Upload
x-paster
View
763
Download
8
Tags:
Embed Size (px)
DESCRIPTION
Hakika idadi ya dini ambazo mwanadamu amejiunga nazo haihesbiki , zile zinazojulikana ni chache sana , na nyingi zinafanana moja kwa moja, na hazitofautiani isipokuwa katika majina ya miungu na katika baadhi ya vipengele ambavyo sio vya msingi. Sababu ya hali hiyo inatokana na ukweli kwamba kila alipokuja mtume yeyote alifuatwa na kaumu yake, na baada ya kifo chake kaumu hiyo, wakishirikiana pamoja na wafuasi wengine, walisimama na kuingiza katika mafundisho yake baadhi ya itikadi za kipagani walizokuwa wakiziamini kabla ya kuja kwake. Hawakuishia hapo , bali walichukua na kuingiza katika dini yao mambo na mafundisho ya dini nyingine za kipagani , kama yaliyotokea kwa Musa na wana wa Israil pale walipomuabudu ndama.Kwa kawaida ni kuwa dini hizi (walizokuja nazo mitume) zilikuwa ni taratibu ambazo Mwenyezi Mungu alimwekea mwanadamu kupitia mitume wake, ili apate kuishi na wenzake maisha ya amani na furaha, na apate kuunyanyua ubinaadamu. Au kwa maana nyingine , dini hizi , kwa kiasi fulani , zilikuwa ni kama kanunu za adabu na maadili zilizokusudia kujenga upendo , na kumtahadharisha mwanadamu kutokuwa na uadui kwa mwenzake. Hii ndiyo iliyokuwa hali ya dini walizokuja nazo mitume kutoka kwa Mwenyezi Mungu, nazo hazitofautiani katika chanzo na malengo. Binaadamu ameziharibu zaidi kwa kuingiza humo uzushi uliozushwa na mawazo yake mabovu , na akadanganywa na fikra zake za mwanzo.
Citation preview
1
IMANI ZA KIPAGANI KATIKA UKRISTO
MWANDISHI
Muhammad Taher bin AbdilWahhab bin Saleem At-Tanneer
MFASIRI
Ibrahimu H. Kabuga
2
YALIYOMO
Dibaji
Utangulizi
SURA YA KWANZA
Imani ya utatu kwa wapagani
Imani ya utatu kwa wakristo
SURA YA PILI
Kumtoa kafara mungu wa wapagani kwa ajili ya utakaso wa dhambi
SURA YA TATU
Wapagani na kiza kilichotokea kwa kufa mmoja wa wakombozi wa ulimwengu
Kiza kilichotokea kwa kifo cha Yesu
SURA YA NNE
Kuzaliwa miungu ya kipagani
Bikira Maria, mama wa mungu-Yesu
SURA YA TANO
Nyota zilizoonekana wakati wa kuzaliwa mungu wa kipagani
Nyota ya mashariki iliyoonekana wakati wa kuzaliwa kwa Yesu
SURA YA SITA
Majeshi yaliyodhihiri kutoka mbinguni na kumtukuza Mungu kwa kuzaliwa mungu wa kipagani
Majeshi ya mbinguni yakimtukuza Mungu kwa kuzaliwa Yesu
SURA YA SABA
Kuonyeshwa mungu-mtoto wa kipagani
Kuonyeshwa mungu-mtoto kwa wakristo
SURA YA NANE
Mahala walipozaliwa baadhi ya miungu wa kipagani
Mahala alipozaliwa Yesu kristo
SURA YA TISA
Imani ya kwamba miungu inayoonekana imetokana na kizazi cha kifalme
Imani ya wakristo kwamba yesu ametokana na kizazi cha kifalme
SURA YA KUMI
Imani ya wapagani kwamba watawala hutaka kuwaua miungu- watu
Imani ya kwamba Herode alitaka kumuua Yesu kristo
3
SURA YA KUMI NA MOJA
Majaribu ya shetani kwa watoto wa miungu ya kipagani
Majaribu ya shetani kwa Yesu
SURA YA KUMI NA MBILI
Kwenda kuzimu kwa watoto wa miungu ya kipagani
Yesu kwenda kuzimu
SURA YA KUMI NA TATU
Kufufuka kwa miungu hao
Kufufuka kwa Yesu
SURA YA KUMI NA NNE
Kurudi duniani kwa miungu- watu
Kurudi kwa Yesu
SURA YA KUMI NA TANO
Imani ya kwamba mwana ndiye Muumba
Imani ya kuwa Yesu ndiye muumba
.
SURA YA KUMI NA SITA
Imani ya ubatizo kwa ajili ya utakaso wa dhambi
Wakristo na ubatizo
SURA YA KUMI NA SABA
Ulinganisho kati ya Krishna na Yesu
SURA YA KUMI NA NANE
Ulinganisho kati ya Budha na Yesu kristo
VITABU REJEA
ORODHA YA FAFANUZI
DIBAJI
4
Muhammad Taher bin AbdilWahhab bin Saleem At-Tanneer, (aliyefariki 1352 A.H. / 1933
A.D), ni mhadhiri mwandamizi katika fani mbalimbali. Alizaliwa Beirut, na kupata elimu ya juu
katika chuo cha kimarekani, na alianzisha gazeti aliloliita Al – Muswawwir. Alielekea
Switzerland ambako alisoma katika moja ya vyuo vikuu vya huko na kisha akarudi nchini kwake
na kuishi katika kitongoji cha Ain Annub. Baadaye aliajiriwa katika ofisi ya gazeti la Ash Sharq
lililoasisiwa kwa amri ya Jamal Baashaa As Saffah. Alikimbia kupitia njia ya mlima wa Hawran
na kujiunga na jeshi la mapinduzi makubwa ya waarabu. Alikwenda Misri na baadaye kurudi
Syria ambapo alifariki Damascus mwezi wa tano mwaka 1933 na kuzikwa hapo.
Miongoni mwa kazi zake za kiuandishi ni :
1. Al aqaidul wathaniyyah fi diyaanat Annasraniyyah,
2. Ilmul falak wattabi‟yyaat – alichoshirikiana na baba yake Bw. AbdulWahaab.
3. Al anwaarus Saniyyah
4. Ad Durr An Nad‟ir
Baada ya kuamaliza kusoma kitabu hiki, msomaji atapata kufahamu kwa uwazi na usahihi zaidi
makusudio ya baadhi ya Aya tukufu zilizoteremka kumhusu Sayyidna Issa (a.s.):
1. Na Wakristo wanasema: Masihi ni mwana wa Mungu, hayo ndiyo wayasemayo kwa
vinywa vyao wanaiga maneno ya wale waliokufuru zamani….” (At – Tawbah: 30)
2. “Na kwa kusema kwao: Sisi tumemuuwa Masihi Isa, mwana wa Maryamu, Mtume wa
Mwenyezi Mungu - nao hawakumuuwa wala hawakumsalibu, bali walifananishiwa tu.
Na hakika walio khitalifiana katika haya wamo katika shaka nayo. Wao hawana ujuzi
nayo wowote, ila ni kufuata dhana tu. Wala hawakumuuwa kwa yakini” (An Nisaa: 157)
Tunamuoamba Allah ajalie kitabu hiki kuwa chenye manufaa na faida.
Amiin!!!!!!
UTANGULIZI
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehma, Mwenye kurehemu
5
Himidi zote ni za Mwenyezi Mungu wa pekee Mwenye sifa ya kupasika kuwepo. Aliyetakasika
dhidi ya kuwa na mke na mwana. Ardhi na mbingu vinatoa ushahidi wa upekee wake kwa dalili
za waziwazi zipatikanazo humo. Yeye ni Mmoja wa pekee, hakuzaa wala hakuzaliwa.
Ametakasika kunako kufanana na chochote, na ametukuka dhidi ya kuzuka, kuwa katika mwili
wala kugawanyika katika sehem mbalimbali. Mwenye kuuendesha ulimwengu kwa uweza wake,
na mwenye kuzibadilisha siku kwa irada yake.
Rehema na amani ziwe juu ya kiongozi wetu Nabii Muhammad (s.a.w.) aliyetumwa kuja
kuuondoa upotofu na kuinyanyua bendera ya uongofu.
Kisha (Rehma na amani) ziwe zuu ya Ahli zake na sahaba zake wema wenye kuigwa.
Hakika idadi ya dini ambazo mwanadamu amejiunga nazo haihesbiki , zile zinazojulikana ni
chache sana , na nyingi zinafanana moja kwa moja, na hazitofautiani isipokuwa katika majina ya
miungu na katika baadhi ya vipengele ambavyo sio vya msingi. Sababu ya hali hiyo inatokana na
ukweli kwamba kila alipokuja mtume yeyote alifuatwa na kaumu yake, na baada ya kifo chake
kaumu hiyo, wakishirikiana pamoja na wafuasi wengine, walisimama na kuingiza katika
mafundisho yake baadhi ya itikadi za kipagani walizokuwa wakiziamini kabla ya kuja kwake.
Hawakuishia hapo , bali walichukua na kuingiza katika dini yao mambo na mafundisho ya dini
nyingine za kipagani , kama yaliyotokea kwa Musa na wana wa Israil pale walipomuabudu
ndama . 1
Kwa kawaida ni kuwa dini hizi (walizokuja nazo mitume) zilikuwa ni taratibu ambazo
Mwenyezi Mungu alimwekea mwanadamu kupitia mitume wake, ili apate kuishi na wenzake
maisha ya amani na furaha, na apate kuunyanyua ubinaadamu. Au kwa maana nyingine , dini
hizi , kwa kiasi fulani , zilikuwa ni kama kanunu za adabu na maadili zilizokusudia kujenga
upendo , na kumtahadharisha mwanadamu kutokuwa na uadui kwa mwenzake. Hii ndiyo
iliyokuwa hali ya dini walizokuja nazo mitume kutoka kwa Mwenyezi Mungu, nazo
hazitofautiani katika chanzo na malengo. Binaadamu ameziharibu zaidi kwa kuingiza humo
uzushi uliozushwa na mawazo yake mabovu , na akadanganywa na fikra zake za mwanzo.
Ni kitu kilichokuwa wazi kuwa, nyumati za kipagani ziliabudu miungu wengi waliozushwa na
mawazo yao potofu. Hawakuiacha nguvu yoyote katika nguvu za kimaumbile (mazingira)
isipokuwa waliifanya kuwa ni mungu na wakaiabudu. Kama vile mungu wa radi, mungu wa maji
, mungu wa upepo , mungu wa moto , mungu wa nyota n.k. Mfano wa hilo ni simulizi
iliyoelezwa katika Qur‟an Tukufu kuhusu Nabii Ibrahimu (a.s): “ Na hivyo tukamuonyesha
Ibrahim ufalme wa mbingu na ardhi , na ili awe miongoni mwa wenye yakini. Na usiku
ulipomwingilia akaona nyota, akasema: Hii ni mola wangu. Lakini ilipotua, akasema: Siwapendi
wanaotua. Na alipouona mwezi unang‟aa, akasema: Huu ni mola wangu. Lakini ulipotua,
akasema: Asiponiongoza Mola wangu, bila shaka nitakuwa miongoni mwa watu wapotofu. Na
alipoliona jua linang‟aa akasema: Hili ni Mola wangu, hili ni kubwa kabisa, lakini lilipotua
akasema: Enyi watu wangu! Simo katika hayo mnayoyashirikisha” (Suratul An‟am: 75 – 78).
Kuna watu walioabudu wanyama kama Wana wa Israil waliomuabudu ndama. Kuna
waliomuabudu na kumtukuza mmoja wa wanadamu , mpaka wakafikia hatua ya kusema kuwa ni
1 Allah Mtukufu anasema katika Suratul Baqarah, 51: “Na tulipo muahidi Musa masiku arubaini, kisha mkachukua
ndama (mkamuabudu) baada yake, na mkawa wenye kudhulumu”.
6
sehemu ya utatu wailouita “Baba, Mwana, na Roho mtakatifu” kama vile Mabudha , Wabrahma ,
wababeli, Waashori na wengineo kama utakavyoona katika maelezo yetu.
Hakuna hatari juu ya ukweli, hakuna kitu kilichosalama kama ukweli, na hakuna afichaye
ukweli au kuuzuia watu wasiupate isipokuwa atakuwa ni mwoga au mhalifu. Waislamu
hawaridhii kumuona binadamu ambaye amefikia maendeleo yanayoonekana kwa sasa , akibaki
kung‟ang‟ania yale aliyokuwa nayo tangu enzi za kuanza kwake, akiitakidi kila kilichozushwa
na mawazo yake yaliyopotoka ambayo yameanzishwa na zama na eneo na hatimaye upagani
wake wa enzi za kiza cha ujahiliyyah ukakuwa kutoka humo.
Huenda baadhi ya watu wakadhani kuwa sababu iliyotupelekea kutunga kitabu hiki ni kutokana
na ushabiki au chuki tuliyonayo dhidi ya wale wasiokuwa katika dini yetu. La hasha, kwani
heshima yetu haistahiki kuangukiwa na dhana hii, na hadhi yetu hailingani na yaliyoelezwa.
Kuna sababu mbili za utunzi wa hiki kitabu:
1. Hivi karibuni tulipata kuona vitabu kadhaa vilivyotungwa na wamisionari na wale
waliopamoja nao dhidi ya Uislam vikiwa katika lugha ya kiarabu , kama vile :
Al Hidayah ( katika juzuu 4)
Bakourah Al Shahiyyah
Tanweerul Afhaam fi Maswaadiril Islam
Mizanul haq
Al kafaarah
Misbahulhudaa ila sirrilfidaa
Alburhanuljaleel ila sihhatil Anaajeel
Da‟watulmuslimeen ila mutaala‟til kitabil muqaddasi al thameen, na vingine vingi ,
achilia mbali makala na hotuba mbalimbali walizoanza kuzitawanya baina ya Waislam,
na halikadhalika vitabu vya kingereza , kwa mfano :
The crusfied of the 20th century
Life of Muhammad ( cha William Muire)
Arabia , the cradle of Islam
Our Muslim Sisters
Islam in China, n.k.
Vile vile kuna magazeti mbalimbali, hasa gazeti la kiingereza la Muslim World2 lililojaa shutma
na uzushi dhidi ya Uislam na Waislamu. Kwa kuwa heshima na dini yetu vinatuzuia kuwajibu
kama walivyofanya , tumeona kuwa njia nzuri na iliyokuwa bora zaidi ni kuwafunulia
ulinganisho wa kidini ili kila mmoja wao aone kama yuko katika upotevu au uongofu wa wazi ,
na ijulikane nani kati yetu aliyeshikamana na uzushi wa kipagani wa watu hao(wa zamani). Kwa
sababu ulinganisho humpelekea msomaji kuzingatia ukweli wa kihistoria na kimaandishi ambao
hauna shaka katika ushuhuda wake, na asaa baada ya hapo akawa miongoni mwa wale
wanaosikiliza maneno na kufuata yale yaliyokuwa mazuri. Kwa kuwa mwanadamu kwa asili
hupendelea kupanda daraja katika ukamilifu wa kimaendeleo, vilevile huegemea kwenye baadhi
ya matendo na maneno makali hasa inapokuwa katika masuala ya kidini ambayo ndiyo chanzo
cha saada ya mwanadam.
2 Ni miongoni mwa magazeti hatari yatolewayo na Mustashrikiin wa Marekani. Lilianzishwa na mmishionari
mwenye chuki dhidi ya Uislamu Samuel Zoemor mwaka 1911, na kwa sasa linatolewa kutoka Hartford Marekani,
mhariri mkuu ni keneth crag.
7
2. Sababu nyingine ni kutaka kuinusuru haki na kusimamia undugu wa kibinadamu, kwa sababu
ni lazima katika dini yetu kwaita watu kwenye ukweli, na ni wajibu kwetu pia kuwaita ili
kushirikiana nasi katika kile kitu kizuri tulichonacho, yaani “DINI YETU”.
Tumejiepusha kuibua hisia ya mfuasi wa dini yoyote, kwani sisi hatujatoa kitu kipya kutoka
kwetu bali tumetoa ukweli usiopingika, na yeyote mwenye shaka juu ya lolote katika hayo ni juu
yake kurejea katika vyanzo vyetu tulivyovitaja katika kila mada na utafiti ili apate kuona ukweli
uliowazi ambao hauhitaji maelezo au fafanuzi.
Aidha, kwa bahati sana, vitabu vyote tulivyotolea ushahidi vimetungwa na wasomi mashuhuri
wa kikristo kutoka Ulaya.
Vilevile tumenukuu baadhi ya michoro ya lazima kwa lengo la kutimiliza faida ili kitabu hiki
kitoke kikiwa kamili. Isipokuwa katika makosa ya uchapishaji ambayo yanaeleweka kwa kila
mwenye akili ambaye hatoacha kutusamehe kwa hilo, hasa akiwa ni mwenye kuangalia
kilichomo ndani na sio kilichokuwa nje.
Wassalaam
Muhammad Taher At – Taneer
8
SURA YA KWANZA
IMANI YA UTATU
(Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu)
Ninaanza sura hii - kama alivyoanza Profesa Doane 3– kwa Aya ya Qur‟an Takatifu. Anasema
Allah Mtukufu:
“Wala msiseme watatu, acheni (itikadi hiyo) ni bora kwenu. Hakika MwenyeziMungu ni Mmoja
tu , ameepukana na kuwa na mtoto. Ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini, na
Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mlinzi”
(Surat An –Nisaa: 17)
UTATU KWA WAPAGANI
Ni katika mambo yasiyopingika kuwa dini za kipagani zinafanana sana, na sababu za hali hiyo ni
nyingi. Lakini mojawapo ni pale ambapo taifa lolote kubwa lilipokuwa likijitanua katika dunia,
basi hapo ndipo dini na ustaarabu wake vilikuwa vikijitanua pia. Wakati huohuo, hupata
kuingizwa katika dini hiyo mambo kadhaa wa kadhaa kutoka katika dini nyingine. Kutokana na
jamii za kale kutawliwa na ujahili, walikuwa wakiyakubali – bila kusita – yale wanayoambiwa
na wakuu wao.
Kiongozi wa dini anapoanzisha dini mpya (kwa kweli inakuwa sio dini mpya, bali anakuwa
ameichukuwa kutoka katika moja ya makundi ya kipagani), alikuwa akiongeza baadhi ya mila za
jamii yake ili wayakubali kwa wepesi yale ayasemayo. Kama ilivokuwa kwa wale walioeneza
moja ya dini kubwa zilizopo mpaka sasa katika taifa la Roma.
Bwana Prichard anasema : “Tafiti zote za kidini zilizochukuliwa kutoka vyanzo vya
mashariki haziepuki kutaja moja ya aina au mlolongo wa utatu ( yaani Baba, Mwana na Roho
Mtakatifu” 4
Naye Bwana Maurice anasema 5: “Mengi ya mataifa ya kipagani yaliyopotea yalikuwa na
mafundisho ya kidini yaliyoelezea imani ya utatu wa Mungu ( yaani Mungu mwenye nafsi tatu ).
Katika kitabu ( wakazi wa mwanzo wa ulaya ) 6 kuna maelezo yafuatayo: “ Wapagani wa
zamani walikuwa wakiamini kuwa Mungu ni mmoja , lakini ana nafsi tatu”.
3 Doane kitabu chake ni: Bible Myths and Their Parelles in other Religions. 4 Prichard katika kitabu chake: An Analysis of the Historical Records of Ancient Egypt. uk. wa 285 5 Maurice, katika kitabu chake cha: Indian Antiquities, juzuu ya 6 , ukurasa 30. 6 Ukurasa wa 197
9
Bwana Doane anasema: “Tukitupia macho upande wa India tutaona kuwa ibada zao kubwa na
mashuhuri za kidini ni utatu (yaani kuamini kuwa Mungu ana nafsi tatu” 7
Mafunzo haya huyaita kwa lugha yao “ TRIMURTI” ambayo ni sentensi inayoundwa na maneno
mawili ya Kisanskrit, ambapo TRI ina maana ya “tatu”, na “MURTI” ina maanisha “maumbo”
au nafsi, ambazo ni “Brahma, Vishnu, na shiva”. Nafsi hizi ni tatu katika umoja kwa maana ya
Mungu, Mwokozi na Shiva. Nafsi hizo zote tatu ni Mungu Mmoja. Aidha miungu hii mitatu
huiwekea kielelezo cha utambulisho ambacho ni herufi tatu za A, W, M, n a kuzitamka
(aum/om). Herufi hizi hutumika tu katika salaa zao na huzipa heshima kubwa wawapo katika
mahekalu yao.
Brahma 8 (muumba wa uhai asiyekuwa na umbo wala sifa za kibinaadamu) alipotaka kuumba
viumbe alichukua sifa ya utendaji akawa mtu-mume ambaye ni “Brahma muumba”. Baadaye
akaendelea katika utendaji akageuka katika sifa ya pili ya uhai akawa “Vishnu mlinzi”. Kisha
akabadilika katika sifa ya tatu akawa Shiva muangamizaji”.
Hizi sifa tatu vilevile huziita “Trimutri” ikiwa na maana ya nafsi tatu, na huzipa kielelezo cha
moto, na hujulikana pia kwa majina ya “Agni, Surya, na Indra” na majina mengine ya utatu.
Imeelezwa katika vitabu vitakatifu na muhimu kwa Wabrahma kwamba, huu utatu mtakatifu
hautengani kimaumbo, utendaji na muunganiko, na huifafanua hali hiyo kwa maelezo yafuatayo:
“Brahma ndiye anayewakilisha misingi ya utengenezaji na uumbaji (muumba mkuu), anaendelea
kuwa muumba, naye ndiye Baba”.
Na Vishnu ndiye mlinzi na mhifadhi, naye ndiye “Mwana” aliyejigeuza kutoka katika hali ya
uungu.
Na Shiva ndiye mwanzilishi, mhilikishaji, muangamizaji na mfufuaji, (naye ni Roho Mtakatifu).
Vilevile humuita kuwa ni “Krishna mungu mwokozi, Roho mkuu, Mlinzi wa ulimwengu, mungu
aliyeleta neema duniani ili kuwaokoa watu. Na ni mmoja wa nafsi tatu ambazo zote ni Mungu
Mmoja.
Katika KABITA , ambacho ni moja ya vitabu vyao vitakatifu vya kidini , imeelezwa kuwa
Krishna aliwahi kusema : “Mimi ndiye Mungu wa viumbe vyote. Mimi ndiye siri ya OM. Mimi
ndiye Brahma na Vishnu na Siva , miungu mitatu ambayo yote ni mungu mmoja”.
7 katika kitabu chake kilichotajwa hapo awali, ukurasa 366 8 Brahman lina maana ya roho wa ulimwengu asiyejulikana, ni lazima kulitofautisha na Brahma ambaye ndilo
maarufu zaidi.
Utatu mtakatifu kwa Wahindu.
Picha hii inapatikana katika
makumbusho mbalimbali huko
India.
10
Nafsi ya tatu – ambayo katika sifa yake mbaya ni “Mhilikishaji”, na sifa yake nzuri ni
“Mrejeshaji” – humuelezea kwa picha ya njiwa , alama ambayo humaanisha uumbaji mpya.
Naye ndiye Roho ambaye hurukaruka juu ya maji.
Kama tulivyoeleza, hizi nafsi tatu za milele na za kimaubile huzipa kielelezo cha A , W, na M =
“Om” na huamini kuwa nafsi hizi tatu ndiye Muumba, Mlinzi na Mhilikishaji , na kwamba
hubadilishana kazi , yaani Mwana kufanya kazi za Baba na Roho Mtakatifu , na Roho Mtakatifu
hufanya kazi za Baba na Mwana , halikadhalika Baba hufanya kazi za Mwana na Roho
Mtakatifu.
Bwana Allen anasema : “ Wabrahma hueleza katika vitabu vyao vya kidini kuwa , mchamungu
mmoja aliyeitwa Etnis , aliona kuwa kuna ulazima wa kumuabudu Mungu Mmoja , akawaomba
Brahma , Vishnu na Siva akisema : “Enyi miungu watatu , fahamuni kuwa mimi natambua
kuwapo kwa mungu mmoja , basi nielezeni ni yupi kati yenu aliye Mungu wa kweli ili nimpe
nadhiri na maombi yangu. Ndipo ilipojitokeza miungu yote mitatu na kumwambia : “ Fahamu
ewe mchamungu ya kwamba hakuna tofauti ya wazi baina yetu. Ama utatu unaouona ni mfano
au umbo tu , na mwili mmoja unaojionyesha kwa nafsi tatu ni moja katika uhalisia wake” 9
Naye Bwana Maurice anasema : “Tuliona sanamu lenye vichwa vitatu kwenye kiwiliwili kimoja
ndani ya hekalu la kale lililopitiwa na karne nyingi , sanamu hilo lilielezea utatu”10
Bwana Faber 11
anasema : “kama tuonavyo utatu utokanao na Brahma ,Vishnu na Siva kwa
wahindu , hali ni hiyohiyo kwa Mabuddha ambao huamini kuwa Budha 12
ni Mungu , na
kuamini kuwa yumo katika utatu. Kadhalika Mabudha wa Genast huamini kuwa Jiva ni mmoja
katika nafsi tatu.
Anasema Sir Jones katika maombi ya mchamungu ( Amora ) kama ifuatvyo : “ Ninakupa
utukufu na unyenyekevu ewe mola , wewe ndiwe Mungu mwenye huruma. Ewe muondoaji wa
mateso na matatizo. Ewe mola wa kila kitu. Ewe mlinzi wa viumbe. Ewe mwenye kuwapa
rehema waja wako. Ewe mfalme wa kila kitu. Ewe hai, wewe ni Brahma, Vishnu, na Siva, Mimi
ninakuabudu wewe. Umejidhihirisha kwa majina yako ya Alphabeti, na maumbo yako
mbalimbali na umbo la Budha Mungu wa rehema”13
Naye Bwana Doane anasema: “Mabudha, ambao ndio wakazi wengi wa China na Japan,
wanamuabudu mungu mwenye nafsi tatu ambaye humuita “FO”. Wanapotaka kuutaja utatu huu
9 Allen, katika kitabu chake cha: India Ancient and Modern, ukurasa 382 10 Indian Antiquities, juzuu ya 4, ukurasa wa 372. 11 Faber: The Life of Christ 12 Muasisi wa dini ya budha ni : Gautama Ieddhartha ( 564 – 483 B.C ) ambaye aliitwa Budha , ikiwa na maana ya
Mwenye kuangaza , au aliyeongoka. Alikuwa ni mtoto wa kiongozi wa jimbo lililopo mpakani mwa Nipal.
Aliukana uongozi wa Veda na Makuhani wa Kibrahma, na kutengeneza kanunu tano za kimaadili , ambazo ni mfano
wa usia. Nazo ni:
• Mtu yeyote asimuue kiumbe yeyote aliye hai.
• Asichukue asichopewa.
• Asiseme uongo • Asinywe kilevi
• Asisimame juu ya uchafu.
Vilevile imani ya Budha anayoiamini kuwa ya kweli, ilieleza kuwa maumivu ni bora kuliko raha katika maisha ya
kibinaadamu. (Qissatul Hadhaarah juzuu ya 3 ukurasa wa 76. 13 Jones, katika kitabu chake kiitwacho: Asiatic Researchs, juzuu ya 3, ukurasa wa 285.
11
matakatifu husema, utatu matakatifu “FO”, na humchora katika mahekalu yao kwa umbo la
masanamu yanayopatikana India. Vilevile husema: FO ni mmoja, lakini ana maumbo matatu.
Katika moja ya majengo maalumu ya ibada huko Botala, huonekana FO akiwa ni sehemu tatu.14
Bwana Davis naye pia ametoa maelezo kama hayo.15
Bwana Faber anatoa maelezo mengine akisema: “Wachina humuabudu Buddha na humuita
“FO” na kusema kuwa ana nafsi tatu, A, U na M kama vile wasemavyo wahindu”.
Bwana Doane anasema : “wafuasi wa Laokamitdha – ambaye ni mwanafalsafa mashuhuri wa
kichina na ambaye alikuwapo miaka 604 kabla ya Kristo – wanajulikana kuwa ni wafuasi wa
“Tao” na humuabudu mungu mwenye nafsi tatu. Msingi wa mafundisho ya falsafa zake za kidini
ni Tao, ambaye ndiye akili ya milele (mwanzo) iliyoitoa nafsi moja , na kutokana na hii moja
ilipatikana ya pili, na kutokana na hii ya pili , ikapatikana ya tatu, ambapo kutokana na hizi nafsi
tatu kila kitu kilipatikana. Imani hii ya kuzaliana ilimshangaza Bwana Doane kwani anayeiamini
ni mpagani”.16
Imeelezwa katika vitabu vya kidini vya China kwamba , asili ya kila kitu ni moja , na hii moja
ambayo ndio chanzo cha uhai , ililazimika kuumba nafsi ya pili , ambapo nafsi ya tatu ilitokana
na hizo nafsi mbili, na halafu kila kitu kilipatikana kwa hizi nafsi tatu.
Wamisri wa kale walikuwa wakiabudu mungu mwenye nafsi tatu 17
aliyekuwa amechorwa katika
mahekalu yao ya zamani. Wataalamu wanadhani kuwa alama wanayoichora katika bendera,
ambayo ni bawa la ndege na pango la nyoka, ni alama ya ule utatu pamoja na sifa zake
mbalimbali.
Naye Bwana Helsly Stevens anasema:
“Wahindu humuamini mungu mwenye nafsi tatu, na wanapotaka kumzungumzia kwa sifa ya
“Muumba” husema “mungu Brahma”. Wanapotaka kumzungumzia kwa sifa ya “Mhilikishaji”
husema “Siva” au “Mahadeva”. Na wanapotaka kumsifia kwa sifa ya “Mlinzi” husema “Mungu
Vishnu” . Huamini kuwa utatu huu upo kila sehemu kwa roho na uweza.18
14 Doane, katka kitabu chake, ukurasa wa 372 15 Davis katika kitabu chake kiitwacho, The Chinese, juzuu ya 2, ukurasa wa 101 na 103. 16 Katika kitabu chake , ukurasa wa 172 17 Katika dini ya zamani ya Kimisri: (Geb) mungu wa ardhi alimuoa (Nut) mungu wa mbinguni, wakamzaa (Ra)
yaani jua. (Angalia katika kitabu kiitwacho: Tareekhush Sharqil Adnal Qadim, ukurasa wa 124. Cha Professa Abdul
Aziz Othman. 18 Katika kitabu chake kijuliknacho kama: Faith and Reason, ukurasa wa 78.
Utatu kwa
Wamisri
12
Bwana Toma Inman anasema: “Picha hii humuelezea Brahma wakati wa kuumba kwake,
ambayo iko katika hali mbili za uume na uke”19
Akaendelea kusema katika ukurasa wa 101 kuwa: “vielelezo na alama zote zitumikazo kwa
Wakristo, vilikuwa vikielezea na kuonyesha kuabudiwa kwa vitu vinavyotia aibu, na
haiwezekani kukana uwepo wake”.
Kisha akasema: “nadhani pindi watu watakapoelewa maana ya alama hizo watazikimbia, na
huwenda baadhi ya watu wakaendelea kushikamana na ibada hizi ambazo , kwa mtazamo wangu
ni mbaya na ni za kipagani”.
Pia, katika kitabu chake hicho, ameeleza mambo mengi ya msingi ambayo hatukuyaelezea, na
hatukuweka mojawapo ya picha zilizoelezewa katika kitabu hicho, kwani ingeweza kuleta hisia
kali kwa watu wengi.
Bwana Doane anasema : Makasisi wa hekalu la Momvis la huko Misri wanapowaeleza
wanafunzi wapya kuhusu utatu , walitoa maelezo yafuatayo : “ Wa kwanza alimuumba wa pili ,
na wote wawili kwa pamoja wakamuumba watatu , na hivi ndivyo ulivopatikana utatu
mtakatifu”20
Mfalme wa Misri Toleso alimtaka kuhani Tnishoki amueleze kama kabla yake alipata kuwapo
mkuu zaidi kuliko yeye, au atakuwa baada yake mwenye ukuu zaidi? Kuhani akasema: “Ndiyo,
yupo aliye mkuu. Wakwanza ni Mwenyezi Mungu, kisha Neno , na pamoja nao ni Roho
Mtakatifu. Na hao watatu wana hali moja na ni wamoja katika uhalisia. Nguvu za milele
zimetokana nao. Ondoka ewe mwenye kutoweka , mwenye maisha mafupi”.
“Hakuna shaka kuwa , nafsi ya pili katika utatu mtakatifu kupewa jina la NENO ina asili ya
upagani wa Kimisri uliopenya katika dini nyingine kama vile Ukristo. Na Apollo aliyezikwa
Delhi huitwa NENO. Vilevile katika mafundisho ya kidini huko Iskandaria , ambayo ndiyo
mafundisho ya Plato kwa miaka mingi kabla ya Kristo, NENO ni mungu wa pili ambaye pia
huitwa Mwana wa pekee wa Mungu.21
Bwana Higgins , katika kitabu chake kiitwacho The Celtic Druids, juzuu ya 2 ukurasa wa 162,
anasema: “Waajemi walikuwa wakimuita Mitrusa kuwa ni NENO, mpatanishi , na mwokozi wa
Waajemi”. Angalia pia katika kitabu cha Almicio Dunlap kiitwacho Vestiges of Spirit History of
Man, ukurasa wa 20. Halikadhalika kitabu cha Bwana Bunsen, kiitwacho The Angel Messiah,
ukurasa wa 57 kuna maelezo kama hayo.
Naye Bwana Bonwick anasema: “Imani ya ajabu iliyoenea katika dini za Wamisri
(wapagani wa zamani ) ni ile ya kuamini “uungu wa NENO”, na kwamba kila kitu kimetokana
na NENO, na NENO ametokana na Mwenyezi Mungu , na kuwa huyo NENO ni Mungu. Na
Plato, Aristo na wengine walikuwa wakiifahamu imani hii ya kipagani iliyokuwapo miaka mingi
kabla ya Kristo. Na hatukuwa na habari ya kwamba Wakeldan na Wamisri walikuwa na imani
hii isipokuwa hivi karibuni tu”.22
Ameendelea kusema katika ukurasa wa 404: “Kama ambavyo NENO anapata heshima kuu kwa
Wamisri (wapagani wa zamani) halikadhalika maneno yafuatayo yanapatikana katika vitabu
19 Toma Inmann, katika kitabu chake cha: Ancient Pagani and Modern Christian Symbolism, ukurasa wa 9. 20 Katika kitabu chake, ukurasa wa 473. 21 Indian Antiquities, ukurasa wa 127. 22 Katika kitabu chake: Egyptian Belief and Modern Thought, ukurasa 402.
13
vyao vitakatifu vya kidini: “Hakika mimi najua zaidi siri ya uungu wa Neno nalo ni Neno la
Mungu wa kila kitu, naye ndiye aliyeliumba”, kwa hiyo Neno ndiye nafsi ya kwanza baada ya
Mungu, ambaye hakuumbwa, na ndiye mwenye kutawala viumbe vyote”.
Bwana Doane anasema: “Waashori walimwita Marduk kuwa ni NENO, na kusema kuwa ni
“mwana wa Pekee wa Mungu”, ambapo vilevile walikuwa wakimuomba kwa maombi
yafuatayo: “Wewe ndiwe muweza , mfanikishaji na mtoaji wa uzima. Wewe ndiwe mwenye
huruma kati ya miungu yote. Wewe ni mwana wa pekee wa Mungu Muumba wa mbingu na
ardhi na mtawala wake. Huna mfano. Wewe ndiwe mwenye huruma na mwenye kufufua wafu”.
Vilevile katika ukurasa wa 374 ameeleza yafuatayo: “Wakeldayo wakiliita NENO kwa jina la
Mimrar kama wasemavyon Wayunani kuwa ndiye Muumba na mtawala wa ulimwengu, na
kwamba hakuna chochote chenye ukuu kuliko yeye isipokuwa Mwenyezi Mungu”.
Bwana Frontingham ametoa maelezo yafuatayo: “Folo alikuwa akiitwa NENO ambapo
walikuwa wakimtukuza sana na kumsifu kwa ibara zifuatazo: “Folo alikuwapo kabla ya
chochote, mwana wa pekee wa Mungu, Chakula cha milele kutoka mbinguni , Chemchem ya
hekima, njia ielekeayo kwa Mungu, mwakilishi wa Mungu, mfano wa Mungu, kuhani, Muumba
wa ulimwengu, mungu wa pili, mkalimani wa Mungu, mjumbe wa mungu, nguvu ya Mungu,
mfalme, malaika, mwanadamu, mpatanishi, nuru ya awali, mwanga, jina la Mungu, mwenye
kujitoa fidia”.23
Wayunan (wapagani wa zamani) walikuwa wakiamini kuwa Mungu ana nafsi tatu. Makasisi wao
wanapoanza kutoa sadaka ya kuteketezwa (kichinjwa) hunyunyiza maji mara tatu juu ya
mnyama anayetaka kuchinjwa (kama alama ya utatu), na kisha huwanyunyizia wale waliopo
hapo mara tatu na kuchukua ubani kwenye chombo maalumu kwa vidole vitatu kwa imani kuwa
vitu vyote vitakatifu lazima viwe katika hali ya utatu. Idadi hii (ya utatu) wanaiwekea mkazo wa
hali ya juu katika mambo yao yote ya kidini.
Naye Bwana Doane, ambaye tumekwishamtaja, amenukuu maelezo yafuatayo kutoka kwa
Orpheus, ambaye ni miongoni mwa waandishi na washairi wa Kiyunan aliyepata kuwapo karne
nyingi kabla ya Kristo: “Vitu vyote vilitendwa na Mungu mmoja, mwenye majina na nafsi tatu”.
Asili ya mafundisho haya ya utatu ni Misri, na wengi wa wazazi katika kizazi cha tatu na
cha nne wanasema: Pythagoras, Herakleitos na Plato waliufahamu utatu kwani falsafa zao
kuhusu utatu walizichukua kwa Orpheus”.
Na Professa Fiske anasema: “Wapagani wa zamani wa Kirumi walikuwa wakiamini utatu ambao
wa kwanza ni Mwenyezi Mungu, Neno na kisha Roho Mtakatifu”24
Bwana Doane anasema: “Waajemi walikuwa wakimuabudu mungu mwenye nafsi tatu, bila
tofauti yoyote na Wahindu. Miungu hao ni Ahuramazda = Muumba, Mithra = mwana wa Mungu
mwokozi na mpatanishi, na Ahriman = mhilikishaji. Katika maandiko ya Zorostarsanaan
ambacho ndiyo sheria ya Waajemi kuna sentensi zifuatazo: “Utatu wa Mungu unaiangazia dunia,
23 Frontingham, katika kitabu chake: The Cradle of Christ, ukurasa wa 112. 24 Fiske, katika kitabu chake kiitwacho Myth and Myth Makers, ukurasa wa 205.
14
na kichwa cha utatu huu ni Monad. Vilevile Waashori na Waphoenic walikuwa wakiabudu
miungu yenye nafsi tatu”.25
Bwana Baccost anasema: “Wafinland (ambao ni wabarbar walioishi kaskazini mwa Perusi)
katika karne nyingi zilizopita walikuwa na mungu waliyemwita Treklaf ambaye sanamu lake
lenye vichwa vitatu katika mwili mmoja lilipatikana huko Hurtongbarg”26
Doane anasema: “Wascandnavia walikuwa wakimuabudu mungu mwenye nafsi tatu ambazo
ni Odin, Thora na Frey, na kusema kuwa hizi nafsi tatu: zote ni Mungu Mmoja.
Sanamu linaloelezea huu utatu mtakatifu linapatikana katika mji wa Opisal nchini Sweden,
ambapo wakazi wa nchi za Sweden, Norway na Denmark walikuwa wakifakhrishiana wao kwa
wao katika ujenzi wa mahekalu ya huu utatu. Kuta za haya mahekalu zilipakwa dhahabu na
kupambwa kwa picha za huu utatu. Wanamchora Odin akiwa na upanga mkononi, na huku
Thora akiwa kushotoni kwake akiwa na taji kichwani na fimbo ya enzi mkononi, naye Frey
akisimama kushotoni mwa Thora ambapo sanamu yake ina alama mbili za uume na uke.
Odin huitwa kuwa ni Baba, na Thora naye ni mwana wa peke wa Odin ambapo Frey ni mtoaji
baraka, kizazi, amani na utajiri”. 27
Wadruid walikuwa wakiabudu mungu mwenye nafsi tatu, ambazo ni Fann, Toulak na Molak.
Na wakazi wa zamani wa Siebaria walikuwa wakimuabudu mungu mwenye nafsi tatu. Nafsi ya
kwanza katika huu utatu mtakatifu wanaiita “Muumba wa kila kitu”, na nafsi ya pili “ mungu wa
majeshi” na nafsi ya tatu “ roho wa upendo wa binguni”, kisha husema kuwa “ nafsi tatu ni
Mungu mmoja”.
Wapagani wa Titer walikuwa wakimuabudu mungu mwenye nafsi tatu, ambapo katika moja ya
pesa zao zilizopo katika makumbusho ya Petersburg huyu mungu mwenye utatu mtakatifu
huonekana akiwa amekaa juu ya majani matatu.
Bwana Knight anasema : “Wakazi wa visiwa vya Ocyanus walikuwa wakimuabudu mungu
mwenye nafsi tatu, wakisema Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho mtakatifu , na
kumchora Roho Mtakatifu katika umbile la ndege”. 28
Lord Kingsbrough anasema: “Wamexico wanamuabudu mungu mwenye nafsi tatu
wanayemwita Tezcatlipoka. Pamoja naye kuna miungu wengine wawili. Mmoja amesimama
kuliani mwake na mwengine kushotoni mwake. Jina la mungu wa kwanza – aliyesimama upande
wa kulia – ni Huitzilopochtli na mwengine ni Tlaloc. Bartholomeo alipoteuliwa kuwa askofu
mkuu mwaka 1445 alimtuma kasisi Francis Hermandiz kwenda Mexico kuhubiri ukristo baina
ya wahindi wekundu, kasisi huyu alikuwa akiijua lugha ya wahindu wekundu. Baada ya mwaka
mmoja alimuandikia askofu mkuu akisema: “Hakika [wahindi wekundu] wanamuamini mungu
aliyeko mbinguni, na kwamba huyo mungu ana nafsi tatu ambazo ni Mungu Baba, Mungu
Mwana na Mungu Roho Mtakatifu, na wote hawa watatu ni Mungu mmoja. Jina la baba ni:
Pezona, na mwana: Bakab aliyezaliwa kwa mwanamke bikira, na roho mtakatifu ni: Ikihia. Pia
25 Ancient Faiths, juzuu ya pili, ukurasa wa 819. 26 Hebrew Lexicon. 27 Doane, ukurasa 377. 28 Knight, katika kitabu chake, The Symbolical Language of Ancient Art and Mythology, ukurasa wa 169.
15
wanaabudu sanamu liitwalo Tincatinca na kusema kuwa ni moja lenye nafsi tatu, na kwamba
hizi nafsi tatu ni Mungu mmoja. 29
Naye Bwana Squire anasema: “Na [wahindu wekundu] Wakanada wanamuabudu mungu
mwenye nafsi tatu na kumchora katika umbile la sanamu lenye vichwa viatatu kwenye mwili
mmoja na kusema kuwa ni [watu] watatu wenye moyo mmoja na maamuzi ya aina moja”.30
Kwahiyo tumeona kuwa kuna kufanana baina ya dini za wapagani, ambapo baadhi yao
walikuwa wakiabudu miungu wengi, na hatukueleza kuwahusu (miungu) kwa sababu lengo letu
ni kuelezea mataifa yaliyokuwa yakiamini utatu.
Na lau kama sio kupendelea kwetu ufupisho, tungetoa ushahidi mwingi mbali na huo tulioutaja
kuhusu imani hii ya kipagani.
* * *
UTATU KWA WAKRISTO
Tumetoa yale yaliyoelezwa kuhusu utatu kwa wapagani, na sasa tutaeleza kidogo yale
yaliyoelezwa na wakristo juu ya imani hiyo kwa kunukuu vifungu kutoka katika vitabu vyao
vitakatifu.
Waraka wa kwanza wa Yohana, sura ya 5 mstari wa 7 inasema: “Kwa maana wako watatu
washuhudiao [mbinguni], Baba, Neno na Roho mtakatifu, na watatu hawa ni umoja”.
Injili ya Yohana, sura ya 1 mstari wa 1: “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno
alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu…” mstari wa tatu unaendelea “Vyote
vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakukufanyika chochote kilichofanyika”.
Waraka wa Paulo mtume kwa Wakolosai, sura ya kwanza mstari wa 16 na 17 : “ kwa kuwa
katika yeye (Kristo) vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi,
vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni viti vya enzi, au usultani, au enzi au mamlaka; vitu
vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake”.
Kuna aya nyingi zaidi ya hizi, na ili tusimchoshe msomaji kwa maelezo marefu, tutatosheka na
hayo tuliyokwishayataja, na atakayetaka nyongeza arejee kwenyi Injili. Aidha, kwa kuwa hapo
awali tulitoa majina mbalimbali waliyoyatumia wapagani kumuelezea mtoto wa Mungu,
inatulazimu kutaja majina ambayo wakristo pia huyatumia kwa Yesu, nayo ni: Yesu Kristo,31
Mungu,32
Bwana,33
Wamilele,34
Mwana wa Mungu,35
Mzawa wa pekee,36
Mkuu,37
Simba wa
29 Antquities of Mexico, juzuu ya tano, ukurasa 164. 30 The Serpent Symbol, ukurasa 181. 31 Luka 1:21. 32 Yohana 1:1. 33
Imetajwa katika Injili zote 34 Waraka kwa Waebrania 9:14 35 Mathayo 3:17 36 Waraka kwa Waebrania 1:6 37 Matendo ya Mitume 5:31
16
kabila la Yuda38
Mkombozi,39
Mpatanishi,40
Mwokozi,41
Mchungaji mwema,42
Mwana wa
Adam,43
Imanueli44
(yaani Mungu pmoja nasi), Mwana wa Mtukufu,45
Mkuu wa uzima,46
mchukuaji dhambi ya ulimwengu,47
Mwanakondoo.48
38 Ufunuo wa Yohana 5:5: [Simba wa kabila la Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu,
na zile muhuri saba]. 39 Luka 1:68 40 Timotheo 2:5 41 Yohana 4:42 42 Yohana 10:11 43 Marko 14:62 44 Mathayo 1:23. 45 Marko 14:61 46 Matendo ya Mitume 3: 15 47 Yohana 1:29 48 Ufunuo wa Yohana 13:8
17
SURA YA PILI
KUMTOA KAFARA MMOJA WA MIUNGU KAMA UTAKASO WA DHAMBI
I- Wapagani:
Anasema Bwana Doane: Fikra ya kukombolewa kwa njia ya kumtoa mmoja wa miungu
kama kafara ya dhambi ni ya zamani sana kwa wapagani na wengineo. Maeleazo ya fikra hii
kwa Wahindu yalikuwapo hata kabla ya enzi ya Vedic49
ambapo kitabu cha Rigveda
kinawaonyesha miungu wakimtoa Prusha - ambaye ni mtoto mume wa kwanza – kuwa
kafara na wanamchukulia kuwa yu sawa na Muumba. Katika kitabu cha Tazyapar hamana
kuna maelezo yafuatayo: “Bwana wa viumbe Prajaapati aliitoa nafsi yake kuwa dhabihu
(kafara) ya miungu”..
Na katika kitabu kiitwacho „Istibana Brahmana‟ kuna maelezo yafuatayo: “Na ulimwengu
kwa dhabihu hii – Berusha Meda (yaani kafara ya mtoto-mume wa kwanza – kila kitu
kitafanyika”.50
Vilevile wapagani walikuwa wakiwatoa watu kuwa kafara, na mara nyingi waliwatoa watumwa
na mateka kama kafara ya utakaso wa dhambi. Sio hivyo tu, bali walifikia hata kuwatoa watoto
wao wenyewe. Na Warumi na Wayunani walikuwa wakijitoa wao wenyewe kama kafara ya
miungu ili wapate kuwaridhia. Huko Misri walikuwa wakiwatoa binaadam kuwa kafara ambapo
desturi hii mbaya iliwatawala mpaka wakawa wanamtoa kafara mtoto wa kwanza wa kiume
kutoka katika familia za kiatanatiyyah. Walimchukua na kumpeleka hekaluni na kumwekea taji
kichwani mwake na kisha humchinja kama sadaka ya miungu kama vile wachinjwavyo
wanyama.
Bwana Hock anasema “ Na Wahindu (wapagani) huamini kuwa mmoja katika miungu
alijibadilisha katika mwili wa kibinadaam na akajitoa kafara kama utakaso wa dhambi za watu”.
Bwana Mourinior Williams anasema: “Wahindu wa kipagani huamini dhambi ya asili, na
linalojulisha hayo ni maelezo yaliyopo katika maombi yao wanayoyaomba baada ya Kiyatara
wakisema: “ Hakika mimi ni mwenye dhambi na makosa, asili yangu ni mbaya, na mama yangu
49 Vedic linatokana na Vide na Vid, na linamaana ya elimu au ya kiroho ambayo ni maandiko na nyimbo za wahindu
zinazoundwa na vitabu vinne ambavyo viliandikwa miaka elfu moja kabla ya kuja kwa Masihi (a.s).
(Qisswatul hadhaarah, juzuu 3 uk. 38).
50 Amenukuu kutoka katika kitabu cha Bwana Lundy, kiitwacho “Monumental Christianity”.
Krishna akiwa msalabani na
taji la dhahabu kichwani
mwake.
18
alinibeba tumboni kwa dhambi, basi nikomboe Ewe mwenye jicho la huruma, ewe mkombozi
wa wakosaji, ewe mwenye kuondosha dhambi na makosa”.51
Naye Professa Doane anatoa maelezo yafuatayo: “Wahindu wanaamini kuwa Krishna, mzawa
wa pekee ambaye ndiye Vishnu na ambaye kwa imani yao hana mwanzo wala mwisho,
aliteremka kuja kuikomboa dunia kutokana na kuelemwa na mizigo ya dhambi. Akamkomboa
mwandamu kwa kujitoa kafara badala yake”.
Naye kasisi George Cox anasema: “Wahindu wanamsifu Krishna kwa ushujaa wa hali ya juu
uliojaa uungu kwa kitendo chake cha kujitoa kafara, na kusema: Hakika hakuna awezaye
kufanya kitendo hiki pasipokuwa yeye” 52
Mwengine ni Bwana Almicio Konew anayetoa maelezo yafuatayo: “Wahindu hukieleza kifo cha
Krishna kwa namna mbalimbali, na iliyokuwa mashuhuri zaidi ni kuwa alikufa kwa kutundikwa
juu ya mti na kupigiliwa kwa mkuki”.
Bwana Doane akifafanua mti huo, anasema: “Mti uliokusudiwa hapa ni “msalaba”, na kwamba
Bwana Mour alimchora Krishna akiwa katika hali ya kusulubiwa kama alivyochorwa katika
vitabu vya kihindu akiwa ametobolewa mikono na miguu, halikadhalika kanzu yake ikiwa
imewekewa picha ya moyo wa mwanadamu”53
“Na katika mafundisho ya Vishnu Purama, tunajua kuwa baada ya mwindaji kumpiga Krishna
kwa mkuki, (mwindaji) alijuta na kuungama mbele yake akisema: “Nihurumie, mimi ndiye
niliyeangamizwa na dhambi zangu, na wewe ndiwe mwenye uwezo wa kuniangamiza. Krisha
akamjibu: Usihofu, nenda mbinguni kunako makazi ya miungu. Alipokwisha kumwambia
maneno hayo, kilitokea kipandwa kilichompeleka mpaka mbinguni”.
Katika sifa apewazo Krishna ni: “Mwenye kusamehe madhambi na Mkombozi dhidi ya joka la
umauti”.
Padri Geogius alimchora mungu Andra anayeabudiwa na watu wa Nepal 54
akiwa amesulubiwa,
kama wamchoravyo siku ya sikukuu yao inayofanyika katika mwezi wa Nane.
Profesa Higgins anasema katika kunukuu maelezo yaliyoandikwa na Andrada ambaye ndiye
mkazi wa mwanzo kutoka Ulaya aliyeingia Nepal na Tibet55
: “Anasema katika kumzungumzia
Mungu Andra ambaye wanamuabudu na kuamini kwamba damu yake ilimwagika kwa
kusulubiwa na kutobolewa kwa misumari ili kuwakomboa watu kutokana na dhambi zao, kuwa:
“Picha za msalaba zipo katika vitabu vyao”. Naye Profesa Doane akasema: “Katika eneo la
kusini mwa India, Tangor na Ayondia wanamuabudu Mungu aliyesulubiwa aitwaye “Pali” na
kuamini kuwa ndiye Vishnu aliyegeuka katika umbile la kibinaadamu, mbapo humchora akiwa
ameatobolewa mbavu na mikono yote miwili”.
51 Imenukuliwa kutoka katika kitabu cha Bwana Lundy, Monumental Christianity 52 Ancient Faiths 53 Doane, ukurasa 184 54 Nepal ni nchi iliyopo pembezoni mwa milima ya Himalaya ya mashariki, kati ya India na Tibet, kwa sasa mji
wake mkuu ni Kathmandu 55 Tibet, iko kusini-magharibi mwa china, mji wake mkuu ni Lasa
19
Katika wimbo wa kidini wa Budha kuna maneno yafuatayo: “Ulikabiliana na mateso, matatizo,
kufungwa, umauti na kuuawa, kwa subira na upendo mkubwa ili kuleta furaha kwa watu na
ukawasamehe waliokukosea”. Kadhalika husema kuwa BUDHA ni tabibu mkuu, mwokozi wa
ulimwengu, mpakwa mafuta (mtakatifu), Masihi, Mzawa wa pekee n.k. Vilevile husema
kwamba alijitoa kafara ili kufuta dhambi za wanadamu na kuwafanya kuwa warithi wa ufalme
wa mbinguni. Na pia, kwa kuzaliwa kwake aliacha utukufu wake ulimwenguni ili awakomboe
watu kutokana na maovu na adhabu kama alivyoahidi.
Profesa Beal anasema: “Pujana alisema: “Nitajifanyia (jibadilisha katika) mwili wa kibinadam,
nitateremka na kuzaliwa kati ya watu ili nipate kuwapa amani na mapumziko, na kuwaondolea
huzuni na mateso ya dunia. Kwa yakini kazi yangu hii siifanyi kwa kutaka chochote katika utajiri
na furaha”. 56
Bwana Hock anasema: “Kwa matazamo wa Mabudha, Budha ni mtu na wakati huohuo ni
Mungu na kwamba alichukua mwili katika ulimwengu huu ili awaongoze watu, kuwakomboa na
kuwabainishia njia ya amani. Mabudha wote wana imani hii kama wanavyoamini kuwa Budha
ndiye Mwokozi wa watu”.
Naye Bwana Max Muller anasema: “Mabudha hudai kuwa Budha alisema: “Acheni makosa
yote yaliyotendeka ulimwenguni niyabebe ili kwamba ulimwengu upate kukombolewa”.57
Profesa Williams naye anasema: “Wahindu husema kuwa: Miongoni mwa huruma zake (yaani
Budha) ni kuwa aliiacha pepo na kuja duniani kwa sababu ya makosa na maovu ya wanadamu ili
awakomboe kutokana na dhambi zao na kuwaondolea adhabu wanayostahiki”.58
Doane anasema: “Imani ya kumtoa kafara mkombozi wa ki-Mungu kwa njia ya mateso na mauti
ni ya zamani sana kwa Wachina. Moja ya vitabu vyao vitukufu kiitwachoYapkink
kinamzungumzia Tiyan kuwa ni mtukufu wa kipekee mwenye fadhila za mbinguni na ardhini, na
kwamba ataurejesha ulimwengu kwenye wema. Vilevile anataabika na kupata mateso, na
hanabudi kupita katika mkondo ambao mawimbi yake hayatamwingia kwa kuwa yeye pekee
ndiye awezaye kumpa Bwana dhabihu inayomstahiki…kwani watu huzitoa nafsi zao kuwa
dhabihu kwa lengo la kutaka ubwana, na wasomi nao hufanya hivyo kwa lengo la kutaka vyeo
na umashuhuri, na viongozi nao pia hufanya hayo kwa lengo la kuziimarisha familia na koo zao.
Lakini mtakatifu Tiyan alifanya hivyo kwa ajili ya watu, na amekufa kwa ajili ya kumkomboa
mtu mwema. Pia huamini kuwa ndiye pekee aliyekuwa pamoja na Mwenyezi Mungu tangu
milele na milele hata kabla ya chochote”.
Bwana Bonwick anasema: “Wamisri wanamchukulia Osiris kuwa miongoni mwa wakombozi
wa watu, ambaye kwa sababu ya juhudi zake za kutenda mambo mema alikumbana na mateso,
na kwa sababu ya kupambana na dhambi alitenzwa nguvu na kuuawa” 59
56 The Romantic Legend of Saki Buddha from Chinese Sanskrit, uk. 33 57 History of Ancient Sanskrit Literature, uk. 80 58 Hinduism, uk, 214 59 Egyptian belief and Modern Thought, ukurasa, 165
20
Naye Bwana Murray anasema: “Wamisri wanamheshimu Osiris na kumchukulia kuwa mfano
wa hali ya juu wa kujitoa kafara ili watu wapate uzima”
Doane anamnukuu Sir Wilkinson akisema: “Mateso na kifo cha Osiris ndiyo siri kubwa katika
dini ya Wamisri, na baadhi ya athari za imani hii zinaonekana wazi katika dini za mataifa.
Humchukulia Osiris kuwa mwanamapinduzi wa Kimungu aliyeleta fikra njema. Na (imani)
kuhusu kuja kwake duniani, kifo na kfufuka kwake katika wafu na kuwa atatengeneza dini ya
wafu siku za mwisho, imani hii inafanana na ile ya miungu wa Wahindu” 60
“Horus alikuwa akiitwa Mwokozi, Mkombozi, Mungu wa uzima, wa milele na mzawa wa pekee.
Vilevile Attis huitwa Mwana Mkombozi wa pekee. Pia Wafrige (ambao ni wakazi wa Asia
ndogo) walikuwa wakimuabudu, ambapo walimfananisha na mtu aliyefungiwa mtini kukiwa na
mwanakondoo miguuni kwake. Hali hii inafanana na ile ya Apollo aliyekuwa akiabudiwa na
Wamilitayo ambao husema kuwa alikufa kwa mwili na kwamba yeye ndiye mtawala wa mambo
ya ajabu. Pia husema kuwa alikamatwa na askari wa Kikeldayo ambao walimuua na kumpigilia
misumari ili apate maumivu zaidi, na kwamba alisulubiwa kwa ajili ya kuwakomboa”.
Naye Mis Jamson anasema: “Wamilitayo walikuwa wakimfananisha Mungu kama mtu
aliyesulubiwa kwa kufungwa kamba mikono na miguu akiwa juu ya mti huku chini ya miguu
yake kukiwa na picha ya mwanakondoo. Na Wasuria husema kuwa Tamuz, mungu aliye mzawa
wa pekee wa mwanamke bikira, alipata mateso kwa ajili ya watu, na kwa ajili hiyo wanamuita
kuwa ni MKOMBOZI aliyejitoa nafsi kwa kusulubiwa.Vilevile walikuwa wakisherehekea
kumbukumbu za kifo chake kwa kutenga siku maalumu kila mwaka ambapo huweka sanamu juu
ya tandiko wakidai kuwa ndiye, na kuanza kumlilia huku wakuu wao wakiimba na kusema:
“Mtumainini Mungu wenu kwani mateso aliyoyapata yametuletea ukombozi”.61
Bwana Doane anasema: “Wapagani walikuwa wakisema kuwa Primecion ni Mkombozi na
kumuita kuwa ni Mungu aliye hai, rafiki wa mwanadam, aliyeitoa nafsi yake kama kafara ya
kuwakomboa watu. Simulizi nyingi za kusulubiwa kwa crasius zilizoandikwa na Esius katika
Athena miaka mia tano kabla ya Masihi (a.s.), ndiyo mashairi ya zamani sana yaliyobaki mpaka
hii leo kuhusiana na suala la kusulubiwa. Ama hila na hadaa zilizotajwa humo, zimechukuliwa
kutoka katika simulizi za zamani sana, na hazina mfano katika kuleta taathira za hisia kwa
watazamaji. Hakuna aliyemtangulia kubainisha na kuelezea mateso yaliyompata huyo Mungu
kwa kiasi kwamba mtazamaji hawezi kujizuia kutoa taswira yake kutokana na muathiriko
mkubwa na jinsi ilivyokuwa taathira kwa wale waliokuwa wakiamini uungu wa shujaa wa
simulizi hii, ambaye ni rafiki yao, muumba wao, mfaidishaji na mkombozi wao aliyevumilia
mateso na huzuni kwa ajili yao, na ambaye, kwa sababu ya dhambi zao, alipata kuumizwa, na
kwa sababu ya maovu yao aliteswa na kustahmili adhabu ili kuwaokoa. Kwa kupigwa na
kuchapwa mijeledi waliponywa. Aliteswa, akanyanyaswa na kudharauliwa na wala hakutetereka.
Subira yake kubwa ilionekana pindi makuhani wa Mungu wa shari walipokuwa wakiipigilia
mikono na miguu yake kwenye mlima wa Caucasus, na kwamba hana mfano wa ukamilifu na
uvumilivu aliouonyesha akiwa ametungikwa na hali mikono yake ikiwa imenyooka kwa namna
ya msalaba ili kuwatumikia na kuwapenda watu ambapo utumishi wake huu ulimsababishia
mateso haya ya kutisha juu ya msalaba.Wakati akiteseka kwa adhabu ya huo usaliti, rafiki yake
Osinus mwindaji alikiri kuwa alishindwa kumfanya akubali kufanya suluhu na Jupiter ili kuacha
60 Doane, uk, 190 61 The History of Our lord
21
kuwakomboa watu, na hapo Osinus mwindaji alikimbia na kumucha akiwa hana yeyote
anayeumizwa na kifo chake zaidi ya kundi la wafuasi wachache wenye moyo ambao walimlilia
na hata wakaweza kuiondoa hali ya kupenda mabaya katika moyo wake”62
Bwana Doane anasema: “Wapagani walikuwa wakimuita Bacchus mwana wa Jupiter atokanaye
na mwanamke bikira, kuwa ni mwokozi, mwana wa pekee wa Mungu, dhabihu, mchukuaji wa
dhambi za watu na mkombozi. Walikuwa wakisema: “maovu yalipozidi ardhini Bandora
alimuomba Jupiter Mungu Mkuu ili aje na kuwakomboa watu kutoka katika makosa na dhambi.
Jupiter akakubali ombi lao na kumtoa mwanaye ili kuwakomboa wenye dhambi duniani.
Bucchus mkombozi akaahidi kuifanya dunia kuwa huru kutokana na mizigo ya dhambi. Pia
huimba na kumuabudu ili kulitukuza jina lake.Ili kukamilisha kazi hii, Mungu Jupiter alimshukia
mwanamke aitwaye Semele ambaye alichukua mimba na hapo akaitwa mama wa Mungu.
Vilevile Bucchus mkombozi wa watu, alisema: Mimi ndiye kiongozi wenu, mlinzi wenu na
mkombozi wenu. Mimi ndimi Alfa na Omega”.
Heracles mtoto wa Zanis alikuwa akiitwa MKOMBOZI, ambapo kulikuwa na pesa
iliyonakshiwa kwa maneno yafuatayo: “Heracles Mkombozi”.Vilevile walikuwa wakimuita:
Mwana wa pekee, Neno, na kwamba alirudi na kuungana pamoja na Mungu, na kuwa yeye ndiye
Muumba wa kila kitu, Baba wa nyakati. Vilevile Escolapius huitwa MKOMBOZI na hekalu
lililojengwa kwa kumbukumbu ya jina lake huitwa hekalu la MKOMBOZI. Mtawala wa Roma
Hadriyan (138 A.D) alikuwa akisema kuwa Serapis ni mungu. Katika moja ya mahekalu ya kale
huko Iskandaria kulipatikana msalaba ambao juu yake kulikuwapo picha ya huyu mkombozi wa
Kimisri.
Waajemi walikuwa wakimuita Mithra kuwa ni mpatanishi baina ya Mwenyezi Mungu na watu,
mkombozi ambaye alikubali mateso ili kuwaokoa na kuwakomboa watu. Vilevile husema kuwa
ni “Neno” na “Mkombozi” na kuamini kuwa Zoroaster ni mtume wa mungu aliyetumwa kuja
kuwakomboa watu kutoka katika njia mbaya. Mpaka sasa tunawaona wafuasi wake wakimuita
Zoroaster “aliyehai”, mbarikiwa, mwana wa pekee, wa milele pamoja na sifa nyingine kama
hizo. Halikadhalika (huamini kuwa) alipozaliwa ilitokea nuru iliyoangaza chumba alichozaliwa,
na kwamba alimchekea mama yake wakati wa kuzaliwa kwake, na humuita kuwa ni “Nuru
iangazayo iliyotokea katika mti wa maarifa na kwamba alitungikwa juu ya mti”.
Ariyan Katika historia yake kuhusu alama za Iskandaria anasema: katka bendera ya majeshi
ya Boreas kuna picha ya mtu aliyesulubiwa”.
Naye Higgins anasema: Hiyo picha inamuelezea ima Ostroba au Silvahana, kwani inaonekana
kwa mtazamaji kana kwamba ni picha ya mtu ambayo Waroma walikuwa wakiibeba katika
vichwa vya bendera zao nayo inafanana na picha ya njiwa ambaye Waashori walikuwa
wameiweka katika bendera zao na hakuna shaka kuwa ile picha ni picha ya “mwana wa mungu
aliyesulubiwa”.
Wamexico walimuabudu mungu aliyesulubiwa wakamwita Mkombozi, na dhabihu. Mwana
wa mungu kwa lugha yao humwita “Bakob” na “Oboukou”. Lau kama Wahispania
wasingevichoma moto vitabu vya wakazi wa Mexico na Peru, kuyabomoa mahekalu yao na
62 Doane, 192- 193
22
kuchora picha na alama zao, tungepata kufahamu mambo mengi kuwahusu, zaidi ya haya
tunayoyafahamu kwa sasa. Na lau kama si vitu vichache vilivyosalimika kutokana na mikono
dhalimu ya Wahispania tusingetambua ya kuwa walikuwa wakimuabudu mungu aliyesulubiwa
kama kafara ya dhambi zao, na ya kwamba walikuwa wakimuita kuwa ni mwana wa mungu
aliyetolewa dhabihu.
Wakazi wa Yokatani walimuabudu mungu aliyesulubiwa kuwa kafara ya dhambi zao na
kumwita kuwa ni mwana wa mungu . Ilipatikana idadi kadhaa ya misalaba iliyokuwa na picha
kamili ya huyu mtoto aliyesulubiwa kwa kafara ya dhambi”.
Bwana Kniht anafafanua zaidi kwa kusema:
Wapagani walikuwa wakimwita Apollo kuwa ni “Mchungaji mwema”,
halikadhalika wakamwita Mercury kuwa ni “ mchungaji mwema”. Na
Krishna mkombozi wa Wahindu aliitwa kuwa ni “mchungaji mwema”,63
na wengine wengi ambao kwa sababu ya kupendelea kufupisha
tunatosheka na tuliyoyaeleza .
II – Wakristo:
Kadhia ya kusulubiwa Kristo na imani ya ukombozi dhidi ya dhambi
ni msingi wa imani kwa wakristo. Habari ya kusulubiwa imeelezwa katika
injili ya Mathayo sura 27,64
Injili ya Marko sura ya 15,65
Injili ya Luka sura
23,66
pamoja na Injili ya Yohana sura ya 19.67
Hatuna haja ya kunukuu
vifungu vyote hivi kwa sababu ni mashuhuri sana. Lakini tunatoa kifungu kimoja kama mfano
wa yale yaliyoelezwa katika Injili kuhusu kusumbuliwa kwake.
Waraka wa Paulo Mtume kwa Wagalatia sura ya 13: “Kristo alitukomboa katika laana ya
Torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu, maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu
63 The Symbolical Language Of Ancient Art,ukurasa wa 22 64
Hata walivyokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene jina lake Simoni, huyu
wakamshurutisha auchukue msalaba wake… Walipokwisha kumsulubisha, waligawa mavazi
yake, walipiga kura. (Mathayo 27:32 -35) 65 Hata wakiisha kumdhihaki wakamvua lile vazi la rangi ya zambarau wakamvika mavazi yake mwenyewe;
wakamchukua nje ili wamsulubishe wakamshurutisha mtu aliyekuwa akipita, akitoka mashamba, Simoni
Mkirene, baba yao Iskanda na Rufo ili auchukue msalaba wake. Wake wakamsulubisha wakagawa mavazi yake,
wakapigia kwa kila mtu atue nini. Basi ilikuwa saa tatu, nao wakamsulubisha. (Marko 15:20 -26) 66 Lakini wakapiga kelele, wakisema, Msulubishe, .Lakini wakatoa sauti zao kwa nguvu sana wakitaka asulubishwe. Na walipokuwa wakimwondoa wakimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa akitoka shamba,
wakamtwisha msalaba auchukue nyuma yake yesu. (Luka 23:21-26) 67
Basi wale wakapiga kelele, Mwondoshe! Mwondoshe! Msulubishe! Pilato akawaambia, Je! Nimsulubishe
mfalme wenu! Wakuu wa makuhani wakamjibu, Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.
Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulubiwe nao wakampokea Yesu. Akatoka hali akijichukulia msalaba
wake mpaka mahali paitwapo Fuvu la kichwa au kwa Kiebrania, Golgotha.Wakamsulubisha huko, na wengine
wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku na Yesu katikati.
Yesu akiwa
msalabani, na
taji la miba
kichwani
mwake.
23
aingikwaye juu ya mti; Ili kwamba baraka ya Ibrahim iwafikie mataifa katika Yesu Kristo,
tupate kupokea ahadi ya roho kwa njia ya imani”.
Suala la kusulubiwa limetajwa katika Injili zote, na kumchora akiwa amesulubiwa moja kwa
moja kama Krishna. Na ama muda aliosulubiwa una khitilafu na kupingana katika maandiko
na hatukutaka kuielezea khitilafu hiyo kwa kuwa iko nje ya lengo letu.
SURA YA TATU
KIZA KILICHOTOKEA KUTOKANA NA KIFO CHA MKOMBOZI WA ULIMWENGU
I – Wapagani:
Wahindu husema kwamba: “Krishna mkombozi wao alipokufa msalabani, masaibu na ishara
nyingi zilitokea ulimwenguni, mwezi ukazungukwa na duara jeusi, kiza kikatokea wakati wa
mchana, mbingu ikanyesha moto na mchanga, ndimi za moto zikatokeza na mashetani
24
yakaanza kufanya uharibifu katika ardhi, na wakati wa kuchomoza na kuzama kwa jua
wakaonekana watu wakipigana kila upande na kila sehemu”.
Bwana Davis anasema kwamba Wahindu husema “Ilipoanza vita baina ya Buddha Mkombozi
wa ulimwengu, na kiongozi wa Mashetani, maelfu ya nyota yalidondoka, kiza kikatanda na
mawingu yakakithiri hata hii dunia yenye mabahari na milima ilitingishika kana kwamba ni
chembe ndogo inayopeperushwa, na bahari zikachafuka kutokana na kuzidi kwa matetemeko.
Maji ya mito yalirejea kwenye vyanzo vyake, milima na miti yake iliyodumu kwa vizazi na
vizazi iligongana. Ngurumo za vimbunga zikashtadi. Sauti ya mgongano ilikuwa kubwa sana.
Jua lilipungua nuru yake na kiza kinene kikatanda. Anga lilijaa ngurumo za roho”.68
Bwana Farar anasema: “Warumi na Wayunan wa zamani waliamini kuwa wakati wa kuzaliwa na
kufa kwa mmoja wa watu watukufu matukio kadhaa yanayoelezea hali hiyo hutokea katika
mbingu. Waliwahi kusema kuwa jua lilipungua nuru yake kwa kifo cha Rumulus muasisi wa
Roma na kutokea giza juu ya uso wa dunia lililodumu kwa muda wa masaa sita”.69
Bwana Gibbon anasema: alipouawa mkombozi Iscolapius jua lilipungua nuru yake, ndege
wakajificha katika viota vyao na miti ikainamisha matawi yake kama ishara ya huzuni. Mioyo ya
watu iliumia, kwani mponyaji wa maradhi na njaa yao alikuwa ameiaga dunia”70
Bwana Doan anasema: wapagani husema: “Heraclus alipokuwa katika hali ya kukata roho
alimwambia mwanamke mwaminifu aitwaye Youl aliyemfuata mpaka eneo alilokata roho: Usilie
kwani kazi yangu imekamilika na sasa ni wakati wa kupumzika, na tutakutana katika nchi yenye
nuru. Pia Mungu Mkombozi alipokufa giza lilitokea ulimwenguni ambapo Mungu Mkuu Zius
alishuka kumchukua mwanaye na kumpeleka kwake, na viwanja vya Ulimpios vikafunguliwa ili
kumlaki shujaa mweye nuru ambaye amepumzika kutokana na mateso makali na kuwa sasa huko
aliko amevaa vazi jeupe na taji kichwani mwake”.
Vilevile husema kwamba Pius alipotaka kuiacha hii dunia yenye kila aina ya mateso na huzuni,
alimwambia Antiyocon: ubaki salama, na usilie ewe mwanangu, kwani nina furaha yakuutua
mzigo wa huzuni na mashaka”, na hapo ulipokaribia muda wa kifo chake, zilijitokeza alama
nyingi mbinguni na ardhini. Ardhi ilitingishika na ngurumo za radi zikaenea angani.
Warumi walikuwa na mungu aliyeitwa Cyirinus aliyetokana na jua na hatimaye kurejea juani.
Alizaliwa baada ya mungu wa majeshi kumshukia mwanamke bikira mwenye asili ya kifalme.
Olius dhalimu alimtesa na akalelewa kwa wachungakondoo. Alipokufa alikatwa vipande
vipande, na alipopaa kwenda mbinguni jua lilipungua nuru yake.
Bwana Kingsbrough anasema: “Wamexico wa zamani walikuwa wakiamini kuwa Quetzalcoatl
mkombozi aliyesulubiwa, alipokufa jua ilififia nuru yake na mwanga wake ukapotea”71
II – Wakristo:
68 Budhism, uk. 36 69 The Life of Christ, uk.52 70 The History of Gibbon, uk.159 na 590 71 Antiquinties of Mexico, juzu ya 6,uk,6
25
Tumetoa maelezo ya waumini wa miungu mbalimbali, kama vile, Krishna, Budha, Andra na
wengineo kuhusu kiza kilichotokea wakati wa kifo cha moja ya miungu hii iliyotajwa, iwe ni
kwa kusulubiwa au kuuawa. Mambo hayo vilevile yameelezwa kutokea wakati wa kusulubiwa
Yesu Kristo.Tazama Injili ya Mathayo, sura ya 27, msitari wa 45: “Basi tangu saa sita palikuwa
na giza juu ya nchi yote hata saa tisa”.72
Injili ya Marko, sura ya 15, msitari wa 33,73
pamoja na
Injili ya Luka,sura ya 23 msitara wa 44.74
72 Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema: Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani Mungu
wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? (Mathayo 27:46) 73 Na ilipokuwa saa sita, palikuwa na giza juu ya nchi yote, hata saa tisa. Na saa tisa Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Maana yake, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? (Marko 15:33 -
34) 74 Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda. Jua limepungua nuru yake; pazia la
hekalu likapasuka katikati.Yesu akalia kwa sauti kuu, akisema, Ee Baba, mikonono mwako naiweka roho yangu.
(Luka 23:44 - 45)
26
SURA YA NNE
KUZALIWA KWA MIUNGU WALIOJITOA DHABIHU ILI KUWAKOMBOA WATU
I – Wapagani:
Bwana Doane anasema: Miongoni mwa imani za Wahindu ni kusema kwao kuwa mmoja wa
miungu alijigeuza katika mwili na akashuka na kuishi nao. Hayo yameelezwa kwa aina
mbalimbali za fikra na simulizi za kimashariki. Krishna mpaka sasa ndiye mungu anayependwa
sana na wanawake wa Kihindu, na kundi linalomheshimu limetopea katika kumuabudu, ambapo
lilieneza mafundisho linaloshikamana nayo sana ambayo husema kuwa Krishna anatofautiana na
miungu wote waliojigeuza katika mwili kwa sababu hao wengine walikuwa na sehemu ndogo ya
uungu, lakini Krishna ndiye Mungu Vishnu aliyedhihiri katika mwili wa kibinadamu”.75
Allen naye anasema: “Krishna ndiye mkuu kuliko miungu wote waliojibadili katika mwili.
Anatofautiana nao sana kwa sababu walikuwa na sehemu ndogo ya uungu, ama yeye (Krishna)
ndiye Mungu Vishnu aliyedhihiri kwa mwili wa kibinaadamu”.76
NayeToma Maurice anasema: “Wahindu huitukuza sana nchi yao kwa kuwa humo ndimo
alimozaliwa Krishna katika mwili”77
Doane anasema: Wahindu husema kuwa Krishna ni mtoto wa mwanamwali, mtakatifu, Devaki
ambaye humuita mama wa Mungu”.
Katika kitabu cha Kihindu kiitwacho “Biha Kafat Purun” kuna maelezo
kuwa Krishna alisema: “Nitajigeuza katika Mitwar katika nyumba ya
Yado na kutoka katika kizazi cha Devaki nitazaliwa na kufa, na sasa
umefika muda wa kuonyesha nguvu zangu na kuikomboa dunia kutokana
na mizigo ya madhambi”.
Na katika kitabu kitakatifu cha Wahindu kiitwacho “Vishnu Purana”
kuna maelezo yafuatayo: “Miungu imemtukuza Devaki ambaye
aliichukua mimba ya Mungu mwenye macho ya huruma – Mkombozi wa
ulimwengu -, na nani awezaye kuutazama uso wa Devaki kwa
sababu ya nuru iangazaye, kwani kila anayeitazama nuru yake huweza
kukimbia (kugeuza uso wake)… Na miungu wasioonekana kwa watu
wamemtukuza tangu Vishnu alipomshukia. Mungu Vishnu ndiye chanzo
cha mti wa mambo yote, hadirikiwi na fikra za miungu, majini, wanafalsafa
na watu wote, hivi sasa na hata baadaye, kama vile ambavyo hazikumdiriki
hapo zamani, na Brahma ndiye Muabudiwa. Miungu wote walipata heshima ya kuukomboa
ulimwengu kutokana na mizigo yake mizito kwa kumtuma Vishnu kwenye tumbo la Devaki,
kuzaliwa naye kama mwanaye na kudhihiri kama Krishna ambaye ndiye Brahma mwenyewe, na
kwamba ni siri ya ajabu kwa Mungu kuwa katika mwili wa binaadamu”. Vilevile akasema: Mimi
75 Doane,ukurasa wa 112 76 India,ukurasa wa 397 77 The history of Hindostan, juz. 3, uk, 43
Devaki, mama
wa mungu akiwa
na Krishna
mwanaye
27
ndiye mkuu wa pekee, nauthibitisha uwepo wangu kwa uweza wangu. Na pindi mema
yanapopungua na machafu kuongezeka ulimwenguni, hudhihiri na kuonekana kutoka kizazi hadi
kizazi ili kumbakisha mtu mwema na kumuangamiza muovu na kurejesha mema ulimwenguni”.
Katika kitabu kiitwacho “Bahaqiqat Jita” imeelezwa kuwa Mungu Krishna alimwambia
mwanafunzi wake aitwaye Arjuna: Nawe Ee Arjuna, ambaye kwa sababu ya imani yako umekiri
uungu wa kuzaliwa kwangu, ungana nami na uingie ndani mwangu”. Vilevile akasema:
“Wajinga hawakiri uungu wangu na kwamba mimi ni Mungu wa kila kitu, na hunidharau kwa
sababu ya kuwa kwangu katika mwili wa kibinaadamu wakiegemea kwenye shari, uovu na
vitimbi vilivyomo katika nyoyo zao, basi matarajio yao, elimu zao, fikra na tabia zao ni chafu.
Ama watu wenye akili zenye uelewa huegemea kwenye maadili yao ya Kimungu na kutambua
kuwa mimi ndiye wa milele niliyekuwapo kabla ya chochote. Huniabudu kwa mioyo
isiyoegemea upande wa miungu wengine”.
Bwana Doane anasema: “Mungu Budha, mtoto wa Bikra Maya ambaye huabudiwa na
Mabuddha wa India na wengineo, huelezewa kuwa aliiacha Paradiso akashuka ulimwenguni na
kudhihiri katika mwili wa kibinadamu kwa sababu ya huruma kwa watu ili apate kuwaokoa
kutokana na dhambi, kuwaongoza kwenye njia iliyonyooka, kuichukua mizigo ya dhambi zao,
kuwakomboa kutokana na adhabu na kuwaondoshea kisasi walichostahiki kukipata”78
Katika kitabu cha Kichina kiitwacho ((Fotinghang)) kuna maelezo yafuatayo: Mungu Budha
alipotaka kuteremka duniani ili azaliwe humo aliwaita malaika wa mbinguni na wakazi wa
ardhini akisema: Enyi wafu! Pambeni ardhi yenu kwa sababu Budhishu Mahte mkuu
atateremka hivi karibuni kutoka Tusiya na kuzaliwa baina yenu, kwa hiyo jiandaeni kwa
mavazi ili kumngojea.Vile vile husema kwamba kizazi (tumbo) atakachoshukia Mungu Budha
ili kuwa katika mwili ni kama chombo kilichowekwa dhahabu ndani yake na hakuna mwanadam
yeyote anayoweza kubebwa humo kama ilivyokuwa kwa Budha kwani yeye atashuka humo
pasipo kwa njia ya manii. Bahamaya alipochukua mimba yake hakupata kutamani mwanaume
tena na akaishi akiwa bikira.
Katika kumzungumzia Budha, Hock ambaye ni mmoja wa wamisionari wa kifaransa ametoa
maelezo yafuatayo: Mabudha humuona kama Mungu aliyechukua mwili (yaani mwili wa
kibinadam) akaja katika hii dunia ili kuwafundisha watu, kuwaongoza, kuwakomboa na
kuwajengea njia ya amani…na imani ya kukombolewa kwa njia ya Mungu anayeonekana kwa
mwili wa kibinadamu imeenea sana kwa Mabuddha.
Wapagani humuelezea kila mungu aliyechukua mwili ili kuwakomboa watu kuwa ni Mungu
Mkuu, Mungu wa ulimwengu, Mweza, Mjuzi, mwenye hekima na mkombozi wa watu wote79
Bwana Bunsen anasema: Na mungu wa pekee humuita kuwa mtakatifu, muumba wa saada,
mfalme wa yote, Bwana mwenye nguvu, asiye na mwanzo wala mwisho, mwenye utukufu, roho
mkuu wa milele, Mungu ambaye ni lazima kwa watu walio huru kumuabudu.
78 Doane, ukurasa wa 115 79 Oriental Religions, uk.604
28
Katika maombi ya mcha mungu Ammora kwa mungu Buddha aliyedhihiri katika mwili, kuna
maelezo yafuatayo: Ukuu ni wako ewe uliyejidhihirisha kwa jinsi ya Budha aliyejichukulia
mwili, Ewe mola wa ulimwengu utukufu ni wako, Ewe mungu wa milele uonekanaye katika
mwili heshima ni yako. Ewe mola wa dhahiri na rehma, Ewe muumba wa mateso na huzuni,
Ewe muumba wa kila kitu, Ewe mlinzi wa ulimwengu, Ewe mjuzi wa rehma na alama zake,
Ewe Mkombozi.
Bunsen anasema: Mabuddha husema kuwa kuzaliwa kwa Budha kulikuwa hivi:Gautama
Buddha alipojichukulia mwili, nguvu ya kimungu iitwyo roho mtakatifu ilimshukia Bikira
Maya, na kuteremka kwake ilikuwa ni kwa namna ya tembo mweupe. Na Mabuddha wa Tekasi
husema kuwa maana ya tembo mweupe ni hekima na nguvu .
Doane anasema: Mabuddha wa India husema kwamba kushuka kwa malaika ambaye alikuja
kuwa Budha na kuwa katika mwili, ilikuwa kwa njia ya rehma, na kwamba tembo ambaye
(Budha)alishuka kwa namna yake ni alama ya nguvu na hekma ya kimungu.Vile vile katika
Tekasi humuelezea kuwa alishuka kutoka mbinguni kwa namna ya tembo mpaka mahali
alipokuwa Bikra Maya . Lakini Mabudha wa China hueleza katika vitabu vyao kuwa roho
mtakatifu ambaye ni “shing shen” Alimshukia Bikra Maya . Katika kitabu cha kichina
kiitwacho Forbinhang kuna maelezo yafuatayo: Mama akiona usingizini mwake kwamba tembo
mweupe ameingia ubavu wake wa kulia, ikiwa atazaa mtoto wa kiume basi atakuwa kiongozi wa
ulimwengu ambaye ni Buddha na kila kiumbe kufaidika naye, nayeye ndiye awezaye kuwaokoa
watu kutoka katika mabahari ya maovu na huzuni.
Anasema Profesa Ferguson: Mabudha humchora Maya akiwa amelala na
kuona usingizini mwake kuwa tembo mweupe anakuja na kuingia katika
ubavu wake wa kulia. Humuimbia nyimbo mbali mbali kuwa amejaa
neema na ni malkia wa mbinguni na muondoshaji wa huzuni na kwamba
mwanaye Budha ni mfufuaji wa watu, tegemeo la mataifa na mwenezaji
wa amani. Na malkia Maya atamzaa mtoto mtakatifu mwenye hekima
ambaye kila kiumbe kitafaidika naye na atautawala ulimwengu.
Anasema Isbans Hard kuwa: mwili wa malkia Maya ukawa angavu kama kioo,
ndani yake akionekana mtoto kwa urahisi kana kwamba ni kuhani aliyeketi juu
ya kiti cha enzi akitoa baraka au kama picha ya dhahabu katika chombo angavu
ambako huonekana maendeleo yake siku hadi siku. Hivyo ndivyo Mabudha
wanavyoamini.Vile katika ukurasa 85 anasema: mwakilishi wa Budha duniani
anaitwa Dlailama au Lama mkuu. Na wakazi wa Siyami humuamini mungu
aliyezaliwa na mwanamke bikira wanayemwita mungu mkombozi ajulikanaye
kama Kodam kwa lugha yao, na mama yake ni binti mzuri, mwanamwali, ambaye alifunuliwa
na mungu akajitenga na watu na kwenda kwenye maeneo ya misitu isiyopitiwa na watu
akisubiri kuchukua mimba ya mungu kama alivyofunuliwa. Ndipo siku moja alipokuwa akisali
alichukua ujauzito kutoka kwenye mionzi ya jua iliyomshukia. Alipohisi kuwa na mimba
alitoka huko na kuelekea pwani ya ziwa lililopo Siyam na Kabodia na huko alijifungua mtoto
wa kiume kutoka mbinguni . Mtoto huyo alipokuwa mkubwa akawa mfano na chemchem ya
hekima na alifanya mambo mengi ya ajabu.
Bikira
Maya
mama wa
mungu
buddha
29
Profesa Doane anasema: Wayuropa waliokwenda Komoron kusini mwa India walishangaa
kuwaona wakazi wa eneo hilo wakimuabudu mungu mkombozi waliyemwita (Slivahana) na
jina la baba yake (Tishaga)na kuwa huyo mwana wa mungu alizaliwa na mwanamwali, na
kwamba huyo ndiyo Vishnu mkuu aliyechukua mwili wa kibinadam.
Wachina huamini miungu walioonekana katika miili akiwemo Fohi, Satin Nong, (Wangat) na
wengineo. Wachina wa Kasaki husema kuwa Bikra Maya alichukua mimba ya Buddha
aliyoipata akiwa usingizini na kumzaa kupitia ubavuni mwake kama ishara ya utakatifu
tofauti na wajawazito wengine wanavyowazaa watoto wao.
Pia huhadithia mambo mengi ya ajabu kuhusu kuzaliwa kwa Laokyon enzi za utawala wa
Tonkong miaka 604 kabla ya Kristo.Wanasema kuwa Budha alikuwepo tangu mwanzo
akashuka duniani na kuzaliwa na mwanamwali mweusi lakini mzuri na mwenye mvuto.
Walijenga mahekalu mengi kwa ajili ya kumuabudu ambapo humuabudu kwa madai kuwa ni
mungu aliyejidhihirisha katika mwili.Wanafunzi wake huitwa walimu kutoka mbinguni na
kuamini kuwa makuhani ndio njia kuu ya kupata utakatifu na ukombozi kwa watu wote.
Hujinyenyekeza mbele yake kama muumba na mtengenezaji wa mbingu na ardhi. Vilevile
huamini kuwa mamayake alimzaa kupitia ubavuni akiwa chini ya miti. Ama kuzaliwa kwa
Hauwoki wanakuelezea kama ifuatavyo: Mama yake alikuwa mgumba akamtolea sadaka bwana
ili apate kumuondolea ugumba, kisha akafuata nyayo za bwana na hapo akachukuliwa kwenye
eneo tukufu akachukua mimba na akajitenga na watu na kumzaa kama mwanakondoo na
kumwita Hauwoki na wakati wa kuzaa hakuhisi machungu ya mimba na hili linaonyesha
uumbwaji wake wa ajabu.
Mungu alimhurumia na kuitazama sadaka yake safi akaikubali na akamzaa mwanaye kwa
urahisi. Kila mtoto azaliwaye na bikra humwita mtoto wa mbinguni ambapo katika lugha ya
kichina humwita Tiyansh.
Wamisri husema kuwa: Horus mkombozi alizaliwa na mwanamwali Isis na kwamba ni mzawa
wa pili wa Ammon. Huchora akiwa mikononi au juu ya mapaja ya mama yake.
Profesa Chamblion ametafsiri yafuatayo kutoka katika maandishi ya kihiroglifu ya zamani:
“Wewe ndiwe mungu mlipa kisasi na mwana wa mungu. Ni wewe Horus mlipa kisasi, wewe
ndiye aliye kutangaza Osiris kwamba utazaliwa na mungu Isis”. Kadhalika Wamisri husema
kuwa mungu Ra alizaliwa kupitia ubavuni mwa mama yake na sio kama wazaliwavyo watu
wengine. Kwenye kuta za hekalu moja huko Tibani kuna picha inayomuonyesha mungu, Tut
mjumbe wa mungu akisema: Malkia bikra Mutemus atamzaa mwana aliye mungu atakaye kuwa
mfalme Omonotov. Walikuwa wakieleza kuwa wafalme wao ni miungu. Vile vile miongoni
mwa wafalme wao kuna waliodai Uungu. Katika kumuelezea Zoroster mtume wa Waajemi
husema kuwa: ametokana na nuru ya mungu sio kama wanavyoumbwa watu wengine.
Aliumbwa bila uchafu yaani mama yake hakuguswa na mwanaume. Plato naye anasema:
Waabudu moto wa Uajemi humwita kwamba ni mwana wa mungu.
Tunashangaa kuona Wayunan walikuwa wakiwaita mashujaa wao hapo zamani kuwa ni
miungu au watoto wa miungu na kwamba walijidhihirisha katika mwili wa kibinadam na baada
ya kufariki waliungana na miungu. Walikuwa wakiwatolea sadaka za kuteketezwa, kuwaabudu
pamoja na mabo mengine. Miongoni mwa watoto wa mungu ni Hercules mwana wa mungu
Jupita aliyezaliwa kwa mwanake wa asili ya Jupita (Kamini) Malkia wa Tibas. Zous Mungu wa
30
miungu anasema kuhusu Hercules: Ni mtoto wake, vilevile akasema leo atazaliwa kwetu mtoto
wa kiume mjukuu wa Prisius atakuwa na nguvu zaidi kuliko watu wengine wote.
Wanaamini pia kuwa Bucchus ni mtoto wa mungu Jupita aliyezaliwa kwa
mwanamke wa kibinadam aitwaye Semele binti wa Kedamus mfalme wa
Tipas, na kwamba aliwahi kusema: Mimi ndiye Bucchus mtoto wa
mungu Zous niliyezaliwa na Semele mwana wa Kedamus niliyekuja
katika nchi ya Tipas. Niliumbwa kwa nuru ya umeme wa radi na
kuchukua mwili wa binadam badala ya mwili wa kimungu. Nimefika
kwenye chemchem ya Dirus na maji ya Isminus.
Mambo hayo pia yanaelezwa kuhusu Amvion mwana wa mungu Jupita
aliyezaliwa kwa mama wa kibinadam Athiub binti wa mfalme Nistius wa
Boataya.
Wanadai kuwa Prumisius (jina hili ni la kiyunan lenye maana ya jicho na
ulinzi wa mungu) ni mungu ambaye Uungu na ubinadam wake viliungana akawa
na maumbile mawili ya uungu na ubinadam katika mwili mmoja ambapo ni
binadam na mungu wa kweli kwa wakati mmoja. Na Pirisius mtoto wa Jupita
aliyezaliwa na bikira Danya mwana wa Krisius mfalme wa Argos walimuabudu wakasema kuwa
ni mungu wakamjengea hekalu katika Athena ambalo lilitumika kwa ajili ya kuabudu.
Wanasema tena kuwa Mercury ni mtoto wa Jupita aliyezaliwa na mama Atlas mwenye asili ya
kibinadam. Husemekana kuwa Silinne huko Arkadia ndipo alipozaliwa na kulelewa na ndipo
lilipojengwa hekalu kubwa kwa ajili ya kumuabudu. Pia wanaamini kuwa Yulus mfalme wa
visiwa vya Libare Sysilia ndiye mwana wa Mungu Jupita aliyezaliwa na Avasta mama mwenye
asili ya kibinadamu.
Na wanasema kuwa Apollo ni mwana wa Mungu Jupita aliyezaliwa na mama mwenye asili ya
kibinadamu aitwaye Latuna. Na Waovis husema kuwa alizaliwa chini ya mti kama wasemavyo
wafuasi wa Budha juu ya Budha na Lao, kuwa Latuna mama yake alikaa chini ya kivuli cha
mzaituni na na kumzaa. Alipomzaa miungu katika Olimpios walifurahi na mbingu ikatabasamu
na kucheka.
Walikuwa wakimuita Artos kuwa ni mwana wa Jupita aliyezaliwa na mwanamke mwenye asili
ya kibinadamu, wakasema vilevile kuwa Aroclos ni mwana wa Jupita aliyezaliwa na mama
mwenye asili ya kibinaadamu. Kuna majina mengine mengi ya wale waliodai kuwa ni wana wa
Jupita waliozaliwa na wanawake wenye asili ya kibinaadamu. Tumeacha kuwataja kwa lengo la
kufupisha.
Ni mambo yaliyowazi kuwa Wayunani na Warumi walikuwa wakibudu miungu na watoto wengi
wa miunmgu ambapo maombi yafuatayo ya Arfius kwa Jupita yandhihirisha hilo: “Wewe
ndiwe muweza,wa kwanza na wa mwisho.Wewe ndiwe Mungu Jupita mpaji wa kila kitu, na
mwanzilishi wa ardhi na mbingu yenye nyota”.
Naye Doane anasema: “Warumi walikuwa wakiwaita wafalme wao kuwa ni miungu,
wakiwaabudu na kuwafanyia masanamu”.
Yafuatayo ni majina ya wafalme wa Kirumi waliofanywa kuwa miungu:
Confucius
31
Mmmoja wapo ni Romulus mwasisi wa taifa la Roma wanayemuita kuwa ni “mwana wa
Mungu” aliyezaliwa na mwanamke bikra aliyeitwa Rasilvia. Na wanasema kuwa Kaisari Yulius
ni mwan wa Mungu.
Vilevile wanasema kuwa Kaisari Augastos ni mwanadamu na ni Mungu. Habari za uungu wake
zimeelezwa katika ushairi wa Virgil ambapo anasema kuwa ni mwana wa Jupita.Walimjengea
mahekalu kwa ajili ya kumuabudu ikiwa ni pamoja na kuwateua wakuu na viongozi wa hayo
mahekalu ili wapate kumuabudu ndani yake. Vilevile walimfanya Clorius kuwa Mungu, na
walikuwa wakiwaita wafalme wa Kirumi kwa majina yafuatayo “Mola wetu, Mwalimu, Bwana
wetu na Mungu wetu”.
Walimzungumzia Alexander Mmacedonia aliyezaliwa miaka 356 kabla ya Kristo, kuwa ni
Mungu wa dunia na mwana wa Jupita aliyezaliwa na mama mweye asili ya kibinaadamu aitwaye
Olimpias. Siku moja alitembelea katika hekalu la Jupita Ammon lililojengwa katikati ya jangwa
la Lipian na huko akasikia sauti ikimwita: “Wewe ni mwana wa Mungu” na tangu hapo akawa
anapitisha amri na hukumu na mengineyo kama ifuatavyo: “Alexander mwana wa Jupita
Ammon”. Vilevile Socrates amemtaja Alexander katika shairi lake kuwa ni Mungu na ni mwana
wa Mungu Jupita. Na Ptolemy - ambaye ni mmoja wa viongozi (wa kijeshi) aliyekuwa pamoja
na Alexander – walimfanya kuwa ni Mungu. Mtu huyu alipata kuitawala Misri baada ya kifo
cha Alexander80
ambapo raia wake walikuwa wakimuita kuwa ni “Ptolemy mkombozi”. Neno
Soter ambalo huitwa kwalo lina maana ya “Mkombozi”.
Wanasema kuhusu Sirus mfalme wa Uajemi kuwa ana asili ya kimungu, na kusema kuwa ni
Masihi au Mungu aliyepakwa mafuta.
Wanasema pia kuwa Plato ni mwana wa Mungu. Alizaliwa katika Athena mwaka wa 429 kabla
ya Masihi Issa (a.s.) na kuamini kuwa alizaliwa na mwanamke bikra, msafi na mtakatifu, na
kwamba Izis ambaye hudaiwa kuwa ndiye baba yake aliweka nadhiri kwa ndoto aliyoiona kuwa
hatamkurubia,wala kumgusa mpaka atakapojifungua, kwa kuwa amechukua mimba ya Mungu
Apollo.
Na mama wa Apollonius alisema kuwa alimuona mmoja wa miungu akimwambia kuwa
atazaliwa kwake na baada ya siku kadhaa kupita alimzaa, na pindi alipokuwa mkubwa aliweza
kuwa miongoni mwa walimu wakubwa ambao walionyesha maajabu na miujiza. Alizaliwa
miaka 40 kabla ya Masihi (a.s).
Wanadai kuwa Phethagorus ni mungu, na kwamba mama yake alichukua mimba kupitia maono,
na hayo maono ni Roho Mtakatifu, na baba yake huitwa kwa jina hilo tu, na kuwa aliambiwa
kwamba mkewe atazaa mwana atakayewanufaisha watu.
Wanaamini pia kuwa Iscolapius mwenye nguvu, miujiza na maajabu ni mwana wa Mungu
aliyezaliwa kwa mama mweye asili ya kibinadamu aitwaye coronius.Wamiscion walipowauliza
wakuu wa makuhani kuhusu muda, mahali atakapozaliwa na jina la baba yake, wakawajibu:
Mungu ndiye baba yake, na mama yake mweye asili ya kibinaadamu ni Coronius, na atazaliwa
katika mji wa Abidus.
80 Alexander the great (356 – 324 B.C) alizaliwa katika mji wa Macedonia na kufia katika mji wa Babel. Alikuwa
mwanafunzi wa Arestote. Alishika madaraka baada ya baba yake Philip na kuishinda Uajemi na kufika kwenye mto
Sind
32
Wakazi wa Roma waliamini uungu wa Simon Msaamari ajulikanaye kama “Magos” au
“Mchawi”, aliyeishi wakati wa Masihi (a.s).Walidai kuwa alitenda miujiza na maajabu ya
kushangaza, na picha yake wakaiweka pamoja na picha za miungu wengine zilizopatikana katika
mji ule. Mwanahistoria Yucipius amemnukuu marehemu Justin kuwa Warumi walikuwa
wakiuamini uungu wa Simon Mchawi, na juu ya daraja lililopo kwenye mto wa Tibris kuna
maneno yafuatayo “Simon Mungu Mtukufu”.
Wakazi wa mataifa ya kaskazini mwa Ulaya kama vile Wanorway, Waholland na wengineo
walikuwa wakiwasifu mashujaa wao kwa uungu, na kwamba wao ni watoto wa Mungu
Odin.Vilevile waliwapa washairi sifa za uungu.
Wanasema kuwa Tour ndiye mwana wa kwanza wa Mungu Odin. Na kuhusu Badora walikuwa
wakisema kuwa ni : “mwema, mkombozi, mwana wa Mungu Odin, na mama yake ni Mungu
Wafrige.
Nao wakazi wa Mexico, vizazi vingi kabla ya ujio wa Colombus, 81
walikuwa wakimuabudu
mungu mkombozi aitwaye “Quetzalcoatl” aliyezaliwa na mwanamke bikra na mtakatifu.
Walikuwa wakidai kwamba mjumbe kutoka mbinguni alikuja na kumpa habari mama yake kuwa
atachukua mimba pasipo kulala na mwanamme, na jina la mama yake ni “Bikra Hoishiqthral
malkia wa mbinguni”. Na wanasema kuwa alimzaa katika nchi ya Nola". Nao jamii ya Mayayo
Gatan wa Amerika huamini kuwa “Dhama” ndiye Mungu Ganishahan.
Wamiotisko wa Columbia wanamuamini mungu aitwaye Boshiga, mwana wa Baba Mkuu.
Nao wakazi wa Nikazako wanaye mungu aitwaye Soma Toyo, ambapo husema kuwa alimtuma
duniani mwanaye Thyobatlahi aliyewafundisha na kuwaongoza njia ya uongofu.
Wakazi wa Peru 82
wanaliabudu jua, na kusema kuwa mungu huyo alipoona ouvu wa watu
unakithiri alimtuma mwanaye aitwaye Malko ili awaelimishe na kuwaongoza njia iliyo sawa
sawa.
Waadios wa Clifarnia wanasema kuwa Muumba Mkuu Niparaga alimtuma mwanaye aje duniani
kuwaongoza Wahindu na kuwafundisha dini. Kwa sababu ya chuki, akauawa na maadui.
Wanamuabudu kwa hoja kwamba ndiye anayestahiki kuabudiwa na kutukuzwa, na ndiye
mpatanishi kati ya wakazi wa ardhini na mungu Niparaga.
Wairoquois wanamuabudu mungu aitwaye Itharangwagan ambaye kwa upande mmoja
wanamchulia kama binadamu na upande mwingine kuwa ni mungu aliyejidhihirisha katika
mwili wa kibinaadam kisha akawaanzishia serikali yao. Husema pia kuwa ni Roho Mkuu.
Waagbobo ambao ni miongoni mwa Wahindu wa Amerika humuamini mungu aitwaye
Michabweh aliyejidhihirisha katika mwili wa binaadamu, na kwamba yeye ndiye mwana wa
pekee wa mungu wa mbinguni. Husema kuwa alizaliwa na mama mwenye asili ya
81 Chritopher Colomb: alizaliwa Janwa Italia na kufia Hispania, aliigundua Amerika mwaka 1492 82 Jamhuri ya Peru, iko katika bara la Amerika ya kusini, ikipakana na Brazil na Bolivia kwa upande wa mashariki,
Ecuador na Colombia kwa upande wa kaskazini, ambapo inapakana pia na Chile kwa upande wa kusini, na ikiwa
karibu kabisa na bahari ya Pacific, na mji wake mkuu ni Lima
33
kibinaadamu.Wanamheshimu sana huyu mungu aliyejifanyia mwili na kusema kuwa ni
“mkombozi wa watu”.
Wapagani wana miungu mingi iliojidhihirisha kwa mwili, tofauti na hao tuliowataja. Anayetaka
kuwafahamu arejee katika vitabu tulivyovitaja.
BIKRA MARIAM MAMA WA MUNGU YESU KRISTO
Ama mtazamo wa Wakristo kuhusu bikra Mariam kuwa mama wa Mungu, ni kama mtazamo wa
wapagani juu ya mama wa miungu. Jambo hili ni mashuhuri sana kwani hufikia hata kumuimbia,
kumtukuza na kujinyenyekeza kwake katika siku maalumu wanazoziita kuwa ni “Siku za
Mariam”. Humuita kuwa ni “Malkia wa Mbinguni, mama wa Mungu aliyejaa neema na mwenye
utukufu na cheo duniani na mbinguni”, pamoja na sifa nyingine nyingi za ukuu na uungu.
Katika Injili ya Luka (chapa ya Christian) msitari wa kwanza kifungu cha 28 kuna maelezo
yafuatayo: “Akaingia nyumbani kwake, akasema, salamu, uliyepewa neema. Bwana yu pamoja
nawe”. Imani ya kwamba ni mama wa Mungu ilipatikana katika kikao cha Afisos mwaka 431
baada ya Kristo.
Bwana Doane ameeleza kwa ufupi yafuatayo: “kama tunavyoona wapagani wakiwa na mama wa
miungu wakiwatukuza na kuwapa majina ya ukuu, vilevile tunaona kuwa Wakristo wana mama
wa Mungu wanayemtukuza na kumpa majina kama yale ambayo Wapagani huwapa mama wa
miungu yao. Hayo yanaungwa mkono na picha wanazozichora zikimuonyesha akiwa amemlea
mwanaye kristo, kwani zinafanana moja kwa moja na picha wanazozichora wapagani kuhusu
mama wa miungu wao” 83
Umeona picha na michoro kadhaa ambayo unaweza kuilinganisha na ile inayopatikana siku hizi
kwa Wakristo na ujaribu kuangalia kipindi kirefu kilichopita baina ya miungu wa kipagani, kama
vile Budha, Krishna na wengine, na baina ya Yesu Mungu wa Wakristo. Na Wachina huiweka
picha ya mungu wao “Shinmo” katika mahali pazuri katika nyumba zao na kuifunika kwa
kitambaa cha hariri. Pia mahekalu mengi yamejengwa kwa jina lake likiwemo hekalu la “mama
wa Mungu Mtsubo” kama wafanyavyo Wakristo kuhusu picha za Mariam na kujenga mahekalu
kwa jina lake kama vile “kanisa la Mtakatifu” na “kanisa la Bikira”.
Wamisri wa zamani walikuwa wakimuita mama wa mungu Isis, au mama wa mwokozi
Horus kwa majina mengi kama vile, MTAKATIFU, MALKIA WA MBINGU, NYOTA YA
BAHARINI, MAMA WA MUNGU, MUOMBEZI, BIKIRA, n.k. na kumchora akiwa
amesimama juu ya mwezi na kuzungukwa na nyota kumi, kama Wakristo wanavyomchora
Mariam akiwa amesimama mwezini akizungukwa na nyota kumi na mbili. Isipokuwa picha za
mama wa miungu ya kipagani zilikuwapo kwa kipindi cha karne nyingi kabla ya zile za Mariam.
Zingatia!!
Mtakatifu Abifanius, akielezea kuhusu Imani ya Wamisri juu ya Bikira aliyetajwa kuwa mama
wa Mungu, anasema “Hapana shaka kuwa walifunuliwa tangu kale kuhusu Bikira na mimba
yake” 84
83 Doane, 336 – 338 84 Egyptian Belief, uk. 143
34
Bonwick anasema: “ katika kitabu cha zamani cha Wakristo kiitwacho “kitabu cha habari za
Alexandria” kuna maelezo yafuatayo: “Tazameni namna Wamisri wanavyochora picha za kuzaa
kwa Bikira na Mwanaye”, na haya ndiyo yasemwayo na Wakristo kuhusu kuzaliwa kwa Masihi,
pamoja na kwamba kipindi kilichopita baina ya simulizi hizi mbili ni kirefu sana.
Na sikukuu ya kuingia kwa Kristo hekaluni na kumtakasa mwanamke mtakatifu, ambayo
hufanyika Februari 2 ya kila mwaka, asili yake ni Misri. Wamisri walikuwa wakiisherehekea
kwa heshima na kumtukuza Bikira Naith, na siku hiyohiyo Wakristo nao pia husherehekea.
Wakazi wa Babeli na Ashori, walikuwa wakimuabudu mwanamke bikira wakidai kuwa ni
mama wa mungu na wakamchora akiwa amemlea mwanaye kama ilivyo kwa Wakristo. Jina la
huyo mwanamke ni MILITA, na jina la mwanaye mwokozi ni TAMUZ ambaye pia huitwa kuwa
ni Mpatanishi na Mkombozi. Katika kisiwa cha Cyprus kulikuwa na hekalu lililojulikana kama
“HEKALU LA BIKIRA MILITA” ambalo ndilo lililokuwa hekalu kubwa katika enzi za utawala
wa Wayunan.
Wayahudi nao pia walitumbukia katika dimbwi la bahari ya upagani, wakafikia hatua ya
kuabudu jua, mwezi na nyota, na wakawatoa binaadamu kama sadaka ya miungu hao. Miongoni
mwa miungu waliowaabudu ni mwanamke bikira waliyemuita kuwa ni MALKIA WA
MBINGUNI kama ilivyoelezwa katika kitabu cha Yeremia sura ya 44 msitari wa 16 – 19.
Wayahudi walimwambia Yeremia: “neno lile ulilotuambia kwa jina la BWANA, sisi
hatutakusikiliza. Lakini bila shaka tutalitimiza kila neno lililotoka katika vinywa vyetu,
kumfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, kama
tulivyotenda sisi, na baba zetu, na wafalme wetu, na wakuu wetu, katika miji ya Yuda, na katika
njia kuu za Yerusalemu; maana wakati huo tulikuwa na chakula tele, na kufanikiwa, wala
hatukuona mabaya. Lakini tulipoacha kumfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia
sadaka za kinywaji, tumepungukiwa na na vitu vyote; na kuangamizwa kwa upanga, na kwa
njaa. Nasi tulipomfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, Je!
Tulimfanyizia mikate, ili kumwabudu, na kummiminia mamiminiko, waume zetu
wasipokuwapo?”
Na yale yaliyoelezwa na Warumi kuhusu MARHA mama wa mungu Bacchus yanafanana moja
kwa moja na yaliyoelezwa katika Injili ya Mathayo sura ya kwanza msitari wa 18 mpaka 24,85
ambapo mtakatifu Jerome ametafsiri jina la MARHA kwamba ni MARIAM. Na walikuwa
wakimuita kuwa ni MUNGU WA BAHARI, ambapo sasa wanamuita Mariam mama wa Yesu
kuwa ni NYOTA YA BAHARI.
85 Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla
hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye Yusufu, mumewe, kwa vile
alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri. Basi alivyokuwa akifikiri hayo,
tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua
Mariamu mkeo, maana mamba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao. Hayo yote yamekuwa, ili litimie neon
lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema, Tazama, bikira atachukua mimba, naye atazaa mwana; nao
watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu Pamoja nasi.
Naye Yusufu alipoamka katika usingizi, alifanya kama malaika wa Bwana alivyomwagiza; akamchukua mkewe;
asimjue kamwe hata alipomzaa mwanawe; akamwita jina lake YESU”
35
Wayunan walikuwa wakimuita mama mtakatifu wa mungu Juno kuwa ni MALKIA WA
MBINGUNI, na kumuabudu kwa imani kuwa ni mlinzi wa wanawake tangu kuzaliwa mpaka
kufa, kama ilivyo imani ya Wakristo wa leo kwa Bkira Mariam.
36
SURA YA TANO
NYOTA ZA MASHARIKI ZILIZOONEKANA KWA KUZALIWA MIUNGU
Na zikawaonyesha Majusi na Makuhani mahali walipozaliwa, na hatimaye wakaja kuwasujudia
miungu watu waliozaliwa na bikira aliyejaa neema
I – WAPAGANI:
Bwana Bunsen anasema: “imeelezwa katika vitabu vitakatifu vya kibudha kuwa mbingu zilitoa
bishara ya kuzaliwa Budha kutokana na nyota iliyoonekana upande wa mshariki ya anga. Katika
vitabu hivyo nyota hiyo imeitwa kuwa ni NYOTA YA MASIHI”86
Bwana Beal anasema: Amesema Fobinhang kuwa wakati alipojidhihirisha Budhitsu kituo cha
nyota ya Liwaa kilikuwa katika hali ya kukutana na jua, na katika vitabu vyao huwaita
wanafalsafa hao kuwa ni “Watakatifu wa Masihi”, nao ni wale waliotambua kuzaliwa kwa
Masihi Budha kupitia ishara za mbinguni. Na imeelezwa katika moja ya vitabu vyao vitakatifu
vya Wahidu kiitwacho RAMYANA kuwa Rama alizaliwa tarehe tisa ya mwezi wa Kitra katika
kipindi ambacho sayari ya Jupita ilikuwa katika nyota ya kaa (Rama ndiye Vishnu aliye katika
mwili)87
Alipozaliwa Krishna, nyota zilidhihiri mbinguni na Naridu mnajimu mkuu alizithibitisha.
Mazazi ya miungu wote waliojionyesha katika miili ya kibinaadamu yalijulishwa na nyota.
Anasema Thorten: “Wachina huamini kuwa wakati alipozaliwa YU, nyota ilidhiri kama ishara
ya tukio hilo. Na YU aliyetajwa ndiye aliyeasisi dola ya kwanza iliyotawala China. Pia
wanasema kuwa wakati wa kuzaliwa Mwanafalsafa LAO-TSEU ilionekana nyota kama ishara ya
kuzaliwa kwake”88
Warumi walikuwa wakiamini kuwa wakati wa kuzaliwa makaisari nyota hudhihiri – kama
wasemavyo Wayunani.Vilevile walikuwa wakisema kuwa wakati wa kifo cha mmoja wa
makaisari, nyota hupoteza nuru yake. Mwanahistoria wa Kirumi Tsitus anasema: “ ilidhihiri
nyota yenye mkia. Na hii inaelezea yale yasemwayo na watu juu ya kubadilika kwa watawala na
kuanguka kwa wafalme. Kudhiri kwa nyota iliyodhaniwa na watu kuwa ni sababu ya
kunganguka kwa utawala wa Niro ni jambo lisilokuwa na mjadala, kwani walianza kuulizana
kuhusu atakayeshika mahala pake”.
Anasema profesa Amberly: “ Katika zama za utawala wa Hadriyan alitokea mtu miaka mia moja
baada ya Masihi(a.s.) aliyedai kuwa ni mtoto wa Kristo na kuwavuta watu wengi wa jamii yake,
akayaongoza majeshi na kumpindua mfalme wa Rumi katika uasi huo, na akajiita kuwa ni
MTOTO WA NYOTA”89
Hakuna shaka kuwa ishara hii ya nyota vilevile ilienea mpaka Amerika, kwa sababu ilikuwa
ndiyo alama ya kuja mwokozi Quetzalcoatl aliyezaliwa na mwanamke bikira.
86 The Angel Messiah, ukurasa wa 22, 23 na 33 87 The History of Buddhism, ukurasa wa 23 na 33 88 The Chinese, juzuu ya 1, ukurasa 173 89 Analysis of religious belief, ukurasa 227
37
Kasisi Dr. Geiekic anasema: Imani ya kutokea matukio ya ajabu ilikuwa imeenea sana, hasa
wakati wa kuzaliwa au kufa kwa mmoja wa watu wakubwa kulikokuwa kukielezewa kwa
kudhihiri nyota (ya kawaida) au yenye mkia au baadhi ya sayari kuungana.90
Inaelezwa kuwa Zoroaster alisema kuwa nyakati za mwisho mwanamke bikira atachukua mimba
ya mtoto wa kiume.Wakati wa kumzaa itadhihiri nyota katika majira ya robo ya mchana
itakayoonekana sana kutokana na ukali wa nuru yake.
* * *
II- Wakristo:
NYOTA ILIYONEKANA UPANDE WA MASHARIKI WAKATI ALIPOZALIWA YESU
KRISTO.
Hapo awali tumeona kile wanachokiamini wapagani kuhusu kuchomoza nyota upande wa
mashariki , ambayo iliwaonyesha makuhani mahali walipokuwa wamezaliwa wana wa miungu
yao. Halikadhalika Majusi walionyeshwa mahali alipozaliwa Yesu Kristo kupitia nyota
wanayodai kuwa ilionekana wakati wa kuzaliwa kwake. Hata hivyo hatujui ikiwa hiyo nyota
ndiyo ileile iliyowaonyesha makuhani mahali walipozaliwa watoto wa miungu tuliowataja au ni
nyingine.Vilevile hatujui ikiwa hiyo nyota ni miongoni mwa jamii ya hizi zilizoenea angani
zikiwa mbali nasi kwa mamilioni ya maili, na ambazo ni kubwa mara kadha kuliko hii dunia, au
ni nyota tofauti iliyoumbwa kwa lengo hili la kuonyesha mahali walipozaliwa miungu. Ilikuwa
umbali gani kutoka ardhini? Na je, kwanini haikutokea mkanganyiko katika nguvu ya mvutano
kwa sababu ya kushuka nyota hii? Lile tunalolijua sisi ni kwamba, Wapagani walikuwa na uhuru
wa moja kwa moja katika kuunda madai na imani potofu zinazowapendeza.
Tunasoma katika Injili ya Mathayo, sura ya pili, msitari wa kwanza na wa pili kuwa: “Yesu
alipozaliwa katika Bethelehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa
mashariki walifika Yerusalemu, wakisema, yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi?
Kwa maana tuliona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia”.
90 Life of Christ, juzuu ya 1, ukurasa 144
38
SURA YA SITA
MAJESHI YA MBINGUNI YALIMTUKUZA MUNGU KWA KUZALIWA MIUNGU
I-Wapagani:
Katika kitabu cha Vishnu Purana kuna maelezo yafuatayo: Bikira Devaki alipochukua mimba ya
mwokozi wa ulimwengu, alitukuzwa na miungu. Alipomzaa, furaha ilienea, nuru ikaangaza
ulimwenguni kote na miungu wa mbinguni waikaimba na roho zikaghani. Alipozaliwa
MKOMBOZI WA WATU WOTE mawingu yalianza kuimba kwa sauti za vinanda na maua
yakadondoka”.
Maneno kama haya huyatoa kuhusu kuzaliwa kwa Budha, na kwamba wakazi wa ardhini
walisikia sauti na ghani za vinanda, mbingu ikanyesha maua na manukato, upepo mwanana
ukavuma na nuru ya ajabu ikaangaza.
Bwana Fonbihang anasema: Roho walimzunguka Bikira Maya na mwanaye mwokozi wakaanza
kumtukuza Mungu wa pekee na kuimba “utukuzwe ewe Malkia Maya, furahi na ushangilie,
kwani mwana uliyemzaa ni mtukufu”. Reshi na Devasi waishio duniani walinadi kwa furaha
kubwa wakisema “Leo amezaliwa Buddha ili kuwapa watu heri na kuondoa ujinga wao”.
Wafalme wa mbingu ya nne nao wakanadi: Sasa amezaliwa Budhistu atakayeupa ulimwengu
raha na furaha”. Kisha akasema: miungu wa mbinguni walikusanyika na kuimba: “Leo
amezaliwa Budhistu katika dunia ili awape watu furaha na amani, aangaze katika kiza na kumpa
kipofu macho”.
Anasema Sir Jones Francis Davis: Wachina husema kuwa, kabla ya kuzaliwa Konfocius,
mwanafalsafa mashuri wa kichina, alama kadhaa zilionekana kutoka mbinguni. Katika jioni ya
kuzaliwa kwake sauti ya vinanda kutoka mbinguni ilisikika masikioni mwa mama yake, na
alipozaliwa, maandishi yafuatayo yalionekana kifuani mwake: MTUNGAJI WA SHERIA
ZITAKAZOIREKEBISHA DUNIA
Naye Prichard anasema: alipozaliwa Osiris mkombozi, sauti ilisikika ikinadi “AMEZALIWA
MTAWALA WA DUNIA 91
Bwana Bonwick naye pia anasema: Wamisri wa zamani wanasema kuwa, pindi Osiris
alipozaliwa, ilisikika sauti ikinadi kuwa AMEZALIWA MUNGU WETU AITWAYE OSIRIS”92
Wengine husema kuwa, mwanamke mmoja alipokuwa akienda kuchukua maji kwa ajili ya
hekalu la Ammon lililopo katika mji wa Tipis, alisikia sauti hii ikimuamuru kunadi kwa sauti ya
juu maneno yafuatayo: “ATAZALIWA MUNGU OSIRIS”.
Alipozaliwa Apolonius mwana wa Mungu, furaha ilienea. Flafius Filostratus, mwandishi wa
maisha ya mtu huyu wa ajabu, anasema kuwa kundi la bata-mzinga walimzunguka mama yake
na kuanza kuimba kwa pamoja kwa sauti tamu na upepo mwanana ukavuma”.
Alipozaliwa Apollo kwa Bikira Latona katika visiwa vya Dilus, miungu wa Olimpos walifurahi
sana, ardhi ikatabasamu na mbingu ikacheka. Na alipozaliwa Heraclus mtoto wa mkombozi,
91 Analysis of the Historical Records of Ancient Egypt, ukurasa wa 56 92 Egyptian Belief, ukurasa wa 325
39
baba yake, Mungu Mkuu Zius alinadi kutoka mbinguni na kusema, LEO ATAZALIWA MWANA
KUTOKA KATIKA UKOO WA PRISIUS NA ATAKUWA NA NGUVU KULIKO WATU WOTE”.
Na Iskolapius alipokuwa mtoto na wakataka kmuua, walisikia sauti ya Mungu Apollo ikisema:
Msimuuwe mtoto pamoja na mama yake kwani ni mtoto atakayefanya mambo makuu, bali
mpelekeni kwa mtakatifu Santor Shrun na mwambieni amfundishe katika hekima, na ushujaa
wake ili watu wapate kunitukuza katika vizazi vijavyo”.
II-Wakristo:
MAJESHI YALIYOONEKANA MBINGUNI WAKATI WA KUZALIWA YESU KRISTO
Tumeona yaliyosemwa na Wapagani wa zamani kuhusu kudhihiri kwa majeshi ya mbinguni
wakati wa kuzaliwa kwa mmoja wa watoto wa miungu wao.
Wakristo nao walisema hayohayo kuhusu kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Isipokuwa, sisi hatuelewi
ikiwa hayo majeshi ya mbinguni yalikuwa na idadi kubwa wakati walipozaliwa watoto wa
miungu wa kipagani au yalikuwa mengi pindi alipozaliwa mungu wa Wakristo au yalikuwa na
idadi sawa katika nyakati zote? Kwa sababu wanadai kuwa watoto wote wa miungu waliozaliwa
walikuja kuwakomboa kwa damu zao, na tunavyojua ni kwamba hakuna aliyepinga madai hayo.
Huwenda hapo baadaye hali hii ikaongezeka. Sasa soma yafuatayo katika agano jipya.
Injili ya Luka msitari wa pili, kifungu cha 13 na 14: “Mara walikuwapo pamoja na huyo
malaika,w ingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu mungu na kusema, Atukuzwe Mungu juu
mbinguni na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia”.
SURA YA SABA
KUONYESHWA MTOTO WA MUNGU NA KUMKIRIMU KWA ZAWADI
I-Wapagani:
Katika simulizi zinazomhusu Krishna, ni kuwa mtoto wa Mungu aliwekwa kwenye kitanda cha
watoto akiwa baina ya wachunga kondoo ambao ndio waliokuwa wa kwanza kuutambua utukufu
wake mkuu unaoonyesha kuwa ni Mungu, na wakatambua kuwa ndiye mkombozi aliyeahidiwa.
Wa kwanza kumtambua miongoni mwao ni Nanda mchunga –kondoo kisha wenzake na wote
wakammsudia. Nabii wa Kihindu – Naredu – alisikia habari zake, akaenda kuwaona wazazi wa
mtoto huyo katika mji wa Cokol. Baada ya kufanya utafiti wa Kimungu. Wachunga kondoo
alimpa Krishna zawadi.
Pia wanasema kuhusu mtoto Budha mwenye asili ya Kimungu kuwa alipozaliwa alitelewa na
Makuhani ambaowalina ishara Uunguwake na kumwita kuwa ni Mungu Mkuu, na kwamba
alikuja pamoja nao Mtakatifu aitwaye Asiufa aliyekuwa na mvi nyingi ili apate kumuona, mzee
huyo alikuwa hasikii mambo ya dunia bali alikuwa akisikia sauti kutoka mbinguni, ndipo
alipokuwa akisali chini ya mti akasikia wimbo wa Rivas juu ya kuzaliwa Budha.
40
Bwana Amberly anasema: wanasema kuwa Asita ambayea ni mmoja waa wachamungu
wakubwa, alimtembelea Budha na kutoa Biashara kuhusu utkufu wake wa baadaye, na akalia
kwa sababu ya kuwa ni mzee asiyeweza kuishi sana ilia apate kuishuhudia siku atakayojifunza “
sheria ya wokovu”kutoka kwa huyo mtoto aliyekuja kushuhuidia utukufuna ukuu wake. Alilia
kwa sababu ya uzee ambao ulimfanya asiweze kuona yale yatayotokea, na kwamba “Baha
Kamen (yaani Mungu muweza) ambaye ni Budha alikuja Duniani ili kuikomboa na awafundishe
sheria,” aponye vikongwe, wagojwa, na wenye ulemavu na wafu, na awaokoewale
waliotumbukia katika mtego wa ufisadi wa kimaadili, na awafumbue macho ya kiroho
yaliyopofuka kwa giza la ujinga, na awabebe mamilioni ya watu kwenda ng‟ambo ya bahari, na
aweze kuwapa manufaa ya maisha ya milele. Huyo Mchamungu alilia Na kuhuzunika Sana Kwa
kudhani kuwa asingemuona Budha mwenye ukamilifu, lakini sasa alirejea nyumbani kutoka
mlimani akiwa ni mwenye furaha kwa sababu aliweza kumuona “Mwokozi aliyezaliwa” akiwa
katika hali ya uchanga.
Picha zilipo katika pango la Ajiwanta zinamuonyesha Asita akiwa amemlea Budha, na
kwamba huyu Mchamungu aliutambua uungu wa Budha kupitia ishara zisizokuwa za kawaida.
Na Watakatifu wazamani walimfahamu na kumtukuza, na walipo kufa walikwenda kwa amani
kwa kuwa wamekwisha kumuona. Pia wanasema kuhusu mama wa huyo Mungu kuwa alimzaa
mtoto wake wa pekee bila kupata machungu wala tabu na hayo yanaonyesha kuwa mtoto
aliyezaliwa alikuwa na miujiza.
Mithra, mkombozi wa Waajemi na mpatanishi baina ya Mungu na watu, alipozaliwa
alitemelewa na majusi wakampa zawadi za dhahabu na manukato.
Kwamujibu wa simulizi ya Plato : alipozaliwa Socrates 94
(miaka 469 kabla ya Kristo)
walikuja majusi kutoka mashariki wakampa zawadi za dhahabu na manemane.
Na mkombozi (iskolapius) aliyezaliwa na mwanamke bikira, alilindwa na kondoo dhidi ya
jambo lolote baya, kwani walipomuona walitambua kuwa ni “Mungu”. Habari za mazazi yake ya
maajabu zilienea, watu kutoka kila sehemu walifika ili kumshuhudia na kumsujudia. Na wengi
katika wale waliopewa nusu ya Uungu, kwa Warumi na Wayunami, walilelewa na wachunga
kondoo ambao waliwasujudia.
Miongoni mwao ni Wardmulos aliyekutwa na wachunga – kondoo katika ukingo wa Tiber 95
,
na Parmi motto wa Paryan alilelewa na wachunga kondoo. Ojisos, alitupwa na mama yake,
akaokotwa na wachunga – kondoo wakamlea.
Halikadhalika Iskolapius na wengineo ambao historia imetuhifadhia majina yao.
* * *
II- WAKRISTO:
Hali iliyotokea katika kuwatambua watoto wa Mungu Kama vile Budha, Krishna Na
wengineo, Na zawadi za thamani zilizotolewa Na wachunga kondoo, majisu au wanajimua,
ndinyo ilinyokuwa kwa Yesu Kristo. Katika Injili ya Mathayo sura ya pili msitari wa 1- 11 kuna
maelezo yafuatayo: Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu zamani za Mfalme Herode, tazama,
mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakasema, yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme
wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia…
wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka
41
wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba
na manemane”.
Maelezo Kama hayo pia yanapatikana katika Injili ya Luka, sura ya pili 96
, isipokuwa yeye
anaeleza kuwa waliyoiona nyota yake ni wachunga-kondoo na sio majusi. Vilevile Injili iitwayo
“ Injili ya Wamisri” inasema kuwa: “waliokuja kumuona na kumpa zawadi ni wachunga-kondoo
na sio majusi.
SURA YA NANE
MAHALI WALIPOZALIWA BAADHI YA MIUNGU WALIOJIDHIHIRISHA KATIKA
MIILI YA KIBINADAMU
I- WAPAGANI:
Krishna alizaliwa Pangoni, na baada ya kuzaliwa aliwekwa katika zizi la kondoo, na
alilelewa na mmoja wa wachunga-kondoo waaminifu.
Hotse mtoto wa Mungu kwa imani ya Wachina, aliachwa namama yake akiwa kichanga,
akazungukwa na ng‟ombe na kondoo wakimlinda sana dhidi ya kila jambo baya. Na Bacchus
mtoto wa Mungu alizaliwa na bikira Semele alizaliwa Pangoni. Inasemekana Kama pia kuwa
alizaliwa sehemu nyingine, Na baada ya kuzaliwa, mama yake alimleta Pangoni.
Phelostratus, mhutubu wa Kiyunani anasema “wakazi wa India wanasema kuwa Bacchus
alizaliwa Nisan a kulelewa katika Pango la mlima Maros.”
Na Iskolapius matoto wa Mungu aliyezaliwa na bikira Kordanis, alipozaliwa aliachwa
amlimani akaokotwa na mchunga - kondoo aliyemlia na kumtunza.
Ropolus mwana wa Mungu aliyezaliwa na bikira Kordanis, alipozaliwa aliachwa mlimani
akaokotwa na mchunga – kondoo aliyemlea na kumtunza .
Romulus mwana wa Mungu alizaliwa na Riyasilvia, aliachwa na mama yake akiwa bado
kichanga katika ukingo wa mto Tibaar, akaokotwa na wachunga – kondoo wakamlia na
kumtunza.
Bwana mwokozi Adoni mara baada ya kuzaliwa aliwekwa katika Pango. Naye Apollo
mwana wa Zeus, mungu mwenye uweza , alizaliwa Pangoni nyakati za asubuhi.
Mithra,mkombozi wa Waajemi,naye alizaliwa pangoni nyakati za asubuhi.Kadhalika Herus
mwana wa Mungu, aliyezaliwa na Bikira Maya,alizaliwa pangoni kwenye mlima wa keliman
wakati wa asubuhi.
Naye Attis,vilevile alizaliwa katika pango.
42
Wahindu wanasema kuwa Krishna alipozaliwa, umbile la mama yake lilibadilika na kuwa na
uzuri na mvuto usiokuwa na mfano. Nuru kutoka mbinguni ikadhihiri na kuangaza ndani ya
pango, na mashavu ya wazazi wake yakatoa mwangaza wenye nuru.
Vilevile wanasema kuwa alipozaliwa Budha, mkombozi wa ulimwengu, mwili wake
ulizungukwa na nuru kutoka mbinguni ambayo ilikuwa makhsusi kwa ajili yake tu,na hivyo
ndivyo alivyokuja duniani na nuru isiyokuwa na mfano.
Na alipozaliwa Bacchus, nuru yenye kung‟aa ilimzunguka na kuangaaza pangoni.
Naye Apollo alipozaliwa, kitanda chake kilizungukwa na nuru, na majeshi kutoka mbinguni
yakamuosha kwa maji safi na kumtakasa kwa dhahabu.
Mkombozi Iskolapius alipozaliwa, shavu lake liltoa mwanga Kama jua na kuzungukwa na
miale ya moto. Vilevile wanasema kuhusu Zoroaster kuwa alizaliwa pasina uchafu (yaani
mama yake hakulala na mwanaume) bali alichukua mimba kutokana na miale ya nuru ya
Mungu, na alipozaliwa ilidhihiri mwilini mwake nuru iliyoangaza chumba chote na kwamba
alimchekea mama yake.
Wahindu wanasema pia kuwa ulipokaribia muda wa kuzaliwa Krishna, Nanda alikwenda
kwa Mfalme ili kumtoa mali (kodi) akisuhubiana na mama wa Krishna aliyekuwa na mimba,
ndipo machungua yalipo mjia akiwa njiani, akamzalia chini ya mti. Na katika simulizi
nyingine inasemakana kuwa alimzaa akiwa katika nyumba ya kulala wageni.
Naye Laotseu, Mwanafalsafa wa Kichina mama yake akiwa safarini alimzaa chini ya mti.
Na Phethaghorus ambaye alikuwepo miaka 570 kabla ya Roho Mtaktifu, na akamzaa akiwa
safarini pamoja na Baba yake kuelekea Seda kwa ajili ya biashara.
Naye Aapolo, alizaliwa wakati mama yake alipokuwa sfarini. Simulizi za kuzaliwa kwake
zinasema kuwa ulipokaribia muda wa kuzaliwa na mama yake akawa hakupata mahala pa
kujifungulia alimzaa chini ya mti, akajua kuwa mtoto huyo atakuwa mkuu atakayeiongoza
Miungu ya watu. Na Ikolapius Mwana wa Mungu aliyezaliwa na Bikira Koronis, mamayake
alimucha juu yam lima baada ya kumzaa akaokotwa na mchunga – kondoo ambaye alimlea
na kumtunza. Naye Rumulus mama yake alimuacha ukingoni mwa mto Tabar akiwa bado
mchanga akaokotwana wachunga – kondoo wakamlea na kumtunza. Vilevile Bwana Adoni
Mkombozi alizaliwa pangoni.
Apolo Mwana wa Mungu Dhus alizaliwa pangoni nyakati za asubuhi.
Na Mithra, mkombozi wa Waajemi, alizaliwa pangoni nyakati za asubuhi. Pia Hermus
Mwana wa Mungu alizaliwa na Bikira Maya, alizaliwa wakati wa asubuhi katika pango la
mlima Keliman.
Attis naye pia alizaliwa pangoni. Na wengine wengi walizaliwa katika maeneo
mbalimbali, tunatosheka na hao tuliowataja.
* * *
II- MAHALI ALIPOZALIWA YESU KRISTO:
Tumetaja yale yanayozungumzwa na Wapagani kuhusu mahala ilipozaliwa Miungu yao,
kama vile Krishna, Budha na wengineo, na sasa tunataja yale yalioelezwa kuhusu mahala
alipozaliwa Yesu Kristo, Mungu wa Wamishionari, ambao huenda wakakoma kuzuia kuenea
kwa dini ya Kiislam, wakawa wavumilivu katika kuzichunguza imni zao, wakakubali kufuata
yale yaliokuwa bora kwao ili mwisho wao uwe mwema, hata kama waliokuwa kabla yao
wameyafanya.
43
Katika Injili ya Luka mstari wa pili, kifungu cha 15,16 na 17 kuna maelezo yafuatayo;
Ikawa, malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana,
Haya, na twendeni mapaka Bethlehem, tukalione hilo lililofanyika, alilotujulisha bwana.
Wakaenda Kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala
horini. Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.
Vifungu tulivyo vitaja vinatosha katika kueleza kadhia hii ya kuzaliwa kwa Masihi katika
silsila ya wafalme. Kama ilivyozaliwa Miungu ya Warumi na Wayunami ambao Injili nyingi
zimetoka kwao, na kama ilivyozaliwa miungu ya Mabudha na Wabrahma na wengineo,
ndivyo alivozaliwa Mungu wa Wamishionari, yaani Yesu, madai na ulinganisho ulioje!
Amesma kweli Allah Mtukufu: “Hayapofuki macho bali hupofuka nyoyo zilizopo vifuani”.
SURA YA TISA
MIUNGU ILIYODHIHIRI KATIKA MWILI INATOKANA NA KIZAZI CHA KIFALME.
Wahindu wanaaminimkuwa mkombozi wao Krishna anatokana Na kizazi cha kifalme, na
kwamba alizaliwa katika hali ya unyenyekevu, Na wanahesabu mababu Kwa upande wa
mama yake, ama Kwa upande wa baba yake, alikuwa ni mwana wa Mungu kwa mda wa
vizazi vingi.
Wanasema kuwa Budha anatokana na kizazi cha kifalme katika nyumba ya Soqya,
ambayo ndiyo kizazi mashuhuri sana cha Wabrahma ambao walikuwa ndio watu wale wa
India. Na wanasema kwamba babu yake wa kwanza, ambaye ni Samatha ndie wa kwanza
kuitawala India na Dunia, na Rama ambayendiye Vishnu katika mwili, alikuwa katika kizazi
cha kifalme.
Na Foni mwana wa Mungu aliyezaliwa na Bikira anatokana na familia ya Kifalme
iliyotawala China katika karne nyingi ziizota.
Wachina wanasema kuwa Confocius anatokana na familia ya kifalme. Na wanawahesabu
babu zake Kama wanavyowahesabu mababu wa wafalme Hwatsaki, ambaye alikuwa mfalme
wa China tangu miaka elfu moja.
Naye Horus mkombozi wa Wamisri aliyezaliwa na mwanamwali, alitokana na kizazi cha
kifalme, na vilevile wanamwita kuwa ni “mchungaji mwema”.
Heraclus Mwana wa Mungu alitoka katika ka familia ya kifalme.
Naye Yosius mwana wa Bikira Danya aliyetoka katika familia ya kifalme.
Na Iskolapius mwana wa Mungu mwenye ishara miujiza alitokana na kizazicha kifalme.
Na kuna wengine wengi katika wale wanaodaiwa na Wapagani kuwa ni watoto wa Miungu
yao, na wote wanatokana na kizazi cha kifalme, na mifano tuliyoitoa inatosha.
* * *
IMANI YA WAKRISTO KWAMBA MUNGU KRISTO ANATOKA KATIKA KIZAZI
CHA KIFALME.
Nyumati za kipagani zilizotangulia zilidai kuwa watoto wa Miungu yao inatokana na kizazi
cha kiflme kama tulivyokwishaeleza. Vivyo hivyo Wakristo nao walisema kuwa Yesu kristo
anatokana na kizazi cha kifalme, na wanaipeleka nasaba yake mpaka kwa Mfalme Daud,
kama ilivyoeleza katika Injili ya Mathayo mstari wa kwanza 97
, na Injili ya Luka sura ya
44
kwanza 98
. Na hivi vifungu vingi vilivyomo ndani ya Injili ambavyo humo ameitwa kuwa ni
“Mwana wa Daudi” hata mashetani walikuwa wakimwita “Mwana wa Daudi”, mojawapo ya
vifungu hivyo ni kutoka katika Injili ya Mathayo mstari wa 22 kifungu cha 41 na 42
kinasema: Na Mafalisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akasema, mwaonaje katika
habari za Kristo? Ni mwana wa nani? Wakaamwambia, ni mwana wa Daudi.
SURA YA KUMI
IMANI YA WAPAGANI, KUHUSU WAFALME WALIOTAKA KUIANGAMIZA
MIUNGU NA JINSI ILIVYOOKOKA DHIDI YA MIKONO YA WAUAJI.
I.WAPAGANI:
Bwana Jocott gangooly ambaye ni mpagani aliyeingia katika Ukristo huko India anasema:
“wapagani wa Kihindu wanaamini kuwa Krishna alipozaliwa walisikia sauti ikinadi kutoka
mbinguni na kumwambia mlezi wake, simama, mchukue mtoto ukimbie naye na uvuke mto
Jomata. Akafanya Kama alivyoamriwa, Kwa sababu Mfalme Qanis alikuwa amekusudia
kumuua mtoto huyo mkombozi wa ulimwengu. Ambapo mfalme huyo alituma ujumbe
kutoka katika utawala wake ili kumuangamiza mtoto huyo 99
”.
Akasema bwana Higgins : Wapagani wa Kihindu huamini kuwa alipozaliwa Krishna
walimchukua usiku na kukimbia naye katika nchi ya mbali kwa kumhufia Mfalme Dhalimu,
ambaye ilisemakana kuwa Krishna angekuwa chanzo cha kuanguka kwake pindi atakapo
kuwa kijana, hivyo Mfalme aliamuru kuuawa watoto wote wa kiume waliozaliwa katika nchi
yake.
Maelezo kama hayo pia yalitolewa na Sir William au Jones na wengineo, ambapo katika
utenzi wa ushairi uliotungwa tangu miaka elfu mbili, kuna simuluzi juu ya kudhihiri kwa
Krishna katika mwili kwa kuzaliwa na Mwanamke Bikira, pamoja na kisa cha mlezi wake
kumkimbia Mfalme aliyeamuru kuuwa kwa watoto wa kiume. Na katika Pango lililopo
Vanta kuna picha za watoto aliowachinja, ambazo ni za zamani sana. Vilevile katika hilo
pango kuna picha zilizochora zikimuonyesha mtu aliyeshikilia upanga mkali na kuanza
kuwaua hao watotowa kiume, na huku kukiwa na picha za wanaume na wanwake wakimsihi
asiwauwe watoto wao.
Na wanasema kuhusu silvahana Mwokozi mtoto wa mwanamke bikira (aliyekuwa
akiabudiwa pia na wakazi wa kamorin india).
kama wasemavyo juu krishna na kukimba kwake, na kwamba alipokuwamkubwa alimuua
mfalme aliyetaka kumuua enzi za utotoni mwake.
45
Wahindu wanasema kuwa maisha ya Budha ya utoto yalikuwa yamezungukwa na hatari, katika
upande wa kusini mwa eneo la Mofadad kulikuwapo na mfalme dhalimu aliyeitwa Bimbasara
ambaye, kwa sababu ya hofu kuwa angetokea mtu atakayemnyang‟anya ufalme, alitaka ushauri
wa wasaidizi wake juu ya kinachotakiwa kufanyika ili kuzuia kile anachokihufia.
Wakamwambia kuwa katika upande wa kaskazini kuna familia kubwa inayoheshimika iitwayo
Saqya, amezaliwa Kwa mtoto mume, ambaye Ni wa pekee aitwayeBudha, ambaye anaweza
kukuletea matatizo makubwa. Wakamshauri kuandaa jeshi na kulituma huko kwa ajili ya
kumuangamiza huyo mtoto. Na Mabudha wa Mogoli wana kisa kama hiki, na Wachina
wanasema kuhusu shujaa wa Kichina Haoki kama wasemavyo Wahindu kuhusu Budha.
Wamisri wanasema kuhusu Horus kuwa alizaliwa kipindi cha kiangazi na kulelewa kwa
siri katika kisiwa cha Bota kwa kumhufia Tifon ambaye alitaka kumuua akiwa bado mtoto.
Na kisa cha Tiros mfalme wa Uajemi (miaka 600 kabla ya Kristo) kinafanana visa tulivyu
kwisha vitaja. Vilevile wanasema kuwa Baba yake aliota ndoto ambayo aliwaeleza Majusi ili
kutaka kujua maana yake, wakamwambia: Binti yako Findau atazaa motto mume ambaye
atakuwa ndiyo chanzo cha kuondoka kwa ufalme wako. Pindi alipozaliwa alimkabidhi
mikononi mwa Hevbagos ili amuuwe naye vilevile akamkabidhi mokononi mwa mchunga
kondoo ili amuuwe. Naye mchunga kondoo akamchukua mtoto nakudai kuwa ni mwanaye
na kuanza kumlea. Mtoto huyo alipo kuwa kijana alipambana na Istiyacis na kuchukua
ufalme kama walivyotabiri Majusi. Na Herdotus mwana historia wa Kiyunan amekielezea
kisa hiki na ndoto waliyoifasiri Majusi.
Na kuhusu Zoroaster mwanzilishi wa dini ya Majusi, wanasema kuwa maisha ya utotoni
mwake yalikuwa yameandamwa na hali ya hatari, kwa hiyo Mama yake akakimbia naye
katika nchi ya Uajem,i ambapo aliona roho usingizini akimwambia : usihofu chochote, kwani
Mungu atamlinda huyu mtoto kwa sababu ni mtume anayengojewa na ulimwengu.
Na maisha ya Prisius Mwana wa Bikira Danya yalikuwa yamezingirwa na hatari tangu
utotoni mwake kwa kuwa Crasius alimweleza Mfalme wa Argos kuwa binti yake atazaa
mwana ambaye atakapo kuwa mkubwa atamuua (yaani atamuua babu yake), akamfungia
binti yake mnarani ili asiweze kufikiwa na mwanamme yeyote kwa lengo la kuyalinda
maisha yake dhidi ya yaliyotabiriwa na Majusi. Siku moja (binti huyo) alitembelewa na
Mungu Jupita na hapo akachukua mimba na kumzaa mtoto wa kiume akamwita Prisius. Baba
yake aliposikia habari ya kuzaliwa kwa mtoto wa kiume, aliamuru kumweka binti yake
pamoja na mwanaye katika sanduku na watupwe baharini, ikafanyika kama ilivyoamriwa,
wakaokotwa na mtu mmoja jina lake Dectis na kuwaokoa kutoka baharini.
Lao-tseu
46
Zama Iskolapius alipoikuwa mtoto, aliwekwa juu ya mlima Alas ili apate kufa, akaokotwa
na wachunga kondoo wakamlea. Na Hevqus mzawa wa Bikira Lito aliwekwa jagwani Ili afe,
akaokotwa na binti mmoja akamlea na kumtunza.
Naye Odbos alitupwa na Mamayake juu yam lima Ksiron, akaokotwa na wachunga
kondoo wakamchukua na kumlea. Na Tifos, Trajan, Yamus, Apollo na wengine miongoni
mwa watoto wa Miungu au wenye sehemu ya Uungu, walitaka kuuliwa na wafalme wa zama
zao kwa hofu ya wafalme hao dhidi yao, lakini kwa amri ya Mungu waliokoka kutoka
mikononi mwa watesaji wao, nasi tukapendea kufanya muhtasi tu bila ya kuwataja wote.
* * *
II- IMANI YA WAKRISTO KWAMBA HERODE ALITAKA KUMUUA KRISTO NA
JINSI ALIVYOOKOKA.
Tumeiyona imani ya nyumati zilizotangulia kuhusu Wafalme kutaka kuwaua na
kuwaangamiza watoto wa Muingu waliozaliwa na wanawake Bikira, na tumeona
yaliyosemwa na Wakristo kuwa yanafanana na yaliyosemwa na Wapagani.
Injiliya Mathayo mstari wa 2 namba 13: na hao walipokwisha kwenda zao, tazama,
malaika wa bwana alimtokea Yusufu katika, ndoto, akasema, ondoka umchukue mtoto na
mama yake, ukimbie Misri, ukae huko hata nikuambie kwa maana Herode anataka kumtafuta
mtoto amwangamize. Akaondoka akamchuka mtoto na mama yake usiku, akaenda zake
Misri.
SURA YA KUMI NA MOJA
MAJARIBU YA SHETANI KWA WATOTO WA MUINGU NA FUNGA YAO YA SIKU
40.
* * *
I- WA PAGANI:
Katika kitabu kiitwacho (Buddha Fasting Life) kilichotungwa na Moncyor Conwe wa
China ukurasa wa 44,172 na 173 kuna maelezo yafuatayo: na Mungu Mkuu Budha aliiweka
nafsi yake katika uchamungu kwa kiasi cha kuacha kula (yaani kufunga ) na hata kupumua
pia- - - Alitokewa na Maraa (yaani kiongozi wa mashetani) ambapo alikusudia kumtia
Buddha majaribuni mara kwa mara akijifanya kumwonea huruma,akamwambia Buddha:
“zinduka ewe kiumbe mkuu, kwani hali yako inamhuzunishakila anayekutazama, kwani
umekonda kwa kiwango kisichoelezeka - - - na hakika unafanya udhalili na kukaabiliana nao
kwa njia batili, nami nadhani huwezi kuendelea kuishi hapa sana”. Ewe bwana umevumilia
sana mateso makali, usiishi maisha ya udhalili bali rejea kwenye ufalme wako na kwa muda
wa siku saba utaweza kutawala mabara manne.
Mungu mkuu Budha akamjibu: “angalia ewe Mara (yaani kiongozi wa mashtani) mimi
najua vyema kuwa kwa muda wa siku sabanaweza kutawala ulimwengu wote, lakini mimi
sipendi ufalme kama huu, kwa sababu kushikamana na dini ni bora kuliko ufalme wa dunia.
Unaikiria kwa tama mbaya, unafaka kunilazimisha niwaache watu bila ya kingozi ili
47
wasiweze kuwa salama dhidi ya mabalaa yako niondokee. Bwana akapaa na kuondoka akiwa
ameshikilia azima yake ileile, na mbingu zikanyesha maua, na anga ikanukia manukato
yenye harufu nzuri sana.
Shetani alimjaribu Zoroaster (mwanzilishi wa dini ya Majusi), na kumpa ahadi nyingi
iwapo angemtii na kumtegemea.Lakini majaribu yake yalikwenda kombo.Vilevile wana
hekaya na visa vingi visivyokuwa na msingi wowote zaidi ya kuelezea juu ya majaribu ya
shetani kwa Zoroaster.
Shetani,pia,alimjaribu Quetzalcoatl, mkombozi wa Wabrazili aliyezaliwa na mwanamke
bikira, na alifunga siku arobaini.
Wayunan walipokuwa wakitaka kujua mambo ya siri zilizofichika, walikuwa wakijizuia kula
vizuri na wakilala juu ya matandiko magumu yenye kuumiza,na hata baada ya siku tatu au
nne hula chakula kitakatifu (yaani kilichobarikiwa na wakuu wao).
Bwana Agosta na wengineo,wanasema: Wakuu wa kidini wa Mexico na Peru walikuwa
wakifunga funga ya mauaji kwani walikuwa wakijizuia kula na kunywa kwa muda wa siku
tano au kumi mfululizo, na usiku hupata kulala kidogo, wakaziweka nafsi zao katika hatari
kwa ajili ya shetani na ili wapate umaarufu wa kwamba wanafunga na kutubu sana.Vilevile
wanasema kuhusu mkombozi wao Quetzalcoatl kuwa alifunga siku arobaini pindi
alipojaribiwa na shetani.
II-MAJARIBU YA SHETANI KWA YESU KRISTO:
Tumeeleza yale yaliyosemwa na wapagani kuwa shetani aliwajaribu watoto wa miungu
yao.Sasa tunatoa yale yaliyoelezwa katika Injili kuhusu majaribu ya shetani kwa Yesu Kristo.
Mathayo sura ya 4 msitari wa 1:KishaYesu alipandishwa na Roho nyikani ili ajaribiwe na
Ibilisi.Akafunga siku arobaini mchana na usiku,mwisho akaona njaa.Mjaribu akamjia
akamwambia,Ukiwa ndiwe mwana wa Mungu,amuru kwamba mawe haya yawe mikate.
Naye akajibu akasema,Imeandikwa,mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila kwa kila neon
litokalo katika kinywa cha Mungu.Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu,akamweka
juu ya kinara cha hekalu,akamwambia,Ukiwa ndiwe mwana wa Mungu jitupe chini;kwa
maana imeandikwa,Atakuagizia malaika zake na mikononi mwao watakuchukua,usije
ukajikwaa mguu wako katika jiwe.Yesu akamwambia,Tena imeandikwa,usimjaribu Bwana
Mungu wako.Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote
za ulimwengu na fahari, kamwambia, Haya yote nitakupa,ukianguka kunisujudia.Ndipo Yesu
akamwambia,Nenda zako,Shetani.Kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu
wako,umwabudu yeye peke yake. Kisha Ibilisi akamwacha;na tazama,wakaja malaika
wakamtumikia.
SURA YA KUMI NA MBILI
KWENDA KUZIMU KWAWATOTO WA MIUNGU ILI KUWAKOMBOA WAFU
48
I- WAPAGANI:
II-
Wapagani wanaamini kuwa miungu yao ilijidhihirisha katika miili, iliteremka kuzimu
baada ya kuawa au kusubiwa, ili kuwakumboa wafu.
Krishna mkombozi wa wahindu, kabla ya kuekea mbinguni aliteremka kuzimu ili
kuwaokoa wafu.
Zoroaster aliteremka kuzimu kuwaokoa wafu.
Adonis mkombozi aliyezaliwa na mwanamke Bikira, aliteremka kuzimu ili kuwakomboa
wafu.
Mercury Neno, aliteremka kuzimu kuwakomboa wafu.
Palador mungu wa Wascandinavia, baada ya kuuawa,alikwenda kuzimu kuwakomboa
wafu.
Na kwa mfano na utaratibu huu huelezewa miungu yote ya Kipagani iliyojionyesha katika
mwili na ikafa ima kwa kusulubiwa au kuuawa kwa ajili ya utakaso wa dhambi.
* * *
KUTEREMKA KWA YESU KRISTO KUZIMU ILI KUWAKOMBOA WANAOTESEKA
HUMO.
Walivyosema Wapagani juuya kuteremka watoto wa miungu yao kwenda kuzimu ili
kuwaokoa wanaoteseka huko, ndivyo walivyosema pia Wakristo kwamba Yesu aliteremka
kuzimu ili kuwakomboa wale waliopata mateso huko.
Katika mafundisho ya Kikristo imeelezwa kuwa Yesu alitermka kuzimu, na kwamba siku ya
pili alifufuka katika wafu.
Mwaka 347 baada ya Kristo, Mtakatifu Cristom alisema: “hakuna akanaye habari ya Yesu
kuteremka kuzimu ili atakuwa kafiri (isipokuwa kafiri).
Mwanzoni mwa kizazi cha tatu baada ya Kristo, Mtakatifu Clemandus wa Alexandria alisema
yafuatayo: Yesu alihubiri juu ya watu wa kuzimu katika Injili, Kama alivyohubiri na kufundisha
Kwa watu wa duniani, ili wapate kumuamini na kukombolewa popote watakapokuwa.
Atakapoteremka bwana kwenda kuzimu, Kama ilivyoelezwa na mafundisho ya Injili, je
atateremka kwa ajili ya watu wote au kwa ajili ya Mayahudi tu? Kama ilitakuwa kwa ajili ya
wote, basi atakayeamuamini ataokolewa, itakuwa ni kwa ajili ya Mataifa ambayo wakati wote
yalimkubali, patakuwapo na msiba mkubwa kwa wengine”. Mtakatifu Origgin amekubaliana na
maneno haya, ambapo anaamini kuteremka kwa Yesu kuzimu.
Vilevile Mtakatifu Nicodemuskatika Injili yake ameelezea kuteremka kwa Masihi kwenda
Jahannamu akatoa maelezo ya mazungumzo baina yake na kiongozi wa mashetani
yanayopatikana katika sura ya kumi na tano na kumina saba, juu ya kuwakomboa watu wa
kuzimu, wanawakea, wanaume na watoto.
Katika kitabu cha matendo ya mitume, sura ya pili mstari wa 31 kuna maelezo yafuatayo:
yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, aliyaja habari ya kufufuka kwake Kristo, ya kwamba
roho yake haikuachwa kuzimu wala mwili wake haokuona uharibifu.
Na katika wakala wa Petro, sura ya tatu, mstari wa 17 – 19 imeelezwa kama ifuatayo: “maana
ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikiwa ndiyo mapenzi ya mungu, kuliko kwa kutenda
mabaya. Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa aijili ya dhambi, mwenye haki kwa
ajili yao wasio na haki, ili atulete kwa Mungu, mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa
ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri”.
49
SURA YA KUMI NA TATU
KUFUFUKA KWA HIYO MIUNGU KATI YA WAFU.
I- WAPAGANI:
Wapagani wa Kihindu huaminimkuwa Krishna alifufuka katika wafu, na kupaa mbinguni
kwa mwili wake. Na kwamba alipokuwa akipaa ilidhihiri nuru iliyoangaza duniani na mbinguni,
akiwa amezungukwa na roho wa mbinguni, alikuwa amezungukwa na wa mbinguni.Nuru ya
usiku aliofufuka katika wafu ilikuwa ni sawa na nuru iliyoonekana wakati wa kuzaliwa kwakle
katika nyumba ya Fasodena.Nuru hiyo ilimfuata mpaka Paradiso, na watu walipoiona wakasema:
Huyo ni Krishna amepaa kuelekea kwake mbinguni”.
Rama,ambaye ndiye Vishnu katika mwili, baada ya kukamilisha kazi zake hapa duniani alipaa
kuelekea mbinguni,akarejea katika uungu wake.Na kwa baraka ya jina la Rama na kumuamini
hupata kusamehewa makosa, na kila alitajaye jina lake na kumsudia kwa moyo wakati wa kifo
chake hupata kusamehewa madhdmbi yake yote.
Na katika kisa cha kufufka kwa Buddha katika wafu kinafana na yaliyoelezwa awali.
Wanamwita kwa majina ya “Gamidiyo,Gama,Gam” na kusema kuwa alipokufa ,machozi
yalimiminika na huzuni ikawatamalaki wakazi wa mbinguni na ardhini kwa sababu
wamempoteza mungu wa upendo, kwa kiasi kwamba Mahadiyo (yaani Mungu Mkuu)
alihuzunika sana na kuita: “Inuka ewe mpendwa mtakatifu”, na hapo Gama (yaani Buddha)
akainuka akiwa hai. Huzuni zikageuka kuwa furaha ,mbingu ikashangilia na kunadi kwa furaha:
“Amerejea Mungu ambaye alidhaniwa kuwa amekufa na kutoweka”.Khofu ya Jehannamu
ikazidi,mbingu ikadhihirisha mshangao wake, sanda ikaondolewa mwilini mwake, kaburi
likafunguliwa kwa nguvu za Mungu kasha akapaa kwa mwili wake kuelekea mbinguni baada ya
kukamilisha kazi zake.Mpaka leo hii wanawaonyesha wafuasi wake alama za nyayo zake katika
eneo la mlimani mahali ambapo alipandia kuelekea mbinguni.Na wafuasi wake wanaamini kuwa
kwa kumuabudu na kumuomba watapata kuingia katika ufalme wa mbinguni na kuungana naye
na kuwa mwili mmoja kama yeye alivyo mmoja pamoja na chemchem ya nuru.
Wachina huamini kuwa Laocyon (mzawa wa mwanamke mtakatifu) alipokamilisha kazi zake
za kisamaria hapa duniani,alipaa kwa mwili wake kuelekea Paradiso;na wanamchukulia kuwa ni
Mungu ambapo kuna mahekalu mengi yaliyojengwa kwa ajili yake na kwa ajili ya kumbukumbu
yake.
Majusi wanaamini uungu wa Zoroaster na kusema kuwa alitumwa kuja kuwakomboa na
kuwaokoa watu kutoka katika njia mbaya, na kwamba baada ya kumaliza kazi zake hapa duniani
alipaa kuelekea mbinguni.Wafuasi wake mpaka leo hii wanamtaja kwa ukuu na heshima na
kusema kuwa Zoroaster yu hai, mbarikiwa, nyota na majina mengine kama hayo.
Naye Mkombozi Iskolapius mwana wa Mungu,baada ya kuuawa alifufuka katika wafu.Na kisa
cha historia yake kimeelezwa katika utenzi wa shairi kikieleza maisha na kazi zake.Anasema
50
mwana mtakatifu: Mama mtakatifu alimuoana Mungu Mwenye nuru, akasimlia kisa chake cha
kinabii,akamwambia, Salaam ewe tabibu mkuu wa ulimwengu. Amani yote iwe juu yako ewe
mtoto ut\k\yeweza kuwaponya mataifa katika miaka mingi ijayo, pindi wafu
watakapozinduka.Ukuaji na kufuzu kwako hakutakuwa na mipaka. Utaziongezea mamlaka ukuu
na watu kuwa wengi. Kwa uweza wako utahuisha wafu, najuu ya kichwa chako utatoka ukulele
na hata kufa, nawe kutoka mahali penye giza utasimama na ushindi na kuwa Mungu”.
Na Mkombozi Adoni (huitwa pia Tamuz) baada ya kuuawa alifufuka katika wafu. kisa cha kifo
na kufufuka kwake kimesimuliwa na Julius Crimicius, ambaye aliishi enzi za Costantine,
anasema: “Katika usiku maalumu, pindi watakatifu walipopita kumpa heshima Adoni, walikuja
na sanamu na kuliweka juu ya kitanda ( cha watoto).Watu hao walianza kulia na kuomboleza
kwa nyimbo mbalimbali za huzuni. Kisha alikuja kiongozi mkuu akaanza kuvipaka mafuta
vinywa vya waimbaji huku akisema: “Tumainini enyi watakatifu kwa kurejea Mungu wenu, na
mtegemeeni Bwana wenu aliyefufuka, kwani kwa mateso yake ametuletea ukombozi”.
Bwana Dupis anasema: "Wakazi wa Alexandria walikuwa wakitengeneza jeneza kwa hadhi na
heshima ili kukumbuka kifo cha Adoni, na kulichukua sanamu lake kwa heshima kubwa mpaka
kwenye kaburi lililoandaliwa kwa lengo hilo na kuliweka humo katika hali ya utulivu wa hali ya
juu. Na kabla ya kuimba nyimbo za kufufuka kwake, hukaa kimya kwa huzuni ya kukumbuka
mateso na kifo chake na kuonyesha jeraha lililompata mwilini mwake kwa kuchomwa mkuki.
Kisha baada ya hapo huanza kufurahi na kushereherkea. Sikukuu hiyo hufanyika tarehe 25 ya
mwezi wa Machi".
Naye Dr. Prichard anasema: "Wasuriya walikuwa kwakisherehekea kwa ajili ya Adoni katika
kipindi cha majira ya Kuchipua. Kwanza walikuwa wakiomboleza kifo chake kwa huzuni
kubwa, kisha huelezea kufufuka kwake katika wafu kwa furaha na shangwe".
Bwana Klematt 100
anasema yafuatayo kuhusu kufufuka kwa Adoni katika wafu : Na baada ya
kuhuzunika na kumwoboleza Adoni hutangaza kuwa amefufuka na kurejea kuwa hai, na alama
ya kufufuka kwake ni wao kuingiza taa mahali alipo, na ndipo kiongozi mkuu huwaambia watu
waliokusanyika mahli hapo akisema: Zifarijini nafsi zenu na mfurahike nyinyi ambao mmepata
siri za uungu zilizohifadhiwa kwa ajili yenu, basi na tufurahike baada ya mateso
yaliyotupata".Kisha husema maneno yafuatayo: "Nimeokolewa kutokana na msiba mkubwa, na
fungu langu sasa ni zuri.Na hapo watu husema baada yake maneno yafuatayo: "Amani iwe juu
ya njiwa aliyerejesha nuru".
Anasema Bwana Alexandria Mrray: "Wayunan wa zamani walikuwqa waakiheshimu na
kuitukuza sana sikukuu ya kufufuka kwa Adoni katika wafu, walikuwa wakileta sanamu kana
kwamba ni Adoni na kulisomea sala ya maiti huku wakilia na kuimba nyimbo za huzuni na
kukata tamaa. Baada ya hapo sauti za furaha hupaa na kunadi kuwa Adoni amefufuka na kurudi
kuwa hai".
Mkombozi Osiris mzawa wa mwanamwali, alifufuka baada ya kifo. Wamisri wanamwita
“MTUME WA PEKEE”.Mohami anasema: Muhimili wa mafundisho ya kidini kwa wapagani
wa Kimisri katika karne nyingi zilizopita ilikuwa ni imani ya kufufuka kwa Mungu, Mpatanishi
aliyejidhihirisha kwa mwili, Mzawa wa mwanamwali, na kwamba ndiye mmiliki wa milele wa
51
ufalme wa mbinguni. Walikuwa wakisherehekea sikukuu ya pasaka katika kipindi cha majira ya
kuchipua kwa kumbukumbu ya kufufuka Mungu Mokmbozi Adoni, wakifurahi na kushangilia,
na kuamini kuwa aliitoa nafsi yake kuwa kafara ya dhambi za watu, na kwamba ndiye mpaji wa
amani na uzima, na ndiye mfunguzi wa haki.
Anasema Bwana Bonwick: Katika mambo ya kushangaza sana, ni kuwa mataifa, tangu miaka
elfu tano iliyopita, walimwamini Osiris ambaye alifufuka katika wafu, na kuamini kuwa ni
mkombozi wao na kwamba nao pia watarejea kuwa hai kama yeye…naye ndiye mashuhri zaidi
katika miungu yao wanayempenda sana na kusema kuwa ndiye mwema na kipenzi chao katika
uzima na umauti. ( Wasomi wa masuala ya dini wamehadharisha kuhusu kisa cha kuzaliwa,
kufa, kufufuka na kupaa kwake kuelekea mbinguni).Kwa sababu ya kupenda mambo ya heri
alipata kuwabeba watu, na ndiyo maana akauawa na kuzikwa, na kaburi lake likawa ni eneo
takatifu zaidi katika nchi ya misri inayotembelewa na watu.Hali hii ilidumu kwa muda wa
maelfu ya miaka, ambapo walikuwa wakiwasha taa juu ya kaburi hilo na kumwimbia nyimbo za
huzuni ambazo zimeelezwa na Herdotis. Kabla ya sikukuu walikuwa wakimhuzunikia kwa
kipindi cha siku tatu kisha husherehekea sikukuu ya kufufuka kwake katika wafu kwa furaha na
shangwe.
Na Mungu Horus motto wa mwanamwali Isis, alipatwa nay ale yaliyompata Osiris, yaani
aliuawa na kufufuka katika wafu. Na wale wanaomwamini wanamfanyia kama afanyiwavyo
huyo aliyetajwa hapo juu, kama kumhuzunikia na kumlilia na kasha kufurahi na kupamba siku
ya kufufuka kwake.
Attis mkombozi na mungu wa Wafrige, aliuawa kwa kuonewa kasha akafufuka katika wafu.Na
wanasimulia kisa cha kuzaliwa na kufufuka kwake kwa mlolongo wa simulizi mbalimbali, lakini
zikiwa na madhui moja. Vilevile humwita kuwa DHABIHU iliyorejea katika uzima tarehe 25
Machi, siku ambayo huiita Helariya au sikukuu asili ya pasaka.
Na Mithra mkombozi wa Waajemi, ambaye ndiye mpatanishi kati ya Mungu na watu, dini yake
ilikuwa imeenea sana katika nchi za Uajemi, Armenia, na Asia ya kati ambapo waliamini kufa na
kufufuka kwake katika wafu, na katika sikukuu ya kufufuka kwake inayofanyika tarehe 25
machi, humleta kijana na kujifisha kwa mdamfupi kisha kuamka kwa maana kwamba amerurudi
kuwa hai. Yote hayo huyafanya ili kufananisha kufanakufufuka kwake. Na wanaamini kwamba
kwa kuteseka kwake walipata kukombolewa na humuita MKOMBOZI. Ifikapo sikuya kufufuka
iliyotajwa hapo juu,wakuuwa dini hukaa pembezoni mwa kaburi ambalo hulitengeneza
mahekaluni mwaonakisha huanza kulia na kuombleza katika hali ya giza kali, kasha huwasha taa
ghafla na kunadi „furahini na mshangilie enyi watakatifu mliokombolewa, kwani amefufuka
bwana wenu ambaye kwa kifo na mateso yake tumepata utakaso‟ na huitukuza sana ijumaa ya
huzuni.
Na mkombozi Bacchus mtoto wa mwanamwali Semele, alifufuka baada ya kuuawa.Na
katika siku ya sikukuu ya kufufuka kwake walikuwa wakimleta mtu aliyekufa na kumuweka
kitandani,kisha huomboleza kifo cha mkombozi wao Bacchus kama wafanyavyo mataifa ya
kipagani yaliyotajwa hapo awali. Na ifikapo asubuhi ya tarehe 25 ya machi hunadi kuwa
amefufuka na hapo huwaza kufurahi kwa imani kuwa kifo chake kilileta ukombozi nafuraha kwa
watu wenye mikosi na husema kuwa baada ya kufufuka alipaa kuelekea mbinguni.
Na wanaamini kuwa Heracles mkombozi mwana wa Mungu Zeus aliyezaliwa na mama
mwenye asili ya kibinadamu, aliuawa na kufufuka katika watu kisha akapaa kuelekea mbinguni
52
akilindwa na radi. Na wale wanaoamini uungu wake walijenga hekalu katika eneo
linalosemekana kuwa mahali alipopaa kuelekea mbinguni.
Naye Mamnuun aliuawa na kufufuka katika wafu akaliliwa na kuhuzunikiwa na mama yake
Wakius. Na Ahfarius naye pia alifufuka katika wafu. Waumini wake wlikuwa wakiwaonyesha
watu mahali alipopaa kuelekea mbinguni.
Yaldor, Mungu na mkombozi wa Wascandnavia aliuliwa na kufufuka kwenye uzima wa
milele, Na wanasema kuwa „Yaldor mwema na mungu mwenye neema, alipoteremka kuzimu
alimwambia Hermod [ambaye alimlilia na kumuomboleza]kuwa „mwambie kila kiumbe aliyoko
ulimwenguni katika wafu na wazima, wanililie ili nipate kurejea kwa Mungu‟.Alipokwisha
kusikia hayo maneno aliwatuma wajumbe kwenda kila kona ya dunia nakuwaambia wamlilie na
kuhuzunikia kifo chake iliYaldor apate kutoka kuzimu.Wakamlilia na hapo akarejea kuwa hai‟
Pia wanamwabudu mu ngumwengine aitwaye Frey na kusema kuwa aliuawa kisha akafufuka
katika wafu. NawaDruids wa zamani huko uingereza walikuwa wakiamini kufa na kufufuka kwa
Bacchus na kutengeneza jeneza katika mahekalu yao kila mwaka kama ishara ya kumbukumbu
ya kifo chake. Jeneza lililokuwa likitengenezwana Warumi na Wajerumani.
Quetzalcatl, Mkombozi wa Wamexco aliyeuawa kwa kusurubiwa na alifufuka katika wafu.
Na kisa cha kufufuka kwake kimeelezwa katika kumbukumbu ya kimexco katika huko „codix
purgiyanus‟kisa ambacho kinapatikana mpaka leohii.
Wanusr,Wajerumani, Wachina na wengineo walikuwa wakipaka mayai kwa rangi mbalimbali
na kuyagawa baina yao, ambapo kati yao kuna waliyoyahifadhi mpaka mwaka ujao kwa ajili ya
siku waliyofufuka miungu, kama ishara ya kurejea kwao katika uzima.
II-KUFUFUKA KWA KRISTO KATIKA WAFU:
Yale yaliyosemwa na wapagani juu ya kufufuka kwa miungu yao ndio yaliyosemwa
moja kwa moja na wakristo kuhusu Yesu Kristo. Kwa nini wasiseme hayo wakati yeye ni
miongoni mwa wema wa miungu waliojidhihirisha kwa mwili kwa mujibu wa imani yao?
Katika injili ya Mathayo sura ya 28 ya mstari wa 5 mpaka 8kuna habari ifuatayo :Malaika
akajibu, akwaambia wale wanawake, msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta
Yesu aliyesurubiwa, hayupo hapa kwani amefufuka kma alivyosema. Njooni, mpatazame mahali
alipolazwa. Nanyi njooni upesi mkawaambie wanafunzi wake, Amefufuka katika wafu.Tazama,
awatangulia kwenda Galilaya, ndiko mtakakomwona. Haya nimekwisha waambia;
Vilevile habari yakufufuka kwake katikawafu imeelezwa katika injiliya Marko, sura ya
16 101
, Injili ya Luka sura ya 24 na katika injili ya Yohana sura ya 20 102
.Hata hivyo injili hizo
zote hazijaafikiwa juu ya namna ya kufufuka kwakwe, bali zimekhitilafiana katika hilo. Na lau
kama kuelezea khitilafu hiyo kusingemaanisha kutoka nje ya mada yetu, tungeielezea kwa
upana.
SURA YA KUMI NA NNE.
KUREJEA DUNIANI KWA AJILI YA HUKUMU .
I-WAPAGANI:
53
Wachina huamini kuwa mkombozi na mlinzi wao Vishnu aliyejidhihirisha kwa mwili wa
kibinadamu kwa jina la Krishna, atakuja kwa mara ya pili katika siku za mwisho.Na vitabu vya
kidini vya kihindu vinasema; Nyota thabiti zitakaporejea mahali zilipoanzia mzunguko wake,
ambao ndio wakati kilipoanza kila kitu [ambayo ni katika nyota ya nge] akatokea Vishnu katika
watu kwa namna ya mpanda farasi aliyejizatiti kwa silaha, akiwa amepanda farasi wa kijivu
mwenye mbawa akishika upanga wenye moto kwa mkono wa kwanza ili apate kuwaangamiza
waovu ambao bado wapo hai katika uso wa dunia.Na katika mkono wa pili kutakuwa na pete
yenye kung‟aa, kama ishara ya kuanza kwa “Yakos” yaani vizazi vitukufu, na kuwa kiyama
kimefika.Wakati wa ujio wake jua na mwezi vitafifia mwanga wake, ardhi itatikisika na nyota
kudondoka.
Na Mabudha wanaamini kuwa Budha huonekana mra nyingi katika mwili wa kibinadamu
ili kuwaandaa na kuwajulisha kuwa wataungana na dhati yake kuu,na kuwa siku za mwisho pia
ataonekana. Ujio huu umetajwa kwenye vitabu vyao vitakatifu kuwa makusudio yake ni
kurejesha nidhamu na saada duniani.
Na Wachina huamini kuwa katika siku za mwisho, itakapomalizika miaka elfu moja atakuja
mtu wa Mungu duniani ili kuirudishia amani na saada, na vitabu vyao vya dini vitano
vimesheheni maelezo ya enzi ya dhahabu huko mbeleni. Majusi wa zamani nao pia huamini
kuwa itapita duniani miaka elfu moja, ambapo watu wote duniani wataamini dini zaZoroaster.
Na Majusi wa zama hizi (ambao ni masalio ya wale Majusi waliokuwa wakiamini mungu wa
Zoroster) wanasema kuwa kuna dhati takatifu katika ardhi iitwayo Kankodar ambayo inatazamia
amri ya Yazidi Sairosh ambaye atakuja nchi ya uajemi na kuirejesha hapo dola ya zamani na
hatimaye kueneza dini ya Zorostar ulimwenguni, na atakapotaka kufufua wtu ata ziamuru ardhi
na bahari kutoa mabaki ya wafu ambapo Auramazda atavika nyama na damu, na wale ambao
watakuwa hai mpaka siku ya mwisho atawafisha na kuwafufua kama watu wengine. Kabla ya
kutokea hayo watatokea mitume wakuu wale tu ambao watafanya maajabu na miujiza, na kwa
mda huu ardhi yte itakumbwa na balaa kubwa, vita njaa na mengineyo. Kisha baada ya
kufufuliwa kila mtu atalipwa kulingana na matendo yake, kama ni kheri atapata kheri na kma ni
shari atapata shari, na wma watabaguliwa dhidi ya waovu, na wale ambao hawakuwa ni wenye
kuridhiwa watatupwa jahannamu ili watakaswe kwa muda wa siku tatu usiku na mchana,
watatakaswa kwa moto wa madini yenye kumiminika, na hivyo watatolewa kwenda kwenye
neema za milele. Ufalme wa shetani utakwisha…… na ardhi itawekwa nuru ili iwe makazi ya
watu wema, na mtawala wao atakuwa Auramazda pekee.
Wafua wa Bucchus pia wanatazamia ujio wake wa mara ya pili ili autawale ulimwengu na
kuwarudishia watu saada.Wacathoni nao walikuwa wakitazamia ujio wa shujaa wao “Kaloebok”
kwa mara ya pili ili awakomboe kutokana na dhulma ya Wajermani, ambapo kwa sasa ametulia
mpaka matatizo yatakapoenea, na hpo atadhihiri na kuwakomboa kutokana na dhulma.
Na Wathelato wanangojea ujio wa mara ya pili wa “Puryaam Puroeham”, baada ya miaka elfu
moja kupita, na wanasma vilele kuwa “Welkardanseck” anasubiri aamke usingzini mwake na
kumsaidia Damis ili kuwqashinda maadui zao wa Perusia.
Wascandinavia wa zamani wanaamini kuwa siku za mwisho watakumbwa na balaa na majanga,
ardhi itatikisika na nyota zitadondoka, kasha baada ya hapo joka kubwa litafungwa na
minyororo,na dini ya Odini kutawala juu ya watu wote.
Na wafuasi wa Quetzalcoatlmkombozi wa Mexco wanatazamia ujio wake wa mara ya pili, na
wanaamini kuwa kabla ya kuondoka duniani aliwaeleza wakazi wa Mitsholola juuya ujio wake
wa mara ya pili na kutawala. Na meli za Wahispania zipoonekana katika pwani ya Brazili
54
mwaka 1518 AD, walizani kuwa ni mahekalu aliyokuja nayo Quetzcoal kama alivyokuwa
amewaahidi.
II- UJIO WA KRISTO KWA MARA YA PILI KWA AJILI YA HUKUMU
.
Tumeeleza waliyoyasema wapagani kuhusu ujio wa watoto wa miungu yao kwa kwa mara
nyengine. Wakristo nao pia wamewaiga, wakiamini ujio wa kristo kwa mara nyengine hapa
duniani na hawakuacha chochote katika yaliyosemwa na wapagani juu ya miungu yao ispokuwa
waliyasema kumhusu yesu kristo, Kwa kudhani kuwa kufanya hivyo ni kumtukuza.Angalia
maelezo katika vitabu vyao vitukufu juu ya jambo hilo:
Katika injili ya Mathayo sura ya 24 msitari wa 27: “kwa maana kama vile umeme utokavyo
mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake mwana wa
Adamu” , ( katika sura hii zimetajwa alama na dalili kadhaa ambazo zitatokea kabla ya ujio
wake, ambazo hatotazitaja kwa sababu ya kutaka kufupisha” 104
Na katika Matendo ya Mitume, sura ya kwanza msitari wa 10 na 11 kuna maelezo yafuatayo:
“walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu waili
wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona
mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu
mbinguni, atakuja jinsi iyo mlivyomwona akienda zake mbinguni”.
Vilevile katika Injili ya Marko sura ya 13 msitari wa 26 kuna maelezo yafuatayo: “Hapo ndipo
watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu”.
Na kwa mfano huu kuna sehemu nyingi zilizoelezea ujio wake wa mara ya pili, vilevile maelezo
ya wakuu wa kanisa na wanatafsiri wameeleza mengi , nasi tunatosheka na hayo tuliyoyaeleza.
SURA YA KUMI NA TANO
IMANI YA KWAMBA MWANA NDIYE MUUMBA
I- WAPAGANI:
Mafundisho yanayopatikana katika vitabu vya kidni vya Wahindu vinaeleza waziwazi kuwa
“Krishna mwana wa Mungu aliyezaliwa na mwanamwali Devaki, ambaye ni nafsi ya pili katika
utatu mtakatifu, ndiye aliyeumba mbingu na ardhi na vilivyomo, naye, kwa imani yao, ndiye wa
kwanza na wa mwisho, ndiye kila kitu, na muumba wa kila kitu.
Katika kitabu kiitwacho “ Bahakwat Gita” ambacho ni mojawapo ya vitabu vitakatifu kwa
wahindu, imeelezwa kuwa Krishna alimwambia mwanafunzi wake Arjon mpendwa maneno
yafuatayo: “Mimi ndiye Bwana na mwanzilishi wa viumbe vyote, nilimuumba mwanadamu kwa
namna nne zenye na majukumu misingi tofauti, tambua kuwa mimi ndiye mtengenezaji na
55
muumba wa binaadamu. Mimi sikuumbwa hivyo sifikiwi na hali ya kutokuwapo”. Vilevile
akasema katika mawaidha ya saba yaitwayo “nguvu ya maumbile na roho mkuu”: “mimi ndiye
muumba, mwangamizaji, na mkuu ambaye kila kitu kinanitegemea”. Akasema pia katika
mawaidha ya tisa yaitwayo (( siri kuu na elimu ya mwanzo)) kuwa: (( mimi niliutandaza
ulimwengu kwa namna yake katika pazia, na mimi ndiye mhifadhi wa kila kitu, na mimi ndiye
baba na mama wa huu ulimwengu huu, na mimi ndiye mkuu, mlinzi, na mimi ndiye Mtakatifu
ambaye ni lazima kumtambua, na mimi ndiyo alama ya siri ( A na Z), nami ndimi njia ya wema ,
mfariji, muumba ashuhudiaye, na rafiki ambaye marejeo ni kwake”. Akasema pia katika
mawaidha ya kumi yaitwayo muuganiko wa asili wa kimungu: “mimi ndimi muumba na mtoaji
wa kila kitu,basi na waamini hivyo wale walioneemeshwa kwa hekima ya kiroho,na nyoyo zao
zifungamane nami wakiabudu na kulitaja jina langu,na wafundishane mafundisho yangu ili
furaha ienee kati yao.”
Na vitabu vitakatifu vya wahindu vinawaelezea Krishna kuwa ndiye chanzo cha (“”uhai, na bila
yeye kusingekuwepo kitu chochote katika ulimwengu huu.Vilevile Wachina wanasema kuwa
Mwenyezmungu hakuumba kitu chochote, bali mwanae ndio muumba wa ulimwengu na sanamu
lililochongwa kwa sura yake huliita Ntikay ” ambapo huliabudu na kuliomba kuwatimizia
shidaszao. Na wanasema kuhusu “Lanotho”, aliyezaliwa na mwanamwali mtakatifu, kuwa ndiye
muumba wa kila kitu.Pia mafundisho ya kidini ya Wakeldayo yanaeleza waziwazi kuwa mwana
wa pekee ndiye muumba wa kila kitu. Vilevile wafuasi wa mungu Tao wanadai kuwa ni mwana
wa mungu na ndiye muumba wa kila kitu.
“
Mafundisho potofu ya kidini ya Waajemi wa zamani yameeleza waziwazi kuwepo kwa mungu
mmoja asyeonekana wala kudirikiwa wanayemwita “Zaroona Aqarena”, na maana ya sentensi
hii ni ( asye na mipaka ya nyakati) (yaani wa milele na milele). Na kutokana na Mungu
alipatikana Auramazda mfalme wa nuru, mwana wa pekee muumbaji, ambaye kila kitu
kilitokana nay eye, nba yeye ndiye Muumba.
Vitabu vitukufu cha majusi kiitwacho “Zandafasta” Kimesheheni sala na maombi ya mwana
wa pekee wa Mungu “. “Auramazda”, na ufuatao ni mfano was ala na maombi yao: “
Nazitanguliza sala zangu kwa Aramazada, yeye ndiye Muumba wa vitu vyote, vilivyokuwepo na
vitakavyokuwepo hata milele, naye ndiye mwenye hekima na mwenye nguvu, Muumba wa
mbingu, jua, mwezi,nyota, upepo mawingu, maji, ardhi, moto, miti, wanyama na binadamu na
ndiye aliyesujudiwa na Zoroaster aliyeleta sheria duniani, na akajua kwa utambuzi wa asili, na
akaamini yaliyokuwepo zamani, ya sasa na yajayo, alipata elimu na neno kuu ambalo kwake
nafsi hupata kulivuka daraja la nuru ambapo huviacha dunia ya maovu na kuelekea kwenye nuru
ambayo ni makazi matakatifu yaliyojaa harufu nzuri. Ewe Mungu hakika mimi nazitii sheria
zako, nafikiri, nazungumza na kutenda kulingana na maamrisho yako, ninajiepusha na kila
dhambi na kutenda matendo mema, na ibada yangu ni kwa ajili ya Auramazda mlipaji wa
matendo mema kwakuwa yeye ndiye aokowaye wale watendao kulingana na maamrisho yake
wakatumaini kufika paradiso makazi ya saada, nuru na harufu nzuri”.
Na waumini wa mkombozi Adoni huamini kuwa ndiye aliyewaumba watu na atawafufua
baada ya umaut.
Katika kitabu cha Wahindu kiitwacho “Gita” imeelezwa kuwa Krisha alisema: “Haikutokea
zama ambayo mimi sikuwapo, mimi niliumba kila kitu, mimindiye mwenye kubaki, wa milele
mwanzilishi na nilyekuwepo kabla ya chochote, mim ndiye mtawala mwenye nguvu juu ya
ulimwengu, mimi ni mwanzo katikati na mwisho wa kila kitu”.
56
Na miongoni mwa maombi yaArjoni mwanafunzi wa Krishna ni hya yafuatyo “Wewe ndiwe
Mungu mkuu mwenye kubaki ambaye ni lazima watu wakujue, wewe ndiye mwenye kufusha
viumbe,wewe ndiwe mlnzi wa dini na muwanzilishi, ninakutukuza ewe Mungu uliyekuwepo
kabla ya miungu wengine”.
Akasema vilevile: “Utukufu ni wako hapo kabla na hata milele, wewe ni vyote katika vyote,
wewe ambaye utukufu na nguvu zako hazidirikiwi, wewe umekizunguka kila kitu, hivyo wewe
ni kila kitu”. Na katika kitabu kitukufu “Vishna Purana” kuna maelezo yafuatayo: “ alipodhihiri
Vishna kwa namna ya Kishna, na kuingia katika mwili wa bikira Devaki na kuzaliwa naye,
alisema kuwa “Yeye hana mwanzo katikati wala mwisho”.
Na baadhi ambaye A na Z, uwepo wake hauna mwanzo wala mwisho, naye ndiye
Bwana,Mfalme, muweza, wa milele na Mungu mkuu atukuzwaye”.
Naye Laokyon mwana wa Mungu aliyezaliwa na mwanamke mwanamwari uwepo wake moja
kwa moja hauna mwanzo wala mwisho.”
Katika upotofu wa wafuasi wa Laotzu huko china,Jauhan safi, muumba war oho ya mwanzo,
chanzo cha mbingu na ardhi, Muumba wa viumbe na kuwa yeye alikuwepo kabla ya viumbe na
kabla ya mtikisiko wa kwanza wa ul;imwengu”. Na katika kitabu cha majusi kiitwacho
“Zandafista” imeelezwa kuwa “Auta mazda mwana wa pekee wa Mungu alikuwepo kabla ya
mwanzo na atendelea kuwepo milele.”
Zeus anayeitwa kuwa nia A na Z alielzewa na Ouzfink kama ifuatavyo: “Zeus ni wa mwanzo
na wa mwisho. Naye ndiye Muumba wa kila kitu kilichopo”.
Na wanamsifu Bacchus kwa sifa ya utangu, ambapo katika maandishi ya zamani
yaliyonakshiwa kwenye Dirham kuna maneno yafuatayo: “ Mimi (yaani Bacchus) ni kiongozi
wenu, na mlinzi wenu, mimi ndiye Ala na Omega”.
II- IMANI YA KUWA MTOTO YESU KRISTO NDIYE MUUMBA WA VIUMBE VYOTE.
Tumeona yaliyoaminiwa na watu waliopotea kuhusu watoto wa miungu yao kuwa ndio
waumbaji na watengenezaji wa ulimwengu na vyote vilivyomo, maneno kama hayo yametolewa
na Wakristo kuhusu Yesu Kristo, yaani wakisema kuwa ndiye Muumba na mwanzilishi wa
viumbe vyote.
Katika injili ya Yohana Sura ya kwanza msitari wa 3 na10: “ Vyote vilifanyika kwa huyo, wala
pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika”. “Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye
ulimwengu ulipata kuwako, wala ulmwengu haukumtambua”.
Vilele katika waraka wa Paulo kwa Wakolosai sura ya kwanza ukurasa wa 16 na 17 kuna
maelezo yafuatayo: “ kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyombinguni na vilivyo
juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; vikiwa ni vitu vya enzi au usultan, au enzi au
kwa mamlaka, viyu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake. Naye amekuwako kabla
ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye”.
Na katika waraka kwa Waebrania, Sura ya kwanza mstari wa pili kuna yafuatayo: “mwisho wa
siku hizi amesema na sisi katika mwana, aliyemuweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye
aliyeufanya ulimwengu”.
Kwa mfano huu, kuna vifungu vingi ambavyo vinaeleza kuwa yeye ndiye Muumba wa
ulimwengu, vilele maelezo ya wakuu wa dini hiyo yanabainisha na kusema waziwazi jambo hilo,
wala sio ajabu kwa jambo hilo, madhali wanamchukulia kuwa ni Mwana wa Mungu kama
walivyofanya waliomtangulia miongoni mwa watoto wa miungu ya kipagani.
57
SURA YA KUMI NA SITA.
UBATIZO KWA AJILI YA KUONDOA DHAMBI.
Bwana Amerly 105
,Bunsen 106,Higgins 107
, na Lillie 108
kwa ufupi wanasema: “ katika nchi za
India, Mongolia naTibet wanapowabatiza watoto huwasha mishumaa,wakachoma vitu vyenye
harufu (ubani) madhabahuni na makuhani husoma sala maalum na kisha humzamisha katika maji
mara tatu, na baada ya hapo humwita jina walitakalo.
Na Wabrahma wa desturi ya kidini ya zamani inafanana na Wamajusi, Wamisri, Wayunani na
Warumi wa zamani, ambayo ndiyo ubatizo wenyewe, na wakati wa kufanya husali na kuliomba
jua, ambapo baada ya kiapo cha imani kutoka kwa anayebatizwa, (akiwa mtu mzima) juu ya
kutekeleza kikamilifu utii kwa wakuu wa kidini na kutunza siri ya usafi wa mwili wake,
humnyunyuzia maji mara tatu na kuzungumza kwa namna inayolingana na cheo hicho; na
kitendo cha kumnyunyuzia maji hukichulia kama “ kuumbwa upya”, na humvika nguo maalum
na taji, na kuchora ,msalaba mashavuni mwake, na humuwekea kfuani mwake msalaba katika
namna ya misalaba ya “TO” na humkabidhi siri ambayo ni neno OM.
Ama kama anayebatizwa ni motto, huchukuliwa na kiongozi wa kidini wa Wabrahma
wanayemwita Koro (yaani mchungaji), na hupakaza kwa tope na kisha humzamisha katika maji
mara tatu huku akisema: “ ewe Mungu Mkuu, hakika huyu mtoto ni mwenye dhambi,
amejipakaza kwa madhambi kama alivyojipakaza kwa tope la huu mto, hivyo kama ambavyo
maji yanamtakasa kutokana na hili tope, basi mtakase na umkomboe kutokana na dhambi”, pia
huamini kuwa ubatizo huondosha madhambi yoyote hata kama yatakuwa na wingi wa kiasi gani.
Viongozi wanaosimamia zoezi la ubatizo huitwa “ wana wa jua”.
Nao wafuasi wa Zoroaster, huwabatiza watoto wao, wakubwa kwa wadogo. Anasema bwana
Pasper : “Majusi wa zamani walikuwa wakiwapeleka watoto wao mahekaluni siku kadhaa baada
ya kuzaliwa, na kuwakabidhi kwa Kuhani mbele ya sanamu la jua ( moto ndio alama ya jua),
kisha huwazamisha katika chombo kilichojazwa maji, na baada ya hapo huwaita kwa majina
wayatakayo”.
Naye Dr. Hidde anasema: “ Ubatizo kwa watu wa zamani ilikuwa ni kwa kuzamishwa katika
maji au kunyunyiziwa maji, na ubatizo huu huuita „kuzaliwa upya”, ambapo baada ya tukio hilo,
huzichukulia nafsi kuwa ni takatifu na zenye saada, kisha huwapa majina wayapendayo”.
Wamisri walikuwa wakiwabatiza watoto wao wa umri mkubwa na kuwapa siri za awali za
kidini, na kuchora mashavuni mwao alama ya msalaba.
Na Waapoliso wa Fedora huko Afrika walikuwa wakiwabatiza watoto wao, ambapo wakati wa
ubatizo husoma sala maalumu, na kuamini kuwa ubatizo unaondosha madhambi.
Naye Bwana Doane anatoa maelezo yafuatayo: “Wapagani wa Kirumi walikuwa wakiwabatiza
watoto wao kwa maji wakiamini kuwa ubatizo ni njia ya kuondosha madhambi” 109
.Naye
mwanahistoria Dhiuginus ameeleza kwamba walikuwa wakiwabaiza watoto wao kwa jina lake,
ambapo watoto wa kiume walikuwa wakibatizwa siku ya tisa baada ya kuzaliwa kwao, na watoto
wa kike wakibatizwa siku ya sita baada ya kuzaliwa. Na maji hayo ya ubatizo huyaita “maji
matakatifu”. Baada ya ubatizo, kuhani huwapa wazazi wa mtoto cheti kinachoonyesha kuwa
mtoto wao amebatizwa na kuumbwa upya . Kisha baada ya hapo, wana haki ya kumhesabu
58
kuwa sehemu ya familia yao, na siku hii huichukulia kuwa sikikuu adhim. Pia walikuwa
wakiwabatiza wale wanaopokea mafindisho ya siri ya Mithra.
Wapagani wa Norwey na Denmark walikuwa wakiwabatiza watoto wao kwa kuwamwagia maji
na kisha kuwa majina. Nao Walifone walishikamana sana na ubatizo na kuuchukulia kuwa nguzo
muhimu katika mambo yao ya kidini. Hali kama hiyo ilijitokeza kwa Wajerumani wa zamani,
Wadruid, wakazi wa Zilanda na wengineo, na wakati wa shughuli ya ubatizo hufanya sala
maalumu kwa kokombolewa kutoka katika dhambi.
Na Wamexico wa zamani walikuwa wakiwabatiza watoto wao muda mfupi baada ya kuzaliwa,
ambapo ndugu na jamaa hukusanyika nyumbani kwa wazazi wa mtoto, na wakati wa kuanza
kwa shughuli ya ubatizaji, mkunga hukishika kichwa cha mtoto mkononi mwake na kukielekeza
kichwa chake upande wa machomozeo ya jua, kisha hufanya sala maalumu kwa Quetzalcoatl
pamoja na miungu wa maji, na baada ya hapo, Kuhani hunawa mikono yake na kisha huushika
mdomo na kifua cha mtoto na kusema: “ tunayaomba maji yaangamize na kuteketeza madhambi
yaliyogandamana na huyu motto kabla ya kuumbwa kwa ulimwengu”, na baada ya hapo huuosha
mwili wake kwa maji, na kutaja kila kitu kinachoweza kumdhuru kiondoke ili apate kuzaliwa
upya baada ya kubatizwa.
Naye Prescott anasema: “ Wamexico walikuwa wakiwabatiza watoto wao kwa manukato na
maji, na kuiomba miungu yao iyaruhusu matone ya maji yaondoshe madhambi yaliyompata
mtoto kabla ya kuumbwa kwa ulimwengu, ili azaliwe mara ya pili kwa ubatizo. Na wakati wa
ubatizo huwalika ndugu na jamaa kuhudhuria shughuli hiyo” 110
Bwana Lundy anasema: “tunapoichunguza historia, tunaona kuwa ibada ya ubatizo ni ya
zamani sana, na ilikuwa imeenea katika maeneo ya Asia na Amerika, ambapo wakazi wa Brazil
walikuwa wakiwabatiza watoto wao wa kike na wa kiume katika hekalu liitwalo “kanisa la
aliyesulubiwa” kwa kuwanyunyizia maji katika birika. Na maji hayo ya ubatizo waliyaita kuwa
ni “ maji ya uzao mpya”.
***
II- WAKRISTO:
Tumeelezea namna ubatizo ulivyokuwa kwa jamii za kipagani na sasa tutaeleza ulivyo kwa
Wakristo.
Injili ya Marko sura ya kwanza msitari wa 9: “Ikawa siku zile, Yesu alikuja kutoka Nazareti ya
Galilaya, akabatizwa na Yohana katika Yordani. Mara alipopanda kutoka majini, akaona mbingu
zinapasuka, na Roho, kama hua, akishuka juu yake”.
Injili ya Mathayo, sura ya 3, msitari wa 11:
“Kweli mimi ( yaani Yohana) nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma
yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa
Roho Mtakatifu na kw Injili ya Marko, sura ya 16, msitari wa 16: “Aaminiye na kubatizwa
ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”, [pia vipengele vya 13 – 17 katika sura hii vinaelezea
ubatizo. Ubatizo umetajwa katika Injili ya Luka 111
, Injili ya Yohana, sura ya tatu, msitari wa 22,
23 na 26, pamoja na sura ya nne, msitari wa 1. Matendo ya Mitume 4: 1, Wakorintho wa
59
kwanza sura ya 1 msitari wa 13, 14,16 na 17. ufunuo wa Yohana, Waraka wa Yohana kwa
Waefeso, waraka wake kw Waebrania, Wakorintho wa pili na nyingine nyingi, tumedokeza hizo
chache tu ili kutaka kufupisha.
SURA YA KUMI NA SABA
ULINGANISHO KATI YA KRISHNA NA YESU
(YASEMWAYO NA WAKRISTO KUHUSU YESU NA YASEMAWYO NA WAHINDU
KUHUSU KRISHNA)
WASEMAVYO WAPAGANI WA
KIHINDU KUHUSU KRISHNA MWANA
WA MUNGU
Krishna ni: “ Mkombozi, kafara, Mfariji,
mchungaji mwema, mpatanishi, mwana wa
Mungu na nafsi ya pili katika utatu
mtakatifu ambao ni Baba, Mwana na Roho
Mtakatifu”
1- Krishna alizaliwa na mwanamwali
Devaki, ambaye Mungu alimchagua kuwa
mama wa mwanaye kwa sababu ya
utakatifu na staha aliyokuwa nayo112
2 – Malaika walimtukuza Devaki mama wa
Krishna Mwana wa Mungu na kusema “
ulimwengu unapaswa kuona fahari kwa
mwana wa huyu mwanamke mtakatifu 113
3 – Watu walitambua kuzaliwa kwa Krishna
kutokana na nyota yake iliyoonekana
mbinguni 115
WASEMAVYO WAKRISTO KUHUSU
YESU KRISTO MWANA WA MUNGU
Yesu Kristo ni: Mkombozi, kafara, mfariji,
mchungaji mwema, mpatanishi, mwana wa
Mungu na nafsi ya pili katika utatu
mtakatifu
ambao ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu”
1- Yesu alizaliwa na mwanamwali Mariam,
ambaye Mungu alimchagua kuwa mama wa
mwanaye kwa sababu ya utakatifu na staha
aliyokuwa nayo.
2 – Malaika akaingia nyumbani kwake,
akasema ,salamu, uliyepewa neema.Bwana
yu pamoja nawe 114
3 – Alipozaliwa Yesu Kristo, nyota yake
ilionekana upande wa
mashariki ambayo kwayo watu walipata
kujua mahali alipozaliwa116
4 – Alipozaliwa Krishna, ardhi ilimtukuza
Mungu, mwezi ukaangza, roho zikaimba,
malaika wakashangilia kwa furaha na
mawingu yakaimba kwa ghani za ajabu117
5-Krishna alitokana na kizazi
Cha kifalme, lakini alizaliwa
Pangoni katika hali ya udhalili
na madhila 119
6- Alipozaliwa Krishna, mwanga mkubwa
uliangaza pango lote na uso wa Devaki
mamaye ukatoa
miale ya nuru ya utukufu 121
60
7- Baada ya kumzaa akaanza kulia na
kuhuzunika juu ya mwisho mbaya wa
ujumbe wake, mara (mtoto) akaongea na
kumfariji123
8- Ng‟ombe walitambua kuwa
Krishna ni Mungu wakamsujudia
9- Watu walimuamini Krishna,
wakautambua uungu wake na kumpa
zawadi na msandali na manukato 126
4- Alipozaliwa Yesu Kristo, malaika
waliimba kwa furaha, na nyimbo na vinanda
vikasikika kutoka mawinguni 118
5- Yesu alitokana na kizazi cha
kifalme, ambapo wanamwita “mfalme wa
Wayahudi”, lakini
alizaliwa zizini katika hali ya
udhalili na madhila 120
6-alipozaliwa Yesu, nuru kubwa iliangaza
na kuwashangaza Yusufu na Mariamu.
7- Akiwa bado mtoto, Yesu Kristo
alimwambia mama yake, “ewe Mariam,
mimi ni Yesu Mwana wa Mungu, nimekuja
kaalivyokueleza malaika Gabriel
aliyetumwa Baba yangu kwako, ya kwamba
nimekuja kuukomboa ulimwengu”.
8 – Wachunga-kondoo walitambua kuwa
Yesu ni Mungu wakamsujudia 125
9- Watu walimuamini Yesu Kristo na
kuamini uungu wake na kumpa zawadi za
marhamu na manemane12
10 – Nared, Mtume wa Wahindu, alipopata
habari za kuzaliwa Krishna mwana wa
mungu, alikwenda kumuona ambapo
kutokana na vipimo Vyake vya
10 – alipozaliwa Yesu katika Bethelehemu
ya uyahudi katika zama za mfalme Herode,
tazama,
majusi kutoka mashariki, wakaja mpaka
Yerusalem wakisema: yu
nyota, alibaini kuwa ni mwana wa mungu 128
11- Alipozaliwa Krishna, Nanda,
mchumba wa Devaki, alikuwa mbali na
mfalme, kwani alikwenda
kwa mfalme kulipa kodi 130
12-Krishna alizaliwa katika mazingira ya
udhalili, na ufakiri japokuwa anatokana na
familia ya kifalme 132
13-Nanda aliye mchumba wa Devaki
mama Krishna, alisika wito kutoka
mbingunu ukimwambia, simama na
kamchukue mototo wa mamaye ukimbiye
nao mpaka Kakol na mvuke mto wa Jamnah
kwani mfalme ataka kumuua 134
14- mtawala wan chi aliposikia juu ya
kuzaliwa kwa Krishna mwana wa Mungu,
alimtafuta ili
amuangamize, na ili kufikia malengo yak e
aliamuru kuuliwa kwa watoto wote wa
kiume waliozaliwa katika usiku huo136
15-Jina la mji aliozaliwa Krshina ni Mitra,
na humo alifanya miujiza na, na mahali hapo
mpaka sasa panaheshimika Na Wahindi
wanaoabudu masanamu na kuamini kuwa
Krisna ni mwana wa Mungu na ni Mungu 138
61
wapi yeye alizaliwa mfalme wa Wayahudi? 129
11-Alipozaliwa Yesu, yusufu mchumba wa
mamaye hakuwepo nyumbani, na alikuja
kwa mfalme ili kumlipa kodi 131
12- yesu Kristo alizaliwa katika hali ya
udhalili, na ufakiri japokuwa anatokana na
kizazi cha kifalme 133
13-Yusufu mchumba wa Maryam
alioteshwa ya kwamba amchukue mototo wa
mama yake na kukimbilia Misri kwani
mfalme anamtafuta amwangamize 135
14-Mtawala wa nchi aliposikia juu ya uzawa
wa Yesu mwana wa Mungu, alimtafuta ili
amuue, na ili kutekeleza azma yake,
aliamuru kuuliwa watoto wote waliozaliwa
usiku huo 137
15-Jina la mji aliohamia Yesu Kristo baada
huko Misri baada ya
betelehemu ni Mitriyah, na husemekana
kuwa humo alifanya miujiza mingi
16-Mtakatifu Rama alizaliwa muda mfupi
kabla ya Krisna kudhihiri katika mwili wa
kibinaadamu ambapo mfalme wa nchi
aliazia kumuuwa kama pia kumua Krishna 139
17- Krishna alilelewa na wachunga kondoo,
na alipoletwa Mitra alihitaji sana kupata
mafunzo, hivyo akaletewa mwalimu
mwenye utaalamu, na baada ya muda mfupi
aliweza kumpita mwalimu wake kwa elimu
na kumshinda katika mambo mengi ya
kielimu katika utaalamu wa ndani wa
Kisanskrit 140
18-Siku moja, nyoka aliwauma baadhi ya
wafuasi ambao Krishna
Alikuwa akicheza nao, akahuzunika sana
kwa kifo chao
na kuwatazama kwa jicho la uungu wake
wakafufuka na kuwa hai142
16-Yohana mbatizaji alizaliwa muda mfupi
kabla ya Kristo,
ambapo mfalme Rohede alitaka
kumuangamiza yohana na pia
kumuangamiza Yesu kristo. Yohana ndiye
alitabiri kuzaliwa kwaYesu Kristo
17- Yesu alipelekwa kwa mwalimu
Dhacchos ili apate kumfundisha,
akamwandikia alphabeti na kumwambia
Yesu, sema „A‟.Bwana Yesu akasema,
niambie kwanza maana ya herufi „A‟ nami
nitasema „B‟.Mwalimu
akamtisha Yesu kuwa atampiga. Yesu
akasimama na kutafsiri maana ya „A‟ na „B‟
na kumweleza kuhusu herufi zilizosimama,
zilizoinama na zilizoungana, pamoja na zile
zenye nukta na irabu, na zile zisizokuwa na
nukta, na kwa nini zimewekwa katika
mpangilio huo, na akaanza kumweleza
62
mambo ambayo mwalimu hakuwahi
kuyasikia wa la kuyasoma 141
18- Yesu alipokuwa akicheza, mara, nyoka
akamuuma mmoja wa watoto aliokuwa
akicheza nao, na hapo Yesu akamshika yule
mtoto kwa mkono wake akarudi kuwa
mzima 143
19- Ishara na miujiza ya mwanzo
aliyoitenda Krishna ni kuponya ukoma 144
20- mwanamke kikongwe aliletwa mbele ya
Krishna, akiwa na chombo chenye
manukato, mafuta, msandali, zafarani na
aina nyingine za manukato na kumpaka
Krishna mashavuni kwa alama maalumu na
kisha kuimimina illiyobaki kichwani
mwake146
21- Krishna alisulubiwa na kufa msalabani
22- Krishna alipokufa yalitokea masaibu
mbalimbali na ishara kuu, mwezi
ukazungukwa na duara jeusi , jua likapoteza
nuru yake wakati wa mchana, mbingu
ikadondosha moto na majivu, miale ya moto
mkali ikatokea, mashetani wakawa
wanafanya uharibifu katik ardhi, na watu
wakashuhudia maelfu ya viumbe
wakipigana angani usiku na mchana, na
hayo yalionekana kila mahali148
23- Krishna alichomwa mkuki ubavuni
mwake 150
24- Krishna akiwa katika hali ya kusulubiwa
alimwambia mwindaji aliyemchoma mkuki
hali ya kuwa:
19- miujiza ya mwanzo aliyoitenda Yesu
Kristo ni kuponya ukoma 145
20- Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika
nyumba ya Simoni mkoma, mwanamke
mwenye kibweta cha marhamu ya thamani
kubwa akaimimina kichwani pake alipoketi
chakulani147
21- Yesu alisulubiwa na kufa msalabani
22- alipokufa Yesu yalitokea masaibu
mbalimbali, pazia la hekalu likapasuka
kutoka juu mbinguni, jua likapoteza nuru
yake tangu saa sita mpaka saa tisa, makaburi
yakafunguliwa na wengi katika watakatifu
wakafufuka kutoka makaburini mwao149
23- Yesu alichomwa mkuki ubavuni mwake 151
24- Yesu alimwambia mmoja wa wezi
waliosulubiwa pamoja naye:
Nenda mbinguni ewe mwindaji kwenye
makazi ya miungu ukiwa umezungukwa na
rehema zangu152
25- Krishna alikufa kisha akafufuka katika
wafu154
63
26- Krishna aliteremka kuzimu156
27- Krishna alipaa mbinguli kwa mwili
wake ambapo wengi walimuoana akipaa 158
28- Siku za mwisho, Krishna atarudi
duniani, na ataonekana akiwa akiwa juu ya
farasi mwenye kuzatitiwa kwa silaha, na
wakati wa kuja kwake jua na mwezi
vitapoteza nuru na ardhi itatetemeka na
kutikisika na nyota zitadondoka kutoka
mawinguni160
29- siku za mwisho Krishna atawahukumu
wafu162
30- wanasema kuwa Krishna ndiye Muumba
wa kila kitu, na pasipokuwa yeye
kisingekuwapo chochote katika
vilivyokuwapo, kwa hiyo yeye ni muumba
wa milele164
31- Krishna ndiye Alfa na Omega, mwanzo,
katikati na mwisho wa kila kitu
“amin, nakwambia, leo hivi utakuwa pamoja
nami peponi”153
25- Yesu alikufa kisha akafufuka katika
wafu 155
26- Yesu aliteremka kuzimu157
27 – Yesu alipaa mbinguli kwa mwili wake
ambapo wengi walimuoana akipaa159
28- Siku za mwisho, Yesu atarudi duniani,
na ataonekana akiwa akiwa juu ya farasi
mwenye kuzatitiwa kwa silaha, na wakati
wa kuja kwake jua na mwezi vitapoteza
nuru na ardhi itatetemeka na kutikisika na
nyota zitadondoka kutoka mawinguni161
29- siku za mwisho Yesu atawahukumu
wafu163
30- wanasema kuhusu Yesu Kristo kuwa
ndiye Muumba wa kila kitu, na pasipokuwa
yeye kisingekuwapo chochote katika
vilivyokuwapo, kwa hiyo yeye ni muumba
wa milele165
31- Yesu ndiye Alfa na Omega,
mwanzo, katikati na mwisho wa kila kitu 166
32- Krishna alipokuwa ardhini alipambana
na viumbe waovu bila kujali madhara
yanayoweza
kumpata, na akaeneza mafundisho wake
kwa kutenda maajabu na miujiza, kama vile
kufufua wafu, kuponya wenye ukoma,
viziwi na vipofu, pamoja na kumsaidia
mnyonge dhidi ya muonevu, na
aliyedhulumiwa dhidi ya dhalimu. Na
wakati huo walikuwa wakimuabudu,
wakisongamana kwake na walikuwa
wakimchukulia kuwa ni Mungu 167
. 33- Krishna alikuwa akimpenda
mwanafunzi wake Arjuna kuliko wanafunzi
wake wengine169
34- Mbele ya Arjuna lilibadilika umbile la
Krishna, uso wake ukang‟ara kama jua,
utukufu wa ukuu ukakusanyika ndani ya
Krishna mungu mkuu, na hapo Arjuna
akainamisha kichwa chake kwa
unyenyekevu na woga, akaifunga mikono
yake na kusimama kwa heshima na kusema,
sasa nimeuona uhalisia wako kama ulivyo,
nami nataraji rehma zako ewe bwanawa
mabwana, basi rudi na ujionyeshe katika
ubinaadamu wako, wewe ndiye mwenye
ufalme wote 171
64
32- Yesu alipokuwa ardhini alipambana na
viumbe waovu bila kujali madhara
yanayoweza kumpata, na akaeneza
mafundisho wake kwa kutenda maajabu na
miujiza, kama vile kufufua wafu, kuponya
wenye ukoma, viziwi na vipofu, pamoja na
kumsaidia mnyonge dhidi ya muonevu, na
aliyedhulumiwa dhidi ya dhalimu. Na
wakati huo walikuwa wakimuabudu,
wakisongamana kwake na walikuwa
wakimchukulia kuwa ni Mungu 168
33- Yesu alikuwa akimpenda mwanafunzi
wake Yohana kuliko wanafunzi wake
wengine 170
34- Baada ya siku sita Yesu akawatwaa
Petro, Yakobo na Yohana nduguye,
akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;
akageuka sura yake mbele yao, uso wake
ukang‟ara kama jua, mavazi yake yakawa
meupe kama nuru… Alipokuwa katika
kusema, tazama, wingu jeupe likawatia
uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile
wingu ikisema, Huyu ni mwanangu,
mpendwa wangu ninayependezwa naye,
msikieni yeye, na wale wanafunzi
waliposikia, walianguka kifulifuli,
wakaogopa sana 172
35- Krishna alikuwa mbora wa watu kwa
tabia na maumbile. Alitoa mafundisho na
ushauri kwa Moyo mkunjufu. Naye ndiye
msafi na mwenye staha, aliye mfano kwa
mwanadamu. Alikubali mateso kwa sababu
aliwapenda
watu, na aliwatawadha Wabrahma miguu,
naye ndiye kuhani mkuu, mwenye uweza
aliyejionyesha kwetu katika mwili wa
kibinadamu173
36- Krishna ndiye Brahma Mungu mkuu, na
kuonekana kwake katika mwili ni siri katika
siri za uungu wake wa ajabu 175
37- Krishna ni nafsi ya pili katika utatu
mtakatifu kwa Wahindu wa kipagani
wanaoamini uungu wake177
38- Krishna alimwamuru yule atakayee
imani kwa moyo mmoja, aziache mali zake
na vyote avipendavyo na kuvitamani katika
ufalme wa ulimwengu huu na aende mahali
pasipokuwa na watu na ziweke fikra zake
kwa Mungu tu 179
39- Krishna alimwambia mwanafunzi wake
mpendwa Arjuna kuwa, lolote ufanyalo,
chochote utoacho kumpa masikini, chochote
unachokula, na sadaka
35- Yesu alikuwa mbora wa watu kwa tabia
na maumbile. Alitoa
mafundisho na ushauri kwa moyo
mkunhjufu. Naye ndiye msafi na mwenye
staha, aliye mfano kwa mwanadamu.
Alikubali mateso kwa sababu aliwapenda
watu, na aliwatawadha wanafunzi miguu
naye ndiye kuhani mkuu, mwenye uweza,
mwenye uweza aliyejionyesha kwetu katika
mwili wa kibinadamu 174
.
36- Yesu ndiyeYehova Mungu mkuu, na
kuonekana kwake katika mwili ni siri katika
siri za uungu wake wa ajabu 176
37- Yesu Kristo ni nafsi ya pili katika utatu
mtakatifu kwa imani ya Wakristo178
65
38- Yesu alimwamuru kila atakaye imani
kwa moyo mmoja afanye yafuatayo, “ Basi
wewe usalipo, ingia katika chumba chako
cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako,
usali mbele za Baba yako aliye sirini; na
Baba yako aonaye sirini atakujazi180
39- Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo
neon lolote, fanyeni yote kwa utukufu wa
Mungu182
yoyote uitoayo
na mambo yoyote mema uyafanyao, basi na
yawe kwa ajili yangu, mimi ndiye 181
40- Krishna alisema, Mimi ndiye chanzo cha
uwepo wa viumbe, katika mimi vilikuwepo,
na katika mimi kila kitu kinaishi, na vitu
vyote ulimwenguni vinanitegemea mimi na
kufungamana na mimi kama lulu katika uzi
(sindano)183
41- Krishna alisema: “Mimi ndimi nuru iliyo
katika jua na mwezi, nami ndiye nuru iliyo
katika moto, nami ndimi nuru ya kila
kiangazacho na nuru ya nuru zote, kwangu
hakuna giza”185
42- Krishna alisema: Mimi ndimi mlinzi,
Bwana, kimbilio na njia ya ulimwengu187
43- Krishna alisema: Mimi ndimi wa
kwanza, katikati, mwisho na wa milele,
nami ndiye muumba wa vyote, nami ndiye
nitakaye 189
40- kila kitu chatokana na Yesu, katika Yesu
na kwa ajili ya Yesu
“vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo
yeye hakikufanyika chochote
kilichofanyika”184
41- Basi Yesu akawaambia tena akasema,
Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye
anifuataye hatakwenda gizani”186
42- Yesu akamwambia: Mimi ndimi njia, na
kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba ili kwa
njia ya mimi188
43- Yesu akasema: Mimi ni wa kwanza na
wa mwisho … Nami ninazo funguo za
mauti, na za kuzimu 190
Haya ni machache katika yale yaliyoelezwa na waumini hao
66
SURA YA KUMI NA NANE
ULINGANISHO KATI YA BUDDHA NA YESU
(YASEMWAYO NA WAKRISTO KUHUSU YESU NA YASEMAWYO NA WAHINDU KUHUSU
BUDDHA)
WASEMAVYO WAPAGANI WA
KIHINDU KUHUSU BUDDHA MWANA
WA MUNGU
WASEMAVYO WAKRISTO KUHUSU
YESU KRISTO MWANA WA MUNGU
1- Buddha alizaliwa na Bikira Maya pasipo
kulala na mwanaume yeyote191
2- Buddha alijibadilisha katika mwili kupitia
roho mtakatifu aliyeingia katika mwili wa
Bikira Maya193
3- Buddha alipoteremka na kuingia katika
mwili wa Bikira Maya, kizazi chake
Gautama Buddha
67
kilikuwa kama kioo king‟aracho, ambapo
Buddha alionekana humo kwa mfano wa ua
zuri 195
4- Nyota iliyoonekana upande wa mashariki
ndiyo iliyojulisha kuzaliwa kwa Buddha,
nyota hiyo huiita “nyota ya Kristo” 197
5- Buddha alizaliwa na bikira Maya,
aliyetokewa na roho mtakatifu, tarehe 25
mwezi wa 12.199
6- alipozaliwa Buddha, majeshi ya mbinguni
yalifurahi, malaika wakaimba mtoto
aliyezaliwa nyimbo utukufu wakisema: “
leo duniani amezaliwa Buddha ili awape
watu furaha na amani, na aangaze kwenye
giza na awape vipofu machio”201
7- Makuhani na wakuu wa dini
walimtambua Buddha na kuona siri ya
uungu wake, ambapo haikupita hata siku
moja baada ya
1- Yesu Kristo alizaliwa na Bikra Mariam
pasipo kulala na mwanaume yeyote 192
2- Yesu Kristoalijibadilisha katika mwili
kupitia roho mtakatifu aliyeingia katika
mwili wa Bikira Mariam194
3- Yesu alipoteremka na kuingia katika
mwili wa Bikira Mariam,
kizazi chake kilikuwa kama kioo
king‟aracho, ambapo Yesu alionekana humo
kwa mfano wa ua zuri 196
4- nyota iliyoonekana upande wa mashariki
ndiyo iliyojulisha kuzaliwa kwa Yesu
(bwana Doane anasema kuwa ni lazima
nyota hiyo iitwe “ nyota ya Kristo”) 198
5- Yesu alizaliwa na bikira Mariam,
aliyetokewa na roho
mtakatifu, tarehe 25 mwezi wa 12200
6- alipozaliwa Yesu, malaika wa mbinguni
walifurahi na kumwimbia mtoto nyimbo za
utukufu wakisema: “atukuzwe Mungu juu
mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu
aliowaridhia”202
. 7- Yesu alitembelewa na Makuhani ambao
waliitambua siri ya uungu wake wakamwita
MUNGU204
kuzaliwa kwake watu wakamsabahi na
kumwita MUNGU 203
8-wakampa mtoto Buddha zawadi za
dhahabu vya na vitu vingine vya thamani205
9- Buddha akiwa bado mtoto mchanga
alimwambia mamaye Maya kwamba yeye ni
mkuu wa watu wote.207
10- Buddha alikuwa mtoto hatari kwa
utawala wa mfalme ambaye alifanya juhudi
zote ili kumwangamiza baada ya kuambiwa
kuwa mtoto yule atauangusha ufalme wake
ikiwa ataendelea kuwa hai209
11- Buddha alipopelekwa shule
aliwashangaza walimu, pamoja na ukweli
kwamba hakuwahi kusoma hapo kabla
lakini aliwashinda wote katika uandishi,
hesabu, falsafa, na ukuhani 211
12- Budha alipopata umri wake miaka kumi
na miwili aliingia katika mahekalu akawa
anawauliza
Maswali magumu, kisha, akawafafanulia
hata akawashinda wanamjadala wote 213
68
8- na wakampa mtoto Yesu zawadi za
dhahabu, marham na manemane206
9- Yesu akiwa mtoto mchanga alimwambia
mamaye Mariam “mimi ni mwana wa
Mungu”208
10- Yesu alikuwa mtoto hatari ambaye
mfalme Herode alifanya kila juhudi
kumuangamiza ili asije akauangusha
utawala wake 210
11-Yesu alipopelekwa shule alimshangaza
mwalimu wake, akamwambia Yusufu
babaye: umeniletea mtoto ili nimfundishe
japokuwa anaujuzi kuliko Walimu wote, na
wote waliosikia walishangazwa kwa uelewa
na ufahamu wake 212
12-Yesu alipopata umri wa miaka kumi na
miwili walimpeleka hekaluni huko
Yerusalemu, akawa anawauliza walimu
maswali magumu, na kuwafafanulia na
kuwashangaza wote 214
13-Siku moja Budha aliingia moja ya
mahekalu,mara masanamu yakasimama
kutoka mahali pake yakajinyoosha miguuni
mwa Budha na kumsujudia 215
14-Nasaba ya Gautama budha kutoka kwa
Baba yake Sadodama, huifungamanisha na
watu mbalimbali, wote wakitokana na kizazi
cha kifalme mpaka kwa adamu Baba wa
wanadamu,na majina na matukio mengi
hutajwa katika kizazi chake yameelezwa
katika Tourati ya Mayahudi. Na hakuna na
uwezekano wa kupata uhakika wa visa vyao,
kutokana na kukizana ndani mwake,
kwasababu wanahistoria wa kibudha
wanaingiza majina na makabila na kubuni
majina yanayowawezesha kutukuza nasaba
ya kiongozi wao kwasababu ya kumchukulia
kama Mungu 216
15- Budha alipotoka kufanya ibada
alitokewa na Maara (yaani shetani) ili
kumtia majaribuni 218
16-Maara alimwambia Budha :
“Usiyaharibu maisha yako katika shughuli
za dini, kwani kwa kipindi cha siku saba
waweza kuwa mfalme wa dunia” 220
17-Budha hakuyasikilza maneno ya shetani
bali alimwambia: “ondoka kwangu” 222
13-sikumoja Yesu alipita karibu na vibao
vya matangazo, nayo matangazo yaliinama
na kusujudia
14-Nasaba ya Yesu kutoka kwa baba yake
Yusufu hufungamana na maisha na watu
mbalimbali wote wakitokana na kizazi cha
kifalme mpaka kwa Adamu, na majina ya
kizazi chake yametajwa katika tourat ya
wayahudi na haiwezekani kupata uhakika
wa visa hivyo kutokana na kukinzana ndani
yake, kwasbabu wanahistoria wa kikristo
walibuni majina kwa lengoo la kuitukuza
nasaba ya kiongozi wao kwa sababu ya
kuamini kuwa ni Mungu 217
15-Yesu alipoanza kuhubiri alitokewa na
shetani ili amtie majaribuni 219
69
16-Shetani akamwambia Yesu: Nitakupa
haya yote ikiwa utaanguka kunisujudia 221
17-yesu akamwambia akisema: “Ondoka
shetani we! 223
18- Maara alipoacha kumjaribu Budha,
mbingu ilinyesha maua na marham yalienea
angani224
19-Budha alifunga kwa kipindi kirefu 226
20- Budha mkombozi alibatizwa, na wakati
wa kubatizwa kwa maji roho wa Mungu
alikuwapo, Naye hakuwa Mungu mkuu
pekee bali roho mtakatifu ambaye katika
yeye, Gamtama alipata kuwa katika mwili
alipomtokea bikira Maria 228
21-Budha alipokuwa ardhini katika siku
zake za mwisho umbile lake lilibadilika
alipokuwa juu yamlima wa bendaqa,na
ghafla nuru ikamzunguka kichwani mwake
kwa namna ya taji. Wanasema kuwa mwili
wake ulitoa nuru Kali, ikawa kama sanamu
la dhahabu likang‟ara kama jua au kama
mwezi, akabadilika katika sehemu tatu
zenye kuangaza, Mashuhuda walipoona
mabadiliko haya
na hapo walisema: huyu sio binadamu!Bali
ni Mungu mkuu230
22-Budha alitenda maajabu na mijiza kwa
ajili ya watu, na visa vyote vinavyoelezea
mambo hayo vitaja maajabu zaidi ya
inavyoweza kufikiriwa 232
18- kisha Ibiliisi akamwacha, na tazama,
malaika wakaja wakamtumikia..225
19-Yesu alifunga kwa kipindi kirefu 227
20- yohana alimbatiza Yesu katika mto
Yordani, na Roho wa Mungu alikuwapo,
naye hakuwa Mungu mkuu pekee, bali na
roho mtakatifu ambaye katika yeye
ulifanyika mwili wake pindi alipomtokea
bikira Maria hivyo naye ndiye baba, mwana
na Roho mtakatifu 229
21-Yesu alipokuwa ardhini alibadilika
umbile lake, na baada ya siku sita yesu
akatwaa Petro na Yakobo na Yohana
ndguye, akawaleta juu yam lima mrefu
faraghani. Akageuka sura yake mbele yao,
uso wake ukang‟ara kama jua, mavazi yake
yakawa meupe kama nuru 231
22-yesu alitenda maajabu na miujiza kwa
ajili ya watu woye, ambapo simulizi za
matukio
hayo zimejaa maajabu zaidi ya inavyoweza
kufikirika 233
23- Katika maombi yao kwa Budha,
waumini hutarajia kuingia Pararadiso 234
24-Budha alipokufa na kuzikwa, sanda
ilipasuka na kaburi likafunguka kwa nguvu
ya kimungu236
25-Budha alipokamilisha kazi zake duniani,
alipaa kwa mwili wake kuelekea mbinguini 238
26- Budha atarudi duniani kwa mara
nyingine ili kurudisha amani na baraka
pamoja na kuwahukumu wafu.240
70
27- Budha ndiye Alfa na Omega, hana
mwanzo wala mwisho, naye ndiye Mungu
Mkuu na wa milele242
28- Buddha alisema, nitabeba dhambi zote
zilizotendeka hapa duniani ili ulimwengu
ukombolewe kutokana na dhambi244
29- Buddha alisema, ficheni mambo
matendo mema myatendayo na mkubali
dhambi zenu waziwazi 246
30- Buddha alisema kuwa hakuja kutangua
Taurat, bali alikuja kuitimiliza, na
alifurahishwa kuwa mmoja wa walimu 248
23- Katika maombi yao kwa yesu, waumini
hutaraji kuingia paradise kwa Uungu wake. 235
24- Yesu alipokufa na kuzikwa, sanda
ilipasuka na kaburi likafunguka kwa kwa
nguvu za ajabu237
25-Yesu alipokamilisha kazi zake za
duniani, alipaa kuelekea mbinguni baada ya
kusulubiwa239
26- Yesu atarudi duniani kwa mara nyingine
ili kurudisha amani na baraka pamoja na
kuwahukumu wafu.241
27- Yesu ndiye Alfa na Omega, hana
mwanzo wala mwisho, naye ndiye Mungu
Mkuu na wa milele243
28- Yesu ni mkombozi wa ulimwengu
ambaye alikubali kubeba dhambi zote
badala ya wale waliozitenda ili ulimwengu
ukombolewe kutokana na dhambi245
29- Yesu alisema, ficheni matendo mema
myatendayo na mkubali makosa yenu
waziwazi 247
30- Yesu alisema, “Msidhani ya kuwa
nalikuja kuitangua torati au manabii; la,
sikuja kutangua, bali kutimiliza” 249
31- Kutokana na mafundisho ya Budha,
maisha yetu pamoja na ndugu na majirani
zetu lazima yawe kwa wema na mapendo 250
32- Siku za mwanzo za mahubiri, alikwenda
katika mji wa Pinaris, akafundisha huko,
akafuatwa na Kondania kisha akafuatwa na
wanaume wangine wengine na wote
wakawa wake, na tokea wakati huo, popote
alipokwenda alifuatwa na wanaume na
wanawake wengi ambao walikuja kuwa
wafuasi na wanafunzi wake252
33- Buddha aliwaambia wanafunzi wake
kuwa waiache dunia na mali zao na waishi
maisha ya ufakiri na umasikini 254
34- imeelezwa katika vitabu vya dini ya
kibuddha kuwa Waandishi walitaka ishara
kutoka kwa Buddha ili wapate
kumwamini256
35-malengo ya Buddha yalikuwa katika
kujenga mamlaka ya kidini, yaani mamlaka
kutoka mbingu 258
36- katika mafundisho ya dini ya kibudha,
wanasema kuwa “ mtu akipatwa na huzuni,
machungu, balaa na kukata tama ni dalili
kuwa alifanya madhambi hapo kabla au
sasa hivi ambayo yanamgharimu 260
31- Yesu alisema, lakini mimi nawaambia,
Wapendeni, adui zenu, waombeeni
wanaowaudhi”251
32- Siku za mwanzo za mafundisho na
mahubiri ya Yesu, alikwenda katika mji wa
71
Kapernaum, kahubiri huko, watu wengi
wakamfuata na kuwa
wanafunzi wake, na tokea wakati huo,
popote alipokwenda alifuatwa na wanaume
na wanawake wengi ambao walikuja kuwa
wafuasi na wanafunzi wake 253
33- Yesu aliwaambia wale waliomfuata
kuwa waache mali zao na waishi maisha ya
ufakiri255
34- imeelezwa katika vitabu vya dini ya
kikristo kuwa waandishi na
mafarisayo walitaka ishara kutoka kwa Yesu
ili wamwamni 257
35-tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri,
na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa
mbinguni umekaribia 259
36- Hata alipokuwa akipita alimwona mtu,
kipofu tangu kuzaliwa. Wanafunzi wake
wakamwuliza wakisema, Rabi, ni yupi
aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi
wake, hata azaliwe kipofu? 261
37- katika kitabu kiitwacho somadeva kuna
simulizi iliyoandikwa na mmoja wa
watakatifu wa kibudha kwamba Krishna
aliling‟oa jicho lake na kulitupa, kwani
lilikuwa likimsumbua 262
37- jicho lako la kuume likikukosesha,
ling‟oe ulitupe mbali nawe 263
72
Miongoni mwa majina na lakabu ambaazo huzitumia kwa Buddha ni:
Saaqiya Sanja ( yaanai simba wa kabila la Saaqiya), Saaqiya Moni (yaani mkuu wa kabila la
Saaqiya), Sogata (mtukufu), Saatha (mwalimu), gina (mshindi), Bihakafad (aliyebarikiwa),
Lokanatha (bwana wa ulimwengu), Sarmagina (mwenye kuwapo), dharmaraja (mfalme wan
chi), mwenye kutoa furaha, mungu wa vyote, mkuu, wa milele, muondoshaji wa taabu na
machungu, mlinzi wa ulimwengu, kielelezo cha rehma, mwokozi wa watu, mungu kati ya
miungu, masihi, mwana wa pekee, njia ya uzima, na majina mengine mengi yaliyopo katika
mlolongo huo.
Yesu naye pia hupewa sifa na majina kama aliyopewa Budha, na tumeonelea kuwa ni vyema
kuyateja kwa mara nyingine ikiwa ni pamoja na kutaja mahali yanapopatikana ili iwe rahisi kwa
msomaji kurejea huko na kufanya ulinganisho wakati atakapo kufanya hivyo.
Simba wa kabila la Yuda 264
, mkombozi 265
, mzawa wa pekee 266
, mtakatifu wa Mungu 267
,
mungu mwenye kuhimidiwa milele 268
, mwana-kondoo wa Mungu 269
, bwana wa utukufu 270
,
muumba wa vyote 271
.
Miongoni mwa majina maarufu ni: kafara, mkombozi, mpatanishi, neon, mwanakondoo wa
Mungu, mwana wa Mungu, mzawa wa pekee, na majina mengine mengi.
VITABU REJEA:
1-Allen: Indian Ancient and Moder
2- Amberly:Analysis of religious belief
3- Kowenio: (a) Ancient Faiths,
(b)Asiatic Reserches
4- Beal - The romantic Legend of Saki Buddha from Chinese Sanskrit
5- Bonwick: Egyptian Belief and Modern Thought
6- Davis: (a) Buddhism
(b) The Chinese
7-Bunsen: Angel Messiah
8- Doane: Bible Myths and their Parellels in other Religions
9-Dunlap: Vestiges of Spirir History of Man
10- Dupis: The Origin of All Religious Worship
11- Faber: The Life of Christ
12- Fergusson: Tree and Serpent Worship
13- Fiske: Myth and myth makers
14- Frontingham: The Cradle of Christ
73
15- Gangooly: Life and Religion of The Hindoos
16- Geickic: Life of Christ
16- Gergoius: Tibetinum Alphabetum
17- Gibbon: The History of the Decline of the Roman
18- Guingniaut: Monumental Christanity
19- Hardy: The Legends and Theories of the Buddhism
20- Hebrew Lexicon
21- Holy Bible
22- Higgins: The Celtic Druids
23- Huxley: Evidence as to Man‟s Place in Nature
24- Helsly Stevens: Faith and Reason
25- Inman: Ancient Pagan and Modern Christian Symbolism
26- Jameson: the History of Our Lord
27- Kingsborough: Antiquities of mexico
28- knight: The Symbolical language of Ancient Art and Mythology
29- Lundy: monumental Christianity
30- Lillie: Buddha and Early Buddism
31- Maurice: (a) Indian Antiquities
(b) The History of Hindostan
32- Muller: History of Ancient Sanskrit Literature
33- Murray: (a) Manual of Mythology
(b) oriental Religions
34- Prescott: History of the Conquest of Mexico
35- Prichard: (a) An Analysis of the historical Records of Ancient Egypt
(b) Progress of Religious ideas
36- Squire: The Serpent Symbol
37 Vishnu Purama (imetafsiriwa kutoka Kisanskrit) na Bwana Wilson
38- William: Indian Wisdom
39- Hinduism
88. The History of Buddhism, ukurasa wa 23 na 33.
89. The Chinese, juzuu ya 1, ukurasa 173.
90. Analysis of religious belief, ukurasa 227.
91. Life of Christ, juzuu ya 1, ukurasa 144.
92. Analysis of the Historical Records of Ancient Egypt, ukurasa wa 56.
93. Egyptian Belief, ukurasa wa 325.
94. Socrates alizaliwa mnamo mwaka 470 BC, na kufa mwaka 399 BC mjini Athena. Binaadamu
kuitambua nafsi yake ndio uliokuwa mhimili wa falsafa za Socrates.
74
95. Tiber: ni mto ulioko katikati mwa Italia, unaanzia katika milima ya Ebnin na kuelekea
upande wa magharibi na kumwaga maji yake katika bahari ya Titani, na pembezoni mwake kuna
mji wa Roma.
96. Luka 2: 8- 11: na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda
kundi lao kwa zamu usiku. Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, utukufu wa Bwana
ukawang‟aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, msiogope; kwa kuwa
mimi nanawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika
mji wa Daud amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana…‟.
97. Injili ya Mathayo, sura ya 1, msitari wa 1: “ kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa
Daudi, mwana wa Ibrahimu.
98. Injili ya Luka, sura ya 1, msitari wa 26- 27: Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na
Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa
ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi”.
99. Katika kitabu chake kiitwacho: Life and Religion of Hindoos, ukurasa wa 134.
100. kitabu chake kinaitwa : Torah Lexicon
101. Marko, sura ya 16, msitari wa 6: “Naye akawaambia, msistaajabu; mnamtafuta Yesu
Mnazareti, aliyesulubiwa; amefufuka; hayupo hapa”.
102. Luka 24, msitari wa 6: “… kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu? Hayupo hapa,
amefufuka”.
103. Yohana, sura ya 20, msitari wa 1- 18. miongoni mwa yaliyoelezwa humo ni: “…kwa maana
hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka….”.
104. miongoni mwa ishara zilizotajwa katika sura hii (Injili ya Mathayo 24: 29) ni: “…jua
litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za
mbinguni zitatikisika; ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni..”.
105. Amberly, katika kitabu chake kiitwacho: Analysis of religious belief, ukurasa wa 61.
106. Bunsen, katika kitabu chake kijulikanacho kama: The Angel Messiah, uk. 42.
107. Higgins, katika kitabu chake, The Celtic Druids, j. 2, uk. 69.
108. Lillie – Buddha and Early Buddhism, ukurasa wa 55 na 134.
109. Doane, katika kitabu chake kilichotajwa mwanzo, uk. 320.
110.Prescott- History of the Conquest of Mexico.
111. Luka 3: 3: “Akafika nchi yote iliyo karibu na Yordani, akihubiri ubatizo wa toba liletalo
ondoleo la dhambi”.
112. Doane, uk. 278.
113. The History of Hindostan, j. 2, uk.329.
114. Luka 1: 28-29.
115. The History of Hindostan, j. 2, uk.317 na 336.
116. Mathayo 2:1-2.
117. Visnu Purana, ukurasa wa 502.
118. Luka 2:13.
75
119, 120, 121.Doane, ukurasa 279.
122. Injili ya uzao wa Yesu Kristo, 12: 13.
123. The History of Hindostan, j. 2, uk.311.
124. Doane, uk.279.
125. Luka, 2: 8-10.
126. Oriental religions, uk.500, na Ancient religions, j.2 uk.353.
127. Mathayo, 2:2.
128. The History of Hindostan, j. 2, uk.317.
129. Mathayo, 2: 1-2.
130. Vishnu Purana, sura ya pili ya kitabu cha tano.
131. Luka 2:1-17.
132. Asiatic Research, j.1 uk.259, na The History of Hindostan, j.2 uk.310.
133. . Angalia mlolongo wa nasaba yake katika Injili za Mathayo na Luka na ni kwa hali gani
kazaliwa.
134. Vishnu Purana, sura ya 3
135. Mathayo, 2:13
136. Doane, uk.280.
137. Mathayo sura ya 2.
138. The History of Hindostan, j. 2, uk.317. na Asiatic Research, j.1, uk.259.
139. Inijlut tufuoliyyah, kilichotungwa na Bwana Higgins.
140. Doane, uk.280, na The History of Hindostan, j. 2, uk.321.
141. Injilut Tufuoliyyah, sura ya ishirini, msitari wa 1-8.
142. The History of Hindostan, j. 2, uk. 343.
143. Injilut Tufuoliyyah, sura ya 18.
144. The History of Hindostan, j. 2, uk. 319.
145. Mathayo 8:2.
146. The History of Hindostan, j. 2, uk. 320.
147. Mathayo 26: 6-7.
148. progress of Religious Ideas, j. 1, uk. 71.
149. Mathayo sura ya ishirini na saba, vilevile, Injili ya Luka sura ya ishirini na tatu.
150. Doane, uk.282.
151. Doane, uk.283.
152. Vishnu Purana, uk.612.
153. Luka, 23:43.
154. Doane, uk.282.
155. Mathayo, 28: 7.
156. Doane, uk.282.
157. Doane, uk.282, na vilevile, vitabu vya imani ya Wakristo n.k.
158, 160 na 164. Doane, uk.282.
159 na 1661. Mathayo, sura ya 24.
162 na 167.Doane, uk.283.
76
163. Mathayo, 24:31, na Warumi 14:10.
165. Yohana, 1:1-3, na 1Wakorinto 8:6 pamoja na Waefeso 3:9.
166. Ufunuo wa Yohana, sura ya 1, msitari wa 8, na sura ya 22 msitari wa 13, na sura ya
21 msitari wa 6.
168. Tazama Injili ili kupata vifungu zaidi ya tulivyovitaja.
169. Bihakfat.
170. Yohana 13:23.
171. Indian Religion, cha Bwana Maurice, uk.219.
172. Mathayo 17:1-9.
173. Indian Religion, cha Bwana Maurice, uk.144.
174. Yohana 13:6-15.
175. Vishnu Purana, ukurasa wa 492, katika ufafanuzi wa msitari wa 3.
176. 1Timotheo, sura ya 3.
177. Maurice katika kitabu chake kiitwacho Indian Antiquities, uk.10.
178. Tazama vitabu vyao vyote vya kidini pamoja Injili zote.
179. Indian Religion, uk.211.
180. Mathayo 6:6.
181 Maurice katika kitabu chake kiitwacho Indian Antiquities, uk.212.
182. 1Wakorinto 10:31.
183. Maurice katika kitabu chake kiitwacho Indian Antiquities, uk.312.
184. Yohana 1:1-3.
185 na 189 .Maurice katika kitabu chake kiitwacho Indian Antiquities, uk.213
186.Yohana 8:12.
187. Doane 283.
188. Yohana 14:6.
190. Ufunuo wa Yohana 1:17-18.
191. Wlliams, katika kitabu chake, Indian Religion, uk.82 na 108.
192. Mathayo 1:18-24.
193. Doane, uk.289 pamoja na kitabu cha Bunsen kiitwacho The Angel Messiah, uk.10 na 25.
194. Mathayo 1:21.
195. Bunsen katika kitabu chake kilichotajwa hapo juu, uk. 20 na Doane uk.290.
196. Katika kitabu cha Doane, ukurasa wa 290, na Bunsen katika The Angel Messiah, ukurasa
wa 20 pamoja na kitabu cha Amberly kiitwacho Analysis of religious belief, ukurasa wa 424.
197,200, 201, 203 na 205. Doane, ukurasa wa 290.
198. Mathayo 2:1-3.
199. The Angel messiah, uk.10.
202. Luka 2:13-14.
204. Mathayo 2:1-11.
206 Mathayo 2:11.
207. Hardy katika kitabu chake kiitwacho The Buddhism Belief, uk.145-146.
208. Injilut Tufouliyyah 1:3.
209. The History of Buddhism cha bwana Beal, uk.103 na 103.
210. Mathayo 2:1.
211. Hardy, The Buddhism Belief, Bunsen katika The Angel Messiah, pamoja na Beal katika
The History of Buddhism.
212 na 214. Luka 2:41- 48.
77
213 na 215.The Angel messiah, uk.37. na History of Buddhism uk.67-69.
216 na 217. Doane, uk.291.
218, 232,234, 235, 238, 240, 242 na 245.Doane, 293. vilevile mafundisho ya kikristo.
219. Mathayo 4:1-18.
220, 222, 224 na 226. Doane, uk.292.
221. Mathayo1:11.
223. Luka 4:8 na Mathayo 4:10.
225. Mathayo 4:11.
227. Mathayo 4:2.
228 na 230. The Angel Messiah, uk.45, na History of Buddhism uk.177.
229. Mathayo 3:1-13.
231. Mathayo 17:1-2.
233. Mathayo 8:23-34.
236. The Angel Messiah, ukurasa wa 49.
237. Mathayo 28:6-8.
239 na 241.matendo ya mitume1:1-12.
243. Yohana 1:1, pamoja na ufunuo wa Yohana 1:8 na 21:6.
244. The History of Ancient Sanskrit Literature, ukurasa wa 80.
246. Muller katika Religious science, ukurasa wa 28.
247. Mathayo 6:1, pamoja na Yakobo 5:16.
248 The Angel Messiah, ukurasa wa 47-48, pamoja na Analysis of religious belief, ukurasa wa
285 n.k.
249. Mathayo 5:17.
250. The Religious science, ukurasa wa 249.
251. Mathayo 5:44.
252. Oriantal Monasticism, uk. 6.
253. Mathayo 4: 13-25.
254. Oriantal Monasticism, ukurasa wa 6 na 62.
255 Mathayo 8:19-20, na 16:25-28.
256. Religious Science, uk.27.
257. Mathayo 12:38.
258. History of Buddhism, uk.10.
259. Mathayo 4:17.
260. Buddhism, cha Davids, uk.103.
261. Yohana 9:1-2.
262.The religious Science, uk.245.
263. Mathayo 5:29.
264. Ufunuo wa Yohana 5:5.
265. Matendo ya mitume 7:35.
266. Waebrania 1:5-6.
267. Luka 4: 34, na matendo ya mitume 3: 14.
268. Ufunuo wa Yohana 71:14.
269. 1Wakorinto 2:8.
270. Ufunuo wa Yohana 17:14.
271. Yohana 2: 3 na 10, 1 Wakorinto 8: 56, na Wakolosai 1:16.
78