78
1 IMANI ZA KIPAGANI KATIKA UKRISTO MWANDISHI Muhammad Taher bin AbdilWahhab bin Saleem At-Tanneer MFASIRI Ibrahimu H. Kabuga

Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

Embed Size (px)

DESCRIPTION

Hakika idadi ya dini ambazo mwanadamu amejiunga nazo haihesbiki , zile zinazojulikana ni chache sana , na nyingi zinafanana moja kwa moja, na hazitofautiani isipokuwa katika majina ya miungu na katika baadhi ya vipengele ambavyo sio vya msingi. Sababu ya hali hiyo inatokana na ukweli kwamba kila alipokuja mtume yeyote alifuatwa na kaumu yake, na baada ya kifo chake kaumu hiyo, wakishirikiana pamoja na wafuasi wengine, walisimama na kuingiza katika mafundisho yake baadhi ya itikadi za kipagani walizokuwa wakiziamini kabla ya kuja kwake. Hawakuishia hapo , bali walichukua na kuingiza katika dini yao mambo na mafundisho ya dini nyingine za kipagani , kama yaliyotokea kwa Musa na wana wa Israil pale walipomuabudu ndama.Kwa kawaida ni kuwa dini hizi (walizokuja nazo mitume) zilikuwa ni taratibu ambazo Mwenyezi Mungu alimwekea mwanadamu kupitia mitume wake, ili apate kuishi na wenzake maisha ya amani na furaha, na apate kuunyanyua ubinaadamu. Au kwa maana nyingine , dini hizi , kwa kiasi fulani , zilikuwa ni kama kanunu za adabu na maadili zilizokusudia kujenga upendo , na kumtahadharisha mwanadamu kutokuwa na uadui kwa mwenzake. Hii ndiyo iliyokuwa hali ya dini walizokuja nazo mitume kutoka kwa Mwenyezi Mungu, nazo hazitofautiani katika chanzo na malengo. Binaadamu ameziharibu zaidi kwa kuingiza humo uzushi uliozushwa na mawazo yake mabovu , na akadanganywa na fikra zake za mwanzo.

Citation preview

Page 1: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

1

IMANI ZA KIPAGANI KATIKA UKRISTO

MWANDISHI

Muhammad Taher bin AbdilWahhab bin Saleem At-Tanneer

MFASIRI

Ibrahimu H. Kabuga

Page 2: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

2

YALIYOMO

Dibaji

Utangulizi

SURA YA KWANZA

Imani ya utatu kwa wapagani

Imani ya utatu kwa wakristo

SURA YA PILI

Kumtoa kafara mungu wa wapagani kwa ajili ya utakaso wa dhambi

SURA YA TATU

Wapagani na kiza kilichotokea kwa kufa mmoja wa wakombozi wa ulimwengu

Kiza kilichotokea kwa kifo cha Yesu

SURA YA NNE

Kuzaliwa miungu ya kipagani

Bikira Maria, mama wa mungu-Yesu

SURA YA TANO

Nyota zilizoonekana wakati wa kuzaliwa mungu wa kipagani

Nyota ya mashariki iliyoonekana wakati wa kuzaliwa kwa Yesu

SURA YA SITA

Majeshi yaliyodhihiri kutoka mbinguni na kumtukuza Mungu kwa kuzaliwa mungu wa kipagani

Majeshi ya mbinguni yakimtukuza Mungu kwa kuzaliwa Yesu

SURA YA SABA

Kuonyeshwa mungu-mtoto wa kipagani

Kuonyeshwa mungu-mtoto kwa wakristo

SURA YA NANE

Mahala walipozaliwa baadhi ya miungu wa kipagani

Mahala alipozaliwa Yesu kristo

SURA YA TISA

Imani ya kwamba miungu inayoonekana imetokana na kizazi cha kifalme

Imani ya wakristo kwamba yesu ametokana na kizazi cha kifalme

SURA YA KUMI

Imani ya wapagani kwamba watawala hutaka kuwaua miungu- watu

Imani ya kwamba Herode alitaka kumuua Yesu kristo

Page 3: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

3

SURA YA KUMI NA MOJA

Majaribu ya shetani kwa watoto wa miungu ya kipagani

Majaribu ya shetani kwa Yesu

SURA YA KUMI NA MBILI

Kwenda kuzimu kwa watoto wa miungu ya kipagani

Yesu kwenda kuzimu

SURA YA KUMI NA TATU

Kufufuka kwa miungu hao

Kufufuka kwa Yesu

SURA YA KUMI NA NNE

Kurudi duniani kwa miungu- watu

Kurudi kwa Yesu

SURA YA KUMI NA TANO

Imani ya kwamba mwana ndiye Muumba

Imani ya kuwa Yesu ndiye muumba

.

SURA YA KUMI NA SITA

Imani ya ubatizo kwa ajili ya utakaso wa dhambi

Wakristo na ubatizo

SURA YA KUMI NA SABA

Ulinganisho kati ya Krishna na Yesu

SURA YA KUMI NA NANE

Ulinganisho kati ya Budha na Yesu kristo

VITABU REJEA

ORODHA YA FAFANUZI

DIBAJI

Page 4: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

4

Muhammad Taher bin AbdilWahhab bin Saleem At-Tanneer, (aliyefariki 1352 A.H. / 1933

A.D), ni mhadhiri mwandamizi katika fani mbalimbali. Alizaliwa Beirut, na kupata elimu ya juu

katika chuo cha kimarekani, na alianzisha gazeti aliloliita Al – Muswawwir. Alielekea

Switzerland ambako alisoma katika moja ya vyuo vikuu vya huko na kisha akarudi nchini kwake

na kuishi katika kitongoji cha Ain Annub. Baadaye aliajiriwa katika ofisi ya gazeti la Ash Sharq

lililoasisiwa kwa amri ya Jamal Baashaa As Saffah. Alikimbia kupitia njia ya mlima wa Hawran

na kujiunga na jeshi la mapinduzi makubwa ya waarabu. Alikwenda Misri na baadaye kurudi

Syria ambapo alifariki Damascus mwezi wa tano mwaka 1933 na kuzikwa hapo.

Miongoni mwa kazi zake za kiuandishi ni :

1. Al aqaidul wathaniyyah fi diyaanat Annasraniyyah,

2. Ilmul falak wattabi‟yyaat – alichoshirikiana na baba yake Bw. AbdulWahaab.

3. Al anwaarus Saniyyah

4. Ad Durr An Nad‟ir

Baada ya kuamaliza kusoma kitabu hiki, msomaji atapata kufahamu kwa uwazi na usahihi zaidi

makusudio ya baadhi ya Aya tukufu zilizoteremka kumhusu Sayyidna Issa (a.s.):

1. Na Wakristo wanasema: Masihi ni mwana wa Mungu, hayo ndiyo wayasemayo kwa

vinywa vyao wanaiga maneno ya wale waliokufuru zamani….” (At – Tawbah: 30)

2. “Na kwa kusema kwao: Sisi tumemuuwa Masihi Isa, mwana wa Maryamu, Mtume wa

Mwenyezi Mungu - nao hawakumuuwa wala hawakumsalibu, bali walifananishiwa tu.

Na hakika walio khitalifiana katika haya wamo katika shaka nayo. Wao hawana ujuzi

nayo wowote, ila ni kufuata dhana tu. Wala hawakumuuwa kwa yakini” (An Nisaa: 157)

Tunamuoamba Allah ajalie kitabu hiki kuwa chenye manufaa na faida.

Amiin!!!!!!

UTANGULIZI

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehma, Mwenye kurehemu

Page 5: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

5

Himidi zote ni za Mwenyezi Mungu wa pekee Mwenye sifa ya kupasika kuwepo. Aliyetakasika

dhidi ya kuwa na mke na mwana. Ardhi na mbingu vinatoa ushahidi wa upekee wake kwa dalili

za waziwazi zipatikanazo humo. Yeye ni Mmoja wa pekee, hakuzaa wala hakuzaliwa.

Ametakasika kunako kufanana na chochote, na ametukuka dhidi ya kuzuka, kuwa katika mwili

wala kugawanyika katika sehem mbalimbali. Mwenye kuuendesha ulimwengu kwa uweza wake,

na mwenye kuzibadilisha siku kwa irada yake.

Rehema na amani ziwe juu ya kiongozi wetu Nabii Muhammad (s.a.w.) aliyetumwa kuja

kuuondoa upotofu na kuinyanyua bendera ya uongofu.

Kisha (Rehma na amani) ziwe zuu ya Ahli zake na sahaba zake wema wenye kuigwa.

Hakika idadi ya dini ambazo mwanadamu amejiunga nazo haihesbiki , zile zinazojulikana ni

chache sana , na nyingi zinafanana moja kwa moja, na hazitofautiani isipokuwa katika majina ya

miungu na katika baadhi ya vipengele ambavyo sio vya msingi. Sababu ya hali hiyo inatokana na

ukweli kwamba kila alipokuja mtume yeyote alifuatwa na kaumu yake, na baada ya kifo chake

kaumu hiyo, wakishirikiana pamoja na wafuasi wengine, walisimama na kuingiza katika

mafundisho yake baadhi ya itikadi za kipagani walizokuwa wakiziamini kabla ya kuja kwake.

Hawakuishia hapo , bali walichukua na kuingiza katika dini yao mambo na mafundisho ya dini

nyingine za kipagani , kama yaliyotokea kwa Musa na wana wa Israil pale walipomuabudu

ndama . 1

Kwa kawaida ni kuwa dini hizi (walizokuja nazo mitume) zilikuwa ni taratibu ambazo

Mwenyezi Mungu alimwekea mwanadamu kupitia mitume wake, ili apate kuishi na wenzake

maisha ya amani na furaha, na apate kuunyanyua ubinaadamu. Au kwa maana nyingine , dini

hizi , kwa kiasi fulani , zilikuwa ni kama kanunu za adabu na maadili zilizokusudia kujenga

upendo , na kumtahadharisha mwanadamu kutokuwa na uadui kwa mwenzake. Hii ndiyo

iliyokuwa hali ya dini walizokuja nazo mitume kutoka kwa Mwenyezi Mungu, nazo

hazitofautiani katika chanzo na malengo. Binaadamu ameziharibu zaidi kwa kuingiza humo

uzushi uliozushwa na mawazo yake mabovu , na akadanganywa na fikra zake za mwanzo.

Ni kitu kilichokuwa wazi kuwa, nyumati za kipagani ziliabudu miungu wengi waliozushwa na

mawazo yao potofu. Hawakuiacha nguvu yoyote katika nguvu za kimaumbile (mazingira)

isipokuwa waliifanya kuwa ni mungu na wakaiabudu. Kama vile mungu wa radi, mungu wa maji

, mungu wa upepo , mungu wa moto , mungu wa nyota n.k. Mfano wa hilo ni simulizi

iliyoelezwa katika Qur‟an Tukufu kuhusu Nabii Ibrahimu (a.s): “ Na hivyo tukamuonyesha

Ibrahim ufalme wa mbingu na ardhi , na ili awe miongoni mwa wenye yakini. Na usiku

ulipomwingilia akaona nyota, akasema: Hii ni mola wangu. Lakini ilipotua, akasema: Siwapendi

wanaotua. Na alipouona mwezi unang‟aa, akasema: Huu ni mola wangu. Lakini ulipotua,

akasema: Asiponiongoza Mola wangu, bila shaka nitakuwa miongoni mwa watu wapotofu. Na

alipoliona jua linang‟aa akasema: Hili ni Mola wangu, hili ni kubwa kabisa, lakini lilipotua

akasema: Enyi watu wangu! Simo katika hayo mnayoyashirikisha” (Suratul An‟am: 75 – 78).

Kuna watu walioabudu wanyama kama Wana wa Israil waliomuabudu ndama. Kuna

waliomuabudu na kumtukuza mmoja wa wanadamu , mpaka wakafikia hatua ya kusema kuwa ni

1 Allah Mtukufu anasema katika Suratul Baqarah, 51: “Na tulipo muahidi Musa masiku arubaini, kisha mkachukua

ndama (mkamuabudu) baada yake, na mkawa wenye kudhulumu”.

Page 6: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

6

sehemu ya utatu wailouita “Baba, Mwana, na Roho mtakatifu” kama vile Mabudha , Wabrahma ,

wababeli, Waashori na wengineo kama utakavyoona katika maelezo yetu.

Hakuna hatari juu ya ukweli, hakuna kitu kilichosalama kama ukweli, na hakuna afichaye

ukweli au kuuzuia watu wasiupate isipokuwa atakuwa ni mwoga au mhalifu. Waislamu

hawaridhii kumuona binadamu ambaye amefikia maendeleo yanayoonekana kwa sasa , akibaki

kung‟ang‟ania yale aliyokuwa nayo tangu enzi za kuanza kwake, akiitakidi kila kilichozushwa

na mawazo yake yaliyopotoka ambayo yameanzishwa na zama na eneo na hatimaye upagani

wake wa enzi za kiza cha ujahiliyyah ukakuwa kutoka humo.

Huenda baadhi ya watu wakadhani kuwa sababu iliyotupelekea kutunga kitabu hiki ni kutokana

na ushabiki au chuki tuliyonayo dhidi ya wale wasiokuwa katika dini yetu. La hasha, kwani

heshima yetu haistahiki kuangukiwa na dhana hii, na hadhi yetu hailingani na yaliyoelezwa.

Kuna sababu mbili za utunzi wa hiki kitabu:

1. Hivi karibuni tulipata kuona vitabu kadhaa vilivyotungwa na wamisionari na wale

waliopamoja nao dhidi ya Uislam vikiwa katika lugha ya kiarabu , kama vile :

Al Hidayah ( katika juzuu 4)

Bakourah Al Shahiyyah

Tanweerul Afhaam fi Maswaadiril Islam

Mizanul haq

Al kafaarah

Misbahulhudaa ila sirrilfidaa

Alburhanuljaleel ila sihhatil Anaajeel

Da‟watulmuslimeen ila mutaala‟til kitabil muqaddasi al thameen, na vingine vingi ,

achilia mbali makala na hotuba mbalimbali walizoanza kuzitawanya baina ya Waislam,

na halikadhalika vitabu vya kingereza , kwa mfano :

The crusfied of the 20th century

Life of Muhammad ( cha William Muire)

Arabia , the cradle of Islam

Our Muslim Sisters

Islam in China, n.k.

Vile vile kuna magazeti mbalimbali, hasa gazeti la kiingereza la Muslim World2 lililojaa shutma

na uzushi dhidi ya Uislam na Waislamu. Kwa kuwa heshima na dini yetu vinatuzuia kuwajibu

kama walivyofanya , tumeona kuwa njia nzuri na iliyokuwa bora zaidi ni kuwafunulia

ulinganisho wa kidini ili kila mmoja wao aone kama yuko katika upotevu au uongofu wa wazi ,

na ijulikane nani kati yetu aliyeshikamana na uzushi wa kipagani wa watu hao(wa zamani). Kwa

sababu ulinganisho humpelekea msomaji kuzingatia ukweli wa kihistoria na kimaandishi ambao

hauna shaka katika ushuhuda wake, na asaa baada ya hapo akawa miongoni mwa wale

wanaosikiliza maneno na kufuata yale yaliyokuwa mazuri. Kwa kuwa mwanadamu kwa asili

hupendelea kupanda daraja katika ukamilifu wa kimaendeleo, vilevile huegemea kwenye baadhi

ya matendo na maneno makali hasa inapokuwa katika masuala ya kidini ambayo ndiyo chanzo

cha saada ya mwanadam.

2 Ni miongoni mwa magazeti hatari yatolewayo na Mustashrikiin wa Marekani. Lilianzishwa na mmishionari

mwenye chuki dhidi ya Uislamu Samuel Zoemor mwaka 1911, na kwa sasa linatolewa kutoka Hartford Marekani,

mhariri mkuu ni keneth crag.

Page 7: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

7

2. Sababu nyingine ni kutaka kuinusuru haki na kusimamia undugu wa kibinadamu, kwa sababu

ni lazima katika dini yetu kwaita watu kwenye ukweli, na ni wajibu kwetu pia kuwaita ili

kushirikiana nasi katika kile kitu kizuri tulichonacho, yaani “DINI YETU”.

Tumejiepusha kuibua hisia ya mfuasi wa dini yoyote, kwani sisi hatujatoa kitu kipya kutoka

kwetu bali tumetoa ukweli usiopingika, na yeyote mwenye shaka juu ya lolote katika hayo ni juu

yake kurejea katika vyanzo vyetu tulivyovitaja katika kila mada na utafiti ili apate kuona ukweli

uliowazi ambao hauhitaji maelezo au fafanuzi.

Aidha, kwa bahati sana, vitabu vyote tulivyotolea ushahidi vimetungwa na wasomi mashuhuri

wa kikristo kutoka Ulaya.

Vilevile tumenukuu baadhi ya michoro ya lazima kwa lengo la kutimiliza faida ili kitabu hiki

kitoke kikiwa kamili. Isipokuwa katika makosa ya uchapishaji ambayo yanaeleweka kwa kila

mwenye akili ambaye hatoacha kutusamehe kwa hilo, hasa akiwa ni mwenye kuangalia

kilichomo ndani na sio kilichokuwa nje.

Wassalaam

Muhammad Taher At – Taneer

Page 8: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

8

SURA YA KWANZA

IMANI YA UTATU

(Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu)

Ninaanza sura hii - kama alivyoanza Profesa Doane 3– kwa Aya ya Qur‟an Takatifu. Anasema

Allah Mtukufu:

“Wala msiseme watatu, acheni (itikadi hiyo) ni bora kwenu. Hakika MwenyeziMungu ni Mmoja

tu , ameepukana na kuwa na mtoto. Ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini, na

Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mlinzi”

(Surat An –Nisaa: 17)

UTATU KWA WAPAGANI

Ni katika mambo yasiyopingika kuwa dini za kipagani zinafanana sana, na sababu za hali hiyo ni

nyingi. Lakini mojawapo ni pale ambapo taifa lolote kubwa lilipokuwa likijitanua katika dunia,

basi hapo ndipo dini na ustaarabu wake vilikuwa vikijitanua pia. Wakati huohuo, hupata

kuingizwa katika dini hiyo mambo kadhaa wa kadhaa kutoka katika dini nyingine. Kutokana na

jamii za kale kutawliwa na ujahili, walikuwa wakiyakubali – bila kusita – yale wanayoambiwa

na wakuu wao.

Kiongozi wa dini anapoanzisha dini mpya (kwa kweli inakuwa sio dini mpya, bali anakuwa

ameichukuwa kutoka katika moja ya makundi ya kipagani), alikuwa akiongeza baadhi ya mila za

jamii yake ili wayakubali kwa wepesi yale ayasemayo. Kama ilivokuwa kwa wale walioeneza

moja ya dini kubwa zilizopo mpaka sasa katika taifa la Roma.

Bwana Prichard anasema : “Tafiti zote za kidini zilizochukuliwa kutoka vyanzo vya

mashariki haziepuki kutaja moja ya aina au mlolongo wa utatu ( yaani Baba, Mwana na Roho

Mtakatifu” 4

Naye Bwana Maurice anasema 5: “Mengi ya mataifa ya kipagani yaliyopotea yalikuwa na

mafundisho ya kidini yaliyoelezea imani ya utatu wa Mungu ( yaani Mungu mwenye nafsi tatu ).

Katika kitabu ( wakazi wa mwanzo wa ulaya ) 6 kuna maelezo yafuatayo: “ Wapagani wa

zamani walikuwa wakiamini kuwa Mungu ni mmoja , lakini ana nafsi tatu”.

3 Doane kitabu chake ni: Bible Myths and Their Parelles in other Religions. 4 Prichard katika kitabu chake: An Analysis of the Historical Records of Ancient Egypt. uk. wa 285 5 Maurice, katika kitabu chake cha: Indian Antiquities, juzuu ya 6 , ukurasa 30. 6 Ukurasa wa 197

Page 9: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

9

Bwana Doane anasema: “Tukitupia macho upande wa India tutaona kuwa ibada zao kubwa na

mashuhuri za kidini ni utatu (yaani kuamini kuwa Mungu ana nafsi tatu” 7

Mafunzo haya huyaita kwa lugha yao “ TRIMURTI” ambayo ni sentensi inayoundwa na maneno

mawili ya Kisanskrit, ambapo TRI ina maana ya “tatu”, na “MURTI” ina maanisha “maumbo”

au nafsi, ambazo ni “Brahma, Vishnu, na shiva”. Nafsi hizi ni tatu katika umoja kwa maana ya

Mungu, Mwokozi na Shiva. Nafsi hizo zote tatu ni Mungu Mmoja. Aidha miungu hii mitatu

huiwekea kielelezo cha utambulisho ambacho ni herufi tatu za A, W, M, n a kuzitamka

(aum/om). Herufi hizi hutumika tu katika salaa zao na huzipa heshima kubwa wawapo katika

mahekalu yao.

Brahma 8 (muumba wa uhai asiyekuwa na umbo wala sifa za kibinaadamu) alipotaka kuumba

viumbe alichukua sifa ya utendaji akawa mtu-mume ambaye ni “Brahma muumba”. Baadaye

akaendelea katika utendaji akageuka katika sifa ya pili ya uhai akawa “Vishnu mlinzi”. Kisha

akabadilika katika sifa ya tatu akawa Shiva muangamizaji”.

Hizi sifa tatu vilevile huziita “Trimutri” ikiwa na maana ya nafsi tatu, na huzipa kielelezo cha

moto, na hujulikana pia kwa majina ya “Agni, Surya, na Indra” na majina mengine ya utatu.

Imeelezwa katika vitabu vitakatifu na muhimu kwa Wabrahma kwamba, huu utatu mtakatifu

hautengani kimaumbo, utendaji na muunganiko, na huifafanua hali hiyo kwa maelezo yafuatayo:

“Brahma ndiye anayewakilisha misingi ya utengenezaji na uumbaji (muumba mkuu), anaendelea

kuwa muumba, naye ndiye Baba”.

Na Vishnu ndiye mlinzi na mhifadhi, naye ndiye “Mwana” aliyejigeuza kutoka katika hali ya

uungu.

Na Shiva ndiye mwanzilishi, mhilikishaji, muangamizaji na mfufuaji, (naye ni Roho Mtakatifu).

Vilevile humuita kuwa ni “Krishna mungu mwokozi, Roho mkuu, Mlinzi wa ulimwengu, mungu

aliyeleta neema duniani ili kuwaokoa watu. Na ni mmoja wa nafsi tatu ambazo zote ni Mungu

Mmoja.

Katika KABITA , ambacho ni moja ya vitabu vyao vitakatifu vya kidini , imeelezwa kuwa

Krishna aliwahi kusema : “Mimi ndiye Mungu wa viumbe vyote. Mimi ndiye siri ya OM. Mimi

ndiye Brahma na Vishnu na Siva , miungu mitatu ambayo yote ni mungu mmoja”.

7 katika kitabu chake kilichotajwa hapo awali, ukurasa 366 8 Brahman lina maana ya roho wa ulimwengu asiyejulikana, ni lazima kulitofautisha na Brahma ambaye ndilo

maarufu zaidi.

Utatu mtakatifu kwa Wahindu.

Picha hii inapatikana katika

makumbusho mbalimbali huko

India.

Page 10: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

10

Nafsi ya tatu – ambayo katika sifa yake mbaya ni “Mhilikishaji”, na sifa yake nzuri ni

“Mrejeshaji” – humuelezea kwa picha ya njiwa , alama ambayo humaanisha uumbaji mpya.

Naye ndiye Roho ambaye hurukaruka juu ya maji.

Kama tulivyoeleza, hizi nafsi tatu za milele na za kimaubile huzipa kielelezo cha A , W, na M =

“Om” na huamini kuwa nafsi hizi tatu ndiye Muumba, Mlinzi na Mhilikishaji , na kwamba

hubadilishana kazi , yaani Mwana kufanya kazi za Baba na Roho Mtakatifu , na Roho Mtakatifu

hufanya kazi za Baba na Mwana , halikadhalika Baba hufanya kazi za Mwana na Roho

Mtakatifu.

Bwana Allen anasema : “ Wabrahma hueleza katika vitabu vyao vya kidini kuwa , mchamungu

mmoja aliyeitwa Etnis , aliona kuwa kuna ulazima wa kumuabudu Mungu Mmoja , akawaomba

Brahma , Vishnu na Siva akisema : “Enyi miungu watatu , fahamuni kuwa mimi natambua

kuwapo kwa mungu mmoja , basi nielezeni ni yupi kati yenu aliye Mungu wa kweli ili nimpe

nadhiri na maombi yangu. Ndipo ilipojitokeza miungu yote mitatu na kumwambia : “ Fahamu

ewe mchamungu ya kwamba hakuna tofauti ya wazi baina yetu. Ama utatu unaouona ni mfano

au umbo tu , na mwili mmoja unaojionyesha kwa nafsi tatu ni moja katika uhalisia wake” 9

Naye Bwana Maurice anasema : “Tuliona sanamu lenye vichwa vitatu kwenye kiwiliwili kimoja

ndani ya hekalu la kale lililopitiwa na karne nyingi , sanamu hilo lilielezea utatu”10

Bwana Faber 11

anasema : “kama tuonavyo utatu utokanao na Brahma ,Vishnu na Siva kwa

wahindu , hali ni hiyohiyo kwa Mabuddha ambao huamini kuwa Budha 12

ni Mungu , na

kuamini kuwa yumo katika utatu. Kadhalika Mabudha wa Genast huamini kuwa Jiva ni mmoja

katika nafsi tatu.

Anasema Sir Jones katika maombi ya mchamungu ( Amora ) kama ifuatvyo : “ Ninakupa

utukufu na unyenyekevu ewe mola , wewe ndiwe Mungu mwenye huruma. Ewe muondoaji wa

mateso na matatizo. Ewe mola wa kila kitu. Ewe mlinzi wa viumbe. Ewe mwenye kuwapa

rehema waja wako. Ewe mfalme wa kila kitu. Ewe hai, wewe ni Brahma, Vishnu, na Siva, Mimi

ninakuabudu wewe. Umejidhihirisha kwa majina yako ya Alphabeti, na maumbo yako

mbalimbali na umbo la Budha Mungu wa rehema”13

Naye Bwana Doane anasema: “Mabudha, ambao ndio wakazi wengi wa China na Japan,

wanamuabudu mungu mwenye nafsi tatu ambaye humuita “FO”. Wanapotaka kuutaja utatu huu

9 Allen, katika kitabu chake cha: India Ancient and Modern, ukurasa 382 10 Indian Antiquities, juzuu ya 4, ukurasa wa 372. 11 Faber: The Life of Christ 12 Muasisi wa dini ya budha ni : Gautama Ieddhartha ( 564 – 483 B.C ) ambaye aliitwa Budha , ikiwa na maana ya

Mwenye kuangaza , au aliyeongoka. Alikuwa ni mtoto wa kiongozi wa jimbo lililopo mpakani mwa Nipal.

Aliukana uongozi wa Veda na Makuhani wa Kibrahma, na kutengeneza kanunu tano za kimaadili , ambazo ni mfano

wa usia. Nazo ni:

• Mtu yeyote asimuue kiumbe yeyote aliye hai.

• Asichukue asichopewa.

• Asiseme uongo • Asinywe kilevi

• Asisimame juu ya uchafu.

Vilevile imani ya Budha anayoiamini kuwa ya kweli, ilieleza kuwa maumivu ni bora kuliko raha katika maisha ya

kibinaadamu. (Qissatul Hadhaarah juzuu ya 3 ukurasa wa 76. 13 Jones, katika kitabu chake kiitwacho: Asiatic Researchs, juzuu ya 3, ukurasa wa 285.

Page 11: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

11

matakatifu husema, utatu matakatifu “FO”, na humchora katika mahekalu yao kwa umbo la

masanamu yanayopatikana India. Vilevile husema: FO ni mmoja, lakini ana maumbo matatu.

Katika moja ya majengo maalumu ya ibada huko Botala, huonekana FO akiwa ni sehemu tatu.14

Bwana Davis naye pia ametoa maelezo kama hayo.15

Bwana Faber anatoa maelezo mengine akisema: “Wachina humuabudu Buddha na humuita

“FO” na kusema kuwa ana nafsi tatu, A, U na M kama vile wasemavyo wahindu”.

Bwana Doane anasema : “wafuasi wa Laokamitdha – ambaye ni mwanafalsafa mashuhuri wa

kichina na ambaye alikuwapo miaka 604 kabla ya Kristo – wanajulikana kuwa ni wafuasi wa

“Tao” na humuabudu mungu mwenye nafsi tatu. Msingi wa mafundisho ya falsafa zake za kidini

ni Tao, ambaye ndiye akili ya milele (mwanzo) iliyoitoa nafsi moja , na kutokana na hii moja

ilipatikana ya pili, na kutokana na hii ya pili , ikapatikana ya tatu, ambapo kutokana na hizi nafsi

tatu kila kitu kilipatikana. Imani hii ya kuzaliana ilimshangaza Bwana Doane kwani anayeiamini

ni mpagani”.16

Imeelezwa katika vitabu vya kidini vya China kwamba , asili ya kila kitu ni moja , na hii moja

ambayo ndio chanzo cha uhai , ililazimika kuumba nafsi ya pili , ambapo nafsi ya tatu ilitokana

na hizo nafsi mbili, na halafu kila kitu kilipatikana kwa hizi nafsi tatu.

Wamisri wa kale walikuwa wakiabudu mungu mwenye nafsi tatu 17

aliyekuwa amechorwa katika

mahekalu yao ya zamani. Wataalamu wanadhani kuwa alama wanayoichora katika bendera,

ambayo ni bawa la ndege na pango la nyoka, ni alama ya ule utatu pamoja na sifa zake

mbalimbali.

Naye Bwana Helsly Stevens anasema:

“Wahindu humuamini mungu mwenye nafsi tatu, na wanapotaka kumzungumzia kwa sifa ya

“Muumba” husema “mungu Brahma”. Wanapotaka kumzungumzia kwa sifa ya “Mhilikishaji”

husema “Siva” au “Mahadeva”. Na wanapotaka kumsifia kwa sifa ya “Mlinzi” husema “Mungu

Vishnu” . Huamini kuwa utatu huu upo kila sehemu kwa roho na uweza.18

14 Doane, katka kitabu chake, ukurasa wa 372 15 Davis katika kitabu chake kiitwacho, The Chinese, juzuu ya 2, ukurasa wa 101 na 103. 16 Katika kitabu chake , ukurasa wa 172 17 Katika dini ya zamani ya Kimisri: (Geb) mungu wa ardhi alimuoa (Nut) mungu wa mbinguni, wakamzaa (Ra)

yaani jua. (Angalia katika kitabu kiitwacho: Tareekhush Sharqil Adnal Qadim, ukurasa wa 124. Cha Professa Abdul

Aziz Othman. 18 Katika kitabu chake kijuliknacho kama: Faith and Reason, ukurasa wa 78.

Utatu kwa

Wamisri

Page 12: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

12

Bwana Toma Inman anasema: “Picha hii humuelezea Brahma wakati wa kuumba kwake,

ambayo iko katika hali mbili za uume na uke”19

Akaendelea kusema katika ukurasa wa 101 kuwa: “vielelezo na alama zote zitumikazo kwa

Wakristo, vilikuwa vikielezea na kuonyesha kuabudiwa kwa vitu vinavyotia aibu, na

haiwezekani kukana uwepo wake”.

Kisha akasema: “nadhani pindi watu watakapoelewa maana ya alama hizo watazikimbia, na

huwenda baadhi ya watu wakaendelea kushikamana na ibada hizi ambazo , kwa mtazamo wangu

ni mbaya na ni za kipagani”.

Pia, katika kitabu chake hicho, ameeleza mambo mengi ya msingi ambayo hatukuyaelezea, na

hatukuweka mojawapo ya picha zilizoelezewa katika kitabu hicho, kwani ingeweza kuleta hisia

kali kwa watu wengi.

Bwana Doane anasema : Makasisi wa hekalu la Momvis la huko Misri wanapowaeleza

wanafunzi wapya kuhusu utatu , walitoa maelezo yafuatayo : “ Wa kwanza alimuumba wa pili ,

na wote wawili kwa pamoja wakamuumba watatu , na hivi ndivyo ulivopatikana utatu

mtakatifu”20

Mfalme wa Misri Toleso alimtaka kuhani Tnishoki amueleze kama kabla yake alipata kuwapo

mkuu zaidi kuliko yeye, au atakuwa baada yake mwenye ukuu zaidi? Kuhani akasema: “Ndiyo,

yupo aliye mkuu. Wakwanza ni Mwenyezi Mungu, kisha Neno , na pamoja nao ni Roho

Mtakatifu. Na hao watatu wana hali moja na ni wamoja katika uhalisia. Nguvu za milele

zimetokana nao. Ondoka ewe mwenye kutoweka , mwenye maisha mafupi”.

“Hakuna shaka kuwa , nafsi ya pili katika utatu mtakatifu kupewa jina la NENO ina asili ya

upagani wa Kimisri uliopenya katika dini nyingine kama vile Ukristo. Na Apollo aliyezikwa

Delhi huitwa NENO. Vilevile katika mafundisho ya kidini huko Iskandaria , ambayo ndiyo

mafundisho ya Plato kwa miaka mingi kabla ya Kristo, NENO ni mungu wa pili ambaye pia

huitwa Mwana wa pekee wa Mungu.21

Bwana Higgins , katika kitabu chake kiitwacho The Celtic Druids, juzuu ya 2 ukurasa wa 162,

anasema: “Waajemi walikuwa wakimuita Mitrusa kuwa ni NENO, mpatanishi , na mwokozi wa

Waajemi”. Angalia pia katika kitabu cha Almicio Dunlap kiitwacho Vestiges of Spirit History of

Man, ukurasa wa 20. Halikadhalika kitabu cha Bwana Bunsen, kiitwacho The Angel Messiah,

ukurasa wa 57 kuna maelezo kama hayo.

Naye Bwana Bonwick anasema: “Imani ya ajabu iliyoenea katika dini za Wamisri

(wapagani wa zamani ) ni ile ya kuamini “uungu wa NENO”, na kwamba kila kitu kimetokana

na NENO, na NENO ametokana na Mwenyezi Mungu , na kuwa huyo NENO ni Mungu. Na

Plato, Aristo na wengine walikuwa wakiifahamu imani hii ya kipagani iliyokuwapo miaka mingi

kabla ya Kristo. Na hatukuwa na habari ya kwamba Wakeldan na Wamisri walikuwa na imani

hii isipokuwa hivi karibuni tu”.22

Ameendelea kusema katika ukurasa wa 404: “Kama ambavyo NENO anapata heshima kuu kwa

Wamisri (wapagani wa zamani) halikadhalika maneno yafuatayo yanapatikana katika vitabu

19 Toma Inmann, katika kitabu chake cha: Ancient Pagani and Modern Christian Symbolism, ukurasa wa 9. 20 Katika kitabu chake, ukurasa wa 473. 21 Indian Antiquities, ukurasa wa 127. 22 Katika kitabu chake: Egyptian Belief and Modern Thought, ukurasa 402.

Page 13: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

13

vyao vitakatifu vya kidini: “Hakika mimi najua zaidi siri ya uungu wa Neno nalo ni Neno la

Mungu wa kila kitu, naye ndiye aliyeliumba”, kwa hiyo Neno ndiye nafsi ya kwanza baada ya

Mungu, ambaye hakuumbwa, na ndiye mwenye kutawala viumbe vyote”.

Bwana Doane anasema: “Waashori walimwita Marduk kuwa ni NENO, na kusema kuwa ni

“mwana wa Pekee wa Mungu”, ambapo vilevile walikuwa wakimuomba kwa maombi

yafuatayo: “Wewe ndiwe muweza , mfanikishaji na mtoaji wa uzima. Wewe ndiwe mwenye

huruma kati ya miungu yote. Wewe ni mwana wa pekee wa Mungu Muumba wa mbingu na

ardhi na mtawala wake. Huna mfano. Wewe ndiwe mwenye huruma na mwenye kufufua wafu”.

Vilevile katika ukurasa wa 374 ameeleza yafuatayo: “Wakeldayo wakiliita NENO kwa jina la

Mimrar kama wasemavyon Wayunani kuwa ndiye Muumba na mtawala wa ulimwengu, na

kwamba hakuna chochote chenye ukuu kuliko yeye isipokuwa Mwenyezi Mungu”.

Bwana Frontingham ametoa maelezo yafuatayo: “Folo alikuwa akiitwa NENO ambapo

walikuwa wakimtukuza sana na kumsifu kwa ibara zifuatazo: “Folo alikuwapo kabla ya

chochote, mwana wa pekee wa Mungu, Chakula cha milele kutoka mbinguni , Chemchem ya

hekima, njia ielekeayo kwa Mungu, mwakilishi wa Mungu, mfano wa Mungu, kuhani, Muumba

wa ulimwengu, mungu wa pili, mkalimani wa Mungu, mjumbe wa mungu, nguvu ya Mungu,

mfalme, malaika, mwanadamu, mpatanishi, nuru ya awali, mwanga, jina la Mungu, mwenye

kujitoa fidia”.23

Wayunan (wapagani wa zamani) walikuwa wakiamini kuwa Mungu ana nafsi tatu. Makasisi wao

wanapoanza kutoa sadaka ya kuteketezwa (kichinjwa) hunyunyiza maji mara tatu juu ya

mnyama anayetaka kuchinjwa (kama alama ya utatu), na kisha huwanyunyizia wale waliopo

hapo mara tatu na kuchukua ubani kwenye chombo maalumu kwa vidole vitatu kwa imani kuwa

vitu vyote vitakatifu lazima viwe katika hali ya utatu. Idadi hii (ya utatu) wanaiwekea mkazo wa

hali ya juu katika mambo yao yote ya kidini.

Naye Bwana Doane, ambaye tumekwishamtaja, amenukuu maelezo yafuatayo kutoka kwa

Orpheus, ambaye ni miongoni mwa waandishi na washairi wa Kiyunan aliyepata kuwapo karne

nyingi kabla ya Kristo: “Vitu vyote vilitendwa na Mungu mmoja, mwenye majina na nafsi tatu”.

Asili ya mafundisho haya ya utatu ni Misri, na wengi wa wazazi katika kizazi cha tatu na

cha nne wanasema: Pythagoras, Herakleitos na Plato waliufahamu utatu kwani falsafa zao

kuhusu utatu walizichukua kwa Orpheus”.

Na Professa Fiske anasema: “Wapagani wa zamani wa Kirumi walikuwa wakiamini utatu ambao

wa kwanza ni Mwenyezi Mungu, Neno na kisha Roho Mtakatifu”24

Bwana Doane anasema: “Waajemi walikuwa wakimuabudu mungu mwenye nafsi tatu, bila

tofauti yoyote na Wahindu. Miungu hao ni Ahuramazda = Muumba, Mithra = mwana wa Mungu

mwokozi na mpatanishi, na Ahriman = mhilikishaji. Katika maandiko ya Zorostarsanaan

ambacho ndiyo sheria ya Waajemi kuna sentensi zifuatazo: “Utatu wa Mungu unaiangazia dunia,

23 Frontingham, katika kitabu chake: The Cradle of Christ, ukurasa wa 112. 24 Fiske, katika kitabu chake kiitwacho Myth and Myth Makers, ukurasa wa 205.

Page 14: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

14

na kichwa cha utatu huu ni Monad. Vilevile Waashori na Waphoenic walikuwa wakiabudu

miungu yenye nafsi tatu”.25

Bwana Baccost anasema: “Wafinland (ambao ni wabarbar walioishi kaskazini mwa Perusi)

katika karne nyingi zilizopita walikuwa na mungu waliyemwita Treklaf ambaye sanamu lake

lenye vichwa vitatu katika mwili mmoja lilipatikana huko Hurtongbarg”26

Doane anasema: “Wascandnavia walikuwa wakimuabudu mungu mwenye nafsi tatu ambazo

ni Odin, Thora na Frey, na kusema kuwa hizi nafsi tatu: zote ni Mungu Mmoja.

Sanamu linaloelezea huu utatu mtakatifu linapatikana katika mji wa Opisal nchini Sweden,

ambapo wakazi wa nchi za Sweden, Norway na Denmark walikuwa wakifakhrishiana wao kwa

wao katika ujenzi wa mahekalu ya huu utatu. Kuta za haya mahekalu zilipakwa dhahabu na

kupambwa kwa picha za huu utatu. Wanamchora Odin akiwa na upanga mkononi, na huku

Thora akiwa kushotoni kwake akiwa na taji kichwani na fimbo ya enzi mkononi, naye Frey

akisimama kushotoni mwa Thora ambapo sanamu yake ina alama mbili za uume na uke.

Odin huitwa kuwa ni Baba, na Thora naye ni mwana wa peke wa Odin ambapo Frey ni mtoaji

baraka, kizazi, amani na utajiri”. 27

Wadruid walikuwa wakiabudu mungu mwenye nafsi tatu, ambazo ni Fann, Toulak na Molak.

Na wakazi wa zamani wa Siebaria walikuwa wakimuabudu mungu mwenye nafsi tatu. Nafsi ya

kwanza katika huu utatu mtakatifu wanaiita “Muumba wa kila kitu”, na nafsi ya pili “ mungu wa

majeshi” na nafsi ya tatu “ roho wa upendo wa binguni”, kisha husema kuwa “ nafsi tatu ni

Mungu mmoja”.

Wapagani wa Titer walikuwa wakimuabudu mungu mwenye nafsi tatu, ambapo katika moja ya

pesa zao zilizopo katika makumbusho ya Petersburg huyu mungu mwenye utatu mtakatifu

huonekana akiwa amekaa juu ya majani matatu.

Bwana Knight anasema : “Wakazi wa visiwa vya Ocyanus walikuwa wakimuabudu mungu

mwenye nafsi tatu, wakisema Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho mtakatifu , na

kumchora Roho Mtakatifu katika umbile la ndege”. 28

Lord Kingsbrough anasema: “Wamexico wanamuabudu mungu mwenye nafsi tatu

wanayemwita Tezcatlipoka. Pamoja naye kuna miungu wengine wawili. Mmoja amesimama

kuliani mwake na mwengine kushotoni mwake. Jina la mungu wa kwanza – aliyesimama upande

wa kulia – ni Huitzilopochtli na mwengine ni Tlaloc. Bartholomeo alipoteuliwa kuwa askofu

mkuu mwaka 1445 alimtuma kasisi Francis Hermandiz kwenda Mexico kuhubiri ukristo baina

ya wahindi wekundu, kasisi huyu alikuwa akiijua lugha ya wahindu wekundu. Baada ya mwaka

mmoja alimuandikia askofu mkuu akisema: “Hakika [wahindi wekundu] wanamuamini mungu

aliyeko mbinguni, na kwamba huyo mungu ana nafsi tatu ambazo ni Mungu Baba, Mungu

Mwana na Mungu Roho Mtakatifu, na wote hawa watatu ni Mungu mmoja. Jina la baba ni:

Pezona, na mwana: Bakab aliyezaliwa kwa mwanamke bikira, na roho mtakatifu ni: Ikihia. Pia

25 Ancient Faiths, juzuu ya pili, ukurasa wa 819. 26 Hebrew Lexicon. 27 Doane, ukurasa 377. 28 Knight, katika kitabu chake, The Symbolical Language of Ancient Art and Mythology, ukurasa wa 169.

Page 15: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

15

wanaabudu sanamu liitwalo Tincatinca na kusema kuwa ni moja lenye nafsi tatu, na kwamba

hizi nafsi tatu ni Mungu mmoja. 29

Naye Bwana Squire anasema: “Na [wahindu wekundu] Wakanada wanamuabudu mungu

mwenye nafsi tatu na kumchora katika umbile la sanamu lenye vichwa viatatu kwenye mwili

mmoja na kusema kuwa ni [watu] watatu wenye moyo mmoja na maamuzi ya aina moja”.30

Kwahiyo tumeona kuwa kuna kufanana baina ya dini za wapagani, ambapo baadhi yao

walikuwa wakiabudu miungu wengi, na hatukueleza kuwahusu (miungu) kwa sababu lengo letu

ni kuelezea mataifa yaliyokuwa yakiamini utatu.

Na lau kama sio kupendelea kwetu ufupisho, tungetoa ushahidi mwingi mbali na huo tulioutaja

kuhusu imani hii ya kipagani.

* * *

UTATU KWA WAKRISTO

Tumetoa yale yaliyoelezwa kuhusu utatu kwa wapagani, na sasa tutaeleza kidogo yale

yaliyoelezwa na wakristo juu ya imani hiyo kwa kunukuu vifungu kutoka katika vitabu vyao

vitakatifu.

Waraka wa kwanza wa Yohana, sura ya 5 mstari wa 7 inasema: “Kwa maana wako watatu

washuhudiao [mbinguni], Baba, Neno na Roho mtakatifu, na watatu hawa ni umoja”.

Injili ya Yohana, sura ya 1 mstari wa 1: “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno

alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu…” mstari wa tatu unaendelea “Vyote

vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakukufanyika chochote kilichofanyika”.

Waraka wa Paulo mtume kwa Wakolosai, sura ya kwanza mstari wa 16 na 17 : “ kwa kuwa

katika yeye (Kristo) vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi,

vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni viti vya enzi, au usultani, au enzi au mamlaka; vitu

vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake”.

Kuna aya nyingi zaidi ya hizi, na ili tusimchoshe msomaji kwa maelezo marefu, tutatosheka na

hayo tuliyokwishayataja, na atakayetaka nyongeza arejee kwenyi Injili. Aidha, kwa kuwa hapo

awali tulitoa majina mbalimbali waliyoyatumia wapagani kumuelezea mtoto wa Mungu,

inatulazimu kutaja majina ambayo wakristo pia huyatumia kwa Yesu, nayo ni: Yesu Kristo,31

Mungu,32

Bwana,33

Wamilele,34

Mwana wa Mungu,35

Mzawa wa pekee,36

Mkuu,37

Simba wa

29 Antquities of Mexico, juzuu ya tano, ukurasa 164. 30 The Serpent Symbol, ukurasa 181. 31 Luka 1:21. 32 Yohana 1:1. 33

Imetajwa katika Injili zote 34 Waraka kwa Waebrania 9:14 35 Mathayo 3:17 36 Waraka kwa Waebrania 1:6 37 Matendo ya Mitume 5:31

Page 16: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

16

kabila la Yuda38

Mkombozi,39

Mpatanishi,40

Mwokozi,41

Mchungaji mwema,42

Mwana wa

Adam,43

Imanueli44

(yaani Mungu pmoja nasi), Mwana wa Mtukufu,45

Mkuu wa uzima,46

mchukuaji dhambi ya ulimwengu,47

Mwanakondoo.48

38 Ufunuo wa Yohana 5:5: [Simba wa kabila la Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu,

na zile muhuri saba]. 39 Luka 1:68 40 Timotheo 2:5 41 Yohana 4:42 42 Yohana 10:11 43 Marko 14:62 44 Mathayo 1:23. 45 Marko 14:61 46 Matendo ya Mitume 3: 15 47 Yohana 1:29 48 Ufunuo wa Yohana 13:8

Page 17: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

17

SURA YA PILI

KUMTOA KAFARA MMOJA WA MIUNGU KAMA UTAKASO WA DHAMBI

I- Wapagani:

Anasema Bwana Doane: Fikra ya kukombolewa kwa njia ya kumtoa mmoja wa miungu

kama kafara ya dhambi ni ya zamani sana kwa wapagani na wengineo. Maeleazo ya fikra hii

kwa Wahindu yalikuwapo hata kabla ya enzi ya Vedic49

ambapo kitabu cha Rigveda

kinawaonyesha miungu wakimtoa Prusha - ambaye ni mtoto mume wa kwanza – kuwa

kafara na wanamchukulia kuwa yu sawa na Muumba. Katika kitabu cha Tazyapar hamana

kuna maelezo yafuatayo: “Bwana wa viumbe Prajaapati aliitoa nafsi yake kuwa dhabihu

(kafara) ya miungu”..

Na katika kitabu kiitwacho „Istibana Brahmana‟ kuna maelezo yafuatayo: “Na ulimwengu

kwa dhabihu hii – Berusha Meda (yaani kafara ya mtoto-mume wa kwanza – kila kitu

kitafanyika”.50

Vilevile wapagani walikuwa wakiwatoa watu kuwa kafara, na mara nyingi waliwatoa watumwa

na mateka kama kafara ya utakaso wa dhambi. Sio hivyo tu, bali walifikia hata kuwatoa watoto

wao wenyewe. Na Warumi na Wayunani walikuwa wakijitoa wao wenyewe kama kafara ya

miungu ili wapate kuwaridhia. Huko Misri walikuwa wakiwatoa binaadam kuwa kafara ambapo

desturi hii mbaya iliwatawala mpaka wakawa wanamtoa kafara mtoto wa kwanza wa kiume

kutoka katika familia za kiatanatiyyah. Walimchukua na kumpeleka hekaluni na kumwekea taji

kichwani mwake na kisha humchinja kama sadaka ya miungu kama vile wachinjwavyo

wanyama.

Bwana Hock anasema “ Na Wahindu (wapagani) huamini kuwa mmoja katika miungu

alijibadilisha katika mwili wa kibinadaam na akajitoa kafara kama utakaso wa dhambi za watu”.

Bwana Mourinior Williams anasema: “Wahindu wa kipagani huamini dhambi ya asili, na

linalojulisha hayo ni maelezo yaliyopo katika maombi yao wanayoyaomba baada ya Kiyatara

wakisema: “ Hakika mimi ni mwenye dhambi na makosa, asili yangu ni mbaya, na mama yangu

49 Vedic linatokana na Vide na Vid, na linamaana ya elimu au ya kiroho ambayo ni maandiko na nyimbo za wahindu

zinazoundwa na vitabu vinne ambavyo viliandikwa miaka elfu moja kabla ya kuja kwa Masihi (a.s).

(Qisswatul hadhaarah, juzuu 3 uk. 38).

50 Amenukuu kutoka katika kitabu cha Bwana Lundy, kiitwacho “Monumental Christianity”.

Krishna akiwa msalabani na

taji la dhahabu kichwani

mwake.

Page 18: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

18

alinibeba tumboni kwa dhambi, basi nikomboe Ewe mwenye jicho la huruma, ewe mkombozi

wa wakosaji, ewe mwenye kuondosha dhambi na makosa”.51

Naye Professa Doane anatoa maelezo yafuatayo: “Wahindu wanaamini kuwa Krishna, mzawa

wa pekee ambaye ndiye Vishnu na ambaye kwa imani yao hana mwanzo wala mwisho,

aliteremka kuja kuikomboa dunia kutokana na kuelemwa na mizigo ya dhambi. Akamkomboa

mwandamu kwa kujitoa kafara badala yake”.

Naye kasisi George Cox anasema: “Wahindu wanamsifu Krishna kwa ushujaa wa hali ya juu

uliojaa uungu kwa kitendo chake cha kujitoa kafara, na kusema: Hakika hakuna awezaye

kufanya kitendo hiki pasipokuwa yeye” 52

Mwengine ni Bwana Almicio Konew anayetoa maelezo yafuatayo: “Wahindu hukieleza kifo cha

Krishna kwa namna mbalimbali, na iliyokuwa mashuhuri zaidi ni kuwa alikufa kwa kutundikwa

juu ya mti na kupigiliwa kwa mkuki”.

Bwana Doane akifafanua mti huo, anasema: “Mti uliokusudiwa hapa ni “msalaba”, na kwamba

Bwana Mour alimchora Krishna akiwa katika hali ya kusulubiwa kama alivyochorwa katika

vitabu vya kihindu akiwa ametobolewa mikono na miguu, halikadhalika kanzu yake ikiwa

imewekewa picha ya moyo wa mwanadamu”53

“Na katika mafundisho ya Vishnu Purama, tunajua kuwa baada ya mwindaji kumpiga Krishna

kwa mkuki, (mwindaji) alijuta na kuungama mbele yake akisema: “Nihurumie, mimi ndiye

niliyeangamizwa na dhambi zangu, na wewe ndiwe mwenye uwezo wa kuniangamiza. Krisha

akamjibu: Usihofu, nenda mbinguni kunako makazi ya miungu. Alipokwisha kumwambia

maneno hayo, kilitokea kipandwa kilichompeleka mpaka mbinguni”.

Katika sifa apewazo Krishna ni: “Mwenye kusamehe madhambi na Mkombozi dhidi ya joka la

umauti”.

Padri Geogius alimchora mungu Andra anayeabudiwa na watu wa Nepal 54

akiwa amesulubiwa,

kama wamchoravyo siku ya sikukuu yao inayofanyika katika mwezi wa Nane.

Profesa Higgins anasema katika kunukuu maelezo yaliyoandikwa na Andrada ambaye ndiye

mkazi wa mwanzo kutoka Ulaya aliyeingia Nepal na Tibet55

: “Anasema katika kumzungumzia

Mungu Andra ambaye wanamuabudu na kuamini kwamba damu yake ilimwagika kwa

kusulubiwa na kutobolewa kwa misumari ili kuwakomboa watu kutokana na dhambi zao, kuwa:

“Picha za msalaba zipo katika vitabu vyao”. Naye Profesa Doane akasema: “Katika eneo la

kusini mwa India, Tangor na Ayondia wanamuabudu Mungu aliyesulubiwa aitwaye “Pali” na

kuamini kuwa ndiye Vishnu aliyegeuka katika umbile la kibinaadamu, mbapo humchora akiwa

ameatobolewa mbavu na mikono yote miwili”.

51 Imenukuliwa kutoka katika kitabu cha Bwana Lundy, Monumental Christianity 52 Ancient Faiths 53 Doane, ukurasa 184 54 Nepal ni nchi iliyopo pembezoni mwa milima ya Himalaya ya mashariki, kati ya India na Tibet, kwa sasa mji

wake mkuu ni Kathmandu 55 Tibet, iko kusini-magharibi mwa china, mji wake mkuu ni Lasa

Page 19: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

19

Katika wimbo wa kidini wa Budha kuna maneno yafuatayo: “Ulikabiliana na mateso, matatizo,

kufungwa, umauti na kuuawa, kwa subira na upendo mkubwa ili kuleta furaha kwa watu na

ukawasamehe waliokukosea”. Kadhalika husema kuwa BUDHA ni tabibu mkuu, mwokozi wa

ulimwengu, mpakwa mafuta (mtakatifu), Masihi, Mzawa wa pekee n.k. Vilevile husema

kwamba alijitoa kafara ili kufuta dhambi za wanadamu na kuwafanya kuwa warithi wa ufalme

wa mbinguni. Na pia, kwa kuzaliwa kwake aliacha utukufu wake ulimwenguni ili awakomboe

watu kutokana na maovu na adhabu kama alivyoahidi.

Profesa Beal anasema: “Pujana alisema: “Nitajifanyia (jibadilisha katika) mwili wa kibinadam,

nitateremka na kuzaliwa kati ya watu ili nipate kuwapa amani na mapumziko, na kuwaondolea

huzuni na mateso ya dunia. Kwa yakini kazi yangu hii siifanyi kwa kutaka chochote katika utajiri

na furaha”. 56

Bwana Hock anasema: “Kwa matazamo wa Mabudha, Budha ni mtu na wakati huohuo ni

Mungu na kwamba alichukua mwili katika ulimwengu huu ili awaongoze watu, kuwakomboa na

kuwabainishia njia ya amani. Mabudha wote wana imani hii kama wanavyoamini kuwa Budha

ndiye Mwokozi wa watu”.

Naye Bwana Max Muller anasema: “Mabudha hudai kuwa Budha alisema: “Acheni makosa

yote yaliyotendeka ulimwenguni niyabebe ili kwamba ulimwengu upate kukombolewa”.57

Profesa Williams naye anasema: “Wahindu husema kuwa: Miongoni mwa huruma zake (yaani

Budha) ni kuwa aliiacha pepo na kuja duniani kwa sababu ya makosa na maovu ya wanadamu ili

awakomboe kutokana na dhambi zao na kuwaondolea adhabu wanayostahiki”.58

Doane anasema: “Imani ya kumtoa kafara mkombozi wa ki-Mungu kwa njia ya mateso na mauti

ni ya zamani sana kwa Wachina. Moja ya vitabu vyao vitukufu kiitwachoYapkink

kinamzungumzia Tiyan kuwa ni mtukufu wa kipekee mwenye fadhila za mbinguni na ardhini, na

kwamba ataurejesha ulimwengu kwenye wema. Vilevile anataabika na kupata mateso, na

hanabudi kupita katika mkondo ambao mawimbi yake hayatamwingia kwa kuwa yeye pekee

ndiye awezaye kumpa Bwana dhabihu inayomstahiki…kwani watu huzitoa nafsi zao kuwa

dhabihu kwa lengo la kutaka ubwana, na wasomi nao hufanya hivyo kwa lengo la kutaka vyeo

na umashuhuri, na viongozi nao pia hufanya hayo kwa lengo la kuziimarisha familia na koo zao.

Lakini mtakatifu Tiyan alifanya hivyo kwa ajili ya watu, na amekufa kwa ajili ya kumkomboa

mtu mwema. Pia huamini kuwa ndiye pekee aliyekuwa pamoja na Mwenyezi Mungu tangu

milele na milele hata kabla ya chochote”.

Bwana Bonwick anasema: “Wamisri wanamchukulia Osiris kuwa miongoni mwa wakombozi

wa watu, ambaye kwa sababu ya juhudi zake za kutenda mambo mema alikumbana na mateso,

na kwa sababu ya kupambana na dhambi alitenzwa nguvu na kuuawa” 59

56 The Romantic Legend of Saki Buddha from Chinese Sanskrit, uk. 33 57 History of Ancient Sanskrit Literature, uk. 80 58 Hinduism, uk, 214 59 Egyptian belief and Modern Thought, ukurasa, 165

Page 20: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

20

Naye Bwana Murray anasema: “Wamisri wanamheshimu Osiris na kumchukulia kuwa mfano

wa hali ya juu wa kujitoa kafara ili watu wapate uzima”

Doane anamnukuu Sir Wilkinson akisema: “Mateso na kifo cha Osiris ndiyo siri kubwa katika

dini ya Wamisri, na baadhi ya athari za imani hii zinaonekana wazi katika dini za mataifa.

Humchukulia Osiris kuwa mwanamapinduzi wa Kimungu aliyeleta fikra njema. Na (imani)

kuhusu kuja kwake duniani, kifo na kfufuka kwake katika wafu na kuwa atatengeneza dini ya

wafu siku za mwisho, imani hii inafanana na ile ya miungu wa Wahindu” 60

“Horus alikuwa akiitwa Mwokozi, Mkombozi, Mungu wa uzima, wa milele na mzawa wa pekee.

Vilevile Attis huitwa Mwana Mkombozi wa pekee. Pia Wafrige (ambao ni wakazi wa Asia

ndogo) walikuwa wakimuabudu, ambapo walimfananisha na mtu aliyefungiwa mtini kukiwa na

mwanakondoo miguuni kwake. Hali hii inafanana na ile ya Apollo aliyekuwa akiabudiwa na

Wamilitayo ambao husema kuwa alikufa kwa mwili na kwamba yeye ndiye mtawala wa mambo

ya ajabu. Pia husema kuwa alikamatwa na askari wa Kikeldayo ambao walimuua na kumpigilia

misumari ili apate maumivu zaidi, na kwamba alisulubiwa kwa ajili ya kuwakomboa”.

Naye Mis Jamson anasema: “Wamilitayo walikuwa wakimfananisha Mungu kama mtu

aliyesulubiwa kwa kufungwa kamba mikono na miguu akiwa juu ya mti huku chini ya miguu

yake kukiwa na picha ya mwanakondoo. Na Wasuria husema kuwa Tamuz, mungu aliye mzawa

wa pekee wa mwanamke bikira, alipata mateso kwa ajili ya watu, na kwa ajili hiyo wanamuita

kuwa ni MKOMBOZI aliyejitoa nafsi kwa kusulubiwa.Vilevile walikuwa wakisherehekea

kumbukumbu za kifo chake kwa kutenga siku maalumu kila mwaka ambapo huweka sanamu juu

ya tandiko wakidai kuwa ndiye, na kuanza kumlilia huku wakuu wao wakiimba na kusema:

“Mtumainini Mungu wenu kwani mateso aliyoyapata yametuletea ukombozi”.61

Bwana Doane anasema: “Wapagani walikuwa wakisema kuwa Primecion ni Mkombozi na

kumuita kuwa ni Mungu aliye hai, rafiki wa mwanadam, aliyeitoa nafsi yake kama kafara ya

kuwakomboa watu. Simulizi nyingi za kusulubiwa kwa crasius zilizoandikwa na Esius katika

Athena miaka mia tano kabla ya Masihi (a.s.), ndiyo mashairi ya zamani sana yaliyobaki mpaka

hii leo kuhusiana na suala la kusulubiwa. Ama hila na hadaa zilizotajwa humo, zimechukuliwa

kutoka katika simulizi za zamani sana, na hazina mfano katika kuleta taathira za hisia kwa

watazamaji. Hakuna aliyemtangulia kubainisha na kuelezea mateso yaliyompata huyo Mungu

kwa kiasi kwamba mtazamaji hawezi kujizuia kutoa taswira yake kutokana na muathiriko

mkubwa na jinsi ilivyokuwa taathira kwa wale waliokuwa wakiamini uungu wa shujaa wa

simulizi hii, ambaye ni rafiki yao, muumba wao, mfaidishaji na mkombozi wao aliyevumilia

mateso na huzuni kwa ajili yao, na ambaye, kwa sababu ya dhambi zao, alipata kuumizwa, na

kwa sababu ya maovu yao aliteswa na kustahmili adhabu ili kuwaokoa. Kwa kupigwa na

kuchapwa mijeledi waliponywa. Aliteswa, akanyanyaswa na kudharauliwa na wala hakutetereka.

Subira yake kubwa ilionekana pindi makuhani wa Mungu wa shari walipokuwa wakiipigilia

mikono na miguu yake kwenye mlima wa Caucasus, na kwamba hana mfano wa ukamilifu na

uvumilivu aliouonyesha akiwa ametungikwa na hali mikono yake ikiwa imenyooka kwa namna

ya msalaba ili kuwatumikia na kuwapenda watu ambapo utumishi wake huu ulimsababishia

mateso haya ya kutisha juu ya msalaba.Wakati akiteseka kwa adhabu ya huo usaliti, rafiki yake

Osinus mwindaji alikiri kuwa alishindwa kumfanya akubali kufanya suluhu na Jupiter ili kuacha

60 Doane, uk, 190 61 The History of Our lord

Page 21: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

21

kuwakomboa watu, na hapo Osinus mwindaji alikimbia na kumucha akiwa hana yeyote

anayeumizwa na kifo chake zaidi ya kundi la wafuasi wachache wenye moyo ambao walimlilia

na hata wakaweza kuiondoa hali ya kupenda mabaya katika moyo wake”62

Bwana Doane anasema: “Wapagani walikuwa wakimuita Bacchus mwana wa Jupiter atokanaye

na mwanamke bikira, kuwa ni mwokozi, mwana wa pekee wa Mungu, dhabihu, mchukuaji wa

dhambi za watu na mkombozi. Walikuwa wakisema: “maovu yalipozidi ardhini Bandora

alimuomba Jupiter Mungu Mkuu ili aje na kuwakomboa watu kutoka katika makosa na dhambi.

Jupiter akakubali ombi lao na kumtoa mwanaye ili kuwakomboa wenye dhambi duniani.

Bucchus mkombozi akaahidi kuifanya dunia kuwa huru kutokana na mizigo ya dhambi. Pia

huimba na kumuabudu ili kulitukuza jina lake.Ili kukamilisha kazi hii, Mungu Jupiter alimshukia

mwanamke aitwaye Semele ambaye alichukua mimba na hapo akaitwa mama wa Mungu.

Vilevile Bucchus mkombozi wa watu, alisema: Mimi ndiye kiongozi wenu, mlinzi wenu na

mkombozi wenu. Mimi ndimi Alfa na Omega”.

Heracles mtoto wa Zanis alikuwa akiitwa MKOMBOZI, ambapo kulikuwa na pesa

iliyonakshiwa kwa maneno yafuatayo: “Heracles Mkombozi”.Vilevile walikuwa wakimuita:

Mwana wa pekee, Neno, na kwamba alirudi na kuungana pamoja na Mungu, na kuwa yeye ndiye

Muumba wa kila kitu, Baba wa nyakati. Vilevile Escolapius huitwa MKOMBOZI na hekalu

lililojengwa kwa kumbukumbu ya jina lake huitwa hekalu la MKOMBOZI. Mtawala wa Roma

Hadriyan (138 A.D) alikuwa akisema kuwa Serapis ni mungu. Katika moja ya mahekalu ya kale

huko Iskandaria kulipatikana msalaba ambao juu yake kulikuwapo picha ya huyu mkombozi wa

Kimisri.

Waajemi walikuwa wakimuita Mithra kuwa ni mpatanishi baina ya Mwenyezi Mungu na watu,

mkombozi ambaye alikubali mateso ili kuwaokoa na kuwakomboa watu. Vilevile husema kuwa

ni “Neno” na “Mkombozi” na kuamini kuwa Zoroaster ni mtume wa mungu aliyetumwa kuja

kuwakomboa watu kutoka katika njia mbaya. Mpaka sasa tunawaona wafuasi wake wakimuita

Zoroaster “aliyehai”, mbarikiwa, mwana wa pekee, wa milele pamoja na sifa nyingine kama

hizo. Halikadhalika (huamini kuwa) alipozaliwa ilitokea nuru iliyoangaza chumba alichozaliwa,

na kwamba alimchekea mama yake wakati wa kuzaliwa kwake, na humuita kuwa ni “Nuru

iangazayo iliyotokea katika mti wa maarifa na kwamba alitungikwa juu ya mti”.

Ariyan Katika historia yake kuhusu alama za Iskandaria anasema: katka bendera ya majeshi

ya Boreas kuna picha ya mtu aliyesulubiwa”.

Naye Higgins anasema: Hiyo picha inamuelezea ima Ostroba au Silvahana, kwani inaonekana

kwa mtazamaji kana kwamba ni picha ya mtu ambayo Waroma walikuwa wakiibeba katika

vichwa vya bendera zao nayo inafanana na picha ya njiwa ambaye Waashori walikuwa

wameiweka katika bendera zao na hakuna shaka kuwa ile picha ni picha ya “mwana wa mungu

aliyesulubiwa”.

Wamexico walimuabudu mungu aliyesulubiwa wakamwita Mkombozi, na dhabihu. Mwana

wa mungu kwa lugha yao humwita “Bakob” na “Oboukou”. Lau kama Wahispania

wasingevichoma moto vitabu vya wakazi wa Mexico na Peru, kuyabomoa mahekalu yao na

62 Doane, 192- 193

Page 22: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

22

kuchora picha na alama zao, tungepata kufahamu mambo mengi kuwahusu, zaidi ya haya

tunayoyafahamu kwa sasa. Na lau kama si vitu vichache vilivyosalimika kutokana na mikono

dhalimu ya Wahispania tusingetambua ya kuwa walikuwa wakimuabudu mungu aliyesulubiwa

kama kafara ya dhambi zao, na ya kwamba walikuwa wakimuita kuwa ni mwana wa mungu

aliyetolewa dhabihu.

Wakazi wa Yokatani walimuabudu mungu aliyesulubiwa kuwa kafara ya dhambi zao na

kumwita kuwa ni mwana wa mungu . Ilipatikana idadi kadhaa ya misalaba iliyokuwa na picha

kamili ya huyu mtoto aliyesulubiwa kwa kafara ya dhambi”.

Bwana Kniht anafafanua zaidi kwa kusema:

Wapagani walikuwa wakimwita Apollo kuwa ni “Mchungaji mwema”,

halikadhalika wakamwita Mercury kuwa ni “ mchungaji mwema”. Na

Krishna mkombozi wa Wahindu aliitwa kuwa ni “mchungaji mwema”,63

na wengine wengi ambao kwa sababu ya kupendelea kufupisha

tunatosheka na tuliyoyaeleza .

II – Wakristo:

Kadhia ya kusulubiwa Kristo na imani ya ukombozi dhidi ya dhambi

ni msingi wa imani kwa wakristo. Habari ya kusulubiwa imeelezwa katika

injili ya Mathayo sura 27,64

Injili ya Marko sura ya 15,65

Injili ya Luka sura

23,66

pamoja na Injili ya Yohana sura ya 19.67

Hatuna haja ya kunukuu

vifungu vyote hivi kwa sababu ni mashuhuri sana. Lakini tunatoa kifungu kimoja kama mfano

wa yale yaliyoelezwa katika Injili kuhusu kusumbuliwa kwake.

Waraka wa Paulo Mtume kwa Wagalatia sura ya 13: “Kristo alitukomboa katika laana ya

Torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu, maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu

63 The Symbolical Language Of Ancient Art,ukurasa wa 22 64

Hata walivyokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene jina lake Simoni, huyu

wakamshurutisha auchukue msalaba wake… Walipokwisha kumsulubisha, waligawa mavazi

yake, walipiga kura. (Mathayo 27:32 -35) 65 Hata wakiisha kumdhihaki wakamvua lile vazi la rangi ya zambarau wakamvika mavazi yake mwenyewe;

wakamchukua nje ili wamsulubishe wakamshurutisha mtu aliyekuwa akipita, akitoka mashamba, Simoni

Mkirene, baba yao Iskanda na Rufo ili auchukue msalaba wake. Wake wakamsulubisha wakagawa mavazi yake,

wakapigia kwa kila mtu atue nini. Basi ilikuwa saa tatu, nao wakamsulubisha. (Marko 15:20 -26) 66 Lakini wakapiga kelele, wakisema, Msulubishe, .Lakini wakatoa sauti zao kwa nguvu sana wakitaka asulubishwe. Na walipokuwa wakimwondoa wakimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa akitoka shamba,

wakamtwisha msalaba auchukue nyuma yake yesu. (Luka 23:21-26) 67

Basi wale wakapiga kelele, Mwondoshe! Mwondoshe! Msulubishe! Pilato akawaambia, Je! Nimsulubishe

mfalme wenu! Wakuu wa makuhani wakamjibu, Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.

Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulubiwe nao wakampokea Yesu. Akatoka hali akijichukulia msalaba

wake mpaka mahali paitwapo Fuvu la kichwa au kwa Kiebrania, Golgotha.Wakamsulubisha huko, na wengine

wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku na Yesu katikati.

Yesu akiwa

msalabani, na

taji la miba

kichwani

mwake.

Page 23: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

23

aingikwaye juu ya mti; Ili kwamba baraka ya Ibrahim iwafikie mataifa katika Yesu Kristo,

tupate kupokea ahadi ya roho kwa njia ya imani”.

Suala la kusulubiwa limetajwa katika Injili zote, na kumchora akiwa amesulubiwa moja kwa

moja kama Krishna. Na ama muda aliosulubiwa una khitilafu na kupingana katika maandiko

na hatukutaka kuielezea khitilafu hiyo kwa kuwa iko nje ya lengo letu.

SURA YA TATU

KIZA KILICHOTOKEA KUTOKANA NA KIFO CHA MKOMBOZI WA ULIMWENGU

I – Wapagani:

Wahindu husema kwamba: “Krishna mkombozi wao alipokufa msalabani, masaibu na ishara

nyingi zilitokea ulimwenguni, mwezi ukazungukwa na duara jeusi, kiza kikatokea wakati wa

mchana, mbingu ikanyesha moto na mchanga, ndimi za moto zikatokeza na mashetani

Page 24: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

24

yakaanza kufanya uharibifu katika ardhi, na wakati wa kuchomoza na kuzama kwa jua

wakaonekana watu wakipigana kila upande na kila sehemu”.

Bwana Davis anasema kwamba Wahindu husema “Ilipoanza vita baina ya Buddha Mkombozi

wa ulimwengu, na kiongozi wa Mashetani, maelfu ya nyota yalidondoka, kiza kikatanda na

mawingu yakakithiri hata hii dunia yenye mabahari na milima ilitingishika kana kwamba ni

chembe ndogo inayopeperushwa, na bahari zikachafuka kutokana na kuzidi kwa matetemeko.

Maji ya mito yalirejea kwenye vyanzo vyake, milima na miti yake iliyodumu kwa vizazi na

vizazi iligongana. Ngurumo za vimbunga zikashtadi. Sauti ya mgongano ilikuwa kubwa sana.

Jua lilipungua nuru yake na kiza kinene kikatanda. Anga lilijaa ngurumo za roho”.68

Bwana Farar anasema: “Warumi na Wayunan wa zamani waliamini kuwa wakati wa kuzaliwa na

kufa kwa mmoja wa watu watukufu matukio kadhaa yanayoelezea hali hiyo hutokea katika

mbingu. Waliwahi kusema kuwa jua lilipungua nuru yake kwa kifo cha Rumulus muasisi wa

Roma na kutokea giza juu ya uso wa dunia lililodumu kwa muda wa masaa sita”.69

Bwana Gibbon anasema: alipouawa mkombozi Iscolapius jua lilipungua nuru yake, ndege

wakajificha katika viota vyao na miti ikainamisha matawi yake kama ishara ya huzuni. Mioyo ya

watu iliumia, kwani mponyaji wa maradhi na njaa yao alikuwa ameiaga dunia”70

Bwana Doan anasema: wapagani husema: “Heraclus alipokuwa katika hali ya kukata roho

alimwambia mwanamke mwaminifu aitwaye Youl aliyemfuata mpaka eneo alilokata roho: Usilie

kwani kazi yangu imekamilika na sasa ni wakati wa kupumzika, na tutakutana katika nchi yenye

nuru. Pia Mungu Mkombozi alipokufa giza lilitokea ulimwenguni ambapo Mungu Mkuu Zius

alishuka kumchukua mwanaye na kumpeleka kwake, na viwanja vya Ulimpios vikafunguliwa ili

kumlaki shujaa mweye nuru ambaye amepumzika kutokana na mateso makali na kuwa sasa huko

aliko amevaa vazi jeupe na taji kichwani mwake”.

Vilevile husema kwamba Pius alipotaka kuiacha hii dunia yenye kila aina ya mateso na huzuni,

alimwambia Antiyocon: ubaki salama, na usilie ewe mwanangu, kwani nina furaha yakuutua

mzigo wa huzuni na mashaka”, na hapo ulipokaribia muda wa kifo chake, zilijitokeza alama

nyingi mbinguni na ardhini. Ardhi ilitingishika na ngurumo za radi zikaenea angani.

Warumi walikuwa na mungu aliyeitwa Cyirinus aliyetokana na jua na hatimaye kurejea juani.

Alizaliwa baada ya mungu wa majeshi kumshukia mwanamke bikira mwenye asili ya kifalme.

Olius dhalimu alimtesa na akalelewa kwa wachungakondoo. Alipokufa alikatwa vipande

vipande, na alipopaa kwenda mbinguni jua lilipungua nuru yake.

Bwana Kingsbrough anasema: “Wamexico wa zamani walikuwa wakiamini kuwa Quetzalcoatl

mkombozi aliyesulubiwa, alipokufa jua ilififia nuru yake na mwanga wake ukapotea”71

II – Wakristo:

68 Budhism, uk. 36 69 The Life of Christ, uk.52 70 The History of Gibbon, uk.159 na 590 71 Antiquinties of Mexico, juzu ya 6,uk,6

Page 25: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

25

Tumetoa maelezo ya waumini wa miungu mbalimbali, kama vile, Krishna, Budha, Andra na

wengineo kuhusu kiza kilichotokea wakati wa kifo cha moja ya miungu hii iliyotajwa, iwe ni

kwa kusulubiwa au kuuawa. Mambo hayo vilevile yameelezwa kutokea wakati wa kusulubiwa

Yesu Kristo.Tazama Injili ya Mathayo, sura ya 27, msitari wa 45: “Basi tangu saa sita palikuwa

na giza juu ya nchi yote hata saa tisa”.72

Injili ya Marko, sura ya 15, msitari wa 33,73

pamoja na

Injili ya Luka,sura ya 23 msitara wa 44.74

72 Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema: Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani Mungu

wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? (Mathayo 27:46) 73 Na ilipokuwa saa sita, palikuwa na giza juu ya nchi yote, hata saa tisa. Na saa tisa Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Maana yake, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? (Marko 15:33 -

34) 74 Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda. Jua limepungua nuru yake; pazia la

hekalu likapasuka katikati.Yesu akalia kwa sauti kuu, akisema, Ee Baba, mikonono mwako naiweka roho yangu.

(Luka 23:44 - 45)

Page 26: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

26

SURA YA NNE

KUZALIWA KWA MIUNGU WALIOJITOA DHABIHU ILI KUWAKOMBOA WATU

I – Wapagani:

Bwana Doane anasema: Miongoni mwa imani za Wahindu ni kusema kwao kuwa mmoja wa

miungu alijigeuza katika mwili na akashuka na kuishi nao. Hayo yameelezwa kwa aina

mbalimbali za fikra na simulizi za kimashariki. Krishna mpaka sasa ndiye mungu anayependwa

sana na wanawake wa Kihindu, na kundi linalomheshimu limetopea katika kumuabudu, ambapo

lilieneza mafundisho linaloshikamana nayo sana ambayo husema kuwa Krishna anatofautiana na

miungu wote waliojigeuza katika mwili kwa sababu hao wengine walikuwa na sehemu ndogo ya

uungu, lakini Krishna ndiye Mungu Vishnu aliyedhihiri katika mwili wa kibinadamu”.75

Allen naye anasema: “Krishna ndiye mkuu kuliko miungu wote waliojibadili katika mwili.

Anatofautiana nao sana kwa sababu walikuwa na sehemu ndogo ya uungu, ama yeye (Krishna)

ndiye Mungu Vishnu aliyedhihiri kwa mwili wa kibinaadamu”.76

NayeToma Maurice anasema: “Wahindu huitukuza sana nchi yao kwa kuwa humo ndimo

alimozaliwa Krishna katika mwili”77

Doane anasema: Wahindu husema kuwa Krishna ni mtoto wa mwanamwali, mtakatifu, Devaki

ambaye humuita mama wa Mungu”.

Katika kitabu cha Kihindu kiitwacho “Biha Kafat Purun” kuna maelezo

kuwa Krishna alisema: “Nitajigeuza katika Mitwar katika nyumba ya

Yado na kutoka katika kizazi cha Devaki nitazaliwa na kufa, na sasa

umefika muda wa kuonyesha nguvu zangu na kuikomboa dunia kutokana

na mizigo ya madhambi”.

Na katika kitabu kitakatifu cha Wahindu kiitwacho “Vishnu Purana”

kuna maelezo yafuatayo: “Miungu imemtukuza Devaki ambaye

aliichukua mimba ya Mungu mwenye macho ya huruma – Mkombozi wa

ulimwengu -, na nani awezaye kuutazama uso wa Devaki kwa

sababu ya nuru iangazaye, kwani kila anayeitazama nuru yake huweza

kukimbia (kugeuza uso wake)… Na miungu wasioonekana kwa watu

wamemtukuza tangu Vishnu alipomshukia. Mungu Vishnu ndiye chanzo

cha mti wa mambo yote, hadirikiwi na fikra za miungu, majini, wanafalsafa

na watu wote, hivi sasa na hata baadaye, kama vile ambavyo hazikumdiriki

hapo zamani, na Brahma ndiye Muabudiwa. Miungu wote walipata heshima ya kuukomboa

ulimwengu kutokana na mizigo yake mizito kwa kumtuma Vishnu kwenye tumbo la Devaki,

kuzaliwa naye kama mwanaye na kudhihiri kama Krishna ambaye ndiye Brahma mwenyewe, na

kwamba ni siri ya ajabu kwa Mungu kuwa katika mwili wa binaadamu”. Vilevile akasema: Mimi

75 Doane,ukurasa wa 112 76 India,ukurasa wa 397 77 The history of Hindostan, juz. 3, uk, 43

Devaki, mama

wa mungu akiwa

na Krishna

mwanaye

Page 27: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

27

ndiye mkuu wa pekee, nauthibitisha uwepo wangu kwa uweza wangu. Na pindi mema

yanapopungua na machafu kuongezeka ulimwenguni, hudhihiri na kuonekana kutoka kizazi hadi

kizazi ili kumbakisha mtu mwema na kumuangamiza muovu na kurejesha mema ulimwenguni”.

Katika kitabu kiitwacho “Bahaqiqat Jita” imeelezwa kuwa Mungu Krishna alimwambia

mwanafunzi wake aitwaye Arjuna: Nawe Ee Arjuna, ambaye kwa sababu ya imani yako umekiri

uungu wa kuzaliwa kwangu, ungana nami na uingie ndani mwangu”. Vilevile akasema:

“Wajinga hawakiri uungu wangu na kwamba mimi ni Mungu wa kila kitu, na hunidharau kwa

sababu ya kuwa kwangu katika mwili wa kibinaadamu wakiegemea kwenye shari, uovu na

vitimbi vilivyomo katika nyoyo zao, basi matarajio yao, elimu zao, fikra na tabia zao ni chafu.

Ama watu wenye akili zenye uelewa huegemea kwenye maadili yao ya Kimungu na kutambua

kuwa mimi ndiye wa milele niliyekuwapo kabla ya chochote. Huniabudu kwa mioyo

isiyoegemea upande wa miungu wengine”.

Bwana Doane anasema: “Mungu Budha, mtoto wa Bikra Maya ambaye huabudiwa na

Mabuddha wa India na wengineo, huelezewa kuwa aliiacha Paradiso akashuka ulimwenguni na

kudhihiri katika mwili wa kibinadamu kwa sababu ya huruma kwa watu ili apate kuwaokoa

kutokana na dhambi, kuwaongoza kwenye njia iliyonyooka, kuichukua mizigo ya dhambi zao,

kuwakomboa kutokana na adhabu na kuwaondoshea kisasi walichostahiki kukipata”78

Katika kitabu cha Kichina kiitwacho ((Fotinghang)) kuna maelezo yafuatayo: Mungu Budha

alipotaka kuteremka duniani ili azaliwe humo aliwaita malaika wa mbinguni na wakazi wa

ardhini akisema: Enyi wafu! Pambeni ardhi yenu kwa sababu Budhishu Mahte mkuu

atateremka hivi karibuni kutoka Tusiya na kuzaliwa baina yenu, kwa hiyo jiandaeni kwa

mavazi ili kumngojea.Vile vile husema kwamba kizazi (tumbo) atakachoshukia Mungu Budha

ili kuwa katika mwili ni kama chombo kilichowekwa dhahabu ndani yake na hakuna mwanadam

yeyote anayoweza kubebwa humo kama ilivyokuwa kwa Budha kwani yeye atashuka humo

pasipo kwa njia ya manii. Bahamaya alipochukua mimba yake hakupata kutamani mwanaume

tena na akaishi akiwa bikira.

Katika kumzungumzia Budha, Hock ambaye ni mmoja wa wamisionari wa kifaransa ametoa

maelezo yafuatayo: Mabudha humuona kama Mungu aliyechukua mwili (yaani mwili wa

kibinadam) akaja katika hii dunia ili kuwafundisha watu, kuwaongoza, kuwakomboa na

kuwajengea njia ya amani…na imani ya kukombolewa kwa njia ya Mungu anayeonekana kwa

mwili wa kibinadamu imeenea sana kwa Mabuddha.

Wapagani humuelezea kila mungu aliyechukua mwili ili kuwakomboa watu kuwa ni Mungu

Mkuu, Mungu wa ulimwengu, Mweza, Mjuzi, mwenye hekima na mkombozi wa watu wote79

Bwana Bunsen anasema: Na mungu wa pekee humuita kuwa mtakatifu, muumba wa saada,

mfalme wa yote, Bwana mwenye nguvu, asiye na mwanzo wala mwisho, mwenye utukufu, roho

mkuu wa milele, Mungu ambaye ni lazima kwa watu walio huru kumuabudu.

78 Doane, ukurasa wa 115 79 Oriental Religions, uk.604

Page 28: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

28

Katika maombi ya mcha mungu Ammora kwa mungu Buddha aliyedhihiri katika mwili, kuna

maelezo yafuatayo: Ukuu ni wako ewe uliyejidhihirisha kwa jinsi ya Budha aliyejichukulia

mwili, Ewe mola wa ulimwengu utukufu ni wako, Ewe mungu wa milele uonekanaye katika

mwili heshima ni yako. Ewe mola wa dhahiri na rehma, Ewe muumba wa mateso na huzuni,

Ewe muumba wa kila kitu, Ewe mlinzi wa ulimwengu, Ewe mjuzi wa rehma na alama zake,

Ewe Mkombozi.

Bunsen anasema: Mabuddha husema kuwa kuzaliwa kwa Budha kulikuwa hivi:Gautama

Buddha alipojichukulia mwili, nguvu ya kimungu iitwyo roho mtakatifu ilimshukia Bikira

Maya, na kuteremka kwake ilikuwa ni kwa namna ya tembo mweupe. Na Mabuddha wa Tekasi

husema kuwa maana ya tembo mweupe ni hekima na nguvu .

Doane anasema: Mabuddha wa India husema kwamba kushuka kwa malaika ambaye alikuja

kuwa Budha na kuwa katika mwili, ilikuwa kwa njia ya rehma, na kwamba tembo ambaye

(Budha)alishuka kwa namna yake ni alama ya nguvu na hekma ya kimungu.Vile vile katika

Tekasi humuelezea kuwa alishuka kutoka mbinguni kwa namna ya tembo mpaka mahali

alipokuwa Bikra Maya . Lakini Mabudha wa China hueleza katika vitabu vyao kuwa roho

mtakatifu ambaye ni “shing shen” Alimshukia Bikra Maya . Katika kitabu cha kichina

kiitwacho Forbinhang kuna maelezo yafuatayo: Mama akiona usingizini mwake kwamba tembo

mweupe ameingia ubavu wake wa kulia, ikiwa atazaa mtoto wa kiume basi atakuwa kiongozi wa

ulimwengu ambaye ni Buddha na kila kiumbe kufaidika naye, nayeye ndiye awezaye kuwaokoa

watu kutoka katika mabahari ya maovu na huzuni.

Anasema Profesa Ferguson: Mabudha humchora Maya akiwa amelala na

kuona usingizini mwake kuwa tembo mweupe anakuja na kuingia katika

ubavu wake wa kulia. Humuimbia nyimbo mbali mbali kuwa amejaa

neema na ni malkia wa mbinguni na muondoshaji wa huzuni na kwamba

mwanaye Budha ni mfufuaji wa watu, tegemeo la mataifa na mwenezaji

wa amani. Na malkia Maya atamzaa mtoto mtakatifu mwenye hekima

ambaye kila kiumbe kitafaidika naye na atautawala ulimwengu.

Anasema Isbans Hard kuwa: mwili wa malkia Maya ukawa angavu kama kioo,

ndani yake akionekana mtoto kwa urahisi kana kwamba ni kuhani aliyeketi juu

ya kiti cha enzi akitoa baraka au kama picha ya dhahabu katika chombo angavu

ambako huonekana maendeleo yake siku hadi siku. Hivyo ndivyo Mabudha

wanavyoamini.Vile katika ukurasa 85 anasema: mwakilishi wa Budha duniani

anaitwa Dlailama au Lama mkuu. Na wakazi wa Siyami humuamini mungu

aliyezaliwa na mwanamke bikira wanayemwita mungu mkombozi ajulikanaye

kama Kodam kwa lugha yao, na mama yake ni binti mzuri, mwanamwali, ambaye alifunuliwa

na mungu akajitenga na watu na kwenda kwenye maeneo ya misitu isiyopitiwa na watu

akisubiri kuchukua mimba ya mungu kama alivyofunuliwa. Ndipo siku moja alipokuwa akisali

alichukua ujauzito kutoka kwenye mionzi ya jua iliyomshukia. Alipohisi kuwa na mimba

alitoka huko na kuelekea pwani ya ziwa lililopo Siyam na Kabodia na huko alijifungua mtoto

wa kiume kutoka mbinguni . Mtoto huyo alipokuwa mkubwa akawa mfano na chemchem ya

hekima na alifanya mambo mengi ya ajabu.

Bikira

Maya

mama wa

mungu

buddha

Page 29: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

29

Profesa Doane anasema: Wayuropa waliokwenda Komoron kusini mwa India walishangaa

kuwaona wakazi wa eneo hilo wakimuabudu mungu mkombozi waliyemwita (Slivahana) na

jina la baba yake (Tishaga)na kuwa huyo mwana wa mungu alizaliwa na mwanamwali, na

kwamba huyo ndiyo Vishnu mkuu aliyechukua mwili wa kibinadam.

Wachina huamini miungu walioonekana katika miili akiwemo Fohi, Satin Nong, (Wangat) na

wengineo. Wachina wa Kasaki husema kuwa Bikra Maya alichukua mimba ya Buddha

aliyoipata akiwa usingizini na kumzaa kupitia ubavuni mwake kama ishara ya utakatifu

tofauti na wajawazito wengine wanavyowazaa watoto wao.

Pia huhadithia mambo mengi ya ajabu kuhusu kuzaliwa kwa Laokyon enzi za utawala wa

Tonkong miaka 604 kabla ya Kristo.Wanasema kuwa Budha alikuwepo tangu mwanzo

akashuka duniani na kuzaliwa na mwanamwali mweusi lakini mzuri na mwenye mvuto.

Walijenga mahekalu mengi kwa ajili ya kumuabudu ambapo humuabudu kwa madai kuwa ni

mungu aliyejidhihirisha katika mwili.Wanafunzi wake huitwa walimu kutoka mbinguni na

kuamini kuwa makuhani ndio njia kuu ya kupata utakatifu na ukombozi kwa watu wote.

Hujinyenyekeza mbele yake kama muumba na mtengenezaji wa mbingu na ardhi. Vilevile

huamini kuwa mamayake alimzaa kupitia ubavuni akiwa chini ya miti. Ama kuzaliwa kwa

Hauwoki wanakuelezea kama ifuatavyo: Mama yake alikuwa mgumba akamtolea sadaka bwana

ili apate kumuondolea ugumba, kisha akafuata nyayo za bwana na hapo akachukuliwa kwenye

eneo tukufu akachukua mimba na akajitenga na watu na kumzaa kama mwanakondoo na

kumwita Hauwoki na wakati wa kuzaa hakuhisi machungu ya mimba na hili linaonyesha

uumbwaji wake wa ajabu.

Mungu alimhurumia na kuitazama sadaka yake safi akaikubali na akamzaa mwanaye kwa

urahisi. Kila mtoto azaliwaye na bikra humwita mtoto wa mbinguni ambapo katika lugha ya

kichina humwita Tiyansh.

Wamisri husema kuwa: Horus mkombozi alizaliwa na mwanamwali Isis na kwamba ni mzawa

wa pili wa Ammon. Huchora akiwa mikononi au juu ya mapaja ya mama yake.

Profesa Chamblion ametafsiri yafuatayo kutoka katika maandishi ya kihiroglifu ya zamani:

“Wewe ndiwe mungu mlipa kisasi na mwana wa mungu. Ni wewe Horus mlipa kisasi, wewe

ndiye aliye kutangaza Osiris kwamba utazaliwa na mungu Isis”. Kadhalika Wamisri husema

kuwa mungu Ra alizaliwa kupitia ubavuni mwa mama yake na sio kama wazaliwavyo watu

wengine. Kwenye kuta za hekalu moja huko Tibani kuna picha inayomuonyesha mungu, Tut

mjumbe wa mungu akisema: Malkia bikra Mutemus atamzaa mwana aliye mungu atakaye kuwa

mfalme Omonotov. Walikuwa wakieleza kuwa wafalme wao ni miungu. Vile vile miongoni

mwa wafalme wao kuna waliodai Uungu. Katika kumuelezea Zoroster mtume wa Waajemi

husema kuwa: ametokana na nuru ya mungu sio kama wanavyoumbwa watu wengine.

Aliumbwa bila uchafu yaani mama yake hakuguswa na mwanaume. Plato naye anasema:

Waabudu moto wa Uajemi humwita kwamba ni mwana wa mungu.

Tunashangaa kuona Wayunan walikuwa wakiwaita mashujaa wao hapo zamani kuwa ni

miungu au watoto wa miungu na kwamba walijidhihirisha katika mwili wa kibinadam na baada

ya kufariki waliungana na miungu. Walikuwa wakiwatolea sadaka za kuteketezwa, kuwaabudu

pamoja na mabo mengine. Miongoni mwa watoto wa mungu ni Hercules mwana wa mungu

Jupita aliyezaliwa kwa mwanake wa asili ya Jupita (Kamini) Malkia wa Tibas. Zous Mungu wa

Page 30: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

30

miungu anasema kuhusu Hercules: Ni mtoto wake, vilevile akasema leo atazaliwa kwetu mtoto

wa kiume mjukuu wa Prisius atakuwa na nguvu zaidi kuliko watu wengine wote.

Wanaamini pia kuwa Bucchus ni mtoto wa mungu Jupita aliyezaliwa kwa

mwanamke wa kibinadam aitwaye Semele binti wa Kedamus mfalme wa

Tipas, na kwamba aliwahi kusema: Mimi ndiye Bucchus mtoto wa

mungu Zous niliyezaliwa na Semele mwana wa Kedamus niliyekuja

katika nchi ya Tipas. Niliumbwa kwa nuru ya umeme wa radi na

kuchukua mwili wa binadam badala ya mwili wa kimungu. Nimefika

kwenye chemchem ya Dirus na maji ya Isminus.

Mambo hayo pia yanaelezwa kuhusu Amvion mwana wa mungu Jupita

aliyezaliwa kwa mama wa kibinadam Athiub binti wa mfalme Nistius wa

Boataya.

Wanadai kuwa Prumisius (jina hili ni la kiyunan lenye maana ya jicho na

ulinzi wa mungu) ni mungu ambaye Uungu na ubinadam wake viliungana akawa

na maumbile mawili ya uungu na ubinadam katika mwili mmoja ambapo ni

binadam na mungu wa kweli kwa wakati mmoja. Na Pirisius mtoto wa Jupita

aliyezaliwa na bikira Danya mwana wa Krisius mfalme wa Argos walimuabudu wakasema kuwa

ni mungu wakamjengea hekalu katika Athena ambalo lilitumika kwa ajili ya kuabudu.

Wanasema tena kuwa Mercury ni mtoto wa Jupita aliyezaliwa na mama Atlas mwenye asili ya

kibinadam. Husemekana kuwa Silinne huko Arkadia ndipo alipozaliwa na kulelewa na ndipo

lilipojengwa hekalu kubwa kwa ajili ya kumuabudu. Pia wanaamini kuwa Yulus mfalme wa

visiwa vya Libare Sysilia ndiye mwana wa Mungu Jupita aliyezaliwa na Avasta mama mwenye

asili ya kibinadamu.

Na wanasema kuwa Apollo ni mwana wa Mungu Jupita aliyezaliwa na mama mwenye asili ya

kibinadamu aitwaye Latuna. Na Waovis husema kuwa alizaliwa chini ya mti kama wasemavyo

wafuasi wa Budha juu ya Budha na Lao, kuwa Latuna mama yake alikaa chini ya kivuli cha

mzaituni na na kumzaa. Alipomzaa miungu katika Olimpios walifurahi na mbingu ikatabasamu

na kucheka.

Walikuwa wakimuita Artos kuwa ni mwana wa Jupita aliyezaliwa na mwanamke mwenye asili

ya kibinadamu, wakasema vilevile kuwa Aroclos ni mwana wa Jupita aliyezaliwa na mama

mwenye asili ya kibinaadamu. Kuna majina mengine mengi ya wale waliodai kuwa ni wana wa

Jupita waliozaliwa na wanawake wenye asili ya kibinaadamu. Tumeacha kuwataja kwa lengo la

kufupisha.

Ni mambo yaliyowazi kuwa Wayunani na Warumi walikuwa wakibudu miungu na watoto wengi

wa miunmgu ambapo maombi yafuatayo ya Arfius kwa Jupita yandhihirisha hilo: “Wewe

ndiwe muweza,wa kwanza na wa mwisho.Wewe ndiwe Mungu Jupita mpaji wa kila kitu, na

mwanzilishi wa ardhi na mbingu yenye nyota”.

Naye Doane anasema: “Warumi walikuwa wakiwaita wafalme wao kuwa ni miungu,

wakiwaabudu na kuwafanyia masanamu”.

Yafuatayo ni majina ya wafalme wa Kirumi waliofanywa kuwa miungu:

Confucius

Page 31: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

31

Mmmoja wapo ni Romulus mwasisi wa taifa la Roma wanayemuita kuwa ni “mwana wa

Mungu” aliyezaliwa na mwanamke bikra aliyeitwa Rasilvia. Na wanasema kuwa Kaisari Yulius

ni mwan wa Mungu.

Vilevile wanasema kuwa Kaisari Augastos ni mwanadamu na ni Mungu. Habari za uungu wake

zimeelezwa katika ushairi wa Virgil ambapo anasema kuwa ni mwana wa Jupita.Walimjengea

mahekalu kwa ajili ya kumuabudu ikiwa ni pamoja na kuwateua wakuu na viongozi wa hayo

mahekalu ili wapate kumuabudu ndani yake. Vilevile walimfanya Clorius kuwa Mungu, na

walikuwa wakiwaita wafalme wa Kirumi kwa majina yafuatayo “Mola wetu, Mwalimu, Bwana

wetu na Mungu wetu”.

Walimzungumzia Alexander Mmacedonia aliyezaliwa miaka 356 kabla ya Kristo, kuwa ni

Mungu wa dunia na mwana wa Jupita aliyezaliwa na mama mweye asili ya kibinaadamu aitwaye

Olimpias. Siku moja alitembelea katika hekalu la Jupita Ammon lililojengwa katikati ya jangwa

la Lipian na huko akasikia sauti ikimwita: “Wewe ni mwana wa Mungu” na tangu hapo akawa

anapitisha amri na hukumu na mengineyo kama ifuatavyo: “Alexander mwana wa Jupita

Ammon”. Vilevile Socrates amemtaja Alexander katika shairi lake kuwa ni Mungu na ni mwana

wa Mungu Jupita. Na Ptolemy - ambaye ni mmoja wa viongozi (wa kijeshi) aliyekuwa pamoja

na Alexander – walimfanya kuwa ni Mungu. Mtu huyu alipata kuitawala Misri baada ya kifo

cha Alexander80

ambapo raia wake walikuwa wakimuita kuwa ni “Ptolemy mkombozi”. Neno

Soter ambalo huitwa kwalo lina maana ya “Mkombozi”.

Wanasema kuhusu Sirus mfalme wa Uajemi kuwa ana asili ya kimungu, na kusema kuwa ni

Masihi au Mungu aliyepakwa mafuta.

Wanasema pia kuwa Plato ni mwana wa Mungu. Alizaliwa katika Athena mwaka wa 429 kabla

ya Masihi Issa (a.s.) na kuamini kuwa alizaliwa na mwanamke bikra, msafi na mtakatifu, na

kwamba Izis ambaye hudaiwa kuwa ndiye baba yake aliweka nadhiri kwa ndoto aliyoiona kuwa

hatamkurubia,wala kumgusa mpaka atakapojifungua, kwa kuwa amechukua mimba ya Mungu

Apollo.

Na mama wa Apollonius alisema kuwa alimuona mmoja wa miungu akimwambia kuwa

atazaliwa kwake na baada ya siku kadhaa kupita alimzaa, na pindi alipokuwa mkubwa aliweza

kuwa miongoni mwa walimu wakubwa ambao walionyesha maajabu na miujiza. Alizaliwa

miaka 40 kabla ya Masihi (a.s).

Wanadai kuwa Phethagorus ni mungu, na kwamba mama yake alichukua mimba kupitia maono,

na hayo maono ni Roho Mtakatifu, na baba yake huitwa kwa jina hilo tu, na kuwa aliambiwa

kwamba mkewe atazaa mwana atakayewanufaisha watu.

Wanaamini pia kuwa Iscolapius mwenye nguvu, miujiza na maajabu ni mwana wa Mungu

aliyezaliwa kwa mama mweye asili ya kibinadamu aitwaye coronius.Wamiscion walipowauliza

wakuu wa makuhani kuhusu muda, mahali atakapozaliwa na jina la baba yake, wakawajibu:

Mungu ndiye baba yake, na mama yake mweye asili ya kibinaadamu ni Coronius, na atazaliwa

katika mji wa Abidus.

80 Alexander the great (356 – 324 B.C) alizaliwa katika mji wa Macedonia na kufia katika mji wa Babel. Alikuwa

mwanafunzi wa Arestote. Alishika madaraka baada ya baba yake Philip na kuishinda Uajemi na kufika kwenye mto

Sind

Page 32: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

32

Wakazi wa Roma waliamini uungu wa Simon Msaamari ajulikanaye kama “Magos” au

“Mchawi”, aliyeishi wakati wa Masihi (a.s).Walidai kuwa alitenda miujiza na maajabu ya

kushangaza, na picha yake wakaiweka pamoja na picha za miungu wengine zilizopatikana katika

mji ule. Mwanahistoria Yucipius amemnukuu marehemu Justin kuwa Warumi walikuwa

wakiuamini uungu wa Simon Mchawi, na juu ya daraja lililopo kwenye mto wa Tibris kuna

maneno yafuatayo “Simon Mungu Mtukufu”.

Wakazi wa mataifa ya kaskazini mwa Ulaya kama vile Wanorway, Waholland na wengineo

walikuwa wakiwasifu mashujaa wao kwa uungu, na kwamba wao ni watoto wa Mungu

Odin.Vilevile waliwapa washairi sifa za uungu.

Wanasema kuwa Tour ndiye mwana wa kwanza wa Mungu Odin. Na kuhusu Badora walikuwa

wakisema kuwa ni : “mwema, mkombozi, mwana wa Mungu Odin, na mama yake ni Mungu

Wafrige.

Nao wakazi wa Mexico, vizazi vingi kabla ya ujio wa Colombus, 81

walikuwa wakimuabudu

mungu mkombozi aitwaye “Quetzalcoatl” aliyezaliwa na mwanamke bikra na mtakatifu.

Walikuwa wakidai kwamba mjumbe kutoka mbinguni alikuja na kumpa habari mama yake kuwa

atachukua mimba pasipo kulala na mwanamme, na jina la mama yake ni “Bikra Hoishiqthral

malkia wa mbinguni”. Na wanasema kuwa alimzaa katika nchi ya Nola". Nao jamii ya Mayayo

Gatan wa Amerika huamini kuwa “Dhama” ndiye Mungu Ganishahan.

Wamiotisko wa Columbia wanamuamini mungu aitwaye Boshiga, mwana wa Baba Mkuu.

Nao wakazi wa Nikazako wanaye mungu aitwaye Soma Toyo, ambapo husema kuwa alimtuma

duniani mwanaye Thyobatlahi aliyewafundisha na kuwaongoza njia ya uongofu.

Wakazi wa Peru 82

wanaliabudu jua, na kusema kuwa mungu huyo alipoona ouvu wa watu

unakithiri alimtuma mwanaye aitwaye Malko ili awaelimishe na kuwaongoza njia iliyo sawa

sawa.

Waadios wa Clifarnia wanasema kuwa Muumba Mkuu Niparaga alimtuma mwanaye aje duniani

kuwaongoza Wahindu na kuwafundisha dini. Kwa sababu ya chuki, akauawa na maadui.

Wanamuabudu kwa hoja kwamba ndiye anayestahiki kuabudiwa na kutukuzwa, na ndiye

mpatanishi kati ya wakazi wa ardhini na mungu Niparaga.

Wairoquois wanamuabudu mungu aitwaye Itharangwagan ambaye kwa upande mmoja

wanamchulia kama binadamu na upande mwingine kuwa ni mungu aliyejidhihirisha katika

mwili wa kibinaadam kisha akawaanzishia serikali yao. Husema pia kuwa ni Roho Mkuu.

Waagbobo ambao ni miongoni mwa Wahindu wa Amerika humuamini mungu aitwaye

Michabweh aliyejidhihirisha katika mwili wa binaadamu, na kwamba yeye ndiye mwana wa

pekee wa mungu wa mbinguni. Husema kuwa alizaliwa na mama mwenye asili ya

81 Chritopher Colomb: alizaliwa Janwa Italia na kufia Hispania, aliigundua Amerika mwaka 1492 82 Jamhuri ya Peru, iko katika bara la Amerika ya kusini, ikipakana na Brazil na Bolivia kwa upande wa mashariki,

Ecuador na Colombia kwa upande wa kaskazini, ambapo inapakana pia na Chile kwa upande wa kusini, na ikiwa

karibu kabisa na bahari ya Pacific, na mji wake mkuu ni Lima

Page 33: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

33

kibinaadamu.Wanamheshimu sana huyu mungu aliyejifanyia mwili na kusema kuwa ni

“mkombozi wa watu”.

Wapagani wana miungu mingi iliojidhihirisha kwa mwili, tofauti na hao tuliowataja. Anayetaka

kuwafahamu arejee katika vitabu tulivyovitaja.

BIKRA MARIAM MAMA WA MUNGU YESU KRISTO

Ama mtazamo wa Wakristo kuhusu bikra Mariam kuwa mama wa Mungu, ni kama mtazamo wa

wapagani juu ya mama wa miungu. Jambo hili ni mashuhuri sana kwani hufikia hata kumuimbia,

kumtukuza na kujinyenyekeza kwake katika siku maalumu wanazoziita kuwa ni “Siku za

Mariam”. Humuita kuwa ni “Malkia wa Mbinguni, mama wa Mungu aliyejaa neema na mwenye

utukufu na cheo duniani na mbinguni”, pamoja na sifa nyingine nyingi za ukuu na uungu.

Katika Injili ya Luka (chapa ya Christian) msitari wa kwanza kifungu cha 28 kuna maelezo

yafuatayo: “Akaingia nyumbani kwake, akasema, salamu, uliyepewa neema. Bwana yu pamoja

nawe”. Imani ya kwamba ni mama wa Mungu ilipatikana katika kikao cha Afisos mwaka 431

baada ya Kristo.

Bwana Doane ameeleza kwa ufupi yafuatayo: “kama tunavyoona wapagani wakiwa na mama wa

miungu wakiwatukuza na kuwapa majina ya ukuu, vilevile tunaona kuwa Wakristo wana mama

wa Mungu wanayemtukuza na kumpa majina kama yale ambayo Wapagani huwapa mama wa

miungu yao. Hayo yanaungwa mkono na picha wanazozichora zikimuonyesha akiwa amemlea

mwanaye kristo, kwani zinafanana moja kwa moja na picha wanazozichora wapagani kuhusu

mama wa miungu wao” 83

Umeona picha na michoro kadhaa ambayo unaweza kuilinganisha na ile inayopatikana siku hizi

kwa Wakristo na ujaribu kuangalia kipindi kirefu kilichopita baina ya miungu wa kipagani, kama

vile Budha, Krishna na wengine, na baina ya Yesu Mungu wa Wakristo. Na Wachina huiweka

picha ya mungu wao “Shinmo” katika mahali pazuri katika nyumba zao na kuifunika kwa

kitambaa cha hariri. Pia mahekalu mengi yamejengwa kwa jina lake likiwemo hekalu la “mama

wa Mungu Mtsubo” kama wafanyavyo Wakristo kuhusu picha za Mariam na kujenga mahekalu

kwa jina lake kama vile “kanisa la Mtakatifu” na “kanisa la Bikira”.

Wamisri wa zamani walikuwa wakimuita mama wa mungu Isis, au mama wa mwokozi

Horus kwa majina mengi kama vile, MTAKATIFU, MALKIA WA MBINGU, NYOTA YA

BAHARINI, MAMA WA MUNGU, MUOMBEZI, BIKIRA, n.k. na kumchora akiwa

amesimama juu ya mwezi na kuzungukwa na nyota kumi, kama Wakristo wanavyomchora

Mariam akiwa amesimama mwezini akizungukwa na nyota kumi na mbili. Isipokuwa picha za

mama wa miungu ya kipagani zilikuwapo kwa kipindi cha karne nyingi kabla ya zile za Mariam.

Zingatia!!

Mtakatifu Abifanius, akielezea kuhusu Imani ya Wamisri juu ya Bikira aliyetajwa kuwa mama

wa Mungu, anasema “Hapana shaka kuwa walifunuliwa tangu kale kuhusu Bikira na mimba

yake” 84

83 Doane, 336 – 338 84 Egyptian Belief, uk. 143

Page 34: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

34

Bonwick anasema: “ katika kitabu cha zamani cha Wakristo kiitwacho “kitabu cha habari za

Alexandria” kuna maelezo yafuatayo: “Tazameni namna Wamisri wanavyochora picha za kuzaa

kwa Bikira na Mwanaye”, na haya ndiyo yasemwayo na Wakristo kuhusu kuzaliwa kwa Masihi,

pamoja na kwamba kipindi kilichopita baina ya simulizi hizi mbili ni kirefu sana.

Na sikukuu ya kuingia kwa Kristo hekaluni na kumtakasa mwanamke mtakatifu, ambayo

hufanyika Februari 2 ya kila mwaka, asili yake ni Misri. Wamisri walikuwa wakiisherehekea

kwa heshima na kumtukuza Bikira Naith, na siku hiyohiyo Wakristo nao pia husherehekea.

Wakazi wa Babeli na Ashori, walikuwa wakimuabudu mwanamke bikira wakidai kuwa ni

mama wa mungu na wakamchora akiwa amemlea mwanaye kama ilivyo kwa Wakristo. Jina la

huyo mwanamke ni MILITA, na jina la mwanaye mwokozi ni TAMUZ ambaye pia huitwa kuwa

ni Mpatanishi na Mkombozi. Katika kisiwa cha Cyprus kulikuwa na hekalu lililojulikana kama

“HEKALU LA BIKIRA MILITA” ambalo ndilo lililokuwa hekalu kubwa katika enzi za utawala

wa Wayunan.

Wayahudi nao pia walitumbukia katika dimbwi la bahari ya upagani, wakafikia hatua ya

kuabudu jua, mwezi na nyota, na wakawatoa binaadamu kama sadaka ya miungu hao. Miongoni

mwa miungu waliowaabudu ni mwanamke bikira waliyemuita kuwa ni MALKIA WA

MBINGUNI kama ilivyoelezwa katika kitabu cha Yeremia sura ya 44 msitari wa 16 – 19.

Wayahudi walimwambia Yeremia: “neno lile ulilotuambia kwa jina la BWANA, sisi

hatutakusikiliza. Lakini bila shaka tutalitimiza kila neno lililotoka katika vinywa vyetu,

kumfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, kama

tulivyotenda sisi, na baba zetu, na wafalme wetu, na wakuu wetu, katika miji ya Yuda, na katika

njia kuu za Yerusalemu; maana wakati huo tulikuwa na chakula tele, na kufanikiwa, wala

hatukuona mabaya. Lakini tulipoacha kumfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia

sadaka za kinywaji, tumepungukiwa na na vitu vyote; na kuangamizwa kwa upanga, na kwa

njaa. Nasi tulipomfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, Je!

Tulimfanyizia mikate, ili kumwabudu, na kummiminia mamiminiko, waume zetu

wasipokuwapo?”

Na yale yaliyoelezwa na Warumi kuhusu MARHA mama wa mungu Bacchus yanafanana moja

kwa moja na yaliyoelezwa katika Injili ya Mathayo sura ya kwanza msitari wa 18 mpaka 24,85

ambapo mtakatifu Jerome ametafsiri jina la MARHA kwamba ni MARIAM. Na walikuwa

wakimuita kuwa ni MUNGU WA BAHARI, ambapo sasa wanamuita Mariam mama wa Yesu

kuwa ni NYOTA YA BAHARI.

85 Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla

hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye Yusufu, mumewe, kwa vile

alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri. Basi alivyokuwa akifikiri hayo,

tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua

Mariamu mkeo, maana mamba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao. Hayo yote yamekuwa, ili litimie neon

lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema, Tazama, bikira atachukua mimba, naye atazaa mwana; nao

watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu Pamoja nasi.

Naye Yusufu alipoamka katika usingizi, alifanya kama malaika wa Bwana alivyomwagiza; akamchukua mkewe;

asimjue kamwe hata alipomzaa mwanawe; akamwita jina lake YESU”

Page 35: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

35

Wayunan walikuwa wakimuita mama mtakatifu wa mungu Juno kuwa ni MALKIA WA

MBINGUNI, na kumuabudu kwa imani kuwa ni mlinzi wa wanawake tangu kuzaliwa mpaka

kufa, kama ilivyo imani ya Wakristo wa leo kwa Bkira Mariam.

Page 36: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

36

SURA YA TANO

NYOTA ZA MASHARIKI ZILIZOONEKANA KWA KUZALIWA MIUNGU

Na zikawaonyesha Majusi na Makuhani mahali walipozaliwa, na hatimaye wakaja kuwasujudia

miungu watu waliozaliwa na bikira aliyejaa neema

I – WAPAGANI:

Bwana Bunsen anasema: “imeelezwa katika vitabu vitakatifu vya kibudha kuwa mbingu zilitoa

bishara ya kuzaliwa Budha kutokana na nyota iliyoonekana upande wa mshariki ya anga. Katika

vitabu hivyo nyota hiyo imeitwa kuwa ni NYOTA YA MASIHI”86

Bwana Beal anasema: Amesema Fobinhang kuwa wakati alipojidhihirisha Budhitsu kituo cha

nyota ya Liwaa kilikuwa katika hali ya kukutana na jua, na katika vitabu vyao huwaita

wanafalsafa hao kuwa ni “Watakatifu wa Masihi”, nao ni wale waliotambua kuzaliwa kwa

Masihi Budha kupitia ishara za mbinguni. Na imeelezwa katika moja ya vitabu vyao vitakatifu

vya Wahidu kiitwacho RAMYANA kuwa Rama alizaliwa tarehe tisa ya mwezi wa Kitra katika

kipindi ambacho sayari ya Jupita ilikuwa katika nyota ya kaa (Rama ndiye Vishnu aliye katika

mwili)87

Alipozaliwa Krishna, nyota zilidhihiri mbinguni na Naridu mnajimu mkuu alizithibitisha.

Mazazi ya miungu wote waliojionyesha katika miili ya kibinaadamu yalijulishwa na nyota.

Anasema Thorten: “Wachina huamini kuwa wakati alipozaliwa YU, nyota ilidhiri kama ishara

ya tukio hilo. Na YU aliyetajwa ndiye aliyeasisi dola ya kwanza iliyotawala China. Pia

wanasema kuwa wakati wa kuzaliwa Mwanafalsafa LAO-TSEU ilionekana nyota kama ishara ya

kuzaliwa kwake”88

Warumi walikuwa wakiamini kuwa wakati wa kuzaliwa makaisari nyota hudhihiri – kama

wasemavyo Wayunani.Vilevile walikuwa wakisema kuwa wakati wa kifo cha mmoja wa

makaisari, nyota hupoteza nuru yake. Mwanahistoria wa Kirumi Tsitus anasema: “ ilidhihiri

nyota yenye mkia. Na hii inaelezea yale yasemwayo na watu juu ya kubadilika kwa watawala na

kuanguka kwa wafalme. Kudhiri kwa nyota iliyodhaniwa na watu kuwa ni sababu ya

kunganguka kwa utawala wa Niro ni jambo lisilokuwa na mjadala, kwani walianza kuulizana

kuhusu atakayeshika mahala pake”.

Anasema profesa Amberly: “ Katika zama za utawala wa Hadriyan alitokea mtu miaka mia moja

baada ya Masihi(a.s.) aliyedai kuwa ni mtoto wa Kristo na kuwavuta watu wengi wa jamii yake,

akayaongoza majeshi na kumpindua mfalme wa Rumi katika uasi huo, na akajiita kuwa ni

MTOTO WA NYOTA”89

Hakuna shaka kuwa ishara hii ya nyota vilevile ilienea mpaka Amerika, kwa sababu ilikuwa

ndiyo alama ya kuja mwokozi Quetzalcoatl aliyezaliwa na mwanamke bikira.

86 The Angel Messiah, ukurasa wa 22, 23 na 33 87 The History of Buddhism, ukurasa wa 23 na 33 88 The Chinese, juzuu ya 1, ukurasa 173 89 Analysis of religious belief, ukurasa 227

Page 37: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

37

Kasisi Dr. Geiekic anasema: Imani ya kutokea matukio ya ajabu ilikuwa imeenea sana, hasa

wakati wa kuzaliwa au kufa kwa mmoja wa watu wakubwa kulikokuwa kukielezewa kwa

kudhihiri nyota (ya kawaida) au yenye mkia au baadhi ya sayari kuungana.90

Inaelezwa kuwa Zoroaster alisema kuwa nyakati za mwisho mwanamke bikira atachukua mimba

ya mtoto wa kiume.Wakati wa kumzaa itadhihiri nyota katika majira ya robo ya mchana

itakayoonekana sana kutokana na ukali wa nuru yake.

* * *

II- Wakristo:

NYOTA ILIYONEKANA UPANDE WA MASHARIKI WAKATI ALIPOZALIWA YESU

KRISTO.

Hapo awali tumeona kile wanachokiamini wapagani kuhusu kuchomoza nyota upande wa

mashariki , ambayo iliwaonyesha makuhani mahali walipokuwa wamezaliwa wana wa miungu

yao. Halikadhalika Majusi walionyeshwa mahali alipozaliwa Yesu Kristo kupitia nyota

wanayodai kuwa ilionekana wakati wa kuzaliwa kwake. Hata hivyo hatujui ikiwa hiyo nyota

ndiyo ileile iliyowaonyesha makuhani mahali walipozaliwa watoto wa miungu tuliowataja au ni

nyingine.Vilevile hatujui ikiwa hiyo nyota ni miongoni mwa jamii ya hizi zilizoenea angani

zikiwa mbali nasi kwa mamilioni ya maili, na ambazo ni kubwa mara kadha kuliko hii dunia, au

ni nyota tofauti iliyoumbwa kwa lengo hili la kuonyesha mahali walipozaliwa miungu. Ilikuwa

umbali gani kutoka ardhini? Na je, kwanini haikutokea mkanganyiko katika nguvu ya mvutano

kwa sababu ya kushuka nyota hii? Lile tunalolijua sisi ni kwamba, Wapagani walikuwa na uhuru

wa moja kwa moja katika kuunda madai na imani potofu zinazowapendeza.

Tunasoma katika Injili ya Mathayo, sura ya pili, msitari wa kwanza na wa pili kuwa: “Yesu

alipozaliwa katika Bethelehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa

mashariki walifika Yerusalemu, wakisema, yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi?

Kwa maana tuliona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia”.

90 Life of Christ, juzuu ya 1, ukurasa 144

Page 38: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

38

SURA YA SITA

MAJESHI YA MBINGUNI YALIMTUKUZA MUNGU KWA KUZALIWA MIUNGU

I-Wapagani:

Katika kitabu cha Vishnu Purana kuna maelezo yafuatayo: Bikira Devaki alipochukua mimba ya

mwokozi wa ulimwengu, alitukuzwa na miungu. Alipomzaa, furaha ilienea, nuru ikaangaza

ulimwenguni kote na miungu wa mbinguni waikaimba na roho zikaghani. Alipozaliwa

MKOMBOZI WA WATU WOTE mawingu yalianza kuimba kwa sauti za vinanda na maua

yakadondoka”.

Maneno kama haya huyatoa kuhusu kuzaliwa kwa Budha, na kwamba wakazi wa ardhini

walisikia sauti na ghani za vinanda, mbingu ikanyesha maua na manukato, upepo mwanana

ukavuma na nuru ya ajabu ikaangaza.

Bwana Fonbihang anasema: Roho walimzunguka Bikira Maya na mwanaye mwokozi wakaanza

kumtukuza Mungu wa pekee na kuimba “utukuzwe ewe Malkia Maya, furahi na ushangilie,

kwani mwana uliyemzaa ni mtukufu”. Reshi na Devasi waishio duniani walinadi kwa furaha

kubwa wakisema “Leo amezaliwa Buddha ili kuwapa watu heri na kuondoa ujinga wao”.

Wafalme wa mbingu ya nne nao wakanadi: Sasa amezaliwa Budhistu atakayeupa ulimwengu

raha na furaha”. Kisha akasema: miungu wa mbinguni walikusanyika na kuimba: “Leo

amezaliwa Budhistu katika dunia ili awape watu furaha na amani, aangaze katika kiza na kumpa

kipofu macho”.

Anasema Sir Jones Francis Davis: Wachina husema kuwa, kabla ya kuzaliwa Konfocius,

mwanafalsafa mashuri wa kichina, alama kadhaa zilionekana kutoka mbinguni. Katika jioni ya

kuzaliwa kwake sauti ya vinanda kutoka mbinguni ilisikika masikioni mwa mama yake, na

alipozaliwa, maandishi yafuatayo yalionekana kifuani mwake: MTUNGAJI WA SHERIA

ZITAKAZOIREKEBISHA DUNIA

Naye Prichard anasema: alipozaliwa Osiris mkombozi, sauti ilisikika ikinadi “AMEZALIWA

MTAWALA WA DUNIA 91

Bwana Bonwick naye pia anasema: Wamisri wa zamani wanasema kuwa, pindi Osiris

alipozaliwa, ilisikika sauti ikinadi kuwa AMEZALIWA MUNGU WETU AITWAYE OSIRIS”92

Wengine husema kuwa, mwanamke mmoja alipokuwa akienda kuchukua maji kwa ajili ya

hekalu la Ammon lililopo katika mji wa Tipis, alisikia sauti hii ikimuamuru kunadi kwa sauti ya

juu maneno yafuatayo: “ATAZALIWA MUNGU OSIRIS”.

Alipozaliwa Apolonius mwana wa Mungu, furaha ilienea. Flafius Filostratus, mwandishi wa

maisha ya mtu huyu wa ajabu, anasema kuwa kundi la bata-mzinga walimzunguka mama yake

na kuanza kuimba kwa pamoja kwa sauti tamu na upepo mwanana ukavuma”.

Alipozaliwa Apollo kwa Bikira Latona katika visiwa vya Dilus, miungu wa Olimpos walifurahi

sana, ardhi ikatabasamu na mbingu ikacheka. Na alipozaliwa Heraclus mtoto wa mkombozi,

91 Analysis of the Historical Records of Ancient Egypt, ukurasa wa 56 92 Egyptian Belief, ukurasa wa 325

Page 39: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

39

baba yake, Mungu Mkuu Zius alinadi kutoka mbinguni na kusema, LEO ATAZALIWA MWANA

KUTOKA KATIKA UKOO WA PRISIUS NA ATAKUWA NA NGUVU KULIKO WATU WOTE”.

Na Iskolapius alipokuwa mtoto na wakataka kmuua, walisikia sauti ya Mungu Apollo ikisema:

Msimuuwe mtoto pamoja na mama yake kwani ni mtoto atakayefanya mambo makuu, bali

mpelekeni kwa mtakatifu Santor Shrun na mwambieni amfundishe katika hekima, na ushujaa

wake ili watu wapate kunitukuza katika vizazi vijavyo”.

II-Wakristo:

MAJESHI YALIYOONEKANA MBINGUNI WAKATI WA KUZALIWA YESU KRISTO

Tumeona yaliyosemwa na Wapagani wa zamani kuhusu kudhihiri kwa majeshi ya mbinguni

wakati wa kuzaliwa kwa mmoja wa watoto wa miungu wao.

Wakristo nao walisema hayohayo kuhusu kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Isipokuwa, sisi hatuelewi

ikiwa hayo majeshi ya mbinguni yalikuwa na idadi kubwa wakati walipozaliwa watoto wa

miungu wa kipagani au yalikuwa mengi pindi alipozaliwa mungu wa Wakristo au yalikuwa na

idadi sawa katika nyakati zote? Kwa sababu wanadai kuwa watoto wote wa miungu waliozaliwa

walikuja kuwakomboa kwa damu zao, na tunavyojua ni kwamba hakuna aliyepinga madai hayo.

Huwenda hapo baadaye hali hii ikaongezeka. Sasa soma yafuatayo katika agano jipya.

Injili ya Luka msitari wa pili, kifungu cha 13 na 14: “Mara walikuwapo pamoja na huyo

malaika,w ingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu mungu na kusema, Atukuzwe Mungu juu

mbinguni na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia”.

SURA YA SABA

KUONYESHWA MTOTO WA MUNGU NA KUMKIRIMU KWA ZAWADI

I-Wapagani:

Katika simulizi zinazomhusu Krishna, ni kuwa mtoto wa Mungu aliwekwa kwenye kitanda cha

watoto akiwa baina ya wachunga kondoo ambao ndio waliokuwa wa kwanza kuutambua utukufu

wake mkuu unaoonyesha kuwa ni Mungu, na wakatambua kuwa ndiye mkombozi aliyeahidiwa.

Wa kwanza kumtambua miongoni mwao ni Nanda mchunga –kondoo kisha wenzake na wote

wakammsudia. Nabii wa Kihindu – Naredu – alisikia habari zake, akaenda kuwaona wazazi wa

mtoto huyo katika mji wa Cokol. Baada ya kufanya utafiti wa Kimungu. Wachunga kondoo

alimpa Krishna zawadi.

Pia wanasema kuhusu mtoto Budha mwenye asili ya Kimungu kuwa alipozaliwa alitelewa na

Makuhani ambaowalina ishara Uunguwake na kumwita kuwa ni Mungu Mkuu, na kwamba

alikuja pamoja nao Mtakatifu aitwaye Asiufa aliyekuwa na mvi nyingi ili apate kumuona, mzee

huyo alikuwa hasikii mambo ya dunia bali alikuwa akisikia sauti kutoka mbinguni, ndipo

alipokuwa akisali chini ya mti akasikia wimbo wa Rivas juu ya kuzaliwa Budha.

Page 40: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

40

Bwana Amberly anasema: wanasema kuwa Asita ambayea ni mmoja waa wachamungu

wakubwa, alimtembelea Budha na kutoa Biashara kuhusu utkufu wake wa baadaye, na akalia

kwa sababu ya kuwa ni mzee asiyeweza kuishi sana ilia apate kuishuhudia siku atakayojifunza “

sheria ya wokovu”kutoka kwa huyo mtoto aliyekuja kushuhuidia utukufuna ukuu wake. Alilia

kwa sababu ya uzee ambao ulimfanya asiweze kuona yale yatayotokea, na kwamba “Baha

Kamen (yaani Mungu muweza) ambaye ni Budha alikuja Duniani ili kuikomboa na awafundishe

sheria,” aponye vikongwe, wagojwa, na wenye ulemavu na wafu, na awaokoewale

waliotumbukia katika mtego wa ufisadi wa kimaadili, na awafumbue macho ya kiroho

yaliyopofuka kwa giza la ujinga, na awabebe mamilioni ya watu kwenda ng‟ambo ya bahari, na

aweze kuwapa manufaa ya maisha ya milele. Huyo Mchamungu alilia Na kuhuzunika Sana Kwa

kudhani kuwa asingemuona Budha mwenye ukamilifu, lakini sasa alirejea nyumbani kutoka

mlimani akiwa ni mwenye furaha kwa sababu aliweza kumuona “Mwokozi aliyezaliwa” akiwa

katika hali ya uchanga.

Picha zilipo katika pango la Ajiwanta zinamuonyesha Asita akiwa amemlea Budha, na

kwamba huyu Mchamungu aliutambua uungu wa Budha kupitia ishara zisizokuwa za kawaida.

Na Watakatifu wazamani walimfahamu na kumtukuza, na walipo kufa walikwenda kwa amani

kwa kuwa wamekwisha kumuona. Pia wanasema kuhusu mama wa huyo Mungu kuwa alimzaa

mtoto wake wa pekee bila kupata machungu wala tabu na hayo yanaonyesha kuwa mtoto

aliyezaliwa alikuwa na miujiza.

Mithra, mkombozi wa Waajemi na mpatanishi baina ya Mungu na watu, alipozaliwa

alitemelewa na majusi wakampa zawadi za dhahabu na manukato.

Kwamujibu wa simulizi ya Plato : alipozaliwa Socrates 94

(miaka 469 kabla ya Kristo)

walikuja majusi kutoka mashariki wakampa zawadi za dhahabu na manemane.

Na mkombozi (iskolapius) aliyezaliwa na mwanamke bikira, alilindwa na kondoo dhidi ya

jambo lolote baya, kwani walipomuona walitambua kuwa ni “Mungu”. Habari za mazazi yake ya

maajabu zilienea, watu kutoka kila sehemu walifika ili kumshuhudia na kumsujudia. Na wengi

katika wale waliopewa nusu ya Uungu, kwa Warumi na Wayunami, walilelewa na wachunga

kondoo ambao waliwasujudia.

Miongoni mwao ni Wardmulos aliyekutwa na wachunga – kondoo katika ukingo wa Tiber 95

,

na Parmi motto wa Paryan alilelewa na wachunga kondoo. Ojisos, alitupwa na mama yake,

akaokotwa na wachunga – kondoo wakamlea.

Halikadhalika Iskolapius na wengineo ambao historia imetuhifadhia majina yao.

* * *

II- WAKRISTO:

Hali iliyotokea katika kuwatambua watoto wa Mungu Kama vile Budha, Krishna Na

wengineo, Na zawadi za thamani zilizotolewa Na wachunga kondoo, majisu au wanajimua,

ndinyo ilinyokuwa kwa Yesu Kristo. Katika Injili ya Mathayo sura ya pili msitari wa 1- 11 kuna

maelezo yafuatayo: Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu zamani za Mfalme Herode, tazama,

mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakasema, yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme

wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia…

wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka

Page 41: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

41

wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba

na manemane”.

Maelezo Kama hayo pia yanapatikana katika Injili ya Luka, sura ya pili 96

, isipokuwa yeye

anaeleza kuwa waliyoiona nyota yake ni wachunga-kondoo na sio majusi. Vilevile Injili iitwayo

“ Injili ya Wamisri” inasema kuwa: “waliokuja kumuona na kumpa zawadi ni wachunga-kondoo

na sio majusi.

SURA YA NANE

MAHALI WALIPOZALIWA BAADHI YA MIUNGU WALIOJIDHIHIRISHA KATIKA

MIILI YA KIBINADAMU

I- WAPAGANI:

Krishna alizaliwa Pangoni, na baada ya kuzaliwa aliwekwa katika zizi la kondoo, na

alilelewa na mmoja wa wachunga-kondoo waaminifu.

Hotse mtoto wa Mungu kwa imani ya Wachina, aliachwa namama yake akiwa kichanga,

akazungukwa na ng‟ombe na kondoo wakimlinda sana dhidi ya kila jambo baya. Na Bacchus

mtoto wa Mungu alizaliwa na bikira Semele alizaliwa Pangoni. Inasemekana Kama pia kuwa

alizaliwa sehemu nyingine, Na baada ya kuzaliwa, mama yake alimleta Pangoni.

Phelostratus, mhutubu wa Kiyunani anasema “wakazi wa India wanasema kuwa Bacchus

alizaliwa Nisan a kulelewa katika Pango la mlima Maros.”

Na Iskolapius matoto wa Mungu aliyezaliwa na bikira Kordanis, alipozaliwa aliachwa

amlimani akaokotwa na mchunga - kondoo aliyemlia na kumtunza.

Ropolus mwana wa Mungu aliyezaliwa na bikira Kordanis, alipozaliwa aliachwa mlimani

akaokotwa na mchunga – kondoo aliyemlea na kumtunza .

Romulus mwana wa Mungu alizaliwa na Riyasilvia, aliachwa na mama yake akiwa bado

kichanga katika ukingo wa mto Tibaar, akaokotwa na wachunga – kondoo wakamlia na

kumtunza.

Bwana mwokozi Adoni mara baada ya kuzaliwa aliwekwa katika Pango. Naye Apollo

mwana wa Zeus, mungu mwenye uweza , alizaliwa Pangoni nyakati za asubuhi.

Mithra,mkombozi wa Waajemi,naye alizaliwa pangoni nyakati za asubuhi.Kadhalika Herus

mwana wa Mungu, aliyezaliwa na Bikira Maya,alizaliwa pangoni kwenye mlima wa keliman

wakati wa asubuhi.

Naye Attis,vilevile alizaliwa katika pango.

Page 42: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

42

Wahindu wanasema kuwa Krishna alipozaliwa, umbile la mama yake lilibadilika na kuwa na

uzuri na mvuto usiokuwa na mfano. Nuru kutoka mbinguni ikadhihiri na kuangaza ndani ya

pango, na mashavu ya wazazi wake yakatoa mwangaza wenye nuru.

Vilevile wanasema kuwa alipozaliwa Budha, mkombozi wa ulimwengu, mwili wake

ulizungukwa na nuru kutoka mbinguni ambayo ilikuwa makhsusi kwa ajili yake tu,na hivyo

ndivyo alivyokuja duniani na nuru isiyokuwa na mfano.

Na alipozaliwa Bacchus, nuru yenye kung‟aa ilimzunguka na kuangaaza pangoni.

Naye Apollo alipozaliwa, kitanda chake kilizungukwa na nuru, na majeshi kutoka mbinguni

yakamuosha kwa maji safi na kumtakasa kwa dhahabu.

Mkombozi Iskolapius alipozaliwa, shavu lake liltoa mwanga Kama jua na kuzungukwa na

miale ya moto. Vilevile wanasema kuhusu Zoroaster kuwa alizaliwa pasina uchafu (yaani

mama yake hakulala na mwanaume) bali alichukua mimba kutokana na miale ya nuru ya

Mungu, na alipozaliwa ilidhihiri mwilini mwake nuru iliyoangaza chumba chote na kwamba

alimchekea mama yake.

Wahindu wanasema pia kuwa ulipokaribia muda wa kuzaliwa Krishna, Nanda alikwenda

kwa Mfalme ili kumtoa mali (kodi) akisuhubiana na mama wa Krishna aliyekuwa na mimba,

ndipo machungua yalipo mjia akiwa njiani, akamzalia chini ya mti. Na katika simulizi

nyingine inasemakana kuwa alimzaa akiwa katika nyumba ya kulala wageni.

Naye Laotseu, Mwanafalsafa wa Kichina mama yake akiwa safarini alimzaa chini ya mti.

Na Phethaghorus ambaye alikuwepo miaka 570 kabla ya Roho Mtaktifu, na akamzaa akiwa

safarini pamoja na Baba yake kuelekea Seda kwa ajili ya biashara.

Naye Aapolo, alizaliwa wakati mama yake alipokuwa sfarini. Simulizi za kuzaliwa kwake

zinasema kuwa ulipokaribia muda wa kuzaliwa na mama yake akawa hakupata mahala pa

kujifungulia alimzaa chini ya mti, akajua kuwa mtoto huyo atakuwa mkuu atakayeiongoza

Miungu ya watu. Na Ikolapius Mwana wa Mungu aliyezaliwa na Bikira Koronis, mamayake

alimucha juu yam lima baada ya kumzaa akaokotwa na mchunga – kondoo ambaye alimlea

na kumtunza. Naye Rumulus mama yake alimuacha ukingoni mwa mto Tabar akiwa bado

mchanga akaokotwana wachunga – kondoo wakamlea na kumtunza. Vilevile Bwana Adoni

Mkombozi alizaliwa pangoni.

Apolo Mwana wa Mungu Dhus alizaliwa pangoni nyakati za asubuhi.

Na Mithra, mkombozi wa Waajemi, alizaliwa pangoni nyakati za asubuhi. Pia Hermus

Mwana wa Mungu alizaliwa na Bikira Maya, alizaliwa wakati wa asubuhi katika pango la

mlima Keliman.

Attis naye pia alizaliwa pangoni. Na wengine wengi walizaliwa katika maeneo

mbalimbali, tunatosheka na hao tuliowataja.

* * *

II- MAHALI ALIPOZALIWA YESU KRISTO:

Tumetaja yale yanayozungumzwa na Wapagani kuhusu mahala ilipozaliwa Miungu yao,

kama vile Krishna, Budha na wengineo, na sasa tunataja yale yalioelezwa kuhusu mahala

alipozaliwa Yesu Kristo, Mungu wa Wamishionari, ambao huenda wakakoma kuzuia kuenea

kwa dini ya Kiislam, wakawa wavumilivu katika kuzichunguza imni zao, wakakubali kufuata

yale yaliokuwa bora kwao ili mwisho wao uwe mwema, hata kama waliokuwa kabla yao

wameyafanya.

Page 43: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

43

Katika Injili ya Luka mstari wa pili, kifungu cha 15,16 na 17 kuna maelezo yafuatayo;

Ikawa, malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana,

Haya, na twendeni mapaka Bethlehem, tukalione hilo lililofanyika, alilotujulisha bwana.

Wakaenda Kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala

horini. Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.

Vifungu tulivyo vitaja vinatosha katika kueleza kadhia hii ya kuzaliwa kwa Masihi katika

silsila ya wafalme. Kama ilivyozaliwa Miungu ya Warumi na Wayunami ambao Injili nyingi

zimetoka kwao, na kama ilivyozaliwa miungu ya Mabudha na Wabrahma na wengineo,

ndivyo alivozaliwa Mungu wa Wamishionari, yaani Yesu, madai na ulinganisho ulioje!

Amesma kweli Allah Mtukufu: “Hayapofuki macho bali hupofuka nyoyo zilizopo vifuani”.

SURA YA TISA

MIUNGU ILIYODHIHIRI KATIKA MWILI INATOKANA NA KIZAZI CHA KIFALME.

Wahindu wanaaminimkuwa mkombozi wao Krishna anatokana Na kizazi cha kifalme, na

kwamba alizaliwa katika hali ya unyenyekevu, Na wanahesabu mababu Kwa upande wa

mama yake, ama Kwa upande wa baba yake, alikuwa ni mwana wa Mungu kwa mda wa

vizazi vingi.

Wanasema kuwa Budha anatokana na kizazi cha kifalme katika nyumba ya Soqya,

ambayo ndiyo kizazi mashuhuri sana cha Wabrahma ambao walikuwa ndio watu wale wa

India. Na wanasema kwamba babu yake wa kwanza, ambaye ni Samatha ndie wa kwanza

kuitawala India na Dunia, na Rama ambayendiye Vishnu katika mwili, alikuwa katika kizazi

cha kifalme.

Na Foni mwana wa Mungu aliyezaliwa na Bikira anatokana na familia ya Kifalme

iliyotawala China katika karne nyingi ziizota.

Wachina wanasema kuwa Confocius anatokana na familia ya kifalme. Na wanawahesabu

babu zake Kama wanavyowahesabu mababu wa wafalme Hwatsaki, ambaye alikuwa mfalme

wa China tangu miaka elfu moja.

Naye Horus mkombozi wa Wamisri aliyezaliwa na mwanamwali, alitokana na kizazi cha

kifalme, na vilevile wanamwita kuwa ni “mchungaji mwema”.

Heraclus Mwana wa Mungu alitoka katika ka familia ya kifalme.

Naye Yosius mwana wa Bikira Danya aliyetoka katika familia ya kifalme.

Na Iskolapius mwana wa Mungu mwenye ishara miujiza alitokana na kizazicha kifalme.

Na kuna wengine wengi katika wale wanaodaiwa na Wapagani kuwa ni watoto wa Miungu

yao, na wote wanatokana na kizazi cha kifalme, na mifano tuliyoitoa inatosha.

* * *

IMANI YA WAKRISTO KWAMBA MUNGU KRISTO ANATOKA KATIKA KIZAZI

CHA KIFALME.

Nyumati za kipagani zilizotangulia zilidai kuwa watoto wa Miungu yao inatokana na kizazi

cha kiflme kama tulivyokwishaeleza. Vivyo hivyo Wakristo nao walisema kuwa Yesu kristo

anatokana na kizazi cha kifalme, na wanaipeleka nasaba yake mpaka kwa Mfalme Daud,

kama ilivyoeleza katika Injili ya Mathayo mstari wa kwanza 97

, na Injili ya Luka sura ya

Page 44: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

44

kwanza 98

. Na hivi vifungu vingi vilivyomo ndani ya Injili ambavyo humo ameitwa kuwa ni

“Mwana wa Daudi” hata mashetani walikuwa wakimwita “Mwana wa Daudi”, mojawapo ya

vifungu hivyo ni kutoka katika Injili ya Mathayo mstari wa 22 kifungu cha 41 na 42

kinasema: Na Mafalisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akasema, mwaonaje katika

habari za Kristo? Ni mwana wa nani? Wakaamwambia, ni mwana wa Daudi.

SURA YA KUMI

IMANI YA WAPAGANI, KUHUSU WAFALME WALIOTAKA KUIANGAMIZA

MIUNGU NA JINSI ILIVYOOKOKA DHIDI YA MIKONO YA WAUAJI.

I.WAPAGANI:

Bwana Jocott gangooly ambaye ni mpagani aliyeingia katika Ukristo huko India anasema:

“wapagani wa Kihindu wanaamini kuwa Krishna alipozaliwa walisikia sauti ikinadi kutoka

mbinguni na kumwambia mlezi wake, simama, mchukue mtoto ukimbie naye na uvuke mto

Jomata. Akafanya Kama alivyoamriwa, Kwa sababu Mfalme Qanis alikuwa amekusudia

kumuua mtoto huyo mkombozi wa ulimwengu. Ambapo mfalme huyo alituma ujumbe

kutoka katika utawala wake ili kumuangamiza mtoto huyo 99

”.

Akasema bwana Higgins : Wapagani wa Kihindu huamini kuwa alipozaliwa Krishna

walimchukua usiku na kukimbia naye katika nchi ya mbali kwa kumhufia Mfalme Dhalimu,

ambaye ilisemakana kuwa Krishna angekuwa chanzo cha kuanguka kwake pindi atakapo

kuwa kijana, hivyo Mfalme aliamuru kuuawa watoto wote wa kiume waliozaliwa katika nchi

yake.

Maelezo kama hayo pia yalitolewa na Sir William au Jones na wengineo, ambapo katika

utenzi wa ushairi uliotungwa tangu miaka elfu mbili, kuna simuluzi juu ya kudhihiri kwa

Krishna katika mwili kwa kuzaliwa na Mwanamke Bikira, pamoja na kisa cha mlezi wake

kumkimbia Mfalme aliyeamuru kuuwa kwa watoto wa kiume. Na katika Pango lililopo

Vanta kuna picha za watoto aliowachinja, ambazo ni za zamani sana. Vilevile katika hilo

pango kuna picha zilizochora zikimuonyesha mtu aliyeshikilia upanga mkali na kuanza

kuwaua hao watotowa kiume, na huku kukiwa na picha za wanaume na wanwake wakimsihi

asiwauwe watoto wao.

Na wanasema kuhusu silvahana Mwokozi mtoto wa mwanamke bikira (aliyekuwa

akiabudiwa pia na wakazi wa kamorin india).

kama wasemavyo juu krishna na kukimba kwake, na kwamba alipokuwamkubwa alimuua

mfalme aliyetaka kumuua enzi za utotoni mwake.

Page 45: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

45

Wahindu wanasema kuwa maisha ya Budha ya utoto yalikuwa yamezungukwa na hatari, katika

upande wa kusini mwa eneo la Mofadad kulikuwapo na mfalme dhalimu aliyeitwa Bimbasara

ambaye, kwa sababu ya hofu kuwa angetokea mtu atakayemnyang‟anya ufalme, alitaka ushauri

wa wasaidizi wake juu ya kinachotakiwa kufanyika ili kuzuia kile anachokihufia.

Wakamwambia kuwa katika upande wa kaskazini kuna familia kubwa inayoheshimika iitwayo

Saqya, amezaliwa Kwa mtoto mume, ambaye Ni wa pekee aitwayeBudha, ambaye anaweza

kukuletea matatizo makubwa. Wakamshauri kuandaa jeshi na kulituma huko kwa ajili ya

kumuangamiza huyo mtoto. Na Mabudha wa Mogoli wana kisa kama hiki, na Wachina

wanasema kuhusu shujaa wa Kichina Haoki kama wasemavyo Wahindu kuhusu Budha.

Wamisri wanasema kuhusu Horus kuwa alizaliwa kipindi cha kiangazi na kulelewa kwa

siri katika kisiwa cha Bota kwa kumhufia Tifon ambaye alitaka kumuua akiwa bado mtoto.

Na kisa cha Tiros mfalme wa Uajemi (miaka 600 kabla ya Kristo) kinafanana visa tulivyu

kwisha vitaja. Vilevile wanasema kuwa Baba yake aliota ndoto ambayo aliwaeleza Majusi ili

kutaka kujua maana yake, wakamwambia: Binti yako Findau atazaa motto mume ambaye

atakuwa ndiyo chanzo cha kuondoka kwa ufalme wako. Pindi alipozaliwa alimkabidhi

mikononi mwa Hevbagos ili amuuwe naye vilevile akamkabidhi mokononi mwa mchunga

kondoo ili amuuwe. Naye mchunga kondoo akamchukua mtoto nakudai kuwa ni mwanaye

na kuanza kumlea. Mtoto huyo alipo kuwa kijana alipambana na Istiyacis na kuchukua

ufalme kama walivyotabiri Majusi. Na Herdotus mwana historia wa Kiyunan amekielezea

kisa hiki na ndoto waliyoifasiri Majusi.

Na kuhusu Zoroaster mwanzilishi wa dini ya Majusi, wanasema kuwa maisha ya utotoni

mwake yalikuwa yameandamwa na hali ya hatari, kwa hiyo Mama yake akakimbia naye

katika nchi ya Uajem,i ambapo aliona roho usingizini akimwambia : usihofu chochote, kwani

Mungu atamlinda huyu mtoto kwa sababu ni mtume anayengojewa na ulimwengu.

Na maisha ya Prisius Mwana wa Bikira Danya yalikuwa yamezingirwa na hatari tangu

utotoni mwake kwa kuwa Crasius alimweleza Mfalme wa Argos kuwa binti yake atazaa

mwana ambaye atakapo kuwa mkubwa atamuua (yaani atamuua babu yake), akamfungia

binti yake mnarani ili asiweze kufikiwa na mwanamme yeyote kwa lengo la kuyalinda

maisha yake dhidi ya yaliyotabiriwa na Majusi. Siku moja (binti huyo) alitembelewa na

Mungu Jupita na hapo akachukua mimba na kumzaa mtoto wa kiume akamwita Prisius. Baba

yake aliposikia habari ya kuzaliwa kwa mtoto wa kiume, aliamuru kumweka binti yake

pamoja na mwanaye katika sanduku na watupwe baharini, ikafanyika kama ilivyoamriwa,

wakaokotwa na mtu mmoja jina lake Dectis na kuwaokoa kutoka baharini.

Lao-tseu

Page 46: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

46

Zama Iskolapius alipoikuwa mtoto, aliwekwa juu ya mlima Alas ili apate kufa, akaokotwa

na wachunga kondoo wakamlea. Na Hevqus mzawa wa Bikira Lito aliwekwa jagwani Ili afe,

akaokotwa na binti mmoja akamlea na kumtunza.

Naye Odbos alitupwa na Mamayake juu yam lima Ksiron, akaokotwa na wachunga

kondoo wakamchukua na kumlea. Na Tifos, Trajan, Yamus, Apollo na wengine miongoni

mwa watoto wa Miungu au wenye sehemu ya Uungu, walitaka kuuliwa na wafalme wa zama

zao kwa hofu ya wafalme hao dhidi yao, lakini kwa amri ya Mungu waliokoka kutoka

mikononi mwa watesaji wao, nasi tukapendea kufanya muhtasi tu bila ya kuwataja wote.

* * *

II- IMANI YA WAKRISTO KWAMBA HERODE ALITAKA KUMUUA KRISTO NA

JINSI ALIVYOOKOKA.

Tumeiyona imani ya nyumati zilizotangulia kuhusu Wafalme kutaka kuwaua na

kuwaangamiza watoto wa Muingu waliozaliwa na wanawake Bikira, na tumeona

yaliyosemwa na Wakristo kuwa yanafanana na yaliyosemwa na Wapagani.

Injiliya Mathayo mstari wa 2 namba 13: na hao walipokwisha kwenda zao, tazama,

malaika wa bwana alimtokea Yusufu katika, ndoto, akasema, ondoka umchukue mtoto na

mama yake, ukimbie Misri, ukae huko hata nikuambie kwa maana Herode anataka kumtafuta

mtoto amwangamize. Akaondoka akamchuka mtoto na mama yake usiku, akaenda zake

Misri.

SURA YA KUMI NA MOJA

MAJARIBU YA SHETANI KWA WATOTO WA MUINGU NA FUNGA YAO YA SIKU

40.

* * *

I- WA PAGANI:

Katika kitabu kiitwacho (Buddha Fasting Life) kilichotungwa na Moncyor Conwe wa

China ukurasa wa 44,172 na 173 kuna maelezo yafuatayo: na Mungu Mkuu Budha aliiweka

nafsi yake katika uchamungu kwa kiasi cha kuacha kula (yaani kufunga ) na hata kupumua

pia- - - Alitokewa na Maraa (yaani kiongozi wa mashetani) ambapo alikusudia kumtia

Buddha majaribuni mara kwa mara akijifanya kumwonea huruma,akamwambia Buddha:

“zinduka ewe kiumbe mkuu, kwani hali yako inamhuzunishakila anayekutazama, kwani

umekonda kwa kiwango kisichoelezeka - - - na hakika unafanya udhalili na kukaabiliana nao

kwa njia batili, nami nadhani huwezi kuendelea kuishi hapa sana”. Ewe bwana umevumilia

sana mateso makali, usiishi maisha ya udhalili bali rejea kwenye ufalme wako na kwa muda

wa siku saba utaweza kutawala mabara manne.

Mungu mkuu Budha akamjibu: “angalia ewe Mara (yaani kiongozi wa mashtani) mimi

najua vyema kuwa kwa muda wa siku sabanaweza kutawala ulimwengu wote, lakini mimi

sipendi ufalme kama huu, kwa sababu kushikamana na dini ni bora kuliko ufalme wa dunia.

Unaikiria kwa tama mbaya, unafaka kunilazimisha niwaache watu bila ya kingozi ili

Page 47: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

47

wasiweze kuwa salama dhidi ya mabalaa yako niondokee. Bwana akapaa na kuondoka akiwa

ameshikilia azima yake ileile, na mbingu zikanyesha maua, na anga ikanukia manukato

yenye harufu nzuri sana.

Shetani alimjaribu Zoroaster (mwanzilishi wa dini ya Majusi), na kumpa ahadi nyingi

iwapo angemtii na kumtegemea.Lakini majaribu yake yalikwenda kombo.Vilevile wana

hekaya na visa vingi visivyokuwa na msingi wowote zaidi ya kuelezea juu ya majaribu ya

shetani kwa Zoroaster.

Shetani,pia,alimjaribu Quetzalcoatl, mkombozi wa Wabrazili aliyezaliwa na mwanamke

bikira, na alifunga siku arobaini.

Wayunan walipokuwa wakitaka kujua mambo ya siri zilizofichika, walikuwa wakijizuia kula

vizuri na wakilala juu ya matandiko magumu yenye kuumiza,na hata baada ya siku tatu au

nne hula chakula kitakatifu (yaani kilichobarikiwa na wakuu wao).

Bwana Agosta na wengineo,wanasema: Wakuu wa kidini wa Mexico na Peru walikuwa

wakifunga funga ya mauaji kwani walikuwa wakijizuia kula na kunywa kwa muda wa siku

tano au kumi mfululizo, na usiku hupata kulala kidogo, wakaziweka nafsi zao katika hatari

kwa ajili ya shetani na ili wapate umaarufu wa kwamba wanafunga na kutubu sana.Vilevile

wanasema kuhusu mkombozi wao Quetzalcoatl kuwa alifunga siku arobaini pindi

alipojaribiwa na shetani.

II-MAJARIBU YA SHETANI KWA YESU KRISTO:

Tumeeleza yale yaliyosemwa na wapagani kuwa shetani aliwajaribu watoto wa miungu

yao.Sasa tunatoa yale yaliyoelezwa katika Injili kuhusu majaribu ya shetani kwa Yesu Kristo.

Mathayo sura ya 4 msitari wa 1:KishaYesu alipandishwa na Roho nyikani ili ajaribiwe na

Ibilisi.Akafunga siku arobaini mchana na usiku,mwisho akaona njaa.Mjaribu akamjia

akamwambia,Ukiwa ndiwe mwana wa Mungu,amuru kwamba mawe haya yawe mikate.

Naye akajibu akasema,Imeandikwa,mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila kwa kila neon

litokalo katika kinywa cha Mungu.Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu,akamweka

juu ya kinara cha hekalu,akamwambia,Ukiwa ndiwe mwana wa Mungu jitupe chini;kwa

maana imeandikwa,Atakuagizia malaika zake na mikononi mwao watakuchukua,usije

ukajikwaa mguu wako katika jiwe.Yesu akamwambia,Tena imeandikwa,usimjaribu Bwana

Mungu wako.Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote

za ulimwengu na fahari, kamwambia, Haya yote nitakupa,ukianguka kunisujudia.Ndipo Yesu

akamwambia,Nenda zako,Shetani.Kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu

wako,umwabudu yeye peke yake. Kisha Ibilisi akamwacha;na tazama,wakaja malaika

wakamtumikia.

SURA YA KUMI NA MBILI

KWENDA KUZIMU KWAWATOTO WA MIUNGU ILI KUWAKOMBOA WAFU

Page 48: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

48

I- WAPAGANI:

II-

Wapagani wanaamini kuwa miungu yao ilijidhihirisha katika miili, iliteremka kuzimu

baada ya kuawa au kusubiwa, ili kuwakumboa wafu.

Krishna mkombozi wa wahindu, kabla ya kuekea mbinguni aliteremka kuzimu ili

kuwaokoa wafu.

Zoroaster aliteremka kuzimu kuwaokoa wafu.

Adonis mkombozi aliyezaliwa na mwanamke Bikira, aliteremka kuzimu ili kuwakomboa

wafu.

Mercury Neno, aliteremka kuzimu kuwakomboa wafu.

Palador mungu wa Wascandinavia, baada ya kuuawa,alikwenda kuzimu kuwakomboa

wafu.

Na kwa mfano na utaratibu huu huelezewa miungu yote ya Kipagani iliyojionyesha katika

mwili na ikafa ima kwa kusulubiwa au kuuawa kwa ajili ya utakaso wa dhambi.

* * *

KUTEREMKA KWA YESU KRISTO KUZIMU ILI KUWAKOMBOA WANAOTESEKA

HUMO.

Walivyosema Wapagani juuya kuteremka watoto wa miungu yao kwenda kuzimu ili

kuwaokoa wanaoteseka huko, ndivyo walivyosema pia Wakristo kwamba Yesu aliteremka

kuzimu ili kuwakomboa wale waliopata mateso huko.

Katika mafundisho ya Kikristo imeelezwa kuwa Yesu alitermka kuzimu, na kwamba siku ya

pili alifufuka katika wafu.

Mwaka 347 baada ya Kristo, Mtakatifu Cristom alisema: “hakuna akanaye habari ya Yesu

kuteremka kuzimu ili atakuwa kafiri (isipokuwa kafiri).

Mwanzoni mwa kizazi cha tatu baada ya Kristo, Mtakatifu Clemandus wa Alexandria alisema

yafuatayo: Yesu alihubiri juu ya watu wa kuzimu katika Injili, Kama alivyohubiri na kufundisha

Kwa watu wa duniani, ili wapate kumuamini na kukombolewa popote watakapokuwa.

Atakapoteremka bwana kwenda kuzimu, Kama ilivyoelezwa na mafundisho ya Injili, je

atateremka kwa ajili ya watu wote au kwa ajili ya Mayahudi tu? Kama ilitakuwa kwa ajili ya

wote, basi atakayeamuamini ataokolewa, itakuwa ni kwa ajili ya Mataifa ambayo wakati wote

yalimkubali, patakuwapo na msiba mkubwa kwa wengine”. Mtakatifu Origgin amekubaliana na

maneno haya, ambapo anaamini kuteremka kwa Yesu kuzimu.

Vilevile Mtakatifu Nicodemuskatika Injili yake ameelezea kuteremka kwa Masihi kwenda

Jahannamu akatoa maelezo ya mazungumzo baina yake na kiongozi wa mashetani

yanayopatikana katika sura ya kumi na tano na kumina saba, juu ya kuwakomboa watu wa

kuzimu, wanawakea, wanaume na watoto.

Katika kitabu cha matendo ya mitume, sura ya pili mstari wa 31 kuna maelezo yafuatayo:

yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, aliyaja habari ya kufufuka kwake Kristo, ya kwamba

roho yake haikuachwa kuzimu wala mwili wake haokuona uharibifu.

Na katika wakala wa Petro, sura ya tatu, mstari wa 17 – 19 imeelezwa kama ifuatayo: “maana

ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikiwa ndiyo mapenzi ya mungu, kuliko kwa kutenda

mabaya. Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa aijili ya dhambi, mwenye haki kwa

ajili yao wasio na haki, ili atulete kwa Mungu, mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa

ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri”.

Page 49: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

49

SURA YA KUMI NA TATU

KUFUFUKA KWA HIYO MIUNGU KATI YA WAFU.

I- WAPAGANI:

Wapagani wa Kihindu huaminimkuwa Krishna alifufuka katika wafu, na kupaa mbinguni

kwa mwili wake. Na kwamba alipokuwa akipaa ilidhihiri nuru iliyoangaza duniani na mbinguni,

akiwa amezungukwa na roho wa mbinguni, alikuwa amezungukwa na wa mbinguni.Nuru ya

usiku aliofufuka katika wafu ilikuwa ni sawa na nuru iliyoonekana wakati wa kuzaliwa kwakle

katika nyumba ya Fasodena.Nuru hiyo ilimfuata mpaka Paradiso, na watu walipoiona wakasema:

Huyo ni Krishna amepaa kuelekea kwake mbinguni”.

Rama,ambaye ndiye Vishnu katika mwili, baada ya kukamilisha kazi zake hapa duniani alipaa

kuelekea mbinguni,akarejea katika uungu wake.Na kwa baraka ya jina la Rama na kumuamini

hupata kusamehewa makosa, na kila alitajaye jina lake na kumsudia kwa moyo wakati wa kifo

chake hupata kusamehewa madhdmbi yake yote.

Na katika kisa cha kufufka kwa Buddha katika wafu kinafana na yaliyoelezwa awali.

Wanamwita kwa majina ya “Gamidiyo,Gama,Gam” na kusema kuwa alipokufa ,machozi

yalimiminika na huzuni ikawatamalaki wakazi wa mbinguni na ardhini kwa sababu

wamempoteza mungu wa upendo, kwa kiasi kwamba Mahadiyo (yaani Mungu Mkuu)

alihuzunika sana na kuita: “Inuka ewe mpendwa mtakatifu”, na hapo Gama (yaani Buddha)

akainuka akiwa hai. Huzuni zikageuka kuwa furaha ,mbingu ikashangilia na kunadi kwa furaha:

“Amerejea Mungu ambaye alidhaniwa kuwa amekufa na kutoweka”.Khofu ya Jehannamu

ikazidi,mbingu ikadhihirisha mshangao wake, sanda ikaondolewa mwilini mwake, kaburi

likafunguliwa kwa nguvu za Mungu kasha akapaa kwa mwili wake kuelekea mbinguni baada ya

kukamilisha kazi zake.Mpaka leo hii wanawaonyesha wafuasi wake alama za nyayo zake katika

eneo la mlimani mahali ambapo alipandia kuelekea mbinguni.Na wafuasi wake wanaamini kuwa

kwa kumuabudu na kumuomba watapata kuingia katika ufalme wa mbinguni na kuungana naye

na kuwa mwili mmoja kama yeye alivyo mmoja pamoja na chemchem ya nuru.

Wachina huamini kuwa Laocyon (mzawa wa mwanamke mtakatifu) alipokamilisha kazi zake

za kisamaria hapa duniani,alipaa kwa mwili wake kuelekea Paradiso;na wanamchukulia kuwa ni

Mungu ambapo kuna mahekalu mengi yaliyojengwa kwa ajili yake na kwa ajili ya kumbukumbu

yake.

Majusi wanaamini uungu wa Zoroaster na kusema kuwa alitumwa kuja kuwakomboa na

kuwaokoa watu kutoka katika njia mbaya, na kwamba baada ya kumaliza kazi zake hapa duniani

alipaa kuelekea mbinguni.Wafuasi wake mpaka leo hii wanamtaja kwa ukuu na heshima na

kusema kuwa Zoroaster yu hai, mbarikiwa, nyota na majina mengine kama hayo.

Naye Mkombozi Iskolapius mwana wa Mungu,baada ya kuuawa alifufuka katika wafu.Na kisa

cha historia yake kimeelezwa katika utenzi wa shairi kikieleza maisha na kazi zake.Anasema

Page 50: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

50

mwana mtakatifu: Mama mtakatifu alimuoana Mungu Mwenye nuru, akasimlia kisa chake cha

kinabii,akamwambia, Salaam ewe tabibu mkuu wa ulimwengu. Amani yote iwe juu yako ewe

mtoto ut\k\yeweza kuwaponya mataifa katika miaka mingi ijayo, pindi wafu

watakapozinduka.Ukuaji na kufuzu kwako hakutakuwa na mipaka. Utaziongezea mamlaka ukuu

na watu kuwa wengi. Kwa uweza wako utahuisha wafu, najuu ya kichwa chako utatoka ukulele

na hata kufa, nawe kutoka mahali penye giza utasimama na ushindi na kuwa Mungu”.

Na Mkombozi Adoni (huitwa pia Tamuz) baada ya kuuawa alifufuka katika wafu. kisa cha kifo

na kufufuka kwake kimesimuliwa na Julius Crimicius, ambaye aliishi enzi za Costantine,

anasema: “Katika usiku maalumu, pindi watakatifu walipopita kumpa heshima Adoni, walikuja

na sanamu na kuliweka juu ya kitanda ( cha watoto).Watu hao walianza kulia na kuomboleza

kwa nyimbo mbalimbali za huzuni. Kisha alikuja kiongozi mkuu akaanza kuvipaka mafuta

vinywa vya waimbaji huku akisema: “Tumainini enyi watakatifu kwa kurejea Mungu wenu, na

mtegemeeni Bwana wenu aliyefufuka, kwani kwa mateso yake ametuletea ukombozi”.

Bwana Dupis anasema: "Wakazi wa Alexandria walikuwa wakitengeneza jeneza kwa hadhi na

heshima ili kukumbuka kifo cha Adoni, na kulichukua sanamu lake kwa heshima kubwa mpaka

kwenye kaburi lililoandaliwa kwa lengo hilo na kuliweka humo katika hali ya utulivu wa hali ya

juu. Na kabla ya kuimba nyimbo za kufufuka kwake, hukaa kimya kwa huzuni ya kukumbuka

mateso na kifo chake na kuonyesha jeraha lililompata mwilini mwake kwa kuchomwa mkuki.

Kisha baada ya hapo huanza kufurahi na kushereherkea. Sikukuu hiyo hufanyika tarehe 25 ya

mwezi wa Machi".

Naye Dr. Prichard anasema: "Wasuriya walikuwa kwakisherehekea kwa ajili ya Adoni katika

kipindi cha majira ya Kuchipua. Kwanza walikuwa wakiomboleza kifo chake kwa huzuni

kubwa, kisha huelezea kufufuka kwake katika wafu kwa furaha na shangwe".

Bwana Klematt 100

anasema yafuatayo kuhusu kufufuka kwa Adoni katika wafu : Na baada ya

kuhuzunika na kumwoboleza Adoni hutangaza kuwa amefufuka na kurejea kuwa hai, na alama

ya kufufuka kwake ni wao kuingiza taa mahali alipo, na ndipo kiongozi mkuu huwaambia watu

waliokusanyika mahli hapo akisema: Zifarijini nafsi zenu na mfurahike nyinyi ambao mmepata

siri za uungu zilizohifadhiwa kwa ajili yenu, basi na tufurahike baada ya mateso

yaliyotupata".Kisha husema maneno yafuatayo: "Nimeokolewa kutokana na msiba mkubwa, na

fungu langu sasa ni zuri.Na hapo watu husema baada yake maneno yafuatayo: "Amani iwe juu

ya njiwa aliyerejesha nuru".

Anasema Bwana Alexandria Mrray: "Wayunan wa zamani walikuwqa waakiheshimu na

kuitukuza sana sikukuu ya kufufuka kwa Adoni katika wafu, walikuwa wakileta sanamu kana

kwamba ni Adoni na kulisomea sala ya maiti huku wakilia na kuimba nyimbo za huzuni na

kukata tamaa. Baada ya hapo sauti za furaha hupaa na kunadi kuwa Adoni amefufuka na kurudi

kuwa hai".

Mkombozi Osiris mzawa wa mwanamwali, alifufuka baada ya kifo. Wamisri wanamwita

“MTUME WA PEKEE”.Mohami anasema: Muhimili wa mafundisho ya kidini kwa wapagani

wa Kimisri katika karne nyingi zilizopita ilikuwa ni imani ya kufufuka kwa Mungu, Mpatanishi

aliyejidhihirisha kwa mwili, Mzawa wa mwanamwali, na kwamba ndiye mmiliki wa milele wa

Page 51: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

51

ufalme wa mbinguni. Walikuwa wakisherehekea sikukuu ya pasaka katika kipindi cha majira ya

kuchipua kwa kumbukumbu ya kufufuka Mungu Mokmbozi Adoni, wakifurahi na kushangilia,

na kuamini kuwa aliitoa nafsi yake kuwa kafara ya dhambi za watu, na kwamba ndiye mpaji wa

amani na uzima, na ndiye mfunguzi wa haki.

Anasema Bwana Bonwick: Katika mambo ya kushangaza sana, ni kuwa mataifa, tangu miaka

elfu tano iliyopita, walimwamini Osiris ambaye alifufuka katika wafu, na kuamini kuwa ni

mkombozi wao na kwamba nao pia watarejea kuwa hai kama yeye…naye ndiye mashuhri zaidi

katika miungu yao wanayempenda sana na kusema kuwa ndiye mwema na kipenzi chao katika

uzima na umauti. ( Wasomi wa masuala ya dini wamehadharisha kuhusu kisa cha kuzaliwa,

kufa, kufufuka na kupaa kwake kuelekea mbinguni).Kwa sababu ya kupenda mambo ya heri

alipata kuwabeba watu, na ndiyo maana akauawa na kuzikwa, na kaburi lake likawa ni eneo

takatifu zaidi katika nchi ya misri inayotembelewa na watu.Hali hii ilidumu kwa muda wa

maelfu ya miaka, ambapo walikuwa wakiwasha taa juu ya kaburi hilo na kumwimbia nyimbo za

huzuni ambazo zimeelezwa na Herdotis. Kabla ya sikukuu walikuwa wakimhuzunikia kwa

kipindi cha siku tatu kisha husherehekea sikukuu ya kufufuka kwake katika wafu kwa furaha na

shangwe.

Na Mungu Horus motto wa mwanamwali Isis, alipatwa nay ale yaliyompata Osiris, yaani

aliuawa na kufufuka katika wafu. Na wale wanaomwamini wanamfanyia kama afanyiwavyo

huyo aliyetajwa hapo juu, kama kumhuzunikia na kumlilia na kasha kufurahi na kupamba siku

ya kufufuka kwake.

Attis mkombozi na mungu wa Wafrige, aliuawa kwa kuonewa kasha akafufuka katika wafu.Na

wanasimulia kisa cha kuzaliwa na kufufuka kwake kwa mlolongo wa simulizi mbalimbali, lakini

zikiwa na madhui moja. Vilevile humwita kuwa DHABIHU iliyorejea katika uzima tarehe 25

Machi, siku ambayo huiita Helariya au sikukuu asili ya pasaka.

Na Mithra mkombozi wa Waajemi, ambaye ndiye mpatanishi kati ya Mungu na watu, dini yake

ilikuwa imeenea sana katika nchi za Uajemi, Armenia, na Asia ya kati ambapo waliamini kufa na

kufufuka kwake katika wafu, na katika sikukuu ya kufufuka kwake inayofanyika tarehe 25

machi, humleta kijana na kujifisha kwa mdamfupi kisha kuamka kwa maana kwamba amerurudi

kuwa hai. Yote hayo huyafanya ili kufananisha kufanakufufuka kwake. Na wanaamini kwamba

kwa kuteseka kwake walipata kukombolewa na humuita MKOMBOZI. Ifikapo sikuya kufufuka

iliyotajwa hapo juu,wakuuwa dini hukaa pembezoni mwa kaburi ambalo hulitengeneza

mahekaluni mwaonakisha huanza kulia na kuombleza katika hali ya giza kali, kasha huwasha taa

ghafla na kunadi „furahini na mshangilie enyi watakatifu mliokombolewa, kwani amefufuka

bwana wenu ambaye kwa kifo na mateso yake tumepata utakaso‟ na huitukuza sana ijumaa ya

huzuni.

Na mkombozi Bacchus mtoto wa mwanamwali Semele, alifufuka baada ya kuuawa.Na

katika siku ya sikukuu ya kufufuka kwake walikuwa wakimleta mtu aliyekufa na kumuweka

kitandani,kisha huomboleza kifo cha mkombozi wao Bacchus kama wafanyavyo mataifa ya

kipagani yaliyotajwa hapo awali. Na ifikapo asubuhi ya tarehe 25 ya machi hunadi kuwa

amefufuka na hapo huwaza kufurahi kwa imani kuwa kifo chake kilileta ukombozi nafuraha kwa

watu wenye mikosi na husema kuwa baada ya kufufuka alipaa kuelekea mbinguni.

Na wanaamini kuwa Heracles mkombozi mwana wa Mungu Zeus aliyezaliwa na mama

mwenye asili ya kibinadamu, aliuawa na kufufuka katika watu kisha akapaa kuelekea mbinguni

Page 52: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

52

akilindwa na radi. Na wale wanaoamini uungu wake walijenga hekalu katika eneo

linalosemekana kuwa mahali alipopaa kuelekea mbinguni.

Naye Mamnuun aliuawa na kufufuka katika wafu akaliliwa na kuhuzunikiwa na mama yake

Wakius. Na Ahfarius naye pia alifufuka katika wafu. Waumini wake wlikuwa wakiwaonyesha

watu mahali alipopaa kuelekea mbinguni.

Yaldor, Mungu na mkombozi wa Wascandnavia aliuliwa na kufufuka kwenye uzima wa

milele, Na wanasema kuwa „Yaldor mwema na mungu mwenye neema, alipoteremka kuzimu

alimwambia Hermod [ambaye alimlilia na kumuomboleza]kuwa „mwambie kila kiumbe aliyoko

ulimwenguni katika wafu na wazima, wanililie ili nipate kurejea kwa Mungu‟.Alipokwisha

kusikia hayo maneno aliwatuma wajumbe kwenda kila kona ya dunia nakuwaambia wamlilie na

kuhuzunikia kifo chake iliYaldor apate kutoka kuzimu.Wakamlilia na hapo akarejea kuwa hai‟

Pia wanamwabudu mu ngumwengine aitwaye Frey na kusema kuwa aliuawa kisha akafufuka

katika wafu. NawaDruids wa zamani huko uingereza walikuwa wakiamini kufa na kufufuka kwa

Bacchus na kutengeneza jeneza katika mahekalu yao kila mwaka kama ishara ya kumbukumbu

ya kifo chake. Jeneza lililokuwa likitengenezwana Warumi na Wajerumani.

Quetzalcatl, Mkombozi wa Wamexco aliyeuawa kwa kusurubiwa na alifufuka katika wafu.

Na kisa cha kufufuka kwake kimeelezwa katika kumbukumbu ya kimexco katika huko „codix

purgiyanus‟kisa ambacho kinapatikana mpaka leohii.

Wanusr,Wajerumani, Wachina na wengineo walikuwa wakipaka mayai kwa rangi mbalimbali

na kuyagawa baina yao, ambapo kati yao kuna waliyoyahifadhi mpaka mwaka ujao kwa ajili ya

siku waliyofufuka miungu, kama ishara ya kurejea kwao katika uzima.

II-KUFUFUKA KWA KRISTO KATIKA WAFU:

Yale yaliyosemwa na wapagani juu ya kufufuka kwa miungu yao ndio yaliyosemwa

moja kwa moja na wakristo kuhusu Yesu Kristo. Kwa nini wasiseme hayo wakati yeye ni

miongoni mwa wema wa miungu waliojidhihirisha kwa mwili kwa mujibu wa imani yao?

Katika injili ya Mathayo sura ya 28 ya mstari wa 5 mpaka 8kuna habari ifuatayo :Malaika

akajibu, akwaambia wale wanawake, msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta

Yesu aliyesurubiwa, hayupo hapa kwani amefufuka kma alivyosema. Njooni, mpatazame mahali

alipolazwa. Nanyi njooni upesi mkawaambie wanafunzi wake, Amefufuka katika wafu.Tazama,

awatangulia kwenda Galilaya, ndiko mtakakomwona. Haya nimekwisha waambia;

Vilevile habari yakufufuka kwake katikawafu imeelezwa katika injiliya Marko, sura ya

16 101

, Injili ya Luka sura ya 24 na katika injili ya Yohana sura ya 20 102

.Hata hivyo injili hizo

zote hazijaafikiwa juu ya namna ya kufufuka kwakwe, bali zimekhitilafiana katika hilo. Na lau

kama kuelezea khitilafu hiyo kusingemaanisha kutoka nje ya mada yetu, tungeielezea kwa

upana.

SURA YA KUMI NA NNE.

KUREJEA DUNIANI KWA AJILI YA HUKUMU .

I-WAPAGANI:

Page 53: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

53

Wachina huamini kuwa mkombozi na mlinzi wao Vishnu aliyejidhihirisha kwa mwili wa

kibinadamu kwa jina la Krishna, atakuja kwa mara ya pili katika siku za mwisho.Na vitabu vya

kidini vya kihindu vinasema; Nyota thabiti zitakaporejea mahali zilipoanzia mzunguko wake,

ambao ndio wakati kilipoanza kila kitu [ambayo ni katika nyota ya nge] akatokea Vishnu katika

watu kwa namna ya mpanda farasi aliyejizatiti kwa silaha, akiwa amepanda farasi wa kijivu

mwenye mbawa akishika upanga wenye moto kwa mkono wa kwanza ili apate kuwaangamiza

waovu ambao bado wapo hai katika uso wa dunia.Na katika mkono wa pili kutakuwa na pete

yenye kung‟aa, kama ishara ya kuanza kwa “Yakos” yaani vizazi vitukufu, na kuwa kiyama

kimefika.Wakati wa ujio wake jua na mwezi vitafifia mwanga wake, ardhi itatikisika na nyota

kudondoka.

Na Mabudha wanaamini kuwa Budha huonekana mra nyingi katika mwili wa kibinadamu

ili kuwaandaa na kuwajulisha kuwa wataungana na dhati yake kuu,na kuwa siku za mwisho pia

ataonekana. Ujio huu umetajwa kwenye vitabu vyao vitakatifu kuwa makusudio yake ni

kurejesha nidhamu na saada duniani.

Na Wachina huamini kuwa katika siku za mwisho, itakapomalizika miaka elfu moja atakuja

mtu wa Mungu duniani ili kuirudishia amani na saada, na vitabu vyao vya dini vitano

vimesheheni maelezo ya enzi ya dhahabu huko mbeleni. Majusi wa zamani nao pia huamini

kuwa itapita duniani miaka elfu moja, ambapo watu wote duniani wataamini dini zaZoroaster.

Na Majusi wa zama hizi (ambao ni masalio ya wale Majusi waliokuwa wakiamini mungu wa

Zoroster) wanasema kuwa kuna dhati takatifu katika ardhi iitwayo Kankodar ambayo inatazamia

amri ya Yazidi Sairosh ambaye atakuja nchi ya uajemi na kuirejesha hapo dola ya zamani na

hatimaye kueneza dini ya Zorostar ulimwenguni, na atakapotaka kufufua wtu ata ziamuru ardhi

na bahari kutoa mabaki ya wafu ambapo Auramazda atavika nyama na damu, na wale ambao

watakuwa hai mpaka siku ya mwisho atawafisha na kuwafufua kama watu wengine. Kabla ya

kutokea hayo watatokea mitume wakuu wale tu ambao watafanya maajabu na miujiza, na kwa

mda huu ardhi yte itakumbwa na balaa kubwa, vita njaa na mengineyo. Kisha baada ya

kufufuliwa kila mtu atalipwa kulingana na matendo yake, kama ni kheri atapata kheri na kma ni

shari atapata shari, na wma watabaguliwa dhidi ya waovu, na wale ambao hawakuwa ni wenye

kuridhiwa watatupwa jahannamu ili watakaswe kwa muda wa siku tatu usiku na mchana,

watatakaswa kwa moto wa madini yenye kumiminika, na hivyo watatolewa kwenda kwenye

neema za milele. Ufalme wa shetani utakwisha…… na ardhi itawekwa nuru ili iwe makazi ya

watu wema, na mtawala wao atakuwa Auramazda pekee.

Wafua wa Bucchus pia wanatazamia ujio wake wa mara ya pili ili autawale ulimwengu na

kuwarudishia watu saada.Wacathoni nao walikuwa wakitazamia ujio wa shujaa wao “Kaloebok”

kwa mara ya pili ili awakomboe kutokana na dhulma ya Wajermani, ambapo kwa sasa ametulia

mpaka matatizo yatakapoenea, na hpo atadhihiri na kuwakomboa kutokana na dhulma.

Na Wathelato wanangojea ujio wa mara ya pili wa “Puryaam Puroeham”, baada ya miaka elfu

moja kupita, na wanasma vilele kuwa “Welkardanseck” anasubiri aamke usingzini mwake na

kumsaidia Damis ili kuwqashinda maadui zao wa Perusia.

Wascandinavia wa zamani wanaamini kuwa siku za mwisho watakumbwa na balaa na majanga,

ardhi itatikisika na nyota zitadondoka, kasha baada ya hapo joka kubwa litafungwa na

minyororo,na dini ya Odini kutawala juu ya watu wote.

Na wafuasi wa Quetzalcoatlmkombozi wa Mexco wanatazamia ujio wake wa mara ya pili, na

wanaamini kuwa kabla ya kuondoka duniani aliwaeleza wakazi wa Mitsholola juuya ujio wake

wa mara ya pili na kutawala. Na meli za Wahispania zipoonekana katika pwani ya Brazili

Page 54: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

54

mwaka 1518 AD, walizani kuwa ni mahekalu aliyokuja nayo Quetzcoal kama alivyokuwa

amewaahidi.

II- UJIO WA KRISTO KWA MARA YA PILI KWA AJILI YA HUKUMU

.

Tumeeleza waliyoyasema wapagani kuhusu ujio wa watoto wa miungu yao kwa kwa mara

nyengine. Wakristo nao pia wamewaiga, wakiamini ujio wa kristo kwa mara nyengine hapa

duniani na hawakuacha chochote katika yaliyosemwa na wapagani juu ya miungu yao ispokuwa

waliyasema kumhusu yesu kristo, Kwa kudhani kuwa kufanya hivyo ni kumtukuza.Angalia

maelezo katika vitabu vyao vitukufu juu ya jambo hilo:

Katika injili ya Mathayo sura ya 24 msitari wa 27: “kwa maana kama vile umeme utokavyo

mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake mwana wa

Adamu” , ( katika sura hii zimetajwa alama na dalili kadhaa ambazo zitatokea kabla ya ujio

wake, ambazo hatotazitaja kwa sababu ya kutaka kufupisha” 104

Na katika Matendo ya Mitume, sura ya kwanza msitari wa 10 na 11 kuna maelezo yafuatayo:

“walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu waili

wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona

mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu

mbinguni, atakuja jinsi iyo mlivyomwona akienda zake mbinguni”.

Vilevile katika Injili ya Marko sura ya 13 msitari wa 26 kuna maelezo yafuatayo: “Hapo ndipo

watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu”.

Na kwa mfano huu kuna sehemu nyingi zilizoelezea ujio wake wa mara ya pili, vilevile maelezo

ya wakuu wa kanisa na wanatafsiri wameeleza mengi , nasi tunatosheka na hayo tuliyoyaeleza.

SURA YA KUMI NA TANO

IMANI YA KWAMBA MWANA NDIYE MUUMBA

I- WAPAGANI:

Mafundisho yanayopatikana katika vitabu vya kidni vya Wahindu vinaeleza waziwazi kuwa

“Krishna mwana wa Mungu aliyezaliwa na mwanamwali Devaki, ambaye ni nafsi ya pili katika

utatu mtakatifu, ndiye aliyeumba mbingu na ardhi na vilivyomo, naye, kwa imani yao, ndiye wa

kwanza na wa mwisho, ndiye kila kitu, na muumba wa kila kitu.

Katika kitabu kiitwacho “ Bahakwat Gita” ambacho ni mojawapo ya vitabu vitakatifu kwa

wahindu, imeelezwa kuwa Krishna alimwambia mwanafunzi wake Arjon mpendwa maneno

yafuatayo: “Mimi ndiye Bwana na mwanzilishi wa viumbe vyote, nilimuumba mwanadamu kwa

namna nne zenye na majukumu misingi tofauti, tambua kuwa mimi ndiye mtengenezaji na

Page 55: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

55

muumba wa binaadamu. Mimi sikuumbwa hivyo sifikiwi na hali ya kutokuwapo”. Vilevile

akasema katika mawaidha ya saba yaitwayo “nguvu ya maumbile na roho mkuu”: “mimi ndiye

muumba, mwangamizaji, na mkuu ambaye kila kitu kinanitegemea”. Akasema pia katika

mawaidha ya tisa yaitwayo (( siri kuu na elimu ya mwanzo)) kuwa: (( mimi niliutandaza

ulimwengu kwa namna yake katika pazia, na mimi ndiye mhifadhi wa kila kitu, na mimi ndiye

baba na mama wa huu ulimwengu huu, na mimi ndiye mkuu, mlinzi, na mimi ndiye Mtakatifu

ambaye ni lazima kumtambua, na mimi ndiyo alama ya siri ( A na Z), nami ndimi njia ya wema ,

mfariji, muumba ashuhudiaye, na rafiki ambaye marejeo ni kwake”. Akasema pia katika

mawaidha ya kumi yaitwayo muuganiko wa asili wa kimungu: “mimi ndimi muumba na mtoaji

wa kila kitu,basi na waamini hivyo wale walioneemeshwa kwa hekima ya kiroho,na nyoyo zao

zifungamane nami wakiabudu na kulitaja jina langu,na wafundishane mafundisho yangu ili

furaha ienee kati yao.”

Na vitabu vitakatifu vya wahindu vinawaelezea Krishna kuwa ndiye chanzo cha (“”uhai, na bila

yeye kusingekuwepo kitu chochote katika ulimwengu huu.Vilevile Wachina wanasema kuwa

Mwenyezmungu hakuumba kitu chochote, bali mwanae ndio muumba wa ulimwengu na sanamu

lililochongwa kwa sura yake huliita Ntikay ” ambapo huliabudu na kuliomba kuwatimizia

shidaszao. Na wanasema kuhusu “Lanotho”, aliyezaliwa na mwanamwali mtakatifu, kuwa ndiye

muumba wa kila kitu.Pia mafundisho ya kidini ya Wakeldayo yanaeleza waziwazi kuwa mwana

wa pekee ndiye muumba wa kila kitu. Vilevile wafuasi wa mungu Tao wanadai kuwa ni mwana

wa mungu na ndiye muumba wa kila kitu.

Mafundisho potofu ya kidini ya Waajemi wa zamani yameeleza waziwazi kuwepo kwa mungu

mmoja asyeonekana wala kudirikiwa wanayemwita “Zaroona Aqarena”, na maana ya sentensi

hii ni ( asye na mipaka ya nyakati) (yaani wa milele na milele). Na kutokana na Mungu

alipatikana Auramazda mfalme wa nuru, mwana wa pekee muumbaji, ambaye kila kitu

kilitokana nay eye, nba yeye ndiye Muumba.

Vitabu vitukufu cha majusi kiitwacho “Zandafasta” Kimesheheni sala na maombi ya mwana

wa pekee wa Mungu “. “Auramazda”, na ufuatao ni mfano was ala na maombi yao: “

Nazitanguliza sala zangu kwa Aramazada, yeye ndiye Muumba wa vitu vyote, vilivyokuwepo na

vitakavyokuwepo hata milele, naye ndiye mwenye hekima na mwenye nguvu, Muumba wa

mbingu, jua, mwezi,nyota, upepo mawingu, maji, ardhi, moto, miti, wanyama na binadamu na

ndiye aliyesujudiwa na Zoroaster aliyeleta sheria duniani, na akajua kwa utambuzi wa asili, na

akaamini yaliyokuwepo zamani, ya sasa na yajayo, alipata elimu na neno kuu ambalo kwake

nafsi hupata kulivuka daraja la nuru ambapo huviacha dunia ya maovu na kuelekea kwenye nuru

ambayo ni makazi matakatifu yaliyojaa harufu nzuri. Ewe Mungu hakika mimi nazitii sheria

zako, nafikiri, nazungumza na kutenda kulingana na maamrisho yako, ninajiepusha na kila

dhambi na kutenda matendo mema, na ibada yangu ni kwa ajili ya Auramazda mlipaji wa

matendo mema kwakuwa yeye ndiye aokowaye wale watendao kulingana na maamrisho yake

wakatumaini kufika paradiso makazi ya saada, nuru na harufu nzuri”.

Na waumini wa mkombozi Adoni huamini kuwa ndiye aliyewaumba watu na atawafufua

baada ya umaut.

Katika kitabu cha Wahindu kiitwacho “Gita” imeelezwa kuwa Krisha alisema: “Haikutokea

zama ambayo mimi sikuwapo, mimi niliumba kila kitu, mimindiye mwenye kubaki, wa milele

mwanzilishi na nilyekuwepo kabla ya chochote, mim ndiye mtawala mwenye nguvu juu ya

ulimwengu, mimi ni mwanzo katikati na mwisho wa kila kitu”.

Page 56: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

56

Na miongoni mwa maombi yaArjoni mwanafunzi wa Krishna ni hya yafuatyo “Wewe ndiwe

Mungu mkuu mwenye kubaki ambaye ni lazima watu wakujue, wewe ndiye mwenye kufusha

viumbe,wewe ndiwe mlnzi wa dini na muwanzilishi, ninakutukuza ewe Mungu uliyekuwepo

kabla ya miungu wengine”.

Akasema vilevile: “Utukufu ni wako hapo kabla na hata milele, wewe ni vyote katika vyote,

wewe ambaye utukufu na nguvu zako hazidirikiwi, wewe umekizunguka kila kitu, hivyo wewe

ni kila kitu”. Na katika kitabu kitukufu “Vishna Purana” kuna maelezo yafuatayo: “ alipodhihiri

Vishna kwa namna ya Kishna, na kuingia katika mwili wa bikira Devaki na kuzaliwa naye,

alisema kuwa “Yeye hana mwanzo katikati wala mwisho”.

Na baadhi ambaye A na Z, uwepo wake hauna mwanzo wala mwisho, naye ndiye

Bwana,Mfalme, muweza, wa milele na Mungu mkuu atukuzwaye”.

Naye Laokyon mwana wa Mungu aliyezaliwa na mwanamke mwanamwari uwepo wake moja

kwa moja hauna mwanzo wala mwisho.”

Katika upotofu wa wafuasi wa Laotzu huko china,Jauhan safi, muumba war oho ya mwanzo,

chanzo cha mbingu na ardhi, Muumba wa viumbe na kuwa yeye alikuwepo kabla ya viumbe na

kabla ya mtikisiko wa kwanza wa ul;imwengu”. Na katika kitabu cha majusi kiitwacho

“Zandafista” imeelezwa kuwa “Auta mazda mwana wa pekee wa Mungu alikuwepo kabla ya

mwanzo na atendelea kuwepo milele.”

Zeus anayeitwa kuwa nia A na Z alielzewa na Ouzfink kama ifuatavyo: “Zeus ni wa mwanzo

na wa mwisho. Naye ndiye Muumba wa kila kitu kilichopo”.

Na wanamsifu Bacchus kwa sifa ya utangu, ambapo katika maandishi ya zamani

yaliyonakshiwa kwenye Dirham kuna maneno yafuatayo: “ Mimi (yaani Bacchus) ni kiongozi

wenu, na mlinzi wenu, mimi ndiye Ala na Omega”.

II- IMANI YA KUWA MTOTO YESU KRISTO NDIYE MUUMBA WA VIUMBE VYOTE.

Tumeona yaliyoaminiwa na watu waliopotea kuhusu watoto wa miungu yao kuwa ndio

waumbaji na watengenezaji wa ulimwengu na vyote vilivyomo, maneno kama hayo yametolewa

na Wakristo kuhusu Yesu Kristo, yaani wakisema kuwa ndiye Muumba na mwanzilishi wa

viumbe vyote.

Katika injili ya Yohana Sura ya kwanza msitari wa 3 na10: “ Vyote vilifanyika kwa huyo, wala

pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika”. “Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye

ulimwengu ulipata kuwako, wala ulmwengu haukumtambua”.

Vilele katika waraka wa Paulo kwa Wakolosai sura ya kwanza ukurasa wa 16 na 17 kuna

maelezo yafuatayo: “ kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyombinguni na vilivyo

juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; vikiwa ni vitu vya enzi au usultan, au enzi au

kwa mamlaka, viyu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake. Naye amekuwako kabla

ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye”.

Na katika waraka kwa Waebrania, Sura ya kwanza mstari wa pili kuna yafuatayo: “mwisho wa

siku hizi amesema na sisi katika mwana, aliyemuweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye

aliyeufanya ulimwengu”.

Kwa mfano huu, kuna vifungu vingi ambavyo vinaeleza kuwa yeye ndiye Muumba wa

ulimwengu, vilele maelezo ya wakuu wa dini hiyo yanabainisha na kusema waziwazi jambo hilo,

wala sio ajabu kwa jambo hilo, madhali wanamchukulia kuwa ni Mwana wa Mungu kama

walivyofanya waliomtangulia miongoni mwa watoto wa miungu ya kipagani.

Page 57: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

57

SURA YA KUMI NA SITA.

UBATIZO KWA AJILI YA KUONDOA DHAMBI.

Bwana Amerly 105

,Bunsen 106,Higgins 107

, na Lillie 108

kwa ufupi wanasema: “ katika nchi za

India, Mongolia naTibet wanapowabatiza watoto huwasha mishumaa,wakachoma vitu vyenye

harufu (ubani) madhabahuni na makuhani husoma sala maalum na kisha humzamisha katika maji

mara tatu, na baada ya hapo humwita jina walitakalo.

Na Wabrahma wa desturi ya kidini ya zamani inafanana na Wamajusi, Wamisri, Wayunani na

Warumi wa zamani, ambayo ndiyo ubatizo wenyewe, na wakati wa kufanya husali na kuliomba

jua, ambapo baada ya kiapo cha imani kutoka kwa anayebatizwa, (akiwa mtu mzima) juu ya

kutekeleza kikamilifu utii kwa wakuu wa kidini na kutunza siri ya usafi wa mwili wake,

humnyunyuzia maji mara tatu na kuzungumza kwa namna inayolingana na cheo hicho; na

kitendo cha kumnyunyuzia maji hukichulia kama “ kuumbwa upya”, na humvika nguo maalum

na taji, na kuchora ,msalaba mashavuni mwake, na humuwekea kfuani mwake msalaba katika

namna ya misalaba ya “TO” na humkabidhi siri ambayo ni neno OM.

Ama kama anayebatizwa ni motto, huchukuliwa na kiongozi wa kidini wa Wabrahma

wanayemwita Koro (yaani mchungaji), na hupakaza kwa tope na kisha humzamisha katika maji

mara tatu huku akisema: “ ewe Mungu Mkuu, hakika huyu mtoto ni mwenye dhambi,

amejipakaza kwa madhambi kama alivyojipakaza kwa tope la huu mto, hivyo kama ambavyo

maji yanamtakasa kutokana na hili tope, basi mtakase na umkomboe kutokana na dhambi”, pia

huamini kuwa ubatizo huondosha madhambi yoyote hata kama yatakuwa na wingi wa kiasi gani.

Viongozi wanaosimamia zoezi la ubatizo huitwa “ wana wa jua”.

Nao wafuasi wa Zoroaster, huwabatiza watoto wao, wakubwa kwa wadogo. Anasema bwana

Pasper : “Majusi wa zamani walikuwa wakiwapeleka watoto wao mahekaluni siku kadhaa baada

ya kuzaliwa, na kuwakabidhi kwa Kuhani mbele ya sanamu la jua ( moto ndio alama ya jua),

kisha huwazamisha katika chombo kilichojazwa maji, na baada ya hapo huwaita kwa majina

wayatakayo”.

Naye Dr. Hidde anasema: “ Ubatizo kwa watu wa zamani ilikuwa ni kwa kuzamishwa katika

maji au kunyunyiziwa maji, na ubatizo huu huuita „kuzaliwa upya”, ambapo baada ya tukio hilo,

huzichukulia nafsi kuwa ni takatifu na zenye saada, kisha huwapa majina wayapendayo”.

Wamisri walikuwa wakiwabatiza watoto wao wa umri mkubwa na kuwapa siri za awali za

kidini, na kuchora mashavuni mwao alama ya msalaba.

Na Waapoliso wa Fedora huko Afrika walikuwa wakiwabatiza watoto wao, ambapo wakati wa

ubatizo husoma sala maalumu, na kuamini kuwa ubatizo unaondosha madhambi.

Naye Bwana Doane anatoa maelezo yafuatayo: “Wapagani wa Kirumi walikuwa wakiwabatiza

watoto wao kwa maji wakiamini kuwa ubatizo ni njia ya kuondosha madhambi” 109

.Naye

mwanahistoria Dhiuginus ameeleza kwamba walikuwa wakiwabaiza watoto wao kwa jina lake,

ambapo watoto wa kiume walikuwa wakibatizwa siku ya tisa baada ya kuzaliwa kwao, na watoto

wa kike wakibatizwa siku ya sita baada ya kuzaliwa. Na maji hayo ya ubatizo huyaita “maji

matakatifu”. Baada ya ubatizo, kuhani huwapa wazazi wa mtoto cheti kinachoonyesha kuwa

mtoto wao amebatizwa na kuumbwa upya . Kisha baada ya hapo, wana haki ya kumhesabu

Page 58: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

58

kuwa sehemu ya familia yao, na siku hii huichukulia kuwa sikikuu adhim. Pia walikuwa

wakiwabatiza wale wanaopokea mafindisho ya siri ya Mithra.

Wapagani wa Norwey na Denmark walikuwa wakiwabatiza watoto wao kwa kuwamwagia maji

na kisha kuwa majina. Nao Walifone walishikamana sana na ubatizo na kuuchukulia kuwa nguzo

muhimu katika mambo yao ya kidini. Hali kama hiyo ilijitokeza kwa Wajerumani wa zamani,

Wadruid, wakazi wa Zilanda na wengineo, na wakati wa shughuli ya ubatizo hufanya sala

maalumu kwa kokombolewa kutoka katika dhambi.

Na Wamexico wa zamani walikuwa wakiwabatiza watoto wao muda mfupi baada ya kuzaliwa,

ambapo ndugu na jamaa hukusanyika nyumbani kwa wazazi wa mtoto, na wakati wa kuanza

kwa shughuli ya ubatizaji, mkunga hukishika kichwa cha mtoto mkononi mwake na kukielekeza

kichwa chake upande wa machomozeo ya jua, kisha hufanya sala maalumu kwa Quetzalcoatl

pamoja na miungu wa maji, na baada ya hapo, Kuhani hunawa mikono yake na kisha huushika

mdomo na kifua cha mtoto na kusema: “ tunayaomba maji yaangamize na kuteketeza madhambi

yaliyogandamana na huyu motto kabla ya kuumbwa kwa ulimwengu”, na baada ya hapo huuosha

mwili wake kwa maji, na kutaja kila kitu kinachoweza kumdhuru kiondoke ili apate kuzaliwa

upya baada ya kubatizwa.

Naye Prescott anasema: “ Wamexico walikuwa wakiwabatiza watoto wao kwa manukato na

maji, na kuiomba miungu yao iyaruhusu matone ya maji yaondoshe madhambi yaliyompata

mtoto kabla ya kuumbwa kwa ulimwengu, ili azaliwe mara ya pili kwa ubatizo. Na wakati wa

ubatizo huwalika ndugu na jamaa kuhudhuria shughuli hiyo” 110

Bwana Lundy anasema: “tunapoichunguza historia, tunaona kuwa ibada ya ubatizo ni ya

zamani sana, na ilikuwa imeenea katika maeneo ya Asia na Amerika, ambapo wakazi wa Brazil

walikuwa wakiwabatiza watoto wao wa kike na wa kiume katika hekalu liitwalo “kanisa la

aliyesulubiwa” kwa kuwanyunyizia maji katika birika. Na maji hayo ya ubatizo waliyaita kuwa

ni “ maji ya uzao mpya”.

***

II- WAKRISTO:

Tumeelezea namna ubatizo ulivyokuwa kwa jamii za kipagani na sasa tutaeleza ulivyo kwa

Wakristo.

Injili ya Marko sura ya kwanza msitari wa 9: “Ikawa siku zile, Yesu alikuja kutoka Nazareti ya

Galilaya, akabatizwa na Yohana katika Yordani. Mara alipopanda kutoka majini, akaona mbingu

zinapasuka, na Roho, kama hua, akishuka juu yake”.

Injili ya Mathayo, sura ya 3, msitari wa 11:

“Kweli mimi ( yaani Yohana) nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma

yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa

Roho Mtakatifu na kw Injili ya Marko, sura ya 16, msitari wa 16: “Aaminiye na kubatizwa

ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”, [pia vipengele vya 13 – 17 katika sura hii vinaelezea

ubatizo. Ubatizo umetajwa katika Injili ya Luka 111

, Injili ya Yohana, sura ya tatu, msitari wa 22,

23 na 26, pamoja na sura ya nne, msitari wa 1. Matendo ya Mitume 4: 1, Wakorintho wa

Page 59: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

59

kwanza sura ya 1 msitari wa 13, 14,16 na 17. ufunuo wa Yohana, Waraka wa Yohana kwa

Waefeso, waraka wake kw Waebrania, Wakorintho wa pili na nyingine nyingi, tumedokeza hizo

chache tu ili kutaka kufupisha.

SURA YA KUMI NA SABA

ULINGANISHO KATI YA KRISHNA NA YESU

(YASEMWAYO NA WAKRISTO KUHUSU YESU NA YASEMAWYO NA WAHINDU

KUHUSU KRISHNA)

WASEMAVYO WAPAGANI WA

KIHINDU KUHUSU KRISHNA MWANA

WA MUNGU

Krishna ni: “ Mkombozi, kafara, Mfariji,

mchungaji mwema, mpatanishi, mwana wa

Mungu na nafsi ya pili katika utatu

mtakatifu ambao ni Baba, Mwana na Roho

Mtakatifu”

1- Krishna alizaliwa na mwanamwali

Devaki, ambaye Mungu alimchagua kuwa

mama wa mwanaye kwa sababu ya

utakatifu na staha aliyokuwa nayo112

2 – Malaika walimtukuza Devaki mama wa

Krishna Mwana wa Mungu na kusema “

ulimwengu unapaswa kuona fahari kwa

mwana wa huyu mwanamke mtakatifu 113

3 – Watu walitambua kuzaliwa kwa Krishna

kutokana na nyota yake iliyoonekana

mbinguni 115

WASEMAVYO WAKRISTO KUHUSU

YESU KRISTO MWANA WA MUNGU

Yesu Kristo ni: Mkombozi, kafara, mfariji,

mchungaji mwema, mpatanishi, mwana wa

Mungu na nafsi ya pili katika utatu

mtakatifu

ambao ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu”

1- Yesu alizaliwa na mwanamwali Mariam,

ambaye Mungu alimchagua kuwa mama wa

mwanaye kwa sababu ya utakatifu na staha

aliyokuwa nayo.

2 – Malaika akaingia nyumbani kwake,

akasema ,salamu, uliyepewa neema.Bwana

yu pamoja nawe 114

3 – Alipozaliwa Yesu Kristo, nyota yake

ilionekana upande wa

mashariki ambayo kwayo watu walipata

kujua mahali alipozaliwa116

4 – Alipozaliwa Krishna, ardhi ilimtukuza

Mungu, mwezi ukaangza, roho zikaimba,

malaika wakashangilia kwa furaha na

mawingu yakaimba kwa ghani za ajabu117

5-Krishna alitokana na kizazi

Cha kifalme, lakini alizaliwa

Pangoni katika hali ya udhalili

na madhila 119

6- Alipozaliwa Krishna, mwanga mkubwa

uliangaza pango lote na uso wa Devaki

mamaye ukatoa

miale ya nuru ya utukufu 121

Page 60: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

60

7- Baada ya kumzaa akaanza kulia na

kuhuzunika juu ya mwisho mbaya wa

ujumbe wake, mara (mtoto) akaongea na

kumfariji123

8- Ng‟ombe walitambua kuwa

Krishna ni Mungu wakamsujudia

9- Watu walimuamini Krishna,

wakautambua uungu wake na kumpa

zawadi na msandali na manukato 126

4- Alipozaliwa Yesu Kristo, malaika

waliimba kwa furaha, na nyimbo na vinanda

vikasikika kutoka mawinguni 118

5- Yesu alitokana na kizazi cha

kifalme, ambapo wanamwita “mfalme wa

Wayahudi”, lakini

alizaliwa zizini katika hali ya

udhalili na madhila 120

6-alipozaliwa Yesu, nuru kubwa iliangaza

na kuwashangaza Yusufu na Mariamu.

7- Akiwa bado mtoto, Yesu Kristo

alimwambia mama yake, “ewe Mariam,

mimi ni Yesu Mwana wa Mungu, nimekuja

kaalivyokueleza malaika Gabriel

aliyetumwa Baba yangu kwako, ya kwamba

nimekuja kuukomboa ulimwengu”.

8 – Wachunga-kondoo walitambua kuwa

Yesu ni Mungu wakamsujudia 125

9- Watu walimuamini Yesu Kristo na

kuamini uungu wake na kumpa zawadi za

marhamu na manemane12

10 – Nared, Mtume wa Wahindu, alipopata

habari za kuzaliwa Krishna mwana wa

mungu, alikwenda kumuona ambapo

kutokana na vipimo Vyake vya

10 – alipozaliwa Yesu katika Bethelehemu

ya uyahudi katika zama za mfalme Herode,

tazama,

majusi kutoka mashariki, wakaja mpaka

Yerusalem wakisema: yu

nyota, alibaini kuwa ni mwana wa mungu 128

11- Alipozaliwa Krishna, Nanda,

mchumba wa Devaki, alikuwa mbali na

mfalme, kwani alikwenda

kwa mfalme kulipa kodi 130

12-Krishna alizaliwa katika mazingira ya

udhalili, na ufakiri japokuwa anatokana na

familia ya kifalme 132

13-Nanda aliye mchumba wa Devaki

mama Krishna, alisika wito kutoka

mbingunu ukimwambia, simama na

kamchukue mototo wa mamaye ukimbiye

nao mpaka Kakol na mvuke mto wa Jamnah

kwani mfalme ataka kumuua 134

14- mtawala wan chi aliposikia juu ya

kuzaliwa kwa Krishna mwana wa Mungu,

alimtafuta ili

amuangamize, na ili kufikia malengo yak e

aliamuru kuuliwa kwa watoto wote wa

kiume waliozaliwa katika usiku huo136

15-Jina la mji aliozaliwa Krshina ni Mitra,

na humo alifanya miujiza na, na mahali hapo

mpaka sasa panaheshimika Na Wahindi

wanaoabudu masanamu na kuamini kuwa

Krisna ni mwana wa Mungu na ni Mungu 138

Page 61: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

61

wapi yeye alizaliwa mfalme wa Wayahudi? 129

11-Alipozaliwa Yesu, yusufu mchumba wa

mamaye hakuwepo nyumbani, na alikuja

kwa mfalme ili kumlipa kodi 131

12- yesu Kristo alizaliwa katika hali ya

udhalili, na ufakiri japokuwa anatokana na

kizazi cha kifalme 133

13-Yusufu mchumba wa Maryam

alioteshwa ya kwamba amchukue mototo wa

mama yake na kukimbilia Misri kwani

mfalme anamtafuta amwangamize 135

14-Mtawala wa nchi aliposikia juu ya uzawa

wa Yesu mwana wa Mungu, alimtafuta ili

amuue, na ili kutekeleza azma yake,

aliamuru kuuliwa watoto wote waliozaliwa

usiku huo 137

15-Jina la mji aliohamia Yesu Kristo baada

huko Misri baada ya

betelehemu ni Mitriyah, na husemekana

kuwa humo alifanya miujiza mingi

16-Mtakatifu Rama alizaliwa muda mfupi

kabla ya Krisna kudhihiri katika mwili wa

kibinaadamu ambapo mfalme wa nchi

aliazia kumuuwa kama pia kumua Krishna 139

17- Krishna alilelewa na wachunga kondoo,

na alipoletwa Mitra alihitaji sana kupata

mafunzo, hivyo akaletewa mwalimu

mwenye utaalamu, na baada ya muda mfupi

aliweza kumpita mwalimu wake kwa elimu

na kumshinda katika mambo mengi ya

kielimu katika utaalamu wa ndani wa

Kisanskrit 140

18-Siku moja, nyoka aliwauma baadhi ya

wafuasi ambao Krishna

Alikuwa akicheza nao, akahuzunika sana

kwa kifo chao

na kuwatazama kwa jicho la uungu wake

wakafufuka na kuwa hai142

16-Yohana mbatizaji alizaliwa muda mfupi

kabla ya Kristo,

ambapo mfalme Rohede alitaka

kumuangamiza yohana na pia

kumuangamiza Yesu kristo. Yohana ndiye

alitabiri kuzaliwa kwaYesu Kristo

17- Yesu alipelekwa kwa mwalimu

Dhacchos ili apate kumfundisha,

akamwandikia alphabeti na kumwambia

Yesu, sema „A‟.Bwana Yesu akasema,

niambie kwanza maana ya herufi „A‟ nami

nitasema „B‟.Mwalimu

akamtisha Yesu kuwa atampiga. Yesu

akasimama na kutafsiri maana ya „A‟ na „B‟

na kumweleza kuhusu herufi zilizosimama,

zilizoinama na zilizoungana, pamoja na zile

zenye nukta na irabu, na zile zisizokuwa na

nukta, na kwa nini zimewekwa katika

mpangilio huo, na akaanza kumweleza

Page 62: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

62

mambo ambayo mwalimu hakuwahi

kuyasikia wa la kuyasoma 141

18- Yesu alipokuwa akicheza, mara, nyoka

akamuuma mmoja wa watoto aliokuwa

akicheza nao, na hapo Yesu akamshika yule

mtoto kwa mkono wake akarudi kuwa

mzima 143

19- Ishara na miujiza ya mwanzo

aliyoitenda Krishna ni kuponya ukoma 144

20- mwanamke kikongwe aliletwa mbele ya

Krishna, akiwa na chombo chenye

manukato, mafuta, msandali, zafarani na

aina nyingine za manukato na kumpaka

Krishna mashavuni kwa alama maalumu na

kisha kuimimina illiyobaki kichwani

mwake146

21- Krishna alisulubiwa na kufa msalabani

22- Krishna alipokufa yalitokea masaibu

mbalimbali na ishara kuu, mwezi

ukazungukwa na duara jeusi , jua likapoteza

nuru yake wakati wa mchana, mbingu

ikadondosha moto na majivu, miale ya moto

mkali ikatokea, mashetani wakawa

wanafanya uharibifu katik ardhi, na watu

wakashuhudia maelfu ya viumbe

wakipigana angani usiku na mchana, na

hayo yalionekana kila mahali148

23- Krishna alichomwa mkuki ubavuni

mwake 150

24- Krishna akiwa katika hali ya kusulubiwa

alimwambia mwindaji aliyemchoma mkuki

hali ya kuwa:

19- miujiza ya mwanzo aliyoitenda Yesu

Kristo ni kuponya ukoma 145

20- Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika

nyumba ya Simoni mkoma, mwanamke

mwenye kibweta cha marhamu ya thamani

kubwa akaimimina kichwani pake alipoketi

chakulani147

21- Yesu alisulubiwa na kufa msalabani

22- alipokufa Yesu yalitokea masaibu

mbalimbali, pazia la hekalu likapasuka

kutoka juu mbinguni, jua likapoteza nuru

yake tangu saa sita mpaka saa tisa, makaburi

yakafunguliwa na wengi katika watakatifu

wakafufuka kutoka makaburini mwao149

23- Yesu alichomwa mkuki ubavuni mwake 151

24- Yesu alimwambia mmoja wa wezi

waliosulubiwa pamoja naye:

Nenda mbinguni ewe mwindaji kwenye

makazi ya miungu ukiwa umezungukwa na

rehema zangu152

25- Krishna alikufa kisha akafufuka katika

wafu154

Page 63: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

63

26- Krishna aliteremka kuzimu156

27- Krishna alipaa mbinguli kwa mwili

wake ambapo wengi walimuoana akipaa 158

28- Siku za mwisho, Krishna atarudi

duniani, na ataonekana akiwa akiwa juu ya

farasi mwenye kuzatitiwa kwa silaha, na

wakati wa kuja kwake jua na mwezi

vitapoteza nuru na ardhi itatetemeka na

kutikisika na nyota zitadondoka kutoka

mawinguni160

29- siku za mwisho Krishna atawahukumu

wafu162

30- wanasema kuwa Krishna ndiye Muumba

wa kila kitu, na pasipokuwa yeye

kisingekuwapo chochote katika

vilivyokuwapo, kwa hiyo yeye ni muumba

wa milele164

31- Krishna ndiye Alfa na Omega, mwanzo,

katikati na mwisho wa kila kitu

“amin, nakwambia, leo hivi utakuwa pamoja

nami peponi”153

25- Yesu alikufa kisha akafufuka katika

wafu 155

26- Yesu aliteremka kuzimu157

27 – Yesu alipaa mbinguli kwa mwili wake

ambapo wengi walimuoana akipaa159

28- Siku za mwisho, Yesu atarudi duniani,

na ataonekana akiwa akiwa juu ya farasi

mwenye kuzatitiwa kwa silaha, na wakati

wa kuja kwake jua na mwezi vitapoteza

nuru na ardhi itatetemeka na kutikisika na

nyota zitadondoka kutoka mawinguni161

29- siku za mwisho Yesu atawahukumu

wafu163

30- wanasema kuhusu Yesu Kristo kuwa

ndiye Muumba wa kila kitu, na pasipokuwa

yeye kisingekuwapo chochote katika

vilivyokuwapo, kwa hiyo yeye ni muumba

wa milele165

31- Yesu ndiye Alfa na Omega,

mwanzo, katikati na mwisho wa kila kitu 166

32- Krishna alipokuwa ardhini alipambana

na viumbe waovu bila kujali madhara

yanayoweza

kumpata, na akaeneza mafundisho wake

kwa kutenda maajabu na miujiza, kama vile

kufufua wafu, kuponya wenye ukoma,

viziwi na vipofu, pamoja na kumsaidia

mnyonge dhidi ya muonevu, na

aliyedhulumiwa dhidi ya dhalimu. Na

wakati huo walikuwa wakimuabudu,

wakisongamana kwake na walikuwa

wakimchukulia kuwa ni Mungu 167

. 33- Krishna alikuwa akimpenda

mwanafunzi wake Arjuna kuliko wanafunzi

wake wengine169

34- Mbele ya Arjuna lilibadilika umbile la

Krishna, uso wake ukang‟ara kama jua,

utukufu wa ukuu ukakusanyika ndani ya

Krishna mungu mkuu, na hapo Arjuna

akainamisha kichwa chake kwa

unyenyekevu na woga, akaifunga mikono

yake na kusimama kwa heshima na kusema,

sasa nimeuona uhalisia wako kama ulivyo,

nami nataraji rehma zako ewe bwanawa

mabwana, basi rudi na ujionyeshe katika

ubinaadamu wako, wewe ndiye mwenye

ufalme wote 171

Page 64: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

64

32- Yesu alipokuwa ardhini alipambana na

viumbe waovu bila kujali madhara

yanayoweza kumpata, na akaeneza

mafundisho wake kwa kutenda maajabu na

miujiza, kama vile kufufua wafu, kuponya

wenye ukoma, viziwi na vipofu, pamoja na

kumsaidia mnyonge dhidi ya muonevu, na

aliyedhulumiwa dhidi ya dhalimu. Na

wakati huo walikuwa wakimuabudu,

wakisongamana kwake na walikuwa

wakimchukulia kuwa ni Mungu 168

33- Yesu alikuwa akimpenda mwanafunzi

wake Yohana kuliko wanafunzi wake

wengine 170

34- Baada ya siku sita Yesu akawatwaa

Petro, Yakobo na Yohana nduguye,

akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;

akageuka sura yake mbele yao, uso wake

ukang‟ara kama jua, mavazi yake yakawa

meupe kama nuru… Alipokuwa katika

kusema, tazama, wingu jeupe likawatia

uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile

wingu ikisema, Huyu ni mwanangu,

mpendwa wangu ninayependezwa naye,

msikieni yeye, na wale wanafunzi

waliposikia, walianguka kifulifuli,

wakaogopa sana 172

35- Krishna alikuwa mbora wa watu kwa

tabia na maumbile. Alitoa mafundisho na

ushauri kwa Moyo mkunjufu. Naye ndiye

msafi na mwenye staha, aliye mfano kwa

mwanadamu. Alikubali mateso kwa sababu

aliwapenda

watu, na aliwatawadha Wabrahma miguu,

naye ndiye kuhani mkuu, mwenye uweza

aliyejionyesha kwetu katika mwili wa

kibinadamu173

36- Krishna ndiye Brahma Mungu mkuu, na

kuonekana kwake katika mwili ni siri katika

siri za uungu wake wa ajabu 175

37- Krishna ni nafsi ya pili katika utatu

mtakatifu kwa Wahindu wa kipagani

wanaoamini uungu wake177

38- Krishna alimwamuru yule atakayee

imani kwa moyo mmoja, aziache mali zake

na vyote avipendavyo na kuvitamani katika

ufalme wa ulimwengu huu na aende mahali

pasipokuwa na watu na ziweke fikra zake

kwa Mungu tu 179

39- Krishna alimwambia mwanafunzi wake

mpendwa Arjuna kuwa, lolote ufanyalo,

chochote utoacho kumpa masikini, chochote

unachokula, na sadaka

35- Yesu alikuwa mbora wa watu kwa tabia

na maumbile. Alitoa

mafundisho na ushauri kwa moyo

mkunhjufu. Naye ndiye msafi na mwenye

staha, aliye mfano kwa mwanadamu.

Alikubali mateso kwa sababu aliwapenda

watu, na aliwatawadha wanafunzi miguu

naye ndiye kuhani mkuu, mwenye uweza,

mwenye uweza aliyejionyesha kwetu katika

mwili wa kibinadamu 174

.

36- Yesu ndiyeYehova Mungu mkuu, na

kuonekana kwake katika mwili ni siri katika

siri za uungu wake wa ajabu 176

37- Yesu Kristo ni nafsi ya pili katika utatu

mtakatifu kwa imani ya Wakristo178

Page 65: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

65

38- Yesu alimwamuru kila atakaye imani

kwa moyo mmoja afanye yafuatayo, “ Basi

wewe usalipo, ingia katika chumba chako

cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako,

usali mbele za Baba yako aliye sirini; na

Baba yako aonaye sirini atakujazi180

39- Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo

neon lolote, fanyeni yote kwa utukufu wa

Mungu182

yoyote uitoayo

na mambo yoyote mema uyafanyao, basi na

yawe kwa ajili yangu, mimi ndiye 181

40- Krishna alisema, Mimi ndiye chanzo cha

uwepo wa viumbe, katika mimi vilikuwepo,

na katika mimi kila kitu kinaishi, na vitu

vyote ulimwenguni vinanitegemea mimi na

kufungamana na mimi kama lulu katika uzi

(sindano)183

41- Krishna alisema: “Mimi ndimi nuru iliyo

katika jua na mwezi, nami ndiye nuru iliyo

katika moto, nami ndimi nuru ya kila

kiangazacho na nuru ya nuru zote, kwangu

hakuna giza”185

42- Krishna alisema: Mimi ndimi mlinzi,

Bwana, kimbilio na njia ya ulimwengu187

43- Krishna alisema: Mimi ndimi wa

kwanza, katikati, mwisho na wa milele,

nami ndiye muumba wa vyote, nami ndiye

nitakaye 189

40- kila kitu chatokana na Yesu, katika Yesu

na kwa ajili ya Yesu

“vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo

yeye hakikufanyika chochote

kilichofanyika”184

41- Basi Yesu akawaambia tena akasema,

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye

anifuataye hatakwenda gizani”186

42- Yesu akamwambia: Mimi ndimi njia, na

kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba ili kwa

njia ya mimi188

43- Yesu akasema: Mimi ni wa kwanza na

wa mwisho … Nami ninazo funguo za

mauti, na za kuzimu 190

Haya ni machache katika yale yaliyoelezwa na waumini hao

Page 66: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

66

SURA YA KUMI NA NANE

ULINGANISHO KATI YA BUDDHA NA YESU

(YASEMWAYO NA WAKRISTO KUHUSU YESU NA YASEMAWYO NA WAHINDU KUHUSU

BUDDHA)

WASEMAVYO WAPAGANI WA

KIHINDU KUHUSU BUDDHA MWANA

WA MUNGU

WASEMAVYO WAKRISTO KUHUSU

YESU KRISTO MWANA WA MUNGU

1- Buddha alizaliwa na Bikira Maya pasipo

kulala na mwanaume yeyote191

2- Buddha alijibadilisha katika mwili kupitia

roho mtakatifu aliyeingia katika mwili wa

Bikira Maya193

3- Buddha alipoteremka na kuingia katika

mwili wa Bikira Maya, kizazi chake

Gautama Buddha

Page 67: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

67

kilikuwa kama kioo king‟aracho, ambapo

Buddha alionekana humo kwa mfano wa ua

zuri 195

4- Nyota iliyoonekana upande wa mashariki

ndiyo iliyojulisha kuzaliwa kwa Buddha,

nyota hiyo huiita “nyota ya Kristo” 197

5- Buddha alizaliwa na bikira Maya,

aliyetokewa na roho mtakatifu, tarehe 25

mwezi wa 12.199

6- alipozaliwa Buddha, majeshi ya mbinguni

yalifurahi, malaika wakaimba mtoto

aliyezaliwa nyimbo utukufu wakisema: “

leo duniani amezaliwa Buddha ili awape

watu furaha na amani, na aangaze kwenye

giza na awape vipofu machio”201

7- Makuhani na wakuu wa dini

walimtambua Buddha na kuona siri ya

uungu wake, ambapo haikupita hata siku

moja baada ya

1- Yesu Kristo alizaliwa na Bikra Mariam

pasipo kulala na mwanaume yeyote 192

2- Yesu Kristoalijibadilisha katika mwili

kupitia roho mtakatifu aliyeingia katika

mwili wa Bikira Mariam194

3- Yesu alipoteremka na kuingia katika

mwili wa Bikira Mariam,

kizazi chake kilikuwa kama kioo

king‟aracho, ambapo Yesu alionekana humo

kwa mfano wa ua zuri 196

4- nyota iliyoonekana upande wa mashariki

ndiyo iliyojulisha kuzaliwa kwa Yesu

(bwana Doane anasema kuwa ni lazima

nyota hiyo iitwe “ nyota ya Kristo”) 198

5- Yesu alizaliwa na bikira Mariam,

aliyetokewa na roho

mtakatifu, tarehe 25 mwezi wa 12200

6- alipozaliwa Yesu, malaika wa mbinguni

walifurahi na kumwimbia mtoto nyimbo za

utukufu wakisema: “atukuzwe Mungu juu

mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu

aliowaridhia”202

. 7- Yesu alitembelewa na Makuhani ambao

waliitambua siri ya uungu wake wakamwita

MUNGU204

kuzaliwa kwake watu wakamsabahi na

kumwita MUNGU 203

8-wakampa mtoto Buddha zawadi za

dhahabu vya na vitu vingine vya thamani205

9- Buddha akiwa bado mtoto mchanga

alimwambia mamaye Maya kwamba yeye ni

mkuu wa watu wote.207

10- Buddha alikuwa mtoto hatari kwa

utawala wa mfalme ambaye alifanya juhudi

zote ili kumwangamiza baada ya kuambiwa

kuwa mtoto yule atauangusha ufalme wake

ikiwa ataendelea kuwa hai209

11- Buddha alipopelekwa shule

aliwashangaza walimu, pamoja na ukweli

kwamba hakuwahi kusoma hapo kabla

lakini aliwashinda wote katika uandishi,

hesabu, falsafa, na ukuhani 211

12- Budha alipopata umri wake miaka kumi

na miwili aliingia katika mahekalu akawa

anawauliza

Maswali magumu, kisha, akawafafanulia

hata akawashinda wanamjadala wote 213

Page 68: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

68

8- na wakampa mtoto Yesu zawadi za

dhahabu, marham na manemane206

9- Yesu akiwa mtoto mchanga alimwambia

mamaye Mariam “mimi ni mwana wa

Mungu”208

10- Yesu alikuwa mtoto hatari ambaye

mfalme Herode alifanya kila juhudi

kumuangamiza ili asije akauangusha

utawala wake 210

11-Yesu alipopelekwa shule alimshangaza

mwalimu wake, akamwambia Yusufu

babaye: umeniletea mtoto ili nimfundishe

japokuwa anaujuzi kuliko Walimu wote, na

wote waliosikia walishangazwa kwa uelewa

na ufahamu wake 212

12-Yesu alipopata umri wa miaka kumi na

miwili walimpeleka hekaluni huko

Yerusalemu, akawa anawauliza walimu

maswali magumu, na kuwafafanulia na

kuwashangaza wote 214

13-Siku moja Budha aliingia moja ya

mahekalu,mara masanamu yakasimama

kutoka mahali pake yakajinyoosha miguuni

mwa Budha na kumsujudia 215

14-Nasaba ya Gautama budha kutoka kwa

Baba yake Sadodama, huifungamanisha na

watu mbalimbali, wote wakitokana na kizazi

cha kifalme mpaka kwa adamu Baba wa

wanadamu,na majina na matukio mengi

hutajwa katika kizazi chake yameelezwa

katika Tourati ya Mayahudi. Na hakuna na

uwezekano wa kupata uhakika wa visa vyao,

kutokana na kukizana ndani mwake,

kwasababu wanahistoria wa kibudha

wanaingiza majina na makabila na kubuni

majina yanayowawezesha kutukuza nasaba

ya kiongozi wao kwasababu ya kumchukulia

kama Mungu 216

15- Budha alipotoka kufanya ibada

alitokewa na Maara (yaani shetani) ili

kumtia majaribuni 218

16-Maara alimwambia Budha :

“Usiyaharibu maisha yako katika shughuli

za dini, kwani kwa kipindi cha siku saba

waweza kuwa mfalme wa dunia” 220

17-Budha hakuyasikilza maneno ya shetani

bali alimwambia: “ondoka kwangu” 222

13-sikumoja Yesu alipita karibu na vibao

vya matangazo, nayo matangazo yaliinama

na kusujudia

14-Nasaba ya Yesu kutoka kwa baba yake

Yusufu hufungamana na maisha na watu

mbalimbali wote wakitokana na kizazi cha

kifalme mpaka kwa Adamu, na majina ya

kizazi chake yametajwa katika tourat ya

wayahudi na haiwezekani kupata uhakika

wa visa hivyo kutokana na kukinzana ndani

yake, kwasbabu wanahistoria wa kikristo

walibuni majina kwa lengoo la kuitukuza

nasaba ya kiongozi wao kwa sababu ya

kuamini kuwa ni Mungu 217

15-Yesu alipoanza kuhubiri alitokewa na

shetani ili amtie majaribuni 219

Page 69: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

69

16-Shetani akamwambia Yesu: Nitakupa

haya yote ikiwa utaanguka kunisujudia 221

17-yesu akamwambia akisema: “Ondoka

shetani we! 223

18- Maara alipoacha kumjaribu Budha,

mbingu ilinyesha maua na marham yalienea

angani224

19-Budha alifunga kwa kipindi kirefu 226

20- Budha mkombozi alibatizwa, na wakati

wa kubatizwa kwa maji roho wa Mungu

alikuwapo, Naye hakuwa Mungu mkuu

pekee bali roho mtakatifu ambaye katika

yeye, Gamtama alipata kuwa katika mwili

alipomtokea bikira Maria 228

21-Budha alipokuwa ardhini katika siku

zake za mwisho umbile lake lilibadilika

alipokuwa juu yamlima wa bendaqa,na

ghafla nuru ikamzunguka kichwani mwake

kwa namna ya taji. Wanasema kuwa mwili

wake ulitoa nuru Kali, ikawa kama sanamu

la dhahabu likang‟ara kama jua au kama

mwezi, akabadilika katika sehemu tatu

zenye kuangaza, Mashuhuda walipoona

mabadiliko haya

na hapo walisema: huyu sio binadamu!Bali

ni Mungu mkuu230

22-Budha alitenda maajabu na mijiza kwa

ajili ya watu, na visa vyote vinavyoelezea

mambo hayo vitaja maajabu zaidi ya

inavyoweza kufikiriwa 232

18- kisha Ibiliisi akamwacha, na tazama,

malaika wakaja wakamtumikia..225

19-Yesu alifunga kwa kipindi kirefu 227

20- yohana alimbatiza Yesu katika mto

Yordani, na Roho wa Mungu alikuwapo,

naye hakuwa Mungu mkuu pekee, bali na

roho mtakatifu ambaye katika yeye

ulifanyika mwili wake pindi alipomtokea

bikira Maria hivyo naye ndiye baba, mwana

na Roho mtakatifu 229

21-Yesu alipokuwa ardhini alibadilika

umbile lake, na baada ya siku sita yesu

akatwaa Petro na Yakobo na Yohana

ndguye, akawaleta juu yam lima mrefu

faraghani. Akageuka sura yake mbele yao,

uso wake ukang‟ara kama jua, mavazi yake

yakawa meupe kama nuru 231

22-yesu alitenda maajabu na miujiza kwa

ajili ya watu woye, ambapo simulizi za

matukio

hayo zimejaa maajabu zaidi ya inavyoweza

kufikirika 233

23- Katika maombi yao kwa Budha,

waumini hutarajia kuingia Pararadiso 234

24-Budha alipokufa na kuzikwa, sanda

ilipasuka na kaburi likafunguka kwa nguvu

ya kimungu236

25-Budha alipokamilisha kazi zake duniani,

alipaa kwa mwili wake kuelekea mbinguini 238

26- Budha atarudi duniani kwa mara

nyingine ili kurudisha amani na baraka

pamoja na kuwahukumu wafu.240

Page 70: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

70

27- Budha ndiye Alfa na Omega, hana

mwanzo wala mwisho, naye ndiye Mungu

Mkuu na wa milele242

28- Buddha alisema, nitabeba dhambi zote

zilizotendeka hapa duniani ili ulimwengu

ukombolewe kutokana na dhambi244

29- Buddha alisema, ficheni mambo

matendo mema myatendayo na mkubali

dhambi zenu waziwazi 246

30- Buddha alisema kuwa hakuja kutangua

Taurat, bali alikuja kuitimiliza, na

alifurahishwa kuwa mmoja wa walimu 248

23- Katika maombi yao kwa yesu, waumini

hutaraji kuingia paradise kwa Uungu wake. 235

24- Yesu alipokufa na kuzikwa, sanda

ilipasuka na kaburi likafunguka kwa kwa

nguvu za ajabu237

25-Yesu alipokamilisha kazi zake za

duniani, alipaa kuelekea mbinguni baada ya

kusulubiwa239

26- Yesu atarudi duniani kwa mara nyingine

ili kurudisha amani na baraka pamoja na

kuwahukumu wafu.241

27- Yesu ndiye Alfa na Omega, hana

mwanzo wala mwisho, naye ndiye Mungu

Mkuu na wa milele243

28- Yesu ni mkombozi wa ulimwengu

ambaye alikubali kubeba dhambi zote

badala ya wale waliozitenda ili ulimwengu

ukombolewe kutokana na dhambi245

29- Yesu alisema, ficheni matendo mema

myatendayo na mkubali makosa yenu

waziwazi 247

30- Yesu alisema, “Msidhani ya kuwa

nalikuja kuitangua torati au manabii; la,

sikuja kutangua, bali kutimiliza” 249

31- Kutokana na mafundisho ya Budha,

maisha yetu pamoja na ndugu na majirani

zetu lazima yawe kwa wema na mapendo 250

32- Siku za mwanzo za mahubiri, alikwenda

katika mji wa Pinaris, akafundisha huko,

akafuatwa na Kondania kisha akafuatwa na

wanaume wangine wengine na wote

wakawa wake, na tokea wakati huo, popote

alipokwenda alifuatwa na wanaume na

wanawake wengi ambao walikuja kuwa

wafuasi na wanafunzi wake252

33- Buddha aliwaambia wanafunzi wake

kuwa waiache dunia na mali zao na waishi

maisha ya ufakiri na umasikini 254

34- imeelezwa katika vitabu vya dini ya

kibuddha kuwa Waandishi walitaka ishara

kutoka kwa Buddha ili wapate

kumwamini256

35-malengo ya Buddha yalikuwa katika

kujenga mamlaka ya kidini, yaani mamlaka

kutoka mbingu 258

36- katika mafundisho ya dini ya kibudha,

wanasema kuwa “ mtu akipatwa na huzuni,

machungu, balaa na kukata tama ni dalili

kuwa alifanya madhambi hapo kabla au

sasa hivi ambayo yanamgharimu 260

31- Yesu alisema, lakini mimi nawaambia,

Wapendeni, adui zenu, waombeeni

wanaowaudhi”251

32- Siku za mwanzo za mafundisho na

mahubiri ya Yesu, alikwenda katika mji wa

Page 71: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

71

Kapernaum, kahubiri huko, watu wengi

wakamfuata na kuwa

wanafunzi wake, na tokea wakati huo,

popote alipokwenda alifuatwa na wanaume

na wanawake wengi ambao walikuja kuwa

wafuasi na wanafunzi wake 253

33- Yesu aliwaambia wale waliomfuata

kuwa waache mali zao na waishi maisha ya

ufakiri255

34- imeelezwa katika vitabu vya dini ya

kikristo kuwa waandishi na

mafarisayo walitaka ishara kutoka kwa Yesu

ili wamwamni 257

35-tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri,

na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa

mbinguni umekaribia 259

36- Hata alipokuwa akipita alimwona mtu,

kipofu tangu kuzaliwa. Wanafunzi wake

wakamwuliza wakisema, Rabi, ni yupi

aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi

wake, hata azaliwe kipofu? 261

37- katika kitabu kiitwacho somadeva kuna

simulizi iliyoandikwa na mmoja wa

watakatifu wa kibudha kwamba Krishna

aliling‟oa jicho lake na kulitupa, kwani

lilikuwa likimsumbua 262

37- jicho lako la kuume likikukosesha,

ling‟oe ulitupe mbali nawe 263

Page 72: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

72

Miongoni mwa majina na lakabu ambaazo huzitumia kwa Buddha ni:

Saaqiya Sanja ( yaanai simba wa kabila la Saaqiya), Saaqiya Moni (yaani mkuu wa kabila la

Saaqiya), Sogata (mtukufu), Saatha (mwalimu), gina (mshindi), Bihakafad (aliyebarikiwa),

Lokanatha (bwana wa ulimwengu), Sarmagina (mwenye kuwapo), dharmaraja (mfalme wan

chi), mwenye kutoa furaha, mungu wa vyote, mkuu, wa milele, muondoshaji wa taabu na

machungu, mlinzi wa ulimwengu, kielelezo cha rehma, mwokozi wa watu, mungu kati ya

miungu, masihi, mwana wa pekee, njia ya uzima, na majina mengine mengi yaliyopo katika

mlolongo huo.

Yesu naye pia hupewa sifa na majina kama aliyopewa Budha, na tumeonelea kuwa ni vyema

kuyateja kwa mara nyingine ikiwa ni pamoja na kutaja mahali yanapopatikana ili iwe rahisi kwa

msomaji kurejea huko na kufanya ulinganisho wakati atakapo kufanya hivyo.

Simba wa kabila la Yuda 264

, mkombozi 265

, mzawa wa pekee 266

, mtakatifu wa Mungu 267

,

mungu mwenye kuhimidiwa milele 268

, mwana-kondoo wa Mungu 269

, bwana wa utukufu 270

,

muumba wa vyote 271

.

Miongoni mwa majina maarufu ni: kafara, mkombozi, mpatanishi, neon, mwanakondoo wa

Mungu, mwana wa Mungu, mzawa wa pekee, na majina mengine mengi.

VITABU REJEA:

1-Allen: Indian Ancient and Moder

2- Amberly:Analysis of religious belief

3- Kowenio: (a) Ancient Faiths,

(b)Asiatic Reserches

4- Beal - The romantic Legend of Saki Buddha from Chinese Sanskrit

5- Bonwick: Egyptian Belief and Modern Thought

6- Davis: (a) Buddhism

(b) The Chinese

7-Bunsen: Angel Messiah

8- Doane: Bible Myths and their Parellels in other Religions

9-Dunlap: Vestiges of Spirir History of Man

10- Dupis: The Origin of All Religious Worship

11- Faber: The Life of Christ

12- Fergusson: Tree and Serpent Worship

13- Fiske: Myth and myth makers

14- Frontingham: The Cradle of Christ

Page 73: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

73

15- Gangooly: Life and Religion of The Hindoos

16- Geickic: Life of Christ

16- Gergoius: Tibetinum Alphabetum

17- Gibbon: The History of the Decline of the Roman

18- Guingniaut: Monumental Christanity

19- Hardy: The Legends and Theories of the Buddhism

20- Hebrew Lexicon

21- Holy Bible

22- Higgins: The Celtic Druids

23- Huxley: Evidence as to Man‟s Place in Nature

24- Helsly Stevens: Faith and Reason

25- Inman: Ancient Pagan and Modern Christian Symbolism

26- Jameson: the History of Our Lord

27- Kingsborough: Antiquities of mexico

28- knight: The Symbolical language of Ancient Art and Mythology

29- Lundy: monumental Christianity

30- Lillie: Buddha and Early Buddism

31- Maurice: (a) Indian Antiquities

(b) The History of Hindostan

32- Muller: History of Ancient Sanskrit Literature

33- Murray: (a) Manual of Mythology

(b) oriental Religions

34- Prescott: History of the Conquest of Mexico

35- Prichard: (a) An Analysis of the historical Records of Ancient Egypt

(b) Progress of Religious ideas

36- Squire: The Serpent Symbol

37 Vishnu Purama (imetafsiriwa kutoka Kisanskrit) na Bwana Wilson

38- William: Indian Wisdom

39- Hinduism

88. The History of Buddhism, ukurasa wa 23 na 33.

89. The Chinese, juzuu ya 1, ukurasa 173.

90. Analysis of religious belief, ukurasa 227.

91. Life of Christ, juzuu ya 1, ukurasa 144.

92. Analysis of the Historical Records of Ancient Egypt, ukurasa wa 56.

93. Egyptian Belief, ukurasa wa 325.

94. Socrates alizaliwa mnamo mwaka 470 BC, na kufa mwaka 399 BC mjini Athena. Binaadamu

kuitambua nafsi yake ndio uliokuwa mhimili wa falsafa za Socrates.

Page 74: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

74

95. Tiber: ni mto ulioko katikati mwa Italia, unaanzia katika milima ya Ebnin na kuelekea

upande wa magharibi na kumwaga maji yake katika bahari ya Titani, na pembezoni mwake kuna

mji wa Roma.

96. Luka 2: 8- 11: na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda

kundi lao kwa zamu usiku. Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, utukufu wa Bwana

ukawang‟aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, msiogope; kwa kuwa

mimi nanawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika

mji wa Daud amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana…‟.

97. Injili ya Mathayo, sura ya 1, msitari wa 1: “ kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa

Daudi, mwana wa Ibrahimu.

98. Injili ya Luka, sura ya 1, msitari wa 26- 27: Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na

Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa

ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi”.

99. Katika kitabu chake kiitwacho: Life and Religion of Hindoos, ukurasa wa 134.

100. kitabu chake kinaitwa : Torah Lexicon

101. Marko, sura ya 16, msitari wa 6: “Naye akawaambia, msistaajabu; mnamtafuta Yesu

Mnazareti, aliyesulubiwa; amefufuka; hayupo hapa”.

102. Luka 24, msitari wa 6: “… kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu? Hayupo hapa,

amefufuka”.

103. Yohana, sura ya 20, msitari wa 1- 18. miongoni mwa yaliyoelezwa humo ni: “…kwa maana

hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka….”.

104. miongoni mwa ishara zilizotajwa katika sura hii (Injili ya Mathayo 24: 29) ni: “…jua

litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za

mbinguni zitatikisika; ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni..”.

105. Amberly, katika kitabu chake kiitwacho: Analysis of religious belief, ukurasa wa 61.

106. Bunsen, katika kitabu chake kijulikanacho kama: The Angel Messiah, uk. 42.

107. Higgins, katika kitabu chake, The Celtic Druids, j. 2, uk. 69.

108. Lillie – Buddha and Early Buddhism, ukurasa wa 55 na 134.

109. Doane, katika kitabu chake kilichotajwa mwanzo, uk. 320.

110.Prescott- History of the Conquest of Mexico.

111. Luka 3: 3: “Akafika nchi yote iliyo karibu na Yordani, akihubiri ubatizo wa toba liletalo

ondoleo la dhambi”.

112. Doane, uk. 278.

113. The History of Hindostan, j. 2, uk.329.

114. Luka 1: 28-29.

115. The History of Hindostan, j. 2, uk.317 na 336.

116. Mathayo 2:1-2.

117. Visnu Purana, ukurasa wa 502.

118. Luka 2:13.

Page 75: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

75

119, 120, 121.Doane, ukurasa 279.

122. Injili ya uzao wa Yesu Kristo, 12: 13.

123. The History of Hindostan, j. 2, uk.311.

124. Doane, uk.279.

125. Luka, 2: 8-10.

126. Oriental religions, uk.500, na Ancient religions, j.2 uk.353.

127. Mathayo, 2:2.

128. The History of Hindostan, j. 2, uk.317.

129. Mathayo, 2: 1-2.

130. Vishnu Purana, sura ya pili ya kitabu cha tano.

131. Luka 2:1-17.

132. Asiatic Research, j.1 uk.259, na The History of Hindostan, j.2 uk.310.

133. . Angalia mlolongo wa nasaba yake katika Injili za Mathayo na Luka na ni kwa hali gani

kazaliwa.

134. Vishnu Purana, sura ya 3

135. Mathayo, 2:13

136. Doane, uk.280.

137. Mathayo sura ya 2.

138. The History of Hindostan, j. 2, uk.317. na Asiatic Research, j.1, uk.259.

139. Inijlut tufuoliyyah, kilichotungwa na Bwana Higgins.

140. Doane, uk.280, na The History of Hindostan, j. 2, uk.321.

141. Injilut Tufuoliyyah, sura ya ishirini, msitari wa 1-8.

142. The History of Hindostan, j. 2, uk. 343.

143. Injilut Tufuoliyyah, sura ya 18.

144. The History of Hindostan, j. 2, uk. 319.

145. Mathayo 8:2.

146. The History of Hindostan, j. 2, uk. 320.

147. Mathayo 26: 6-7.

148. progress of Religious Ideas, j. 1, uk. 71.

149. Mathayo sura ya ishirini na saba, vilevile, Injili ya Luka sura ya ishirini na tatu.

150. Doane, uk.282.

151. Doane, uk.283.

152. Vishnu Purana, uk.612.

153. Luka, 23:43.

154. Doane, uk.282.

155. Mathayo, 28: 7.

156. Doane, uk.282.

157. Doane, uk.282, na vilevile, vitabu vya imani ya Wakristo n.k.

158, 160 na 164. Doane, uk.282.

159 na 1661. Mathayo, sura ya 24.

162 na 167.Doane, uk.283.

Page 76: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

76

163. Mathayo, 24:31, na Warumi 14:10.

165. Yohana, 1:1-3, na 1Wakorinto 8:6 pamoja na Waefeso 3:9.

166. Ufunuo wa Yohana, sura ya 1, msitari wa 8, na sura ya 22 msitari wa 13, na sura ya

21 msitari wa 6.

168. Tazama Injili ili kupata vifungu zaidi ya tulivyovitaja.

169. Bihakfat.

170. Yohana 13:23.

171. Indian Religion, cha Bwana Maurice, uk.219.

172. Mathayo 17:1-9.

173. Indian Religion, cha Bwana Maurice, uk.144.

174. Yohana 13:6-15.

175. Vishnu Purana, ukurasa wa 492, katika ufafanuzi wa msitari wa 3.

176. 1Timotheo, sura ya 3.

177. Maurice katika kitabu chake kiitwacho Indian Antiquities, uk.10.

178. Tazama vitabu vyao vyote vya kidini pamoja Injili zote.

179. Indian Religion, uk.211.

180. Mathayo 6:6.

181 Maurice katika kitabu chake kiitwacho Indian Antiquities, uk.212.

182. 1Wakorinto 10:31.

183. Maurice katika kitabu chake kiitwacho Indian Antiquities, uk.312.

184. Yohana 1:1-3.

185 na 189 .Maurice katika kitabu chake kiitwacho Indian Antiquities, uk.213

186.Yohana 8:12.

187. Doane 283.

188. Yohana 14:6.

190. Ufunuo wa Yohana 1:17-18.

191. Wlliams, katika kitabu chake, Indian Religion, uk.82 na 108.

192. Mathayo 1:18-24.

193. Doane, uk.289 pamoja na kitabu cha Bunsen kiitwacho The Angel Messiah, uk.10 na 25.

194. Mathayo 1:21.

195. Bunsen katika kitabu chake kilichotajwa hapo juu, uk. 20 na Doane uk.290.

196. Katika kitabu cha Doane, ukurasa wa 290, na Bunsen katika The Angel Messiah, ukurasa

wa 20 pamoja na kitabu cha Amberly kiitwacho Analysis of religious belief, ukurasa wa 424.

197,200, 201, 203 na 205. Doane, ukurasa wa 290.

198. Mathayo 2:1-3.

199. The Angel messiah, uk.10.

202. Luka 2:13-14.

204. Mathayo 2:1-11.

206 Mathayo 2:11.

207. Hardy katika kitabu chake kiitwacho The Buddhism Belief, uk.145-146.

208. Injilut Tufouliyyah 1:3.

209. The History of Buddhism cha bwana Beal, uk.103 na 103.

210. Mathayo 2:1.

211. Hardy, The Buddhism Belief, Bunsen katika The Angel Messiah, pamoja na Beal katika

The History of Buddhism.

212 na 214. Luka 2:41- 48.

Page 77: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

77

213 na 215.The Angel messiah, uk.37. na History of Buddhism uk.67-69.

216 na 217. Doane, uk.291.

218, 232,234, 235, 238, 240, 242 na 245.Doane, 293. vilevile mafundisho ya kikristo.

219. Mathayo 4:1-18.

220, 222, 224 na 226. Doane, uk.292.

221. Mathayo1:11.

223. Luka 4:8 na Mathayo 4:10.

225. Mathayo 4:11.

227. Mathayo 4:2.

228 na 230. The Angel Messiah, uk.45, na History of Buddhism uk.177.

229. Mathayo 3:1-13.

231. Mathayo 17:1-2.

233. Mathayo 8:23-34.

236. The Angel Messiah, ukurasa wa 49.

237. Mathayo 28:6-8.

239 na 241.matendo ya mitume1:1-12.

243. Yohana 1:1, pamoja na ufunuo wa Yohana 1:8 na 21:6.

244. The History of Ancient Sanskrit Literature, ukurasa wa 80.

246. Muller katika Religious science, ukurasa wa 28.

247. Mathayo 6:1, pamoja na Yakobo 5:16.

248 The Angel Messiah, ukurasa wa 47-48, pamoja na Analysis of religious belief, ukurasa wa

285 n.k.

249. Mathayo 5:17.

250. The Religious science, ukurasa wa 249.

251. Mathayo 5:44.

252. Oriantal Monasticism, uk. 6.

253. Mathayo 4: 13-25.

254. Oriantal Monasticism, ukurasa wa 6 na 62.

255 Mathayo 8:19-20, na 16:25-28.

256. Religious Science, uk.27.

257. Mathayo 12:38.

258. History of Buddhism, uk.10.

259. Mathayo 4:17.

260. Buddhism, cha Davids, uk.103.

261. Yohana 9:1-2.

262.The religious Science, uk.245.

263. Mathayo 5:29.

264. Ufunuo wa Yohana 5:5.

265. Matendo ya mitume 7:35.

266. Waebrania 1:5-6.

267. Luka 4: 34, na matendo ya mitume 3: 14.

268. Ufunuo wa Yohana 71:14.

269. 1Wakorinto 2:8.

270. Ufunuo wa Yohana 17:14.

271. Yohana 2: 3 na 10, 1 Wakorinto 8: 56, na Wakolosai 1:16.

Page 78: Imani Za Kipagani Ndani Ya Ukristo

78