76
www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 1 MASWALI NA MAJIBU Kidato cha 1 6 Tumia muongozo huu kupata umahiri wa jinsi ya kujibu maswali kwa usahihi, aidha usiishie hapo kwani maswali ni mengi na si rahisi kuyachambua yote lakini kwa muongozo huu utaweza kupata msingi bora wa kujibia maswali mbalimbali. Iwapo una maoni, mapendekezo au ushauri wowote tafadhali wasiliana name kwa njia zilizopo hapa chini. Kwa mawasiliano zaidi: Simu: 0717104507 0766104507 0735104507 0684104507 Baruapepe: [email protected] Tovuti: www.mwalimuwakiswahili.co.tz MAENEO YALIYOGUSWA: 1. FASIHI KWA UJUMLA 2. SARUFI NA UTUMIZI WA LUGHA 3. UFAHAMU NA UTUNGAJI 4. MAENDELEO YA KISWAHILI 5. JINSI YA KUJIBU MASWALI YA VITABU

MASWALI NA MAJIBU · simulizi kama ngoma, nyimbo, matambiko na hadithi katika fasihi andishi. Husaidia kukuza lugha kutokana na watunzi wa fasihi simulizi kutumia lugha kisanaa 7

  • Upload
    others

  • View
    266

  • Download
    19

Embed Size (px)

Citation preview

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 1

    MASWALI NA MAJIBU

    Kidato cha 1 – 6

    Tumia muongozo huu kupata umahiri wa jinsi ya kujibu maswali kwa usahihi, aidha usiishie hapo

    kwani maswali ni mengi na si rahisi kuyachambua yote lakini kwa muongozo huu utaweza kupata

    msingi bora wa kujibia maswali mbalimbali.

    Iwapo una maoni, mapendekezo au ushauri wowote tafadhali wasiliana name kwa njia zilizopo

    hapa chini.

    Kwa mawasiliano zaidi:

    Simu: 0717104507

    0766104507

    0735104507

    0684104507

    Baruapepe: [email protected]

    Tovuti: www.mwalimuwakiswahili.co.tz

    MAENEO YALIYOGUSWA:

    1. FASIHI KWA UJUMLA

    2. SARUFI NA UTUMIZI WA LUGHA

    3. UFAHAMU NA UTUNGAJI

    4. MAENDELEO YA KISWAHILI

    5. JINSI YA KUJIBU MASWALI YA VITABU

    mailto:[email protected]

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 2

    Fasihi kwa Ujumla

    1. Eleza maana ya Fasihi.

    Au: Ni nini maana ya Fashi?

    Majibu:

    Fasihi ni Sanaa itumiayo lugha kufiksha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa kwa njia ya masimulizi yam

    domo au maandishi. Fasihi husemwa kuwa ni Sanaa kwa sababu kwanza yenyewe ni mojawapo ya

    matawi ya Sanaa (yaani ni sawa na kusema mtoto wa nyoka ni nyoka) lakini pili ni kuwepo kwa

    vipengele vya kisanaa (kifani) katika kazi ya fasihi. Nyenzo kuu ya fasihi ni maneno teule ya lugha.

    2. Taja dhima za fasihi katika jamii

    Au: Taja faida za fasihi katika jamii

    Au: Fafanua kazi za fasihi katika maisha ya mwanadamu

    Au: Fasihi ina umuhimu gani katika jamii?

    Majibu:

    Fasihi ni Sanaa itumiayo lugha kufiksha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa kwa njia ya masimulizi yam

    domo au maandishi. Fasihi ina umuhimu mkubwa kwa jamii kama ifuatavyo:

    Hukuza lugha ya jamii husika kupitia mawasiliano na kupashana habari za kifasihi miongoni

    mwa wanajamii.

    Huhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii husika

    Huchochea maendeleo ya jamii kupitia kuhimiza kazi mfano nyimbo za kazi na majigambo.

    Hudumisha umoja na mshikamano baina ya wanajamii kupitia tanzu kama ngoma

    Hutoa malezi kwa jamii kupitia tanzu kama hadithi, michezo ya watoto na jando na unyago

    Huchochea mabadiliko ya kijamii kifikra, kisiasa na kiuchumi na hivyo fasihi ni sawa na silaha

    ya ukombozi wa jamii

    Huhifadhi na kurithisha amali mbalimbali za jamii kwa vizazi mbalimbali.

    3. Je, kuna tanzu ngapi za fasihi? Fafanua tofauti zinazojitokeza katika tanzu hizo.

    Majibu:

    Kuna tanzu mbili za fasihi ambazo ni fasihi simulizi na fasihi andishi. Fasihi simulizi ni ile

    inayowasilishwa kwa njia ya masimulizi yam domo na kupokezwa kizazi kimoja na kingine. Usanii

    wake humtegemea fanani ambaye huwasiliana ana kwa ana na hadhira yake.

    Fasihi andishi ni ile ambayo huwasilishwa kwa njia ya maandishi. Usanii wake humtegemea mwandishi

    ambaye hukaa peke yake akaibuni, akaitunga na kuiandika kazi yote ya fasihi.

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 3

    Tofauti kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi

    Fasihi Simulizi Fasihi andishi

    Huwasilishwa na fanani kwa njia ya masimulizi

    yam domo

    Huwasilishwa na mwandishi kwa njia ya

    maandishi

    Huhifadhiiwa kichwani na kusambazwa kwa njia

    ya masimulizi

    Huhifadhiwa kwa maandishi na kusambazwa kwa

    maandishi

    Ina tanzu nyingi kuliko fasihi andishi (hadithi,

    semi, ushairi, Sanaa za maonesho)

    Ina tanzu chache kuliko fasihi simulizi (ushairi,

    riwaya, tamthiliya)

    Ina uhuru wa kutumia wahusika wa aina

    mbalimbali kama vile binadamu na viumbe

    vinginevyo

    Haina uhuru huo. Mara nyingi wahusika wake ni

    binadamu wa kawaida tu

    Ni mali ya jamii nzima inayohusika Ni mali ya mwandishi/mtunzi

    Hadhira yake ni watu wote katika jamii – watoto,

    wazee, wanaojua kusoma na wasiojua kusoma

    Hadhira yake ni wale wanaojua kusoma na

    kuandika tu

    Ina hali ya utendaji – inapowasilishwa

    huambatana na utendaji wa viungo vya mwili mf.

    Kupiga makofi, vigelegele, kutingisha kichwa.

    Haina utendaji wala ushiriki wa hadhira

    Ni kongwe kuliko fasihi andishi. Ilianza baada ya kugunduliwa kwa maandishi

    hivyo si kongwe

    Hubadilika kulingana na wakati na mazingira Haibadiliki baada ya kuandikwa

    4. Fafanua kwa mifano dhana zifuatazo:

    (a) Nahau (b) Tashihisi (c) Tarihi (d) Mubalagha (e) Methali

    Majibu:

    (a) Nahau: ni semi fupifupi zenye kutoa maana iliyokinyume kwa kutumia lugha ya picha.

    Mfano:

    Amevaa miwani (amelewa)

    Amepata jiko (ameoa)

    Kumkalia kitako (kumsema)

    Kumlamba kisogo (kumsengenya)

    (b) Tashihisi: ni tamathali ya semi inayovipa uwezo wa kibinadamu vitu au viumbe visivyo na sifa ya

    utendaji wa kibinadamu.

    Mfano:

    Kaburi lilimsitiri na aibu

    Mawimbi yalipiga makofi

    Misitu ikatabasamu

    Mawingu yakafunga kumuondolea udhia

    (c) Tarihi: ni kipera cha hadithi kinachosimuliwa kuhusu matukio ya kihistoria yaliyowahi kuikumba

    jamii. Tarihi aghalabu huambatana na wakati wa utokeaji wa tukio lenyewe.

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 4

    (d) Mubalagha: ni tamathali ya semi inayotia chumvi mazungumzo kwa lengo la kuleta uhalisia wa

    tukio lenyewe.

    Mfano:

    Tulimlilia Nyerere tukajaza bahari ya machozi

    Watu walikuwa wengi kama sisimizi

    Chakula kilikuwa kingi kama mchanga

    (e) Methali: ni semi zenye hekima na busara zitumikazo kuonya, kuadibu na kuadilisha jamii.

    Mfano:

    Aisifuye mvua, karowa mwilini mwake

    Asiyejua maana haambiwi maana, akiambiwa maana hiyo si maana.

    Mwana wa muhunzi asiposana, hufukuta

    Ada yam ja hunena, muungwana vitendo

    5. Fafanua sifa mbalimbali za fasihi simulizi

    Majibu:

    Fasihi simulizi ni kazi ya Sanaa inayotumia lugha kufikisha ujumbe kwa hadhira kwa njia ya masimulizi

    yam domo.

    Sifa za fasihi simulizi:

    Inahusisha utendaji wa viungo vya mwili

    Fanani na hadhira huonana ana kwa ana

    Haina gharama za maandalizi

    Haibagui watu kwa kigezo cha kujua kusoma na kuandika

    Hadhira yake hushiriki katika uwasilishaji

    Hubadilika kulingana na wakati na mazingira

    Huwa ni mali ya jamii nzima

    Huhifadhiwa kichwani

    Huwa na uwanja maalumu wa kutendea mf. Matambiko (chini ya miti mikubwa, milimani au

    mapangoni)

    6. Fasihi simulizi ina dhima gani katika jamii?

    Majibu:

    Fasihi ni Sanaa itumiayo lugha kufiksha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa kwa njia ya masimulizi yam

    domo au maandishi.

    Fasihi Simulizi ina dhima zifuatazo katika jamii:

    Kuelimisha na kufundisha jamii ili ifuate mkondo mwema wa maisha mf. Jando na Unyago

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 5

    Kuburudisha na kuliwaza jamii baada ya kazi ngumu mf. Ngoma

    Kutoa maadili mema katika jamii mf. Vigano

    Huhimiza umuhimu wa kazi katika jamii mf. Majigambo

    Hutunza historia ya jamii mf simulizi kama tarihi

    Huchangia katika uandishi wa fasihi andishi kutokana na kutumiwa kwa vipengele vya fasihi

    simulizi kama ngoma, nyimbo, matambiko na hadithi katika fasihi andishi.

    Husaidia kukuza lugha kutokana na watunzi wa fasihi simulizi kutumia lugha kisanaa

    7. Fafanua aina tano za wahusika wa fasihi simulizi

    Majibu:

    Wahusika katika fasihi simulizi ni watu, wanyama, vitu na mahali. Wahusika hao kimsingi hujengwa na

    fanani ili waweze kukidhi uwakilishaji wa sifa na tabia za binadamu katika fasihi.

    Aina tano za wahusika wa fasihi simulizi ni:

    Msimuliaji (fanani) – ndiye anayewasilisha na kutamba kazi husika ya fasihi simulizi.

    Wasikilizaji (hadhira) – hawa hushirikiana na fanani katika uwasilishaji wa kazi ya

    fasihi. Ushiriki wa hadhira husaidia kumpa fanani tathmini juu ya uwasilishaji wake.

    Wanyama – hupewa sifa za kutenda kama binadamu. Huwakilisha tabia na sifa za watu

    katika jamii.

    Simba – huwakilisha watu wababe

    Fisi – huwakilisha watu waoga/walafi/wenye tamaa

    Nyoka – huwakilisha watu wenye tabia ya unafiki/uchonganishi/uongo

    Pono (ndege/samaki)- huwakilisha watu wenye usingizi mwingi

    Mkizi – huwakilisha watu wenye hasira za hovyo

    Sungura – huwakilisha watu wenye kutumia akili nyingi sana

    Kobe – huwakilisha watu wenye hekima na busara

    Binadamu – wahusika wa aina hii huwa na sifa za kibinadamu kufuatana na hulka zao,

    sifa na matendo yao. Mfano mzee mmoja, malkia wan chi, n.k

    Vitu na mahali – hadithi inapohusisha sehemu kama vile vichakani, kaburini, bwawani,

    porini au msituni, vitu hivyo na sehemu hizo hutumika kama aina fulani ya wahusik.

    8. Elezea maana na kazi ya methali katika jamii.

    Au: Methali kama utanzu wa fasihi simulizi una dhima gani kwa jamii?

    Majibu:

    Methali ni semi zenye hekima na busara zitumiwazo kuonya, kuadilisha na kuadimu jamii. Ni semi

    ambazo hutolewa ili kufikisha ukweli fulani katika maisha.

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 6

    Kazi/dhima za methali:

    Kuelimisha jamii – mfano: asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu

    Kuburudisha jamii – methali huburudisha, hufurahisha na kuliwaza jamii

    Methali huhimiza ushujaa – mfano: kunguru mwoga hukimbiza ubawa wake

    Methali huadibu – mfano: kiburi si maungwana

    Methali huhimiza ushirikiano – mfano: umoja ni nguvu, utengani ni udhaifu

    Methali hukuza lugha – matumizi ya lugha kisanii katika methali huchangia kukuza lugha

    9. Eleza maana na kazi ya vitendawili katika jamii

    Majibu:

    Vitendawili ni semi zenye kuchochea fikra na udadisi wa mambo. Ni mafumbo yenye kufikirisha

    kulingana na mazingira halisi ya jamii husika.

    Kazi za vitendawili ni:

    Hutumika kuelimisha jamii

    Huchochea utafiti kwa watoto, husaidia watoto kuwa wachunguzi wa mambo mbalimbali

    Hutumika kukuza lugha, watoto hupata ujuzi wa kujieleza kwa lugha fasaha kwa kutumia

    vitendawili

    Hutumika kuonya na kukosoa jamii

    Hutumika kufurahisha na kuburudisha jamii

    Huchochea udadisi wa mambo na uwezo wa kufikiri haraka

    Wakati mwingine vitendawili vina dhima ya kukejeli mfano: Wazungu wawili wanachungulia

    dirisha = kamasi

    10. Fafanua maana na sifa za hadithi za fasihi simulizi

    Majibu:

    Hadithi ni masimulizi yenye mtiririko wa matukio (visa) na wakati. Matukio hayo yaweza kuwa ya

    kubuni au ya kweli kulingana na harakati mbalimbali za maisha ya binadamu. Hadithi za fasihi simulizi

    ni kama vile ngano, tarihi, visasili na soga.

    Hadithi za fasihi simulizi huwa na sifa zifuatazo:

    Fanani na hadhira ni hai – yaani si wa kubuni na hukutana uso kwa uso wakati wa masimulizi

    Huwa na mahali maalumu pa kutendea

    Huelezea tukio maalumu

    Huwa na mianzo maalumu mfano:

    Hadithi hadithi………hadithi njoo

    Paukwa……………..Pakawa

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 7

    Atokeani……………twaibu

    Lengo la mianzo hiyo ni:

    Kuonesha mwanzo wa hadithi

    Kuitayarisha hadhira ili ifuatilie hadithi

    Kumhakiki msikilizaji

    Sifa nyingine ni kuwa msimuliaji wa hadithi wakati wa kusimulia hutumia sauti

    kuwabainisha wahusika wote waliomo na pia hutumia vitendo au kushangaa ili mradi kufikia

    lengo lake.

    Sifa ingine ni kuwa msimuliaji anaweza kutumia mhusika hai au mfu, wa kidhanifu au

    kiyakinifu ili mradi amechorwa vema na kufikisha ujumbe kwa jamii husika.

    Hadithi za fasihi simulizi zina kazi (dhima) zifuatazo katika maisha (Taz. Swali la 10 hapa

    chini):

    11. Je, hadithi za fasihi simulizi zina dhima gani katika maisha?

    Majibu:

    Hadithi ni simulizi ya kweli au ya kubuni yenye mtiririko wa visa na wakati. Ni masimulizi ya mfululizo

    wa nathari juu ya mambo yaliyotokea au juu ya mambo ya kubuni katika maisha ya jamii.

    Hadithi za fasihi simulizi zina kazi (dhima) zifuatazo katika maisha:

    Kujenga jamii na kuipa mielekeo mizuri ya maisha

    Kuelimisha, kuadibu na kuonya jamii

    Ni chombo cha kurithisha elimu na amali za jamii kutoka kizazi hadi kizazi

    Husisitiza ushirikiano katika jamii – (ushirikiano huo ni katika shughuli mbalimbali za kijamii

    mfano: kilimo, harusi, mzishi, n.k)

    Huhifadhi kumbukumbu za watu katika jamii

    Huhifadhi historia ya jamii husika mfano: ngano

    12. Fafanua maana, aina na sifa za ushairi wa fasihi simulizi

    Majibu:

    Ushairi ni Sanaa inayopambanuliwa katika beti lugha ya mkato yenye kunata na kuvuta akili na mawazo

    ya msikilizaji. Ushairi hujumuisha vipera kama vile mashairi, nyimbo, ngonjera, maghani, tenzi na

    ngonjera.

    Sifa za ushairi wa fasihi simulizi ni kama vile:

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 8

    Huwa na mpangilio maalumu wa maneno

    Huwa na mapigo ya kimuziki

    Huwa na uchaguzi na matumizi ya maneno

    Huendana na mabadiliko/tukio maalumu katika jamii

    Huwa na mwimbaji au waimbaji wanaoimba kwa sauti

    Kuwepo kwa hadhira inayoimbiwa

    Huelezea tukio maalumu katika jamii.

    13. Ushairi (kama utanzu mmojawapo wa fasihi simulizi) una faida gani kwa jamii ya sasa?

    Majibu:

    Ushairi ni Sanaa inayopambanuliwa katika beti lugha ya mkato yenye kunata na kuvuta akili na mawazo

    ya msikilizaji. Ushairi hujumuisha vipera kama vile mashairi, nyimbo, ngonjera, maghani, tenzi na

    ngonjera.

    Kazi/faida za ushairi katika jamii ni kama vile:

    Hufundisha jamii mambo mbalimbali ya maisha – mfano nyimbo za jando na unyago

    Huhimiza umuhimu wa kazi – mfano nyimbo za jando na unyago

    Hufurahisha, huburudisha na kuliwaza jamii hasa baada ya kazi au wakati wa matatizo kama vile

    misiba mfano nyimbo za msiba.

    Huelimisha, huonya, huasa na kuadilisha jamii – mfano nyimbo za kanisani

    Husifu mafanikio yanaypatikana kutokana na juhudi za wanajamii – mfano nyimbo za siasa

    Hutunza historia ya jamii na utamaduni wa jamii – mfano nyimbo za jando na unyago

    Hutatua migogoro katika jamii – mfano nyimbo za kanisani

    Hukuza lugha ya jamii inayohusika.

    14. Fafanua maana ya hadithi za ngano za fasihi simulizi ukizingatia sifa na wahusika wake.

    Majibu:

    Ngano ni hadithi za mwanzo kabisa. Ni hadithi za kimapokeo ambazo husimuliwa juu ya matukio katika

    maisha ya binadamu (historia) pamoja na kuingiza mambo yanayosadikiwa na jamii fulani ya watu

    (itikadi).

    Hadithi za ngano zina sifa zifuatazo:

    - Ni hadithi fupi fupi ili kuweza kukaririwa

    - Hadithi za ngano huingia moja kwa moja katika kulitoa wazo kuu – mfano:- ridhika na kipato

    chako, uzembe haufai, n.k

    - Hadithi za ngano haziingilii mambo kwa undani sana

    - Hadithi za ngano huwa na mwisho wenye matumaini na furaha. Mfano: Wakaishi raha

    mustarehe.

    - Hadithi za ngano zina sentensi fupi fupi ili kutoa nafasi kwa waitikiaji

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 9

    - Hadithi za ngano huwa na mianzo mahususi

    Mfano:

    Paukwa - Pakawa

    Hadithi, hadithi - Hadithi njoo, ubunifu njoo utamu kolea

    Atokeani - Naam twaibu

    Umuhimu wa mianzo ya kihadithi ni:

    - Kumtayarisha msikilizaji

    - Kumhakiki msikilizaji

    - Kuonesha mwanzo wa hadithi

    Wahusika wa hadithi za ngano huwa na sifa zifuatazo:

    - Hawaumbwi sana – hawapambanuliwi kwa undani sana

    - Huwa viwakilishi/vielelezo vya tabia na mienendo fulani

    - Aghalabu wahusika hawa hawana majina halisi ila mtu mmoja, mfalme mmoja, Bi. Kizee

    mmoja, n.k

    - Mhusika mkuu hupewa jina maalumu au hapewi jina maalumu

    - Wahusika wa hadithi za ngano huwa wachache sana ama hutajwa kwa makundi

    - Wahusika wa hadithi za ngano hulazimika/hawalazimiki kuainishwa kama viumbe halisi;

    wanaweza kuwa wanyama, wadudu, mashetani, n.k

    15. Fasihi simulizi inajipambanua katika tanzu zipi?

    Majibu:

    Fasihi simulizi ni Sanaa itumiayo lugha kufikisha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa kwa njia ya

    masimulizi yam domo. Fasihi simulizi inaundwa na tanzu nne ambazo ni : Hadithi, Semi, Ushairi na

    Sanaa za maonesho. Tanzu hizo na vipera vyake huweza kuoneshwa kwa kielelezo kifuatacho:

    FASIHI SIMULIZI

    Hadithi Semi Ushairi Sanaa za maonesho

    Ngano Misemo Mashairi Maigizo

    Tarihi Methali Nyimbo Matambiko

    Visasili Vitendawili Ngonjera Utani

    Vigano Mafumbo Maghani Michezo ya watoto

    Soga Mizungu Tenzi Majigambo

    Nahau Ngonjera

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 10

    Lakabu Miviga

    Ngoma

    16. Eleza maana, kazi na matatizo yanayokwamisha maendeleo ya Sanaa za maonesho hapa nchini.

    Majibu:

    Sanaa za maonesho ni utanzu wowote wenye jumla ya mambo yafuatayo: dhana inayotendeka (tendo),

    mtendaji (fanani), hadhira (wasikilizaji) na uwanja wa kutendea (mandhari).

    Vijitanzu vya Sanaa za maonesho ni kama vile: majigambo, tambiko, miviga, michezo ya watoto, utani

    na ngoma.

    Kwa ujumla katika Sanaa za maonesho maneno huambatana na vitendo ili kukamilisha mawasiliano.

    Lengo (kazi) kuu la Sanaa za maonesho ni: kujifurahisha au kuwafurahisha watazamaji, kujikumbusha

    yaliyotokea zamani, kufufua utamaduni wa jamii, kuelezea/kuendeleza upendo katika jamii, kudumisha

    ujasiri katika maisha.

    Matatizo yanayokwamisha maendeleo ya Sanaa za maonesho hapa nchini ni:

    Uhaba wa fedha za kuendeleza Sanaa hizo

    Elimu duni kwa wananchi kuhusiana na Sanaa hizo na hivyo huzidharau

    Kukosekana kwa uongozi imara na mipango thabiti

    Ukosefu wa wataalamu wa kutosha

    Uhaba wa kumbukumbu za awali zilizohusu Sanaa za maonesho

    Kasumba ya baadhi ya watu kupenda Sanaa za nje zaidi na kudharau zile za ndani kwa kuziona

    za kishamba

    Changamoto ya maendeleo ya sayansi na teknolojia ambayo imebadili kabisa misingi ya Sanaa

    za asili katika uwasilishaji na kibaya zaidi baadhi ya Sanaa haziwezi kuwekwa katika njia za

    uhifazi kutokana na usiri wake mf. Matambiko.

    17. Fafanua maana, aina, na hasara za utani katika jamii.

    Majibu:

    Utani ni maneno ya mzaha ambayo pengine huambatana na vitendo ambayo husaidia kukuza mahusiano

    miongoni mwa wanajamii. Asili ya utani ilitokana na vita, koo kuoana, hama hama ya watu na biashara.

    Aina za utani ni kati ya mtu na mtu, ukoo na ukoo, kabila na kabila – mfano:- Wahaya kwa Wakurya,

    Wapare kwa Wachaga, au taifa na taifa n.k.

    Faida za utani ni :

    Kutoa maadili na mafunzo fulani

    Kuimarisha umoja na mshikamano (udugu)

    Kuhimiza ujasiri na juhudi katika maisha

    Kuhimiza upendo katika maisha

    Watu huambiana ukweli, hivyo hukosoana na kurekebishana

    Hukuza mila na desturi

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 11

    Hufariji, hustarehesha na kuburudisha

    Hasara za utani ni:

    Husababisha ugomvi katika jamii hasa utani unapozidi

    Huleta hasara ya kuchukuliana vitu bila malipo, mfano mifugo

    Huvunja au kuvunjiana heshima miongoni mwa wahusika

    18. Eleza maana, aina, sehemu, faida na hasara za matambiko.

    Majibu:

    Matambiko ni ibada inayoambatana na sadaka itolewayo kwa miungu kupitia wahenga, mahoka au

    mizimu. Sadaka itolewayo katika matambiko hujulikana pia kama kafara. Kafara huweza kuwa

    mnyama, mazao kama nafaka au vinywaji kama maziwa au pombe ya asili kutegemeana na jamii husika.

    Shabaha ya matambiko ni:

    Kutoa shukrani juu ya jambo lililofanikiwa

    Kuomba msaada fulani mfano mvua

    Kuondoa balaa mfano ukame, mafuriko, njaa au vifo.

    Kupatanisha wahusika na wahenga au miungu yao

    Kuzuia matatizo fulani katika jamii

    Kutambua au kukiri ukuu wa nguvu ya miungu au wahenga

    Kukuza na kuendeleza mila na desturi za jamii husika

    Aina za matambiko ni: aina za matambiko hutofautiana kati ya jamii moja na nyingine ingawa aina

    zilizo kuu ni :

    Matambiko ya wanyama – mifugo au mawindo

    Matambiko ya vinywaji au vyakula maalumu

    Matambiko ya mazao maalumu ya shambani

    Matambiko ya ngoma/michezo maalumu

    Matambiko ya watu maalumu

    Sehemu za matambiko ni: sehemu za kufanyia matambiko ni kama vile: mapangoni, makaburini,

    milimani au chini ya miti mikubwa.

    Faida / umuhimu wa matambiko ni kama vile:

    Kujenga Imani kama chombo cha kutatulia matatizo ya jamii

    Kuendeleza mila na desturi za jamii husika

    Kujenga na kuimarisha mahusiano miongoni mwa wanajamii

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 12

    Kuleta jamii pamoja na kuepusha mwingiliano usiokubalika

    Kuhimiza uwajibikaji na kujituma katika uzalishaji mali

    Kudumisha uadilifu ndani ya jamii

    Huchochea uhifadhi wa mazingira kwa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya matambiko

    Hasara za matambiko ni:

    Hujenga dhana potofu katika jamii – watu huamini nguvu fulani bila kuwa na uhakika

    Huleta utengano miongoni mwa wanajamii – mfano waumini wa dini na wasiowaumini

    (wapagani)

    Husababisha matumizi makubwa ya mali bila sababu za msingi na kuleta uharibifu wa mali kama

    mazao na vyakula

    Ni chanzo kikubwa cha kushamiri kwa imani za kishirikina

    Husababisha uhaba wa maeneo ya kufanyia shughuli kama za kilimo kutokana na maeneo

    kutengwa kwa shughuli za matambiko

    19. Fafanua maana ya miviga (sherehe) ukionesha faida na hasara zake kwa jamii.

    Majibu:

    Miviga ni sherehe zinazofanywa katika kipindi maalumu cha mwaka hasa baada ya mavuno. Mara

    nyingi sherehe hizi huwa na lengo la kumtoa mtu kutoka kundi moja na kumuingiza kundi jingine, mfano

    vijana kuingia utu uzima, harusi, kufuzu masomo, n.k

    Umuhimu wa miviga/sherehe za jadi ni:

    Hufundisha umuhimu wa kazi mfano ukulima, uwindaji, n.k

    Huhimiza ujasiri katika maisha

    Hufundisha masuala ya unyumba na malezi kwa ujumla

    Husisitiza ushirikiano miongoni mwa wanajamii

    Huleta ushindani, hivyo huchochea maendeleo

    Hasara za miviga katika jamii

    Ni ghali kuiendesha – huhitaji pesa na mali nyingi

    Huleta mashindano na matokeo yake husababisha baadhi ya watu wasio na uwezo kujiingiza

    katika wizi, utapeli, ujambazi, n.k

    Sherehe hujenga ufahari ambao huwaacha wenye sherehe kwenye matatizo mbalimbali mfano

    kulipa madeni

    Sherehe huweza kusababisha ugomvi, chuki, tamaa, n.k

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 13

    20. Majigambo kama utanzu wa Sanaa za maonesho una faida na hasara gani?

    Majibu:

    Majigambo ni vitendo vinavyoambatana na maneno ya kujisifu kwa ujasiri wa mtu binafsi au jamii

    nzima. Katika majigambo fanani huweza kutamba kwa ushairi wa kimapokeo au wa kisasa. Mtambaji

    hujiona ni bora kuliko watu wengine kwa kujiona, kujisifu na kujivuna.

    Katika majigambo lazima pawepo mtendaji, hadhira, mandhari na hali ya utendaji. Utendaji huendana

    na umri/rika mfano vijana kwa vijana au wazee kwa wazee.

    Faida za majigambo

    Hukuza ushujaa katika jamii kwa kukemea uoga, ulegevu na uzembe

    Hukuza na kuendeleza mila na desturi za jamii

    Huburudisha jamii maana fanani atambapo huonesha vichekesho vya kila aina

    Huimarisha utendaji kazi katika jamii

    Hukuza, huimarisha na kuchochea fani ya utambaji, lugha na kujieleza

    Hujenga uaminifu katika jamii

    Hasara za majigambo

    Hukuza na kuendeleza ubinafsi kwani fanani huonekana ni bora kuliko watu wengine

    Mkusanyiko wa hadhira hutumia fedha au vyakula kwa wingi hivyo husababisha hasara

    Huleta chuki, uhasama, fitina katika jamii

    Husababisha unafiki katika jamii

    Fanani hutamba upande wa mafanikio tu wakati wote kitu ambacho si kweli katika maisha.

    21. Ngoma ni aina ya mchezo unaochezwa kulingana na jamii inayohusika. Fafanua faida na hasara

    za mchezo huu.

    Majibu:

    Ngoma huchezwa kutegemea jamii inayohusika. Hushirikisha watu wa rika moja mfano wazee, vijana

    au watoto. Ngoma huchezwa katika eneo maalumu lililotengwa na jamii husika.

    Faida za ngoma katika jamii ni:

    Huhimiza ushujaa na ujasiri katika jamii

    Hufurahisha, huburudisha na kuliwaza jamii

    Hufafanua na kuendeleza mila na desturi za jamii

    Hutunza historia ya jamii

    Ngoma kwa kupitia maneno ya wimbo hutoa mafunzo fulani, hutoa taarifa fulani au sifa fulani

    na kukosoa makossa ya watu

    Hudumisha ari ya kufanya kazi kwa bidi

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 14

    Hasara za ngoma katika jamii ni:

    Ngoma huweza kugharimu pesa, vyakula na vinywaji na hivyo hutia hasara

    Ngoma huchezwa katika mazingira yanayoweza kuchochea vitendo vya zinaa na kusababisha

    kuenea kwa magonja hata UKIMWI

    Ngoma huweza pia kusababishamigogoro katika familia mathalani mke anapokwenda kwenye

    ngoma na kuchelewa kurudi nyumbani kumuandalia mumewe

    Ngoma hufanya watu wasifanye kazi kwa muda wote wa uchezaji ngoma na hivyo kushusha

    uzalishaji mali

    Huchochea ushindani ndani ya jamii na pengine kuzalisha chuki na kusemana

    22. Michezo ya watoto ina faida na hasara katika jamii. Eleza.

    Majibu:

    Michezo ya watoto ni maigizo yanayofanywa na watoto kutokana nay ale wanayoyaona katika jamii

    wanamoishi. Watoto huiga tabia na matendo ya wazazi wao. Washiriki wa michezo hii ni watoto

    wenyewe. Sehemu ya mchezo ni mahali popote pale kulingana na aina ya michezo.

    Faida za michezo ya watoto:

    Kuwajenga watoto kimawazo, busara, utii na hekima

    Kuimarisha viungo vya watoto kiafya

    Husaidia watoto kusadifu mazingira wanamoishi

    Watoto huanza kujifunza umuhimu wa kazi na ujasiri kupitia michezo hii

    Watoto hujifunza mbinu mbalimbali za kupambana na maadui

    Watoto hujifunza utamaduni wa jamii yao

    Watoto hujifurahisha kupitia michezo hii

    Watoto hujijengea uhusiano mzuri miongoni mwao.

    Husaidia kuibua, kuchochea na kuendeleza vipaji vya watoto

    Hasara za michezo ya watoto:

    Watoto huweza kuharibika kitabia iwapo watachangamana na watoto wenye tabia chafu

    Watoto huweza kuumizana iwapo watacheza michezo ya hatari bila uangalizi

    Huweza kuleta mifarakano baina ya wazazi kutokana na michezo mibaya

    Michezo ya watoto huweza kuathiri maendeleo ya kitaaluma iwapo mtoto atavutwa kwenye

    michezo na kukosa usimamizi katika masomo yake

    Huweza kuleta hasara ya uharibifu wa mali mfano mchezo wa kupika huweza kusababisha

    majanga ya moto

    Michezo hii pia hushawishi tabia ya udokozi kutokana na watoto kulazimishana kuleta vitu vya

    kuchezea

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 15

    23. Fafanua matatizo yanayoipata fasihi simulizi ikihifadhiwa katika maandishi, kichwa na kwenye

    vinasa sauti.

    Majibu:

    Uhifadhi wa fasihi simulizi katika maandishi, kichwa na vinasa sauti husababisha matatizo kama

    yafuatayo:

    Uhifadhi wa maandishi:

    Hukuna utendaji wa viungo vya mwili

    Huwezi kusikia sauti ya fanani

    Hakuna ushiriki wa hadhira

    Uhalisia wake hupungua

    Ni gharama

    Huwa mali ya mwandishi

    Haibadili kwa urahisi

    Uhifadhi wa kichwa:

    Ni rahisi kusahau

    Huweza kuongeza au kupunguza mambo muhimu

    Huweza kupotea au kusahaulika kutokana na hali ya aliyehifadhi

    Huifanya ishindwe kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia

    Uhifadhi wa vinasa sauti:

    Hakuna ushiriki wa hadhira

    Hupoteza utendaji

    Hukosa uhalisia

    Ni gharama

    Haibadiliki

    Huwa mali ya mtunzi

    Hubagua wasio na uwezo kiuchumi

    24. Ni kwa sababu gani vitendo vya wahusika katika fasihi simulizi ni vya muhimu sana?

    Majibu:

    Vitendo vya wahusika katika fasihi simulizi huimarisha hali ya utendaji katika fasihi simulizi. Fasihi hii

    hutegemea utendaji ili kukamilisha mawasiliano. Hivyo vitendo vya wahusika katika fasihi simulizi ni

    vya muhimu sana kwa sababu:

    (a) Huamsha msisimko wa kutamba na kusikiliza

    (b) Huleta ushiriki kati ya fanani na hadhira

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 16

    (c) Huvuta umakini wa fanani na hadhira

    (d) Huvuta usikivu wa hadhira

    (e) Husaidia kueleweka kwa ujumbe kwa urahisi

    (f) Husaidia kumpa fanani tathmini ya uwasilishaji wake

    (g) Humpa fanani kujiamini na kuchochea ubunifu wake wa kisanii

    25. Eleza maana ya maudhui katika kazi ya fasihi.

    Majibu:

    Maudhui katika kazi ya fasihi ni jumla ya mambo ambayo mtunzi wa kazi ya fasihi anakusudia

    kuyaeleza kwa hadhira yake. Maudhui hujengwa na vipengele kama vile: dhamira, ujumbe, migogoro,

    falsafa, msimamo na mtazamo. Kwa ujumla maudhui ni sawa na chakula kilichomo ndani ya chungu na

    chungu ndiyo fani yenyewe.

    26. Fafanua vipengele vinavyounda fani katika kazi ya fasihi.

    Majibu:

    Fani katika kazi ya fasihi ni mbinu za kisanaa anazozitumia mtunzi ili kufikisha ujumbe wake kwa

    hadhira aliyoikusudia. Vipengele vya fani ni kama vile: muundo, mtindo, wahusika, mandhari, matumizi

    ya lugha.

    27. Eleza maana ya (a) Ngano (b) Tarihi (c) Visasili (d) Vigano (e) Soga

    Majibu:

    Ngano – ni hadithi za kimapokeo zenye kusimulia matukio yenye kushabihiana na maisha halisi

    ya mwanadamu. Ngano huanza kwa maneno ya kuvutia wasikilizaji kama

    Paukwa……Pakawa……ngano hutumia wahusika wanyama, binadamu, vitu na mahali.

    Tarihi – ni hadithi fupi zinazohusu matukio ya kihistoria yaliyowahi kutokea katika jamii fulani.

    Tarihi husimuliwa ili kuikumbusha jamii ilipotoka, ilipo na ifanye nini kupiga hatua zaidi. Tarihi

    huweza kuwa na mwisho wa furaha au huzuni.

    Visasili – ni hadithi fupi zinazoeleza jinsi maumbile au tabia fulani zilivyoanza katika maisha ya

    jamii fulani. Hutumiwa sana kutoa majibu ya maswali ya kisayansi au kiasili ambayo kimsingi

    upeo wa maarifa yake hauwezi kufafanuliwa kwa wototo wadogo wakaelewa. Mfano: asili ya

    jogoo kuwika, asili ya kiboko kuishi majini, n.k

    Vigano – ni hadithi fupi za kimaadili ambazo husimuliwa kwa lengo la kukemea tabia na

    mienendo isiyokubalika katika jamii kama vile ulafi, uchoyo, udokozi na tamaa. Wahusika hasa

    huwa ni wanyama ambao hubebeshwa sifa na tabia za binadamu. Mfano: kigano cha mtoto

    mchoyo aliyeficha kitumbua katika sanduku la nguo na kukisahau. Siku alipokumbuka kitumbua

    chake akakuta panya wamekila na kisha kutafuna na nguo zake mpya za sikukuu. Vigano huishia

    na methali inayotumiwa kuacha funzo.

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 17

    Soga – ni hadithi fupi za kuchekesha na kupoteza muda. Soga hutumia wahusika binadamu na

    hasa watu wa kubuni. Wahusika hawa husadifu hali halisi ya mazingira fulani. Kupitia soga watu

    hukosoana, hutupiana kejeli na dhihaka kwa njia ya utani kwa lengo la kurekebishana tabia.

    28. Taja aina za nyimbo unazozifahamu hapa Tanzania.

    Majibu:

    Nyimbo ni tungo zenye mahadhi ya sauti inayopanda na kushuka. Huundwa kwa lugha ya mkato,

    matumizi ya lugha ya picha na mapigo ya kisilabi. Aina za nyimbo zinazofahamika hapa Tanzania ni

    kama vile:

    Nyimbo za siasa

    Nyimbo za ngoma (jando na unyago)

    Nyimbo za watoto

    Nyimbo za vita

    Nyimbo za kazi

    Nyimbo za kidini

    Nyimbo za misiba

    Nyimbo za tumbuizo

    Nyimbo za kuaga mwaka

    Nyimbo za mawaidha

    Nyimbo za uvuvi.

    29. Taja matatizo yanayojitokeza katika ukusanyaji wa kazi za fasihi simulizi.

    Majibu:

    Ukusanyaji wa fasihi simulizi ni hali ya kukusanya tanzu mbalimbali za fasihi hii. Tanzu hizo ni kama

    vile: semi, Sanaa za maonesho, hadithi na ushairi. Matatizo yanayojitokeza katika kipengele hiki cha

    ukusanyaji ni pamoja na:

    Vyombo duni vya ukusanyaji

    Changamoto za usafiri

    Tatizo la tafsiri kwa kazi zilizo katika lugha za asili

    Uhaba wa wataalamu

    Kasumba ya kutothamini kazi za fasihi za asili kwa kuona zimepitwa na wakati

    Ukosefu wa fedha

    Mila na desturi kutoruhusu baadhi ya tanzu kukusanywa na kuhifadhiwa katika njia nyingine.

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 18

    30. (a) Taja sehemu tano za kitendawili

    Majibu:

    Muundo wa kitendawili hugawanyika katika sehemu tano kama ifuatavyo:

    (i) Kiingizi – mfano: Kitendawili –tega

    (ii) Kitendawili chenyewe

    (iii) Swali la msaada – mfano: Ni nini hicho?

    (iv) Kichocheo – mfano: Naomba jibu

    (v) Jibu lenyewe.

    (b) Tegua vitendawili vifuatavyo:

    (i) Chiriku alimwambia mwanawe, “Nikiinama nikiinuka ni mauti yetu”

    (ii) Chukua ungo, wewe na mimi tupepete kisichopepeteka

    (iii) Kuku wangu hutagia miibani

    (iv) Mwenye kuitwa amefika lakini mjumbe bado hajarudi

    (v) Babaangu amenipa visu viwili: kimoja nakitumia lakini cha pili siwezi kukitumia

    (vi) Pana ng’ombe miongoni mwa kundi la ndama

    (vii) Chini chakula, kati kuni, juu mboga

    (viii) Hulala tulalapo, huamka tuamkapo

    (ix) Nilianika unga wangu, asubuhi sikuukuta

    (x) Mzazi ana miguu bali mzaliwa hana miguu

    Majibu:

    (i) Mtego (ii) Maji (iii) Nanasi (iv) Nazi na mkwezi (v) Ardhi na anga (vi) Mwezi na nyota (vii)

    Muhogo (viii) Jua (ix) Umande au nyota za angani (x) Kuku na yai

    31. Eleza maana ya misemo ifuatayo.

    (i) Akina baba kabwela

    (ii) Jikaza kisabuni

    (iii) Alikaa eda

    (iv) Elimu ni bahari

    (v) Toka nitoke

    (vi) Mtu mwenye utu

    (vii) Usingizi umepaa

    (viii) Kula chumvi nyingi

    (ix) Hawapikiki chungu kimoja

    (x) Kuzunguka mbuyu

    (xi) Kuvaa miwani

    (xii) Piga vijembe

    (xiii) Jipalia mkaa

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 19

    (xiv) Kazi ya kijungu jiko

    (xv) Ndege mbaya

    Majibu:

    (i) Akina baba kabwela = Watu wenye kipato kidogo (wanyonge)

    (ii) Jikaza kisabuni = Jitahidi hadi mwisho

    (iii) Alikaa eda = Alitimiza muda wa kumlilia mumewe

    (iv) Elimu ni bahari = Elimu haina mwisho

    (v) Toka nitoke = Fuatana katika uzazi

    (vi) Mtu mwenye utu = Muungwana

    (vii) Usingizi umepaa = Usingizi umehama

    (viii) Kula chumvi nyingi = Kuishi miaka mingi

    (ix) Hawapikiki chungu kimoja = Hawaelewani/Hawapatani

    (x) Kuzunguka mbuyu = Kula rushwa

    (xi) Kuvaa miwani = Kulewa pombe

    (xii) Piga vijembe = Sema mtu kwa mafumbo

    (xiii) Jipalia mkaa = Jiingiza katika matatizo

    (xiv) Kazi ya kijungu jiko = Kazi ya kumpatia mtu posho tu

    (xv) Ndege mbaya = Bahati mbaya (mkosi)

    32. Kwa kila methali hapa chini, andika methali yenye kufanana nayo.

    Mfano: Akili nyingi huondoa maarifa >>> Werevu mwingi mbele kiza/giza

    (i) Baada ya kisa mkasa

    (ii) Baada ya dhiki faraja

    (iii) Bandubandu humaliza gogo

    (iv) Bendera hufuata upepo

    (v) Dalili ya mvua mwaingu

    (vi) Dawa ya moto ni moto

    (vii) Jembe halimtupi mkulima

    (viii) Kamba hukatikia pabovu/pembamba

    (ix) Mbio za panya sakafuni huishia ukingoni

    (x) Mgema akisifia tembo hulitia maji

    (xi) Mpanda ngazi hushuka

    (xii) Usitukane wakunga na uzazi ungalipo

    (xiii) Ngozi ivute i maji

    (xiv) Ukuukuu wa Kamba si upya wa ukambaa

    (xv) Penye nia pana njia

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 20

    Majibu:

    (i) Baada ya chanzo kitendo

    (ii) Mtaka cha uvunguni sharti ainame Au: Mvumilivu hula mbivu Au: Mchumia juani hulia kivulini

    (iii) Haba nah aba hujaza kibaba

    (iv) Maji hufuata mkondo AU: Wengi wape

    (v) Mwanzo wa ngoma ni lele

    (vi) Sumu ya neno ni neno

    (vii) Mgaagaa na upwa hali wali mkavu

    (viii) Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu

    (ix) Njia ya mwongo ni fupi Au: Siku za mwizi ni arobaini

    (x) Ngoma ikilia sana hupasuka

    (xi) Aliyejuu mngoje chini Au: Cheo ni dhamana

    (xii) Fadhili ya punda mateke

    (xiii) Samaki mkunje angali mbichi Au: Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo

    (xiv) Usidhani yote yang’aayo ni dhahabu

    (xv) Abadi abadi Kamba hukata jiwe.

    33. Kwa kila methali kati ya zifuatazo andika maana, busara (faida) na hasara yake kwa jamii.

    (a) La kuvunda halika ubani

    Maana: kitu kikiharibika kimeharibika, hakiwezi kurekebishwa.

    Busara: hatuna budi kutupilia mbali vitu vilivyoharibika

    Hasara: kuna vitu ambavyo vikiharibika huweza kurekebishwa na vikarudia hali yake ya

    kawaida

    (b) Yote yang’aayo usidhani dhahabu

    Maana: si kila kitu katika dunia hii kina maana/thamani

    Busara: inatulazimu tuwe makini katika uchaguzi au uteuzi wa vitu vionekanavyo machoni petu.

    Hasara: tunaweza kuacha vitu vyenye manufaa katika maisha kwa kuzingatia kuwa si kila

    king’aacho ni dhahabu.

    (c) Kikulacho ki nguoni mwako

    Maana: anayekufanyia unyama au uadui ni mtu uliyenaye karibu.

    Busara: ni lazima tuwe macho na marafiki zetu wa karibu

    Hasara: unaweza kupoteza uhusiano mzuri kwa marafiki au ndugu zako au jirani kwa ajili ya

    kudhania tu.

    (d) Mvumilivu hula mbivu

    Maana: mtu anayevumilia mwisho wake hufanikiwa

    Busara: tuwe na subira katika mipango yetu ili hatimaye tupate mafanikio hapo baadaye

    Hasara: tunaweza kuvumilia lakini mwishowe tusifanikiwe.

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 21

    (e) Haraka haraka haina barak:

    Maana: kufanya kitu kwa utaratibu au mipangilio mizuri huleta mafanikio mbeleni.

    Busara: tusiwe na pupa na papara katika mambo tuyatendayo

    Hasara: methali hii inaweza kuleta hasara kwa jamii kwani kuna mambo yanatakiwa kufanywa

    haraka kama vile kumkimbiza mgonjwa hospitalini

    34. Eleza maana ya:

    (a) Fanani

    (b) Hadhira

    (c) Sanaa

    (d) Lugha ya picha

    (e) Wahusika katika fasihi

    Majibu:

    (a) Fanani katika kazi ya fasihi simulizi ni yule anayewasilisha kazi ya fasihi simulizi kwa hadhira yake.

    Fanani ndiye anasimulia, kuimba na kutamba kazi ya fasihi simulizi.

    (b) Hadhira ni wale wapokeaji, watazamaji au wasikilizaji wa kazi ya fasihi simulizi inayowasilishwa

    na fanani.

    (c) Sanaa ni uzuri unaojitokeza katika umbo lililosanifiwa. Kuna aina nyingi za Sanaa

    (d) Lugha ya picha ni taswira inayotumiwa na fanani/mwandishi kuwakilisha dhana maalumu. Ni lugha

    inayomfanya msikilizaji/msomaji atafakari zaidi na ndipo anagundua taswira hiyo inawakilisha nini.

    (e) Wahusika katika kazi ya fasihi simulizi/fasihi andishi ni watu, wanyama, vitu au mahali. Wahusika

    hao hujengwa na fanani ili waweze kukidhi na kuwakilisha dhana mbalimbali za maisha katika jamii.

    35. Eleza maana ya semi na taja vipera vinavyounda semi.

    Majibu:

    Semi ni tungo fupi zinazoundwa kwa lugha ya picha, ishara na tamathali. Semi huwa inabeba busara,

    hekima na ushauri mahususi kwa jamii. Semi za fasihi simulizi zina vipera kama vile: misemo,

    mafumbo, vitendawili, mizungu, lakabu, methali, nahau.

    36. Taja mambo matano yanayoifanya fasihi iwe Sanaa.

    Majibu:

    Fasihi ni Sanaa kwa sababu ya mambo yafuatayo:

    Ufundi wa kutumia lugha kueleza jambo (matumizi ya lugha)

    Mpangilio maalumu wa matukio (muundo)

    Namna nzuri ya uwasilishaji (mtindo)

    Uumbaji wa wahusika (wahusika)

    Kuwepo kwa mandhari (sehemu ya matukio)

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 22

    37. Eleza tofauti baina ya kazi ya fasihi na isiyo ya fasihi.

    Majibu:

    Fasihi ni kielelezo cha kisanaa kitumiacho maneno kufikisha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa.

    Vipengele vinavyotofautisha kazi ya fasihi na ile isiyo ya kifasihi ni kama vile:

    (a) Lugha – fasihi hutumia lugha kiufundi lakini kazi zingine zisizo fasihi hazitumii lugha kiufundi

    (b) Wahusika – fasihi hutumia wahusika kubeba ujumbe tofauti na kazi zisizo za kifasihi

    (c) Mandhari – kazi za kifasihi hasa simulizi huwa na uwanja maalumu wa kutendekea k.v. mapangoni,

    milimani, kwenye miti mikubwa tofauti na matukio yasiyo ya kifasihi

    (d) Fani na maudhui – kazi ya fasihi lazima iwe na umbo la nje (fani) na umbo la ndani (maudhui) kitu

    ambacho huwezi kukikuta katika kazi isiyo ya kifasihi

    (e) Muundo – kazi ya kifasihi huwa na msuko maalumu unahusu mpangilio wa visa na matukio tofauti

    na kazi isiyo ya kifasihi

    (f) Mtindo – huu ni upekee wa uwasilishaji wa kazi ya kifasihi ambao huweza kuwa masimulizi,

    majibizano au kinudhumu lakini huwezi kukuta mtindo kama huu katika kazi isiyo ya kifasihi.

    38. Kwa kutumia mifano, taja sifa nne za fasihi.

    Majibu:

    Fasihi ni kazi ya Sanaa inayotumia lugha ili kufikisha ujumbe wake kwa jamii iliyokusudiwa.

    Zifuatazo ni sifa nne za fasihi:

    (i) Fasihi ni Sanaa, maana yake ni matokeo ya kiufundi. Kitu chochote kilichotengenezwa kwa

    ufundi hupendeza, huvutia na huamsha hisia ndani ya mhusika

    (ii) Fasihi ni Sanaa itumiayo lugha. Fasihi ni ufundi wa kutumia lugha ili kuleta mchomo au hisia

    fulani. Katika fasihi kuna aina mbalimbali ya matumizi ya lugha: kuna misemo, nahau, tamathali

    za semi, na matumizi ya lugha ya picha.

    (iii) Fasihi ni kielelezo, haina budi ieleze hali halisi ya maisha ya jamii inayohusika. Kueleza huku

    hutumia na huzingatia ufundi wa kutumia lugha. Vilevile hubeba ujumbe maalumu ambao

    unapelekwa kwa jamii inayohusika. Jamii hii huwakilishwa na watazamaji, wasomaji na

    wasikilizaji. Hawa kifasihi huitwa hadhira.

    (iv) Fasihi ni maelezo yenye fani na maudhui. Fani inaundwa na vipengele kama: muundo, mtindo,

    wahusika, mandhari na matumizi ya lugha. Maudhui huundwa na: dhamira, ujumbe, migogoro,

    falsafa, msimamo na mtazamo.

    39. Taja mambo matano muhimu yanayotambulisha wimbo.

    Majibu:

    Wimbo ni kile kinachoimbwa. Hivyo hii ni dhana inayojumuisha tanzu nyingi. Hata baadhi ya tanzu za

    kinathari kama vile hadithi huweza kuingia katika kundi la nyimbo pindi zinapoimbwa.

    Mambo muhimu matano yanayotambulisha wimbo ni:

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 23

    (a) Muziki wa sauti ya mwimbaji au waimbaji

    (b) Muziki wa ala (kama upo)

    (c) Matini au maneno yanayoimbwa

    (d) Hadhira inayoimbiwa

    (e) Muktadha unaofungamana na wimbo husika mfano: msiba, sherehe, ibada, n.k

    40. Eleza kazi ya makofi katika nyimbo za fasihi simulizi.

    Majibu:

    Kazi ya makofi katika nyimbo za fasihi simulizi ni kukata shauri juu ya mwendo wa wimbo (polepole

    au haraka haraka). Katika makabila mengi, makofi huchukua nafasi kubwa katika nyimbo ambazo watu

    huimba wamekaa au wamesimama bila kucheza.

    Vilevile hutumika sana kumpa hamasa mchezaji aliyekatikakati na kadiri makofi yanavyoongezeka

    ndivyo mchezaji anavyozidisha madoido na mbwembwe.

    Makofi pia hutumiwa sana na wanawake katika nyimbo za harusi kutoa alama ya mwendo wa kasi na

    hamasa ya waimbaji, wachezaji na namna ya kuishirikisha hadhira.

    Vilevile makofi husaidia kuondoa usingizi na kumpa mwimbaji nafasi ya kupumzika na kumeza mate.

    41. Andika maana ya tanzu zifuatazo za fasihi andishi.

    (a) Riwaya (b) Ushairi (c) Tamthiliya

    Majibu:

    (i) Riwaya ni hadithi ndefu ya kubuni yenye mawanda mapana, lugha ya kinathari, mchanganyiko

    wa visa na dhamira, wahusika kadhaa na matukio yaliyosukwa kimantiki yenye kufungamana

    na wakati ikishabihiana na maisha halisi.

    (ii) Ushairi ni Sanaa inayopambanuliwa kwa mpangilio maalumu wa maneno fasaha na yenye

    mvuto, kwa lugha ya mkato, picha au sitiari au ishara, katika usemi, maandishi au ,ahadhi ya

    wimbo ili kueleza wazo au mawazo, kufunza au kueleza tukio au hisia fulani kuhusu maisha au

    mazingira ya binadamu kwa njia inayogusa moyo.

    (iii) Tamthiliya ni utungo wa kidrama ambao ni aina moja ya maandishi ya Sanaa za maonesho. Ni

    Sanaa inayooneshwa kwa vitendo vya wahusika waliotumiwa na msanii na kuvitafakari kwa

    makini.

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 24

    SARUFI NA UTUMIZI WA LUGHA

    42. Taja aina nane za maneno katika lugha ya Kiswahili. Kwa kila aina tunga sentensi moja na

    pigia mstari aina ya neno ulilotumia katika sentensi.

    Majibu:

    Aina nane za maneno katika lugha ya Kiswahili ni:

    (a) Jina/Nomino – (J/N): sentensi: Baba yangu ni mkulima hodari.

    (b) Kivumishi – (V): sentensi: Baba yangu amesafiri.

    (c) Kiwakilishi – (W): sentensi: Yule amefaulu.

    (d) Kiunganishi – (U): sentensi: Baba na mama wanalima.

    (e) Kihusishi – (KH): sentensi: John amepigwa kwa fimbo kubwa.

    (f) Kitenzi – (T): sentensi: baba analima shambani.

    (g) Kielezi – (E): sentensi: Nguo zimo kabatini.

    (h) Kihisishi/Kiingizi – (H/I): sentensi: Lo! Baba amefariki.

    43. (a) Eleza maana ya tungo.

    (b) Taja aina nne za tungo katika lugha ya Kiswahili.

    Majibu:

    Tungo ni matokeo ya kuweka pamoja vipashio vidogo zaidi na sahili ili kuunda kipashio

    kikubwa zaidi ya vyenyewe. Kwa mfano mofu hushikamanishwa pamoja na kuunda

    tungo neno.

    Kuna aina nne za tungo katika lugha ya Kiswahili ambazo ni:

    (a) Tungo neno – ni tungo inayoundwa kwa kushikamanisha pamoja mofu/mofimu

    (b) Tungo kirai/kikundi – ni tungo inayoundwa na neno moja au zaidi

    (c) Tungo kishazi – ni tungo inayotawaliwa na kitenzi kinachotoa taarifa kamili au isiyokamili

    kutokana na kushushwa hadhi kwa kupachikwa kiambishi rejeshi.

    (d) Tungo sentensi – ni tungo yenye muundo wa kiima na kiarifu na inayotoa taarifa iliyokamili.

    44. (a) Mofimu ni nini?

    (b) Kuna aina ngapi za mofimu?

    Majibu:

    Mofimu ni neno au sehemu ya neno isiyogawanyika zaidi na yenye maana ya kisarufi au

    kileksika.

    Kuna aina mbili za mofimu ambazo ni:

    (a) Mofimu huru: ni maumbo ya maneno yasiyogawanyika zaidi na yanayojitosheleza kimuundo na

    kimaana. Mfano: baba, mama, maji, hewa.

    (b) Mofimu tegemezi: hivi ni viambishi ambavyo hujiegemeza kwenye mzizi wa neno na kukamilisha

    muundo na maana ya neno. Mfano:

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 25

    Analima = A-na-lim-a

    Mofimu tegemezi hapo ni: A, na, a

    45. Lugha yoyote ina vipashio vitano. Vitaje kwa mifano.

    Majibu:

    Vipashio ni vipande vitumikavyo kuunda lugha katika darajia mbalimbali kuanzia na darajia ndogo

    kabisa ambayo ni mofu/mofimu hadi sentensi.

    Vipashio hivyo vya lugha ni:

    (a) Mofimu/mofu – ni kipashio kidogo kabisa chenye uamilifu wa kisarufi au kileksika. Mfano:

    baba, maji, hewa,

    a-na-som-a, tu-me-lim-iw-a

    (b) Neno – ni kipashio kinachoundwa kwa mofimu moja au zaidi. Neno linaloundwa kwa mofimu moja

    huwa ni neno huru na lile linaloundwa kwa mofimu zaidi ya moja huwa ni neno changamano lenye

    mzizi na viambishi. Mfano: paka, mtoto, chama, kikosi.

    (c) Kirai/kikundi – ni kipashio kinachoundwa kwa neno moja au zaidi. Kirai huundwa kwa neno kuu na

    kijalizo kimoja au zaidi. Mfano: mtoto, kijana mvivu, anasoma, amelima shamba.

    (d) Kishazi – ni kipashio kinachotawaliwa na kitenzi kichojitosheleza au kisichojitosheleza, kishazi huru

    huwa kina hadhi ya sentensi sahili na kishazi tegemezi hupewa hadhi ya kirai. Mfano:

    Baba aliyekuja amesafiri leo asubuhi.

    Baba aliyekuja……. (kitenzi hakijitoshelezi)

    Baba amesafiri …… (kitenzi kinajitosheleza)

    (e) Sentensi – ni tungo yenye muundo wa kiima na kiarifu na inayotoa taarifa iliyokamili.

    Mfano: Baba yangu / amesafiri leo

    K A

    Baba na mama / wanalima shamba

    K A

    46. (a) Viwakilishi ni nini?

    (b) Taja aina za viwakilishi unavyovifahamu.

    Majibu:

    (i) Viwakilishi (W) ni maneno yanayosimama badala ya nomino pindi nomino inapokosekana

    kwenye nafasi yake katika tungo. Mfano: Wewe unaishi wapi?

    (ii) Kuna aina tisa za viwakilishi kama ifuatavyo:

    - Kiwakilishi kimilikishi – mfano: kwetu ni mbali

    - Kiwakilishi cha idadi – mfano: Watano wamefika

    - Kiwakilishi cha sifa – mfano: Wafupi waje mbele

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 26

    - Kiwakilishi cha a-unganifu – mfano: ya moto imeisha

    - Kiwakilishi kioneshi – mfano: Huyu ni mweusi

    - Kiwakilishi kiulizi – mfano: Yupi ni mrembo?

    - Kiwakilishi nafsi – mfano: Mimi nitalima

    - Kiwakilishi cha amba – mfano: ambaye hakuniona apite mbele

    - Kiwakilishi cha pekee – mfano: yeyote ajitolee kuandika

    47. Fafanua dhima ya mofimu katika lugha.

    Majibu:

    Mofimu ni kipashio kidogo cha lugha ambacho huwakilisha maana maalumu kisarufi au kileksika.

    Mofimu tegemezi ndizo hasa hubeba maana ya kisarufi na hivyo huwa na dhima mbalimbali kama

    ifuatavyo:

    (i) Kudokeza nafsi – mfano: a- katika anacheza (nafsi ya tatu umoja)

    (ii) Kudokeza njeo/wakati – mfano: na- katika analima (njeo iliyopo)

    (iii)Kudokeza idadi – mfano: ki- katika viatu (wingi)

    (iv) Kudokeza urejeshi – mfano: ye- katika aliyetuita

    (v) Kudokeza ukanushi – mfano: ha- katika hakufika

    (vi) Kudokeza kauli ya utendeshi – mfano: ish-katika anaimbisha

    *Kimsingi mofimu zina dhima nyingi sana katika lugha hizo ni kwa uchache tu.

    48. (a) Eleza maana ya sentensi.

    (b) sentensi inaundwa na sehemu kuu ngapi?

    (c) Kuna aina ngapi za sentensi? Zitaje.

    (d) Taja aina ya sentensi zifuatazo.

    a. Baba yangu ni mkulima hodari.

    b. Kijana aliyekuja jana ameondoka.

    c. John angefika leo tungeondoka.

    d. Baba na mama wanalima shambani.

    e. Ng’ombe aliyezaa amekufa na ndama aliyezaliwa amepotea

    Majibu:

    i. Sentensi ni kifungu cha maneno, kuanzia neno moja na kuendelea chenye kiima na kiarifu na

    kinachotoa maana kamili.

    ii. Sentensi inaundwa na sehemu kuu mbili ambazo ni: Kiima (K) na Kiarifu (A)

    Mfano: Baba / analima shamba

    K A

    iii. Kuna aina nne za sentensi ambazo ni:

    Sentensi sahihi/huru

    Sentensi changamano

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 27

    Sentensi ambatano

    Sentensi shurutia

    iv. Sentensi zilizotajwa kwenye (47d) ni :

    Sentensi sahili

    Sentensi changamano

    Sentensi shurutia

    Sentensi sahili

    Sentensi ambatano

    49. (a) Eleza maana ya nomino.

    (b) Taja na fafanua aina za nomino.

    Majibu:

    (i) Nomino (N) ni neno linalotaja vitu, viumbe, hali, matendo au mahali ili kuviainisha na

    kuvitofautisha vitajwa miongoni mwa vingine.

    (ii) Kuna aina zifuatazo za nomino:

    Nomino za kawaida – ni majina ambayo si maalumu kwa vitajwa. Majina haya yatokeapo katika

    maandishi huanza kwa herufi za kawaida isipokuwa mwanzoni mwa sentensi huanza kwa herufi

    kubwa. Mfano:

    Baba analima shamba

    Mimi na baba tutaondoka kesho

    Nomino za pekee – ni majina maalumu kwa vitajwa. Nomino hizi huanza kwa herufi kubwa

    popote katika maandishi. Mfano:

    Juma amenunua gari

    Mimi na Juma tumenunua gari

    Nomino dhahania – ni majina ya viumbe au hali zisizoonekana wala kushikika. Mfano:

    Majina ya hali kama vile: afya, kiu, njaa, hasira

    Majina ya tabia kama vile: upole, ukatili, ujasiri

    Majina ya viumbe kama vile: malaika, zimwi, shetani, Mungu

    Majina ya jamii – ni majina yanayotaja watu au vitu katika makundi. Mfano: jeshi, bunge, chama,

    kikosi.

    Majina ya wingi – haya hutaja vitu katika wingi ingawa vinavyotajwa havina umoja wala wingi.

    Mfano: maziwa, maji, mafuta, mawasiliano, mazungumzo.

    50. (a) Nini maana ya sentensi tata?

    (b) Sentensi zifuatazo ni tata. Toa maana mbili au zaidi ili kuthibitisha utata wake.

    (i) Wizi wa silaha umeongezeka

    (ii) Majaliwa ameijia fedha yake

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 28

    (iii)Mwalimu wa Kiingereza ni mkali

    (iv) Mwanangu amelalia uji

    (v) Mama yangu anaota

    Majibu:

    (a) Sentensi tata ni ile inayowezesha wasikilizaji au wasomaji wake kuibua maana zaidi ya moja.

    (b) Majibu ya (49c i-v) hapo juu ni kama ifuatavyo:

    (i) Wizi wa silaha umeongezeka

    Maana: 1. Wizi wa kutumia silaha umeongezeka

    2. Kuibiwa kwa silaha kumeongezeka

    (ii) Majaliwa ameijia fedha yake

    Maana: 1. Ametumia fedha yake kama nauli

    2. Amekuja kuchukua fedha yake

    (i) Mwalimu wa Kiingereza ni mkali

    Maana: 1. Mwalimu wa somo la Kiingereza ni mkali

    2. Mwalimu mwenye asili ya Uingereza ni mkali

    (iv) Mwanangu amelalia uji

    Maana: 1. Amekunywa uji tu akalala

    2. Amelala juu ya uji uliomwagika

    (v) Mama yangu anaota

    Maana: 1. Anaota ndoto usingizini

    2. Anaota moto kujipa joto

    3. Anamea

    51. (a) Ni nini maana ya kivumishi?

    (b) Taja aina nane za vivumishi.

    Majibu:

    (a) Kivumishi (V) ni neno au kikundi cha maneno kinachotoa maelezo zaidi juu ya jina au kiwakilishi

    kingine.

    Mfano: Mtoto mzuri anakimbia

    V

    (b) Aina nane za vivumishi ni kama ifuatavyo:

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 29

    Vivumishi vya sifa – mfano: Mtoto mzuri, mrefu, mfupi, mtulivu, hodari, n.k

    Vivumishi vya idadi – mfano: chakula kingi, haba, chote, mbuzi wanne, watano

    Vivumishi vya vimilikishi – mfano: chumba chetu, chao, changu

    Vivumishi vioneshi – mfano: kijiji hiki, kile, mtoto yule,

    Vivumishi vya pekee – mfano: mtoto mwenyewe, yeyote,

    Vivumishi vya a-unganifu – mfano: nguo za shule, za kijana, wavulana

    Vivumishi vya jina kwa jina – mfano: mtoto kiziwi, kipofu,

    Vivumishi viulizi – mfano: shule gani, ipi,

    52. (a) Eleza maana ya Kiarifu katika sentensi.

    (b) Taja vipashio vyote vinavyounda kiarifu.

    Majibu:

    (a) Kiarifu ni sehemu ya sentensi inayojazwa na maneno yanayoarifu tendo lililofanywa, linalofanywa

    au litakalofanywa. Hutokea baada ya kiima.

    Mfano: Baba yangu | analima shambani

    A

    (b) Vipashio vinavyounda kiarifu ni:

    Aina zote za vitenzi

    Mfano: Juma analima, Juma alikuwa analima, Juma ni mtoto

    Shamirisho/kikundi jina

    Mfano: Juma anafundisha mtoto Kiswahili

    Chagizo/kikundi kielezi

    Mfano: mama anasoma kitabu polepole

    Juma anakimbia vibaya sana

    53. (a) Eleza maana ya kielezi.

    (b) Taja aina zote za vielezi

    (c) Eleza matumizi ya kielezi

    Majibu:

    (a) Kielezi ni neno au maneno yanayotoa taarifa zaidi kuhusu kitenzi, kivumishi au kielezi kingine.

    Mfano: Tulicheza vizuri, tulicheza vizuri sana, anasoma kitabu kizuri sana

    (b) Kuna aina nane za vielezi kama ifuatavyo:

    Vielezi vya namna/jinsi – mfano: John aliondoka kwa haraka

    Vielezi vya mahali – mfano: anaishi porini

    Vielezi vya idadi/kiasi – mfano: alimpiga mara nne

    Vielezi vya wakati – mfano: mvua imenyesha asubuhi

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 30

    (c) Matumizi ya vielezi ni:

    Kuonesha namna au jinsi tendo lilivyofanyika

    Kuonesha mahali tendo lilipotendekea

    Kuonesha wakati tendo lilipotendeka

    Kuonesha kiasi au idadi ya kutendeka kwa jambo

    Kuonesha sababu ya kutendeka kwa tendo

    54. Fafanua maana na dhima ya uambishaji katika lugha.

    Majibu:

    Uambishaji ni kitendo cha kupachika viambishi kwenye mzizi wa neno pasipokubadili kategoria ya

    neno husika. Viambishi vya uambishaji huitwa viambishi ambatishi na hutokea kwa wingi kabla ya

    mzizi wa neno.

    Mfano: Neno cheza = anacheza, walivyocheza, wachezavyo

    Dhima ya uambishaji katika lugha ni kama vile:

    Kupanua maana ya neno mfano: lima-analima-walilima-wanaolima-walimavyo

    Kudokeza nafsi mfano: amempiga

    Kutaja njeo mfano: atampiga

    Kutaja mtendwa mfano: aliyenisomea

    Kudokeza mtendewa mfano: tuliowaita

    Kudokeza urejeshi mfano: tulivuomkimbiza

    * Zipo dhima nyingi sana za uambishaji hizo ni chache tu.

    55. (a) Eleza maana ya viambishi.

    (b) Taja aina za viambishi katika lugha ya Kiswahili.

    Majibu:

    (a) Viambishi ni mofimu zinazopachikwa kwenye mzizi wa neno na kukamilisha muundo na maana

    ya neno. Viambishi huweza kupachikwa kabla na baada ya mzizi wa neno.

    (b) Viambishi katika Kiswahili ni vya aina kuu mbili ambazo ni:

    Viambishi awali/tangulizi: hivi ni vile ambavyo hutokea kabla ya mzizi. Huitwa viambishi

    awali kwa sababu huutangulia mzizi wa neno.

    Mfano: a-na-ye-soma

    Wa-li-vyo-ni-piga

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 31

    Viambishi tamati/fuatishi: ni vile vinavyotokea baada ya mzizi wa neno. Hufuata mzizi wa

    neno.

    Mfano: anawalim-ish-a

    Walivyoimb-ian-a

    56. Tenga viambishi vya maneno yafuatayo kisha eleza kazi ya kila kiambishi.

    (a) Anacheza

    (b) Umependa

    (c) Tuliongozana

    (d) Analimisha

    (e) Tutamwendeshea

    (f) Atapika

    (g) Amefika

    (h) Tumecheka

    (i) Waliompiga

    Majibu:

    (a) Anacheza = A-na-chez-a

    A = kiambishi awali cha nafsi ya tatu umoja, uyakinishi, kipatanishi cha kisarufi.

    na = kiambishi awali cha wakati uliopo hali ya kuendelea

    chez = mzizi wa neno

    a = kiambishi tamati maana.

    (b) Umependa = U-me-pend-a

    U = kiambishi awali nafsi ya pili umoja

    me = kiambishi awali wakati uliopita hali timilifu

    pend = mzizi wa neno

    a = kiambishi tamati maana

    (c) Tuliongozana = Tu-li-ongoz-an-a

    Tu = kiambishi awali nafsi ya kwanza wingi

    li = kiambishi cha wakati uliopita

    ongoz = mzizi wa neno

    an = kiambishi cha kauli ya kutendana

    a = kiambishi tamati maana

    (d) Analimisha = A-na-lim-ish-a

    A = kiambishi cha nafsi ya tatu umoja

    na = kiambishi cha wakati uliopo hali ya kuendelea

    lim = mzizi wa neno

    ish = kauli ya kutendesha

    a = kiambishi tamati maana

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 32

    (e) Tutamwendeshea = Tu-ta-mw-ende-sh-e-a

    Tu = nafsi ya kwanza wingi

    ta = wakati ujao

    mw = mtendewa/yambiwa

    ende = mzizi wa neno

    sh = kauli ya kutendesha

    e = kauli ya kutendea

    a = kiambishi tamati maana

    (f) Atapika = A-ta-pik-a

    A = nafsi ya tatu umoja

    ta = wakati ujao

    pik = mzizi wa neno

    a = kiambishi tamati maana

    (g) Amefika = A-me-fik-a

    A = nafsi ya tatu umoja

    me = wakati uliopita hali timilifu

    fik = mzizi wa neno

    a = kiambishi tamati maana

    (h) Tumecheka = Tu-me-chek-a

    Tu = nafsi ya kwanza wingi

    me = wakati uliopita hali timilifu

    chek = mzizi wa neno

    a = kiambishi tamati maana

    (i) Waliompiga = Wa-li-o-m-pig-a

    Wa = nafsi ya tatu wingi

    li = wakati uliopita

    o = kirejeshi cha watenda

    m = kiambishi cha mtendwa

    pig = mzizi wa neno

    a = kiambishi tamati maana

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 33

    57. Eleza maana na dhima ya mnyambuliko katika lugha.

    Majibu:

    Mnyambuliko ni kitendo cha kupachika viambishi kwenye mzizi wa neno na kubadili kategoria ya

    neno. Mnyambuliko huweza kutokea kabla au baada ya mzizi wa neno. Viambishi vya mnyambuliko

    huitwa viambishi nyambuaji.

    Mfano: cheza = chezeana, walichezesha, wanamchezea, mchezo, wachezaji

    Dhima ya mnyambuliko katika lugha ni:

    Kuzalisha maneno mapya kutokana na mzizi mmoja

    Kupanua maana ya neno kwa kubadili viambishi

    Kutambulisha kauili mbalimbali za vitenzi

    Kuwezesha vitenzi kubeba nomino moja au zaidi

    58. (a) Fafanua maana ya kiima katika sentensi.

    (b) Fafanua vipashio vinavyounda kiima.

    Majibu:

    (a) Kiima ni sehemu katika sentensi ambayo hujaza nafasi ya mtenda wa jambo linaloelezwa na

    hutokea kushoto mwa kitenzi katika sentensi.

    Mfano: Juma / alikuwa anakimbia

    K

    (b) Vipashio vya kiima ni kama ifuatavyo:

    Nomino peke yake mfano: Mtoto anacheza

    Nomino + kivumishi mfano: Mzee mrefu amefika

    Kiwakilishi peke yake mfano: Mimi ninaandika

    Kiwakilishi + kivumishi mfano: Yule mweusi amekamatwa

    Kitenzi jina + kivumishi mfano: Kucheza kwao kunavutia sana

    Nomino + kishazi tegemezi vumishi mfano: Mzee aliyeumia ametibiwa

    Nomino + kishazi tegemezi vumishi na nomino mfano: Mzee aliyeumia mguu ametibiwa

    59. (a) Nini maana ya kitenzi.

    (b) Kuna aina ngapi za vitenzi? Fafanua kwa mifano.

    Majibu:

    (a) Kitenzi ni neno linaloarifu jambo linalofanywa na mtu, kitu au kiumbe chochote chenye uwezo

    wa kutenda jambo.

    Mfano: Farida analima shamba, Maeda anafundisha Kiswahili.

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 34

    (b) Kuna aina kuu mbili za vitenzi ambazo ni:

    Vitenzi halisi: aina hii inahusisha vitenzi vikuu (T), vitenzi visaidizi (Ts)

    Vitenzi vishirikishi/husishi => t

    Vitenzi halisi hueleza matendo yanayofanyika.

    Mfano: kusema, kulima, kucheza, kuimba, n.k

    Kitenzi kikuu hubeba wazo kuu katika tungo.

    Mfano:

    Nyumba hii imeezekwa vizuri sana.

    Wanafunzi wamefuzu mtihani wao.

    Vitenzi visaidizi (Ts) husaidia kitenzi kikuu kukamilisha ujumbe fulani. Vitenzi visaidizi

    huweza kutokea zaidi ya kimoja katika tungo.

    Mfano:

    Baba alikuwa anataka kwenda kuoga

    Upepo ulikwisha ezua mapaa ya nyumba.

    Vitenzi vishirikishi (t) huonesha kuwepo au kutokuwepo kwa sifa au tabia fulani katika

    nomino au kiwakilishi kinachohusishwa.

    Mfano:

    Ibrahim ni mpole sana

    Gift si mkorofi

    Huyu ndiye mgeni rasmi

    60. (a) Eleza maana ya kiunganishi.

    (b) Taja aina za viunganishi.

    (c) Eleza matumizi ya kiunganishi.

    Majibu:

    (a) Kiunganishi ni neno au kikundi cha maneno chenye kuunganisha maneno, kikundi cha maneno,

    kishazi au sentensi.

    Mfano: Baba na mama wanalima

    Kuruka na kuimba ni kazi nzuri

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 35

    (b) Kuna aina mbili za viunganishi ambazo ni:

    Viunganishi huru (vinavyojitegemea) – mfano: kaka na dada wanacheza

    Viunganishi tegemezi (visivyojitegemea) – mfano: Ali-po-fika

    (c) Matumizi ya viunganishi ni kuunga vipashio viwili au zaidi vyenye hadhi sawa kisarufi.

    Mfano:

    Jina na jina = shangazi na mjomba wanalima

    Kishazi na kishazi = alichelewa kwa sababu alichelewa kuamka

    Sentensi na sentensi = Baba analima lakini mama anapika jikoni

    61. Eleza tofauti kati ya:

    (a) Kihisishi (H) na Kihusishi (KH)

    (b) Kitenzi kisaidizi na kitenzi kishirikishi

    (c) Shamirisho na chagizo

    Majibu:

    (a) Kihisishi (H) ni maneno yanayodokeza miguso ya moyo au ya akili. Vionjo vya moyo huweza

    kuwa vya furaha au huzuni, lakini vihusishi (KH) ni maneno yanayoonesha uhusiano baina ya

    neno moja na jingine au baina ya kikundi kimoja na kingine.

    Mfano wa kihisishi (H) ni: Kha! Ebo! Na mfano wa kihusishi ni (KH) ni chini ya, kwa ajili ya,

    wa.

    (b) Kitenzi kisaidizi (Ts) ni maneno yanayosaidia kitenzi kikuu (T) kukamilisha ujumbe lakini

    kitenzi kishirikishi (t) ni maneno yanayoonesha kuwepo au kutokuwepo kwa hali fulani.

    Mfano wa Ts ni: Juma alikuwa analima. Mfano wa kitenzi kishirikishi ni: ni, si, ndi, n.k.

    (c) Shamirisho (Sh) ni jina au kikundi cha jina kinachojaza nafasi ya mtenda katika tungo na

    hutokea baada ya kitenzi kikuu au kitenzi kishirikishi katika tungo hiyo lakini chagizo (Ch) ni

    neno au kikundi cha maneno ambacho hujaza nafasi ya kielezi katika mpangilio wa sentensi.

    Mfano wa (Sh) ni: Baba yangu analima shamba kubwa.

    Mfano wa Ch ni: Baba yangu amekwenda shambani

    62. Fafanua kauli mbalimbali zitumikazo katika vitenzi.

    Majibu:

    Kauli ya kutenda mfano: Lima, cheza, kimbia

    Kauli ya kutendwa mfano: pigwa, somwa, limwa

    Kauli ya kutendea mfano: imbia, somea, chezea

    Kauli ya kutendewa mfano: somewa, imbiwa, chezewa, limiwa

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 36

    Kauli ya kutendeana mfano: someana, chezeana, limiana, imbiana

    Kauli ya kutendeka mfano: imbika, pikika, chezeka, someka,

    Kauli ya kutendesha mfano: imbisha, somesha, kalisha, zolesha, washa, ogopesha, ogofya,

    lewesha, levya

    Kauli ya kutendana mfano: imbana, somana, chekana, pigana

    Kauli ya kutendua mfano: pindua, umbua, chomoa, tegua

    63. Kwa kawaida sentensi yoyote ile ya Kiswahili inajieleza katika hali kuu tano. Fafanua hali hizo.

    Majibu:

    Hali ya maelezo (taarifa) mfano: Mwanaisha anakimbia vizuri sana

    Hali ya kuuliza (swali) mfano: Baba amerudi?

    Hali ya kushangaa mfano: Mwaka umeisha!

    Hali ya ombi mfano: chukua kitabu hiki

    Hali ya amri mfano: kimbia

    64. Bainisha kiima na kiarifu katika sentensi zifuatazo:

    (a) Mwimbaji yule maarufu aliyepewa zawadi amefariki dunia

    (b) Kuimba kwake kunanifurahisha sana

    (c) Baada ya hotuba hatukufanya kazi tena

    (d) Mtoto aliyeumia mguu amelazwa hospitali

    (e) Kijana yule mwembamba sana amefeli mtihani

    Majibu:

    (a) Mwimbaji yule maarufu aliyepewa zawadi / amefariki dunia

    K A

    (b) Kuimba kwake / kunanifurahisha sana

    K A

    (c) Baada ya hotuba / hatukufanya kazi tena

    K A

    (d) Mtoto aliyeumia mguu / amelazwa hospitali

    K A

    (e) Kijana yule mwembamba sana / amefeli mtihani

    K A

    65. Sarufi imegawanyika katika sehemu kuu nne (4). Taja sehemu hizo na fafanua kazi ya kila moja.

    Majibu:

    Sarufi ni mfumo wa taratibu na kanuni zinazotawala matumizi sahihi ya lugha. Sarufi hugawanyika

    katika sehemu zifuatazo:

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 37

    (a) Sarufi matamshi/fonolojia – hushughulika na jinsi sauti za lugha zinavyotamkwa kwa kuchunguza

    mahali zinapotamkiwa na jinsi zinavyotamkwa. Sarufi matamshi ndiyo ghala la malighafi ya

    kuundia maneno ambazo ni fonimu. Hivyo bila sarufi matamshi hatuwezi kuunda maneno ya

    lugha. Mfano: neno baba linaundwa na fonimu = /b/, /a/, /b/, /a/

    (b) Sarufi maumbo/mofolojia – ni tawi la sarufi linaloshughulika na maumbo ya maneno jinsi

    yanavyoundwa na kazi za maneno hayo katika lugha. Sarufi matamshi ndiye mmiliki wa maumbo

    ya maneno. Hivyo bila mofolojia hatuwezi kuunda tungo kama sentensi. Mfano kutokana na

    maneno baba, shamba, analima, kubwa tunaweza kupata tungo kama:

    Baba analima shamba kubwa

    Baba analima shamba

    Baba analima

    (c) Sarufi miundo/sintaksia – ni tawi linaloshughulika na mpangilio na mfuatano wa vipashio ili

    kuleta tungo yenye maana inayokubaliwa au iliyokusudiwa. Sintaksia ni kama fundi wa ujenzi

    mwenye ujuzi wa kupangilia tofali (fonimu/maneno) ili kujenga ukuta ulionyoka. Ili kupata

    maumbo ya maneno yanayokubalika ni lazima mpangilio wa fonimu uwe sahihi na pia ili kupata

    sentnesi inayokubalika ni lazima mpangilio wa maneno uwe sawa na hiyo ni kazi ya sarufi miundo.

    Mfano:

    Neno abab halikubaliki lakini neno baba linakubalika kwa sababu ya mpangilio wa fonimu.

    Tungo mdogo baba shamba analima kubwa haikubaliki lakini baba mdogo analima

    shamba kubwa inakubalika kwa sababu ya mpangilio wake sahihi kwa sarufi ya Kiswahili.

    (d) Sarufi maana/semantiki – hushughulika na maana zinazobebwa na maneno au sentensi katika

    lugha. Maana huweza kuwa ya msingi au ya ziada hivyo ni kazi ya semantiki kupambanua maana

    zote zilizosetiriwa na tungo husika. Mfano: Mzee amewachezea wanangu tungo hiyo ina maana

    zaidi ya moja kama vile:

    Mzee amecheza ili kuwafurahisha

    Mzee amewaroga

    Mzee amewadhalilisha kwa kuwaingilia

    Mzee amecheza kwa niaba yao

    66. Onesha aina za maneno yanayounda sentensi zifuatazo:

    (a) Baba yake ni mfanyabiashara maarufu sana

    (b) Mji huu ni mchafu

    (c) Watoto hawakujua alimojificha kanga

    (d) Maeda alikuwa anataka kwenda kununua sukari dukani

    (e) Kiswahili kinaweza kufundishia masomo yote shuleni

    (f) Baba na mama tunawaheshimu sana

    (g) Nilikwenda kukopa kwa matajiri wangu

    (h) Karoli alikunywa maji machafu sana

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 38

    Majibu:

    (a) Baba yake ni mfanyabiashara maarufu sana

    N V t N V E

    (b) Mji huu ni mchafu

    N V t V

    (c) Watoto hawakujua alimojificha kanga

    N Ts T N

    (d) Maeda alikuwa anataka kwenda kununua sukari dukani

    N Ts Ts Ts T N E

    (e) Kiswahili kinaweza kufundishia masomo yote shuleni

    N Ts T N V E

    (f) Baba na mama tunawaheshimu sana

    N U N T E

    (g) Nilikwenda kukopa kwa matajiri wangu

    Ts T H N V

    (h) Karoli alikunywa maji machafu sana

    N T N V E

    67. Kwa kila sentensi zifuatazo ainisha vivumishi vilivyopigiwa mstari.

    (a) Watoto wazuri wanapanda ngazi.

    (b) Mzee yule mrefu mwembamba ni baba yangu mkubwa

    (c) Kwetu kuna bwana mmoja mchoma nyama

    (d) Ng’ombe wa maziwa amepotea

    (e) Watoto watano wamefuzu mtihani wa Kiswahili

    (f) Vijana wametunza nguo zao kabatini

    (g) Mwanafunzi hodari husoma kwa bidii

    Majibu:

    (a) wazuri = kivumishi cha sifa

    (b) yule = kivumishi kioneshi

    (c) mmoja = kivumishi cha idadi

    (d) wa maziwa = kivumishi cha A-unganifu

    (e) watano = kivumishi cha idadi

    (f) zao = kivumishi cha kumiliki

    (g) hodari = kivumishi cha sifa

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 39

    68. onesha aina za vielezi katika sentensi zifuatazo:

    (a) Aliahidi kumpenda Hidari daima dumu

    (b) Jumba lile limepasuka mara tano

    (c) Mtoto yule alinijibu kihuni

    (d) Huko Shinyanga kuna imani ya uchawi

    (e) Simfahamu vizuri yule mtu tuliyempita

    (f) Niwekee kikombe changu kabatini

    (g) Leo ni sikukuu ya mashujaa

    (h) Bunge hukutana mara kwa mara

    Majibu:

    (a) daima dumu = kielezi cha wakati

    (b) mara tano = kielezi cha idadi

    (c) kihuni = kielezi cha namna/jinsi

    (d) huko Shinyanga = kielezi cha mahali

    (e) vizuri = kielezi cha namna/jinsi

    (f) kabatini = kielezi cha mahali

    (g) leo = kielezi cha wakati

    (h) mara kwa mara = kielezi cha idadi/kiasi

    69. bainisha aina za maneno yaliyopigiwa mstari katika sentensi zifuatazo:

    (a) Kucheza kunafurahisha watazamaji

    (b) Anakusubiri kwa hamu sana

    (c) Hapa ndipo mahali mtakapokutania

    (d) Ng’ombe huyu ana matata sana

    (e) La haula! kijana yule ameuawa

    (f) Wewe ndiye kijana unipendezaye

    (g) Anatembea kwa maringo sana

    (h) Baba analima lakini mama anaimba nyimbo

    Majibu:

    (a) Kucheza = nomino (inatokana na kitenzi)

    (b) kwa hamu sana = kielezi

    (c) ndipo = kitenzi kishirikishi

    (d) huyu = kivumishi

    (e) La haula! = kihisishi

    (f) Wewe = kiwakilishi

    (g) lakini = kiunganishi

    70. Andika “E” kwa kielezi au “V” kwa kivumishi katika maneno yaliyopigiwa mstari katika

    sentensi zifuatazo.

    (a) Hata ndege hukaa wawili wawili

    (b) Viti hivi vizuri

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 40

    (c) Mariam anaimba vizuri

    (d) Macho yake malegevu

    (e) Kitanda cha cha kwanza kushoto ndicho amelalia

    (f) Mrembo yule asiye na kiuno amepewa zawadi

    Majibu:

    (a) E (b) V (c) E (d) V (e) V (f) V

    71. Bainisha viwakilishi vilivyomo katika sentensi zifuatazo:

    (a) Lile limetiwa rangi nyeupe

    (b) Nyinyi mlifanya uchaguzi vizuri

    (c) Ambao wamefika hapa ni wanasayansi

    (d) Wangu hawatafika mapema

    (e) Upi umepatikana?

    Majibu:

    (a) Lile = W-kioneshi

    (b) Nyinyi = W-nafsi

    (c) Ambao = W-cha urejeshi

    (d) Wangu = W-kimilikishi

    (e) Upi = W-kiulizi

    72. Tunga sentensi zenye vipashio vifuatavyo:

    (a) W + Ts + T + E

    (b) N + V + V + T + N + E

    (c) N + V + E + T + N + V + E

    (d) N + V + T + N + V + E

    (e) N + V + V + E + T + N + V

    Majibu:

    (a) Mimi nilikuwa naenda shuleni

    (b) Watoto wawili warefu wanasoma kitabu polepole

    (c) Mtoto aliyekuja jana ameweka kitabu kikubwa kabatini

    (d) Mwanafunzi hodari anasoma kitabu kizuri sana

    (e) Mwalimu mzuri aliyefika jana anafundisha somo zuri

    73. Eleza maana ya:

    (a) Kifungu tenzi

    (b) Njeo

    (c) Mzizi

    (d) Sentensi shurutia

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 41

    Majibu:

    (a) Kifungu tenzi (fT) ni kitenzi kinachoambatana na viambishi awali na viambishi tamati.

    Mfano: analima = a-na-lim-a

    Anayekuja = A-na-ye-kuj-a

    (b) Njeo katika kitenzi huwakilisha hali na wakati katika mpangilio wa vitenzi. Njeo hudokeza

    wakati wa utendekaji wa jambo.

    Mfano:

    Anapika = a-na-pika (na- ni njeo iliyopo hali ya kuendelea)

    Amelima = a-me-lima (me- inadokeza hali timilifu)

    (c) Mzizi ni sehemu ye neno isiyobadilika baada ya neno kufanyiwa mnyambuliko au sehemu ya

    neno inayobakia baada ya kuondolewa viambishi vyote awali na tamati.

    Mfano:

    Anasoma (mzizi = -som-)

    Tumemuona (mzizi = -on-)

    (d) Sentensi shurutia – ni sentensi inayotoa masharti kutokana na kubeba viambishi vya masharti

    ambavyo ni (ki, nge, ngeli na ngali).

    Mfano:

    Ukisoma kwa bidi utafaulu

    Angesoma kwa bidi angefaulu mtihani

    Mngeliwahi mapema mngelimkuta nyumbani

    Angalinisalimia ningalimuonesha

    74. Pigia mstari vitenzi vishirikishi katika sentensi zifuatazo:

    (a) Kiria ni mwanafunzi hodari sana

    (b) Msichana huyu si mkorofi

    (c) Joseph alikuwa mpole

    (d) Huyu ndiye kiongozi wetu

    (e) Wazee wa wakorofi

    (f) Embe li kabatini

    (g) Wewe u mlafi

    Majibu:

    (a) ni (b) si (c) alikuwa (d) ndiye (e) wa (f) li (g) u

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 42

    75. Eleza tofauti iliyopo baina ya mzizi wa kitenzi na shina la kitenzi.

    Majibu:

    Mzizi wa kitenzi ni sehemu ya neno inayobakia baada ya kuondolewa viambishi vyote awali na tamati

    lakini shina la kitenzi ni mzizi wowote uliofungiliwa kiambishi tamati maana.

    Mfano:

    Mzizi Shina

    Lim- Lima

    Chez- Cheza

    Imb- Imba

    Pig- Piga

    Som- soma

    76. Taja na fafanua tabia mbalimbali za vitenzi vya Kiswahili.

    Majibu:

    Kitenzi cha Kiswahili kina tabia tofautitofauti. Tabia hizo huonekana pale kitenzi kinapotoa taarifa

    mbalimbali. Tabia hizo ni:

    (a) Kutambulisha tendo linalotendeka mfano: cheza, imba, ruka, soma

    (b) Kutambulisha wakati kama vile: wakati uliopita, wakati uliopo, wakati ujao

    Mfano:

    Aliniona (li- wakati uliopita)

    Wanasoma (na- wakati uliopo)

    Tutamuona (ta-wakati ujao)

    (c) Kutambulisha nafsi

    Mfano:

    Ninasoma (ni-nafsi ya kwanza umoja)

    Tumefika (tu-nafsi ya kwanza wingi)

    Umeniona (u-nafsi ya pili umoja)

    Mmewahi (nafsi ya pili wingi)

    Analima (a-nafsi ya tatu umoja)

    Wanalima (wa-nafsi ya tatu wingi)

    (d) Kutambulisha hali ya tendo.

    Mfano:

    Anasoma (na- hali ya kuendelea)

    Amefundisha (me- hali timilifu)

    Husoma (hu- hali ya mazoea)

    Akiwahi tutaondoka (ki- hali ya masharti)

    (e) Kutambulisha kauli mbalimbali

    Mfano:

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 43

    Alinipigia (i – kauli ya kutendea)

    Anamsomesha (esh – kauli ya kutendesha)

    Watapigana (an- kauli ya kutendana)

    (f) Kuonesha urejeshi

    Aliyeimba (ye – urejeshi wa mtenda)

    Walivyoimba (vyo – kirejeshi cha watenda/namna)

    Kilicholetwa (cho – kirejeshi cha kitendwa)

    77. Kirai ni nini? Kwa kutumia mifano orodhesha aina tano (5) za virai unazozifahamu.

    Majibu:

    Kirai ni neno au kifungu cha maneno chenye neno kuu moja. Aina ya kirai hutambulishwa na neno

    kuu katika kirai husika. Kirai huwa ni kikubwa kuliko neno kihadhi na kidogo kuliko kishazi.

    Aina tano za virai ni kama zifuatazo:

    (a) Kirai nomino (KN) – mfano: watu wawili, baba mkubwa

    (b) Kirai kivumishi (KV) – mfano: mtu mzuri kabisa, kijana mweupe mrefu amefika

    (c) Kirai kitenzi (KT) – mfano: analima, anapika, tutamuona

    (d) Kirai kielezi (KE) – mfano: sana sana, jana jioni, polepole mno

    (e) Kirai kihusishi (KH) – mfano: kwa miguu, na mjomba, katika duka

    78. Fafanua sifa tatu za sentensi sahili.

    Majibu:

    Sentensi sahili ni ile yenye kishazi huru kimoja tu. Sifa za sentensi sahili ni kama vile:

    (a) Ina kiima ambacho kimetajwa wazi. Kiima hicho huweza kuwa jina, jina na jina au jina na

    kivumishi.

    (b) Ina kiarifu ambacho kimeundwa na kitenzi kikuu kimoja au kitenzi kishirikishi au kitenzi kisaidizi

    na kitenzi kikuu pamoja na shamirisho na chagizo.

    (c) Haifungamani na sentensi nyingine, na hivyo inajitosheleza kimuundo na kimaana.

    Mifano ya sentensi sahili ni:

    Paakwai analima shamba

    Haidari ni mzembe sana

    Hadija alikuwa anapika chakula

    Kamenge alikuwa anataka kwenda kumpiga mke wake

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 44

    79. Vifupisho vifuatavyo huwakilisha nini katika sarufi ya Kiswahili?

    (a) KH (b) Ch (c) Sh (d) K (e) A (f) KN (g) KE (h) t (i) Ts (j) fT

    Majibu:

    (a) KH = kirai kihusishi

    (b) Ch = chagizo

    (c) Sh = shamirisho

    (d) K = Kiima

    (e) A = kiarifu

    (f) KN = kikundi nomino/kirai nomino

    (g) KE = kikundi/kirai kielezi

    (h) t = kitenzi kishirikishi

    (i) Ts = kitenzi kisaidizi

    (j) fT = fungu tenzi

    80. (a) Lugha ni mfumo wa sauti nasibu ”Fafanua.

    (b) Je, wanyama wana lugha? Toasababu.

    Majibu:

    (a) Lugha husemwa ni nasibu kwa sababu kuu zifuatazo:

    Mwanadamu huwa hazaliwi na lugha bali hukutana nayo katika mazingira yake kwa bahati tu na kujifunza.

    Hakuna kikao kilichowahi kukaa na kuamua juu ya kutumiwa lugha, lugha ilizuka tu.

    Hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya maneno ya lugha na maumbo ya vitu halisi. Mfano: neno “maji” halina uhusiano na kile kinachoitwa kwa neno hilo bali ni mazoea tu ya

    watumiaji lugha.

    (b) Wanyama hawana lugha kwa sababu hawana sifa za kumudu lugha kama mfumo wa mawasiliano. Lugha ni mali ya mwanadamu pekee na hutawaliwa na sifa zifuatazo.

    Sauti: Lugha huambatana na sauti za binaadamu kutoka kinywani mwake. Binaadamu lazima atamke

    jambo kwa kutoa sauti, zinazotamkwa kwa utaratibu maalumu kutoka kwenye maumbile yaliyo

    ndani ya mwili wa mwanaadamu hususan kinywa, ambayo kiisimu huitwa ala za sauti.

    Lugha ni lazima imhusu MwanadamuKimsingi hakuna kiumbe kisichokuwa mwanaadamu

    (mtu) kinachoweza kuzungumza Lugha. Lugha ni chombo maalumu wanachokitumia binaadamu

    kwa lengo la mawasiliano.

    Lugha huzingatia utaratibu maalum;Sauti za lugha yoyote huwa zimepangwa kwa kufuata

    utaratibu fulani unaokubaliwa

    na jamii ya watu wanaotumia lugha inayohusika. Kwa maneno mengine, si kila sauti

    itokayo kinywani mwa mwanaadamu kuwa ni lugha. Sauti za vilio vya watoto, hoi

    hoi na vigelegele vya waliofurahi, vikohozi vya wagonjwa wa pumu na vifua,

    vicheko na kelele nyenginezo haziwezi kuitwa lugha.

    Utaratibu huo maalumu unaofuatwa na lugha za wanaadamu huitwa sarufi.

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 45

    Lugha hufuata misingi ya fonimu Wanaisimu wanakubaliana kwa ujumla kwamba fonimu ni

    sauti yenye uwezo wa

    kuleta tofauti katika maana ikipachikwa katika neno la lugha husika. Dhana ya

    fonimu inatarajiwa kuzungumziwa kwa kirefu sana katika muhadhara wa sabaa. Kwa

    mfano baadhi ya fonimu za Kiswahili ni .

    /a/, /e/, /i/, /o/, /u/, kama zinavyoweza kubadilisha maana katika maneno

    yafuatayo:-/tata/~ /teta/~/tita/~/tota/~ /tuta/.

    /p/, /b/, /t/, /d/, /c/, /k/, /g/, /s/, /z/. kama zinavyoweza kubadilisha maana

    katika maneno yafuatayo:-pawa~ bawa~ tawa~ dawa~ chawa~ jawa~ kawa~ sawa~ zawa, n.k

    Lugha hufuata mpangilio wa vipashio unaoleta maana Muundo wa Lugha huwa unafuata

    mpangilio wa vipashio vyake maalumu na

    lazima vipashio hivyo vifahamike. Mpangilio wa vipashio huo huanza na

    fonimu, neno ambalo huundwa kwa mkusanyiko wa silabi au muunganiko wa

    mofimu mbalimbali, kirai, kishazi na sentensi

    Lugha inajizalishaVipashio vinavyoiunda lugha husika huwa na sifa ya kuweza

    kunyumbulishwa ili

    kupata maneno mapya. Kwa mfano vitenzi hunyambulishwa kwa kuongezwa

    viambishi nz kwa hivyo, lugha hujiongezea maneno mapya. Kwa mfano tuangalie

    mifano ifuatayo.

    i) chez-a-------ku-chez-a-------ku-m-chez-a-------tu-li-m-chez-a.

    ii) chez-e-a-------chez-ek-a----------chez-e-an-a-------chez-esh-a-------chez-w-a

    iii) chez-esh-a- chez-esh-an-a- chez-esh-e-an-a

    Lugha husharabu

    Lugha husharabu kwa maana ya kwamba huchukuwa maneno kutoka lugha

    nyengine ili kujiongezea msamiati wake.Tabia hii inazisaidia sana Lugha

    zinazokua.

    81. Kwa kutumia mifano miwili kwa kila muundo, taja miundo mine ya silabi. Majibu

    a) Muundo wa kwanza ni ule unaojengwa na irabu peke yake.(I)

    Hebu chunguza mifano ifuatayo:

    silabi “a” katika neno “angalia” $a$ $nga$ $li$ $a$

    silabi “u” katika neno “ugua” $u$ $gu$ $a$

    silabi “I” katika neno “niite” $ni$ $i$ $te$

    b) Muundo wa silabi wa Konsonanti na Irabu. (KI)

    Mifano :

    Zungumza =$zu$ $ngu$ $m$ $za$

    Tapatapa =$ta$ $pa$ $ta$ $pa$

    Maliza = $ma$ $li$ $za$

    c) Muundo wa silabi wa Konsonanti, kiyeyusho na irabu (KkI)

    Mifano:

    Bwana =$bwa$

    Fyata =$fya$

    Mpya =$pya$

    Upwa =$pwa$

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 46

    Ukwezi =$kwe$

    d) Muundo wa silabi wa konsonanti, konsonanti na irabu (KKI)

    Mifano:

    Mwandani =$nda$

    Chongo =$cho$ $ngo$

    Nguru =$ngu$

    Daftari =$fta$

    Boksi =$ksi$

    Sekta = $kta$

    82. Chunguza kwa makini nomino zifuatazo. Kisha kwa kuzingatia aina za nomino, tenganisha

    nomio hizo katika makundi yake: mbuzi, Ashura, usingizi, kijiko, Januari, jeshi, matatizo,

    Zanzibar, kamati, Mungu.

    Majibu:

    AINA ZA NOMINO NOMINO

    Nomino za Pekee Ashura, Januari, Zanzibar,

    Nomino za Kawaida Mbuzi, kijiko,

    Nomino za wingi Matatizo,

    Nomino za Jamii Jeshi, kamati,

    Nomino dhahania Usingizi, Mungu

    83. Changanua sentensi ifuatazo kwa kutumia njia ya jedwali.

    Mwizi aliyeiba jana amekamatwa

    Majibu:

    S. Changamano

    K

    A

    KN

    KT

    N

    V

    E

    T

    Mwizi aliyeiba ja

    n

    a

    amekamatwa

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 47

    84. Moja ya faida za misimu ni kuhifadhi historia ya jamii. Toa mfano mmoja wa misimu zagao

    iliyovuma Tanzania katika vipindi vifuatavyo:

    Majibu:

    (a) Miaka ya Azimio la Arusha

    Kabaila

    Bwanyenye

    Ukupe

    Mchumia tumbo

    Ujamaa

    Kujitegemea

    (b) Njaa ya mwaka 1974/1975

    Unga wa yanga

    Kufunga mkanda

    kumbakumba

    (b) Kipindi cha mfumo wa vyama vingi

    Ngangari

    Wapambe

    Wakereketwa

    Wafurukutwa

    (c) Awamu ya tano ya serikali ya Tanzania

    Hapa kazi tu

    Vyuma vimekaza

    85. Sentensi zifuatazo zina makosa, zichunguze kwa makini kisha uziandike kwa usahihi.

    Majibu:

    a) Ninyi wote mmechelewa

    Sahihi: Nyinyi nyote mmechelewa

    b) Wanafunzi waliyosoma wamefaulu

    Sahihi: Wanafunzi waliosoma wamefaulu

    c) Ngombe zake zimeuzwa

    Sahihi: Ng’ombe wake wameuzwa

  • www.mwalimuwakiswahili.co.tz || MWL. MAEDA || 0717104507 48

    d) Walimu wamewakilisha michango yao

    Sahihi: Walimu wamewasilisha michango yao.

    UFAHAMU NA UTUNGAJI

    86. (a) Eleza maana ya ufahamu.

    (b) Taja aina za ufahamu.

    Majibu: