MAWASILIANO: Katibu, Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu, Mtaa wa Mtendeni S.L.P 353, DODOMASimu: +255 (26) 2322402-4 Barua Pepe: [email protected] Tovuti: www.tsc.go.tz
Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania tumeyautumishiwawalimutanzania
TOLEO NA.5 JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
MWELI AWASHUKIA WATENDAJI WANAOSUASUA KUINGIZA KWENYE MFUMO WALIMU WALIOPANDA MADARAJA
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu, Gerald Mweli akizungumza na Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Wilaya wanaoshughulikia Shule za Msingi (hawapo pichani) katika mkutano uliofanyika Juni 8, 2021 mjini Mtwara. Pembeni yake ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia (Elimu) Prof. Carolyne Nombo akifuatiwa na Mwenyekiti wa TSC, Prof. Willy Komba.
TAHARIRI 2
Itakumbukwa kuwa siku kadhaa zilizopita, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan alitoa
agizo kuwa Watumishi wa Umma wenye zifa za kupanda madaraja vyeo wapandishwe.
Mara baada ya agizo hilo, Mamlaka zinazohusika katika kupandisha vyeo watumishi zilianza kutekeleza agizo hilo ambapo taratibu za kuwabaini watumishi wenye sifa zilifanyika na hatimaye watumishi wakapandishwa vyeo.
Kila mtu anakiri kwamba Mhe Rais wetu mpendwa
amedhamiria kuangalia kwa namna ya pekee haki na maslahi ya Watumishi wa Umma wakiwemo walimu, lengo likiwa ni kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa bidii zaidi.
Kutokana na hatua hiyo, kila mtumishi ana wajibu wa kumshukuru Mhe. Rais kwa jitihada zake za maksudi za kuboresha maslahi ya watumishi wa umma, na namna bora ya kutekeleza hilo ni kufanya kazi kwa bidii, weledi na uzalendo ili tuweze kukidhi matarajio yake katika kuifanya Tanzania ipige hatua zaidi kimaendeleo.
Kwa upande wa walimu,
tunao wajibu wa kufanya
kazi kwa kuzingatia Miiko na
Maadili ya kazi ya ualimu na
tuachane na tabia za uvivu,
uzembe, utoro na tabia
nyingine ambazo ni kinyume
na kazi ya ualimu.
Ni wito wangu kuwa kila
Mtumishi wa Umma awajibike
kikamilifu katika eneo lake la
kazi, na hiyo ndiyo itakuwa
njia nzuri ya kumshukuru Rais
na kuenzi kaulimbiu yake ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Kazi Iendelee.
Wasiliana nasi kwa Simu: +255 782 366 622 & +255 735-255238 Barua Pepe: [email protected] Au fika Ofisi ya Mawasiliano, Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Mtaa wa Mtendeni, S.L.P 353, DODOMA.
Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania tumeyautumishiwawalimutanzania
MwenyekitiPaulina Nkwama
WajumbeMoses Chitama Christina Hape Richard OdongoRevocatus MisongeMectildis KapingaLameck Mbeya
Mhariri MkuuGerard Chami
MhaririAdili Mhina
Msanifu KurasaLucas GordonBO
DI YA
UHA
RIRI KATUNI
TUMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUFANYA KAZI KWA BIDII
Na Adili Mhina.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) a n a y e s h u g h u l i k i a
Elimu, Gerald Mweli ametoa onyo kwa watumishi wa Halmashauri zote nchini wanaosuasua kuingiza kwenye mfumo walimu waliopanda madaraja ikiwa ni sehemu ya kukamilisha taratibu za kiutumishi.
Ametoa kauli Juni 8, 2021 mjini Mtwara wakati wa kikao chake kilichowahusisha Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma pamoja na Maafisa Elimu wa Wilaya wa Shule za Msingi ambao wapo mkoani hapo kwa lengo la kushiriki michenzo ya kitaifa ya wanafunzi wa shule za msingi (UMITASHUMTA) na sekondari
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
HABARI 3
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama akiongea na Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Wilaya wanaoshughulikia Shule za Msingi (hawapo pichani) wakati alipokutana nao kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya kuboresha utumishi wa walimu nchini. Mkutano huo ulifanyika Juni 8, 2021 mjini Mtwara.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu, Gerald Mweli akizungumza na Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Wilaya wanaoshughulikia Shule za Msingi (hawapo pichani) katika mkutano uliofanyika Juni 8, 2021 mjini Mtwara. Pembeni yake ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia (Elimu) Prof. Carolyne Nombo akifuatiwa na Mwenyekiti wa TSC, Prof. Willy Komba.
Baadhi ya Wajumbe na watumishi wa TSC wakiwa katika mkutano uliowahusisha Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa
pamoja na Maafisa Elimu wa Wilaya wanaoshughulikia Shule za Msingi uliofanyika Juni 8, 2021 mjini Mtwara.
MWELI AWASHUKIA WATENDAJI WANAOSUASUA KUINGIZA KWENYE
MFUMO WALIMU WALIOPANDA MADARAJA
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
HABARI 4
(UMISSETA).Alisisitiza kuwa kila mwalimu
aliyepandishwa daraja ni lazima aingizwe kwenye mfumo kabla ya Juni 12 ambayo ndiyo siku ya mwisho ya kufanya zoezi hilo kwa mujibu wa maelekezo kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
“Tumeshatoa maelekezo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote kwamba zoezi la kuingiza watumishi kwenye mfumo linatakiwa limalizike Juni 12. Sasa ninashindwa kuelewa kwa nini baadhi ya watumishi wanaohusika bado wanajivuta katika kukamilisha zoezi hili,” alihoji.
Aliongeza kuwa ni wajibu wa Afisa Elimu katika kila Halmashauri kuhakikisha anafanya kazi kwa karibu na Maafisa Utumishi ili kuhakikisha walimu waliopandishwa madaraja wanaingizwa kwenye mfumo ndani ya muda uliopangwa huku akiwataka Maafisa Elimu ambao
Halmashauri zao hazijaanza zoezi hilo kurudi kwenye maeneo yao ya kazi mara moja kushughulikia zoezi hilo.
“Najua tumekuja hapa kwa ajili ya michezo, lakini hakuna sababu ya Afisa Elimu kuendelea kukaa hapa wakati huko kwake zoezi la kuingiza walimu kwenye mfumo halifanyiki na siku zimebaki chache. Hivyo, ninasema wale wote wanaojua kuwa hawajaanza kutekeleza zoezi hilo kesho (leo) warudi kwenye vituo vyao vya kazi na kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kama ilivyoelekezwa” alisisitiza.
Aliendelea kueleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan aliamua kumaliza kero ya watumishi wa Umma wakiwemo walimu kuhusu kutopanda madaraja kwa muda mrefu na kutoa maelekezo kuwa watumishi wenye sifa wapandishwe, hivyo ofisi yake haiko tayari kuona mtumishi yeyote anakwamisha
zoezi hilo. “Siku chache tu zilizopita
ilikuwa kila ninapokutana na walimu kilio chao kikubwa kilikuwa ni suala la kupanda madaraja, leo Mheshimiwa Rais ametoa kibali tuwapandishe halafu tunaanza kujivuta tena. Ninasisitiza mtumishi yeyote anayejaribu kukwamisha zoezi tutashughulika naye bila kuchelewa,” mweli alisisitiza.
Awali, Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama alisema kuwa ofisi yake inafuatilia kwa karibu zoezi la kuingiza walimu kwenye mfumo na imejiwekea utaratibu wa kupata taarifa ya idadi ya walimu wanaoingizwa kwenye mfumo kutoka Halmashauri zote kila siku.
Alisema pamoja na kwamba Halmashauri nyingi zinaendelea kutekeleza zoezi hilo, zipo baadhi ya Halmasahuri ambazo utendaji wao hauridhishi jambo ambalo lisipofanyiwa kazi kwa wakati linaweza kuathiri kukamilika kwa kazi hiyo kwa wakati.
“Tumekuwa tukikusanya taarifa za Halmashauri zote kila siku ili kujua idadi ya walimu walioingizwa kwenye mfumo. Tumeona kuna haja kwa watendaji wanaoshughulika na zoezi hilo kuongeza kasi zaidi ili tusije tukajikuta tunachelewa,” alifafanua.
Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anayeshughulikia Elimu, Prof. Carolyne Nombo, Mwenyekiti wa TSC, Prof. Willy Komba, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), wajumbe pamoja na Menejimenti ya TSC.
Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Wilaya wanaoshughulikia Shule za Msingi wakiwa
wanamsililiza Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu, Gerald
Mweli (hayupo pichani) wakati wa mkutano.
MWELI AWASHUKIA WATENDAJI WANAOSUASUA KUINGIZA KWENYE
MFUMO WALIMU WALIOPANDA MADARAJA
HABARI 5
Na Adili Mhina.
Katika kuadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma, watumishi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) wametembelea
kituo cha watoto yatima cha Nyumba ya Matumaini kilichopo eneo la Miyuji, jijini Dodoma.
Ziara hiyo iliyofanyika Juni 23, 2021 iliongozwa na Katibu wa TSC, Paulina Nkwama ambaye alieleza kuwa pamoja na kuwahudumia wateja wanaofika ofisi za TSC katika Wiki ya Utumishi wa Umma, wafanyakazi wa Tume hiyo waliona ni vyema kuwatembelea watoto kituoni hapo kwa lengo la kuwasalimia.
“Pamoja na kwamba
tumeendelea kutoa huduma kwa wateja wanaotembelea ofisi zetu, watumishi wa Tume kwa hiari yao waliamua kuchangishana fedha kidogo wakanunua baadhi ya mahitaji ya watoto na wamekuja kuwaona,” alisema Nkwama wakati akizungumza na uongozi wa kituo hicho.
Katibu huyo aliwaasa watoto katika kituo hicho kuhakikisha wanazingatia masomo yao kikamilifu ili waweze kufanya vizuri na baadae kumudu maisha yao wenyewe na kuwa na mchango katika kulitumikia Taifa.
“Pamoja na uwepo wa changamoto za hapa na pale ambazo tumeelezwa na Sister, tunawaomba mhakikishe mnasoma kwa bidii. Tume ya Utumishi wa Walimu inashughulika na walimu katika masuala ya ajira, maadili na
TSC YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KWA KUTEMBELEA WATOTO YATIMA
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama (kushoto) akikabidhi fedha taslim kwa uongozi wa kituo cha kulelea
watoto yatima cha Nyumba ya Matumaini kilichopo Miyuji, Dodoma ikiwa ni miongoni mwa zawadi zilizokabidhiwa kituoni hapo na
Watumishi wa TSC Juni 23, 2021.
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama akigawa zawadi kwa watoto wanaolelewa katika kituo cha watoto
yatima cha Nyumba ya Matumaini wakati watumishi wa Tume hiyo walipotembelea kituo hicho Juni 23, 2021.
maendeleo yao. Walimu hao ndio wanaowafundisha ninyi, na wakiwafundisha tunatarajia tupate matokeo chanya,” alisema Nkwama.
Nkwama aliongeza kuwa, “elimu ni haki yenu, hakikisheni kwamba walimu wanaingia darasani na wanawafundisha, na ninyi mnaofundishwa mpokee yale mnayofundishwa na myazingatie, mwanadamu atajikomboa pale ambapo atakuwa amejikomboa kifikra.”
Kwa upande wake Mkuu wa Kituo hicho, Aurea Kyara alieleza kuwa kwa sasa kituo kinahudumia watoto 67 ambao wanaanzia umri wa miaka mitatu hadi miaka ishirini na tano na wanasoma madarasa tofauti tofauti.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama (wa pili kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na watoto wa Kituo cha kulelelea watoto yatima cha Nyumba ya Matumaini, watumishi wa TSC pamoja na mmoja wa viongozi wa kituo hicho (wa kwanza upande wa kulia) kilichopo Miyuji,
jijini Dodoma. Watumishi hao walikabidi zawadi mbalimbali ikiwemo unga wa ngano, sukari, sabuni, daftari, mabegi ya shule, dagaa, pipi, vinywaji pamoja na fedha taslim.
HABARI 6
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
TSC YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KWA KUTEMBELEA WATOTO YATIMA
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Moses Chitama akigawa zawadi kwa watoto wa Kituo cha Nyumba ya Matumaini kilichopo Miyuji, Dodoma wakati Watumishi wa TSC
walipotembelea watoto hao Juni 23, 2021 kwa lengo la kuwasalimia.
Alimshukuru Katibu pamoja na watumishi wa TSC kwa kuwatembelea huku akieleza kuwa wanakaribisha mtu yeyote anayependa kuwatembelea watoto hao kwa kuwa wakiona wageni wanakuja kuwasalimia wanapata faraja na kuona kuwa jamii inawajali.
“Tunawashukuru sana kwa moyo wenu wa upendo, mnapokuja watoto hawa wanajisikia faraja na wanaona wamezungukwa na jamii ya watu wanaowapenda na kuwajali. Tunamkaribisha mtu yeyote anayependa kuja
kuwaona na kuzungumza nao,” alisema.
Kwa upande wa watoto hao, waliwashukuru watumishi wa Tume kwa kuwatembelea na kuomba watu wengine wenye moyo wa kuwajali wasisite kuwatembelea.
Miongoni mwa zawadi zilizowasilishwa na wafanyakazi hao ni unga wa ngano, sukari, sabuni, daftari, mabegi ya shule, dagaa, pipi, vinywaji pamoja na fedha taslim.
Baadhi ya Watumishi wa TSC wakiwa kwenye gari kuelekea kituo cha kulelea watoto yatima cha Nyumba ya Matumaini
kilichopo eneo la Miyuji jijini Dodoma.
7
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
HABARITSC YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA
UMMA KWA KUTEMBELEA WATOTO YATIMA
Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Nyumba ya Matumaini,
Sister Aurea Kyara akitoa historia fupi ya kituo hicho kwa watumishi wa TSC
(hawapo pichani) wakati watumishi hao walipotembelea kituo hicho Juni 23, 2021.
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
HABARI 8Na Adili Mhina.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama amewataka watendaji wa Tume hiyo kujikita
zaidi katika kutoa elimu kwa walimu ili wazingatie maadili ya kazi yao badala ya kukaa na kusubiri watende makosa ili wawachukulie hatua za kinidhamu.
Agizo hilo amelitoa hivi karibuni alipofanya ziara katika ofisi za TSC Wilaya ya Dodoma na Chamwino kwa lengo la kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa majukumu ya kila siku pamoja na kuona namna ofisi hizo zinavyotoa huduma kwa wateja katika wiki ya Utumishi wa Umma.
Nkwama alisema kuwa TSC ina wajibu wa kuwasaidia walimu katika masuala ya maadili na maendeleo ya utumishi wao ili wawe na ustawi mzuri na kufanya watoe elimu bora kwa wanafunzi.
“Tumepewa dhamana ya
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama (kushoto) akiongea na watumishi wa TSC Wilaya ya Dodoma
alipofanya ziara ofisini hapo hivi karibuni. Pembeni yake ni Kaimu Katibu Msaidizi wa TSC Wilaya ya Dodoma, Leticia Mwakasitu.
Baadhi ya Watumishi wa TSC Wilaya ya Dodoma wakisikiliza maelekezo ya kiutendaji kutoka kwa
Katibu wa TSC, Paulina Nkwama (hayupo pichani) wakati wa ziara ya Katibu huyo katika ofisi za TSC Dodoma. Pichani, anayeandika ni Afisa
anayeshughulikia Nidhamu na Maadili ya Walimu kutoka TSC Makao Makuu, Julius Mshana.
Kaimu Katibu Msaidizi wa TSC Wilaya ya Dodoma, Leticia Mwakasitu (kulia) akitoa ufafanuzi kuhusu
utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake kwa Katibu wa TSC, Paulina Nkwama.
NKWAMA: TUSISUBIRI WALIMU WATENDE MAKOSA ILI TUWAADHIBU
kuwahudumia walimu katika masuala ya ajira, maadili na maendeleo yao. Sasa ni lazima tujikite katika kuzuia walimu wasijiingize katika vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa kuwa wakiwa na maadili mema ndipo tunaweza kujivunia kuwa
tunafanya kazi,” alisema.Aliwataka watendaji wa ofisi
hizo kuhakikisha wanatumia muda wao kuwafikia walimu na kuwapa elimu kuhusu haki, wajibu na maadili ya utumishi ili kuwaepusha na makosa ya kinidhamu.
Aliongeza kuwa mamlaka za nidhamu ambazo ni wakuu wa shule na TSC ngazi ya wilaya hawajatekeleza wajibu wao ipasavyo katika kuwasaidia walimu kuelewa umuhimu wa kuzingatia miiko na maadili ya kazi yao katika utendaji wa kazi.
Alifafanua kuwa mamlaka hizo zinapaswa kubaini mienendo ya walimu isiyofaa na kuwarekebisha mapema kabla ya kufikia hatua ya kuanzisha shauri la nidhamu ambalo linaweza kusababisha mwalimu apoteze ajira yake.
“Haiwezekani mkuu wa shule anaona mwalimu siku ya kwanza hayupo shuleni, siku ya pili hayupo halafu badala ya kufanya
9
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
Katibu wa TSC, Paulina Nkwama akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili ofisi za TSC Chamwino kwa ziara ya kikazi iliyofanyika hivi karibuni.
HABARINKWAMA: TUSISUBIRI WALIMU WATENDE MAKOSA ILI TUWAADHIBU
jitihada za kumtafuta ili ajue tatizo na kuona namna ya kumsaidia, anasubiri siku tano ziishe apeleke taarifa kwa mkurugenzi ili hatua za kinidhamu zichukuliwe, hii siyo sawa,” alisema.
Aliongeza kuwa pale inapotokea mwalimu anafukuzwa kazi ni lazima mamlaka za nidhamu zijitafakari kama zinatekeleza
wajibu wao wa kuwaelimisha walimu inavyotakiwa.
“Hatuwezi kujivunia kuwa tumefanya kazi nzuri endapo tunaona bado walimu wanafukuzwa kazi kwa makosa ya kinidhamu. Pale inapotokea tumemfukuza kazi mwalimu lazima tujiulize kuwa tumetekeleza wajibu wetu wa
kutoa elimu na kumrekebisha mwalimu kama inavyotakiwa,” alisisitiza.
Pamoja na kusisitiza hayo, Katibu huyo alisema pale ambapo mwalimu amerekebishwa lakini hataki kubadilika ni lazima mamlaka za nidhamu zimchukulie hatua kwa mujibu wa sheria na taratibu husika.
Katika kuadhimisha wiki ya utumishi wa Umma, Katibu huyo alipata fursa ya kuona namna ofisi hizo zinavyopokea wateja na kuwahudumia, pia alipokea malalamiko na changamoto za watumishi wa ofisi hizo na kuahidi kuzifanyia kazi haraka iwezekanavyo ili waendelee kuwa na mazingira mazuri ya kufanyia kazi ya kuwahudumia walimu.
10
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
Katibu wa TSC, Paulina Nkwama (Kulia) akipitia orodha ya Walimu waliopanda Madaraja katika Wilaya ya Chamwino wakati wa ziara yake katika ofisi za TSC wilayani hapo aliyoifanya hivi karibuni. Pichani,
upande wa kushoto ni Kaimu Katibu Msaidizi wa TSC Wilaya ya Chamwino, Paulina Kanumba na katikati ni Afisa Ajira na Maendeleo ya Walimu wa ofisi hiyo, Pater Nassa.
HABARINKWAMA: TUSISUBIRI WALIMU WATENDE MAKOSA ILI TUWAADHIBU
HABARI 11NKWAMA AHIMIZA USHIRIKIANO TSC, MAAFISA ELIMU NA WATHIBITI UBORA
Na Adili Mhina.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina N k w a m a
amewataka watendaji wa TSC, Maafisa Elimu na Wathibiti Ubora wa Shule kuwa na ushirikiano wa karibu ili kuongeza ufanisi katika kuwahudumia walimu.
H a y o ameyazungumza wakati alipotembelea ofisi za TSC Wilaya ya Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine alipata fursa ya kufanya kikao kifupi kilichowahusisha watumishi wa TSC,
Mthibiti Ubora wa Shule pamoja na Maafisa Elimu Taaluma kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
Alieleza kuwa ofisi hizo zinategemeana kwa kiasi kikubwa katika kukamilisha majukumu yao ya kutoa huduma kwa walimu hivyo, ushirikiano wa karibu utasaidia kutatua changamoto za walimu kwa wakati.
“Sote tunajenga nyumba moja, ili nyumba yetu iweze kuwa imara ni lazima tufanye kazi kama timu
moja. Lakini mkisema kila mtu afanye kazi kivyake na kwa wakati wake hatutaweza kufikia malengo ya Serikali katika kutoa huduma bora kwa walimu,” alisema Nkwama.
Alielekeza kuwa watendaji hao wanapopanga kufanya ziara shuleni kwa lengo la kukutana na walimu ni vyema wawasiliane na wafanye ziara kwa pamoja ili kurahisisha utoaji elimu na utatuzi wa changamoto za walimu kwa wakati.
“Ukienda Afisa Elimu
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
Katibu wa TSC, Paulina Nkwama akizungumza na Watumishi wa TSC Wilaya ya Dodoma, Maafisa
Elimu pamoja na Mthibiti Ubora wa Shule wote kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma (hawapo
pichani) wakati wa ziara yake katika Ofisi za TSC Wilaya ya Dodoma iliyofanyika hivi karibuni.
Maafisa Elimu Taaluma, Mthibiti Ubora wa Shule (aliyesuka) pamoja na Watumishi wa TSC wakimsikiliza Katibu wa TSC, Paulina Nkwama (hayupo
pichani) akisisitiza juu ya ushirikiano katika utendaji kazi. Kikao hicho kimefanyika hivi karibuni wakati Katibu huyo alipofanya ziara katika ofisi za TSC
Wilaya ya Dodoma kwa lengo la kufanya ufuatiliaji wa majukumu ya kila siku ofisini hapo.
HABARI 12NKWAMA AHIMIZA USHIRIKIANO TSC, MAAFISA ELIMU NA WATHIBITI UBORA
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
peke yako utajikuta unaulizwa maswali ya TSC au ya Mthibiti ubora ambayo huna majibu yake, hali kadhalika kwa ofisi ya TSC na Mthibiti ubora. Huko shuleni walimu wanajua sisi ni kitu kimoja hivyo akiuliza swali lolote anatarajia kupata majibu ya uhakika. Mkienda pamoja kila mmoja ataona kazi yake inakuwa nyepesi,” alisema Nkwama.
Aliongeza kuwa kufanya kazi kwa ushirikiano kunasaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa vitendea kazi kwa baadhi ya Ofisi ambavyo kwa namna
moja au nyingine v i n g e s a b a b i s h a kutofikiwa kwa malengo ya kutoa huduma bora kwa walimu.
“Ofisi zetu za TSC wilayani hazina magari, lakini kama mkifanya kazi kwa ushirikiano nao wataweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi kwa kutumia rasilimali zilizopo ofisi ya Mkurugenzi au kwa Mthibiti Ubora na mwisho wote tukajikuta tumetimiza malengo”, alifafanua.
Afisa anayeshughulikia masuala ya Maadili na Nidhamu kutoka TSC Makao Makuu, Julius Mshana akitoa maelezo mafupi kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria na taratibu wakati wa kushughulikia mashauri ya nidhamu kwa walimu.
Pembeni yake ni Afisa wa TSC Wilaya ya Dodoma, Key Musa.
Baadhi ya watumishi wa TSC Wilaya ya Dodoma wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Katibu wa TSC, Paulina Nkwama (hayupo pichani) wakati wa ziara yake
ofisini hapo aliyiofanya hivi karibuni.
13
Afisa Utumishi, George Ndatta akitoa maelezo kwa Katibu wa TSC,
Paulina Nkwama (wa kwanza upande wa kulia) kuhusu mali mbalimbali
za ofisi hiyo katika ukaguzi wa mali za ofisi
uliofanywa na Katibu huyo Juni 2, 2021.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC)
Prof. Willy Komba wakati mwenyekiti huyo alipomtembelea
Katibu Mkuu ambapo walifanya mazungumzuzo
kuhusu masuala ya Utumishi wa Walimu, hivi karibuni.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama akiwa katika zoezi la kukagua mali za ofisi hiyo. Katibu huyo alifanya ukaguzi wa mali mbalimbali za ofisi Juni 2, 2021.
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
HABARI KATIKA PICHA
14
Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi TSC, Lameck Mbeya akijadiliana jambo na Mtumishi wa TSC, Dickson Ishemo mjini Mtwara hivi karibuni.
Wataalam wa Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini wa TSC wakiwa wanaendelea na utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Pichani, aliyekaa ni Mchumi Mkuu, Elia Malaki akiwa na Frank
Makundi.
Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Assela Luwena (kushoto) na Huruma
Mageni wakizungumza jambo wakati wa Mkutano wa Tume hiyo uliofanyika mjini Mtwara hivi
karibuni.
Mkurugenzi Msaidizi wa Ajira na Maendeleo ya Walimu kutoka TSC, Mectildis Kapinga akiwa pamoja na Afisa kutoka Idara ya Elimu TAMISEMI, Richard Makota wakiendelea na zoezi la kukusanya taarifa za walimu walioingizwa kwenye mfumo baada ya kupandishwa vyeo.
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
HABARI KATIKA PICHA
15
Baadhi ya wanafunzi
waliohudhuria ufunguzi wa michezo ya
UMITASHUMTA na UMISSETA
katika uwanja wa Nangwanda Sijaona
mjini Mtwara.
Baadhi ya Wajumbe na Wakurugenzi wa TSC wakiwa katika uwanja
wa Nangwanda Sijaona mjini
Mtwara kushiriki ufunguzi wa michezo
ya shule za msingi (UMITASHUMTA)
na sekondari (UMISSETA)
uliofanyika Juni 8, 2021.
Picha ya pamoja ya viongozi mbalimbali walioshiriki ufunguzi wa michezo ya shule za msingi (UMITASHUMTA) na sekondari (UMISSETA) uliofanyika Juni 8, 2021 mjini Mtwara. Pichani, wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, akifuatiwa na Mwenyekiti wa TSC, Prof. Willy Komba, watatu kutoka kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania, Dkt. Charles Msonde na wa pili kutoka kushoto ni Katibu wa TSC, Paulina Nkwama. Wengine ni Wajumbe pamoja na Wakurugenzi wa TSC.
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
HABARI KATIKA PICHA
16
Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Prof. Willy Komba (katikati kwa waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe
pamoja na Menejimenti ya TSC wakati wa Mkutano wa Tume hiyo uliofanyika mkoani Mtwara hivi karibuni. Upande wa kulia (waliokaa) ni Katibu wa TSC, Paulina Nkwama na kushoto ni Mjumbe wa TSC,
Assela Luwena.
Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Prof. Willy Komba (katikati kwa waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wajumbe wa
TSC wakati wa Mkutano wa Tume uliofanyika mkoani Mtwara hivi karibuni. Upande wa kulia
(waliokaa) ni Katibu wa TSC, Paulina Nkwama na kushoto ni Mjumbe wa TSC, Assela Luwena.
Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Prof. Willy Komba (katikati kwa waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe, Menejimenti pamoja na baadhi ya Watumishi wa TSC wakati wa Mkutano wa Tume hiyo uliofanyika mkoani Mtwara hivi karibuni. Upande wa kulia (waliokaa) ni Katibu wa TSC, Paulina Nkwama na kushoto ni Mjumbe wa TSC, Assela Luwena.
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
HABARI KATIKA PICHA
Baadhi ya wanafunzi wanaoshiriki michezo ya UMITASHUMTA na UMISSETA wakiwa katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Na. Adili Mhina
Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) i m e k u t a n a na Maafisa
Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri wanaosimamia shule za msingi kwa lengo la kutoa elimu juu ya majukumu mbalimbali yanayotekelezwa na ofisi hiyo.
Akitoa neno la
utangulizi katika kikao hicho kilichofanyika hivi karibuni mjini Mtwara wakati wa michezo ya UMITASHUMTA na UMISSETA, Mwenyekiti wa TSC, Prof. Willy Komba ambaye alieleza kuwa TSC imekuwa na utaratibu wa kukutana na wadau mbalimbali wa Sekta ya Elimu na kuwapa uelewa juu ya sheria kanuni na taratibu za utumishi wa walimu ili kuwa na uelewa wa pamoja katika kuwahudumia walimu.
Aliongeza kuwa utekelezaji wa majukumu ya TSC kwa kiasi kikubwa unategemea sana ushirikiano kutoka ofisi ya mkurugenzi hususan Idara ya Elimu na
HABARI 17TSC YAWAPIGA MSASA MAAFISA ELIMU MIKOA, WILAYA
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
Mwenyekiti wa TSC, Prof. Willy Komba akitoa neno la ukaribisho katika kikao kilichowakutanisha TSC na Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri
wanaosimamia shule za msingi. Kikao hicho kilichofanyika hivi karibuni mjini Mtwara kililenga kutoa elimu kwa wadau hao kuhusu utekelezaji wa
majukumu ya TSC.
Katibu wa TSC, Paulina Nkwama akiongea mbele ya Maafisa Elimu na Maafisa Taluma (hawapo
pichani) katika kikao kilichofanyika hivi karibuni mjini Mtwara. Kikao hicho kililenga kutoa elimu kuhusu majukumu ya TSC katika kuwahudumia
walimu.
Mkurugenzi wa Ajira, Maadili na Maendeleo ya Walimu kutoka TSC, Christina Hape akiwasilisha
mada kuhusu Historia ya TSC katika kikao kilichowakutanisha Maafisa Elimu wa Mikoa,
Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri wanaosimamia shule za
msingi mjini Mtwara hivi karibuni.
HABARI 18
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
Utumishi ambazo ndizo zinazofanya kazi moja kwa moja na TSC katika kuwahudumia walimu.
Naye Katibu wa TSC, Paulina Nkwama alieleza kuwa Tume hiyo inatekeleza kazi zake kwa mujibu wa Sheria ya Tume ya Utumishi wa Walimu Na. 25 ya mwaka 2015 ambayo imeainisha majukumu mbalimbali yanayofanywa na Tume hiyo tofauti na baadhi ya watu wanaodhani TSC ipo kwa ajili ya kuwaadhibu walimu tu.
“Tume sio chombo ambacho kipo kwa
ajili ya kuwaadhibu walimu, bali tumejikita katika kuwaelimisha kuhusu sheria kanuni na taratibu za utumishi ili wajiepushe na makosa ya kinidhamu,” alisema Nkwama.
Katika mkutano huo mada tano ziliwasilishwa na wakurugenzi kutoka TSC Makao Makuu ambapo Mkurugenzi wa Ajira, Maadili na Maendeleo ya Walimu Chrisrina Hape alizungumzia juu ya historia ya Tume hiyo na kueleza kuwa tangu Nchi ipate uhuru, Serikali imekuwa na chombo cha kuwahudumia walimu.
Alisema kuwa lengo la kuwa na chombo mahususi kwa ajili ya walimu ni kusaidia kutatua changamoto mbalimbali ili mwalimu
TSC YAWAPIGA MSASA MAAFISA ELIMU MIKOA, WILAYA
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu kutoka TSC, Moses Chitama
akiwasilisha mada kuhusu Muundo wa TSC katika kikao kilichowakutanisha Maafisa Elimu wa Mikoa,
Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri wanaosimamia shule za
msingi mjini Mtwara hivi karibuni.
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria kutoka TSC, Wakili Richard Odongo akiwasilisha mada kuhusu
masuala ya sheria na hatua za kinidhamu kwa walimu katika kikao kilichowakutanisha Maafisa
Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri
wanaosimamia shule za msingi mjini Mtwara hivi karibuni.
Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia Nidhamu na Maadili ya Walimu kutoka TSC, Robert Lwikolela
akiwasilisha mada kuhusu Nidhamu na Maadili ya Walimu katika kikao kilichowakutanisha Maafisa
Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri
wanaosimamia shule za msingi mjini Mtwara hivi karibuni.
aweze kutoa elimu bora kwa wanafunzi.
Mada ya pili iliwasilishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Moses Chitama ambaye alieleza kuwa Tume hiyo inaundwa na Mwenyekiti, Katibu pamoja na wajumbe nane ambao wanatoka katika Ofisi mbalimbali za Serikali.
Aliongeza kuwa TSC ina ofisi katika ngazi ya wilaya ambapo
huongozwa na Kamati za Wilaya ambazo ndizo zinazohusika kutoa uamuzi wa masuala ya Ajira na Nidhamu kwa walimu, huku akieleza kuwa Katibu Msaidizi wa TSC ngazi ya Wilaya ndiye mtendaji mkuu wa shughuli za kila siku katika ngazi hiyo.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Huduma za Sheria, Wakili Richard Odongo alisema kuwa pale mwalimu anapokuwa ametenda kosa la kinidhamu na kuchukuliwa hatua, ni lazima haki zake ambazo zipo kwa mujibu wa sheria zizingatiwe.
Alitaja baadhi ya haki hizo kuwa ni mtuhumiwa kupewa hati ya mashtaka, kupewa
HABARI 19
Baadhi ya Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri wanaosimamia shule za msingi wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika kikao
kilichafanyika hivi karibuni mjini Mtwara.
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
TSC YAWAPIGA MSASA MAAFISA ELIMU MIKOA, WILAYA
Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia masuala ya Ajira na Maendeleo ya Walimu kutoka TSC, Mectildis Kapinga akiwasilisha mada kuhusu Ajira na Maendeleo ya Walimu katika kikao
kilichowakutanisha Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri wanaosimamia shule za
msingi mjini Mtwara hivi karibuni.
HABARI 20
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
muda wa kutosha kuwasilisha utetezi wake na pale ambapo kamati ya uchunguzi itaundwa kwa ajili ya kuchunguza shauri hilo mtuhumiwa ana haki ya kujulishwa siku, muda na mahali shauri lake litakaposikilizwa.
Aliongeza kuwa mtuhumiwa ana haki ya kusikilizwa, haki ya kuhoji mashahidi na kupatiwa nyaraka yoyote inayotumiwa kama ushahidi dhidi yake.
A k i z u n g u m z i a
masuala ya maadili na nidhamu kwa walimu, Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia masuala hayo, Robert Lwikolela alieleza kuwa walimu wana wajibu mkubwa wa kumlea mwanafunzi tangu akiwa mtoto hadi kufikia umri wa mtu mzima kwa kuwa muda mwingi wa mchana ambao ndio mtoto anautumia kujifunza yupo shuleni.
Alifafanua kuwa mwalimu mwenye maadili mema ataweza kutengeneza
mwanafunzi bora na hatimaye Taifa imara, hivyo walimu wanapaswa kuzingatia nguzo kuu za maadili ya kazi ya ualimu ili kuweza kumlea vizuri mwanafuzi kimwili, kiroho, kiakili na kijamii.
Mada nyingine ilihusu Ajira na Maendeleo ya Walimu ambayo iliwasilishwa na Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia masuala ya Ajira na Maendeleo ya Walimu, Mectildis Kapinga ambaye alieleza kuwa TSC
imhudumia mwalimu tangu anapoingia kwenye ajira hadi pale anapohitimisha utumishi wake.
Alitaja baadhi ya huduma ambazo TSC inatoa kwa mwalimu kuwa ni kusajili, kuthibitisha kazini, kupandisha cheo, kubadilisha cheo kwa mwalimu aliyejiendeleza kimasomo pamoja na kutoa kibali cha kustaafu kazi ya ualimu.
TSC YAWAPIGA MSASA MAAFISA ELIMU MIKOA, WILAYA
Baadhi ya Maafisa Elimu wa Mikoa, Maafisa Taaluma wa Mikoa pamoja na Maafisa Elimu wa Halmashauri wanaosimamia shule za msingi wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika kikao
kilichafanyika hivi karibuni mjini Mtwara.
Na Adili Mhina.
Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) i m e a z i m i s h a wiki ya utumishi
wa umma kwa kuweka utaratibu maalum wa kuhudumia wateja mbalimbali wanaofika ofisini hapo.
Utaratibu huo ni pamoja na kuwasikiliza wateja kutatua changamoto zao, kugawa vitabu na vipeperushi vinavyohusu taratibu za upatikanaji wa huduma kwa mujibu wa sheria ya Tume ya Utumishi wa Umma Na. 25 ya mwaka 2025 pamoja na Kanuni zake za mwaka 2016.
Wateja mbalimbali walihudhuria na kupatiwa huduma ambapo ofisi hiyo ilitenga eneo lake la ukumbi wa mikutano kwa ajili ya kuwasikiliza wateja kwa muda wa kuanzia saa moja na nusu asubuhi hadi saa tisa na nusu alasiri.
Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa
Umma kwa mwaka 2021 yamefanyika Juni 16-23, na yalikuwa na kaulimbiu inayosema ‘ kujenga Afrika tunayoitaka kupitia utamaduni wa uadilifu ambao unastawisha uongozi wenye maono hata katika mazingira ya migogoro’.
HABARI 21TSC YAENDELEA KUWAHUDUMIA
WATEJA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
Afisa Utumishi Mwandamizi kutoka TSC, Jenipha Maagi (kushoto) akimsikiliza mteja katika Wiki ya Utumishi wa Umma iliyofanyika Juni 16-23, 2021.
Mmoja wa wateja waliofika kupata huduma katika ofisi za TSC wakati wa Wiki ya Utumishi wa
Umma, akisoma kipeperushi kinachoelezea masuala mbalimbali ya utumishi wa walimu.
Maafisa wa TSC wakiwa katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo tayari kwa kuhudumia wateja
katika Wiki ya Utumishi wa Umma. Upande wa kushoto ni Peter Nassa akifuatiwa na Aisha Kayumba
(katikati) na upande wa kulia ni Key Musa.
Mtumishi wa TSC, Aisha Kayumba (aliyesimama) akimhudumia mteja katika Wiki ya Utumishi wa
Umma iliyofanyika Juni 16-23, 2021.
Adili Mhina.
Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Wilaya ya Mtwara ni miongoni mwa Ofisi za TSC zinazohudumia walimu
kutoka Halmashauri zaidi ya moja. Ofisi hiyo inahudumia Halmashauri tatu ambazo ni Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara, Halmashauri ya Mji Nanyamba pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara.
Wilaya ya Mwara ina jumla ya shule 208 za msingi na sekondari zinazomilikiwa na Serikali. Katika idadi hiyo shule 44 ni za Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara, 78 Halmashauri ya Mji Nanyamba na shule 86 ni za Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara.
Kwa upande wa Walimu, TSC Mtwara inahudumia walimu 2,149 ambapo walimu 832 ni wa Manispaa ya Mtwara, 561 Halmashauri ya Mji Nanyamba na walimu 756 ni wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara.
Jukumu la kuhudumia walimu wa halmasahuri hizo linabebwa na watumishi sita (6) ambao ndiyo wanaoendesha ofisi ya TSC katika Wilaya ya Mtwara. Watumishi hao ni Kaimu Katibu Msaidizi mmoja (1), Maafisa wanne (4) pamoja na Msaidizi wa Ofisi mmoja (1).
Duncan Bushiri ni Kaimu Katibu Msaidizi wa TSC Wilaya ya Mwara, anaeleza kuwa ofisi yake imefanya juhudi mbalimbali katika kuwafikia walimu katika halmashauri zote tatu japokuwa anakiri kuwepo kwa changamoto ya umbali kulingana na jiografia ya maeneo hayo.
“Mara nyingi walimu wanaohitaji kuhudumiwa wanakuja hapa ofisini lakini wakati mwingine tunapanga kufanya ziara kwenda kuwaona, kuzungumza nao na kutatua changamoto mbalimbali katika
MAKALA 22
Kaimu Katibu Msaidizi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Wilaya ya Mtwara, Duncan Bushiri akiwa anaendelea na majukumu
yake ya kila ofisini kwake.
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
Afisa anayesimamia Nidhamu na Maadili ya walimu katika ofisi ya TSC Wilaya ya Mtwara, Scholastica Millanzi akiwa anaendelea
kutekeleza majukumu yake ya kila siku.
TSC MTWARA, OFISI INAYOHUDUMIA HALMASHAURI TATU
MAKALA 23
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
maeneo yao ya kazi,” Duncan anaeleza.
Anafafanua kuwa kwa kiasi kikubwa ofisi yake imepata mafanikio katika kuwafikia walimu kutokana na ushirikiano anaoupata kutoka kwa wakurugenzi wa Halmashauri zote tatu.
“Kwa kiasi kikubwa tunapata ushirikiano kutoka kwa maafisa elimu, mara kwa mara wakiandaa mikutano yao wanatuita tunakwenda kutoa mada kwa walimu. Sisi hatuna magari ya kutembelea walimu lakini pale tunapohitaji kufanya hivyo wakurugenzi wanatusaidia,” anaeleza.
Katika eneo la nidhamu kwa walimu, Duncan anaeleza kuwa
ofisi yake inaendelea na mikakati ya kuwaelimisha walimu ili wasijiingize kwenye uvunjifu wa maadili na hivyo kupunguza mashauri ya nidhamu kwa kiasi kikubwa.
Kwa mujibu wa Kaimu Katibu huyo, mwaka 2018/2019 walimu 23 walifunguliwa mashauri ya nidhamu, 2019/2020 mashauri 7 na 2020/2021 mashauri 12 yalifunguliwa. Katika mashauri hayo makosa yanayoongoza ni utoro na kughushi nyaraka za uhamisho.
Pamoja na hayo, anaeleza kuwa kumekuwa na changamoto mpya ya baadhi ya walimu wa kiume kuvaa mavazi yasiyoendana na maadili ya kazi kulingana na Mwongozo wa Mavazi kwa Watumishi wa Umma kwa mujibu wa Waraka wa Utumishi wa Umma na. 5 wa mwaka 2020.
“Tatizo hili lipo zaidi katika Halmasahuri ya Mji Nanyamba, kule unakuta mwalimu anaingia darasani amaevaa t-shirt yenye mapicha, maandishi na chini unakuta amevaa ndala. Sio kwamba hawajui kuwa ni kinyume na taratibu za utumishi wa Umma
Kaimu Katibu Msaidizi wa TSC Wilaya ya Mtwara, Duncan Bushiri (wapili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya
watumishi wa TSC Wilaya ya Mtwara.
Afisa anayeshughulikia Ajira na Maendeleo ya Walimu kutoka TSC Wilaya ya Mtwara, Fakihi Maskati akiwa afisini kwake.
TSC MTWARA, OFISI INAYOHUDUMIA HALMASHAURI TATU
MAKALA 24
JARIDA LA TUME YA UTUMISHI WA WALIMU TANZANIA (TSC) JULAI 2021
lakini wanafanya hivyo kwa kuona kuwa wapo mbali hawaonekani kwa urahisi” alisema.
Anaeleza kuwa Wakuu wa Shule ambao ndiyo mamlaka ya kwanza ya nidhamu bado hawajatekeleza wajibu wao kikamilifu katika kusimamia walimu waliopo kweye shule zao, ndiyo maana wengine wanakiuka maadili kwa kuona kuwa hakuna anayewakemea.
Suala jingine linalojitokeza kwa kiasi kikubwa ni wimbi kubwa la walimu kutaka kuhama kutoka Mtwara kwenda maeneo mengine, kwa maelezo ya Duncan, hawa ni walimu ambao hawana muda mrefu kazini na wanaomba uhamisho wakitaka kwenda maeneo ya mjini.
Anaeleza kuwa walimu wengi wanaopangiwa vituo vya kazi maeneo ya pembezoni wanakuwa hawajajiandaa kufanya kazi katika mazingira yoyote na jambo hilo linawafanya baadhi yao kufanya kazi kwa kujilazimisha kwa kuwa hawataki kukubaliana na mazingira ya kazi.
Hata hivyo, Kaimu Katibu huyo anaona mazingira ya Mtwara kwa sasa ni mazuri kutokana na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika kuboresha miundombinu na huduma za jamii, hivyo walimu hawana sababu ya kutaka kukimbilia maeneo mengine.
“Unajua Serikali imefanya kazi kubwa ya kuboresha miundombinu, ukiangalia Mtwara ya sasa ni tofauti na zamani. Hakuna kitu ambacho
unakitafuta Mtwara ukakikosa, ni vizuri watumishi wetu hususan walimu wasiendelee kuishi na ile dhana ya zamani kuwa sehemu flani ni bora zaidi kuliko huku” alisema.
Kaimu Katibu Msaidizi huyo anaona kuwa TSC Mtwara kuhudumia Halmashauri tatu ni kazi kubwa inayoweza kusababisha walimu kutopata huduma vizuri na kufanya TSC isifikie malengo yake kwa wakati.
Duncan anaeleza kuwa umbali wa kutoka Ofisi za TSC hadi zilipo ofisi za Halmashauri ya Mji Nanyamba ni kilomita 70 na zilipo ofisi za Halmasahauri ya Wilaya ya Mtwara ni kilomita 40 hivyo inakuwa ni vigumu kwa TSC kuweza kuwafikia walimu wote kwa wakati.
“Kilomita 70
ninazozizungumzia ni kufika pale zilipo ofisi za Halmashauri, lakini ukisema utembelee shule utakuta kuna shule zipo mbali kwa takriban kilomita 200 kutoka hapa mtwara mjini. Sasa hapo unaweza ukaona changamoto inayoweza kutokea kwa mwalimu aliyeko huko anayehitaji kuja TSC kupata huduma,” anasema.
Duncan anashauri kuwa ni wakati mwafaka kuangalia upya Sheria ya Tume ya Utumishi wa Walimu Na. 25 ya mwaka 2015 ili Tume iwe na ofisi katika ngazi ya Halmashauri tofauti na ilivyo sasa ambapo TSC ipo katika ngazi ya Wilaya.
“Naona ni busara kwa sheria yetu kuangaliwa upya ili iruhusu kuwa na ofisi katika ngazi ya halmashauri. Tukiangalia walimu wote tunaowahudumia wapo kwenye halmashauri. Ninaamini lengo la Serikali ni kurahisisha utoaji wa huduma, hivyo tukiwa na ofisi ngazi ya halmasahuri tutakuwa tumewasaidia walimu kwa kiasi kikubwa,” alisema.
Mwonekano wa jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara ambapo ndipo zilipo ofisi za TSC Mtwara. Katika jengo hilo, TSC Mtwara
ilipewa chumba kimoja cha ofisi ambacho bado hakijakidhi mahitaji kulingana na idadi ya watumishi pamoja na walimu wanaohudumiwa
na Ofisi hiyo.
TSC MTWARA, OFISI INAYOHUDUMIA HALMASHAURI TATU
Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania tumeyautumishiwawalimutanzania
MAWASILIANO: Katibu, Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Walimu, Mtaa wa Mtendeni S.L.P 353, DODOMASimu: +255 (26) 2322402-4 Barua Pepe: [email protected] Tovuti: www.tsc.go.tz