Upload
others
View
46
Download
1
Embed Size (px)
Citation preview
Je, Walimu Wetu wana Sifa za Ualimu na Hamasa ya Kufundisha?
Ripoti ya utafiti kuhusu sifa za walimu kitaaluma, hamasa na moyo walio nao
katika kufundisha na athari zake katika kutoa elimu bora
Oktoba, 2011
Je, Walimu Wetu wana Sifa za Ualimu na Hamasa ya Kufundisha?
Ripoti ya utafiti kuhusu sifa za walimu kitaaluma,
hamasa na moyo walio nao katika kufundisha na athari zake katika kutoa elimu bora
Oktoba, 2011
iv
Shukrani
Utafiti huu ni jitihada za pamoja kati ya HakiElimu na Idara ya Saikolojia ya Elimu na Mafunzo ya Mitaala
ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kwa ushirikiano na Wafanyakazi wa HakiElimu Dk. Kitila Mkumbo
aliandaa mpango na tafiti pendekezo na kutoa mafunzo kwa wafanyakazi kuhusu njia za ukusanyaji wa
taarifa. Pia alisimamia mchakato mzima wa utafiti na kuandika ripoti kuu.
Wafanyakazi wafuatao walifanya kazi ya utafiti kwa kutembelea maeneo ya utafiti kwa lengo la kukusanya
data: Elizabeth Missokia, Daniel Luhamo, Charles Mtoi, Robert Mihayo, Glory Mosha, Fausta Musokwa,
Naomi Mwakilembe, Edwin Mashasi, Benedicta Mrema, Boniventura Godfrey, Lilyan Omary, Anastazia
Rugaba, Frederick Rwehumbiza, Nyanda Shuli, Vicent Mnyanyika na Esther Mashoto.
Ripoti hii iliandikwa na Dk. Kitila Mkumbo. Uhariri, tathmini pamoja na ushauri vilitolewa na Elizabeth
Missokia, Mtemi Gervas Zombwe, Robert Mihayo na Tony Baker.
Kazi hii isingefanikiwa bila ya ushirikiano wa wanafunzi, wazazi, wajumbe wa kamati za shule, walimu
pamoja na wafanyakazi katika ofisi za wilaya ambao tulifanya nao mahojiano. Tunawashukuru sana kwa
michango yao pamoja na utayari wao kufanya kazi nasi.
© HakiElimu 2011
ISBN: 978-9987-18-019-6
HakiElimu, S.L. P 79401, Dar es Salaam, Tanzania
Simu: (255 22) 2151852/3, Faksi: (255 22) 2152449
Sehemu yoyote ya ripoti hii inaweza kunukuliwa kwa ajili ya matumizi ya elimu na si ya kibiashara, ili mradi tu
chanzo kitatajwa na kwamba nakala mbili zitatumwa HakiElimu.
v
Yaliyomo
Majedwali na Vielelezo . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . vi
Majedwali . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . vi
Vielelezo . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . vi
Sehemu ya Kwanza: Usuli wa tatizo la utafiti . . . . . . . . . . . . . . . . . 1
1.1 Utangulizi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 1
1.2 Malengo ya utafiti . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 3
Sehemu ya Pili: Methodolojia ya utafiti . . . . . . . . . . . . . . . . . . 4
2.1 Mbinu . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 4
2.2 Maeneo ya utafiti . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 4
2.3 Sampuli na washiriki wa utafiti . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 4
2.4 Zana za kukusanyia data . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 5
2.5 Uchambuzi wa data . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 5
Sehemu ya Tatu: Matokeo ya utafiti . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 6
3.1 Matokeo kuhusu miongozo ya taarifa za shule . . . . . . . . . . . . . . 6
3.1.1 Taarifa kuhusu shule zilizotafitiwa . . . . . . . . . . . . . . . . . . 6
3.1.2 Ufaulu wa wanafunzi kitaaluma kwa kuzingatia umiliki wa shule . . . . . . . . . 8
3.1.3 Uhusiano kati ya sifa za waalimu kitaaluma na ufaulu wa wanafunzi kitaaluma . . . . 8
3.1.4 Tofauti ya ufaulu kwa kigezo cha zana za kufundishia na kujifunzia . . . . . . . 9
3.2 Hamasa na moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kazi ya ualimu . . . . . . 10
3.2.1 Taarifa kuhusu waalimu . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 10
3.2.2 Ushiriki wa waalimu katika programu za kuendeleza waalimu kitaaluma . . . . . . 11
3.2.3 Hamasa na mitazamo ya waalimu kuhusu ualimu . . . . . . . . . . . . . 12
3.2.4 Moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kazi ya ualimu . . . . . . . . . . . 15
3.2.5 Kiwango cha moyo wa kujitolea wa waalimu kwa kigezo cha umiliki wa shule . . . . 17
3.2.6 Moyo wa kujitolea na kuridhika na ualimu kwa kigezo cha jinsia . . . . . . . . 19
3.2.7 Moyo wa kujitolea na kuridhika na ualimu kwa kuzingatia uzoefu
na masomo ya kufundisha . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 20
3.3 Ufanisi wa uongozi wa shule . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 21
3.4 Muhtasari: Uhusiano uliopo baina ya ufaulu wa shule kitaaluma na sifa
za waalimu kitaaluma, moyo wao wa kujitolea kwa kazi ya ualimu na maoni
yao kuhusu ufanisi wa uongozi wa shule . . . . . . . . . . . . . . . . 22
3.5 Maoni ya waalimu kuhusu kazi ya ualimu: Matokeo ya Majadiliano ya Vikundi . . . 23
3.5.1 Utangulizi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 23
3.5.2 Kwa nini waalimu walichagua kazi ya ualimu . . . . . . . . . . . . . . . 23
3.5.3 Mitazamo ya waalimu kuhusu kazi ya ualimu . . . . . . . . . . . . . . . 25
3.5.4 Mitazamo ya waalimu kuhusu wanafunzi kufanya vibaya kitaaluma
na nini kifanyike kuboresha kiwango cha elimu . . . . . . . . . . . . . . 27
Sehemu ya Nne: Muhtasari, Hitimisho na Mapendekezo . . . . . . . . . . . . . 30
4.1 Muhtasari . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 30
4.2 Hitimisho na mapendekezo . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 31
Marejeo . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 34
vi
Majedwali na Vielelezo
MajedwaliJedwali 1: Ufaulu wa Wanafunzi Kitaaluma Kulingana na Umiliki wa Shule . . . . . . . . . . . 8
Jedwali 2: Hamasa na Mitazamo ya Waalimu Kuhusu Kazi ya Ualimu . . . . . . . . . . . . . . 13
Jedwali 3: Moyo wa Kujitolea wa Waalimu kwa Kazi ya Ualimu . . . . . . . . . . . . . . . . . 15
Jedwali 4: Moyo wa Kujitolea wa Waalimu kwa Masomo Wanayofundisha na Sifa za Kitaaluma . 20
Jedwali 5: Asilimia ya Waalimu Waliotathmini Ufanisi wa Uongozi wa Shule Zao . . . . . . . . . 21
VielelezoKielelezo 1: Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne Mwaka 2010 . . . . . . . . . . . 2
Kielelezo 2: Umiliki wa shule zilizotafitiwa . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 7
Kielelezo 3: Kipindi cha kuanzishwa kwa shule zilizotafitiwa . . . . . . . . . . . . . . . . . . 7
Kielelezo 4: Kipindi cha kuanzishwa kwa shule kulingana na umiliki . . . . . . . . . . . . . . 7
Kielelezo 5: Ufaulu wa wanafunzi kitaaluma kwa kigezo cha umiliki wa shule . . . . . . . . . . 8
Kielelezo 6: Idadi ya waalimu wenye shahada au zaidi kwa kigezo cha umiliki wa shule . . . . . 9
Kielelezo 7: Idadi ya shule zenye maktaba na maabara kwa kigezo cha umiliki . . . . . . . . . 10
Kielelezo 8: Mgawanyo wa washiriki kulingana na mahali (mkoa) . . . . . . . . . . . . . . . . 10
Kielelezo 9: Mgawanyo wa washiriki kulingana na masomo wanayofundisha . . . . . . . . . . 11
Kielelezo 10: Mgawanyo wa washiriki kulingana na sifa za ualimu . . . . . . . . . . . . . . . . 11
Kielelezo 11: Uzoefu wa kazi wa waalimu walioshiriki . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 11
Kielelezo 12: Idadi ya waalimu walioonyesha kuhudhuria programu za mafunzo
kazini katika miaka miwili iliyopita . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 12
Kielelezo 13: Mambo yaliyowahamasisha waalimu kuchagua kazi ya ualimu . . . . . . . . . . . 13
Kielelezo 14: Vigezo vilivyowavutia waalimu kuwa waalimu kwa kuzingatia umiliki wa shule . . . 15
Kielelezo 15: Idadi ya waalimu walioarifu kuwa na moyo wa kujitolea katika
vipengele mbalimbali vya kazi ya ualimu . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 17
Kielelezo 16: Moyo wa kujitolea wa waalimu na kuridhika kwao na shule walizofundisha . . . . . 18
Kielelezo 17: Idadi ya waalimu walioarifu kuridhishwa na mazingira ya kazi ya shule zao . . . . . 19
Kielelezo 18: Moyo wa kujitolea wa waalimu kwa kigezo cha jinsia . . . . . . . . . . . . . . . 19
Kielelezo 19: Idadi ya waalimu ‘waliokubaliana sana’ na ‘waliokubaliana’ na kauli
kuwa uongozi wa shule yao una ufanisi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 22
1
SEHEMU YA KWANZA
Usuli wa hitaji la kufanya utafiti
1.1. UtanguliziUtoaji wa elimu bora ni jambo muhimu katika kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Kwa
hakika, waandishi wengi wanaona kuwa elimu bora ndiyo njia yenye ufanisi zaidi katika kujenga
maadili, mitazamo, tabia na maarifa muhimu kwa watu binafsi ili waweze kutumika kwa manufaa katika
jamii iliyotangamana. Kikao cha tatu cha Mkutano Mkuu wa 61 wa Umoja wa Mataifa (GA/SHC/3847)
kilisisitiza umuhimu wa elimu bora katika kuleta maendeleo ya jamii, kikitaja kwamba elimu bora ni jambo
muhimu sana katika kuleta demokrasia ya kweli na ajira ya kweli. Hali kadhalika, Dira ya Maendeleo
ya Taifa (2025) inataja kwamba elimu bora ni muhimu ikiwa taifa litakubali kikamilifu kupambana na
changamoto za maendeleo zinazolikabili.
Kuna viashiria kadhaa vya elimu bora. Viashiria viwili kati ya hivyo ni muhimu sana, navyo hutumiwa
mara kwa mara katika nchi nyingi. Kiashiria cha kwanza huangalia utendaji wa wanafunzi katika maarifa
ya msingi, ambayo ni kusoma, kuandika na kuhesabu. Ripoti iliyotolewa hivi karibuni (Uwezo, 2010)
inaonyesha kuwa, ingawa kumekuwa na mafanikio makubwa katika kuandikisha watoto shule, kujenga
shule na kutoa mafunzo kwa waalimu, wanafunzi hujifunza maarifa machache mno nchini Tanzania; kiasi
kwamba pindi wanapohitimu elimu ya msingi, wanafunzi huwa hawana maarifa ya msingi ya kusoma,
kuandika na kuhesabu. Na kiashiria cha pili huangalia matokeo ya mitihani ya taifa.
Nchini Tanzania, mitihani hii ya taifa ni ile inayoandaliwa na kusimamiwa na Baraza la Mitihani la Tanzania.
Mitihani ya taifa ni mojawapo ya viashiria vyenye nguvu kuhusu kiwango cha elimu, navyo hutumiwa
kufanya maamuzi yahusuyo watu binafsi na taasisi kupitia matokeo ya mitihani. Mitihani ni kiashiria
muhimu pia cha kupima watoto wamejifunza kiasi gani, nayo ni chanzo muhimu cha taarifa kwa wazazi
pindi wanapofanya maamuzi kuhusu watoto wao. Kwa kutumia kipimo hiki, tunaweza kutoa maoni
kwamba kiwango chetu cha elimu kimekuwa kikiporomoka katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Mathalani, kama Kielelezo 1 kinavyoonyesha, Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne Mwaka
2010 yalitikisa nchi nzima baada ya wanafunzi wengi kufeli. Kati ya watahiniwa 354,042 waliofanya
Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne Mwaka 2010, watahiniwa 177,021 (sawa na 50%) walipata Daraja la
Sifuri, nao watahiniwa 136,633 (38.6%) walipata Daraja la Nne. Watahiniwa 15,335 (4.3%) pekee ndio
waliopata Daraja la Kwanza na la Pili, ilihali asilimia 88.6 ya watahiniwa walipata Daraja la Nne na Daraja
la Sifuri!
Hivyo basi, kusema kweli, asilimia 88.6 ya watahiniwa walifeli Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne
Mwaka 2010 kwani hawawezi kuendelea na elimu ya ngazi yoyote ya juu. Athari za kufeli huku ni kubwa
mno. Itawawia vigumu mno wanafunzi hawa waliofeli kupata ajira kwani hawana maarifa ya msingi ya
kusoma, kuandika na kuhesabu. Pia wanakosa stadi za msingi za maisha kama kujiamini, ubunifu na
mbinu za kutatua matatizo.
2
Kielelezo 1: Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne Mwaka 2010. (NECTA 2011)
Sababu kadhaa zimetajwa kuwa chanzo cha hali duni ya elimu hapa nchini. Mosha (2011) ameeleza
kwa muhtasari sababu hizo, akiziweka katika makundi makuu mawili, ambayo ni: sababu za kimazingira
na sababu za vitendea kazi. Kwa mujibu wa Mosha, sababu za kimazingira hujumuisha mazingira ya
kisiasa, kiuchumi, kisheria, kidemografi a, kiutamaduni na kimataifa. Sababu za vitendea kazi hujumuisha
uongozi duni katika taasisi, ufadhili duni kwa sekta ya elimu, hali duni ya miundombinu ya kufundishia
na kujifunzia, walimu wenye sifa duni na matatizo ya mitaala. Elimu bora imehusishwa pia na utoaji na
ustadi wa waalimu (Oduro, Dachi & Fertig, 2008). Oduro na wenzie wamedai kuwa mabadiliko katika
elimu barani Afrika yamelenga zaidi kuongeza idadi ya watu wanaopata elimu, huku ubora wa elimu
inayotolewa ukipewa umakini mdogo.
Sababu nyingi za kuwepo kwa hali duni ya elimu zilizobainishwa na tafi ti zilizotangulia zimekuwa
zikizungumzia zaidi kuwepo kwa miundombinu isiyofaa ya kufundishia na kujifunzia. Hususan, kumekuwa
na tafi ti chache sana ambazo zimelenga kuzungumzia ubora wa waalimu na moyo wao wa kujitolea
kama mambo yanayoukilia ujifunzaji wenye ufanisi ambao hatimaye huleta mafanikio kitaaluma. Hakika,
uchunguzi wa kina wa programu mbalimbali za zamani na za sasa za kuleta mabadiliko katika elimu
zilizoasisiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi unaonyesha, miongoni mwa mambo mengine,
kuwepo kwa msisitizo mdogo sana kwa waalimu kama sehemu muhimu katika kuleta mabadiliko katika
mfumo wa elimu, hususan linapokuja suala la kuboresha ustawi wao na weledi wao. Kwa mfano, kati
ya maeneo 39 ya programu zilizopewa kipaumbele katika Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Elimu ya
Sekondari (MMES II), ni programu mbili tu zinazogusia kwa mbali suala la kuboresha ustawi na weledi
wa walimu.
Walimu ni sehemu muhimu katika kuleta elimu bora. Elimu bora inahusiana moja kwa moja na ufundishaji
bora na ujifunzaji bora. Kuna mambo mengi yanayoukilia ufundishaji bora, miongoni mwayo ni sifa na
uzoefu wa waalimu, kiwango cha hamasa waliyo nayo, moyo wa kujituma na hisia za kufundisha na
mazingira ya kazi. Tafi ti zinaonesha kuwa pindi waalimu wanapokuwa na hamasa na wenye kuipenda kazi
ya ualimu, wanafunzi huwa na hamasa ya kujifunza na hujifunza maarifa yanayofundishwa na waalimu
wao kwa ufanisi zaidi (Caprara na wenzie, 2006). Hivyo basi, ni muhimu kuwatia hamasa waalimu kama
hatua mojawapo ya kushughulikia tatizo la kushuka kwa ubora wa elimu. Kwa sababu hiyo, utafi ti huu
ulifanywa, kwa upande mmoja, kama hatua ya kujaribu kuondoa pengo hili katika maarifa, na kwa
3
upande mwingine, kuchunguza kwa utaratibu maalumu hatua na mikakati ya kuongeza hamasa na
moyo wa kujitolea wa waalimu katika kufundisha.
1.2. Malengo ya UtafitiUtafiti huu ulilenga kuchunguza jinsi sifa za waalimu kitaaluma na moyo wao wa kujitolea katika kufundisha
vinavyoathiri ubora wa elimu kama unavyopimwa kwa kutumia ufaulu wa wanafunzi kitaaluma. Utafiti
huu ulilenga zaidi:
na jinsi zinavyohusiana na ufaulu wa wanafunzi kitaaluma
ufaulu wa wanafunzi kitaaluma
moyo walio nao wa kufundisha masomo hayo
Ripoti hii inaonesha matokeo ya utafiti unaozungumziwa hapa. Ripoti hii ina sehemu kuu nne, nazo ni
usuli wa hitaji la utafiti, mbinu za utafiti, matokeo ya utafiti, muhtasari, hitimisho na mapendekezo.
4
SEHEMU YA PILI
Methodolojia ya Utafiti
2.1. MbinuUtafiti huu ulishughulikia vipengele kadhaa vya ubora wa elimu. Kwanza, utafiti ulitathimini sifa za walimu
kitaaluma katika shule za aina tatu, yaani shule za sekondari za serikali, shule za binafsi na shule za
jamii (kata). Pili, utafiti ulichunguza moyo wa kujitolea walio nao waalimu na kuridhika kwao na kazi ya
ualimu na jinsi mambo haya yanavyohusiana na ufaulu wa wanafunzi. Kujituma na moyo wa kujitolea wa
waalimu ulipimwa kwa kutumia hojaji iliyofanyiwa marekebisho kutokana na zana ambazo zimekuwa
zikitumiwa na kuthibitishwa kimataifa, na vilevile kuwashirikisha waalimu katika majadiliano ya vikundi
lengwa (imeelezwa chini). Tatu, utafiti ulikusanya kwa mapana maoni ya waalimu kuhusu namna ya
kuboresha elimu mashuleni.
Hivyo basi, ni wazi kuwa utafiti huu ulichunguza suala la ubora wa elimu kwa kutumia mitazamo ya
waalimu. Utafiti huu ulitumia mbinu mseto na vyanzo mbalimbali vya ukusanyaji data ambazo zilikuwa
na msingi wake katika mkabala wa kiidadi na mkabala wa kiubora. Mkabala wa kiidadi ulitumiwa katika
kukusanya taarifa za msingi za kiidadi kuhusu demografia ya walimu na alama walizopata kuhusu
mitazamo na moyo wa kujitolea walio nao. Mkabala wa kuangalia ubora ulitumiwa kukusanya maoni ya
walimu kuhusu kazi ya ualimu, na vilevile maoni yao kuhusu hatua na mikakati ya kuboresha elimu nchini.
2.2. Maeneo ya UtafitiUtafiti huu ulifanywa katika mikoa sita, ambayo ni Pwani, Mbeya, Kigoma, Singida, Dodoma na Mtwara.
Mikoa hii ilichaguliwa kwa makusudi kwa kuzingatia ufaulu wake katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha
Nne Mwaka 2010, ambapo mikoa miwili ilichaguliwa kutoka kwenye makundi ya mikoa iliyokuwa na
ufaulu wa kiwango cha juu, kiwango cha kati, na kiwango cha chini. Mikoa ya Pwani na Mbeya ilikuwa
na ufaulu wa kiwango cha juu zaidi, ilhali mikoa ya Kigoma na Singida ilikuwa na ufaulu wa kiwango cha
kati, nayo Dodoma na Mtwara ni mikoa iliyokuwa na ufaulu wa kiwango cha chini zaidi.
Katika kila mkoa, shule sita zilichaguliwa kwa makusudi kushiriki katika utafiti huu. Kati ya shule hizi,
mbili zilikuwa ni shule kongwe za serikali, ambazo ziliitwa ‘shule za kitaifa za serikali’, mbili zilikuwa
ni shule za binafsi na mbili zilikuwa ni shule za jamii, ambazo ziliitwa ‘shule za kata za serikali’. Shule
zilichaguliwa kwa kutumia kigezo cha ufaulu wake iwapo ni wa juu au chini na iwapo mahali ilipo shule
ni mjini au kijijini.
Kwa faida ya utafiti huu, ‘shule za kitaifa za serikali’ zilitafsiriwa kuwa ni zile shule zinazomilikiwa na
kuendeshwa na serikali ambazo zilianzishwa kuanzia wakati wa uhuru hadi mwaka 2000, kabla ya
kuanzishwa kwa programu maalumu ya serikali ya kujenga shule katika kila kata. ‘Shule za kata za
serikali’ zinatafsiriwa kuwa ni shule ambazo zimejengwa na wanajamii katika ngazi ya kata kwa msaada
wa serikali, ambazo zinamilikiwa na serikali. Hizi ni shule ambazo zimeanzishwa katika miaka ya 2000
kama sehemu ya juhudi za serikali kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari.
2.3. Sampuli ya washiriki wa utafiti Sampuli ya utafiti ilihusisha zaidi walimu na wakuu wa shule. Walimu walishiriki kwa kujaza hojaji
na kushiriki katika usaili/majadiliano ya vikundi lengwa (taarifa zaidi zimetolewa katika kipengele
5
kinachofuata). Sampuli ya waalimu iliteuliwa kwa namna ifaayo kwani waalimu wote waliohudhuria
shuleni siku ambayo shule husika ilitembelewa ndio waliombwa kujaza hojaji. Aidha, kati ya walimu sita
hadi wanane katika kila shule waliombwa kushiriki katika majadiliano ya kikundi. Hali kadhalika, wakuu
wote wa shule na Maafisa elimu wa wilaya zilizoshiriki walisailiwa.
2.4. Zana za kukusanyia dataZana kuu nne zilitumiwa kukusanya data katika utafiti huu. Kwanza, hojaji ziligawiwa kwa waalimu.
Hojaji ya waalimu ilitumiwa kutathmini vipengele vikuu vitano, ambavyo ni: sifa za awali za walimu,
mazingira ya kazi, hamasa waliyo nayo waalimu na mitazamo yao kuhusu ufundishaji, moyo wao wa
kujitolea kufundisha, na ufanisi wa uongozi wa shule.
Pili, majadiliano ya vikundi lengwa na usaili vilifanywa kwa waalimu na wakuu wa shule. Kwa kiasi
kikubwa mambo haya yalilenga kuchunguza sababu za kushuka kwa kiwango cha elimu na maoni na
mitazamo kuhusu ufanisi wa walimu na moyo wao wa kujitolea kwa kazi ya ualimu.
Tatu, kulikuwa na mwongozo wa taarifa za shule. Zana hii ilitumiwa kukusanya data za msingi kuhusu
shule, ikijumuisha idadi ya walimu na sifa zao kitaaluma, upatikanaji na ubora wa zana za kufundishia
na kujifunzia, na ufaulu wa shule katika mitihani ya taifa katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.
2.5. Uchambuzi wa dataData za kiidadi kutoka katika hojaji na miongozo ya taarifa za shule iliingizwa katika programu ya
kompyuta ya SPSS Toleo la 17.0. Kisha data hizo zilisafishwa na uchambuzi muafaka ulifanywa. Kwa
kiasi kikubwa uchambuzi ulihusisha takwimu za kiuelezaji, ingawa uchambuzi wa takwimu unaofikia
matokeo kwa kujua sababu zake ulifanywa pia kwa kiwango kidogo.
Usaili na majadiliano ya vikundi lengwa yalirekodiwa neno kwa neno katika vinasa sauti. Usaili na
mahojiano haya yalinakiliwa katika maandishi kwa Kiswahili na kutafsiriwa kwa Kiingereza. Mijalada
ya lugha zote mbili, Kiswahili na Kiingereza, ilihifadhiwa katika kompyuta na katika diski mwako (flash
discs) kama nakala za kumbukumbu. Data za kiubora zilichambuliwa kwa kufuata kiunzi cha uchambuzi
wa kimaudhui, ambapo maudhui yalibainishwa na kufafanuliwa kwa kutumia nukuu za washiriki.
6
SEHEMU YA TATU
Matokeo ya utafiti
Matokeo ya utafiti huu yamewasilishwa katika sehemu kuu nne. Katika sehemu ya kwanza kumewasilishwa
matokeo ya utafiti kuhusu miongozo ya taarifa za shule, ambayo yanajumuisha data muhimu kuhusu
shule kama vile taarifa kuhusu historia yake, idadi ya walimu na sifa zao kitaaluma, na vilevile ufaulu wa
shule katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne Mwaka 2010. Aidha, katika sehemu hii kumewasilishwa
uhusiano uliopo kati ya sifa za waalimu kitaaluma na ufaulu wa wanafunzi katika mtihani huo wa taifa.
Katika sehemu ya pili kumewasilishwa matokeo kuhusu hamasa waliyo nayo walimu na moyo wao wa
kujitolea katika kufundisha. Katika sehemu ya tatu kumewasilishwa matokeo kuhusu mitazamo waliyo
nayo walimu kuhusu kazi ya ualimu na hatua zipi zichukuliwe kuboresha elimu nchini.
3.1. Matokeo kuhusu miongozo ya taarifa za shule
3.1.1 Taarifa kuhusu shule zilizotafitiwa
Kama ilivyoelezwa awali, jumla ya mikoa sita ilifanyiwa utafiti. Katika kila mkoa, shule sita ziliingizwa
katika sampuli ya utafiti, na kufanya jumla yake kuwa shule 36 katika mikoa yote sita. Jumla ya shule 30
zilishiriki kikamilifu katika utafiti (sawa na 83.3%). Hata hivyo, shule 24 tu ndizo zilizojumuishwa katika
uchambuzi wa mwisho. Shule zilizobaki ziliondolewa kwa sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na
ukweli kwamba baadhi ya shule hizo zilikuwa zikitoa elimu ya juu ya sekondari tu (kidato cha tano
na sita), ilhali kimsingi utafiti huu ulilenga shule zinazotoa elimu ya awali ya sekondari (kidato cha
kwanza hadi cha nne).
Kati ya shule hizo 24, kama Kielelezo 2 kinavyoonyesha, asilimia 29.2 zilikuwa shule za kitaifa za serikali,
asilimia 37.5 zilikuwa shule za kata za serikali, asilimia 20.8 zilikuwa shule binafsi zinazomilikiwa na
asasi za Kikristo, asilimia 4.2 zilikuwa shule binafsi zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu na asilimia 8.3
zilikuwa shule binafsi zinazomilikiwa na watu binafsi.
Idadi kubwa ya shule zilizotafitiwa zilianzishwa kati ya mwaka 1990 na 2000 au baada ya mwaka 2000
(tazama Kielelezo 3). Kama ilivyotarajiwa, na kama inavyooneshwa katika Kielelezo 4, idadi kubwa
(85.7%) ya shule za kitaifa za serikali zilizotafitiwa zilianzishwa kabla ya miaka ya 1990, wakati idadi
kubwa (88.9%) ya shule za kata za serikali zilizotafitiwa zilianzishwa baada ya mwaka 2000. Idadi kubwa
(60%) ya shule binafsi zinazomilikiwa na asasi za Kikristo na Kiislamu zilianzishwa kati ya mwaka 1990
na 2000, ilhali idadi kubwa ya shule binafsi zinazomilikiwa na asasi za watu binafsi zilianzishwa kabla
ya mwaka 2000. Hii inaashiria kuwa, katika miaka ya karibuni, serikali, kupitia juhudi mbalimbali za
wanajamii, imekuwa mwanzilishi mkuu wa shule za sekondari nchini.
7
Kielelezo 2: Umiliki wa shule zilizotafitiwa (Jumla = 24)
Kielelezo 3: Kipindi cha kuanzishwa kwa shule zilizotafitiwa
Kielelezo 4: Kipindi cha kuanzishwa kwa shule kulingana na umiliki
Za Watu
Bina
fsi
Za Watu
Bina
fsi
8
3.1.2 Ufaulu wa wanafunzi kitaaluma kwa kuzingatia umiliki wa shule
Uchambuzi ulifanywa kuchunguza ufaulu wa wanafunzi kitaaluma kwa kuzingatia umiliki wa shule.
Ufaulu wa shule kitaaluma ulichunguzwa kwa kuzingatia Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha
Nne Mwaka 2010 ya shule husika. Matokeo hayo yameoneshwa kwa muhtasari katika Jedwali 1 na
katika Kielelezo 5.
Pindi matokeo haya yalipochambuliwa kwa kuzingatia kigezo cha umiliki, yalionyesha kuwa shule binafsi
zinazomilikiwa na asasi za Kikristo zilifaulu kwa kiwango cha juu sana kuliko zile zinazomilikiwa na asasi
nyingine. Kadhalika, kama ilivyotarajiwa, kwa ujumla, shule za kata za serikali zilifanya vibaya sana
katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne Mwaka 2010. Mathalani, asilimia 65 ya watahiniwa katika
shule za kata za serikali walipata Daraja la Sifuri, huku asilimia 29.3 wakipata Daraja la Nne na asilimia
5.2 tu wakipata kati ya Daraja la Kwanza na Daraja la Tatu.
Jedwali 1: Ufaulu wa Wanafunzi Kitaaluma Kulingana na Umiliki wa Shule.1
Daraja Serikali-Kitaifa Serikali-Kata Binafsi-Kikristo Za Watu Binafsi
Daraja la I & II 13.8 1.2 71.9 2.9
Daraja la III 15.7 4 5 14.5
Daraja la IV 37.5 29.3 13.7 66.7
Daraja la 0 33.0 65.5 9.4 15.9
Kielelezo 5: Ufaulu wa wanafunzi kitaaluma kwa kigezo cha umiliki wa shule
3.1.3 Uhusiano kati ya sifa za walimu kitaaluma na ufaulu wa wanafunzi kitaaluma
Sifa za waalimu kitaaluma zilipimwa katika viwango vinne. Shule ambayo asilimia 80-100 ya waalimu
wake walikuwa na shahada ilichukuliwa kuwa na ‘sifa bora’, ilhali shule ambayo asilimia 50-79 ya
waalimu wake walikuwa na shahada ilichukuliwa kuwa na ‘sifa nzuri’. Shule ambayo asilimia 40-49 ya
waalimu wake walikuwa na shahada ilichukuliwa kuwa na ‘sifa ya wastani’. Nayo shule ambayo pungufu
ya asilimia 40 ya waalimu wake walikuwa na shahada ilichukuliwa kuwa na ‘sifa duni’.
1 Shule zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu ziliondolewa katika uchambuzi huu kutokana na idadi ndogo sana ya shule hizo katika
sampuli hii. Shule moja tu ndiyo iliyokuwa na sifa za kujumuishwa katika uchambuzi wa mwisho.
Za Watu Binafsi
9
Kama Kielelezo 7 kinavyoonyesha, shule za kitaifa za serikali zilikuwa na idadi kubwa zaidi ya waalimu
wenye sifa nzuri kitaaluma, zikifuatiwa na shule binafsi zinazomilikiwa na asasi za Kikristo. Shule binafsi
zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu na watu binafsi zilikuwa na idadi ndogo zaidi za waalimu wenye sifa
nzuri kitaaluma. Mathalani, wakati asilimia 85.7 ya waalimu katika shule za kitaifa za serikali zilizotafitiwa
na asilimia 40 ya waalimu katika shule binafsi zilizotafitiwa zinazomilikiwa na asasi za Kikristo walikuwa
na shahada, hakukuwa na mwalimu hata mmoja aliyekuwa na shahada katika shule binafsi zilizotafitiwa
zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu.
Hata hivyo, ikumbukwe kwamba, kati ya waalimu 303 waliotafitiwa, waalimu 11 (3.6%) tu ndio waliotoka
katika shule zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu, waalimu 21 (6.9%) tu ndio waliotoka katika shule
zinazomilikiwa na asasi za Kikristo, na waalimu 39 (12.9%) tu ndio waliotoka katika shule zinazomilikiwa
na asasi za watu binafsi. Waalimu walio wengi walitoka katika shule za kitaifa za serikali (116) na shule
za kata za serikali (116).
Kielelezo 6: Idadi ya waalimu wenye shahada au zaidi kwa kigezo cha umiliki wa shule
3.1.4 Tofauti ya ufaulu kwa kigezo cha zana za kufundishia na kujifunzia
Katika kipengele hiki, zana kuu mbili za kufundishia na kujifunzia ziliangaliwa, nazo ni maabara na
maktaba. Kwa mujibu wa sera ya taifa, kila shule ya sekondari inapaswa kuwa na maabara tatu – moja
kwa somo la fizikia, moja kwa kemia, na moja kwa biolojia. Hata hivyo, shule chache tu ndizo zilizokuwa
na maabara zote tatu. Kwa sababu hiyo, kigezo kikuu cha uchambuzi na ulinganishi kilikuwa ni kuwepo
kwa maabara walau moja na maktaba. Kama Kielelezo 6 kinavyoonyesha, shule za kitaifa za serikali
na shule binafsi zinazomilikiwa na asasi za Kikristo pekee ndizo zilizokuwa na maabara walau moja
na maktaba.
Kulikuwa na tofauti kubwa kitakwimu katika ufaulu wa wanafunzi kitaaluma kati ya shule zilizokuwa na
maabara (X2= [N=24, 4] =18.80, p=.001, Phi=.89) na maktaba (X2= [N=24, 8] =21.38, p=.006, Phi=.94)
na zile ambazo hazikuwa nazo, hali iliyoashiria kuwa vigezo hivi viwili vilikuwa muhimu kwa ufaulu wa
wanafunzi kitaaluma.
Za Watu
Bina
fsi
10
Kielelezo 7: Idadi ya shule zenye maktaba na maabara kwa kigezo cha umiliki.2
3.2. Hamasa na moyo wa kujitolea walio nao walimu kwa kazi ya ualimu
3.2.1 Taarifa kuhusu waalimu
Jumla ya waalimu 303 walijaza hojaji. Kati yao, asilimia 70.5 walikuwa wanaume na asilimia 29.5
walikuwa wanawake. Umri wao wa wastani ulikuwa miaka 33.0 (Achano Kuu (SD)=9.2), nao ulianzia
miaka 19 hadi 67.
Kulikuwa na mgawanyo sawa wa washiriki katika mikoa yote iliyoshiriki, ingawa kulikuwa na idadi ya
juu kidogo ya washiriki kutoka mkoa wa Pwani (tazama Kielelezo 8). Idadi kubwa (40%) ya waalimu
waliojaza hojaji walikuwa waalimu wa masomo ya Sanaa na Sayansi za Jamii, kulinganisha na waalimu
wa Sayansi na Hisabati (37%) na waalimu wa Lugha (23%) (tazama Kielelezo 9).
Waalimu walio wengi ama walikuwa na stashahada (38%) au shahada (42%) ya elimu (Kielelezo 10).
Zaidi ya hayo, kama Kielelezo 10 kinavyoonyesha, waalimu wengi waliojaza hojaji walikuwa na uzoefu
wa kufundisha usiozidi miaka mitano.
Kielelezo 8: Mgawanyo wa washiriki kulingana na mahali (mkoa)
2 Shule zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu ziliondolewa katika uchambuzi huu kutokana na idadi ndogo sana ya shule hizo katika
sampuli hii. Shule moja tu ndiyo iliyokuwa na sifa za kujumuishwa katika uchambuzi wa mwisho.
Za Watu Binafsi
11
Kielelezo 9: Mgawanyo wa washiriki kulingana na masomo wanayofundisha
Kielelezo 10: Mgawanyo wa washiriki kulingana na sifa za ualimu
Kielelezo 11: Uzoefu wa kazi wa waalimu walioshiriki
3.2.2 Ushiriki wa waalimu katika programu za kuendeleza waalimu
Ili kuchunguza ushiriki wao katika programu za kuendeleza waalimu, waalimu waliombwa kuonyesha
iwapo walipata kuhudhuria mafunzo yoyote ya ualimu/programu zozote za kujiendeleza wakiwa kazini
katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.
12
Matokeo yanaonesha kuwa asilimia 15.3 tu ya waalimu ndio walioonyesha kuwa walipata kushiriki katika
programu fulani ya kujiendeleza kitaaluma katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. Majibu yaliyotolewa
na waalimu wote, pasipo kuzingatia umiliki wa shule zao, yalielekea kufanana kwa kiasi fulani, ingawa
idadi kubwa kidogo ya waalimu wa shule binafsi zinazomilikiwa na asasi za Kikristo walionesha kuwa walipata
kuhudhuria programu za kujiendeleza kitaaluma kuliko waalimu wa shule nyingine (Kielelezo 12).
Kielelezo 12: Idadi ya waalimu walioonyesha kuhudhuria programu za mafunzo kazini katika miaka miwili iliyopita.3
3.2.3 Hamasa na mitazamo ya walimu kuhusu ualimu
Katika kuchunguza hamasa na mitazamo waliyo nayo kuhusu ualimu, waalimu walipewa vifungu 19
vya maelezo na kuombwa kutoa maoni yao kwa kuchagua jibu mojawapo kati ya majibu ya aina tano
yaliyoanzia na ‘ninakubaliana sana’ hadi ‘sikubaliani kabisa’. Jedwali 3 linaeleza kwa muhtasari matokeo
hayo. Uchunguzi wa makini wa matokeo hayo ulionyesha kuwepo sababu kuu nne kwa nini walimu
wanaweza kuchagua kazi ya ualimu na kuendelea nayo. Sababu hizo ni kama vile ‘ni rahisi kupata ajira’,
‘kwa sababu ualimu hutoa fursa zaidi za kujiendeleza kielimu’, ‘shauku ya kusaidia wengine’ na ‘shauku
ya kufundisha somo/masomo niyapendayo’. Zaidi ya asilimia 60 ya waalimu ama ‘walikubaliana sana’
au ‘walikubaliana’ na maelezo haya.
Uchambuzi wa vigezo ulifanywa kwa kuchunguza muundo wa ndani wa vifungu hivi 19 vya maelezo
kwa lengo la kubainisha vigezo vikuu vinavyowahamasisha waalimu kuchagua kazi ya ualimu. Vigezo
vikuu vitatu vilijitokeza, navyo ni shauku na moyo wa kupenda kusaidia wengine, kuvutiwa na watu
wengine mashuhuri, na mazingira mazuri ya kazi. Matokeo yanaonesha kuwa ‘shauku na moyo wa
kupenda kusaidia wengine’ ndicho kigezo kikuu kinachoweza kuwahamasisha walimu kuchagua kazi ya
ualimu, ambapo asilimia 45 ya washiriki walichagua kipengele hiki kuwa ndiyo sababu kuu iliyowafanya
kuchagua na kuendelea kufanya kazi ya ualimu. Kulikuwa na vifungu vikuu vinne vya maelezo katika
kipengele hiki. Vifungu hivyo ni ‘shauku ya kusaidia watu wengine’, ‘moyo wa kupenda kufanya kazi na
watoto’, ‘shauku ya kufundisha somo/masomo niyapendayo’ na ‘inaendana na haiba yangu’.
3 Ikumbukwe kuwa waalimu 11 tu kutoka shule moja ya Kiislamu ndio waliounda sampuli hii.
Za Watu
Bina
fsi
13
Kuvutiwa na watu wengine mashuhuri ni kigezo kilichoonesha kuwa huwahamasisha waalimu wachache
zaidi kuchagua kazi ya ualimu, ambapo asilimia 11.4 tu ya washiriki ndio walioonesha kuwa hii ndiyo
sababu iliyowafanya kuchagua kazi hii. Asilimia 16 tu ya waalimu walioshiriki walichagua kazi ya ualimu
kwa sababu kuna ‘mazingira mazuri ya kazi’ (tazama Kielelezo 13).
Kielelezo 13: Mambo yaliyowahamasisha waalimu kuchagua kazi ya ualimu
Jedwali 2: Hamasa na Mitazamo ya Waalimu Kuhusu Kazi ya Ualimu
% (N=)
Maelezo Nina-kubaliana
Sana
Nina-kubaliana
Sikubali Wala
Sikatai
Si-kubaliani
Si-kubaliani
Kabisa
SA+A SD+D
1. Ni rahisi kupata
ajira
28.7 31.4 19.8 10.2 7.6 60.1 17.8
2. Ndiyo kazi pekee
niwezayo kuipata
kwa sifa nilizo
nazo kitaaluma
8.6 20.8 12.2 34.3 21.1 29.4 55.4
3. Kazi ya ualimu
inanipa uhakika
wa ajira
14.9 25.7 21.5 20.1 14.2 40.6 34.3
4. Kuna mshahara
mkubwa
1.7 3.3 11.9 26.1 53.5 5 79.6
5. Kuna mazingira
mazuri ya kazi
5.0 16.8 21.8 26.1 27.1 21.8 53.2
6. Inakupa hadhi
kubwa katika
jamii
4 17.5 20.8 28.4 24.1 21.5 52.5
14
7. Ualimu unanipa
matazamio mazuri
ya kupata kazi
8.6 29.7 21.1 18.8 16.5 38.3 35.3
8. Kwa kuwa ualimu
hunipa fursa zaidi
za kujiendeleza
kielimu
23.8 37 14.9 9.6 10.9 60.8 20.5
9. Kwa kuwa serikali
inajali elimu
9.6 19.8 26.1 24.1 15.8 29.4 39.9
10. Moyo wa
kupenda kufanya
kazi na watoto/
vijana wadogo
11.6 29.4 16.8 20.1 17.5 41 37.6
11. Inaendana na
haiba yangu
13.2 27.7 25.7 15.5 13.2 40.9 28.7
12. Shauku ya
kusaidia watu
wengine
30.7 37.3 13.5 7.9 7.6 68 15.5
13. Shauku ya
kufundisha
masomo
niyapendayo
27.1 37 13.5 9.9 9.6 64.1 19.5
14. Kuvutiwa
na waalimu
mashuhuri
6.6 19.1 21.5 29.7 18.8 25.7 48.5
15. Kuvutiwa na
wanafamilia
5.9 16.8 22.1 29.7 21.5 22.7 51.2
16. Kuvutiwa
na wanarika
wenzangu
3.3 12.5 19.5 33.7 27.1 15.8 60.8
17. Kuvutiwa na
vyombo vya
habari
4.3 9.6 16.8 35 30.4 13.9 65.4
18. Kuakisi imani
yangu ya kidini
7.6 15.2 16.8 28.4 27.4 22.8 55.8
19. Ugumu wa kupata
ajira
10.9 22.8 24.4 18.2 20.1 33.7 38.3
Pindi matokeo yalipochambuliwa kwa kuzingatia kigezo cha umiliki wa shule, ilibainika kuwa ‘mazingiria
mazuri ya kazi’ kilikuwa ndicho kigezo muhimu zaidi kilichowavutia walimu wa shule binafsi zinazomilikiwa
na asasi za Kiislamu, ilhali waalimu wa shule za kitaifa za serikali, shule za kata za serikali na shule
15
binafsi zinazomilikiwa na asasi za Kikristo kwa kiasi kikubwa walivutiwa na vigezo vinavyohusiana na
‘shauku na moyo wa kupenda kuwasaidia wengine’ (tazama Kielelezo 14).
Kielelezo 14: Vigezo vilivyowavutia walimu kuwa waalimu kwa kuzingatia umiliki wa shule
3.2.4 Moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kazi ya ualimu
Vipengele kumi na saba vilijumuishwa katika hojaji kuchunguza moyo wa kujitolea walio nao waalimu
kwa kazi ya ualimu. Matokeo yake yameelezwa kwa muhtasari katika Jedwali 4 na Jedwali 5. Kwa jumla,
kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kazi ya ualimu kilikuwa cha chini. Mathalani,
asilimia 40.6 tu ya waalimu ndiyo ‘waliokubaliana sana’ na ‘kukubaliana’ na kauli kwamba ‘Matamanio
yangu ni kuendelea kuwa mwalimu’, huku asilimia 45.2 tu ya walimu ndio ‘wakikubaliana sana’ na
‘kukubaliana’ na kauli kwamba ‘Ninaiona kazi ya ualimu kuwa ya kuvutia sana na yenye kuridhisha mno’.
Zaidi ya hayo, asilimia 33.7 tu ndio walioarifu kuwa ‘Ninapenda maisha ya shuleni na niko radhi
kufundisha kwa maisha yangu yote’, ilhali asilimia 35.3 tu ya waalimu ndio ‘waliokubaliana’ na kauli kuwa
‘Ikiwa nitapewa kuchagua kazi moja tu miongoni mwa nyinginezo, bado nitachagua kuwa mwalimu’.
Kadhalika, asilimia 42.5 tu ndio ‘waliokubaliana sana’ na ‘kukubaliana’ na kauli kwamba ‘Ninaridhishwa
sana na shule ninayofundisha’.
Jedwali 3: Moyo wa Kujitolea wa Waalimu kwa Kazi ya Ualimu
%
Maelezo SA A N D SD SA+A SD+D
1. Matamanio yangu ni
kuendelea kuwa mwalimu
12.9 27.7 22.8 17.5 17.2 40.6 34.7
2. Ninapenda kufundisha
kuliko ilivyokuwa siku za
nyuma
12.5 30.7 21.5 17.5 14.9 43.2 32.4
3. Ninapenda kufundisha
somo nilipendalo kwa
wanafunzi wangu
30.0 47.2 13.2 3.3 3.3 77.2 6.6
Za Watu
Bina
fsi
16
4. Niko radhi kusaidia
kuendeleza shule yangu
kadri niwezavyo
38.6 46.5 5.9 3.0 2.6 85.1 5.6
5. Hata wanafunzi wawe na
tabia mbaya kiasi gani,
bado nitajaribu kadri
niwezavyo kuwafundisha
38.6 37.0 8.9 6.6 5.0 75.6 11.6
6. Ninaiona kazi ya ualimu
kuwa ya kuvutia sana na
yenye kuridhisha mno
16.5 29.7 18.5 17.2 14.2 46.2 31.4
7. Kazi ya ualimu ilikuwa/ni
mojawapo ya machaguo
yangu matatu ya kwanza
ya kazi
22.1 36.3 15.5 11.9 10.6 58.4 22.5
8. Ualimu ni mgumu mno na
hakuna faida ya maana
unayoipata
23.8 24.8 17.5 18.8 12.2 48.6 31.0
9. Mitazamo na tabia za
wanafunzi zimefifisha
shauku yangu ya
kufundisha
11.6 22.1 17.5 31.7 13.2 33.7 44.9
10. Kazi ya kufundisha ni
ngumu mno kwangu na
ninataka kuachana nayo
7.9 12.2 20.8 35.6 20.1 20.1 55.7
11. Ninapenda maisha ya
shuleni na niko radhi
kufundisha kwa maisha
yangu yote
10.9 22.8 23.1 24.8 15.2 33.7 40.0
12. Sijakata tamaa; ninayo
malengo ninayotaka
kuyatimiza katika ualimu
14.9 17.8 18.8 27.7 17.5 32.7 45.2
13. Hata kukiwa na kazi
nzuri zaidi, nitaendelea
kufundisha
29.0 19.5 18.5 17.5 12.5 48.5 30.0
14. Kuthaminiwa kwangu na
shule/mkuu wa shule
kulinichochea kufanya
kazi
10.9 30.0 23.8 16.8 13.9 40.9 30.7
15. Ikiwa nitapewa kuchagua
kazi moja tu miongoni
mwa nyinginezo, bado
nitachagua kuwa
mwalimu
10.2 25.1 24.4 18.2 18.2 35.3 36.4
17
16. Ninaridhishwa sana na
shule ninayofundisha
15.5 37.0 21.8 12.5 10.2 52.5 22.7
17. Kwa jumla, ninapenda
kuwafundisha wanafunzi
wangu
32.0 46.5 11.2 4.0 3.6 78.5 7.6
Alama za wastani 19.9 30.2 17.9 16.7 12.0 50.0 28.8
Uchambuzi wa vigezo ulifanywa kuchunguza miundo ya ndani ya viwango vya moyo wa kujitolea
walio nao waalimu ambapo vipengele hivi 17 vilifanyiwa uchambuzi wa sehemu kuu. Sehemu kuu tatu
zilijitokeza zikiakisi hali tatu za viwango vya moyo wa kujitolea walio nao waalimu. Hali hizo tatu ni ‘moyo
wa kujitolea walio nao waalimu na kuridhika kwao na kazi ya ualimu’, ‘moyo wa kujitolea walio nao
waalimu katika kuwasaidia wanafunzi’ na ‘moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa shule na kuridhika
kwao na shule’. Matokeo yake yameelezwa kwa muhtasari katika Kielelezo 15 na Kielelezo 16. Kielelezo
15 kinaonesha kiwango cha jumla cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu katika hali zote tatu na
Kielelezo 16 kinaonyesha kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kuzingatia kigezo cha
umiliki wa shule.
Kama Kielelezo 15 kinavyoonyesha, waalimu waliarifu kuwa na moyo wa kujitolea wa hali ya juu katika
kuwasaidia wanafunzi, ambapo asilimia 80.1 ya waalimu waliarifu kuwa na moyo wa kuwasaidia
wanafunzi. Kiwango cha moyo wa kujitolea kwa kazi ya ualimu kilikuwa cha chini sana ambapo asilimia
36.6 tu ya waalimu ndio walioarifu kuwa na moyo wa kujitolea na walioridhika na kazi ya ualimu. Hali
kadhalika, kiwango cha moyo wa kujitolea kwa ajili ya shule kilikuwa cha chini, ambapo asilimia 42.4
tu ya waalimu ndio walioarifu kuwa na moyo wa kujitolea kwa ajili ya shule walizokuwa wakifundisha.
Kielelezo 15: Idadi ya waalimu walioarifu kuwa na moyo wa kujitolea katika vipengele mbalimbali vya kazi ya ualimu
3.2.5 Kiwango cha moyo wa kujitolea wa waalimu kwa kigezo cha umiliki wa shule
Uchambuzi ulifanywa kuchunguza kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kuzingatia
kigezo cha umiliki wa shule. Hii ilifanywa kwa kulinganisha kiwango cha moyo wa kujitolea na kuridhishwa
na kazi ya ualimu miongoni mwa waalimu wa shule za serikali na za binafsi. Matokeo yake yameelezwa
18
kwa muhtasari katika Kielelezo 16. Kwa jumla, waalimu wa shule binafsi za Kikristo walionyesha kuwa
na moyo wa kujitolea wa hali ya juu na walioridhishwa na kazi ya ualimu kuliko waalimu wa shule
nyinginezo. Mathalani, wakati asilimia 73 ya waalimu katika shule binafsi za Kikristo waliarifu kuwa
na moyo wa kujitolea na kuridhishwa na kazi ya ualimu, pungufu ya asilimia 55 ya waalimu wa shule
nyinginezo ndio walioarifu kuwa na moyo wa kujitolea na kuridhishwa na kazi ya ualimu.
Kiwango cha moyo wa kujitolea wa waalimu kwa shule wal izofanyia kazi kilikuwa cha chini zaidi
miongoni mwa waalimu wa shule binafsi zinazomilikiwa na watu binafsi na wale wa shule za kata za
serikali, lakini kilikuwa cha juu kwelikweli miongoni mwa waalimu wa shule binafsi za Kikristo. Mathalani,
wakati asilimia 71 ya waalimu wa shule binafsi za Kikristo waliarifu kuwa na moyo wa kujitolea na
walioridhika na shule walizofundisha, asilimia 32 tu ya waalimu wa shule binafsi zinazomilikiwa na watu
binafsi ndio walioarifu hivyo. Asilimia 36 tu ya waalimu wa shule za kata za serikali na asilimia 46 tu ya
waalimu wa shule za kitaifa za serikali ndio walioarifu kuwa na moyo wa kujitolea na walioridhika na
shule walizokuwa wakifundisha. Kwa kiasi fulani kulikuwepo pia na moyo wa kujitolea wa hali ya juu kwa
shule miongoni mwa waalimu wa shule binafsi za Kiislamu, ambapo asilimia 56 ya waalimu wa shule hizi
waliarifu kuwa na moyo wa kujitolea na walioridhika na shule walizofundisha.
Kielelezo 16: Moyo wa kujitolea wa waalimu na kuridhika kwao na shule walizofundisha.4
Kwa jumla, na kwa wastani, asilimia 58.6 tu ya walimu walioshiriki katika utafiti ndio walioarifu kuwa
walikuwa wameridhika na mazingira ya kazi katika shule walizokuwa wakifundisha. Pindi uchambuzi
ulipofanywa kwa kuzingatia kigezo cha shule, kama Kielelezo 17 kinavyoonyesha, matokeo yalionyesha
kuwa idadi kubwa zaidi kitakwimu (X2=[N=297, 12]=49.9, p<.0005) ya walimu wa shule binafsi
zinazomilikiwa na asasi za Kikristo (95%) na wale wa shule binafsi zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu
(82%) waliarifu kuridhishwa na mazingira ya kazi ya shule zao kulinganisha na waalimu wa shule
za kitaifa za serikali (59%), shule za kata za serikali (51%) na shule binafsi zinazomilikiwa na watu
binafsi (51%).
4 Kwa mara nyingine, ikumbukwe kwamba waalimu 11 tu kutoka shule moja tu ndio waliounda sampuli ya shule binafsi zinazomilikiwa
na asasi za Kiislamu.5 Data kuhusu waalimu wa shule za Kiislamu hazina budi kuchambuliwa kwa uangalifu kwani sampuli yao iliundwa na washiriki
wachache tu.
Za Watu
Bina
fsi
19
Kielelezo 17: Idadi ya waalimu walioarifu kuridhishwa na mazingira ya kazi ya shule zao.5
3.2.6 Moyo wa kujitolea na kuridhika na ualimu kwa kigezo cha jinsia
Uchambuzi ulifanywa pia kuchunguza kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kuzingatia
jinsia yao. Cha kushangaza, ingawa tofauti haikuwa kubwa kitakwimu, idadi kubwa ya waalimu wa kiume
waliarifu kuwa walikuwa na moyo wa kujitolea na walioridhika na masuala mbalimbali kuliko waalimu
wenzao wa kike. Mathalani, kwa jumla, asilimia 55.4 ya waalimu wa kiume waliarifu kuwa na moyo wa
kujitolea na kuridhika na kazi ya ualimu kulinganisha na asilimia 46 ya waalimu wa kike.
Pindi uchambuzi ulipofanywa kwa kuzingatia vipengele vitatu vya moyo wa kujitolea walio nao waalimu,
matokeo yalionyesha mwelekeo unaofanana huku idadi kubwa ya waalimu wa kiume wakiarifu kuwa na
moyo wa kujitolea kwa masuala mbalimbali katika kazi ya ualimu kuliko waalimu wa kike.
Mathalani, asilimia 38.5 ya waalimu wa kiume waliarifu kuwa na moyo wa kujitolea na wenye kuridhika
na kazi ya ualimu, kulinganisha na asilimia 27 ya waalimu wa kike. Zaidi ya hayo, wakati asilimia 82 ya
waalimu wa kiume waliarifu kuwa na moyo wa kujitolea kuwasaidia wanafunzi, asilimia 76.5 ya waalimu
wa kike ndio walioarifu hivyo. Kadhalika, asilimia 45.8 ya waalimu wa kiume waliarifu kuwa na moyo wa
kujitolea na walioridhika na shule walizokuwa wakifundisha kulinganisha na asilimia 34.9 ya waalimu
wa kike (tazama Kielelezo 18).
Kielelezo 18: Moyo wa kujitolea wa waalimu kwa kigezo cha jinsia
Za Watu
Bina
fsi
20
3.2.7 Moyo wa kujitolea na kuridhika na ualimu kwa kuzingatia uzoefu na masomo ya kufundisha
Uchambuzi ulifanywa kuchunguza kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kuzingatia
uzoefu wa kufundisha na masomo ya kufundisha. Matokeo yake yameelezwa kwa muhtasari katika
Jedwali 5.
Matokeo hayo yanaonesha kuwa, kwa wastani, waalimu wa masomo ya lugha walikuwa na moyo wa
kujitolea zaidi na walioridhika zaidi na kazi ya ualimu kuliko walimu wa masomo ya sanaa na ya sayansi.
Mathalani, asilimia 85.4 ya waalimu wa masomo ya lugha waliarifu kuwa na moyo wa kujitolea katika
kuwasaidia wanafunzi, kulinganisha na asilimia 78.1 ya waalimu wa masomo ya sanaa na asilimia 79.6
ya walimu wa sayansi. Kadhalika, asilimia 45.1 ya waalimu wa masomo ya lugha waliarifu kuwa na
moyo wa kujitolea na walioridhika na shule walizokuwa wakifundisha, kulinganisha na asilimia 37.3 ya
waalimu wa sayansi na asilimia 44.8 ya waalimu wa masomo ya sanaa. Lakini, idadi kubwa (39.9%)
ya waalimu wa sayansi waliarifu kuwa na moyo wa kujitolea na walioridhika na kazi ya ualimu kuliko
waalimu wa lugha (35.4%) na waalimu wa masomo ya sanaa (34.9%). Hata hivyo, uchambuzi uliofanywa
kwa njia ya chi-square ulionyesha kutokuwepo kwa tofauti kubwa kitakwimu miongoni mwa makundi
haya matatu ya waalimu.
Walimu kuwa na sifa nzuri kitaaluma hakukuashiria kwa namna mbalimbali kuwa na sifa ya moyo wa
kujitolea katika kufundisha, kwani waalimu wenye sifa za kiwango cha chini waliarifu kuwa na moyo
wa kujitolea wa hali ya juu katika kufundisha kuliko waalimu wenye sifa za kiwango cha juu. Mathalani,
idadi kubwa kitakwimu (64.3%) ya waalimu wa ngazi ya cheti waliarifu kuwa na moyo wa kujitolea
na walioridhika na kazi ya ualimu kuliko wale wa ngazi ya stashahada (40.1%) na shahada (28.4%).
Kadhalika, asilimia 93.3 ya waalimu wenye cheti cha ualimu waliarifu kuwa na moyo wa kujitolea
kuwasaidia wanafunzi, kulinganisha na asilimia 75.5 ya waalimu wenye stashahada na asilimia 79.6
ya waalimu wenye shahada. Hata hivyo, idadi kubwa ya waalimu wa ngazi ya shahada waliarifu kuwa
na moyo wa kujitolea na walioridhika na shule walizokuwa wakifundisha kuliko waalimu wa ngazi ya
stashahada (38.3%) na wa ngazi ya cheti (35.7%).
Jedwali 4: Moyo wa Kujitolea wa Waalimu kwa Masomo Wanayofundisha na Sifa za Kitaaluma
Masomo ya kufundisha Uzoefu wa kufundisha
Sanaa Lugha Sayansi p Stashahada Shahada Cheti p
1. Moyo wa kujitolea
na kuridhika na
kazi ya ualimu
34.9 35.4 39.9 0.70 40.1 28.4 64.3 0.03
2. Moyo wa kujitolea
kusaidia wanafunzi
78.1 85.4 79.6 0.90 75.5 79.6 93.3 0.68
3. Moyo wa kujitolea
kwa shule na
kuridhika na shule
44.8 45.1 37.3 0.45 38.3 44.5 35.7 0.28
21
3.3. Ufanisi wa uongozi wa shuleUongozi wa shule ni kigezo muhimu kinachoukilia kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu
katika kufundisha. Katika utafiti huu, tuliwaomba waalimu kutathmini uongozi wa shule zao katika
vipengele mbalimbali. Walipewa vifungu 12 vya maelezo na kuombwa kutathmini ni kwa kiasi gani
walikubaliana na maelezo hayo kwa kuchagua jibu mojawapo kati ya majibu ya aina tano yaliyoanzia na
‘ninakubaliana sana’ hadi ‘sikubaliani kabisa’. Matokeo yake yameelezwa kwa muhtasari katika Jedwali
6 na Kielelezo 19.
Kama Kielelezo 19 kinavyoonyesha, ukiacha waalimu wa shule binafsi za Kikristo, maoni ya waalimu
kuhusu kiwango cha ubora wa uongozi wa shule zao yalionyesha kuwa kilikuwa cha chini kabisa.
Mathalani, kwa wastani, wakati asilimia 79.8 ya waalimu wa shule binafsi za Kikristo waliarifu kuwa
uongozi wa shule zao ulikuwa ni wenye ufanisi katika masuala mbalimbali, asilimia 48 tu ya waalimu
wa shule za kata za serikali, asilimia 37.9 tu ya waalimu wa shule binafsi za Kiislamu na asilimia 47 tu ya
waalimu wa shule zinazomilikiwa na watu binafsi ndio waliokuwa na maoni sawa na hayo. Hivyo, ingawa
tofauti haikuwa kubwa kitakwimu (X2= [N=266, 16]=16.82, p=.40), kulikuwa na tofauti za wazi kabisa
katika maoni kuhusu ufanisi wa uongozi wa shule miongoni mwa waalimu wa shule za makundi hayo
matano, ambapo idadi kubwa ya waalimu wa shule binafsi za Kikristo walikuwa na maoni yaliyounga
mkono uongozi wa shule zao kuliko waalimu wa shule nyingine.
Kadhalika, pindi uchambuzi ulipofanywa kwa kuzingatia vipengele kadhaa, waalimu wa shule binafsi za
Kikristo walipata alama za juu mno kuliko waalimu wa shule nyingine. Mathalani, wakati asilimia 76.2 ya
waalimu wa shule binafsi za Kikristo ‘walikubaliana sana’ na pia ‘walikubaliana’ na mtazamo kwamba
uongozi wa shule zao ‘hutengeneza mazingira mazuri ya kazi’, asilimia 49.1 tu ya waalimu wa shule
za kitaifa za serikali, asilimia 37 tu wa shule za kata za serikali, asilimia 45.5 tu ya waalimu wa shule
binafsi za Kiislamu na asilimia 35.9 tu ya waalimu wa shule za watu binafsi ndio waliokuwa na maoni
sawa na hayo. Jambo la kuvutia, hata hivyo, ni kwamba idadi kubwa ya waalimu wa shule binafsi za
Kiislamu walikuwa na maoni chanya kuhusu vipengele viwili vya kupima ufanisi wa uongozi wa shule,
navyo ni ‘(uongozi wa shule) husisitiza nidhamu ya kiwango cha juu’ na ‘(uongozi wa shule) ni mfano
wa kuigwa’. Mathalani, asilimia 72.7 ya waalimu wa shule hizi ‘walikubaliana sana’ au ‘walikubaliana’ na
kauli kwamba uongozi wa shule zao ‘ni mfano wa kuigwa’.
Jedwali 5: Asilimia ya Waalimu Waliotathmini Ufanisi wa Uongozi wa Shule Zao
% ‘Ninakubaliana Sana’ na ‘Ninakubaliana’
Maelezo Serikali-Kitaifa
Serikali-Kata
Binafsi-Kikristo
Binafsi-Kiislamu
Binafsi-Watu
1. Hutengeneza mazingira mazuri ya
kazi
49.1 37.0 76.2 45.5 35.9
2. Huhakikisha kuna umoja/
ushirikiano baina ya uongozi/
waalimu/ watumishi/ jamii
57.7 54.3 81.0 18.2 48.7
3. Una mipango kabambe, utaratibu
mzuri
55.2 49.1 85.7 0 46.2
22
4. Huhamasisha kushiriki katika
kuendesha masuala ya shule
52.7 53.4 81.0 27.3 48.8
5. Huchochea ushirikiano 60.3 48.3 85.7 45.5 59.0
6. Huruhusu kupata taarifa kirahisi 55.2 49.1 76.2 27.3 50.0
7. Huonyesha kuwa na sifa za juu za
uongozi
50.9 44.8 66.6 27.3 51.3
8. Hufanya tathmini ya mara kwa
mara na ya haki kwa watumishi
54.3 45.7 76.2 36.4 38.5
9. Huhakikisha kuna vifaa bora vya
kufundishia na kujifunzia
55.2 48.3 76.2 45.5 41.0
10. Husisitiza nidhamu ya kiwango
cha juu
62.1 56.9 90.5 72.7 56.4
11. Ni mfano wa kuigwa 51.8 43.1 80.9 72.8 43.6
12. Huonyesha sifa za kuigwa za
mwalimu mzuri
60.4 46.5 81.0 36.4 53.8
Wastani 55.4 48.0 79.8 37.9 47.8
Kielelezo 19: Idadi ya waalimu ‘waliokubaliana sana’ na ‘waliokubaliana’ na kauli kuwa uongozi wa shule yao una ufanisi
3.4. Muhtasari: Uhusiano uliopo baina ya ufaulu wa shule kitaaluma na sifa za walimu kitaaluma, moyo wao wa kujitolea kwa kazi ya ualimu na maoni yao kuhusu ufanisi wa uongozi wa shuleKwa matokeo ya hapo juu, ni dhahiri kuwa vipengele vitatu vinaonyesha kuwa ni muhimu zaidi katika
kuukilia ufaulu wa shule kitaaluma. Vipengele hivyo ni sifa za waalimu kitaaluma, moyo wa kujitolea
walio nao waalimu kwa kazi ya ualimu na mtazamo wao chanya kuhusu ufanisi wa uongozi wa shule.
Matokeo ya utafiti huu yanaonyesha dhahiri kuwa waalimu wenye sifa nzuri kitaaluma wanao uwezo wa
kuwafanya wanafunzi kufaulu vizuri, lakini hii inawezekana ikiwa tu vigezo vingine vitatiliwa maanani,
Za Watu Binafsi
23
navyo ni moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kazi yao na vilevile kuridhishwa kwao na uongozi wa
shule. Hii ina maana kuwa kuboresha sifa za waalimu kitaaluma hakuna budi kwenda bega kwa bega na
kuboresha mazingira ya kazi ya waalimu na ufanisi wa uongozi wa shule ili waalimu waweze kuifurahia
kazi yao na hivyo kuboresha moyo wao wa kujitolea kazini.
Hata hivyo, pindi uchambuzi ulipofanywa kwa njia ya chi-square, moyo wa kujitolea walio nao waalimu
na maoni yao kuhusu ufanisi wa uongozi wa shule ndivyo vigezo pekee vilivyoonyesha kuleta matokeo
muhimu kitakwimu.
3.5. Maoni ya waalimu kuhusu kazi ya ualimu: Matokeo ya Majadiliano ya Vikundi3.5.1 Utangulizi
Ili kutimiliza utafiti uliofanywa kwa njia ya hojaji, waalimu walipewa fursa ya kubadilishana uzoefu wao
kuhusu kazi ya ualimu na mazingira yao ya kazi kwa jumla kupitia majadiliano ya vikundi lengwa.
Majadiliano yalifanywa kwa kikundi walau kimoja katika kila shule iliyoshiriki, na kila kikundi kilikuwa
na washiriki kuanzia watano (5) hadi tisa (9). Majadiliano haya ya vikundi lengwa yalirekodiwa kwenye
vinasa sauti na kunakiliwa neno kwa neno katika maandishi. Kisha majadiliano yaliyonakiliwa yalifanyiwa
uchambuzi wa kimaudhui, ambapo maudhui makuu yalibainishwa na kufafanuliwa kwa kutumia nukuu
za washiriki.
Maudhui makuu manne yalibainishwa, nayo ni: (i) kwa nini waalimu walichagua kazi ya ualimu; (ii)
mitazamo ya waalimu kuhusu kazi ya ualimu; na (iii) maoni ya waalimu kuhusu sababu za wanafunzi
kufanya vibaya kitaaluma na nini kifanyike kuboresha kiwango cha elimu na kiwango cha ufundishaji.
3.5.2 Kwa nini waalimu walichagua kazi ya ualimu
Uchambuzi wa majadiliano ya vikundi lengwa ulibainisha sababu kuu tano zilizowavutia waalimu
kuchagua kazi ya ualimu. Sababu ya kwanza na iliyo muhimu zaidi ni urahisi wa kupata ajira waliouona
waalimu baada ya kuhitimu mafunzo. Waalimu wengi walieleza kwamba walichagua kazi ya ualimu kwa
sababu waliamini kuwa ingekuwa rahisi kwao kupata ajira baada ya kumaliza masomo yao kulinganisha
na kazi nyingine. Walimu walieleza pia kwamba kazi ya ualimu iliwapa uhakika mkubwa zaidi wa kusaidia
familia zao kwani kuna uhakika wa kupata ajira mara tu mtu anapohitimu mafunzo yake. Nukuu za
maoni ya baadhi ya washiriki zilizopo hapa chini zinathibitisha hili:
Nadhani sababu kubwa iliyonifanya kuchagua kazi hii (ualimu) ilikuwa ni ukweli kwamba nilifikiri
itakuwa rahisi kupata ajira baada ya masomo yangu. Lakini kama ingewezekana kupata ajira katika
fani nyingine, kamwe nisingeweza kuchagua kazi ya ualimu (Mwalimu, Shule A1, Mkoa wa Pwani).
Nilichagua kuwa mwalimu kwa sababu nilijua ilikuwa rahisi kupata kazi katika sekta ya elimu.
Nina ndugu wengi ambao walisomea kozi nyingine na niliwaona walivyohangaika kupata ajira;
sikutaka kuhangaika kama wao, kwa hiyo nikaamua kuwa mwalimu. Lakini ualimu siyo kazi
ninayopanga kuifanya kwa muda mrefu; mwishowe nitaachana na kazi hii (Mwalimu, Shule Z,
Mkoa wa Pwani).
Kwa kweli, nilikuwa mwalimu kwa bahati mbaya tu! Ni kwa sababu ilikuwa rahisi zaidi kwangu
kupata kazi. Lakini, kwa kweli, baada ya kujiunga na kazi hii, hakuna kitu ambacho kweli
kinanihamasisha kuendelea kuwa mwalimu. Ni suala la wakati tu; bila shaka nitaachana na kazi hii
(Mwalimu, Shule H, Mkoa wa Dodoma).
24
Mtu asikudanganye. Tupo hapa kwa sababu tulitaka ajira na ualimu ndiyo njia rahisi zaidi ya kupata
kazi (Mwalimu, Shule D, Mkoa wa Singida).
Sababu ya pili iliyotajwa mara kwa mara kama kigezo kilichowafanya waalimu kuchagua kazi hii ilikuwa
ni kutokuwa na sifa za kujiunga na kazi nyingine. Waalimu walieleza kuwa baadhi yao walichagua kazi
ya ualimu baada ya kushindwa kupata sifa zinazohitajika kujiunga na kazi nyingine, kama vile katika
sekta ya fedha, uchumi, tiba, uhandisi, na kadhalika. Hivyo, waliona kuwa kazi ya ualimu ingekuwa njia
ya kupatia kazi nyingine wazipendazo. Kwa sababu hiyo, ualimu ulichukuliwa zaidi kuwa ni kazi ‘ya
mpito tu’ wakati mtu akisubiria kazi nyingine nzuri ijitokeze. Ni dhahiri kuwa hali hii huwafanya waalimu
kutojihusisha sana na kazi ya ualimu na kutokuwa na moyo wa kujitolea kwa kazi hii. Nukuu chache za
maoni zilizopo hapa chini zinathibitisha hili:
Watu huchagua kazi hii (ualimu) kama chaguo la mwisho – wameshindwa kupata kitu kingine
chochote cha maana maishani mwao na, kwa hiyo, kazi ya ualimu ndilo chaguo pekee lililobaki.
Mimi ni mfano halisi: niko hapa kwa sababu matokeo yangu ya kidato cha sita yalikuwa ovyo.
Nilitaka kusomea Uchumi, lakini matokeo yangu hayakuniruhusu. Vinginevyo, kamwe nisingekuwa
mwalimu (Mwalimu, Shule Z1, Mkoa wa Pwani).
...Halafu, hii ndiyo kazi pekee ambayo mtu yeyote anaweza kujiunga nayo. Ukifeli, huku ndiko
unakoishia. Kwa hiyo niko hapa kwa sababu, kwa kweli, nilishindwa kupata matokeo mazuri ya
kujiunga na kazi nyingine. Ningeenda wapi kwingine na matokeo yangu mabaya kwa kila somo
nililofanya? Kwa mfano, nilikuwa na ‘credit’ mbili tu, zote zilikuwa ‘E’; ningeenda wapi kwingine
kama siyo Diploma ya Ualimu? (Mwalimu, Shule D, Mkoa wa Singida)
Ualimu haukuwa chaguo langu la kwanza. Chaguo langu la kwanza lilikuwa utalii, na nilichagua
ualimu kama chaguo la tatu. Nililazimishwa kuwa mwalimu; walinipa chaguo la tatu. Tangu hapo
nimekuwa sina furaha (Mwalimu, Shule A, Mkoa wa Singida).
Kwa upande wangu, nilijiunga na kazi ya ualimu kwa sababu nilipata Daraja la Tatu na sikupata
alama nzuri za kuniwezesha kujiunga na kidato cha tano, kwa hiyo ilibidi niende Diploma ya Ualimu.
Kwa hiyo ualimu haukuwa chaguo langu hata kidogo, lakini mazingira yamenilazimisha kujiunga
nao kwa sababu ya matokeo yangu mabaya. Lakini kama kitu kingine kizuri kikijitokeza, nitaachana
mara moja na kazi hii bila kujiuliza maswali (Mwalimu, Shule J, Mkoa wa Dodoma).
Ingawa waalimu wengi walioshiriki katika majadiliano haya ya vikundi walitaja sifa duni kitaaluma
na urahisi wa kupata ajira kuwa ndizo sababu kuu zilizowavutia kuchagua kazi ya ualimu, waalimu
wengine wachache walitaja sababu nyingine kama vile ‘kupenda kwa mtu na kuvutiwa na watu wengine
mashuhuri’. Baadhi ya waalimu walieleza kwamba walichagua kazi ya ualimu kwa sababu waliipenda
kazi hii na waliamini ilikuwa ndiyo njia bora zaidi ya kuitumikia jamii. Aidha, waliiona kazi ya ualimu kuwa
ni kazi ya uadilifu iliyohitaji watu waadilifu.
Waalimu wengine walieleza kuwa walichagua kazi ya ualimu kwa sababu ya kuvutiwa na wazazi na/
au ndugu wengine wa karibu. Walidai kwamba walichagua kazi ya ualimu kwa sababu tu wazazi wao
au watu wengine wa karibu waliokuwa wa muhimu kwao walikuwa waalimu. Zaidi ya hayo, waalimu
wengine walisema kuwa walichagua kazi ya ualimu kwa sababu walishauriwa kufanya hivyo na watu
wengine wa muhimu kwao. Hapa chini kuna baadhi ya nukuu zinazothibitisha maoni hayo:
25
Ninaipenda Historia, na niliona kwamba kuwa mwalimu wa Historia ingekuwa ni njia bora zaidi ya
kupanua maarifa yangu katika eneo hili (Mwalimu, Shule J, Mkoa wa Dodoma).
Ninapenda tu kufundisha wengine; kwa hiyo kujiunga na kazi ya ualimu lilikuwa ni chaguo langu
kwa asilimia mia moja kwa sababu ninapenda ualimu (Mwalimu, Shule Z, Mkoa wa Pwani).
Kwangu mimi, ni kwa sababu nilivutiwa na mazingira niliyokuwemo. Kijiji ninachotoka ualimu ndiyo
kazi pekee ambayo watu wanaijua, kwa hiyo kila mtu ni kama anapenda ualimu, na mimi ni zao lake
(Mwalimu, Shule M, Mkoa wa Kigoma).
‘Nilirithi’ kutoka kwa wazazi wangu. Wazazi wangu wote, baba na mama, ni waalimu na nilikua
nikiwa ninaupenda ualimu, na kwa kweli nina furaha kuwa mwalimu (Mwalimu, Shule T, Mkoa wa
Mtwara).
Siipendi kazi ya ualimu. Nilitaka kusomea utawala, lakini wazazi wangu walinishauri kusomea
elimu maalumu, nikakubali na nilikuwa ninategemea kwamba ningefundisha watoto wenye mahitaji
maalumu. Lakini nipo hapa, nikifanya mambo ambayo kamwe sikutaka kuyafanya. Badala ya
kunipeleka kwenye shule maalumu ambako ningeweza kufundisha wanafunzi wenye ulemavu,
walinileta hapa, na kunilazimisha kufundisha somo ambalo kamwe sikulitaka (Mwalimu, Shule A,
Mkoa wa Singida).
3.5.3 Mitazamo ya waalimu kuhusu kazi ya ualimu
Uchambuzi wa majadiliano ya vikundi lengwa vya waalimu ulionyesha masuala kadhaa yanayoweza
kuchukuliwa kuwa ndiyo mitazamo waliyo nayo kuhusu kazi ya ualimu. Mitazamo hiyo inaweza kuwekwa
katika makundi makuu mawili, nayo ni mitazamo chanya na mitazamo hasi. Hapa tutaonyesha baadhi
ya mitazamo iliyo muhimu.
Mitazamo chanya (sababu zinazotia hamasa)
Mitazamo kadhaa chanya au sababu zinazotia hamasa kuhusu kazi ya ualimu zilibainishwa katika
majadiliano haya. Kwanza, waalimu walieleza kwamba walifurahia ukweli kwamba kazi ya ualimu
iliwapa fursa ya kuendelea kujifunza. Walidai kuwa ni ualimu pekee unaomwezesha mtu kujifunza
na kuongeza upeo wa maarifa yake kila mara. Pili, waalimu walibainisha pia ukweli kwamba ilikuwa
rahisi zaidi kwa waalimu kujiendeleza zaidi kimasomo kulinganisha na kazi nyingine. Hivyo basi, hali hii
iliwapa uwezekano wa kujiendeleza katika kazi zao na vilevile urahisi wa kubadili kazi. Tatu, waalimu
waliona kuwa walisikia faraja pindi kazi yao ilipothaminiwa, hususan na wanafunzi waliowafundisha.
Waliona kuwa wanafunzi wengi walithamini kazi yao. Nne, uwezekano wa kukutana na watu mbalimbali
na kujipatia marafiki wapya ulichukuliwa kuwa ni jambo chanya. Hapa chini kuna baadhi ya nukuu
zinazothibitisha mitazamo hiyo:
Ualimu umekuwa mzuri kwangu kwa sababu ninapata marafiki na kukutana na watu wapya kila
siku. Vilevile unatupatia fursa ya kujua maisha halisi ya Tanzania: nimeona jinsi nchi hii ilivyo
maskini na tajiri kupitia kwa watoto ninaowafundisha. Huu ni uzoefu mzuri kwangu mimi (Mwalimu,
Shule Z1, Mkoa wa Pwani).
Kitu kizuri kuhusu ualimu ni kwamba inabidi usome kila siku. Aina ya watoto tunaowafundisha siku
hizi ‘inatulazimisha’ kusoma. Kwa kuwa wanajua mambo mengi, usipopiga msasa akili yako,
26
utakuwa kichekesho darasani. Kwa hiyo katika ualimu inabidi usome kila siku na hii ni nzuri kwangu
(Mwalimu, Shule U, Mkoa wa Mtwara).
Wakati pekee ninaoufurahia katika kazi hii ni pale ninapoona wanafunzi wangu wakifanya vizuri
katika somo langu, nitaenda kuwaambia wenzangu na pale unapoonana na mkuu wa shule na
kuona anatabasamu; na hii inanifanya nijisikie vizuri (Mwalimu, Shule H, Mkoa wa Dodoma).
Inaleta faraja; ni vizuri kujua kuwa na mimi pia ninachangia kuboresha maisha ya mtu na kwamba
mimi pia ninajenga taifa (Mwalimu, Shule C, Mkoa wa Singida).
Mitazamo hasi (sababu zinazovunja moyo)
Walimu walibainisha mitazamo mingi hasi katika kazi ya ualimu, ambayo pia inaweza kuelezwa kuwa
ni sababu zinazoondoa hamasa au sababu ‘zinazovunja moyo’. Mitazamo hii kwa kiasi kikubwa ilihusu
maeneo makuu mawili, nayo ni mazingira duni ya kazi na mtazamo hasi kuhusu kazi ya ualimu (walio nao
wanajamii, wanafunzi na hata serikali). Hapa chini tumeonyesha na kufafanua baadhi ya hisia muhimu
za moyoni walizo nazo waalimu kuhusu maeneo haya.
Walimu wengi walilalamika kwamba wanafunzi wao hawawapi heshima wanayostahili walimu wao na
walikuwa na mitazamo hasi sana kuhusu kazi ya ualimu. Hii ilijitokeza zaidi katika baadhi ya shule
binafsi ambazo huchukua wanafunzi wanaotoka katika familia zenye uwezo. Kwa mujibu wa waalimu,
wanafunzi wa shule hizi waliamini kuwa waalimu wao wanafanya kazi ya ualimu kwa sababu ni maskini.
Hapa chini kuna maoni ya baadhi ya waalimu kuhusu suala hili:
...wanafunzi wananiona kama ‘nimechemsha’, mtu ambaye nimepotea. Wanaamini mwalimu ni mtu
maskini, hana mwelekeo maishani. Kuna wakati wanafunzi wananiuliza, “Mwalimu, una akili sana,
lakini sasa kwa nini uliamua kuwa mwalimu?” Maswali ya aina hii yanakera. Ina maana wanaamini
mwalimu ni mtu aliyefeli, asiye na akili. Ninapowaambia, “Nilipenda tu kuwa mwalimu”, wananiambia,
“Huoni kwamba ‘unachelewa katika maisha’?” Haya ndiyo maisha tunayoishi katika shule hii
(Mwalimu, Shule Z, Mkoa wa Pwani).
Ahaa, haa! Ngoja nikuambie kitu ... kuna mwanafunzi mmoja darasani mwangu ambaye ana akili
kwelikweli. Siku moja, ehee, nilimwambia, “Utakuwa mwalimu mzuri sana.” Kauli hiyo ilimfanya
alie sana. Nikashangaa kwa nini analia. Baadaye akaniambia kamwe hataki kuwa mwalimu,
na kwamba nilikuwa ninamtakia mabaya kumwambia atakuwa mwalimu mzuri. Nilijisikia vibaya
sana (Mwalimu, Shule Z, Mkoa wa Pwani).
Ama kuhusu mitazamo ya jamii na serikali kuhusu waalimu, waalimu walisema:
Hii ni kazi ngumu sana. Hakuna anayejali – si jamii ambako unafundisha, si serikali. Jamii inatuona
tumepotea, hatuna la maana na tutaishia kushindwa. Jamii inafanya maisha yetu hapa kuwa ya
ovyo sana kwa sababu hawathamini kile tunachokifanya. Halafu, mzazi wetu, serikali, ndiyo mbaya
zaidi. Wanawatupa tu mashuleni, wanaacha hivyo tu. Hakuna anayejali – hakuna nyumba, hakuna
usafiri. Unahangaika hata kupata mshahara wako; wala sizungumzii mishahara kuwa midogo
sana. Kuchagua kuwa mwalimu ni kuchagua kuhangaika maisha yako yote (Mwalimu, Shule C,
Mkoa wa Singida).
27
Pengine sababu zinazovunja moyo zilizobainishwa zaidi ni zile zilizohusiana na mazingira duni ya kazi
kama yanavyodhihirishwa na kuwepo kwa mishahara midogo na ukosefu wa zana za kufundishia na
kujifunzia. Waalimu wengi walizungumza kwa ukali kuhusu mishahara midogo waliyolipwa, na vilevile
ukweli kwamba shule nyingi hazikuwa na zana muhimu za kufundishia. Waalimu pia ‘walilia’ kwa ukali
kuhusu ukosefu wa programu za mafunzo kazini. Huku wakikosoa zaidi, walisema kuwa pindi fursa za
aina hiyo zinapotokea, wakuu wa shule zao ndio wanaohudhuria kwani zina marupurupu.
3.5.4 Mitazamo ya waalimu kuhusu wanafunzi kufanya vibaya kitaaluma na nini kifanyike
kuboresha kiwango cha elimu
Katika sehemu ya mwisho ya majadiliano ya vikundi lengwa, washiriki waliombwa kubainisha
mambo waliyodhani kuwa yalisababisha wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani ya taifa, hususan
wakitilia maanani Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne ya mwaka jana. Waliombwa pia
kupendekeza hatua zinazopaswa kuchukuliwa kurekebisha hali hiyo na kuboresha kiwango cha
elimu nchini kwa jumla.
Mambo makuu mawili yalibainishwa kuwa ndiyo husababisha wanafunzi kufanya vibaya. Kwanza,
waalimu walio wengi walitaja mazingira duni ya kazi kuwa ndiyo sababu kuu ya kufanya vibaya. Waalimu
walieleza bayana kwamba kwa mazingira duni ya kazi yaliyopo, waalimu hawakuwa wakifundisha kwa
uwezo wao wote na kwamba mazingira ya shule yalikuwa yakiwavunja moyo katika kutimiza wajibu wao
kwa ukamilifu na kwa ufanisi. Masuala makuu matatu yalitajwa bayana kuwa yalisababisha kuwepo
kwa mazingira duni ya kazi. Masuala hayo ni uduni wa mishahara na marupurupu mengine ya waalimu,
ukosefu wa zana za kufundishia na kujifunzia na uongozi na usimamizi mbaya wa shule.
Pengine mishahara duni ndiyo sababu iliyokuwa ikiwavunja moyo zaidi waalimu walio wengi. Walidai,
kwa mfano, kuwa mwalimu mwenye shahada alikuwa akipata mshahara ulio pungufu ya shilingi
500,000/- anapoajiriwa kwa mara ya kwanza, nao wakajiuliza ni waajiriwa wengine wangapi wa serikali
wenye kiwango cha elimu kilicho sawa na hicho ambao humudu kuendesha maisha yao kwa mwezi
kwa kiwango hiki cha mshahara? Walisema vilevile kwamba, licha ya mishahara midogo waliyokuwa
wakiipata, kuna makato mengi yanayozidi kupunguza kipato halisi wanachopokea.
Vilevile kulikuwa na suala la kupandishwa madaraja kazini. Waalimu wengi walilalamika kuwa upandishaji
wa madaraja hufanywa na mamlaka kama fadhila badala ya haki stahili ya mwalimu kulingana na sifa
njema alizo nazo. Waalimu walilalamikia zaidi urasimu mwingi uliopo katika kupandishwa daraja, na
vigezo vinavyotumiwa kumpandisha mwalimu daraja havikuwa wazi, jambo linalofanya mchakato mzima
kuwa na walakini. Mathalani, waalimu walilalamika kuwa ili waweze kufikiriwa kupandishwa daraja,
inawapasa ‘kuwa wema na kuwa karibu’ na maofisa wa Idara ya Huduma kwa Walimu (TSD), chombo
kinachoshughulikia masuala ya kitaaluma ya waalimu, ikiwa ni pamoja na upandishaji wa madaraja.
Pia, waalimu walilalamikia kuwepo kwa upungufu wa nyumba, hali iliyowalazimu kuishi maisha duni
sana kwani hawakuweza kumudu gharama za makazi mazuri mijini kwa sababu ya mishahara duni
waliyoipata. Tatizo la makazi duni lilikuwa kubwa zaidi kwa shule za vijijini, hususan shule za kata
za serikali. Shule nyingi za kata za serikali zilizotafitiwa hazikuwa na huduma ya umeme na hii
ilifanya maisha ya waalimu kuwa duni zaidi. Hapa chini kuna nukuu za maoni ya baadhi ya waalimu
zinazothibitisha hali hiyo:
28
...Kama unavyoona shule yetu iko kilometa 20 kutoka mjini. Hakuna umeme hapa, hakuna nyumba
za waalimu. Tunatakiwa kupanga nyumba kwa wenyeji, lakini nyumba zenyewe umeziona? Hivi,
serikali hii inatufikiriaje? Hivi hawajui kuwa na sisi ni binadamu, tumesoma na tunataka maisha
mazuri? Na mimi ninapenda kuona Manchester wakicheza, lakini ona: niko hapa, hakuna umeme,
hakuna usafiri kwenda mjini, na unataka nifundishe kwa furaha? (Mwalimu, Shule C, Mkoa wa
Singida.)
Ni bahati mbaya tu kuwa mwalimu katika nchi hii. Unapokea mshahara mdogo sana, na mshahara
huohuo unakatwa vibaya mno, makato mengi mno, ehee. Kwa mfano, kwa nini mchango wangu
wa bima ya afya uongezeke pale mshahara wangu unapoongezeka? Kwa nini wasiendelee na
kiwango kilekile, ukizingatia kwamba hata huwa siumwi kila siku? Kwa nini inakuwa hivi kwa
waalimu? (Mwalimu, Shule U, Mkoa wa Mtwara.)
Ufundishaji duni na vifaa/zana duni za kufundishia ilikuwa ni sababu nyingine iliyotajwa mara kwa mara
ya wanafunzi kufanya vibaya kitaaluma. Waalimu walilalamika kuwa shule zao kwa jumla hazikuwa
katika hali nzuri ya kuwezesha ufundishaji na ujifunzaji kufanyika. Mitazamo ya waalimu katika eneo hili
kwa kiasi kikubwa ilithibitisha matokeo ya utafiti uliofanywa kwa njia ya hojaji na miongozo ya taarifa
za shule. Mathalani, shule nyingi hazina maabara na maktaba zinazofaa. Kadhalika, masomo mengi
hayakuwa na vitabu vya kutosha vya kiada na ziada. Kwa sababu hiyo, ufundishaji uliachwa ufanywe
kwa kutegemea juhudi za mwalimu mwenyewe, na hili halingewezekana ukitilia maanani kiwango cha
chini cha hamasa na moyo wa kujitolea kilichopo katika kazi ya ualimu. Kwa mfano, waalimu walikuwa
na maoni kama:
Shule zimekuwa mahali pa vijana kukulia, hakuna ujifunzaji unaofanyika. Hakuna maktaba hapa,
hakuna maabara, hakuna vitabu. Waalimu wamechoka na wana huzuni wakati wote. Sasa utaiita
hii shule, hee? (Mwalimu, Shule A, Mkoa wa Singida.)
Hata hivyo, licha ya kukosolewa sana kwa hali duni ya mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji, kulikuwa
vilevile na maoni chanya katika shule chache, hususan shule binafsi zinazomilikiwa na asasi za Kikristo.
Katika shule hizi, hali ya zana za kufundishia na kujifunzia, kama ilivyoonyeshwa katika matokeo ya utafiti
kwa njia ya hojaji, ilikuwa nzuri mno na yenye kutia moyo kuliko katika shule nyinginezo. Kwa sababu
hiyo, waalimu wa shule hizi waliamini kuwa shule zao zilikuwa zikifanya vizuri zaidi katika mitihani kwa
sababu zilikuwa na mazingira yanayofaa na yenye kurahisisha mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji.
Kwa mfano, mwalimu mmoja, ambaye aliungwa na mkono kwa kauli moja na wengine katika kipindi
cha majadiliano ya vikundi lengwa, aliyetoka katika shule moja ya binafsi ya Kikristo mkoani Singida,
alikuwa na maoni haya:
Kwa jumla matokeo katika shule yetu ni mazuri. Hii ni kwa sababu shule ina zana bora za kufundishia
na kujifunzia, zikiwemo maabara. Vilevile tuna maktaba nzuri sana. Vilevile waalimu wanahudhuria
mara kwa mara programu mbalimbali za mafunzo zinazolenga kuboresha ufundishaji wao na
kubadilishana mawazo na ujuzi, ambazo huandaliwa na Tume ya Huduma za Jamii ya Kikristo.
Jambo jingine lililotajwa kusababisha wanafunzi kufanya vibaya kitaaluma lilikuwa ni uongozi na
usimamizi mbaya wa shule. Walimu walio wengi katika shule nyingi zilizotafitiwa walikosoa uongozi wa
shule zao, wakidai kuwa haukuwa makini na mahitaji ya waalimu. Waalimu pia walitoa maoni kwamba
kulikuwa na mawasiliano duni kati ya waalimu na uongozi wa shule zao. Wakikosoa zaidi, waalimu
29
walitoa maoni kwamba hapakuwa na utaratibu wa kutathmini kazi za waalimu hata pale walipofanya kazi
kwa uwezo wao wote katika mazingira magumu sana, badala yake uongozi wa shule ulikuwa mwepesi
kuwalaumu waalimu pindi wanafunzi walipofanya vibaya katika mitihani. Hapa chini kuna nukuu za
maoni ya baadhi ya waalimu kuhusu uongozi wa shule zao:
Uongozi wetu ni tatizo kubwa. Kwa mkuu wetu wa shule, maendeleo ya taaluma ni suala lisilo
muhimu sana. Hajali kama kuna zana za kufundishia au la. Halafu, kuna mawasiliano duni sana kati
yetu (waalimu) na yeye: ni vigumu sana kumwona, hakuna mikutano. Anajifanyia kila kitu yeye
mwenyewe (Mwalimu, Shule A, Mkoa wa Singida).
Uongozi wetu wa shule hauko makini katika kushughulikia matatizo ya waalimu. Hakuna usimamizi
wa shughuli za ufundishaji, hakuna semina kwa waalimu, hakuna anayejali. Mwalimu anaweza
kufundisha kwa mwaka mzima bila kuwa na andalio la somo, na hakuna atakayekuuliza. Shule
haina mwenyewe! (Mwalimu, Shule A, Mkoa wa Singida.)
Msingi duni wa wanafunzi kitaaluma na kitabia ni jambo jingine lililotajwa kusababisha wanafunzi
kufanya vibaya kitaaluma. Hali hii ilihusishwa zaidi na ukosefu wa maarifa ya msingi yanayohitajika ili
kumudu elimu ya sekondari. Waalimu walitoa maoni kwamba wanafunzi wengi wanaojiunga na elimu
ya sekondari, hususan shule za kata za serikali, wana msingi duni sana wa kitaaluma kiasi kwamba
hawawezi kumudu matakwa ya elimu ya sekondari. Kwa mfano, waalimu walitoa maoni kwamba
kiwango cha ujuzi wa kusoma na kuandika cha wanafunzi wengi kilikuwa cha chini sana huku baadhi
ya wanafunzi wakiwa hawajui kusoma na kuandika. Zaidi ya hayo, baadhi ya wanafunzi walikuwa na
ufahamu mdogo sana wa lugha ya Kiswahili. Ni dhahiri kwamba hili ni tatizo kubwa kwa sababu ikiwa
wanafunzi hawawezi kuwasiliana kwa ufasaha kwa Kiswahili pindi wanapojiunga na elimu ya sekondari,
watatarajiwa vipi waweze kumudu masomo yao ya sekondari yanayofundishwa kwa lugha ya Kiingereza?
Hapa chini kuna nukuu za maoni ya baadhi ya waalimu zinazothibitisha hali hii:
...kuna wanafunzi wengi wasiojua kusoma na kuandika katika shule yetu. Ninafundisha kidato cha
kwanza, na ninafahamu karibu wanafunzi kumi ambao hawajui kusoma wala kuandika. Sasa,
unategemea mimi nitawasaidiaje? (Mwalimu, Shule U, Mkoa wa Mtwara.)
Hii ni shule ya kata (ya serikali). Tunapokea wanafunzi duni sana, na kwa kweli tunapokea makombo:
wale ambao hawakuweza kuchaguliwa na shule za kitaifa za serikali. Wengi wa wanafunzi
tunaowapokea hawawezi kuandika vizuri, ujuzi wao wa Kiingereza ni mdogo sana na wanahitaji
muda mwingi ili waweze kumudu elimu ya sekondari (Mwalimu, Shule D, Mkoa wa Singida).
30
SEHEMU YA NNE
Muhtasari, Hitimisho na Mapendekezo
4.1. MuhtasariKwa kutumia mikabala yote miwili, mkabala wa kiidadi na mkabala wa kiubora, utafiti huu umechunguza
jinsi sifa za waalimu kitaaluma, hamasa na moyo wa kujitolea walio nao katika kufundisha vinavyoathiri
ufaulu wa wanafunzi kitaaluma katika elimu ya sekondari. Utafiti huu ulifanywa katika mikoa sita (6)
katika shule 36, ukishirikisha waalimu zaidi ya 300 kutoka shule za sekondari za serikali na za binafsi.
Waalimu walishiriki katika utafiti huu kwa kujaza hojaji na kupitia majadiliano ya vikundi lengwa.
Matokeo ya utafiti huu yameonyesha kuwepo kwa masuala kadhaa yanayohusiana na sifa za waalimu
kitaaluma, hamasa na moyo wa kujitolea kufundisha walio nao waalimu na jinsi masuala hayo
yanavyoathiri ufaulu wa wanafunzi kitaaluma. Masuala hayo yanajumuisha haya yafuatayo:
i. Sifa za waalimu kitaaluma, hamasa na moyo wa kujitolea walio nao katika kufundisha ni vigezo
muhimu mno vinavyoukilia ufaulu wa wanafunzi kitaaluma. Mwalimu kuwa na sifa nzuri za kitaaluma
pekee bila moyo wa kujitolea hakusababishi kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi kitaaluma kuimarika.
ii. Shule zenye waalimu wenye moyo wa kujitolea wa hali ya juu bila kujali iwapo walikuwa na sifa za juu
kitaaluma (shahada au zaidi) au la zilifanya vizuri katika mitihani ya taifa. Kwa upande mwingine,
shule zenye waalimu wenye sifa za juu kitaaluma lakini wenye kiwango kidogo cha moyo wa kujitolea
katika kazi ya ualimu si lazima kwamba zilifanya vizuri katika mitihani ya taifa kuliko zile zenye waalimu
wenye sifa za wastani kitaaluma (stashahada au chini). Hivyo, kwa mfano, shule za serikali zenye
idadi kubwa zaidi ya waalimu wenye sifa za juu kitaaluma hazikufanya vizuri kama shule binafsi za
Kikristo zenye idadi ya chini kiasi ya waalimu wenye sifa za juu kitaaluma.
iii. Mazingira mazuri ya kazi ndicho kigezo muhimu zaidi kinachoukilia kiwango cha moyo wa kujitolea
walio nao waalimu katika kufundisha, na matokeo yake kigezo hiki huwa na nguvu sana katika kuleta
matokeo mazuri ya wanafunzi kitaaluma. Matokeo ya utafiti huu yanazidi kuonyesha kuwa waalimu
wa shule binafsi za Kikristo wameridhika kwa kiasi kikubwa mno na mazingira ya kazi ya shule zao
kuliko waalimu wa shule za serikali na shule binafsi zinazomilikiwa na watu binafsi. Hali hii, kwa kiasi
fulani, huonyesha kwa nini wanafunzi wa shule binafsi za Kikristo hufaulu vizuri mno kitaaluma kuliko
wale wa shule za serikali na shule nyingine za watu binafsi.
iv. Waalimu walio wengi katika shule za serikali, shule za Kiislamu na shule za watu binafsi waliona
kuwa uongozi wa shule zao ulifanya kazi kwa ufanisi mdogo sana. Zaidi ya hayo, waalimu walioona
kuwa uongozi wa shule zao ulifanya kazi kwa ufanisi mkubwa walielekea kuwa na moyo wa kujitolea
zaidi katika kazi ya ualimu, na matokeo yake shule zao zilifanya vizuri zaidi katika mitihani ya taifa
kuliko shule ambazo waalimu wake waliona kuwa uongozi wa shule haukufanya kazi kwa ufanisi.
v. Matokeo ya uchunguzi wa majadiliano ya vikundi lengwa (matokeo ya kiubora) yanaonyesha kuwa
kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kazi ya ualimu ni cha chini kupindukia.
Hali hii hujitokeza zaidi kwa waalimu wa shule za serikali na shule za watu binafsi. Matokeo haya
yanaonyesha kuwa, kwanza, waalimu wachache tu ndio waliochagua kwa hiari yao kufanya kazi ya
31
ualimu na kwamba mazingira duni ya kazi yaliyopo katika shule nyingi za serikali na mishahara midogo
wanayoipata husaidia tu kuonyesha na kusisitiza jinsi waalimu hao wasivyoipenda kazi ya ualimu.
Athari za kiwango kidogo cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu ni kubwa mno na zinaonekana
bayana kwa kuwepo matokeo mabaya ya wanafunzi kitaaluma katika shule za serikali na za watu
binafsi. Zaidi ya hayo, kiwango kidogo cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kazi ya ualimu
kwa kiasi fulani kinaweza kuonyesha msuguano mkubwa uliopo miongoni mwa waalimu.
vi. Matokeo ya utafiti huu hayaonyeshi jinsi hali ilivyo katika shule zote zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu.
Mathalani, wakati kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kilikuwa na uhusiano mkubwa
na ufaulu wa wanafunzi katika shule za serikali na shule za Kikristo, hapakuwa na uhusiano wa
moja kwa moja kati ya kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu na ufaulu wa wanafunzi
miongoni mwa shule zinazomilikiwa na asasi za Kiislamu. Hali hii inaonyeshwa na ukweli kwamba,
wakati kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu katika shule hizi kilikuwa cha juu kwelikweli,
ufaulu wa wanafunzi kitaaluma katika shule hizi ulikuwa duni kwelikweli. Hata hivyo, matokeo haya
hayana budi kutafsiriwa kwa uangalifu kwani ukubwa wa sampuli ya waalimu katika shule za Kiislamu
kwa kiasi fulani ilikuwa ndogo mno kulinganisha na shule nyingine.
vii. Utafiti huu haukuchunguza kwa kina suala la vigezo vinavyotumiwa katika kuwapangia waalimu
masomo ya kufundisha, suala ambalo lilikuwa mojawapo ya malengo ya utafiti huu. Sababu kubwa ni
kwamba ilidhihirika kwamba hakika waalimu hufundisha masomo waliyosomea katika vyuo vya
ualimu au vyuo vikuu. Hivyo, kigezo kikuu kilichotumiwa na wakuu wa shule kuwapangia waalimu
masomo ya kufundisha ni kwamba mwalimu anatakiwa kuwa amesoma somo hilo chuoni.
4.2. Hitimisho na MapendekezoUtafiti huu umeonesha mambo makuu matatu kuhusiana na waalimu ambayo huchangia/kuamua ufaulu
wa wanafunzi kitaaluma, nayo ni sifa za walimu kitaaluma, kujituma na moyo wao wa kujitolea kwa kazi
ya ualimu na mtazamo walio nao kuhusu ufanisi wa uongozi wa shule. Pindi waalimu wanapokuwa na
moyo wa kujitolea na mtazamo chanya kuhusu uongozi wa shule, wanafunzi huelekea kufanya vizuri
zaidi katika kazi zao za kitaaluma.
Hata hivyo, ukiacha shule binafsi zinazomilikiwa na asasi za Kikristo, matokeo ya utafiti huu yanaonesha
kuwa kiwango cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kazi ya ualimu ni cha chini sana na
kwamba waalimu walio wengi wanaona uongozi wa shule zao kuwa ni duni na usiofanya kazi kwa
ufanisi. Kiwango duni cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu na uongozi mbaya wa shule kwa kiasi
fulani husababisha wanafunzi wa shule nyingi nchini kufanya vibaya kitaaluma.
Kwa kuzingatia hitimisho hili, mapendekezo yafuatayo yanatolewa kwa lengo la kuboresha kiwango
cha kujituma na moyo wa kujitolea walio nao waalimu kwa kazi ya ualimu, na vilevile ufanisi wa uongozi
wa shule, ambapo matokeo yake kufanya hivyo kunaweza kuleta manufaa katika ufaulu wa wanafunzi
kitaaluma na kubadilisha hali duni ya matokeo ya mitihani ya taifa ya kidato cha nne. Mapendekezo haya
yamefikiwa kutokana na matatizo yanayojitokeza katika matokeo hayo, na vilevile kutokana na maoni ya
washiriki kuhusu namna ya kuboresha kiwango cha elimu nchini.
i) Kujituma na moyo wa kufanyakazi walio nao waalimu umejitokeza kama tatizo kuu linaloathiri ufaulu
wa wanafunzi kitaaluma, huku waalimu walio wengi, hususan katika shule za serikali, wakionyesha
kuwa na kiwango cha chini sana cha moyo wa kujitolea kwa kazi ya ualimu. Kiwango hiki kidogo sana
32
cha moyo wa kujitolea walio nao waalimu kinasababishwa zaidi na malipo duni na mazingira duni ya
kazi katika shule na kile ambacho waalimu wanakiita ‘serikali kutojali’ kazi ya ualimu. Ili kuinua moyo wa
kujitolea wa waalimu kwa kazi ya ualimu, hatua zifuatazo hazina budi kutiliwa maanani:
a. Serikali na wadau wengine wanapaswa kushughulikia kwa dhati tatizo la mazingira duni ya kazi
wanayokabiliana nayo waalimu, ikiwa ni pamoja na tatizo la makazi, huduma za jamii kama vile
maji na umeme.
b. Suala la malipo duni lilijitokeza kama tatizo kubwa katika kuvutia waalimu kujiunga na kuendelea
na kazi ya ualimu. Mishahara ya waalimu bado ni midogo mno kiasi cha kusikitisha. Ikumbukwe
kwamba utafiti huu na tafiti nyingine nyingi zimeonyesha kila mara kwamba malipo duni ndiyo
sababu inayowakatisha tamaa sana waalimu. Hivyo basi, tatizo hili halina budi kushughulikiwa
kama tatizo la dharura iwapo tunataka kuboresha kiwango cha elimu na kubadilisha hali duni
ya matokeo ya mitihani ya taifa. Sambamba na kuboresha malipo ya waalimu, suala la kuwapandisha
waalimu madaraja kwa wakati halina budi kushughulikiwa kwa kupunguza urasimu usio wa
lazima katika mchakato huo. Kwa sasa waalimu wengi wamefanywa kuamini kuwa kupandishwa
daraja ni suala la wateule wachache, badala ya kuwa suala la stahili ya mwalimu kulingana na sifa
njema alizo nazo.
c. Tunapaswa kuwa na viwango vya chini kabisa vinavyokubalika vya shule kuitwa shule. Kwa sasa,
kuna tofauti kubwa sana miongoni mwa shule, kwani kuna zile zinazohangaika hata kupata chaki
na shule zenye vifaa vya kutosha kama vile maktaba na maabara. Programu zetu za elimu ambazo
zinaonesha kwa muda mrefu mno zimekuwa zikijishughulisha zaidi na idadi hazina budi kupitiwa
upya na kutilia maanani zaidi suala la kuongeza ubora.
d. Ni muhimu kuwa na taratibu za kuwatambua na kuwatuza waalimu wanaofanya kazi kwa
kiwango kizuri sana kuzidi wengine. Kwa sasa, juhudi za ziada za waalimu hazitambuliwi wala
kutuzwa. Wakati wa majadiliano ya vikundi lengwa, waalimu wengi walilalamika kwamba
wanafunzi pekee ndio wanaotambuliwa na kutuzwa pindi wanapofaulu vizuri sana. Lakini
tunaelekea kusahau kwamba kwa kila mwanafunzi anayefaulu vizuri sana, kuna mwalimu aliyefanya
juhudi zaidi kumwezesha kufaulu, na juhudi hizi hazina budi kutambuliwa na kutuzwa ipasavyo.
e. Ni suala muhimu sana kwenye kazi ya ualimu, walimu wenyewe wakifahamu kikamilifu Sera ya
Elimu na Mafunzo na maelekezo/maagizo mengine yote na program/mipango inayotolewa na
viongozi ngazi za juu kuletwa kwao. Walimu kuzielewa sera na mipango ni muhimu sana ili
wazitekeleze vyema na kwa tija, hatimaye waboreshe ufanisi wa sekta ya elimu na uwajibikaji
f. Mchakato wa kudahili wanafunzi wanaokwenda kujiunga na kozi ya ualimu tarajali vyuoni kuna
haja ya kuupitia upya na kuuboresha. Tanzania inahitaji watu ambao si tu wana shauku ya
kufundisha bali wawe na nia thabiti na uwezo wa kufundisha kwa ufanisi. Vigezo vya kudahili
wanafunzi wanaokwenda kusomea ualimu na kufundisha vinapaswa kuwa sawa kwa wale
waliofaulu vizuri tu masomo yao ngazi za sekondari kama ilivyo kwa wanaochukuliwa kusomea
udaktari na sheria. Kushindwa kufanya hivyo tutaendelea kudhoofisha ubora wa elimu na
maendeleo katika nchi yetu.
33
g. Maadili kwa Walimu, kujituma uwajibikaji na uaminifu ni muhimu sana katika kurejesha hadhi na
thamani ya taaluma yao kwa ujumla. Walimu wakumbuke kuwa wamebeba jukumu kubwa la
maendeleo ya Tanzania na wana mchango wa kipekee kwenye kujenga mustakabli na mwelekeo
wa nchi yetu. Walimu wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwenye jamii na kwenye taaluma yao.
h. Walimu kufahamu haki zao na kusubiri wengine kuzitetea na kuzilinda hakutoshi, ni lazima
wajipange na kuchukua hatua kamili na za uhakika bila kukata tamaa hadi watakapoona haki zao
zimetekelezwa, huku wakihakikisha wanawajibika kwa viwango kubalifu kwa jamii.
ii) Ili kuboresha utendaji kazi wa waalimu kitaaluma, kuna haja ya kufufua programu endelevu za mafunzo
kazini kwa waalimu. Kwa sasa, programu hizi ni adimu, nazo hutolewa mara moja moja huku zikiwa
na nguvu ndogo ya kuboresha weledi wa waalimu. Hapana budi vilevile kuwa na programu za mara
kwa mara za mafunzo ya uongozi wa shule kwa sababu utafiti huu umeonesha kuwa waalimu wengi
katika shule nyingi wanasikitishwa sana na uongozi wa shule zao, jambo ambalo hatimaye huathiri
moyo wa kujitolea walio nao na hamasa yao ya kufundisha.
iii) Misingi duni ya kitaaluma ya wanafunzi ilijitokeza kama mojawapo ya sababu kuu za kuongezeka
kwa kiwango cha wanafunzi waliofeli katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne. Katika baadhi ya
shule, hali ilishtua kwa kiasi fulani kubaini kuwa baadhi ya wanafunzi wa shule za sekondari hawakujua
kuandika! Hivyo basi, kuna haja ya kuchunguza tena mwenendo wa Mtihani wa Darasa la Saba na
pengine kufikiria kuimarisha Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Pili kwa kurejesha tena viwango vya
kufaulu mtihani huo.
iv) Utafiti huu ulitumia sampuli ndogo tu ya shule zilizochaguliwa kwa kufuata utaratibu maalumu badala
ya kuzichagua kiholela. Hakika, baadhi ya vipengele vya shule kama vile shule za Kiislamu
viliwakilishwa kwani idadi ndogo sana kutokana sampuli nasibu. Kwa sababu hiyo, majumuisho
kuhusu matokeo haya hayana budi kufanywa kwa tahadhari na umakini sana.
v) Utafiti huu umechunguza kiwango cha kujituma na moyo wa kujitolea katika kazi miongoni mwa
waalimu. Ili kufanya ulinganifu, tafiti zitakazofuatia hazina budi kulenga namna ya kupata kiwango
cha kujituma, nia ya kufanya kazi na moyo wa kujitolea miongoni mwa walimu na taaluma nyingine
ili kuoanisha matokeo ya utendaji kwa ujumla.
34
Marejeo
Caprara, G.V., Barbaranelli, C., Steca, P. & Malone, P.S. (2006). Teachers’ self-efficacy beliefs as
determinants of job satisfaction and students’ academic achievement: A study at the school level.
Journal of School Psychology, 44, 473-490.
Ministry of Education and Vocational Training (MoEVT, June 2010). Secondary Education
Development Programme II (July 2010-June 2015).
Mosha, H.J. (1988). A reassessment of the indicators of primary education quality in developing
countries: Emerging evidence from Tanzania. International Review of Education, 17-45.
Mosha, H.J. (2011). The state of quality of education in Tanzania: A candid reflection. Makala
iliyowasilishwa katika Kongamano la Elimu, Dar es Salaam (Juni 2011).
National Examinations Council of Tanzania (NECTA, 2011). Examination results – Statistics for October
2010 results.
Oduro, G.K.T., Dachi, H., & Fertig, M. (2008). Educational leadership and quality education in
disadvantaged communities in Ghana and Tanzania. Makala iliyowasilishwa kwenye Mkutano wa
Baraza la Jumuiya ya Madola la Uongozi na Usimamizi wa Elimu, Durban, Afrika Kusini (Septemba
2008).
Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa (wa 61, Oktoba 2006). Wazungumzaji wanasisitiza umuhimu wa
elimu katika kufikia malengo ya maendeleo ya kijamii, Taarifa kwa Vyombo vya Habari, Inapatikana
katika intaneti: http://www.un.org/News/Press/docs/2006/gashc3847.doc.htm
Uwezo (2010). Are our children learning? Annual Learning Assessment Report Tanzania 2010. Dar es
Salaam: Uwezo, TENMET & Hivos/Twaweza.
01
Walimu ni sehemu muhimu katika kuleta elimu bora. Elimu bora inahusiana
moja kwa moja na ufundishaji bora na ujifunzaji bora. Kuna mambo mengi
yanayochangia ufundishaji bora na elimu bora, miongoni mwayo ni sifa za
kitaaluma na uzoefu wa waalimu, kujituma kwa walimu, viwango vya hamasa
waliyo nayo, moyo wa kujituma na hisia za kufundisha pamoja na mazingira
ya kazi.
Tafiti zinaonesha kuwa pindi waalimu wanapokuwa na moyo wa kujituma,
hamasa na wenye kuipenda kazi ya ualimu, wanafunzi pia huwa na hamasa
ya kujifunza na hujifunza maarifa yanayofundishwa na waalimu wao kwa ufanisi zaidi.
Kushuka kwa viwango vya elimu ya sekondari hapa nchini kumeleta mjadala mpana miongoni mwa
jamii ya Tanzania.
Hali hii ilipelekea Shirika la HakiElimu mwaka 2011 kufanya utafiti kuhusu sifa za walimu kitaaluma,
moyo wa kujituma na kufanya kazi na namna vinavyohusiana na utoaji elimu bora.
Chapisho hili ni taarifa kwa wananchi juu ya matokeo ya utafiti huo ambao umejumuisha maoni,
mawazo na mapendekezo ya wananchi juu ya namna ya kuwaboresha walimu na elimu yetu.
Tunawasihi wananchi, serikali na wapenda elimu wote waungane nasi kwa kusoma ripoti hii kisha
kuchukua hatua pale walipo.
HakiElimu inawezesha wananchi
kuleta mabadiliko katika elimu na
demokrasia
S.L.P. 79401 Dar es Salaam, Tanzania
Simu: (255 22) 2151852/3
Faksi: (255 22) 2152449