46
Figa la tabia katika elimu ya juu: Tusomeshe nini, tusomeshaje? Kassim Hussein, PhD [email protected] Cell: 0754360174

Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Figa la tabia katika elimu ya juu: Tusomeshe

nini, tusomeshaje?

Kassim Hussein, PhD

[email protected] Cell: 0754360174

Page 2: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Maudhui • Katika mchakato wa kusoma na

kusomesha, sufuria ya ya elimu huwekwa juu ya mafiga matatu:

–Maarifa (knowledge)

–Stadi (skills)

–Tabia (behaviors)

Page 3: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Msukumo • Yako mambo kadhaa yamenipa msukumo:

– Kwanza tukiunda mitaala huwa rahisi kuanisha maarifa na stadi zinazotakiwa kusoma au kusomesha.

Mathalani:

– Tunafahamu kazi za mhasibu na ili mhasibu au awe na maarifa husika tunaoorodhesha yanayohitajika. Mitaala yetu hutaja maarifa pia huoorodhesha vitabu vya kiada na vya kurejelea kufikia malengo hayo.

Page 4: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Msukumo • Kuhusu tabia, mitaala yetu huwa

kimya na hakuna malengo wala, tabia husika hazijaooridheshwa na hakuna hata vitabu vya kiada au machapisho ya kurejelea.

Page 5: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Msukumo • Katika kuanzisha mwaka mpya wa

masomo na hata wakati wa mahafali, wageni rasmi husisitiza tabia njema kwa wanafunzi au wahitimu. Aghlabu tabia zenyewe huwa haziwekwi wazi.

Page 6: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Msukumo • Niliombwa na wenzagu

niwape nasaha na uzoefu wangu, nikawa sina. Ila nikatoa ahadi na leo ninatimiza kwa maswali mawili.

Page 7: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Msukumo • Maswali ni juu ya tabia:

tusomeshe nini na tusomesheje? Maswali ambayo nikaona yanahitaji kuanzisha mjadala juu ya tabia ili kuyatafutia majibu

Page 8: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Msukumo • Itakuwa nimefungua mlango

wa kutambua, kuchagua na kuzisoma/kusomesha tabia husika.

Page 9: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Msukumo • Ilikuwa haja yangu kujaribu tafiti

shirikishi kuhusu jambo la msingi katika elimu ya Tanzania.

• Hivi ni nini kimefanya wanafunzi kuandika matusi au bongo flavour katika mitihani?

Page 10: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Msukumo • Ni nini kinafanya wahitimu

wengine wapendelewe katika soko la ajira ?

Page 11: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Tabia - maana • Ni sehemu ya elimu iliokamilika au

UWEZO

• Inahusika na tathmini ya utu, vitu, mambo au matukio

– Inaelekeza fikira (cognitive function)

– Inashawishi hisia (affective function)

– Inaathiri hatua (conative function)

Page 12: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Organizational Behavior 12

USAWA WA BAHARI TABIA

MIKO – VIGEZO – UAMUZI

Mtazamo DHAMIRA – MAADILI - IMANI

Wengine huiona

Wengine hawaioni

Page 13: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Nadharia ya tabia • Hulka ambazo mtu huzaliwa nazo….

Vipaumbele juu ya kufikiri, kutoa maamuzi, mahusiano na nishati ya mwili.

• Kuna tabia zitokanazo na malezi, upendo na mazingira ya mtu kutokana na wazazi na jamii aliyokulia.

• Kuna tabia zianzofunzwa sambamba na taaaluma yaani kuzisoma na kusomesha.

Page 14: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Asiefunzwa na ……, hufunzwa na ….

•Katika nadharia ya tatu, juu ya tabia katika mchakato wa elimu ya juu, kuna orodha ndefu ya tabia stahiki.

Page 15: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Asiefunzwa na ….., hufunzwa na ….

• Tabia zote ni muhimu, ila kwa wahadhiri kuna haja ya kuziainisha, na kuamua kuziiingiza baadhi kwenye mitaala rasmi au iliokubalika na wengi.

Page 16: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Kuna haja, ulazima wowote?

• Chimbuko la haja: hutokana na wasomi wenyewe; yaani msomaji na msomeshaji

• Wadau wengine: taasisi, serikali, jamii nk

Page 17: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Kuna haja? • Dunia ni soko la ajira inahitaji wahitimu

walioelimika yaani wenye uwezo (maarifa + stadi + tabia)

• Uwezo ( au competency) ni jumuisho la maarifa (applied), stadi za kazi na tabia (attributes/ behaviours/attitudes) ili kufanya kazi nzuri zaidi ya kiwango cha kawaida. (McClelland, 1973)

Page 18: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Haja za Wasomi •Kuna nadharia moja ya

muundo, tabia na utendaji (S – C – P) kwamba utendaji wa mtu unaathriwa na tabia na inatokana na muundo.

Page 19: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Haja za Wasomi • Muundo huenda ukawa umiliki,

vyanzo vya mapato, kipimo (ukubwa), jiografia, wakati , jinsia nk hulazimisha kusoma au kusomesha tabia fulani.

• Mathlani kuhusu umiliki: kuna vyuo vya serikali , vya dini au vya binafsi?

Page 20: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Mifano – vyuo vya dini

• Vyuo vya taasisi za dini hutaka kutambuliwa kuwepo kwa mungu, kujenga tabia za dini husika na hairuhusu kufuru kwa mfano dhana za Charles Darwin kuhusu asili ya binadamu.

Page 21: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Mifano – vyuo vya dini

• Vyuo hivi hufundisha tabia zinazo endana na imani za dini kama vile haramu, halali , makuruhu, utumishi wa mungu nk

Page 22: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Mifano – vyuo vya dini

• Kwa mfumo huu, chuo ni zizi, walimu na wachungaji na wanafunzi ni wachungwa. Kwa hiyo wachungaji ni masuuli – wataulizwa mbele ya mungu juu ya dhima ya tabia za waliowachunga kama zimeenda kombo

Page 23: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Mifano: Vyuo vya serikali • Vyuo vya serikali hustawisha fikra ya kutafuta

ukweli na kuruhusu imani mbalilmbali na hata zile zinazo kubali kuwepo kwa mungu na zile zinazokataa kuwepo kwa mungu.

• Wakati wa kupigania uhuru, au wa ukombozi vyuo hivi hukazania fikra za walioshika uongozi wa serikali.

• Mathlani serikali ya kijamaa ilizaa watu wenye tabia za uzalendo, wapenda haki na utu na haya yalikuwepo ndani ya mitaala.

Page 24: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Vyuo binafsi

• wadhamini huwa na malengo ya kufikia ndoto za walengwa na hulenga kufanikiwa, kushinda, na ujasiria mali. Tabia zinazowekwa makazo ni pamoja na kuwa mshindani, mjasiriamali, kiongozi nk

Page 25: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Vyuo binafsi

• Sera za vyuo zimeelemea kuwa mwanafunzi ni mteja na mteja anahaki ya kuchagua atakachotaka kusoma au kusomeshwa.

Page 26: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Vyuo binafsi

• Msomeshaji anawajibu wa kumridhisha kila mteja, mara ya kwanza na kila mara. Elimu ni bidhaa na kwa hiyo mfumo wa masomo ni wasoko huria.

Page 27: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Vyuo binafsi

• Mwanafunzi huamua atakacho soma yeye na msomeshaji atalazimika kumridhia mteja wake. Kwa maana hii, tabia hata figa la tabia katika elimu ni uchaguzi wa msomi mwenyewe.

Page 28: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Vyuo binafsi • Tabia nazo huwa katika bidhaa kama

vile Entrepreneurship, Diversity, nk.

• Wasomeshaji/ wahadhiri hufanikiwa kama wanasajili wanafunzi wengi na kutathminiwa kuwa wanawajali na kuwaridhisha wateja wao.

Page 29: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Swali letu la msingi

• Tufundishe nini, tufundishaje?

–kuandaliwa orodha ya tabia muhimu zinazostahiki kila mhitimu awe nazo

–Tuainishe zile za muhimu,

–Tuzifundishe vipi?

Page 30: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Jitihada za kuanisha ‘Tabia’

• Azimio la UNESCO juu ya tabia ni pamoja na uraia, tabia za kushirikiana na jamii, uwezo, kuchunga haki za binadamu, maendeleo endelevu, demokrasia, na amani katika misingi ya haki.

• Nyingine ni utamaduni wa kujiendeleza na kuleta maendeleo

Page 31: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Jitihada za kuanisha ‘tabia’ – JKN (Elimu ya Kujitegemea)

• Mwalim alibainisha tabia za kujitegemea, tabia za kuhudumia umma na tabia za kutatua au kuwaondelea watu (wananchi) matatizo na migogoro.

Ameainisha:

• Ushirikiano ( na sio maendeleo ya mtu binafsi)

• Fikra za usawa

• Wajibu wa kutoa huduma

Page 32: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Jitihada za kuanisha ‘tabia’ – JKN (Elimu ya Kujitegemea)

• Akili ya kuchunguza

• Uwezo wa kujifunza

• Uwezo wa kukataa au kukubali vitu wanavyofanya wengine kufuatana na mahitaji binafsi

• Kujiamini kama mtu sawa na huru

• Anaethamini wengine na anathaminiwa … kwa anachokifanya na si anachokipata

Page 33: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Jitihada za kuanisha

• SAUT- “To prepare and mould men and women of integrity, devotion, commitment, principled, accountable, capable of taking risk; for future performance of leadership roles in society, and occupying positions of influence in public life, professions, industry and commerce in order to be able to realize the ideals of a good and just society”

Page 34: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Jitihada za kuanisha

• SAUT……. ‘In other words to have personnel who are mentally and morally fit. ... to us, through the Word of God, Catholic Tradition and Teaching of the Church’

Page 35: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

MUM works to produce highly educated and well trained human

resources inculcated with the appropriate aptitudes and attitudes for

the material, moral and spiritual development of the society through:

Knowledge Seeking

Community Built on Respect and

Tolerance

Academic freedom,

Creativity and Innovation

Integrity and

Prudence

Collegiality and

Collaboration

Spiritual and

Academic Balance

Excellence Responsibility

and Accountability

Trust and Teamwork

Page 36: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

1. Kufanya kazi katika timu

2. Kuwezana na wafanyakazi

wengine

3. Kuheshimika na wengine

4. Kujieleza kimaandishi

5. Kujieleza kwa kusema

6. Usiikvu na kuelewa

7. Kujifunza na kuwafundisha

unaowasimamia

8. Kupangana kupangilia

9. Kuongoza, kuhamasisha na

kutatua migogoro

10.Kuanzisha na ubunifu

11.Kuwasilisha kazi sahihi kwa

wakati

12.Bidii na kutochoka

13. Kuridhisha unachohitajika kutimiza

14. Kufanya kazi za ziada

15. Kukubali majukumu na kuyatimiza

16. Kufanya maamuzi sahihi

17. Kuwahudumia wateja

18. Kuonyesha unafuata na wasaidiza

wako

19. Kuwasaidia viongozi wako

20. Utii wa maelekezo halali ya viongozi

wako

21. Kutumia muda wa kazi kufanya

mambo ya kazi

22. Kutoa huduma bora bila ya kichocheo

chochote

Serikali katika OPRAS inataka tabia hizi

Page 37: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Tufundishe ‘Utu’ • Utu au kwa lugha za kusini “ubuntu” ni

ufundi au tasnia ya a kuwa binadamu (Ivorgba, 2009).

• Utu au “ubuntu” kwa semi za Zulu: “umuntu ngumuntu ngabantu”, inamaanisha utu wa mtu unapatikana toka kwa mtu mwingine

Page 38: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Tufundishaje? • Kwanza: Tukumbuke kuwa

huwezi kufundisha usichokijua au kuwa nacho!!

• Haja ya kujiandaa/kuandaliwa kuwa na tabia husika.

Page 39: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Tufundishaje?

• Pili, maandalizi ni pamoja na njia za kufundisha, kupima na kutathmini tabia

• Tatu, kuikimu nidhamu na kuiweka hali shwari ya kusoma na kusomesha. Kowalski, (2003) anatoa mifano ya tabia za kitoto, za kuudhi na inajumuisha kuchelewa, kuundoka kabla ya wakati, kuongea pembeni, kuchelewesha kazi, udanganyifu, kujipatia alama zisizo haki.

Page 40: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Tufundishaje? • Boice (1998) anaona tabia hizi

pia huchangiwa na wasomeshaji kwa kutoweka misingi ya nidhamu na kuisimamia.

Page 41: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Tufundishaje? • Tabia za kuharibu uendeshaji wa

masomo, usumbufu, kuwapunguzia wasomaji wengine ari na kuwavunjia heshima.

• Tunasimamia vipi nidhamu?

Page 42: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Tufundishaje? • Wasomeshaji, wajifunze tabia

husika

• Watayarishaji wa mitaala…. Ziwekwe vipi? Zipimwaje?

Page 43: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Tufundishaje? • Kuweka masomo maalumu yenye kufundisha

tabia husika

• Baadhi ya tabia ziwe ni sehemu ya masomo mengine

• Njia za kuwasilisha somo juu ya tabia zitokane na utaalamu wa msomeshaji na ari ya msomaji

Page 44: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Hitimisho • Haja ya kuzitambua tabia husika

• Kuziweka katika mitaala

• Kuwaandaa walimu kuzisomesha

• Kuwaandaa wanafunzi kujifunza

Page 45: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Marejeo

• Boice, R. (1998). "Classroom incivilities." In K. A. Feldman & M. B. Paulson (Eds.), Teaching and learning in the college classroom (2nd ed.) (347-369). Needham Heights, MA: Simon & Schuster Custom Pub

• Kowalski, R. M. (2003). Complaining, teasing, and other annoying behaviours. New Haven, CT: Yale University Press.

• Ivorgba, E.A. (2009) Values in African thought. (http://valuesinworldthought.authorfriendly.com/pages/p....) • McClelland, D. (1973). Testing for competence rather than

for "intelligence." American Psychologist, 28, 1-14 • McClelland, D. (1978) Guide to Behavioral Event

Interviewing, Boston: McBer and Company.

Page 46: Figa la tabia katika elimu ya juu:tufundishe nini, tufundishaje?

Marejeo

• Nyerere, J. Elimu na Kujitegemea, Oxford University Press

• Nyerere, J. Uhuru na Maendeleo. Oxford University Press 1968

• UNESCO. 1998. The Role of Higher Education in Society: Quality and Pertinence. Paris, UNESCO.

• URT, OPRAS form