Upload
phungnga
View
446
Download
15
Embed Size (px)
Citation preview
1
[SURA ya 1 T.L. 2002] Sheria ya Utafsiri wa Sheria
___
SURA YA KWANZA
_______
SHERIA YA UTAFSIRI WA SHERIA
[SHERIA KUU]
MPANGILIO WA VIFUNGU
Kifungu Jina
SEHEMU YA KWANZA
MASHARTI YA UTANGULIZI
1. Jina la sheria na tarehe ya kuanza kutumika kwa Sheria
2. Matumizi
3. Jamhuri kufungwa na Sheria
SEHEMU YA PILI
MASHARTI YA JUMLA YA TAFSIRI
4. Ufafanuzi utumikao katika sheria.
5. Matumizi.
6. Sheria hunena daima
7. Sehemu ya matamshi na miundo ya fasihi.
8. Jinsia na tarakimu.
9. Rejeo ya neno Waziri katika sheria.
10. Marejeo kwa tarakimu, kujumuishwa.
11. Tafsiri ya rejeo ndani ya kifungu, n.k.
12. Rejeo kwenye sheria kama ilivyorekebishwa.
13. Tafsiri ya neno “au”.
SEHEMU YA TATU
KUANZA KUTUMIKA NA KUTAJWA KWA SHERIA
14. Tarehe ya kuanza kutumika kwa sheria.
15. Muda wa kuanza kutumika kwa sheria.
16. Kuanza kutumika kwa sheria palipo na kifungu cha masharti ya kutolewa
kwa taarifa ya kuanza kutumika.
17. Tafsiri ya uwezo wa kupanga tarehe ya kuanza kutumika kwa sheria.
18. Ushahidi wa tarehe ya kusainiwa.
19. Utekelezaji wa uwezo kabla ya kuanza kutumika.
20. Kutajwa kwa sheria.
21. Marejeo ya sheria kwa siku ya kuanza kutumika.
2
SEHEMU YA NNE
MASHARTI YA UTUNGAJI NA UTUMIKAJI WA SHERIA.
22. Sheria kuwa sheria za umma.
23. Vifungu kujitosheleza kama sheria kamili.
24. Sheria yaweza kurekebishwa au kufutwa katika kikao hicho hicho.
25. Utangulizi na Majedwali.
26. Vichwa, maelezo ya pembeni, rejeo chini ya ukurasa na marekebisho ya
makosa.
SEHEMU YA TANO
MAREKEBISHO NA KUFUTWA KWA SHERIA
27. Fasiri ya sheria inayorekebisha sheria nyingine pamoja na marekebisho
yake.
28. Kufutwa kwa sheria kama ilivyorekebishwa.
29. Kufuta kwa kufuta.
30. Kufuta na kubadilisha.
31. Athari ya masharti mbadala.
32. Vifungu vya jumla vinavyobakizwa baada ya kufutwa.
33. Athari ya kufutwa kwa sheria kwenye sheria ndogo.
34. Athari ya kumalizika kwa muda wa kutumika kwa sheria.
SEHEMU YA SITA
MASHARTI YANAYOHUSU SHERIA NDOGO
35. Rais anaweza kutunga sheria ndogo.
36. Masharti ya jumla kuhusu uwezo wa kutunga sheria ndogo.
37. Utangazaji na kuanza kutumika kwa sheria ndogo.
38. Kuwasilisha wa Kanuni Bungeni na kukataliwa.
39. Tafsiri ya sheria ndogo.
40. Kutajwa kwa sheria ndogo.
41. Marejeo ya sheria kujumuisha sheria ndogo.
42. Matendo chini ya sheria ndogo kuchukuliwa kama yamefanyika chini ya
sheria.
43. Ada na tozo.
SEHEMU YA SABA
UWEZO NA WAJIBU WA KISHERIA
44. Muda wa utekelezaji wa uwezo au wajibu kwa mujibu wa sheria.
45. Rejeo kwa mshika ofisi itajumuisha warithi.
46. Tafsiri ya maneno ya kuwezesha.
47. Uwezo wa kutoa leseni, n.k.., ni wa hiari.
48. Uwezo wa kuteua unajumuisha uwezo wa kusimamisha au kufukuza n.k.
49. Uteuzi kwa jina au ofisi n.k., na uteuzi wa Mwenyekiti, n.k. Bodi, n.k...,.
3
50. Uwezo wa walio wengi, akidi, n.k.
51. Utekelezaji wa uwezo unaweza kusahihishwa.
52. Athari ya uteuzi wakati afisa anayestaafu akiwa likizo.
53. “Inaweza/Anaweza”, itakuwa na maana ya hiari, “ata/ita”, itakuwa na
maana ya lazima.
54. Uwezo wa Bodi, n.k. hautaathirika kwa nafasi iliyowazi au mapungufu
mengine.
55. Utekelezaji wa mamlaka fulani kwa anayekaimu.
56. Rejeo kwa eneo kwa kutumia mipaka.
57. Tafsiri ya uwezo wa kukasimu.
58. Ni nani ataweka lakiri ya kampuni.
59. Haki za Serikali.
SEHEMU YA NANE
MASHARTI KUHUSU MUDA NA UMBALI
60. Kukokotoa muda..
61. Kuhesabu miezi.
62. Masharti pale muda haujapangwa.
63. Tafsiri ya uwezo wa kuongeza muda.
64. Kwenda kinyume na fomu.
65. Vipimo vya umbali.
SEHEMU YA TISA
TARATIBU NA ADHABU
66. Mashauri ya wadhifa wa kiofisi hayakomi baada ya kifo.
67. Kanuni za Mahakama.
68. Kutolewa kwa adhabu, si kizuizi cha kesi ya madai.
69. Upatikanaji wa faini na adhabu.
70. Kutia hatiani maradufu.
71. Matumizi ya sheria za adhabu kwa makampuni.
72. Masharti ya makosa chini ya sheria mbili au zaidi.
73. Marekebisho ya adhabu.
74. Maagizo ya adhabu ya juu, ya chini, ya siku, na za pamoja.
75. Vifungu vinavyohusu kujaribu.
76. Utoaji wa mali au vitu vilivyotwaliwa.
77. Uwajibikaji wa mwajiri au mkuu.
78. Ushahidi wa agizo, kibali au ridhaa ya mtumishi wa umma.
79. Utekelezaji wa mamlaka ya Mkurugenzi wa Mashtaka wakati hayupo.
80. Tamko la adhabu mwishoni mwa kifungu.
81. Makosa yanayoendelea.
4
SEHEMU YA KUMI
MASHARTI MBALIMBALI
82. Uwasilishaji wa nyaraka kwa njia ya posta.
83. Uwasilishaji wa nyaraka kwa ujumla.
84. Lugha ya sheria za Tanzania.
85. [Kufutwa kwa Sheria Na. 30 ya mwaka 1972.]
JEDWALI
(Kifungu cha 4 )
5
[SURA ya 1 T.L. 2002] Sheria ya Utafsiri wa Sheria
______________________________________________________________________
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SURA YA KWANZA
______
SHERIA YA UTAFSIRI WA SHERIA
Sheria ya majumuisho ya kanuni za msingi zinazohusu maana,ufafanuzi na
matumizi ya sheria zilizotungwa, na mambo mengine yanayohusiana na hayo.
[............................]
Sheria Na.
4 ya1996 na
17 ya 1996
SEHEMU YA KWANZA
MASHARTI YA UTANGULIZI
Jina la sheria na
tarehe ya kuanza
kutumika kwa
sheria
1.-(1) sheria hii inaitwa Sheria ya Utafsiri wa Sheria.
(2) Sheria hii itaanza kutumika tarehe ambapo Toleo la 2002 la
Sheria zilizofanyiwa marekebisho zitakapoanza kutumika. (3) Katika kifungu hiki “Toleo la 2002 la Sheria zilizofanyiwa
marekebisho” ina maana ya Sheria za Tanzania zilizofanyiwa
marekebisho na kuchapishwa. Matumizi 2.-(1) Sheria hii itatumika Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar,
kwa minajili ya sheria zitumikazo sehemu zote za Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania. (2) Vifungu vya Sheria hii vitatumika katika, na kuhusiana na
Sheria yoyote iliyotungwa, nyaraka za umma, hata kama sheria na
nyaraka hizo zimetungwa, kupitishwa au kutolewa kabla au baada ya
kuanza kutumika kwa Sheria hii, isipokuwa kama Sheria na nyaraka
hizo:– (a) Zitakuwa na vifungu vinavyoelekeza vinginevyo, na
kuhusiana na sheria, dhamira na malengo yake au maudhui,
muktadha au mazingira ya sheria hiyo hayaruhusu, au sheria
yenyewe imetoa ufafanuzi; (b) zinahusu sheria ndogo, kama madhumuni na malengo ya
sheria kuu ambayo chini yake sheria ndogo zimetungwa,
haziruhusu matumizi ya ufafanuzi huo; au
6
(c) Zinahusu sheria ndogo, kama madhumuni na malengo ya
sheria kuu ambayo sheria ndogo zimetungwa, hayapatani na
matumizi ya ufafanuzi huo. (3) Vifungu vya Sheria hii vitatumika katika Sheria hii kama
vitumikavyo katika sheria iliyotungwa baada ya kuanza kutumika kwa
Sheria hii. (4) Katika vifungu 13, 15, 19, 20, 22, 23, 24, 33, 36(6), 43, 46, au
62 marejeo katika sheria yoyote au sheria ndogo iliyopitishwa au
kutungwa baada ya kuanza kutumika kwa Sheria hii yatatafsiriwa ili
yasiwe na maana ya kugusa sheria yoyote ambayo inaendelea kutumika
au ambayo inarekebisha moja kwa moja sheria nyingine, lakini
haibatilishi au kufuta sheria iliyopo. Jamhuri
kufungwa na
sheria
3. Jamhuri kufungwa na sheria.
SEHEMU YA PILI
MASHARTI YA JUMLA YA TAFSIRI Ufafanuzi
utumikao katika
sheria,
Sura ya 16.
4. Katika Sheria hii na katika sheria zingine:–
"shiriki kutenda jinai" kwa maana ya maneno yenye asili hii au misemo
inayoshabihiana itakuwa na maana kama ilivyoainishwa katika
sheria ya Kanuni za Adhabu; "tendo" ikitumiwa kuainisha kosa la jinai au kosa la madai itajumuisha
kushindwa kutenda wajibu na itahusu msururu wa vitendo vya
kushindwa kutekeleza wajibu; "Sheria" itumikapo kuhusiana na sheria yoyote, itakuwa na maana ya
sheria za zamani, amri au sheria zilizotungwa na Bunge la
Jamhuri au Baraza la Wakilishi la Zanzibar au Baraza lolote lenye
mamlaka ya kutunga sheria Tanzania au kuhusiana na Zanzibar,
sheria, amri au sheria za zamani zilizoridhiwa na au kwa niaba ya
Rais au mamlaka yoyote ya kutunga sheria, lakini haitahusu sheria
ya Jumuiya; "afisa tawala" maana yake ni afisa tawala wa ngazi yoyote; "wakili" maana yake ni mtu yeyote anayeruhusiwa kuendesha shughuli
za uwakili katika Mahakama Kuu au Mahakama za chini yake,
kwa mujibu wa sheria inayohusu uratibu wa shughuli za
mawakili; "hati ya kiapo" kuhusiana na watu wanaoruhusiwa kushuhudia viapo au
kupokea ushuhuda badala ya kiapo, itahusu vile vile tamko la
dhati, uthibitisho au azimio; "rekebisha au batilisha" maana yake ni kubadilisha, kufuta au kurekebisha
sehemu yote au sehemu tu, au kuongeza au kupunguza au kufanya
aina yoyote ya marekebisho kwenye sheria au sehemu yake; "sheria ya mapokeo" maana yake ni Sheria yoyote ya India au Sheria ya
7
Uingereza, ikijumuisha Amri za Baraza la Kifalme ambayo katika
wakati huu inatumika Tanzania; "sheria ndogo" maana yake ni sheria ndogo iliyotungwa kwa mujibu wa
sheria kuu; "mwezi" maana yake ni kipindi kuanzia siku ya kwanza ya mwezi hadi
siku ya mwisho ya mwezi husika; "mwaka" maana yake ni kipindi kuanzia siku ya kwanza ya mwezi wa
Januari hadi siku ya thelathini na moja ya mwezi wa Desemba ya
mwaka husika; "sura", "sehemu", "kifungu" na "Nyongeza" maana yake ni sura, sehemu,
kifungu na Nyongeza ya sheria husika na “kifungu kidogo” maana
yake ni kifungu kidogo cha kifungu ambamo neno hilo
limetumika; "Katibu Mkuu Kiongozi" maana yake ni mtu aliyeteuliwa kuwa Katibu
Mkuu kwenye Ofisi ya Rais; "hakimu" maana yake ni hakimu mkazi, hakimu wa wilaya, hakimu wa
mahakama ya mwanzo na maelezo mengine yoyote kuhusu
hakimu yaliyotolewa chini ya Sheria ya Mahakama za Mahakimu; "sarafu" maana yake ni kipande cha chuma cha aina yoyote, kiwe chuma
cha thamani au kisicho cha thamani na ambacho kwa wakati
husika, kinatumika kama fedha halali ya Jamhuri ya Muungano; "mwanzo wa kutumika" itumikapo kuhusiana na sheria maana yake ni
wakati ambapo sheria husika itaanza kutumika; "sheria zisizoandikwa" maana yake ni sheria zisizoandikwa za Uingereza; "Jumuiya ya Madola" maana yake ni mfungamano wa nchi za Madola na
nchi tegemezi ndani ya Jumuiya; na “mwanachama wa Jumuiya”
au “nchi ya Jumuiya in maana ya Jamhuri ya Muungano na nchi
zilizoorodheshwa katika Nyongeza ya Sheria hii; "Jumuiya" maana yake ni Jumiya ya Afrika ya Mashariki iliyoundwa
chini ya Mkataba wa Jumuiya;
Sura ya 2
"Mfuko Mkuu wa Hazina" maana yake ni Mfuko Mkuu wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
"Katiba" maana yake ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya
Mwaka 1977 iliyotungwa na Bunge Maalumu la Jamhuri ya
Muungano; "vunja" itumikapo kuhusiana na matakwa au wajibu kisheria au ruhusa
au idhini, hakimiliki, leseni au mamlaka kwa mujibu wa sheria
itajumuisha vile vile kushindwa kutii masharti au maelekezo ya
sheria; "mahakama" maana yake ni mahakama yoyote yenye mamlaka katika
Jamhuri ya Muungano;
Sura ya 141 "Mhakama ya Rufaa" maana yake ni mahakama inyosikiliza rufaa zote
zikatwazo kwa mujibu wa Sehemu ya Pili ya Sheria ya Mamlaka
ya Mahakama ya Rufaa; "Wakala wa Mfalme" maana yake ni watu kwa wakati huu wanafanya
kazi kama Wakala wa Mfalme kwa Serikali na Utawala wa kigeni
8
au yeyote wa namna hiyo;
Sura ya 358
"Sheria ya Kimila" maana yake ni kanuni au mfungamano wa kanuni
ambazo zinaainisha haki na wajibu, na ambazo zinatokana na
mazoea, kurithiwa au kutungwa, na zinakubaliwa na Jamii ya
Kiafrika nchini Tanzania na zenye nguvu ya kisheria, ikijumuisha
matangazo ya kanuni mpya au marekebisho yake yanayotungwa
chini ya kifungu cha 12 cha sheria ya Usimamiaji wa Haki na
Matumizi ya Sheria, na marejeo kwa, “Sheria za Jadi” au Sheria
za Jadi na Mila zitakuwa na tafsiri sawa; "ufafanuzi" maana yake ni ufafanuzi uliotolewa kwa mujibu wa sheria
ukitoa maana kwa neno au msemo; "Naibu Waziri" maana yake ni Naibu wa Waziri aliyeteuliwa kwa mujibu
wa Ibara ya 55 ya Katiba; "Wilaya" maana yake ni sehemu yoyote ya Jamhuri iliyotangazwa au
kubainishwa hivyo kwa mujibu wa Ibara ya 2 (2) ya Katiba; "hakimu wa wilaya" inajumuisha hakimu mkazi; "Hati" inajumuisha chapisho la aina yoyote, waraka wa maandishi ya aina
yoyote, yaliyoandikwa au kuelezwa kwenye kitu chochote kwa
herufi, tarakimu alama kwa namna moja zaidi ya hizo zilizotajwa,
kwa madhumuni ya kutumiwa kwa lengo la kuweka kumbukumbu
ndani au juu yake; "Mamlaka ya Afrika ya Mashariki" maana yake ni Mamlaka ya Afrika ya
Mashariki iliyoundwa chini ya Mkataba husika; "sheria iliyotungwa" maana yake ni sheria iliyotungwa au sehemu ya
sheria husika; "shamba", ikitumika kuhusiana na ardhi, itajumuisha vile vile haki ya
kisheria au maslahi, maslahi ya haki, haki ya njia katika ardhi,
hakimiliki, dai, dai la kumiliki hadi deni lilipwe, au zuio juu ya
miliki ya ardhi; "mwaka wa fedha" maana yake ni kipindi cha miezi 12 kinachoishia
tarehe 30 Juni; "Afisa Mambo ya Nje" maana yake ni afisa aliyeteuliwa au anayekaimu
nafasi ya Afisa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Muungano; "shughuli/kazi" itajumuisha mamlaka, kazi, wajibu, uwezo wa kisheria
na mamlaka ya kisheria; "Gazeti" au "Gazeti la Serikali" maana yake ni Gazeti linalopigwa chapa
na kutangazwa na Mpiga Chapa wa Serikali ya Jamhuri kwa amri
ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na inajumuisha nyongeza
zake na toleo Maalum la Gazeti hilo; "Taarifa ya Kawaida" maana yake ni tangazo lisilohusiana na utungwaji
wa sheria lililochapishwa katika Gazeti au kwa idhini ya Rais au
Waziri; "Serikali" maana yake ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano; "Mkemia Mkuu wa Serikali" inajumuisha msaidizi wake au mkemia
yeyote aliyeajiriwa na Serikali; "Tangazo la Serikali" maana yake ni sheria ndogo iliyotungwa na Rais,
9
Waziri au afisa wa serikali au mamlaka yoyote yenye uwezo
kutunga sheria ndogo kwa mujibu wa sheria husika; "Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali" maana yake ni Mpiga Chapa wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano na mpiga chapa yeyote
aliyeidhinishwa kuchapa sheria na nyaraka zingine za Serikali; "Kamisheni" maana yake ni Kamisheni ya Afrika ya Mashariki
iliyoundwa kwa Maagizo ya Mfalme ya Kuanzishwa kwa
Kamisheni ya Afrika ya Mashariki, kati ya miaka ya 1947 na 1961
na rejeo katika sheria yoyote kuhusu Kamisheni yatafafanuliwa
kama ifuatavyo:– (a) kwa kipindi ambacho Sheria ya Mkataba wa Uendelezaji wa
Huduma za Pamoja katika Afrika ya Mashariki ilikuwa
ikitumika, kipindi hicho kitafafanuliwa kama Mfumo wa
Huduma za Pamoja; (b) kwa kipindi baada ya kufutwa kwa Sheria iliyounda
Kamisheni, kitafafanuliwa kama kipindi cha Jumuiya; "Mahakama Kuu" maana yake ni Mahakama Kuu ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania au Mahakama Kuu ya Zanzibar; "Sheria za Kifalme" maana yake ni Sheria zilizotungwa na Bunge la
Ufalme wa Uingereza;
"mtu binafsi" maana yake ni mtu mmoja;
"Jaji" maana yake ni Jaji wa Mahakama Kuu na inajumuisha vile vile
Naibu Jaji;
"mlinzi wa amani" maana yake ni mtu mwenye mamlaka ya kutunza
amani;
"ardhi" inajumuisha majengo na aina nyingine ya majengo, na
iliyofunikwa na maji, milki yoyote, maslahi, haki ya kutumia njia
na haki ya vilivyomo juu au chini ya ardhi husika; "Afisa Sheria" maana yake ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na afisa
mwingine mzoefu kwenye taaluma ya sheria katika Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuanzia ngazi ya Wakili wa
Serikali Mkuu Mwandamizi au Mwandishi wa Sheria Mkuu
Mwandamizi; "mamlaka ya serikali za mtaa" maana yake ni–
Sura ya 287
(a) baraza la kijiji, kitongoji, mji, wilaya au mamlaka yoyote ya
serikali ya mtaa iliyoundwa chini ya sheria ya Serikali za
Mtaa na Mamlaka ya Wilaya; au
Suraya .288
(b) katika sehemu za mji, ni baraza la mtaa, mji, manispaa au
baraza la Jiji liloundwa chini ya Sheria ya Serikali za Mtaa
(Mjini);
Sura ya 11
"hakimu" maana yake ni hakimu mkazi, hakimu wa wilaya hakimu wa
mahakama ya mwanzo na mwingine yeyote aliyeteuliwa kama
hakimu kwa mujibu wa Sheria ya Mahakimu;
Sura ya 29
"ndoa" maana yake ni ndoa iliyofungwa na inayotambuliwa kwa mujibu
wa Sheria ya Ndoa, na neno “mume”, “mke” au “mwanandoa”
litafafanuliwa kutokana na neno la msingi la aliyeoa au kuolewa;
10
"Waziri" ina maana kama ilivyofafanuliwa katika kifungu cha 9 cha
sheria hii na vile vile itajumuisha Makamu wa Rais, Waziri Mkuu;
na Waziri maana yake ni waziri mwenye dhamana ya kusimamia
shughuli husika na itajumuisha Naibu Waziri kwa wakati huu
anayetekeleza kazi za Waziri au kama hakuna waziri wa
kusimamia jambo husika, maana yake ni Rais; "mtoto" maana yake ni mtu ambaye hajafikia umri wa miaka kumi na
minane, na neno “mtoto” na mtoto mchanga” yatafafanuliwa kwa
maana hiyo; "mwezi" maana yake ni mwezi katika mwaka, isipokuwa kama neno la
sayari limeongezwa ikimaanisha mwezi wa sayari; hivyo, mwezi
ukitajwa kuanza au kuhesabiwa katika tarehe isiyokuwa ya
kwanza ya mwezi husika, basi mwezi utatimia katika siku ya pili
ya tarehe ya mwezi unaofuata, hata kama kipindi husika
kinajumuisha siku nyingi au pungufu ya siku thelathini; "mwenyeji " maana yake ni mtu yeyote mwenye asili ya Kiafrika; "kiapo" na "hati ya kiapo", anayetakiwa au anayeruhusiwa kuthibitisha
bila ya kula kiapo, inajumuisha tamko la dhati na azimio, na
“kuapa”, itajumuisha “tamka kwa dhati” na “azimia”; "Sheria ya zamani" inajumuisha sheria ya ina yoyote, tangazo la kisheria
au sheria iliyotungwa au kutolewa kabla ya Amri ya Kifalme
kuhusu Tanganyika ya mwaka 1920, na iliyoidhinishwa na Amri
hiyo ya Baraza la Kifalme, na sheria ndogo zilizotungwa na
kuidhinishwa kutumika chini ya Amri hiyo ya Kifalme, na
(isipokuwa ufafanuzi wa neno “Sheria” na “Bunge” katika
kifungu hiki) itajumuisha Sheria ya Bunge na sheria ndogo
zilizotungwa chini ya sheria husika; "Bunge":- (a) katika Sheria za zamani, au katika nyaraka za serikali
zilizotolewa au kutangazwa kabla ya tarehe tisa, Desemba,
1961, ina maana ya Bunge la Uingereza na “Bunge la
Mfalme” ina maana kama hiyo; (b) katika sheria za Bunge la Tanganyika au za Bunge la
Jamhuri ya Muungano, au nyaraka za Serikali iliyotungwa
au kutolewa baada ya siku ya nane, ya Desemba, 1961, au
sheria ya Bunge Maalum la Tanganyika itakuwa na maana
ya Bunge le Jamhuri ya Muungano (na matumizi ya neno
“Sheria ya Bunge” yatajumuisha sheria iliyotungwa na
Bunge Maalum la Tanganyika); "tekeleza" itumikapo kuhusiana na kazi au shughuli, itajumuisha vile vile
kutumia uwezo uliotolewa kisheria, kutekeleza wajibu au
mamlaka ya kisheria; "Katibu Mkuu" maana yake ni mtu aliyeteuliwa na Rais kushika wadhifa
wa Katibu Mkuu; “mtu" maana yake ni neno au msemo utumikao kuelezea mtu binafsi au
kampuni, shirika au mamlaka iliyoundwa kisheria, au isiyopewa
11
hadhi ya nafsi;
Sura ya 322
"afisa polisi" maana yake ni askari yeyote wa Jeshi la Polisi mwenye cheo
cha konstebo au zaidi kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Jeshi
la Polisi na Majeshi ya Nyongeza; "uwezo" inajumuisha hadhi, mamlaka au hiari ya kuamua; "iliyoagizwa au ainishwa" ina maana ya– (a) iliyoainishwa na au chini ya sharia husika ambapo neno hilo
limetumika; (b) kwa pale litumikapo kurejelea kwenye kitu chochote
kilichoainishwa kwenye sheria nyingine ukiacha sheria
ambamo neno hilo limetumika, itajumuisha kitu chochote
kilichoainishwa ndani ya sheria ndogo iliyotungwa kwa
mujibu wa sheria husika; "Rais" maana yake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, na inajumuisha mtu
yeyote mwenye mamlaka ya kutekeleza majukumu ya Rais kwa
mujibu wa kifungu cha 137 cha Katiba; "Tangazo" maana yake ni tangazo la Rais lililochapishwa katika Gazeti la
Serikali; "Chapisho" maana yake ni:- (a) maandiko au machapisho ya aina zote; (b) kumbukumbu ya aina yoyote, kinasa sauti, waya, maandishi
ya matundu, filamu ya senema, au vivuli, kumbukumbu
zitokanazo na uvumbuzi wowote, zitokanazo kwa njia ya
elektronik au umeme, zilizorudufuliwa au kuainishwa na
kupelekwa kwa njia hizo; (c) kitu cha aina yoyote kinachofanana na vile vilivyoelezwa
katika kifungu kidogo cha (b) cha ufafanuzi huu au hata
kama haviwiani, vikiwa katika hali ya kuweza kuonekana
aidha kwa jinsi vilivyo, maumbile yake au kwa namna
yoyote vinaweza kutoa au kurudufu au kunakilisha au
kuwasilisha maneno au mawazo; na (d) kila nakala na rudufisho la chapisho lolote lililoainishwa
katika vifungu vidogo vya (a), (b) au (c);
Sura ya 212
"shirika la umma" maana yake ni kampuni iliyoundwa kwa sheria ya
kipekee na si chini ya Sheria ya Makampuni, na inajumuisha
shirika dogo la kipekee lililoundwa kwa utaratibu usio chini ya
Sheria ya Makampuni;
Sura ya 35
"siku ya mapumziko" maana yake ni siku ambayo imetangazwa kuwa
siku ya mapumziko chini ya Sheria ya Siku za Mapumziko;
"mtumishi wa umma" au "idara ya umma" inajumuisha kila afisa au idara
iliyopewa mamlaka ya kushughulikia mambo ya umma, aidha
chini ya maelekezo ya moja kwa moja kutoka kwa Rais au
vinginevyo, na inajumuisha afisa au idara chini ya Mamlaka ya
Serikali ya Mtaa, Jumuiya au Shirika la Umma; "sehemu ya wazi au umma" inajumuisha:- (a) mtaa, barabara, gati au bustani ya umma;
12
(b) jengo, mahala au chombo kitumikacho kwa usafiri wa umma
au ambacho kila mtu anayo haki au anaruhusiwa kukitumia
au kuwemo aidha bila ya masharti au kwa masharti au kwa
kulipa ada au kiingilio; (c) jengo au mahala au chombo kitumikacho kwa umma kwa
ajili ya shughuli za mikutano ya kidini au mkusanyiko wa
watu au kama mahakama; "mhuri wa umma" maana yake ni mhuri wa Jamhuri ya Muungano; "Mkoa" maana yake ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano iliyotangazwa
au inayofahamika kutolewa Tamko na Rais chini ya Ibara ndogo
(2) ya Ibara ya 2 ya Katiba kuwa ni mkoa; "Mkuu wa Mkoa " maana yake ni mtu aliyeteuliwa na Rais kuwa mkuu
wa mkoa, na “Mkuu wa Mkoa” ni mkuu wa mkoa husika; "kanuni" maana yake ni kanuni zilizotungwa chini ya sheria ambamo
neno hilo limetumika; "futa au batilisha" inajumuisha kutengua, kubadili, kusawazisha au
kufuta; "Jamhuri" maana yake ni Jamhuri ya Tanganyika na inajumuisha Jamhuri
ya Muungano;
Sura ya 11 "hakimu mkazi" maana yake ni hakimu mkazi wa daraja lolote
aliyeteuliwa hivyo chini ya Sheria ya Mahakama ya Mahakimu; "afisa mapato" maana yake ni afisa aliyeteuliwa na Katibu Mkuu wa
Hazina kufanya shughuli za kukusanya mapato ya Jamhuri ya
Muungano; "taratibu" maana yake ni, taratibu zilizotungwa chini ya sheria husika
ambamo neno hilo limetumika; "taratibu za mahakama" itumikapo kuhusiana na mahakama, maana yake
ni taratibu zilizotungwa na mamlaka yenye uwezo wa kutunga
kanuni, kutoa maagizo ya kuratibu utendaji na taratibu za
uendeshaji wa shughuli za mahakama; "uza au kuuza" inajumuisha kubadilishana bidhaa, kutoa kwa ajili ya
kuuza na kutandaza bidhaa hadharani kwa ajili ya kuuza; "wasilisha " pale sheria inaporuhusu au kuhitaji hati yoyote kuwasilishwa
kwa mtu yeyote, ikiwa msemo wa “kuwasilisha”, au msemo wa
“toa” au “peleka” au msemo mwingine wowote ukitumika basi
isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo, kuwasilisha
kutakamilika kwa kuandika anuani sahihi na kuituma kwa posta,
baada ya kulipa tozo husika, barua yenye hati na isipokuwa kama
kinyume chake kimedhibitishwa, uwasilishaji utachukuliwa kama
umeshawasilishwa katika muda wa kawaida wa huduma za posta; "saini" ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya kisarufi chake na asili ya
msemo wa neno hili, itajumuisha jina au alama, kwa mtu
asiyeweza kuandika; "siku za vikao" likitumika kuhusiana na Bunge, maana yake ni siku
ambapo Bunge limekaa; "tamko la kisheria", kama likitolewa:-
13
Sura ya 34
(a) nchini Tanzania, maana yake ni tamko lililofanywa chini ya
Sheria ya Viapo na Matamko ya Kisheria;
(b) katika nchi nyingine ya Jumuiya ya Madola, maana yake ni
tamko chini ya kiapo kilichotolewa mbele ya mlinzi wa
amani, mthibitishaji rasmi au mtu mwingine yeyote
mwenye mamlaka ya kutoa au tamko kupokea viapo kwa
mujibu wa sheria yoyote inayotumika katika nchi hiyo; (c) katika nchi nyingine yoyote, maana yake tamko chini ya
kiapo kilichotolewa mbele ya Afisa wa Mambo ya Nchi za
Nje mwenye mamlaka ya chini ya sheria yoyote kuhusu
kupokea viapo au mtu mwingine yeyote aliyeteuliwa na
kukasimiwa madaraka hayo na Waziri wa Mambo ya nje
kwa mujibu wa Tangazo lililochapishwa katika Gazeti la
Serikali; "sheria ndogo" maana yake ni amri, tamko la kisheria, kanuni, kanuni za
mahakama, tangazo, sheria ndogo za miji, kijiji au chama au hati
ya kisheria iliyotolewa na mamlaka yoyote kwa mujibu wa Sheria
husika; "tia hatiani/papohapo" maana yake ni kutolewa kwa hukumu na
mahakama yenye mamlaka ya kutoa hukumu papo hapo; "apa/apisha" kwa mtu anayeruhusiwa kwa mujibu wa sheria kutoa tamko
la dhati au uthibitisho badala ya kiapo, itajumuisha kutoa tamko la
dhati kutoa uthibitisho wa dhati; "maji ya taifa" maana yake ni maji ya bahari, mto au ziwa yaliyopo ndani
ya mipaka ya Jamhuri ya Muungano; "himaya" maana yake ni Tanganyika;
Sura ya 323
"Mkataba" maana yake ni Mkataba wa Ushirikiano wa Afrika ya
Mashariki ulioainishwa katika Nyongeza ya Sheria ya
(Kutekeleza) Mkataba wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki ya
mwaka 1967 ambayo ilifutwa chini ya Sheria ya Mkataba wa
Usuluhishi wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki; "chini" itumikapo kuhusiana na sheria au kifungu chochote cha sheria,
itajumuisha “ya”, “kwa mujibu wa” “kufuatana na” na “kutokana
na”; "Siku ya Muungano" maana yake ni tarehe 26 Aprili, 1964;
"Falme Zilizoungana" maana yake ni Uingereza na Ireland ya Kaskazini;
"Jamhuri ya Muungano" maana yake– (a) kwa kipindi baada ya terehe 11 Desemba, 1964 ni Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania; (b) kwa kipindi kilichoanzia Siku ya Muungano na kuishia
tarehe 11 Desemba, 1964 ni Jamhuri ya Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar;
"Makamu wa Rais" maana yake ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano;
"wosia" inajumuisha sehemu ya wosia, kiambatanisho cha wosia au
14
kiambatanisho cha wosia kinachotangua sehemu ya wosia;
"maneno" yanajumuisha tarakimu na alama; "maandiko/maandishi", na maelezo yanayotaja maandiko au maandishi
yatajuisha vilevile picha, lithographia, kuandika au kuchora na
jiwe na aina zozote za kuonyesha maandiko au kurudufu maneno
kwa namna ya kuonekana; "sheria za Bunge" maana yake ni Sheria zote zilizotungwa na Bunge
ambazo kwa wakati husika zinatumika pamoja na sheria ndogo
zote zinazotumika zikiwepo na Sheria za Jumuiya pamoja na
sheria zote zilizoazimwa; "mwaka" maana yake ni kipindi cha miezi kumi na miwili.
Matumizi 5. Fasili au kanuni za ufafanuzi zilizomo katika sheria yoyote
zitatumika kufafanua vipengele vya sheria ambamo vipo au kanuni za
ufafanuzi zilizopo katika sheria hiyo, pamoja na vipengele vingine vya
sheria hiyo. Sheria hunena
daima 6. Sheria ya Bunge itachukuliwa kama inanena wakati wote na
litokeapo jambo au kitu kimeelezwa katika wakati wa sasa, ifahamike
kuwa inajumuisha nyakati zote, ili kila sehemu yoyote ya sheria husika
ipewe maana yake halisi kulingana na maudhui na malengo ya sheria
husika. Sehemu ya
matamshi na
miundo ya fasihi
7. Mahali ambapo neno au fungu la maneno vimefafanuliwa
katika sheria, sehemu zingine za msemo au vifungu vya maneno vitakuwa
na maana sawia. Jinsia na
tarakimu 8. Katika sheria yoyote:-
(a) maneno yanayoonyesha jinsia ya kiume yatajumuisha
vilevile jinsia ya kike;
(b) maneno yanayoonyesha jinsia ya kike yatajumuisha vilevile
jinsia ya kiume;
(c) maneno ya umoja yatajumuisha vilevile uwingi na maneno
ya uwingi yatajumuisha umoja; Rejeo ya neno
Waziri katika
sheria
9. Anapotajwa Waziri katika sheria tafsiri yake itakuwa ni moja
ya zifuatazo–
(a) anapotajwa Waziri ndani ya sheria, ifafanuliwe kuwa ndiye
waziri mwenye dhamana ya kusimamia utekelezaji wa sheria
hiyo, au kama ni katika vifungu vya sheria ambamo au kwa
mujibu wa vifungu hivyo neno hilo limetumika, itakuwa na
maana kwamba mwenye dhamana wakati huo ni Rais; (b) iwapo ni kwenye sheria ndogo, neno waziri mwenye
dhamana ya kusimamia utekelezaji wa Sheria au vifungu vya
sheria, itakuwa na maana mwenye dhamana wakati huo ni
Rais; na
15
(c) itajumuisha Kaimu Waziri badala ya Waziri husika kama
ilivyoelekezwa katika kifungu (a) au (b). Marejeo kwa
tarakimu
kujumuishwa
10. Rejeo kwenye sheria kwa kutumia namba au herufi au kwa
namba na herufi kwa pamoja, au kwa sehemu mbili au zaidi ya sheria
husika, itatafsiriwa kama inajumuisha sehemu iliyoelezwa kwa kutumia
rejeo iliyofafanuliwa awali na ile iliyorejewa mwishoni.
Tafsiri ya rejeo
ndani ya kifungu,
n.k.
11.-(1) Endapo katika sheria, rejeo imefanywa kwenye sura,
sehemu, nyongeza, kiambatanisho au fomu bila ya maelezo mengine ya
kuonyesha rejeo imefanywa kwenye sura, sehemu, kifungu nyongeza,
kiambatanisho au fomu ya au kwa mujibu wa sheria nyingine, basi rejeo
hiyo itatafsiriwa kana kwamba inahusiana na sheria husika ambamo rejeo
limefanywa. (2) Endapo katika kifungu cha sheria, rejeolimefanywa kwenye
kifungu kidogo, aya, aya ndogo, au kipengele chini ya hivyo, na bila ya
maelezo mengine ya kuonyesha kama rejeo la kifungu kidogo, aya, aya
ndogo au kipengele kidogo chini ya hivyo imefanywa kwa mujibu wa
sehemu nyingine au kifungu kingine, basi rejeo hilo litakuwa kwa mujibu
wa na itatafsiriwa kana kwamba ni rejeo kwa kifungu kidogo, aya, aya
ndogo au sehemu ya kifungu ambamo rejeo hilo limefanyika. (3) Endapo katika nyongeza ya sheria, rejeo imefanywa kwenye
kipengele, aya, au sehemu nyingine bila ya maelezo ya kuonyesha kwa
mahsusi, kipengele, kipengele kidogo, aya au sehemu nyingine mahsusi,
basi rejeo hilo litakuwa kwa mujibu wa na litatafsiriwa kana kwamba ni
rejeo kwenye kipengele, kipengele kidogo, aya, au sehemu nyingine ya
nyongeza ambayo rejeo hilo limefanyika. (4) Masharti ya vifungu (1), (2), na (3) yatatumika baada ya
kuzingatia mabadiliko ya lazima kuhusiana na ufafanuzi wa maudhui ya
sheria ndogo husika. Rejeo kwenye
sheria kama
ilivyorekebishwa
12.-(1) Rejeo katika sheria kwenye sheria nyingine, litachukuliwa
kujumuisha rejeo kwenye sharia hiyo kama ilivyorekebishwa.
(2) Rejeo katika sheria kwenye kifungu cha sheria, litatafsiriwa kama
rejeo kwenye kifungu husika kama kitakavyorekebishwa. (3) Rejeo katika sheria kwenye Sheria ya Kifalme, au kwenye kifungu
cha Sheria ya Kifalme, litatafsiriwa kujumuisha rejeo kwenye sheria hiyo
ya Kifalme au kifungu kama kitakavyorekebishwa. Tafsiri ya neno
"au" kitofauti 13. Kuhusiana na sheria iliyotungwa au kupitishwa baada ya
kuanza kutumika kwa Sheria hii, lakini kwa kuzingatia kifungu cha 2 (4),
"au", "ingine" na "vinginevyo" yatatafsiriwa kuelezea tofauti na sio
lazima kuonyesha usawa au uwiano, isipokuwa kama neno "a kufanana"
au maneno mengine yenye maana hiyo yameongezwa.
16
SEHEMU YA TATU
KUANZA KUTUMIKA NA KUTAJWA KWA SHERIA Tarehe ya kuanza
kutumika kwa
sheria
14. Kila sheria itaanza kutumika katika tarehe ya kuchapishwa
kwake katika Gazeti la Serikali, isipokuwa kama imeelekezwa
vinginevyo au kama imeelekezwa katika sheria husika au katika sheria
nyingine kwamba sheria hiyo itaanza kutumika katika tarehe nyingine. Muda wa kuanza
kutumika kwa
sheria
15. Ikielekezwa kwamba sheria itaanza kutumika siku Fulani, basi
sheria hiyo itaanza kutumika kuanzia alfajiri ya siku hiyo.
Kuanza kutumika
kwa sheria palipo
na kifungu cha
masharti ya
kutolewa taarifa
ya kuanza
kutumika
16. Bila ya kuathiri masharti ya kifungu cha 14, kwa pale ambapo
sheria imeelekeza au kifungu cha sheria hiyo kimeelekeza kuwa sheria
itaanza kutumika katika tarehe itakayoteuliwa kwenye tangazo, kifungu
hicho na kile kinachotoa jina la sheria, vitaanza kutumika tarehe Sheria
inaposainiwa na Rais, isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo.
Tafsiri ya uwezo
wa kupanga siku
ya kuanza
kutumika kwa
sheria
17. Uwezo wa kutangaza siku ya kuanza kutumika kwa sheria
haujumuishi uwezo wa kuainisha au kutangaza-
(a) siku ya nyuma kabla ya tarehe ambapo tangazo hilo
linachapishwa katika Gazeti la Serikali; au (b) siku tofauti kwa vifungu tofauti vya sheria hiyo, isipokuwa
kama kuna vifungu dhahiri vinavyoruhusu kufanya hivyo. Ushahidi wa
tarehe ya
kusainiwa
18. Pale ambapo inaonekana tarehe katika nakala ya Sheria
iliyochapishwa, au inayodaiwa kuchapishwa na Mchapa Mkuu wa
Serikali, ikionyeesha kuwa ndiyo tarehe ambapo Rais aliridhia na kusaini
Sheria hiyo au sehemu yake, tarehe hiyo inayoonekana ndiyo
itakayochukuliwa kama ushahidi kuwa siku hiyo ndiyo ambamo Rais
aliweka saini yake katika Sheria hiyo, na mahakama zitaridhia hivyo. Utekelezaji wa
uwezo kabla ya
kuanza kutumika
19.-(1) Endapo kifungu cha sheria hakianzi kutumika baada ya
kutungwa kwa sheria husika na kifungu hicho kama kingeanza kutumika
kingeweza kutoa mamlaka ya– (a) kutolewa hati/agizo la kisheria au kiutawala;
(b) kutoa notisi au hati ya aina nyingine;
(c) kuteua mtu kushika madaraka fulani;
(d) kuanzisha mamlaka inayoundwa na watu fulani, mamlaka
ambayo ni ya kisheria au siyo ya kisheria, au
(e) kufanya jambo lolote kwa mujibu wa sheria hiyo; Basi, uwezo huo wa kisheria, bila ya kujali kwamba kifungu hicho
hakijaanza kutumika, lakini kwa kuzingatia masharti ya vifungu vya (3)
na (4), uwezo huo waweza kutumika wakati wowote baada ya kutungwa
kwa sheria hiyo kwa jinsi ikatavyoonekana ni lazima au ni muhimu kwa
lengo la kuwezesha sheria hiyo au vifungu vyake kuanza kutumika, au
17
vifungu vyake kutumika mara baada vifungu hivyo kuanza kutumika. -(2) Kwa pale ambapo– (a) kifungu cha sheria hakianzi kutumika baada ya kutungwa
kwa sheria na kifungu hicho kingerekebisha Sheria kama
kingeanza kutumika; (b) kifungu cha ile sheria nyingine kingeweza, kama kifungu
kilichotajwa awali kingeanza kutumika kutoa uwezo wa– (i) kutoa amri au hati yenye nguvu kisheria au
kiutawala;
(ii) kutoa notisi au hati ya aina nyingine;
(iii) kuteua mtu kushika wadhfa au madaraka ya ofisi
fulani;
(iv) kuunda chombo maalumu chenye au kisichokuwa
na taaswira ya kampuni; au
(v) kufanya jambo lolote kwa madhumuni ya ile sheria
nyingine, basi, uwezo huo, bila ya kujali kuwa kifungu kilichotajwa awali
hakijaanza kutumika, lakini kwa kuzingatia matakwa ya vifungu vya (3)
na (4) vyaweza kutumika wakati wowote baada ya kupitishwa kwa sheria
ambamo kifungu kilichotajwa awali kimo, na kwa jinsi ilivyo lazima au
muhimu kwa lengo la kuwezesha ile sheria nyingine iweze kutumika au
vipengele vya sheria ile, mnamo au baada ya kifungu kilichotajwa awali
kuanza kutumika. -(3) Kwa pale ambapo uwezo wa kutoa hati au amri zenye nguvu
kisheria au kiutawala upo, au uwezo wa kutoa notisi au hati nyingine,
uwezo huo waweza kutumiwa kama ilivyoelekezwa katika kifungu
kidogo cha (1) au cha (2), na hati hiyo, au notisi yaweza kuwa na
nguvu/kuanza kutumika:- (a) katika siku ambayo sharti lililorejewa katika kifungu kidogo
cha (1) au, kama itakavyokuwa, sharti lililotajwa mwanzo
katika kifungu kidogo cha (2) kinaanza kutumika; au (b) katika siku ambayo kingeanza kutumika, iwapo muda ule
ambapo hati ilipotolewa, au notisi au waraka , kifungu
kilichotajwa au kilichotajwa awali kitakuwa kimeanza
kutumika, kutegemea na kitakachotokea mwishoni. -(4) Pale uwezo wa kuteua mtu katika ofisi fulani, au kuunda
taasisi unatekelezwa kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1) au cha (2),
mtu aliyeteuliwa kushika wadhifa huo anaweza kutekeleza majukumu ya
ofisi hiyo, au vyovyote itakavyokuwa, taasisi iliyoundwa inaweza
kukutana na kutekeleza kazi, wajibu na uwezo, lakini tu kwa kuzingatia
madhumuni yaliyorejewa katika kifungu kidogo cha (1) au cha (2)
kutegemeana na kifungu kidogo kitakachotumika; na kwa madhumuni ya
kifungu chochote kinachohusu muda, kitachukuliwa kutokuanza mpaka
kifungu husika kilichorejewa katika kifungu cha (1) au cha (2) kwa
vyovyote itakavyokuwa, kuanza kutumika. (5) Kwa kuzingatia masharti ya kifungu kidogo cha (4) cha
18
kifungu cha (2), kifungu hiki kitatumika katika sheria zilizopitishwa
baada ya kuanza kutumika kwa Sheria hii. Kutajwa kwa
Sheria 20.-(1) Pale sheria imerejewa, itakuwa inatosheleza kwa
madhumuni yote kutaja au kurejea sheria hiyo kwa:- (a) jina fupi au mtajo (kama upo) kwa jinsi ambavyo sheria hiyo
imetajwa; (b) kama ni sheria, mwaka ilipopitishwa na namba yake kati ya
sheria nyingine za mwaka huo; (c) kama ni sheria, namba ya Sura ya sheria hiyo katika Juzuu za
sheria zilizorekebishwa. (2) Kifungu cha sheria kinaweza kutajwa kwa rejeo la sehemu,
kifungu, kanuni, taratibu, ibara au mgawanyo wowote wa sheria ambapo
kifungu hicho kinapatikana. (3) Mtajo wa sheria yoyote utafanywa kutegemeana na nakala ya
chapisho la sheria, au chapisho linalodhaniwa kuwa limechapwa na
Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali. Marejeo ya sheria
kwa siku ya
kuanza kutumika
21. Rejeo la sheria kuhusu siku ya kuanza kutumika itakuwa,
pale, baadhi ya vifungu vinaanza kutumika katika tarehe tofauti, itakuwa
siku ile ambayo kifungu husika cha sheria hiyo kinaanza kutumika.
SEHEMU YA NNE
MASHARTI YA UTUNGWAJI WA SHERIA NA UTUMIKAJI WA SHERIA Sheria kuwa
sheria ya Umma 22. Kila sheria itahesabiwa kuwa iko wazi na inafahamika kwa
umma wote, isipokuwa kama kutakuwa na maelezo ya kuonyesha
vinginevyo, na mahakama zote zitatilia maanani kuwa sheria zote
zinafahamika kwa umma. Vifungu
kujitosheleza
kama sheria
kamili
23. Kila kifungu cha sheria kitakuwa na maana na uwezo timilifu
kama sheria bila ya kuwa na haja ya / ulazima wa maelezo ya utangulizi /
dibaji. Kifungu
kinaweza
kurukwa au
kufutwa katika
Kikao hicho
hicho
24. Sheria inaweza kurekebishwa au kufutwa katika kikao hicho
hicho cha Bunge kama kile kilichopitisha sheria hiyo.
Utangulizi na
Majedwali 25.-(1) Utangulizi katika sheria, ni sehemu ya sheria husika, na
unapaswa kutafasiriwa kama sheria yenyewe, kwa madhumuni ya
kusaidia kutoa ufafanuzi na madhumuni ya sheria hiyo. (2) Kiambatanisho au Jedwali au orodha katika sheria pamoja na
maelezo mafupi vitakuwa ni sehemu ya sheria hiyo. Vichwa, maelezo 26.-(1) Vichwa vya habari ya sehemu, mgawanyo na sehemu ya
19
ya pembeni, na
marejeo chini ya
ukurasa na
marekebisho
makosa ya Na 17
ya 1996 Jedwali.
mgawanyo vitahesabika kama sehemu ya sheria hiyo.
(2) Maelezo ya pembeni au rejeo za chini ya kurasa katika sheria,
na bila ya kuathiri kifungu cha (1), kichwa cha sehemu ya sheria, kanuni,
taratibu sheria-ndogo au ibara ya sheria havitahesabika, kama sehemu ya
sheria. (3) Ikiwa kutakuwa na kosa lolote la maandishi au uchapishaji wa
Muswada wa Sheria au Sheria yenyewe kwenye Gazeti la Serikali,
Mwandishi Mkuu wa Sheria au afisa yeyote wa Ofisi ya Mwanasheria
Mkuu wa Serikali aliyepewa madaraka kwa maandishi kwa niaba hiyo na
Mwandishi Mkuu wa Sheria anaweza kwa amri iliyochapishwa katika
gazeti la Serikali kutoa maelekezo ya kusahihisha makosa hayo na kila
agizo litasomeka pamoja na Muswada au Sheria inayohusiana nayo na
Mswada huo au Sheria, kuanzia tarehe ya kuchapishwa itaanza kutumika
kama ilivyosahihishwa.
SEHEMU YA TANO
MAREKEBISHO NA KUFUTWA KWA SHERIA Fasiri ya sheria
inayorekebisha
Sheria pamoja na
marekebisho
yake
27. Pale ambapo sheria inarekebisha sheria nyingine,
marekebisho ya Sheria hiyo, kama yatakuwa yamebeba maudhui ya
Sheria inayorekebishwa bila ya kuwa na madhumuni mengine,
itafafanuliwa na kufasiriwa kama sehemu ya Sheria iliyorekebishwa. Kufutwa kwa
Sheria kama
ilivyorekebishwa
28. Pale ambapo Sheria iliyorekebishwa kwa Sheria nyingine
imefutwa, kufutwa kwa Sheria hiyo kutahusu pia kufutwa kwa vipengele
vyote vya ile Sheria ya mwanzo ambayo ilirekebishwa. Kufuta kwa
kufuta 29. Pale ambapo Sheria inafuta Sheria inayorekebisha, kufuta
huko hakutahuisha sheria yoyote ambayo ilikuwa imefutwa, isipokuwa
kama yameongezwa maneno ya kuhuisha sheria hiyo. Kufuta na
Kubadilisha 30. Pale ambapo Sheria inarekebisha Sheria nyingine na kuweka
vifungu vingine mbadala, Sheria iliyorekebishwa itabakia hai na
itaendelea kutumika hadi hapo vifungu vilivyowekwa mbadala
vitakapoanza kutumika. Amri ya masharti
mbadala 31. Pale ambapo Sheria inarekebisha na inatunga sheria nyingine
pamoja na au bila ya mabadiliko, katika sheria yoyote iliyotungwa:- (a) wilaya zote au mgawanyo wa maeneo mengine;
(b) halmashauri zote, mashirika, bodi, mabaraza, kamisheni,
bodi za wadhamini au mamlaka zingine zilizoundwa na
chaguzi zote na uteuzi wowote uliofanywa; na
(c) ofisi zote zilizoanzishwa na uteuzi wowote wa maafisa
uliofanywa;
(d) sheria ndogo zote, hati, vyeti na nyaraka zilizotolewa; na
(e) matendo mengine yote, mambo na vitu,
20
ambavyo wakati sheria inayofuta inaanza kutumika yalikuwepo, au
yalikuwa na nguvu kisheria, kwa mujibu wa vifungu vya sheria hiyo,
yataendelea kuwa halali kama kwa mujibu wa vifungu hivyo
yanaruhusiwa kuendelea, au yamehuishwa, yamefanywa au kutendwa na
yamechimbuka au kuhalalishwa au kutendwa kwa mujibu wa sheria hiyo. Vifungu vya
jumla
vinavyobakizwa
baada ya kufutwa
32.-(1) Pale ambapo Sheria inafuta au kurekebisha Sheria
nyingine, sheria iliyofutwa, isipokuwa kama kuna madhumuni tofauti-
(a) haitahuisha jambo lolote ambalo halikutumika au
halikuwepo wakati ufutwaji unaanza kutumika; (b) hautaathiri matumizi yaliyopita ya sheria iliyofutwa au kitu
chochote kilichofanywa kwa usahihi kuhamishwa chini ya
sheria hiyo; (c) haitaathiri haki yoyote, maslahi, hatimiliki, uwezo,
upendeleo uliotolewa, uliopatikana, uliojitokeza,
ulioanzishwa au uliotekelezwa au hadhi yoyote au uwezo
kabla ya ufutwaji; (d) haitaathiri wajibu wowote, shuruti, kuwiwa au wajibu wa
kuthibitisha uliotwikwa, uliotolewa au ulioingiwa; (e) haitaathiri utwaaji adhabu au utwaaji ulioingiwa au wajibu
wa kuingiwa kutokana na kosa lililotendwa dhidi ya sheria
hiyo; (f) haitaathiri uchunguzi wowote, mwenendo wa kisheria au
nafuu kuhusiana na haki yoyote, maslahi, hakimiliki, uwezo,
hadhi, wajibu, shuruti au wajibu wa kuthibitisha, adhabu au
kutwaliwa kwa mali; na uchunguzi wowote, mwenendo wa kisheria au unafuu unaweza
kuanzishwa, kuendelezwa au kutekelezwa na adhabu yoyote hiyo au
utwaaji unaweza kutwikwa na kutekelezwa kama vile sheria inayofutwa
hayapitishwa au kutolewa. (2) Kuwepo kwa vifungu vinavyobakizwa dhahiri kuhusiana na
kufutwa kulikofanyika hakutachukuliwa kuathiri matumizi ya kifungu
hiki kuhusiana na athari ya kufutwa kulikofanyika. Athari ya
kufutwa kwa
sheria kwenye
sheria ndogo
33.-(1) Pale ambapo sheria:-
(a) inafuta au kurekebisha sheria nyingine na kuweka vifungu
mbadala au ;
(b) inafuta na kutunga sheria nyingine bila ya au pamoja na
marekebisho, Sheria ndogo zote zilizotungwa chini ya Sheria inayofutwa na ambazo
zilikuwa zinatumika kabla ya kuanza kutumika kwa sheria inayofuta
sheria nyingine, kama zinzenda sambamba na Sheria inayofuta Sheria
nyingine, zitaendelea kutumika na kuwa na nguvu kisheria kana kwamba
sheria ndogo hizo zimetungwa chini ya Sheria inayofuta sheria nyingine.. (2) Sheria ndogo inayoendelea kutumika chini ya kifungu kidogo
cha (1), inaweza kurekebishwa au kufutwa kama vile imetungwa chini ya
21
Sheria inayofuta sheria nyingine. Athari ya
kumalizika kwa
muda wa
kutumika kwa
sheria
34. Mara baada ya muda wa kutumika kwa Sheria utakapoisha, au
kutumika kwa Sheria kutakapofikia tamati, kifungu cha 33 kitatumika
kama vile Sheria iliyotungwa itakuwa imefutwa .
SEHEMU YA SITA
MASHARTI YANAYOHUSU SHERIA NDOGO Rais anaweza
kutunga Sheria
Ndogo
35. Iwapo sheria yoyote inaruhusu au imeweka masharti ya
kutungwa kwa sheria ndogo na haielekezi ni nani mwenye mamlaka ya
kutunga sheria ndogo hizo, basi ndogo hizo zinaweza kutungwa na Rais. Masharti ya
jumla kuhusu
uwezo wa
kutunga Sheria
Ndogo
36.-(1) Sheria ndogo haitakuwa kinyume na masharti ya Sheria
Kuu ambayo imetoa mamlaka ya kutungwa kwa, Sheria Ndogo hiyo, au
sheria nyingine, na Sheria Ndogo itakuwa batili kwa kiasi ilivyokuwa
kinyume na matakwa ya Sheria Kuu.
(2) Pale Sheria Ndogo inaelekea kutungwa kwa kutekeleza
mamlaka fulani au mamlaka nyingine, itachukuliwa kuwa imetungwa
kwa kutekeleza mamlaka zote ambazo zimepelekea kutungwa kwa Sheria
hiyo . (3) Itachukuliwa kwamba panapokuwa hakuna ushahidi
vinginevyo, masharti yote na hatua za mwanzo muhimu ya kutungwa kwa
Sheria Ndogo zitakuwa zimefuatwa na kufanywa. (4) Pale Sheria inatoa uwezo wa kutunga Sheria Ndogo,
itachukuliwa kwamba imejumuisha mamlaka ya kutekeleza kwa utaratibu
kwa namna hiyo na kwa mujibu wa masharti (kama yatakuwepo) ya
kurekebisha au kufuta Sheria Ndogo yoyote; na kama mtu aliyepewa
mamlaka hayo atakuwa amebadilishwa kabisa au kupewa mtu mwingine,
uwezo uliotolewa chini ya kifungu kidogo hiki, juu ya mtu wa mwanzo
unaweza ukafanywa na mtu aliyebadilishwa juu ya mambo yote au vitu
ambavyo viko chini ya mamlaka yake kama vile ni mtu wa mwanzo (5) Pale ambapo Sheria inampa uwezo mtu wa kutunga Sheria
Ndogo kwa madhumuni ya jumla na pia kwa madhumuni yoyote maalum
yanayohusiana na maudhui hayo, kutajwa kwa madhumuni maalum
hakutaathiri ujumla wa mamlaka au uwezo wa kutunga Sheria kwa
madhumuni ya jumla yaliyoainishwa. (6) Kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (4) cha Kifungu cha 2,
Sheria Ndogo inaweza kuweka masharti kwamba kukiukwa kwa sheria
ndogo ni kosa linaloweza kuadhibiwa kwa kutozwa faini kuhusiana na
kosa hilo kwa kiwango kisichozidi shilingi laki sita. (7) Uwezo wa kutunga Sheria Ndogo unaweza ukafanywa– (a) ama kuhusiana na jambo lolote ambalo uwezo huo
umetolewa, au kuhusiana na mambo yote ambayo
yametolewa maelezo maalum, au kuhusiana na jambo
maalum au mambo yaliyoainishwa; na
22
(b) kwa ajili ya kuweka, kwa ajili ya mambo ambayo
yanatekelezeka – (i) sharti sawa kwa mambo yote yanayohusu uwezo
unaotekelezwa au kifungu tofauti kwa mambo
tofauti au aina au mambo au masharti tofauti kwa
jambo linalofanana au aina mbalimbali ya mambo
kwa madhumuni tofauti ya sheria; au (ii) sharti jingine lolote ama bila masharti au kwa sharti
lolote maalum. (8) Sheria Ndogo inaweza kutungwa– (a) kwa ajili ya kutumika– (i) muda wote au muda maalum; (ii) wakati wote au katika sehemu maalumu ya; (b) kwa ajili ya kuhitaji jambo lolote litakalokuwa limeathiriwa
na sheria kuwa–
(i) kwa mujibu wa viwango maalum au matakwa
maalum; (ii) iliyoidhinishwa na au kwa kuridhika kwa mtu
maalum au chombo au aina ya watu maalum au
chombo; (c) kwa ajili ya kumpa mamlaka ya ridhaa kwa mtu maalum au
chombo au aina maalum ya watu au chombo; na (d) kwa ajili ya kutoa katika jambo maalum au aina ya mambo
kwa ajili ya kutoa watu au vitu au aina ya watu au vitu
kutoka kwenye masharti ya sheria ndogo ama kwa masharti
maalum ama vyote au kwa kiwango maalum kilichoelezwa. (9) Kwenye vifungu vidogo vya (7) na (8), neno “Maalum” maana
yake maalum kwenye Sheria Ndogo. Utangazaji na
kuanza kutumika
kwa Sheria
Ndogo
37.-(1) Pale Sheria inapotoa mamlaka ya kutunga Sheria Ndogo,
Sheria Ndogo zote zilizotungwa chini ya mamlaka hiyo isipokuwa kama
nia iliyokinyume inajitokeza – (a) inatangazwa kwenye Gazeti la Serikali; (b) Kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (2) na kifungu cha 39,,
itaanza kutumika siku ya kutangazwa, au pale siku nyingine
maalum itakapotamkwa au kutolewa katika Sheria Ndogo
kwenye siku hiyo. (2) Sheria Ndogo haitatamka kuanza kutumika katika siku kabla
ya siku ya kutangazwa, pale inapotokea iwapo Sheria Ndogo imeanza
kutumika:- (a) haki ya mtu yeyote (ambaye si Serikali au taasisi ya serikali)
iliyopo mara kabla ya siku ya utangazaji itaathiriwa kwa
namna ambayo itamuathiri mtu huyo; au (b) wajibu utatwikwa kwa mtu yeyote (ambaye si serikali wala
Serkali au taasisi ya serikali) kuhusiana na kitu chochote
kilichofanywa au kutofanywa kabla ya siku ya utangazaji,
23
na iwapo sharti lolote limefanywa kinyume na kifungu kidogo hiki, sharti
hilo litakuwa batili. (3) Mamlaka ya kupanga siku ambayo Sheria Ndogo itaanza
kutumika haitajumisha mamlaka ya kupanga siku tofauti kwa masharti
tofauti ya Sheria hiyo, labda kama sharti la wazi limefanywa kwa ajili
hiyo . Kuwasilisha
Kanuni Bungeni
na kukataliwa
38.-(1) Kanuni au sheria ndogo zote zitawasilishwa Bungeni ndani
ya kipindi cha siku sita za kukaa kwa Bunge kufuatia utangazaji
utakaofuata wa kanuni katika Gazeti la Serikali. (2) Bila ya kuathiri kifungu chochote kinachoelekeza vinginevyo
katika sheria, iwapo Bunge litapitisha Azimio la kukataa kanuni yoyote
ambayo taarifa ya azimio hilo litatolewa ndani ya siku 14 ya kukaa kwa
bunge baada kanuni hizo zimekwishawasilishwa bungeni au kama
kanuni zozote hazijawasilishwa Bungeni kwa mujibu wa kifungu kidogo
cha (1), kanuni hizo zitakoma kutumika , lakini bila ya kuathiri uhalali au
kuhalalisha chochote kilichotendwa au kilichoachwa kutendwa katika
wakati huo. (3) Kifungu kidogo cha (2) kitatumika bila ya kujali
kwambakipindi cha siku 14 kichotajwa katika kifungu kidogo hicho au
sehemu ya kipindi hicho hakitatokea katika au wakati wa kikao hicho
hicho cha Bunge kile ambacho kanuni zimewasilishwa Bungeni
kinahusika . (4) Bila ya kujali sharti lolote katika Sheria yoyote iliyo kinyume,
kama Bunge katika kipindi chochote litapitisha azimio la kubadilisha
kanuni yoyote au kuweka kanuni mbadala au sehemu ya kanuni ambayo
imekataliwa na Bunge chini ya kifungu kidogo cha (2), katika kupitisha
azimio lolote– (a) linalorekebisha Kanuni au sehemu ya kanuni, kanuni
iliyobadilishwa baada ya kuisha kwa siku saba, kutoka siku
ya kutangazwa katika Gazeti la Serikali ya taarifa iliyotolewa
katika kifungu kidogo cha (5), itaanza kutumika kama
ilivyorekebishwa. (b) kuweka kanuni mbadala au sehemu ya kanuni, kanuni
iliyobadilishwa baada ya kuisha kwa siku saba, kutoka siku
ya kutangazwa katika Gazeti la Serikali ya taarifa iliyotolewa
katika kifungu kidogo cha (5), itaanza kutumika kama
ilivyorekebishwa. (5) Baada ya kupitishwa kwa Azimio kwa mujibu wa kifungu
kidogo cha (2) cha kifungu cha (4), Taarifa ya Azimio hilo itachapishwa
kwenye Gazeti la Serikali ndani ya muda wa siku 21 baada ya kupitishwa
kwa Azimio hilo. (6) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (1) cha
kifungu cha 34, pale ambapo– (a) kanuni hazikubaliki chini ya kifungu hiki; na
24
(b) kanuni hizo zilizorekebishwa au kufuta kanuni ambazo
zilikuwa zinatumika mara kabla ya kanuni zilizotajwa kwa
mara ya kwanza hazijaanza kutumika,
kukataliwa kwa kanuni hizo kutahuisha kanuni za awali kwenye ile siku
na siku ya kukataliwa. (7) Iwapo Sheria ambayo inatoa uwezo au inaelekeza
kutengeneza kwa kanuni na mtu yeyote isipokuwa Rais,na inataka
kanuni hizo kukubalika au kuthibitishwa na Rais au mtu mwingine
yeyote au taasisi kabla kanuni hizo hazijatakuwa na nguvu za kisheria,
kifungu kidogo cha (1) hakitatumika kwenye kanuni hizo isipokuwa
kama zitakubalika au kuthibitiswa kama inavyotakiwa. (8) Katika kifungu hiki, neno “kanuni” linajumuisha kanuni na
Sheria Ndogo. Tafsiri ya sheria
ndogo 39.-(1) Maneno na misamiati inayotumiwa katika Sheria Ndogo
itakuwa na maana sawa na Sheria iliyotungwa chini ya Sheria Ndogo. (2) Rejeo katika Sheria Ndogo kwa neno “Sheria” litafafanuliwa
kumaanisha rejeo kwenye Sheria ambayo, Sheria Ndogo imetungwa.
Kutajwa kwa
sheria ndogo
40. Sheria Ndogo itatajwa kwa kurejea kwenye jina fupi kama
litakuwepo, au kwa kurejea kwenye namba ya Tangazo inayotolewa
kwenye Gazeti la Serikali. Marejeo ya
sheria
kujumuisha
sheria ndogo
41.-(1) Rejeo kwenye Sheria liltafchukuliwa kujumuisha rejeo
kwenye Sheria Ndogo yeyote iliyotungwa kwa mujibu wa Sheria
mama/kuu husika.
(2) Rejeo kwenye Sheria kwa Sheria ya mapokezi litafafanuliwa
vilevile kuhusu rejeo kwenye Sheria Ndogo iliyotungwa chini ya Sheria
mama. Matendo chini ya
sheria ndogo
kuchukuliwa
kama
yamefanyika
chini ya Sheria
42. Rejeo chini ya Sheria Ndogo kwenye sheria inayotumika
litatafsiriwa kujumuisha rejeo kwenye Sheria Ndogo iliyotungwa chini ya
Sheria mama.
Ada na tozo 43.-(1) Sheria Ndogo inaweza kuweka masharti ya kutozwa kwa
ada na tozo zinazohusiana na jambo lolote kwa kutilia maanani masharti
yaliyo wekwa katika Sheria Ndogo au katika Sheria ambayo, Sheria
Ndogo imetungwa. (2) Pale kifungu kimewekwa na Sheria Ndogo kinachohusu ada au
tozo, Sheria Ndogo husika yaweza kuweka mojawapo au baadhi ya
masharti yafuatayo– (a) ada maalumu au tozo;
(b) kuweka kiwango cha juu au cha chini cha ada au tozo ya aina
25
nyingine;
(c) kiwango cha juu na cha chini cha ada au tozo;
(d) ada au tozo kulingana na thamani ya kitu;
(e) kulipwa kwa ada au tozo kwa pamoja au kwa chini ya
masharti maalumu au mazingira yaliyoainishwa; na
(f) kupunguziwa, kusamehewa au kurejeshewa, kiasi chote au
sehemu ya ada au tozo. (3) Iwapo patakuwa na punguzo, msamaha au kurejeshewa, kwa
ada yeyote au sehemu ya ada au tozo ilivyotozwa na Sheria Ndogo,
punguzo hilo au msamaha au rejesho vyaweza kuchukuliwa kutumika au
kutumika kwa ujumla au kwa masharti maalum– (a) kuhusiana na mambo fulani au shughuli fulani au mambo au
aina ya mambo au shughuli;
(b) kuhusiana na nyaraka fulani au aina ya nyaraka;
(c) pale tukio linapotokea au wakati tukio linapoacha kutokea;
(d) kuhusiana na watu wa aina fulani au tabaka la watu fulani;
au
(e) kuhusiana na mchanganyiko wa mambo, shughuli, nyaraka,
matukio au watu, na yaweza kuelezewa kutumika au
kutumika kwa masharti yaliyoainishwa katika Sheria Ndogo
au kwa uamuzi wa mtu yeyote aliyeainishwa katika Sheria
Ndogo. (4) Kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (4) cha kifungu cha 2
cha kifungu hiki kitatumika kwenye Sheria Ndogo zilizotungwa chini ya
mamlaka iliyopewa ya kutunga Sheria baada ya kuanza kutumika kwa
Sheria hii.
SEHEMU YA SABA
UWEZO NA WAJIBU WA KISHERIA Muda wa
utekelezaji
uwezo au wajibu
kwa mujibu wa
sheria
44. Pale ambapo Sheria imetoa mamlaka au kuweka wajibu,
mamlaka hayo ya waweza kutekelezwa na wajibu huo kutekelezwa mara
kwa mara wakati tukio litahitaji.
Rejeo kwa
mshika ofisi
itajumuisha
warithi
45. Pale Sheria itatoa mamlaka au kutoa wajibu kwa afisa
aliyeshika madaraka ya ofisi ya umma, mamlaka hayo yanaweza
kutekelezwa na wajibu utafanywa na mtu ambaye kwa wakati uliopo
atakuwa ameshika nafasi hiyo kihalali, anakaimu au kutekeleza
majukumu ya ofisi. Tafsiri ya
maneno ya
kuwezesha.
46.-(1) Pale ambapo sheria imetoa mamlaka kwa mtu kufanya au
kupelekea kufanyika kwa kitu chochote au jambo, uwezo huo
utachukuliwa kuwa umetolewa kwa watu, ili kumwezesha mhusika
kufanya jambo au kusimamia kisheria utekelezwaji wa kitu au jambo. (2) Bila ya kuathiri ujumla wa matakwa ya kifungu kidogo cha
26
(1), pale sheria inatoa uwezo– (a) wa kutoa ,kuzuia ,kudhibiti au kusimamia jambo lolote,
uwezo huo utajumuisha uwezo wa kufanya hivyo sawa kwa
kutoa leseni au kusajili au kutoa vibali na uwezo wa kuzuia
vitendo kwa njia ya makatazo, kudhibiti au kusimamia kitu
hicho kunaweza kuepukwa; (b) kutoa leseni, kusajili,kupangisha, kutoa hakimiliki,
kibali,mamlaka, kuithibitisha au kutoa msamaha, uwezo huo
unajumuisha uwezo wa kutoa masharti kulingana na, leseni,
usajili,kupangisha, kumiliki, kibali,mamlaka, idhini au
msamaha vinaweza kutolewa; (c) kuithibitisha mtu yoyote, jambo au kitu, na uwezo huo
utajumuisha uwezo wa kufuta idhini iliyotolewa; (d) kutoa maelekezo, na uwezo huo utajumuisha uwezo wa
kutoa maelekezo sawa kwa aina ya makatazo. (3) Kwa kuzingatia kifungu kidogo cha (4) cha kifungu cha 2,
kifungu hiki kitatumika kwenye Sheria zilizotungwa au kupitishwa baada
ya kuanza kutumika kwa Sheria hii. Uwezo wa kutoa
leseni, nk., kwa
kwa hiari
47.-(1) Pale ambapo sheria inapotoa uwezo kwa mtu kutoa leseni
au kuhuisha,kutoa au kuisajiri tena leseni yeyote, kusajili,kupangisha,
kutoa hakimiliki,mamlaka, kuthibitisha, kutoa kibali, au msamaha, mtu
huyo aliyepewa uwezo huo anaweza kutumia mamlaka yake ,kutoa,
kuhisha leseni,au kukataa kutoa, usajili tena leseni
hiyo,kusajiri,kupangisha, kumiliki, mamlaka, kuidhinisha, kumpakibali
au kusamehe. (2) Hakuna katika Kifungu hiki kitakachoathiri haki iliyotolewa
na sheria nyingine yeyote kwa mtu yeyote kukata rufaa dhidi ya kukataa
kutoa,kumpa, kuhuishiwa leseni yeyote, kusajiliwa,kupangisha, kumiliki,
kuidhinishiwa au kupewa msamaha. Uwezo wa kuteua
unajumuisha
uwezo wa
kusimamisha, au
kuondoa
madarakani nk.
48.-(1) Pale ambapo Sheria inapotoa mamlaka au inapotoa wajibu
kwa mtu yeyote kuteua afisa au nafasi,ikijumuisha uteuzi wa kukaimu
nafasi, mtu aliyepewa mamlaka hayo atakuwa pia na uwezo wa–
(a) kumuondoa, kumsimamisha mtu aliyeteuliwa kwenye ofisi
au nafasi hiyo, na kumteua tena au kumrejesha kwenye
nafasi hiyo,mtu yeyote aliyeteuliwa kutekeleza uwezo au
wajibu huo; (b) pale mtu aliyeteuliwa kushika madaraka ya ofisi au nafasi,
atasimamishwa au atashindwa, au anaelekea kushindwa kwa
sababu yoyote kutekeleza kazi za ofisi hiyo au nafasi
aliyoteuliwa, atateua mtu mwingine kukaimu nafasi hiyo
kwa muda kwa niaba ya yule aliyeteuliwa, aliyesimamishwa
kwa muda wote ambao mtu huyo amesimamishwa au hawezi
kutekeleza wajibu wake, lakini mtu huyo atateuliwa kukaimu
27
kama tu anastahili nakuwa na sifa za kuteuliwa kwenye ofisi
au nafasi hiyo; na (c) kuainisha muda ambao mtu yeyote aliyeteuliwa kutekeleza
mamlaka au wajibu atashika madaraka ya nafasi
aliyoteuliwa. (2) Kwa mujibu wa aya ya (b) ya kifungu kidogo cha (1)
“sababu” linajumuisha– (a) ugonjwa;
(b) kutokuwepo kwa muda, ndani ya Jamhuri ya Muungano; na
(c) mgongano wa kimaslahi. (3) Uhalali wa jambo lolote lililotendwa au kufanywa na mtu
yeyote kwa madai ya kuteuliwa chini ya ibara ya (c) ya kifungu kidogo
cha (1) haitahojiwa kwa madai kuwa uteuzi wake haukukamilika au
ulikoma. (4) Pale ambapo Sheria imetoa mamlaka au imetoa wajibu kwa
mtu yoyote kufanya uteuzi kwenye ofisi au nafasi na uwezo huo au
wajibu huo waweza kutekelezwa tu baada ya uteuzi au mapendekezo ya
majina, au kama uteuzi huo shurti uridhiwe, au uthibitishwe au ukubaliwe
na watu wengine, basi uwezo uliotolewa kwa mujibu wa aya ya (a) hadi
(c) za kifungu kidogo cha (1) utatumiwa kwa kuzingatia uteuzi au
mapendekezo au kwa kuzingatia uthibitisho, kuungwa mkono au ridhaa. (5) Hakuna jambo lolote katika kifungu hiki litaathiri muda wa
kushika madaraka ya ofisi au wadhifa wa mtu yoyote, kwa mujibu wa
masharti ya Sheria yeyote ya Bunge. Uteuzi kwa jina
au ofisi, nk. Na
uteuzi wa
Mwenyekiti wa
Bodi,
49.-(1) Pale ambapo Sheria inatoa mamlaka au kutoa wajibu kwa
mtu kuteua au kutaja mtu na kumpa madaraka ya–
(a) kufanya kazi yeyote;
(b) kuwa mjumbe wa Bodi, baraza la nyumba, kamisheni,
kamati au baraza au kitu kingine kilichoundwa kwa namna
hiyo; au
(c) kuwa au kufanya jambo lolote, mtu huyo aweza kuteua kwa kumtaja mtu kwa jina lake au kwa kuteua
mtu aliyeshika kwa masharti ya uteuzi wa ofisi yake; na uteuzi wowote
wa afisa anayeshikilia ofisi hiyo kutatafsiriwa kama uteuzi wa mtu huyo
mara kwa mara atakayeshikilia nafasi hiyo,tatakayekaimu, au
atakayekuwa akitekeleza kihalali kazi za ofisi hiyo. (2) Pale kwa au chini ya Sheria yoyote imetoa mamlaka kwa mtu
yoyote au mamlaka kuteua wajumbe wa bodi, kamisheni, kamati au
chombo chochote kinachofanana nayo, mtu huyo au, mamlaka
hiyo,inaweza isipokuwa kama itaenda kinyume na dhamira
itakayojitokeza itateua au kuweka kanuni, za uteuzi wa Mwenyekiti au
Makamu Mwenyekiti na katibu wa bodi, kamisheni, kamati au chombo
kingine kinachofanana na aina hiyo. Uwezo wa walio
wengi, akidi nk. 50.-(1) Pale ambapo Sheria inapotoa mamlaka au majukumu kwa
28
bodi au idadi ya watu ambao hawapungui watatu,kazi hiyo inaweza
ikafanywa na wengi kati ya watu hao. (2) Pale ambapo Sheria imeunda bodi, kamisheni, kamati au
baraza au aina yeyote ya chombo kinachofanana na hivyo na yenye
wajumbe 3 au zaidi (katika kifungu hiki ikijulikana kama “ushirika”)– (a) katika mkutano wa jumuiya, idadi ya wajumbe iko sawa na– (i) angalau nusu ya idadi ya wajumbe iliyotolewa na
sheria yeyote ya bunge, kama namba hiyo imetajwa
maalum;na
(ii) kama namba ya wajumbe imeainishwa katika
sheria haikutaja idadi kamili, lakini ipo katika
kiwango cha juu au chini, angalau nusu ya idadi ni
wanachama wapo katika ofisi kama idadi hiyo iko
katika kiwango, kinachofikia akidi; na (b) tendo au jambo lolote liliofanywa na idadi kubwa ya
wajumbe waliohudhuria kwenye mkutano, kama wajumbe
waliopo wanafikia akidi, kuchukuliwa kuwa imeamuliwa na
ushirika. Utekelezaji wa
uwezo unaweza
kusahihishwa
51. Pale ambapo Sheria inatoa uwezo au jukumu kwa mtu
kufanya jambo au kitu cha kiutawala au cha madaraka au kufanya uteuzi
wowote, uwezo au jukumu linaweza kufanywa au kutekelezwa mara
kwa mara kama itakavyoonekana inafaa, kusahihisha makosa yoyote au
kuacha jambo ambalo lilitakiwa kufanywa huko nyuma au kutekelezwaji
wa uwezo au jukumu, bila ya kujali kuwa uwezo au jukumu hilo haliwezi
kutekelezeka kwa ujumla au kufanyika mara kwa mara. Athari ya uteuzi
wakati afisa
anayestaafu
yuko likizo
52. Wakati afisa anayeshikilia madaraka katika ofisi yeyote
iliyoundwa chini ya Sheria yeyote yuko kwenye likizo akisubiri kuachia
madaraka kwenye ofisi yake, itakuwa halali kisheria kwa mtu mwingine
kuteuliwa rasmi kushika wadhifa wa ofisi hiyo. "Inaweza au
anaweza” ina
maana ya hiari
na neno “ata” au
“ita” lina maana
ya lazima
53.-(1)Pale katika Sheria, litumikapo neno “inaweza” au
“anaweza” litatumika kutoa uwezo, neno hilo litatafiriwa kumaanisha
kuwa uwezo uliotolewa unaweza kutekelezeka au kutokutekelezeka kwa
kuamuwa.
(2) Katika Sheria litumikapo neno “ata” au “ita” litatumika
kutwisha jukumu, na neno hilo litatafsiriwa kumaanisha majukumu
yaliotwishwa sharti yafanyike. Uwezo wa bodi
n.k
havitaathiriwa
kwa nafasi
iliyowazi au
mapungufu
mengine
54. Pale ambapo bodi, baraza la nyumba, tume, kamati au baraza
au chombo kingine kinachofanana na hicho ,yaweza ikawa shirika au
kampuni ,litaanzishwa chini ya Sheria, mamlaka ya chombo hicho
havitaathiriwa na–
(a) kuwepo kwa nafasi yoyote ya wazi ya mwanachama wa
29
bodi;
(b) mapungufu yoyote yatakayojitokeza katika uteuzi au sifa ya
mtu yeyote aliyetarajiwa kuwa mjumbe wa bodi au kukaimu
nafasi ya mjumbe;
(c) kasoro ndogo itakayotokea katika kuitisha au kuendesha
mikutano ya bodi, au
(d) kuwepo au kushiriki katika mikutano kwa mtu ambaye
hastahili kuwepo au kushiriki katika mkutano. Utekelezaji wa
mamlaka Fulani
kwa anayekasimu
55. Pale ambapo Sheria ianelekeza kuwa utendaji wa kazi yoyote
na mtu utategemea na maoni, imani au ufahamu wa mtu huyo juu ya kitu
chochote na kazi hiyo alivyokasimiwa chini ya sheria yoyote, kazi hiyo
inaweza kutekelezwa na muwakilishi kwa kuzingatia maoni, imani, au
ufahamu wa mtu anayekasimu kuhusiana na jambo hilo. Rejeo kwenye
eneo kwa
kutumia mipaka
56.-(1) Pale Sheria inaporejea au kutaja sehemu yoyote ya
Jamhuri ya Muungano kwa tamko maalum, itatumika kumaanisha, kwa
jinsi hiyo, sehemu hiyo kama itakavyotajwa ambayo mara kwa mara
imefafanuliwa, mpaka wake umewekwa au kuainishwa, isipokuwa kama
imeelekezwa vinginevyo. (2) Pale ambapo eneo limetengwa kwa, kurejea kwenye eneo
lolote ambalo limebadilishwa, marejeo katika sheria yeyote juu ya eneo
liliyobadilishwa kutoka kwenye eneo la zamani, yatafafanuliwa kama
rejeo la eneo lililotengwa.
Tafsiri ya Uwezo
wa kukasimu
57.-(1) Pale Sheria inatoa uwezo kwa mtu kukasimu utekelezaji
wowote wa mamlaka au majukumu ya wajibu wowote aliopewa au
kuwekwa juu yake chini ya sheria– (a) uwakilishi huo hautamzuia mtu aliyekasimiwa, kutekeleza na
kufanya katika muda wowote mamlaka au majukumu yake
aliyokasimiwa; (b) uwakilishi huo unawaweza kufanywa kwa kuzingatia
masharti yoyote, sifa, ukomo au vigezo maalumu ambavyo
mtu aliyeteuliwa anaweza kuainisha; (c) iwapo uwakilishi unaweza kufanywa tu kwakuthibitiswa na
uteuzi huo na marekebisho yoyote ya kukasimu, yanaweza
yakafanywa kwa kuzingatia masharti,sifa , ukomo au sababu
maalumu ambazo mtu aliyethibitishwa ataziainisha; (d) uwakilishi huo unaweza ukafanywa kwa mtu aliyeainishwa
au watu lililoainishwa katika daraja, au yaweza ikafanywa
kwa mtu aliyeshikilia madaraka au watu walioshikilia
madaraka kwa wakati huo wanakuwa kwenye ofisi au aina
za ofisi; (e) uwakilishi huo unaweza kurekebishwa au kufutwa kwa hati
iliyoandikwa na kusainiwa na mtu aliyekasimiwa madaraka;
30
(f) ikiwa mamlaka aliyopewa mtu kwa ambapo uwezo wa
kuteua mwakilishi umetolewa kwa mtu kwa kuzingatia
masharti yaliyoanzisha ofisi, kukasimu huko
hakutachukuliwa kuwa na madhara kwa sababu tu za
kubadilishwa, mtu anayeshikilia ofisi kihalali, anayekaimu
au kutekeleza kazi za ofisi hiyo. (2) Kukasimu madaraka kutachukuliwa kujumuisha uwakilishi
unaoambatana au uanohusiana na majukumu, na kukasimu kwa
uwakilishi huoutachukuliwa kujumuisha uwakilishi unaoambatana au
kuhusiana na uwezo huo. (3) Pale chini ya Sheria, kitendo au jambo laweza au linatakiwa
kufanywa kwa kurejea kwenye au kuhusiana na mtu, na mtu huyo kwa
mujibu wa sheria amepewa uwezo wa kukasimu kazi iliyopewa au
kuwekwa kwake kuhusiana na au matokeo yanayotokana na kufanya kwa
kitendo hicho au jambo hilo, kwa kurejea kwenye kitendo au kuhusiana
na mtu ambaye amekasimiwa jukumu hilo. Ni nani ataweka
lakiri ya kampuni
au shirika
58. Pale ambapo Sheria inaruhusu bodi au kamati kufanya kitu
chochote, jambo lolote, au kitu itachukuliwa kumaanisha kwambakitendo
hiko,jambo hilo au kitu hicho kinaweza au kufanywa na bodi au kamati
kama itatokea.
Haki za Serikali 59. Hakuna Sheria kwa namna yoyote itakayoibana au kuathiri
haki za Serikali ya Jamhuri ya Muungano, isipokuwa kama Sheria hiyo
imetamka, au kama itaonekana ni muhimu kwamba Serikali ya Jamhuri
kubanwa na sheria hiyo.
SEHEMU YA NANE
MASHARTI KUHUSU, MUDA NA UMBALI Kukokotoa Muda 60.-(1) Katika kukokotoa wakati kwa mujibu wa Sheria ya
Bunge– (a) pale ambapo muda umeelezwa kwa, juu ya au katika siku
iliyoainishwa, siku hiyo itajumuishwa katika kipindi hicho; (b) pale kipindi kimeelezwa kuwa kinakokotolewa tokea, au
baada , siku maalumu, siku hiyo haitajumuishwa katika
kipindi hicho; (c) pale ambapo jambo fulani linatakiwa kufanywa ndani ya
muda kabla ya siku iliyoainishwa, muda huo
hautajumuisha kwenye siku iliyotajwa; (d) pale ambapo muda umeelezwa kukoma mnamo,juu au
ndani ya siku iliyotajwa, au kuendelea hadi siku iliyotajwa,
siku hiyo itajumuishwa katika kipindi hicho; (e) pale ambapo muda wa kutendwa jambo fulani unakoma,
31
au unaangukia katika siku ambayo imetolewa katika
orodha, jambo hilo laweza kufanywa katika siku inayofuata
ambayo haijaondolewa katika orodha; (f) pale ambapo kuna rejeo ya idadi ya siku kamili, au
“angalau” au “isiyopungua”au “isiyozidi”, idadi ya siku
yaliyotajwa, siku hizo zitahesabiwa kwa kuondoa siku
ambazo zimo ndani ya matukio yaliyotajwa; (g) pale ambapo kuna rejeo kwenye idadi ya siku ambazo
hazikutajwa au “angalau siku”, au “isiyopungua siku” idadi
ya siku katika matukio mawili, katika kuhesabu idadi ya
siku inatakiwa kuondoa siku ambayo tukio la kwanza
linatokea na kuondoa siku ambapo tukio la pili linatokea
zitaondolewa katika orodha; (h) Pale ambapo kitendo au mwenendo umeelekezwa moja
kwa moja au unaruhusu kufanyika au kufanywa katika siku
fulani, au kwenye hiyo siku au kabla ya siku fulani, basi
kama siku hiyo imeondolewa katika orodha, tendo hilo au
mwenendo huo vitafanywa au vitahesabika kuwa
vimefanywa katika siku muafaka iwapo vitafanyika
aukuchukuliwa kufanyika siku ya pili ambayo sio siku
ambayo imeondolewa kwenye orodha. (2) Kwa minajili ya kifungu hiki, “siku zilizoachwa nje ya
orodha” ina maana siku za Jumamosi, Jumapili au siku yoyote ya likizo
au ile sehemu inayohusiana na siku ambayo tukio, tendo, kitu, hatua au
mwenendo kuchukuliwa.
Kuhesabu miezi 61.-(1) Katika Sheria, neno “mwezi” lina maana ya mwezi wa
kalenda, ikimaanisha, mwezi unaohesabiwa kwa kufuata kalenda. (2) Kama kipindi cha mwezi mmoja kilichoainishwa katika
Sheria ya Bunge kinaanza katika siku isiyokuwa siku ya kwanza kati ya
miezi 12 ya kalenda, siku hiyo itahesabiwa kuanzia siku ambapo inaanza
hadi siku kama hiyo ya mwezi unaofuata, baada ya kutoa moja, au kama
hakuna tarehe iliyo sawa, itakuwa siku ya mwisho ya mwezi huo. Kwa mfano: mwezi unaoanzia tarehe 15 Januari utashia tarehe 14
Februari na mwezi unaoanzia tarehe 30, 31 Januari utaishia tarehe 28
Februari (au 29 Februari katika mwaka mrefu). (3) Kama kipindi kilichotajwa katika Sheria ya Bunge ni miezi 2,
3 au mwezi mrefu, kitaanza kuhesabiwa kuanzia tarehe kipindi hicho
kinatakiwa kuanza hadi namba inayowiana, ukiondoa moja ,katika ya pili,
ya tatu au miezi mingine inayofuata baada ya hapo, au kama hakuna
tarehe zinazofanana, siku ya mwisho ya mwezi huo unaofuata. Kwa mfano: kipindi cha miezi 6 kinachoanza tarehe 15 Agosti,
kinaishia tarehe 14 Februari na kipindi cha miezi 6 kinachoanzia tarehe
30 au 31 Agosti kinaishia tarehe 28 Februari (au tarehe 29 Februari katika
mwaka mrefu).
32
Masharti
palemuda
haujapangwa
62. Pale ambapo muda kamili haukutajwa au kuruhusu kufanya
tendo au kitu, kitendo hicho au jambo hilo laweza kufanywa kwa haraka
iwezekanavyo, na kwa nyakati mbalimbali, kadri matukio yatakavyo
jitokeza. Tafsiri uwezo
kuongeza muda 63.-(1) Pale ambapo Sheria ya Bunge imeweka muda maalumu au
imeruhusu jambo fulani kutendwa au kufanya mwenendo wowote na
kimahakama imepewa uwezo au mamalaka nyingine kuongeza muda,
uwezo huo waweza kufanywa na mahakama au mamlaka nyingine
ingawaje kuongeza muda hakukufanywa mpaka baada ya kuisha kwa
muda uliowekwa au kuruhusiwa. (2) Kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1) kifungu hiki yatumika
kuhusiana na Sheria za Bunge ziliotungwa au kupitishwa baada ya kuanza
kutumika kwa Sheria hii. Mkengeuko wa
matumizi ya
fomu, taratibu
64. Isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo, fomu
zilizoainishwa, kukengeuka huko hakutaathiri msingi na hakutahesabiwa
kupotosha, kupunguza nguvu au uzito wa taarifa zake. Vipimo vya
umbali 65. Katika kupima umbali kwa ajili ya madhumuni ya Sheria
yeyote ya Bunge, umbali utapimwa kwa mstari ulionyooka katika mlalo
ulio sawa.
SEHEMU YA TISA
TARATIBU NA ADHABU Mashauri ya
wadhifa wa
kiofisi hayakomi
baada ya kifo.
66. Mashauri ya madai au jinai dhidi ya mtu yeyote kwa misingi
ya wadhfa wake hayatasimamishwa au kukoma kutokana na kifo,
kujiuzulu, kutokuwepo au kuondolewa madarakani kwa mtu huyo, bali
yaweza kuendelezwa na au dhidi ya mtu mwingine yeyote,kama
itakavyowezekana, na mtu ambaye, atakuwa ameshikilia madaraka ya
ofisi hiyo. Kanuni za
mahakama 67.-(1) Katika Sheria ya Bunge, maneno “kanuni za mahakama”
kuhusiana na mahakama, yana maana ya kanuni zilizotungwa na
mamlaka yenye uwezo kwa wakati uliopo, wa kutunga kanuni au amri za
kusimamia utendaji na mwenendo katika mahakama husika. (2) Uwezo wa mamlaka uliotajwa katika kifungu kidogo cha (1)
unajumuisha uwezo wa kutunga kanuni za mahakama kwa ajili ya sheria
yoyote inayoelekeza au kuruhusu jambo lolote lifanywe na au kwa
mujibu wa kanuni za mahakama. kutolewa kwa
adhabu si kizuizi
cha kesi ya
madai
68. Kutolewa kwa adhabu au faini na au kwa mujibu wa
mamlaka ya Sheria yeyote, kama hakuna masharti yaelekezavyo
vinginevyo, hakutatoa ahueni ya wajibu kwa mtu kushtakiwa kwa
33
madhumuni ya kumwajibisha mtu huyo kutoa fidia kwa mtu yeyote
aliyejeruiwa Upatikanaji wa
faini na adhabu
Sura ya .20
69. Pale ambapo faini au adhabu za aina nyingine zimetozwa
chini ya Sheria, na hakuna taratibu zilizowekwa na Sheria za namna ya
upatikanaji wa faini au adhabu, itachukuliwa kwamba faini au adhabu
hizo zinaweza kutozwa au kupatikana kwa dharura, chini ya vifungu vya
Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai kwa mashauri ya dharura kwa njia
ya muhtasari au chini ya sheria nyingine yoyote ambayo itakuwa
inatumika kwa ajili hiyo. Kutia hatiani
mara dufu 70. Pale ambapo tendo limetamka kosa mara mbili au zaidi iwe ni
kwa mujibu wa Sheria moja au vinginevyo, mkosaji atashtakiwa kwa
kosa lolote au makosa yote lakini hataadhibiwa mara mbili kwa kosa la
aina moja. Matumizi ya
Sheria ya Kanuni
za Adhabu kwa
Makampuni.
71.-(1) Sheria yoyote inayo ainisha makosa ambayo adhabu zake
baada ya kutiwa hatiani, au kwa kutiwa hatiani kwa muhtasari, itahusisha
pia kampuni, mashirika, taasisi na watu binafsi. (2) Pale ambapo Sheria kukamatwa kwa mali kwa ajili ya kufidia
mwathirika wa kosa,au adhabu inatolewa kwa kwa mtu aliyeudhiwa,
faini, tozo au fidia hiyo italipwa kwa shirika, kampuni au taasisi
iliyodhurika kama taasisi hiyo itakuwa ni sehemu ya waasirika wa kosa
husika. (3) Isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo, pale ambapo
adhabu imeainishwa katika Sheria dhidi ya kosa ambalo adhabu yake
haijumuishi kulipwa kwa faini, mahakama ambayo inasikiliza kesi hiyo
inaweza , kwa mkosaji ambaye ni shirika, kampuni au taasisi kutoza
faini– (a) pale ambapo adhabu ni kifungo kisichozidi miezi sita, faini
itozwe ya Shilingi Milioni Mbili; (b) pale ambapo adhabu ni kifungo kisichozidi miezi sita lakini
kisochozidi mwaka mmoja itatolewa, faini itozwe ya Shilingi
Milioni Tatu; (c) pale ambapo adhabu ni kifungo kinachozidi mwaka mmoja
lakini hakizidi miaka miwili itatolewa, itozwe faini ya
Shilingi Milioni Tano; (d) pale ambapo adhabu ni kifungo kinachozidi miaka mitatu
itatolewa, itozwe faini ya Shilingi Milioni Kumi.
Masharti ya
makosa chini ya
sheria mbili au
zaidi
72. Pale ambapo tendo la aina moja limeainishwa kama kosa chini ya
Sheria mbili au zaidi, mkosaji isipokuwa kama dhamira itajitokeza,
litashitakiwa na kuadhibiwa kwa mujibu wa Sheria yoyote mojawapo,
lakini hataadhibiwa zaidi ya mara moja kwa kosa linalofanana.
34
Marekebisho ya
adhabu 73. Pale ambapo tendo limepelekea kosa,na adhabu kwa kosa hilo
imerekebishwa kati ya muda ambao kosa hilo limetendeka na baada ya
kutiwa hatiani, mshtakiwa isipokuwa kama marekebisho ya adhabu
yameelekeza dhamira yake vinginevyo,, ataadhibiwa kwa kutumia
adhabu iliyokuwa ikitumika wakati wa kutendeka kwa kosa hilo. Maagizo ya
adhabu ya juu ,
ya chini, ya kila
siku na ya
pamoja
74.-(1) Pale ambapo Sheria ya Bunge imeainisha adhabu kwa
kosa, ile adhabu iliyoainishwa ndiyo itakayokuwa ya juu kwa kosa hilo.
(2) Pale ambapo Sheria imeainisha adhabu zaidi ya moja kwa kosa
moja, matumizi ya neno “na” katikati ya adhabu hizo mbili, itamaanisha
adhabu hizo zaweza kutozwa moja pekee au zitozwe zote mbili kwa
pamoja. (3) Pale ambapo Sheria imeainisha kiwango cha juu cha adhabu
na cha adhabu ya chini kwa kosa moja, kosa hilo laweza kutolewa
adhabu isiyopungua kiwango cha chini cha adhabu na isiyozidi kiwango
cha juu. (4) Pale ambapo Sheria imeainisha kiwango cha chini cha adhabu
kwa kosa, kosa hilo litatolewa adhabu isiyo chini ya kiwango cha chini
cha adhabu. (5) Pale ambapo Sheria imeainisha adhabu inayotolewa au
kutozwa kila siku kwa kosa llilotamkwa, elekezo hilo lina maana
kwamba, adhabu isiyopungua adhabu iliyotamkwa kwa kila sikuinaweza,
ikatolewa na nyongeza ya adhabu nyingine kwa kosa hilo, na itatozwa
kwa kila siku au sehemu ya siku ambapo kosa hilo litaendelea kutendwa. Vifungu
vinavyohusu
kujaribu
75. Kifungu katika Sheria kinachopelekea kosa, isipokuwa kama
dhamira itajitokeza litachukuliwa kama jaribio la kutaka kutenda kosa
litakuwa ni kosa chini ya kifungu hicho, linalostahili adhabu kana
kwamba kosa lenyewe limetendwa. Utoaji wa mali
au vitu
vilivyotwaliwa
76.-(1) Pale ambapo chini ya Sheria yoyote inaelekeza
kukamatwa kwa mnyama au kitu chochote kwa amri ya mahakama au
mamlaka yoyote, itaweza isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo au kama
itaelezwa na sheria kuchukuliwa na mtu yeyote ,kuchukuliwa na Serikali
ya Jamhuri ya Muungano, na mapato yote yatakayopatikana, kama
yataamuliwa na mamlaka husika kuuzwa, gharama zitalipwa na
kuhesabiwa kama sehemu ya mapato ya umma, isipokuwa kama vifungu
vingine vitaelekeza vinginevyo. (2) Hakuna kitu chochote katika kifungu hiki kitakachoathiri
kifungu chochote katika Sheria yoyote ya Bunge ambayo kwayo, sehemu
ya faini au mali iliyotwaliwa, au mwenendo wa mali yoyote iliyotwaliwa,
vimeelekezwa vitwaliwe na mtu yeyote au vitolewe na mtu au mamlaka
yoyote kwa mtu yeyote . Uwajibikaji wa
mwajiri au mkuu 77. Pale kosa lolote chini ya Sheria limetendwa na mtu kama
35
wakala au mtumishi , isipokuwa kama dhamira nyingine imeelezwa, na
wakala huyo au mwajiriwa, pamoja na mwajiri au mkuu wa sehemu hiyo
watakuwa wametenda kosa na endapo watapatikana na hatia wanaweza
kushtakiwa na kuadhibiwa sawia, isipokuwa kama ataithibitishia
mahakama kwamba hakujua chochote kuhusu uhalifu huo, na kwa
kutumia busara ya kawaida, asingeweza kufahamu kutendeka kwa kosa
hilo. Ushahidi wa
agizo , kibali au
ridhaa ya
mtumishi wa
umma
78. Wakati wowote ambapo amri au agizo la kiutawala, idhini au
kibali cha afisa wa serikali kinahitajiwa kabla ya kuanza kuendesha kesi
au mashauri, hati yoyote inayoonyesha kuwa amri, agizo au ridhaa
imetolewa, itachukuliwa kama ushahidi wa kutosha katika kesi au
mashauri, bila ya kuhitaji ushahidi mwingine kuthibitisha kwamba saini
iliyoko kwenye hati hiyo, ni ya afisa wa serikali mhusika. Utekelezaji wa
mamlaka ya
Mkurugenzi wa
Mashtaka (DPP)
wakati hayupo
79. Mamlaka ya Mkurugenzi wa Mashtaka yanaweza
kutekelezwa na Afisa wa Sheria aliyeteuliwa na Mwanasheria Mkuu wa
Serikali kwa madhumuni hayo, iwapo Mkurugenzi wa Mashtaka.
atakuwa hayupo Makao Makuu ya Ofisi yake, au atakuwa hawezi
kutekeleza majukumu yake kutokana na ugonjwa au kwa sababu nyingine
yoyote , Tamko la adhabu
mwishoni mwa
kifungu
80.-(1) Pale ambapo katika Sheria, adhabu–
(a) imeainishwa bila ya masharti yoyote kutajwa mwishoni mwa
kifungu, (b) imeainishwa mwishoni mwa kifungu kidogo cha Sheria,
lakini sio chini ya kifungu;au (c) imeainishwa mwishoni mwa kifungu cha Sheria na kuelezwa
kuwa kitatumika kwenye na kifungu kidogo katika kifungu
hicho, basi, isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo, kuainishwa huko
kunamaanisha kwamba ukiukwaji wa kifungu au kifungu kidogo, au
kama itakavyohusu, kifungu chochote kidogo, ni kosa ambalo
linaadhibiwa kwa adhabu isiyopungua ile iliyotajwa. Makosa
yanayoendelea 81.-(1) Pale ambapo–
(a) kwa mujibu au chini ya Sheria, kitendo au kitu inatakiwa au
imeelekezwa kifanywe ndani ya muda fulani au kabla ya
wakati fulani; na (b) kushindwa kutenda kitendo hicho au kitu hicho ndani ya
muda au kabla ya wakati ilioelezwa katika aya(a) litakuwa ni
kosa; na (c) kitendo hicho au jambo hilo litafanyika ndani ya muda
uliotajwa au katika wakati uliotajwa kama ilivyoelezwa aya
(a), vifungu vifuatavyo vitahusika– (i) jukumu la kutenda kitendo au jambo hilo
litaendelea, bila ya kujali kwamba kipindi
36
kilichopangwa kimepita au muda uliowekwa
umepita, hadi hapo kitendo hicho au jambo hilo
litakuwa limetendwa; (ii) pale ambapo mtu ametiwa hatiani kwa kosa
ambalo, kwa mujibu aya (i) limetokana na
kushindwa kutenda kitendo au jambo baada ya
kuisha kwa kipindi kilichowekwa au baada ya
muda uliopangwa,kama utakuwepo , mtu huyo
atakuwa ametenda makosa tofauti, na kosa jingine
yanayofuata kwa kila siku baada ya siku ya
kuhukumiwa, kwa kosa hilo au jambo hilo kwa kila
siku inayoendelea; na (iii) isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo, adhabu
itozwayo kwa kila kosa pekee na makosa mengine
yanayofuata itakuwa ni kiasi kilicho sawa na
Shilingi Elfu Thelathini. (2) Pale ambapo– (a) kwa mujibu wa au chini ya Sheria, tendo au kitu kinatakiwa
au kimeelekezwa kifanywe lakini hakuna kipindi au muda
uliowekwa wa kufanya kitendo au kitu hicho; na (b) kushindwa kufanya kitendo hicho au kitu hicho ni kosa; na (c) mtu anatiwa hatiani kwa kosa la kushindwa kufanya kitendo
hicho au kufanya jambo hilo, mtu huyo atakuwa ametenda kosa la kipekee na kosa jingine linalofuata
kwa kila siku baada ya siku ya kutiwa hatiani,na iwapo atashindwa
kutenda kitendo hicho au kufanya jambo hilo kunaendelea na, isipokuwa
kama imeelekezwa vinginevyo, adhabu itozwayo kwa kila kosa ambalo ni
tofauti na makosa mengine yanayofuata atatozwa kiasi cha Shilingi Elfu
Thelathini. (3) Mashtaka dhidi ya mtu mmoja kwa makosa mbalimbali chini
ya aya ya (ii) cha kifungu kidogo cha (1) au kifungu kidogo cha (2)
yaweza kuunganishwa katika taarifa moja au mashtaka kama makosa
husika yanahusiana na kushindwa kufanya kitendo kinachofanana au kitu. (4) Kama mtu atatiwa hatiani kwa kosa zaidi ya mojawapo ya
chini ya aya (ii) cha kifungu cha (1) au zaidi ya makosa chini ya kifungu
kidogo cha (2), mahakama yaweza kutoa adhabu moja kwa makosa yote
ambayo mtuhumiwa ametiwa hatiani chini ya kifungu kidogo husika,
lakini adhabu yake haitazidi kiwango cha juu cha adhabu inayoweza
kutozwa kama adhabu hiyo ingetozwa otfauti kwa kila kosa.
SEHEMU YA KUMI
MASHARTI YA JUMLA Uwasilishaji wa
Nyaraka kwa njia 82.-(1) Pale ambapo Sheria ya Bunge inaruhusu au kutaka kuwa
37
ya posta hati iwasilishwe kwa njia ya posta, iwapo neno “wasilisha” au maneno
mengine kama vile, “patia”, “kupata”, au “peleka” au maneno mengine ya
yanayofanana, au tafsiri itakayotumika ,kuwasilisha kutachukuliwa kuwa
kuwasilisha kwa utimilifu kwa kuandika anuani sahihi na kuposti kwa
(kulipa gharama stahiki) hati ya kupeleka barua kwa kutumia anuani ya
mwisho ya anayepelekewa, na isipokuwa kama itathibitiswa vinginevyo,
itahesabiwa kwamba kutaathiri muda ambao barua hiyo ingewasilishwa
kwa njia ya kawaida ya posta. (2) Pale ambapo Sheria inaruhusu au inaelekeza kuwa hati ya
kuwasilishwa iwasilishwe kwa njia ya rejesta ya posta, hata kama neno la
“wasilisha” au maneno mengine kama “patia”, “peleka” au “wasilisha” au
maneno mengine ya msemo kama huo yametumika, basi kama hati hiyo
inasomeka na inakubalika kwa kuwasilishwa kama barua iliyothibitishwa,
kuwasilishwa kwa hati hiyo kwaweza kufanywa ama kwa rejesta ya
posta, au kwa njia ya barua iliyothibitishwa. (3) Vifungu vidogo vya (1) na (2) vitahusika, isipokuwa kama
dhamira nyingine inaonekana na kifungu kidogo cha (2) hakitahusika pale
ambapo Sheria imeelekeza kutolewa kwa uthibitisho au stakabadhi
iliyosainiwa na mtu ambaye hati hiyo imepelekwa kupitia anuani yake na
hiyo itaashiria kuwa hati hiyo imewasilishwa kwa mhusika. Uwasilishaji wa
Nyaraka kwa
ujumla
83. Pale ambapo Sheria inaruhusu au kuelekeza kuwa hati
iwasilishwe, hata kama neno “wasilisha”, “patia”,”peleka” au “wasilisha”
au neno lingine kama hilo au msemo wa aina hiyo umetumika lakini bila
ya kuelekeza kuwa uwasilishwaji ufanywe kwa namna gani, basi hati
hiyo itakuwa imewasilishwa kikamilifu kwa mhusika:– (a) kwa kupeleka hati hiyo kwa mtu huyo binafsi; au
(b) kwa njia ya posta kulingana na maelekezo ya kifungu kidogo
cha (1) cha kifungu cha 82; au
(c) kwa kuacha hati kwa mhusika kwenye makazi yake ya
kawaida au yale ya mwisho yaliyokuwa yanafahamika, au
kama ni mkuu wa biashara makao makuu ya biashara zake,
au
(d) kama mhusika ni kampuni au shirika au taasisi au chama, au
jumuiya ya watu (bila ya kujali kama imeandikishwa kama
kampuniau la), kwa kuwasilisha, au kuiacha nyaraka au
kuiposti kama barua kwa anuani ya kampuni, shirika, taasisi
au chama kwenye makao makuu ya biashara au ofisi kuu
zilizomo ndani ya Jamhuri ya Muungano. Lugha ya sheria
za Tanzania 84.-(1) Lugha za Sheria za Tanzania zitakuwa ni Kiswahi au
Kiingereza au lugha zote mbili. (2) Pale ambapo Sheria yoyote imetafsiriwa kutoka lugha moja
kwenda lugha nyingine na kuchapishwa kwa lugha zote mbili, na iwapo
itatokea mgongano au kutakuwa na mashaka ya maana ya maneno au
maelezo, lugha ambayo imetumika wakati wa kupitisha Sheria hiyo na
38
Bunge, ndiyo itakayokuwa ya kipaumbele (3) Pale ambapo Sheria imeandikwa kwa lugha zote mbili na
ukatokea mgongano au mashaka kuhusiana na maana ya neno lolote au
maelezo, tafsiri ya Kiingereza ndiyo itakayotumika. Kufutwa kwa
Sheria ya Bunge
Na 30 ya mwaka
1972
85. [Inafuta Sheria ya Kanuni za Ufafanuzi wa Sheria na Vifungu
vya Ujumla]
___
NYONGEZA
______
(Kifungu cha 4)
NCHI ZA JUMUIYA YA MADOLA
Antigua and Bermuda Namibia
Australia Nauru
The Bahamas New Zealand
Bangladesh Nigeria
Barbados Papua New Guinea
Belize Visiwa vya Ushelisheli
Botswana Sierra Leone
Brunei Darusalaam Singapura
Canada Visiwa vya Solomoni
Maurishas Afrika ya Kusini
Cyprus Shiri Lanka
Dominica St. Kitts and Nevis
The Gambia St. Lucia
Ghana St. Vincent and the Grenadines
Grenada Swaziland
Pakistan Tanzania
Guiyana Tonga
India Trinidad na Tobago
Jamaika Tuvalu
Kenya Uganda
Kiribati Ufalme wa Uingereza [United Kingdom]
Lesotho Vanuatu
Malawi Samoa ya Magharibi [Western Somoa]
Malaysia Zambia
Maldives Zimbabwe
Malta Rwanda
Msumbiji
39
_________________