28
UTOKEZO (AL-BADAA) Kimeandikwa na: Sayyid Abdul-Karim al-Bahbahani Kimetarjumiwa na: Abdul-Karim J. Nkusui

Utokezo al-Badaa

Embed Size (px)

DESCRIPTION

Maudhui ya Utokezo (Badaa’) yanazingatiwa kuwa ni kati ya masuala ya falsafa ya Kitawhidi ambayo yamechochea utafiti wenye wigo mpana baina ya maulamaa wa elimu ya falsafa, hiyo ni kutokana na yanayopatikana humo miongoni mwa masuala ya kina na ya muhimu.

Citation preview

UTOKEZO(AL-BADAA)

Kimeandikwa na:

Sayyid Abdul-Karim al-Bahbahani

Kimetarjumiwa na:

Abdul-Karim J. Nkusui

©Haki ya kunakili imehifadhiwa na:

AL-ITRAH FOUNDATION

ISBN: 978 - 9987 - 512 - 26 - 3

Kimeandikwa na:

Sayyid Abdul-Karim al-Bahbahani

Kimetarjumiwa na:Abdul-Karim J. Nkusui

Kimepangwa katika Kompyuta na:

Hajat Pili Rajab

Toleo la kwanza: Julai, 2009

Nakala: 1000

Kimetolewa na kuchapishwa na:

Alitrah Foundation

S.L.P. 19701 Dar es Salaam, Tanzania

Simu: +255 22 2110640

Simu/Nukushi: +255 22 2127555

Barua Pepe: [email protected]

Tovuti: www.alitrah.org

Katika mtandao: www.alitrah.info

YALIYOMO

1. Al – badau katika Qur’an tukufu............................................................2

2. Kauli za Maulama wa Shia ithna ashariyah juu ya Al-badau.................7

3. Nafasi ya itikadi na malezi yenye kujenga ya Al-badau......................10

4. Maswali juu ya itikadi ya Al-badau.......................................................13

5. Hitimisho...............................................................................................15

NENO LA MCHAPISHAJI

Kitabu kilichoko mikononi mwako ni tarjumi ya kitabu cha Kiarabu

kiitwacho, al-Badaa’. Sisi tumekiita, Utokezo.

Kitabu hiki ni matokeo ya kazi ya kielimu iliyofanywa na mwanachuoni

wa Kiislamu, Sayyid Abdul-Karim al-Bahbahani.

Kumekuwepo na kutokuafikiana katika miji yetu ya Kiislamu, hususanmiongoni mwa wanavyuoni kuhusu usahihi wa itikadi ya Badaa’ - yaaniutokezo wa jambo fulani kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Baadhi wanase-ma kwamba itikadi hii ni sahihi na wengine wanasema si sahihi. Baadhi yawanavyuoni wamekwenda mbali zaidi hadi kufikia kuwaita Waislamuwenzao wanaoitakidi juu ya Utokezo (Badaa’) kuwa ni washirikina aumakafiri.

Lakini je, Badaa’ haina asili katika dini? Ukweli ni kwamba ina asili kati-ka dini kama utakavyoona katika kitabu hiki.

Kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa maendeleo

makubwa ya elimu katika nyanja zote, ambapo uwongo, ngano za kale na

upotoshaji wa historia ni mambo ambayo hayana nafasi tena katika akili za

watu. Kutokana na ukweli huu, Taasisi yetu ya Al-Itrah Foundation imea-

mua kukichapisha kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili kwa madhumuni

yake yaleyale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji wa

Kiswahili, ili kuongeza ujuzi wao katika masuala ya dini na ya kijamii.

Tunamshukuru ndugu yetu, Abdul-Karim J. Nkusui kwa kukubali jukumu

hili la kukitarjumi kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote

walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa

kwake.

Mchapishaji:Al-Itrah FoundationS. L. P. 19701Dar-es-Salaam, Tanzania.

NENO LA JUMUIYA

Hakika mirathi ya AHLUL-BAYT ambayo imehifadhiwa na kambi yao na

wafuasi wao dhidi ya upotovu inaonyesha kambi iliyokusanya aina mbal-

imbali za taaluma za kiislamu.

Kambi hii imeweza kulea nafsi mbalimbali zilizo tayari kunywa kutoka

kwenye chemchemu hiyo, na kuupa umma wa kiislamu wanachuoni

wakubwa wenye kufuata nyayo za ujumbe wa Ahlul-Bayt.

Wanachuoni waliyokusanya vidodosa na maswali mbalimbali ya madhe-

hebu na mitazamo tofauti ya kifikra kuanzia ndani ya desturi ya kiislamu

hadi nje ya desturi hiyo, huku wao wakitoa majibu na utatuzi makini juu

ya maswali hayo ndani ya karne zote.

Jumuiya ya kimataifa ya Ahlul-Bayt imefanya hima kutetea tukufu za

ujumbe wa Uislamu na ukweli wake ambao umechafuliwa na makundi,

madhehebu na wanaharakati mbalimbali wenye chuki na uislamu.

Jumuiya imefuata nyayo za Ahlul-Bayt na za wafuasi wa kambi yao njema

ambayo imefanya hima kujibu madai yenye kuendelea na daima ikajaribu

kubaki ndani ya msitari wa mapambano kwa kiwango kinachohitajika

ndani ya kila zama.

Hakika uzoefu ambao umehifadhiwa ndani ya vitabu vya wanachuoni wa

kambi ya Ahlul-Bayt katika dhamira hii ni vya aina ya pekee, kwa sababu

una nguzo ya kielimu inayotegemea akili na hoja, huku ukijiepusha na

matamanio na uzalendo uliokatazwa.

Unazungumza na wasomi na wanaharakati wenye fani maalumu

mazungumzo ambayo yanaituliza akili na yanapokewa na maumbile sala-

F

ma.

Jaribio hili la Jumuiya ya kimataifa ya Ahlul-Bayt limekuja kuwapa

watafuta ukweli hatua mpya ya uzoefu wa thamani katika ulingo wa

mazungumzo na maswali na kujibu hoja za utata zilizotolewa zama zilizo-

pita au zinazotolewa leo kwa njia ya Tovuti, na hasa kwa kupewa nguvu na

baadhi ya nchi zenye chuki dhidi ya uislamu na waislamu.

Jumuiya imejiepusha na udadisi uliokatazwa na ni yenye kuhangaikia

kuzidadisi akili zenye kufikiria na nafsi zenye kutafuta haki ili ziweze

kufikia kwenye haki ambayo inatolewa na kambi ya Ahlul-Bayt ulimwen-

gu mzima, ndani ya zama ambazo akili inaerevuka na nafsi na roho zina-

boreka kwa kasi ya pekee.

Ni lazima tugusie kuwa mfululizo huu wa tafiti hizi umeandaliwa na

Kamati maalum toka jopo la wanachuoni watukufu, hivyo tunatoa shuku-

rani njema kwa hawa wote na kwa wasomi na wahakiki kwa kila mmoja

miongoni mwao kupitia sehemu ya tafiti hizi na kutoa mchango wao wa

thamani kuhusu tafiti hizi.

Tunategemea na kutaraji kuwa tutakuwa tumetoa kile tunachokiweza kati-

ka juhudi za kutekeleza baadhi ya wajibu tulio nao mbele ya ujumbe wa

Mtukufu Mola wetu Mlezi ambaye alimtuma Mtume Wake na uongofu na

dini ya haki ili aidhihirishe juu kuliko dini zote. Na Mwenyezi Mungu

anatosha kuwa shahidi.

JUMUIYA YA KIMATAIFA YA AHLUL-BAYT

KITENGO CHA UTAMADUNI

G

H

2

Utokezo (al-Badaa)

AL-BADAU KATIKA

QUR’AN TUKUFU

Maudhui ya Badau yanazingatiwa kuwa ni kati ya masuala ya falsafa ya

kitauhidi ambayo yamechochea utafiti wenye wigo mpana baina ya maula-

maa wa elimu ya falsafa, hiyo ni kutokana na yanayopatikana humo mion-

goni mwa mas’ala ya kina na ya muhimu.

Al-Badau katika lugha: Ina maana ya kudhihiri baada ya kufichikana, na

inatumika katika mijadala ya kawaida katika nyanja za kubadilishana rai,

fikra, maoni, malengo na makusudio. Hivyo husemwa: “Rai yake ilikuwa

hivi kisha akabadili.”

Ni dhahiri kwamba Al-Badau kwa maana hii ni kutotambua jambo mwan-

zo kisha ukalitambua baadaye na yote mawili hayapatikani kwa Mwenyezi

Mungu (s.w.t.) kwa sababu elimu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ni ya

dhati ambapo haijatanguliwa na ujahili. Lakini tukichunguza Al-Badau

katika maana yake ya kilugha tunaikuta inaundwa na vitu viwili:

Ujahili wa mwanzo na elimu mpya.

Kubadilika kwa rai, nia na malengo kufuatana na elimu mpya aliyoipata.

Kisha tunaulizana ni kipi kati ya hivi viwili kinapingana na tawhidi? Cha

kwanza au cha pili au vyote viwili?

Je, kuna uwezekano wa kutenganisha baina yake kiasi kwamba tunasal-

imika na aina ya kubadili na kugeuza ambapo hakutokani na ujahili

uliotangulia wala elimu inayokuja baadaye?

Ama kuhusiana na suala la kwanza: Kwa wepesi tunaona kwamba jambo

la kwanza linapingana na tawhidi na hakuna Mwislamu anaekubali kuna-

3

Utokezo (al-Badaa)

sibisha ujahili kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na wala hatuhitaji kuleta

aya wala riwaya juu ya hilo.

Ama suala la pili: Ikiwa mabadiliko yanalazimiana na dhati ya kuwepo

ujahili wa awali na kupatikana kwa elimu baadaye basi hali hii inapingana

na tawhidi pia. Kama ambavyo ujahili unapingana na tawhidi vivyo hivyo

unapingana na kila mabadiliko na mageuzi yanayosababishwa na hilo. Na

ikiwa mabadiliko yana sababu nyingine katika hali hii hayapingani na

tawhidi.

Kubadili rai na mtazamo – mfano - ni kati ya mambo ya lazima ya dhati

kwa ajili ya kudhihiri elimu na kuondoka kwa ujahili, hivyo basi hai-

wezekani kunasibisha ujahili kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Vivyo

hivyo haiwezekani kunasibisha mabadiliko ya rai na mtazamo kwa

Mwenyezi Mungu Mtukufu. Bali dhana ya rai na mtazamo peke yake hai-

wezekani kunasibishwa kwa Mwenyezi Mungu tukiachilia mbali mabadi-

liko na mageuzi kwa sababu dhana hii inategemea maana ya kupata na

kujifunza elimu, na elimu ya Mwenyezi Mungu haipatikani kwa njia ya

kujifunza hadi isemwe kuwa huu ni mtazamo wa Mwenyezi Mungu na rai

yake bali ni elimu ya dhati na inasimama juu ya dhati yake.

Baada ya jawabu la maswali mawili kuwa wazi tunajaribu kutazama

Qur’anTukufu ili tuangalie je, kunapatikana aya inayonasibisha mabadi-

liko au mageuzi katika jambo miongoni mwa mambo au nyanja kati ya

nyanja?

Kuna ambao wanafanya haraka kusema Qur’an inakataa kuwepo mabadi-

liko au mageuzi kwa Mwenyezi Mungu na hiyo ni kutokana na kauli yake

(s.w.t.): “Lakini hutopata mabadiliko katika kawaida ya Mwenyezi

Mungu”1 na kauli yake (s.w.t.): “Na wala hutopata mabadiliko katika

kawaida ya Mwenyezi Mungu.”2

1 Suratu Fatir: 432 Suratul Ahzab: 62

4

Utokezo (al-Badaa)

Ila jawabu hili halitoshelezi kwa sababu uhalisia wa Qur’ani ni jambo

linalotokana na Qur’ani yote na kinachopatikana katika upande mmoja tu

hakiwakilishi isipokuwa nusu ya Qur’ani kwa sababu kinatokana na

upande mmoja tu wa Qur’ani Tukufu.

Kuna upande mwingine umenasibisha mabadiliko na mageuzi kwa

Mwenyezi Mungu Mtukufu mfano kauli yake (s.w.t.): “Mwenyezi Mungu

hufuta ayatakayo na huimarisha (anayoyataka) na asili ya hukumu

iko kwake.”3 Na kauli yake (s.w.t.): “Hakika Mwenyezi Mungu

habadilishi yaliyoko kwa watu hadi wabadilishe yaliyoko katika nafsi

zao.” 4

Aya ya kwanza inaonyesha kwamba Mwenyezi Mungu anafuta na

kuthibitisha na katika hilo kunaashiria mabadiliko na mageuzi.

Ama Aya ya pili imeweka wazi kwamba Mwenyezi Mungu anabadilisha

hali za watu pindi wanapobadilisha yaliyopo katika nafsi zao. Hivyo hali

ya kidini na kisiasa ya watu ni makadirio ya kiungu yanakubali mabadiliko

pindi watu wanapoamua kubadilisha hali zao za kinafsi na kiutamaduni

kutoka katika shirki kwenda kwenye imani, na kutoka kwenye upotovu

kwenda kwenye uongofu. Hivyo kuna makadirio ya aina mbili, makadirio

ya kiungu katika hali ya watu katika utii na makadirio ya kiungu katika hali

zao katika maasi. Wanapochagua utiifu anawapitishia makadirio ya mwan-

zo, na wanapochagua uasi anawapitishia makadirio ya pili. Na aina hii Aya

na riwaya zimeonyesha kuathiri baadhi ya vitendo katika riziki, vifo na

balaa.

Na haya hayakatai yeyote kati ya Waislamu bali ikhitilafu inatokea katika

uelewa wa badau ilipochukuliwa kwa maana yake ya kilugha inayopin-

gana na tawhidi, na ikhitilafu inaisha inapogundulika kuwa makusudio

3 Suratu Raad: 394 Suratu Raad: 11

5

Utokezo (al-Badaa)

yake ni maana ya kiistilahi isiyolazimu kunasibisha ujahili kwa Mwenyezi

Mungu (s.w.t.). Hakika makusudio ya badau kwa Ahlul–Bait (a.s.) ni

kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamkadiria mja wake kulingana na

hali fulani kisha Mwenyezi Mungu anabadilisha makadirio yake kutokana

na hali mpya inayodhihiri kwa mja kutokana na amali fulani anayoifanya,

pamoja na kutambua Kwake tangu awali mambo yote mawili na hali zote

mbili. Na lau wangefahamu maana hii wangetambua kuwa ni kati ya

mambo ambayo Waislamu wanaafikiana juu yake na ikhitilafu ipo katika

matamshi tu.

Amesema kweli Allammah as-Sayid Abdul-Husein Sharaf Diyn alipose-

ma: “Ikhitilafu katika mas’ala haya baina yetu na Ahlus-Sunna ni ya

matamshi tu.”

Kisha amesema: “Aking’ang’ania asiyekuwa sisi tutamtaka arejee katika

hukumu yake, hivyo abadilishe tamko la badau kama anavyotaka lakini

amuogope Mwenyezi Mungu kwa ndugu yake muumini.”5

Na kabla yake alishaandika Sheikh Al-Mufiyd: “Ama kutamka tamko la

badau, hakika nimelifahamu kupitia yaliyopokewa baina ya mja na

Mwenyezi Mungu Mtukufu na lau kusingepokewa ambayo najua usahihi

wake basi nisingekubali kutamka. Kama ambavyo lau nisingepokea kwam-

ba Mwenyezi Mungu anakasirika na anaridhika, anapenda na kuchukia

basi nisingesema hayo. Ninasema kwa maana ambayo haipingwi na akili

na hakuna ikhitilafu baina yangu na Waislamu wote katika mlango huu,

bali amekhalifu aliyewapinga katika tamko bila ya kupinga maana yake, na

nimeshaeleza sababu yangu ya kusema hayo kwa kifupi, na huu ndio msi-

mamo wa Mashia wote na kila aliyewakhalifu katika madhehebu anapinga

niliyoyaeleza kwa jina tu bila ya kupinga maana yake na wala hayaridhii.”6

5 Ajiwibatul-Masa’ail Jarullah Uk: 796 Awaailul Maqalaat Uk: 92 - 93

6

Utokezo (al-Badaa)

Na kabla yake amesema Imamu Swadiq (a.s.) katika tafsiri ya kauli yake

(s.w.t.): “Mwenyezi Mungu anafuta ayatakayo na huimarisha anay-

otaka na asili ya hukmu iko kwake.” Kila jambo analolitaka basi liko

katika elimu yake kabla ya kulifanya, hakuna kitu kinachodhihiri ila kil-

ishakuwa katika elimu yake. “Hakika Mwenyezi Mungu hakidhihiri kitu

kwake ambako kunatokana na kutotambua.”7

Na amesema (a.s.): “Mwenye kudai kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu

linadhihiri kwake jambo asilolijua basi jitengeni naye.”8

Kisha nguvu ya hoja za Shia katika mas’ala ya badau ni mambo matatu:

Kauli yake (s.w.t.): “Mwenyezi Mungu anafuta ayatakayo na kuimar-

isha ayatakayo na asili ya hukumu iko kwake.”9 Na kauli yake (s.w.t.):

“Humuomba Yeye kila kilichomo mbinguni na ardhini kila siku Yeye

yumo katika mambo.”10

Kufanana mas’ala ya kufuta (nasikh) katika sharia, na badau ni nasikh

katika maumbile, na nasikh ni badau ya kisharia, kama ambavyo waislamu

wamethibitisha nasikh katika sharia kama vile kubadili kibla toka

Masjidul-Aqsaa kuelekea Al-Ka’aba tukufu na hakukhalifu yeyote kati yao

hilo, na hajazingatia yeyote kuwa hilo linakhalifu elimu ya milele ya

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) wala hailazimu kuthibiti ujahili wa mwanzo,

vivyo hivyo katika badau na kubadilika katika hukumu za maumbile bila

ya kulazimu ujahili wa mwanzo wala haikhalifu elimu ya Mwenyezi

Mungu ya milele, kama yeyote atapinga badau basi upinzani wake pia

utapinga nasikh na atakayoyataja katika mas’ala ya nasikh basi tunaweza

kuyajibu pia katika mlango wa badau bila ya tofauti yeyote baina ya

mambo hayo mawili.

7.Bihrul Anuwari Juz: 4 uk: 121 Hadith Na.: 63

8 " " " " : 30 9.Suratu Rad: 39

10. Suratu Rahman: 29

7

Utokezo (al-Badaa)

Mushkeli katika badau ni kukariri mushkeli waliotoa mayahudi juu

nasikh katika sharia, ambapo wao wanaona ubatili wa hilo na

kutowezekana kunasibisha nasikh kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu,

kama ambavyo wamejibu maulamaa wa Kiislamu kwa mushkeli huu

na kuthibitisha kwao uwezekano wa nasikh katika sharia bila kulazimu

upungufu wowote katika uungu wake mtukufu inawezekana kutumiwa

katika nasikh katika ulimwengu wa kimaumbile na mamlaka.

Kitendo huathtiri katika maisha ya mwanadamu, na huu ni ukweli wa

Qur’ani uliothibiti kwa kuongezea yaliyopo katika Sunna za Nabii

(s.a.w.w.) kwa kutilia mkazo, nayo ni kwamba amali za mwanadamu

imani, shiriki, utii, maasi wema kwa wazazi wawili na kuwaasi kwao,

kuwasaidia mafakiri, kutoa, kuunga udugu na kuukata n.k kunaathiri kati-

ka riziki, baraka, kurefusha umri na furaha. Na mambo haya Qur’ani imey-

ataja mara nyingi na Sunna zinaunga mkono mara nyingi na Qur’ani

imeyafupisha kwa kusema: “Hakika Mwenyezi Mungu habadilishi

yaliyopo kwa watu hadi wabadilishe yaliyopo katika nafsi zao.”

Na ambaye anapinga badau lazima atambue kwamba upinzani wake

unapelekea kupinga mfano wa ukweli huu ulio wazi, na ikiwa anauamini

basi atambue ya kuwa haya anayoyaamini ndio ambayo Shia wanayoyaita

al-Badau.

KAULI ZA MAULAMAA WA SHIA

KATIKA BADAU

Hii ndio maana ya badau ambayo maulamaa wa Shia waliotangulia na

waliokuja baadae wametilia mkazo. Sheikh Mufiyd anasema: “Kauli ya

Shia katika al-badau njia yake ni ya kusikiwa na wala sio ya kutafakari, na

makusudio yake sio kubadili rai na kutambua jambo lililokuwa

limefichikana kwake, vitendo vya Mwenyezi Mungu vyote viko dhahiri

kwa viumbe vyake kabla hata ya kuvimba, navyo vinatambulikana Kwake

8

Utokezo (al-Badaa)

na bado vingali vinatambulika.”11

Sheikh Tusi amesema: “Al-Badau katika lugha ni kudhihiri, hivyo

husemwa umedhihri kwetu uzio wa mji na imetudhihirikia rai …”

Ama likinasibishwa tamko hili kwa Mwenyezi Mungu humo kuna ambayo

hayafai kunasibishwa Kwake; Ama ambayo yanafaa ni ambayo yanakusu-

dia nasikh (kufuta) na kunasibisha hayo Kwake kuna wigo mpana, katika

upande huu yanachukuliwa yote yaliyopokelewa kutoka kwa wakweli

miongoni mwa habari zenye maana ya kunasibisha badau kwa Mwenyezi

Mungu bila ya kunasibisha yasiyofaa kwake miongoni mwa kutambua

baada ya kutotambua, na wajihi wa kuyasema hayo ni kwamba ikiwa

yanayoonyesha nasikh inayodhihiri kwa mkalafu ambayo hayakuwa

dhahiri kwao na kupata kwao elimu baada ya kutokuwa nayo, hayo huitwa

“Al–badau.”12

Na amesema As-Sayyid Abdallah Shubar: “Al-Badau ina maana nyingi,

baadhi yake zinajuzu na zingine hazijuzu nayo ni - kwa fatiha na madda

-aghlab hutumika katika lugha kwa maana ya kudhihiri kitu baada ya

kufichikana na kupata elimu kwayo baada ya kutojua.

Na umma umeafikiana kukanusha hayo kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ila

yale ambayo hayachupi mpaka Kwake, na mwenye kunasibisha hayo kwa

Shia basi ameshawazulia uongo na Shia wako mbali nao.”13

As-Sayyid Abdul-Husein Sharaf Diyn amesema: “Na matokeo wanayose-

ma Shia hapa ni kwamba Mwenyezi Mungu anapunguza riziki na

kuongeza humo, vivyo hivyo katika vifo, afya maradhi furaha, matatizo,

mitihani, balaa, imani ukafiri n.k. kama ilivyosema kauli Yake tukufu:

“Mwenyezi Mungu hufuta atakayo na kuimarisha ayatakayo na asili

11 Taswihihul-Itiqaadatil Imamiyah Uk; 66 chapa ya Darul Mufiyd12 Maswabihu Durar Juz: 1 Uk: 3313 Udstul–Usul Juz: 2 Uk: 29

9

Utokezo (al-Badaa)

ya hukumu iko kwake.”14 Na huu ndio mtazamo wa Umar bin Khattab

na Ibnu Mas’ud, Abi Wail na Qatadah. Na amepokea Jabir kutoka kwa

Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) na wengi wa Salaf wanaomba na

kunyenyekea kwa Mwenyezi Mungu awajaalie wawe wema na wala wasi-

we waovu, na yamepokewa hayo kwa tawaatur kutoka kwa Maimamu

wetu katika dua zao zilizopokelewa, na imepokewa katika Sunna kwamba

sadaka kwa namna yake, wema kwa wazazi wawili, kufanya wema, haya

yanabadili uovu kuwa wema na yanaongeza umri.

Na imesihi kwa Ibnu Abbas kwamba yeye amesema: “Tahadhari hainu-

faishi kitu katika Qadar lakini Mwenyezi Mungu anafuta kwa dua anay-

otaka miongoni mwa Qadar.” Hii ndio badau ambayo wanaisema Shia,

inajuzu kuinasibisha badau kwake kwa uhusiano wa kufanana. Ikhitilafu

katika hili baina yetu na Ahlus-Sunna ni ya matamshi tu, na anayosema

Shia katika badau kwa maana tuliyoitaja wanaisema Waislamu wote.15

Sheikh Agha Bazarak at-Twaharaniy anasema: “Al-Badau maana yake

katika lugha ni kudhihiri rai ambayo haikuwepo na kusahihisha kitu kili-

chojulikana baada ya kutojulikana, lakini haifai kunasibishwa kwa

Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kulazimu kudhihiri rai juu ya kitu amba-

cho hakikuwepo kwa kutokijua Kwake awali au kushindwa Kwake na

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ametakasika na hayo.

Al-Badau wanayoisema Shia ni kwa maana ambayo lazima kila mwislamu

anaitakidi mkabala na wayahudi wanaosema kwamba Mwenyezi Mungu

amemaliza kazi hivyo hakidhihiri kitu chochote kwake: “Mkono wa

Mwenyezi Mungu umefumba” au mwenye kufuata kauli za wayahudi

wenye kudai kwamba Mwenyezi Mungu ameumba vyote vilivyopo mara

moja hivyo hakuna kitu ila alichokiumba awali au alikuwa anaitakidi

mfumo wa ulimwengu kwa kusema kwamba Mwenyezi Mungu ameumba

14 Suratu Raad: 3915 Ajuwibatu Masaail Jarullah Uk: 101 -103

10

Utokezo (al-Badaa)

mfumo wa ulimwengu nao uko nje umevuliwa katika mamlaka yake, mifu-

mo mingine ndio inaoiendesha, ambapo lazima kila mwislamu akanushe

kauli hizi na aitakidi kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu “ kila siku

yuko katika mambo”16

NAFASI YA ITIKADI NA MALEZI YENYE

KUJENGA KATIKA BADAU

Imedhihiri katika yaliyotangulia kwamba al- badau ina maana ya Qur’ani

imeenea baina ya waislamu wote na kwamba Shia hawatofautiani na wais-

lamu wengine isipokuwa katika jina ambalo kwalo linafahamika kosa la

kunasibisha ujahili kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na imebainika kutosi-

hi kunasibisha huku, na kilicho muhimu kwetu sasa ni kueleza upande

mwingine wa utafiti, nao ni umuhimu wa fikra ya badau kuhusu itikadi ya

mwanadamu mwislamu, kwani fikra zinapimwa kwa misingi yake ya kie-

limu na hoja zake za kimantiki na kwa malengo yake na matunda yake kwa

upande mwingine.

Na katika maudhui ya badau inaweza kusemwa kwa njia ya kuuliza: Ikiwa

makadirio ya awali hayatakuwa na kazi bali yatamalizikia kwa kufutwa,

nini faida ya kutoa taarifa juu yake? Na nini matunda yanayopatikana kwa

kuitakidi al-Badau wakati huo?

Jawabu: Hakika kuitakidi al-Badau kunarejea kwenye umuhimu mkubwa

sana katika pande mbili: Upande wa itikadi na upande wa malezi.

Ama upande wa kiitikadi yanatutosha maneno ya Allammah al-Majlisiy

ambapo ameandika anasema: “Hakika wamevuka mpaka katika al-Badau

kwa kuwajibu Wayahudi ambao wanasema: “Hakika Mwenyezi Mungu

amemaliza kazi na utawala.” Na baadhi ya Mu’tazila wanasema: “Hakika

16 Suratu Rahman: 29

11

Utokezo (al-Badaa)

Mwenyezi Mungu ameumba viumbe mara moja kama ilivyo hivi sasa

miongoni mwa madini, mimea, wanyama, wanadamu, na wala kuumbwa

Adamu hakujatangulia kuumbwa watoto wake, na kutangulia ni katika

kudhihiri kwake sio katika kuumbwa kwake na kuwepo kwake, bali

wamechukua makala haya kwa watu wa falsafa wenye kusema kuhusiana

na mfumo wenye kuendesha ulimwengu, na wenye kusema kwamba mam-

laka ya Mwenyezi Mungu hayakuathiri isipokuwa katika uumbaji wa awali

tu, hivyo wao wanamuengua Mwenyezi Mungu (s.w.t.) katika mamlaka

Yake na wananasibisha uendeshaji kwenye mfumo wa ulimwengu na wala

sio kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.” 17

Kwa maana kwamba mkazo wa Maimamu (a.s.) juu ya al-Badau umekuja

ili kubatilisha kila fikra zinazofanya uwezo wa Mwenyezi Mungu na

matakwa Yake (s.w.t.) kuwa na kiwango maalum, na kuthibitisha kuwa ni

uhakika wa jumla kwa pande zote hata katika upande wa Qadar ambayo

anaikadiria Mwenyezi Mungu Mtukufu mwenyewe katika ulimwengu wa

maumbile, uumbaji, uendeshaji na malezi. Na kwamba makadirio ya

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) katika makadirio hayo, hayamfanyi kuwa ni

mwenye kupokonywa hiari Yake na matakwa Yake kutokana na hayo.

Kama ambavyo al-Badau imekuja ili kutilia mkazo juu ya hiari ya

mwanadamu na matakwa yake wakati wa kubainisha uwezo wa kiungu,

humo kuna Lauhul-Mahfuudh haikubali mabadiliko, na Lauhu nyingine ni

ya kufuta na kuthibitisha ambayo anayakadiria Mwenyezi Mungu (s.w.t.)

tangu mwanzo wa kuumba, hii inakubali mabadiliko kulingana na anayoy-

afanya mwanadamu miongoni mwa amali katika dunia. Kana kwamba

itikadi ya al-Badau imekuja ili kukamilisha itikadi ya Qadhwaa na Qadar

ili kuondolewa “Ghuluu” kuchupa mpaka na kufifiliza katika itikadi ya

Qadhwaa na Qadar, na isichukuliwe kwa maana ambayo itapokonya hiari

kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na kwa mwanadamu. Hivyo hakuna budi

kuikamilisha kwa itikadi ya badau ambayo imekuja kutilia mkazo kwam-

17 Biharul-Anwar Juz: 4, Uk: 129 – 130 chapa ya Tehran

12

Utokezo (al-Badaa)

ba Qadar haifikii kiwango cha kupokonya hiari ya Mwenyezi Mungu wala

haipokonyi hiari ya mwandamu.

Na katika upande wa malezi tunaona kwamba itikadi ya al-Badau ina

athari ya kimalezi yenye kujenga katika maisha ya wanadamu, na

Allammah al-Majlisiy anabainisha athari hii katika kukamilisha maana

yake yaliyopita juu ya sababu za kutilia mkazo Maimamu (a.s.) juu ya al-

Badau, ambapo kwanza anataja faida ya kuitakidi ambazo tumezitaja na

akaongezea kwa kutaja faida ya kimalezi kwa kusema: “Hivyo Maimamu

(a.s.) wakakataza hayo na wakathibitisha kwamba (s.w.t.) kila siku yuko

katika kazi miongoni mwa kuondoa, kuleta kingine, kumfisha mtu na

kumhuisha mwingine, n.k. ili waja wasiache kunyenyekea kwa Mwenyezi

Mungu, kuomba, kutii, kujikurubisha kwake kwa yale yanayofaa katika

mambo ya dunia yao na akhera yao, na ili wataraji wanapotoa sadaka kwa

mafakiri, kuunga udugu, kuwafanyia wema wazazi wawili, kufanya mema

na ihsani kwa yale waliyoahidiwa katika kuongezewa umri na kuongeze-

wa riziki.”

Na katika upande mwingine itikadi ya al-Badau ni kuhamasisha juu ya

uzuri wake katika itikadi ya toba na masharti ya kukubaliwa mbele ya

Mwenyezi Mungu, kama ambavyo toba ina athari nzuri katika kumjenga

mwanadamu, na kwa upande mwingine ni kufunga mianya ya kukata

tamaa na kufungua milango ya matumaini na matarajio na kujenga moyo

wa mageuzi na maandalizi ya mafanikio, vivyo hivyo badau ina athari hii

katika maisha ya mwandamu, bali badau ni dharura kati ya dharura za toba

na vigezo vyake ni katika amali, kwani kati ya dharura za toba ni mwenye

kutubia kuitakidi kwamba kalamu ya Mwenyezi Mungu bado wino wake

haujakauka katika ubao wa kufuta na kuthibitisha, hivyo Mwenyezi

Mungu anaweza kufuta na kuthibitisha anayotaka, anamneemesha

amtakaye na kumfanya amtakaye kuwa muovu kulingana na anavyojipam-

ba mja miongoni mwa tabia njema na amali njema, au kulingana na anavy-

ofanya amali mbaya, na wala matakwa ya Mwenyezi Mungu hayaji bure

bure tu, bila ya kudhibitiwa na hekima. Bali lau mja akitubu na kutekeleza

13

Utokezo (al-Badaa)

ya wajibu na kushikamana na wema anatoka katika kundi la watu waovu

na kuingia katika kundi la waja wema, na kinyume chake pia ni sahihi.

Na katika hayo yote tunaweza kufahamu maana ya maneno ya Maimamu

(a.s.) kwamba: “Hajaabudiwa Mwenyezi Mungu kwa chochote mfano wa

anavyoabudiwa kwa badau.”18 Na wala “Hajatukuzwa Mwenyezi Mungu

mfano wa anavyotukuzwa kwa al-Badau.”19 Na “Mwenyezi Mungu haja-

tuma Nabii hadi achukue kwake ahadi ya mambo matatu: Kukubali ibada

ya Mwenyezi Mungu, kuivua shirki, na kwamba Mwenyezi Mungu hutan-

guliza ayatakayo na huchelewesha ayatakayo.” 20

MASWALI KUHUSU ITIKADI YA BADAU

Hapa tunatoa maswali yanayotaka majibu yenye kutosheleza nayo:

1. Hakika kauli ya al-Badau inasababisha Mwenyezi Mungu kufanya upu-

uzi kwani pamoja na kutambua yatakayotokea kwake miongoni mwa

mabadiliko na kudhihiri, basi kutoa taarifa kwa makadirio ya mwanzo

itakuwa ni upuuzi?

Jawabu: Hakika itakuwa ni upuuzi kama tutajaalia kutokuwepo lengo na

manufaa yanayotarajiwa kutokana na kutoa taarifa ya makadirio ya

mwanzo, na haya ni ambayo hatuwezi kuyathibitisha, hivyo

inawezekana kuwepo lengo na manufaa yanayorejea kwa mja kwa faida

kubwa kutokana na taarifa hiyo.

2. Hakika Nabii au Imamu akitoa taarifa ya kitu kisha ikatokea al-Badau

katika kutokea kwake, ni lazima ategemee katika taarifa yake ya awali

kwenye kitu kinachokuwa ni chanzo (rejea) cha taarifa yake na asili ya

chanzo cha elimu yake, sasa ni kwa jambo gani atategemea Nabii au

Imamu katika taarifa yake ya awali?

18 Usulul-Kafiy Juz: 1, Uk: 14619 Usulul-Kafiy : Jz. 1, Uk. 146 kitabu Tawhid Babul-Badai20 Usulul-Kafiy : Jz. 1, Uk. 146 kitabu Tawhid Babul-Badai

14

Utokezo (al-Badaa)

Jawabu: Inahitaji kubainisha mfano kama lau mwanadamu akila sumu

yenye kuangamiza inayosababisha kifo chake hakika utakapoona tukio hili

unaweza kumpa taarifa ya kutokea kifo chake baada ya masaa, nayo ni

habari ya kweli kulingana na hali halisi isiyo na shaka, na kama mauti

hayakutokea kwa sababu ya kutokea kizuizi kisichotarajiwa kama vile

kutokea tabibu wa kumtibu mwenye ujuzi wa hali ya juu, taarifa hiyo haiwi

ya uongo wala haihesabiwi kuwa ni taarifa isiyo na chanzo, vivyo hivyo

katika taarifa ya mbinguni ambayo inatoa taarifa za kutokea baadhi ya

mambo katika siku zijazo, kwani ni za kweli kulingana na hali ya

kutokuwepo na kizuizi wala hakuna ubaya katika jambo hili isipokuwa

kutotambua Nabii au Imamu kupatikana kwa kizuizi hapo baadae. Hivyo

tuseme kwamba Mwenyezi Mungu amempa Nabii taarifa ya jambo na

hakutaka kumpa taarifa ya kutokea kwa kizuizi baadaye kwa maslahi

yanayohusiana na waja.

3. Hakika kutokea badau inasababisha Nabii au Imam kutuhumiwa kwa

uongo.

Jawabu: Hakika kutuhumiwa Nabii au Imamu kwa uongo ni jambo amba-

lo dhambi yake inamwangukia mwenye kulifanya, na tuhuma kama itato-

ka kwa kafiri basi hii sio ajabu kwake baada ya kukataa kuamini asili ya

tawhidi, utume na marejeo, na kama itatoka kwa muumini tunajaalia kuwa

imani yake itamzuia juu ya hilo, na kama haitamzuia basi hiyo ni dalili ya

udhaifu wa imani yake.

Cha muhimu ni kwamba badau sio sababu ya kimantiki ya kumtuhumu

kwa uongo bali hali nyingi za badau zilikuwa zikiambatana na

yanayosadikisha ukweli, kama ilivyo katika kisa cha Ibrahim (a.s.) pale

alipoamrishwa kumchinja mtoto wake, kwani amri mpya ya fidia ina-

maanisha kusadikisha amri ya awali ya kumchinja Ismail (a.s.) na kama

hiyo taarifa ya awali haikuwa ya kweli basi amri ya kuchinja kondoo

isingekuja ni fidia badala yake, hivyo fidia ni kwa maana ya badala.

15

Utokezo (al-Badaa)

HITIMISHO

Hakika al-Badau kwa maana ya kubadili rai haitokei kwa Mwenyezi

Mungu na wala Shia hawasemi hivyo, bali wanasema kutowezekana hilo

na ukafiri wa mwenye kusema hivyo, na kwamba inalazimu kujiepusha na

anayesema hivyo.21

Ndio, al-Badau inayokubaliwa na ambayo ni wajibu kuitakidi kwayo

imeelezwa na Aya za Qur’ani tukufu: “Mwenyezi Mungu anafuta

ayatakayo na huimarisha anayoyataka na asili ya hukumu iko

kwake.”

Na kufuta huku na kuimarisha kunakuwa wazi na kuthibiti katika anayoy-

adhihirisha Mwenyezi Mungu miongoni mwa mambo kwa ulimi wa Nabii

wake au Walii wake katika dhahiri kwa masilahi yanayohitajia kudhi-

hirishwa, kisha anayafuta na yanakuwa yale yasiyodhihiri mwanzo pamo-

ja na kutambua hilo tangu mwanzo kwa elimu yake. Badau inafanana na

nasikh (kufuta) hukumu za kisharia zilizotangulia kabla ya Nabii

Muhammad (s.a.w.w.) au nasikh ya baadhi ya hukumu ambazo zimekuja

katika sharia ya Nabii wetu (s.a.w.w.) kwa hukumu zilizofuata baadaye.22

Hakika ambaye haamini itikadi hii ya badau basi atakuwa amemuwekea

Mwenyezi Mungu kikomo katika uwezo Wake na matakwa Yake yasiyo na

mpaka, kama ilivyoashiria Qur’ani tukufu juu ya hilo katika itikadi ya

kiyahudi kwa kauli yake: “Wamesema Wayahudi mkono wa Mwenyezi

Mungu umefumba, bali imefumba mikono yao.”23 Na haya ndio

ambayo yameenea kwa baadhi ya makundi ya Kiislamu yasiyokuwa Shia

Ithina Ashariyah.

21 Aqaidul-Imamiyah cha Mudhafar uk: 45 chapa ya pili ya Najaf

22 Aqaidul-Imamiyah cha Mudhafar uk: 45 chapa ya pili ya Najaf

23 Suratul Maida: 64

ORODHA YA VITABU VILIVYO CHAPISHWA NA

AL-ITRAH FOUNDATION:

1. Qur'an Al-Kariim - Tafsir Al-Kashif Juzuu ya kwanza mpaka

Ishirini na Nne

2. Uharamisho wa Riba

3. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya kwanza

4. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya pili

5. Hekaya za Bahlul

6. Muhanga wa Imamu Husein (A.S.)

7. Mikingamo iliyomzunguka Imamu Ali (A.S.)

8. Hijab vazi Bora

9. Ukweli wa Shia Ithnaashari

10. Madhambi Makuu

11. Mbingu imenikirimu

12. Abdallah Ibn Saba

13. Khadijatul Kubra

14. Utumwa

15. Umakini katika Swala

16. Misingi ya Maarifa

17. Kanuni za Ndoa na maadili ya Familia

18. Bilal wa Afrika

19. Abudharr

20. Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu

21. Salman Farsi

22. Ammar Yasir

23. Qur'an na Hadithi

24. Elimu ya Nafsi

25. Yajue Madhehebu ya Shia

26. Ukusanyaji na Uhifadhi wa Qur'an Tukufu

27. Al-Wahda

16

Utokezo (al-Badaa)

28. Ponyo kutoka katika Qur'an.

29. Uislamu mfumo kamili wa maisha ya kijamii

30. Mashukio ya Akhera

31. Al Amali

32. Dua Indal Ahlul Bayt

33. Udhuu kwa mujibu wa Kitabu na Sunna.

34. Haki za wanawake katika Uislamu

35. Mwenyeezi Mungu na sifa zake

36. Amateka Na Aba'Khalifa

37. Nafasi za Ahlul Bayt (a.s)

38. Adhana.

39 Upendo katika Ukristo na Uislamu

40. Nyuma yaho naje kuyoboka

41. Amavu n’amavuko by’ubushiya

42. Kupaka juu ya khofu

43. Kukusanya swala mbili

44. Bismillah ni sehemu ya Qur’ani na husomwa kwa Jahara

45. Kuwaongoza vijana wa kizazi kipya

46. Kusujudu juu ya udongo

47. Kusheherekea Maulidi Ya Mtume (s)

48. Tarawehe

49. Malumbano baina ya Sunni na Shia

50. Kupunguza Swala safarini

51. Kufungua safarini

52. Umaasumu wa Manabii

53. Qur’an inatoa changamoto

54. as-Salaatu Khayrun Mina -'n Nawm

55. Uadilifu wa Masahaba

56. Dua e Kumayl

57. Sauti Ya Uadilifu wa Binadamu

58. Umaasumu wa Mitume - Faida Zake Na Lengo Lake

59. Umaasumu wa Mitume - Majibu Ya Aya Zenye Utata

60. Umaasumu wa Mitume - Umaasumu wa Mitume Muhammad (s)

17

Utokezo (al-Badaa)

61. Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Kwanza

62. Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Pili

63. Kuzuru Makaburi

64. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Kwanza

65. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Pili

66. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Tatu

67. Tujifunze Misingi Ya Dini

68. Sala ni Nguzo ya Dini

69. Mikesha Ya Peshawar

70. Malezi Ya Mtoto Katika Uislamu

71. Ubora wa Imam 'Ali Juu ya Maswahaba Na Ushia ndio njia iliy

onyooka

72. Shia asema haya, Sunni asema haya, Wewe wasemaje?

73. Liqaa-u-llaah

74. Muhammad (s) Mtume wa Allah

75. Amani na Jihadi Katika Uislamu

76. Uislamu Ulienea Vipi?

77. Uadilifu, Amani na Mtume Muhammad (s)

78. Mitala na Ndoa za Mtume Muhammad (s)

79. Urejeo (al-Raja’a )

80. Shahidi kwa ajili ya Ubinadamu

81. Kuanzia ndoa hadi kuwa wazazi

82. Myahudi wa Kimataifa

83. Uislamu na dhana

84. Mtoto mwema

85. Adabu za Sokoni

86. Johari za hekima kwa vijana

87. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Kwanza

88. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Pili

89. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Tatu

90. Tawasali

91. Imam Mahdi katika Usunni na Ushia

92. Maana ya laana na kutukana katika Qur’ani Tukufu

18

Utokezo (al-Badaa)

93. Hukumu ya kujenga juu ya makaburi

94. Swala ya maiti na kumlilia maiti

95. Shiya na Hadithi (kinyarwanda)

96. Mariamu, Yesu na Ukristo kwa mtazamo wa Kiislamu

97. Hadithi ya Thaqalain

98. Fatima al-Zahra

99. Tabaruku

100. Sunan an-Nabii

101. Historia na sera ya viongozi wema (Sehemu ya Kwanza)

100. Idil Ghadiri

102. Mahdi katika sunna

103. Kusalia Nabii (s.a.w)

104. Ujumbe -Sehemu ya Kwanza

105. Ujumbe - Sehemu ya Pili

106. Ujumbe - Sehemu ya Tatu

107. Ujumbe - Sehemu ya Nne

108. Shiya N’abasahaba

109. Iduwa ya Kumayili

110. Maarifa ya Kiislamu.

111. Ukweli uliopotea sehemu ya Kwanza

112. Ukweli uliopotea sehemu ya Pili

113. Ukweli uliopotea sehemu ya Tatu

114. Ukweli uliopotea sehemu ya Nne

115. Ukweli uliopotea sehmu ya Tano

19

Utokezo (al-Badaa)

BACK COVER

Maudhui ya Utokezo (Badaa’) yanazingatiwa kuwa ni kati ya masuala ya

falsafa ya Kitawhidi ambayo yamechochea utafiti wenye wigo mpana

baina ya maulamaa wa elimu ya falsafa, hiyo ni kutokana na yanay-

opatikana humo miongoni mwa masuala ya kina na ya muhimu.

Kumekuwepo na kutokuafikiana katika miji yetu ya Kiislamu, hususan

miongoni mwa wanavyuoni kuhusu usahihi wa itikadi ya Badaa’ - yaani

utokezo wa jambo fulani kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Baadhi wanase-

ma kwamba itikadi hii ni sahihi na wengine wanasema si sahihi. Baadhi ya

wanavyuoni wamekwenda mbali zaidi hadi kufikia kuwaita Waislamu

wenzao wanaoitakidi juu ya Utokezo (Badaa’) kuwa ni washirikina au

makafiri .

Lakini je, Badaa’ haina asili katika dini? Ukweli ni kwamba ina asili kati-

ka dini kwani uhalisi wake umeelezwa katika Qur’ani Tukufu, kama

utakavyoona katika kitabu hiki. Hivyo ungana na mwaandishi wa kitabu

hiki, Sayyid Abdul-Karim al-Bahbahani katika utafiti wake huu wa kie-

limu.

Kimetolewa na kuchapishwa na:

Alitrah Foundation

S.L.P. 19701 Dar es Salaam, Tanzania

Simu: +255 22 2110640

Simu/Nukushi: +255 22 2127555

Barua Pepe: [email protected]

Tovuti: www.alitrah.org

Katika mtandao: www.alitrah.info

20

Utokezo (al-Badaa)