Upload
others
View
5
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
NSURANC TH IN HEALT
NHIIF 0 7avang guaity bealtk Cr
ISO 9001:2015 CERTIFIED
MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA
MACHINGA AFYA
Machinga Afya ni nini?
Ni utaratibu wa bima ya afya unaowalenga wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Wamachinga walio katika
umoja unaotambuliwa na mamlaka za Serikali. Utaratibu huu unawawezesha Wamachinga hao kuchangia huduma za
afya kwa um
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuhudumia wanachama wake ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
wao na kunufaika na bima ya afya kupitia mtandao mpana wa vituo zaidi ya 7,700 vilivyosajiliwa na
Wanufaika ni akina nani?
Wanufaika ni Wamachinga walio katika umoja, wenza wao na watoto wasiozidi wanne wa kuzaa au kuasili wenye umri
chini ya miaka 18.
Madhumuni ya Mpango wa Machinga Afya
a) Kutoa fursa kwa Wamachinga kujisajili na kunufaika na huduma za bima ya afya zinazotolewa na Mfuko kupitia
umoja wao.
b) Kulinda kipato cha wanachama kwa kuwapa uhakika wa matibabu kupitia kadi ya bima ya afya.
Jinsi ya Kujisajili na Mambo Muhimu ya Kuzingatia
a) Mwanachama anatakiwa kujaza fomu ya kujiunga ambayo inapatikana katika ofisi zote za Mfuko nchi nzima na
Tovuti ya Mfuko www.nhif.or.tz. Mwanachama anaweza kusajiliwa pía kupitia mtandao baada ya kikundi chake
kuwasilisha taarifa za wanachama wote
b) Usajli utafanyika kwa wanachama wote katika shirikisho/umoja uliosajiliwa na kutambulika na mamlaka za Serikali.
c) Utaratibu wa Machinga Afya utahusisha usajili wa kundi zima na siyo mwanachama mmoja mmoja na fomu za
uanachama, viambatanisho na taarifa zote muhimu za wategemezi zitawasilishwa kwenye Mfuko kupitia Umoja
wao.
d) Mchango wa kila mwanachama ni Shilingi 100,000 kwa mwaka. Aidha, mwanachama atamlipia mwenza Shilingi
100,000 na mtoto Shilingi 50,400 pindi atakapotaka kuwaunganisha. e) Michango ya wanachama wote italipwa kwa mkupuo kupitia kwa shirikisho au umoja husika
Mwanachama anatakiwa kuwa na Kitambulisho cha Taifa au namba ya kitambulisho cha uraia wakati wa usajil.
9) Mwanachama atapata kitambulisho cha matibabu kwa kuzingatia vigezo na masharti ya mpango wa MACHINGA
AFYA
Kwa maelezo zaidi wasiliana na ofisi ya Mfuko iliyo karibu na wewe au wasiliana nasi kupitia
simu ya huduma kwa wateja bila malipo 0800 110063
NSURANCE TH INS NAL FHEAL,
NH Dedicatod lo providing quality veah Caro
ISO 9001:2015 CERTIFIED
MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA HUDUMA ZA MATIBABU KWA MACHINGA AFYA
NA MAFAO UPATIKANAJI Ada ya kujiandikisha na
kumwona daktari 1 Inalipiwa hadi Hospitali za Rufaa za Mikoa
Inapatikana hadi siku 30 kwa mwaka kwa kuzingatia ushauri wa daktaril kwa kila mnufaika.
2 Huduma za kulazwa
Dawa zinazoruhusiwa kutumika kwa mujibu wa Mwongozo wa Matibabu wa Tanzania katika Vituo vya huduma za afya ngazi ya Zahanati na Kituo cha Afya.
3 Huduma za dawa
VIPIMO
X-RAY Inapatikana
ECHO & EEG Inapatikana
Ultrasound Inapatikana
HUDUMA ZA MENO 5
Kung'oa na kuziba Inapatikana
HUDUMA ZA MACHO 6
Matibabu ya macho Inapatikana
HUDUMA ZA UZAZI
Kujifungua kawaida Inapatikana
Kujifungua kwa upasuaji Inapatikana
HUDUMA ZA KIBINGWNA
Huduma za kibingwa Zinapatikana mpaka ngazi ya Hospitali za Mkoa.
HUDUMA ZA UPASUAJI
9 Upasuaji mdogo Inapatikana
Upasuaji mkubwa Inapatikana
Mfuko wa Bima ya Afya, NHIF House, Tambukareli
Barabara ya Jakaya Kikwete. S.L.P 1437, DODOMA, TANZANIA Simu: +255 26 2963887/ +255 26 2963888
HUDUMA KWA WATEJA BILA MALIPO: 0800 110063