Upload
others
View
3
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
Lesson 2 for January 11, 2020
“Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimuna hekima; Danielii naye alikuwa na ufahamukatika maono yote, na ndoto” (Danieli 1:17)
Nebukadreza aliingia Yerusalemu mara tatu ili kuitawala.
Mara ya mwisho ilikuwa 586 KK. Yerusalemu iliharibiwa naWaisraeli wakachukuliwa hadi Babeli.
Mara ya pili ilikuwa 597KK. Mfalme akachukuwamafundistadi na wafuavyuma na watu wengine muhimu(akiwemo Ezekieli).
Mara ya kwanza ilikuwa 605KK. Wana wa watuwalichukuliwa hadi Babeli. Nia ilikuwa kuwafundisha“ubabeli” hao wana ili wawe waaminifu kwa Babeli. Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria walikuwa sehemu ya kundi hili.
Mungu anadhibiti. Danieli 1:1-2, 21
Mafunzo:
Upagani. Danieli 1:3-7
Chakula. Daniel 1:8-16
Matokeo:
Kamili. Danieli 1:4, 17
Bora. Danieli 1:18-20
“Bwana akamtia Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, katika mkonowake, pamoja na baadhi ya vyombo vya nyumba ya Mungu; naye akavichukua mpaka nchi ya Shinari, mpaka nyumba yaMungu wake; akaviingiza vile vyombo katika nyumba ya munguwake (Danieli 1:2)
Mungu wa kweli aweza kuonekana kushindwa na mkimbiziambaye hawezi kuwalinda watu wake.
Hata hivyo, maelezo “Bwana akamtia…” yanabadilisha kila kitu.
Mungu alikuwa akitumia Babeli kuadhibu kufuru yawatu Wake (Habakuki 1:5-11).
Mungu anadhibiti historia. Alizuia adhabu kwa miaka 70.
Alimtumia Koreshi kuwapatia uhuru watu Wake.(Ezra 1:1).
Tunaweza kuwa na uhakikakwamba mara zote Munguatadhibiti historia. Atawalindawatu Wake hadi mwisho, mpakakurudi Kwake mara ya pili.
“Mkuu wa matowashi akawapa majina; alimwita Danieli Belteshaza na Hanania akamwitaShadraka; na Mishaeli akamwita Meshaki; na Azaria akamwita Abednego. Danieli 1:7)
Nebukadreza alitaka kuwageuza wana wa kifalme wa Kiebrania kuwa Wababeliwaaminifu. Alijaribu kugeuza mawazo yao na ibada.
Alibadili makaoyao, kutokaYerusalemu
nyenyekevu kwaBabeli yenye
anasa.
Alibadili majinayao,
akaunganishautambulisho
wao na miunguya Babeli.
Alibadili elimuyao, na
kuwafundishautamaduni nadini ya Babeli
Alibadili chakulachao, kuwafanya
waabudu miungu yaBabeli
Kama wangekubali yote hayo, wangekuwa wanawa kifalme wa utumishi wa umma. Je wangeuzakanuni zao kwa wepesi wa maisha na ya anasa?
“Lakini Danieli aliazimu moyonimwake ya kuwa hatajitia unajisikwa chakula cha mfalme, walakwa divai aliyokunywa; basiakamwomba yule mkuu wa
matowashi ampe ruhusa asijitieunajisi.” (Danieli 1:8)
Inavyoonekana, vjana waKiebrania hawakuwezakufanya lolote la kujizuiana mabadiliko.
Hata hivyo, Danielihakuwa tayarikujisalimisha kwa vituambavyo vilikuwakinyume na imani yake .
Chakula cha mfalme kilijumuisha nyamaambazo zilikuwa zimekatazwa na Mungu(Walawi 11).Vyakula hivyo vilikuwa vimetolewa kafara kwamiungu ya Babeli. Kula chakula hicho ilikuwa nisehemu ya ibada (Mdo 15:28-29).
Daniel alishauri aina ya chakula ili kujiepusha na masualayote.
Pamoja na hayo, aliomba kunywa kitu kitakachomuwezeshakufikiri kwa umakini.
Zaidi ya yote, alimtumaini Mungu. Aliamini kuwa Atatendajambo la kushangaza katika kipindi kifupi (siku kumi).
"Kuna wengi kati ya watu wanaodai kuwa Wakristo
leo ambao wangeamua kwamba Danieli alikuwa mtu
wa pekee na wangemtangaza kuwa mfinyu na
king’ang’anizi wa imani. Wanazingatia suala la kula
na kunywa kwa matokeo kidogo sana kuhitaji
msimamo kama huo, ambao unahusisha na kujitolea
kwa faida yo yote ya kidunia. Lakini wale
wanaofikiria hivyo watajikuta siku ya hukumu
kwamba waligeuka kutoka kwenye matakwa ya
wazi ya Mungu kwa kuanzisha maoni yao kama
kiwango cha haki na kosa. Watagundua kuwa kile
kilichoonekana kwao kuwa cha maana
hakikuzingatiwa sana na Mungu. Matakwa yake ni ya
kutii."
E.G.W. (Counsels on Health, p. 69)
“Basi kwa habari za hao vijana wane, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katikaelimu na hekima; Daniel naye alikuwa naufahamu katika maono yote, na ndoto.”
(Danieli 1:17)
Ashpenazi alichagua vijana “wasiokuwana kasoro ya maumbile” (Danieli 1:4). Hiiilikuwa ni alama ya kafara ya shukrani yaNabukadreza kwa mungu wake Marduki.
.Vijana wote walikuwa hawana dosarikimwili au kiakili. Hata hivyo ni wanne tuwalioonyesha kutokuwa na dosari kiroho.
Mungu alizawadia uaminifu wao kwakuwapatia nyuso nzuri na maarifa kulikovijana wengine wa Kiebrania (f15, 17).
Mungu pia hutupatia hekima tukidumukuwa waaminifu Kwake katika dunia iliyoharibiwa na visa vya kutunga na uongo.
BORA
Walilazimika kujifunza mambo yaliyo kinyumena imani zao. Kwa sasa, sisi pia tunalazimikakujifunza mambo mabaya yanayofundishwakama kweli .
Mungu anadhibiti historia
Mungu hutupatia hekima ya kushinda mazingira yenye uhasama
Mungu huwazadia wale wote wanaoamua kumtii bila kujali hali/mazingira
Shukrani kwa maamuzi waliyofanya kutetea Imani yao, Mungu aliwabariki kwa kuwapatia maarifa naujuzi bora. Walifaulu mitihani yao kwa heshima!
Tunaweza kujifunza yafuatayo kutokana na uzoefuwao:
“Daniel alikabiliwa na majaribu magumu
ambayo yanaweza kushambulia vijana wa leo;
lakini bado alikuwa mkweli kwa mafundisho
ya kidini aliyoyapokea mapema katika maisha
ya utotoni. Alizungukwa na vishawishi
vilivyohesabiwa kupindua wale ambao
watayumba kati ya kanuni na mwelekeo;
lakini bado neno la Mungu linamuelekeza
kama aliye na tabia isiyo na hatia. Daniel
hakuthubutu kuamini nguvu yake mwenyewe
ya uadilifu. Maombi kwake yalikuwa jambo la
lazima. Alimfanya Mungu kuwa nguvu yake,
na hofu ya Mungu ilikuwa mbele yake katika
shughuli zote za maisha yake.”
E.G.W. (Fundamentals of Christian Education, cp. 8, p. 78)