Upload
others
View
12
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
Taarifa Fupi ya Matokeo ya Utafiti 11 Uhifadhi wa bionuwai, Migogoro na Haki
Uhifadhi, Masoko na Haki– Utafiti wa kulinganisha dhana ya Ndani na za Kimataifa
Idadi ya maeneo yaliyo hifadhiwa yameongezeka mara dufu katika kipindi cha miaka 20 ili-
yopita, hii imepelekea kuwepo na malalamiko kuwa uhifadhi unaathiri uchumi na maswala ya
kitamaduni kwa jamii zilizo karibu na bionuwai. Wengine wanaona uhifadhi unajikita katika
masoko kama njia ya kutatua tatizo hili, wakati huohuo wengine wanaona kuwa njia hii italeta
matabaka makubwa kwa jamii zilizo karibu na msitu.
Jarida hili linafafanua taarifa za awali za utafiti wa kimataifa unaofanyika Bolivia, China, Tan-
zania na Venezuela. Dhanio la mradi ni kwamba migogoro ya uhifadhi kwa kiasi fulani
inawezakueleweka kama mvutano na kutofautiana katika dhana mbalimbali za haki za kimaz-
ingira. Hususani tuna nia ya kufahahamu jinsi gani jamii huwa na mawazo tofauti kuhusu haki za kimazingira kwa wale ambao wanauzoefu wakukutana nao kila siku kwenye sera za ya misitu na miradi. Malengo yetu yamejikita hasa katika uhifadhi wa misitu katika ukanda wa joto, hususani katika mazingira ambapo baadhi ya shughuli za kimasoko zinaunda sehemu ya mchanganyiko wa usimamizi wa ndani ya hifadhi. Sasa hivi kumekuwa na ongezeko la mwitikio wa watu kujua maswala ya haki za kimazingira
duniani kote hii inajumuisha kwa mfano, Mradi wa Uhifadhi wa haki za binadamu. Lakini
bado tunauelewa mdogo wa maswala ya haki za kimazingira katika makundi na watu
mbalimbali na jinsi gani mawazo haya huchukuliwa kulinga na matatizo yaliyopo ya kimaz-
ingira duniani. Tunatarajia, mitazamo hii tofauti 'ya dunia halisi’ kuhusu haki za kimazingira
kuwa zenye kuhusiana sana na wenyeji. Mitizamo hii inaundwa kulingana na tamaduni,
kiuchumi na hali halisi ya kimazingira, na kwa uzoefu maalum na maslahi ya wadau
mbalimbali. Kile kinachoonekana haki na Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la
uhifadhi wa Uingereza linaweza kuwa tofauti kwa baadhi ya watu ndani ya nchi. Tunap-
endekeza kwamba mitazamo hii tofauti ya haki ina umuhimu sana kwa sababu ina athiri
pande zote za uhifadhi na matokeo ya ustawi wa binadamu katika sera na hatua za mradi.
Muundo wa Utafiti: kuchunguza na kulinganisha dhana ya haki Bolivia, China, Tanzania na Venezuela
Kwa kiasi kikubwa utafiti unalenga katika kuangalia mawazo ya wanajamii kuhusu haki za kimazingira- zinazo jikita hasa katika uhi-fadhi na usimamizi wa wana jamii. Tumecha-gua maeneo tofauti manne ya kufanyia uta-fiti duniani yenye utofauti wa kijografia, kiu-tamaduni na kisiasa ili kuongeza uelewa wa dhana mbalim-bali kuhusu haki ya kimazingira.
Maeneo yote ya utafiti yamesha wahi kuwa na dhana ya uanzishwaji wa uhifadhi kimasoko (utalii wa ndani, uthibitishaji wa mauzo ya mbao na miradi ya majaribio wa MKUHUMI). Katika tafiti hizi zote zinasohusiana na shughuli za kimasoko zinatakiwa ziende sambamba na shughuli zingine za uhifadhi kama usimamizi shirikishi wa misitu na maeneo / makazi ya kiasili. Kwa kila Nchi maeneo mawili yalicha-guliwa, kwa kuangilia utofauti za mazingira, utofauti wa asili, kiwango na maendeleo/mafanikio ya shughuli za kimasoko.
Dhana ya Kitaifa na Kimataifa ya
Haki za Uhifadhi
Dhana ya Ndani ya Haki za
Uhifadhi
School of International Development University of East Anglia, Norwich, NR4 7TJ • Tel: +44 (0)1603 592329 • Fax: +44 (0)1603 451999 • E: [email protected] • W: www.uea.ac.uk/dev
Uh
ifadh
i, Maso
ko n
a Haki–
Utafiti w
a kulin
ganish
a dh
ana ya N
dan
i na za K
imataifa
Mfano,Tanzania eneo moja la utafiti wameshauza mbao kwa kupitia cheti cha uthibitishaji misitu. Pia wapo katika hatua zakuweza kuuza hewa ya ukaa katika masoko huruia, wakati huo eneo lingine la utafiti wamesitishwa katika kutekeleza swala la uhi-fadhi kutokana na migogoro ya mipaka.
Katika kila eneo la utafiti tumelenga kufanyia utafiti maeneo matatu.
Kwanza, tulifanya utafiti kuelewa mazingira na maswala ya kijamii na kiuchumi katika maeneo yanayofanya usimamizi wa mazingira.
Pili, tumefanya utafiti katika dhana halisi ya haki ya kimazingira kwa mfano kuangalia utofauti wa ma-kundi na mtu mmoja mmoja katika kufanya maa-muzi ya usimamizi wa misitu, na njia gani wanad-hani zitakuwa na usawa katika kufanya mgawanyo wa gharama na faida.
Tatu, tunafafanua dhana ya haki katika sera ya mazingira na utekelezwaji wa sera husika katika jamii.
Njia za ukusanyaji taarifa: utambuzi wa
kanuni za haki kwa njia ya tafiti, michezo ya
majaribio ya kuigiza na utafiti wa watu na
tamaduni
Kwa sababu kuna uelewa ndogo kuhusu
dhana ya haki, na pia hakuna njia maalumu
ya kufanyia tafiti, kwa hiyo tutatumia njia
mbalimbali zitakazo tuwezesha kulingani-
sha uhalisia wa matokeo.
1. Muundo nusu wa utafiti. Tafiti hii hu-
chunguza mapendekezo yaliyoelezwa
kwenye kanuni za haki katika matukio
maalum Kwa mfano, washiriki
wanapewa nafasi ya kuonyesha map-
endekezo ya kufanya maamuzi ya ma-
pato ya msitu kulingana na kanuni kama
vile 'uhitaji, usawa na mambo mazuri
zaidi.
2. Michezo ya majaribio ya kiuchumi. Njia hii
inajaribu kujua tabia za watu katika mas-
wala ya haki kupitia majaribio ya michezo
ya kuigiza. Michezo hii inajaribu kuangalia
kanuni za haki ambazo watu wanatumia
kutambua usawa.
Kata ya Teng-chong Misitu ya ukanda wa
baridi na ukanda wa joto kidogo
Misitu ya watu binafsi, jumuiya na hifadhi ya taifa
Eneo A: msitu chini ya USM na utalii wa maz-ingira
Eneo B: misitu chini ya USM na mbao endelevu
Wilaya ya Kilwa Ukanda wa miombo:
Nyika na misitu. Misitu ya Kijiji Eneo A:Uhifadhi wa
misitu kwenye USM, Uthibitishaji wa misitu na eneo la majaribio la MKUHUMI.
Eneo B: Msitu wa Kijiji ambao USM hakuweza kufanya kazi
Santa Cruz de la Sierra Misitu ya ukame Eneo la wazawa Eneo A: wanahu-sika na biashara ya uuzaji wa mbao Eneo B: shughuli za kimasoko zenye maendeleo duni.
Canaima National Park Misitu ya savana Hifadhi ya taifa yenye wazawa walio na haki ya ardhi Biashara ya Utalii wa kimazingira lakini isiyo na maendeleo
China Tanzania
Bolivia Venezuela
Kielelezo 2. Maeneo ya Tafiti
3.Utafiti wa watu na tamaduni. Tumetumia njia hii ili kuweza kujua dhana ya haki katika majadiliano yaliyofikiwa katika usimamizi wa msitu. Dhamira yetu ni kuweza kujua majadili-ano ambayo yamejitokeza katika majadiliano ya mtu mmoja na ya makundi katika mikutano ya kijiji.
4. Filamu/video shirikishi. Tumejaribu kutumia uta-fiti wa watu na tamaduni na pia mikutano ya pamoja ambayo ilishafanyiwa utafiti. Utumiaji wa video shirikishi umeshatumika kwa zaidi ya karne tano katika kuwawezesha wanajamii kuelezea ma-hitaji yao na pia kwasilisha mawazo muhimu yanayopelekea katika kutoa maamuzi. Filamu shirikishi hutumika mara chache kama njia ya uta-fiti, lakini tumeona itasaidia kutoa muonekana to-fauti katika jamii katika kutambua na kupambanua mawazo kuhusiana na dhana ya haki za kimaz-ingira.
Wanajamii wa Bolivia wakishiriki katika utengeneza wa filamu shirikishi
Zoezi la utafiti shirikishi, Tanzania
Uchambuzi matukio: Warsha inayoju-muisho wadau wa tamaduni/mataifa mbalimbali Wakati wa kipindi cha baridi cha 2015 tuta-fanya mikutano miwili Uingereza. Mkutano wa kwanza tutaalika wadau mbalimbali pamoja na wanajamii kwenye nchi ambazo utafiti ulifanyika ili kujadili matokeo yali-yopatikana kwenye utafiti wa kila nchi. Hii itahusisha kuonyesha filamu zilizoten-genezwa na vipeperushi vinavyo elezea ma-tokeo ya miradi kwa ufupi. Tukio lenyewe li-tahusisha tafsiri kwenye hayo mataifa sawia ili kuwawezesha kubadilishana mawazo. Msisitizo utakuwa katika kuangalia utofauti na usawa katika dhana ya haki. Baada ya mkutano wa mataifa mbalimbali utafuata mkutano mkubwa utakao wahusisha wadau mbalimbali kama watendaji na watunga sera katika uhifadhi wa misitu na bionuwai katika maeneo ya ukanda wa baridi. Mkazo utakuwa katika kujadili kwa kina ma-tokeo ya utafiti uliofanyika awali kwa kuzin-gatia athari na jinsi gani tunaweza kuboresha ufanisi wa kazi katika uhifadhi. Mbali na mkutano huu wa kimataifa pia kuta fanyika warsha katika nchi za Tanzania, China na Bolivia. Lengo ni kuleta pamoja watendaji na watunga sera ili kujadili ni jinsi gani tunaweza kuboresha unganishwaji wa tafiti na nadharia.
Uchambuzi: Mbinu kulinganisha Kwa mtizamo wa mbele kutakuwepo na msisi-tizo wa kutumia mlinganisho katika uchambuzi wa taarifa. 1. Kulinganisha mbinu: Je, mbinu mbalimbali
zinatoa matokeo sawa kuhusu dhana ya ndani ya haki? Hii ni pamoja na mtizamo wa mtu mmojammoja, kwa kuangalia jinsi watu wanavyoelezea kanuni haki katika mazingira tofauti ya utafiti.
2. Kulinganisha maeneo ya nchi. Kwa mfano, kulinganisha matokeo ya majaribio michezo ya kuigiza kiuchumi kutambua maoni tofauti ya haki.
3. Kulinganisha maeneo: mfano kwenye mae-neo yenye shughuli za masoko je kutaonye-sha utofauti wa dhana ya haki za kimaz-ingira?
4. Kulinganisha dhana ya ndani na kimataifa
Mfano ni jinsi gani kanuni za mgawanyo wa faida zilizoonyeshwa na wadau zinaweza ku-fanana na kutofautiana na zinazo patikana kwenye sera za misitu na sera ya MKUHUMI?
Uh
ifadh
i, Maso
ko n
a Haki–
Utafiti w
a kulin
ganish
a dh
ana ya N
dan
i na za K
imataifa
Uh
ifadh
i, Maso
ko n
a Haki– U
tafiti wa ku
lingan
isha d
han
a ya Nd
ani n
a za Kim
ataifa
Kuweza kuwasiliana na sisi
Mashirika ya siyo ya kiserikali ya ndani na nje yamechangia moja kwa moja katika kuandaa utafiti kupitia majadiliano ya mwanzo.
Tunataka kuendelea kuwahusisha wadau mbalimbali kama wanaharakati, watunga sera wa kitaifa
na kimataifa, mashirika yasiyo ya kiserikali yanayohusika na uhifadhi na wanataaluma.
Tunapenda kusikia kutoka kwako kama umevutiwa na kazi hii. Kwa mfano, kama unapenda ku-tumiwa nakala zingine baadaye, kama unapenda kuhudhuria mikutano ya wadau mbalimbali; au un-afanya utafiti unaofanana. Tunapenda kusikia kutoka kwako kama kuna mtu yeyote anafanya utafiti kuhusu haki za kimazingira ili kulinganisha matokeo ya tafiti.
Jarida hili linaelezea kwa ufupi misingi ya mradi wa utafiti wa uhifadhi, masoko na haki: huu Utafiti ni wa kulinganisha dhana za ndani na kimataifa. Umedhaminiwa na Shirika la ESRC- Ruzuku za utafiti Na. ES/K005812/1. Utafiti unaongozwa na Adrian Martin (Chuo Kikuu cha East Anglia, UEA-Uingereza) Mawasiliano Timu ya Uingereza: Dokta Adrian Martin ([email protected]); Dokta Nicole Gross-Camp; Dokta Bereket Kebede, Dokta Iokiñe Rodríguez and Prof. Thomas Sikor. Wabia Bolivia: Mirna Inturias, Universidad NUR ([email protected]) China: Dr He Jun, Eco-watch ([email protected]) Tanzania: Glory Massao ([email protected]); Makala Jasper , Shirika la Kuhifadhi Mpingo na Maendeleo (MCDI)
School of International Development University of East Anglia, Norwich, NR4 7TJ • Tel: +44 (0)1603 592329 • Fax: +44 (0)1603 451999 • E: [email protected] • W:www.uea.ac.uk/