa Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na.11 ya mwaka 2008 na Kanuni zake za mwaka 2009. Hata hivyo, jitihada zinahitajika ili kuboresha rasilimali za kufanyia kazi ili kunisaidia kufanya vyema katika kutekeleza majukumu na wajibu wangu wa kikatiba.
Natarajia kuwa Serikali, Bunge, washirika wa maendeleo na umma kwa ujumla wataichukulia taarifa hii kuwa ni muhimu katika kuelewa jinsi maafisa masuuli wanavyosimamia miradi ya maendeleo na namna mafanikio katika miradi ya maendeleo yanavyosaidia katika kutatua matatizo yanayowakabili Watanzania. Hivyo, ili kuboresha ripoti hii siku zijazo nitashukuru kupata maoni kutoka kwa jamii na watumiaji wengine wa taarifa hii kwa muda muafaka.
Prof. Mussa Juma Assad MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI ___________________________________________ Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Dar es Salaam, Machi, 2018
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 x
Shukrani
Natoa shukrani za dhati kwa wadau wetu waliotuwezesha katika kutuwezesha kutimiza majukumu yetu ya kikatiba. Nao ni pamoja na Bunge na kamati zake, hususani Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Bunge ya Bajeti, Mlipaji Mkuu wa Serikali, Maafisa Masuuli wote wa wizara, mashirika ya umma na tawala za mikoa ambao wanasimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na walipa kodi. Napenda kutoa shukrani zangu kwa watumishi wa ofisi yangu kwa kujitolea na kujituma katika kutimiza majukumu yetu ya kikatiba. Ni matumaini yangu kuwa wataendelea kutoa huduma ya kutosha na yenye ufanisi katika ukaguzi ili kuongeza uwazi na uwajibikaji katika ukusanyaji na matumizi ya rasilimali za umma.
Aidha, natoa shukrani zangu za dhati kwa wafadhili, hasa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Shirika la Kimataifa ya Maendeleo ya Uingereza (DFID), Shirika la Kimataifa la Kijerumani la Ushirikiano wa Kimataifa (GIZ), Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ya Sweden (SNAO), Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID), Benki ya Dunia (WB) na washirika wetu wengine ambao wametoa mchango mkubwa katika ofisi yangu na kuzifanya kazi za ukaguzi ziwe za kitaalam zaidi kwa kutoa fedha kwa ajili ya kujenga uwezo kwa wafanyakazi na kutoa vitendea kazi. Wakati nawasilisha taarifa zangu za ukaguzi mwezi Machi 2017, Mheshimiwa Rais alimuagiza Waziri Mkuu kuhakikisha kwamba naziwasilisha taarifa hizo pia kwa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa na Maafisa Tawala wa Mikoa. Kutokana na juhudi za Waziri Mkuu mkutano uliandaliwa na niliwasilisha taarifa hizo kama ilivyoagizwa.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 xi
Aidha, kutokana na mkutano huo nimeona kuwa kuna juhudi za makusudi zinazofanywa na watekeleza miradi ambapo ufuatiliaji wa mapendekezo yaliyomo kwenye taarifa zangu umeboreka. Mwisho, natoa shukrani zangu kwa mchapishaji wa taarifa hii kwa kuniwezesha kuitoa kwa wakati.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 xii
MUHTASARI WA MAMBO MUHIMU
i. Utangulizi Sehemu hii ya ripoti inatoa maelezo ya jumla ya matokeo ya ukaguzi wa taarifa za hesabu yanayotakiwa kuzingatiwa kwa umakini na Serikali, Bunge, Maafisa Masuuli na Wadau wengine wa miradi ya maendeleo.
Taarifa hii inajumuisha muhtasari wa mambo muhimu yaliyotokana na ukaguzi ambapo taarifa zake kwa ujumla zimeelezwa katika barua ya mapungufu na katika taarifa ya ukaguzi inapelekwa kwa watekelezaji wa miradi. Katika ripoti hii tumewasilisha mambo ambayo tumeona ni ya muhimu kuletwa kwa Serikali, wasimamizi wa taasisi pamoja na Umma.
Aidha, nimegundua mapungufu katika masuala ya usimamizi wa fedha na bajeti, mifumo ya ndani, na usimamizi wa kanuni na sheria. Mapungufu haya yanahitaji kufanyiwa kazi na watekeleza miradi ili kuboresha utendaji katika siku zijazo.
ii. Hoja Muhimu Zilizojitokeza Wakati wa Ukaguzi Aya hii inaelezea hoja muhimu zilizojitokeza kwenye ukaguzi zinazohitaji kufanyiwa kazi kipekee kama mapendekezo yanavyoonesha katika aya ya 6.2 ya taarifa hii.
a) Kutolipwa Fidia kwa Watu Waliothiriwa na Miradi Sh.Tz. bilioni 11.9 Nimeibaini kuwa watu walioathiriwa na utekelezaji wa miradi mitatu; Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP II), Programu ya Msaada wa Sekta ya Usafiri (TSSP) na Mradi wa Barabara ya Arusha-Taveta / Holili-Voi hawajalipwa fidia ya jumla ya Sh.Tz. 11,870,767,751 (kiambatisho 1(i)).
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 xiii
b) Kutolipa Gharama za Uchangiaji Kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na “Global
Fund” Sh.Tz. bilioni 61.4 Ukaguzi wangu umegundua kuwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na Malaria, UKIMWI na Kifua Kikuu (Global Fund) wameshindwa kuchangia jumla ya Sh.Tz. 61,441,762,383.76 kwenda Bohari ya Dawa (MSD). Kiasi hiki kinatokana na kutochangia asilimia 5.6 kwa ajili ya gharama za uhifadhi na usambazaji wa dawa na vifaa-tiba kama inavyoelekezwa na mkataba wa makubaliano baina yao (kiambatisho 1(ii)).
c) Malipo ya Riba Iliyotokana na Adhabu kwa Kuchelewesha
Malipo ya Wakandarasi Sh.Tz. bilioni 3.9 Ilibainika kuwa jumla ya Sh.Tz. 3,889,404,110 zililipwa kama riba kutokana na adhabu ya kutolipa madai ya wakandarasi kwa wakati. Malipo haya yalihusisha miradi ya Programu ya Msaada katika Sekta ya Barabara Awamu ya Kwanza (RSSP I), RSSP II na Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji awamu ya pili (WSDP II). Aidha nilifahamishwa kwamba malipo ya wakandarasi yalishindikana kufanyika kwa wakati kutokana na Hazina kutopeleka fedha za miradi kwa wakati (kiambatisho 1(iii)).
d) Fedha za Ushuru wa Mafuta na Usafirishaji Zilizokusanywa
na Mamlaka ya Mapato Tanzania Zimepelekwa Pungufu Kwenye Akaunti ya Mfuko wa Barabara Sh.Tz. bilioni 14.8 Kwa kawaida Mamlaka ya Mapato Tanzania hukusanya fedha za ushuru wa mafuta na usafirishaji kisha huzihamishia kwenye Akunti ya Mfuko wa Barabara kupitia Wizara ya Fedha na Mipango.
Ukaguzi wangu umebaini kwamba Mamlaka ya Mapato Tanzania haikupeleka kiasi cha Sh.Tz. 14,828,686,613.55 kwenye Akaunti ya Mfuko wa Barabara. Hii inatokana na Mamlaka ya Mapato Tanzania kukusanya kiasi cha Sh.Tz. 755,688,604,775.57 na kupeleka kiasi pungufu kwenye
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 xiv
akaunti ya mfuko wa barabara ambacho ni Sh.Tz. 740,859,918,162.02.
e) Kutorejeshwa kwa Fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
Ambazo Zililipwa kwa Kaya Zisizostahili Sh.Tz. milioni 593.3 Iligundulika kuwa jumla ya Sh.Tz. 593,320,300 zililipwa kwa kaya zisizostahili kutoka kwenye maeneo 13 ya mamlaka ya mradi (PAA). Aidha, kaya hizo bado hazijarejesha kiasi hicho cha fedha kinyume na Ibara 1.7 ya Muongozo wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (kiambatisho 1(iv)).
f) Matumizi Yaliyofanyika Nje ya Bajeti Iliyoidhinishwa Sh.Tz.
bilioni 4.3 Watekeleza miradi 46 walitumia jumla ya Sh.Tz. 4,296,264,090.79 kufanyia shughuli ambazo zilikuwa nje ya bajeti iliyoidhinishwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Kufanya matumizi nje ya shughuli zilizoidhinishwa na bajeti kulisababisha kutokamilika kwa baadhi ya shughuli za miradi hiyo zilizokuwa kwenye mpango (kiambatisho 1(v)).
g) Kutolewa Fedha Pungufu kwa Ajili ya Utekelezaji wa Miradi
ya Maendeleo Sh.Tz. bilioni 274. 6 Wakati wa ukaguzi nilibaini kuwa watekeleza miradi 257 sawa na asilimia 35 ya watekeleza miradi wote walipokea fedha pungufu kwa Sh.Tz. 274,647,963,420.86 kinyume na bajeti iliyoidhinishwa. Hazina na baadhi ya Wafadhili walichelewa kutoa fedha hizi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo upelekeji wa taarifa za fedha zenye mapungufu kwenda kwa wafadhili kinyume na makubaliano. Aidha, utoaji wa fedha pungufu hupelekea miradi hiyo kutokukamilika kwa wakati na kuwa kwenye uwezekano wa kukabiliwa na ongezeko la gharama za miradi (viambatisho 1(vi) na 1(vii)).
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 xv
h) Malipo Yaliyofanyika na Viambatisho Pungufu Sh.Tz. bilioni 8.7 Nilibaini uwepo wa malipo ya jumla ya Sh.Tz. 7,248,937,125.89 ambayo yalifanywa na watekeleza miradi 163 bila kuwa na viambatisho vya kutosha. Aidha, nilishindwa kupata hati za malipo kwa matumizi ya Sh.Tz. 1,464,506,137.88 ambazo zililipwa na watekeleza miradi 21. Hivyo, kwa ujumla nimeshindwa kutambua uhalali wa malipo ya Sh.Tz. 8,713,443,263.77 kutokana na kukosekana kwa nyaraka za viambatisho (viambatisho 1(viii) na 1(ix)).
i) Kutokudai Marejesho ya Kodi ya Ongezeko la Thamani
(VAT) Sh.Tz. bilioni 1.6 Niligundua kuwa watekeleza miradi 16 wameshindwa kudai kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jumla ya Sh.Tz. 1,588,581,132.46 kutokana na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kinyume na makubaliano yaliyosainiwa kati ya Serikali na Wafadhili (kiambatisho 1(x)).
j) Malipo Yaliyofanyika Kwenye Vifungu vya Matumizi Visivyo Sahihi Sh.Tz. bilioni 1.1 Nimebaini kuwa jumla ya Sh.Tz. 1,091,406,059 zililipwa kupitia vifungu vya matumizi ambavyo siyo sahihi, kinyume na Agizo Na.23 (1) la Randama ya Fedha za Serikali za Mitaa (LGFM) 2009. Kuchanganya vifungu vya matumizi kunasababisha baadhi ya vifungu kupungukiwa na fedha, hivyo kushindwa kutumika kufanya kazi zilizokusudiwa (kiambatisho 1(xi)).
iii. Utekelezaji wa Mapendekezo ya Ukaguzi Yatokanayo na Ripoti za Kaguzi za Miaka Iliyopita Imeonekana kuwa Maafisa Masuuli na watendaji wakuu wa taasisi zinazotekeleza miradi ya maendeleo hawatekelezi kikamilifu mapendekezo yangu; ambapo, mapendekezo 2,720, sawa na asilimia 35 ya mapendekezo yangu ya mwaka uliopita, hayakutekelezwa kama ilivyooneshwa kwa undani kwenye Sura ya 2.1 ya ripoti hii.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 xvi
iv. Mwelekeo wa Hati za Ukaguzi Zilizotolewa Nimekagua jumla ya miradi ya maendeleo 742 ndani ya mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni 2017. Idadi hiyo inajumuisha miradi ya maendeleo 664 kutoka katika ripoti kubwa tano, yaani Mradi wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP), Mfuko wa Uchangiaji wa Sekta ya Afya (HBF), Mfuko wa Barabara (RF), Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) na Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP) ikiwa na idadi ya hati 56, 181, 177, 70 na 180 mtawalia. Aidha miradi mingine ilikuwa na hati 78.
Nimetoa jumla ya hati za ukaguzi 742 kwa mwaka wa fedha 2016/2017; ambapo hati 697, sawa na asilimia 94 ya hati zote zilizotolewa zilipata hati zinazoridhisha; hati 44, sawa na asilimia 6, zilipata hati zenye mashaka. Hati chafu ilitolewa kwa halmashauri moja; hakuna hati mbaya iliyotolewa. Aidha, sijagundua mabadiliko makubwa kwenye hati za ukaguzi zilizotolewa katika mwaka huu kulinganisha na mwaka wa fedha uliopita.
Hata hivyo, hati zenye shaka zimejitokeza kwa wingi kwenye
mradi wa Mfuko Mkuu wa Afya na Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji zikiwa na jumla ya hati zenye shaka 14 na 13 mtawalia.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 1
SURA YA KWANZA
USULI NA TAARIFA ZA UJUMLA
1.0 Utangulizi Ukaguzi wa Kisheria wa taarifa za fedha za miradi ya maendeleo inayotekelezwa nchini kwa mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni 2017 umekamilika. Ukaguzi huu umejumuisha miradi mitano mikubwa ambayo ni ASDP, HBF, RF, TASAF na WSDP, aidha, ilijumuisha miradi mingineyo inayofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika, Benki ya Dunia, Umoja wa Mataifa na makubaliano ya kifedha baina ya JMT na nchi nyingine kupitia taasisi zao.
Ofisi yangu ilipanga kukagua jumla ya miradi 768 ikijumuisha miradi mikubwa mitano na miradi mingineyo. Kufikia tarehe 31 Machi 2018, nilimaliza ukaguzi wa miradi 742 kama ifuatavyo; ASDP, HBF, RF, TASAF, WSDP na miradi mingineyo kwa idadi ya 56, 181, 177, 70, 180 na 78 mtawalia, ilhali ukaguzi wa miradi 26 ukiwa unaendelea. Hata hivyo, nimefanikiwa kumaliza ukaguzi wa miradi 31 iliyokuwa haijakamilika kwenye mwaka wa fedha 2015/2016
Muhtasari wa mambo muhimu yaliyotokana na ukaguzi yameonyeshwa katika taarifa hii ya jumla. Aidha, taarifa kamili zilipelekwa kwa uongozi wa kila mkaguliwa anayesimamia utekelezaji wa mradi na wadau wengine wanaohusika na miradi.
1.1 Mamlaka na Umuhimu wa Ukaguzi Kutokana na Ibara ya 143 ya Katiba ya JMT, ninapaswa kukagua taarifa zote za hesabu za fedha katika ofisi zote za Umma, Mahakama na Mamlaka zote za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutoa taarifa kwa Mheshimiwa Rais ambaye atahakikisha zinawasilishwa mbele ya Bunge.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 2
Katika kutimiza wajibu huu, kifungu Na.10 cha Sheria Na. 11 ya Ukaguzi wa Umma ya mwaka 2008 kinanitaka kujiridhisha kwamba fedha zote zinazotolewa zinatumika kulingana na malengo yaliyokusudiwa.
1.2 Wajibu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Wajibu wangu kama Mkaguzi wa Hesabu ni kutoa maoni ya ukaguzi kuhusu taarifa za fedha za miradi ya maendeleo kutokana na ukaguzi nilioufanya. Nilifanya ukaguzi kulingana na viwango vya kimataifa vinavyosimamia ukaguzi katika Taasisi za Umma za Ukaguzi (ISSAIs), mkataba wa makubaliano na taratibu nyingine nilizoona zinafaa.
Aidha, kifungu Na. 10(1) cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na.11 ya mwaka 2008 kinanitaka nijiridhishe kama taarifa za hesabu zimeandaliwa kwa misingi ya viwango vya kihasibu, na tahadhari za kutosha zimechukuliwa kulinda ukusanyaji wa mapato, stakabadhi, uhifadhi, uuzwaji, uhamasishwaji pamoja na matumizi sahihi wa mali ya umma. Na, ni wajibu wangu kuona kuwa sheria, kanuni maelekezo na maagizo yanafuatwa katika matumizi ya fedha za umma, na kwamba, yameidhinishwa ipasavyo.
Zaidi, kifungu 48(3) cha Sheria ya Manunuzi ya Umma Na. 7 ya mwaka 2011 kinanitaka katika ripoti yangu nitoe tathmini kama taarifa nilizokagua zinakidhi matakwa ya sheria na kanuni zake.
1.3 Muundo wa Kazi za Ukaguzi katika Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Ripoti hii inatoa kwa muhtasari matokeo ya mwisho ya zoezi la ukaguzi ambalo lilifanywa na ofisi yangu nchini kote katika mwaka huu. Ili ofisi yangu iweze kushughulikia kikamilifu kazi hii kubwa ya kukagua miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Halmashauri zote nchini, wakala wa serikali, na wabia wengine, nimeunda ofisi katika mikoa yote Tanzania Bara ili kurahisisha utendaji. Ofisi hizo zinaongozwa na Wakaguzi Wakuu wa Nje. Aidha, nafanya kaguzi zangu kwa kuzingatia
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 3
viashiria hatarishi (risk based audit) zinazotekelezwa kwa kutumia teknolojia maalum ya kompyuta (Computer Assisted Audit Techniques (CAATs)).
Wakati mwingine niliazima wakaguzi kutoka nje ya ofisi yangu ili kusaidia ukaguzi kama ninavyoruhusiwa na Sheria Namba 33 ya Ukaguzi wa Umma ambayo inanipa mamlaka ya kumthibitisha mkaguzi yeyote mwenye sifa na aliyesajiliwa na Bodi ya Uhasibu nchini chini ya Sheria Namba 33 ya Usajili wa Wahasibu Na Wakaguzi ya mwaka 1972 (iliyorekebishwa mwaka 1995).
1.4 Mawanda na Viwango vya Ukaguzi Vinavyotumika 1.4.1 Mawanda ya Ukaguzi
Mawanda ya Ukaguzi yalihusisha tathmini ya ufanisi wa mifumo ya kihasibu pamoja na udhibiti wa ndani wa shughuli, upimaji na uthibitishaji wa viambatisho vya nyaraka za fedha, taarifa za utekelezaji na taratibu nyingine za kikaguzi zilizopaswa kuzingatiwa ili kupatikana kwa taarifa ya ukaguzi. Kaguzi zimefanyika kwa kuzingatia vihatarishi na uzito wa tatizo lilioibuliwa. Hivyo, hoja za ukaguzi zimetokana na taarifa zilizopokelewa kwa ajili ya kukaguliwa.
Lengo kuu la kufanya ukaguzi ni kumsaidia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kutoa maoni yake kwa uhuru kuhusiana na taarifa za fedha za miradi ya maendeleo zilizoandaliwa na kuwasilishwa kwa ajili ya kuzikagua. Vilevile, kuona kama zimeandaliwa kwa kuzingatia miongozo ya uandaaji wa taarifa za fedha wa kimataifa.
1.4.2 Viwango vya Ukaguzi Vinavyotumika Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali (NAOT) ni mwanachama wa Jumuiya Kuu ya Kimataifa ya Asasi Kuu za Ukaguzi wa Hesabu (INTOSAI) na Jumuiya ya Afrika ya Asasi Kuu za Ukaguzi kwa Nchi Zinazozungumza Lugha ya Kiingereza (AFROSAI-E). Hivyo basi, taratibu zilizotumika zimezingatia
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 4
Viwango vya Kimataifa vya Ukaguzi kama vile ISSAI na ISA vinavyotolewa na INTOSAI na IFAC mtawalia.
Viwango hivi vinanitaka kuzingatia maadili katika kuandaa na kutekeleza ukaguzi wangu ili kupata uhakika kwamba taarifa za hesabu zipo sahihi na hazina makosa makubwa. Hata hivyo, taarifa za kifedha za Miradi ya Maendeleo ziwe zimeandaliwa kwa mujibu wa makubaliano baina ya wabia yaliyosainiwa.
1.5 Wajibu wa Maafisa Masuuli Kifungu Na. 25(4) cha Sheria ya Fedha Na. 6 ya mwaka 2001 (iliyorekebishwa 2004) kinamtaka Afisa Masuuli kuandaa taarifa za fedha zilizo sahihi kwa kila kipindi cha mwaka kuonyesha mapato na matumizi ya mradi hadi kufikia mwisho wa mwaka.
Aidha, maagizo namba 11, 14 na 31 (1) ya Randama ya Fedha za Serikali za Mitaa ya 2009, na Mkataba wa Makubaliano (MoU) baina ya watekelezaji wa Mradi na wadau wa maendeleo yanawataka wahusike kuhakikisha kwamba kumbukumbu sahihi za kihasibu za miradi zinatunzwa vizuri; na mfumo wa udhibiti wa ndani udhibitiwe.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 5
SURA YA PILI
HALI YA UTEKELEZAJI WA MAPENDEKEZO YA RIPOTI ZA KAGUZI ZA MIAKA YA NYUMA
2.0 Utangulizi Sura hii inalenga kutoa taarifa ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa katika ripoti za kaguzi za miaka ya nyuma. Pia, ni muhtasari wa masuala ya kifedha na yasiyo ya kifedha yaliyoibuliwa katika kila ripoti ya mradi yaliyokuwa yametekelezwa kwa sehemu au hayajatekelezwa kabisa. Mapendekezo ya ukaguzi yanayotolewa kwa wakaguliwa hulenga kuwezesha kufanya maboresho na kurekebisha kasoro zilizoonekana wakati wa ukaguzi wa taarifa za hesabu.
2.1 Hali ya Utekelezaji wa Mapendekezo ya Kaguzi Zilizopita Kama inavyoonekana kwenye Kiambatisho Na.3, kulikuwa na mapendekezo ambayo hayajatekelezwa kwenye Miradi ya Maendeleo kwa mwaka wa Fedha unaoishia 30 Juni, 2017. Kati ya hayo, 2,220 sawa na asilimia 29 yalitekelezwa; 1,325 sawa na asilimia 17 yanaendelea kutekelezwa; 2,720 sawa na asilimia 35 hayakutekelezwa; na 1,475 sawa na asilimia 19 yamefutika kutokana na mazingira na wakati.
Ingawa utekelezaji wa mapendekezo yangu umeboreka kidogo kwa asilimia 5 ingawa kwa ujumla utekelezaji wa mapendekezo yangu bado hauridhishi ambapo asilimia 35 ya mapendekezo yangu hayajatekelezwa ikilinganishwa na asilimia 40 ya mwaka uliopita. Aidha, utekelezaji wa mapendekezo ya ukaguzi bado hauridhishi kutokana na idadi kubwa ya mapendekezo yaliyopita. Uchambuzi unaonesha kwamba mapendekezo 145 kati ya 408 ya Programu ya Maendeleo Sekta ya Kilimo ambayo ni sawa na asilimia 36 bado hayajatekelezwa; mapendekezo 728 kati ya 2,043 ya Mfuko wa Barabara ambayo ni sawa na asilimia 36 hayajatekelezwa. Aidha, mapendekezo 1,014 kati ya 2,437 ya Mfuko wa Uchangiaji Sekta ya Afya ambayo ni sawa na
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 6
asilimia 42 bado hayajatekelezwa; mapendekezo 678 kati ya 2,058 ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji ambayo ni sawa na asilimia 33 bado hayajatekelezwa; na mapendekezo 84 kati ya 424 Mfuko wa Maendeleo ya Jamii ambayo ni sawa na asilimia 20 bado hayajatekelezwa. Zaidi ya hayo, mapendekezo 71 kati ya 370 ya Miradi Mingineyo ambayo ni asilimia 19 bado hayajatekelezwa. Rejea jedwali hapa chini kwa maelezo zaidi:
Jedwali Na. 1: Utekelezaji wa Mapendekezo Katika Ripoti za Kaguzi za Miaka ya Nyuma Jina la Mradi Mapendek
ezo ya Miaka ya Nyuma
Mapendekezo Yaliyotekelezwa
Mapendekezo Yanayoendelea kutekelezwa
Mapendekezo
ambayo hayajateke
lezwa
Mapendekezo yaliyofutika kutokana na Mazingira na
Wakati Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
408 76 87 145 100
Mfuko wa Barabara
2,043 566 309 728 440
Mfuko wa Uchangiaji wa Afya
2,437 651 332 1014 440
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
424 221 74 84 45
Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
2,058 517 436 678 427
Miradi mingineyo
370 189 87 71 23
Jumla 7,740 2,220 1,325 2,720 1,475 Asilimia 100 29 17 35 19
Chanzo: Ripoti za Ukaguzi za miaka iliyopita
Kwa hiyo, nasisitiza kuwa watekeleza miradi wahakikishe wanayafanyia kazi ili kuepusha kujirudiarudia kwa mapungufu hayo, hatimaye kuboresha uwajibikaji katika matumizi ya fedha zilizopokelewa. Aidha, nashauri kuwa mapendekezo yote ambayo yametekelezwa kwa sehemu au
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 7
hayajatekelezwa kabisa yatekelezwe kwa wakati ili kuboresha usimamizi wa miradi hiyo.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 8
SURA YA TATU
AINA NA MWENENDO WA HATI ZA UKAGUZI ZILIZOTOLEWA
3.0 Utangulizi Katika kutimiza wajibu wangu wa kisheria, nina jukumu la kuwahakikishia wadau wote wa miradi ya maendeleo kuwa taarifa za fedha za miradi ya maendeleo yam waka unaoishia tarehe 30 Juni, 2017 zimeandaliwa kulingana na taratibu na miongozo sahihi ya kutengenezea hesabu.
Hati ya ukaguzi inachukuliwa kama chombo muhimu wakati wa kuwasilisha taarifa ya kifedha kwa walengwa wanaotumia taarifa hizi. Katika sekta ya umma, inakusudiwa kulishauri Bunge na watumiaji wengine wa taarifa za Wizara, Idara na Sekretarieti za Mikoa kama taarifa za fedha zimetayarishwa kwa kuzingatia viwango vinavyoendana na IPSAS na kwa namna inavyotakiwa chini ya Kifungu cha 25(4) cha Sheria ya Fedha za Umma ya mwaka 2001 (iliyorekebishwa 2004) na Agizo namba 11-14 ya Randama ya Fedha ya Serikali za Mitaa ya mwaka 2009, na mkataba wa makubaliano kati ya watekelezaji na wadau wa maendeleo, ambayo inawataka kuhakikisha kuwa usimamizi wa kumbukumbu za uhasibu na mfumo wa udhibiti wa ndani unaimarika. Kwa upande wa miradi ya maendeleo, nimetoa aina kuu tatu za hati kutokana na kukagua vitabu vya hesabu, mifumo ya udhibiti wa ndani, na uziangatiaji wa taratibu. Nimetoa jumla ya hati 742 kutokana na ukaguzi wa vitabu vya hesabu, hati 35 kutokana na ukaguzi wa mifumo ya udhibiti wa ndani, na hati 6 kutokana na ukaguzi wa uziangatiaji wa taratibu. Aidha sijabaini mapungufu makubwa kiasi cha kutolea taarifa katika hati hizo 41 za mifumo ya udhibiti wa ndani na uzingatiaji wa taratibu, ambapo zimetokana na ukaguzi wa miradi iliyofadhiliwa na Programu ya Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP), Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 9
Watoto na Elimu na Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na Malaria, UKIMWI na Kifua Kikuu.
3.1 Aina za Hati za Ukaguzi Katika mwaka huu wa fedha nimekagua jumla ya miradi ya maendeleo 742 na kutoa aina tatu za hati za ukaguzi ambazo ni hati inayoridhisha, hati isiyoridhisha na hati mbaya kama inavyoonekana kwenye jedwali namba mbili hapo chini:
Jedwali Na 2: Muhtasari wa Hati za Ukaguzi Zilizotolewa Jina la Mradi Hati za Ukaguzi
Hati Zinazoridhisha
Hati Zenye Shaka
Hati Zisizoridhisha
Hati Mbaya
Jumla
Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
55 1 56
Mfuko wa Uchangiaji wa Afya
167 14 181
Mfuko wa Bara Bara 169 8 177 Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania
66 4 70
Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
166 13 1 180
Miradi Mingineyo 74 4 78 Jumla Kuu 697 44 1 742 Chanzo: Taarifa za Ukaguzi za miradi ya maendeleo za unaoishia 30 Juni 2017
3.1.1 Hati Inayoridhisha Aina hii ya hati (kama ilivyoelezewa katika ISSAI 1700.16) hutolewa wakati taarifa za fedha zilizowasilishwa na kukaguliwa zinakutwa hazina makosa mengi na zimezingatia matakwa ya viwango vya Kimataifa vya Uhasibu katika Sekta ya Umma ikihusisha uzingatiwaji wa Sheria na Kanuni.
Jumla ya hati zinazoridhisha 697 sawa na asilimia 94 zilitolewa kwenye Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo, Mfuko wa Pamoja wa Afya, Mfuko wa Barabara, Mfuko wa Maendeleo ya Jamii, Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji na Miradi Mingineyo zikiwa ni 55, 167, 169, 66,166 na 74 mtawalia, ikimaanisha kwamba hesabu zilizokaguliwa
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 10
hazikuwa na matatizo sana. Kama inavoonekana kwenye aya ya 3.2 hali ya hati hizo imeboreka kidogo kwa asilimia 3 ikilinganishwa na mwaka 2015/2016 ambapo kulikuwa na hati 725 zinazoridhisha sawa na asilimia 91 ya hati zote zilizotolewa (Kiambatisho 4(i) na 4(ii)).
3.1.2 Hati Yenye Mashaka Hati yenye mashaka (Kama ilivyoelezwa katika ISSAI 1705.7) hutolewa wakati: (a) Mkaguzi anapopata ushahidi na vielelezo vya kutosha kujiridhisha kwamba mapungufu yaliyojitokeza ni makubwa lakini hayana athari kwenye hesabu kwa ujumla; (b) Mkaguzi hakuweza kupata vielelezo na ushahidi wa kutosha lakini amejiridhisha kwamba athari ya kukosekana kwa vilelezo hivyo siyo kubwa kwenye hesabu zilizokaguliwa. Kwa hali hiyo, hati yenye shaka inaonyesha kuwa taarifa za fedha zilizowasilishwa ni sahihi isipokuwa kwa madhara yatokanayo na masuala halisi ya kiukaguzi yaliyogunduliwa.
Aidha, jumla ya hati za mashaka 44 sawa na asilimia 6 ya hati za ukaguzi zilitolewa kwa miradi ya maendeleo iliyokaguliwa ya ASDP, HBF, RF, TASAF, WSDP, na miradi mingineyo kwa 1, 14, 8, 4, 13 na 4 mtawalia. Katika mradi wa afya nimegundua hati 14 zisidhoridhisha ambazo ni sawa na asilimia 32 ya hati zote zisidhoridhisha. Idadi kubwa ya miradi hii imepata hati zisizoridhisha kutokana na malipo mengi kukosa viambatisho pamoja na vitabu vya hesabu kuandaliwa vikiwa na makosa mengi ambayo hayakurekebishwa kwa wakati mpaka ukaguzi ulipomalizika (kiambatisho 4(iii)).
Kuwapo kwa matumizi yasiyo na viambatisho kunaonesha kuna tatizo kubwa katika udhibiti wa matumizi na utunzaji wa kumbukumbu za hesabu katika miradi hiyo. Hii inaweza kusababisha malengo kusudiwa ya miradi kutofikiwa, hivyo Serikali na Watekeleza miradi wanatakiwa kuchukua hatua za kuhakikisha kwamba matumizi ya miradi yanakuwa na viambatisho stahiki.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 11
3.1.3 Hati Isiyoridhisha Hati isiyoridhisha (Kama ilivyoelezewa kwenye ISSAI 1705.8) hutolewa inapogundulika kuwa taarifa za fedha kwa kiasi kikubwa si sahihi zinapoangaliwa katika ujumla wake; na kwamba, hazikuandaliwa kwa kuzingatia mifumo ya kihasibu. Maelezo ya hati isiyoridhisha huwa wazi ambapo inaeleza wazi kwamba taarifa za fedha hazikuzingatia na kufuata mfumo wa uhasibu na viwango vya Kimataifa vya Uhasibu katika sekta ya Umma.
Katika ukaguzi huu nimetoa hati moja isiyoridhisha kwa Halmashauri ya Wilaya ya Makete kwa mradi wa programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji.
3.1.4 Hati Mbaya Hati mbaya (kama ilivyoelezewa katika ISSAI 1705.9&10) inaweza kusababishwa na kukosekana kwa uhuru au ufinyu mkubwa wa mawanda ya ukaguzi ama kwa makusudi au la. Mkaguliwa kukataa kutoa ushahidi na taarifa kwa mkaguzi katika maeneo muhimu kwenye taarifa za fedha na panapokuwa na mashaka makubwa katika uendeshaji wa shughuli za mkaguliwa. Katika mwaka wa fedha unaoishia 30 Juni 2017 sijatoa hati mbaya kwa mtekelezaji yeyote wa miradi ya maendeleo.
3.2 Mwelekeo wa Hati za Ukaguzi Nawasilisha mchanganuo wa hati za ukaguzi kwa muda wa miaka miwili ya nyuma. Aidha, hakuna mabadiliko makubwa yaliyoonekana katika hati za ukaguzi zilizotolewa ikilinganishwa na mwaka 2015/2016 kama inavyoonekana kwenye jedwali namba 3 hapo chini:
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 12
Jedwali Na. 3: Mwelekeo wa hoja za ukaguzi Mwaka wa
Fedha Hati zilizotolewa
Jumla Zinazoridhisha Zenye shaka Zisizoridhisha
No. % No. % No. %
2016/2017 697 94 44 6 1 0.13 742
2015/2016 725 91 71 9 1 0.13 797
2014/2015 739 92 60 8 - - 799
Chanzo: Taarifa za Ukaguzi wa Miradi ya Mendeleo za miaka ya nyuma
Jedwali hapo juu linaonesha uborekaji katika hati zilizotolewa ambapo zinazoridhisha zimeongezeka kwa asilimia 3 na hati zenye shaka zimepungua kwa asilimia 3 pia. Aidha hakuna mabadiliko kwenye hati zisizoridhisha ambapo zimebakia kuwa asilimia 0.13 kwa miaka miwili mfululizo. Kama ilivoelezewa kwenye aya za 3.1.2 na 3.1.3, kwamba nimetoa hati 44 zenye shaka na hati 1 isiyoridhisha zilizotokana na makosa yasiyorekebishwa kwenye ufungaji wa hesabu pamoja na malipo yenye viambatanisho pungufu.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 13
SURA YA NNE
UTENDAJI WA KIFEDHA WA MIRADI
4.0 Utangulizi Sura hii inatoa mchanganuo wa kina wa utendaji wa kifedha katika miradi ya maendeleo ikiwemo Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP), Mfuko wa Uchangiaji wa Afya (HBF), Mfuko wa Barabara (RF), Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP) pamoja na miradi mingine ya maendeleo. Inatoa mchanganuo wa kiasi cha fedha kilichotumwa na kutumiwa na watekelezaji wa miradi. Undani wa utendaji wa kifedha kwa kila mradi ni kama inavyooneshwa kwenye kiambatisho 5.
4.1 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
4.1.1 Utangulizi Programu hii inajumuisha mipango ya kuendeleza kilimo kitaifa na kisekta inayofadhiliwa kwa pamoja na Serikali ya Tanzania na Washirika wa Maendeleo kupitia Mfuko wa pamoja wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo ambao ulitanguliwa na Programu ya kusaidia Sekta ya Kilimo (ASSP) na Programu ya Maendeleo ya Kilimo ya Wilaya (DADP). Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) inatekelezwa na Wizara na Serikali za Mitaa na malengo yake yamewekwa chini ya Mfumo wa Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDS).
4.1.2 Ufadhili
Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) inafadhiliwa na michango na mikopo kutoka Washirika wa Maendeleo kupitia Ubalozi wa Ireland, Shirika la Kimaendeleo la Kimataifa (IDA), Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD) na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA). Fedha zinapokelewa kupitia akaunti kuu ya mradi iliyoko Hazina na kisha kupelekwa kwa watekeleza miradi
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 14
Programu ilianza mwaka kwa salio anzia la kiasi cha Dola za Kimerakani (DK) 4,218,560.28 (Sh.Tz. 9,361,194,080.05) katika akaunti ya mfuko mkuu na haikupokea fedha kutoka kwa wadau wa maendeleo. Kiasi cha DK 344,849.35 (Sh.Tz. 765,237,777.69) kilihamishwa na kubaki salio ishia la DK 3,873,710.93(Sh.Tz. 8,595,956,302.36). Wakati mfuko mkuu wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo awamu ya pili wa Matokeo Makubwa Sasa ulikuwa na salio anzia DK 611,972.01 (Sh.Tz. 1,357,996,182.80) na kupokea kiasi cha DK 351,312.23 (Sh.Tz. 779,579,228.33) kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa. Jumla ya DK 361,287.48 (Sh.Tz. 801,714,801.85) na DK 157,537.47 (Sh.Tz. 349,583,444.03) zilitumwa Wizara ya Kilimo na Wizara ya Maji na Umwagiliaji na kubakiwa na salio la DK 444,459.29 (Sh.Tz. 986,277,165.24) Jedwali hapo chini linaonesha.
Jedwali Na. 4: Jumla ya Fedha za Mpango wa Maendeleo Sekta ya Kilimo Zilizopokelewa na Kuhamishwa
Maelezo
Kiasi (DK) Akaunti ya Mfuko mkuu wa ASDP
Akaunti ya Mfuko mkuu wa ASDP II-Matokeo Makubwa Sasa
Salio anzia 1 Julai 2016 4,218,560.28 611,972.01
Fedha iliyopokelewa: Shirika la Maendeleo la Kimataifa
- 351,312.23
Jumla ya fedha zilizopokelewa
4,218,560.28 963,284.24
Fedha zilizohamishwa
Wizara ya Maji na Umwagiliaji - 157,537.47
Wizara ya Kilimo 204,958.14 361,287.48
Fedha zilizorudishwa kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa
139,891.21 -
Jumla ya fedha zilizohamishwa 344,849.35 518,824.95
Salio Ishia 30 Juni 2017 3,873,710.93 444,459.29 Chanzo: Taarifa ya fedha Mfuko mkuu wa Mpango wa Maendeleo ya sekta ya Kilimo ya 30 June 2017.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 15
4.1.3 Fedha za Mradi kwa Serikali za Mitaa Mamlaka za serikali za mitaa zilikuwa na jumla ya Sh.Tz. 14,496,390,704.20 kwa ajili ya utekelezaji wa Programu ya Maendeleo katika Sekta ya Kilimo; ambapo Sh.Tz. 13,348,387,781.20 ilikuwa salio anzia na Sh.Tz. 1,148,002,923 zilipokelewa mwaka huu kwa ajili utekelezaji wa miradi iliyopangwa. Aidha Sh.Tz. 9,177,271,288 zilitumika na kubaki na salio ishia la Sh.Tz. 5,319,119,416.20 ambalo ni sawa na asilimia 37 ya fedha iliyokuwepo kwa ajili ya kukamilisha kazi zilizopangwa.
4.2 Fedha za Mfuko wa Uchangiaji wa Afya (HBF) 4.2.1 Utangulizi
Washiriki wa Mfuko wa Uchangiaji wa Afya nchini huchangiwa fedha na wadau wa kupitia akaunti maalum katika Benki Kuu ya Tanzania na baadaye kuhamisha fedha hizo kwenda Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, OR-TAMISEMI na SM kwa kutoa fedha kwa mgawo wa robo mwaka kupitia Akaunti kuu ya Hazina. Ufadhili hufuata utaratibu wa kawaida wa Serikali ya Tanzania (JMT) ambapo fedha za Washirika wa maendeleo hujumuishwa katika bajeti kuu.
4.2.2 Ufadhili
Mfuko wa Uchangiaji wa Afya ulianza mwaka 2016/2017 ukiwa na salio anzia la DK 15,547,235.25 (Sh.Tz. 33,704,866,845.71) na kupokea kiasi cha DK 74,682,274.4 (Sh.Tz.161,616,252,402.8) kisha kupeleka jumla ya DK 68,008,853.98 (Sh.Tz. 148,705,727,340) kwa watekeleza miradi 181. Mpaka kufikia mwisho wa mwaka, Mfuko ulibaki na bakaa ishia la DK 22,220,655.67 (Sh.Tz. 49,308,745,964.51). Wachangiaji wakuu katika mwaka huu wa fedha ni Denmark (asilimia 12) Ireland (asilimia12), Uswisi(asilimia8.2), KOICA (asilimia1.34), UNICEF (asilimia1.34), IDA (asilimia46) na Canada (asilimia 19) ya jumla ya fedha yote iliyochangwa. Jedwali hapo chini linaonesha mchanganuo huu:
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 16
Jedwali Na. 5: Jumla ya Fedha Zilizokusanywa Kutumwa Mfuko wa Uchangiaji wa Afya
Maelezo Kiasi (DK) Michango
kwa asilimia Salio anzia 1 Julai 2016 15,547,235.25 Mapokezi ya Fedha
Denmark 8,724,129.27 12 Ireland 8,981,600 12 Uswisi 6,105,000 8.2 Shirika la Misaada la Kijapani (KOICA) 1,000,000 1.34
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu na Watoto (UNICEF) 1,000,000 1.34
Shirika la Maendeleo la Kimataifa (IDA) 34,671,730.70 46
Canada 14,137,472.79 19 Kurudishwa kwa fedha za ziada 62,341.64 Jumla ya fedha iliyopokelewa 74,682,274.40 Jumla ya Fedha iliyopo 90,229,509.65 Fedha zilizohamishwa
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto 67,879,547.02 OR-TAMISEMI 129,306.96 Jumla ya fedha zilizohamishwa 68,008,853.98 Salio ishia 30 Juni 2017 22,220,655.67
Chanzo: Taarifa ya fedha ya Mfuko wa Uchangiaji wa Afya inayoishia 30 Juni 2017
4.2.3 Fedha zilizotumwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto, OR-TAMISEMI na SM Jumla ya Sh.Tz. 8,768,477,000, Sh.Tz. 30,085,677,840; na Sh. 105,827,586,360 ilipokelewa na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto, OR-TAMISEMI na SM mtawalia kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Afya; ambapo Sh.Tz. 7,357,570,608, Sh.Tz. 6,192,407,085.06 na Sh.Tz. 115,546,902,047.11 zilitumika na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto, OR-TAMISEMI, SM kama jedwali linavyoonesha hapa chini:
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 17
Jedwali Na. 6: Fedha zilizotumwa kwa Watekelezaji wa Miradi Maelezo Kiasi (Sh.Tz.)
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia,
Wazee na Watoto
OR-TAMISEMI SM
Salio anzia 1 Julai 2016
149,913,966
4,545,282,036.06 20,593,701,658
Ongeza: Fedha iliyopokelewa
8,768,477,000
30,085,677,840 105,827,586,360
Fedha iliyokuwepo 8,918,390,966 34,630,959,876.06 126,970,149,017.83 Matumizi yaliyofanyika
7,357,570,608
6,192,407,085.06 115,546,902,047.11
Marejesho kwenye akaunti kuu
149,913,966
- -
Salio ishia 30 Juni 2017
1,410,906,392
28,438,552,791.00 11,423,246,969.72
Chanzo: Taarifa ya fedha inayoishia 30 Juni 2017 ya Mfuko wa Afya
4.3 Mfuko wa Barabara 4.3.1 Utangulizi
Vyanzo vikuu vya mapato ya Bodi ya Mfuko wa Barabara ni pamoja na kodi itokanayo na mafuta, ushuru wa usafirishaji wa bidhaa na mali kwenda nje ya nchi, tozo ya kupakia mizigo kupita kiasi, riba, na mapato mengineyo, hasa kutoka Shirika la Kimataifa ya Maendeleo ya Uingereza. Fedha yote inayokusanywa kama mapato ya Mfuko wa Barabara inagawanywa kwa watekeleza miradi ya barabara ambao ni Mfuko wa Barabara, Wizara ya Ujenzi, Wakala wa Barabara wa Tanzania, OR-TAMISEMI na SM wakizingatia asilimia ya mgawanyo uliopitishwa na Bunge. Angalau asilimia 90 ya fedha zote zilizowekwa kwenye Mfuko wa Barabara zinatakiwa zitumike kwa ajili ya matengenezo na ukarabati wa dharura wa barabara zilizoainishwa. Pia, fedha hizo zinatumika kwenye shughuli za kiutawala zinazohusiana na matengenezo na ukarabati kwa upande wa Tanzania Bara kulingana na mpango kazi wa utekelezaji ulioidhinishwa. Kiasi kilichosalia pia hutumika kwenye miradi ya maendeleo
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 18
ikiambatana na gharama za utawala kwa upande wa Tanzania Bara.
4.3.2 Ufadhili Mfuko wa barabara ulikuwa na kiasi cha Sh.Tz. 870,518,855,605 ikiwemo na Sh.Tz. 92,806,884,046 kutoka kwa wafadhili kwa utekelezaji wa kazi zilizopangwa, angalia jedwali hapa chini. Jedwali Na. 7: Mwenendo wa Makusanyo ya mapato kwa Miaka
Chanzo cha Mapato Mwaka wa Fedha (Kiasi-Sh.Tz.) 2016/17 2015/16 2014/15
Ushuru wa Mafuta 744,100,055,085 705,091,411,698 623,175,176,771.09 Ushuru wa usafirishaji 11,588,549,889 9,491,496,859 7,904,356,679.48 Tozo ya kuzidisha mizigo
10,976,051,955 8,052,957,501 11,348,406,232
Shirika la maendeleo la Uingereza (DFID)
92,806,884,046 26,114,158,400 19,772,448,112
Mfuko wa hifadhi ya barabara
10,000,578,282 - 588,939,182
Mapato Mengineyo 284,678,382 278,491,547 198,310,481 Mapato yanayotokana na Riba
762,057,966 818,778,313
Jumla 870,518,855,605 749,847,294,318 662,987,637,457.57 Chanzo: Taarifa ya fedha ya Mfuko wa barabara inayoishia 30 Juni 2017
Mchanganuo wa hapo juu unaonesha kuwa mwenendo wa fedha zinazopokelewa kutoka bodi ya mfuko wa barabara zimeongezeka kwa asilimia 16; na ongezeko kubwa limetokana na Shirika la Maendeleo la Uingereza na Mfuko wa Hifadhi ya Barabara kwa asilimia 255 na 100 mtawalia.
4.3.3 Ufadhili wa Mfuko wa Barabara kwa SM
SM zilikuwa na salio anzia la Sh.Tz. 54,555,130,277.46 zilipokea Sh.Tz. 219,391,809,477.54 ambapo Sh.Tz. 191,941,807,039.36 zilitumika na kubaki na salio ishia la Sh.Tz. 82,005,132,715.64 ambalo ni sawa na asilimia 30 ya fedha zilizokuwepo kwa ajili ya kukamilisha miradi iliyopangwa.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 19
4.4 Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Awamu ya Tatu – Mpango Uhaulishaji wa Fedha kwa Kaya Maskini
4.4.1 Utangulizi
Mradi wa Maendeleo ya Jamii awamu ya tatu uliombatana na mpango wa uhaulishaji kwa kaya maskini ulianzishwa tarehe 15 June 2012 kufuatia makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia kupitia Shirika la Kimataifa la Maendeleo (IDA). Mfuko wa Maendeleo ya Jamii uliruhusiwa kupata mkopo wa thamani sawa na haki ya kutoa fedha (SDR) 141,900,000 inayolingana na DK 220,000,000 kwa kipindi cha miaka mitano (5) kuanzia tarehe 13 Agosti 2012 hadi tarehe 31 Desemba 2017
Mradi wa Maendeleo ya Jamii ni sehemu ya mpango mkakati wa kitaifa wa kuondoa umasikini ulioanzishwa ili kujenga uwezo wa jamii kupata fursa zinazochangia kuboresha maisha kuendana na malengo ya milenia yenye mkakati wa kupunguza umaskini. Lengo la mradi ni kutengeneza mtandao salama wa uzalishaji wa kina, wenye ufanisi na unaolenga kaya maskini kwa jamii ya Tanzania.
4.4.2 Ufadhili
Katika Mwaka wa fedha 2016/2017 Mradi wa Maendeleo ya Jamii ulipokea jumla ya Sh.Tz. 318,577,767,464.44 Pia ulikuwa na salio anzia la Sh.Tz. 36,027,176,101.46 na kufanya jumla ya kiasi kilichokuwepo kwa matumizi kuwa Sh.Tz. 354,604,943,565.90. Aidha mradi umetumia jumla ya Sh.Tz. 324,188,446,473.51 (inajumuisha fedha zilizopelekwa kwa watekeleza miradi) hivyo kubakiwa na kiasi cha Sh.Tz. 30,416,497,092.39, maelezo zaidi yanaoneshwa kwenye jedwali hapo chini:
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 20
Jedwali Na. 8: Ufadhili wa Mfuko Mradi wa Maendeleo ya Jamii Wachangiaji Kiasi (Sh.Tz.)
Salio anzia 1 Julai 2016 36,027,176,101.46 Mapokezi ya Fedha: Shirika la Maendeleo ya Kimataifa 211,484,550,359.60 Programu ya Maendeleo ya Umoja wa Mataifa 339,926,500
Wadau wa Maendeleo 101,631,309,004.60
Jumuiya ya Nchi zinazozalisha Mafuta 5,016,791,166.84
Programu ya Uhifadhi Misitu Binafsi 105,190,433.40
Jumla ya fedha iliyoko 354,604,943,565.90
Matumizi 324,188,446,473.51
Salio ishia Juni 2017 30,416,497,092.39 Chanzo: Taarifa ya fedha ya Mradi wa Maendeleo ya Jamii inayoishia 30 Juni 2017
4.4.3 Fedha za Mradi kwa Serikali za Mitaa
Mamlaka ya serikali za mitaa zilikuwa na jumla ya Sh.Tz 3,074,534,134.34 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za mradi wa maendeleo ya jamii. Ambapo Sh.Tz. 738,939,532.45 zilikua ni salio anzia ambapo Sh.Tz. 2,335,594,601.89 zilipokelewa mwaka huu kwa ajili utekelezaji wa miradi iliyopangwa. Kiasi cha Sh.Tz. 2,124,715,848.17 kilitumika na kubaki na salio ishia la Sh.Tz. 949,818,289.17 ambalo ni sawa na asilimia 31 ya fedha iliyokuwepo kwa ajili ya kukamilisha kazi zilizopangwa.
4.5 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP)
4.5.1 Utangulizi Utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji ulianza mwaka 2007/2008 chini ya usimamizi wa Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Maendeleo ya Sekta ya Maji (NWSDS) ili kutekeleza Mfumo Mkakati wa Sera ya Maji ya Kitaifa ya mwaka 2002. Programu inakusudia kuboresha usimamizi wa vyanzo vya maji kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kwa mazingira endelevu. Pia, inalenga kuhakikisha kuwa makundi yote ya kijamii mijini na vijijini yanapata huduma ya kutosha ya maji safi na salama na usafi wa mazingira. Programu hii
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 21
imefadhiliwa na Serikali ya Tanzania na wadau wa maendeleo, ambapo michango yao inakusanywa katika akaunti ya Mfuko Mkuu wa Sekta ya Maji ulioko Hazina. Fedha huhamishiwa katika akaunti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa ajili ya kuzigawa kwa watekelezaji.
4.5.2 Ufadhili Programu hii imefadhiliwa zaidi na wafadhili watatu ambao ni Shirika la Maendeleo la Shirika la Maendeleo la Kimataifa (IDA) na Shirika la Maendeleo la Ufaransa ambao walichanga fedha katika akaunti ya mfuko wa pamoja wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji iliyoko Hazina. Serikali ya Tanzania na wadau wa maendeleo huchangia fedha hizo kupitia mfuko mkuu wa Hazina.
Katika mwaka huu wa fedha, Programu ya Maendeleo katika Sekta ya Maji ilikuwa na Sh.Tz. 327,444,233,944.32 kwa ajili ya kutekeleza shughuli zake, kati ya hizo, Sh.Tz. 323,165,998,923.32 zilichangwa na wadau wa maendeleo. Matumizi kwa mwaka wa fedha yalikuwa ni Sh.Tz. 317,476,708,862.76 hivyo salio ishia lilikuwa ni Sh.Tz. 9,967,525,081.56. Mchanganuo unaoneshwa kwenye jedwali hapo chini:
Jedwali Na. 9: Vyanzo vya Fedha Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji Wachangiaji Kiasi(Sh.Tz.) Salio anzia 1 Julai 2016 4,278,235,021 Mchango wa Serikali ya Tanzania 67,474,979,764 Mfuko wa Uwekezaji wa Maji Kitaifa (NWIF) 137,429,567,945 Wadau wa Maendeleo – Mfuko Mkuu 65,959,245,377 Wadau wa Maendeleo - Miradi maalumu 50,403,025,774.74 Mchango kutoka kwa Jamii 804,788,043.00 Rekebisho: Kutokana na kubadilika kwa thamani ya kubadilisha fedha za kigeni
1,094,392,019.58
Jumla ya kiasi kilichokuwepo kwa mwaka 327,444,233,944.32 Toa: Matumizi kwa mwaka 317,476,708,862.76 Salio ishia 30 Juni 2017 9,967,525,081.56
Chanzo: Taarifa ya fedha ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji inayoishia 30 Juni 2017
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 22
4.5.3 Fedha zilizopelekwa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, OR-TAMISEMI na SM Kampeni ya Kitaifa ya Usafi wa Mazingira chini ya Programu ya Maendeleo katika Sekta ya Maji (WSDP-NSC) kwa mwaka wa fedha ilikuwa na jumla ya Sh.Tz. 1,219,925,810.55 ambazo zinajumuisha Sh.Tz. 789,256,499 zilizopokelewa na salio anzia kiasi cha Sh.Tz. 430,669,311.55. Kiasi cha Sh.Tz. 817,396,711.27 Kilitumika na kubaki na Sh.Tz. 402,529,099.28. Pia Jumla ya Sh.Tz. 104,296,994,806 zilitumwa kwa SM 180 ambapo salio anzia lilikuwa ni Sh.Tz. 36,112,091,297 na kufanya jumla ya matumizi kuwa Sh.Tz. 140,409,086,103. Mpaka kufikia mwisho wa mwaka, Sh.Tz. 109,015,286,092 zilitumika na kubaki na salio la Sh.Tz. 31,393,800,011. OR-TAMISEMI ilikuwa na jumla ya Sh.Tz. 263,960,572.60. Mwishoni mwa mwaka ilibakia Sh.Tz. 2,672,649.16, ikimaanisha kuwa kiasi cha Sh.Tz. 261,287,923.52 kilitumika ambacho ni sawa na asilimia 99 ya fedha zote kama inavyooneshwa kwenye jedwali la hapo chini:
Jedwali Na. 10: Ufadhili
Maelezo
Kiasi (Sh.Tz.) Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia,
Wazee na Watoto
OR-TAMISEMI SM
Salio anzia 01/07/2016
430,669,311.55 1,933,504.68
36,112,091,297
Ongeza: Fedha iliyopokelewa
789,256,499 262,027,068.52
104,296,994,806
Jumla ya Fedha iliyopo
1,219,925,810.55 263,960,572.68
140,409,086,103
Toa: Matumizi yaliyofanyika
817,396,711.27 261,287,923.52
109,015,286,092
Salio ishia 30/6/2017 402,529,099.28 2,672,649.16
31,393,800,011
Chanzo: Taarifa za fedha Wizara ya Afya na Serikali za Mitaa inayoishia tarehe 30 Juni 2017
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 23
4.6 Miradi Mingine Nimekagua miradi mingine 78 ukiwemo Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na Malaria, UKIMWI na Kifua Kikuu, Taasisi za Umoja wa Mataifa, Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika pamoja na wachangiaji wengine kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo kama vile uboreshaji wa afya, elimu, miundombinu, kupunguza umaskini na kuongeza weledi. Katika mwaka wa Fedha 2016/2017, Miradi Mingine ilipokea kiasi cha Sh.Tz. 1,557,495,429,551.36. Salio anzia kwa Miradi hiyo lilikuwa ni Sh.Tz. 196,728,362,020.74, ambapo kiasi cha Sh.Tz. 1,605,725,330,731.88 kilitumika na kufanya salio ishia kuwa Sh.Tz. 148,498,460,840.22. Bakaa katika miradi hii imetokana na kuchelewa kupokea fedha za miradi; aidha, fedha hizo zilitumika kutekeleza shughuli za miradi ambazo zilikuwa bado kukamilika.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 24
SURA YA TANO
MUHTASARI WA MATOKEO YA UKAGUZI
5.0 Utangulizi Sura hii inatoa mapungufu yaliyobainika wakati wa ukaguzi mbali na mapungufu muhimu kama ilivyooneshwa kwenye Aya namba (ii) ya muhtasari wa mambo muhimu. Mapungufu yaliyobainika ni kama ifuatavyo:
5.1 Masuala ya Usimamizi wa Fedha na Bajeti 5.1.1 Bajeti Iliyoathiriwa Kutokana na Malipo kwa Ajili ya
Matumizi ya Mwaka Uliopita Bila Kibali Sh.Tz. milioni 222.3 Nilibaini kuwa malipo ya kiasi cha Sh.Tz. 222,320,191 yamefanywa na watekeleza miradi ya maendeleo 19 kwa ajili ya kulipia madeni ya mwaka uliopita.
Hata hivyo, hakuna uthibitisho wa kuonesha kwamba malipo hayo ni madeni ya mwaka wa fedha 2015/2016 au yalikuwepo katika bajeti ya mwaka huu wa fedha kinyume na Agizo 22 (1) la Memoranda ya Fedha za Serikali za Mitaa, 2009. Kazi zilizoainishwa kwenye bajeti hazikutekelezwa kama ilivyokusudiwa kutokana na tatizo hili, hivyo, kuathiri malengo ya miradi kwa kiasi kilichoelezwa. Mchanganuo umeoneshwa kwenye kiambatisho Na. 6 (i).
5.1.2 Matumizi ya Fedha za Bakaa Bila Idhini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI Sh.Tz. milioni 872.5 Halmashauri nne (4) zilitumia fedha za bakaa za Mfuko wa Barabara kiasi cha Sh.Tz. 872,487,546 kutekeleza shughuli za mwaka wa fedha 2015/2016 bila kupata kibali toka OR-TAMISEMI kinyume na Aya 3.5 ya Makubaliano ya Mwaka ya Utekelezaji wa Kazi za Barabara Wilayani, Mijini na Mitaani ambayo inaelekeza kuwa matumizi ya fedha za bakaa yapate kibali hicho kutekeleza shughuli mbalimbali zilizobaki. Mchanganuo umeoneshwa kwenye kiambatisho Na. 6 (ii)
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 25
5.1.3 Fedha za Tahadhari Hazikuhamishiwa Kwenye Akaunti ya Mfuko wa Barabara Sh.1.3 Bilioni Nilibaini kuwa Halmashauri 18 zilikata fedha ya tahadhari Sh. 1,275,721,226 na kuweka Mfuko wa Amana bila kuzipeleka kwenye Akaunti ya Mfuko wa Barabara kinyume na Kifungu Na. 5.19 cha Mwongozo wa Kihasibu kwa Serikali za Mitaa, 2009 kinachoelekeza kuwa fedha za tahadhari zilizokatwa zipelekwe kwenye akaunti ya Mfuko wa Barabara (kiambatisho 6 (iii)).
5.1.4 Masurufu Yasiyorejeshwa Sh.Tz. milioni 998.9 Nilibaini kuwa masurufu ya jumla ya Sh.Tz. 998,939,001.22 yaliyotolewa kwa watekeleza miradi 51 kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za mradi hayakurejeshwa katika kipindi cha siku 14 baada ya kukamilika kwa shughuli zilizokusudiwa kinyume na Agizo Na. 40 (3) la Memoranda ya Fedha za Serikali za Mitaa, 2009 na Kanuni Na. 103(1) ya Sheria ya Fedha za Umma, 2001 (kiambatisho Na. 6(iv)).
5.1.5 Malipo Yaliyofanyika kwa Manunuzi ya bidhaa na Huduma Bila Uthibitisho wa Stakabadhi za Kielektroniki Sh.Tz. bilioni 20.5 . Malipo kiasi cha Sh.Tz. 20,465,716,628.81 yalifanywa na watekeleza miradi 199 kwa ajili ya manunuzi ya bidhaa na huduma mbalimbali bila uthibitisho wa stakabadhi za kielekitroniki kinyume na Kanuni Na. 10(5) na 29(1) ya Kanuni za Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mwaka 2012. Kutokudai stakabadhi za kielekitroniki kunapunguza jitihada za Serikali za kukusanya kodi (kiambatisho Na. 6(v)).
5.1.6 Kodi ya Zuio Haikukatwa Kwenye Malipo Sh.Tz. milioni 626.4 Watekeleza miradi walipaswa kwa mujibu wa Kifungu 83(1) (b) cha Sheria ya Kodi ya 2006 kukata kodi ya zuio kutoka kwa wazabuni wa bidhaa na huduma. Kinyume na sheria hiyo, nilibaini kuwa watekeleza miradi 46 hawakukata kodi ya zuio kiasi cha Sh.Tz. 626,419,208.70, hivyo, Serikali kukosa
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 26
mapato kutokana na kodi ambayo haikukusanywa (kiambatisho Na. 6(vi)).
5.1.7 Malipo Yasiyokubalika Sh.Tz. bilioni 6.5 Nilibaini malipo yasiyokubalika kiasi cha Sh.Tz. 6,496,891,250.54 kutoka kwa watekeleza miradi 30 yaliyotokana na kutozingatia matakwa ya makubaliano ya mkataba kuhusu msamaha wa kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambao haukuombwa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA); aidha, kiasi hiki kinahusisha malipo yaliyofanywa kwenye shughuli zisizokubalika (kiambatisho Na. 6(vii)).
5.1.8 Kutokuandaliwa kwa Taaarifa za Mkaguzi wa Ndani Tathmini niliyofanya kwenye idara za ukaguzi wa ndani kwenye miradi inaonesha kuwa idara hizo katika Halmashauri 31 hazikuweza kufanya ukaguzi wa kina wa miradi pamoja na kuandaa taarifa za ukaguzi za robo mwaka zinazohusiana na shughuli za miradi ya Kilimo, Afya, Barabara na Maji. Kushindwa kwa Mkaguzi wa Ndani kufanya ukaguzi wa kina kwenye miradi kunafanya Halmashauri kushindwa kufanya ufuatiliaji na uangalizi wa kutosha wa miradi yao. Kwa mujibu wa nyaraka za makubaliano za miradi, kutokuwa na taarifa za ukaguzi wa ndani kwenye shughuli za miradi ya maendeleo ni kinyume na Aya 8.5 ya Taratibu za Mradi wa Maendeleo ya Kilimo 2006, Aya 6.3(b) ya Mwongozo ya Mpango wa Afya wa Halmashauri 2011, na Aya Na. 8.2.2 ya Mkataba wa Makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Washirika wa Maendeleo ya Februari 2007 (kiambatisho Na. 6(viii)).
5.1.9 Malipo Kwenye Shughuli Zisikokubalika kwa Mujibu wa Kanuni za Mradi Sh.Tz. 1.2 Nilibaini kuwa kiasi cha Sh.Tz. 1,228,926,474 kililipwa na watekeleza miradi kwenye shughuli mbalimbali za afya ambazo ni kinyume na Aya Na. 3.5 (j) ya Mpango Kabambe wa Afya kwa Halmashauri za mwaka 2011 (kiambatisho Na. 6(ix)).
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 27
5.2 Masuala Yanayohusu Manunuzi na Usimamizi wa Mikataba 5.2.1 Mapungufu Kwenye Usimamizi wa Mikataba
Kadhia nyingi za utekelezaji wa majukumu ya kimikataba kwenye manunuzi hutokea kwa sababu ya usimamizi wa mikataba usioridhisha. Ukaguzi wangu ulibaini kasoro mbalimbali kwenye usimamizi wa Mikataba kwa watekeleza miradi 8. Kasoro hizo ni kama vile kutokuwasilishwa kwa dhamana ya utendaji kutoka kwa wakandarasi, kutokukata fedha ya tahadhari, mikataba ambayo haijaidhinishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa mujibu wa sheria, maombi ya kuongeza muda pamoja na mabadiliko ya gharama za mikataba yasiyoridhisha. Ninashauri uboreshaji ufanywe kwenye maeneo niliyoyaainisha; hii ni kwa sababu usimamizi wa mikataba usioridhisha huathiri utekelezaji wa malengo yaliyokusudiwa (kiambatisho Na. 6(x)).
5.2.2 Manunuzi Bila Kibali cha Bodi za Zabuni Sh.Tz. bilioni 1.1 Ukaguzi wangu ulibaini kuwa manunuzi ya bidhaa na huduma ya Sh.Tz 1,136,982,268 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa 27 yalifanyika bila kuwa na kibali cha Bodi za Zabuni kinyume na Kanuni Na. 57 (3) (a) cha Kanuni za Ununuzi wa Umma za 2013 (kiambatisho Na. 6(xi)).
5.2.3 Manunuzi Yaliyofanywa Bila Kushindanisha Wazabuni Sh.Tz. bilioni 1.2 Bilioni Bidhaa zenye thamani ya Sh.Tz. 1,198,574,396.16 zilinunuliwa na watekeleza miradi 51 kutoka kwa wazabuni bila ushindanishi wa bei kwa angalau wazabuni halali 3 kama inavyotakiwa na Kanuni Na. 76 ya Kanuni ya Ununuzi wa Umma, 2013 na Jedwali la Kwanza la Kanuni zinazoongoza taratibu za zabuni katika Halmashauri ya mwaka 2007 (kiambatisho Na. 6 (vxii)).
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 28
5.2.4 Manunuzi ya Bidhaa na Huduma yenye Thamani ya Sh.Tz. milioni 68.3 kwa Fedha Taslimu Nilibaini kuwa watekeleza miradi 8 waliwapa watumishi fedha taslimu Sh.Tz. 68,337,800 kwa ajili ya kununua bidhaa na huduma mbalimbali kinyume na Agizo Na. 68 la Randama ya Fedha za Serikali za Mitaa ya mwaka 2009 na Kanuni 131 ya Ununuzi wa Umma za mwaka 2013 kwa manunuzi ya bidhaa na huduma ambazo zinaelekeza kuwa manunuzi yafanyike kupitia hati maalumu ya manunuzi na hundi (kiambatisho Na. 6(xiii)).
5.2.5 Manunuzi ya Bidhaa na Huduma Kutoka kwa Wazabuni Wasioidhinishwa Sh.Tz. milioni 35.8 Nilibaini kuwa Halmashauri 4 zilifanya manunuzi ya bidhaa na huduma za Sh.Tz. 35,796,483 kutoka kwa wazabuni ambao hawajaidhinishwa na Wakala wa Manunuzi wa Serikali au Bodi ya Zabuni kinyume na Kanuni Na. 57(3) (a) ya Kanuni za Ununuzi wa Umma za mwaka 2013 inayotaka kuwa orodha ya wazabuni waliopendekezwa iidhinishwe na Bodi ya Zabuni ndipo maombi ya nukuu ya bei yapelekwe kwa wazabuni (kiambatisho Na. 5 (xiv)).
5.2.6 Bidhaa Zilizonunuliwa Lakini Hazijapokelewa Sh.Tz. bilioni 6.9 Watekeleza miradi 26 hawakuweza kutoa uthibitisho wa kupokelewa kwa bidhaa zenye thamani ya Sh.Tz. 6,944,728,519.36 zilizonunuliwa kutoka kwa wazabuni mbalimbali kinyume na Agizo Na. 71(1) (b) la Randama ya Fedha za Serikali za Mitaa 2009 na Kanuni Na. 114 za Ununuzi ya Umma, 2013 (kiambatisho Na. 6(xv)).
5.2.7 Vifaa na Mali Ambazo Hazijaandikishwa Kwenye Leja ya Vifaa Sh.Tz. milioni 411.3 Vifaa na mali zenye thamani ya Sh.Tz. 411,311,518 zilinunuliwa na watekeleza miradi 46 havikuandikishwa kwenye leja ya vifaa husika hivyo haikuwa rahisi kwa ukaguzi kufuatilia matumizi ya vifaa hivyo (kiambatisho Na. 6(xvi)).
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 29
5.2.8 Ununuzi wa Vifaa Tiba Bila Idhini ya Bohari Kuu ya Dawa Sh.Tz. milioni 943.8 Nimebaini kwamba Halmashauri 30 walifanya manunuzi ya vifaa tiba vyenye thamani ya Sh.Tz. 943,766,485.50 kutoka kwa wauzaji binafsi bila idhini ya Bohari Kuu ya Dawa (kiambatanisho Na.6 (xvii)).
5.3 Utekelezaji wa Miradi
5.3.1 Miradi Iliyokamilika Lakini Haitumiki Nimefanya uhakiki kwa kutembelea miradi 14 ya ujenzi inayotekelezwa na Halmashauri na kubaini kwamba ujenzi wa miradi hiyo umeshakamilika lakini miradi haijaanza kutumika hivyo faida iliyotarajiwa bado haijapatikana kwa walengwa waliokusudiwa (kiambatisho Na. 6(xvii)).
5.3.2 Upungufu wa Watumishi Katika Idara Zinazotekeleza Miradi Nimebaini upungufu wa watumishi 15,342 katika Halmashauri 335 zinazotekeleza miradi iliyo chini ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo, Mfuko wa Uchangiaji wa Afya, Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji na Mfuko wa Barabara. Upungufu huu wa watumishi huathiri utendaji wa shughuli za miradi (kiambatisho Na. 6(xix)).
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 30
SURA YA SITA
HITIMISHO NA MAPENDEKEZO
6.0 Utangulizi Sura hii inatoa muhtasari wa hitimisho na mapendekezo ya ujumla juu ya mapungufu yaliyobainika wakati wa kaguzi za miradi. Kwa mujibu wa Kifungu Na. 40 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma Namba 11 ya mwaka 2008 na Kanuni 86 na 94 ya Kanuni za Ukaguzi wa Umma za mwaka 2009, Maafisa Masuuli wanatakiwa kuandaa majibu na kuyawasilisha kwa Mlipaji Mkuu wa Serikali.
Mapungufu yaliyobainika yanahusu uzingatiaji wa taratibu, usimamizi wa fedha, udhibiti wa ndani na utawala, ambayo, kwa ujumla, yanahitaji juhudi za uongozi kutekeleza mapendekezo ili kuboresha hali.
Mapungufu mengi yaliyobainika kwa mwaka 2016/2017 yanafanana na yale yaliyojitokeza miaka ya nyuma. Hali hii inaashiria kuwa mapendekezo ya ukaguzi hayazingatiwi na kutekelezwa. Ufuatao hapa chini ni muhtasari wa mapungufu na mapendekezo yaliyotokana na ukaguzi wa miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni 2017.
6.1 Hitimisho la Jumla 6.1.1 Utawala na Uzingatiaji wa Taratibu
Utekelezaji wa mapendekezo ya ukaguzi hayaridhishi, Maafisa Masuuli na watendaji wakuu wa taasisi wamekuwa hawashughulikii mapendekezo yangu ipasavyo; ambapo, mwaka huu kulikuwa na mapendekezo 2,720 sawa na asilimia 35 ya mapendekezo yote ikilinganishwa na mwaka uliopita uliokuwa na mapendekezo 2,688 sawa na asilimia 40.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 31
Kutokutekeleza mapendekezo yangu kunasababisha miradi kuwa na matatizo yanayojirudiarudia.
Matatizo ya kutozingatia taratibu za kibajeti yaligundulika ambapo, nilibaini ucheleweshaji wa fedha katika miradi 257 yenye thamani ya Sh.Tz. bilioni 274.6 kwenda kwa watekeleza miradi 40. Pia nilibaini kuwapo kwa malipo yaliyofanywa kwa kazi ambazo zilikuwa nje ya bajeti ambapo jumla ya Sh.Tz. bilioni 4.3 zilitumika, pamoja na malipo yaliyofanywa kwa kutumia vifungu vya malipo visivyo sahihi ambapo jumla ya Sh.Tz. bilioni 1.1 zililipwa kwa utaratibu huo. Hali ya kutozingatia bajeti huiathiri serikali katika kutekeleza na kufanikisha malengo yake pamoja na kutoa taswira isiyo sawa juu ya matumizi yaliyofanyika kutekeleza kazi za miradi.
6.1.2 Usimamizi wa Fedha na Bajeti
Malipo yenye nyaraka pungufu na kutokuwapo kwa hati za malipo limeendelea kuwa tatizo kubwa na linalotokea kila mwaka. Katika mwaka huu wa ukaguzi nimebaini kutokuwapo kwa hati za malipo yenye thamani ya Sh.Tz. bilioni 8.7 kutoka kwa watekeleza miradi 184. Kama ilivyoelezwa awali, asilimia 52 ya hati zenye mashaka zimesababishwa na ama kuwepo hati za malipo zenye nyaraka pungufu au kukosekana kwa nyaraka za malipo, hivyo kufanya wakaguzi kushindwa kuthibitisha uhalali wa malipo hayo. Tatizo hili linaashiria upungufu katika udhibiti wa ndani ambao umeshindwa kuondolewa na Maafisa Masuuli na watendaji wakuu.
6.1.3 Usimamizi wa Manunuzi
Mapungufu mengi yaliyobainika kwenye upande wa manunuzi yamekuwa yakijirudia mwaka hadi mwaka hali inayofanya nisiridhike na utekelezaji wa mapendekezo ya ukaguzi juu ya manunuzi. Mapungufu yaliyobainika yalikuwa zaidi kwenye manunuzi ya bidhaa, usimamizi wa mikataba ambayo haijahakikiwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kukosekana
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 32
kwa dhamana ya utendaji, pamoja na kuongeza muda wa mikataba iliyokwisha muda bila kufuata utaratibu.
Mapungufu yaliyobainika kwa upande wa manunuzi ya bidhaa na huduma ni manunuzi yaliyofanyika bila kuidhinishwa na bodi ya manunuzi yenye thamani ya Sh.Tz. bilioni 1.1, manunuzi yaliyofanyika kwa fedha taslimu ya Sh.Tz. bilioni 68.3, pamoja na bidhaa zilizonunuliwa lakini hazijapokelewa Sh.Tz. bilioni 7. Mengine ni manunuzi yaliyofanyika bila ushindanishi Sh.Tz. bilioni 1.2, na manunuzi yaliyofanyika toka kwa wazabuni wasioidhinishwa Sh.Tz. bilioni 35.8.
6.2 Mapendekezo ya Jumla Mwisho, kwa mujibu wa mamlaka yaliyokasimishwa kwangu chini Sheria ya Ukaguzi Na. 11 ya Mwaka 2008 kifungu cha 12, nimetoa mapendekezo kadhaa kwa watekeleza miradi ya maendeleo ambayo baadhi ni marejeo ya mapendekezo ya kipindi cha nyuma. Ni imani yangu kuwa, mapendekezo haya yakitekelezwa ipasavyo yatasaidia kuboresha usimamizi wa miradi hii. Mapendekezo hayo ni:- i. Serikali itoe fidia mapema kwa watu waliothibitika
kuwa wameathiriwa na miradi. ii. Maafisa Masuuli na Watendaji Wakuu wanaosimamia
miradi ya maendeleo waweke nguvu zaidi kuhakikisha wanatekeleza mapendekezo ya kaguzi zilizopita kwa muda muafaka ili kuboresha udhibiti wa ndani ili kupunguza uwezekano wa mapungufu hayo kujirudia tena.
iii. Watekeleza miradi wahakikishe kuwa kazi zinatekelezwa kama zilivyoainishwa na bajeti na zinatumika kutoka katika vifungu sahihi vya matumizi.
iv. Watekeleza miradi wahakikishe kuwa wanapeleka kwa
wakati taarifa za uwajibikaji wa fedha kwa wafadhili kwa mujibu wa makubaliano.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 33
v. Maafisa Masuuli wanashauriwa kuongeza udhibiti wa ndani kwenye malipo na usimamizi wa nyaraka ili kuhakikisha kuwa malipo yote yanaidhinishwa ipasavyo na yanakuwa na nyaraka zote zinazohitajika kama inavyotakiwa na Kanuni za Fedha za Umma za mwaka 2001 na Agizo namba 8 (2) (c) ya Randama ya Fedha ya Serilkari za Mitaa ya mwaka 2009.
vi. Maafisa masuuli, watendaji wakuu, bodi za zabuni na
vitengo vya manunuzi wanashauriwa kuhakikisha manunuzi ya bidhaa na huduma yanafuata taratibu za manunuzi kwa mujibu wa Sheria Na. 7 ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2011 na Kanuni zake za mwaka 2013, Agizo Na. 272 la Ramdama ya Fedha ya Serikali za Mitaa ya mwaka 2009 pamoja na makubaliano na wadau wa maendeleo.
vii. Hazina inatakiwa itoe fedha kwa watendaji kulingana
na bajeti.
viii. Watekeleza miradi wawasiliane na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili warejeshewe kodi ya ongezeko la thamani (VAT) waliyolipa.
ix. Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto na Mfuko wa Kimataifa wa Malaria, UKIMWI na Kifua kikuu walipe kiasi cha Sh. 61.4 bilioni kama sehemu ya kuchangia gharama za Bohari ya Dawa ya Taifa. Aidha taratibu zifanyike ili kutambua deni la nyuma na kuweza kuwa na makubaliano ya jinsi ya kulilipa.
x. Watekeleza miradi wanatakiwa kuwasiliana na Hazina ili kuhakikisha kuwa madai ya wakandarasi ya yanalipwa kwa wakati ili kuepuka gharama zitokanazo na ucheleweshaji wa malipo. Aidha watekeleza miradi wanashauriwa kuyapa kipaumbele na kuyawasilisha Hazina madai ya wakandarasi ambayo yana uwezekano wa kuwa na adhabu ya ucheleweshaji endapo hayatalipwa kwa wakati.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 34
xi. Menejimenti ya Mfuko wa Barabara inatakiwa iwasiliane na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) warejeshewe kiasi cha Sh.Tz. 14,828,686,613.55 kinachotokana na makusanyo ya ushuru wa mafuta na usafirishaji.
xii. Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
inatakiwa kurejesha kiasi cha Sh.Tz. 593,320,300 kutoka kwa walipwaji ambao hawakustahili.
xiii. Watekeleza miradi ya Afya wa Halmashauri wanatakiwa kuhakikisha kuwa fedha za miradi ya Afya zinatumika kwa kuzingatia kanuni za Mpango Kabambe wa Afya kwa Halmashauri.
xiv. Halmashauri zinatakiwa kuhakikisha zinapata kibali
kutoka Bohari Kuu ya Dawa kwa manunuzi ya vifaa vya afya kutoka kwa wazabuni binafsi.
xv. Halmashauri ziwasialiane na Ofisi ya Rais Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kuweza kuajiri wafanyakazi kwenye idara zenye upungufu.
xvi. Watekeleza miradi wanatakiwa kukata kodi ya zuio
kutoka kwa watoa huduma na wazabuni kisha kuwasilisha kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndani ya siku saba kama inavyoelekezwa na sheria ya kodi.
xvii. Watekeleza miradi wanatakiwa kutumia fedha
kutokana na vifungu vya matumizi vilivyoidhinishwa ili kuepuka matumizi yasiyohusiana na vifungu hivyo.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 35
VIAMBATISHO
Kiambatisho Na1: Majedwali Yanayochanganua Matokeo ya Uchaguzi 1(i) Fidia Haikulipwa kwa Watu walioathiriwa Kutokana na Utekelezaji wa Miradi
Sh.Tz. 11,870,767,751 – Miradi Mingineyo Na. Jina la Mradi Kiasi (Sh.Tz.)
1 Programu ya Kusaidia Sekta ya Usafirishaji (TSSP) 36,826,419 2 Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Kimataifa Arusha
Taveta/Holili-Voi 308,069,842
3 Programu ya Maendeleo Sekta ya Maji Awamu ya Pili (WSDP II)
11,525,871,490
Jumla 11,870,767,751 1(ii) Kutolipwa kwa Gharama za uchangiaji wa MoHCDGEC na Mfuko wa Global
Sh.Tz. 61,441,762,383.76 – Miradi Mingineyo Na. Jina la Mradi Kiasi (Sh.Tz.)
1 Mfuko Mkuu Mradi wa Ukimwi 58,740,555,793
2 Mfuko Mkuu-Mradi wa Kuimarisha Mifumo ya Afya/Malaria (TZA-H-MoF)
2,701,206,591
Jumla 61,441,762,383.76 1(iii) Tozo ya Riba kwa Kuchelewa Kulipa Madai ya Wakandarasi Kinyume na
Mikataba Iliyoingiwa Sh.Tz. 3,889,404,109.89 – Miradi Mingineyo Na. Jina la Mradi Kiasi (Sh.Tz.)
1 Mradi wa Kusaidia Secta ya Barabara Awamu ya Pili (RSSP II)
368,827,729
2 Mradi wa Kusaidia Secta ya Barabara Awamu ya Kwanza (RSSP I)
425,969,165
3 Programu ya Maendeleo Sekta ya Maji Awamu ya Pili (WSDP II)
3,094,607,216
Jumla 3,889,404,109.89 1(iv) Fedha za Mradi ambazo Hazikurejesha na Zilizolipwa kwa Wasiostahili Sh.Tz.
593.3 Milioni
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi
(Sh.Tz.)
1 Manispaa ya Ilemela 110,616,000 8 Wilaya ya
Kwimba 35,744,000
2 Wilaya ya Tunduru 104,040,000 9 Wilaya ya
Mbinga 29,808,000
3 Wilaya ya Nyasa 55,176,000 10 Wilaya ya
Hanan’g 27,486,800
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 36
4 Wilaya ya Misungwi 54,230,000 11 Wilaya ya
Songea 24,981,500
5 Manispaa ya Songea 53,114,000 12 Wilaya ya
Magu 17,340,000
6 Jiji la Mwanza 38,820,000 13 Wilaya ya
Ukerewe 5,116,000
7 Wilaya ya Babati 36,848,000 Jumla 593,320,300
1(v) Matumizi Yaliyofanywa Nje ya Bajeti Iliyoidhinishwa Sh.Tz. 4,296,264,090.79
Na.
Mradi 2016/17 2015/16 Kiambatisho Kiasi (Sh) Idadi ya
Watekelezaji
Kiasi (Sh) Idadi ya Watekelezaji
1 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
- -
2 Mfuko wa Afya
317,477,737
15
3 Mfuko wa Barabara
2,478,018,798 22 360,822,235
9 2(i)
4 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
1,684,842,224 21
153,398,125
8
2(ii)
5 Mradi wa Maendeleo ya Jamii
99,881,057
.95 1
6 Miradi Mingine
133,403,068.79
3 - -
2(iii)
Jumla 4,296,264,090.79
46 931,579,154.95
33
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 37
1(vi) Fedha za Ruzuku Zilizopelekwa kwenye Miradi Pungufu ya Makadirio Sh.Tz. 274,647,963,420.86
Na.
Mradi 2016/17 2015/16 Kiambatisho Kiasi
(Sh.Tz.)
Idadi ya Watekelezaji
Kiasi (Sh.Tz.) Idadi ya Watekelezaji
1
Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
12,422,089,195
22
32,112,617,666
82 2(iv)
2 Mfuko wa Afya
- -
2,484,410,599 4
3 Mfuko wa Barabara
54,434,454,840 101
51,198,910,064.90
112 2(v)
4
Mradi wa Maendeleo ya Jamii
-
-
- -
5
Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
115,619,475,913.86
128
45,750,660,553.43
79 2(vi)
6 Miradi Mingine
92,171,943,47
1
6
- -
2(vii)
Jumla 274,647,963,
420.86 257
131,546,598,883.33
277
1(vii) Kuchelewa Kukamilika kwa Kazi za Miradi
Na. Mradi 2016/17 2015/16 Kiambatisho Upungufu wa
Rasilimali Watu
Idadi ya Watekelezaji
Upungufu wa
Rasilimali Watu
Idadi ya
Watekelezaji
2 Mfuko wa 2,567,237,86 10 2(viii)
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 38
Barabara 0 3 Programu
ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
49,930,751,595
22
- -
2(ix)
Jumla 52,497,989,455
32 - -
1(viii) Malipo Yenye Nyaraka Pungufu Sh.Tz. 7,248,937,125.89 Na. Mradi 2016/17 2015/16 Kiambatish
o Kiasi (Sh.Tz.) Idadi ya Watekelezaj
i
Kiasi (Sh.Tz.)
Idadi ya
Watekelez
aji
1 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
19,741,484 5
2 Mfuko wa Afya
948,295,388.66
52 1,392,755,769
49 2(x)
3 Mfuko wa Barabara
1,701,447,185 28 2,170,524,788.33
35 2(xi)
4 Mradi wa Maendeleo ya Jamii
234,228,822.36
11 1,663,559,25
7.53 39
2(xii)
5 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
946,059,557 56
3,162,270,377.15
45
2(xiii)
6 Miradi Mingine
3,492,827,252.81
18 - -
2(xiv)
Jumla 7,248,937,125.89
163 8,408,851,676
173
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 39
1(ix) Kukosekana kwa Hati za Malipo Na. Mradi 2016/17 2015/16 Kiamba
tisho Kiasi (Sh.Tz.) Idadi ya
Watekelezaji
Kiasi (Sh.Tz.) Idadi ya
Watekelezaji
1 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
85,077,600 1
- -
2(xv)
2 Mfuko wa Afya
165,568,036 13 385,397,225.15 14
2(xvi)
3 Mfuko wa Barabara
- - 1,509,442,825.
67 9
4 Mradi wa Maendeleo ya Jamii
- -
- -
5 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
411,013,346.88 6
307,362,062.88 14
2(xvii)
6 Miradi Mingine
802,847,155 1
2(xviii)
Jumla 1,464,506,137
.88 21 2,202,202,114 37
1(x) Kutokuomba madai ya marejesho ya kodi ya ongezeko la thamani Sh.Tz. 1,588,581,132.46
Na. Mradi 2016/17 2015/16 Kiambatisho Kiasi (Sh.Tz.) Idadi
ya Watekelezaji
Kiasi (Sh.Tz.)
Idadi ya
Watekelez
aji
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 40
1 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
- -
2 Mfuko wa Afya
3 Mfuko wa Barabara
- -
4 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
309,357,157.86
9
- -
2(xix)
5 Mradi wa Maendeleo ya Jamii
- -
6 Miradi Mingine
1,279,223,974.60
7 - -
2(xx)
Jumla 1,588,581,132.46
16 - -
1(xi) Matumizi Yaliyofanywa kwa Kutumia Vifungu Visivyohusika Sh.Tz.
1,091,406,059
Na Mradi
2016/17 2015/16
Kiambatisho
Kiasi (Sh.Tz.)
Idadi ya Watekel
ezaji
Kiasi (Sh.Tz.)
Idadi ya
Watekelezaji
1 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
5,117,000 1
- -
2(xxi)
2 Mfuko wa Afya
323,787,186 20 148,597,260
17 2(xxii)
3 Mfuko wa Barabara
25,772,473 4
119,867,143 11
2(xxiii)
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 41
4 Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
123,053,297 16
272,249,303
12
2(xxiv)
5 Miradi Mingine
613,676,103 2 -
2(xxv)
Jumla 1,091,406,
059 43 540,713,706 40
Kiambatisho Na 2: Cha Majedwali Yanayochanganua Kiambatisho Na. 1 2(i) Matumizi Yaliyofanywa Nje ya Bajeti Iliyoidhinishwa Sh.Tz. 2,478,018,798 -
Mfuko wa Barabara
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Manispaa ya Ilemela 670,228,757 12 Wilaya ya
Magu 13,936,970
2 Wilaya ya Makete 589,059,776 13 Wilaya ya
Mbarali 11,822,200
3 Mji wa Makambako 588,897,903.60 14 Wilaya ya
Kalambo 9,673,810
4 Wilaya ya Nyasa 245,371,625 15 Wilaya ya
Pangani 6,907,800
5 Manispaa ya Kigoma Ujiji 132,932,664 16 Wilaya ya
Muheza 5,000,000
6 Wilaya ya Kigoma 56,998,720 17 Wilaya ya
Singida 3,350,000
7 Wilaya ya Busokelo 46,450,000 18 Wilaya ya
Turiani 3,266,202
8 Wilaya ya Mbeya 22,718,670 19 Wilaya ya
Moshi 3,250,000
9 Wilaya ya Momba 22,613,000 20 Wilaya ya
Bagamoyo 3,046,200
10 Mji wa Tarime 19,712,500 21 Mji wa Kasulu 2,650,000
11 Wilaya ya Sumbawanga 17,852,000 22 Mji wa Nzega 2,280,000
Jumla 2,478,018,798 2(ii) Matumizi Yaliyofanywa Nje ya Bajeti Iliyoidhinishwa Sh.Tz. 1,684,842,224 - Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya 703,286,324 12 Wilaya ya 11,078,400
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 42
Wanging’ombe Mafia
2 Manispaa ya Songea 294,056,000 13
Wilaya ya Kondoa 10,172,014
3 Wilaya ya Arusha 226,741,332 14
Wilaya ya Mkuranga 9,468,760
4 Wilaya ya Makete 213,612,832 15
Wilaya ya Chemba 8,546,000
5 Wilaya ya Ileje 57,182,673 16 Wilaya ya Chalinze 7,339,000
6 Wilaya ya Namtumbo 40,000,000 17
Wilaya ya Hanang’ 2,569,000
7 Wilaya ya Mkuranga 23,144,500 18
Wilaya ya Mpanda 2,330,000
8 Wilaya ya Iringa 20,689,000 19 Wilaya ya Buchosa 2,321,389
9 Manispaa ya Iringa 19,578,000 20
Wilaya ya Nzega 2,090,000
10 Wilaya ya Kilolo 16,790,000 21 Wilaya ya Missenyi 1,847,000
11 Wilaya ya Itilima 12,000,000 Jumla
1,684,842,224
2(iii) Matumizi Yaliyofanywa Nje ya Bajeti Iliyoidhinishwa Sh.Tz. 133,403,068.79 –
Miradi Mingine Na. Jina la Mradi Kiasi (Sh.Tz.)
1 Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani 51,853,500 2 Mradi wa Mtandao wa Afya kwa Umma Afrika
Mashariki (EAPHN) 76,989,568.79
3 Mradi wa Upanuzi wa Uzalishaji wa Mpunga (ERPP) 4,560,000
Jumla 133,403,068.79 2(iv) Fedha za Ruzuku Zilizopelekwa kwenye Miradi Pungufu ya Makadirio Sh.Tz.
12,422,089,195 - Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo Na. Halmashauri Kiasi (Sh) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Tunduru 2,242,225,000 13
Wilaya ya Kalambo 256,358,919
2 Wilaya ya Mpanda 1,809,693,900 14
Wilaya ya Nkasi 241,858,400
3 Wilaya ya Mbozi 1,661,743,099 15
Wilaya ya Geita 166,750,000
4 Wilaya ya Momba 1,081,755,000 16
Manispaa ya Sumbawanga 154,078,000
5 Wilaya ya Mufindi 1,031,484,000 17
Wilaya ya Ruangwa 144,500,000
6 Wilaya ya Hai 949,982,500 18
Wilaya ya Itilima 128,242,100
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 43
7 Wilaya ya Simanjiro 485,165,000 19
Wilaya ya Mlele 121,000,000
8 Manispaa ya Mpanda 410,817,500 20
Wilaya ya Songea 107,000,000
9 Wilaya ya Maswa 374,135,200 21
Wilaya ya Meatu 70,050,800
10 Mji wa Korogwe 323,462,070 22
Wilaya ya Nsimbo 65,000,000
11
Wilaya ya Sumbawanga 302,787,707 Jumla 12,422,089,195
12 Wilaya ya Bagamoyo 294,000,000
2(v) Fedha za Ruzuku Zilizopelekwa kwenye Miradi Pungufu ya Makadirio Sh.Tz. 54,434,454,840 - Mfuko wa Barabara
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Jiji la Tanga 2,753,827,477 52 Mji wa Bunda 443,369,201
2 Wilaya ya Ruagwa 1,865,078,049 53 Wilaya ya
Manyoni 438,473,710.05
3 Wilaya ya Temeke
1,807,791,112.12 54 Wilaya ya
Kyela 426,442,103
4 Manispaa ya Moshi
1,686,873,478.34 55 Wilaya ya
Mpimbwe 424,128,159
5 Wilaya ya Kigamboni 1,674,532,003 56 Wilaya ya
Longido 410,715,061
6 Wilaya ya Bahi
1,620,701,854.55 57 Manispaa ya
Bukoba 401,702,856.80
7 Jiji la Mwanza 1,329,389,520 58 Wilaya ya
Hanang' 401,331,083.50
8 Jiji la Arusha 1,278,888,060 59 Wilaya ya Kasulu 395,852,784
9 Manispaa ya Kilwa 1,128,578,970 60 Wilaya ya
Karagwe 394,624,250
10 Wilaya ya Maswa DC
1,038,259,630.76 61 Mji wa
Kabaha 387,595,317
11 Manispaa ya Tabora
1,016,876,208.08 62 Wilaya ya
Babati 384,125,976
12 Wilaya ya Kilwa 988,841,698 63 Wilaya ya
Buhigwe 359,291,426
13 Wilaya ya Chamwino 987,495,903 64 Mkalama 356,077,947
14 Wilaya ya Karatu 959,843,956 65 Wilaya ya
Shinyanga 354,359,741.15
15 Manispaa ya Dodoma 859,521,152 66 Wilaya ya
Ikungi 349,987,609
16 Mji wa Njombe 857,028,742 67 Wilaya ya
Tunduru 311,874,367
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 44
17 Wilaya ya Urambo 856,916,409.71 68 Wilaya ya
Muleba 307,610,844
18 Wilaya ya Handen 834,319,137 69 Manispaa ya
Iringa 294,479,128
19 Wilaya ya Kongwa 820,261,463 70 Wilaya ya
Songwe 291,845,421
20 Wilaya ya Geita 797,016,625 71 Manispaa ya
Sumbawanga 262,854,336
21 Wilaya ya Igunga 773,196,282.53 72 Manispaa ya
Shinyanga 259,895,764.11
22 Manispaa ya Mpanda 739,802,047 73 Wilaya ya
Nachingwea 247,895,130
23 Wilaya ya Monduli 735,274,061.46 74 Mji wa
Babati 220,443,605
24 Wilaya ya Liwale 724,123,864 75 Wilaya ya
Ngorongoro 197,992,738
25 Mji wa Kondoa 698,799,887.91 76 Mji wa
Bariadi 197,770,255.31
26 Wilaya ya Muheza 698,509,991 77 Wilaya ya
Ludewa 195,716,263
27 Wilaya ya Lushoto 681,832,865 78 Wilaya ya
Bumbuli 188,319,075
28 Mji wa Mbinga 676,953,212 79 Wilaya ya
Missenyi 182,555,413
29 Wilaya ya Kyerwa 669,184,171 80 Mji wa Geita 156,278,893.22
30 Wilaya ya Kilindi 660,854,154 81 Wilaya ya
Nyang'hwale 153,600,627
31 Manispaa ya Ilala 655,503,604 82 Wilaya ya
Bukoba 152,020,506.08
32 Wilaya ya Kibondo 612,208,257 83 Wilaya ya
Rorya 146,895,631
33 Mji wa Kasulu 611,149,676 84 Wilaya ya
Butiama 144,174,446
34 Wilaya ya Sengerema 610,005,516 85 Wilaya ya
Chemba 142,937,784.68
35 Manispaa ya Songea 551,849,413 86 Wilaya ya
Hai 138,227,891
36 Wilaya ya Bukombe 528,595,870.65 87 Wilaya ya
Namtumbo 133,529,942.18
37 Jiji la Mbeya 521,144,983 88 Wilaya ya Kakonko 119,319,250
38 Wilaya ya Iramba 514,974,501 89 Wilaya ya
Sumbawanga 115,947,334
39 Mji wa Mafinga 514,437,364 90 Wilaya ya
Ngara 112,785,467
40 Wilaya ya Kabaha 506,316,527 91 Wilaya ya
Biharamulo 106,602,544
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 45
41 Wilaya ya Makete 502,003,818 92 Wilaya ya
Kondoa 99,719,648
42 Wilaya ya Pangani 501,473,413 93 Wilaya ya
Kalambo 91,758,970
43 Mji wa Mbulu 499,777,858 94 Wilaya ya Meru 80,743,725
44 Wilaya ya Bagamoyo 492,577,385 95 Wilaya ya
Rombo 80,263,746.48
45 Wilaya ya Kwimba 492,405,138 96 Wilaya ya
Mbarali 78,444,652
46 Wilaya ya Kishapu 471,239,635 97 Wilaya ya
Chato 70,000,000
47 Wilaya ya Mkinga 468,813,640 98 Wilaya ya
Same 51,618,130
48 Wilaya ya Momba 460,652,597 99 Wilaya ya
Korogwe 34,282,004
49 Wilaya ya Buchosa 455,658,858 100 Mji wa
Tunduma 25,752,289
50 Wilaya ya Rufiji 454,208,761 101 Wilaya ya
Mwanga 13,010,676.68
51 Mji wa Handeni 453,642,320 Jumla 54,434,454,84
0 2(vi) Fedha za Ruzuku Zilizopelekwa kwenye Miradi Pungufu ya Makadirio Sh.Tz.
115,619,475,913.86 - Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Longido
5,383,177,978.85 65 Wilaya ya
Gairo 603,991,052
2 Wilaya ya Kilindi 3,338,291,328 66 Mji wa
Tarime 603,821,886.36
3 Wilaya ya Geita 3,073,381,401 67 Wilaya ya
Karatu 592,818,397
4 Wilaya ya Mbinga 2,971,890,230 68 Wilaya ya
Handeni 578,052,893
5 Wilaya ya Nkasi 2,949,204,911 69 Wilaya ya
Namtumbo 551,076,346
6 Wilaya ya Kwimba 2,817,934,350 70 Wilaya ya
Korogwe 547,330,302
7 Wilaya ya Kakonko 2,709,291,881 71 Wilaya ya
Pangani 547,109,947
8 Wilaya ya Mbeya 2,696,272,729 72 Wilaya ya
Kishapu 525,957,784
9 Wilaya ya Morogoro 2,506,109,645 73 Mji wa Geita 505,913,353
10 Wilaya ya Uvinza 2,476,781,765 74 Manispaa ya
Mpanda 504,876,029
11 Wilaya ya Mkinga 2,467,339,069 75 Mji wa
Masasi 493,669,208
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 46
12 Wilaya ya Musoma 2,384,476,034 76 Mji wa
Mafinga 487,000,000
13 Wilaya ya Mlele 2,307,614,801 77 Wilaya ya
Nzega 477,162,858
14 Wilaya ya Rombo 2,205,666,104 78 Jiji la
Mwanza 474,908,873
15 Wilaya ya Missenyi 2,187,874,055 79 Manispaa ya
Bukoba 461,231,216
16 Wilaya ya Wanging’ombe
2,012,417,182 80 Wilaya ya Kibondo 429,467,284
17 Wilaya ya Mbulu
1,971,994,772.53 81 Wilaya ya
Muheza 383,055,130.88
18 Wilaya ya Kibaha 1,820,721,507 82 Wilaya ya
Tabora 359,181,812
19 Wilaya ya Misungwi 1,811,666,335 83 Manispaa ya
Moshi 355,167,448
20 Wilaya ya Ulanga 1,784,558,014 84 Wilaya ya
Busokelo 342,586,199
21 Manispaa ya Iringa 1,768,542,550 85 Wilaya ya
Chamwino 334,732,073
22 Wilaya ya Meru
1,749,388,692.30 86 Wilaya ya
Tandahimba 322,581,070.21
23 Wilaya ya Chemba 1,735,576,234 87 Wilaya ya
Muleba 290,179,820
24 Mji wa Makambako 1,645,455,434 88 Manispaa ya
Mtwara 285,665,622
25 Wilaya ya Kongwa 1,617,237,990 89 Wilaya ya
Igunga 282,971,845
26 Wilaya ya Monduli
1,471,526,146.37 90 Wilaya ya
Buhigwe 280,252,217
27 Wilaya ya Ngara 1,448,997,886 91 Wilaya ya
Nachingwea 265,159,089
28 Wilaya ya Lindi 1,440,282,370 92 Wilaya ya
Kyerwa 263,116,552
29 Wilaya ya Kigoma 1,424,139,736 93 Wilaya ya
Tarime 228,301,000
30 Wilaya ya Babati 1,416,616,666 94 Wilaya ya
Kiteto 221,589,043.60
31 Wilaya ya Makete 1,357,523,088 95 Wilaya ya
Ngorongoro 213,616,665
32 Wilaya ya Songea 1,348,174,613 96 Wilaya ya
Sengerema 207,338,355
33 Wilaya ya Mpwapwa 1,331,169,121 97 Manispaa ya
Singida 207,017,906
34 Wilaya ya Arusha
1,162,489,613.72 98 Wilaya ya
Urambo 195,491,140
35 Mji wa Kasulu 1,146,677,125 99 Wilaya ya
Bukombe 191,182,349.40
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 47
36 Mji wa Handeni 1,129,939,000 100 Wilaya ya
Newala 185,000,000
37 Wilaya ya Bariadi 1,111,514,000 101 Mji wa
Bunda 184,990,000
38 Wilaya ya Butiama 1,102,223,283 102 Wilaya ya
Singida 183,388,133
39 Wilaya ya Kisarawe 1,084,910,209 103 Manispaa ya
Kigamboni 178,000,000
40 Mji wa Kondoa 1,068,386,580 104 Mji wa
Kahama 168,491,351
41 Wilaya ya Bahi 1,042,102,617 105 Wilaya ya
Manyoni 164,068,000
42 Wilaya ya Mkuranga 1,033,794,800 106 Wilaya ya
Momba 162,818,967
43 Wilaya ya Nyang’hwale 1,030,358,836 107 Wilaya ya
Mkalama 154,743,737
44 Wilaya ya Ikungi 1,024,178,721 108 Wilaya ya
Bukoba 120,486,349
45 Wilaya ya Nyasa 1,004,923,378 109 Mji wa
Babati 118,629,653.36
46 Wilaya ya Mvomero 991,758,098 110 Wilaya ya
Kilolo 104,059,726
47 Wilaya ya Lushoto 967,297,857 111 Manispaa ya
Temeke 95,741,520
48 Manispaa ya Songea 909,383,838 112 Manispaa ya
Tabora 93,735,157
49 Wilaya ya Njombe 889,472,416 113 Jiji la Mbeya 75,124,149
50 Wilaya ya Mpimbwe 862,967,578 114 Wilaya ya
Msalala 74,332,363
51 Wilaya ya Mufindi 857,601,677 115 Wilaya ya
Same 66,648,003
52 Manispaa ya Sumbawanga 816,814,147 116 Wilaya ya
Rorya 65,838,409
53 Wilaya ya Kaliua 801,352,219 117 Jiji la Arusha 64,697,294
54 Wilaya ya Kalambo 767,690,017 118 Wilaya ya
Kilombero 63,252,733
55 Wilaya ya Hai 755,482,522.74 119 Wilaya ya
Liwale 59,344,511
56 Wilaya ya Kondoa 731,460,188 120 Wilaya ya
Simanjiro 49,522,529.57
57 Mji wa Tunduma 719,274,000 121 Wilaya ya
Tunduru 49,241,761
58 Wilaya ya Malinyi 707,000,000 122 Wilaya ya
Kibiti 46,966,960
59 Wilaya ya Nsimbo 700,804,416 123 Manispaa ya
Kinondoni 45,528,760
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 48
60 Wilaya ya Mpanda 689,500,386 124 Manispaa ya
Ilala 43,433,922
61 Wilaya ya Chalinze 689,500,000 125 Wilaya ya
Serengeti 41,171,446.60
62 Wilaya ya Iramba 650,536,670 126 Manispaa ya
Musoma 22,845,321
63 Wilaya ya Kasulu 626,687,457 127 Mji wa Mbulu 8,908,000
64 Manispaa ya Shinyanga
606,258,124.37 128 Wilaya ya
Siha 1,260,000
Jumla 115,619,475,91
3.86 2(vii) Fedha za Ruzuku Zilizopelekwa kwenye Miradi Pungufu ya Makadirio Sh.Tz.
92,169,943470.94 – Miradi Mingine Na. Jina la Mradi Kiasi (Sh.Tz.)
1 Programu ya Miundombinu ya Masoko, Ongezeko la Thamani na Msaada wa Fedha Vijijini (MIVARF) 50,964,553,843
2 Mradi wa Maboresho ya Mahakama Yanayomlenga Mwananchi na Utoaji wa Haki 8,788,077,105
3 Programu ya Kusaidia Elimu ya Ufundi, Mafunzo na Elimu ya Ualimu (STVET-TE)
23,041,670,839
4 Mfuko Mkuu-Mradi wa Kuimarisha Mifumo ya Afya/Malaria (TZA-H-MoF)
671,442,554
5 Programu ya Maendeleo Sekta ya Maji Awamu ya Pili (WSDP II) 4,472,231,940
6 Programu ya Mageuzi/Mabadiliko ya Usimamizi wa Fedha za Umma IV (PFMRP)
4,231,967,190
7 Programu ya Maendeleo Sekta ya Maji Awamu ya Pili (WSDP II) 2,000,000
Jumla 92,171,943,471 2(viii) Kuchelewa Kukamilika kwa Kazi za miradi zenye thamani ya Sh.Tz. 49,930,751,595 - Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Karagwe
7,933,095,024 12
Wilaya ya Iramba
966,174,000
2 Wilaya ya Uvinza
6,628,991,988 13
Wilaya ya Tunduru
931,018,891
3 Mji wa Njombe
4,767,460,498 14
Wilaya ya Monduli
868,071,873
4 Wilaya ya Mbarali
4,691,403,987 15
Wilaya ya Kigoma
786,642,000
5 Wilaya ya 4,088,187,022 16 Wilaya ya 614,500,000
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 49
Kasulu Chato
6 Wilaya ya Namtumbo
3,985,728,126 17
Wilaya ya Biharamulo
562,540,800
7 Wilaya ya Missenyi
3,414,923,930 18
Wilaya ya Karatu
505,883,635
8 Wilaya ya Ulanga
3,006,636,441 19
Manispaa ya Lindi
483,720,490
9 Wilaya ya Kondoa
1,913,272,568 20
Wilaya ya Chunya
405,317,000
10 Wilaya ya Kibaha
1,490,202,720 21
Manispaa ya Bukoba
378,290,088
11 Wilaya ya Arusha
1,335,490,514.16 22
Wilaya ya Mwanga
173,200,000
Jumla 49,930,751,59
5 2(ix) Kuchelewa Kukamilika kwa Kazi za Mkataba zenye thamani ya Sh.Tz.
2,567,237,860 – Mfuko wa Barabara Na Halmash
auri Mkandarasi Jumla ya
Mkataba (Sh)
Tarehe ya Ukomo
Tarehe ya
Uhakiki
Ucheleweshaji(Siku)
1
Wilaya ya Bukoba
Nyamweza Enterprises of Karagwe
99,607,000 24/08/2017
10-06-17 43
2
Wilaya ya Makambako
M/s GS Contractor CO LTD
293,979,300
28/03/2017
21/09/17 178
3
Wilaya ya Mbeya
Globalink General Contractors Limited
613,042,214
27/04/2017
08-01-17 92
4
Wilaya ya Karagwe
M/S Jossam and Company Limited
678,230,960
1-8-2017 29/08/17 28
5
Wilaya ya Ngorongoro
M/S Maheris Construction and General Supplies
60,245,000 3-8-2017 09-01-17 31
6
MS RAY 69,470,000 27/08/2017
10-01-17 35
Wilaya ya M/S J.P.Traders
121,800,190
21/6/2017 17/08/17 56
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 50
M/S Sengo Construction Co. Ltd
197,247,856
22/6/2017 17/08/17 55
7 Buhigwe Various 336,173,533
13/09/2017
28/09/17 9
9 Wilaya ya Moshi
Chome construction Co. LTD
97,441,807 23/02/2017
15/11/17 265
10 Wilaya ya Mkuranga
M/S Kerry Company Limited
147,091,720
13/10/2017
11-11-17 29
M/S Mashauri Trading Company Limited
119,313,460
21/09/2017
11-10-17 50
M/S Jonenac Construction Limited
43,084,750 21/07/2017
11-10-17 112
Jumla 2,567,237,860
2(x) Malipo Yenye Nyaraka Pungufu Sh.Tz. 948,295,388.66 - Mfuko wa Afya
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Chalinze 80,870,477 27 Wilaya ya Magu 9,771,300
2 Wilaya ya Siha 52,388,044 28 Wilaya ya Same 9,380,000
3 Manispaa ya Shinyanga 49,318,460 29 Wilaya ya
Sumbawanga 8,772,796
4 Wilaya ya Rombo 49,095,714 30 Mji wa Geita 8,475,000
5 Wilaya ya Kongwa 48,903,210 31 Manispaa ya
Ilemela 8,270,000
6 Wilaya ya Hai 47,728,851.06 32 Wilaya ya Kisarawe 7,620,411
7 Mji wa Kahama 45,876,317 33 Wilaya ya
Misungwi 7,606,000
8 Wilaya ya Iramba 45,152,517 34 Wilaya ya
Bumbuli 7,000,000
9 Manispaa ya Temeke 41,035,923 35 Wilaya ya Nyasa 6,781,980
10 Wilaya ya Msalala 37,327,305.60 36 Wilaya ya Nzega 6,655,000
11 Wilaya ya Chato 31,531,806 37 Wilaya ya Mbozi 6,000,000
12 Wilaya ya Urambo 27,225,000 38 Wilaya ya
Hanang 5,885,500
13 Wilaya ya Longido 26,027,378 39 Wilaya ya
Kasulu 5,142,000
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 51
14 Manispaa ya Moshi 25,105,000 40 Wilaya ya
Bagamoyo 4,503,329
15 Wilaya ya Rufiji 24,343,700 41 Mji wa Kondoa 4,275,540
16 Mji wa Korogwe 23,066,739 42 Mji wa Mbulu 4,226,570
17 Wilaya ya Moshi 22,872,946 43 Wilaya ya
Songwe 3,655,400
18 Mji wa Kibaha 21,141,073 44 Wilaya ya Busokelo 3,636,915
19 Wilaya ya Tandahimba 19,776,000 45 Mji wa Njombe 3,613,000
20 Wilaya ya Nkasi 18,149,339 46 Mji wa
Nanyamba 3,336,000
21 Wilaya ya Karatu 17,640,839 47 Wilaya ya
Mkuranga 3,230,000
22 Wilaya ya Wang'ing'ombe
16,931,058 48 Manispaa ya Singida 3,050,000
23 Wilaya ya Mbogwe 14,011,471 49 Wilaya ya Mbulu 2,309,000
24 Manispaa ya Songea 13,641,680 50 Manispaa ya
Dodoma 1,373,000
25 Wilaya ya Lushoto 12,155,800 51 Wilaya ya
Sikonge 1,210,000
26 Wilaya ya Muheza 9,900,000 52 Wilaya ya
Igunga 1,200,000
Jumla 948,295,388.66
2(xi) Malipo Yenye Nyaraka Pungufu Sh.Tz. 1,701,447,185 – Mfuko wa Barabara
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Manispaa ya Moshi 403,345,869 15 Wilaya ya
Kondoa 24,036,317
2 Wilaya ya Nanyumbu 190,679,576 16 Wilaya ya
Kilolo 21,369,052
3 Wilaya ya Kishapu 154,653,126 17 Wilaya ya
Meru 19,787,495
4 Wilaya ya Momba 149,979,439 18 Wilaya ya
Makete 14,020,000
5 Wilaya ya Kibaha 136,288,525 19 Wilaya ya
Longido 11,912,773
6 Wilaya ya Serengeti 124,678,077.13 20 Wilaya ya
Magu 9,325,000
7 Wilaya ya Busokelo 86,913,137 21 Wilaya ya
Iringa 8,915,239
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 52
8 Manispaa ya Mpanda 85,298,060 22 Wilaya ya
Kigoma 7,598,017
9 Wilaya ya Shinyanga 64,221,546.90 23 Wilaya ya
Nsimbo 7,333,353
10 Mji wa Babati 43,188,013 24 Wilaya ya
Moshi 4,740,503.80
11 Wilaya ya Songea 35,571,114 25 Mji wa Geita 3,500,000
12 Wilaya ya Mbozi 32,242,084 26 Wilaya ya
Mkuranga 2,265,000
13 Mji wa Makambako 31,374,981 27 Manispaa ya
Dodoma 1,619,004
14 Wilaya ya Bagamoyo 25,514,505 28 Wilaya ya
Nyang'hwale 1,077,378
Jumla 1,701,447,185
2(xii) Malipo Yenye Nyaraka Pungufu Sh.Tz. 234,228,822.39 - Mradi wa Maendeleo ya Jamii
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Ngara 66,421,500 7 Wilaya ya
Kyela 6,060,000
2 Mji wa Makambako 54,517,117 8 Wilaya ya
Bukombe 3,427,720
3 Wilaya ya Mbinga 42,244,500 9 Wilaya ya
Kyerwa 2,600,000
4 Wilaya ya Wang’ing’ombe
22,574,001 10 Wilaya ya Makete 1,717,640
5 Wilaya ya Musoma 21,254,908.36 11 Wilaya ya
Nkasi 1,666,436
6 Wilaya ya Misenyi 11,745,000 Jumla
234,228,822.36
2(xiii) Malipo Yenye Nyaraka Pungufu Sh.Tz. 946,059,557 – Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Ukerewe 207,477,136 29
Wilaya ya Mbinga 9,295,800
2 Wilaya ya Missenyi 119,479,431 30 Wilaya ya
Bunda 9,239,880
3 Wilaya ya Simanjiro 48,840,000 31
Wilaya ya Kwimba 8,698,328
4 Wilaya ya Musoma 32,650,793 32
Wilaya ya Mafia 8,290,700
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 53
5 Wilaya ya Ngorongoro 30,675,534.40 33
Wilaya ya Kibiti 7,898,400
6 Wilaya ya Nkasi 30,064,817 34 Wilaya ya Kibaha 7,716,024.52
7 Wilaya ya Kasulu 26,846,933 35
Wilaya ya Iramba 7,583,480
8 Mji wa Korogwe 25,365,141 36
Wilaya ya Uvinza 7,138,000
9 Wilaya ya Sumbawanga 23,166,423 37
Wilaya ya Kisarawe 6,452,000
10 Wilaya ya Mkuranga 22,950,000 38 Wilaya ya
Itigi 5,982,065
11 Wilaya ya Ileje 21,024,614 39 Wilaya ya Kongwa 5,117,680
12 Wilaya ya Makete 20,598,160 40
Wilaya ya Mbeya 4,920,000
13 Wilaya ya Momba 20,349,010 41
Manispaa ya Temeke 4,920,000
14 Manispaa ya Mtwara 18,019,000 42 Manispaa ya
Singida 4,504,000
15 Wilaya ya Buchosa 15,541,389 43
Wilaya ya Moshi 4,439,191.40
16 Wilaya ya Kibondo 14,083,000 44
Mji wa Kahama 3,972,669
17 Wilaya ya Longido 14,000,646.68 45
Manispaa ya Kigoma Ujiji 3,556,896
18 Wilaya ya Hai 13,256,000 46 Wilaya ya Mufindi 3,146,140
19 Wilaya ya Kilindi 13,113,294 47
Wilaya ya Kiteto 3,035,000
20 Wilaya ya Rufiji 12,809,527 48
Wilaya ya Madaba 2,923,100
21 Wilaya ya Msalala 11,459,440 49
Wilaya ya Buhigwe 2,919,500
22 Wilaya ya Pangani 10,720,000 50 Wilaya ya
Mkinga 2,583,639
23 Wilaya ya Nsimbo 10,425,000 51 Mji waTarime 2,368,400
24 Wilaya ya Karagwe 10,000,000 52
Wilaya ya Hanang’ 1,775,000
25 Jiji la Mwanza 10,000,000 53 Wilaya ya Bukombe 1,610,000
26 Wilaya ya Rombo 9,956,000 54 Jiji la Arusha 1,440,000
27 Manispaa ya Shinyanga 9,595,000 55
Wilaya ya Sengerema 1,360,000
28 Wilaya ya Monduli 9,547,374.60 56
Wilaya ya Manyoni 1,160,000
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 54
Jumla 946,059,557 2(xiv) Malipo Yenye Nyaraka Pungufu Sh.Tz. 3,418,906,172.87 – Miradi Mingine
Na. Jina la Mradi Kiasi (Sh.Tz.) 1 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – Idara ya Uchumi
(UDSM DoE) 9,247,000
2 Mradi wa Maendeleo ya Mji Mkuu wa Dar es Salaam (DMDP)
293,224,791
3 Mradi wa Usimamizi wa Uvuvi na Ukuaji wa Pamoja Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi (SWIOFish)
8,932,000
4 Mradi wa Maliasili Stahimivu kwa Ajili ya Maendeleo ya Uongozi (REGROW)
60,025,000
5 Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali za Madini (SMMRP-II)
350,429,676.60
6 Mradi wa Maendeleo ya Nishati ya Gesi Asilia 61,578,500 7 Programu ya Maendeleo ya Elimu katika Shule za
Sekondari(SEDEP II) 947,730,345.51
8 Mradi wa Upanuzi wa Uzalishaji wa Mpunga (ERPP)
8,688,810.24
9 Matokeo Makubwa Sasa Katika Mradi wa Elimu ya Malipo kwa Matokeo (BRNED)
188,183,422.60
10 Wakala wa Usafiri wa Mwendokasi (DART) 9,915,047.74 11 Programu ya Kuboresha Miji Tanzania (TSCP) - PO
RALG 894,223,329.57
12 Programu ya Kuimarisha Afya ya Msingi kwa Matokeo (SPHCRP)
13,204,398.55
13 Mfuko Mkuu- Mradi wa Kifua Kikuu (TZA-T-MoFP) 119,022,060 14 Mfuko Mkuu- Mradi wa Ukimwi 81,593,450 15 Mradi wa Ubunifu Ulio wazi Katika Tasnia ya
Uchimbaji Madini Tanzania (TEITI CIDA) 81,593,450
16 Mradi wa Ubunifu Ulio wazi Katika Tasnia ya Uchimbaji Madini Tanzania (TEITI - Umoja Wa Ulaya)
3,748,896
17 Programu ya Mageuzi/Mabadiliko ya Usimamizi wa Fedha za Umma IV (PFMRP)
287,565,995
18 Mradi wa SPANEST kwa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA/SPANEST)
73,921,080
Jumla 3,492,827,252.81 2(xv) Kukosekana kwa Hati za Malipo Sh.Tz. 85,077,600 - Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) 1 Wilaya ya Bariadi 85,077,600
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 55
2(xvi) Kukosekana kwa Hati za Malipo Sh.Tz. 182,039,950 - Mfuko wa Afya
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi
(Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Ukerewe 56,000,000 8
Wilaya ya Kongwa 4,380,000
2 Wilaya ya Bunda 36,800,460 9
Wilaya ya Misungwi 4,190,000
3 Wilaya ya Kishapu 32,283,791 10 Wilaya ya Nkasi 3,631,000
4 Wilaya ya Arusha 15,795,000 11
Wilaya ya Iramba 2,590,914
5 Wilaya ya Mbogwe 9,825,000 12 Mji wa Kondoa 1,680,000
6 Wilaya ya Bariadi 7,443,785 13
Wilaya ya Rombo 1,640,477
7 Wilaya ya Siha 7,420,000 Jumla 165,568,036
2(xvii) Kukosekana kwa Hati za Malipo Sh.Tz. 411,013,346.88 - Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Musoma
368,646,288.78 4
Wilaya ya Mpwapwa 3,505,916
2 Wilaya ya Simanjiro 25,020,749.10 5
Mji wa Makambako 3,337,993
3 Wilaya ya Chemba 9,002,400 6
Wilaya ya Rufiji 1,500,000
Jumla 411,013,346.8
8 2(xviii) Kukosekana kwa Hati za Malipo Sh.Tz. 802,847,155 – Miradi Mingine
Na. Jina la Mradi Kiasi (Sh.Tz.) 1 Matokeo Makubwa Sasa Katika Mradi wa Elimu ya
Malipo kwa Matokeo (BRNED) 802,847,155
2(xix) Kutokuomba madai ya marejesho ya kodi ya ongezeko la thamani (VAT)
Sh.Tz. 309,357,157.86 - Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Monduli
96,225,895.88 6
Jiji la Arusha 16,501,260
2 Wilaya ya Biharamulo
90,387,580 7
Wilaya ya Iringa
6,311,209
3 Wilaya ya Namtumbo
58,750,289 8
Wilaya ya Maswa
2,203,205.03
4 Wilaya ya Arusha
20,504,583.95 9
Wilaya ya Nachingwea
949,500
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 56
5 Wilaya ya Kishapu
17,523,634 Jumla
309,357,157.86
2(xx) Kutokuomba madai ya marejesho ya kodi ya ongezeko la thamani (VAT)
Sh.Tz. 1,279,223,974.60 – Miradi Mingine Na. Jina la Mradi Kiasi (Sh.Tz.)
1 Mradi wa Vitabu vya Watoto Tanzania (CBPT) 830,290 2 Mradi wa Maendeleo ya Mji Mkuu wa Dar es
Salaam (DMDP) 27,900,889.80
3 Mfuko Mkuu- Mradi wa Ukimwi 395,781,031
4 Mfuko Mkuu-Mradi wa Kuimarisha Mifumo ya Afya/Malaria (TZA-H-MoF)
399,400,156
5 Taasisi ya Afya ya Msingi (PHCI) 12,200,400 6 Programu ya Kitaifa ya Kudhibiti Malaria (NMCP) 63,702,764.52
7 Programu ya Maendeleo Sekta ya Maji Awamu ya Pili (WSDP II)
379,408,443.28
Jumla 1,279,223,974.60 2(xxi) Matumizi Yaliyofanywa kwa Kutumia Vifungu Visivyohusika Sh.Tz. 5,117,000 - Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) 1 Wilaya ya Bagamoyo 5,117,000
2(xxii) Matumizi Yaliyofanywa kwa Kutumia Vifungu Visivyohusika Sh.Tz.
323,787,186 - Mfuko wa Afya Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Manispaa ya Ilemela 111,092,460 11 Wilaya ya
Same 9,142,240
2 Wilaya ya Momba 41,766,000 12 Wilaya ya
Mkuranga 6,679,000
3 Wilaya ya Sumbawanga 24,133,557 13 Wilaya ya
Kisarawe 6,106,000
4 Mji wa Bariadi 20,040,800 14 Wilaya ya
Kilolo 5,615,400
5 Wilaya ya Meru 19,612,320 15 Wilaya ya
Bumbuli 5,315,000
6 Wilaya ya Handeni 14,898,000 16 Wilaya ya
Igunga 3,840,000
7 Manispaa ya Morogoro 13,735,000 17 Wilaya ya
Mbinga 2,905,000
8 Wilaya ya Bariadi 11,689,105 18 Wilaya ya
Moshi 2,660,000
9 Wilaya ya Kasulu 11,494,750 19 Wilaya ya
Kibaha 1,941,200
10 Wilaya ya 9,850,000 20 Wilaya ya 1,271,354
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali AGR/DP/2016/2017 57
Madaba Monduli
Jumla 323,787,186 2(xxiii) Matumizi Yaliyofanywa kwa Kutumia Vifungu Visivyohusika Sh.Tz.
25,772,473 – Mfuko wa Barabara
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.)
1 Wilaya ya Sumbawanga 12,404,853 3
Wilaya ya Bariadi 3,384,500
2 Manispaa ya Sumbawanga 7,010,320 4
Wilaya ya Same 2,972,800
Jumla 25,772,47
3 2(xxiv) Matumizi Yaliyofanywa kwa Kutumia Vifungu Visivyohusika Sh.Tz.
121,043,297 – Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji
Na. Halmashauri Kiasi (Sh.Tz.) Na. Halmashauri Kiasi
(Sh.Tz.)
1 Manispaa ya Sumbawanga 19,229,500 10
Wilaya ya Kishapu 4,004,000
2 Wilaya ya Kibondo 17,490,000 11
Wilaya ya Bagamoyo 3,948,287
3 Wilaya ya Nsimbo 16,110,000 12
Wilaya ya Mbinga 3,078,180
4 Wilaya ya Kisarawe 15,062,000 13
Wilaya ya Meru 2,090,000
5 Manispaa ya Singida 11,521,000 14
Wilaya ya Ruangwa 2,010,000
6 Wilaya ya Ileje 10,470,300 15 Wilaya ya Rufiji 720,000
7 Wilaya ya Msalala 6,514,440 16
Wilaya ya Arusha 472,000
8 Manispaa ya Iringa 5,504,000 Jumla 123,053,297
9 Mji wa Korogwe 4,829,590 2(xxv) Matumizi Yaliyofanywa kwa Kutumia Vifungu Visivyohusika Sh.Tz.
613,676,103 – Miradi Mingine Na. Jina la Mradi Kiasi (Sh.Tz.)
1 Mradi wa SPANEST kwa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA/SPANEST)
21,043,051
2 Programu ya Mabadiliko ya Usimamizi wa Fedha za Umma IV (PFMRP)
592,633,052
Jumla 613,676,103
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
58
Kiam
bati
sho
Na
3: U
teke
leza
ji w
a M
apen
deke
zo K
atik
a Ri
poti
za
Kagu
zi z
a M
iaka
ya
Nyu
ma
N
a.
Jina
la M
radi
M
koa
Hal
mas
haur
i Ju
mla
ya
Map
ende
kezo
ya
M
iaka
ya
Nyu
ma
Map
ende
kezo
Ya
liyot
ekel
ezw
a
Map
ende
kezo
Ya
nayo
ende
lea
ku
teke
lezw
a
Map
ende
kezo
am
bayo
ha
yaja
teke
lezw
a
Map
ende
kezo
ya
liyof
utik
a ku
toka
na
na
Maz
ingi
ra
1 Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo y
a Se
kta
ya K
ilim
o Ar
usha
W
ilaya
ya
Arus
ha
2 0
0 1
1
2
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Kara
tu
25
1 1
4 19
3
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Mer
u 5
0 0
5 0
4
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Coas
t W
ilaya
ya
Baga
moy
o 2
0 0
1 1
5
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
M
ji w
a Ki
baha
3
0 1
2 0
6 Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo y
a
Wila
ya y
a Ru
fiji
6
0 3
2 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
59
Sekt
a ya
Kili
mo
7
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Gei
ta
Wila
ya y
a G
eita
12
1
2 9
0
8
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Irin
ga
Wila
ya y
a Ir
inga
4
1 2
0 1
9
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
M
anis
paa
ya
Irin
ga
7 6
1 0
0
10
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Kilo
lo
2 0
1 1
0
11
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Muf
indi
2
0 0
0 2
12
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Kata
vi
Wila
ya y
a M
lele
5
0 3
0 2
13
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Mpa
nda
2 0
0 2
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
60
Sekt
a ya
Kili
mo
14
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
M
anis
paa
ya
Mpa
nda
8 6
1 0
1
15
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Nsi
mbo
6
0 0
5 1
16
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Kilim
anja
ro
Wila
ya y
a H
ai
4 0
4 0
0
17
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Lind
i W
ilaya
ya
Kilw
a 5
1 2
0 2
18
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Ruan
gwa
4 0
3 0
1
19
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Man
yara
W
ilaya
ya
Baba
ti
13
0 3
7 3
20
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
M
ji w
a Ba
bati
6
0 1
0 5
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
61
Sekt
a ya
Kili
mo
21
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Han
ang'
12
1
7 3
1
22
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Kite
to
7 0
3 4
0
23
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Mbu
lu
6 0
1 5
0
24
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Sim
anji
ro
6 0
2 1
3
25
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Mbe
ya
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
2 0
1 0
1
26
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Chun
ya
2 2
0 0
0
27
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Kyel
a 0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
62
Sekt
a ya
Kili
mo
28
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Mba
rali
6 2
3 0
1
29
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Ji
ji la
Mbe
ya
1 0
0 1
0
30
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Mbe
ya
3 1
0 1
1
31
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Rung
we
7 5
0 1
1
32
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Song
we
Wila
ya y
a Ile
je
14
0 0
1 13
33
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Mbo
zi
4 0
0 2
2
34
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Mom
ba
8 2
2 3
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
63
Sekt
a ya
Kili
mo
35
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Song
we
0 0
0 0
0
36
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Mor
ogor
o W
ilaya
ya
Kilo
sa
3 1
0 0
2
37
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Mor
ogor
o 4
0 4
0 0
38
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Ula
nga
4 0
3 0
1
39
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Mw
anza
W
ilaya
ya
Mag
u 9
2 0
6 1
40
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Ji
ji la
Mw
anza
15
13
0
0 2
41
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Rukw
a W
ilaya
ya
Kala
mbo
13
5
2 6
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
64
Sekt
a ya
Kili
mo
42
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Nka
si
29
2 5
22
0
43
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
M
anis
paa
ya
Sum
baw
anga
14
2
2 5
5
44
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Sum
baw
anga
30
6
2 17
5
45
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Ruvu
ma
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
5
2 1
2 0
46
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Mbi
nga
6 2
2 2
0
47
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Nya
sa
16
2 3
11
0
48
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Song
ea
23
5 4
0 14
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
65
Sekt
a ya
Kili
mo
49
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
M
anis
paa
ya
Song
ea
4 1
0 3
0
50
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Tund
uru
4 0
3 0
1
51
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Sim
iyu
Wila
ya y
a Ba
riad
i 5
0 1
3 1
52
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Mas
wa
6 4
0 1
1
53
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Mea
tu
0 0
0 0
0
54
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
W
ilaya
ya
Itili
ma
6 0
2 2
2
55
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Tang
a M
ji w
a Ko
rogw
e 5
0 3
1 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
66
Sekt
a ya
Kili
mo
56
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Kili
mo
Ji
ji la
Tan
ga
6 0
3 3
0
57
Mfu
ko w
a Af
ya
ARU
SHA
Wila
ya y
a Ar
ush
45
0 4
19
22
58
Mfu
ko w
a Af
ya
Ji
ji la
Aru
sha
4 0
4 0
0
59
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mon
duli
44
1 2
19
22
60
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Long
ido
48
6 23
19
0
61
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mer
u 15
0
0 13
2
62
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kara
tu
52
26
0 17
9
63
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Ngo
rong
oro
39
0 0
27
12
64
Mfu
ko w
a Af
ya
MAN
YARA
W
ilaya
ya
Kite
to
13
0 4
7 2
65
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mbu
lu
18
0 0
8 10
66
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Baba
ti
15
2 0
12
1
67
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Han
ang
28
4 0
18
6
68
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Sim
anji
ro
24
5 0
19
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
67
69
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a M
bulu
0
0 0
0 0
70
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a Ba
bati
38
1
6 11
20
71
Mfu
ko w
a Af
ya
KILI
MAN
JARO
W
ilaya
ya
Mos
hi
9 0
0 9
0
72
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Rom
bo
7 0
0 7
0
73
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Hai
12
0
2 8
2
74
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Sam
e 5
0 0
3 2
75
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Mos
hi
10
3 0
2 5
76
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mw
anga
7
0 0
4 3
77
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Siha
10
2
0 4
4
78
Mfu
ko w
a Af
ya
TAN
GA
Wila
ya y
a H
ande
ni
33
0 5
25
3
79
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mki
nga
7 3
0 0
4
80
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kilin
di
16
2 0
8 6
81
Mfu
ko w
a Af
ya
Ji
ji la
Tan
ga
10
0 6
2 2
82
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Pang
ani
32
1 0
11
20
83
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Koro
gwe
41
0 3
13
25
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
68
84
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Muh
eza
14
2 3
5 4
85
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Lush
oto
17
3 1
5 8
86
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a Ko
rogw
e 33
2
0 27
4
87
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Bum
buli
19
3 1
10
5
88
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a H
ande
ni
4 1
0 0
3
89
Mfu
ko w
a Af
ya
DAR
Man
ispa
a ya
Te
mek
e 10
6
0 2
2
90
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Kino
ndon
i 12
10
0
2 0
91
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Ilala
7
3 3
0 1
92
Mfu
ko w
a Af
ya
LIN
DI
Wila
ya y
a 15
7
1 5
2
93
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Liw
ale
9 0
0 7
2
94
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Lind
i 3
0 0
3 0
95
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Ruan
gwa
4 2
0 1
1
96
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Lind
i 5
0 0
5 0
97
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Nac
hing
wea
4
0 0
4 0
98
Mfu
ko w
a Af
ya
MO
ROG
OR
O
Wila
ya y
a Ki
lom
bero
12
9
1 0
2
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
69
99
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kilo
sa
7 6
0 0
1
100
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mvo
mer
o 3
0 0
1 2
101
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mor
ogor
o 5
3 1
0 1
102
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Mor
ogor
o 25
1
13
6 5
103
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Ula
nga
8 4
0 0
4
104
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a If
akar
a 0
0 0
0 0
105
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mal
inyi
0
0 0
0 0
106
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Gai
ro
11
7 4
0 0
107
Mfu
ko w
a Af
ya
MTW
ARA
Man
ispa
a ya
M
twar
a 5
1 2
1 1
108
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a M
asas
i 22
1
1 19
1
109
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mas
asi
23
3 11
8
1
110
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mtw
ara
14
0 8
6 0
111
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a N
anya
mba
0
0 0
0 0
112
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Tand
ahim
ba
14
0 1
13
0
113
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Nan
yum
bu
6 2
0 3
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
70
114
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a N
ewal
a 0
0 0
0 0
115
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
New
ala
14
0 1
12
1
116
Mfu
ko w
a Af
ya
COAS
T W
ilaya
ya
Kisa
raw
e 9
0 0
4 5
117
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kiba
ha
2 0
0 0
2
118
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Maf
ia
8 0
0 8
0
119
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Baga
moy
o 11
0
2 8
1
120
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mku
rang
a 4
0 1
3 0
121
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a Ki
baha
5
0 0
5 0
122
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Rufi
ji
10
4 0
5 1
123
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Chal
inze
0
0 0
- 0
124
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kibi
ti
0 0
0 0
0
125
Mfu
ko w
a Af
ya
KIG
OM
A W
ilaya
ya
Buhi
gwe
5 0
0 4
1
126
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Kigo
ma
38
5 1
13
19
127
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kigo
ma
13
7 0
2 4
128
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kibo
ndo
21
2 2
12
5
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
71
129
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kasu
lu
12
0 2
10
0
130
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a Ka
sulu
3
2 0
1 0
131
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kako
nko
12
2 0
8 2
132
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Uvi
nza
8 3
1 3
1
133
Mfu
ko w
a Af
ya
SIN
GID
A W
ilaya
ya
Iram
ba
28
11
0 11
6
134
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mka
lam
a 19
1
4 12
2
135
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Man
yoni
26
10
8
7 1
136
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Sing
ida
10
2 2
2 4
137
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Sing
ida
25
7 6
3 9
138
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Ikun
gi
15
1 8
1 5
139
Mfu
ko w
a Af
ya
TABO
RA
Wila
ya y
a Ka
liua
13
10
2 0
1
140
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Ura
mbo
8
5 0
3 0
141
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Igun
ga
15
5 2
2 6
142
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Tabo
ra
3 0
1 2
0
143
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Siko
nge
5 3
0 1
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
72
144
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Nze
ga
4 0
4 0
0
145
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Tabo
ra
4 0
1 1
2
146
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Itig
i 0
0 0
0 0
147
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a N
zega
0
0 0
0 0
148
Mfu
ko w
a Af
ya
DODO
MA
Wila
ya y
a M
pwap
wa
9 0
2 7
0
149
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Bahi
5
1 2
2 0
150
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Cham
win
o DC
5
1 0
4 0
151
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Chem
ba
8 3
0 2
3
152
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Dodo
ma
16
5 2
5 4
153
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kond
oa
7 1
1 3
2
154
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kong
wa
7 2
1 1
3
155
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a Ko
ndoa
0
0 0
0 0
156
Mfu
ko w
a Af
ya
MAR
A M
anis
paa
ya
Mus
oma
15
3 2
10
0
157
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Rory
a 2
1 0
1 0
158
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Bund
a 3
0 0
3 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
73
159
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Tari
me
4 2
2 0
0
160
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a Ta
rim
e 11
6
1 4
0
161
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Sere
nget
i 7
4 0
0 3
162
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mus
oma
15
1 6
8 0
163
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Buti
ama
12
1 2
9 0
164
Mfu
ko w
a Af
ya
MW
ANZA
W
ilaya
ya
Seng
erem
a 48
39
3
6 0
165
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Uke
rew
e 31
4
11
15
1
166
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kwim
ba
35
21
6 7
1
167
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Ilem
ela
34
2 0
31
1
168
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Buch
osa
0 0
0 0
0
169
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mis
ungw
i 39
3
0 35
1
170
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mag
u 15
10
0
0 5
171
Mfu
ko w
a Af
ya
Ji
ji la
Mw
anza
47
4
3 38
2
172
Mfu
ko w
a Af
ya
SHIN
YAN
GA
Mji
wa
Kaha
ma
6 2
1 2
1
173
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Ush
etu
18
7 4
4 3
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
74
174
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kish
apu
18
7 4
4 3
175
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Msa
lala
18
8
4 4
2
176
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Shin
yang
a 12
3
3 5
1
177
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Shin
yang
a 5
1 2
1 1
178
Mfu
ko w
a Af
ya
GEI
TA
Wila
ya y
a G
eita
27
0
0 24
3
179
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a G
eita
7
4 3
0 0
180
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Chat
o 5
3 0
1 1
181
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Buko
mbe
9
0 1
8 0
182
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Nya
ng’h
wal
e 7
0 0
5 2
183
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mbo
gwe
10
0 0
10
0
184
Mfu
ko w
a Af
ya
SIM
IYU
W
ilaya
ya
Bari
adi
15
0 0
15
0
185
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a Ba
riad
i 15
9
2 2
2
186
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mas
wa
11
9 0
1 1
187
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mea
tu
9 6
0 0
3
188
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Buse
ga
11
4 1
0 6
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
75
189
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Itili
ma
9 4
0 2
3
190
Mfu
ko w
a Af
ya
KAG
ERA
Wila
ya y
a Bu
koba
13
4
5 0
4
191
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mul
eba
12
6 1
2 3
192
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kara
gwe
22
15
0 5
2
193
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mis
senv
i 13
6
0 4
3
194
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Nga
ra
13
8 1
1 3
195
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Biha
ram
ulo
11
6 2
1 2
196
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Buko
ba
15
11
1 2
1
197
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kyer
wa
9 4
0 0
5
198
Mfu
ko w
a Af
ya
IRIN
GA
Wila
ya y
a M
ufin
di
15
13
2 0
0
199
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a M
afin
ga
5 0
0 5
0
200
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kilo
lo
31
5 10
9
7
201
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Irin
ga
13
0 0
12
1
202
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Irin
ga
15
13
2 0
0
203
Mfu
ko w
a Af
ya
MBE
YA
Jiji
la M
beya
6
5 1
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
76
204
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mbe
ya
6 1
2 3
0
205
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kyel
a 29
14
10
4
1
206
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Rung
we
7 6
0 1
0
207
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mba
rali
14
2 8
4 0
208
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Chun
ya
6 5
0 1
0
209
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Buso
kelo
22
15
4
1 2
210
Mfu
ko w
a Af
ya
SON
GW
E W
ilaya
ya
Mbo
zi
10
7 0
3 0
211
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Ileje
6
1 1
4 0
212
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mom
ba
8 2
6 0
0
213
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Song
we
- 0
0 0
0
214
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a Tu
ndum
a 6
6 0
0 0
215
Mfu
ko w
a Af
ya
NJO
MBE
W
ilaya
ya
Njo
mbe
10
4
2 2
2
216
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a N
jom
be
9 3
2 3
1
217
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mak
ete
11
6 0
5 0
218
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Lude
wa
13
5 3
2 3
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
77
219
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a M
akam
bako
7
1 0
4 2
220
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Wan
g'in
g'om
be
14
10
2 2
0
221
Mfu
ko w
a Af
ya
KATA
VI
Wila
ya y
a M
pand
a 9
2 0
6 1
222
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Nsi
mbo
9
5 2
2 0
223
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mle
le
6 0
0 5
1
224
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mpi
mbw
e -
0 0
0 0
225
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Mpa
nda
5 2
1 2
0
226
Mfu
ko w
a Af
ya
RUKW
A W
ilaya
ya
Sum
baw
anga
34
13
3
14
4
227
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Sum
baw
anga
33
10
4
19
0
228
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Nka
si
31
7 1
22
1
229
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Kala
mbo
4
0 1
3 0
230
Mfu
ko w
a Af
ya
RUVU
MA
Wila
ya y
a Tu
ndur
u 14
3
6 5
0
231
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mbi
nga
13
10
3 0
0
232
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Nam
tum
bo
4 3
1 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
78
233
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Song
ea
32
3 5
3 21
234
Mfu
ko w
a Af
ya
M
anis
paa
ya
Song
ea
16
2 6
8 0
235
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Nya
sa
26
14
7 5
0
236
Mfu
ko w
a Af
ya
W
ilaya
ya
Mad
aba
- 0
0 0
0
237
Mfu
ko w
a Af
ya
M
ji w
a M
bing
a -
0 0
0 0
238
Mfu
ko w
a ba
raba
ra
Arus
ha
Wila
ya y
a Ar
usha
35
9
7 19
0
239
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Ji
ji la
Aru
sha
14
4 2
6 2
240
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kara
tu
41
0 0
15
26
241
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Long
ido
40
1 18
19
2
242
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mer
u 43
3
2 12
26
243
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mon
duli
8 0
1 7
0
244
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Ngo
rong
oro
37
0 0
27
10
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
79
245
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Pwan
i W
ilaya
ya
Baga
moy
o 4
0 0
4 0
246
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kiba
ha
5 0
1 3
1
247
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a Ki
baha
7
1 1
3 2
248
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kisa
raw
e 3
1 0
1 1
249
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Maf
ia
12
0 0
11
1
250
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mku
rang
a 16
1
12
1 2
251
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Rufi
ji
11
1 2
6 2
252
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Chal
ize
0 0
0 0
0
253
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kibi
ti
0 0
0 0
0
254
Mfu
ko w
a Da
r es
Sa
laam
M
anis
paa
ya
Ilala
12
6
0 5
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
80
Bara
bara
255
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Kino
ndon
i 16
6
2 8
0
256
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Tem
eke
9 1
2 6
0
257
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Kiga
mbo
ni
0 0
0 0
0
258
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Dodo
ma
Wila
ya y
a Ba
hi
20
17
1 0
2
259
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Cham
win
o 4
1 1
0 2
260
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Chem
ba
7 3
0 1
3
261
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Dodo
ma
12
1 1
5 5
262
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kond
oa
10
2 1
4 3
263
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a Ko
ndoa
0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
81
264
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kong
wa
9 0
0 8
1
265
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mpw
apw
a 22
0
0 22
0
266
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Gei
ta
Wila
ya y
a Bu
kom
be
10
5 3
0 2
267
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Chat
o 15
6
0 4
5
268
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Gei
ta
12
0 0
7 5
269
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a G
eita
15
1
3 10
1
270
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mbo
gwe
17
0 0
17
0
271
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Nya
ng'h
wal
e 1
1 0
0 0
272
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Irin
ga
Wila
ya y
a Ir
inga
30
16
0
1 13
273
Mfu
ko w
a
Man
ispa
a ya
Ir
inga
7
3 2
1 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
82
Bara
bara
274
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kilo
lo
19
0 0
19
0
275
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Muf
indi
5
5 0
0 0
276
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a M
afin
ga
2 2
0 0
0
277
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Kage
ra
Wila
ya y
a Bi
hara
mul
o 7
1 0
2 4
278
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Buko
ba
16
4 2
5 5
279
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Buko
ba
21
8 3
1 9
280
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kara
gwe
9 2
0 5
2
281
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kyer
wa
10
1 1
0 8
282
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mis
enyi
6
1 0
4 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
83
283
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mul
eba
11
5 1
1 4
284
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Nga
ra
12
1 2
3 6
285
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Kata
vi
Wila
ya y
a M
lele
9
0 3
6 0
286
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mpa
nda
5 3
0 2
0
287
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Mpa
nda
15
15
0 0
0
288
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Nsi
mbo
9
7 0
2 0
289
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mpi
mbw
e 0
0 0
0 0
290
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Kigo
ma
Wila
ya y
a Bu
higw
e 5
0 0
4 1
291
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kako
nko
16
1 3
7 5
292
Mfu
ko w
a
Wila
ya y
a Ka
sulu
13
8
0 1
4
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
84
Bara
bara
293
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a Ka
sulu
3
2 0
0 1
294
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kibo
ndo
3 2
0 1
0
295
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kigo
ma
10
2 1
5 2
296
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Uvi
nza
10
0 5
3 2
297
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Kigo
ma
Uji
ji
21
3 7
9 2
298
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Kilim
anja
ro
Wila
ya y
a H
ai
6 3
2 1
0
299
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mos
hi
14
2 1
5 6
300
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
pa y
a M
oshi
8
1 0
5 2
301
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mw
anga
9
0 0
4 5
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
85
302
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Rom
bo
8 2
0 4
2
303
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Sam
e 13
11
0
0 2
304
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Siha
11
3
3 2
3
305
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Lind
i W
ilaya
ya
Kilw
a 3
1 1
0 1
306
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Lind
i 5
0 1
4 0
307
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Lind
i 11
4
2 3
2
308
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Liw
ale
6 1
4 1
0
309
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Nac
hing
wea
8
5 0
0 3
310
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Ruan
gwa
14
9 1
3 1
311
Mfu
ko w
a M
anya
ra
Wila
ya y
a Ba
bati
10
2
0 6
2
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
86
Bara
bara
312
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a Ba
bati
14
6
0 1
7
313
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Han
ang'
7
1 1
3 2
314
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kite
to
13
1 3
7 2
315
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mbu
lu
11
0 0
3 8
316
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a M
bulu
0
0 0
0 0
317
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Sim
anji
ro
8 0
0 2
6
318
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mar
a M
anis
paa
ya
Mus
oma
14
9 1
4 0
319
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mus
oma
5 0
0 3
2
320
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Rory
a 5
0 1
1 3
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
87
321
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Bund
a 13
13
0
0 0
322
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Sere
nget
i 12
10
0
2 0
323
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Buti
ama
9 3
1 3
2
324
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a Ta
rim
e 8
2 4
2 0
325
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a Bu
nda
0 0
0 0
0
326
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mbe
ya
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
4 1
3 0
0
327
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Chun
ya
5 5
0 0
0
328
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kyel
a 3
0 3
0 0
329
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mba
rali
7 0
4 3
0
330
Mfu
ko w
a
Man
ispa
a ya
M
beya
10
9
0 1
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
88
Bara
bara
331
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mbe
ya
11
2 6
2 1
332
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Rung
we
8 1
0 4
3
333
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Song
we
Wila
ya y
a Ile
je
1 0
1 0
0
334
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mbo
zi
5 2
0 3
0
335
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mom
ba
5 4
0 1
0
336
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Tund
uma
5 4
0 0
1
337
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Song
we
0 0
0 0
0
338
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mor
ogor
o W
ilaya
ya
Gai
ro
10
7 2
1 0
339
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kilo
mbe
ro
9 8
1 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
89
340
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kilo
sa
29
12
0 0
17
341
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mor
ogor
o 7
4 1
0 2
342
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Mor
ogor
o 14
8
0 6
0
343
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mvo
mer
o 5
3 1
0 1
344
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a If
akar
a 0
0 0
0 0
345
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mal
inyi
0
0 0
0 0
346
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mtw
ara
Wila
ya y
a M
asas
i 25
0
16
6 3
347
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a M
asas
i 15
0
0 15
0
348
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mtw
ara
19
7 1
7 4
349
Mfu
ko w
a
Man
ispa
a ya
M
twar
a 22
0
3 19
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
90
Bara
bara
350
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Nan
yum
bu
15
1 1
12
1
351
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Tand
ahim
ba
18
0 6
5 7
352
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Nan
yam
ba
0 0
0 0
0
353
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mw
anza
M
anis
paa
ya
Ilem
ela
22
0 0
20
2
354
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kwim
ba
11
1 4
3 3
355
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mag
u 10
3
3 4
0
356
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Ji
ji la
Mw
anza
31
1
1 29
0
357
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Seng
erem
a 26
3
5 18
0
358
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Buch
osa
0 0
0 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
91
359
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Njo
mbe
W
ilaya
ya
Lude
wa
9 0
5 1
3
360
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a M
akam
bako
2
1 0
0 1
361
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mak
ete
9 7
0 2
0
362
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Njo
mbe
13
1
3 0
9
363
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a N
jom
be
10
1 8
1 0
364
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Wan
ging
'om
be
8 5
1 2
0
365
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Rukw
a W
ilaya
ya
Kala
mbo
17
8
0 4
5
366
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Nka
si
28
15
3 3
7
367
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Sum
baw
anga
37
12
4
21
0
368
Mfu
ko w
a
Wila
ya y
a Su
mba
wan
ga
6 1
0 5
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
92
Bara
bara
369
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Ruvu
ma
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
12
3
8 1
0
370
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mbi
nga
12
0 9
3 0
371
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a M
bing
a 0
0 0
0 0
372
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Nya
sa
15
9 5
1 0
373
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Song
ea
23
6 0
3 14
374
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Song
ea
10
5 4
1 0
375
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Tund
uru
18
2 11
5
0
376
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mad
aba
0 0
0 0
0
377
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Shin
yang
a M
ji w
a Ka
ham
a 11
4
0 5
2
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
93
378
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kish
apu
20
10
0 8
2
379
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Msa
lala
15
4
0 9
2
380
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Shin
yang
a 14
6
1 3
4
381
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Shin
yang
a 7
1 1
4 1
382
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Ush
etu
6 1
1 1
3
383
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Sim
iyu
Wila
ya y
a Ba
riad
i 10
10
0
0 0
384
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a Ba
riad
i 15
6
4 4
1
385
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mas
wa
9 7
0 1
1
386
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Itili
ma
6 4
2 0
0
387
Mfu
ko w
a
Wila
ya y
a Bu
sega
8
3 2
0 3
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
94
Bara
bara
388
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mea
tu
19
6 5
3 5
389
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Sing
ida
Wila
ya y
a Ir
amba
15
7
3 1
4
390
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Ikun
gi
19
4 11
0
4
391
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Man
yoni
15
4
1 7
3
392
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mka
lam
a 21
5
3 3
10
393
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Sing
ida
15
2 6
5 2
394
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Sing
ida
15
1 4
5 5
395
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Itig
i 0
0 0
0 0
396
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Tabo
ra
Wila
ya y
a Ig
unga
11
8
0 2
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
95
397
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kaliu
a 14
7
1 2
4
398
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Nze
ga
1 0
1 0
0
399
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a N
zega
7
6 0
1 0
400
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Siko
nge
8 4
0 3
1
401
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Tabo
ra
5 2
0 0
3
402
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
anis
paa
ya
Tabo
ra
7 0
2 5
0
403
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Ura
mbo
12
10
0
1 1
404
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Tang
a W
ilaya
ya
Bum
buli
12
0 1
3 8
405
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Han
deni
12
2
0 3
7
406
Mfu
ko w
a
Mji
wa
Han
deni
11
5
0 4
2
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
96
Bara
bara
407
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Kilin
di
13
0 8
5 0
408
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Koro
gwe
28
9 0
3 16
409
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
M
ji w
a Ko
rogw
e 14
0
3 9
2
410
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Lush
oto
10
1 0
9 0
411
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Mki
nga
17
8 0
0 9
412
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Muh
eza
27
1 7
11
8
413
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
W
ilaya
ya
Pang
ani
17
0 2
12
3
414
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Ji
ji la
Tan
ga
10
4 1
2 3
415
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
IRIN
GA
Wila
ya y
a M
ufin
di
8 5
3 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
97
Jam
ii
416
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ki
lolo
3
0 3
0 0
417
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Man
ispa
a ya
Ir
inga
7
5 2
0 0
418
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ir
inga
11
9
2 0
0
419
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii KA
GER
A W
ilaya
ya
Buko
ba
7 0
0 3
4
420
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
uleb
a 8
0 0
2 6
421
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ka
ragw
e 9
3 3
3 0
422
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Mis
seny
i 12
0
0 5
7
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
98
Jam
ii
423
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a N
gara
13
1
0 6
6
424
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Bi
hara
mul
o 9
3 0
5 1
425
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Man
ispa
a ya
Bu
koba
7
0 1
2 4
426
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ky
erw
a 13
2
0 6
5
427
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii M
ARA
Man
ispa
a ya
M
usom
a 6
1 4
1 0
428
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ro
rya
5 2
3 0
0
429
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Bund
a 10
2
7 1
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
99
Jam
ii
430
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Se
reng
eti
4 2
1 1
0
431
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
usom
a 9
5 1
1 2
432
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Bu
tiam
a 10
6
0 4
0
433
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii M
BEYA
Ji
ji la
Mbe
ya
1 0
1 0
0
434
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
beya
3
3 0
0 0
435
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ky
ela
8 4
3 0
1
436
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Rung
we
4 3
0 1
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
100
Jam
ii
437
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
bara
li 3
2 1
0 0
438
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ch
unya
5
4 1
0 0
439
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii SO
NG
WE
Wila
ya y
a M
bozi
1
0 1
0 0
440
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ile
je
7 5
1 1
0
441
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
omba
2
1 0
1 0
442
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii M
WAN
ZA
Wila
ya y
a Se
nger
ema
12
8 4
0 0
443
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Uke
rew
e 9
7 2
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
101
Jam
ii
444
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Kw
imba
8
5 0
3 0
445
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Man
ispa
a ya
Ile
mel
a 7
4 2
1 0
446
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
isun
gwi
9 3
4 2
0
447
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
agu
6 5
1 0
0
448
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Jiji
la M
wan
za
10
6 2
2 0
449
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii RU
KWA
Wila
ya y
a Su
mba
wan
ga
9 4
1 4
0
450
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
M
anis
paa
ya
Sum
baw
anga
13
5
5 3
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
102
Jam
ii
451
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a N
kasi
11
8
0 1
2
452
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ka
lam
bo
4 1
0 3
0
453
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii RU
VUM
A W
ilaya
ya
Tund
uru
2 1
0 1
0
454
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
bing
a 3
1 1
1 0
455
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
4
3 1
0 0
456
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a So
ngea
1
1 0
0 0
457
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
M
anis
paa
ya
Song
ea
1 1
0 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
103
Jam
ii
458
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a N
yasa
3
1 2
0 0
459
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii SH
INYA
NG
A M
ji w
a Ka
ham
a 3
2 0
1 0
460
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a U
shet
u 2
2 0
0 0
461
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ki
shap
u 3
3 0
0 0
462
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
sala
la
2 2
0 0
0
463
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Sh
inya
nga
5 3
0 2
0
464
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
M
anis
paa
ya
Shin
yang
a 2
2 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
104
Jam
ii
465
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii G
EITA
W
ilaya
ya
Gei
ta
4 0
0 4
0
466
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Mji
wa
Gei
ta
7 4
1 1
1
467
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ch
ato
7 2
1 3
1
468
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Bu
kom
be
1 0
0 1
0
469
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a N
yang
’hw
ale
4 3
0 1
0
470
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
bogw
e 2
0 0
1 1
471
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
SIM
IYU
W
ilaya
ya
Bari
adi
1 1
0 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
105
Jam
ii
472
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
asw
a 4
1 2
0 1
473
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
eatu
1
1 0
0 0
474
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a It
ilim
a 3
2 1
0 0
475
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii N
JOM
BE
Wila
ya y
a N
jom
be
8 7
1 0
0
476
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Mji
wa
Njo
mbe
6
3 0
1 2
477
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
aket
e 15
12
1
2 0
478
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Lude
wa
13
11
1 0
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
106
Jam
ii
479
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Mji
wa
Mak
amba
ko
6 6
0 0
0
480
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a W
ang'
ing'
ombe
7
7 0
0 0
481
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii KA
TAVI
W
ilaya
ya
Mpa
nda
11
9 2
0 0
482
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a N
sim
bo
3 3
0 0
0
483
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
lele
3
0 0
3 0
484
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Man
ispa
a ya
M
pand
a 4
3 1
0 0
485
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Arus
ha
Jiji
la A
rush
a 16
2
3 4
7
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
107
Sekt
a y
a M
aji
486
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Arus
ha
16
0 4
10
2
487
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kara
tu
26
8 4
8 6
488
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Long
ido
49
8 2
29
10
489
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mer
u 8
3 0
2 3
490
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mon
duli
13
1 1
8 3
491
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Ngo
rong
oro
27
2 7
11
7
492
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Coas
t W
ilaya
ya
Baga
moy
o 13
13
0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
108
Sekt
a y
a M
aji
493
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kiba
ha
8 0
4 3
1
494
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a Ki
baha
5
0 0
4 1
495
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kisa
raw
e 10
2
2 6
0
496
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Maf
ia
11
0 0
8 3
497
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mku
rang
a 11
0
3 7
1
498
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Rufi
ji
11
0 7
4 0
499
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Chal
inze
0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
109
Sekt
a y
a M
aji
500
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kibi
ti
0 0
0 0
0
501
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Dar
es
Sala
am
Man
ispa
a ya
Ila
la
13
2 6
4 1
502
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Kino
ndon
i 3
2 1
0 0
503
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Tem
eke
9 0
2 7
0
504
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Kiga
mbo
ni
0 0
0 0
0
505
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Dodo
ma
Wila
ya y
a Ba
hi
9 7
0 0
2
506
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Cham
win
o 9
5 0
0 4
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
110
Sekt
a y
a M
aji
507
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Chem
ba
8 3
0 1
4
508
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Dodo
ma
14
6 0
4 4
509
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kond
oa
16
8 1
2 5
510
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kong
wa
1 0
0 1
0
511
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mpw
apw
a 6
0 0
2 4
512
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a Ko
ndoa
0
0 0
0 0
513
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Gei
ta
Wila
ya y
a Bu
kom
be
12
0 1
11
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
111
Sekt
a y
a M
aji
514
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Chat
o 11
3
2 4
2
515
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Gei
ta
23
10
6 4
3
516
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a G
eita
10
2
3 0
5
517
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mbo
gwe
12
0 0
12
0
518
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Nya
ng'h
wal
e 11
1
4 5
1
519
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Irin
ga
Wila
ya y
a Ir
inga
12
8
2 0
2
520
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
M
anis
paa
ya
Irin
ga
15
12
0 2
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
112
Sekt
a y
a M
aji
521
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kilo
lo
17
0 3
11
3
522
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Muf
indi
7
4 0
2 1
523
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a M
afin
ga
0 0
0 0
0
524
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Kage
ra
Wila
ya y
a Bi
hara
mul
o 21
8
5 0
8
525
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Buko
ba
9 2
0 1
6
526
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Buko
ba
9 0
3 1
5
527
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Kara
gwe
7 3
1 0
3
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
113
Sekt
a y
a M
aji
528
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kyer
wa
9 2
3 1
3
529
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mis
seny
i 19
2
1 8
8
530
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mul
eba
18
4 4
4 6
531
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Nga
ra
14
6 2
2 4
532
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Kata
vi
Wila
ya y
a M
pand
a 8
5 1
2 0
533
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Mpa
nda
6 5
1 0
0
534
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Mle
le
6 1
5 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
114
Sekt
a y
a M
aji
535
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Nsi
mbo
10
5
1 4
0
536
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mpi
mbw
e 0
0 0
0 0
537
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Kigo
ma
Wila
ya y
a Bu
higw
e 7
0 0
2 5
538
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kako
nko
5 1
1 1
2
539
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kasu
lu
15
1 1
6 7
540
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kibo
ndo
10
0 4
6 0
541
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Kigo
ma
6 2
2 0
2
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
115
Sekt
a y
a M
aji
542
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Kigo
ma
14
6 0
4 4
543
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Uvi
nza
17
4 4
2 7
544
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji K
asul
u 0
0 0
0 0
545
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Kilim
anja
ro
Wila
ya y
a H
ai
12
3 0
4 5
546
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mos
hi
14
2 1
2 9
547
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Mos
hi
7 4
1 0
2
548
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Mw
anga
17
2
0 9
6
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
116
Sekt
a y
a M
aji
549
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Rom
bo
14
0 0
14
0
550
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Sam
e 9
4 0
1 4
551
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Siha
8
5 2
0 1
552
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Lind
i W
ilaya
ya
Kilw
a 9
3 1
2 3
553
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Lind
i 5
0 4
1 0
554
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Lind
i 16
0
0 7
9
555
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Liw
ale
6 0
2 2
2
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
117
Sekt
a y
a M
aji
556
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Nac
hing
wea
18
1
9 4
4
557
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Ruan
gwa
8 4
1 0
3
558
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Man
yara
W
ilaya
ya
Baba
ti
10
1 3
4 2
559
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a Ba
bati
14
6
0 1
7
560
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Han
ang’
21
3
5 12
1
561
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kite
to
6 1
1 1
3
562
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Mbu
lu
11
2 4
3 2
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
118
Sekt
a y
a M
aji
563
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Sim
anji
ro
10
1 5
1 3
564
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a M
bulu
0
0 0
0 0
565
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Mar
a W
ilaya
ya
Bund
a 12
0
0 12
0
566
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Buti
ama
10
0 0
10
0
567
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mus
oma
7 2
1 2
2
568
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Mus
oma
1 1
0 0
0
569
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Rory
a 9
2 0
7 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
119
Sekt
a y
a M
aji
570
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Sere
nget
i 6
2 2
1 1
571
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Tari
me
7 3
0 1
3
572
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a Ta
rim
e 4
1 3
0 0
573
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a Bu
nda
0 0
0 0
0
574
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Mbe
ya
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
7 1
5 1
0
575
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Chun
ya
6 4
2 0
0
576
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Kyel
a 19
7
4 0
8
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
120
Sekt
a y
a M
aji
577
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mba
rali
13
1 8
4 0
578
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Ji
ji la
Mbe
ya
13
4 4
5 0
579
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mbe
ya
10
2 5
2 1
580
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Rung
we
15
9 0
2 4
581
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mor
ogor
o 4
1 1
0 2
582
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kilo
sa
30
0 4
23
3
583
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Ula
nga
9 5
0 0
4
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
121
Sekt
a y
a M
aji
584
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kilo
mbe
ro
12
8 0
2 2
585
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mvo
mer
o 15
0
9 5
1
586
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Gai
ro
19
10
5 4
0
587
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mal
inyi
0
0 0
0 0
588
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a If
akar
a 0
0 0
0 0
589
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Mtw
ara
Wila
ya y
a M
asas
i 21
0
9 12
0
590
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
M
ji w
a M
asas
i 8
0 0
8 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
122
Sekt
a y
a M
aji
591
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mtw
ara
21
0 1
16
4
592
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Mtw
ara
10
0 0
10
0
593
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Nan
yum
bu
13
2 4
6 1
594
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
New
ala
16
6 2
6 2
595
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Tand
ahim
ba
14
1 5
7 1
596
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a N
anya
mba
0
0 0
0 0
597
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
M
ji w
a N
ewal
a 0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
123
Sekt
a y
a M
aji
598
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Mw
anza
W
ilaya
ya
Mag
u 8
2 3
2 1
599
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kwim
ba
11
2 2
3 4
600
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Ji
ji la
Mw
anza
8
1 2
5 0
601
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mis
ungw
i 17
3
3 4
7
602
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Seng
erem
a 37
13
7
11
6
603
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Uke
rew
e 18
1
4 11
2
604
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Buch
osa
0 0
0 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
124
Sekt
a y
a M
aji
605
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Njo
mbe
W
ilaya
ya
Lude
wa
15
5 4
1 5
606
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a M
akam
bako
10
0
2 4
4
607
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mak
ete
12
7 2
3 0
608
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Njo
mbe
14
0
6 5
3
609
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a N
jom
be
7 4
1 0
2
610
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Wila
ya y
a W
ang’
ing’
omb
e 8
5 2
1 0
611
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Rukw
a W
ilaya
ya
Kala
mbo
20
10
1
3 6
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
125
Sekt
a y
a M
aji
612
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Nka
si
22
1 9
12
0
613
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
S’w
anga
17
4
3 9
1
614
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
S’w
anga
20
6
5 9
0
615
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Ruvu
ma
Wila
ya y
a M
bing
a 16
1
6 9
0
616
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a M
bing
a 0
0 0
0 0
617
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Nam
tum
bo
13
4 8
1 0
618
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Nya
sa
15
9 6
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
126
Sekt
a y
a M
aji
619
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Song
ea
34
1 3
13
17
620
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Song
ea
4 3
1 0
0
621
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Tund
uru
15
1 9
5 0
622
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mad
aba
0 0
0 0
0
623
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Shin
yang
a M
ji w
a Ka
ham
a 6
0 1
2 3
624
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kish
apu
9 2
2 2
3
625
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Wila
ya y
a W
ilaya
ya
Msa
lala
6
2 0
1 3
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
127
Sekt
a y
a M
aji
626
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Shin
yang
a 17
6
3 5
3
627
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Shin
yang
a 15
5
4 2
4
628
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Ush
etu
6 2
1 3
0
629
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Sim
iyu
Wila
ya y
a Ba
riad
i 14
6
6 1
1
630
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a Ba
riad
i 16
9
1 2
4
631
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Buse
ga
14
8 1
0 5
632
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Itili
ma
21
9 9
1 2
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
128
Sekt
a y
a M
aji
633
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mas
wa
14
7 3
0 4
634
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mea
tu
10
1 2
2 5
635
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Sing
ida
Wila
ya y
a Ik
ungi
11
3
5 0
3
636
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Iram
ba
41
4 19
6
12
637
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Man
yoni
14
3
3 5
3
638
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mka
lam
a 15
0
1 7
7
639
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Sing
ida
11
3 3
1 4
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
129
Sekt
a y
a M
aji
640
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
ya
Sing
ida
18
4 6
7 1
641
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Itig
i 0
0 0
0 0
642
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Song
we
Wila
ya y
a Ile
je
21
5 13
3
0
643
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mbo
zi
9 4
0 3
2
644
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mom
ba
9 1
0 6
2
645
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a Tu
ndum
a 0
0 0
0 0
646
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Song
we
0 0
0 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
130
Sekt
a y
a M
aji
647
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Tabo
ra
Wila
ya y
a Ig
unga
19
17
0
1 1
648
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kaliu
a 10
8
1 0
1
649
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Nze
ga
8 0
4 4
0
650
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Siko
nge
5 2
1 1
1
651
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Tabo
ra
7 6
0 0
1
652
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
anis
paa
yaTa
bora
11
4
2 5
0
653
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Ura
mbo
17
15
1
0 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
131
Sekt
a y
a M
aji
654
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Tang
a W
ilaya
ya
Bum
buli
14
1 6
7 0
655
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Han
deni
15
0
0 15
0
656
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a H
ande
ni
8 2
0 3
3
657
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Kilin
di
24
0 7
15
2
658
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Koro
gwe
30
11
8 4
7
659
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
M
ji w
a Ko
rogw
e 17
1
7 8
1
660
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
W
ilaya
ya
Lush
oto
9 0
5 1
3
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
132
Sekt
a y
a M
aji
661
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Mki
nga
8 0
0 0
8
662
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Muh
eza
2 0
1 0
1
663
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
W
ilaya
ya
Pang
ani
8 0
0 6
2
664
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sekt
a y
a M
aji
Ji
ji la
Tan
ga
10
0 1
4 5
Na.
Ji
na la
Mra
di
Mfa
dhili
Jum
la y
a M
apen
deke
zo y
a M
iaka
ya
Nyu
ma
Map
ende
kezo
Ya
liyot
ekel
ezw
a
Map
ende
kezo
Ya
nayo
ende
lea
ku
teke
lezw
a
Map
ende
kezo
am
bayo
ha
yaja
teke
lezw
a
Map
ende
kezo
ya
liyof
utik
a ku
toka
na
na
Maz
ingi
ra
665
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la
Kusa
idia
W
atot
o (U
NIC
EF)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la K
usai
dia
Wat
oto
0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
133
(UN
ICEF
)
666
Shir
ika
la
Hud
uma
za
Mis
aada
la
Kika
tolik
i (CR
S)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
)
1 1
0 0
0
667
PACT
Tan
zani
a Sh
irik
a la
Ki
mat
aifa
la
Kus
aidi
a W
atot
o (U
NIC
EF)
0
0 0
0 0
668
CUAM
M
Tanz
ania
Sh
irik
a la
Ki
mat
aifa
la
Kus
aidi
a W
atot
o (U
NIC
EF)
2
2 0
0 0
669
Mra
di w
a Vi
tabu
vya
W
atot
o Ta
nzan
ia
(CBP
T)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
)
0 0
0 0
0
670
Bayl
or T
anza
nia
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
134
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
)
671
Wiz
ara
ya A
fya
Mae
ndel
eo y
a Ja
mii,
Jin
sia,
W
azee
Na
Wat
oto
(MoH
CDG
EC)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
)
0 0
0 0
0
672
Jukw
aa la
M
aend
eleo
(P
DF)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
)
0 0
0 0
0
673
Ofi
si y
a M
wan
ashe
ria
Mku
u (A
GC)
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
674
Wiz
ara
ya
Fedh
a na
M
ipan
go-
Idar
a ya
Kuo
ndoa
U
mas
kini
.
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
1
0 0
1 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
135
675
Ofi
si y
a W
azir
i M
kuu
(Kui
mar
isha
Ta
arif
a ya
Hal
i ya
Hew
a na
M
fum
o w
a Ku
toa
Taha
dhar
i ya
Map
ema)
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
4
4 0
0 0
676
Shir
ika
la
Uza
lisha
ji M
ali
la J
eshi
la
Kuje
nga
Taif
a (S
UM
A JK
T)
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
677
Mra
di w
a SP
ANES
T kw
a Sh
irik
a la
H
ifad
hi z
a Ta
ifa
(TAN
APA/
SPAN
EST)
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
6
1 0
5 0
678
Mfu
ko w
a uh
ifad
hi w
a W
anya
map
ori
Tanz
ania
(T
WPF
)
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
136
679
Chuo
Kik
uu c
ha
Dar
es S
alaa
m –
Id
ara
ya
Uch
umi (
UDS
M
DoE)
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
14
13
1
0 0
680
Taas
isi y
a U
ongo
zi
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
681
Bodi
ya
Maj
i ya
Bond
e la
W
ami/
Ruvu
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
682
Taas
isi y
a U
tafi
ti w
a Ki
uchu
mi n
a Ki
jam
ii (E
SRF)
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
2
2 0
0 0
683
Tum
e ya
M
ipan
go
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
1
1 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
137
(UN
DP)
684
Bung
e la
Ta
nzan
ia
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
685
Kati
bu T
awal
a w
a M
koa
- Ta
bora
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
4
4 0
0 0
686
Bodi
ya
Maj
i ya
Bond
e la
Ru
vum
a na
Pw
ani y
a Ku
sini
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
687
Kitu
o ch
a El
imu
Kiba
ha
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
138
688
Wiz
ara
ya
Nis
hati
na
Mad
ini,
Mra
di
wa
Kuje
nga
Uw
ezo
kati
ka
Sekt
a ya
Nis
hati
na
Tas
inia
ya
Uch
imba
ji
Mad
ini (
MEM
-M
radi
wa
CADE
SE)
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
689
Bodi
ya
Maj
i ya
Bond
e la
Pa
ngan
i
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
690
Wak
ala
wa
Hud
uma
za
Mis
itu
Tanz
ania
(T
FSA)
Shir
ika
la
mae
ndel
eo
la u
moj
a w
a m
atai
fa
(UN
DP)
0
0 0
0 0
691
Prog
ram
u ya
Ku
said
ia S
ekta
ya
Usa
firi
shaj
i (T
SSP)
Benk
i ya
Duni
a
7 0
1 6
0
692
Mra
di w
a U
wez
esha
ji
Bias
hara
na
Usa
firi
shaj
i Ku
sini
mw
a Af
rika
(SA
TTFP
)
Benk
i ya
Duni
a
1
1 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
139
693
Mra
di w
a Ku
said
ia S
ecta
ya
Bar
abar
a Aw
amu
ya P
ili
(RSS
P II)
Benk
i ya
mae
ndel
eo
Afri
ka
3
0 1
2 0
694
Mfu
mo
wa
Mab
asi y
a M
wen
doka
si
Dar
es S
alaa
m
(BRT
) Aw
amu
ya P
ili
Benk
i ya
mae
ndel
eo
Afri
ka &
AG
TF
0
0 0
0 0
695
Mra
di w
a U
jenz
i wa
Bara
bara
ya
Kim
atai
fa
Arus
ha–
Tave
ta/H
olili
-Vo
i
Benk
i ya
mae
ndel
eo
Afri
ka
5
2 1
0 2
696
Mra
di w
a Ku
said
ia S
ekta
ya
Bar
abar
a Aw
amu
ya
Kwan
za (
RSSP
I)
Benk
i ya
mae
ndel
eo
Afri
ka &
JI
CA)
5
0 5
0 0
697
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra y
a Zi
wa
Vict
oria
(L
VEM
P II)
Benk
i ya
Duni
a
2
1 0
1 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
140
698
Mra
di w
a U
sim
amiz
i na
Uhi
fadh
i Vy
anzo
vya
M
aji K
ihan
si
(KCC
MP)
Benk
i ya
Duni
a
16
11
5
699
Mra
di w
a U
safi
rish
aji
Kand
a ya
Kat
i Aw
amu
ya P
ili
(CTC
P II)
Benk
i ya
Duni
a
4
4 0
0 0
700
Regi
onal
Co
mm
unic
atio
ns
Infr
astr
uctu
re
Proj
ect
(RCI
P)
Mra
di w
a M
iund
ombi
nu
ya M
awas
ilian
o Ki
mko
a (R
CIP)
Benk
i ya
Duni
a
7
5 2
0 0
701
Taas
isi y
a Ku
jeng
a U
wez
o Af
rika
(AC
BF)
Mra
di -
AC
BF/N
M-A
IST
Benk
i ya
Duni
a
0
0 0
0 0
702
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Mji
Mku
u w
a Da
r es
Sal
aam
(D
MDP
)
Benk
i ya
Duni
a
2
0 0
2
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
141
703
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Uvu
vi n
a U
kuaj
i w
a Pa
moj
a Ku
sini
M
agha
ribi
mw
a Ba
hari
ya
Hin
di
(SW
IOFi
sh)
Benk
i ya
Duni
a
2
1 1
0 0
704
Mra
di w
a M
alia
sili
Stah
imiv
u kw
a Aj
ili y
a M
aend
eleo
ya
Uon
gozi
(R
EGRO
W)
Benk
i ya
Duni
a
0
0 0
0 0
705
Mra
di w
a U
wek
ezaj
i ka
tika
Kuk
uza
Kilim
o Ku
sini
m
wa
Tanz
ania
(S
AGCO
T SI
P)
Benk
i ya
Duni
a
2
2
0 0
706
Prog
ram
u ya
M
iund
ombi
nu
ya M
asok
o,
Ong
ezek
o la
Th
aman
i na
Msa
ada
wa
Fedh
a Vi
jiji
ni
(MIV
ARF)
IFAD
5
4 0
1 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
142
707
Mra
di w
a M
abor
esho
ya
Mah
akam
a Ya
nayo
mle
nga
Mw
anan
chi n
a U
toaj
i wa
Hak
i
Benk
i ya
Duni
a
0
0 0
0 0
708
Mra
di w
a H
udum
a ya
Af
ya y
a M
sing
i (B
HSP
)
Benk
i ya
Duni
a
6 6
0 0
0
709
Mra
di w
a M
tand
ao w
a Af
ya k
wa
Um
ma
Afri
ka
Mas
hari
ki
(EAP
HN
)
Benk
i ya
Duni
a
7
4 3
0 0
710
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Upa
tika
naji
na
Uku
zaji
wa
Nis
hati
Ta
nzan
ia
(TED
AP -
MEM
)
Benk
i ya
Duni
a
0
0 0
0 0
711
Mra
di w
a U
sim
amiz
i En
dele
vu w
a Ra
silim
ali z
a M
adin
i (SM
MRP
-II)
Benk
i ya
Duni
a
6
4 0
1 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
143
712
Mra
di w
a Ku
jeng
a U
wez
o Se
kta
ya N
isha
ti
(ESC
BP)
Benk
i ya
Duni
a
2 2
0 0
0
713
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Nis
hati
ya
Gas
i As
ilia
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
Oth
er D
Ps
4
4 0
0 0
714
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Elim
u ka
tika
Sh
ule
za
Seko
ndar
i(SE
DEP
II)
Benk
i ya
Duni
a
31
5
16
7 3
715
Mra
di w
a Ku
fund
isha
Sa
yans
i,
His
abat
i na
Kiin
gere
za
Kati
ka S
hule
za
Seko
ndar
i za
Seri
kali
kwa
Kutu
mia
TE
HAM
A (M
oEST
)
Swed
en
15
14
0
0 1
716
Prog
ram
u ya
El
imu
na U
juzi
kw
a Aj
ili y
a Ka
zi z
a U
zalis
haji
(E
SPJ)
Benk
i ya
Duni
a
0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
144
717
Mra
di w
a U
panu
zi w
a U
zalis
haji
wa
Mpu
nga
(ERP
P)
Benk
i ya
Duni
a
6 4
1 1
0
718
Mat
okeo
M
akub
wa
Sasa
Ka
tika
Mra
di w
a El
imu
ya M
alip
o kw
a M
atok
eo
(BRN
ED)
IDA
&
Swed
en
17
1
14
0 2
719
Prog
ram
u ya
Ku
said
ia E
limu
ya U
fund
i,
Maf
unzo
na
Elim
u ya
U
alim
u (S
TVET
-TE
)
Benk
i ya
mae
ndel
eo
Afri
ka
4
1 0
2 1
720
Wak
ala
wa
Usa
firi
wa
Mw
endo
kasi
(D
ART)
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
Wad
au w
a m
aend
eleo
11
3 6
2 0
721
Mra
di w
a U
shin
dani
Sek
ta
Bina
fsi (
PSCP
)
IDA
19
12
6
1 0
722
Prog
ram
u ya
Ku
bore
sha
Mij
i Ta
nzan
ia
(TSC
P) -
PO
RA
LG
IDA
55
41
4
10
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
145
723
Mfu
mo
wa
Kita
ifa
wa
Kubo
resh
a Se
cta
Mba
limba
li (N
MSF
)
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
Wad
au w
a m
aend
eleo
0 0
0 0
0
724
Prog
ram
u ya
Ku
imar
isha
Af
ya y
a M
sing
i kw
a M
atok
eo
(SPH
CRP)
IDA
0
0 0
0 0
725
wek
ezaj
i wa
Nda
ni K
atik
a H
ali y
a H
ewa
(LIC
) -
PO-R
ALG
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
Wad
au w
a m
aend
eleo
2 2
0 0
0
726
Mra
di w
a Se
ra
ya U
tete
zi n
a U
cham
buzi
(U
NIC
EF)
PO-
RALG
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
Wad
au w
a m
aend
eleo
0 0
0 0
0
727
Mfu
ko M
kuu-
M
radi
wa
Kifu
a Ki
kuu
(TZA
-T-
MoF
P)
Mfu
ko
Mku
u (G
loba
l Fu
nd)
9
0 4
5 0
728
Mfu
ko M
kuu-
M
radi
wa
Uki
mw
i
Mfu
ko
Mku
u (G
loba
l Fu
nd)
8
5 3
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
146
729
Mfu
ko M
kuu-
Mra
di w
a Ku
imar
isha
M
ifum
o ya
Af
ya/M
alar
ia
(TZA
-H-M
oF)
Mfu
ko
Mku
u (G
loba
l Fu
nd)
26
10
5
11
0
730
Kitu
o ch
a M
afun
zo K
anda
ya
Kig
oma
(KZT
C)
Shir
ika
la
mis
aada
la
kim
arek
ani
(USA
ID)
0
0 0
0 0
731
Taas
isi y
a Af
ya
ya M
sing
i (P
HCI
)
Shir
ika
la
mis
aada
la
kim
arek
ani
(USA
ID)
0
0 0
0 0
732
Prog
ram
u ya
Ki
taif
a ya
Ku
dhib
iti
Mal
aria
(N
MCP
)
Shir
ika
la
mis
aada
la
kim
arek
ani
(USA
ID)
0
0 0
0 0
733
Kitu
o ch
a M
aend
eleo
ya
Elim
u ya
Afy
a Ar
usha
(CE
DH
A)
Shir
ika
la
mis
aada
la
kim
arek
ani
(USA
ID)
0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
147
734
Mam
laka
ya
Udh
ibit
i wa
Man
unuz
i ya
Um
ma
(PPR
A) –
ku
piti
a gr
ant
agre
emen
t nu
mbe
r 62
1-00
4.08
Shir
ika
la
mis
aada
la
kim
arek
ani
(USA
ID)
0
0 0
0 0
735
Prog
ram
u ya
Ku
ondo
a M
alar
ia
Zanz
ibar
i (Z
AMEP
) ku
piti
a co
oper
ativ
e ag
reem
ent
num
ber:
621
-00
11.0
1
Shir
ika
la
mis
aada
la
kim
arek
ani
(USA
ID)
4
4 0
0 0
736
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
Se
kta
ya M
aji
Awam
u ya
Pili
(W
SDP
II)
Benk
i ya
Duni
a
25
3
3 6
13
737
Mra
di w
a U
buni
fu
Ulio
waz
i Kat
ika
Tasi
nia
ya
Uch
imba
ji
Mad
ini
Tanz
ania
(TE
ITI
CIDA
)
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
CIDA
0
0 0
0 0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
148
738
Mra
di w
a U
buni
fu
Ulio
waz
i Kat
ika
Tasi
nia
ya
Uch
imba
ji
Mad
ini
Tanz
ania
(TE
ITI
- U
moj
a W
a U
laya
)
Um
oja
Wa
Ula
ya
1
0 0
1 0
739
Prog
ram
u ya
M
ageu
zi/M
abad
iliko
ya
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
za U
mm
a IV
(PF
MRP
)
Benk
i ya
Duni
a
15
7
2 6
0
740
Mam
laka
ya
Map
ato
Tanz
ania
–
Mfu
ko w
a Pa
moj
a w
a M
abor
esho
ya
Kisa
sa y
a U
kusa
naji
Kod
i
Nor
way
&
Denm
ark
0
0 0
0 0
741
Prog
ram
u ya
Ku
said
ia E
limu
ya S
ekon
dari
(P
SSE)
Mfu
ko
wa
Fedh
a w
a Pa
moj
a
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
Wad
au w
a m
aend
eleo
0 0
0 0
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
149
742
Mfu
ko w
a Pa
moj
a w
a Ku
chan
gia
Mra
di w
a M
pang
o w
a Ku
fuat
ilia
Um
aski
ni
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
Wad
au w
a m
aend
eleo
1 0
1 0
0
Jum
la
7740
22
20
1325
27
20
1475
Ki
amba
tani
sho
Na.
4:
Hat
i za
Uka
guzi
Zili
zoto
lew
a 4(
i) W
atek
elez
aji W
alio
pata
Hat
i Ina
yori
dhis
ha (
ASD
P, H
BF,
RF,T
ASA
F &
WSD
P)
N
a . M
koa
Ji
na la
M
radi
H
alm
asha
uri
Hat
i In
ayor
idhi
sha
Na .
Mko
a
Jina
la
Mra
di
Hal
mas
haur
i H
ati
Inay
orid
hish
a 1
Arus
ha
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a Ar
usha
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ru
ngw
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a Ka
ratu
1
15
Song
we
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ile
je
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
150
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a M
eru
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Mbo
zi
1
2 Co
ast
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a Ba
gam
oyo
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Mom
ba
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Mji
wa
Kiba
ha
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Tund
uma
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a Ru
fiji
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a So
ngw
e 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
151
Sekt
a ya
Ki
limo
3 G
eita
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Sekt
a ya
Ki
limo
Wila
ya y
a G
eita
1
16
Mor
ogor
o M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Gai
ro
1
4 Ir
inga
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Sekt
a ya
Ki
limo
Wila
ya y
a Ir
inga
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ki
lom
bero
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Man
ispa
a ya
Ir
inga
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ki
losa
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a Ki
lolo
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
orog
oro
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
152
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a M
ufin
di
1
M
fuko
wa
Bara
bara
M
anis
pa y
a M
orog
oro
1
5 Ka
tavi
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Sekt
a ya
Ki
limo
Wila
ya y
a M
lele
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
vom
ero
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a M
pand
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Ifak
ara
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Man
ispa
a ya
M
pand
a
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Mal
inyi
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
153
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a N
sim
bo
1 17
M
twar
a M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Mas
asi
1
6 Ki
liman
jaro
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Sekt
a ya
Ki
limo
Wila
ya y
a H
ai
1
M
fuko
wa
Bara
bara
M
ji w
a M
asas
i 1
7 Li
ndi
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a Ki
lwa
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Mtw
ara
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a Ru
angw
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
M
twar
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
154
Sekt
a ya
Ki
limo
8 M
anya
ra
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a Ba
bati
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ta
ndah
imba
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Mji
wa
Baba
ti
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Nan
yam
ba
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a H
anan
g'
1 18
M
wan
za
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
Ile
mel
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a Ki
teto
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Kw
imba
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
155
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a M
bulu
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
agu
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a Si
man
jiro
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Jiji
la
Mw
anza
1
9 M
beya
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Sekt
a ya
Ki
limo
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Seng
erem
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a Ch
unya
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Bu
chos
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
156
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a Ky
ela
1 19
N
jom
be
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Lu
dew
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a M
bara
li 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Mak
amba
ko
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Jiji
la M
beya
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
aket
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a M
beya
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a N
jom
be
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
157
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a Ru
ngw
e 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Njo
mbe
1
10
Song
we
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a Ile
je
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Wan
ging
'om
be
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a M
bozi
1
20
Rukw
a M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Kala
mbo
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a M
omba
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
ya
Sum
baw
anga
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
158
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a So
ngw
e 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Su
mba
wan
ga
1
11
Mor
ogor
o Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Sekt
a ya
Ki
limo
Wila
ya y
a Ki
losa
1
21
Ruvu
ma
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a M
orog
oro
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Mbi
nga
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a U
lang
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Mbi
nga
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
159
Sekt
a ya
Ki
limo
12
Mw
anza
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Sekt
a ya
Ki
limo
Wila
ya y
a M
agu
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Nya
sa
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Jiji
la
Mw
anza
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a So
ngea
1
13
Rukw
a Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Sekt
a ya
Ki
limo
Wila
ya y
a Ka
lam
bo
1
M
fuko
wa
Bara
bara
M
anis
paa
ya
Song
ea
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a N
kasi
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Tu
ndur
u 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
160
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Man
ispa
a ya
Su
mba
wan
ga
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Mad
aba
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a Su
mba
wan
ga
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Msa
lala
1
14
Ruvu
ma
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Sh
inya
nga
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a M
bing
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
Sh
inya
nga
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
161
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a N
yasa
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a U
shet
u 1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a So
ngea
1
22
Sim
iyu
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ba
riad
i 1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Man
ispa
a ya
So
ngea
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Bari
adi
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Wila
ya y
a Tu
ndur
u 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
asw
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
162
Sekt
a ya
Ki
limo
15
Sim
iyu
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a It
ilim
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a It
ilim
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a M
asw
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Bu
sega
1
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Wila
ya y
a M
eatu
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
eatu
1
16
Tang
a Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Mji
wa
Koro
gwe
1 23
Si
ngid
a M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Iram
ba
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
163
Sekt
a ya
Ki
limo
Prog
ram
u ya
M
aend
ele
o ya
Se
kta
ya
Kilim
o
Jiji
la T
anga
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ik
ungi
1
1 AR
USH
A M
fuko
wa
Afya
Ji
ji la
Aru
sha
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Man
yoni
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
ondu
li 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
kala
ma
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Lo
ngid
o 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Si
ngid
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
eru
1
M
fuko
wa
Bara
bara
M
anis
paa
ya
Sing
ida
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ka
ratu
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a It
igi
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a N
goro
ngor
o 1
24
Tabo
ra
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ig
unga
1
2 M
ANYA
RA
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ki
teto
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ka
liua
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
bulu
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a N
zega
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ba
bati
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Nze
ga
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a H
anan
g’
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Siko
nge
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
164
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Mbu
lu
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Tabo
ra
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Baba
ti
1
M
fuko
wa
Bara
bara
M
anis
paa
ya
Tabo
ra
1
3 KI
LIM
ANJA
RO
M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Mos
hi
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Ura
mbo
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ro
mbo
1
25
Tang
a M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Bum
buli
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a H
ai
1
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Han
deni
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Sa
me
1
M
fuko
wa
Bara
bara
M
ji w
a H
ande
ni
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
M
oshi
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ki
lindi
1
4 TA
NG
A M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Han
deni
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ko
rogw
e 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
king
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Koro
gwe
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ki
lindi
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Lu
shot
o 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Jiji
la T
anga
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
king
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Pa
ngan
i 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
uhez
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ko
rogw
e 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Pa
ngan
i 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
uhez
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Jiji
la T
anga
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Lu
shot
o 1
1 M
BEYA
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Jiji
la M
beya
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
165
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Bu
mbu
li 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
beya
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Han
deni
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
bara
ri
1
4 DA
R M
fuko
wa
Afya
M
anis
paa
ya
Tem
eke
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a Ru
ngw
e 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
Ki
nond
oni
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a Ch
unya
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
Ila
la
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a Ky
ela
1
6 LI
NDI
M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Kilw
a 1
2 SO
NG
WE
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
bozi
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Li
wal
e 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ile
je
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Li
ndi
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
omba
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ru
angw
a 1
3 IR
ING
A M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Man
ispa
a ya
Ir
inga
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
Li
ndi
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a Ir
inga
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
166
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a N
achi
ngw
ea
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
ufin
di
1
7 M
ORO
GO
RO
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ki
lom
bero
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ki
lolo
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ki
losa
1
4 G
EITA
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a G
eita
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
vom
ero
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Mji
wa
Gei
ta
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
orog
oro
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a Ch
ato
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
M
orog
oro
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a Bu
kom
be
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a U
lang
a 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a N
yang
’hw
ale
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Ifak
ara
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
bogw
e 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
alin
yi
1 5
KAG
ERA
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Man
ispa
a ya
Bu
koba
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a G
airo
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Bu
koba
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
167
8 M
TWAR
A M
fuko
wa
Afya
M
anis
paa
ya
Mtw
ara
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
isen
yi
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Mas
asi
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a Bi
hara
mul
o 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
asas
i 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ky
erw
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
twar
a 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ka
ragw
e 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Nan
yam
ba
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
uleb
a
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ta
ndah
imba
1
6 KA
TAVI
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
pand
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a N
anyu
mbu
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Man
ispa
a ya
M
pand
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
New
ala
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a N
sim
bo
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a N
ewal
a 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
lele
1
9 CO
AST
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ki
sara
we
1 7
NJO
MBE
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a N
jom
be
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
168
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ki
baha
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Mji
wa
Njo
mbe
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
afia
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Lu
dew
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ba
gam
oyo
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Mji
wa
Mak
amba
ko
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
kura
nga
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a W
ang'
ing'
omb
e
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ru
fiji
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
aket
e 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ch
alin
ze
1 8
RUVU
MA
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Man
ispa
a ya
So
ngea
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Kiba
ha
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a So
ngea
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ki
biti
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Tu
ndur
u 1
10
KIG
OM
A M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Buhi
gwe
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
bing
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Kigo
ma
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
169
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ki
bond
o 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a N
yasa
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Kasu
lu
1 9
RUKW
A M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Man
ispa
a ya
S’
wan
ga
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ka
konk
o 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a S’
wan
ga
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a U
vinz
a 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a N
kasi
1
11
SIN
GID
A M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Iram
ba
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a Ka
lam
bo
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
kala
ma
1 10
SI
MIY
U
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ba
riad
i 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
anyo
ni
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
asw
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
Si
ngid
a 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a M
eatu
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Si
ngid
a 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a It
ilim
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a It
igi
1 11
SH
INYA
NG
A M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Man
ispa
a ya
Sh
inya
nga
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
170
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ik
ungi
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Sh
inya
nga
1
12
TABO
RA
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ka
liua
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
sala
la
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a U
ram
bo
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a U
shet
u 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ig
unga
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Mji
wa
Kaha
ma
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
Ta
bora
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ki
shap
u 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Si
kong
e 1
12
MW
ANZA
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
agu
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a N
zega
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Kw
imba
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ta
bora
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Jiji
la
Mw
anza
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Nze
ga
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a M
isun
gwi
1
13
DODO
MA
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
pwap
wa
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Man
ispa
a ya
Ile
mel
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
171
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ba
hi
1
M
radi
wa
Mae
ndel
eo
ya J
amii
Wila
ya y
a Se
nger
ema
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ch
amw
ino
1 13
M
ARA
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Man
ispa
a ya
M
usom
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ch
emba
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Ro
rya
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
Do
dom
a 1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Bu
nda
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ko
ndoa
1
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii
Wila
ya y
a Se
reng
eti
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Kond
oa
1 1
ARU
SHA
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Jiji
la A
rush
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ko
ngw
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Lo
ngid
o 1
14
MAR
A M
fuko
wa
Afya
M
anis
paa
ya
Mus
oma
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ka
ratu
1
Mfu
ko w
a W
ilaya
ya
1
Pr
ogra
mu
Wila
ya y
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
172
Afya
Ro
rya
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Mer
u
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ta
rim
e 1
2 CO
AST
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ch
alin
ze
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Tari
me
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ba
gam
oyo
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Se
reng
eti
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ki
baha
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
usom
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
Kiba
ha
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Bu
tiam
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ki
biti
1
15
MW
ANZA
M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Buch
osa
1
Pr
ogra
mu
ya
Wila
ya y
a Ki
sara
we
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
173
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Afya
M
anis
paa
ya
Ilem
ela
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
afia
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
isun
gwi
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
kura
nga
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
agu
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ru
fiji
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Jiji
la
Mw
anza
1
3 DA
R Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Man
ispa
aa y
a Ila
la
1
16
SHIN
YAN
GA
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Kaha
ma
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Man
ispa
a ya
Ki
gam
boni
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a U
shet
u 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
Man
ispa
a ya
Ki
nond
oni
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
174
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Kish
apu
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Man
ispa
a ya
Te
mek
e 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
sala
la
1 4
DODO
MA
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ba
hi
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Sh
inya
nga
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ch
amw
ino
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
Sh
inya
nga
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Man
ispa
a ya
Do
dom
a 1
17
GEI
TA
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Gei
ta
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ko
ndoa
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ch
ato
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
Mji
wa
Kond
oa
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
175
ya M
aji
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Bu
kom
be
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ko
ngw
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a N
yang
’hw
ale
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
pwap
wa
1
18
SIM
IYU
M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Bari
adi
1 23
G
EITA
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Bu
kom
be
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Bari
adi
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ch
ato
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
asw
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a G
eita
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
eatu
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
Gei
ta
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
176
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Bu
sega
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
bogw
e 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a It
ilim
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a N
yang
’hw
ale
1
19
KAG
ERA
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Bu
koba
1
5 IR
ING
A Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ir
inga
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
uleb
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Man
ispa
a ya
Ir
inga
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ka
ragw
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ki
lolo
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
isse
nyi
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Mji
wa
Maf
inga
1
Mfu
ko w
a W
ilaya
ya
1
Pr
ogra
mu
Wila
ya y
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
177
Afya
N
gara
ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Muf
indi
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Bi
hara
mul
o 1
26
KATA
VI
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
lele
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
Bu
koba
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
pand
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ky
erw
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Man
ispa
a ya
M
pand
a 1
20
IRIN
GA
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
ufin
di
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
pim
bwe
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Maf
inga
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a N
sim
bo
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ki
lolo
1
6 KA
GER
A Pr
ogra
mu
ya
Wila
ya y
a Bi
hara
mul
o 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
178
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Afya
M
anis
paa
ya
Irin
ga
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Bu
koba
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ir
inga
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Man
ispa
a ya
Bu
koba
1
21
MBE
YA
Mfu
ko w
a Af
ya
Jiji
la M
beya
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ka
ragw
e 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
beya
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ky
erw
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ky
ela
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
uleb
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ru
ngw
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
Wila
ya y
a N
gara
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
179
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Mba
rali
1 7
KIG
OM
A Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Bu
higw
e 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ch
unya
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ka
konk
o 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Mji
wa
Kasu
lu
1
22
SON
GW
E M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Mbo
zi
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ki
bond
o 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a So
ngw
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Man
ispa
a ya
Ki
gom
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ile
je
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
Wila
ya y
a Ki
gom
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
180
ya M
aji
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
omba
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a U
vinz
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Tund
uma
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
oshi
1
23
NJO
MBE
M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Njo
mbe
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Man
ispa
a ya
M
oshi
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Njo
mbe
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
wan
ga
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
aket
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ro
mbo
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Lu
dew
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Sa
me
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
181
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Mak
amba
ko
1 9
LIN
DI
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ki
lwa
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a W
ang'
ing'
omb
e
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Li
wal
e 1
24
KATA
VI
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
pand
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Li
ndi
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a N
sim
bo
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ru
angw
a 1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
lele
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Man
ispa
a ya
Li
ndi
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
pibw
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a N
achi
ngw
ea
1
Mfu
ko w
a M
anis
paa
ya
1 25
N
JOM
BE
Prog
ram
u W
ilaya
ya
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
182
Afya
M
pand
a ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Lude
wa
25
RUKW
A M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Sum
baw
anga
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
Mak
amba
ko
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
Su
mba
wan
ga
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a N
jom
be
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Ka
lam
bo
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Mji
wa
Njo
mbe
1
26
RUVU
MA
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a Tu
ndur
u 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a W
ang'
ing'
omb
e
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
bing
a 1
10
MAN
YARA
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ba
bati
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
1
Prog
ram
u ya
M
ji w
a Ba
bati
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
183
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Afya
W
ilaya
ya
Song
ea
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a H
anan
g'
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Man
ispa
a ya
So
ngea
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ki
teto
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a N
yasa
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
bulu
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Wila
ya y
a M
adab
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
Mbu
lu
1
Mfu
ko w
a Af
ya
Mji
wa
Mbi
nga
1 11
M
ARA
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Bu
nda
1
1 Ar
usha
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Arus
ha
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
Mji
wa
Bund
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
184
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Bara
bara
Ji
ji la
Aru
sha
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Bu
tiam
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ka
ratu
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Man
ispa
a ya
M
usom
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Lo
ngid
o 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Se
reng
eti
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
eru
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ta
rim
e 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
ondu
li 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
Tari
me
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a N
goro
ngor
o 1
12
MBE
YA
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
185
ya M
aji
2 Co
ast
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ba
gam
oyo
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ch
unya
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ki
baha
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ky
ela
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Kiba
ha
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
bara
li 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ki
sara
we
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
beya
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
afia
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Jiji
la M
beya
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
kura
nga
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ru
ngw
e 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
186
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ru
fiji
1
13
MO
ROG
OR
O
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a G
airo
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ch
aliz
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
Ifak
ara
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ki
biti
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ki
lom
bero
1
3 Da
r Es
Sa
laam
M
fuko
wa
Bara
bara
M
anis
paa
ya
Ilala
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ki
losa
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
Ki
nond
oni
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
alin
yi
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
Te
mek
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
orog
oro
1
Mfu
ko w
a M
anis
paa
ya
1
Pr
ogra
mu
Wila
ya y
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
187
Bara
bara
Ki
gam
boni
ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mvo
mer
o
4 Do
dom
a M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Bahi
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a U
lang
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ch
amw
ino
1 14
M
TWAR
A Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
asas
i 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ch
emba
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
Mas
asi
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
Do
dom
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a N
anyu
mbu
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Kond
oa
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Mji
wa
Nan
yam
ba
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ko
ngw
a 1
Prog
ram
u ya
W
ilaya
ya
New
ala
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
188
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Mpw
apw
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
New
ala
1
5 G
eita
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Buko
mbe
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
twar
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ch
ato
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Man
ispa
a ya
M
twar
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a G
eita
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ta
ndah
imba
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Gei
ta
1 15
M
WAN
ZA
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Bu
chos
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
bogw
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
Wila
ya y
a Kw
imba
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
189
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Nya
ng'h
wal
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
agu
1
6 Ir
inga
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Irin
ga
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
isun
gwi
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
Ir
inga
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Jiji
la
Mw
anza
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ki
lolo
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Se
nger
ema
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
ufin
di
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a U
kere
we
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Maf
inga
1
16
RUKW
A Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
Wila
ya y
a Su
mba
wan
ga
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
190
ya M
aji
7 Ka
gera
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Biha
ram
ulo
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Man
ispa
a ya
Su
mba
wan
ga
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Bu
koba
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ka
lam
bo
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
Bu
koba
1
17
RUVU
MA
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
adab
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ka
ragw
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
bing
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ky
erw
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
Mbi
nga
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
isen
yi
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
191
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
uleb
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a N
yasa
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a N
gara
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a So
ngea
1
8 Ka
tavi
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Mle
le
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Man
ispa
a ya
So
ngea
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
pand
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Tu
ndur
u 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
M
pand
a 1
24
SIM
IYU
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ba
riad
i 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a N
sim
bo
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Mji
wa
Bari
adi
1
Mfu
ko w
a W
ilaya
ya
1
Pr
ogra
mu
Wila
ya y
a 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
192
Bara
bara
M
pim
bwe
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Buse
ga
9 Ki
gom
a M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Buhi
gwe
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a It
ilim
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ka
konk
o 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
asw
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ka
sulu
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
eatu
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Kasu
lu
1 18
SH
INYA
NG
A Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Mji
wa
Kaha
ma
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ki
bond
o 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ki
shap
u 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a U
vinz
a 1
Prog
ram
u ya
W
ilaya
ya
Msa
lala
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
193
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Bara
bara
M
anis
paa
ya
Kigo
ma
Uji
ji
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Sh
inya
nga
1
10
Kilim
anja
ro
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a H
ai
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Man
ispa
a ya
Sh
inya
nga
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
oshi
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a U
shet
u 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
M
oshi
1
19
SIN
GID
A Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ik
ungi
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
wan
ga
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ir
amba
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ro
mbo
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
Wila
ya y
a It
igi
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
194
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Sam
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
anyo
ni
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Si
ha
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
kala
ma
1
11
Lind
i M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Kilw
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Si
ngid
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Li
ndi
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Man
ispa
a ya
Si
ngid
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Man
ispa
a ya
Li
ndi
1 20
SO
NG
WE
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a Ile
je
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Li
wal
e 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
Wila
ya y
a M
bozi
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
195
ya M
aji
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a N
achi
ngw
ea
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
omba
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ru
angw
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a So
ngw
e 1
12
Man
yara
M
fuko
wa
Bara
bara
W
ilaya
ya
Baba
ti
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Mji
wa
Tund
uma
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Baba
ti
1 21
TA
BORA
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ig
unga
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a H
anan
g'
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ka
liua
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
bulu
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a N
zega
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
196
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Mbu
lu
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Si
kong
e 1
13
Mar
a M
fuko
wa
Bara
bara
M
anis
paa
ya
Mus
oma
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ta
bora
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
usom
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Man
ispa
a ya
Ta
bora
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ro
rya
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a U
ram
bo
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Bu
nda
1 22
TA
NG
A Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Bu
mbu
li 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Se
reng
eti
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a H
ande
ni
1
Mfu
ko w
a W
ilaya
ya
1
Pr
ogra
mu
Mji
wa
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
197
Bara
bara
Bu
tiam
a ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Han
deni
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Tari
me
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Ki
lindi
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Mji
wa
Bund
a 1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Mji
wa
Koro
gwe
1
14
Mbe
ya
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a Lu
shot
o 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ch
unya
1
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
Sek
ta
ya M
aji
Wila
ya y
a M
king
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a Ky
ela
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Wila
ya y
a M
uhez
a 1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
bara
li 1
Prog
ram
u ya
W
ilaya
ya
Pang
ani
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
198
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
M
fuko
wa
Bara
bara
Ji
ji la
Mbe
ya
1
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya S
ekta
ya
Maj
i
Jiji
la T
anga
1
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra
Wila
ya y
a M
beya
1
Jum
la
623
4(ii)
Wat
ekel
ezaj
i W
alio
pata
Hat
i Ina
yori
dhis
ha –
Mir
adi M
ingi
neyo
N
a.
Jina
la M
radi
W
afad
hili
Hat
i in
ayor
idhi
sha
1 Sh
irik
a la
Kim
atai
fa la
Kus
aidi
a W
atot
o (U
NIC
EF)
Shir
ika
la K
imat
aifa
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
) 1
2 Sh
irik
a la
Hud
uma
za M
isaa
da la
Kik
atol
iki (
CRS)
Sh
irik
a la
Kim
atai
fa la
Kus
aidi
a W
atot
o (U
NIC
EF)
1 3
PACT
Tan
zani
a Sh
irik
a la
Kim
atai
fa la
Kus
aidi
a W
atot
o (U
NIC
EF)
1 4
CUAM
M T
anza
nia
Shir
ika
la K
imat
aifa
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
) 1
5 M
radi
wa
Vita
bu v
ya W
atot
o Ta
nzan
ia (
CBPT
) Sh
irik
a la
Kim
atai
fa la
Kus
aidi
a W
atot
o (U
NIC
EF)
1 6
Bayl
or T
anza
nia
Shir
ika
la K
imat
aifa
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
) 1
7 W
izar
a ya
Afy
a M
aend
eleo
ya
Jam
ii, J
insi
a, W
azee
N
a W
atot
o
Shir
ika
la K
imat
aifa
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
) 1
8 Ju
kwaa
la M
aend
eleo
(PD
F)
Shir
ika
la K
imat
aifa
la K
usai
dia
Wat
oto
(UN
ICEF
) 1
9 O
fisi
ya
Mw
anas
heri
a M
kuu
(AG
C)
Shir
ika
la M
aend
eleo
la U
moj
a w
a M
atai
fa (
UN
DP)
1 10
W
izar
a ya
Fed
ha n
a M
ipan
go-
Idar
a ya
Kuo
ndoa
U
mas
kini
. Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
11
Ofi
si y
a W
azir
i M
kuu
(Kui
mar
isha
Taa
rifa
ya
Hal
i ya
H
ewa
na M
fum
o w
a Ku
toa
Taha
dhar
i ya
Map
ema)
Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
199
12
Shir
ika
la U
zalis
haji
Mal
i la
Jes
hi l
a Ku
jeng
a Ta
ifa
(SU
MA
JKT)
Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
13
Mra
di w
a SP
ANES
T kw
a Sh
irik
a la
Hif
adhi
za
Taif
a (T
ANAP
A/SP
ANES
T)
Shir
ika
la M
aend
eleo
la U
moj
a w
a M
atai
fa (
UN
DP)
1
14
Mfu
ko
wa
uhif
adhi
w
a W
anya
map
ori
Tanz
ania
(T
WPF
) Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
15
Chuo
Kik
uu c
ha D
ar e
s Sa
laam
– I
dara
ya
Uch
umi
(UDS
M D
oE)
Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
16
Taas
isi y
a U
ongo
zi
Shir
ika
la M
aend
eleo
la U
moj
a w
a M
atai
fa (
UN
DP)
1 17
Bo
di y
a M
aji y
a Bo
nde
la W
ami/
Ruvu
Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
18
Taas
isi y
a U
tafi
ti w
a Ki
uchu
mi n
a Ki
jam
ii (E
SRF)
Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
19
Tum
e ya
Mip
ango
Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
20
Bung
e la
Tan
zani
a Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
21
Kati
bu T
awal
a w
a M
koa
- Ta
bora
Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
22
Bodi
ya
Maj
i ya
Bon
de l
a Ru
vum
a na
Pw
ani
ya
Kusi
ni
Shir
ika
la M
aend
eleo
la U
moj
a w
a M
atai
fa (
UN
DP)
1
23
Kitu
o ch
a El
imu
Kiba
ha
Shir
ika
la M
aend
eleo
la U
moj
a w
a M
atai
fa (
UN
DP)
1
24
Wiz
ara
ya
Nis
hati
na
M
adin
i,
Mra
di
wa
Kuje
nga
Uw
ezo
kati
ka
Sekt
a ya
N
isha
ti
na
Tasn
ia
ya
Uch
imba
ji M
adin
i (M
EM-M
radi
wa
CADE
SE)
Shir
ika
la M
aend
eleo
la U
moj
a w
a M
atai
fa (
UN
DP)
1
25
Bodi
ya
Maj
i ya
Bond
e la
Pan
gani
Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
26
Wak
ala
wa
Hud
uma
za M
isit
u Ta
nzan
ia (
TFSA
) Sh
irik
a la
Mae
ndel
eo la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
) 1
27
Prog
ram
u ya
Kus
aidi
a Se
kta
ya U
safi
rish
aji (
TSSP
) Be
nki y
a D
unia
1
28
Mra
di w
a U
wez
esha
ji B
iash
ara
na U
safi
rish
aji K
usin
i m
wa
Afri
ka (
SATT
FP)
Benk
i ya
Dun
ia
1
29
Mra
di w
a Ku
said
ia S
ecta
ya
Bara
bara
Aw
amu
ya P
ili
(RSS
P II)
Be
nki y
a M
aend
eleo
Afr
ika
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
200
30
Mfu
mo
wa
Mab
asi
ya M
wen
doka
si D
ar e
s Sa
laam
(B
RT)
Awam
u ya
Pili
Be
nki y
a M
aend
eleo
Afr
ika
& A
GTF
1
31
Mra
di w
a U
jenz
i w
a Ba
raba
ra y
a Ki
mat
aifa
Aru
sha–
Tave
ta/H
olili
-Voi
Be
nki y
a M
aend
eleo
Afr
ika
1
32
Mra
di w
a Ku
said
ia S
ekta
ya
Bara
bara
Aw
amu
ya
Kwan
za (
RSSP
I)
Benk
i ya
Mae
ndel
eo A
frik
a &
JIC
A)
1
33
Mra
di w
a U
sim
amiz
i w
a M
azin
gira
ya
Ziw
a Vi
ctor
ia
(LVE
MP
II)
Benk
i ya
Dun
ia
1
34
Mra
di w
a U
sim
amiz
i na
Uhi
fadh
i Vy
anzo
vya
Maj
i Ki
hans
i (KC
CMP)
Be
nki y
a D
unia
1
35
Mra
di w
a U
safi
rish
aji
Kand
a ya
Kat
i Aw
amu
ya P
ili
(CTC
P II)
Be
nki y
a D
unia
1
36
Mra
di
wa
Miu
ndom
binu
ya
M
awas
ilian
o Ki
mko
a (R
CIP)
Be
nki y
a D
unia
1
37
Taas
isi
ya K
ujen
ga U
wez
o Af
rika
(AC
BF)
Mra
di -
AC
BF/N
M-A
IST
Benk
i ya
Dun
ia
1
38
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Mji
Mku
u w
a Da
r es
Sal
aam
(D
MDP
) Be
nki y
a D
unia
1
39
Mra
di w
a U
sim
amiz
i w
a U
vuvi
na
Uku
aji
wa
Pam
oja
Kusi
ni M
agha
ribi
mw
a Ba
hari
ya
Hin
di (
SWIO
Fish
) Be
nki y
a D
unia
1
40
Mra
di
wa
Mal
iasi
li St
ahim
ivu
kwa
Ajili
ya
M
aend
eleo
ya
Uon
gozi
(RE
GRO
W)
Benk
i ya
Dun
ia
1
41
Mra
di w
a U
wek
ezaj
i ka
tika
Kuk
uza
Kilim
o Ku
sini
m
wa
Tanz
ania
(SA
GCO
T SI
P)
Benk
i ya
Dun
ia
1
42
Prog
ram
u ya
Miu
ndom
binu
ya
Mas
oko,
Ong
ezek
o la
Th
aman
i na
Msa
ada
wa
Fedh
a Vi
jiji
ni (
MIV
ARF)
IF
AD
1
43
Mra
di w
a M
abor
esho
ya
Mah
akam
a Ya
nayo
mle
nga
Mw
anan
chi n
a U
toaj
i wa
Hak
i Be
nki y
a D
unia
1
44
Mra
di w
a H
udum
a ya
Afy
a ya
Msi
ngi (
BHSP
) Be
nki y
a D
unia
1
45
Mra
di
wa
Mta
ndao
w
a Af
ya
kwa
Um
ma
Afri
ka
Benk
i ya
Dun
ia
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
201
Mas
hari
ki (
EAPH
N)
46
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Upa
tika
naji
na
Uku
zaji
wa
Nis
hati
Tan
zani
a (T
EDAP
- M
EM)
Benk
i ya
Dun
ia
1
47
Mra
di
wa
Usi
mam
izi
Ende
levu
w
a Ra
silim
ali
za
Mad
ini (
SMM
RP-I
I)
Benk
i ya
Dun
ia
1
48
Mra
di
wa
Kuje
nga
Uw
ezo
wa
Sekt
a ya
N
isha
ti
(ESC
BP)
Benk
i ya
Dun
ia
1
49
Mra
di w
a M
aend
eleo
ya
Nis
hati
ya
Ges
i Asi
lia
Seri
kali
ya T
anza
nia
& W
adau
wa
Mae
ndel
eo
1
50
Prog
ram
u ya
Mae
ndel
eo y
a El
imu
kati
ka S
hule
za
Seko
ndar
i(SE
DEP
II)
Benk
i ya
Dun
ia
1
51
Mra
di
wa
Kufu
ndis
ha
Saya
nsi,
H
isab
ati
na
Kiin
gere
za K
atik
a Sh
ule
za S
ekon
dari
za
Seri
kali
kwa
Kutu
mia
TEH
AMA
(MoE
ST)
Swed
en
1
52
Prog
ram
u ya
Elim
u na
Uju
zi k
wa
Ajili
ya
Kazi
za
Uza
lisha
ji (
ESPJ
) Be
nki y
a D
unia
1
53
Mra
di w
a U
panu
zi w
a U
zalis
haji
wa
Mpu
nga
(ERP
P)
Benk
i ya
Dun
ia
1
54
Mat
okeo
Mak
ubw
a Sa
sa K
atik
a M
radi
wa
Elim
u ya
M
alip
o kw
a M
atok
eo (
BRN
ED)
Shir
ika
la M
aend
eleo
la K
imat
aifa
& S
wed
en
1
55
Prog
ram
u ya
Kus
aidi
a E
limu
ya U
fund
i, M
afun
zo n
a El
imu
ya U
alim
u (S
TVET
-TE)
Be
nki y
a M
aend
eleo
Afr
ika
1
56
Wak
ala
wa
Usa
firi
wa
Mw
endo
kasi
(DA
RT)
Seri
kali
ya T
anza
nia
& W
adau
wa
Mae
ndel
eo
1 57
M
radi
wa
Ush
inda
ni S
ekta
Bin
afsi
(PS
CP)
Shir
ika
la M
aend
eleo
la K
imat
aifa
1
58
Prog
ram
u ya
Kub
ores
ha M
iji
Tanz
ania
(TS
CP)
- PO
RA
LG
Shir
ika
la M
aend
eleo
la K
imat
aifa
1
59
Mfu
mo
wa
Kita
ifa
wa
Kubo
resh
a Se
cta
Mba
limba
li (N
MSF
)
Seri
kali
ya T
anza
nia
& W
adau
wa
Mae
ndel
eo
1
60
Prog
ram
u ya
Ku
imar
isha
Af
ya
ya
Msi
ngi
kwa
Mat
okeo
(SP
HCR
P)
Shir
ika
la M
aend
eleo
la K
imat
aifa
1
61
wek
ezaj
i w
a N
dani
Kat
ika
Hal
i ya
Hew
a (L
IC)
- PO
-Se
rika
li ya
Tan
zani
a &
Wad
au w
a M
aend
eleo
1
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
202
RALG
62
Mra
di w
a Se
ra y
a U
tete
zi n
a U
cham
buzi
(U
NIC
EF)
PO-
RALG
Se
rika
li ya
Tan
zani
a &
Wad
au w
a M
aend
eleo
1
63
Mfu
ko w
a Ki
mat
aifa
- M
radi
wa
Kifu
a Ki
kuu
(TZA
-T-
MoF
P)
Mfu
ko w
a Ki
mat
aifa
wa
Mal
aria
, Ki
fua
Kiku
u na
U
KIM
WI (
Glo
bal F
und)
1
64
Mfu
ko w
a Ki
mat
aifa
- M
radi
wa
UKI
MW
I M
fuko
wa
Kim
atai
fa w
a M
alar
ia,
Kifu
a Ki
kuu
na
UKI
MW
I (G
loba
l Fun
d)
1
65
Mfu
ko
wa
Kim
atai
fa
- M
radi
w
a M
alar
ia(T
ZA-T
-M
oFP)
M
fuko
wa
Kim
atai
fa w
a M
alar
ia,
Kifu
a Ki
kuu
na
UKI
MW
I (G
loba
l Fun
d)
1
66
Mam
laka
ya
Udh
ibit
i w
a M
anun
uzi
ya U
mm
a (P
PRA)
–
kupi
tia
gran
t ag
reem
ent
num
ber
621-
004.
08
Shir
ika
la m
isaa
da la
kim
arek
ani (
USA
ID)
1
67
Prog
ram
u ya
Kuo
ndoa
Mal
aria
Zan
ziba
ri
(ZAM
EP)
kupi
tia
mak
ubal
iano
ya
Ush
irik
iano
Na.
621
-001
1.01
Sh
irik
a la
mis
aada
la k
imar
ekan
i (U
SAID
) 1
68
Prog
ram
u ya
Mae
ndel
eo S
ekta
ya
Maj
i Aw
amu
ya
Pili
(WSD
P II)
Be
nki y
a D
unia
1
69
Mra
di
wa
Ubu
nifu
U
lio
waz
i Ka
tika
Ta
sini
a ya
U
chim
baji
Mad
ini T
anza
nia
(TEI
TI C
IDA)
Se
rika
li ya
Tan
zani
a &
CID
A 1
70
Mra
di
wa
Ubu
nifu
U
liow
azi
Kati
ka
Tasi
nia
ya
Uch
imba
ji
Mad
ini
Tanz
ania
(T
EITI
-
Um
oja
Wa
Ula
ya)
Um
oja
Wa
Ula
ya
1
71
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
/Mab
adili
ko y
a U
sim
amiz
i w
a Fe
dha
za U
mm
a IV
(PF
MRP
)
Benk
i ya
Dun
ia
1
72
Mam
laka
ya
Map
ato
Tanz
ania
– M
fuko
wa
Pam
oja
wa
Mab
ores
ho y
a Ki
sasa
ya
Uku
sana
ji K
odi
Nor
way
& D
enm
ark
1
73
Prog
ram
u ya
Kus
aidi
a El
imu
ya S
ekon
dari
(PS
SE)
Mfu
ko w
a Fe
dha
wa
Pam
oja
Seri
kali
ya T
anza
nia
& W
adau
wa
Mae
ndel
eo
1
74
Mfu
ko w
a Pa
moj
a w
a Ku
chan
gia
Mra
di w
a M
pang
o w
a Ku
fuat
ilia
Um
aski
ni
Seri
kali
ya T
anza
nia
& W
adau
wa
mae
ndel
eo
1
Jum
la
74
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
203
4(iii
) W
atek
elez
aji
Mir
adi W
alio
pata
Hat
i Yen
ye S
haka
na
Isiy
orid
hish
a N
a.
Wat
ekel
ezaj
i M
ambo
Yal
iyop
elek
ea K
upat
a H
ati Y
enye
Sha
ka n
a Is
iyor
idhi
sha
Pr
ogra
mu
ya
Mae
ndel
eo
ya
Sekt
a ya
Ki
limo
1 W
ilaya
ya
Ba
riad
i H
ati
za m
alip
o ze
nye
kias
i ch
a Sh
.Tz.
85,
077,
600
hazi
kuw
akili
shw
a kw
a aj
ili y
a uk
aguz
i, h
ivyo
ni
mes
hind
wa
kuha
kiki
uh
alal
i w
a m
alip
o ya
liyof
anyi
ka
kam
a ili
vyoo
nyes
hwa
kwen
ye
taar
ifa
ya
uten
daji
wa
fedh
a.
H
BF
1
Wila
ya
ya
Kasu
lu
H
ati
za m
alip
o na
via
mba
tish
o vy
a ny
arak
a m
abal
imba
li v
yeny
e ju
mla
ya
Sh.T
z. 5
,142
,000
ha
ziku
letw
a kw
a aj
ili y
a ku
haki
kiw
a, h
ivyo
uka
guzi
ulis
hind
wa
kuth
ibit
isha
uha
lali
wa
mal
ipo
hayo
kam
a ya
livyo
ones
hwa
kwen
ye t
aari
fa y
a he
sabu
za
Fedh
a
Uka
guzi
a ul
ishi
dwa
kuji
ridh
isha
uh
alal
i w
a m
atum
izi
ya
kias
i ch
a Sh
.Tz.
9,
228,
448
kilic
hotu
mw
a ka
tika
Hos
pita
li ya
Isok
o.
Ku
likuw
a na
ong
ezek
o la
kia
si c
ha S
h.Tz
. 24
1,00
0 na
kia
si S
h.Tz
. (9
,931
) am
balo
hal
ikuw
a na
m
aele
zo k
wen
ye d
ham
ana
ya r
uzuk
u ili
yo a
hilis
hwa
na k
usan
yiko
la
ziad
a kw
a m
fuat
ano
huo
kati
ka v
itab
u vy
a m
ahes
abu.
2
Wila
ya
ya
Kigo
ma
Ong
ezek
o la
kia
si c
ha S
h.Tz
. 1
0,77
8,60
1 zi
lizoi
ngiz
wa
kati
ka v
itab
u vy
a m
ahes
abu
kam
a m
apat
o ya
ru
zuku
yal
iyot
umik
a m
wak
a hu
u ha
kiku
wa
na m
aele
zo.
Hiv
yo k
usab
abis
ha v
itab
u vy
a m
ahes
abu
kuto
ones
ha u
halis
ia.
3 W
ilaya
ya
G
eita
U
kagu
zi u
lishi
ndw
a ku
thib
itis
ha u
hala
li w
a m
atum
izi
yeny
e ki
asi
cha
Sh.T
z. 3
1,53
1,80
6 ku
toka
na n
a ku
toku
was
ilish
wa
kwa
hati
za
mal
ipo.
4
Wila
ya
ya
Mbo
ngw
e U
kagu
zi u
lishi
ndw
a ku
thib
itis
ha u
hala
li w
a m
atum
izi
ya k
awai
da y
enye
kia
si c
ha S
h.Tz
. 23
,836
,471
ku
toka
na n
a ku
toku
was
ilish
wa
kwa
nyal
aka
za m
alip
o.
5 W
ilaya
ya
Bu
nda
Uka
guzi
ulis
hind
wa
kuth
ibit
isha
uha
lali
wa
mat
umiz
i yen
ye k
iasi
cha
Sh.
Tz.
36,8
00,4
60
kam
a ili
vyor
ipot
iwa
kati
ka t
aari
fa y
a u
tend
aji
wa
kife
dha
kuto
kana
kut
ojit
oshe
leza
kw
a ny
arak
a za
m
alip
o.
6 W
ilaya
ya
Ar
usha
Uka
guzi
ulis
hind
wa
kuth
ibit
isha
uha
lali
wa
mat
umiz
i ya
kaw
aida
yen
ye k
iasi
cha
Sh.
Tz.1
5,79
5,00
0 ku
toka
na n
a ku
toku
was
ilish
wa
kwa
hati
za
mal
ipo.
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
204
O
ngez
eko
la k
iasi
cha
Sh.
Tz.
2,80
0,00
0 a
mba
lo l
iliin
gizw
a ka
ma
mat
umiz
i ka
tika
vit
abu
vya
mah
esab
u bi
la k
uwa
na m
aele
zo.
Ki
asi
cha
Sh.T
z. 2
8,55
2,28
0 am
bach
o ni
mat
umiz
i ya
mw
aka
ulio
pita
hak
ikui
ngiz
wa
kati
ka t
aari
fa
ya u
tend
aji w
a fe
dha
ya m
wak
a hu
sika
, hi
vyo
kusa
babi
sha
taar
ifa
ya u
tend
aji w
a fe
dha
ya m
wak
a hu
u ku
wa
na o
ngez
eko
la m
atum
izi k
wa
kias
i hic
ho.
7 W
ilaya
ya
M
wan
ga
U
kagu
zi u
lishi
ndw
a ku
thib
itis
ha u
hala
li w
a m
atum
izi
ya k
awai
da y
enye
kia
si c
ha S
h.Tz
. 1,
640,
477
kuto
kana
na
kuto
kuw
asili
shw
a kw
a ha
ti z
a m
alip
o.
U
kagu
zi u
lishi
ndw
a ku
thib
itis
ha u
hala
li w
a m
atum
izi
yeny
e ki
asi
cha
Sh.T
z. 2
,120
,000
kam
a ili
vyor
ipot
iwa
kati
ka t
aari
fa y
a ut
enda
ji w
a ki
fedh
a ku
toka
na k
utoj
itos
hele
za k
wa
nyar
aka
za
mal
ipo.
8
Wila
ya y
a Si
ha
O
ngez
eko
la k
iasi
cha
Sh.
Tz.
8,15
0,00
0 a
mba
lo l
iingi
zwa
kam
a m
atum
izi
kati
ka v
itab
u vy
a m
ahes
abu
bila
kuw
a na
mae
lezo
Uka
guzi
ulis
hind
wa
kuth
ibit
isha
uha
lali
wa
mat
umiz
i ya
kaw
aida
yen
ye k
iasi
cha
Sh.
Tz.
7,42
0,00
0 ku
toka
na n
a ku
toku
was
ilish
wa
kwa
hati
za
mal
ipo.
Uka
guzi
ulis
hind
wa
kuth
ibit
isha
uha
lali
wa
mat
umiz
i ye
nye
kias
i ch
a Sh
.Tz.
5,1
95,0
00 k
ama
ilivy
orip
otiw
a ka
tia
taar
ifa
ya u
tend
aji
wa
kife
dha
kuto
kana
kut
ojit
oshe
leza
kw
a ny
arak
a za
m
alip
o.
O
ngez
eko
la
kias
i ch
a Sh
. 9,
999,
986
amba
lo
liliin
gizw
a ka
ma
mat
umiz
i ka
tika
vi
tabu
vy
a m
ahes
abu
bila
kuw
a na
mae
lezo
. 9
Wila
ya
ya
Sim
anji
ro
Uka
guzi
ul
ishi
ndw
a ku
thib
itis
ha
uhal
ali
wa
mat
umiz
i ye
nye
kias
i ch
a Sh
.Tz.
8,
075,
000
kam
a ili
vyor
ipot
iwa
kati
a ta
arif
a ya
ute
ndaj
i w
a ki
fedh
a ku
toka
na n
a ku
toji
tosh
elez
a kw
a ny
arak
a za
m
alip
o.
10
W
ilaya
ya
Ko
rogw
e
Ki
asi
cha
Sh.T
z. 1
2,05
3,51
8 ki
licho
ham
ishw
a kw
enda
Hos
pita
li ya
Mag
unga
hak
ijap
okel
ewa
kam
a ili
vyoo
nyes
hwa
kati
ka t
aari
fa z
a fe
dha.
Mad
awa
yeny
e th
aman
i ya
Sh.
Tz.
5,71
6,55
2 ya
liyot
olew
a ku
toka
Sto
o ya
Mad
awa
ya H
alm
asha
uri
haya
japo
kele
wa
na z
ahan
ati h
usik
a ka
ma
ilivo
onye
shw
a kw
enye
taa
rifa
za
fedh
a.
11
Wila
ya
ya
Nka
nsi
M
apat
o ya
ruz
uku
ya m
taji
yal
iyot
umik
a ka
ma
ilivy
oony
eshw
a ka
tika
taa
rifa
ya
uten
daji
wa
fedh
a in
atof
auti
ana
na m
chan
ganu
o ul
ioai
nish
wa
kati
ka j
edw
ali
Na.
41,
hivy
o ku
pele
kea
tofa
uti
ya k
iasi
ch
a Sh
.Tz.
9,1
64,0
00.
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
205
Ki
asi
cha
ruzu
ku
ya
mat
umiz
i ya
ka
wai
da
iliyo
poke
lew
a ki
licho
onye
shw
a ka
tika
ta
arif
a ya
m
tiri
riko
wa
fedh
a ni
Sh.
Tz.
942,
187,
000;
hat
a hi
vyo,
jed
wal
i la
mch
anga
nuo
Na.
11 l
inao
nesh
a ki
asi
cha
ruzu
ku y
a m
atum
izi
ya k
awai
da k
ilich
opok
elew
a kw
a m
wak
a w
a fe
dha
2016
/201
7 ni
Sh
.Tz.
864
,756
,000
. H
ii in
apel
ekea
uto
faut
i wa
kias
i cha
Sh.
Tz.
77,4
31,0
00.
H
ati
za
mal
ipo
za
kias
i ch
a Sh
.Tz.
3,
631,
000
zilik
osek
ana
wak
ati
wa
ukag
uzi
kwa
ajili
ya
ku
haki
kiw
a,
hivy
o uk
aguz
i ul
ishi
ndw
a ku
jiri
dhis
ha
na
uhal
ali
wa
mal
ipo
yaliy
ofan
yika
na
ku
onye
shw
a kw
enye
taa
rifa
ya
hesa
bu z
a fe
dha.
12
W
ilaya
ya
U
kere
we
Kuko
sa
kwa
uhal
ali
wa
kias
i ch
a fe
dha
na
mlin
gani
sho
wa
fedh
a Sh
.Tz.
18
7,68
2,23
5 ki
licho
onye
shw
a kw
enye
taa
rifa
ya
hali
ya f
edha
Hat
i za
mal
ipo
zeny
e ju
mla
ya
Sh.
56,0
00,0
00 z
iliko
seka
na w
akat
i w
a uk
aguz
i kw
a aj
ili y
a ku
haki
kiw
a, h
ivyo
uka
guzi
ulis
hind
wa
kuji
ridh
isha
kuh
usu
uhal
ali
wa
mal
ipo
yaliy
ofan
yika
na
kuon
yesh
wa
kwen
ye t
aari
fa y
a he
sabu
za
fedh
a.
13
Wila
ya
ya
Kwim
ba
Uka
guzi
ulis
hind
wa
kuji
ridh
isha
kuh
usu
uwep
o na
uha
lali
wa
kias
i ch
a fe
dha
na m
linga
nish
o w
a fe
dha
Sh.T
z. 9
7,94
1,50
3 zi
lizor
ipot
iwa
kati
ka t
aari
fa y
a ha
li ya
fed
ha.
14
Wila
ya
ya
Seng
erem
a
Kias
i ch
a fe
dha
na m
linga
nish
o w
a fe
dha
kilic
hori
poti
wa
kati
ka t
aari
fa y
a ha
li ya
fed
ha
Sh.T
z.
364,
734,
426
haki
onye
shi u
halis
ia k
utok
ana
na u
tofa
uti
wa
salio
ishi
a
lililo
onye
shw
a ka
tika
taa
rifa
ya
map
ato
na m
atum
izi n
a sa
lio li
lilok
o ka
tika
aka
unti
ya
Sekt
a ya
Afy
a.
RF
1 W
ilaya
ya
Kigo
ma
M
alip
o ki
asi
cha
Sh.T
z. 1
9,02
1,05
0 ya
nayo
husu
mat
enge
nezo
na
man
unuz
i ya
bid
haa
mba
limba
li ya
liyof
anyw
a m
wak
a w
a fe
dha
2015
/201
6 ya
lijum
uish
wa
kam
a m
atum
izi
ya
mw
aka
wa
fedh
a 20
16/2
017.
Hii
ilisa
babi
sha
mat
umiz
i na
map
ato
ya r
uzuk
u ya
liyoa
hiri
shw
a ku
zidi
kw
a ki
asi c
ha S
h.Tz
.
19,0
21,0
50 m
wak
a w
a fe
dha
2016
/17
pam
oja
na k
utok
uone
shw
a ka
ma
mat
umiz
i na
map
ato
linga
nifu
kw
a m
wak
a w
a fe
dha
2015
/16.
2
Wila
ya y
a Ko
ndoa
U
kagu
zi
wan
gu
ulis
hind
wa
kuth
ibit
isha
uh
alal
i w
a m
alip
o ki
asi
cha
Sh.T
z.
24,0
36,0
17
amba
yo
yalif
anyi
ka k
wa
saba
bu y
a ku
kose
kana
kw
a ny
arak
a za
mal
ipo
kam
a vi
le o
rodh
a ya
mal
ipo,
nya
raka
za
kure
jesh
a m
asur
ufu
na h
ati z
a m
alip
o za
wak
anda
rasi
mba
limba
li.
3 W
ilaya
ya
Nka
si
To
faut
i ya
Sh.
Tz.
532,
926,
010
kwa
mw
aka
wa
fedh
a 20
15/1
6 na
201
6/17
kw
enye
Mal
i, V
ifaa
na
Mit
ambo
kat
i ya
Taa
rifa
ya
Fedh
a (
Sh.
3,87
5,57
7,00
0 kw
a 20
16/1
7 na
Sh.
Tz.
4,41
0,70
6,00
0 kw
a 20
15/1
6) n
a M
chan
anuo
Na.
29
wa
Taar
ifa
za F
edha
(Sh
. 4,
097,
552,
000
kwa
2016
/17
na S
h.Tz
.
4,72
1,65
7,01
0 kw
a 20
15/1
6).
Kadh
ia k
ama
hiyo
hap
o ju
u ili
jito
keza
kw
enye
uch
akav
u w
a M
ali,
Vifa
a na
Mit
ambo
am
bapo
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
206
kulik
uwa
na t
ofau
ti y
a Sh
.Tz.
1,3
56,0
61,5
20 k
wa
mw
aka
wa
fedh
a 20
15/1
6 na
201
6/17
. Ta
arif
a ya
U
tend
aji i
lione
sha
Sh.T
z. 1
,456
,028
,000
kw
a 20
16/1
7 na
Sh.
Tz.
1,30
3,54
1,00
0 kw
a 20
15/1
6 w
akat
i M
chan
ganu
o N
a. 2
9 w
a Ta
arif
a za
Fed
ha k
wen
ye u
chak
avu
ulio
nesh
a Sh
.Tz.
1,2
34,0
53,0
00 k
wa
2016
/17
na S
h.Tz
. 16
9,45
4,48
0 kw
a 20
15/1
6.
H
ali
kadh
alik
a, m
anun
uzi
ya M
ali,
Vif
aa n
a M
itam
bo k
ama
ilivy
oone
shw
a kw
enye
Taa
rifa
ya
Mti
riri
ko w
a Fe
dha
kwa
mw
aka
wa
fedh
a ul
iois
hia
30 J
uni
2017
ni
Sh.T
z. 6
09,9
48,0
00 w
akat
i m
chan
ganu
o N
a.
55
umeo
nesh
a Sh
.Tz.
59
6,05
8,00
0;
hivy
o,
kusa
babi
sha
tofa
uti
ya
Sh.T
z.
13,8
90,0
00.
4
Wila
ya y
a Ki
shap
u U
kagu
zi
wan
gu
ulis
hind
wa
kuth
ibit
isha
uh
alal
i w
a m
alip
o ki
asi
cha
Sh.T
z.
154,
653,
126
amba
yo
yalik
uwa
na n
yara
ka p
ungu
fu z
a m
alip
o.
5 W
ilaya
ya
Kite
to
Oro
dha
ya m
alip
o ki
asi
cha
Sh.T
z. 5
,855
,000
hai
kuw
asili
shw
a kw
a aj
ili y
a uk
aguz
i, h
ivyo
nili
shin
dwa
kuth
ibit
isha
uha
lali
wa
mal
ipo
hayo
kam
a ya
livyo
ones
hwa
kwen
ye t
aari
fa z
a fe
dha.
6
Wila
ya y
a Si
man
jiro
H
ati
za m
alip
o ki
asi
cha
Sh.T
z. 5
1,64
4,24
0 ha
ziku
was
ilish
wa
kwa
ajil
ya u
kagu
zi i
lihal
i m
alip
o ya
Sh
.Tz.
2,8
10,0
00 y
alik
uwa
na n
yara
ka p
ungu
fu z
a m
alip
o.
7 M
ji w
a Ka
ham
a
Mal
ipo
ya S
h.Tz
. 12
9,07
2,98
0 ya
likuw
a na
nya
raka
pun
gufu
, hi
vyo
siku
wez
a ku
jiri
dhis
ha u
hala
li w
a m
alip
o ha
yo.
8 W
ilaya
ya
Nan
yum
bu
U
kagu
zi w
angu
ulis
hind
wa
kuth
ibit
isha
uha
lali
wa
mal
ipo
kias
i cha
Sh.
Tz.
190,
679,
576
amba
yo
yalif
anyi
ka n
a ku
wa
na n
yara
ka p
ungu
fu z
a m
alip
o.
Ku
kata
liwa
kwa
Mza
buni
aliy
ekuw
a na
gha
ram
a nd
ogo
kuto
kana
na
mak
osa
yaliy
ofan
ywa
na
Kam
ati y
a Ta
thm
ini y
azab
uni h
ivyo
kus
abab
isha
has
ara
ya S
h.Tz
. 9,
154,
440.
TASA
F
1 W
ilaya
ya
Buti
ama
U
kagu
zi u
lishi
ndw
a ku
thib
itis
ha u
hala
li w
a ki
asi c
ha m
alip
o ch
a Sh
.Tz.
51,
484,
545
kam
a ili
vyoo
nesh
wa
kati
ka t
aari
fa y
a ut
enda
ji w
a Fe
dha
kwa
saba
bu y
a ku
toku
wap
o kw
a ha
ti z
a m
alip
o zi
nazo
thib
itis
ha
zina
zoth
ibit
isha
uha
lali
wa
mal
ipo
hayo
. 2
Wila
ya y
a
Nga
ra
Mal
ipo
ya S
h.Tz
. 66
,421
,500
hay
akua
mba
tani
shw
a na
nya
raka
zin
azow
eza
kuth
ibit
isha
uha
lali
wa
mal
ipo
yaliy
ofan
yika
hiv
yo il
iwek
a vi
kwaz
o kw
enye
maw
anda
ya
ukag
uzi.
3
Wila
ya y
a U
kere
we
Ta
kwim
u zi
naon
yesh
a Ru
zuku
ya
Dha
man
a ya
fed
ha z
ilizo
ahir
ishw
a (D
iffe
red
Capi
tal
Gra
nt)
kias
i ch
a Sh
.Tz.
972
,379
,004
tan
gu m
wak
a ul
iopi
ta h
aiku
ripo
tiw
a kw
enye
Taa
rifa
za
Fedh
a za
mw
aka
huu.
4
Wila
ya y
a
Mus
oma
Ba
raza
lili
ham
isha
fed
ha z
a m
fuko
wa
TASA
F Sh
.Tz.
21,
254,
908.
36 k
utek
elez
a sh
ughu
li za
TAS
AF
Kwen
ye v
ijij
i 34
. H
ata
hivy
o, h
ii ni
kin
yum
e na
maa
gizo
ya
TASA
F ya
tar
ehe
31 M
achi
, 20
17,
mae
lezo
ya
mat
umiz
i ya
kias
i kili
choh
amis
hwa
haya
kuw
asili
shw
a na
men
ejim
enti
ya
halm
asha
uri k
wa
wak
aguz
i
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
207
ili k
ujir
idhi
sha;
hi
vyo,
hii
ilipe
leke
a ku
kwam
isha
maw
anda
ya
ukag
uzi w
angu
.
WSD
P
1 W
ilaya
ya
Ar
usha
M
alip
o kw
a w
akan
dara
si 5
yam
ezid
ishw
a kw
a Sh
.Tz.
226
,741
,332
hiv
yo k
upel
ekea
has
ara
ya f
edha
za
umm
a.
2 W
ilaya
ya
M
ondu
li
Kulip
wa
mar
a m
bili
kwa
hati
za
mad
ai z
a m
kand
aras
i ki
asi
cha
Sh.T
z. 1
59,0
93,5
00 h
ivyo
kup
elek
ea
hasa
ra y
a fe
dha
za u
mm
a.
3 W
ilaya
ya
N
goro
ngor
o
U
kagu
zi u
lishi
ndw
a ku
jiri
dhis
ha k
wa
kuw
a ki
asi
cha
Sh.T
z. 3
0,67
5,53
4.40
zili
lipw
a bi
la k
uwa
na
viam
bati
sho
vina
vyoo
nyes
ha u
hala
li w
a m
alip
o ha
yo
ilhal
i ya
meo
nesh
wa
kwen
ye t
aari
fa y
a ut
enda
ji
M
atum
izi y
amez
idis
hwa
kwa
Sh.T
z. 4
,208
,970
kat
ika
taar
ifa
ya u
tend
aji w
a fe
dha.
4
Wila
ya
ya
Chem
ba
Hat
i za
mal
ipo
ya S
h.Tz
. 9,
002,
400
zilik
osek
ana
wak
ati
wa
ukag
uzi
kwa
ajili
ya
kuji
ridh
isha
na
mal
ipo
yaliy
ofan
yika
. H
ivyo
uka
guzi
ulis
hind
wa
kuji
ridh
isha
kuh
usu
uhal
ali
wa
mal
ipo
yaliy
ofan
yika
na
am
bayo
yal
ikuw
a ya
meo
nesh
wa
kwen
ye t
aari
fa y
a he
sabu
za
fedh
a.
5 W
ilaya
ya
M
isse
nyi
Fe
dha
za t
ahad
hari
kia
si c
ha S
h.Tz
. 32
,821
,356
haz
ikui
ngiz
wa
kwen
ye a
kaun
ti y
a ba
raba
ra w
ala
kuon
eshw
a kw
enye
taa
rifa
ya
hali
ya f
edha
kam
a de
ni.
Ko
di y
a zu
io k
iasi
cha
Sh.
Tz.
1,25
6,15
5 ili
yoku
sany
wa
laki
ni h
aiku
pele
kwa
Mam
laka
ya
Map
ato
na
wal
a ha
ikuo
nyes
hwa
kam
a de
ni k
atik
a ta
arif
a ya
hal
i ya
fedh
a.
6 W
ilaya
ya
Ka
sulu
Ku
ones
hwa
pung
ufu
kwa
wad
aiw
a ki
asi c
ha S
h.Tz
. 12
,041
,000
kat
ika
taar
ifa
ya h
ali y
a fe
dha.
7 W
ilaya
ya
Hai
U
kagu
zi u
lishi
ndw
a ku
jiri
dhis
ha n
a ki
asi
cha
Sh.T
z. 1
3,25
6,00
0 zi
lizop
wa
bila
kuw
a na
via
mba
tish
o vi
navy
oony
esha
uha
lali
wa
mal
ipo
hayo
am
bayo
yam
eony
eshw
a kw
enye
taa
rifa
ya
uten
daji
8
Wila
ya
ya
Sim
anji
ro
Hat
i za
mal
ipo
ya S
h.Tz
. 25
,020
,749
zili
kose
kana
wak
ati
wa
ukag
uzi
kwa
ajili
ya
kuji
ridh
isha
na
mal
ipo
yaliy
ofan
yika
. H
ivyo
, uk
aguz
i ul
ishi
ndw
a ku
jiri
dhis
ha n
a uh
alal
i w
a m
alip
o ya
liyof
anyi
ka i
lhal
i ya
likuw
a ya
meo
nyes
hwa
kwen
ye t
aari
fa y
a he
sabu
za
fedh
a 9
Wila
ya
ya
Mus
oma
H
ati
za m
alip
o ya
Sh.
Tz.
368,
646,
288.
78 z
iliko
seka
na w
akat
i w
a uk
aguz
i kw
a aj
iri
ya k
ujir
idhi
sha
na
mal
ipo
yaliy
ofan
yika
. H
ivyo
uka
guzi
ulis
hind
wa
kuji
ridh
isha
na
uhal
ali
wa
mal
ipo
yaliy
ofan
yika
na
yalik
uwa
yam
eony
eshw
a kw
enye
taa
rifa
ya
hesa
bu z
a fe
dha.
10
W
ilaya
ya
Rory
a
Uka
guzi
ulis
hind
wa
kuji
ridh
isha
uha
lali
wa
mal
ipo
ya k
iasi
cha
Sh.
Tz.
73,6
22,3
44 z
ilizo
lipw
a kw
a m
shau
ri k
utok
ana
na k
ukos
ekan
a kw
a vi
amba
tish
o vy
a m
atum
izi y
aliy
ofan
ywa.
11
W
ilaya
ya
Nka
si
U
kagu
zi u
lishi
ndw
a ku
jiri
dhis
ha k
uhus
u ki
asi
cha
Sh.T
z. 3
0,06
4,81
7 zi
lizol
ipw
a bi
la k
uwa
na
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
208
viam
bati
sho
vina
vyoo
nyes
ha u
hala
li w
a m
alip
o ha
yo
ilhal
i ya
meo
nesh
wa
kwen
ye t
aari
fa y
a ut
enda
ji
Th
aman
i ya
mal
i vi
faa
na m
itam
bo S
h.Tz
. 2,
714,
746,
000
viliv
yoon
eshw
a ka
tika
taa
rifa
ya
hali
ya
fedh
a in
atof
auti
ana
na j
edw
ali
la m
chan
ganu
o na
29
Sh.T
z. 4
,410
,706
,000
na
kupe
leke
a to
faut
i ya
Sh.
Tz.
1,69
5,96
0,00
0.
U
chak
avu
wa
Sh.T
z. 6
31,6
07,0
00 u
lioon
eshw
a ka
tika
taa
rifa
ya
uten
daji
wa
fedh
a un
atof
auti
ana
na
jedw
ali
la
mch
anga
nuo
na
29
Sh.T
z.
1,30
3,54
1,00
0 hi
vyo
kupe
leke
a to
faut
i w
a Sh
.Tz.
67
1,93
4,00
0.
Ki
asi
kilic
hotu
mik
a ku
nunu
a M
ali,
Vif
aa n
a m
itam
bo k
atik
a m
wak
a w
a fe
dha
2015
/201
6 na
20
16/2
017
kilic
hori
poti
wa
kati
ka t
aari
fa y
a m
tiri
riko
wa
fedh
a ki
nato
faut
ioan
a na
mch
anga
nuo
wak
e ka
ma
iliyo
ones
hwa
kwen
ye j
edw
ali
Na.
55 n
a 29
, hi
vyo
kusa
babi
sha
tofa
uti
ya j
umla
ya
Sh.T
z. 1
57,5
71,2
50
12
Wila
ya
ya
Koro
gwe
Hal
mas
haur
i im
eone
sha
kutu
mw
a kw
a ru
zuku
kia
si c
ha S
Sh.
Tz.
97,9
96,8
61 k
atik
a ta
arif
a ya
m
tiri
riko
wa
fedh
a la
kini
hai
kuon
esha
kat
ika
taar
ifa
ya u
tend
aji w
a fe
dha
Ku
tofa
utia
na k
wa
kias
i cha
fed
ha k
ilich
opok
elew
a ki
licho
onye
shw
a kw
enye
taa
rifa
ya
mti
riri
ko w
a fe
dha
Sh.T
z. 1
50,8
13,1
54 n
a ta
arif
a ya
ute
ndaj
i w
a fe
dha
Sh.T
z. 5
2,88
6,29
3, h
ivyo
, ku
saba
bish
a to
faut
i ya
Sh.T
z. 9
7,92
6,86
1 13
W
ilaya
ya
Siha
M
ali
za m
radi
zili
zoju
mui
shw
a kw
enye
kw
enye
mal
i vi
faa
na m
itam
bo h
azij
awez
a ku
thib
itis
hwa
kuto
kana
na
kuto
kuw
epo
kwa
taar
ifa
zake
kw
enye
rej
ista
ya
mal
i za
kudu
mu.
Mir
adi M
ingi
ne
1
Kitu
o ch
a M
afun
zo K
anda
ya
Kig
oma
(KZT
C)
Kias
i ch
a Sh
.Tz.
1,5
80,4
06,9
45.1
2 (D
K 71
2,20
3) k
iliju
mui
sha
mat
umiz
i ya
nayo
husi
ana
na m
isha
hara
, m
afun
zo n
a gh
aram
a za
zia
da z
ilifa
nyw
a bi
la n
yara
ka z
a ku
tosh
a zi
lizoe
nda
kiny
ume
na m
akub
alia
no
ya S
hiri
ka la
Mis
aada
la K
imar
ekan
i (U
SAID
).
2 Ta
asis
i ya
Afya
ya
Msi
ngi (
PHCI
) Ki
asi
cha
Sh.T
z. 1
2,83
0,48
9.28
na
Sh.T
z. 1
,408
,222
,755
.36
(DK
5,78
2 na
634
,609
) ch
a pe
sa z
a
mat
umiz
i
iliju
mui
shw
a kw
enye
m
atum
izi
yasi
okub
alik
a ku
lipw
a ka
ma
VAT;
na
M
atum
izi
hayo
ha
yaku
amba
tish
wa
na n
yara
ka k
uony
esha
uha
lali
wa
mat
umiz
i.
Hii
ni k
inyu
me
na m
akub
alia
no y
a Sh
irik
a la
Mis
aada
la K
imar
ekan
i (U
SAID
).
3 Pr
ogra
mu
ya
Kita
ifa
ya
Kudh
ibit
i
Kias
i ch
a Sh
. 63
,071
,773
.92
(Dol
a za
kim
arek
ani
28,4
23)
kilij
umlis
hwa
kam
a m
atum
izi
ya m
radi
ya
nayo
toka
na n
a m
akat
o ya
VAT
am
bayo
yan
atak
iwa
kure
jesh
wa
kwen
ye m
radi
na
hii i
liend
a ki
nyum
e na
mak
ubal
iano
yal
iyoi
ngiw
a na
Shi
rika
la m
isaa
da la
kim
arek
ani (
USA
ID).
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
209
Mal
aria
(N
MCP
) 4
Kitu
o ch
a M
aend
eleo
ya
Elim
u ya
Afy
a Ar
usha
(CE
DH
A)
Kias
i ch
a Sh
.Tz.
2,5
78,5
24.4
8 na
Sh.
Tz.
698,
773,
476.
96 (
DK1
,162
na
314,
899)
pes
a za
M
atum
izi
zilij
umui
shw
a kw
enye
m
atum
izi
yasi
okub
alik
a ku
lipw
a ka
ma
VAT
na
Mat
umiz
i ha
yo
haya
kuam
bata
nish
wa
na n
yara
ka k
uony
esha
uha
lali
wa
mat
umiz
i h
ii ni
kin
yum
e na
mak
ubal
iano
ya
Shir
ika
la m
isaa
da la
kim
arek
ani (
USA
ID).
WSD
P-A
DV
ERSE
O
PIN
ION
1 W
ilaya
ya
M
aket
e
U
kagu
zi
ulis
hind
wa
kuji
ridh
isha
ku
husu
uh
alal
i w
a m
alip
o ya
ju
mla
ya
Sh
.Tz.
20
,598
,160
ya
liyon
yesh
wa
kati
ka t
aari
fa z
a fe
dha
kuto
kana
na
kuko
seka
na k
wa
viam
bata
nish
o vy
a m
atum
izi
yaliy
ofan
ywa.
Ruzu
ku y
a m
taji
ya
Sh.T
z. 2
24,8
26,5
80 i
liyop
okel
ewa
kati
ka m
wak
a hu
u ha
ikur
ipot
iwa
kati
ka
taar
ifa
za f
edha
.
Ruzu
ku
ya
mta
ji
iliyo
ones
hwa
kwen
ye
taar
ifa
ya
hali
ya
fedh
a in
a up
ungu
fu
wa
Sh.T
z.
2,85
0,10
3,32
8
Wad
ai w
a ju
mla
ya
Sh.T
z. 5
0,53
9,41
9 w
alio
ripo
tiw
a ka
tika
taa
rifa
ya
hali
ya f
edha
ya
mw
aka
wa
fedh
a 20
15/2
016
imep
elek
ea u
pung
ufu
kati
ka s
alio
anz
ia l
a w
adai
kat
ika
taar
ifa
ya h
ali
ya f
edha
ya
mw
aka
wa
fedh
a 20
16/2
017
kwa
kias
i saw
a.
Kiam
bati
sho
Na
5: U
tend
aji w
a Ki
fedh
a w
a M
irad
i ya
Mae
ndel
eo
Ute
ndaj
i wa
Kife
dha
wa
Pro
gram
u ya
Mae
ndel
eo y
a Se
kta
ya K
ilim
o –
(Kia
si S
h.Tz
.)
Na.
M
koa
H
alm
asha
uri
Salio
anz
ia
Fedh
a ili
yopo
kele
wa
Jum
la y
a Fe
dha
iliyo
kuw
epo
Mat
umiz
i Sa
lio Is
hia
1 AR
USH
A W
ilaya
ya
Arus
ha
1,55
8,00
0,00
0 -
1,55
8,00
0,00
0 1,
558,
000,
000
-
Wila
ya y
a 5,
594,
137
- 5,
594,
137
- 5,
594,
137
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
210
Mer
u
Wila
ya y
a Ka
ratu
12
1,72
9,00
9 -
121,
729,
009
75,2
00,0
00
46,5
29,0
09
2 CO
AST
-
- -
- -
Wila
ya y
a Ba
gam
oyo
86
8,00
0,65
3 -
868,
000,
653
860,
074,
653
7,92
6,00
0
Mji
wa
Kiba
ha
709,
100
- 70
9,10
0 -
709,
100
Wila
ya y
a Ru
fiji
37
0,66
8,88
1 4,
500,
000
375,
168,
881
362,
500,
000
12,6
68,8
81
3 IR
ING
A
- -
- -
-
W
ilaya
ya
Muf
indi
-
- -
- -
Wila
ya y
a Ki
lolo
-
- -
- -
Man
ispa
a ya
Ir
inga
9,
866,
300
- 9,
866,
300
9,86
6,30
0 -
Wila
ya y
a Ir
inga
1,
093,
582,
049
265,
393,
671
1,35
8,97
5,72
0 1,
014,
090,
849
344,
884,
871
4 KI
LIM
ANJ
ARO
- -
- -
-
Wila
ya y
a H
ai
855,
072,
242
- 85
5,07
2,24
2 63
6,13
8,82
8 21
8,93
3,41
4 5
LIN
DI
-
- -
- -
Wila
ya y
a Ki
lwa
39
,455
,803
-
39,4
55,8
03
34,3
60,0
00
5,09
5,80
3
Wila
ya y
a Ru
angw
a 40
6,33
4,89
1 -
406,
334,
891
404,
000,
000
2,33
4,89
1
6 M
ANYA
RA
-
- -
- -
Wila
ya y
a 14
0,24
8,27
4 12
,429
,990
15
2,67
8,26
4 15
2,67
8,26
4 -
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
211
Kite
to
Wila
ya y
a M
bulu
-
- -
- -
Wila
ya y
a Ba
bati
-
39,2
65,0
00
39,2
65,0
00
39,2
65,0
00
-
Wila
ya y
a H
anan
g'
- 30
,685
,000
30
,685
,000
30
,685
,000
-
Wila
ya y
a Si
man
jiro
1,
903,
532,
000
- 1,
903,
532,
000
6,10
2,00
0 1,
897,
430,
000
Mji
wa
Baba
ti
9,53
9,50
1 55
,820
,155
65
,359
,656
65
,359
,656
-
7 M
BEYA
- -
- -
-
Ji
ji la
Mbe
ya
35,4
38,0
00
- 35
,438
,000
-
35,4
38,0
00
Wila
ya y
a M
beya
25
0,00
0,00
0 -
250,
000,
000
35,5
99,5
80
214,
400,
420
Wila
ya y
a Ky
ela
-
- -
- -
Wila
ya y
a Ru
ngw
e
- -
- -
-
Wila
ya y
a M
bara
li
- -
- -
-
Wila
ya y
a Ch
unya
94
,945
,851
-
94,9
45,8
51
88,7
18,8
51
6,22
7,00
0
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
50,8
90,6
48
- 50
,890
,648
22
,197
,317
28
,693
,331
8 SO
NG
WE
-
- -
- -
Wila
ya y
a M
bozi
-
- -
- -
Wila
ya y
a Ile
je
150,
000,
000
- 15
0,00
0,00
0 63
,593
,645
86
,406
,355
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
212
Wila
ya y
a M
omba
1,
060,
058,
171
4,89
7,12
0 1,
064,
955,
291
332,
389,
517
732,
565,
774
Wila
ya y
a So
ngw
e
- -
- -
-
9 M
ORO
GO
RO
- -
- -
-
Wila
ya y
a Ki
losa
68
0,14
1,15
8 -
680,
141,
158
680,
141,
158
-
Wila
ya y
a M
orog
oro
1,
009,
000,
000
27,1
26,0
00
1,03
6,12
6,00
0 1,
036,
126,
000
-
Wila
ya y
a U
lang
a
680,
415,
000
4,71
2,00
0 68
5,12
7,00
0 13
7,86
2,00
0 54
7,26
5,00
0
10
MW
ANZA
- -
- -
-
W
ilaya
ya
Mag
u
25,3
05,8
34
- 25
,305
,834
-
25,3
05,8
34
Jiji
la
Mw
anza
9,
300,
927
- 9,
300,
927
- 9,
300,
927
11
RUKW
A
- -
- -
-
W
ilaya
ya
Sum
baw
anga
(1
2,30
0,25
6)
18,7
60,5
00
6,46
0,24
4 11
,116
,570
(4
,656
,326
)
Man
ispa
a ya
Su
mba
wan
ga
1,03
8,12
0 -
1,03
8,12
0 -
1,03
8,12
0
Wila
ya y
a N
kasi
1,
093,
000
- 1,
093,
000
- 1,
093,
000
Wila
ya y
a Ka
lam
bo
- -
- -
-
12
RUVU
MA
-
- -
- -
Wila
ya y
a Tu
ndur
u
- -
- -
-
Wila
ya y
a 11
6,20
0 -
116,
200
- 11
6,20
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
213
Mbi
nga
W
ilaya
ya
Nam
tum
bo
413,
000,
000
- 41
3,00
0,00
0 22
4,79
0,10
1 18
8,20
9,89
9
Wila
ya y
a So
ngea
28
8,14
2,28
6 68
4,41
3,48
7 97
2,55
5,77
3 96
0,41
4,25
4 12
,141
,519
Man
ispa
a ya
So
ngea
-
- -
- -
Wila
ya y
a N
yasa
22
2,12
7.20
-
222,
127.
20
- 22
2,12
7.20
13
TAN
GA
-
- -
- -
Jiji
la T
anga
48
7,68
1 -
487,
681
480,
000
7,68
1
M
ji w
a Ko
rogw
e
285,
000,
000
- 28
5,00
0,00
0 14
0,14
8,60
0 14
4,85
1,40
0
14
GEI
TA
-
- -
- -
Wila
ya y
a G
eita
4,
795,
000
- 4,
795,
000
4,79
5,00
0 -
15
SIM
IYU
- -
- -
-
W
ilaya
ya
Bari
adi
919,
221,
000
- 91
9,22
1,00
0 18
5,07
7,60
0 73
4,14
3,40
0
Wila
ya y
a M
asw
a
- -
- -
-
Wila
ya y
a M
eatu
-
- -
- -
Wila
ya y
a It
ilim
a
73,4
75
- 73
,475
-
73,4
75
15
KATA
VI
-
- -
- -
Wila
ya y
a M
pand
a
13,0
11,2
25
- 13
,011
,225
4,
477,
225
8,53
4,00
0
Wila
ya y
a 3,
740,
297
- 3,
740,
297
- 3,
740,
297
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
214
Nsi
mbo
W
ilaya
ya
Mle
le
1,02
3,32
0 -
1,02
3,32
0 1,
023,
320
-
Man
ispa
a ya
M
pand
a
1,89
5,87
7 -
1,89
5,87
7 -
1,89
5,87
7
Jum
la
13,3
48,3
87,7
81.2
0 1,
148,
002,
9 23
14,4
96,3
90,7
04.2 0
9,17
7,27
1,28
8 5,
319,
119,
416.
20
Ute
ndaj
i wa
Kife
dha
wa
Mfu
ko w
a A
fya
(Kia
si S
h.Tz
.)
Na.
M
koa
Hal
mas
haur
i Sa
lio a
nzia
Fe
dha
iliyo
poke
lew
a Ju
mla
ya
Fedh
a ili
yoku
wep
o M
atum
izi
Salio
Ishi
a
1 AR
USH
A W
ilaya
ya
Arus
ha
155,
483,
595
650,
414,
000
805,
897,
595
705,
843,
359.
75
100,
054,
235.
25
Jiji
la
Arus
ha
89,0
40,2
23
798,
774,
000
887,
814,
223
887,
272,
126
542,
097
Wila
ya y
a M
ondu
li
64,2
70,5
21
505,
995,
000
570,
265,
521
530,
772,
483
39,4
93,0
38
Wila
ya y
a Lo
ngid
o
22,7
95,8
05.9
3 43
6,36
4,00
0 45
9,15
9,80
5.93
41
9,17
3,00
0 39
,986
,805
.93
Wila
ya y
a M
eru
12
5,79
9,90
6 54
6,56
4,00
0 67
2,36
3,90
6 63
2,42
4,77
6.37
39
,939
,129
.63
Wila
ya y
a Ka
ratu
10
9,64
5,12
4 53
0,98
4,00
0 64
0,62
9,12
4 59
3,83
3,67
3 46
,795
,451
Wila
ya y
a N
goro
ngor
o
74,1
93,7
73.9
2 61
7,52
0,00
0 69
1,71
3,77
3.92
66
6,08
6,42
0 25
,627
,353
.92
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
215
2 M
ANYA
RA
-
Wila
ya y
a Ki
teto
21
,675
,389
85
1,35
0,29
5 87
3,02
5,68
4 83
3,97
3,38
7 39
,052
,297
Wila
ya y
a M
bulu
26
,976
,930
46
1,99
9,00
0 48
8,97
5,93
0 39
1,48
5,09
6 97
,490
,834
Wila
ya y
a Ba
bati
14
6,19
6,72
3 76
4,23
4,00
0 91
0,43
0,72
3 90
6,35
7,46
8 4,
073,
255
Wila
ya y
a H
anan
g
52,2
26,3
90
640,
543,
000
692,
769,
390
634,
923,
687
57,8
45,7
03
Wila
ya y
a Si
man
jiro
16
2,46
6,54
2.72
64
5,18
7,00
0 80
7,65
3,54
2.65
76
3,46
6,33
4.82
44
,187
,207
.83
Mji
wa
Mbu
lu
- 26
8,93
8,00
0 26
8,93
8,00
0 26
0,95
8,52
9.99
7,
979,
470.
01
Mji
wa
Baba
ti
46,6
81,5
27
193,
940,
000
240,
621,
527
240,
465,
285
156,
242
3 KI
LIM
ANJA
RO
-
Wila
ya y
a M
oshi
15
2,09
8,01
4 90
2,82
2,40
0 1,
054,
920,
414
1,03
5,20
9,83
8 19
,710
,576
Wila
ya y
a Ro
mbo
17
1,46
8,45
5 51
7,98
4,00
0 68
9,45
2,45
5 47
1,78
5,16
7 21
7,66
7,28
8
Wila
ya y
a H
ai
227,
757,
480
409,
583,
000
637,
340,
480
486,
236,
090.
31
151,
104,
389.
69
Wila
ya y
a Sa
me
18
9,98
0,54
7 67
2,60
3,00
0 86
2,58
3,54
7 74
7,68
9,98
1 11
4,89
3,56
6
Man
ispa
a ya
Mos
hi
52,8
87,3
60
337,
124,
000
390,
011,
360
373,
683,
681.
91
16,3
27,6
78.0
9
Wila
ya y
a M
wan
ga
56,5
10,6
68.8
6 29
2,68
7,00
0 34
9,19
7,66
8.86
33
6,69
7,62
7 12
,500
,041
.86
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
216
Wila
ya y
a Si
ha
23,0
34,5
29.0
4 24
7,24
0,00
0 27
0,27
4,52
9.04
26
0,19
0,74
4.20
10
,083
,784
.84
4 TA
NG
A
-
W
ilaya
ya
Han
deni
19
8,45
3,15
4 70
4,66
0,00
0 90
3,11
3,15
4 87
4,63
9,64
1 28
,473
,513
Wila
ya y
a M
king
a 80
,111
,961
29
8,56
0,00
0 37
8,67
1,96
1 33
8,05
8,76
2 40
,613
,199
Wila
ya y
a Ki
lindi
58
,581
,311
65
2,22
8,38
8 71
0,80
9,69
9 59
6,37
2,15
3 11
4,43
7,54
6
Jiji
la
Tang
a
81,8
07,2
79
525,
180,
000
606,
987,
279
569,
910,
185
37,0
77,0
94
Wila
ya y
a Pa
ngan
i 30
,810
,186
.64
151,
636,
000
182,
446,
186.
64
164,
186,
416
18,2
59,7
70.6
4
Wila
ya y
a Ko
rogw
e
63,1
57,2
97.5
8 54
3,33
5,00
0 60
6,49
2,29
7.58
46
4,93
7,89
7 14
1,55
4,40
0.58
Wila
ya y
a M
uhez
a
41,8
28,1
68
423,
761,
000
465,
589,
168
421,
095,
390
44,4
93,7
78
Wila
ya y
a Lu
shot
o
85,4
67,6
00
713,
400,
000
798,
867,
600
798,
867,
599
-
Mji
wa
Koro
gwe
18
,875
,179
.52
133,
457,
000
152,
332,
179.
52
144,
446,
435
7,88
5,74
4.52
Wila
ya y
a Bu
mbu
li
36,9
97,8
18.5
4 32
1,13
3,00
0 35
8,13
0,81
8.54
35
7,87
2,38
7 25
8,43
1.54
Mji
wa
Han
deni
21
,621
,789
17
1,27
1,00
0 19
2,89
2,78
9 16
8,64
6,35
1 24
,246
,438
5 DA
R
-
M
anis
paa
ya
Tem
eke
423,
793,
414
2,73
2,23
1,00
0 3,
156,
024,
414
3,07
4,25
3,60
4 81
,770
,810
Man
ispa
a 67
0,66
3,25
7.20
3,
595,
370,
931
4,26
6,03
4,18
8.20
4,
240,
894,
022
25,1
40,1
66.2
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
217
ya
Kino
ndon
i
M
anis
paa
ya Il
ala
22
9,51
9,70
3 2,
427,
978,
000
2,65
7,49
7,70
3 2,
574,
370,
065
83,1
27,6
38
6 LI
NDI
-
W
ilaya
ya
Kilw
a
141,
649,
157
641,
311,
000
782,
960,
157
761,
543,
397
21,4
16,7
60
Wila
ya y
a Li
wal
e
43,3
91,8
93
307,
230,
000
350,
621,
893
305,
824,
652
44,7
97,2
41
Wila
ya y
a Li
ndi
69,1
00,8
67
532,
184,
000
601,
284,
867
586,
681,
118
14,6
03,7
49
Wila
ya y
a Ru
angw
a 17
1,56
3,49
1 31
5,04
4,00
0 48
6,60
7,49
1 36
8,78
9,94
6 11
7,81
7,54
5
Man
ispa
a ya
Lin
di
900,
000
169,
456,
000
170,
356,
000
163,
474,
738
6,88
1,26
2
Wila
ya y
a N
achi
ngw
ea
142,
117,
995
503,
277,
000
645,
394,
995
626,
952,
000
18,4
42,9
95
7 M
ORO
GO
RO
-
Wila
ya y
a Ki
lom
bero
49
6,66
0,36
8 87
2,68
8,00
0 1,
369,
348,
368
1,34
9,13
9,61
9 20
,208
,749
Wila
ya y
a Ki
losa
38
1,23
8,07
4 1,
202,
662,
000
1,58
3,90
0,07
4 1,
243,
451,
437
340,
448,
637
Wila
ya y
a M
vom
ero
12
0,87
8,93
1 80
5,51
2,00
0 92
6,39
0,93
1 88
8,15
1,54
3 38
,239
,388
Wila
ya y
a M
orog
oro
25
6,30
6,17
0 92
4,63
3,00
0 1,
180,
939,
170
940,
498,
348
240,
440,
822
Man
ispa
a ya
M
orog
oro
162,
359,
785.
39
598,
310,
000
760,
669,
785.
39
758,
455,
820
2,21
3,96
5.39
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
218
Wila
ya y
a U
lang
a
130,
773,
441
476,
347,
000
607,
120,
441
519,
887,
998
87,2
32,4
43
Mji
wa
Ifak
ara
-
322,
782,
000
322,
782,
000
322,
782,
000
-
Wila
ya y
a M
alin
yi
- 47
2,07
5,00
0 47
2,07
5,00
0 44
3,10
2,86
1 28
,972
,139
Wila
ya y
a G
airo
12
1,98
7,96
9 47
9,30
5,00
0 60
1,29
2,96
9 52
3,95
7,49
2 77
,335
,477
8 M
TWAR
A
-
-
Man
ispa
a ya
Mtw
ara
42,5
94,0
00
196,
997,
000
239,
591,
000
237,
305,
456
2,28
5,54
4
Mji
wa
Mas
asi
150,
884,
455
204,
564,
000
355,
448,
455
313,
166,
944
42,2
81,5
11
Wila
ya y
a M
asas
i 8,
987,
873.
50
579,
863,
000
588,
850,
873.
50
555,
262,
174
33,5
88,6
99.5
0
Wila
ya y
a M
twar
a
252,
596,
215
291,
550,
000
544,
146,
215
411,
619,
497
132,
526,
718
Mji
wa
Nan
yam
ba
- 24
1,83
2,00
0 24
1,83
2,00
0 21
0,02
8,53
7 31
,803
,463
Wila
ya y
a Ta
ndah
imba
169,
885,
184
484,
556,
000
654,
441,
184
531,
708,
311
122,
732,
873
Wila
ya y
a N
anyu
mbu
84
,998
,946
.52
433,
430,
980
518,
429,
926.
52
515,
555,
188
2,87
4,73
8.52
Mji
wa
New
ala
-
111,
619,
000
111,
619,
000
111,
506,
164
112,
836
Wila
ya y
a N
ewal
a
59,1
00,0
38
323,
870,
000
382,
970,
038
375,
252,
666
7,71
7,37
2
9 CO
AST
-
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
219
Wila
ya y
a Ki
sara
we
36
,805
,041
.93
344,
228,
000
381,
033,
041.
93
354,
766,
327
26,2
66,7
14.9
3
Wila
ya y
a Ki
baha
37
,501
,049
18
0,35
3,00
0 21
7,85
4,04
9 20
4,52
2,26
8.82
13
,331
,780
.18
Wila
ya y
a M
afia
26
,321
,207
10
9,07
0,00
0 13
5,39
1,20
7 12
5,98
4,88
2.70
9,
406,
324.
30
Wila
ya y
a Ba
gam
oyo
22
0,57
4,56
9 20
2,22
0,00
0 42
2,79
4,56
9 40
9,04
4,35
1 13
,750
,218
Wila
ya y
a M
kura
nga
94
,646
,568
.43
516,
009,
000
610,
655,
568.
43
539,
904,
713
70,7
50,8
55.4
3
Wila
ya y
a Ru
fiji
29
4,13
6,92
2.76
33
5,62
5,00
0 62
9,76
1,92
2.76
48
7,05
4,56
3 14
2,70
7,35
9.76
Wila
ya y
a Ch
alin
ze
- 65
0,89
2,00
0 65
0,89
2,00
0 63
8,51
0,74
0 12
,381
,260
Mji
wa
Kiba
ha
67,2
37,6
61
258,
574,
000
325,
811,
661
295,
409,
093
30,4
02,5
68
Wila
ya y
a Ki
biti
-
350,
933,
000
350,
933,
000
339,
831,
850
11,1
01,1
50
10
KIG
OM
A
-
1
Wila
ya y
a Bu
higw
e
4,53
1,90
5 54
6,49
2,90
0 55
1,02
4,80
5 54
6,57
9,72
0 4,
445,
085
2
Man
ispa
a ya
Kig
oma
27
,479
,910
40
5,91
0,00
0 43
3,38
9,91
0 40
2,37
4,33
1 31
,015
,579
3
Wila
ya y
a Ki
gom
a
108,
232,
432
446,
141,
000
554,
373,
432
474,
317,
432
80,0
56,0
00
4
Wila
ya y
a Ki
bond
o 23
0,45
9,42
1.50
90
7,18
6,00
0 1,
137,
645,
421.
50
928,
525,
804
209,
119,
617.
50
5
Wila
ya y
a Ka
sulu
18
4,06
5,00
0 1,
050,
931,
000
1,23
4,99
6,00
0 1,
198,
483,
000
36,5
13,0
00
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
220
6
Mji
wa
Kasu
lu
- 41
6,29
3,00
0 41
6,29
3,00
0 39
5,26
1,76
7 21
,031
,233
7
Wila
ya y
a Ka
konk
o
92,1
80,4
60
395,
394,
000
487,
574,
460
420,
186,
851
67,3
87,6
09
8
Wila
ya y
a U
vinz
a
199,
048,
000
1,05
1,12
4,00
0 1,
250,
172,
000
1,08
9,57
0,00
0 16
0,60
2,00
0
11
SIN
GID
A
-
W
ilaya
ya
Iram
ba
61,4
99,4
33.3
2 58
7,53
1,00
0 64
9,03
0,43
3.32
62
5,48
0,52
6 23
,549
,907
.32
Wila
ya y
a M
kala
ma
44
,240
,259
45
5,79
4,00
0 50
0,03
4,25
9 45
0,75
3,84
0.76
49
,280
,418
.24
Wila
ya y
a M
anyo
ni
176,
364,
127
696,
396,
000
872,
760,
127
872,
427,
704
332,
423
Man
ispa
a ya
Sin
gida
81
,941
,474
.50
301,
482,
000
383,
423,
474.
50
380,
128,
641
3,29
4,83
3.50
Wila
ya y
a Si
ngid
a
6,98
3,73
1.80
50
5,87
1,00
0 51
2,85
4,73
1.80
50
9,89
9,55
3 2,
955,
178.
80
Wila
ya y
a It
igi
- 38
9,96
9,64
7 38
9,96
9,64
7 38
9,96
5,12
4 4,
523
Wila
ya y
a Ik
ungi
8,
265,
060
785,
973,
000
794,
238,
060
679,
868,
466.
05
114,
369,
593.
95
12
TABO
RA
-
Wila
ya y
a Ka
liua
18
6,68
7,73
9 1,
245,
386,
000
1,43
2,07
3,73
9 1,
369,
987,
468.
78
62,0
86,2
70.2
2
Wila
ya y
a U
ram
bo
181,
667,
432
547,
553,
000
729,
220,
432
706,
671,
169.
16
22,5
49,2
62.8
4
Wila
ya y
a Ig
unga
30
0,68
3,46
5 1,
013,
853,
000
1,31
4,53
6,46
5 1,
216,
223,
587
98,3
12,8
78
Man
ispa
a ya
Tab
ora
13
7,58
0,48
9 47
7,22
5,00
0 61
4,80
5,48
9 52
4,98
0,31
7.72
89
,825
,171
.28
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
221
Wila
ya y
a Si
kong
e
214,
382,
013.
20
661,
404,
000
875,
786,
013.
20
831,
300,
992
44,4
85,0
21.2
0
Wila
ya y
a N
zega
52
2,89
5,06
2 1,
107,
877,
000
1,63
0,77
2,06
2 1,
547,
264,
406.
80
83,5
07,6
55.2
0
Wila
ya y
a Ta
bora
25
2,63
8,00
0 1,
150,
560,
000
1,40
3,19
8,00
0 1,
323,
564,
000
79,6
34,0
00
Mji
wa
Nze
ga
81,3
90,4
45
130,
859,
000
212,
249,
445
175,
412,
962
36,8
36,4
83
13
DODO
MA
-
Wila
ya y
a M
pwap
wa
54,3
74,8
32
800,
907,
000
855,
281,
832
853,
313,
750
1,96
8,08
2
Wila
ya y
a Ba
hi
19,0
79,4
43
588,
227,
000
607,
306,
443
607,
306,
413
30
Wila
ya y
a Ch
amw
ino
96
,279
,671
90
0,66
2,00
0 99
6,94
1,67
1 93
0,72
7,82
5 66
,213
,846
Wila
ya y
a Ch
emba
30
,255
,263
66
3,45
4,00
0 69
3,70
9,26
3 69
3,60
7,48
3 10
1,78
0
Man
ispa
a ya
Do
dom
a
230,
213,
387
834,
556,
000
1,06
4,76
9,38
7 95
6,55
4,91
0 10
8,21
4,47
7
Wila
ya y
a Ko
ndoa
14
1,14
6,70
0 53
7,57
4,00
0 67
8,72
0,70
0 65
9,29
8,30
8 19
,422
,392
Wila
ya y
a Ko
ngw
a
161,
691,
319
708,
334,
000
870,
025,
319
869,
105,
374
919,
945
Mji
wa
Kond
oa
- 14
3,00
6,00
0 14
3,00
6,00
0 14
1,46
2,55
4 1,
543,
446
14
MAR
A
- -
- -
-
M
anis
paa
ya
Mus
oma
35,2
07,8
68.3
4 25
3,94
7,00
0 28
9,15
4,86
8.34
28
6,07
0,69
3 3,
084,
175.
34
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
222
Wila
ya y
a Ro
rya
209,
456,
337
591,
249,
000
800,
705,
337
620,
599,
113
180,
106,
224
Wila
ya y
a Bu
nda
18
3,99
7,49
5 53
1,87
6,00
0 71
5,87
3,49
5 71
5,39
8,61
7.70
47
4,87
7.30
Wila
ya y
a Ta
rim
e
248,
292,
580.
45
544,
373,
000
792,
665,
580.
45
605,
021,
847.
80
187,
643,
732.
65
Mji
wa
Tari
me
43
,712
,947
17
1,03
0,00
0 21
4,74
2,94
7 21
4,74
2,94
7 -
Wila
ya y
a Se
reng
eti
32,8
27,3
80.4
5 82
6,41
1,00
0 85
9,23
8,38
0.45
74
2,78
2,89
4.20
11
6,45
5,48
6.25
Wila
ya y
a M
usom
a
39,1
99,5
58.6
5 38
9,51
9,00
0 42
8,71
8,55
8.65
40
6,28
3,24
8 22
,435
,310
.65
Wila
ya y
a Bu
tiam
a
39,6
05,3
84
548,
861,
00
588,
466,
384
548,
643,
374
39,8
23,0
10
15
MW
ANZ
A
-
Wila
ya y
a Se
nger
ema
604,
460,
249
792,
506,
000
1,39
6,96
6,24
9 87
6,58
1,08
6 52
0,38
5,16
3
Wila
ya y
a U
kere
we
19
6,76
2,76
8 72
7,41
1,00
0 92
4,17
3,76
8 70
9,38
2,15
7 21
4,79
1,61
1
Wila
ya y
a Kw
imba
22
0,72
8,09
4 93
0,05
7,00
0 1,
150,
785,
094
1,05
2,84
3,59
1 97
,941
,503
Ilem
ela
20,2
22,8
56
665,
616,
000
685,
838,
856
599,
891,
359
85,9
47,4
97
Wila
ya y
a M
isun
gwi
236,
392,
927
797,
577,
000
1,03
3,96
9,92
7 1,
002,
411,
822
31,5
58,1
05
Wila
ya y
a Bu
chos
a
- 66
1,63
0,00
0 66
1,63
0,00
0 64
4,96
2,00
0 16
,668
,000
Wila
ya y
a M
agu
80
,078
,756
66
0,46
6,00
0 74
0,54
4,75
6 64
2,32
5,70
3 98
,219
,053
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
223
Jiji
la
Mw
anza
30
7,96
8,00
4 75
2,75
9,00
0 1,
060,
727,
004
995,
119,
090
65,6
07,9
14
16
SHIN
YAN
GA
-
Mji
wa
Kaha
ma
19
3,12
2,10
0.06
48
6,34
8,00
0 67
9,47
0,10
0.06
59
1,75
3,81
2 87
,716
,288
.06
Wila
ya y
a U
shet
u
173,
250,
830
663,
157,
000
836,
407,
830
804,
317,
830
32,0
90,0
00
Wila
ya y
a Ki
shap
u 28
1,97
0,27
0.46
65
4,72
6,26
2 93
6,69
6,53
2.46
77
7,18
3,72
8.94
15
9,51
2,80
3.52
Wila
ya y
a M
sala
la
129,
153,
470
553,
318,
000
682,
471,
470
611,
825,
038.
47
70,6
46,4
31.5
3
Wila
ya y
a Sh
inya
nga
28
7,19
7,27
4 75
4,96
1,00
0 1,
042,
158,
274
766,
363,
253.
22
275,
795,
020.
78
Man
ispa
a ya
Sh
inya
nga
113,
111,
755
313,
769,
000
426,
880,
755
362,
185,
684
64,6
95,0
71
17
GEI
TA
-
Wila
ya y
a G
eita
31
6,22
7,00
0 1,
413,
716,
000
1,72
9,94
3,00
0 1,
493,
872,
000
236,
071,
000
Mji
wa
Gei
ta
20,0
74,3
62
335,
396,
000
355,
470,
362
355,
070,
964.
75
399,
397.
25
Wila
ya y
a Ch
ato
32
,582
,264
82
8,47
7,00
0 86
1,05
9,26
4 83
4,07
7,71
2 26
,981
,552
Wila
ya y
a Bu
kom
be
76,3
59,0
02
682,
879,
000
759,
238,
002
729,
167,
268.
86
30,0
70,7
33.1
4
Wila
ya y
a N
yang
’hw
ale
55,0
31,0
30
346,
988,
000
402,
019,
030
377,
011,
000
25,0
08,0
30
Wila
ya y
a M
bogw
e
- 45
3,38
5,00
0 45
3,38
5,00
0 41
9,17
7,87
4.39
34
,207
,125
.61
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
224
18
SIM
IYU
-
W
ilaya
ya
Bari
adi
214,
891,
258
654,
659,
000
869,
550,
258
672,
565,
175.
66
196,
985,
082.
34
Mji
wa
Bari
adi
82,1
44,5
14
304,
847,
000
386,
991,
514
319,
139,
513
67,8
52,0
01
Wila
ya y
a M
asw
a
151,
527,
880
770,
380,
000
921,
907,
880
855,
950,
889
65,9
56,9
91
Wila
ya y
a M
eatu
24
,669
,481
.95
840,
592,
000
865,
261,
481.
95
851,
741,
403.
70
13,5
20,0
78.2
5
Wila
ya y
a Bu
sega
49
,870
,905
43
6,39
3,00
0 48
6,26
3,90
5 42
7,02
9,34
3 59
,234
,562
Wila
ya y
a It
ilim
a
190,
987,
054
741,
942,
000
932,
929,
054
849,
496,
608.
74
83,4
32,4
45.2
6
19
KAG
ERA
Wila
ya y
a Bu
koba
51
,909
,674
.16
653,
278,
000
705,
187,
674.
16
625,
665,
448.
14
79,5
22,2
26.0
2
Wila
ya y
a M
uleb
a
125,
662,
849
1,22
1,72
6,00
0 1,
347,
388,
849
1,32
0,81
0,39
9 26
,578
,450
Wila
ya y
a Ka
ragw
e
36,2
19,8
13.3
8 83
7,42
4,00
0 87
3,64
3,81
3.38
85
7,02
2,78
5.14
16
,621
,028
.24
Wila
ya y
a M
isse
nvi
502,
090,
000
502,
090,
000
1,00
4,18
0,00
0 50
2,30
7,93
1 50
1,87
2,06
9
Wila
ya y
a N
gara
32
,788
,573
75
9,30
6,00
0 79
2,09
4,57
3 76
7,62
2,30
5 24
,472
,268
Wila
ya y
a Bi
hara
mul
o
33,0
51,5
55
887,
694,
000
920,
745,
555
885,
701,
251.
80
35,0
44,3
03.2
0
Man
ispa
a ya
Buk
oba
48
,029
,840
.15
251,
587,
000
299,
616,
840.
15
263,
378,
544
36,2
38,2
96.1
5
Wila
ya y
a 14
,031
,878
74
0,02
7,00
0 75
4,05
8,87
8 75
4,03
7,47
3 21
,405
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
225
Kyer
wa
20
IR
ING
A
-
Wila
ya y
a M
ufin
di
112,
157,
572
718,
714,
000
830,
871,
572
744,
421,
154
86,4
50,4
18
Mji
wa
Maf
inga
34
,039
,700
10
8,63
5,00
0 14
2,67
4,70
0 13
5,76
5,19
7 6,
909,
503
Wila
ya y
a Ki
lolo
10
9,83
1,12
5.11
67
9,49
5,00
0 78
9,32
6,12
5.11
75
8,16
2,97
0 31
,163
,155
.11
Man
ispa
a ya
Iri
nga
11
,039
,026
27
8,81
3,00
0 28
9,85
2,02
6 28
3,81
7,29
5 6,
034,
731
Wila
ya y
a Ir
inga
71
,650
,011
86
6,49
9,00
0 93
8,14
9,01
1 93
2,92
1,56
1 5,
227,
450
21
MBE
YA
-
Jiji
la
Mbe
ya
292,
088,
067.
50
738,
397,
000
1,03
0,48
5,06
7.50
82
1,31
6,06
7 20
9,16
9,00
0.50
Wila
ya y
a M
beya
18
1,96
4,85
8.30
69
6,70
6,00
0 87
8,67
0,85
8.30
64
4,48
5,14
5 23
4,18
5,71
3.30
Wila
ya y
a Ky
ela
34
,922
,357
.76
467,
954,
000
502,
876,
357.
76
431,
530,
897
71,3
45,4
60.7
6
Wila
ya y
a Ru
ngw
e
85,4
39,4
16.9
7 52
2,48
0,00
0 60
7,91
9,41
6.97
58
5,29
0,78
4 22
,628
,632
.97
Wila
ya y
a M
bara
li
176,
078,
204
1,02
6,07
3,00
0 1,
202,
151,
204
1,17
7,13
0,58
8 25
,020
,616
Wila
ya y
a Ch
unya
12
,359
,605
57
2,90
9,00
0 58
5,26
8,60
5 58
5,26
8,60
5 -
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
70,3
81,7
29
223,
161,
000
293,
542,
729
252,
218,
136
41,3
24,5
93
22
SON
GW
E
W
ilaya
ya
Mbo
zi
36,7
96,5
66
1,01
1,08
4,00
0 1,
047,
880,
566
903,
880,
566
144,
000,
000
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
226
Wila
ya y
a Ile
je
72,7
91,5
41
305,
371,
000
378,
162,
541
339,
155,
494
39,0
07,0
47
Wila
ya y
a So
ngw
e
23
7,01
0,50
0 23
7,01
0,50
0 23
7,01
0,50
0 -
Wila
ya y
a M
omba
33
,210
,398
53
6,73
9,00
0 56
9,94
9,39
8 56
7,91
3,58
9 2,
035,
809
Mji
wa
Tund
uma
61
,269
,967
18
7,64
9,00
0 24
8,91
8,96
7 23
1,24
3,43
7 17
,675
,530
23
NJO
MBE
-
W
ilaya
ya
Njo
mbe
50
,337
,763
25
9,33
7,00
0 30
9,67
4,76
3 26
8,75
9,86
4 40
,914
,899
Mji
wa
Njo
mbe
26
5,59
8,17
6 33
0,56
3,00
0 59
6,16
1,17
6 49
2,92
3,86
0 10
3,23
7,31
6
Wila
ya y
a M
aket
e
44,0
35,4
32
296,
649,
000
340,
684,
432
310,
461,
441
30,2
22,9
91
Wila
ya y
a Lu
dew
a
47,9
25,1
80
428,
751,
000
476,
676,
180
449,
283,
735
27,3
92,4
45
Mji
wa
Mak
amba
ko
35,7
11,3
92
189,
502,
000
225,
213,
392
215,
371,
732
9,84
1,66
0
Wila
ya y
a W
ang'
ing'
om
be
104,
924,
926
399,
998,
000
504,
922,
926
453,
247,
398
51,6
75,5
28
24
KATA
VI
-
Wila
ya y
a M
pand
a
65,3
66,4
65
669,
466,
000
734,
832,
465
721,
251,
493
13,5
80,9
72
Wila
ya y
a M
pim
bwe
-
387,
253,
000
387,
253,
000
231,
115,
835
156,
137,
165
Wila
ya y
a N
sim
bo
129,
835,
029
539,
087,
714
668,
922,
743
474,
350,
059.
46
194,
572,
683.
54
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
227
Wila
ya y
a M
lele
92
,602
,655
12
9,67
9,00
0 22
2,28
1,65
5 21
9,52
8,18
4 2,
753,
471
Man
ispa
a ya
Mpa
nda
52
,702
,568
38
6,75
0,34
3 43
9,45
2,91
1 42
8,42
2,27
7 11
,030
,634
25
RUKW
A
-
W
ilaya
ya
Sum
baw
anga
88,3
98,7
80.3
5 78
1,35
4,00
0 86
9,75
2,78
0.35
80
0,84
7,96
7 68
,904
,813
.35
Man
ispa
a ya
Su
mba
wan
ga
84,9
23,6
51.7
0 44
6,67
1,00
0 53
1,59
4,65
1.70
42
8,35
5,49
1 10
3,23
9,16
0.70
Wila
ya y
a N
kasi
88
,563
,000
86
4,75
6,00
0 95
3,31
9,00
0 94
2,81
7,00
0 10
,502
,000
Wila
ya y
a Ka
lam
bo
112,
177,
002
589,
816,
000
701,
993,
002
595,
557,
000
106,
436,
002
26
RUVU
MA
-
Wila
ya y
a Tu
ndur
u 78
,350
,762
1,
056,
038,
000
1,13
4,38
8,76
2 1,
074,
256,
634
60,1
32,1
28
Wila
ya y
a M
bing
a
169,
214,
954.
09
536,
832,
000
706,
046,
954.
09
520,
699,
518
185,
347,
436.
09
Wila
ya y
a N
amtu
mb
o
79,9
65,0
08
713,
887,
000
793,
852,
008
626,
848,
694
167,
003,
314
Wila
ya y
a So
ngea
15
2,82
5,93
9 42
9,91
4,00
0 58
2,73
9,93
9 48
2,32
1,57
1 10
0,41
8,36
8
Man
ispa
a ya
Son
gea
77
,953
,511
.27
393,
275,
000
471,
228,
511.
27
443,
179,
791
28,0
48,7
20.2
7
Wila
ya y
a N
yasa
7,
069,
511
390,
496,
000
397,
565,
511
374,
481,
926
23,0
83,5
85
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
228
Wila
ya y
a M
adab
a
- 18
5,49
3,00
0 18
5,49
3,00
0 17
1,26
1,71
4 14
,231
,286
Mji
wa
Mbi
nga
-
278,
858,
000
278,
858,
000
255,
681,
461
23,1
76,5
39
Jum
la
20,5
93,7
01,6
57 .90
105,
827,
586,
360
126,
970,
149,
017.
83
115,
546,
902,
047. 11
11
,423
,246
,969 .72
Ute
ndaj
i wa
Kife
dha
wa
Mfu
ko w
a Ba
raba
ra -
(Ki
asi S
h.Tz
.)
Na.
M
koa
H
alm
asha
uri
Salio
anz
ia
Fedh
a ili
yopo
kele
wa
Jum
la y
a Fe
dha
iliyo
kuw
epo
Mat
umiz
i Sa
lio Is
hia
1 Ar
usha
W
ilaya
ya
Ar
usha
45
5,87
7,80
0 1,
816,
183,
350
2,27
2,06
1,14
9.63
1,
086,
406,
518.
61
1,18
5,65
4,63
1. 02
Jiji
la
Ar
usha
78
,530
,066
2,
336,
491,
940
2,41
5,02
2,00
6 2,
414,
803,
471
218,
535
Wila
ya
ya
Kara
tu
342,
712,
005.
34
902,
668,
044.
05
1,24
5,38
0,04
9.39
1,
051,
015,
846.
05
194,
364,
203.
34
Wila
ya
ya
Long
ido
74
,193
,620
.48
496,
718,
118
570,
911,
738.
48
567,
233,
000
3,67
8,73
8.48
W
ilaya
ya
M
eru
22
2,14
6,25
4.83
56
4,75
6,27
5 78
6,90
2,52
9.83
65
9,00
9,33
4.98
12
7,89
3,19
4.85
W
ilaya
ya
M
ondu
li
2,78
2,31
1 1,
235,
007,
895. 48
1,
237,
790,
206.
48
1,17
7,05
9,92
2.18
60
,730
,284
.30
Wila
ya
ya
Ngo
rong
oro
10
9,01
7,90
6.03
1,
065,
727,
262
1,17
4,74
5,16
8.03
69
8,19
0,30
7 47
6,55
4,86
1.03
2
Coas
t W
ilaya
ya
Ba
gam
oyo
26
1,70
4,08
1 83
6,04
0,11
1 1,
097,
744,
192
806,
347,
159
291,
397,
033
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
229
Wila
ya
ya
Kiba
ha
83,6
20,0
90
614,
805,
633
698,
425,
723
683,
086,
915
15,3
38,8
08
Mji
w
a Ki
baha
37
6,11
2,24
3 1,
068,
114,
683
1,44
4,22
6,92
6 1,
162,
103,
552
282,
123,
374
Wila
ya
ya
Kisa
raw
e
50,1
13,2
33
2,01
5,45
1,81
0 2,
065,
565,
043
808,
393,
387
1,25
7,17
1,65
6
W
ilaya
ya
M
afia
54
,348
,806
38
9,05
8,96
8 44
3,40
7,77
4 22
9,97
5,72
7 21
3,43
2,04
7
W
ilaya
ya
M
kura
nga
14
6,26
1,53
5 58
9,58
4,72
4 73
5,84
6,25
9 43
2,10
3,25
7 30
3,74
3,00
2
W
ilaya
ya
Ru
fiji
26
2,31
4,99
8 1,
022,
106,
237
1,28
4,42
1,23
5 74
8,74
5,67
7 53
5,67
5,55
8
W
ilaya
ya
Ch
alin
ze
0 31
1,06
3,47
3.01
31
1,06
3,47
3.01
12
,034
,000
29
9,02
9,47
3.01
W
ilaya
ya
Ki
biti
0
125,
724,
482.
55
125,
724,
482.
55
48,3
98,2
78
77,3
26,2
04.5
5 3
Dar-
es
- Sa
laam
M
anis
paa
ya
Ilala
2,
763,
723,
926
5,86
3,81
6,39
6 8,
627,
540,
322
6,68
7,72
8,26
5 1,
939,
812,
057
Man
ispa
a ya
Ki
nond
oni
5,51
6,81
9,55
3 9,
265,
602,
500
14,7
82,4
22,0
53
1,30
0,72
3,90
1 13
,481
,698
,152
M
anis
paa
ya
Tem
eke
1,
240,
972,
740
3,46
1,20
8,88
7. 88
4,70
2,18
1,62
7.88
2,
744,
487,
624.
68
1,95
7,69
4,00
3. 20
Man
ispa
a ya
Ki
gam
boni
0
744,
467,
997
744,
467,
997
40,8
97,4
93
703,
570,
504
4 Do
dom
a W
ilaya
ya
Ba
hi
703,
719,
534
4,56
3,52
5,55
9 5,
267,
245,
093
4,22
8,43
7,60
0 1,
038,
807,
493
Wila
ya
ya
Cham
win
o
17,5
47,0
87
2,15
5,75
9,49
2. 91
2,17
3,30
6,57
9.91
1,
702,
350,
058
470,
956,
521.
91
Wila
ya
ya
Chem
ba
28,2
80,5
10
565,
446,
042.
06
593,
726,
552.
06
590,
274,
659
3,45
1,89
3.06
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
230
Man
ispa
a ya
Do
dom
a
1,03
9,67
3,22
3.0 4
5,85
5,63
6,94
7 6,
895,
310,
170.
04
3,87
8,84
2,15
6 3,
016,
468,
014. 04
W
ilaya
ya
Ko
ndoa
1,
145,
358,
635
787,
830,
352
1,93
3,18
8,98
7 1,
097,
443,
087
835,
745,
900
Mji
w
a Ko
ndoa
8,
484
571,
840,
112
571,
848,
596
28,7
39,2
50
543,
109,
346
Wila
ya
ya
Kong
wa
13
5,61
7,80
7 1,
499,
029,
212
1,63
4,64
7,01
9 1,
488,
230,
350
146,
416,
669
Wila
ya
ya
Mpw
apw
a
836,
457,
267
2,21
8,22
5,29
0 3,
054,
682,
557
1,06
4,96
0,68
1 1,
989,
721,
876
5 G
eita
W
ilaya
ya
Bu
kom
be
24,9
00,0
00
524,
187,
141.
29
549,
087,
141.
29
548,
175,
037.
59
912,
103.
70
Wila
ya
ya
Chat
o
352,
732,
497.
51
3,04
6,55
2,78
0 3,
399,
285,
277.
51
2,23
0,63
0,82
0.71
1,
168,
654,
456. 80
W
ilaya
ya
G
eita
69
,556
,252
.96
1,34
9,20
3,37
4. 79
1,41
8,75
9,62
7.75
1,
311,
016,
608.
38
107,
743,
019.
37
Mji
wa
Gei
ta
528,
896,
953.
94
1,42
8,32
4,09
3. 78
1,95
7,22
1,04
7.72
1,
385,
064,
947.
04
572,
156,
100.
68
Wila
ya
ya
Mbo
gwe
17
3,40
9,96
5 1,
046,
843,
618. 52
1,
220,
253,
583.
52
1,19
8,10
3,96
9 22
,149
,614
.52
Wila
ya
ya
Nya
ng'h
wal
e
192,
726,
331.
43
596,
569,
372.
94
789,
295,
704.
37
679,
441,
606.
70
109,
854,
097.
67
6 Ir
inga
W
ilaya
ya
Ir
inga
49
6,01
4,67
5 2,
645,
118,
248
3,14
1,13
2,92
3 3,
015,
643,
137
125,
489,
786
Man
ispa
a ya
Ir
inga
-9
3,32
2,06
8.86
1,
254,
980,
872
1,16
1,65
8,80
3.14
1,
191,
156,
346
-29,
497,
542.
86
Wila
ya
ya
Kilo
lo
539,
478,
248.
18
3,61
1,84
4,51
8 4,
151,
322,
766.
18
3,94
0,31
1,60
8 21
1,01
1,15
8.18
W
ilaya
ya
M
ufin
di
558,
547,
060.
66
1,23
6,87
4,55
8 1,
795,
421,
618.
66
1,26
3,22
5,44
5 53
2,19
6,17
3.66
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
231
Mji
w
a M
afin
ga
251,
227,
470
517,
189,
041
768,
416,
511
766,
761,
844
1,65
4,66
7 7
Kage
ra
Wila
ya
ya
Biha
ram
ulo
27
,292
,586
.60
532,
147,
455.
68
559,
440,
042.
28
550,
145,
252.
28
9,29
4,79
0
W
ilaya
ya
Bu
koba
24
2,12
2,41
2 64
7,83
9,49
3.92
88
9,96
1,90
5.92
38
0,42
8,12
4.75
50
9,53
3,78
1.17
M
anis
paa
ya
Buko
ba
225,
237,
357.
85
1,16
9,63
4,14
3. 20
1,39
4,87
1,50
1.05
81
3,98
6,93
6.32
58
0,88
4,56
4.73
W
ilaya
ya
Ka
ragw
e
83,8
75,2
71
1,58
4,30
5,75
0. 12
1,66
8,18
1,02
1.12
1,
668,
165,
933.
73
15,0
87.3
9
W
ilaya
ya
Ky
erw
a
898,
742,
610.
08
1,82
8,63
4,29
8 2,
727,
376,
908.
08
1,60
2,83
4,13
4 1,
124,
542,
774. 08
W
ilaya
ya
M
isse
nyi
154,
283,
380
664,
134,
586.
95
818,
417,
966.
95
766,
825,
126.
56
51,5
92,8
40.3
9
W
ilaya
ya
M
uleb
a
940,
888,
861
1,25
0,29
9,00
0 2,
191,
187,
861
1,46
8,30
1,11
2 72
2,88
6,74
9
W
ilaya
ya
N
gara
43
,464
,476
93
1,15
6,27
3.53
97
4,62
0,74
9.53
96
3,59
5,06
5.72
11
,025
,683
.81
8 Ka
tavi
W
ilaya
ya
M
lele
18
3,63
7,29
1 1,
040,
745,
864
1,22
4,38
3,15
5 1,
208,
855,
771
15,5
27,3
84
Wila
ya
ya
Mpa
nda
25
3,59
7,53
7 62
0,46
5,89
1 87
4,06
3,42
8 33
7,38
4,18
0 53
6,67
9,24
8
M
anis
paa
ya
Mpa
nda
5,
719,
720
811,
127,
424
816,
847,
144
496,
234,
763
320,
612,
381
Wila
ya
ya
Nsi
mbo
16
2,01
8,98
4 83
4,13
4,70
9 99
6,15
3,69
3 62
6,82
3,48
8 36
9,33
0,20
5
W
ilaya
ya
M
pim
bwe
0 35
1,89
1,84
0 35
1,89
1,84
0 32
0,98
2,31
0 30
,909
,530
9
Kigo
ma
Wila
ya
ya
Buhi
gwe
87
,886
,256
45
7,15
8,27
8 54
5,04
4,53
4 32
0,31
1,96
9 22
4,73
2,56
5
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
232
Wila
ya
ya
Kako
nko
11
6,96
7,99
9.78
49
3,32
0,75
0 61
0,28
8,74
9.78
55
4,25
2,75
0 56
,035
,999
.78
Wila
ya
ya
Kasu
lu
106,
138,
999.
43
899,
967,
959
1,00
6,10
6,95
8.43
99
4,34
2,00
0 11
,764
,958
.43
Mji
w
a Ka
sulu
2,
931,
382.
79
714,
885,
588
717,
816,
970.
79
716,
769,
737
1,04
7,23
3.79
W
ilaya
ya
Ki
bond
o 18
8,41
1,97
9 91
0,73
2,18
4 1,
099,
144,
163
1,09
1,54
3,59
5 7,
600,
568
Wila
ya
ya
Kigo
ma
12
0,01
1,06
2.22
47
5,22
3,44
1.83
59
5,23
4,50
4.05
38
1,24
3,50
4.05
21
3,99
1,00
0
W
ilaya
ya
U
vinz
a
257,
606,
710.
29
447,
155,
800.
44
704,
762,
510.
73
364,
123,
510
340,
639,
000.
73
Man
ispa
a ya
Ki
gom
a U
jiji
2,
375,
243
1,46
1,15
7,24
4. 54
1,46
3,53
2,48
7.54
1,
441,
348,
375.
46
22,1
84,1
12.0
8 10
Ki
liman
jar
o W
ilaya
ya
H
ai
65,4
31,2
45
1,17
8,30
2,10
9 1,
243,
733,
354
1,22
4,26
4,88
0 19
,468
,474
W
ilaya
ya
M
oshi
39
7,91
4,51
0 1,
674,
129,
838. 61
2,
072,
044,
348.
61
1,23
9,25
0,97
3.44
83
2,79
3,37
5.17
M
anis
paa
ya
Mos
hi
538,
284,
188.
30
2,45
8,33
7,75
2. 06
2,99
6,62
1,94
0.36
2,
751,
852,
611.
56
244,
769,
328.
80
Wila
ya
ya
Mw
anga
24
,165
,963
73
8,78
6,31
0.32
76
2,95
2,27
3.32
73
4,01
5,59
9.32
28
,936
,674
W
ilaya
ya
Ro
mbo
50
,271
,189
.11
707,
459,
396.
05
757,
730,
585.
16
757,
272,
699.
70
457,
885.
46
Wila
ya
ya
Sam
e
119,
133,
425
1,14
8,94
6,74
4 1,
268,
080,
169
1,21
7,97
2,28
8 50
,107
,881
W
ilaya
ya
Si
ha
1,12
8,83
0,71
4.4 0
874,
018,
116.
91
2,00
2,84
8,83
1.31
1,
321,
361,
079.
42
681,
487,
751.
89
11
Lind
i W
ilaya
ya
Ki
lwa
21
2,33
9,01
5 1,
242,
140,
808
1,45
4,47
9,82
3 66
5,42
9,14
5 78
9,05
0,67
8
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
233
Wila
ya
ya
Lind
i 14
2,24
4,48
9 85
9,18
1,24
2 1,
001,
425,
731
994,
766,
617
6,65
9,11
4
M
anis
paa
ya
Lind
i 26
1,03
2,85
6 1,
717,
766,
030
1,97
8,79
8,88
6 1,
556,
338,
000
422,
460,
886
Wila
ya
ya
Liw
ale
85
,802
,820
1,
254,
219,
083
1,34
0,02
1,90
3 1,
339,
927,
646
94,2
57
Wila
ya
ya
Nac
hing
wea
90
,314
,870
1,
043,
304,
870
1,13
3,61
9,74
0 1,
123,
556,
657
10,0
63,0
83
Wila
ya
ya
Ruan
gwa
1,
084,
793
1,97
8,88
9,73
3 1,
979,
974,
526
1,95
3,40
8,94
3 26
,565
,583
12
M
anya
ra
Wila
ya
ya
Baba
ti
12,4
95,0
91
1,45
7,85
8,94
8. 85
1,47
0,35
4,03
9.85
86
7,03
0,11
2.21
60
3,32
3,92
7.64
M
ji
wa
Baba
ti
92,0
78,0
63.2
7 1,
004,
104,
082. 96
1,
096,
182,
146.
23
1,07
4,33
2,92
4.80
21
,849
,221
.43
Wila
ya
ya
Han
ang'
50
5,40
9,71
6 96
2,04
4,03
0.33
1,
467,
453,
746.
33
1,45
1,83
0,71
1.96
15
,623
,034
.37
Wila
ya
ya
Wila
ya
ya
Kite
to
476,
749,
396.
65
836,
330,
982.
17
1,31
3,08
0,37
8.82
95
6,11
7,70
8.16
35
6,96
2,67
0.66
W
ilaya
ya
M
bulu
29
3,40
5,00
0 62
5,69
8,79
5.90
91
9,10
3,79
5.90
85
9,81
3,41
9.97
59
,290
,375
.93
Mji
w
a M
bulu
0
533,
207,
195
533,
207,
195
531,
856,
169
1,35
1,02
6
W
ilaya
ya
Si
man
jiro
38
6,80
8,31
2 74
3,48
4,03
8.60
1,
130,
292,
350.
60
1,09
8,16
9,45
7.67
32
,122
,892
.93
13
Mar
a M
anis
paa
ya
Mus
oma
11
4,23
7,72
2.90
1,
588,
354,
235. 89
1,
702,
591,
958.
79
1,63
5,04
3,25
2.90
67
,548
,705
.89
Wila
ya
ya
Mus
oma
97
,557
,651
69
6,54
5,71
2.67
79
4,10
3,36
3.67
71
5,44
9,50
0 78
,653
,863
.67
Wila
ya
ya
Rory
a
11,7
32,1
03.6
6 59
8,30
4,36
9.43
61
0,03
6,47
3.09
60
7,34
3,78
4.43
2,
692,
688.
66
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
234
Wila
ya
ya
Bund
a
143,
712,
938
665,
641,
111.
53
809,
354,
049.
53
541,
711,
530.
16
267,
642,
519.
37
Wila
ya
ya
Sere
nget
i 67
9,61
9,00
0 1,
320,
123,
681
1,99
9,74
2,68
1 1,
494,
801,
946
504,
940,
735
Wila
ya
ya
Buti
ama
47
7,44
5,03
4.16
55
1,14
5,55
4 1,
028,
590,
588.
16
1,02
4,12
7,17
3 4,
463,
415.
16
Mji
w
a Ta
rim
e
419,
980,
518.
96
552,
074,
055.
28
972,
054,
574.
24
966,
856,
772.
28
5,19
7,80
1.96
M
ji
wa
Bund
a
0 27
2,39
0,79
9 27
2,39
0,79
9 26
2,05
2,44
7.69
10
,338
,351
.31
14
Mbe
ya
Wila
ya
ya
Buso
kelo
11
9,98
5,16
7.42
5,
343,
743,
509
5,46
3,72
8,67
6.42
1,
740,
510,
056
3,72
3,21
8,62
0. 42
Wila
ya
ya
Chun
ya
37,9
13,9
00
625,
645,
941
663,
559,
841
663,
544,
021
15,8
20
Wila
ya
ya
Kyel
a
736,
264,
824
631,
093,
944
1,36
7,35
8,76
8 1,
198,
130,
077
169,
228,
691
Wila
ya
ya
Mba
rali
34
,160
,754
94
3,41
5,34
8 97
7,57
6,10
2 97
7,54
8,69
9 27
,403
Ji
ji la
Mbe
ya
528,
675,
000
2,80
6,40
5,01
7 3,
335,
080,
017
2,01
4,02
7,00
0 1,
321,
053,
017
Wila
ya
ya
Mbe
ya
230,
957,
755
1,85
3,50
7,05
1 2,
084,
464,
806
1,44
3,84
9,45
0 64
0,61
5,35
6
W
ilaya
ya
Ru
ngw
e
252,
547,
657.
99
2,65
3,02
0,57
9 2,
905,
568,
236.
99
1,32
1,05
3,28
0 1,
584,
514,
956. 99
15
So
ngw
e W
ilaya
ya
M
bozi
23
5,63
0,66
4.28
96
6,27
6,66
9 1,
201,
907,
333.
28
827,
968,
273
373,
939,
060.
28
Wila
ya
ya
Ileje
31
1,84
3,44
6 77
6,67
5,33
6 1,
088,
518,
782
636,
305,
830
452,
212,
952
Wila
ya
ya
Mom
ba
-4,7
67,1
05.0
5 55
5,48
7,17
8 55
0,72
0,07
2.95
55
0,68
5,84
3 34
,229
.95
Wila
ya
ya
92,9
43,9
60
691,
867,
711
784,
811,
671
783,
907,
234
904,
437
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
235
Tund
uma
Wila
ya
ya
Song
we
0
111,
025,
079
111,
025,
079
89,1
95,1
09
21,8
29,9
70
16
Mor
ogor
o W
ilaya
ya
G
airo
46
2,81
0,23
1 53
4,34
9,58
4 99
7,15
9,81
5 40
4,82
0,05
6 59
2,33
9,75
9
W
ilaya
ya
Ki
lom
bero
89
9,37
9,32
7 56
8,82
9,06
5 1,
468,
208,
392
1,12
1,41
9,68
9 34
6,78
8,70
3
W
ilaya
ya
Ki
losa
39
4,98
9,85
1 1,
813,
063,
552
2,20
8,05
3,40
3 1,
068,
473,
875
1,13
9,57
9,52
8
W
ilaya
ya
M
orog
oro
26
,613
,139
1,
168,
779,
035
1,19
5,39
2,17
4 88
3,39
8,19
5 31
1,99
3,97
9
M
anis
paa
ya
Mor
ogor
o
532,
941,
010
1,83
1,84
2,12
2 2,
364,
783,
132
1,69
1,18
2,21
7 67
3,60
0,91
5
W
ilaya
ya
M
vom
ero
15
1,14
3,73
5.16
85
3,22
0,22
7 1,
004,
363,
962.
16
538,
895,
359
465,
468,
603.
16
Mji
w
a If
akar
a
0 24
9,61
4,18
5 24
9,61
4,18
5 19
,656
,500
22
9,95
7,68
5
W
ilaya
ya
M
alin
yi
281,
249,
080
147,
912,
892
429,
161,
972
416,
752,
783
12,4
09,1
89
17
Mtw
ara
Wila
ya
ya
Mas
asi
855,
961,
750
957,
302,
511.
16
1,81
3,26
4,26
1.16
1,
376,
539,
848.
57
436,
724,
412.
59
Mji
w
a M
asas
i 11
5,04
5,59
2 78
3,16
5,32
9 89
8,21
0,92
1 58
3,27
6,80
6 31
4,93
4,11
5
W
ilaya
ya
M
twar
a
363,
223,
877
1,06
8,72
5,13
4 1,
431,
949,
011
1,39
5,30
8,66
6 36
,640
,345
M
anis
paa
ya
Mtw
ara
41
0,36
1,22
0.46
1,
765,
968,
698
2,17
6,32
9,91
8.46
1,
603,
751,
486
572,
578,
432.
46
Wila
ya
ya
Nan
yum
bu
87,1
78,8
88.4
5 76
6,97
2,80
6 85
4,15
1,69
4.45
47
8,30
1,86
4 37
5,84
9,83
0.45
W
ilaya
ya
98
,113
,624
.84
945,
412,
492
1,04
3,52
6,11
6.84
98
7,53
4,19
1 55
,991
,925
.84
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
236
Tand
ahim
ba
Wila
ya
ya
Nan
yam
ba
0 65
8,00
0,64
4 65
8,00
0,64
4 46
2,90
2,56
3 19
5,09
8,08
1 18
M
wan
za
Man
ispa
a ya
Ile
mel
a
632,
231,
941
1,73
6,71
8,75
7 2,
368,
950,
698
2,06
1,69
5,75
1 30
7,25
4,94
7
W
ilaya
ya
Kw
imba
47
0,89
7,83
1 58
3,15
3,12
1 1,
054,
050,
952
1,02
3,31
0,00
1 30
,740
,951
W
ilaya
ya
M
agu
26
1,64
5,86
1 40
1,98
4,75
6 66
3,63
0,61
7 49
3,37
5,15
3 17
0,25
5,46
4
Ji
ji
la
Mw
anza
28
1,04
9,19
6 2,
498,
750,
480
2,77
9,79
9,67
6 2,
037,
315,
529
742,
484,
147
Wila
ya
ya
Seng
erem
a
96,4
76,9
66
563,
552,
636
660,
029,
602
108,
737,
250
551,
292,
352
Wila
ya
ya
Buch
osa
0 27
9,94
1,14
2 27
9,94
1,14
2 26
6,35
4,14
2 13
,587
,000
19
N
jom
be
Wila
ya
ya
Lude
wa
27
1,76
4,40
4 1,
228,
633,
739
1,50
0,39
8,14
3 1,
499,
115,
885
1,28
2,25
8
M
ji
wa
Mak
amba
ko
301,
856,
299
943,
843,
326
1,24
5,69
9,62
5 1,
203,
040,
796
42,6
58,8
29
Wila
ya
ya
Mak
ete
13
8,42
9,16
3 1,
054,
552,
471
1,19
2,98
1,63
4 1,
038,
623,
660
154,
357,
974
Wila
ya
ya
Njo
mbe
10
3,63
9,66
1 1,
268,
361,
834
1,37
2,00
1,49
5 1,
288,
193,
818
83,8
07,6
77
Mji
w
a N
jom
be
478,
606,
886.
01
1,47
4,22
1,25
8 1,
952,
828,
144.
01
1,13
0,53
4,33
6 82
2,29
3,80
8.01
W
ilaya
ya
W
angi
ng'o
mbe
73
1,50
2,66
9 2,
408,
789,
459. 35
3,
140,
292,
128.
35
2,19
2,01
2,18
6 94
8,27
9,94
2.35
20
Ru
kwa
Wila
ya
ya
Kala
mbo
51
0,83
0,54
5.21
93
8,11
8,03
0 1,
448,
948,
575.
21
1,44
7,90
5,02
6 1,
043,
549.
21
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
237
Wila
ya
ya
Nka
si
60,8
13,0
00
1,26
1,42
4,22
1 1,
322,
237,
221
651,
889,
946
670,
347,
275
Man
ispa
a ya
Su
mba
wan
ga
63
,798
,785
.17
1,22
7,26
5,66
5 1,
291,
064,
450.
17
973,
499,
032
317,
565,
418.
17
Wila
ya
ya
Sum
baw
ang
a
1,85
5,05
4.78
62
0,75
1,41
0 62
2,60
6,46
4.78
51
4,93
9,78
9 10
7,66
6,67
5.78
21
Ru
vum
a W
ilaya
ya
N
amtu
mbo
1,
043,
133,
435
1,52
1,81
0,05
7. 82
2,56
4,94
3,49
2.82
1,
915,
202,
390.
64
649,
741,
102.
18
Wila
ya
ya
Mbi
nga
45
,942
,298
96
1,59
9,52
7.12
1,
007,
541,
825.
12
966,
795,
271
40,7
46,5
54.1
2
M
ji
wa
Mbi
nga
0
415,
896,
787
415,
896,
787
415,
610,
414
286,
373
Wila
ya
ya
Nya
sa
384,
017,
096
1,27
9,03
7,72
6 1,
663,
054,
822
1,52
2,02
0,01
0 14
1,03
4,81
2
W
ilaya
ya
So
ngea
48
8,49
4,79
7 88
5,09
1,31
8 1,
373,
586,
115
993,
025,
502
380,
560,
613
Man
ispa
a ya
So
ngea
94
,792
,945
97
5,66
0,58
7 1,
070,
453,
532
850,
093,
317
220,
360,
215
Wila
ya
ya
Tund
uru
2,
270,
448,
565
967,
305,
633
3,23
7,75
4,19
8 2,
957,
742,
142
280,
012,
056
Wila
ya
ya
Mad
aba
0 15
3,22
1,72
7.34
15
3,22
1,72
7.34
16
,380
,900
.34
136,
840,
827
22
Shin
yang
a M
ji
wa
Kaha
ma
36
5,63
7,87
8 81
0,14
5,22
5.81
1,
175,
783,
103.
81
861,
526,
012.
09
314,
257,
091.
72
Wila
ya
ya
Kish
apu
54
7,31
4,23
2 2,
260,
465,
517. 98
2,
807,
779,
749.
98
1,92
0,80
7,67
6.49
88
6,97
2,07
3.49
W
ilaya
ya
M
sala
la
531,
340,
588
1,27
3,17
7,23
0 1,
804,
517,
818
1,23
5,34
0,51
5 56
9,17
7,30
3
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
238
Wila
ya
ya
Shin
yang
a
778,
204,
547
870,
700,
258.
85
1,64
8,90
4,80
5.85
1,
546,
068,
583.
30
102,
836,
222.
55
Man
ispa
a ya
Sh
inya
nga
17
8,66
0,24
0 1,
341,
241,
388
1,51
9,90
1,62
8 1,
207,
017,
267
312,
884,
361
Wila
ya
ya
Ush
etu
11
3,83
3,30
7.59
66
8,65
7,23
5.99
78
2,49
0,54
3.58
76
8,27
4,78
0.35
14
,215
,763
.23
23
Sim
iyu
Mji
w
a Ba
riad
i 30
,742
,084
.43
557,
212,
002.
54
587,
954,
086.
97
583,
444,
007.
56
4,51
0,07
9.41
W
ilaya
ya
Ba
riad
i 29
7,62
8,48
1.35
48
6,49
3,90
8.69
78
4,12
2,39
0.04
55
0,98
6,82
0.90
23
3,13
5,56
9.14
W
ilaya
ya
M
asw
a
59,9
15,1
51
1,08
3,09
9,42
1. 49
1,14
3,01
4,57
2.49
1,
141,
910,
940.
67
1,10
3,63
1.82
W
ilaya
ya
M
eatu
15
,566
,198
.33
1,13
1,44
2,66
9. 11
1,14
7,00
8,86
7.44
1,
146,
985,
955.
24
22,9
12.2
0
W
ilaya
ya
Bu
sega
34
,797
,140
.64
526,
492,
673.
86
561,
289,
814.
50
561,
069,
009
220,
805.
50
Wila
ya
ya
Itili
ma
10
0,47
8,39
3 91
1,24
2,76
4.74
1,
011,
721,
157.
74
664,
937,
228.
73
346,
783,
929.
01
24
Sing
ida
Wila
ya
ya
Iram
ba
34,7
86,8
36.8
4 2,
451,
332,
091. 38
2,
486,
118,
928.
22
1,07
6,37
8,47
1.82
1,
409,
740,
456. 40
W
ilaya
ya
Ik
ungi
35
7,01
8,00
0 77
8,61
7,95
2 1,
135,
635,
952
1,13
5,63
0,39
6 5,
556
Wila
ya
ya
Man
yoni
13
3,05
7,70
4 62
9,43
4,41
8.90
76
2,49
2,12
2.90
76
1,49
2,12
2.51
1,
000,
000.
39
Wila
ya
ya
Mka
lam
a
103,
904,
488.
78
638,
752,
652
742,
657,
140.
78
741,
805,
246
851,
894.
78
Wila
ya
ya
Sing
ida
91
,942
,388
58
9,05
0,73
7.02
68
0,99
3,12
5.02
62
6,29
3,12
5 54
,700
,000
.02
Man
ispa
a ya
Si
ngid
a
56,0
24,3
13
1,18
7,06
6,45
5 1,
243,
090,
768
1,24
2,61
4,63
9 47
6,12
9
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
239
Wila
ya
ya
Itig
i 8,
074,
173.
37
312,
547,
284.
21
320,
621,
457.
58
308,
558,
341.
75
12,0
63,1
15.8
3 25
Ta
bora
W
ilaya
ya
Ig
unga
43
7,12
6,82
5.02
88
7,59
2,89
7 1,
324,
719,
722.
02
1,32
1,94
0,48
7 2,
779,
235.
02
Wila
ya
ya
Kaliu
a
49,7
90,2
61.7
9 64
0,62
9,66
6.90
69
0,41
9,92
8.69
48
6,68
6,98
0 20
3,73
2,94
8.69
W
ilaya
ya
N
zega
20
9,95
7,51
1 62
7,61
1,75
2.17
83
7,56
9,26
3.17
80
2,15
1,14
0.79
35
,418
,122
.38
Mji
w
a N
zega
10
9,06
4,92
9.26
56
5,40
4,96
9 67
4,46
9,89
8.26
65
3,48
4,54
2 20
,985
,356
.26
Wila
ya
ya
Siko
nge
43
,889
,893
73
2,25
3,48
9.70
77
6,14
3,38
2.70
54
1,44
2,76
6.70
23
4,70
0,61
6
W
ilaya
ya
Ta
bora
22
7,65
4,00
0 1,
259,
593,
699. 13
1,
487,
247,
699.
13
1,48
7,10
8,69
9.13
13
9,00
0
M
anis
paa
ya
Tabo
ra
297,
908,
943.
71
1,32
2,23
7,23
6. 45
1,62
0,14
6,18
0.16
1,
615,
684,
850.
17
4,46
1,32
9.99
W
ilaya
ya
U
ram
bo
32,4
31,7
76.2
8 85
0,31
8,98
9.26
88
2,75
0,76
5.54
59
1,19
6,15
5.01
29
1,55
4,61
0.53
26
Ta
nga
Wila
ya
ya
Bum
buli
37
,907
,586
.84
586,
240,
925
624,
148,
511.
84
624,
145,
415
3,09
6.84
W
ilaya
ya
H
ande
ni
238,
671,
189.
58
856,
979,
960
1,09
5,65
1,14
9.58
71
6,40
5,66
0 37
9,24
5,48
9.58
M
ji
wa
Han
deni
21
2,04
8,03
8.50
59
0,42
2,24
7 80
2,47
0,28
5.50
59
0,78
1,62
8 21
1,68
8,65
7.50
W
ilaya
ya
Ki
lindi
28
8,05
3,71
9 1,
631,
014,
223
1,91
9,06
7,94
2 1,
407,
911,
689
511,
156,
253
Wila
ya
ya
Koro
gwe
27
0,33
6,32
3 81
6957
996
1,08
7,29
4,31
9 18
1,08
8,35
5 90
6,20
5,96
4
M
ji
wa
Koro
gwe
1,
843,
881,
910.
6 7 7,
905,
122,
987. 99
9,
749,
004,
898.
66
894,
229,
389.
14
8,85
4,77
5,50
9. 52
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
240
Wila
ya
ya
Lush
oto
15
9,97
0,55
1 1,
535,
761,
363
1,69
5,73
1,91
4 1,
695,
731,
914
0
W
ilaya
ya
M
king
a
142,
545,
111
560,
972,
353
703,
517,
464
597,
577,
535
105,
939,
929
Wila
ya
ya
Muh
eza
3,
460,
844.
32
1,01
5,22
9,66
4 1,
018,
690,
508.
32
996,
083,
696
22,6
06,8
12.3
2
W
ilaya
ya
Pa
ngan
i 69
,740
,816
46
8,43
4,08
7 53
8,17
4,90
3 53
1,99
1,74
5 6,
183,
158
Jiji
la T
anga
80
,997
,308
.37
2,70
2,36
4,76
5 2,
783,
362,
073.
37
2,27
6,66
7,50
3 50
6,69
4,57
0.37
Jum
la
54,5
55,1
30,2
77.
46
219,
391,
809,
477
.54
273,
946,
939,
75 5 19
1,94
1,80
7,03
9.36
82
,005
,132
,71
5.64
U
tend
aji w
a Ki
fedh
a w
a M
radi
wa
Mae
ndel
eo y
a Ja
mii
Tanz
ania
- (
Kias
i Sh.
Tz.)
Na.
M
koa
H
alm
asha
uri
Salio
anz
ia
Fedh
a ili
yopo
kele
wa
Jum
la y
a Fe
dha
iliyo
kuw
epo
Mat
umiz
i Sa
lio Is
hia
1 IR
ING
A
- -
-
Wila
ya y
a M
ufin
di
1,08
6,56
5 2,
620,
680,
995
2,62
1,76
7,56
0 2,
618,
898,
306
2,86
9,25
4
Wila
ya y
a Ki
lolo
0
1,25
8,67
3,72
6 1,
258,
673,
726
1,25
7,34
7,85
8 1,
325,
868
Man
ispa
a ya
Ir
inga
28
0,09
3 68
7,81
6,44
3 68
8,09
6,53
6 68
2,61
2,40
7 5,
484,
129
Wila
ya y
a Ir
inga
6,
382,
368
1,86
8,14
9,00
0 1,
874,
531,
368
1,87
2,18
6,11
5 2,
345,
253
2 KA
GER
A
-
-
Wila
ya y
a Bu
koba
74
6,30
2 1,
731,
306,
250
1,73
2,05
2,55
2 1,
729,
394,
262
2,65
8,29
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
241
Wila
ya y
a M
uleb
a
0 3,
280,
727,
320.
2 9 3,
280,
727,
320.
29
3,28
0,72
7,32
0.29
-
Wila
ya y
a Ka
ragw
e
4,33
1,89
0 2,
031,
782,
105
2,03
6,11
3,99
5 2,
037,
920,
460.
18
-
1,80
6,46
5.18
Wila
ya y
a M
isse
nvi
5,84
3,55
8. 37
1,32
9,59
5,62
5 1,
335,
439,
183.
37
1,33
5,43
9,18
3.37
-
Wila
ya y
a N
gara
0
2,05
3,93
3,82
6.9 9
2,05
3,93
3,82
6.99
1,
955,
840,
814.
99
98,0
93,0
12
Wila
ya y
a Bi
hara
mul
o
0 1,
560,
584,
100
1,56
0,58
4,10
0 1,
560,
461,
478
122,
622
Man
ispa
a ya
Bu
koba
44
,689
83
0,58
5,85
3 83
0,63
0,54
2 83
0,56
9,28
7 61
,255
Wila
ya y
a Ky
erw
a
4,76
3,84
9. 98
1,96
4,27
9,37
5 1,
969,
043,
224.
98
1,96
0,67
0,76
2.85
8,
372,
462.
13
3 M
ARA
-
-
Man
ispa
a ya
M
usom
a
61
2,00
6,58
4.99
61
2,00
6,58
4.99
61
1,15
1,82
9.99
85
4,75
5
Wila
ya y
a Ro
rya
0 1,
574,
718,
998
1,57
4,71
8,99
8 1,
571,
729,
007.
85
2,98
9,99
0.15
Wila
ya y
a Bu
nda
43
,164
,120 .94
1,43
4,51
7,76
2.3 2
1,47
7,68
1,88
3.26
1,
473,
658,
710.
88
4,02
3,17
2.38
Wila
ya y
a Se
reng
eti
85
2,06
9,61
0 85
2,06
9,61
0 85
0,39
5,60
9.07
1,
674,
000.
93
Wila
ya y
a M
usom
a
119,
346.
49
1,37
6,93
2,45
0 1,
377,
051,
796.
49
1,37
1,25
8,04
0.56
5,
793,
755.
93
Wila
ya y
a Bu
tiam
a
2,08
2,44
2 1,
762,
574,
500.
3 2 1,
764,
656,
942.
32
1,76
4,54
6,44
2.32
11
0,50
0
4 M
BEYA
-
-
Jiji
la M
beya
58
7,93
4 1,
383,
026,
250
1,38
3,61
4,18
4 1,
381,
514,
000
2,10
0,18
4
Wila
ya y
a 4,
230,
569
2,06
9,71
2,72
0 2,
073,
943,
289
2,07
3,93
9,95
5 3,
334
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
242
Mbe
ya
Wila
ya y
a Ky
ela
95
0,00
0 1,
120,
478,
360
1,12
1,42
8,36
0 1,
121,
423,
768
4,59
2
Wila
ya y
a Ru
ngw
e
0 2,
306,
106,
129
2,30
6,10
6,12
9 2,
306,
106,
129
-
Wila
ya y
a M
bara
li
0 2,
227,
343,
215
2,22
7,34
3,21
5 2,
226,
043,
215
1,30
0,00
0
Wila
ya y
a Ch
unya
5,
477
2,14
5,92
9,00
0 2,
145,
934,
477
2,14
5,06
3,89
4 87
0,58
3
5 SO
NG
WE
Wila
ya y
a M
bozi
7,
490,
373
2,06
5,85
4,73
0 2,
073,
345,
103
2,07
3,34
5,10
3 -
Wila
ya y
a Ile
je
87
4,39
8,30
0 87
4,39
8,30
0 87
3,85
4,59
6 54
3,70
4
Wila
ya y
a M
omba
2,
786,
376
1,35
1,92
0,33
0 1,
354,
706,
706
1,35
4,40
5,32
1 30
1,38
5
Mji
wa
Tund
uma
-
-
6 M
WAN
ZA
-
-
Wila
ya y
a Se
nger
ema
26
,940
,884
3,
842,
420,
305
3,86
9,36
1,18
9 3,
830,
059,
189
39,3
02,0
00
Wila
ya y
a U
kere
we
4,
605,
181
1,58
2,05
1,18
0 1,
586,
656,
361
1,58
6,65
6,36
1 -
Wila
ya y
a Kw
imba
3,
842,
042
2,38
7,80
6,99
0 2,
391,
649,
032
2,39
0,50
3,44
8 1,
145,
584
Man
ispa
a ya
Ile
mel
a
0 1,
085,
003,
675
1,08
5,00
3,67
5 1,
085,
003,
675
-
Wila
ya y
a M
isun
gwi
12,0
87,6
50
2,86
8,08
6,29
6 2,
880,
173,
946
2,86
3,78
0,71
8 16
,393
,228
Wila
ya y
a M
agu
5,
107,
463
1,44
3,08
8,55
0 1,
448,
196,
013.
43
1,44
7,89
3,56
2.07
30
2,45
1.36
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
243
Jiji
la
Mw
anza
2,
289,
893
1,63
4,24
7,85
5 1,
636,
537,
748
1,63
4,44
6,90
1 2,
090,
847
7 RU
KWA
-
-
Wila
ya y
a Su
mba
wan
ga
0 2,
189,
772,
104
2,18
9,77
2,10
4 2,
189,
772,
104
-
Man
ispa
a ya
Su
mba
wan
ga
13,6
45,6
36
1,62
2,04
7,64
5 1,
635,
693,
281
1,63
4,35
2,96
5 1,
340,
316
Wila
ya y
a N
kasi
0
1,28
5,58
1,00
0 1,
285,
581,
000
1,28
5,28
4,00
0 29
7,00
0
Wila
ya y
a Ka
lam
bo
1,
125,
122,
115
1,12
5,12
2,11
5 1,
121,
693,
000
3,42
9,11
5
8 RU
VUM
A
-
-
Wila
ya y
a Tu
ndur
u 23
,060
,853
5,
038,
736,
790
5,06
1,79
7,64
3 5,
059,
227,
196
2,57
0,44
7
Wila
ya y
a M
bing
a
1,31
8,00
5 2,
448,
184,
400
2,44
9,50
2,40
5 2,
449,
410,
068.
59
92,3
36.4
1
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
22
1,88
7 1,
343,
003,
025
1,34
3,22
4,91
2 1,
338,
282,
556
4,94
2,35
6
Wila
ya y
a So
ngea
27
1,04
2 2,
235,
226,
234
2,23
5,49
7,27
6 2,
234,
645,
506
851,
770
Man
ispa
a ya
So
ngea
1,61
2,46
7,76
0 1,
612,
467,
760
1,61
2,46
7,76
0 -
Wila
ya y
a N
yasa
3,
559,
724. 65
1,
259,
508,
100
1,26
3,06
7,82
4.65
1,
260,
791,
491
2,27
6,33
3.65
9 SH
INYA
NG
A
-
-
Mji
wa
Kaha
ma
7,
183,
490
1,35
4,47
3,03
7.4 3
1,36
1,65
6,52
7.43
1,
354,
281,
758.
85
7,37
4,76
8.58
Wila
ya y
a U
shet
u
2,19
2,59
1. 77
1,12
7,28
8,03
5 1,
129,
480,
626.
77
1,12
8,71
5,62
6.77
76
5,00
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
244
Wila
ya y
a Ki
shap
u 4,
769,
480
1,48
2,59
9,17
0 1,
487,
368,
650
1,48
6,65
7,86
0 71
0,79
0
Wila
ya y
a M
sala
la
240,
614.
51
1,47
5,95
6,11
2 1,
476,
196,
726.
51
1,47
4,43
2,81
4.55
1,
763,
911.
96
Wila
ya y
a Sh
inya
nga
23
,831
,572
2,
111,
737,
580
2,13
5,56
9,15
2 2,
130,
762,
542.
92
4,80
6,60
9.08
Man
ispa
a ya
Sh
inya
nga
0
957,
888,
175
957,
888,
175
957,
888,
175
-
10
GEI
TA
-
-
Wila
ya y
a G
eita
44
0,00
0 2,
179,
522,
875
2,17
9,96
2,87
5 2,
173,
008,
875
6,95
4,00
0
Mji
wa
Gei
ta
0 1,
216,
624,
485
1,21
6,62
4,48
5 1,
216,
624,
485
-
Wila
ya y
a Ch
ato
0
1,99
2,68
2,69
0 1,
992,
682,
690
1,98
9,42
7,73
0 3,
254,
960
Wila
ya y
a Bu
kom
be
0 1,
282,
560,
360
1,28
2,56
0,36
0 1,
282,
560,
360
-
Wila
ya y
a N
yang
’hw
ale
319,
502
800,
936,
610
801,
256,
112
801,
256,
112.
69
-
0.
69
Wila
ya y
a M
bogw
e
0 1,
558,
126,
291.
8 2 1,
558,
126,
291.
82
1,50
3,16
5,55
2 54
,960
,739
.82
11
SIM
IYU
-
-
Wila
ya y
a Ba
riad
i 6,
489,
090. 76
3,
056,
560,
225
3,06
3,04
9,31
5.76
3,
061,
429,
688.
41
1,61
9,62
7.35
Mji
wa
Bari
adi
-
-
Wila
ya y
a M
asw
a
20,0
94
2,71
1,93
4,21
0 2,
711,
954,
304
2,70
1,79
5,40
5 10
,158
,899
Wila
ya y
a M
eatu
18
5,22
5 1,
287,
704,
145
1,28
7,88
9,37
0 1,
287,
670,
210.
74
219,
159.
26
Wila
ya y
a
-
-
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
245
Buse
ga
Wila
ya y
a It
ilim
a
-3,4
21,1
95
2,41
2,12
0,25
0.5 8
2,40
8,69
9,05
5.58
2,
407,
799,
399.
11
899,
656.
47
12
NJO
MBE
-
-
Wila
ya y
a N
jom
be
90,8
34,4
05
1,30
3,79
9,47
0 1,
394,
633,
875
1,36
6,31
1,61
1 28
,322
,264
Mji
wa
Njo
mbe
14
4,19
1,07 3
1,22
0,87
3,68
4 1,
365,
064,
757
1,12
3,85
3,28
4 24
1,21
1,47
3
Wila
ya y
a M
aket
e
142,
624,
43 2 1,
311,
326,
717
1,45
3,95
1,14
9 1,
330,
186,
554
123,
764,
595
Wila
ya y
a Lu
dew
a
-766
,005
1,
245,
439,
611
1,24
4,67
3,60
6 89
5,83
6,72
1 34
8,83
6,88
5
Mji
wa
Mak
amba
ko
128,
487,
77 1 63
8,19
2,33
7 76
6,68
0,10
8 68
9,46
8,61
9 77
,211
,489
Wila
ya y
a W
ang'
ing'
omb
e
236,
214,
34 9 1,
043,
811,
757
1,28
0,02
6,10
6 1,
215,
102,
040
64,9
24,0
66
13
KATA
VI
-
-
Wila
ya y
a M
pand
a
122,
368,
16 9 74
3,55
2,14
1 86
5,92
0,31
0 85
9,42
8,31
0 6,
492,
000
Mji
wa
Mpa
nda
-
-
Wila
ya y
a N
sim
bo
3,70
4,48
4 30
1,88
2,36
3 30
5,58
6,84
7 30
1,31
1,54
3 4,
275,
304
Wila
ya y
a M
lele
51
,844
,828
62
9,11
2,07
9 68
0,95
6,90
7 67
8,62
5,90
0 2,
331,
007
Man
ispa
a ya
M
pand
a
77,4
46,4
00
588,
367,
442
665,
813,
842
637,
425,
169
28,3
88,6
73
Jum
la
1,22
1,04
6,58
5.90
11
5,41
3,12
9,4
35.7
4 11
6,63
4,17
6,02
1. 64
115,
399,
800,
724
.05
1,23
4,37
5,29
7.59
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
246
Ute
ndaj
i wa
Kife
dha
wa
Pro
gram
u y
a M
aend
eleo
ya
Sekt
a ya
Maj
i - (
Kias
i Sh.
Tz.)
N
a M
koa
H
alm
asha
uri
Salio
anz
ia
Fedh
a ili
yopo
kele
wa
Jum
la y
a Fe
dha
iliyo
kuw
epo
Mat
umiz
i Sa
lio Is
hia
1 AR
USH
A Ji
ji la
Aru
sha
86
7,70
7,02
7 60
,302
,706
92
8,00
9,73
3 92
8,00
9,73
3 -
Wila
ya y
a Ar
usha
1,
078,
040,
939.
3 8 33
7,83
2,94
7.66
1,
415,
873,
887.
04
1,33
5,49
0,51
4.1 6
80,3
83,3
72.8
8
Wila
ya y
a Lo
ngid
o
338,
830,
593.
06
2,32
1,51
1,12
5.15
2,
660,
341,
718.
21
2,53
6,99
0,54
6.9 7
123,
351,
171.
24
Wila
ya y
a Ka
ratu
17
1,49
6,68
8 58
6,73
6,60
3 75
8,23
3,29
1 41
6,58
0,60
7 34
1,65
2,68
4
Wila
ya y
a M
eru
58
8,92
9,42
4 1,
171,
516,
308
1,76
0,44
5,73
2 1,
750,
775,
713
9,67
0,01
9
Wila
ya y
a M
ondu
li
294,
276,
622
1,21
7,81
2,85
3.33
1,
512,
089,
475.
33
1,48
4,30
1,93
7.9 6
27,7
87,5
37.3
7
Wila
ya y
a N
goro
ngor
o 77
,047
,459
.11
116,
507,
376.
07
193,
554,
835.
18
139,
830,
284.
40
53,7
24,5
50.7
8
2 CO
AST
Wila
ya y
a Ch
alin
ze
- 60
,500
,000
60
,500
,000
35
,358
,316
25
,141
,684
Wila
ya y
a Ba
gam
oyo
78
,354
,574
39
2,33
5,20
4 47
0,68
9,77
8 14
8,05
8,63
2 32
2,63
1,14
6
Wila
ya y
a Ki
baha
13
,279
,839
97
4,75
3,88
0.10
98
8,03
3,71
9.10
46
7,16
7,98
6.10
52
0,86
5,73
3
Mji
wa
Kiba
ha
122,
258,
792
390,
402,
933
512,
661,
725
288,
792,
728
223,
868,
997
Wila
ya y
a Ki
biti
-
60,5
00,0
00
60,5
00,0
00
60,1
83,9
60
316,
040
Wila
ya y
a Ki
sara
we
41
,926
,102
31
0,55
4,79
1 35
2,48
0,89
3 34
4,39
5,97
1 8,
084,
922
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
247
Wila
ya y
a M
afia
32
,852
,823
71
3,92
9,39
7.97
74
6,78
2,22
0.97
55
5,09
5,78
2.64
19
1,68
6,43
8.33
Wila
ya y
a M
kura
nga
45
,378
,199
15
3,99
0,20
0 19
9,36
8,39
9 17
4,00
3,65
6 25
,364
,743
Wila
ya y
a Ru
fiji
68
,382
,305
.08
161,
385,
060.
81
229,
767,
366
220,
942,
893.
09
8,82
4,47
2.91
3 DA
R M
anis
paa
ya
Ilala
69
5,71
2,48
7 49
,745
,078
74
5,45
7,56
5 74
4,95
6,13
8 50
1,42
7
Man
ispa
a ya
Ki
gam
boni
-
45,0
00,0
00
45,0
00,0
00
28,5
00,0
00
16,5
00,0
00
Man
ispa
a ya
Ki
nond
oni
75,8
23,8
47
109,
751,
241
185,
575,
088
163,
529,
318
22,0
45,7
70
Man
ispa
a ya
Te
mek
e
73,8
64,9
52
439,
543,
332
513,
408,
284
490,
679,
026
22,7
29,2
58
4 DO
DOM
A W
ilaya
ya
Bahi
26
1,06
4,75
3 86
9,16
0,93
5.72
1,
130,
225,
688.
56
573,
378,
370.
98
556,
847,
317.
58
Wila
ya y
a Ch
amw
ino
23
,923
,115
72
0,26
7,92
7 74
4,19
1,04
2 45
1,98
5,84
8 29
2,20
5,19
4
Wila
ya y
a Ch
emba
52
,594
,806
72
,605
,566
12
5,20
0,37
2 99
,753
,666
25
,446
,706
Man
ispa
a ya
Do
dom
a
213,
209,
349
1,32
8,81
0,71
8 1,
542,
020,
067
822,
791,
022
719,
229,
045
Wila
ya y
a Ko
ndoa
29
2,27
0,10
5 36
7,86
6,45
4 66
0,13
6,55
9 60
2,50
3,41
9 57
,633
,140
Mji
wa
Kond
oa
- 58
,000
,000
58
,000
,000
57
,828
,966
17
1,03
4
Wila
ya y
a Ko
ngw
a
449,
302,
434.
76
635,
269,
483
1,08
4,57
1,91
8 65
5,66
0,77
7 42
8,91
1,14
1
Wila
ya y
a M
pwap
wa
5 25
1,45
2,87
9 25
1,45
2,88
4 25
2,79
8,01
0 -
1,
345,
126
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
248
5 G
EITA
W
ilaya
ya
Buko
mbe
8,
618,
222.
71
185,
263,
150.
65
193,
881,
373.
36
191,
543,
314.
80
2,33
8,05
8.56
Wila
ya y
a Ch
ato
62
7,31
1,40
9.26
1,
518,
923,
567.
03
2,14
6,23
4,97
6.29
2,
026,
928,
711.
9 8 11
9,30
6,26
4.31
Wila
ya y
a G
eita
12
3,88
0,09
6.11
1,
117,
725,
598.
96
1,24
1,60
5,69
5.07
70
1,94
3,84
1.75
53
9,66
1,85
3.32
Mji
wa
Gei
ta
12,7
81,4
65
65,7
87,6
47.4
3 78
,569
,112
.43
76,1
95,4
56
2,37
3,65
6.43
W
ilaya
ya
Mbo
gwe
3,
220,
211.
67
71,4
82,2
13.5
8 74
,702
,425
.25
52,3
05,7
70
22,3
96,6
55.2
5
Wila
ya y
a N
yang
’hw
ale
1,07
1,25
2,06
4.8 8
1,12
8,24
1,16
3.98
2,
199,
493,
228.
86
2,05
7,66
4,64
6.9 5
141,
828,
581.
91
6 IR
ING
A W
ilaya
ya
Irin
ga
236,
875,
553
772,
739,
838
1,00
9,61
5,39
1 99
1,24
3,87
8 18
,371
,513
Man
ispa
a ya
Ir
inga
15
,985
,534
.32
116,
313,
449
132,
298,
983
99,8
42,8
02
32,4
56,1
81
Wila
ya y
a Ki
lolo
85
,772
,383
74
2,23
0,46
2 82
8,00
2,84
5 71
0,39
6,76
3 11
7,60
6,08
2
Mji
wa
Maf
inga
-
58,0
00,0
00
58,0
00,0
00
29,7
64,5
20
28,2
35,4
80
Wila
ya y
a M
ufin
di
162,
082,
290
70,8
95,2
77
232,
977,
567
193,
392,
263
39,5
85,3
04
7 KA
TAVI
W
ilaya
ya
Mle
le
83,4
20,4
99
734,
580,
199
818,
000,
698
817,
852,
429
148,
269
Wila
ya y
a M
pand
a
192,
167,
535
90,2
25,6
14
282,
393,
149
280,
784,
690
1,60
8,45
9
Man
ispa
a ya
M
pand
a
16,7
22,0
71
52,0
96,9
71
68,8
19,0
42
62,7
48,4
93
6,07
0,54
9
Wila
ya y
a M
pim
bwe
-
450,
916,
421
450,
916,
421
204,
804,
500
246,
111,
921
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
249
Wila
ya y
a N
sim
bo
28,7
22,9
40
66,7
32,5
83
95,4
55,5
23
73,3
21,8
34
22,1
33,6
89
8 KA
GER
A W
ilaya
ya
Biha
ram
ulo
12
8,13
9,39
2 54
8,92
2,19
2.31
67
7,06
1,58
4.31
57
3,11
0,87
3.65
10
3,95
0,71
0.66
Wila
ya y
a Bu
koba
17
0,58
5,09
5.98
22
6,00
8,65
0.33
39
6,59
3,74
6.31
38
7,87
2,96
5.72
8,
720,
780.
59
Man
ispa
a ya
Bu
koba
12
5,04
5,13
1 81
,421
,784
20
6,46
6,91
5 10
3,50
7,13
5 10
2,95
9,78
0
Wila
ya y
a Ka
ragw
e
1,00
9,89
9,38
2.9 7
907,
675,
096.
61
1,91
7,57
4,47
9.58
1,
911,
175,
468.
3 0 6,
399,
011.
28
Wila
ya y
a Ky
erw
a
21,5
15,0
21
55,0
14,4
48
76,5
29,4
69
65,6
35,4
19
10,8
94,0
50
Wila
ya y
a M
isse
nyi
654,
629,
725
65,9
82,9
45
720,
612,
670
720,
304,
846
307,
824
Wila
ya y
a M
uleb
a
296,
060,
250
913,
329,
275.
27
1,20
9,38
9,52
5.27
1,
179,
032,
379.
6 3 30
,357
,145
.64
Nga
ra
75,2
29,9
25.4
6 55
6,04
8,50
1.26
63
1,27
8,42
6.72
57
0,06
6,16
8.37
61
,212
,258
.35
9 KI
GO
MA
Wila
ya y
a Bu
higw
e 17
,026
,786
71
,470
,783
88
,497
,569
64
,604
,950
23
,892
,619
Kako
nko
9,
716,
000
53,9
69,1
19
63,6
85,1
19
61,7
85,4
55
1,89
9,66
4
W
ilaya
ya
Kasu
lu
308,
858,
961
886,
477,
379
1,19
5,33
6,34
0 94
6,22
8,59
8 24
9,10
7,74
2
Mji
wa
Kasu
lu
- 24
3,32
2,87
5 24
3,32
2,87
5 23
0,07
3,66
3 13
,249
,212
Wila
ya y
a Ki
bond
o
246,
643,
420
447,
178,
923
693,
822,
343
309,
446,
849
384,
375,
494
Man
ispa
a ya
Ki
gom
a
12,2
39,4
92
595,
439,
521
607,
679,
013
343,
390,
301
264,
288,
712
Wila
ya y
a Ki
gom
a
432,
480,
456
614,
322,
264.
04
1,04
6,80
2,72
0.04
77
2,87
9,72
0.04
27
3,92
3,00
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
250
Wila
ya y
a U
vinz
a
788,
183,
542
1,08
5,01
2,23
5 1,
873,
195,
777
1,77
4,08
3,14
3 99
,112
,634
10
KILI
MA
NJA
RO
Wila
ya y
a H
ai
341,
937,
724.
33
149,
165,
477.
26
491,
103,
201.
59
489,
839,
134
1,26
4,06
7.59
Wila
ya y
a M
oshi
10
,647
,812
.61
508,
522,
318.
93
519,
170,
131.
54
504,
475,
957.
70
14,6
94,1
73.8
4
Man
ispa
a ya
M
oshi
18
,888
,888
26
8,82
0,62
5 28
7,70
9,51
3 24
0,55
8,28
4.30
47
,151
,228
.70
Wila
ya y
a M
wan
ga
263,
915,
112
1,42
7,11
6,25
0 1,
691,
031,
362
809,
571,
663
881,
459,
699
Wila
ya y
a Ro
mbo
32
,820
,582
88
3,30
7,89
6 91
6,12
8,47
8 84
4,76
1,24
5 71
,367
,233
Wila
ya y
a Sa
me
19
4,59
4,18
1 74
5,34
1,51
8 93
9,93
5,69
9 57
8,63
9,22
4 36
1,29
6,47
5
Wila
ya y
a Si
ha
1,14
2,19
1 1,
131,
462,
907
1,13
2,60
5,09
8 1,
033,
016,
762
99,5
88,3
36
11
LIN
DI
Wila
ya y
a Ki
lwa
47
,307
,409
3,
829,
004,
965
3,87
6,31
2,37
4 3,
863,
314,
883
12,9
97,4
91
Wila
ya y
a Li
wal
e
1,01
8,00
0 22
4,66
0,48
9 22
5,67
8,48
9 22
5,09
9,40
0 57
9,08
9
Wila
ya y
a Li
ndi
6,77
3,43
6 38
8,55
5,63
1 39
5,32
9,06
7 39
2,93
0,69
1 2,
398,
376
Wila
ya y
a Ru
angw
a
540,
983,
026
1,28
0,64
6,76
3 1,
821,
629,
789
1,05
3,31
5,60
9 76
8,31
4,18
1
Man
ispa
a ya
Li
ndi
22,0
79,7
95
1,58
2,44
8,54
0 1,
604,
528,
335
1,57
1,97
6,75
7 32
,551
,578
Wila
ya y
a N
achi
ngw
ea
356,
876,
487
76,4
25,9
11
433,
302,
398
278,
488,
895
154,
813,
503
12
NJO
MB
E W
ilaya
ya
Lude
wa
34
,924
,336
30
0,62
1,93
4 33
5,54
6,27
0 26
6,49
4,03
2 69
,052
,238
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
251
Mji
wa
Mak
amba
ko
235,
257,
761
44,5
44,5
66
279,
802,
327
210,
090,
833
69,7
11,4
94
Wila
ya y
a M
aket
e
45,6
39,7
85
970,
787,
990
1,01
6,42
7,77
5 1,
016,
370,
000
57,7
75
Wila
ya y
a N
jom
be
71,8
29,1
67
850,
206,
140
922,
035,
307
555,
324,
953
366,
710,
354
Mji
wa
Njo
mbe
25
4,20
2,15
5 43
9,00
0,81
3 69
3,20
2,96
8 68
2,40
0,79
1 10
,802
,177
Wila
ya y
a W
ang'
ing'
omb
e
18,0
65,2
57
387,
582,
818
405,
648,
075
249,
750,
382
155,
897,
693
13
MAN
YARA
W
ilaya
ya
Baba
ti
226,
312,
593.
43
146,
289,
334.
04
372,
601,
927.
47
364,
439,
471.
76
8,16
2,45
5.71
Mji
wa
Baba
ti
39,0
96,6
53.3
3 88
6,55
7,00
0.62
92
5,65
3,65
3.95
27
7,70
5,59
7.80
64
7,94
8,05
6.15
W
ilaya
ya
Han
ang'
33
,612
,644
.32
994,
980,
057.
20
1,02
8,59
2,70
1.52
79
3,51
6,99
0.05
23
5,07
5,71
1.47
Wila
ya y
a Ki
teto
46
8,62
3.69
11
0,12
6,11
6.43
11
0,59
4,74
0.12
10
5,22
4,05
3.13
5,
370,
686.
99
Wila
ya y
a M
bulu
11
4,33
5,72
5.02
47
9,88
7,22
7.47
59
4,22
2,95
2.49
53
9,01
3,58
5.10
55
,209
,367
.39
Mji
wa
Mbu
lu
- 55
,000
,000
55
,000
,000
30
,261
,938
24
,738
,062
W
ilaya
ya
Sim
anji
ro
379,
242,
376.
58
509,
009,
470.
43
888,
251,
847.
01
752,
353,
893.
49
135,
897,
953.
52
14
MAR
A W
ilaya
ya
Bund
a
25,7
33,9
41.9
6 79
3,96
6,70
2.54
81
9,70
0,64
4.50
76
7,40
0,68
9.90
52
,299
,954
.60
Mji
wa
Bund
a
- 55
,010
,000
55
,010
,000
37
,845
,218
17
,164
,782
W
ilaya
ya
Buti
ama
21
,969
,803
77
,973
,717
.18
99,9
43,5
20.1
8 94
,409
,962
5,
533,
558.
18
Wila
ya y
a M
usom
a
316,
306,
502
870,
614,
876
1,18
6,92
1,37
8 53
5,91
0,65
2 65
1,01
0,72
6
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
252
Man
ispa
a ya
M
usom
a
22,8
45,3
21
35,3
00,0
00
58,1
45,3
21
37,4
68,0
64
20,6
77,2
57
Wila
ya y
a Ro
rya
49,6
95,8
48
1,37
7,10
5,16
1.46
1,
426,
801,
009.
46
1,33
7,93
5,48
0.6 3
88,8
65,5
28.8
3
Wila
ya y
a Se
reng
eti
46,1
02,0
40
112,
594,
553.
40
158,
696,
593.
40
132,
481,
355
26,2
15,2
38.4
0
Wila
ya y
a Ta
rim
e
46,8
22,7
09.7
9 50
,980
,745
.15
97,8
03,4
54.9
4 87
,474
,340
.75
10,3
29,1
14.2
1
Mji
wa
Tari
me
10
,518
,967
38
,439
,001
48
,957
,968
48
,894
,926
63
,042
15
MBE
YA
Wila
ya y
a Bu
soke
lo
227,
585,
010
299,
026,
801
526,
611,
811
210,
136,
528
316,
475,
283
Wila
ya y
a Ch
unya
96
,314
29
9,23
3,30
1 29
9,32
9,61
5 20
4,80
9,26
2 94
,520
,353
Wila
ya y
a Ky
ela
16
1,03
3,05
5 27
8,64
4,09
7 43
9,67
7,15
2 24
8,86
6,50
4 19
0,81
0,64
8
Wila
ya y
a M
bara
li
472,
912,
008
785,
859,
036
1,25
8,77
1,04
4 1,
233,
268,
440
25,5
02,6
04
Wila
ya y
a M
beya
88
6,72
1,65
0 90
,743
,270
97
7,46
4,92
0 32
3,31
7,19
6 65
4,14
7,72
4
Jiji
la M
beya
36
0,67
0,17
8 57
0,48
1,85
1 93
1,15
2,02
9 33
2,62
5,53
7 59
8,52
6,49
2
W
ilaya
ya
Rung
we
65
6,27
9,67
5 1,
995,
363,
206
2,65
1,64
2,88
1 2,
298,
497,
864
353,
145,
017
16
MO
ROG
ORO
W
ilaya
ya
Gai
ro
127,
483,
954
48,2
42,9
48
175,
726,
902
68,9
95,1
42
106,
731,
760
Mji
wa
Ifak
ara
-
55,0
00,0
00
55,0
00,0
00
49,6
54,8
50
5,34
5,15
0
Wila
ya y
a Ki
lom
bero
55
7,78
6,63
0 59
9,73
7,48
0 1,
157,
524,
110
1,05
1,62
2,01
3 10
5,90
2,09
7
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
253
Wila
ya y
a Ki
losa
16
0,11
3,78
4 91
0,56
4,95
3 1,
070,
678,
737
780,
123,
152
290,
555,
585
Wila
ya y
a M
alin
yi
- 62
,390
,000
62
,390
,000
46
,001
,000
16
,389
,000
Wila
ya y
a M
orog
oro
65
9,87
6,68
9 2,
696,
468,
182
3,35
6,34
4,87
1 3,
330,
703,
171
25,6
41,7
00
Wila
ya y
a M
vom
ero
67
,084
,637
12
3,40
6,90
2 19
0,49
1,53
9 14
1,11
7,07
8 49
,374
,461
Wila
ya y
a U
lang
a
401,
341,
482
1,40
1,08
6,98
6 1,
802,
428,
468
1,73
3,11
6,35
3 69
,312
,115
17
MTW
ARA
Wila
ya y
a M
asas
i 1,
952,
761,
552
2,77
8,79
0,50
7 4,
731,
552,
059
3,36
4,00
6,33
9 1,
367,
545,
720
Mji
wa
Mas
asi
54,4
18,8
68
65,2
45,7
92
119,
664,
660
116,
631,
467
3,03
3,19
3
W
ilaya
ya
Nan
yum
bu
10,0
97,0
63
390,
301,
174.
02
400,
398,
237.
02
226,
216,
235.
02
174,
182,
002
Mji
wa
Nan
yam
ba
5,92
1,28
2 46
1,50
0,00
0 46
7,42
1,28
2 46
6,35
9,12
4 1,
062,
158
Wila
ya y
a N
ewal
a
741,
353,
902
3,51
6,38
9,38
2 4,
257,
743,
284
4,19
0,27
8,19
6 67
,465
,088
Mji
wa
New
ala
-
55,0
00,0
00
55,0
00,0
00
17,5
63,0
00
37,4
37,0
00
Wila
ya y
a M
twar
a
24,9
03,7
05
1,12
3,38
0,95
6 1,
148,
284,
661
1,08
6,13
1,13
4 62
,153
,527
Man
ispa
a ya
M
twar
a
148,
591,
000
38,7
34,3
78
187,
325,
378
166,
801,
000
20,5
24,3
78
Wila
ya y
a Ta
ndah
imba
65
1,19
3,63
0 64
1,91
8,52
9 1,
293,
112,
159
1,13
4,69
9,97
8 15
8,41
2,18
1
18
MW
ANZ
A W
ilaya
ya
Buch
osa
-
60,5
00,0
00
60,5
00,0
00
56,8
93,0
00
3,60
7,00
0
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
254
Wila
ya y
a Kw
imba
21
4,03
6,73
5 87
4,87
1,65
0 1,
088,
908,
385
540,
131,
009
548,
777,
376
Wila
ya y
a M
agu
49
2,27
8,47
3 99
9,92
6,91
3 1,
492,
205,
386
1,42
4,53
9,42
2 67
,665
,964
Wila
ya y
a M
isun
gwi
493,
884,
197.
99
740,
191,
664.
69
1,23
4,07
5,86
3 92
3,15
7,72
4 31
0,91
8,13
9
Jiji
la
Mw
anza
37
,341
,961
36
6,11
1,12
7 40
3,45
3,08
8 29
1,28
5,46
0 11
2,16
7,62
8
Wila
ya y
a Se
nger
ema
35
4,19
0,44
2 64
0,46
8,94
7 99
4,65
9,38
9 89
4,37
9,74
2 10
0,27
9,64
7
Wila
ya y
a U
kere
we
63
,320
,482
1,
181,
090,
496
1,24
4,41
0,97
8 1,
240,
300,
809
4,11
0,16
9
19
RUKW
A W
ilaya
ya
Sum
baw
anga
91
9,30
6,00
1 26
4,22
8,10
7 1,
183,
534,
108
1,00
4,78
1,04
9 17
8,75
3,05
9
Man
ispa
a ya
Su
mba
wan
ga
543,
101,
692
56,4
48,8
53
599,
550,
545
236,
047,
341
363,
503,
204
Wila
ya y
a N
kasi
48
,231
,815
2,
050,
795,
089
2,09
9,02
6,90
4 1,
945,
152,
704
153,
874,
200
Wila
ya y
a Ka
lam
bo
247,
281,
504
238,
455,
983
485,
737,
487
349,
734,
488
136,
002,
999
20
RUVU
MA
Wila
ya y
a M
adab
a
- 45
,100
,000
45
,100
,000
13
,810
,700
31
,289
,300
Wila
ya y
a M
bing
a
274,
189,
681
267,
223,
360
541,
413,
041
379,
539,
684
161,
873,
357
Mji
wa
Mbi
nga
-
55,0
00,0
00
55,0
00,0
00
47,5
28,6
24
7,47
1,37
6
Wila
ya y
a N
amtu
mbo
23
9,82
1,35
5 88
4,92
4,82
5 1,
124,
746,
180
1,09
3,71
8,32
9 31
,027
,851
Wila
ya y
a N
yasa
74
,671
,883
77
1,10
8,62
2 84
5,78
0,50
5 37
5,37
4,54
8 47
0,40
5,95
7
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
255
Wila
ya y
a So
ngea
1,
290,
387,
736
211,
852,
194
1,50
2,23
9,93
0 71
4,78
6,12
6 78
7,45
3,80
4
Man
ispa
a ya
So
ngea
37
,872
,420
59
8,16
4,66
0 63
6,03
7,08
0 63
3,15
4,43
9 2,
882,
641
Wila
ya y
a Tu
ndur
u
60,7
74,8
77
464,
802,
177
525,
577,
054
468,
455,
403
57,1
21,6
51
21
SIM
IYU
W
ilaya
ya
Bari
adi
275,
079.
07
1,06
0,93
9,01
2.79
1,
061,
214,
091.
86
926,
766,
444.
02
134,
447,
647.
84
Mji
wa
Bari
adi
122,
196,
358
879,
248,
384.
79
1,00
1,44
4,74
2.79
36
9,76
4,49
7.79
63
1,68
0,24
5
Wila
ya y
a Bu
sega
49
,939
,021
.51
529,
812,
117.
57
579,
751,
139.
08
437,
161,
029.
30
142,
590,
109.
78
Wila
ya y
a It
ilim
a
204,
375,
801.
42
1,94
7,99
7,07
2.96
2,
152,
372,
874.
38
488,
778,
998.
96
1,66
3,59
3,87
5. 42
Wila
ya y
a M
asw
a
16,7
29,8
28.8
7 1,
061,
770,
485.
47
1,07
8,50
0,31
4.34
65
2,98
5,46
7.70
42
5,51
4,84
6.64
Wila
ya y
a M
eatu
15
3,07
4,01
2.89
1,
358,
574,
035.
30
1,51
1,64
8,04
8.19
1,
404,
967,
836.
5 4 10
6,68
0,21
1.65
22
SHIN
YAN
GA
Mji
wa
Kaha
ma
30
,186
,875
38
,177
,921
68
,364
,796
45
,999
,984
22
,364
,812
Wila
ya y
a Ki
shap
u
75,4
79,9
55
191,
919,
530
267,
399,
485
243,
968,
863
23,4
30,6
22
Wila
ya y
a M
sala
la
15,6
46,5
35.3
8 23
3,36
1,14
1.86
24
9,00
7,67
7.24
20
9,19
9,91
6.98
39
,807
,760
.26
Wila
ya y
a Sh
inya
nga
18
3,26
9,21
0 2,
227,
782,
886
2,41
1,05
2,09
6 1,
219,
878,
536
1,19
1,17
3,56
0
Man
ispa
a ya
Sh
inya
nga
14
,471
,734
.28
39,9
64,9
82.6
3 54
,436
,716
.91
54,1
58,4
08.5
8 27
8,30
8.33
Wila
ya y
a U
shet
u
19,9
27,9
81
1,20
6,25
3,12
2 1,
226,
181,
103
729,
302,
344.
67
496,
878,
758.
33
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
256
23
SIN
GID
A W
ilaya
ya
Ikun
gi
508,
149
308,
994,
278.
46
309,
502,
427.
46
302,
934,
689.
04
6,56
7,73
8.42
Wila
ya y
a Ir
amba
24
,068
,716
58
0,55
4,33
0 60
4,62
3,04
6 59
5,63
8,06
0 8,
984,
986
Wila
ya y
a It
igi
- 1,
117,
914,
388.
13
1,11
7,91
4,38
8.13
11
1,79
8,58
5.13
1,
006,
115,
803
Wila
ya y
a M
anyo
ni
33,4
72,1
80
68,0
49,3
52.3
1 10
1,52
1,53
2.31
97
,947
,929
3,
573,
603.
31
Wila
ya y
a M
kala
ma
78
,444
,000
51
2,00
4,86
6.70
59
0,44
8,86
6.70
56
0,25
3,86
6.70
30
,195
,000
Wila
ya y
a Si
ngid
a
5,50
0,02
2.61
46
1,49
5,86
7.47
46
6,99
5,89
0.08
11
8,65
7,71
4 34
8,33
8,17
6.08
Man
ispa
a ya
Si
ngid
a
2,03
2,19
4 38
,424
,094
40
,456
,288
34
,044
,900
6,
411,
388
24
SON
GW
E W
ilaya
ya
Ileje
35
0,52
4,89
1 55
7,36
8,42
1 90
7,89
3,31
2 55
9,44
0,12
2 34
8,45
3,19
0
Wila
ya y
a M
bozi
20
2,11
1,53
6 44
1,09
7,24
7 64
3,20
8,78
3 63
2,76
8,74
0 10
,440
,043
Wila
ya y
a M
omba
19
,858
,045
69
,900
,433
89
,758
,478
72
,520
,110
17
,238
,368
Wila
ya y
a So
ngw
e
- 60
,500
,000
60
,500
,000
35
,620
,000
24
,880
,000
Mji
wa
Tund
uma
-
34,0
95,0
00
34,0
95,0
00
14,5
50,9
91
19,5
44,0
09
25
TABO
RA
Wila
ya y
a Ig
unga
18
7,73
2,35
5 77
,899
,510
26
5,63
1,86
5 17
6,88
5,76
9 88
,746
,096
Wila
ya y
a Ka
liua
10
,031
,671
14
5,13
4,78
0.41
15
5,16
6,45
1.41
93
,166
,437
.97
62,0
00,0
13.4
4
Wila
ya y
a N
zega
70
,096
,804
74
2,20
9,50
7.28
81
2,30
6,31
1.28
70
9,35
0,65
1.66
10
2,95
5,65
9.62
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
257
Wila
ya y
a Si
kong
e
52,2
47,3
95
943,
943,
874.
69
996,
191,
269.
69
560,
688,
667.
72
435,
502,
601.
97
Wila
ya y
a Ta
bora
64
,806
,000
34
3,23
5,98
8 40
8,04
1,98
8 39
8,22
3,98
8 9,
818,
000
Man
ispa
a ya
Ta
bora
17
,239
,659
.56
44,0
59,8
43.1
7 61
,299
,502
.73
55,0
16,4
18
6,28
3,08
4.73
Wila
ya y
a U
ram
bo
43,6
35,7
71
50,7
93,2
36.9
7 94
,429
,007
.97
76,3
34,2
98.7
0 18
,094
,709
.27
26
TAN
GA
Wila
ya y
a Bu
mbu
li
10,4
74,6
49
1,30
6,66
2,26
4 1,
317,
136,
913
420,
820,
783
896,
316,
130
Wila
ya y
a H
ande
ni
1,34
3,27
6,24
0.1 0
54,3
17,6
89
1,39
7,59
3,92
9 60
5,63
2,22
9 79
1,96
1,70
0
Mji
wa
Han
deni
32
2,60
0 58
0,45
3,00
0 58
0,77
5,60
0 24
,027
,690
.27
556,
747,
909.
73
Wila
ya y
a Ki
lindi
56
4,85
3,33
0.37
54
1,61
9,67
2 1,
106,
473,
002
697,
725,
350
408,
747,
652
Wila
ya y
a Ko
rogw
e
327,
671,
336
52,8
86,2
93
380,
557,
629
247,
993,
119
132,
564,
510
Mji
wa
Koro
gwe
33
,526
,689
.14
395,
149,
858
428,
676,
547
236,
130,
238
192,
546,
309
Wila
ya y
a Lu
shot
o
8,28
5,90
7 72
9,16
9,45
9 73
7,45
5,36
6 73
7,39
0,01
2 65
,354
Wila
ya y
a M
king
a
454,
617,
881
1,24
7,56
2,21
5 1,
702,
180,
096
1,63
8,37
9,11
3 63
,800
,983
Wila
ya y
a M
uhez
a
17,2
82,9
31
770,
422,
869
787,
705,
800
781,
597,
094
6,10
8,70
6
Wila
ya y
a Pa
ngan
i 44
6,74
0,81
5 15
7,23
8,05
3 60
3,97
8,86
8 48
3,04
0,61
7 12
0,93
8,25
1
Jiji
la T
anga
38
4,68
0,86
4 37
5,41
0,66
2 76
0,09
1,52
6 47
6,43
3,03
3 28
3,65
8,49
3
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
258
Jum
la
36,1
12,0
91,2
9 7 10
4,29
6,99
4,80
6.04
14
0,40
9,08
6,10
2.6
2 10
9,01
5,28
6,0
91.8
5 31
,393
,800
,01
1.79
U
tend
aji w
a Fe
dha
wa
Mir
adi M
ingi
ne (
Kias
i Sh.
Tz.)
N
a.
Jina
la M
radi
/ W
atek
elez
aji
Waf
adhi
li Sa
lio a
nzia
Fe
dha
iliyo
poke
lew
a Ju
mla
ya
Fedh
a ili
yoku
wep
o M
atum
izi
Salio
Ishi
a
1 Sh
irik
a la
Ki
mat
aifa
la
Ku
said
ia
Wat
oto
(UN
ICEF
)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la
Kusa
idia
W
atot
o (U
NIC
EF)
- 1,
166,
177,
051
1,16
6,17
7,05
1 71
7,14
6,65
3 44
9,03
0,39
8
2 Sh
irik
a la
Hud
uma
za
Mis
aada
la
Ki
kato
liki (
CRS)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la
Kusa
idia
W
atot
o (U
NIC
EF)
280,
157,
579
986,
171,
860
1,26
6,32
9,43
9 1,
266,
329,
439
-
3 PA
CT T
anza
nia
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la
Kusa
idia
W
atot
o (U
NIC
EF)
404,
928,
064
733,
278,
962
1,13
8,20
7,02
6 1,
124,
507,
391
13,6
99,6
35
4 CU
AMM
Tan
zani
a Sh
irik
a la
Ki
mat
aifa
la
Ku
said
ia
Wat
oto
- 1,
452,
653,
347
1,45
2,65
3,34
7 1,
452,
653,
347
-
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
259
(UN
ICEF
)
5 M
radi
w
a Vi
tabu
vy
a W
atot
o Ta
nzan
ia (
CBPT
)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la
Kusa
idia
W
atot
o (U
NIC
EF)
100,
000
1,06
0,02
5,59
8 1,
060,
125,
598
486,
267,
667
573,
857,
931
6 Ba
ylor
Tan
zani
a Sh
irik
a la
Ki
mat
aifa
la
Ku
said
ia
Wat
oto
(UN
ICEF
)
145,
511,
584
570,
885,
586
716,
397,
170
548,
871,
363.
1 0 16
7,52
5,80
6. 90
7 W
izar
a ya
Af
ya
Mae
ndel
eo
ya
Jam
ii,
Jins
ia,
Waz
ee N
a W
atot
o (M
oHCD
GEC
)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la
Kusa
idia
W
atot
o (U
NIC
EF)
170,
875,
000
364,
966,
850
535,
841,
850
459,
907,
290
75,9
34,5
60
8 Ju
kwaa
la
M
aend
eleo
(PD
F)
Shir
ika
la
Kim
atai
fa
la
Kusa
idia
W
atot
o (U
NIC
EF)
- 92
4,01
5,31
1 92
4,01
5,31
1 59
7,46
6,39
9 32
6,54
8,91
2
9 O
fisi
ya
M
wan
ashe
ria
Mku
u (A
GC)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
- 11
0,08
7,60
0 11
0,08
7,60
0 11
0,08
7,60
0 -
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
260
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
10
Wiz
ara
ya
Fedh
a na
Mip
ango
- Id
ara
ya
Kuon
doa
Um
aski
ni.
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
- 1,
338,
055,
000
1,33
8,05
5,00
0 1,
338,
055,
000
-
11
Ofi
si
ya
Waz
iri
Mku
u (K
uim
aris
ha
Taar
ifa
ya H
ali
ya
Hew
a na
M
fum
o w
a Ku
toa
Taha
dhar
i ya
M
apem
a)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
369,
448,
000
636,
845,
000
1,00
6,29
3,00
0 60
4,75
3,25
3 40
1,53
9,74
7
12
Shir
ika
la
Uza
lisha
ji
Mal
i la
Je
shi
la
Kuje
nga
Taif
a (S
UM
A JK
T)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
8,56
5,00
0 46
8,82
7,00
0 47
7,39
2,00
0 40
0,17
2,20
4 77
,219
,796
13
Mra
di w
a SP
ANES
T kw
a Sh
irik
a la
H
ifad
hi
za
Taif
a (T
ANAP
A/SP
ANES
T)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
205,
831,
081. 41
1,
298,
916,
500
1,50
4,74
7,58
1.4 1
1,38
3,58
3,45
4.9
9 12
1,16
4,12
6. 42
14
Mfu
ko w
a uh
ifad
hi
wa
Wan
yam
apor
i Ta
nzan
ia (
TWPF
)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
- 60
7,39
0,00
0 60
7,39
0,00
0 55
8,65
4,14
0 48
,735
,860
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
261
Mat
aifa
(U
NDP
)
15
Chuo
Ki
kuu
cha
Dar
es
Sala
am
– Id
ara
ya
Uch
umi
(UDS
M D
oE)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
110,
346,
009
1,40
5,83
8,59
7 1,
516,
184,
606
1,43
6,50
3,42
9 79
,681
,177
16
Taas
isi y
a U
ongo
zi
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
- 54
,150
,000
54
,150
,000
44
,309
,000
9,
841,
000
17
Bodi
ya
M
aji
ya
Bond
e la
W
ami/
Ruvu
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
- 66
4,43
7,50
0 66
4,43
7,50
0 65
8,57
2,07
5 5,
865,
425
18
Taas
isi
ya
Uta
fiti
w
a Ki
uchu
mi
na
Kija
mii
(ESR
F)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
- 3,
195,
323,
679
3,19
5,32
3,67
9 2,
901,
436,
415
293,
887,
264
19
Tum
e ya
Mip
ango
Sh
irik
a la
M
aend
eleo
la
U
moj
a w
a M
atai
fa (
UN
DP)
225,
088,
667. 60
20
3,30
0,00
0 42
8,38
8,66
7.60
42
1,71
6,48
8.4 0
6,67
2,17
9.20
20
Bung
e la
Tan
zani
a Sh
irik
a la
M
aend
eleo
la
-
1,55
3,18
0,00
0 1,
553,
180,
000
1,55
3,18
0,00
0 -
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
262
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
21
Kati
bu T
awal
a w
a M
koa
- Ta
bora
Sh
irik
a la
M
aend
eleo
la
U
moj
a w
a M
atai
fa (
UN
DP)
70,6
55,5
67.4 7
693,
108,
227
763,
763,
794.
47
737,
574,
839.
4 2 26
,188
,955
.0 5
22
Bodi
ya
M
aji
ya
Bond
e la
Ru
vum
a na
Pw
ani y
a Ku
sini
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
- 51
,808
,440
51
,808
,440
41
,491
,560
10
,316
,880
23
Kitu
o ch
a El
imu
Kiba
ha
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
98,8
41,6
50
300,
141,
504
398,
983,
154
398,
983,
154
-
24
Wiz
ara
ya
Nis
hati
na
M
adin
i,
Mra
di
wa
Kuje
nga
Uw
ezo
kati
ka
Sekt
a ya
N
isha
ti n
a Ta
sini
a ya
U
chim
baji
M
adin
i (M
EM-M
radi
w
a CA
DESE
)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
7,95
0,80
8 29
8,52
4,42
5 30
6,47
5,23
3 79
,901
,893
22
6,57
3,34
0
25
Bodi
ya
M
aji
ya
Bond
e la
Pan
gani
Sh
irik
a la
M
aend
eleo
la
U
moj
a w
a M
atai
fa (
UN
DP)
- 1,
044,
072,
000
1,04
4,07
2,00
0 1,
044,
072,
000
-
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
263
26
Wak
ala
wa
Hud
uma
za M
isit
u Ta
nzan
ia (
TFSA
)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Um
oja
wa
Mat
aifa
(U
NDP
)
- 1,
515,
221,
711
1,51
5,22
1,71
1 1,
333,
629,
529
181,
592,
182
27
Prog
ram
u ya
Ku
said
ia
Sekt
a ya
U
safi
rish
aji (
TSSP
)
Benk
i ya
Dun
ia
1,35
7,00
0,00 0
2,04
7,71
8,00
0 3,
404,
718,
000
851,
679,
000
2,55
3,03
9,00 0
28
Mra
di
wa
Uw
ezes
haji
Bi
asha
ra
na
Usa
firi
shaj
i Ku
sini
m
wa
Afri
ka
(SAT
TFP)
Benk
i ya
Dun
ia
24,1
15,7
42.4 0
173,
085,
698.
2 9 19
7,20
1,44
0.69
85
,379
,118
.89
111,
822,
321. 80
29
Mra
di w
a Ku
said
ia
Sect
a ya
Bar
abar
a Aw
amu
ya
Pili
(RSS
P II)
Benk
i ya
M
aend
eleo
Af
rika
45,7
23,0
00
153,
386,
781,
0 00
153,
432,
504,
000
153,
230,
835,
0 00
201,
669,
000
30
Mfu
mo
wa
Mab
asi
ya
Mw
endo
kasi
Da
r es
Sa
laam
(B
RT)
Awam
u ya
Pi
li
Benk
i ya
M
aend
eleo
Af
rika
& A
GTF
1,09
5,96
6,36 0
719,
769,
474.
5 7 1,
815,
735,
834.
5 7 78
5,31
1,66
9.5 8
1,03
0,42
4,16
4.99
31
Mra
di
wa
Uje
nzi
wa
Bara
bara
ya
Ki
mat
aifa
Ar
usha
–Ta
veta
/Hol
ili-V
oi
Benk
i ya
M
aend
eleo
Af
rika
6,82
6,00
0,00 0
40,2
52,0
00,0
0 0 47
,078
,000
,000
46
,985
,000
,00 0
93,0
00,0
00
32
Mra
di w
a Ku
said
ia
Sekt
a ya
Bar
abar
a Aw
amu
ya K
wan
za
(RSS
P I)
Benk
i ya
M
aend
eleo
Af
rika
& J
ICA)
130,
895,
000
52,9
99,8
90,0
0 0 53
,130
,785
,000
52
,815
,877
,00 0
314,
908,
000
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
264
33
Mra
di
wa
Usi
mam
izi
wa
Maz
ingi
ra y
a Zi
wa
Vict
oria
(LVE
MP
II)
Benk
i ya
Dun
ia
7,44
9,98
0,29
9.72
8,
970,
308,
575
.02
16,4
20,2
88,8
74.
74
12,4
16,2
30,0
62.
10
4,00
4,05
8,81
2.64
34
Mra
di
wa
Usi
mam
izi
na
Uhi
fadh
i Vy
anzo
vy
a M
aji
Kiha
nsi
(KCC
MP)
Benk
i ya
Dun
ia
1,33
0,15
1,86 9
2,07
8,36
6,93
6 3,
408,
518,
805
3,07
8,63
4,87
5.4
2 32
9,88
3,92
9. 58
35
Mra
di
wa
Usa
firi
shaj
i Ka
nda
ya K
ati
Awam
u ya
Pi
li (C
TCP
II)
Benk
i ya
Dun
ia
11,5
98,6
27,1
16.2
5 17
,119
,003
,93 4
28,7
17,6
31,0
50.
25
28,7
16,8
53,3
39.
97
777,
710.
28
36
Regi
onal
Co
mm
unic
atio
ns
Infr
astr
uctu
re
Proj
ect
(RCI
P)
Mra
di
wa
Miu
ndom
binu
ya
M
awas
ilian
o Ki
mko
a (R
CIP)
Benk
i ya
Dun
ia
1,05
6,21
5,72
7.36
42
,229
,656
,99
7.80
43
,285
,872
,725
.16
38
,311
,028
,15 7
4,97
4,84
4,56
8.16
37
Taas
isi
ya K
ujen
ga
Uw
ezo
Afri
ka
(ACB
F)
Mra
di
- AC
BF/N
M-A
IST
Benk
i ya
Dun
ia
21,6
47,3
75.1 4
133,
523,
979.
7 7 15
5,17
1,35
4.90
15
5,10
3,75
9.1 1
67,5
95.8
0
38
Mra
di
wa
Mae
ndel
eo
ya
Mji
M
kuu
wa
Dar
es
Sala
am (
DMD
P)
Benk
i ya
Dun
ia
17,9
44,4
98,1
23.1
7 25
,571
,263
,69
8.82
43
,515
,761
,821
.99
22
,992
,026
,93
3.79
20
,523
,734
,888
.20
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
265
39
Mra
di
wa
Usi
mam
izi
wa
Uvu
vi
na
Uku
aji
wa
Pam
oja
Kusi
ni
Mag
hari
bi
mw
a Ba
hari
ya
H
indi
(S
WIO
Fish
)
Benk
i ya
Dun
ia
1,64
6,79
7,88
7.09
1,
590,
467,
681
.55
3,23
7,26
5,56
8.6 4
2,63
2,67
2,70
0.4
7 60
4,59
2,86
8. 17
40
Mra
di w
a M
alia
sili
Stah
imiv
u kw
a Aj
ili y
a M
aend
eleo
ya
U
ongo
zi
(REG
ROW
)
Benk
i ya
Dun
ia
159,
011,
348. 88
1,
061,
260,
461
.50
1,22
0,27
1,81
0.3 8
1,01
1,76
2,23
0.7
2 20
8,50
9,57
9. 66
41
Mra
di
wa
Uw
ekez
aji
kati
ka
Kuku
za
Kilim
o Ku
sini
m
wa
Tanz
ania
(SA
GCO
T SI
P)
Benk
i ya
Dun
ia
37,4
46,6
37.9 2
9,86
1,45
6,00
0 9,
898,
902,
637.
9 2 29
7,78
6,83
5.0 8
9,60
1,11
5,80
2.84
42
Prog
ram
u ya
M
iund
ombi
nu
ya
Mas
oko,
Ong
ezek
o la
Th
aman
i na
M
saad
a w
a Fe
dha
Viji
jini
(M
IVAR
F)
Mfu
ko
wa
Kim
atai
fa
wa
Mae
ndel
eo
ya
Kilim
o
7,39
6,84
2,96
9.87
52
,045
,512
,64
7.94
59
,442
,355
,617
.81
54
,860
,828
,62
5.76
4,
581,
526,
992.
05
43
Mra
di
wa
Mab
ores
ho
ya
Mah
akam
a Ya
nayo
mle
nga
Mw
anan
chi
na
Uto
aji w
a H
aki
Benk
i ya
Dun
ia
1,08
6,79
2,10 0
12,4
86,8
64,7
94.
98
13,5
73,6
56,8
94.
98
8,03
9,64
1,59
2.3
1 5,
534,
015,
302.
67
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
266
44
Mra
di w
a H
udum
a ya
Afy
a ya
Msi
ngi
(BH
SP)
Benk
i ya
Dun
ia
732,
821,
234. 18
71
,850
,239
.13
804,
671,
473.
31
803,
791,
627.
9 7 87
9,84
5.34
45
Mra
di w
a M
tand
ao
wa
Afya
kw
a U
mm
a Af
rika
M
asha
riki
(EA
PHN
)
Benk
i ya
Dun
ia
12,1
02,5
26,2 81
1,
326,
738,
843
.41
13,4
29,2
65,1
24.
41
6,28
8,01
9,96
4.6
6 7,
141,
245,
159.
75
46
Mra
di
wa
Mae
ndel
eo
ya
Upa
tika
naji
na
U
kuza
ji w
a N
isha
ti
Tanz
ania
(TE
DAP
- M
EM)
Benk
i ya
Dun
ia
18,0
07,2
20.5 0
20,2
00,0
00
38,2
07,2
20.5
0 32
,755
,474
.20
5,45
1,74
6.30
47
Mra
di
wa
Usi
mam
izi
Ende
levu
w
a Ra
silim
ali
za
Mad
ini (
SMM
RP-I
I)
Benk
i ya
Dun
ia
5,58
9,47
0,82 5
21,2
23,5
61,5
6 2 26
,813
,032
,387
21
,248
,581
,54
9.58
5,
564,
450,
837.
42
48
Mra
di w
a Ku
jeng
a U
wez
o Se
kta
ya
Nis
hati
(ES
CBP)
Benk
i ya
Dun
ia
8,92
6,07
0,65
3.48
1,
156,
891,
802
.32
10,0
82,9
62,4
55.
80
3,52
5,00
9,42
9.6
9 6,
557,
953,
026.
11
49
Mra
di
wa
Mae
ndel
eo
ya
Nis
hati
ya
G
asi
Asili
a
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
W
adau
W
engi
ne
wa
Mae
ndel
eo
1,25
2,02
3,12
2.83
70
0,00
0,00
0 1,
952,
023,
122.
8 3 1,
282,
573,
732
669,
449,
390. 83
50
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
ya
El
imu
kati
ka S
hule
za
Se
kond
ari(
SEDE
P
Benk
i ya
Dun
ia
1,99
7,25
5,89
2.99
11
,555
,750
,82
4.20
13
,553
,006
,717
.19
11
,493
,958
,82
4.20
2,
059,
047,
892.
99
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
267
II)
51
Mra
di
wa
Kufu
ndis
ha
Saya
nsi,
H
isab
ati
na
Kiin
gere
za
Kati
ka
Shul
e za
Se
kond
ari
za
Seri
kali
kwa
Kutu
mia
TE
HAM
A (M
oEST
)
Swed
en
402,
325,
838
- 40
2,32
5,83
8 -
402,
325,
838
52
Prog
ram
u ya
Elim
u na
Uju
zi k
wa
Ajili
ya
Ka
zi
za
Uza
lisha
ji (
ESPJ
)
Benk
i ya
Dun
ia
- 44
3,86
5,36
0 44
3,86
5,36
0 40
,076
,001
40
3,78
9,35
9
53
Mra
di w
a U
panu
zi
wa
Uza
lisha
ji
wa
Mpu
nga
(ERP
P)
Benk
i ya
Dun
ia
2,97
9,06
1,57
9.96
1,
824,
160,
449
.12
4,80
3,22
2,02
9.0 8
1,87
6,01
0,75
0.7
1 2,
927,
211,
278.
37
54
Mat
okeo
Mak
ubw
a Sa
sa K
atik
a M
radi
w
a El
imu
ya
Mal
ipo
kwa
Mat
okeo
(BR
NED
)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Kim
atai
fa
&
Swed
en
17,0
88,5
76,7 71
16
4,81
5,16
9,6 37
181,
903,
746,
408
175,
387,
728,
7 74
6,51
6,01
7,63 4
55
Prog
ram
u ya
Ku
said
ia
Elim
u ya
U
fund
i,
Maf
unzo
na
El
imu
ya
Ual
imu
(STV
ET-T
E)
Benk
i ya
M
aend
eleo
Af
rika
- 2,
756,
796,
204
.28
2,75
6,79
6,20
4.2 8
23,0
41,6
70,8
3 9 -
20,2
84,8
74,6
34.7
2
56
Wak
ala
wa
Usa
firi
w
a M
wen
doka
si
(DAR
T)
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
W
adau
w
a
6,
106,
977,
668
6,10
6,97
7,66
8 4,
746,
533,
640
1,36
0,44
4,02 8
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
268
Mae
ndel
eo
57
Mra
di
wa
Ush
inda
ni
Sekt
a Bi
nafs
i (PS
CP)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Kim
atai
fa
21,6
65,6
81,5
86.7
2 20
,852
,140
,60
2.84
42
,517
,822
,189
.56
21
,594
,049
,31
5.08
20
,923
,772
,874
.48
58
Prog
ram
u ya
Ku
bore
sha
Mij
i Ta
nzan
ia (
TSCP
) -
PO R
ALG
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Kim
atai
fa
32,0
40,0
36,3
95.7
6 53
,073
,742
,18
1.89
85
,113
,778
,577
.65
58
,984
,909
,54
0.02
26
,128
,869
,037
.62
59
Mfu
mo
wa
Kita
ifa
wa
Kubo
resh
a Se
kta
Mba
limba
li (N
MSF
)
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
W
adau
w
a m
aend
eleo
43,8
78,9
29.2 5
24,3
24,2
23.4
7 68
,203
,152
.72
66,6
51,9
69
1,55
1,18
3.72
60
Prog
ram
u ya
Ku
imar
isha
Af
ya
ya
Msi
ngi
kwa
Mat
okeo
(SP
HCR
P)
Shir
ika
la
Mae
ndel
eo
la
Kim
atai
fa
- 44
3,34
5,00
0 44
3,34
5,00
0 44
2,93
7,45
4.6 5
407,
545.
35
61
Uw
ekez
aji
wa
Nda
ni
Kati
ka
Hal
i ya
H
ewa
(LIC
) -
PO-R
ALG
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
W
adau
w
a M
aend
eleo
9,40
5,43
3 54
,000
,000
63
,405
,433
63
,451
,694
-
46
,261
62
Mra
di w
a Se
ra y
a U
tete
zi
na
Uch
ambu
zi
(UN
ICEF
) PO
- RA
LG
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
W
adau
w
a m
aend
eleo
183,
744,
540
378,
225,
000
561,
969,
540
561,
969,
540
-
63
Mfu
ko M
kuu-
Mra
di
wa
Kifu
a Ki
kuu
(TZA
-T-M
oFP)
Mfu
ko
wa
Kim
atai
fa
wa
Mal
aria
, Ki
fua
Kiku
u na
U
KIM
WI
- 17
,716
,825
,26 8
17,7
16,8
25,2
68
17,7
16,8
25,2
6 8 -
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
269
64
Mfu
ko M
kuu-
Mra
di
wa
Uki
mw
i
Mfu
ko w
a Ki
mat
aifa
wa
Mal
aria
, Ki
fua
Kiku
u na
U
KIM
WI
- 31
2,55
2,30
8,5
23.8
5 31
2,55
2,30
8,52
3.8
5 31
2,55
2,30
8,5
23.8
5 -
65
Mfu
ko
Mku
u-M
radi
w
a Ku
imar
isha
M
ifum
o ya
Af
ya/M
alar
ia
(TZA
-H-M
oF)
Mfu
ko w
a Ki
mat
aifa
wa
Mal
aria
, Ki
fua
Kiku
u na
U
KIM
WI
- 10
5,13
1,84
9,6 78
105,
131,
849,
678
105,
131,
849,
6 78
-
66
Kitu
o ch
a M
afun
zo
Kand
a ya
Ki
gom
a (K
ZTC)
Shir
ika
la
Mis
aada
la
Ki
mar
ekan
i (U
SAID
)
- 6,
274,
458,
959
.52
6,27
4,45
8,95
9.5 2
6,27
4,45
8,95
9.5
2 -
67
Taas
isi
ya A
fya
ya
Msi
ngi (
PHCI
) Sh
irik
a la
M
isaa
da la
Ki
mar
ekan
i (U
SAID
)
- 7,
508,
154,
000
7,50
8,15
4,00
0 7,
483,
713,
277
.80
24,4
40,7
22.2 0
68
Prog
ram
u ya
Ki
taif
a ya
Ku
dhib
iti
Mal
aria
(N
MCP
)
Shir
ika
la
Mis
aada
la
Kim
arek
ani
(USA
ID)
- 4,
492,
375,
074
.60
4,49
2,37
5,07
4.6 0
4,18
4,06
3,37
6.4
8 30
8,31
1,69
8. 12
69
Kitu
o ch
a M
aend
eleo
ya
El
imu
ya
Afya
Shir
ika
la
Mis
aada
la
Kim
arek
ani
- 6,
549,
010,
147
6,54
9,01
0,14
7 6,
540,
050,
282
.49
8,95
9,86
4.51
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
270
Arus
ha (
CED
HA)
(U
SAID
)
70
Mam
laka
ya
U
dhib
iti
wa
Man
unuz
i ya
U
mm
a (P
PRA)
–
kupi
tia
mak
ubal
iano
ya
m
saad
a na
mba
62
1-00
4.08
Shir
ika
la
Mis
aada
la
Kim
arek
ani
(USA
ID)
- 1,
311,
828,
274
1,31
1,82
8,27
4 1,
235,
010,
648
.36
76,8
17,6
25.6 4
71
Prog
ram
u ya
Ku
ondo
a M
alar
ia
Zanz
ibar
i (Z
AMEP
) ku
piti
a m
akub
alia
no
ya
ushi
riki
ano
nam
ba:
621-
0011
.01
Shir
ika
la
Mis
aada
la
Kim
arek
ani
(USA
ID)
- 5,
559,
525,
811
.92
5,55
9,52
5,81
1.9 2
5,55
9,36
6,68
3.8
8 15
9,12
8.04
72
Prog
ram
u ya
M
aend
eleo
Se
kta
ya M
aji
Awam
u ya
Pi
li (W
SDP
II)
Benk
i ya
Dun
ia
4,27
8,23
5,02 1
323,
165,
998,
923
.32
327,
444,
233,
944
.32
317,
476,
708,
862
.76
9,96
7,52
5,08
1.56
73
Mra
di w
a U
buni
fu
Ulio
w
azi
Kati
ka
Tasn
ia
ya
Uch
imba
ji
Mad
ini
Tanz
ania
(T
EITI
CI
DA)
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
CI
DA
33,4
79,5
76
40,8
97,9
97
74,3
77,5
73
73,7
36,9
21
640,
652
Mdh
ibit
i na
Mka
guzi
Mku
u w
a H
esab
u za
Ser
ikal
i
AG
R/DP
/201
6/20
17
271
74
Mra
di w
a U
buni
fu
Ulio
waz
i Ka
tika
Ta
sini
a ya
U
chim
baji
M
adin
i Ta
nzan
ia
(TEI
TI
- U
moj
a W
a U
laya
)
Um
oja
Wa
Ula
ya
644,
730,
444
9,72
3,10
0 65
4,45
3,54
4 35
3,21
6,88
7 30
1,23
6,65
7
75
Prog
ram
u ya
M
ageu
zi/M
abad
ilik
o ya
Usi
mam
izi
wa
Fedh
a za
Um
ma
IV
(PFM
RP)
Benk
i ya
Dun
ia
5,56
8,69
5,50
9.19
27
,172
,609
,73
1.78
32
,741
,305
,240
.98
31
,898
,254
,74
6.51
84
3,05
0,49
4. 46
76
Mam
laka
ya
M
apat
o Ta
nzan
ia –
M
fuko
wa
Pam
oja
wa
Mab
ores
ho
ya
Kisa
sa
ya
Uku
sana
ji K
odi
Nor
way
&
De
nmar
k 18
,348
,118
,305
.75
7,75
7,79
2,83
6.4
7 26
,105
,911
,142
.22
8,
368,
457,
940
.99
17,7
37,4
53,2
01.2
3
77
Prog
ram
u ya
Ku
said
ia E
limu
ya
Seko
ndar
i (P
SSE)
M
fuko
w
a Fe
dha
wa
Pam
oja
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
W
adau
w
a M
aend
eleo
1,08
5,38
8,04
3.39
-
1,08
5,38
8,04
3.3 9
- 1,
085,
388,
043.
39
78
Mfu
ko w
a Pa
moj
a w
a Ku
chan
gia
Mra
di
wa
Mpa
ngo
wa
Kufu
atili
a U
mas
kini
Seri
kali
ya
Tanz
ania
&
W
adau
w
a M
aend
eleo
432,
818,
250. 46
-
432,
818,
250.
46
430,
152,
071.
3 5 2,
666,
179.
10
Jum
la
19
6,72
8,36
2,0
20.7
4 1,
557,
495,
429,
551.
36
1,75
4,22
3,79
1,57
2.10
1,
605,
725,
330,
731.
88
148,
498,
460
,840
.22