Upload
natalie-hill
View
306
Download
0
Embed Size (px)
DESCRIPTION
Tafadhali pokea tahadhari ya Upepo mkali pamoja na mawimbi makubwa katika maeneo yote ya ukanda wa pwani kuanzia tarehe 01 mpaka 02 Septemba 2014.Imetolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania/ Issued by TanzaniaMeteorological Agency.
Citation preview
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UCHUKUZI
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Simu: 255 22 2460735/2460706
FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056
Barua pepe: [email protected] DAR ES SALAAM
Tovuti: www.meteo.go.tz
Unapojibu tafadhali nakili:
Kumb. Na.: TMA/1622 31 Ogasti, 2014
Taarifa kwa umma: Upepo mkali unaoambatana na mawimbi makubwa
vinatarajiwa katika maeneo yote ya ukanda wa Pwani.
Taarifa Na. 201408-02
Muda wa Kutolewa
Saa za Afrika Mashariki Saa 6:00 Mchana
Daraja la Taarifa: Tahadhari
Kuanzia:
Tarehe 01 Septemba, 2014
Mpaka:
Tarehe 02 Septemba, 2014
Aina ya Tukio Linalotarajiwa
Hali ya Upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa pamoja na
mawimbi makubwa yanayozidi mita 2.0 inatarajiwa katika
ukanda wote wa Pwani.
Kiwango cha uhakika: Juu: (70%)
Maeneo yatakayoathirika Pwani ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
Maelezo:
Hali hii inatokana na kuimarika kwa mgandamizo mkubwa wa hewa
katika maeneo ya kusini mwa Afrika hivyo kusababisha upepo mkali
wa Kusi, mashariki mwa Pwani ya Tanzania.
Angalizo: Wakazi wa maeneo yaliyotajwa wanashauriwa kuchukua tahadhari.
Maelezo ya Ziada Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa
mrejeo pale itakapobidi.
Imetolewa na
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.