Upload
others
View
41
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
1
Agricultural Non State Actors Forum
KAULI YA WADAU KUHUSU
MAENDELEO YA SEKTA YA MIFUGO
TANZANIA
2
KAULI YA WADAU KUHUSU MAENDELEO YA SEKTA YA MIFUGO TANZANIA
Wito wa kuchukua Hatua
Katika kauli hii, wadau waliotia saini (asasi za kiraia, wafugaji, watafiti, watu binafsi, vyama vya wakulima na
wadau wengine) wanatoa wito wa kuchukua hatua pamoja na wanabainisha mapendekezo yaliyomo katika
mkakati wa uchechemuzi wa kisera unaozingatia upekee na fursa za maendeleo zilizomo katika sekta ya
mifugo nchini Tanzania.
Muhtasari
Sekta ya mifugo ni mhimili wa ukuaji wa uchumi nchini Tanzania ambako asilimia 50 ya kaya hutegemea aina
fulani ya mifugo kama chanzo cha sehemu au kipato chao chote.1
Tanzania ni nchi ya tatu kwa kuwa na idadi kubwa ya mifugo barani Afrika baada ya Ethiopia na Sudan, Wakati
bidhaa mbalimbali za mifugo—kama vile maziwa, nyama, kuku, mayai na bidhaa za Ngozi—huzalishwa
Tanzania, bado nchi hii inategemea uagizaji wa bidhaa hizo kutoka nje ili kukidhi ongezeko la mahitaji yake.
Leo hii, sekta ya mifugo inahitaji kupewa msukumo mkubwa kuliko wakati mwingine wowote ili sekta iweze
kuwa kichocheo cha ukuaji wa maendeleo jumuishi nchini.
Sekta ya mifugo inaonekana kuchangia kufikia Dira ya Maendeleo Tanzania ya mwaka 2025. Uchambuzi
uliofanywa hivi karibuni umeonesha kuwa sekta hii huchangia kati ya asilimia 7.4 hadi asilimia 10 ya pato la
taifa2, japokuwa bajeti inayotengwa kwa ajili ya maendeleo ya sekta hii imebakia kuwa ndogo na kuendelea
kushuka hadi kufikia TZS 10.6 bilioni kwa mwaka wa fedha 2016/17. 3 Sekta ya mifugo inakua na kubadilika
kwa haraka sana wakati huo huo mahitaji ya chakula na malighafi yatokanayo na mifugo ikiongezeka mara
dufu kunakochangiwa na ongezeko la idadi ya watu wa kipato cha kati pamoja na ukuaji wa miji. Uwezo na
mchango wa sekta ya mifugo katika kufikia malengo ya maendeleo ni kiashiria cha fursa ya kipekee katika
kuleta mabadiliko makubwa.
1 Ministry of Livestock and Fisheries “Smallholder Livestock Sector: A review based on the 2012/13 National Panel Survey, February 2016: http://www.mifugouvuvi.go.tz/wp-2 Ministry of Livestock and Fisheries “The State of Livestock Development in Tanzania: Evidence from the 2012/13 National Panel Survey” presentation. May 2015 TLMI Workshop3 ANSAFs analysis of the Ministry of Agriculture Food Security and Cooperatives’ (MAFSC) budget and the 2015/16 and 2016/17 livestock development budgets
Printed by iprint Ltd
Photos used byGoogle and Shutterstock
i
Usuli
Uzalishaji wa mifugo nchini Tanzania, kama ulivyo uzalishaji wa mazao, hufanywa zaidi na wafugaji wadogo na
wachungi wa asili, wengi wao wakiwa wanawake, wanaokumbana na changamoto za upatikanaji wa pembejeo,
huduma za ugani na masoko. Mifugo mara nyingi hutumiwa kama dhamana miongoni mwa mamilioni ya
familia wasioweza kupata huduma rasmi za kifedha pamoja na wanawake wasiomiliki ardhi.
Kwa mara nyingi ni asilimia 20 tu ya wafugaji na wakulima wadogo nchini ndio wanaoweza kupata huduma za
ugani na wachache wanamiliki mifugo walioboreshwa na wanaozalisha kwa tija. 4 Wafugaji wengi huhangaika
na magonjwa yanayozuilika kutokana na kukosa huduma za chanjo zenye viwango ambapo asilimia 50
wanaripotiwa kutofikiwa na huduma za afya ya mifugo. 5Kwa nyongeza, kumekuwa na aina mbali mbali za
sera zinazoleta madhara katika ufanisi wa sekta binafsi kwa namna tofauti tofauti na kwa sekta ya mifugo kwa
ujumla kama vile kodi zinazohusiana na ufugaji, viwanda vidogo vidogo, nishati na miundombinu, uagizwaji
wa vifaa vya uzalishaji na vifungashio.
6Uzalishaji mdogo usio wa kawaida huenda ukaathiri mahitaji ya vyakula vitokanazo na mazao ya mifugo
pamoja na maligafi yake nchini, na ukweli ni kwamba mifugo ina mchango muhimu sana katika kipato na
maisha ya familia maskini.
Sekta ya mifugo Tanzania ina nafasi kubwa katika kukuza ukuaji wa uchumi lakini kuna haja kubwa ya serikali
kuongeza uwekezaji wake pamoja na kutengeneza mazingira wezeshi kwa wafugaji wadogo na wale wa asili
kulifikia lengo hili.
Mapendekezo
Mapendekezo yaliyopo hapa chini kwa pamoja yamefanywa na kikundi cha wadau wa mifugo ikijumuisha
Asasi za Kiraia, Wafugaji, watafiti, watu binafsi, vyama vya wakulima na wadau wengine waliohudhuria mkutano
uliowezeshwa na Jukwaa huru la Wadau wa Kilimo(ANSAF) na TrustAfrica, iliyofanyika mjini Dodoma mnamo
tarehe 21 Febuari 2017.
Mapendekezo haya hutoa mfumo wa kushirikisha wakulima wadogo na wafugaji wa asili katika sekta ya
mifugo kuinua mchango wao katika kuinua uchumi wa Tanzania.
Kuutambua kwa mapana mchango mkubwa wa mifugo kwa uchumi wa taifa na hivyo kutafsiriwa katika
ongezeko la uwekezaji wa serikali na sekta binafsi kuisaidia sekta hii. Kuwekeza kwa wazalishaji wadogo
inaweza kuongeza kasi ya ukuaji wa sekta ya mifugo na kuwa chachu ya ukuaji wa uchumi, uhakika wa chakula
na lishe nchini, kukidhi mahitaji ya vyakula vya asili ya mifugo yanayoongezeka na kupunguza umaskini.
Mwonekano wa kimkakati wenye kujali mchango wa sekta ya mifugo katika uchumi wa Tanzania na Jumuiya
ya Afrika Mashariki lazima uwe kivutio cha kuongezeka kwa uwekezaji wa rasilimali za serikali na za sekta
binafsi pamoja na utengenezaji wa sera na mikakati za kuwezesha kuwaunganisha wote pamoja.
Kuongeza ushiriki wa wadau wasio wa serikali katika kutambua na kuunda sera za mifugo rafiki kwa wakulima
wadogo na wafugaji wa asili chini. Inafahamika dhahiri kuwa uboreshaji wa mifugo, huduma za afya na
mikakati ya malisho pamoja na upatikanaji wa huduma za ugani na masoko husaidia kuwezesha wakulima 4 Ministry of Livestock and Fisheries “Smallholder Livestock Sector: A review based on the 2012/13 National Panel Survey, February 2016: http://www.mifugouvuvi.go.tz/wp-content/
uploads/2016/04/1_MALF_Tanzania_smallholder_livestock_sector_Report.pdf5 Ministry of Livestock and Fisheries “Smallholder Livestock Sector: A review based on the 2012/13 National Panel Survey, February 2016: http://www.mifugouvuvi.go.tz/wp-content/up-
loads/2016/04/1_MALF_Tanzania_smallholder_livestock_sector_Report.pdf6 ANSAF, “Final Budget Analysis 2015-2016
ii
wadogo na wafugaji wa asili kuongeza uzalishaji kukidhi ongezeko la mahitaji ya bidhaa za mifugo. 7 Vivyo
hivyo, kupunguzwa kwa gharama sizizo za lazima katika mnyororo wa thamani ina manufaa kwa wakulima
wadogo na wafugaji wa asili katika kuwasaidia kukidhi ongezeko la mahitaji kupitia uzalishaji wa ndani. Kupitia
mjadala mpana na ushirikiano kati ya asasi za kiraia, serikali, sekta binafsi na wadau wengine huwezesha zaidi
taarifa za kuimarisha uthibiti wa kimazingira kwa wakulima wadogo na wafugaji wa asili kujumuishwa katika
kukuza mnyororo wa thamani na viwanda na muunganiko imara.
Ushiriki wa Wanawake na Vijana katika Mnyroro wa thamani wa mifugoWakati wanawake ni wadau wakuu katika
uzalishaji wa maziwa na kuku8, sera za mifugo hazielezi dhahiri ni kwa jinsi gani wanawake wanawezeshwa
kushiriki kiufanisi katika sekta hii. Pia, sekta ya mifugo inatoa fursa nyingi za ajira kwa vijana wajasiriamali lakini
bado hazijatumika ipasavyo. Ushirikishwaji wa wanawake na vijana katika mnyororo wa thamani wa mifugo
hautaishia kuboresha maisha yao tu, bali pia utachangia kufikia malengo ya taifa ya uhakika wa chakula na
lishe bora.
Kuhakikisha uwajibikaji wa uwekezaji wa sekta binafsi katika kutekeleza ushirikishwaji wa wafugaji wadogo na
wafugaji wa asili kuhusu fursa za maendeleo katika sekta ya mifugo. Wakati sekta binafsi inaongeza uwekezaji
katika kukuza uzalishaji wa sekta ya mifugo na uwekezaji mwingine muhimu, kuna ulazima wa kuendelea
kutetea maendeleo jumuishi katika sekta ya mifugo kama vile zile zilizo chini ya Mpango wa Kuendeleza
Kilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania(SAGCOT) na ule Mkakati Madhubuti wa Maendeleo ya Mifugo (TLMP).
Mipango hii lazima ilete manufaa ya pamoja kwa wakulima wadogo na kwa wafugaji pia. Uzalishaji endelevu
ulio wazi ni sehemu muhimu katika kufikia uwajibikaji wa kimaendeleo wa sekta binafsi kwa sekta ya mifugo.
Waraka huu umepitishwa na makundi pamoja na watu binafsi wanaounda mtandao wa uchechemuzi unaojali
kanuni mbali mbali za kisera ili kuleta ushirikishwaji na uwazi wa mabadiliko katika sekta ya mifugo.
7 Ministry of Livestock and Fisheries “The State of Livestock Development in Tanzania: Evidence from the 2012/13 National Panel Survey” presentation. May 2015 TLMI Workshop8 Ministry of Livestock and Fisheries “The State of Livestock Development in Tanzania: Evidence from the 2012/13 National Panel Survey” presentation. May 2015 TLMI Workshop