10
Ijue Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (Livestock Training Agency - LITA) Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (Livestock Training Agency - LITA) ni miongoni mwa wakala tatu za Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi. Kuanzishwa kwa LITA ni moja ya utekelezaji wa programu ya Mageuzi kwa Umma (PSRP II) ya kuanzisha Wakala wa Serkali ambazo huchukuwa maju- kumu ya kutekeleza kazi mbalimbali kwa niaba ya Serikali. Lengo likiwa ni kuboresha utendaji na uwajibikaji katika taasisi za umma. Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo ulianzishwa tarehe 1 September, 2011. Wakala huu ulianzishwa kwa kuunganisha Vyuo Sita vya Ma- funzo ya Mifugo (Livestock Training Institutes -LITIs) sam- bamba na kupanua majukumu ambayo yalifanywa na LITIs, kulingana na Sheria ya Wakala wa Serikali (Executive Agen- cies Act Cap 245 - R.E. 2009). Wakala ina malengo ya kutoa mafunzo bora ya mifugo, kufanya tafiti, ushauri, na uzalishaji wa mazao mbalimbali ya mifugo ili kukidhi mahitaji ndani na nje ya nchi. Mgeni rasmi Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya \mifugo na |Uvuvi Mh. Dr. Titus Mlengeya Kamani (MB) akizindua rasmi Baraza la Wafanyakazi wa LITA, Uzinduzi ulifanyika tarehe 2/4/2014, Morogoro Hotel Baraza la wafanyakazi wa LITA katika picha ya pamoja pamoja Baraza la wafanyakazi wa LITA katika picha ya pamoja pamoja na Mh. Dr. Titus Mlengeya Kamani (MB) baada ya uzinduzi wa Balaza la Wafanyakazi wa LITA Kiongozi Mkuu wa Wakala ni Mtendaji Mkuu (CEO) ambaye huteuliwa na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi. Mtendaji Mkuu anasaidiwa na wakurugenzi watatu ambao ni; Mkurugenzi wa Uzalishaji (DP), Mkurugenzi wa Mafunzo, Utafiti na Ushauri (DTRC) na Mkurugenzi wa Huduma (DBS). Pia Wakala ina vitengo huru viwili ambavyo ni; Ukaguzi wa ndani chini ya usimamizi wa Mkaguzi Mkuu wa ndani (Principal Internal Auditor), na kitengo cha Manunuzi kinachosimamiwa na Mkuu wa Manunuzi (Principal Sup- plies Officer) Wakala una Kampasi kuu sita na vituo viwili kama ifuatavyo; Tengeru (Arusha) Mpwapwa (Dodoma), Morogoro, Madaba (Ruvuma), Buhuri (Tanga), Temeke (Dar es Salaam), Kituo cha Ma- buki (Mwanza) and Kituo cha Kikulula (Kagera). Katika ngazi ya Kampasi Mtendaji Mkuu ana wakilishwa na Mkurugenzi wa Kam- pasi au Mkuu wa Kituo husika. Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo inayo Bodi ya ushauri (Ministerial Advisory Board) ambayo humshauri Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kuhusu muelekeo na utendaji wa wakala kwa ujumla. Dira Kuwa taasisi inayotoa mafunzo bora ya mifugo na huduma zina- zoendana ifikapo 2025. Majukumu ya Wakala Jukumu kubwa la Wakala ni kutekeleza malengo ya maendeleo ya sekta ya mifugo kama ilivyo ainishwa katika Sera ya Taifa ya Mifugo ya mwaka 2006. (National Livestock Policy 2006) na Mpango Mkakati wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi. Majukumu ya Wakala ni kama ifuatavyo: Kutoa mafunzo bora juu ya uzalishaji na afya ya mifugo; Uzalishaji bora wa mifugo na mazao yake;

Ijue Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (Livestock Training

  • Upload
    vancong

  • View
    717

  • Download
    62

Embed Size (px)

Citation preview

Ijue Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya

Mifugo

(Livestock Training Agency - LITA)

Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (Livestock Training

Agency - LITA) ni miongoni mwa wakala tatu za Wizara ya

Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi. Kuanzishwa kwa LITA ni moja

ya utekelezaji wa programu ya Mageuzi kwa Umma (PSRP II)

ya kuanzisha Wakala wa Serkali ambazo huchukuwa maju-

kumu ya kutekeleza kazi mbalimbali kwa niaba ya Serikali.

Lengo likiwa ni kuboresha utendaji na uwajibikaji katika

taasisi za umma. Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo

ulianzishwa tarehe 1 September, 2011.

Wakala huu ulianzishwa kwa kuunganisha Vyuo Sita vya Ma-

funzo ya Mifugo (Livestock Training Institutes -LITIs) sam-

bamba na kupanua majukumu ambayo yalifanywa na LITIs,

kulingana na Sheria ya Wakala wa Serikali (Executive Agen-

cies Act Cap 245 - R.E. 2009). Wakala ina malengo ya kutoa

mafunzo bora ya mifugo, kufanya tafiti, ushauri, na uzalishaji

wa mazao mbalimbali ya mifugo ili kukidhi mahitaji ndani na

nje ya nchi.

Mgeni rasmi Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya \mifugo na

|Uvuvi Mh. Dr. Titus Mlengeya Kamani (MB) akizindua

rasmi Baraza la Wafanyakazi wa LITA, Uzinduzi ulifanyika

tarehe 2/4/2014, Morogoro Hotel

Baraza la wafanyakazi wa LITA katika picha ya pamoja pamoja

Baraza la wafanyakazi wa LITA katika picha ya pamoja pamoja

na Mh. Dr. Titus Mlengeya Kamani (MB) baada ya uzinduzi wa

Balaza la Wafanyakazi wa LITA

Kiongozi Mkuu wa Wakala ni Mtendaji Mkuu (CEO) ambaye

huteuliwa na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi. Mtendaji

Mkuu anasaidiwa na wakurugenzi watatu ambao ni; Mkurugenzi

wa Uzalishaji (DP), Mkurugenzi wa Mafunzo, Utafiti na Ushauri

(DTRC) na Mkurugenzi wa Huduma (DBS). Pia Wakala ina vitengo

huru viwili ambavyo ni; Ukaguzi wa ndani chini ya usimamizi wa

Mkaguzi Mkuu wa ndani (Principal Internal Auditor), na kitengo cha

Manunuzi kinachosimamiwa na Mkuu wa Manunuzi (Principal Sup-

plies Officer)

Wakala una Kampasi kuu sita na vituo viwili kama ifuatavyo;

Tengeru (Arusha) Mpwapwa (Dodoma), Morogoro, Madaba

(Ruvuma), Buhuri (Tanga), Temeke (Dar es Salaam), Kituo cha Ma-

buki (Mwanza) and Kituo cha Kikulula (Kagera). Katika ngazi ya

Kampasi Mtendaji Mkuu ana wakilishwa na Mkurugenzi wa Kam-

pasi au Mkuu wa Kituo husika. Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya

Mifugo inayo Bodi ya ushauri (Ministerial Advisory Board) ambayo

humshauri Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi

kuhusu muelekeo na utendaji wa wakala kwa ujumla.

Dira

Kuwa taasisi inayotoa mafunzo bora ya mifugo na huduma zina-

zoendana ifikapo 2025.

Majukumu ya Wakala

Jukumu kubwa la Wakala ni kutekeleza malengo ya maendeleo ya

sekta ya mifugo kama ilivyo ainishwa katika Sera ya Taifa ya Mifugo

ya mwaka 2006. (National Livestock Policy 2006) na Mpango

Mkakati wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi. Majukumu

ya Wakala ni kama ifuatavyo:

Kutoa mafunzo bora juu ya uzalishaji na afya ya mifugo;

Uzalishaji bora wa mifugo na mazao yake;

Uzalishaji bora wa mifugo na mazao yake;

Kutoa ushauri bora juu ya uzalishaji na afya ya mifugo;

Kufanya utafiti juu ya uzalishaji, afya ya mifugo na masuala

yanayohusiana.

Lengo Kuu

Lengo la LITA ni kutoa maarifa na ujuzi juu ya uendelezaji wa

mifugo kwa umma kwa njia ya mafunzo, utafiti na huduma za

ushauri pamoja na uzalishaji ili kuifanya sekta ya mifugo iwe

endelevu.

Malengo Mahsusi

Aidha, malengo mahsusi ya LITA ni kama ifuatavyo:

Kuongeza udahili wa wanafunzi wa muda mrefu na mfupi kwa

ajili ya program za mafunzo ya uzalishaji na afya ya mifugo;

Kuboresha na kuongeza uzalishaji katika mashamba ya Wakala;

Kufanya utafiti na huduma za ushauri bora juu ya uzalishaji na

afya ya mifugo;

Kuimarisha miundo mbinu ya kutoa mafunzo na uzalishaji;

Kuboresha usimamizi wa fedha na rasilimali za Wakala;

Kuimarisha usimamizi wa rasilimali watu;

Kuimarisha mifumo ya usimamizi wa utendaji katika wakala;

Kushughulikia masuala mtambuka mfano VVU/UKIMWI, jinsia,

utawala bora, na mazingira.

Jengo la Utawala la Kampasi ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo

Tengeru—Arusha

Udahili wa wanafunzi

Chati 1 hapo juu inaonyesha udahili wa wanafunzi tangu

mwaka 2000. Ni dhahiri kumekuwa na ongezeko la wana-

funzi waliodahiliwa tangu LITA ilipoanzishwa. Idadi ya wana-

funzi waliodahiliwa iliongezeka toka 1622 (2011) mpaka

2216 (2013). Wakala inakusudia kuongeza idadi ya udahili

mwaka hadi mwaka kulingana na upanuzi na ukarabati wa

miundo mbinu katika Vituo/Kampasi zake, sambamba na

kuongeza idadi ya wakufunzi.

Idadi ya wahitimu tangu mwaka 1998

Chati 2 hapo juu inaonyesha idadi ya wanafunzi walio-

hitimu tangu mwaka 2000, ni dhahiri kwamba idadi ya wa-

hitimu imeongezeka tangu Wakala ilipoanzishwa. Miradi

mbalimbali imetekelezwa katika Kampasi za LITA mfano

ujenzi wa hosteli na madarasa pamoja na ukarabati. Maa-

bara mpya zimejengwa na zingine kukarabatiwa ikiwa ni

pamoja na kuweka vifaa mbalimbali kwa ajili ya kutoa ma-

funzo bora.

Wakala una mikakati ya kujenga madarasa, hostel na maa-

bara mpya ili kuongeza udahili. Vitengo vya uzalishaji vitai-

marishwa kwa ajli ya mafunzo kwa vitendo na kuongeza

pato la Wakala. Kufikia malengo yake Wakala unatumia

mikakati mbalimbali ili kuiwezesha Wakala kukua.

Madarasa ya Kampasi ya Temeke iliyoko Dar es Sa-

laam

Kufikia malengo yake Wakala unatumia mikakati

mbalimbali ili kuiwezesha Wakala kukua. Umuhimu

wa kuimarishwa kwa LITA na ungezeko la udahili ni

dhahiri, kwani sekta ya mifugo nchini inahitaji maaf-

iza ugani wa mifugo 17,325, wakati walioko ni 5,157

(30%). Lengo la Wakala ni udahili wa wanafunzi 5,000

kwa mwaka ifikapo mwaka 2016.

Madarasa ya Kampasi ya Temeke iliyoko Dar es Sa-

laam

Kuboresha mafunzo ni miongoni mwa jitihada za Wa-

ziri wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mh.

Dr. Titus Mlengeya Kamani (MB). Picha hapo juu ni

Waziri (kulia) akielezewa jambo na Kaimu Mtendaji

Mkuu Mama M. Pallangyo, wakati waziri alipokitem-

belea Kituo cha Kikulula

Kozi zinazotolewa na Wakala wa Vyuo vya Mafunzo

Stashahada ya uendeshaji wa nyanda za malisho na udhibiti

wa ndorobo (DRMTC)

Stashahada ya uendeshaji wa nyanda za malisho na

udhibiti wa ndorobo (DRMTC)

Astashahada ya afya na uzalishaji wa mifugo –

CAHP

Astashahada ya ufundi sanifu wa maabara ya vet-

erinari – CVLT Kozi maalumu zinatolewa pia kulin-

gana na mahitaji ya wateja

Wanafunzi wa Kampasi ya Tengeru katika ma-

funzo kwa vitendo

Wanafunzi wa Kampasi ya Tengeru wakichoma

sindano ya madini ya chuma kwa vitoto vya ngu-

ruwe na kukata meno (tooth clipping)

Kozi fupi kwa wakulima wafugaji zinazotolewa na

LITA:

Ufugaji bora wa ngómbe wa maziwa;

Ufugaji bora wa ngómbe wa nyama;

Unenepeshaji wa ngómbe wa nyama (Beef Fatten-

ing);

Ufugaji bora wa nguruwe;

Ufugaji bora wa mbuzi wa maziwa;

Ufugaji bora wa kuku wa kisasa na kienyeji;

Usindikaji wa maziwa;

Uboreshaji wa ngozi na mazao yake;

Kutoa Mafunzo kwa Wakulima-wafugaji

Kampasi za LITA zinatoa mafunzo kwa wakulima wa-

fugaji tangu mwaka 1984, wengi kati yao wakiwa wa-

kulima wadogo toka maeneo mbalimbali ya nchi ya

Tanzania. Wakulima-wafugaji huendesha shughuli za

kilimo na ufugaji ili waweze kujikimu katika maisha

yao ya kila siku. Wengi wao hupata tatizo la uhaba

wa chakula kila mwaka haswa wakati wa kiangazi.

Mafunzo kwa wakulima-wafugaji yameleta manufaa

kwao kwani yameendeshwa kwa vitendo (kujifunza

kwa kufanya).

Mafunzo kwa Wafugaji

Wakulima wafugaji hupata mafunzo katika Kampasi

za Wakala katika maeneo mbalimbali ya ufugaji

mfano ufugaji bora wa ngómbe wa maziwa, kusindika

maziwa, uboreshaji wa malisho, ufugaji bora wa

kuku, Uhudumu wa afya ya mifugo katika jamii,

kilimo hai n.k. Mafanikio katika kozi hizo fupi yanato-

kana na ushirikiano wa LITA na wadau wengine

mfano World Vision, KKKT-Mradi wa Mitamba, Heifer

International Tanzania, Halmashauri mbalimbali za

miji Tanzania n.k. LITA inakusudia kuimarisha kozi za

wakulima-wafugaji kwa kupanua na kukarabati mi-

undo mbinu yake sambamba na kutafuta wadau

mbalimbali ambao wanaweza kufadhili mafunzo kwa

wakulima-wafugaji. Mafunzo kwa wakulima-wafugaji

yameboresha maisha ya wafugaji kutokana na uzal-

ishaji kuongezeka, na hivyo kuongeza kipato na

usalama wa chakula katika kaya.

Uzalishaji katika Vitengo na Mashamba ya LITA

LITA ina eneo la Hekari 4,731.4 ambazo ziko

kwenye Kampasi mbalimbali za LITA; Tengeru

(320.4 ha), Mpwapwa (500 ha), Morogoro (50

ha), Madaba (1,400 ha), Buhuri (855 ha), Temeke

(6 ha), Mabuki (500 ha) and Kikulula (1,600 ha).

Mashamba ya Wakala hutumika kuzalisha mifugo

mfano; ngómbe wa maziwa, ngómbe wa wan-

yama, kondoo, mbuzi, mabata, nguruwe, farasi.

Mashamba hayo pia hutumika kuzalisha malisho

kwa ajili ya kulishia wa mifugo pamoja na kuuza

ziada kwa wafugaji walio jirani. Mazao ya chakula

ya aina mbalimbali pia huzalishwa katika

mashamba ya LITA mfano mahindi, alizeti na ma-

harawe. Mashamba ya Wakala pia yana misitu ya

asili na ya kupandwa.

Ngómbe wa maziwa kampasi ya Tengeru

Uzalishaji wa Mabata Kampasi ya Mpwapwa

Uzalishaji Malisho

Ili uzalishaji wa ngómbe wa maziwa na nyama una

tija endapo malisho ya kutosha yanazalishwa

kufikia kiwango cha mahitaji ya mifugo. Ili kukidhi

mahitaji ya msingi ya mnyama LITA imetekeleza

miradi ya umwagiliaji ili kuwezesha uzalishaji wa

malisho ya kutosha hasa katika misimu ya kian-

gazi. Miradi ya umwagiliaji wa malisho umeon-

geza na kuboresha uzalishaji wa malisho ya kuto-

sha na kupunguza athari za kiangazi na ukame.

Ngómbe wameweza kutoa maziwa mengi bila ku-

pungua uzito katika msimu wa kiangazi. Pia mal-

ekta ya mifugo ina mchango mkubwa katika pato la taifa na

haswa kwa jamii zilizoko vijijini, hivyo kuimarishwa

kwa sekta hii kutaleta mchango mkubwa kwa maisha

vijijini na umma wa Tanzania kwa ujumla. Uzalishaji

wa mifugo ulio thabiti nchini utaiwezesha jamii ya

Tanzania kuwa na maisha bora, na kustahimili changa-

moto za ukame utokanao na mabadiliko ya tabia nchi

ambazo hufanya mazao kukauka shambani au ku-

sombwa na mafuriko wakati wa mvua nyingi. Hivyo

uzalishaji bora wa mifugo huchangia kwa kiasi ki-

kubwa usalama wa chakula katika kaya.

Uzalishaji wa malisho Kampasi ya Tengeru

Utengenezaji wa Hei (Hay baling) Kampasi ya

Morogoro

Sera ya matokeo makubwa sasa (BRN) inaweza pia

kuweka mipango mkakati ya kuongeza uzalishaji wa

malisho nchini kwa kuanzisha miradi mbalimbali ya

umwagiliaji wa malisho. Kwa kufanya hivyo malisho

yatapatikana wakati wa kiangazi. Mipango hiyo

inaweza kwenda sambamba na kuhifadhi pamoja na

kumboresha masalia ya mazao mbalimbali mfano ma-

salia ya maharagwe, mahindi, ngano n.k. Mafunzo kwa

wakulima-wafugaji wadogo juu ya uzalishaji wa mal-

isho bora, kuhifadhi/kuboresha masalia ya mazao ita-

saidia kupunguza athari za ukame kwa mifugo. Mifugo

ikiwa na afya nzuri hata wakati wa kiangazi itawezesha

ngómbe wa nyama kupata bei nzuri na wale wa

maziwa kuendelea kutoa maziwa vizuri. Unenepeshaji

Dume la Mbegu – kwenye Kampasi ya Buhuri

Utafiti na Huduma za Ushauri

Utafiti pamoja na huduma za Ushauri juu ya Afya

na Uzalishaji wa Mifugo ni muhimu sana katika

kuboresha na kuleta maendeleo katika sekta ya

mifugo. LITA ni mdau mpya katika nyanja ya uta-

fiti kwani kabla ya LITA kuanzishwa LITI haziku-

jishughulisha na kazi za utafiti. Baada ya LITA

kuanzishwa na kuongeza majukumu yake utafiti

imekuwa ni moja ya majukumu ya Wakala. Hata

hivyo shughuli za utafiti zinahitaji fedha nyingi,

hivyo ushirikiano na taasisi zingine zinazofadhili

tafiti ni muhimu. Katika kufanya utafiti na

huduma za ushauri Wakala utaongeza kasi ya ku-

leta maendeleo katika sekta ya mifugo. Wakala

imefanya mchakato wa kuboresha na kuongeza

uwezo wa wakufunzi wake kwa kuwapa mafunzo

ya muda mfupi.

LITA inatoa huduma ya ushauri katika maeneo

mbalimbali ya ujuzi kama ifuatavyo:

Ufugaji wa ngombe wa maziwa na nyama,

Ufugaji wa mbuzi wa maziwa na nyama,

Usindikaji wa maziwa,

Kutathimini miradi kwa mbinu shirikishi,

Mafunzo ya mbinu bora za ufundishaji kwa wa-

kufunzi,

Jinsia na maendeleo

Uzalishaji wa mifugo na hifadhi ya mazingira,

Ufugaji/kilimo hai

LITA inafanya tafiti katika maeneo mbalimbali

kama ifuatavyo:

Kuboresha uzalishaji wa kuku wa kienyeji,

Kuboresha afya na uzalishaji wa mifugo,

Maendeleo endelevu ya sekta ya mifugo,

Mifumo ya masoko na kuongeza thamani,

Picha ya pamoja baada ya kuhitimu mafunzo ya kuende-

sha tafiti

Vituo na Kampasi za LITA

SN Kampasi/Kituo

Mkoa/Eneo

Anuani

KAMPASI YA TENGERU

ARUMERU ARUSHA

S. L. P. 3101, Arusha

KAMPASI YA MPWAPWA

S. L. P. 51, Mpwapwa

DODOMA

KAMPASI YA MOROGORO

S. L. P.603, Morogoro

KAMPASI YA MADABA

S.L.P 368

MADABA SONGEA

KAMPASI YA BUHURI

S.L.P

TANGA

KAMPASI YA TENMEKE

S.L.P

TENEKE - VETENARY