Upload
others
View
7
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
Somo la 12 kwa ajiliya Juni 22, 2019
Kila familia ya Kikristo ni kituo cha ushawishi ambacho Munguhukitumia kuwabariki wale wanaokizunguka.
Nini watu wanaona pale wanapokutana na familia yako? Ni maneno gani wanayoyasikia? Ni mtazamo gani wanaouangalia? Ni mbaraka gani wanaopokea?
Mbaraka kwa watembeleaji.
Mbaraka kwa ndugu.
Mbaraka kwa wasio Wakristo.
Mbaraka kwa jamii.
Mbaraka kwa wageni.
“Ndipo akasema, wameona nini katika nyumba yako? Hezekia akajibu, wameviona vitu vyote vilivyomonyumbani mwangu; hapana kitu katika hazina yangunisichowaonyesha.’” (Isaya 39:4)
Isaya alimwambia mfalme Hezekia kwambaanaenda kufa kwa ugonjwa. Hezekia alilia nakuomba kwa ajili ya hilo, hivyo Mungualimwongezea miaka 15 zaidi.
Jua lilirudi nyuma kimiujiza kama ishara kwaHezekia. Wanaanga wa Babeli walishangazwana tukio hilo, hivyo walituma wawakilishikwenda Yuda kufuatilia jambo hilo.
Hii ilikuwa ni fursa kubwa zaidi ya kuongeleauweza mkubwa wa Mungu!
Hata hivyo, “…Hezekia hakumrudishia vivyo...” (2Mambo ya nyakati. 32:25). Aliwaonyeshautajiri wake, na Mungu aliwekwa pembeni.
MBARAKA KWA WATEMBELEAJI
Kila nyumba ya Mkristo nimbaraka kwa wale wanaoitembelea.
Hawabarikiwi na TV zetu zilizomondani au mapambo mazuri ndanimwetu.
Mbaraka wanaoupata ni sawa nanamna ambayo Yesu anaakisiwandani yetu.
Maneno na matendo yetu yanaongea hadithi ya upendona upole wa Yesu. Wanaotutembelea watasemakwamba mibaraka yetu inatoka kwa Mungu pekee.
Je, wanaokutembelea wanaweza kuihisi amani katikafamilia yako? Ni hisia gani unawapatia pale wanapoingianyumbani mwako?
“Huyu akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambiatumemwona Masihi (maana yake, Kristo). Akampeleka kwa Yesu naye Yesu…”
(Yohana 1:41-42)
Wakati Andrea alipokutana na Yesu, aliishirikisha shaukuyake na kaka yake kwanza. Baraka zetu mara zote lazimakwanza tuzishirikishe kwa ndugu zetu. Mbaraka mkubwatunaoweza kuutoa ni Yesu.
Tumeitwa kumshiriki Yesu hasa kwa watoto wetu(Kumbukumbu la Torati 6:6-7).
Toa muda na jitihada za kutosha mara kwa mara kwa ajili ya ibada yako binafsi naibada ya familia. Nyakati hizo zitatunzwa katika akili na mioyo ya wanafamiliawako.
Kumbuka mfanoNaomi,ambaye aliishikishaimani yake na mkwe wake Ruthu ambaye alimpokeaMungu wa kweli.
Je, ni kwa jinsi gani mtu asiyeamini atakaswe namwenzi wake?
Mtu asiyeamini hupokea mibaraka ya Mungukupitia wenzi wao walio waumini.
Je, inampasa Mkristo kumwacha mwenziasiyeamini ikiwa mwenzi huyo ataleta taabu?
Katika aya ya 13, Paulo anaeleza kuwa wasifanyehivyo. Hata hivyo, katika aya ya 15, alielezakuwa ikiwa mtu asiyeamini atatata kuachana, basi kuachana kukubaliwe (kwa ajili ya kutafutaamani).
Kumbuka kuwa kuendeleza mfano wa wauaminifu na utii kwa Kristo itaongoza katikauongofu wa mwenzi asiyeamini (1 Petro 3:1-2).
“Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo.” (1 Wakorintho 11:1)
Tunashauriwa kumufuata Kristo, nakuwafuata wale wanaomfuata Kristo (1 Wakorintho 4:16; Waefeso 5:1; 1 Wathesalonike 1:6; Waebrania 6:12; 13:7; 3 Yohana 11). Kwanini?
Mfano ni njia bora ya ufundishaji. Tunaigakile tunachokiona. Kama familia, sisi nimfano kwa wale wanaoona mitazamomuhimu ndani yetu.
Upedo tunaouonyesha, namnatunavyoelimisha watoto wetu, namnatunavyotatua migogora, namnatunavyowatendea wengine. Tunawezakumwaksi Kristo katika kila kitu tunachofanya.
Ingawa kuaksiwa kwa Kristo ndani yetu siyokamili, kila nyumba ya Mkristo inayomfuataKristo ni mbaraka kwa jamii inayowazunguka.
Ukarimu unahusisha kufungua nyumbazetu kwa ajili ya wale wanaohitajipumziko, chakula au usaidizi.
Waumini katika Agano la kale na Aganojipya waliufanya ukarimu kuwa tabia yamara kwa mara (Mwz. 18:1-8; 19:1-3; 24:17-31; Lk. 5:19; 19:1-9).
Tunapokuwa wenyeji wa mtu fulani kwamasaa au siku kadhaa, tunawezakuanzisha urafiki, kuongea juu ya Yesu, kuomba, kushirikisha kweli za Biblia, nakuonyesha upendo wetu kwa Yesu kwamaneno yetu na matendo yetu.
Ukarimu ni mbaraka kwa wote wagenikwa wenyeji (Waebrania13:2).
“Wigo wetu wa ushawishi unaweza
ukaonekana mdogo, uwezo wetu
mdogo, fursa zetu chache, kupata
kwetu kidogo; lakini bado uwezekano
wa ajabu ni wetu kupitia kutumia kwa
uaminifu fursa zilizoko nyumbani
mwetu wenyewe. Kama tutafungua
mioyo na nyumba zetu kwa kanuni za
Mungu za uzima tutakuwa mifereji ya
umeme unaotoa nguvu ya uzima.
Kutoka nyumbani mwetu itatililika
mifereji ya uponyaji, kuleta uzima, na
uzuri, na kuzaa matunda pale ambapo
sasa pana huruma na vifo”
E.G.W. (The Adventist Home, cp. 4, p. 32)