7
1 TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR HOTUBA YA MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI MHE. JECHA SALIM JECHA KATIKA MKUTANO NA WADAU WA UCHAGUZI KUHUSIANA NA KAZI YA UCHUNGUZI WA IDADI, MAJINA NA MIPAKA YA MAJIMBO YA UCHAGUZI WA ZANZIBAR Waheshimiwa Makamishna wa Tume ya Uchaguzi, Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa; Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya; Wakuu wa Vyombo vya Serikali; Viongozi na Wawakilishi wa Vyama vya Siasa; Viongozi wa Asasi za Kijamii; Wawakilishi wa Vyombo vya Habari; Maafisa wa Tume ya Uchaguzi; Mabibi na Mabwana Itifaki imezingatiwa Asslam -Aleyikum Nachukuwa nafasi hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuwa pamoja tukiwa salama na wazima wa afya. Pili, nichukuwe nafasi hii kutoa shukurani kwenu kwa kuupokea kwa mikono miwili mwaliko wetu na

Hotuba Ya Mwenyekiti Wa Tume Kwa Wadau Wa Majimbo--

Embed Size (px)

DESCRIPTION

Siasa za Tanzania

Citation preview

  • 1

    TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

    HOTUBA YA MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI MHE. JECHA

    SALIM JECHA KATIKA MKUTANO NA WADAU WA UCHAGUZI KUHUSIANA NA KAZI YA UCHUNGUZI

    WA IDADI, MAJINA NA MIPAKA YA MAJIMBO YA UCHAGUZI WA ZANZIBAR

    Waheshimiwa Makamishna wa Tume ya Uchaguzi,

    Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa;

    Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya;

    Wakuu wa Vyombo vya Serikali;

    Viongozi na Wawakilishi wa Vyama vya Siasa;

    Viongozi wa Asasi za Kijamii;

    Wawakilishi wa Vyombo vya Habari;

    Maafisa wa Tume ya Uchaguzi;

    Mabibi na Mabwana

    Itifaki imezingatiwa

    Asslam -Aleyikum

    Nachukuwa nafasi hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha

    kuwa pamoja tukiwa salama na wazima wa afya. Pili, nichukuwe nafasi hii

    kutoa shukurani kwenu kwa kuupokea kwa mikono miwili mwaliko wetu na

  • 2

    kuhudhuria katika mkutano huu. Mwitikio huu unatupa imani kuwa mko na

    Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na mtaendelea kushirikiana nasi katika

    utekelezaji wa majukumu yetu ya Kitaifa.

    Waheshimiwa Viongozi, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar imeitisha mkutano

    huu kwa madhumuni makuu matatu. Kwanza kabisa, kutoa shukurani kwa

    msaada mnaoipatia Tume katika kutekeleza majukumu yake. Pili, kutoa taarifa

    juu ya kazi kubwa ambayo imepangwa kutekelezwa na Tume katika kipindi

    hiki na kuomba ushirikiano wenu katika kuifanikisha kazi hiyo. Na tatu, kutoa

    maelezo ya namna ambavyo wadau tumewapangia utaratibu wa kutusaidia

    kuifanya kazi hii mpaka kukamilika kwake. Na hatimaye tutatoa nafasi kwa

    kuuliza maswali kwa pale ambapo panahitajia ufafanuzi juu ya kazi hii.

    Katika mkutano huu hatukupanga kupokea maoni yenu, kwani tutakuwa na

    muda mrefu wa kupokea maoni hayo kuhusiana na kazi hiyo baadaye.

    Naomba tuusubiri muda huo na tuwe pamoja katika mkutano huu.

    Waheshimiwa Viongozi, mwaka uliopita Wajumbe wote saba wa Tume ambao

    wapo mbele yenu, mara tu baada ya kuapishwa kuwa Wajumbe wa Tume

    tarehe 4 Mei 2013 walikutana nanyi katika mikutano ambayo lengo lake kuu

    lilikuwa ni kujitambulisha kwenu na kuelezea majukumu ambayo

    yatatekelezwa na Wajumbe hao katika kipindi cha miaka mitano ya utumishi

    wao. Majukumu hayo kama vile:-

    Usimamizi wa jumla wa mienendo ya uchaguzi wa Rais, Wajumbe

    wa Baraza la Wawakilishi na viongozi wa Serikali za Mitaa;

    Kuandikisha Wapiga Kura;

  • 3

    Kusimamia Daftari la Kudumu la Wapiga kura;

    Kufanya mapitio ya mipaka ya Majimbo;

    Kukuza na kuratibu Elimu ya Wapiga Kura; na

    Kuendesha kura ya Maoni.

    Waheshimiwa Viongozi, nachukua nafasi hii kuwajulisha kuwa Wajumbe wa

    Tume kwa ushirikiano na msaada wa wadau wameanza kutekeleza majukumu

    hayo. Katika kipindi cha mwaka mmoja cha utendaji wa Wajumbe hawa,

    Tume imeendesha chaguzi ndogo tatu kujaza nafasi wazi Unguja na Pemba.

    Chaguzi hizo ni uchaguzi mdogo wa Wadi ya Ngombeni katika Baraza la Mji la

    Mkoani uliofanyika tarehe 23 Juni 2013, Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la

    Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi uliofanyika tarehe 02 Februari 2014 na

    Uchaguzi Mdogo wa Wadi ya Kiboje Wilaya ya Kati uliofanyika tarehe 27 Aprili

    2014.

    Aidha, katika kipindi hicho cha mwaka mmoja, Tume iliendesha jukumu la

    Uandikishaji wa wapiga kura wapya na Uendelezaji wa Daftari la Kudumu la

    Wapiga Kura. Kazi hii ilianza tarehe 29 Juni 2013 katika Wilaya ya Kaskazini

    A na kumalizika tarehe 5 Novemba 2013, Wilaya ya Mkoani. Tume ya

    Uchaguzi ya Zanzibar inatoa wingi wa shukurani kwa wadau wote vikiwemo

    vyombo vya ulinzi na usalama, vyama vya siasa, vyombo vya habari, asasi za

    kijamii na Viongozi wa Serikali katika ngazi ya Mikoa na Wilaya kwa

    ushirikiano waliotupatia katika utekelezaji wa majukumu yetu kwa kipindi cha

    mwaka mmoja uliopita. Ushirikiano huo kwa kweli umetuwezesha

    kuyakamilisha baadhi ya majukumu niliyoyataja kwa mafanikio.

  • 4

    Kukamilika kwa chaguzi ndogo tatu na kukamilika kwa kazi za Uandikishaji wa

    wapiga kura na Uendelezaji wa Daftari la Kudumu la wapiga kura

    kusingewezekana kama mngeamua kuiachia Tume hii peke yake kuzifanya

    kazi hizi. Lakini ushirikiano wenu nasi katika kila hatua umetuwezesha kufikia

    malengo. Tunaomba muendelee kushirikiana nasi katika utekelezaji wa

    majukumu haya.

    Waheshimiwa Viongozi, baada ya shukurani hizo, sasa naomba kuchukua

    nafasi hii kutoa taarifa juu ya kazi inayotarajiwa kufanywa na Tume ya

    Uchaguzi ya Zanzibar katika kipindi cha miezi sita ijayo. Tume ya Uchaguzi

    ya Zanzibar inakabiliwa na kazi ya uchunguzi wa idadi, majina na mipaka ya

    majimbo ya uchaguzi wa Zanzibar. Kazi hii inaendeshwa kwa matakwa ya

    Katiba na inaelekeza kufanyika katika kipindi cha kila baada ya miaka 8 hadi

    10. Mara ya mwisho kazi hii ilifanywa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar

    mwaka 2005.

    Waheshimiwa Viongozi, historia ya Zanzibar inaonyesha kuwa kazi ya

    uchunguzi wa idadi, majina na mipaka ya majimbo ya uchaguzi hapa

    Zanzibar inafanywa kila baada ya kipindi maalum kama inavyoelekezwa

    katika sheria. Jambo hili limetokea tangu miaka ya 1957, 1961 na 1963 wakati

    visiwa vyetu vilipoanzisha utaratibu wa kuchagua viongozi wake kwa njia ya

    uchaguzi. Aidha, kazi kama hizo zimeendeshwa mara mbili na Tume hii

    mwaka 2000 na mwaka 2005.

  • 5

    Waheshimiwa Viongozi, hivi sasa ni miaka tisa tangu Tume ya Uchaguzi ya

    Zanzibar ilipofanya uchunguzi wa idadi, mipaka na majina ya majimbo ya

    uchaguzi ya Zanzibar na Sheria inatuelekeza kuwa kazi hiyo inaweza kufanyika

    katika kipindi cha miaka minane hadi miaka kumi. Kwa maelekezo hayo,

    hesabu zinatuonyesha kuwa hivi sasa tayari tumechelewa kuifanya kazi hiyo

    kwa mwaka mmoja na tuna mwaka mmoja wa kuifanya kazi hii, vyenginevyo,

    tutakuwa tumekiuka maelekezo ya Katiba. Kwa hivyo, uamuzi wa Tume ya

    Uchaguzi ya Zanzibar kupanga kuifanya kazi ya uchunguzi wa idadi, majina na

    mipaka ya majimbo ya uchaguzi katika kipindi hiki unatokana na matakwa ya

    Katiba.

    Waheshimiwa Viongozi, kazi ya kufanya uchunguzi wa idadi, majina na

    mipaka ya majimbo ya uchaguzi tayari imepangiwa utaratibu wake na Tume

    ya Uchaguzi ya Zanzibar na utekelezaji wake unaanza rasmi katika mwezi

    huu wa Juni 2014 na inategemewa itaendelea mpaka mwanzoni mwa 2015.

    Ripoti kamili ya kazi hii imeainishwa katika ratiba ambayo mtapatiwa baada ya

    mkutano huu.

    Waheshimiwa Viongozi, kazi hii pamoja na kuwa inasimamiwa na kutekelezwa

    na Tume ya Uchaguzi kisheria, utendaji wake mpaka kufikia maamuzi

    umepangwa kukushirikisheni nyote kila mmoja kwa nafasi yake katika jamii

    ya Zanzibar. Tume ya Uchaguzi katika kuifanya kazi hii inategemea kwa kiasi

    kikubwa kupata maoni yenu juu ya hali halisi ya majimbo ya uchaguzi ilivyo

    hivi sasa katika Wilaya mbalimbali za Unguja na Pemba. Ili kupata maoni yenu

  • 6

    Tume imeandaa utaratibu wa kukusanya maoni juu ya majimbo kwa utaratibu

    ufuatao:-

    Kukutana na Wakuu wa Mikoa yote mitano,

    Kukutana na Vyama vyote vilivyopata usajili wa kudumu,

    Kukutana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali;

    Kukutana na Idara ya Utawala Bora,

    Kukutana na Uongozi wa Baraza la Wawakilishi,

    Kukutana na Halmashauri za Wilaya,

    Kukutana na Baraza la Manispaa la Zanzibar;

    Kukutana na Mabaraza ya Miji ya Mkoani, Chake Chake na Wete,

    Kukutana na Asasi za Kijamii;

    Kufanya mikutano ya Wananchi kwa Wilaya zote, na

    Kufanya ziara za kuyatembelea maeneo yote yatakayotajwa katika

    mikutano ya kuchukua maoni.

    Kwa taasisi au watu ambao hawatapata kutoa maoni ana kwa ana mbele

    ya Tume ya Uchaguzi juu ya uchunguzi wa idadi, majina na mipaka ya

    majimbo ya uchaguzi wanaweza kutoa maoni hayo kwa maandishi.

    Watendaji wa vyombo vya habari wanaombwa washiriki katika kazi hii kwa

    kutoa taarifa mbalimbali za kuielimisha jamii juu ya kazi hii. Tume ya

    Uchaguzi itakuwa tayari kutoa msaada wowote utakaohitajika ili

    kufanikisha kazi hiyo ya kutoa elimu. Vyombo vya Ulinzi na Usalama navyo

    kwa upande wao, vinaombwa vishirikiane na Tume ya Uchaguzi katika

    jukumu hili.

    Waheshimiwa Viongozi, naomba kuwasilisha.

  • 7

    Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.

    JECHA SALIM JECHA

    MWENYEKITI

    TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

    ZANZIBAR