Upload
others
View
18
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko ya Jamii
Mwongozo wa Walalamikaji
Kimeidhinishwa na North Mara Gold Mine Limited [TAREHE] kwa kufuata mashauriano ya jamii za nje na ya wataalamu
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
2
MALENGO YA MWONGOZO HUU
Iwapo unaamini kwamba shughuli za Mgodi au taasisi zinazohusiana na Mgodi zimekuwa na athari mbaya au zinaelekea kuleta athari mbaya katika haki za wanajamii wa jamii ya North
Mara, unaweza kuwasilisha Lalamiko katika Mchakato wa Mgodi wa Kushughulikia Malalamiko ya
Jamii ("Mchakato wa Kushughulikia Lalamiko"). Lalamiko lako litafanyiwa kazi na pale panapobidi, lalamiko litajibiwa kwa suluhu kupitia Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko
Mchakato wa kushughulikia Malalamiko ni moja kati ya utaratibu wa Mgodi wa kushauriana na
jamii na ushirikishaji. Husaidia Mgodi kubaini pale ambapo shughuli zake au shughuli za taasisi
zingine zinazohusiana na Mgodi zimesababisha au kuchangia katika kuleta athari mbaya au ziko katika hatari ya kusababisha athari mbaya iwapo hatua hazitachukuliwa. Vilevile husaidia Mgodi
kuzuia, kupunguza au kufanya marekebisho ya athari mbaya.
Utaratibu wa kushughulikia Malalamiko ndio njia pekee zilizopo za kusikilizia malalamiko yanayohusiana na madai ya madhara katika Mgodi na kuzunguka eneo la Mgodi. Ni utaratibu
usio wa kimahakama ambao unaendeshwa na Mgodi na hivyo haujaandaliwa kutatua madai ya
kisheria au kuwa mbadala wake au kuzuia kwenda mahakamani au taratibu nyingine za suluhu. Haukukusudiwa kuwaondolea wengine majukumu yoyote waliyo nayo katika madhara
yaliyojitokeza katika Mgodi na eneo la kuzunguka Mgodi.
Mwongozo huu wa Walalamishi ("Mwongozo") umekusudiwa kuwapa taarifa za msingi watu
ambao wangependa kuwasilisha Malalamiko katika Mgodi kuhusu dhana za msingi wanazopaswa kufahamu kabla ya kuwasilisha lalamiko. Unatoa taswira ya aina ya mambo yanayoshughulikiwa
na Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko ya Mgodi, Jinsi lalamiko linavyoweza kuwasilishwa, mahitaji ambayo yanapaswa kufikiwa na hatua ambazo lazima zichukuliwe.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
3
YALIYOMO
I. UTANGULIZI KATIKA UTARATIBU WA KUSHUGHULIKIA MALALAMIKO................................ 4
LALAMIKO NI NINI? ..................................................................................................................... 4
SULUHU NI NINI? ........................................................................................................................ 4
JISNI GANI ATHARI NA SULUHU ZINAVYOAMULIWA? ................................................................ 4
KUNA HATUA GANI KATIKA MCHAKATO WA LALAMIKO? .......................................................... 6
MCHAKATO WA KUSHUGHULIKIA MALALAMIKO YA JAMII UMEPANGILIWA VIPI? ................... 7
II. MWONGOZO WA KUWASILISHA LALAMIKO ...................................................................... 8
JINSI GANI NINAWEZA KUWASILISHA LALAMIKO? ..................................................................... 8
UTARATIBU WA LALAMIKO NI NINI? .......................................................................................... 9
NI KITU GANI ZAIDI NINAPASWA KUFAHAMU KUHUSU MCHAKATO WA MALALAMIKO? ...... 11
III. HALI MBAYA NA ZA DHARURA ........................................................................................ 14
HATUA ZA TAHADHARI NI NINI? ............................................................................................... 14
MSAADA WA KIBINADAMU NI NINI? ........................................................................................ 15
FOMU YA KUSAJILI MALALAMIKO……………………………………………………………………………17
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
4
I. UTANGULIZI KATIKA UTARATIBU WA KUSHUGHULIKIA MALALAMIKO
A. LALAMIKO NI NINI?
Lalamiko ni wasilisho kuhusu ukiukaji wa haki unaodhaniwa kutendeka unaohusisha athari mbaya
kutokana na shughuli za Mgodi au taasisi zinazohusiana na Mgodi kuhusu haki au maslahi ya mwanajamii mmoja au zaidi au kikundi katika jamii ya North Mara ("Lalamiko"). Athari mbaya ni
hali, kitendo au upungufu ambao unazuia wanajamii kufurahia haki au maslahi yao ("Athari").
Lalamiko linaweza kutatua aina yoyote ya athari mbaya, ikijumuisha athari mbaya katika:
haki za binadamu; mazingira;
matumizi ya ardhi au mali nyingine;
makao na njia za kujipatia riziki; au afya na usalama.
Malalamiko mengi yatatatuliwa na Mgodi kupitia Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko ya Jamii
ulioelezewa katika Mwangozo huu. Malalamiko ambayo yanahitaji uamuzi wa haki au maslahi
kuhusu Mgodi kutwaa ardhi na kufidia hiyo ardhi na maslahi ya mali, au kwa ajili ya makazi mapya, yatapelekwa na kushughulikiwa na Idara ya Ardhi ya Mgodi kwa kusaidiana na utaratibu wowote wa
kiserikali kulingana na kanuni za kisheria na kiutawala za Tanzania.
B. SULUHU NI NINI?
Pale ambapo itakubaliwa au kuamuliwa kupitia Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko ya Jamii
kwamba shughuli za Mgodi au taasisi zinazohusiana na Mgodi zimesababisha au zinaelekea kusababisha athari mbaya, Mlalamikaji ataulizwa awasilishe ombi la suluhu ("Ombi la Suluhu") na
Mgodi unaweza kutoa au kusaidia kutoa Suluhu. Suluhu ni hatua au mkusanyiko wa hatua za
kuzuia athari mbaya au kurudisha, kadri iwezekanavyo, hali iliyokuwepo kabla ya athari mbaya haijatokea ("Suluhu")
Mgodi unaweza kutoa aina tofauti za Suluhu kupitia Mchakato wa Kushughulikia Malamiko ya Jamii.
Katika kila tukio, inakusudia kutoa Suluhu ambazo zinalingana, zimefanyiwa uchunguzi kulingana na tukio husika, zinazoendana na tamaduni na zinazoendana na asili na uwiano wa athari yoyote
mbaya. Suluhu hazitalenga kurekebisha hali iliyokuwepo kabla ya athari, kumtajirisha mpokeaji au
au kuuadhibu Mgodi. Suluhu zitatolewa kwa namna ambayo itajaribu kuhakikisha kwamba zitadumu kwa muda mrefu.
C. JINSI GANI ATHARI NA SULUHU ZINAVYOAMULIWA?
Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko pia unatoa mbinu mbili tofauti za kushughulikia Malalamiko:
Ushirikishaji & Mazungumzo: Kwanza, juhudi zanafanyika kutatua lalamiko kupitia
ushirikishwaji na mazungumzo kati ya Mgodi na mtu mwenye Lalamiko. Afisa Malalamiko
atawezesha mchakato huo. Malalamiko mengi yanaweza kutatuliwa kwa namna hii.
Tathmini Huru: Pili, iwapo hakuna makubaliano yaliyofikiwa kupitia ushirikishaji na
mazungumzo, Kamati huru ya watu watatu ya Malalamiko itashughulikia suala hilo. Mara
nyingi yale malalamiko makubwa au changamano ndiyo huhitaji kutatuliwa kwa njia hii.
Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko umepangiliwa kuwa wa haraka na wenye ufanisi kadri
iwezekanavyo. Hivyo, Malalamiko madogo madogo na rahisi yanaweza kutatuliwa ndani ya siku chache, wakati malalamiko makubwa na changamano yanaweza kuchukua miezi kadhaa. Timu ya
Kushughulikia Malalamiko ya Jamii itaendelea kukupa taarifa kuhusu maendeleo ya Lalamiko lako na kuwasiliana na wewe angalau kila baada ya silku 30.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
5
D. JE, NI ZIPI HATUA ZA UTARATIBUWAKUSHUGHULIKIALALAMIKO?
Kuna ngazi mbili katika Mchakato wa Kushughulikia Lalamiko la Jamii:
Ubainishaji wa Athari: Ngazi ya kwanza inaangalia pale ambapo kazi za Mgodi au taasisi ambazo zinahusiana na Mgodi zimesababisha au zina hatari ya kusababisha athari katika haki
au maslahi ya mwanajamii mmoja au zaidi au makundi ya wanajamii.
o Iwapo utawasilisha Lalamiko, utatakiwa kutoa maelezo ya kina ya tukio au hali na kama kuna ushahidi wowote unaoweza kutoa kuhusu athari inayodaiwa, ukijumuisha
maelezo yoyote kutoka kwa wanajamii wengine.
o Timu ya Mgodi ya Uchunguzi wa Athari na Suluhu itaongoza uchunguzi wa Mgodi kuhusu hali husika. Unaweza kuomba kwamba hii Timu au mtu yeyote unayetaka,
ikijumuisha mashirika ya kijamii au wataalamu wakusaidie katika ukusanyaji wa ushahidi.
o Kisha Afisa wa Kushughulikia Malalamiko atakutana na wewe na mjumbe wa Timu ya
Uchunguzi kujadiliana kuhusu ushahidi na iwapo kumekuwa au kuna hatari ya athari
mbaya inayohusisha Mgodi (Mchakato wa Ushirikishaji & Majadiliano).
o Iwapo hamtafikia makubaliano na Mtafiti wa Mgodi kuhusu iwapo kuna athari kubwa
au kuna hatari ya kuwepo kwa athari kubwa inayohusisha Mgodi, unaweza kuomba
Kamati ya Malalamiko kuamua suala hilo (Utaratibu wa Tathmini).
Ubainishaji wa Suluhu: Iwapo imekubaliwa au kuamuliwa kwamba shughuli za Mgodi
au taasisi zingine zinazohusiana na Mgodi zina au zinaelekea kuwa na athari mbaya, mchakato unasogea kwenda katika hatua ya pili kuangalia jinsi ya kusuluhisha hali husika.
o Iwapo utawasilisha Ombi la Suluhu, utatakiwa kutoa maelezo ya kina kuhusu jinsi
athari ilivyokuathiri au kumuathiri mwanajamii mwigine na kama kuna ushahidi wowote unaoweza kutoa, ikijumuisha maelezo kutoka kwa kila mwanajamii
kuhusiana na suluhu sahihi zinazohitajika.
o Timu ya Mgodi ya Uchunguzi wa Athari na Suluhu itaongoza uchunguzi wa Mgodi
kuhusu Suluhu zinazofaa. Unaweza kuomba kwamba timu au mtu yeyote unayemtaka, ikijumuisha mashirika ya kijamii au wataalamu wakusaidie katika
ukusanyaji wa ushahidi.
o Kisha Afisa wa Kushughulikia Malalamiko atakutana na wewe na mjumbe wa timu ya wachunguzi kujadiliana kuhusu ushahidi na kitu gani kitakuwa ni suluhu kulingana na
ushahidi. (Mchakato wa Ushirikishaji & Majadiliano).
o Iwapo hamuwezi kufikia makubaliano na Mchunguzii wa Mgodi kuhusu Suluhu inayofaa, unaweza kuiomba tena Kamati ya Kushughulikia Malalamiko kuamua suala
hilo (Mchakato Huru wa wa Tathimini)
Ufuatao ni mchoro wa jinsi mchakato unavyofanya kazi. Kila hatua itaelezewa zaidi katika
Mwongozo huu hiki na imefafanuliwa kwa kina katika Mwongozo wa Utaratibu wa Kushughulikia Malalamiko ya Jamii ambao unapatikana katika mtandao.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
6
E. .
Mazungumzo & Ushirikishaji:
Kuwezesha mazungumzo ya kuwepo athari mbaya au hatari ya kutokea athari
Tathmini Huru:
Kamati ya Malalamiko inabainisha iwapo kulikuwa na athari au kuna hatari kutokea athari mabaya
Usajili na uainishaji kulingana na aina ya Lalamiko
(mf. haki za binadamu; mazingira; athari katika matumizi ya ardhi au mali ngingine; nyumba na nja za riziki; kutwaliwa kwa ardhi na makazi mapya)
Taarifa ya Lalamiko
Mazungumzo & Ushirikishaji:
Kuwezesha majadiliano kuhusu athari sahihi, suluhu inayofaa
Tathmini Huru:
Kamati ya Malalamiko inabainisha athari, kiwango na suluhu zinazostahili
Wasilisha Lalamiko Ingiza katika mfumo wa
kielektroniki
Michakato mingine wa Suluhu: Uwezekano wa kwenda kwenye taasisi
yoyote inayohusika katika kuleta athari au
mchakato tofauti wa suluhu.
Iwapo hakuna makubaliano kuhusu athari, chagua
kutafuta tathmini
Appe
Iwapo hakuna makubaliano kuhusu marekenisho, chagua kutafuta tathmini
Makubaliano kuhusu athari
Ubainishaji wa athari mbaya
Ubainishaji wa athari:
Timu ya Uchunguzi wa Athari katika Jamii na Suluhu itaongoza
Ubainishaji wa Suluhu
Timu ya Uchunguzi wa Athari katika Jamii na Suluhu itaongoza
Ngazi za Mchakato wa Kushughulikia
Lalamiko
Ngazi ya 1: Kubainisha iwapo kuna athari
mbaya
Hatua ya 2: Ubainishaji wa Suluhu
Hitimisho: Lalamiko limetatuliwa
Yanapelekwa katika Idara ya
Ardhi ya North Mara
Kushughulikiwa
Kutwaliwa kwa ardhi na utatuzi wa Malalamiko
Malalamiko Mengine yoyote
Appe
Uwezekano wa Rufaa kwa
Mamlaka kwa usambamba: Mshauri wa Kisheria wa Mgodi
Uhalali wa Malalamiko yanayodai matendo
yanaweza kuwa ya uhalifu
Athari za Marekebisho: Suluhisho la Mwisho la Lalamiko au Ripoti
ya Kamati ya Malalamiko na risiti ya Suluhu
kufuatia suluhu zozote .
Mkubaliano kuhusu Marekebisho
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
7
E. MCHAKATO WA KUSHUGHULIKIA MALALAMIKO YA JAMII UMEPANGILIWA VIPI?
1. Timu ya Kushughulikia Malalamko ya Jamii ni nini?
Timu ya Kushughulikia Malalamiko ya Jamii ("Timu ya Malalamiko") inaweza kupatikana katika Ofisi ya Mahusiano ya Jamii. Inaongozwa na Kiongozi wa Timu ya Malalamiko ya Jamii na
inaundwa na Afisa wa Malalamiko wa jamii anayeweza kuongea Kiswahili.
Afisa wa Kushughulikia Malalamiko hupokea na kushughulikia malalamiko yote. Kiongozi wa Timu
ya Kushughulikia Malalamiko anayapanga malalamiko kulingana na aina, kuyaandikisha iwapo yatakuwa na taarifa zote za muhimu na kuushauri Mgodi kuhusu namna ambavyo yanapaswa
kufanyiwa uchunguzi.
Afisa wa Kushughulikia Malalamiko watakusaidia na kuendelea kukuarifu wakati wa Mchakato wa Lalamiko. Pia watawezesha mchakato wa Ushirikishaji & Mazungumzo kati yako na Mgodi. Iwapo
huwezi kutatatua Malalamiko yako kupitia Ushirikishaji na Mazungumzo na Mgodi, Unaweza kuomba Timu ya Kushughulikia Malalamiko kuandaa tathimini au huru ya Lalamiko lako itakayofanywa na
Kamati ya Kushughulikia Malalamiko.
2. Timu ya Uchunguzi wa Athari kwa Jamii na Suluhu ni nini?
Timu ya Uchunguzi wa Athari kwa jamii na Suluhu ("Timu ya Uchunguzi") itachunguza Malalamiko
kwa niaba ya Mgodi na kuwakilisha Mgodi katika Mchakato wa Lalamiko. Inajumuisha wachunguzi
ambao wamepata mafunzo ya kufanya aina tofauti za uchunguzi unaohusiana na masuala ya Mgodi.
Timu ya Uchunguzi itaongoza ukusanyaji wa vifaa vinavyohusika kutoka katika idara ya Mgodi inayoendana na aina ya Lalamiko. Iwapo utaomba msaada, Timu ya Uchunguzi itakusaidia
kukusanya ushahidi kuhusu Lalamiko lako, kama vile nyaraka na taarifa kutoka kwa watu wenye ujuzi kuhusu kilichotokea.
3. Kamati ya Kushughulikia Malalamiko ya Jamii ni nini?
Kamati ya Malalamiko ya Jamii ("Kamati ya Malalamiko") inajumuisha wajumbe huru watatu ambao hawahusiani na Mlalamikaji wala Mgodi. Kila Kamati ya Malalamiko inajumuisha mjumbe
kutoka katika kila orodha tatu za majina (Orodha ya mwenyekiti, Orodha ya Mgodi, na Orodha ya
jamii), ambayo kila moja itajumuisha wote wanawake na wanaume.
Kamati ya Malalamiko huteuliwa na Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko ya Jamii
akizingatia aina ya Lalamiko, utaalamu unaotakiwa na utambulisho wa wale wanaohusika.
4. Baraza la Ushauri kwa Jamii ni nini?
Baraza la Ushauri kwa Jamii ("CCB") inajumuisha watu 22, wanaume 11 na wanawake 11, ambapo watu wawili wanateuliwa na kila kijiji katika vijiji vyote 11 vinavyozunguka Mgodi.
CCB watateua wajumbe wa orodha ya majina ya jamii. CCB inaombwa ushauri na Mgodi kuhusu
Utaratibu wa Malalamiko mara kwa mara.
5. Bodi ya Washauri ni nini?
Bodi ya Washauri inaundwa na watu watano, Watanzania na watu kutoka nje ya Tanzania, wenye
ujuzi unaotambulika katika sekta ya haki za binadamu, usimamizi wa mazingira ua masuala mengine ya kijamii ambao wanatambuliwa na kuchaguliwa na Mgodi.
Bodi ya Washauri inapendekeza wajumbe wa Orodha ya Mwenyekiti na Orodha ya Wataalamu. Bodi
ya Washauri huombwa ushauri na Mgodi kuhusu Utaratibu wa Malalamiko mara kwa mara.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
8
II. MWONGOZO WA KUWASILISHA LALAMIKO
A. JINSI GANI NINAWEZA KUWASILISHA LALAMIKO?
1. Nani anaweza kuwasilisha Lalamiko?
Mtu yeyote au kikundi cha watu au shirika la kijamii linaweza kuwasilisha Lalamiko. Mtu anaweza kuwasilisha Lalamiko kwa niaba yake mwenyewe au kwa kumuwakilisha mtu mwingine.
Walalamikaji ambao sio ambao haki zao zimaathiriwa vibaya lazima wawasilishe ushahidi wa
mamlaka yao ya kuchukua hatua hiyo.
Maafisa wa Kushughulikia Malalamiko kwa ujumla watakuwa wanawasiliana na Mlalamikaji. Hata
hivyo, Maafisa wa Kushughulikia Malalamiko pia wanaweza kuwasiliana na watu wengine ambao nao wameathirika na athari zinazodaiwa au na tathmini au utoaji wa suluhu yoyote kuhakikisha
kuwa maoni yao yanafanyiwa kazi katika mchakato wa Kushughulikia Lalamiko.
2. Ninaweza kuwasilisha Lalamiko wapi?
Unaweza kuwasilisha lalamiko wewe binafsi kwa Afisa Mahusisano ya Jamii wa Mgodi. Vilevile
unaweza kuwasilisha Lalamiko kwa njia zifuatazo:
Afisa wa Malalamiko wa Mgodi au Timu ya Ushirikishaji wa Jamii wakati wa mashauriano na jamii.
Barua Pepe: [email protected]
Barua: Mgodi wa North Mara, S.L.P 422, Tarime
Afisa Mshirikishi wa Kijiji kwa Ofisi ya Kijiji katika:
o Kijiji cha Kerende
o Kijiji cha Kewanja o Kijiji cha Nyakunguru
o Kijiji cha Matongo o Kijiji cha Mjini kati
o Kijiji cha Nyabichune
o Kijiji cha Nyangoto o Kijiji cha Komalela
o Kijiji cha Nyamwaga o Kijiji cha Genkuku
o Kijiji cha Msege
3. Kitu gani kinapaswa kujumuishwa katika Lalamiko?
Unaweza kutumia Fomu ya Kupokelea Malalamiko iliyoko mwishoni mwa Mwongozo huu. Unaweza kuambatanisha kurasa za nyongeza na nakala za nyaraka za ushahidi. Kila Lalamiko linapaswa
kujumuisha taarifa zifuatazo:
jina na taarifa za mawasiliano ya (wa)mtu ambaye haki zake au maslahi yake yanadaiwa
kuathiriwa vibaya na wategemezi ambao wanaaminika kuwa wameathiriwa na athari au madharamabaya;
iwapo tofauti, jina na taarifa za mawasiliano ya (Wa)Mlalamikaji (pamoja na, iwapo itapatikana, barua pepe na sanduku la barua kwa ajili ya kupokelea mawasiliano) na
ushahidi wa mamlaka ya kuchukua hatua; maelezo taarifa na asili ya Lalamiko, yakibainisha mahali, tarehe na muda wa tukio
linalodaiwa kusababisha athari;
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
9
kutambua taasisi zote na\au watu binafsi ambao anadhaniwa na mlalamikaji kusababisha,
kwa kutenda au kutotenda, athari zinazodhaniwa, na taarifa za kwa nini Mlalamikaji anadhani kuwa Mgodi unahusika;
Kubainisha maslahi au haki zinazoathiriwa na suala linalolalamikiwa katika Lalamiko; Ushahidi wa kuambatanisha (Iwapo utakuwepo), ikijumuisha nakala za nyaraka zozote
kutoka kwa daktari na maelezo ya mashahidi (au maombi ya msaada wa kupata vitu hivyo);
hata kama Lalamiko linahusiana na Lalamiko lililopita, Ombi la Hatua za Tahadhari au Ombi Msaada wa Kibinadamu;
hatua zilizochukuliwa (kama zipo) kulalamikia suala la Lalamiko kupitia utaratibu mwingine (kwa mfano, Polisi, taasisi nyingine za kiserikali, Mahakama) na hali ya mchakato huo
ikijumuisha jina la mamlaka ya umma ambayo inashughulikia suala husika la Lalamiko; Hatua zilizochukiliwa (kama zipo) kupata Suluhu kutoka kwa taasisi nyingine mbali na Mgodi
na/au taarifa na maelezo kuhusu kushindwa kufanya hivyo; na
iwapo Mlalamishi au mtu/watu walioathirika wanaomba utambulisho wao usiwekwe bayana katika Mgodi, Polisi au taasisi nyingine zozote na hali maalum ambazo zinahalalisha ombi
hilo.
Ni muhimu kuipa taarifa Timu ya Kushughulikia Malalamiko kuhusu mabadiliko yoyote ya taarifa za
mawasiliano zilizoko katika Lalamiko.
4. Jinsi gani nitapata msaada wa kujaza Lalamiko au kukusanya ushahidi?
Unaweza kuwasilisha Lalamiko lako wewe binafsi au kusaidiwa na mtu yeyote unayetaka, akiwemo
mwanasheria au mashirika za kijamii.
Afisa wa Kushughulikia Malalamiko anaweza kukusaidia kujaza fomu ya kuwasilisha Lalamiko.
Iwapo utawapa idhini ya kukusaida, Timu ya Uchunguzi inaweza kukusaidia kupata nyaraka na maelezo ya mashahidi kuunga mkono utokeaji wa athari na kubainisha suluhu zinazofaa.
Unaweza kuomba vocha kutoka kwa Afisi ya Kushughulikia Malalamiko kwa ajili ya kupata saa nne
za msaada na ushauri wa kisheria kutoka kwa mwanasheria unayemtaka mwenye ujuzi na aliyesajiliwa kisheria kwa gharama za Mgodi ikiwa utatahitaji msaada wa mwanasheria.
B. UTARATIBU WA LALAMIKO NI UPI?
1. Nitakuwa na uhakika gani kuwa Timu ya Malalamiko imepokea Lalamiko langu?
Afisa wa Kushughulikia Malalamiko atatuma taarifa ya Lalamiko kwa maandishi ndani ya siku saba
tangu Timu ya Malalamiko ilipopokea na kusajili Lalamiko (Tafadhali kumbuka kwamba Lalamiko lililopokelewa nje ya Mgodi linaweza kuchukua muda mrefu kidogo kufika kwenye Timu ya
Malalamiko). Taarifa ya Lalamiko itathibitisha kupokewa kwa Lalamiko na kuonyesha namba ya kumbukumbu ya Lalamiko. Taarifa ya Lalamiko itatumwa katika anuani iliyotolewa na Mlalamikaji
katika Lalamiko.
2. Nini kinafuata baada ya Timu ya Malalamiko ya Jamii kukiri kupokea Lalamiko?
Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko atatenga Malalamiko katika makundi kulingana na
aina, atasajili malalamiko iwapo yatakuwa na taarifa zote muhimu zilizotajwa hapo juu na
ataushauri Mgodi kuhusu jinsi Malalamiko yanavyoweza kufanyiwa Uchunguzi. Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko atamuandikia Mlalamikaji ndani ya siku 14 baada ya kutuma taarifa ya
Lalamiko kwa ajili ya:
kumuarifu Mlalamikaji kuwa Lalamiko tayari limeshasajiliwa kwa ajili ya kushughulikia, na
kuonyesha kwa awali aina ya Lalamiko; kuomba taarifa za nyongeza au nyaraka zinazohitajika kutoka kwa Mlalamikaji; au
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
10
kumtaarifu Mlalamikaji kuwa Lalamiko haliwezi kushughulikiwa kwa sababu suala
linalolalamikiwa tayari liko katika mchakato mwingine wa suluhu au tayari lilishawahi kulalamikiwa na hivyo hakuna hali ambazo zinalazimu kulishughulikia upya.
3. Nini kinatokea baada ya lalamiko kusajiliwa?
Timu ya Kushughulikia Malalamiko itamuomba Mlalamikaji na Timu ya Uchunguzi kutoa maelezo yoyote ya ziada au ushahidi wa kuunga mkono Lalamiko ndani ya muda maalumu. Mlalamikaji
atakuwa na uwezekano zaidi wa kuthibitisha Malalamiko yake iwapo atatoa:
Maelezo ya kina kuhusu athari inayodaiwa;
maelezo ya kina kutoka kwa mashahidi; na nakala za nyaraka zozote za ushahidi.
Timu ya uchunguzi pia itatoa ugunduzi au ushahidi wowote na Ropoti ya Uchunguzi kulingana na Lalamiko. Iwapo itaidhinishwa na Mlalamikaji, Timu ya Uchunguzi ya Mgodi inaweza kumsaidia
Mlalamikaji kukusanya nyaraka za kuambatanisha au maelezo ya mashahidi. Mlalamikaji anaweza kuwasilisha taarifa za kitaalamu, kwa gharama za Mgodi iwapo mtaalamu atakuwa amechaguliwa
kutoka katika Orodha ya Wataalamu ya Mchakato wa Malalamiko.
Baada ya kubadilishana ugunduzi na ushahidi kati ya Timu ya Uchunguzi na Mlalamikaji, Timu ya
Kushughulikia Malalamiko itamwalika Mjumbe wa Timu ya Uchunguzi pamoja na Mlalamikaji katika kikao cha Ushirikishaji na Mazungumzo kujadilana kuhusu Lalamiko. Timu ya Kushughulikia
Malalamiko itawapatia wajumbe wa pande zote mwongozo wowote utakaofaa wa marejeo ya athari zinazohusiana na Mgodi.
4. Kikao cha Ushirikishaji & Mazungumzo ni nini?
Wakati wa kikao cha Ushirikishaji & Mazungumzo, Afisa wa Kushughulikia Malalamiko anapania kusuluhisha Lalamiko kupitia kwa Mchunguzi wa Mgodi na Mlalamikaji. Lengo la mazungumzo
katika hatua ya kwanza ni kufikia maelewano ya pamoja kuonyesha iwapo kumetokea athari mbaya
inayohusisha Mgodi au kutakuwa na athari kubwa iwapo hatua hazitachukuliwa. Iwapo hakuna maelewano ya pamoja yaliyofikiwa baada ya vikao kadhaa, Mlalamikaji anaweza kuiomba Timu ya
Kushughulikia Malalamiko kupeleka suala hilo katika Kamati ya Malalamiko.
5. Kikao cha Tathmini Huru ya Malalamiko ni nini?
Jopo la Kamati ya Malalamiko litamsikiliza Mlalamikaji na Mgodi na kuzishughulikia taarifa
zilizotolewa zinazohusiana na Lalamiko wakati wa kikao huru cha kusikiliza Malalamiko. Lengo la Kikao ni kusaidia Kamati ya Malalamiko kuamua iwapo kumetokea athari mbaya inayohusisha
Mgodi au kunaweza kuwa na athari mbaya iwapo hakuna hatua zitakazochukuliwa. Kamati ya
Kushughulikia itajadiliana baada ya Kikao cha Kusikiliza Malalamiko na kufikia uamuzi.
6. Nini kinatokea baada ya Kikao cha Ushirikishaji na Mazungumzo au Kikao cha
Kusikiliza Tathmini Huru ya Malalamiko?
Baada ya pande zote kukubaliana au Kamati ya Malalamiko kuamua kwamba Mgodi umehusika katika kuleta athari mbaya, Mlalamikaji atapatiwa Fomu ya Maombi ya Marekebisho. Mlalamikaji
atakuwa na uwezekano zaidi wa kuthibitisha ombi lake la Marekebisho iwapo atatoa:
maelezo ya kina kuhusu hali halisi na mazingira ya wanajamii ambao wameathirika kutokana na athari kabla na baada ya athari;
maelezo ya kina kuhusu hatua ambazo zinaweza kuchukuliwa kwa ajili ya kurejesha, kadri
iwezekanavyo, maslahi na haki za wale walioathirika; na
nakala za nyaraka zozote muhimu za ushahidi.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
11
Timu ya Uchunguzi pia itatoa ugunduzi wowote au ushahidi na Ropiti ya Uchunguzi kulingana na Suluhu
zinazohusika. Iwapo itaidhinishwa na Mlalamikaji, Timu ya Uchunguzi ya Mgodi inaweza kumsaidia Mlalamikaji kukusanya nyaraka za kuambatanisha au maelezo ya mashahidi. Mlalamikaji anaweza
kuwasilisha ripoti za kitaalamu, kwa gharama za Mgodi iwapo mtaalamu atakuwa amechaguliwa kutoka katika Orodha ya Wataalamu ya Mchakato wa Malalamiko.
Baada ya kubadilishana ugunduzi na ushahidi kati ya Timu ya Uchunguzi na Mlalamikaji, Timu ya
Malalamiko itamwalika Mjumbe wa Timu ya Uchunguzi pamoja na Mlalamikaji katika kikao cha Ushirikishaji na Mazungumzo kujadiliana kuhusu Marekebisho. Timu ya Kushughulikia Malalamiko
itawapatia wajumbe wa pande zote mwongozo wowote utakaofaa wa marejeo ya Suluhu za athari
zinazohusiana na Mgodi.
7. Jinsi gani Suluhu zinavyobainishwa?
Wakati wa kikao cha Ushirikishaji & Mazungumzo Mgodi na Mlalamikaji watajaribu kufikia maelewano ya
pamoja kuhusu Marekebisho yanayofaa. Iwapo hakuna maelewano ya pamoja yaliyofikiwa baada ya vikao kadhaa, Mlalamikaji anaweza kuiomba Timu ya Malalamiko kupeleka suala hilo katika Kamati ya
Kushughulikia Malalamiko.
8. Ripoti ya Suluhisho la Lalamiko au Ripoti ya Kamati ya Kushughulikia Malalamiko ni nini?
Ripoti ya mwisho ya Suluhisho la Lalamiko au Taarifa ya Kamati ya Kushughulikia Malalamiko huweka kumbukumbu ya makubaliano na/au uamuzi iwapo Mgodi ulihusika katika kuleta athari mbaya na kutaja
aina yoyote ya Suluhu ambazo Mgodi umekubali kutoa au ambazo Kamati ya Kushughulikia Malalamiko imependekeza zitolewe. Ripoti ya mwisho itatolewa kwa Mlalamikaji ndani ya miezi mitatu baada ya
kikao cha mwisho au kikao cha Kusikiliza Malalamiko na mara nyingi huwa mapema zaidi.
9. Jinsi gani Marekebisho yanavyotolewa?
Wapokeaji watarajiwa wa Suluhu wataulizwa kwa siri wakati wa Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko
kujua jinsi gani Suluhu zinapaswa kuwasilishwa kuhakikisha usalama wa wapokeaji pamoja na ufanisi na kudumu kwa suluhu. Suluhu hutolewa kwa bidhaa/vitu au kupitia malipo ya moja kwa moja ya ada kwa
watoa huduma, taasisi au vituo vya matibabu pale inapowezekana. Suluhu hutolewa moja kwa moja na
kwa siri kwa mpokeaji, ambaye baada ya hapo huombwa kutia sahihi katika risiti ya Suluhu.
C. NI KITU GANI ZAIDI NINAPASWA KUFAHAMU KUHUSU MCHAKATO WA LALAMIKO?
1. Je, kuna kikomo katika muda wa kuwasilisha Lalamiko?
Hakuna kikomo katika muda wa kuwasilisha Lalamiko. Hata hivyo, kupita kwa muda mrefu kunaweza
kuathiri uwezo wa Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko kubainisha iwapo kumetokea athari na kuhusu suluhu inayofaa.
2. Je, Mchahato wa Kushughulikia Lalamiko ni wa siri?
Mashitaka yote pamoja na ushahidi wote unaobadilishana kati yako na Mgodi wakati wa Mchakato wa Kushughulikia Lalamiko utakuwa wa siri isipokuwa kwa makubaliano ya pende zote au, katika ushahidi,
pale ambapo unaendana na shitaka jingine linalohusiana na kiini la Lalamiko.
3. Jinsi gani Mchakato wa Kushughulikia Lalamiko unavyoshughulikia uhalifu au taasisi
nyingine zinahusiana na Mgodi?
Mgodi unaweza kushindwa kufanya uchunguzi wa kina au kutoa suluhu kamilifu kivyake pale
ambapo uhalifu, wahusika wa serikali au taasisi nyingine zinapokuwa zinahusika katika athari zinazodaiwa. Katika hali kama hizo, Mgodi unaweza kuhitaji kupeleka madai ya halali kwa mamlaka
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
12
husika za Tanzania au kwa taasisi zinazohusika kwaajili ya uchunguzi au kufanya marekebisho kwa
ruhusa ya Mlalamikaji au pale inapotakiwa kisheria.
Katika mazingira maalumu na kulingana na sheria mwafaka, Mgodi unaweza kuzuia utambulisho wa
mwanajamii (ikijumuisha Mlalamikaji, watu waliopata athari au mashahidi) usitolewe kwa mamlaka au taasisi nyingine patakapokuwa na ombi. Hii itaathiri uwezo wa Mchakato wa Kushughulikia
Malalamiko kubaini iwapo athari mbaya imetokea au kutambua Suluhu inayofaa.
4. Je, Malalamiko nyeti au changamani huchukuliwa kwa makini?
Wakati ambapo Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko anapopangilia malalamiko kwa aina,
kuyasajili na kuushauri Mgodi kuhusu jinsi yanavyopaswa kufanyiwa uchunguzi, atabainisha masuala
nyeti, wahusika walio hatarini au masuala changamani ili yaweze kushughulikiwa kwa makini.
Masuala ambayo ni nyeti kwa wanawake yatashughulikiwa ipasavyo. Umakinifu utazingatiwa
kuepusha ufichuaji wa utambulisho wa wanawake na aina ya malalamiko yao, na kutoa suluhu kwa namna ambayo inawahatarisha. Mchakato wa Kushughulikia Lalamiko unawezwa kujumuisha
wataalamu katika masuala nyeti au changamani.
5. Ni kiasi gani cha ushahidi ninapaswa kutoa katika Mchakato wa Kushughulikia Lalamiko?
Kiwango cha uthibitisho kinachotumika katika Utaratibu wa Lalamiko sio mgumu kama ilivyo katika
utaratibu wa mahakama, kwani Utaratibu wa Malalamiko hauamui haki za kisheria au uwajibikaji. Pale ambapo Mgodi unatambua kuwa ushahidi unaweza kuwa mgumu kupatikana katika baadhi ya
Malalamiko, unaegemea kukosea katika tahadhari. Hata hivyo, Mchakato wa Kushughulikia Lalamiko utajaribu kutenganisha madai halali kutoka katika madai ya uongo kupitia kwa uchunguzi
wa ushahidi uliopo na tathmini ya uhalali wa Mlalamikaji.
6. Je, nitatakiwa kutia sahihi hati ya kisheria au kuachana na haki zangu zozote?
Hautatakiwa kutia sahihi hati zozote za kisheria kwa ajili ya kupokea suluhu katika Mchakato wa
Kushughulikia Malalamiko. Mgodi utatekeleza suluhu zilizoelezewa katika Ripoti ya Utatuzi wa
Lalamiko au katika Ripoti ya Kamati ya Malalamiko. Risiti ya Suluhu inayoeleza kuwa Suluhu zimepokelewa inaweza kutumiwa na Mgodi iwapo Lalamiko lingine litaletwa dhidi ya Mgodi kwa
hoja zinazofanana kupitia mchakato mwingine.
7. Nini kitatokea iwapo, baada ya kuwasilisha Lalamiko langu, sitajishirikisha
katika Mchakato wa Lalamiko kwa muda mrefu?
Lengo la Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko ni kusuluhisha malalamiko kwa haraka na kwa ufanisi na kwa kupitia ushirikishaji na mazungumzo. Iwapo, baada ya kuwasilisha Lalamiko,
hutaonyesha ushirikiano kwa Timu ya Malalamiko pasipo maelezo kwa zaidi ya miezi mitatu, Timu
ya Malalamiko inaweza kuamua kuhifadhi Lalamiko lako. Kwa mfano, Lalamiko lako litahifadhiwa iwapo, licha ya kukumbushwa kwa miezi kadhaa, hutaitikia ndani ya miezi mitatu baada ya Timu ya
Malalamiko kukuuliza iwapo ungependa Lalamiko lako lipitiwe na Kamati ya Malalamiko.
8. Nini kitatokea iwapo Mgodi hautatoa suluhu au nitaona kuwa suluhu
zilizotolewa na Mgodi hazitoshi?
Iwapo unaamini kuwa Mgodi hautoi suluhu zilizoainishwa katika Ripoti ya Suluhisho la Lalamiko au
Ripoti ya Kamati ya Malalamiko au Suluhu zilizotolewa hazitoshi, unaweza kuwasilisha ombi la tathmini. Kiongozi wa Timu ya Malalamiko atapeleka Ombi la kufanyika kwa tathmini ya Suluhu
zilizokubaliwa tayari au zilizoamuliwa katika Kamati ya Malalamiko kwa ajili ya kuangaliwa upya pale tu utakapokuwa umewasilisha taarifa ambayo ilipaswa kushughulikiwa wakati suluhu ilipokuwa
inapitishwa. Kamati ya Kushughulikia Malalamiko inaweza kukagua suluhu pale tu itakapoonyesha
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
13
kuwa haitoshi au haiendani na athari au hatari iliyopatikana wakati suluhu ilipokuwa iinakubaliwa au
kuamuliwa.
9. Ni katika hali zipi ambapo Mgodi hautaweza kunisaidia kupitia Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko ya Jamii?
Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko ya Jamii hauwezi kufanya na hatafanya haya:
Kufanya maamuzi yoyote ya kisheria ya hoja au sheria;
Kuamua iwapo Mgodi, au vyombo vingine vyovyote au mtu yeyote anawajibika kisheria au anawajibika kihalifu katika athari mbaya;
Kutoa maelekezo yoyote kwa polisi kuhusiana na kesi za jinai dhidi ya chombo chochote au mtu binafsi; au
kufanyia kazi Lalamiko lolote wakati suala hilo bado linaendelea dhidi ya Mgodi katika mchakato mwingine wa marekebisho kama vile taratibu za mahakama za kiraia.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
14
III. HALI MBAYA NA ZA DHARURA
A. HATUA ZA TAHADHARI NI NINI?
Katika hali mbaya na za dharura ambapo haki zitakuwa zimeathiriwa au zinaweza kuathiriwa iwapo hatua hazitachukuliwa, Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko anaweza kupendekeza
kwamba Mgodi uchukue Hatua za Tahadhari. Hatua za Tahadhari zipo kwa ajili ya hali ambazo
haziwezi kusubiri mpaka matokeo ya Mchakato wa Lalamiko utakapokamilika ili kuweza kuzuia au kurekebisha.
1. Ni katika hali gani ambapo Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko ataweza kupendekeza Mgodi uchukue hatua za tahadhari?
Mwongozo wa Utaratibu wa kushughulikia Malalamiko ya jamii unaeleza kwamba:
Ibara ya 60: Hatua za Tahadhari
1. Kiongozi wa Timu ya Malalamiko kwa juhudi zake mwenyewe au kwa maombi ya Mlalamikaji au mtu mwingine, anaweza kupendekeza kuwa Mgodi uchukue Hatua za Tahadhari haraka
kufuatana na mbaya au hali ya dharura ambayo inaonekana kuhusisha Mgodi na ambayo, iwapo haitakabiliwa, ina hatari ya kusababisha athari zisizoweza kurekebishika katika haki au
maslahi ya wanajamii.
2. Hatua za Tahadhari zitachukuliwa kwa ajili ya kukabiliana na hali ambazo, kwa asili yake,
haziwezi kusubiri mpaka Mchakato wa Malalamiko utakapokamilika ili kuzuiliwa au kufanyiwa marekebisho.
3. Hatua za Tahadhari zinaweza kuhusisha, kwa mfano, utoaji wa matibabu au msaada
mwingine wa dharura unaohitajika kwa mtu ambaye amewasilisha Lalamiko ambalo bado halijaamuliwa au Mgodi umesimamisha shughuli fulani au kumuomba mkandarasi au taasisi
zingine kusimamisha shughuli fulani. Hatua za Tahadhari mara nyingi huwa hazihusishi
msaada wa kifedha.
Ibara ya 61: Maombi ya kuchukuliwa kwa Hatua za Tahadhari
1. Maombi ya kuchukuliwa kwa Hatua za tahadhari yatajumuisha:
a. kubainisha taarifa za mtu yoyote aliyeathirika;
b. maelezo ya kina ya kihistoria ya hoja zinazochochea ombi na taarifa nyingine zozote zilizopo; na
c. maelezo ya Hatua za Tahadhari zinazoombwa.
2. Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko atamshauri mwombaji wa Hatua za Tahadhari kuhusu uamuzi wa Mgodi ndani ya saa 48 tangu kupokelewa kwa ombi.
3. Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko atatoa majibu kwa maandishi kwa mwombaji
wa Hatua za Tahadhari akielezea uamuzi wa Mgodi na sababu, watakaonufaika, aina ya Hatua za Tahadhari zilizotolewa, na kubainisha iwapo kuna Lalamiko lililobaki.
4. Mwombaji wa Hatua za Tahadhari aliyefanikiwa atakubali rasmi kupokea majibu ya Mgodi kwa
maandishi na Hutua husika za Tahadhari. Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko atafuatilia haraka na ufanisi wa Mgodi katika kuwasilishwa Hatua zozote za Tahadhari.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
15
2. Ninaweza kuwasilisha ombi la kupata Hatua za Tahadhari pasipo kuwasilisha au
kuwa nimewasilisha Lalamiko?
Ndiyo. Hata hivyo, hali ambayo imeelezewa katika ombi lazima ipendekeze kwamba haki zinaathiriwa au zinaweza kuathiriwa iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa.
3. Je maamuzi kuhusu Hatua za Tahadhari yanaathiri matokeo ya Lalamiko?
Hapana. Kwa kuwa ni taratibu mbili zinazotofautiana, hata kama Mgodi utaamua kuchukua Hatua za
Tahadhari, Lalamiko litaendelea na utaratibu wake mpaka litakapotatuliwa kupitia Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko.
B. MSAADA WA KIBINADAMU NI NINI?
1. Msaada wa Kibinadamu ni nini?
Katika hali mbaya na za dharura, Kiongozi wa Timu ya Malalamiko anaweza kupendekeza kwamba Mgodi utoe Msaada wa Kibinadamu kwa wanajamii walioumia katika maeneo ya Mgodi au kuhusiana
na shughuli za Mgodi. Misaada ya Kibinadamu ni kwa ajili ya hali ambayo Lalamiko linalohusika limekataliwa, au hakuna Lalamiko litakalotolewa au kukubaliwa, na kwa hiyo hakutakuwa na
Suluhisho chini ya Mchakato wa Kushughulikia Lalamiko.
2. Ni katika hali gani ambapo Kiongozi wa Timu ya Malalamiko anaweza kupendekeza Mgodi kutoa Msaada wa Kibinadamu?
Mwongozo wa Utaratibu wa Uendeshaji wa Malalamiko ya jamii unaeleza kwamba:
Ibara ya 62: Msaada wa kibinadamu
1. Kiongozi wa Timu ya Malalamiko kwa juhudi zake mwenyewe au kwa ombi la Mlalamikaji
au mtu mwingine, anaweza kupendekeza kuwa Mgodi utoe Msaada wa Kibinadamu kulingana na hali mbaya na ya dharura ya matibabu ambayo inaonekana kuhusisha
majeraha yaliyopatikana katika Eneo la Mgodi.
2. Msaada wa Kibinadamu utatolewa pale tu ambapo Hatua za Tahadhari au Suluhu kupitia
Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko hazitoshi (Mf, Iwapo Lalamiko limeshawasilishwa lakini limekataliwa au pale ambapo hakuna Lalamiko lililowasilishwa au litakalowasilishwa).
Zitafikiriwa tu pale ambapo ni lazima kusitisha, kuzuia au kutibu majeraha yanayotishia
maisha au majeraha yanayoweza kubadilisha maisha na athari zake za awali.
3. Msaada wa Kibinadamu unaweza kujumuisha, kwa mfano, utoaji wa huduma za matibabu ya muda mfupi, vitu au msaada mwingine unaohitajika kwa haraka kwa mtu ambaye
ameumia katika ajali wakati akiwa anapita bila ruhusa katika eneo la Mgodi. Msaada wa Kibinadamu mara nyingi huwa hauhusishi msaada wa kifedha.
Ibara ya 63: Maombi ya Msaada wa Kibinadamu
1. Ombi la msaada wa Kibinadamu litakuwa na:
a. taarifa za utambuzi wa mwombaji yeyote au mtegemezi;
b. maelezo ya kina ya kihistoria ya hoja zinazochochea ombi na habari nyingine zozote zilizopo; na
c. maelezo ya msaada wa kibinadamu unaoombwa.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
16
3. Ninaweza kuwasilisha ombi la Msaada wa Kibinadamu pasipo kuwasilisha au kuwa nimewasilisha Lalamiko?
Ndiyo.
4. Ninaweza kuwasilisha ombi la Msaada wa Kibinadamu baada ya kutokufanikiwa kuwasilisha Lalamiko?
Ndiyo. Iwapo hukufanikiwa kupitia Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko ya Jamii, unaweza
kuomba Msaada wa Kibinadamu kupitia Ofisi ya Kushughulikia Malalamiko.
2. Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko atamshauri mwombaji wa Msaada wa Kibinadamu kuhusu uamuzi wa Mgodi ndani ya saa 48 tangu kupokelewa kwa ombi.
3. Kiongozi wa Timu ya Malalamiko atatoa majibu kwa maandishi kwa mwombaji wa Msaada
wa Kibinadamu akielezea uamuzi wa Mgodi na sababu, watakaonufaika, aina ya Msaada
wa Kibinadamu uliotolewa, na kubainisha iwapo pia kuna Lalamiko lililobaki au lililokwisha hitimishwa.
4. Mwombaji wa Msaada wa Kibinadamu aliyefanikiwa atakubali rasmi kupokea majibu ya
Mgodi kwa maandishi na Msaada husika wa Kibinadamu. Kiongozi wa Timu ya
Kushughulikia Malalamiko atafuatilia uharaka na ufanisi wa Mgodi katika kuwasilishwa Msaada wowote wa Kibinadamu.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
17
Utaratibu wa Kushughulikia Malalamiko ya Jamii
Form ya Kupokea Malalamiko
Fomu hii inaendana na taarifa ambazo zinahitajika na Mwongozo wa Mchakato uliokubalika wa kushughulikia Malalamiko ya Jamii wa Mgodi wa North Mara kwa ajili ya kushughulikia
Malalamiko. Malalamiko yanaweza kuwasilishwa kwa kutuma fomu hii (kuongeza mistari na kurasa kadri unavyohitaji) kwa njia zozote kati ya hizi zifuatazo:
Kuwasilisha wewe binafsi (kwa njia maandishi au kwa mdomo):
kwa Maafisa Malalamiko wa Jamii katika Ofisi ya Mgodi ya Mahusiano ya Jamii au kwa wajumbe wa Timu ya Ushirikishaji wa Jamii wakati wa washauriano na jamii; au
kwa Maafisa Washirikishi wa Vijiji katika Ofisi za Vijiji katika vijiji vifuatavyo:
o Kijiji cha Kerende o Kijiji cha Kewanja
o Kijiji cha Nyakunguru o Kijiji cha Matongo
o Kijiji cha Mjini kati
o Kijiji cha Nyabichune o Kijiji cha Nyangoto
o Kijiji cha Komalela o Kijiji cha Nyamwaga
o Kijiji cha Genkuku
o Kijiji cha Msege
Barua: Mgodi wa North Mara, S.L.P 422, Tarime
Barua pepe: [email protected]
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
18
SEHEMU A: TAARIFA KUHUSU MLALAMIKAJI NA/AU WANAJAMII AMBAO MASLAHI YAO
AU HAKI ZAO ZIMEATHIRIWA AU ZINAWEZA KUATHIRIWA VIBAYA
1. Taarifa kuhusu mwanajamii (wanajamii) wa jamii ya North Mara aliyeathirika
Tafadhali toa taarifa kuhusu mwanajamii (wanajamii) ambaye haki zake zimeathiriwa au zitaathiriwa vibaya.
Jina (majina) la mwanajamii (mwanajamii):
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Jinsia ya mwanajamii: K M
Tarehe ya kuzaliwa ya mwanajamii: (Siku/Mwezi/Mwaka)
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Anuani ya Posta ya mwanajamii (wanajamii) (ikijumuisha taarifa zote zilizopo):
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Namba za simu za mwanajami (wanajamii)i:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Anuani za Barua pepe za mwanajamii (wanajamii):
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Je, mwanajamii (wanajamii) amenyimwa uhuru?
Ndio
Hapana
Taarifa za ziada:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
19
2. Taarifa kuhusu wanafamilia?
Tafadhali toa taarifa kuhusu wanafamilia wa karibu wa mwanajamii (wanajamii) ambaye ameathirika kutokana na athari zinazidaiwa.
Majina ya wanafamilia na uhusiano:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… Jinsia ya mwanajamii (wanajamii) K M
Tarehe yakuzaliwa ya mwanajamii (wanajamii): (Siku/Mwezi/Mwaka)
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Anuani za Posta za wanafamila (ikijumuisha maelezo yote yaliyopo)
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… Namba za simu za wanafamilia:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Anuani za Barua pepe za wanafamilia:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Taarifa za nyongeza kuhusu wanafamilia:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
3. Taarifa kuhusu Mlalamikaji
Tafadhali toa taarifa kuhusu mtu, kikundi cha watu au shirika la kijamii ambalo limewasilisha lalamiko.
Ni muhimu kutoa taarifa katika Ofisi ya Kushughulikia Malalamiko haraka kuhusu
mabadiliko yoyote ya anuani ya posta.
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
20
Jina la Mlalamikaji (ikijumuisha jina la mwakilishi wake wa kisheria, kama yupo ambaye atapokea
mawasiliano. Iwapo ni zaidi ya taasisi au mtu mmoja, jumuisha taarifa za nyongeza katika nafasi iliyotolewa):
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Kifupisho cha jina la taasisi (kama kinahitajika):
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Anuani ya Posta ya Mlalamikaji (ikijumuisha maelezo yote yaliyopo)
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
(KUMBUKA: Afisi ya Kushughulikia Malalamiko inahitaji anuani ya posta kutuma ujumbe
unaohusiana na Lalamiko lako)
Namba ya simu ya Mlalamikaji:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Barua pepe ya Mlalamikaji:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Taarifa za nyongeza kuhusu Mlalamikaji: …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
4. Je, Lalamiko lako linaibua usiri fulani au wasiwasi mwingine?
Je, mtu ambaye ndiye anahusika na Lalamiko anahitaji kuweka utambulisho wake kuwa siri kwa
polisi? Ndio
Hapana
Je, mtu ambaye ndiye anahusika na Lalamiko anahitaji kuweka utambulisho wake kuwa siri kwa
wengine, ikiwemo familia au wanajamii? Ndio
Hapana
Je, mtu ambaye ndiye anahusika na Lalamiko anachukuliwa kama mtu aliye hatarini (mf. ana sababu
za msingi za kuogopa kutishiwa au kudhuriwa, mtoto, mwanamke mwenye hofu ya kulipiziwa kisasi,
mlemavu au mengineyo)? Ndio
Hapana
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
21
Iwapo jibu ni ndio katika swali lolote hapo juu, onyesha sababu husika:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
SEHEMU B: UKWELI WA MADAI
1. Lalamiko linahusu nini?
Tafadhali weka tiki katika yote yanayohusika.
Haki za binadamu
Manunuzi ya ardhi au mali
Uharibifu wa mali
Uharibifu wa mazingira, kama vile hewa au uchafuzi wa maji
Afya na Usalama
Magari au usafirishaji
Usalama wa Mgodi
Polisi
Mtu binafsi kuumia
Vifo
Fidia ya ardhi
Makazi mapya
Mengine
Iwapo kuna mengine, Elezea kwa kifupi:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
2. Tukio lilitokea wapi au hali hiyo ilitokea wapi?
Tafadhali weka tiki.
Katika Eneo la Mgodi
Karibu na Eneo la Mgodi
Kungineko / huna uhakika
Tafadhali Bainisha:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
22
3. Maelezo ya tukio au hali
Toa maelezo ya tukio au hali kwa utaratibu na hatua kwa hatua kwa uwazi kadri iwezekanavyo. Hasa
bainisha mahali, muda, tarehe na hali ambayo athari inayodaiwa ilitokea, inaweza kutokea au inatokea. (Ongeza kurasa zaidi iwapo zitahitajika au ambatanisha hati tofauti ambayo
umeelezea hoja za madai)
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
4. Watu au taasisi zinazodaiwa kuwajibika
Bainisha mtu au taasisi ambazo unadhani zinawajibika katika hoja ya madai na toa taarifa za ziada za
kwa nini unadhani Mgodi unapaswa kuwajibika katika athari zinazodaiwa:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
5. Maslahi au haki zinazodaiwa kuathirika
Onyesha maslahi au haki zozote ambazo unadhani kuwa zimethiriwa au zinaweza kuathiriwa vibaya.
Iwapo itawezekana na inafaa, bainisha haki zozote au maslahi yanayolindwa na sheria au viwango vya wajibu wa kijamii au kanuni za maadili au mikataba na haki za binadamu au viwango vingine vya kimataifa: ………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
6. Je, tukio au hali hii inaendelea?
Ndio
Hapana
Iwapo ndio, tafadhali elezea. …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
23
SEHEMU C: USHAHIDI ULIOPO
1. Ushahidi wa hati
Hati zinaweza kusaidia kuonyesha iwapo kuna athari mbaya (kwa mfano, ushahidi wa kimatibabu, ripoti za kisayansi, ripoti za kitaalamu, ripoti za kichunguzi, picha, na video au rekodi za filamu,
miongoni mwa vingine)
Ikiwezekana, ambatanisha nakala za hati hizi. (Nakala hazina haja ya kuthibitishwa au
kuhalalishwa kisheria). Tafadhali usiambatanishe nakala halisi. Iwapo haiwezekani kutuma au kutoa hati, unapaswa kuelezea ni kwa nini na kuonyesha
iwapo utaweza kuzituma hapo baadaye au iwapo utatoa ruhusa kwa Timu ya Wachunguzi ya Mgodi kukusaidia kuzipata. Katika tukio lolote, unapaswa kuonyesha ni hati gani zinafaa
kuthibitisha ukweli wa madai.
Orodhesha au onyesha ushahidi ambao kwao ndio msingi wa Lalamiko lako, na ikiwezekana, onyesha
ushahidi gani unaoambatanisha au kutuma pamoja na Lalamiko lako:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Je, kuna ushahidi wowote ambao unaweza kupata tabu ya kuupata na hivyo unatoa idhini kwa Timu
ya Uchunguzi ya Mgodi kufuatilia kwa ajili yako? Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, onyesha ushahidi gani unautolea idhini kwa Timu ya Uchunguzi ya Mgodi kufuatilia.
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Iwapo umeambatanisha ripoti za kimatibabu au hati nyingine kutoka katika hospitali inayokutibu au
daktari katika orodha hapo juu, tafadhali ambatanisha na taarifa ya matibabu iliyosainiwa.
Ninaambatanisha taarifa ya matibabu iliyosainiwa
Siambatanishi taarifa ya matibabu iliyosainiwa)
2. Mashahidi
Tambua, ikiwezekana, mashahidi wa athari mbaya inayodaiwa. Onyesha iwapo kuna umuhimu wa kuficha utambulisho wa mashahidi na kama ni hivyo, toa sababu. Ambatanisha maelezo ya
mashahidi au taja ni lini unatarajia kutoa maelezo ya mashaihidi.
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
24
Je, ni vigumu kwako kupata maelezo ya mashahidi na je, unatoa idhini kwa Timu ya Uchunguzi ya
Mgodi kuchukua maelezo ya mashaihidi kwa ajili yako? Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, bainisha ni mashahidi gani unaidhinisha wahojiwe na Timu ya Wachunguzi ya Mgodi
na kutoa taarifa zao za mawasiliano:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
SEHEMU D: TAARIFA KUHUSU MALALAMIKO MENGINE AU UTARATIBU
1. Je, Lalamiko lako linahusiana na Lalamiko lililopita au ombi la hatua za tahadhari?
Je, wewe au watu waliothirika walishawahi kuwasilisha Lalamiko katika Ofisi ya Kushughulikia
Malalamiko kuhusu ukweli huu na/au tukio hili? Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, onyesha namba ya kumbukumbu ya Lalamiko au toa maelezo:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Je, umewasilisha ombi la Hatua za Tahadhari kwenye Ofisi ya Malalamiko kuhusu ukweli huu na/au tukio hili?
Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, onyesha namba ya kumbukumbu:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
2. Je, umewahi kuchukua hatua yoyote ya kuwasilisha malalamiko kuhusu mada ya
Lalamiko kwenye mchakato wowote mwingine wa suluhu?
Je, wewe au watu walioathirika wanawakilishwa na mwanasheria au mtu mwingine yeyote kuhusiana
na mchakato mwingine wa suluhu? Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, onyesha jina na taarifa za mawasiliano za mwakilishi: …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
25
Je, wewe au watu walioathirika walishachukua hatua hapo awali za kuwasilisha lalamiko kuhusu hoja
hizi na/au tukio hili kwenye chombo chochote cha kisheria au hatua zisizo za kisheria dhidi ya Mgodi au kampuni mame au washirika wake?
Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, onyesha mchakato, ombi la msaada, hali ya mchakato na matokeo yoyote:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Je, wewe au watu walioathirika walishachukua hatua hapo awali za kuwasilisha lalamiko kuhusu hoja
hizi na/au tukio hili kwenye chombo chochote cha kisheria au hatua zisizo za kisheria dhidi ya chombo kingine chochote ikiwemo serikali au polisi?
Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, onyesha mchakato, ombi la msaada, hali ya mchakato na matokeo yoyote:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
3. Umezifahamisha mamlaka zozote za umma kuhusu suala unalolalamikia?
Umetoa taarifa kwa mamlaka yoyote ya umma kuhusu hoja na/au tukio linalolalamikiwa? Hii inaweza kujumuisha polisi au mamlaka ya kimatibabu.
Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, onyesha mamlaka za umma na toa maelezo yoyote. …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
RASIMU YA KAZI ILIYOREKEBISHWA Desemba 2017
26
SEHEMU E: HATUA ZA TAHADHARI
Katika baadhi ya hali mbaya na za dharura, Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko anaweza
kupendekeza kwamba Mgodi uchukue Hatua za Tahadhari kudhibiti athari zisizorekebishika kwenye haki za mtu binafsi, kikundi au jamii.
1. Je, kuna hali ya hatari na dharura ya athari zisizoweza kurekebishika kwenye haki za mtu binafsi, kikundi au jamii?
Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, tafadhali eleza sababu na orodhesha watu wowote ambao wako katika hatari:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
2. Tafadhali eleza Hatua zozote za Tahadhari zinazohitajika:
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
SEHEMU F: MSAADA YA KIBINADAMU
Katika baadhi ya hali mbaya na za dharura, Kiongozi wa Timu ya Kushughulikia Malalamiko anaweza kupendekeza kwamba Mgodi utoe Msaada wa Kibinadamu kwa mtu ambaye ameumia akiwa Mgodini
au kuhusiana na shughuli za Mgodi hata pale ambapo haki za mtu huyo, kikundi au jamii hazitakuwa zimeathiriwa au kutishiwa na hakuna suluhu chini ya Mchakato wa Kushughulikia Malalamiko
itatolewa.
1. Je kuna hali ya hatari na ya dharura inayohusisha hofu ya kifo au majeraha yenye
athari kubwa yanayohusiana na shughuli za Mgodi? Ndio
Hapana
Iwapo ni ndio, tafadhali eleza sababu na orodhesha watu wowote ambao wako katika hatari:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
2. Tafadhali elezea msaada wowote wa kibinadamu unaohitajika:
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………