of 133 /133
1 Simulizi katika mtiririko kama wa kitambaa kilichofumwa vizuri Kuwawezesha wanawake kuelezea simulizi za Mungu zinazosisimua juu ya upendo na tumaini

StoryTapestry Manual - Swahili

Embed Size (px)

DESCRIPTION

The StoryTapestry Manual in the Swahili language.

Text of StoryTapestry Manual - Swahili

1

Simulizi katika mtiririko kama wa kitambaa kilichofumwa vizuri

Kuwawezesha wanawake kuelezea simulizi za Mungu zinazosisimua juu ya upendo na tumaini

2

Shukurani Tunapenda kuwashukuru watu wengi waliowezesha kukamilika kwa kitabu hiki cha mwongozo. Carol Green Jon Haahr Sarah Haahr Bob Mahone Kevin Manous Marcia Meyer Beth Smith Tricia Stringer Sarai Torme

YALIYOMO

3 1. Uumbaji hadi Kanisa*

2. Ulimwengu wa Roho 3. Uumbaji*4. Ukaidi/Uasi* 5. Mwito wa Ibrahimu*

6. Sara aahidiwa mtoto wa kiume7. Imani ya Ibrahimu yajaribiwa* 8. Kupakwa Mafuta kwa Daudi

9. Daudi na Bethsheba10. Simulizi ya Nathani

11. Ahadi*12. Malaika anawatembelea Mariamu na Yosefu**

13. Kuzaliwa kwa Yesu** 14. Ubatizo wa Yesu** 15. Mwanamke Kisimani** 16. Binti wa Yairo na Mwanamke aliyetokwa na Damu** 17. Yesu awalisha 5000** 18. Viongozi wa Dini wenye wivu**19. Mwanamke Mwenye Dhambi Asamehewa** 20. Njama na karamu wa Mwisho** 21. Yesu Asalitiwa** 22. Mashtaka ya Yesu) Yesu ashtakiwa mbele ya hakimu** 23. Yesu Achukua Msalaba Wake na Asulubiwa**

24. Kufufuka kwa Yesu** 25. Baada ya ufufuo

4

26. Roho wa Mungu27. Mwafrika

28. Paulo akutana na Yesu29. Petro aponya na kumfufua Tabitha kutoka kwa wafui 30. Mwanamagereza Mfilipi

31. Kurudi *Simuliza za utangulizi kutoka Agano la Kale Magdalena: Afunguliwa toka katika Aibu **Simulizi kutoka Magdalena: afunguliwa toka katika Aibu 2006 Inspirational Films, Inc. Zimetolewa na kusambazwa na Nardine Productions. Haki zote zimehifadhiwa http://www.magdalenatoday.com Simulizi Inaanza

Mwonekano Uumbaji hadi KanisaHapo mwanzo kabla wakati haujaanza, kulikuwa na Mungu wa Kweli mmoja tu. Alipoongea, aliuumba ulimwengu, mbingu na nchi na vitu vyote vilivyomo. Kisha Mungu akaamua kufanya uuambaji Wake maalumu, mwanaume na mwanamke. Mwanaume na mwanamke walikuwa na mahusiano mema/safi na Mungu. Walitembea na kuongea Naye. Lakini siku moja, mwanamme na mwanamke hawakumtii Mungu, na ule uhusiano wao safi na Mungu ukaharibika. Ulimwengu wote ulilaaniwa kutokana na kutotii kwao. Mwanamume na mwanamke wakawa na na uzao mwingi, na matokeo yake ulimwengu wote ukajazwa. Watu waliendelea kutokumtii Mungu lakini Mungu hakuwasahau. Siku moja, Mungu alisema/aliongea na mtu aliyeitwa Ibrahimu. Mungu alimwambia Ibrahimu, Nitakwenda kukupa wazao wengi kuliko zilivyo nyota za angani. Nitawafanya kuwa taifa kubwa. Nao wataitwa watu wangu, nao watakuwa baraka kwa ulimwengu wote. Ijapokuwa Ibrahimu alikuwa mzee, alimwamini Mungu. Mungu alitimiza ahadi yake na Ibrahimu akapata mtoto wa kiume. Kupitia mwanaye, Ibrahimu akawa na uzao mwingi. Wakawa taifa kubwa, kama Mungu alivyosema. Lakini watu waliendelea kutomtii Mungu na wakatengana naye. Mungu alimtuma mjumbe kwa watu wake aliyeitwa Isaya. Isaya aliwaambia watu wale juu ya mkombozi aliyeahidiwa ambaye siku moja angekuja. Isaya alisema, Sisi wote tumetenda dhambi dhidi ya Mungu. Siku moja, mkombozi atakuja ambaye atateswa na kufa kwa ajili ya dhambi zetu. Kisha Mungu atamrejezea uzima tena, naye ataishi milele. Watu wote

5

watakaomwamini imani yao kwake watasamehewa dhambi zao na wataishi katika uhusiano safi/mwema/mkamilifu na Mungu milele. Hatimaye, kama Mungu alivyosema, mkombozi Yule aliyeadiwa alikuja. Alikuwa wa ukoo wa Ibrahamu. Jina lake aliitwa Yesu na alikuwa mkamilifu katika namna zote. Aliponya wagonjwa, alitoa pepo wachafu, na kutenda miujiza. Baadhi ya watu walimfuata Yesu, lakini wengine hawakumfuata. Yesu aliwaambia watu, Natoa uzima wa milele kwa kila anayenifuata na hakuna atakayeweza atakayewanyanganya toka kwangu kwa sababu Mungu na mimi tu wamoja/sawa. Si kila mtu alipendezwa na kile ambacho Yesu alisema na kufanya. Wale ambao hawakumwamini Yesu walimfanya akamatwe, apigwe na kisha kuuawa. Yesu aliteseka na kufa, kama Mungu alivyosema atatendewa. Lakini pia, kama Mungu alivyosema Yesu alikuwa hai tena. Alitembea na kuongea, na kula pamoja na wafuasi wake ili kuthibitisha kuwa hai kwake. Na aliahidi kuwatumia Roho wa Mungu ili kuwafariji na kuwaongoza. Kisha Mungu alimtwaa Yesu kwenda mbinguni. Kama vile Yesu alivyoahidi, alimtuma Roho wa Mungu kukaa ndani yao wale waliomwamini Yeye. Watu walijionyesha kuwa wafuasi wake kwa ishara ya kuoshwa kwa maji ili kuonyesha kwamba wamebadilishwa mioyo na maisha yao. Walikusanyika pamoja. Waliomba na kuabudu pamoja. Walijifunza mafundisho yake na kusaidiana katika mahitaji yao. Waliyakumbuka maisha ya Yesu kwa kusikiliza simulizi na kufuata mafundisho Yake. Na waliwashikisha simulizi hizo na watu wote waliokutana nao. Leo hii, wafuasi wa Yesu wanaendelea kufanya mambo hayo yote na wanasubiri siku ile ambapo Yesu atakuja kuwachukua ili wakaishi pamoja Naye milele.

6

Ulimwengu wa RohoMaandiko ya Msingi Ayubu 39:4-7; Zaburi 103:20-21; Zaburi 148:2, 5; Mathayo 9:34; Mathayo 25:41; Yohana 1:1,2; Waefeso 6:11, 12; 1Timotheo 1:17; 2Timotheo 3:16; Yakobo 2:19; 2Petro 2:4; Yuda 6 Hii ni simulizi ya kweli inayoanzia mwanzo wa wakati. Tunajua juu ya mambo hayo, kwa sababu Mungu aliwaambia watu juu yake hapo zamani kupitia wasemaji wake. Hapo mwanzo kabisa, kabla ya kitu cho chote kuwepo, Mungu alikuwepo. Amekuwepo siku zote tangu milele. Aliumba viumbe visivyoonekana kwa macho kuwa watumishi wake. Wanaitwa malaika. Viumbe hawa roho/wasioonekana walimsifu Mungu na walifuata amari zake. Waliimba kwa furaha pale Mungu alipoumba ardhi na nchi, kuifanya kamilifu namna alivyotaka. Kuna kipindi fulani viumbe hawa roho waligeuka kuwa waovu. Hawakuzifurahia nyadhifa walizopewa na Mungu. Walikosa utii dhidi ya Mungu na mambo yote mazuri aliyowapa Mungu. Viumbe hawa wakaidi wakawa roho wachafu tunawajua kama mapepo au mashetani wabaya. Mmoja kati hao anaitwa Shetani, ni mtawala wa wengine wote. Roho hawa wabaya wanaendelea kutenda kazi kinyume na yale Mungu anayofanya hapa duniani, na kinyume na wale wanaozifuata njia za Mungu. Mungu alitamka hukumu juu ya hawa roho wabaya wote. Alisema, siku moja wataadhibiwa katika moto wa milele.

7

Maneno/Vifungu vya Maneno ya Kuzingatia Roho Viumbe roho vilivyoumbwa na Mungu. Angalia Faharasa kwa ajili ya: Malaika Ukaidi/kutokutii Roho chafu Shetani Wasemaji Mtazamo wa walimwengu Wengi wa watazamaji wengi wa ulimwengu wataitazama simulizi hii kuwa ni ya kubuniwa (ya uongo). Hakikisha kuwa haieleweke (kutambulika) katika mtazamo huo. Muundo na Simulizi Simulizi hii imefupishwa kutoka vifungu mbalimbali vya maandiko katika Agano la Kale na Jipya. Neno roho katika vifungu vilivyomo katika utangulizi huu halitakiwi kuchanganywa na Roho wa Mungu. Simulizi hii inaelezea wapi Shetani alikotokea. Kama unafanya kazi katika jamii ya Kihindu, Kibudha, au ulimwengu wa kianimist, simulizi hii itakuwa ni nzuri kuifanyia kazi. Kama unafanya kazi katika lugha ambayo filamu haina tafsiri, itakuwa vema kuiacha kabisa filamu hii. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Mungu ni Muumbaji wa kila kitu; Mungu ni mzuri katika kila jambo analolifanya.

8

UumbajiMwanzo 1:1-28; 31; 2:2, 3, 7-9, 15-18, 21-25 Imetumia tafsiri ya Biblia ya NLT Mwanzo 1:1-27 Hapo mwanzo alikuwako Mungu. Alitamka, na alipofanya hivyo, aliumba ulimwengu wote na vyote vilivyomo/vilivyo ndani yake. Mungu alifanya nuru (mwanga) na maji. Alitengeneza nchi kavu na aina zote za mimea na miti. Mungu alitengeneza jua, mwezi na nyota. Aliumba aina zote za samaki, ndege na wanyama. Kisha Mungu aliwaumba watu, aliwafanya kwa mfano wake mwenyewe. Mwanzo 2:7-9, 15 Mungu aliunda mwili wa mwanaume kutoka udongo wa ardhini na akampulizia pumzi na akaanza kuishi. Kisha Mungu akamweka mwanaume katika bustani ya miti ya matunda. Mungu alipanda aina zote za miti katika bustani. Ilikuwa miti mizuri ambayo ilizaa matunda matamu sana. Kati kati ya bustani aliweka miti miwili mti ambao ulitoa uzima na mti ambao ulitoa ufahamu wa mema na mabaya. Mwanzo 2: 16, 17 Mungu alimwambia mwanaume, Adamu, Unaweza kula tunda lo lote katika bustani isipokuwa tunda kutoka mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Iwapo utakula matunda ya mti huo, utakufa. Mwanzo 2:18, 21-25 Mungu akasema si vema mtu awe peke yake. Kwa hiyo Mungu akamsababishia Adamu usingizi kulala mzito. Akachukua mmoja wa ubavu wa Adamu na akamfanya mwanamke kutoka kwenye ubavu huo na akamleta kwa Adamu. Hatimaye! Adamu kwa mshangao/furaha akatamka, Anayo nyama na mifupa kama mimi! Adamu na mkewe, Hawa, walikuwa uchi, lakini hakuna kati yao aliyeona haya. Walikuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Mwanzo 1:28, 31 Mungu akawabariki na kuwaambia, Zaeni muongezeke/jiongezeni na kuwa watawala juu ya samaki, ndege na wanyama wote. Kisha Mungu akayaangalia yote aliyoyatengeneza, na akaona kwamba ni mema katika namna zote. Mungu aliuumba ulimwengu na vyote vilivyo ndani yake kwa siku sita.

9

Mwanzo 2:2, 3 Siku iliyofuata, siku ya saba, Mungu aliacha kufanya kazi. Mungu aliitenga siku moja katika juma kwa ajili yake kwa sababu alikuwa amemaliza uumbaji wa ulimwengu.

10

Maneno/Vifungu vya Maneno vya Kuzingatia nyama na mifupa kama mimi Kifungu hiki kinarejea Adamu alipokuwa akitamka kwa furaha kwamba hatimaye amempata mtu kama yeye mwenyewe. Inaachana kidogo na wazo halisi la matamshi ya kiebrania ya, nyama katika nyama yangu, mfupa katika mfupa wangu. Njema sana ( kwa kila hali) Mungu alipoona uumbaji wake kuwa ni mzuri sana katika hali zote, inaonyesha kwamba ilikuwa ni ya kuridhisha kwa Mungu aliamua kuwa ni njema na iliyofaa kwa kusudi lake. Angalia Faharasa kwa ajili ya; Barikiwa Uhusiano (Mtazamo wa ulimwengu) Halisia Uwe na hakika kuwa neno Uchi lililotumika hapa lipo sahihi. Kwa baadhi ya tamaduni; ni vizuri zaidi kusema, (walikuwa utupu) Umahiri wa Simulizii Waongeaji wengi wanaona kuwa ni vigumu kukumbuka orodha ya siku saba za uumbaji katika kitabu cha Mwanzo 1. Mwanzo 1 kwa hakika ilikuwa kama utenzi hata hivyo. Mwanzo 2 inarejea kusimulia hadithi ya uumbaji katika namna (mtindo wa) ya simulizi. Mwanzo 1 imeandikwa kwa ufupisho. Hadithi imechukuliwa zaidi katika Mwanzo 2. Inaonekana ni rahisi watu kukumbuka hadithi inapokuwa imeelezewa namna hii. Majina ya mito katika Mwanzo 2 yameachwa kwa ajili ya urahisi wa kurudia simulizi. Hata hivyo, iwapo kundi la watu wanaipenda mito kwa sababu fulani, basi ijumuishwe. Mwanzo 2:3 maneno yaliwekwa mengine ili kufanya iwe rahisi kuyaelewa na kupunguza ugumu wakati wa kutafsiri. Kwa mfano, badala ya kusema Mungu alizifanya siku ya saba takatifu, imeieleza kama ni ya kujitenga. Mti wenye ujuzi wa mema na mabaya ni jina linaloonyeshs tendo, ili kwamba waliohudhuria (hadhara) waweze kuelewa zaidi kusudi kamili la mti. Kanuni Tabia na kawaida ya Mungu

11

Muumbaji; Anahusiana ana nguvu za kubariki Kanisa Kutenga siku maalumu, kuikabidhi kwa Mungu ambayo inaweka msingi wa Kanisa.

12

KukaidiMwanzo 3:1-19a, 21-24 Imetumia tafsiri ya: NLT Mwanzo 3:1-5 Basa nyoka alikuwa mwerevu kupita wanyama wote Mungu aliowafanya. Shetani alimwingia nyoka na akamuuliza Hawa, Hivi kweli Mungu alisema msile matunda yoyote katika bustani? Hakika tunaweza kula haswa, Hawa alimwambia. isipokuwa matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya ndio haturuhusiwi kula. Mungu anasema tusiule wala tusiuguse au sivyo tutakufa Hamtakufa! nyoka alifoka. Mungu anajua kwamba mtakapokula tunda hili mtakuwa kama yeye, mkijua kila kitu, mema na mabaya. Mwanzo 3:6, 7 Hawa alishawishika. Tunda lilionekana zuri na tamu, na lingemfanya kuwa na hekima! Kwa hiyo akala sehemu ya tunda. Akampa sehemu mme wake, ambaye alikuwa pamoja naye. Adamu akala pia. Wakati huo, kitu fulani ndani yao kilibadilika; ghafla walijisikia aibu kwa kuwa wako utupu Kwa hiyo wakashona majani na kuyavaa ili kuufunika uchi wao. Mwanzo 3:8-18 Kuelekea nyakati za jioni, Adamu na Hawa walimsikia Mungu akitembea bustanini, kwa hiyo wakajificha kati ya miti. Mungu akamwita Adamu, Uko wapi? Adamu akajibu, nilikusikia, kwa hivyo nikajificha. Niliogopa kwa sababu niko uchi. Ni nani aliyekuambia kwamba uko uchi? Mungu aliuliza. Je, umekula matunda niliyokuamuru usile? Ndio, Adamu akakiri, lakini ni mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea tunda na nikalila. Kisha Mungu akamuuliza Hawa, Umewezaje kufanya jambo kama hilo? Nyoka alinilaghai,akajibu. Ndiyo maana nikalila. Mwanzo 3:14, 15 Hivyo Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umefanya hivi, utaadhibiwa. Utatambaa katika mavumbi muda wote utakaoishi. Kuanzia sasa, uzao wako na uzao wa mwanamke watakuwa maadui. Utamuuma katika kisigono, lakini yeye atakuponda kichwa. Mwanzo 3:16 19a Kisha Mungu akamwambia Hawa, Utazaa watoto kwa maumivu makali na mateso. Mungu akamwambia Adamu, Kwa sababu umekula matunda niliyokuamru usiyale, nimeweka laana

13

juu ya ardhi. Maisha yako yote utasumbuka/utaishi kwa taabu ili kuishi kutokana na hiyo. Nchi itazaa miiba na mbigili. Utazalisha chakula kwa kutoa jasho hadi kufa kwako. Mwanzo 3:21-24 Kisha Mungu akasema, Sasa watu wanajua kila kitu, mema na mabaya. Itakuwaje kama watakula matunda kutoka katika mti wa uzima? Kisha wakaishi milele! Hiyo Mungu akawatoa Adamu na Hawa nje ya bustani na akawazuia wasirudi kwenye mti unaotoa uzima.

14

Maneno/Vifungu vya maneno ya kuzingatia Laana Neno hili katika kifungu hiki, linamaanisha adhabu, hukumu, au kitu fulani kisichokizuri kinakwenda kumtokea mtu. Lugha nyingi zina namna ya kutamka laana kwa mtu au kitu, kwa hiyo uwe na hakika neno unalochagua halina pendekezo la namna yoyote ya mazingaombwe. Angalia Faharasa kwa ajili ya: Wazao Uovu/Ubaya Busara/Hekima (Mtizamo wa kidunia ki ulimwengu) Baadhi ya watu wanaweza kuabudu nyoka, kwa hiyo ni muhimu kwamba nyoka akaonekana kama mtu mbaya katika simulizi hii. Baadhi ya makundi ya watu wameisikia simulizi hii, lakini hawaamini kama kweli ilitokea kwa sababu mnyama anaongea. Wanadhani hii ni hadithi ya kubuni ya wanyama zaidi au ngano za kienyeji. Karibu wanazuoni wasomi wote wa Biblia wanakubali kwamba nyoka ni Shetani kwa kuzingatia nukuu kama vile Ufunuo 12:9; 20:2; 2Korintho 11:3. Ikiwa kutahitajika uelewa zaidi, mfano unaweza kuongezwa katika simulizi kwamba nyoka ni Shetani. Mwambatano wa simulizi Hakikisha unatumia maneno yale yale kwa ajili ya: mema na mabaya, utupu, Shetani, hekima na wazao yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia Umahiri wa Simulizi Simulizi inakuwa rahisi kuielezea iwapo maneno adhabu/laana yamerahisishwa. Wazo la mwanamke kumtamani mwanamme na mwanamme kumtawala mwanamke limeachwa kwa sababu ni gumu kwa wasikilizaji wengi kulielewa. Kwa sababu hizo hizo, kufukuzwa kwa mwanamme na mwanamke kutoka bustanini kumerahisishwa. Kanuni Tabia na kawaida ya Mungu Anajua yote; amejitenga na uovu na dhambi; hupinga dhambi na uovu; ni wa haki; Anayeadhibu dhambi na ukaidi, hujenga mahusiano/anahusiana. Hakika ya Wokovu Msingi uliwekwa kwa kuweka uadui kati ya mwanadamu na Shetani kwa mwanadamu kuwa mshindi.

15

Maisha ya Uchaji Msingi uliwekwa kwa mwanadamu kutembea na kuongea na Mungu na Mungu kutembea na kuongea na mwanadamu. Maombi Huonyesha Mungu na mwanadamu wakuwasiliana

16

Mwito wa IbrahimuMwanzo 12:1-7; 15:1-6 Imetumia tafsiri ya Biblia: NLT Badiliko: Kwa sababu ya ukaidi wa Adamu na Hawa, uhusiano wao na Mungu ulivunjika. Hata hivyo, Mungu hakuusahau uumbaji wake maalumu. Miaka mingi ilipita na Mungu akamchagua mmoja katika uzao wao, aliyeitwa Ibrahimu. Hii ni simulizi ya Abrahamu. Mwanzo 12:1-3 Mungu akamwambia Ibrahamu, Toka wewe katika nchi yako, na ukoo/ndugu zako, na nyumba ya baba yako, uende mpak nchi nitakayokuonyesha. Nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kukufanya maarufu ; nawe utakuwa baraka,jamaa zote zilizo duniani zitabarikiwa kupitia wewe. Mwanzo 12:4-6 Hivyo Ibrahimu akaondoka kama alivyoelekezwa. Ibrahimu alikuwa mzee sana alipoondoka nyumbani kwao. Alimchukua mke wake Sara na mali zake zote- mifugo yake na watu wake wote aliokuwa akiishi nao katika nyumba yake na akaelekea kwenye nchi ambayo Mungu angemwonyesha. Walipofika huko, Ibrahimu alisafiri kupitia nchi ile. Hatimaye aliposimama; aliweka kambi kando ya mti mkubwa. Mwanzo 12:7 Kisha Mungu akamtokea Ibrahimu na kusema, Nitawapa kizazi chako nchi hii. Ibrahimu akamwabudu Mungu aliyemtokea. Mwanzo 15:1-3 Baada ya muda fulani, Mungu aliongea na Ibrahimu katika maono na akamwambia, Usiogope, nitakulinda, na utapata zawadi kubwa. Lakini Ibrahimu alijibu, Ee Mungu, kuna raha gani kupata baraka zote hizo ikiwa mimi sina mwana wa kiume ? Kwa vile hujanipa watoto, mtumishi wa nyumbani mwangu atarithi utajiri wangu wote. Hujanipa uzao wangu mwenyewe, kwa hiyo mmoja wa watumishi wangu atakuwa mrithi Mwanzo 15: 4, 5 Kisha Mungu akamwambia Ibrahimu, Hapana, mtumishi wako hatakuwa mrithi wako, kwa kuwa utapata mwana wa kiume wa kwako mwenyewe ambaye atakuwa mrithi wako. Mungu akamchukua Ibrahimu nje na akamwambia, Tazama angani na uhesabu nyota kama utaweza. Hivi ndivyo wingi wa uzao wako utakavyokuwa. Mwanzo 15:6 Ibrahimu akamwamini Mungu, na kwa sababu ya hiyo, Mungu akamhesabia kuwa na uhusiano mzuri naye.

Maneno/Vifungu vya Kuzingatia

17Uadilifu/Uhusiano sahihi Katika Agano la Kale wazo la uadilifu limetokana na uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu, au kati ya mwanadamu na mwanadamu. Uadilifu unaelekeza kwenye utakatifu. Katika Toleo la kingereza cha kisasa (CEV) dhana hiii inatafsiri katika Isaya 53:11katika namna ifuatayo: Ataadhibiwa kwa ajili ya dhambi za wengine, ili kwamba wengi wao wasiwe na hatia tena. Kwa maneno mengine, uadilifu huondoa hatia. Angalia Faharasi kwa ajili ya: Kusadiki /kuamini Imani/ Bariki/Barikiwa/Kubariki; Ukaidi/uasi; na Kuabudu Mtazamo wa kidunia Ibrahimu ni mtu wa muhimu katika pande zote mbili, mtazamo wa maisha ya Kibiblia na Kiislamu. Ikiwa unafanya kazi kati kati ya Waislamu, kumjumulisha Ibrahamu katika simulizi itaweka daraja kati ya utamaduni wa Kibiblia na utamaduni wao. Kwa kuwa miti inaabudiwa katika baadhi ya tamaduni, hakikisha haitafsiriwi kuwa Ibrahimu aliabudu mti katika simulizi hii. (Mtiririko uhalisia katika simulizi) Hakikisha unatumia neno lile lile kwa ajili ya, wazawa, uhusiano, na kubarikiwa yalivyotumika katika simulizi zilizopita. Umahiri wa Simulizi Mungu hakuwa amebadilisha jina la Abramu kuwa Ibrahimu bado, bali kwa ajili ya kurahisisha Ibrahimu limetumika. Iwapo baadaye itaonekana kwamba kubalishwa kwa jina la Abrahamu kuna umuhimu katika mpangilio wa simulizi, jumuisha simulizi na badilisha jina lake tena kuwa Abramu katika simulizi hii. Kanaani na maeneo mengine yaliyotajwa yameachwa kwa makusudi ili hadithi iwe rahisi kukumbukwa na kurejea Malengo katika hadithi hii ni kuandaa ahadi ya Mungu kwa Ibrahimu. Ahadi ni kuwa Mungu atamfanya Ibarahimu kuwa taifa kubwa na kupitia taifa hilo, watu wote watabarikiwa. Ahadi hii ilitunzwa na Mungu. Ibrahimu alivyoishi katika uhusiano mzuri na Mungu, amepewa umuhimu. Kanuni Tabia na kawaida ya Mungu Anayetoa ahadi; anayebariki, anayehusiana, ndiye atakayemuumba mtu kwa ajili yake mwenyewe, ndiye anayeongoza na kuelekeza, ndiye anayejifunua na kulifunua mapenzi yake, anayestahili kuabudiwa, aliye na nguvu za kubariki, anayelinda na kutupa thawabu, anayezungumza na watu, anayejali watu wake, anayewaita watu wake kwa ajili ya kusudi lake. Kanisa Mungu atawainua/atawajenga watu wake akiweka msingi kwa ajili ya kanisa; Ibada Maisha ya Uchaji Katika msingi wa uhusiano na kuamini, kutembea na kuongea na Mungu Maombi Mfano mzuri wa mawasiliano kati ya Mungu na mwanadamu iliyo sahihi na binafsi, huweka msingi kwa ajili ya maombi.

Sara aahidiwa mtoto wa kiume

18 Mwanzo 18:1-5, 6-9, 10-15; 21:1, 2 Imetumia tafsiri ya: NLT Badiliko: Miaka mingi ilipita. Ibrahimu na Sara walikuwa wazee sana na bado hawakuwa na wamepata watoto. Wakati huu sasa Sara alikuwa amekwishapita umri wa kuwa na watoto. Mwanzo 19:1-5 Mungu alimtokea Ibrahimu alipokuwa ameketi mlangoni pa hema lake. Ibrahimu aliangalia kwa mbali na aliwaona wageni watatu wamesimama. Alipowaona alikimbia mbio kukutana nao na kuwakaribisha, akainama mpaka nchi kuwasalimu. Ibrahimu akasema karibu, Pumzikeni kwenye kivuli cha mti huu wakati maji yanaletwa muoshe miguu yenu. Na kwa kuwa mmemheshimu mtumwa wenu na kunitembelea, naomba niandae chakula ili kuwaburudisha kabla hamjaendelea na safari yenu. Sawa Walijibu. Fanya kama ulivyosema. Mwanzo 18:6-9 Kwa hiyo Ibrahimu akarudi mbio kwenye hema na akamwambia Sara, Harakisha! Tengeneza mkate. Kisha Ibrahimu akaandaa chakula kizuri kwa ajili ya wageni wake. Yuko wapi Sara mkeo? Wageni waliuliza. Yupo ndani ya hema, Ibrahimu alijibu. Mwanzo 18:10-15 Kisha Mungu akasema, Nitakurudia wakati huu mwakani, na tazama mkeo Sara atapata mwana wa kiume! Sara alikuwa akiyasikiliza mazungumzo haya na akacheka moyoni mwake na akashangaa itakuwaje mwanamke mzee kama yeye aweza kupata mtoto. Kisha Mungu akamwambia Ibrahimu, Kwa nini Sara amecheka? Kwa nini amesema, inawezekanaje mwanamke mzee kama mimi kupata mtoto? Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda Mungu? Nnitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume. Sara akaogopa, na akasema Sikucheka Bali Mungu akasema, umecheka. Mwanzo 21: 1, 2 Mungu alitunza neno lake na akafanya vile vile kama alivyoahidi. Akapata mimba, na akamzaa mtoto wa kiume katika umri wake mkongwe. Hii ilitokea katika wakati ule ule Mungu alivyosema itakuwa/itatokea.

19

Maneno/Vifungu vya Maneno ya Kuzingatia Osheni miguu yenu Kuosha miguu ya mtu mwingine ilikuwa ni ishara ya heshima kwa mgeni. Mtazamo wa kiulimwengu Wageni wale watatu wanaweza kuelezewa kuwa ni Mungu na malaika wawili. Inasaidia kufafanua wageni hawa walikuwa akina nani. Mwanzo 18:17-33 na Mwanzo 10:1-26 ni mistari inayotoa msaada kwa kueleza kwamba alikuwa Mungu na malaika wawili. Umahiri katika Simulizi Sara alitambulishwa katika simulizi iliyotangulia. Hakikisha unatumia jina lake hapa. Simulizi hii ni utimilifu wa ahadi iliyofanywa kwa Ibrahimu na Sara miaka 25 kabla iliyotangulia (katika simulizi za mwito wa Ibrahimu) Katika baadhi ya tamaduni, desturi ya kuinama mbele ya mtu mwingine inaweza isiwepo au inaweza kuwa na maana tofauti. Katika simulizi hii, Ibrahimu alikuwa anaonyesha heshima kwa wageni wake. Iwapo maana hii haieleweki kwa hadhira, basi hii inaweza kurahisishwa kwa kusema tu kwamba Ibrahimu aliwasalimia wageni wake kwa heshima. Kanuni Tabia na kawaida ya Mungu Mungu anatiminza ahadi zake; Mungu huwatembelea watu wake binafsi; Mungu anajua hata mawazo yetu; Mungu hutenda kazi katika kila jambo kwa ajili ya kukamilisha mpango wake.

20

Imani ya Abrahamu yajaribiwaMwanzo 22:1-4; 6-8; 9-13; 15-18 Imetumia tafsiri ya : NLT

Mwanzo 22:1-4 Siku moja Mungu aliijaribu imani na utii wa Ibrahimu. Ibrahimu! Mungu aliita, Ndio, aliitika, Mimi hapa. Mchukue mwanao, mwanao wa pekee Isaka, ambaye unampenda sana na uende kwenye nchi nyingine. Mtoe sadaka huko katika moja ya milima nitakayokuonyesha. Asubuhi iliyofuata Ibrahimu aliamka mapema akawachukua watumishi wake wawili pamoja na mwanaye Isaka. Siku ya tatu ya safari, Ibrahimu aliunua macho na akapaona mahali kwa mbali. Mwanzo 22:6-8 Ibrahimu alimvisha Isaka kuni mabegani mwake, wakati, yeye akiwa amechukua kisu na moto. Hao wawili walipokuwa wakienda pamoja, Isaka akamgeukia Ibrahimu na akasema, Baba? Ndio, mwanangu, Ibrahimu alijibu.. Tunazo kuni na moto, alisema kijana, lakini mwanakondoo kwa ajili ya sadaka yuko wapi? Mungu atatupatia huyo mwanakondoo, mwanangu. Ibrahimu alijibu. Na wakaendelea mbele pamoja. Mwanzo 22:9-13 Walipofika mahali ambapo Mungu alimwambia, Ibrahimu aende akaandaa mahali pa kufanyia ibada na akapanga kuni juu yake. Kisha akamfunga mwanaye Isaka na akamweka juu ya kuni. Na Ibrahimu akatoa kisu chake ili kumchinja mwanaye kama sadaka kwa Mungu. Wakati huo, Malaika wa Mungu alimwita kwa sauti kubwa, Ibrahimu! Ibrahimu! Ndio, akajibu, Ninasikiliza. Usimnyoshee kijana mkono! Malaika alisema. Usimdhuru kijana kwa namna yoyote, kwa kuwa sasa nimejua kwamba hakika unamwogopa Mungu. Hukumzuilia hata mwanao, mwanao wa pekee. Kisha Ibrahimu akatazama juu na akamwona mwana kondoo dume kichakani. Kwa hiyo akamchukua mwanakondoo na akamtoa sadaka mahali pa mwanaye. Mwanzo 22:15-18 Kisha malaika wa Bwana akamwita tena Ibrahimu, Hivi ndivyo Mungu anavyosema, Kwa sababu umenitii na hukunizuilia hata mwanao, nimekuahidi kuwa nitakubariki nitauzidisha uzao wako kuwa mamilioni yasiyohesabika, kama nyota za angani na mchanga wa pwani. Watawashinda/watawateka maadui zao kupitia uzao wako, mataifa yote yatabarikiwa yote ni sababu umenitii mimi.

21

Maneno/Vifungu vya kuzingatia Kujaribiwa Hii inamaanisha kuangalia iwapo Ibrahimu kweli alimwamini Mungu au alikuwa na imani katika Mungu. Utii. Hii inamaanisha kutekeleza au kufanya kile unachotakiwa au umeamriwa kufanya. Malaika/Malaika wa Mungu Angalia Faharasa kwa ajili ya: Imani Kafara/sadaka Mtiririko halisi ndani ya simulizi) Hakikisha kuwa unatumia maneno yale yale kwa: uzao, imani, bariki, Mungu, kuabudu na kuamini yaliyotumika katika simulizi zilizopita. Umahiri wa Simulizi Ili kuifanya ivutie zaidi, mazungumzo mengi yamejumuishwa katika simulizi hii. Simulizi hii imemtambulisha Isaka kama mwana wa kiume wa Ibrahimu. Katika baadhi ya tamaduni inaweza kuwa bora kusema alimtoa mwanaye wa kiume bila kutaja jina la Isaka. Hakikisha unaonyesha hii si kafara ya mtoto bali ni namna tu ambayo Mungu aliujaribu utayari wa Ibrahimu katika kumtii yeye. Kanuni Tabia na kawaida ya Mungu Mungu anatarajia utiifu kutoka kwa watu wake hata kama hatuelewi; Mungu hutoa kila kitu kinachohitajika; Mungu ni mwaminifu siku zote katika ahadi zake; Mungu hutuma malaika wake kuongea na watu; Wakati mwingine Mungu atatutaka tumpe au tumtolee yeye kitu ambacho ni maalumu sana au cha thamani sana kwetu.

22

Daudi apakwa mafuta 1Samweli 16:1-13 Imechukuliwa toka tafsiri ya: NLT Pitio: Mungu aliitunza ahadi yake kwa Ibrahimu na wazao wake wakawa taifa kubwa mno. Siku moja walidai kwamba Mungu awape mfalme wa kidunia ili wawe kama mataifa mengine. Hili halikumpendeza Mungu lakini akawaruhusu. Mungu alianza kusema na taifa hili kupitia watu walioitwa wasemaji. Miaka mingi baadaye, Mungu alimchagua mtu kuwa mfalme juu ya taifa hili. Hivi ndivyo alivyofanyika kuwa mfalme 1Samweli 16:1-3 Mungu alisema kwa mmoja wa wasemaji wake, Samweli, Ijaze chupa yako mafuta na uende hadi Bethlehemu. Mtafute mtu aitwaye Yese ambaye anaishi huko, maana nimemchagua mmoja wa watoto wake kuwa mfalme Wangu. Lakini Samweli aliuliza, Nawezaje kufanya hilo? Ikiwa mfalme atalisikia, ataniua. Chukua ndama pamoja nawe, Mungu alijibu, na useme kwamba umekuja kuniabudu mimi. Mwalike Yese na wanaye na mimi nitakuonyesha yupi utamtia mafuta kwa ajili yangu. 1Samweli 16:4-10 Samweli alifanya kama alivyoagizwa na Mungu. Alipofika Bethlehemu, wazee wa mji walikuja kumlaki wakitetemeka. Kuna tatizo gani? Waliuliza. Je, umekuja kwa amani? Ndiyo, Samweli alijibu. Nimekuja kumwabudu Mungu. Jitakaseni na njooni pamoja nami. Kisha Samweli alimwalika Yese na wanawe pia. Walipofika Samweli alimwangalia mtoto wa kwanza na akafikiri, Hakika huyu ndiye mpakwa mafuta wa Mungu! Lakini Mungu alimwambia Samweli, Usimchague kwa mwonekano au kimo chake,kwa maana mimi nimemkataa. Mimi siangalii kama ninyi muangaliavyo. Maana wanadamu huangalia sura ya nje, bali mimi huutazama moyo. Kisha waliobakia kila mtoto akapita mbele ya Samweli lakini Mungu hakumchagua yeyote kati yao. Hivyo, Samweli akamwambia Yese, Mungu hakumchagua yeyote kati ya hawa. 1Samweli 16:11-13 Kisha Samweli akauliza, Je hawa ndio watoto ulionao wote? Bado yupo mdogo, Yese alijibu. Lakini yuko nje uwandani akichunga kondoo na mbuzi. Tuma aletwe haraka, Samweli akamwambia, Hatutaketi kula hadi afike. Kwa hiyo Yese akatuma aletwe. Alikuwa mweusi na mzuri, mwenye macho mazuri. Na Mungu akasema, Huyu huyu ndiye, mtie mafuta. Kwa hiyo Daudi alipokuwa amesimama kati ya ndugu zake, Samweli akachukua pembe ya mafuta ya mzeituni aliyokuja nayo na akampaka kwa yale mafuta Daudi. Na Roho wa Mungu akaja juu ya Daudi kwa nguvu sana kuanzia siku ile.

23 Maneno/Vifungu vya Maneno ya Kuzingatia Angalia Faharasa kwa ajili ya: Kupaka mafuta Roho wa Mungu Wasemaji Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha kutumia maneno yale yale kwa ajili ya kuabudu na uzao yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahiri wa Simulizi Baadhi ya majina yameachwa ili kurahisisha kuikumbuka na kuisimulia tena. Sababu ya Samweli kuja Bethlehemu limerahisishwa kama, kuabudu ili kwamba simulizi iwe rahisi kukumbuka na kuisimulia tena, na kuondoa uwezekano wa kutoka kwenye mpango mkuu uliowekwa. Sehemu ya simulizi ambayo watoto wote saba walipitishwa kwa Samweli imerahisishwa. Kama itakuwa na msaada kipande hiki ikijumuishwa kama sehemu kifaa cha simulizi, i.e. hadhira yako kweli inataka kurudia na kusika kwamba kila mtoto, kwa zamu, alikataliwa, basi unaweza kukijumuisha katika sehemu hii ya simulizi. Kanuni Tabia na kawaida ya Mungu Hutunza ahadi zake; anastahili kuabudiwa; hujifunua yeye mwenyewe na kusudi lake; anaongea na watu; anajua mawazo na nia za watu; hufanya maamuzi tofauti na wanadamu; Roho wake huja juu ya watu; anawaita watu kwa ajili ya kusudi lake; upendo wake haushindwi. Kanisa Nyumba ya ibada; wazo Mungu wa Milele Hakika ya Wokovu Ufalme wa Mungu ni wa Milele Maisha ya Uchaji Kutembea na kuongea na Mungu; ibada nyumbani

24

Daudi na Batsheba2Samweli 11:1-18, 22-25, 26, 27 Kigezo katika: NLT

2Samweili 11:1-5 Muda fulani, wakati wa majira ya mwaka ya majani kuchipuka wakati wafalme waendapo vitani, Daudi alituma jeshi lake kupigana bali yeye alibaki nyumbani. Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme. Na alipotazama mjini, alimwona mwanamke mzuri akioga. Alimtuma mtu kuangalia alikuwa ni nani, na aliambiwa, Ni Betsheba, mke wa mmoja wa askari wako waaminifu na waliojitoa kikamilifu. Kisha Daudi akamchukua. Alipokuja katika jumba la kifalme (ikulu), Daudi akalala naye na kisha akarudi nyumbani. Baadaye, Betsheba alipogundua amekuwa mjamzito, alituma ujumbe kwa Daudi ili kumjulisha, na hakukuwa na shaka kwamba mtoto alikuwa wake kwani hakuwa na mimba mme wake alipokuwa nyumbani. 2Samweli 11:6-13 Kwa hiyo Daudi akamtumia ujumbe kamanda wa jeshi lake kumrudisha mme wake nyumbani. Alipofika, Daudi alimuuliza mme wake jinsi gani vita inaendelea. Kisha Daudi akamwambia, Nenda zako nyumbani na ukapumzike, lakini yeye hakwenda nyumbani. Usiku ule alibakia kwenye lango la nyumba ya mfalme pamoja na watumishi wa mfalme. Daudi aliposikia hakwenda nyumbani, alimuuliza, Kwa nini hukwenda nyumbani kwako jana usiku baada ya kuwa mbali kwa muda mrefu? Alijibu, jeshi linalala viwanjani. Ningewezaje kwenda nyumbani na kupumzika? Kisha Daudi akamwalika kwa chakula cha usiku siku iliyofuata na akamlevya. Bali hata hivo, hakumfanya askari kwenda nyumbani kwa mke wake. Kwa mara nyingine tena akalala langoni pa jumba la mfalme. 2Samweli 11:14-17 Siku iliyofuata asubuhi Daudi aliandika barua kwenda kwa kamanda wa jeshi lake na akampa mmewe Betsheba aupeleke. Barua ilitoa maelekezo kwa kamanda, Mweke askari huyu mstari wa mbele ambako vita ni kali. Kisha ondokeni ili kwamba auawe. Kwa hiyo kamanda akafanya kama alivyoambiwa. Mme wa Batsheba akauawa pamoja na askari kadhaa wengine. 2Samweli 11:18, 22-25 Kisha kamanda wa jeshi akamtuma mjumbe kwa Daudi kumpa taarifa za vita. Mjumbe alisema kwamba, mme wa Betsheba ameuawa pamoja na wengine. Vema. Mwambie kamanda asivunjike moyo, Daudi alisema. Watu wameuawa katika vita! Wakati mwingine piganeni kwa bidii! 2Samweli 11:26, 27 Na Betsheba aliposikia kwamba mme wake amekufa, akamwombolezea mmewe. Na kipindi cha maombolezo kilipokwisha, Daudi alimchukua katika jumba la mfalme, na akawa mmoja wa wake zake. Baadaye akamzaa mtoto wa kiume. Lakini Mungu alichukizwa sana na kile Daudi alichokifanya.

25

Falsafa za Maisha akalala naye Lugha nyingi zina namna mbalimbali za kuelezea uhusiano wa mapenzi. Tumia misemo sahihi ambayo haitaidhalilisha hadhira (walengwa). Umahiri wa Simulizi na hapakuwa na shaka kwamba mtoto alikuwa wake Kifungu hiki cha maneno kimeongezewa katika simulizi, kwa kuzingatia maelezo yaliyopo kwenye maandiko. Mwanamke amekwisha kutakasika unajisi wake baada ya kumaliza siku zake za mwezi Maandiko yanajumuisha taarifa hii kuonyesha kwamba mtoto lazima alikuwa wa Daudi. Hakuwa mtoto wa mmewe. Baadhi ya majina yameachwa kwa ajili ya kurahisha ukumbukaji na kuisimulia tena. Kanuni Tabia na Asili ya Mungu Hapendezwi na dhambi

26

Simulizi ya Nathani2Samweli 12:1-18, 24, 25 Kigezo NLT Mpito: Kwa sababu Mungu aliksirishwa na kile ambacho Daudi alifanya, 2Samweli 12:1-4 Mungu alimpeleka msemaji wake Nathani kumwambia Daudi hadithi hii: Palikuwa na watu wawili katika mji mmoja; mmoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa maskini. Yule tajiri alikuwa na kondoo na ngombe wengi. Yule maskini hakuwa na kitu, ila mwana kondoo mmoja, mdogo. Alimkuza na kumlea kama vile alikuwa mmoja wa watoto wake. Siku moja mgeni alifika katika nyumba ya Yule tajiri. Badala ya kuchinja mnyama kutoka katika kundi la mifugo yake, alimchukua kondoo wa yule msikini, akamchinja na kumwandalia mgeni wake. 2Samweli 12:5, 6 Daudi akakasirika. Akasema, Mtu yeyote anayeweza kufanya kitu kama hicho anastahili kufa! Ni lazima amrudishe mwanakondoo mara nne kwa yule maskini kwa yule mmoja aliyemwiba. 2Samwili 12:7-12 Kisha Nathani akamwambia Daudi, Wewe ndiwe mtu huyo! Mungu anasema, Nilikutia mafuta kuwa mfalme. Nilikupa ufalme wote. Na kama hayo yangalikuwa machache, ningelikuongezea zaidi, mambo kadhaa wa kadhaa. Kwa nini umeniasi na kufanya mambo haya mabaya? Umeua mtu na kuiba mke wake. Kwa sababu umemtendea Mungu dharau, kuanzia sasa na kuendelea, vurugu zitakuwa kwenye familia yako. Ulilolifanya kwa siri litatokea kwako wazi wazi. 2Samweli 13, 14 Kisha Daudi akakiri kwa Nathani, Nimemtenda Mungu Dhambi. Nathani akamjibu, Ndiyo, lakini Mungu amekusamehe na hutakufa kwa ajili ya dhambi. Lakini kwa sababu ya kile ulichokifanya mtoto wako atakufa. 2Samweli 12:15 18 Baada ya Nathani kurudi nyumbani kwake, mtoto wa Betsheba akaugua sana. ? Daudi akamsihi Mungu kumponya mtoto. Lakini siku saba baadaye mtoto alikufa. 2Samweli 12: 24, 25 Daudi akamfariji Betsheba na kisha akalala naye. Akapata mimba na akamzaa mtoto wa kiume. Wakampa jina la Sulemani, ambaye Mungu alimpenda.

27

Maneno/Vifungu vya Maneno ya Kujadili Ufalme Ni milki au eneo ambalo mfalme anatawala au kumiliki. Angalia Faharasa kwa ajili ya: Kusamehe Dhambi Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha unatumia maneno yale yale kwa upako, ukaidi/uasi na msemaji yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahiri wa Simulizi Kwa sababu umemtenda Mungu kwa dharau Kuweka wazi matendo ya ukaidi/uasi dhidi ya Mungu ni yapi; Fanya kwa uwazi kwa kusema, kitu kama, kwa sababu umenikaidi kwa kumuua na kufanya uzinzi. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Hapendezwi na dhambi; Hutumia wasemaji kukabiliana na dhambi; hutumia hadithi; hutoa; hapendi ukaidi, aliadhibu dhambi; husamehe dhambi; hutunza ahadi.

28

AhadiIsaya 53 Kigezo katika: NLT Simulizi hii ni ngumu kuielezea. Tunao mfano hapa chini wa simulizi yenye umahiri Mfano wa Simulizi yenye umahiri Kama mfalme Daudi, watu wa Mungu waliendelea kumtenda dhambi na kumkadi Mungu. Lakini Mungu hakuwasahau watu wake. Kwa sababu ya uasi wao, aliruhusu nchi zilizowazunguka kuingia na kuwateka na watu walitawanywa ulimwengu kote. Kabla hili halijatokea, Mungu alimtuma msemaji, Isaya, ili kuwapa ujumbe wake wa tumaini. Aliwaambia: Mungu atatupelekea Mkombozi. Kuna watu watamchukia na kumtenda vibaya. Atateswa kwa niaba yetu. Atachukua mizigo yetu na huzuni zetu. Atachapwa kwa mijeledi na kupigwa ili kutuletea amani. Sisi ni kama kondoo. Unajua jinsi kondoo walivyo. Wanazunguka zungaka nje ya njia na kupotea, tunazunguka nje ya njia ya Mungu. Tunamtenda dhambi, tunamkaidi Mungu. Bali, Mungu anaziweka dhambi zetu zote juu ya Mkombozi. Kwa hakika, Yeye ni kama kondoo apelekwaye machinjoni. Hawezi kusema lolote. Ataadhibiwa na kuawa kwa ajili ya dhambi zetu. Lakini kitu cha kushangangaza ni kwamba atauona uzima tena. Na kwa sababu ya hilo, watu wengi watarejesha uhusiano na Mungu. Huu ni ujumbe ambao Isaya aliupeleka kwa watu, na kuanzia wakati huo na kuendelea watu walisubiri kwa matarajio kwa ajili ya Mkombozi Aliyeahiwa kuja.

29

Maneno/Vifungu vya Maneno ya Kujadili Angalia Faharasa kwa ajili ya: Mkombozi/Mkombozi aliyeahidiwa Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha umatumia maneno yale yale kwenye ukaidi, uhusiano, dhambi na msemaji yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Chagua misemo ile ile kuielezea kwa watu wa Mungu katika mpangilio wote wa simulizi. Umahiri wa Simulizi Maelezo (commentaries) yanayokubaliana na kifungi hiki kuhusisha na matukio yajayo. Unabii katika muda uliopita yametumika mara nying katika mipito, lakini yanahusishwa na matukio ya baadaye. Vitenzi vimebadilika kwenda kwenye muda ujao ili kuonyesha usahihi zaidi, maana na kurahisisha simulizi kwenye hadhira. Mkombozi Aliyeahidiwa limetumika hapa badala ya mtumishi kuweka muda na wajibu wa ukombozi wa Yesu kwa uthabiti katika mpangilio wote wa simulizi. (Angalia hotuba ya Simeoni katika hadithi ya kuzaliwa). Maelezo yanakubaliana mtumishi huyu, yanamzungumzia Masihi atakayekuja Tumia msemo wowote unaozungumzia wazi zaidi kwenye makundi ya watu. Ni viuzri kutunza misemo hii kwa udhabiti katika mfululizo wote wa simulizi. aliongozwa kama mwanakondoo apelekwaye machinjoni Kama inaonekana inachanganya, uondoe mstari huu na kusema, Yeye ataongozwa kwenda kufa Sisi ni kama kondoo Kama maelezo ya watu kuwa kama kondoo aliyetoka nje ya njia ya Mungu yanawachanganya, maneno kama Tumetangatanga nje ya njia ya Mungu, tumetenda dhambi, yanaweza kutumika. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Huadhibu uasi/ukaidi, hujifunua, hutumia wasemaji wake; anaahidi Mkombozi, anarejesha uhusiano, na anasamehe; analeta tumaini; analeta njia ya wokovu; analeta amani, anazichukua dhambi; anateka kifo. Hakika ya Wakovu Mungu ana mpango kwa ajili yetu ili tuokolewa kutoka dhambi zetu na kuwa na uhusiano na yeye kupitia Mkombozi Aliyeahidiwa.

30

Malaika awatembelea Mariamu na YusufuMathayo 1:19-21, 24, 25; Luka 1:26-30, 34-39, 46-50, 56 Kigezo NLT

Mpito: Baada ya miaka mingi, hatimaye Mungu alimpeleka Mkombozi Aliyeahidiwa. Hii ni simulizi yake. Luka 1:26-30 Mungu alimtuma malaika kwa bikira aliyeitwa Mariamu. Alikuwa amechumbiwa ili aoelewe na mwanamme aliyeitwa Yusufu. Malaika akamtokea na Mariamu na kumwambia, Salaam, mwanamke uliyepata neema! Mungu yuko pamoja nawe! Akiwa amechanganyikiwa na kusumbuka, Mariamu alijaribu kufikiri malaika anaweza kumaanisha nini. Usiogope, Mariamu, malaika akamwambia, kwa kuwa Mungu ameamua kukubariki! Utachukua mimba na utapata mtoto wa kiume, na utamwita jina lake Yesu. Atakuwa mtu mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu. Luka 1:34-39 Mariamu akamuuliza malaika, Lakini nitawezaje kupata mtoto? Mimi ni bikira. Yule malaika akajibu, Roho wa Mungu atakujilia juu yako. Mtoto atakayezaliwa kwako atakuwa mtakatifu, na ataitwa Mwana wa Mungu. Kwa kuwa hakuna lisilowezekana kwa Mungu. Mariamu akaiitikia, Mimi ni mtumishi wa Bwana, na niko tayari kukubali chochote Anachokitaka. Yote uliyoyanena na yawe dhahiri. Na kisha malaika akaondoka. Mariamu akaenda kumtembelea ndugu yake Elizabeti aliyeishi kaktika mji mwingine. Luka 1:41 50, 56 Elizabeti na Mariamu walipoonana, walifurahi pamoja. Kisha Mariamu akasema Oo ni kwa jinsi gani ninamsifu Bwana. Ninafurahi katika Mungu mkombozi wangu! Kwa kuwa amemtazama mtumishi mdogo wa kike, na sasa vizazi na vizazi vitamwita mbarikiwa. Kwa kuwa aliye Mkuu ni Mtakatifu, na amefanya mambo makuu kwa ajili yangu. Rehema zake zinakwenda kizazi hadi kizazi, kwa wote wanaomhofu yeye. Mariamu akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu na kisha alirudi nyumbani kwao.

31

Mathayo 1:19-21 Yusufu, mchumba wake hakutaka kumwaibisha mchumba wake, kwa hiyo akaamua kuvunja uchumba kimya kimya. Alipokuwa akifikiri hayo, alilala usingizi, na malaika kutoka kwa Mungu akamotkea katika ndoto. Yusufu, mwana wa Daudi, malaika alisema, Usiogope, kuendelea na mipango yako ya harusi kumuoa Mariamu. Mtoto aliye ndani yake ametungwa kwa uwezo wa Roho wa Mungu. Atapata mtoto wa kiume, na utamwita jina lake Yesu, kwa sababu ndiye atakayewakomboa watu kutoka kwenye dhambi zao. Mathayo 1:24, 25 Yusufu alipoamka, alifanya kile alichoaamriwa na malaika na akamchukua Mariamu kama mke wake. Bali hakuwa na uhusiano naye wa kimapenzi mpaka baada ya mtoto wake kuzaliwa.

Maneno/Vifungu vya Maneno ya Kujadili Utakatifu Kuwa na uhusiano na Mungu, kuwekwa wakfu Kwake au kama Yeye. Tumia neno au kifungu cha maneno ambayo ni sahihi kuulezea utakatifu kama umetoka kwa Mungu Rehema Hii ni pale Mungu anapoonyesha ukarimu usio na sababu au huruma kwa mtu. Angalia Faharasa kwa ajili ya: Bwana Okoa Mwana wa Mungu Falsafa za Maisha Matumizi ya neno bikira linamaanisha, kabla hawajaishi pamoja kama mme na mke. Inaweza pia kumaanisha. kabla hawajawa na uhusiano wa kimapenzi. Tumia maelezo yoyote katika lugha itakayoonyesha wazi kwamba Mariamu hakuwa na mwanamme. Hakikisha kwamba linafaa kwa ajili ya kusanyiko la watu mchanganyiko kusikia na kusema. Ili kuuelewa mkangonyo aliokuwa nao Yusufu, ni muhimu kujua kwa namna gani utamaduni unautazza uchumba. Ikiwa unaandaa kwa ajili ya kusanyiko la wa Wamarekani, ongeza baadhi ya taarifa za kitamaduni ili kuonyesha ni kwa namna gani kufunga uchumba kunavyokuwa. Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha unatumia maneno yale yale kwa: Roho wa Mungu, malaika, Mkombozi Aliyeahidiwa, bariki, mkombozi, dhambi, wazao yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia.

32

Umahiri wa Simulizi Jina la malaika limeondolewa ili kurahisha simulizi. Roho wa Mungu atakuja juu yako. Namna ya kusema hili inaweza kuwa Roho wa Mungu alisababisha Mariamu kuwa mjamzito au nguvu ya Roho wa Mungu iliwezesha hili kutokea Hata hivyo, unaweza kusema hivi, hakikisha kwamba tendo la ndoa kati ya Roho wa Mungu na Mariamu HALITAFSIRIWI VIBAYA. Mwana wa ALiye Juu Aliye juu mara nyingi hutumika katika nafasi ya jina la Mungu kama ishara ya ukuu. Iwakiwa hadhira ina cheo (jina) sawa na hilo kwa ajili ya Mungu, hii inaweza kwenda vizuri. Kama sivyo, hakikisha kuwa linamaanisha Mungu. Kama sivyo sema tu, Mwana wa Mungu. Tumia kanuni hiyo hiyo, kwa Aliye Mkuu kama jina au cheo cha Mungu. Kwa kuwa yeye, Aliye Mkuu, ni Mtakatifu Utakatifu huu unamaanisha kuwa kitu fulani kujitenga kutoka dhambini au kisafi. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Hutunza ahadi zake; Roho wake yuko hai; Huongea na hulifunua kusudi lake; Anawahikikisha watoto wake; Huongea katika ndoto; hutumia wasemaji; humtuma mkombozi.

33

Kuzaliwa kwa YesuLuka 2:21, 22, 25, 28, 30-40 Kigezo kwenye NLT Mpito: Miezi michache baadaye, mtoto wa kiume alizaliwa na Mariamu katika Bethlehemu. Luka 2:21, 22, 25, 28 Siku nane baada ya kuzaliwa kwake. Aliitwa Yesu, jina alilopewa na malaika. Wazazi wake walimchukua kwenda Yerusalemu, mji maalumu kwa ajili ya Ibada ili kumweka wakfu mtoto kwa Mungu mahali pao pa kuabudia. Walipokwenda huko, walikutana na mzee mmoja ambaye alikuwa akimsubiri mkombozi aliyeahidiwa kuja na kuokoa watu wake. Alipomwona Yesu alimchukua mtoto mikononi mwake na akamtukuza Mungu, kwa kusema: Luka 2:30-32 Nimemwona mwokozi uliyemtoa kwa watu wote. Yeye ni nuru ya kumfunua Mungu kwa mataifa. Luka 2:33, 34 Yusufu na Mariamu walikuwa wakiyastaajabia yale yaliyonenwa kuhusu Yesu. Kisha yule mzee aliwabariki, na akamwambia Mariamu, Mtoto huyu atakataliwa na wengi na itakuwa kwa kuanguka kwa wengi. Lakini atakuwa ni mtu mkuu kwa wengine wengi. Na upanga utaingia moyoni mwako. Luka 2: 39, 40 Wazazi wa Yesu walirejea nyumbani. Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu. Akijaa hekima na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.

34

Maneno/Vifungu vya maneno ya Kujadili Angalia faharasa Yerusalemu Hekima Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha unatumia maneno yale yale kwa ajili ya mkombozi aliyeahidiwa, malaika, mkombozi/mwokozi, kuokoa, kuabudu na kubarikiwa yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahiri wa Simulizii mji ambapo walimwabudu Mungu Mji huo uliitwa Yerusalemu na utatokea mara kwa mara katika mpangilio wa simulizi. mahali pa ibada/kuabudu Mahali pa ibada/kuabudu limetumika badala ya Hekalu Kuwekwa wakfu kwa Yesu, katika Hekalu kumewekwa kuonyesha kwamba Yesu ni utimilifu wa unabii wa Isaya kutoka kwenye simulizi ya Ahadi. Kifungu cha kuwekwa wakfu katika simulizi kimetumiwa ili mfumo wa kafara katika hekalu usiweze kuelezewa katika mpangilio wa simulizi. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Hutunza ahadi yake; Roho wake yu hai; Anazungumza na kulifunua kusudi lake; anawakilisha watoto wake; anamtuma mkombozi. Kanisa Kwenda mahali pa kuabudia, kuabudu, kuweka wakfu watoto Uchaji Kuabudu/ibada.

35

Ubatizo wa YesuLuka 3:1-3, 10-16, 21-22; Mathayo 3:7-9, 13-15 Kigezo katika: NLT Mpito: Yesu akakua na kuwa kijana. Mungu alimtuma mjumbe mbele yake kuandaa njia kwa ajili ya watu kumpokea mkombozi aliyeahidiwa, Yesu. Luka 3:1, 2 Baada ya muda, ujumbe kutoka kwa Mungu ulimjia mtu aliyeitwa Yohana ambaye alikuwa akiishi nje nyikani. Luka 3:3 Yohana alikwenda sehemu mbalimbali akiwaambia watu wabatizwe kuonyeshwa kwamba wamegeuka kutoka dhambini na kumgeukia Mungu ili wasamehe. Mathayo 3:7-9 Baadhi ya viongozi wa dini walikuja kumsikiliza Yohana, na akawaambia, Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira ya Mungu inayokuja? Maisha yenu yadhihirishe kwamba mmemgeukia Mungu. Msismezane nini kwa ninyi kwamba, sisi tu salama, kwa kuwa tu wa uzao wa Ibrahimu. Hiyo haina maana yo yote. Mungu anaweza kuyabadili mawe haya kuwa uzao Ibrahimu. Luka 3:10-14 Makutano wakamuuliza, Tufanye nini basi? Yohana akajibu, Ikiwa una kanzu mbili, mpe maskini, ikiwa una chakula wape wale walio na njaa. Hata watoza ushuru mafisadi wakamjia ili kubatizwa na wakauliza, Mwalimu, tufanyeje sisi nasi? Onyesheni uaminifu wenu, akajibu. Hakikisheni hammtozi mtu zaidi ya kodi ambayo serikali inawataka ninyi kukusanya. Tufanyeje sisi nasi? Wakamjia baadhi ya askari. Yohana akajibu, msimdhulumu mtu, wala msimshitaki mtu kwa mambo manayojua hawakufanya. Mtoshewe na mshahara wenu. Luka 3:15, 16 Kila mtu alikuwa akimtarajia Mkombozi Aliyeahdiwa kuja haraka, na walikuwa na shauku kujua ikiwa Yohana ndiye. Yohana aliwajibu maswali yao kwa kusema, Mimi nabatiza kwa maji, bali yupo mtu anakuja karibuni, huyo ni mkuu kuliko mimi mkubwa sana kiasi ambacho mimi sistahili hata kuwa mtumwa wake. Yeye atawabatiza ninyi kwa Roho wa Mungu na kwa moto.

36

Luka 3:21a Siku moja makutano walipokuwa wakibatizwa, Mathayo 3:13 15 Yesu mwenyewe akaja ili abatizwe na Yohana japokuwa Yesu hakutenda dhambi. Lakini Yohana alijaribu kusema naye juu ya hilo. Mimi ndiye ninayestahili kubatizwa na wewe, akasema, hivyo kwa nini unakuja kwangu? Lakini Yesu alisema, Hivi ndivyo itupasavyo kufanya, kwa kuwa tunavyopaswa kuyatimiza yote tuliyoamuriwa na Mungu: Kwa hiyo Yohana akakubali kumbatiza. Luka 3:21b-22 Baadaye, Yesu alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka, na Roho wa Mungu akashuka juu yake katika mfano wa hua. Na sauti kutoka mbinguni ilisema, Wewe ni mwanangu, ninakupenda na ninapendezwa nawe.

37 Maneno/Vifungu vya maneno ya Kujadili Sauti kutoka mbinguni Sauti kutoka mbinguni tayari imekubalika kuwa ni sauti ya Mungu mwenyewe. Inakubalika kutumiwa sauti ya Mungu waligeuka kutoka dhambini na kumgeukia Mungu ili wasamehewe. Hivi ndivyo NLT inavyosema. majuto makubwa. Hii ni picha nzuri ya nini hasa kinatokea pale tunapotubu au kujuta, na limependekezwa badala yake litumike neno moja tubu. Angalia Faharasa kwa ajili ya: Ubatizo Viongozi wa Dini Falsafa za Maisha Kumbuka kwamba katika tamaduni na dini nyingi watu wana taratibu za kunawa/kujiosha mara kwa mara kuondoa dhambi. Fafanua kwamba, huu ni utaratibu unaofanyika mara moja tu. Ikiwa ni lazima ishara ya kuoshwa inaweza kutumika. Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha unatumia maneno yale yale kwa ajili ya: msemaji, dhambi, Mkombozi Aliyeahidiwa, kusamehe, wazao wa Ibrahimu na Roho wa Mungu kama yalivyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahiri wa Simulizi Wazao wa Ibrahimu Tafadhali zingatia kwamba uzao wa Ibrahimu katika maandiko ya NLT inamaanisha watoto wa Ibrahimu. Kifungu hiki cha maneno pia kinakazia mwambatano ndani ya simulizi kwa kutumia wazao wa Ibrahimu mahali pa watu wa Mungu katika mfululizo wote wa simulizi. kwa moto Kifungu hiki cha maneno kimujumuishwa kwenye masimulizi ya Mathayo na Luka, lakini si katika masimulizi ya Marko. Watoa maelezo wana maoni tofauti kuhusiana na kinachoitwa kwa moto. Ikiwa kutumia kifungu kwa moto linaichanganya zaidi hadhira, yanaweza kuachwa. hata kama Yesu hakutenda dhambi Kwa sababu Yesu hakutenda dhambi; kifungu hiki kilijumuishwa ili kuzuia rabsha (kuchanganyikiwa). Imetiliwa mkazo katika 1Korintho 5:21.

38 Kanuni Tabia na asili ya Mungu Mungu hutuma Roho wake, Hutumia wasemaji, anamkubali Yesu kama mwanaye, anatunza ahadi zake, anasamehe dhambi, anahukumu dhambi, huzungumza na kulifunua kusudi na utashi wake. Kanisa Ubatizo: Watu wa Mungu inajumuisha watu wengi zaidi ya wazao wa Ibrahimu. Maisha ya Uchaji Mfano wa Yesu akiomba Kushirikisha Injili Yesu aliwaambia watu wabatizwe, wageuke kutoka dhambi zao na kumgeukia Mungu Maombi Yesu alipokuwa akiomba, Roho wa Mungu alishuka juu yake katika mfano wa hua.

39

Mwanamke KisimaniYohana 4:5-19, 25-30, 42 Kigezo katika: NLT Mpito: Baada ya hayo, Yesu aliwachangua wanaume kumi na mbili kuwa wafuasi wake wa karibu. Walisafiri maeneo mbalimbali wakihubiri ujumbe wa Ufalme wa Mungu kila walipokwenda. Wanaume na wanawake wengi walianza kumfuata. Yohana 4:5-8 Yesu alikwenda katika kijiji cha Samaria karibu na kisima. Alikuwa amechoka kutokana na safari ndefu na akaketi chini kando ya kisima. Mara mwanamke msamaria alikuja kuchota maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe. Naye alikuwa pekee yake wakati huo kwa sababu wafuasi wake wa karibu walikwenda kijijini kununua chakula. Yohana 4:9-15 Mwanamke alishangazwa, kwa sababu wazao wa Ibrahimu walikataa kuwa na uhusiano wowote na Wasamaria. Mwanamke akamwambia Yesu, Wewe ni wa uzao wa Ibrahimu, na mimi ni mwanamke Msamaria. Kwa nini unaniomba maji ya kunywa? Yesu akamjibu, . Watu hupata kiu tena baada ya kunywa maji haya. Lakini maji nikupayo huondoa kiu kabisa. Maji hayo yatakuwa chemichemi ibubujikayo ndani yao, ikiwapa uzima wa milele au maisha halisi ambayo hayatakuwa na mwisho. Tafadhali Bwana, Mwanamke akasema, Unipe maji hayo kisha sitakuwa nafuata maji hapa tena. Yohana 4:16-19 Nenda umlete mmeo, Yesu akamwambia. Sina mume, mwanamke akajibu. Yesu akasema, Sawa, umesema vema! Huna mume kwa kuwa umekuwa na waume watano na hata sasa huyo unayeishi naye hujaolewa naye. Kwa hakika umesema kweli. Bwana, mwanamke akasema, Wewe lazima utakuwa msemaji wa Mungu. (**) Yohana 4:25-30 Mwanamke akasema, Mimi najua Mkombozi Aliyeahidiwa anakuja yule aitwaye Kristo. Huyo atakapokuja, atatueleza mambo yote. Kisha Yesu akamwambia, Mimi ndiye mkombozi aliyeahidiwa! Mara kitambo wafuasi wake wakarudi. Walistaajabu kumkuta akiongea na mwanamke. Mwanamke aliacha mtungi wake karibu na kisima na alikimbia kwenda kijijini, akimwambia kila mtu, Njooni na mmuone mtu aliyeniambia mambo yote niliyofanya.

40

Yawezekana kuwa ndiye Mkombozi Aliyeadiwa? Kwa hiyo watu wakaja kwa wingi kutoka kijijini kumwona Yeye (Yesu). Yohana 4:42 Kisha watu wakamwambi mwanamke, Sasa tunaamini, siyo tu kwa sababu ya yale uliyotuambia, bali kwa sababu tumekwisha msikia wenye. Sasa tunajua hakika huyu ndiye mwokozi wa ulimwengu.

41

Maneno/Vufungu vya Maneno ya Kujadili Msamaria Wasamaria si wa uzao wa Ibrahimu. Wazao wa Ibrahimu waliwachukia Wasamaria. Ikiwa tamaduni za watu unaofanya nao kazi zina kitu hicho hicho, tumia majina hayo. Vinginevyo itazalisha chuki kwa kutumia majina hayo ya . Angalia Faharasa kwa ajili ya: Wafuasi wa Karibu Uzima wa milele Wafuasi Ufalme wa Mungu Falsafa za Maisha Yesu alichukua hatua kuvuka mipaka ya uhusiano kati ya wazao wa Ibrahimu/Msamaria wa kiume/kike kwa kuongea na mwanamke huyo. Hakikisha walengwa wanaelewa kwamba Yesu alifanya kwa namna inayofaa na heshima kwa mwanamke huyo; na kwamba hakukuwa na tabia isiyofaa iliyojitokeza, kiasi kwamba yule mwanamke alimwita Yesu Bwana. Tumia neno katika lugha ambayo ni ya heshima na itatoa mtazamo mzuri (chanya) wa Yesu. Ikiwa kutamka kwamba Yesu alikuwa pekee yake na mwanamke, pale mwanzo wa simulizi, kunaweza kusababisha wasikilizaji kwa haraka kumfikiria vibaya Yesu, itoe sentensi hiyo. Itazuia kuleta picha mbaya ya Yesu kabla hadhira haijapata fursa ya kusikia mazungumzo kati ya Yesu na mwanamke. Inaweza kuwa muhimu kusema Wasamaria pia walikuwa wakiutarajia ujio wa Mkombozi Aliyeahidiwa. Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha unatumia maneno yale yale kwa ajili ya: Wazao wa Ibrahimu, Kuabudu, Roho wa Mungu, Msemaji, Mkombozi, na Mkombozi aliyeahidiwa yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia Umahiri wa Simulizi Neno Uzima wa milele katika simulizi limejuishwa ili kufafanua kwamba maji anayoyatoa Yesu yanakuwa kama chemichemi. Baadhi ya lugha zinazaweza kuhitaji ufafanuzi ili sentensi zilete maana au zieleweke.

42

Mazungumzo kati ya Yesu na mwanamke ni vigumu kuyarudia na kuyakumbuka. Baadhi ya mambo yaliyojirudia yamerahishwa na sehemu ya mazungumzo ambayo hayahusiani moja kwa moja na sababu za kuwa na simulizi hii katika mpangilio wa hadithi yameondoelewa. (**) Yohana 4:20-24; Yaliyopigiwa mstari hapa chini, yanaweza kuingizwa isipokuwa kama hayatailetea rabsha hadhira. Niambie, ni mahal gani sahihi pa kumwabudu Mungu? Aliuliza mwanamke. Yesu alijibu, Haijalishi wapi unaabudu. Kwa nguvu za Roho wa Mungu watu watamwabudu Mungu katika uhalisia wake, wakimfanyia ibada kamili anayoitaka Kanuni Tabia na Asili ya Mungu Hutaka vitu maalumu kwa watu; anataka watu kumjua Yeye; Huwaambia watu ukweli hata kama hawauelewi; Hukabiliana na watu katika hali ya upendo; Huwapa mwaliko kupokea kile alicho nacho kwa ajili yao; Huwasaidia watu kuondokana na udini na kuingia katika uhusiano halisi na Mungu; Hukabiliana na dhambi zetu; Husaidia watu kutafuta kumjua Yeye. Kushirikisha Injili Mwanamke alipoifahamu kweli, alitaka kushirikiana na watu wa mji wote. Ushuhudiaji Ni vizuri kwa waamini wapya kuwaeleza watu wote katika jamii juu ya imani yao. Hawahitaji kusubiri mpaka wawe wamefundishwa.

43

Binti wa Yairo na Mwanamke aliyetokwa na DamuLuka 8:40-56 Kigezo katika: NLTMpito: Yesu aliendelea kusafiri maeneo mbalimbali akifundisha watu na kufanya miujiza mingi. Luka 8:40-42 Makutano walimkaribisha Yesu, kwa sababu walikuwa wakimsubiri Yeye. Mwanamme aliyeitwa Yairo, kiongozi katika kusanyiko la kuabudia la mahali pamoja, alikuja na kuanguka miguuni pa Yesu, akamsihi kwenda naye nyumbani kwake. Binti yake wa pekee, ambaye alikaribia miaka kumi na miwili alikuwa kufani. Yesu alipokuwa akienda na Yairo, alikuwa amezungukwa na makutano. Luka 8:43-46 Mwanamke katikati ya makutano alikuwa ameteswa kwa miaka kumi na mbili kwa kutokwa na damu, na hakuweza kupata tiba. Akija nyuma ya Yesu, aligusa pindo la nguo Yake. Ghafla damu ilikoma. Ni nani aliyenigusa? Yesu aliuliza. Kila mtu alikataa, na mmoja kati ya wafuasi wa karibu wa Yesu alisema, Bwana, makutano hawa wote wanakusonga wewe. Lakini Yesu akasema, Kuna mtu kwa hakika amenigusa, kwa kuwa nimehisi nguvu ya kuponya ikinitoka. Luka 8:47, 48 Mwanamke alipogundua kwamba hawezi kuendelea kujificha, alianza kutetemeka na akaanguka magotini mbele Yake. Mkutano wote walisikia mwanamke akieleza kwa nini alikuwa amemgusa Yesu na kwamba aliponywa saa ile ile. Mwanamke, Alimwambia mwanamke, imani yako imekufanya uwe mzima. Nenda kwa amani. Luka 8:49-56 Alipokuwa akiendelea kuongea na mwanamke, mjumbe alifika kutoka nyumbani kwa Yairo, kiongozi wa mahali pa kuabudia. Akamwambia, Binti yako amekufa. Hakuna haja ya kumsumbua Mwalimu sasa. Lakini Yesu aliposikia kile kilichotokea, akamwambia Yairo, Usiogope. Uwe na imani tu, na ataponywa. Walipofika katika nyumba, Yesu hakuruhusu mtu yeyote kuingia ndani pamoja naye isipokuwa watatu kati ya wafuasi wake wa karibu, Petro, Yohana, Yakobo, na baba na mama wa binti mdogo. Nyumba ilikuwa imejaa watu wakilia na kumboleza, lakini aliwaambia, Nyamazeni! Hakufa; Amelala tu. Bali makutano walimcheka kwa sababu walijua alikuwa amekufa. Kisha Yesu akamshika binti mkono na akasema kwa sauti, Mwanangu, inuka! Na wakati ule uhai wake ukarejea, na ghafla

44 akasimama! Kisha Yesu akawaambia mpeni chakula ale. Wazazi wake wakastaajabu sana, bali Yesu akasisitiza kwamba wasimwambie mtu kile kilichotokea.

Maneno/Vifungu vya Maneno ya Kujadili Angalia Faharasi kwa ajili ya: Imani Bwana Muujiza Falsafa za Maisha Kutokwa damu kwa mwanamke kutakuwa kulimfanya awe najisi katika mfumo dini yao. Hili linaweza kumwelezea kwa nini alikuwa na tabia isiyo ya kawaida. Tumia maneno kulielezea tatizo lake la kutoka damu kwamba si la kuchikiza katika mkusanyiko wa watu. Watu walikuwa wanalia na kuomboleza. Hii inaonyesha uzito wa maombelezo kwa ajili ya mtu aliyekufa. Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha kutumia maneno yale yale kwa ajili ya: mahali pa kuabudia na wafuasi wa karibu yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahiri wa Simulizi Hakikisha tafsiri ya kifungu cha maneno Nilihisi nguvu za kuponya zikinitoka haimaanishi kwamba Yesu alipoteza cho chote katika nguvu yake ya kuponya kwa sababu ya mama kumgusa. Mwanangu haimaanishi msichna ni binti wa Yesu kibaolojia. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Mungu anamjua kila mtu hata kama ni maskini na mgonjwa; anajali juu ya masuala ya watu wanayoyapitia; anajali juu ya wanawake, anatuhamasisha kumwamini na kumtumaini Yeye; Anahuruma kubwa kwa ajili ya watu wake, Ana nguvu dhidi ya kifo. Imani Mungu anatutegemea sisi kumwendea yeye kwa imani, tukiamini atatuponya na kutusaidia wakati wa uhitaji.

45

Yesu Awalisha 5,000Luka 9:10-17 Kigezo kwenye NLT Mpito: Yesu aliwapa nguvu na mamlaka wafuasi wake wa karibu. Siku moja aliwatuma waende vijijini ambako waliwafundisha watu na kufanya miujiza mingi. Luka 9:10-12 Wakati wafuasi wa Yesu wa karibu waliporudi, walimweleza Yesu kila kitu walichofanya. Kisha akaondoka nao kimya kimya kwenda kwenye mji wa karibu. Lakini makutano walijua wapi alikuwa akienda, na wakamfuata. Aliwakaribisha na akawafundisha juu ya Ufalme wa Mungu, na akawaponya wale waliokuwa wagonjwa. Baadaye jioni wafuasi wake wa karibu walimwendea na kusema, Waruhusu makutano waende kwenye vijiji na mashamba ya karibu, ili waweze kutafuta chakula na mahali pa kulala kwa ajili ya usiku. Hakuna chakula cho chote katika eneo hili la porini. Luka 9:13-14 Lakini Yesu akasema, Wapeni ninyi chakula. Lakini tunayo mikate mitano tu na samaki wawili, walijimjibu. Au unatutegema sisi tuende nje na kununua chakula cha kwa kuwatosha hawa makutano wote? Kulikuwa na zaidi ya watu 5,000 wanaume ukijumulisha wanawake na watoto. Yesu akajibu, Waketisheni chini katika makundi ya kama watu hamsini. Luka 9:15-17 Kwa hiyo watu wakakaa chini. Yesu akaichukua mikate mitano na samaki wawili, akaangalia kuelekea mbinguni, na akavibarikia. Kisha, akaikata mikate katika vipande vipande, Aliendelea kuwagawa mikate na samaki kwa wafuasi wake wa karibu ili waweze kuigawa kwa watu. Wote walikula kwa kadri walivyotaka, na baadaye, wafuasi wa karibu walikusanya makapu kumi na mbili yaliyojaa mabaki!

46

Mwambatano Ndani ya Simulizi Hakikisha unatumia maneno yale yale kwa ajili ya: wafuasi wa karibu, miujiza, Ufalme wa Mungu, mbinguni, na kubarikiwa yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahiri wa Simulizi Mkate na Samaki Kuongezeka kulikuwa kwa tendo la kimuujiza au muujiza. Hakikisha kulihusisha katika namna ambayo ni rahisi kueleweka. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Anazo nguvu za kufanya miujiza; Mungu anajali juu ya mahitaji ya watu; Mungu anaweza kuchukua kidogo mtu alicho nacho na kukiongeza; Mungu anawaamini wafuasi wake.

47

Viongozi wa Dini wenye WivuLuka 19:47, 48; 20:1-8 Kigezo kwenye NLT Mpito: Watu wengi waliomfuata Yesu walipenda kile alichokifanya, lakini siyo Viongozi wa Dini. Walikuwa na wivu juu ya Yesu. Luka 19:47, 48 Baada ya hayo, Alifundisha kila siku mahali pa kuabudia, lakini viongozi wa dini wa watu walijaribu namna wakatakavyomuua. Lakini kwa sababu watu walimsikiliza Yeye kwa karibu, hawakufikiria kwa njia gani. Luka 20:1, 2 Siku moja wakati Yesu akiwafundisha watu na kuhubiri ujumbe wa Mungu katika mahali pa kuabudia, viongozi wa dini walimjia. Walimtaka, Kwa mamlaka ya nani unafanya haya yote? Nani aliyekupa wewe haki? Luka 20:3-8 Ngojeni niwaulize swali kwanza, Yesu aliwajibu. Je, mamlaka ya Yohana kubatiza ilitoka mbinguni, au ilitoka tu kwa wanadamu? Wakasemezana wao kwa wao. Kama tukisema ulitoka mbinguni, Atatuuliza kwa nini hatukumwamini Yohana. Lakini tukisema ulitoka tu kwa wanadamu, watu watatupiga mawe sisi kwa sababu kwa sababu wamemkubali Yohana kuwa alikuwa mmoja wa wajumbe wa Mungu. Kwa hiyo mwishowe walijibu kwamba hawakujua. Na Yesu akajibu, Basi sitawaambia kwa mamlaka ya nani nafanya mambo haya yote.

48

Falsafa za Maisha Viongozi wa dini hawakuwa na haki ya kisheria kumuua mtu au kumfanya mtu auwe. Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha kutumia maneno yaleyale kwa ajili ya: viongozi wa dini, mahali pa kuabudia, Ujumbe wa Mungu, Batiza, mbinguni, na Msemaji wa Mungu (mjumbe) yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahiri wa Simulizi Tupige sisi kwa mawe Njia ya kifo (adhabu ya kifo). Kanuni Tabia na asili ya Mungu Yesu hakuwaogopa watu au viongozi; Yesu alikabiliana na kutokuamini.

49

Mwanamke Mwenye Dhambi AsamehewaYohana 8:1-11 Kigezo katika: NLT Mpito: Yesu alisafiri kwenda Yerusalemu, mji ambapo wazao wa Ibrahimu walimwabudu Mungu. Wakati wa mchana, alikuwa akifundisha katika mahali pa kuabudia. Yohana 8:2 6 Siku moja, alipokuwa akifundisha makutano ghafla walikusanyika, na alikaa chini na kuwafundisha. Alikuwa akiongea, viongozi wa dini walimleta mwanamke waliyemkamata katika tendo la uzinzi. Walimweka mbele ya makutano. Mwalimu, walimwambia Yesu, mwanamke huyu amekamatwa katika tendo la uzinzi. Sheria ya dini yetu inasema auwe kwa kupigwa mawe. Je wewe unasemaje? Walikuwa wakijaribu kumkamata katika kusema kitu watakachokitumia dhidi yake, lakini Yesu hakujibu mara moja. Yohana 8:7, 8 Waliendelea kudai jibu, kwa hiyo akasimama tena na kusema, Sawa, mpigeni mawe. Lakini wale ambao hawajawahi kutenda dhambi warushe jiwe la kwanza! Yohana 8:9-11 Wale washitaki waliposikia hili, waliondoka taratibu mmoja mmoja, kuanzia ya yule mkubwa, hadi Yesu alipoachwa katikati ya kundi na mwanamke. Yesu alisimama tena na kumwambia mwanamke, Wako wapi washitaki wako? Hakuna hata mmoja aliyekuhukumu? Hapana, Bwana, mwanamke alisema. Na Yesu alisema, Na mimi sikuhumu. Nenda na usitende dhambi tena.

50

Mwambatano ndani za Simulizi Hakikisha unatumia maneno yaleyale kwa ajili ya: wazao wa Ibrahimu, mahali pa kuabudia, Yerusalemu, Kuabudu, viongozi wa dini, dhambi, na Bwana yaliyotumika katika simulizi zilizopita. Umahiri wa Simulizi Viongozi wa dini walikuwa wakijaribu kuthibitisha kwamba Yesu alikuwa akiwafundisha watu kuikaidi sheria. Viongozi wa dini wanarejea kwenye Sheria ya Musa, lakini kwa sababu hatumtaji Musa katika mpangilio wa simulizi, tumekirahisisha kifungu cha maneno kuwa, sheria za dini yetu. Zingatia kwamba hawakumleta mwanamme aliyeshirikiana naye katika tendo. Sheria inataka kwamba wote wawili wanatakiwa kupigwa mawe. Kifungu cha maneno auawe kwa kupigwa mawe kimejumuishwa ili walengwa ambao hawana uzoefu wa kupigwa mawe wataweza kuelewa kwamba inamaanisha ni namna ya adhabu ya kifo. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Wakati dini inalaumu watu, Mungu anataka kuwaokoa; Mungu huwatendea sawa sawa, wanawake na wanaume.

51

Njama na Mlo wa Mwisho wa Jioni.Luka 22:1-6, 14, 15, 19-23; Yohana 13:3-5, 12-17; Mathayo 26:30 Imetumia tafsiri ya Biblia ya: NLT Badiliko: Viongozi wa dini wa wakati ule walianza kukosa amani kwa sababu Yesu alitoa madai, kamaMimi na Baba tu umoja; Yeye anaionaye mimi amemwona Baba/Mungu. Walikuwa na wivu kwa sababu watu wengi walimwamini na walikuwa wakimsifu Yeye. wakajikusanya pamoja kupanga namna ya kumuua. Luka 22:1-6 Sikukuu kubwa ya kidini ilikuwa inakaribia. Wakuu wa viongozi wa dini walichangamkia mpangowa mauaji ya Yesu. Lakini walitaka kumuua bila kuanzisha machafuko, uwezekano ambao waliuhofia sana. Kisha Shetani akamuingia Yuda, ambaye alikuwa mmoja wa wafuasi kumi na wawili wa karibu, na alikwenda kwa viongozi wa dini kujadilana nao ana njia nzuri ya kumsaliti Yesu kwao. Walifurahishwa kwamba alikuwa tayari kuwasaidia, na wakamuahidi zawadi. Kwa hiyo akaanza kutafuta fursa ya kumsaliti Yesu ili waweze kumkamata kimya kimya wakati makutano hawatakuwapo. Luka 22:14, 15 Yesu na wafuasi wake kumi na mbili wa karibu, walikaa pamoja mezani kusherehekea mlo kwa ajili ya sikukuu ya kidini. Yesu akasema, Nimekuwa nikitazamia kula mlo huu pamoja nanyi kabla yakuanza kwa mateso yangu. Yohana 13:3-5, 12-17 Yesu alijua Mungu amempa mamlaka juu ya kila kitu. Aliondoka kutoka mezani, akavua vazi lake, akajifunga taulo kiunoni mwake, na akamiminamaji kwenye beseni. Kisha akaanza kuwanawisha wafuasi wake wa karibu miguu na kuwafuta kwa taulo alilojifunga kiunoni. Baada ya kuwatawadha miguu yao, alivaa vazi lake tena na kukaa chini na akawauliza, Mnaelewa kile nilichokuwa nafanya? Mnaniita Mwalimu na Bwana, Na mko sahihi, kwa sababu ni kweli. Kwa kuwa Mimi, Bwana na Mwalimu wenu, nimewaosha miguu yenu, imewapasa kuoshana miguu ninyi kwa ninyi. Nimewapeni mfano wa kufuata. Fanyeni hivyo ninyi kwa ninyi kama nilivyowatendea. Ni kweli mtumishi si mkuu kuliko Bwana.Mnayajua mambo haya yote-sasa ya fanyeni! Luka 22:19-23 Yesu pia alichukua sehemu ya mkate, akamshukuru Mungu na akawagawia wafuasi wake wa karibu wapate kula. Akasema, Mkate huu unawakilisha Mwili wangu, umetolewa kwenu. Fanyeni hivi ili kunikumbuka mimi. Baada ya chakula cha jioni alichukua kikombe cha mvinyo na kusema, Mvinyo ni ishara ya ahadi mpya ya Mungu kuwaokoa ninyi makubaliano yaliyofungwa kwa damu nitakayoimwaga kwa ajili yenu.

52 Mathayo 26:30 Kisha wakaimba wimbo wa sifa, na wakaenda mahali palipoachwa ukiwa katika mlima wa Mizeituni nje ya mji.

53

Maneno/Vifungu vya Maneno vya kujadili mtumishi si mkuu kuliko Bwana Maana yake ni kwamba Wafuasi wa Yesu hawawezi kujihesabia kuwa wa muhimu sana kutenda kama watumishi, kwa sababu Yesu mwenyewe alijifanya mtumishi. Wao pia wasitegemee kutendewa vizuri zaidi kutoka kwenye ulimwengu kuliko Yesu alivyopewa. Mkate Hadhira inaweza isilielewe neno mkate. Neno lingine la mkate kama vile mikate kwa lugha nyingine inaweza kutumika kutumika. Viwakilishi/Ishara Baadhi ya wasomi wa Biblia wanakubaliana kwamba Yesu alikuwa akitumia mkate na mvinyo kama ishara au viwakilishi ya mwili na damu yake. Yesu alitumia,viwakilishi vinavyoshabihiana katika hotuba alipotoa matamshi kama vile; Mimi ni mlango na Mimi ni mkate wa uzima Wimbo wa Sifa Huu unawezakana kabisa ulikuwa wimbo ulioimbwa kama sehemu ya Mlo wa Pasaka uliojulikana kama Hallel, wimbo wa sifa kwa Mungu.Kwa kawaida ya tafsiri msemo huu ni wimbo wa shukrani au wimbo wa sifa kwa Mungu Angalia faharasa kwa ajili ya: Baba Falsafa za Maisha Katika tamaduni ambapo kutaja neno mvinyo ni machukizo ya hali juu au kutasababisha watu kutomheshimu Yesu, sema kikombe au kikombe cha kinywaji. Mwambatano ndani ya Simulizi Hakikisha kutumia maneno yale yale kwa ajili; Wafuasi wa karibu, Shetani, Bwana, viongozi wa dini na Okoa, yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahili wa simulizi Kuokoa Hadhira haielewi Mungu anatuokoa kutoka wapi, tengeneza ahadi mpya iliyo wazi kwa kusema kitu kama, kuwaokoa ninyi kutoka dhambi zenu kuwasamehe ninyi kutoka dhambi zenu n.k. Agano lililofungwa kwa damu nitakayoimwaga kwa ajili yenu Hadhira inaweza kuifahamu au kutoifahamu ahadi/agano lililofungwa katika damu. Ikiwa sivyo, badilisha kifungu hiki cha maneno kuwa kitu kama, makubaliano yaliyowezeshwa na kifo

54

change kwa kuwaruhusu watu waniue mimi. Tukio la Yesu kuwatawadha miguu wafuasi wake limejumuishwa kwa sababu limeonekana kuwa la muhimu sana katika utamaduni wa Asia kuonyesha wazo la uongozi wa kitumishi. Hii imedhihirishwa wazi katika tamaduni nyingi kwa neno picha kutawadha miguu. Simulizi hii ilipokuwa ikijaribiwa, watu wengi walisema hii ndio ilikuwa sehemu ya muhimu sana katika simulizi. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Mungu amelitoa agano au ahadi mpya; anao mpango. Kanisa Utumishi/huduma; Mlo wa Mwisho uliasisiwa; Kuabudu Maombi Yesu alimshukuru Mungu kwa ajili ya elementi za Mlo wa Mwisho

55

Yesu AsalitiwaLuka 22:47-54, 63-71 Kigezo katika: NLT Mpito: Yesu na wafuasi wake wa karibu, waliondoka mahali pa kuabudia na kwenda mahali penye utulivu kuongea na kuomba. Yuda alikubali kwa siri kumsaliti Yesu kwa viongozi wa dini kwa hiyo aliondoka kwenda kukutana nao. Luka 22:47-54 Wakati Yesu alipokuwa akiongea na wafuasi wake wa karibu, kundi la watu lilimkaribia likiongozwa na Yuda aliyekuwa akimsaliti Yesu. Yuda alikwenda moja kwa moja kwa Yesu kumsalimia kwa busu. Lakini Yesu akamwambia, Yuda, unaweza kunisaliti mimi kwa busu? Wafuasi wengine wa karibu waliposogea waliona nini kilikuwa kinakwenda kutokea, wakatamka ghafla, Je tunaweza kupigana nao? Tumekuja na mapanga yetu! Mmoja wao akamshambulia kichwani mmoja wa watumishi wa viongozi wa dini, akamkata na kuliondoa sikio lake la kuume. Lakini Yesu akasema, hakuna tena haya Akaligusa sikio la mtu huyu na kumponya. Kisha Yesu akazungumza na viongozi wa dini waliokuja kumkamata. Je mimi ni mhalifu hatari, aliuliza, kwamba mnanijia kwa mapanga na marungu kunikamata? Kwa nini hamkunikamata katika mahali pa kuabudia? Nilikuwa pale kila siku. Lakini huu ni wakati wenu, wakati ambao mamlaka za giza hutawala. Kwa hiyo wakamkamata na kumpekeka nyumbani kwa kiongozi wa dini. Petro alimfuata kwa mbali. Luka 22: 63-71 Walinzi waliomlinda Yesu walianza kumdhihaki na kumpiga. Walimfunga macho yake na kusema, Tuambie ni nani aliyekupiga wakati ule? wakamtolea maneno mengi mengi ya kumtukana. Kulipokucha viongozi wote wa dini walikusanyika. Yesu aliongozwa mbele ya mkutano wa dini, na walisema, Tuambie, wewe ni Mkombozi Aliyeahidiwa? Akajibu, Ikiwa nitawaambia hamtaniamini. Na kama nikiwauliza swali, hamwezi kunijibu. Lakini tangu sasa, Nitakuwa nimeketi mahali penye nguvu, mkono wa kuume wa Mungu. Wakapaza sauti, Kwa hiyo unadai kuwa Mwana wa Mungu? Na akajibu, Ninyi mnasema mimi ndiye. Kwa nini tunahitaji mashahidi wengine? walisema, Sisi wenyewe tumesikia alichokisema.

56

Falsafa za Maisha Mwana wa Mungu Kama unafanya kazi katikati ya makundi ya watu wa Kiislamu ambao wanaweza kukasirishwa kwa neno Mwana, au ikiwa inamaanisha mtoto wa kuzaliwa kibaiolojia tu katika lugha yao, jaribu kutafuta neno kwa ajili ya mwana ambalo halitamaanisha mtoto aliyezaliwa kibaiolojia. Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha unatumia maneno yale yale kwa ajili ya: wafuasi wa karibu, viongozi wa dini, Mkombozi Aliyeahidiwa, mahali pa kuabudia, mkutano wa dini, Kuhani mkuu, kusaliti, uovu, na Mwana wa Mungu yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Neno/ahadi za Mungu zilitimizwa; Yesu anasema Yeye ni Mwana wa Mungu.

57

Hukumu ya YesuLuka 23:1-5, 13-16, 21-24 Kigezo katika: NLT

Luka 23:1-5 Kisha wale walikuwepo kwenye mkutano wa dini walimchukua Yesu kwenda kwa Pilato, gavana. Walianza kueleza mashitaka yao. Mtu huyu amekuwa akiwapotosha watu wetu na kuwazuia watu kulipa kodi zao Serikalini kwa kudai kuwa ni Mkombozi Aliyeahiwa, mfalme. Kwa hiyo Pilato akamuuliza, Je wewe ni mfalme wa watu hawa? Yesu akajibu, Wewe wasema. Pilato akawageukia viongozi wa dini na makutano na kusema, Sioni kosa lo lote kwa mtu huyu! Kisha wakaweka msisitizo. Lakini anasababisha machafuko kwa mafundisho yake kila anakokwenda! Luka 23:13-16 Kisha Pilato akawakutanisha pamoja viongozi wa dini, pamoja na watu na akatangaza hukumu yake. Ninyi mmleta mtu huyu kwangu, mkimshitaki kwa mba anapotosha watu. Mimi nimemchunguza kwa makini mbele yenu na kumkuta hana hatia. Hakuna neno lolote alilolitenda mtu huyu limpasalo adhabu ya kifo. Atachapwa mijeledi, na kisha nitamfungua. Luka 23:21, 22 Bali waliendelea kupiga kelele, Auawe! Auawe!. Kwa mara ya tatu akawauliza, Kwanini? Huyu ametenda uovu gani? Luka 23:23, 24 Lakini sauti za watu zikawa na nguvu zaidi, wakimtaka kwamba Yesu auawe, na sauti zao zikashinda. Pilato akamhukumu Yesu kuawa kama walivyotaka.

58

Falsafa za Maisha Katika baadhi tamaduni, swali la kiongozi wa wakuu dini juu ya Yesu kuwa Mwana wa Mungu na majibu yake ya nguvu ya uthibitisho wa Yesu kwamba Alikuwa ni Masihi, Mwana wa Mungu ni sahihi kabisa. Jina hili linaweza kutoeleweka kumaanisha uzao wa kibaiolojia wa Mungu. Simulizi hii haijitoshelezi kujenga hoja ya Yesu kama Mwana wa Mungu. Itakuwa vema kutumia maelezo ya Luka ya hukumu ambapo kiongozi wa wakuu wa dini ambaye aliuliza tu ikiwa Yesu ni Masihi (Mkombozi Aliyeahidiwa) (Luka 22:67). Viongozi wa dini hawakuwa na mamlaka ya kutoa adhabu ya hukumu ya kifo, kwa hiyo walitakiwa kumshawishi gavana wa Kirumi kufanya hivyo. Kama inachanganya kwa hadhira kwa nini walikwenda kwa gavana, fanya hili kuwa uwazi katika simulizi. Mwambatano wa ndani wa simulizi Hakikisha kutumia maneno yale yale kwa ajili: viongozi wa dini na Mkombozi Aliyeahidiwa, yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahili wa Simulizi Yesu kuchapwa mijeledi, na kupewa hukumu isiyo ya haki yote ni kutimizwa kwa unabii kutoka Isaya 53. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Neno la Mungu/Kutimizwa kwa ahadi; Yesu hana dhambi; Yesu hakufanya kosa lo lote; Yesu kwa hiyari yake alijitoa kukidhi matakwa ya watu. Kushirikishana Injili Yesu hakuhukumiwa kifo kwa ajili ya dhambi zake, bali dhambi zetu.

59

Yesu aliubeba Msalaba Wake na AlisulubiwaLuka 23:26-28, 31-35, 39-46, 50-56 Kigezo kwenye NLT Luka 23:26-27 Na walipokuwa wakimtoa Yesu, mtu aitwaye Simon, aliyekuwa anatokea mji mwingine, ilitokea alikuwa akiingia kutokea mashambani. Askari walimchukua na kuweka msalaba juu yake na wakamtaka auchukue nyuma ya Yesu. Kundi kubwa la watu lilitembea nyuma, ikiwa ni pamoja na wanawake waliokuwa wameshikwa na majonzi. Luka 23:28, 31 Yesu akawaambia wanawake, Enyi wanawake, msinililie mimi, bali lieni kwa ajili yenu na watoto wenu. Ikiwa Mungu amenitoa mimi katika mateso haya kwa sababu nimejitoa kuwa kafara/sadaka kwa ajili ya dhambi, je atafanya nini kwa watenda dhambi wenyewe? Luka 23: 32-35 Wahalifu wawili walitolewa ili wauawe pamoja na Yesu. Wakachukuliwa kwenda mahali palipoitwa Fuvu la Kichwa. Huko walimpiga misumari kwenye viganja na miguu yake na wakampigilia misumari juu ya mbao za mti. Akainuliwa juu mhalifu mmoja mkono wake wa kuume, mwingine mkono wa kushoto kwake. Yesu alisema, Baba Mungu, uwasamehe hao wanaoniua mimi, kwa kuwa hawajui walitendalo. Askari walipiga kura kuona ni nani atakayepata mavazi yake. Makutano waliangalia na viongozi walifanya dhihaka. Aliokoa wengine, walisema, na ajiokoe mwenyewe ikiwa ndiye Mkombozi Aliyeahidiwa na Mungu. Luka 23:39-43 Mmoja wa wale wahalifu aliyekuwa akininginia alimdhihaki, kwa hiyo wewe ndiye Mkombozi Aliyeahidiwa, Ni wewe? Dhihirisha hili kwa kujiokoa mwenyewe na sisi pia wakati huu! Lakini mhalifu mwingine alipinga, Humwogopi Mungu hata wakati huu ambao umehukumiwa kufa? Tunastahili kufa kwa ajili ya uhalifu wetu, lakini mtu huyu hakufanya lo lote baya. Kisha akasema, Yesu, nikumbuke mimi utakaporudi tena kwa nguvu kutawala. Yesu akajibu, Ninakuhakikishia, siku ya leo ikiisha, utakuwa nami mbinguni. Luka 23:44-46 Muda wa saa sita mchana, na giza likatanda katika nchi yote hadi saa tisa . Kisha Yesu akapaza sauti, Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu! Kwa maneno hayo akafa.

60

Luka 23:50-53 Kulikuwa na kiongozi wa dini mzuri ambaye hakukubaliana na yale ambayo wengine waliyafanya. Alikwenda kwa gavana na akauomb mwili wa Yesu. Aliuchukua mwili kutoka kwenye mbao za mti, akaufunga katika sanda na akaulaza kwenye kaburi ambalo lilikuwa limechongwa mwambani. Jiwe kubwa likawekwa mbele ya mlango wa kaburi. Kisha wakaenda nyumbani na kuandaa manukato ya kuweka kwenye mwili wake kwa ajili ya maziko. Siku yao ya dini ya kupumzika ilikuwa imeanza, kwa hiyo walitakiwa na sheria zao za dini kusubiri hadi ipite ndipo wangeweza kwenda tena kwenye kaburi.

61

Maneno/Vifungu vya Maneno ya Kujadili Angalia Faharasi kwa ajili ya: Roho Kaburi Falsafa za Maisha Ikiwa hadhira hailielewi msalaba, uelezee kama ni kitu fulani kama mbao za mti au msalaba ulitengenezwa kwa mbao mbili za mti Baadhi ya tamaduni hawaamini mwanamke anaweza kuona maiti. Wanaweza kuhisi matendo ya wanawake hapa kuwa si sahihi au ya kigeni. Kwa hiyo, chagua kusema baadhi ya wafuasi wa Yesu Mwambatano wa ndani wa Simulizi Hakikisha kutumia maneno yale yale kwa ajili ya: Baba, kafara/sadaka, dhambi, kusamehe, kuokoa, wafuasi, viongozi wa dini, Mkombozi Aliyeahidiwa, mbinguni, na kuuawa yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahili wa Simulizi Simulizi hii inaonyesha mwitikio wa mhalifu kwa Yesu alipomkubali Yesu kama Mkombozi Aliyeahidiwa na Mungu/Masihi. utakaporudi na nguvu kutawala Hii ni kukubalika kunakotafsiriwa kuwa kuja kwa ufalme wako Maelezo ya Luka juu ya Yesu Kubeba Msalaba Wake na simulizi ya kusulubiwa imetumika kwa sababu inaonyesha kutimizwa kwa unabii katika mpangilio wa simulizi hii. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Mungu ni Baba Hakika ya Wokovu Yesu alisema, Ninakuhakikishia kuwa, utakuwa naimi. Maombi Yesu aliongea na Baba wakati wa adhabu yake.

62

Kufufuka kwa YesuLuka 24:1-7; Yohana 20:11-18 Kigezo katika: NLT Luka 24:1-4 Mapema sana asubuhi baada ya kifo cha Yesu wanawake walikwenda kaburini kuuandaa mwili wa Yesu sawa sawa na mila zao. Walikuta kwamba jiwe limeondolewa kutoka mlangoni. Waliingia ndani, lakini hawakuuona mwili Wake. Wanaume wawili waliovaa mavazi ya kumeta meta waliwatokea. Luka 24:5-7 Wanawake waliogopa na kuinama kifudifudi hata nchi. Wanaume wakauliza, Kwa nini mnaangalia ndani ya kaburi kwa ajili ya mtu ambaye yuko hai? Hayupo hapa! Amefufuka kutoka kwa wafu! Kumbukeni alipowaambia kwamba, ni lazima asalitiwe na kuhukumiwa, na kwamba atafufuka tena siku ya tatu. Luka 24:8-12 Kisha walikumbuka kwamba Yesu alisema hayo. Walikimbia kutoka kaburini kwenda kuwaambia wafuasi wake wa karibu na kila mtu kile kilichootokea. Alikuwa ni Mariamu Magdalena na wanawake wengine wengi waliowaambia wafuasi wake wa karibu nini kilichotokea lakini hawakuwaamini. Moja wao alikimbia kwenda kaburini kuangalia. Alitazama na kuona vile vitambaa vya sanda tu. Kisha alirudi nyumbani tena, wakistaajabu nini kilikuwa kimetokea. Yohana 20:11-18 Mariamu alikuwa akisimama nje ya kaburi akilia, na alipokuwa akilia, alitulia na kutazama ndani ya kaburi. Aliwaona malaika wawili wenye mavazi meupe. Ee mwanamke, kwa nini unalia? Malaika walimuuliza. Kwa sababu wamemchukua Bwana wangu, alijibu, na sijui wamemweka wapi? Mwanamke aligeuka na alipokuwa akiondoaka alimwona mtu amesimama pale. Alikuwa Yesu, lakini hakuweza kumtambua. Ee mwanamke, kwa nini unalia? Yesu alimuuliza mwanamke. ni nani unamtafuta? Mwanamke alifikiri kuwa alikuwa ni mtunza bustani na kusema, Bwana, ikiwa umemuondoa, niambie wapi umemweka, na nitakwenda na kumchukua. Mariamu! Yesu akasema. Alimgeukia na kulia kwa sauti, Mwalimu! Usiniguse, Yesu alisema, Kwa kuwa bado sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini nenda watafute ndugu zangu na uwaambie kwamba huko ndiko ninakokwenda. Mariamu Magdalena aliwakuta wafuasi wake wa karibu na kuwaambia kwamba, Nimemwona Bwana Kisha akawapa ujumbe Wake.

63

Falsafa za Maisha kwa kadri ya desturi/mila zao Kifungu hiki cha maneno kimejumuishwa katika maelezo ya wanawake kwenda kaburini kwa sababu tamaduni nyingi haziandai maiti kwa maziko. Mwambatano ndani ya Simulizi Hakikisha kutumia maneno yale yale kwa ajili ya: kaburi, Bwana, wafuasi wa karibu, kuamini, malaika, na Baba yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahili wa Simulizi Hakikisha kwamba hadhira inaelewa kwamba Yesu alikuwa amekufa lakini yu hai sasa. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Kila kitu ambacho Yesu aliwaambia wafuasi wake wa Karibu kimetimia; Yesu alikuwa mwema/upendo katika utendaji wake kwa wanawake; Yesu anawaagiza wafuasi wake kuwaambia wengine ujumbe Wake; Yesu hayuko tenda kifoni bali yu hai.

64

Baada ya KufufukaMathayo 28:18-20; Matendo 1:3-5, 8-14 Kigezo katika: NLT Mpito: Baada ya Yesu kufufuka kutoka kwa wafu, Aliwatokea wafuasi wake mara kadhaa. Aliwapa maagizo muhimu kuhusu nini cha kufanya. Mathayo 28:18-20 Yesu alikuja kwa wanafunzi wake na kusema, Mamlaka yote mbinguni na duniani nimepewa. Nendeni mkawafanye kuwa wafuasi wote mtakaokutana nao, mkiwabatiza na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi. Kumbukeni, niko pamoja nanyi siku zote. Matendo 1:3-5 Kipindi cha siku arobaini baada ya kuuawa na kufufuka kwake, Yesu alijitokeza kwa wafuasi wake wa karibu na kuwathibitishia kwa namna mbalimbali kwamba kwa hakika alikuwa hai. Wakati fulani alipokuwa akila nao chakula, Aliwaambia, Msitoke katika mji mnaoabudia mpaka Baba (Mungu) anapowapa ninyi kile alichoahidi. Katika siku chache tu mtapokea Roho wa Mungu. Matendo 1:8 Roho wa Mungu atakapowajilia, mtapokea nguvu na mtawaambia watu habari zangukila mahali - hapa, maeneo yote yanayozunguka vijiji, katika miji iliyo karibu na hata mwisho wa nch. Matendo 1:9-11 Haikuchukua muda mrefu tangu Yesu aliposema haya Alichukuliwa juu kwenda mbinguni. Wafuasi wake walipokuwa wakimtazama, alipotelea katika mawingu. Walipokuwa wakikaza macho kumtazama, wanaume wawili waliovalia kanzu nyeupe ghafla walisimama karibu nao. Wakasema, Kwa nini mmesimama hapa mkiangalia mbinguni? Yesu amekwisha twaliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni. Siku moja, kama mlivyomwona akienda, Atarudi tena! Matendo 1:12-14 Wafuasi wa Yesu walitembea kurudi mjini mahali walipoabudu na kwenda kwenye nyumba ambayo walikuwa wakikaa. Hapo, walikutanika kwa pamoja wakiendelea na maombi, pamoja na mama yake Yesu, wanawake wengine wengi na ndugu zake Yesu.

65

Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha kutumia maneno yale yale kwa ajili ya: wafuasi wa karibu, Baba, Roho wa Mungu, mbinguni, batiza, utii, wafuasi, mji ambao wanaabudu, na kuabudu yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Mungu alikuwa mwaminifu kwenye Neno Lake na alimpeleka Roho Mtakatifu kwao; Nguvu huja kutoka kwa Mungu; Yesu aliishinda nguvu ya uvutano. Kushirikisha Injili Chukua ujumbe huu kwa watu wote; pata nguvu kutoka kwa Mungu.

66

Roho wa MunguMdo 1:15, 16, 18, 20-26; 2:1-12 Kigezo katika: NLT Mpito: Wafuasi wa Yesu walikaa mjini wakisubiri Roho wa Mungu kama walivyoagizwa. Mdo 1:15, 16 Walipokuwa wakisubiri, siku ambayo karibu wafuasi mia na ishirini walikuwepo, Petro alisimama na kusema, Ndugu zangu, ilikuwa lazima kwamba Neno la Mungu limtizwe katika habari ya Yuda aliyewaongoza viongozi wa dini waliomkata Yesu. Hili lilitabiriwa zamani za kale na Roho wa Mungu. Mdo 1:18 Tunajua kwamba alikufa mara tu baada kumsaliti Yesu Mdo 1:20-22 Petro aliendelea, Imeandikwa katika ujumbe wa Mungu kwamba mtu mwingine atachukua nafasi yake ya uongozi. Sasa ni lazima tuchague mtu mwingine. Ni lazima awe mtu ambaye amekuwa pamoja nasi wakati wote tulipokuwa pamoja na Yesu kutoka wakati alipobatizwa, mpaka siku aliyochukuliwa kutoka kwetu kwenda kuwa na Mungu. Mdo 1:23-26 Kisha wote wakaomba kwa ajili ya kumchagua mtu sahihi. Mathiya alichaguliwa na akawa mmoja wa wale kumi na wawili, kundi la wafuasi wa karibu wa Yesu ambao walikuwa sasa viongozi wa wale waliomfuata Yesu. Mdo 2:1 Baadaye, katika siku ya sikukuu muhimu ya kidini, baada ya Yesu kufufuka kutoka kwa wafu, wafuasi wake walikuwa wakikutana mahali pamoja. Mdo 2:2-4 Ghafla, kulikuwa na sauti kama ya upepo mkuu uvumao., na ukaijaza nyumba mahali walipokuwa wakikutana. Kisha kile kilichoonekana kama ndimi za moto zilitokea na kuwakalia juu yao kila mmoja aliyekuwepo alijazwa kwa Roho wa Mungu na wakaanza kunena kwa lugha nyingine kadri Roho wa Mungu alivyowapa uwezo huo. Mdo 2:5-12 Wazao wa Ibrahimu kutoka pande zote za dunia walikuwa mjini ajili ya sikukuu. Walikuja na wakawasikia wafuasi wa karibu wa Yesu wakinena. Walisema, Watu hawa ni wenyeji wa mahali hapa, na bado tunawasikia wakiongea lugha za nchi tulikozaliwa juu ya mambo makuu

67

aliyoyafanya Mungu! Walisimama pale wakishangaa na kuchanganyikiwa. Maana yake nini mambo haya? Waliulizana wao kwa wao.

Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha unatumia maneno yale yale kwa ajili ya: wafuasi, Roho/Roho wa Mungu, wafuasi wa karibu, viongozi wa dini na wazao wa Ibrahimu yaliyotumika katika simulizi zilizotangulia. Kanuni Tabia na asili ya Mungu Mungu ni Roho; Mungu anao mpango; Mungu anamwadhimisha Yesu ambaye ni Bwana na Mkombozi Aliyeahidiwa Kanisa Waamini wanakusanyika pamoja katika eneo moja; wamejazwa Roho. Maisha ya uchaji Kujazwa Roho.

68

MwafrikaMdo 8:26 32, 34-39 Kigezo katika: NLT Mpito: Wafuasi wa Yesu walikwenda kila mahali wakiwaambia watu habari za ajabu juu ya Yesu. Roho wa Mungu aliwapa baadhi yao maelekezo juu ya wapi pa kwenda. Mmoja wa wafuasi hawa aliitwa Filipo. Mdo 8:26, 27 Malaika kutoka kwa Mungu alimwambia Filipo, Nenda pande za chini kusini kwenye barabara ya jangwa inayoetelemkia Yerusalemu. Mdo 8:27, 28 Kwa hiyo akaenda, na akakutana na mtunza hazina wa taifa la Afrika ambaye sasa alikuwa akirudi nyumbani kwao baada ya kuabudu huko Yerusalemu. Akiwa ameketi katika gari lake, alikuwa akisoma kwa sauti kutoka kitabu cha Nabii Isaya. Mdo 8:29-32 Roho wa Mungu akamwambia Filipo, Nenda karibu, na ukatembee kando ya gari. Filipo akaenda mbio na akamsikia yule mtu akisoma, kwa hiyo akamuuliza, Je, umeyaelewa hayo unayoyasoma? Yule mtu akajibu, Nitawezaje kuyaelewa, wakati hakuna mtu wa kunielekeza? Na akamsihi Filipo apande garini na kukaa naye. Haya ndiyo aliyokuwa akiyasoma: Aliongozwa kama kondoo aendaye machinjoni. Na kama vile mwana kondoo alivyo kimya mbele ya amkataye manyoya, hakufumbua kinywa chake. Mdo 8:34, 35 Mwafrika alimuuliza Filipo, Je msemaji alikuwa akiongea habari zake mwenyewe au mtu mwingine? Filipo alianza na ujumbe huo huo wa msemaji wa Mungu na akamweleza kitu gani Mungu alikuwa akisema juu ya Yesu. Mdo 8:36-39 Walipokuwa wakiendela pamoja, wakafika mahali penye maji na yule mtu wa Afrika akasema, Tazama, maji haya! Kwa nini nisibatizwe? Unaweza, Filipo akajibu, kama kweli unaamini. Na yule Mwafrika akajibu, Ninamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu. Yule Mwafrika akamuru gari lisimame, wakatelemka chini majini na Filipo akambatiza. Kisha yule Mwafrika akaenda njiani akifurahi.

69

Maneno/Vifungu vya maneno ya kujali Garini Garini linaweza kumaanisha pia mkokoteni au gari fulani linalovutwa na farasi au ngombe. Mwambatano ndani ya simulizi Hakikisha kutumia maneno yaleyele kwa ajili ya: wafuasi, Yerusalemu, kuabudu, malaika, msemaji, Roho wa Mungu, kubatiza na Mwana wa Mungu kama yalivyotumika katika simulizi zilizotangulia. Umahili wa Simulizi Simulizi hii ilichaguliwa kwa sababu ya uwiano wake na simulizi ya Isaya 53 na inaweka mfano wa mwitikio wa Yesu unaofuatiwa na utii wa kubatizwa mara moja. Kanuni Kanisa Ubatizo, kazi ya maandiko Kushirikisha Injili Wale walioamini walikwenda kila mahali wakishikisha ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho.

70

Paulo Akutana na YesuMdo 8: 1, 3, 9:1-13, 15, 17-21 Kigezo katika: NLT Mpito: Wafuasi wa Yesu walikuwa wakienda kila mahali wakizungumza juu yake. Paulo, kiongozi wa dini, alikuwa pia akisafiri kila mahali akijaribu kuliharibu kanisa. Mdo 8:1, 3; 9:1-2 Paulo alikuwa akitamka vitisho na alidhamiria kuwaharibu waamini. Alielekea kwenye mji mwingine ili kuwakamata waamini na kuwaleta Yerusalemu katika vifungo. Mdo 9:3-6 Alipokuwa akiukaribia mji, mwanga mkali kutoka mbinguni ukamwangazia juu yake. Akaanguka chini hata nchi na akasikia sauti ikimwambia, Paulo, Paulo! Kwa nini unaniudhi? Ni nani wewe Bwana? Paulo akauliza. Sauti ikajibu, Yesu, unayeniudhi! Sasa inuka na uingie mjini na utaambiwa yakupasayo kufanya. Mdo 9:7-12 Watu waliokuwa na Paulo walisimama kimya wakiwa na mshangao, kwa kuwa waliisikia sauti ya mtu lakini hawakuona mtu! Paulo alipoinuka katika nchi alijikuta amekuwa kipofu. Watu aliokuwa nao walimwongoza kwa kumshika mkono kwenda mjini. Alibakia pale akiwa kipofu kwa siku tatu. Basi palikuwa na mwamini aliyeitwa Anania katika mji. Yesu alisema naye katika maono, akamwita! Ndiyo Bwana! alijibu. Yesu akasema, Nenda kwenye nyumba moja. Utakapofika umuulizie Paulo. Anaomba kwangu saa hii. Nimemwonyesha kuwa utakuja na kuweka mikono juu yake ili kwamba aweze kuona tena. Mdo 9:13, 15 Lakini Bwana, akajibu Anania. Nimesikia juu ya mambo ya kutisha mtu huyu aliyoyafanya kwa waamini katika Yerusalemu! Lakini Yesu akasema, Nenda na ufanye kile ninachosema. Nimemchagua Paulo kuuchukua ujumbe wangu kwa mataifa, wafalme na kwa wazao wa Ibrahimu pia. Mdo 9:17, 18 Kama Mungu alivyomwambia, Anania alikwenda na kumkuta Paulo. Aliweka mikono yake juu yake na kusema, Paulo, Yesu aliyekutokea Yerusalemu amenituma mimi ili kwamba uweze kuona tena na ujazwe kwa Roho wa Mungu. Ghafla vitu kama magamba vilianguka machoni kwa Paulo, na akapata kuona tena. Kisha akainuka na akabatizwa.

71

Mdo 9:19-21 Paulo alikaa na waamini katika mji ule kwa siku kadhaa, mara akaanza kusema juu ya Yesu akisema, Yeye ni Mwana wa Mungu hakika! Wote waliomsikia walikuwa wakishangaa. Je huyu si mtu yule yule ambaye aliwatesa wafuasi wa Yesu katika Yerusalemu? Maneno/Vifungu vya Maneno ya Kujadili kanisa Ikiwa neno kanisa linatoa kitu fulani kutoka kwenye tafsiri ya Agano Jipya, jaribu kulielezea neno katika kifungu cha maneno badala ya kutumia neno kanisa. Katika Agano Jipya, neno kamwe halikumaanisha jengo, ba